Sitta: Tuna wakati mgumu

Sitta: Tuna wakati mgumu

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
12,279
Reaction score
38,855
Kwa mara ya kwanza hapa Dodoma, Samwel Sitta kiongozi wa bunge maalum la katiba amekiri kwamba wana wakati mgumu.

Hayo ameyaongea wakati akiwa na kikao na kamati ya uongozi pamoja na ile iliyoandaa rasimu ya tatu ya katiba, nimethibitisha.

"Kwa kweli muda unavyozidi kwenda na kila jambo tunalofanya tunakumbana na upinzani mkali kinyume kabisa na matarajio yetu" alisema Sitta.

Sitta pia katika kikao hicho amesema kuwa anajiuliza sana ni kwa nini upepo unawabadilikia hivyo na anaonekana kukata tamaa kama rais Kikwete ataridhia rasimu ipigiwe kura mapema.

Sitta kwa mara ya kwanza tangu aanze mchakato huu wa katiba amesikika akisema kuwa ana wasiwasi huenda akageukwa siku za usoni na mahasimu wake kisiasa ndani ya CCM kwa lengo la kulipa kisasi ingawa hakugusia ni kisasi cha aina gani.

Ni ukweli usiopingika kuwa Samwel Sitta amejikuta akipoteza kabisa mvuto aliokuwa nao kisiasa baada ya kulingoza bunge la katiba na kujikuta akikosolewa na kutupiwa shutuma nzito waziwazi kama msaliti mkubwa wa wananchi kwa sasa.
 
Huyu Mzee ni msanii tu, alikuwa ameishajipigia bajeti ya laki tatu tatu na mkewe hadi October 4 halafu UKAWA wakataka kumpora kitumbua. Huyu mzee viwango vyake viko chini sana mkimpa uraisi kuna hatari tukarudi kupanga foleni ya sukari na sabuni au kuvaa makaniki yale. Amechoka kiakili
 
..Miradi yake yote ya kutetea wanachofanya Dodoma Imegonga mwamba. Aliwatumia St. Thomas Moore, akafweli.. akatumia BAKWATA Kristo nako hoi.. Sasa anaona hana uwezekano wa kupata 2/3.. anahaha kama kunguru wa Zanzibar ndani ya kizimba..Pole sana Sam 6.
 
Enzi za uspika alijenga heshima na aliheshimiwa na wengi. Not anymore, go directly to hell, do not pass go, do not collect £200!
 
keshatupiga hela analeta kebehi! haya bwana watz tumekuwa chunabuzi.
 
Na badooooo!! Sitta anavuna alichopanda. Huwezi kupanda mtama ukavuna mahindi !!!
 
Yeye so amejifanya mjuaji ngoja wammalize kabisa na akome na ubabe wake,binafsi nilikuwa namheshimu sana huyu mzee nakufikiria yawezekana akawa rais mzuri lakini kwa haya nimemtoa maanani kabisa yaheri el.
 
Kama ni ktk bunge hakusema hivyo unapotosha wananchi ambao hawakusikiliza wala kuangalia, alichosema ni kwamba chadema wameweka namba yao ya simu ktk mitandao na kuna wahuni wanamtumia msg za kumtukana, na akaahidi hajari wanaendelea na mchakato na katiba itapatikana.
 
6 ni mzee mpuuzi kuliko maelezo...sijui kama kweli ni mnyamwezi/msukuma yule babu yuko tofauti na wenzake.
 
Kama ni ktk bunge hakusema hivyo unapotosha wananchi ambao hawakusikiliza wala kuangalia, alichosema ni kwamba chadema wameweka namba yao ya simu ktk mitandao na kuna wahuni wanamtumia msg za kumtukana, na akaahidi hajari wanaendelea na mchakato na katiba itapatikana.

Sasa mkuu mimi nikudanganye ili iweje? kabla rasimu haijatoka nilileta hapa jamvini mambo ambayo rasimu imeyapendekeza ikiwamo waziri mkuu wa Tanzania kuwa makamu wa rais wa muungano kinyume na taratibu kwani anachaguliwa na watu wa jimbo moja, nikaleta lile la rais wa Zanzibar kuwa makamu wa kudumu wa Jamhuri ya muungano hali inayosambaratisha Zanzibar kama nchi yenye maslahi katika muungano achilia mbali kupoteza cheo chake cha mkuu wa nchi ya Zanzibar, pia nikatoa yale Kikwete na UKAWA waliyoongea kabla hayajawekwa hadharani, juzi nikaripoti namna Wazanzibar ambao wapo BMK wanavyotishwa..hujayaona hayo yakiripotiwa baadaye? pia ile thread ya Kikwete kuahirisha BMK hadi maridhiano wakati akiwa Marekani hukuona matokeo alipokuja? hili limetokea leo na Sitta anaonekana dhahiri kukata tamaa ingawa akija kwenu haonyeshi hivyo!
 
Mnaishi kwa ndoto.
Na ndoto zenu hazina athari kwa 6,ccm wala watanzania. Uzuri ni kwamba, mnatunga uongo kisha mnajidanganya then mnauamini uongo huohuo.
We keep on keeping on. Tunawatungia katiba
 
Back
Top Bottom