+255
JF-Expert Member
- Jan 1, 2012
- 1,939
- 762
yeye SITTA kwanini hawataji,Anataka nani awataje?Hebu awe mzalendo bana
Kwa hiyo unataka awataje hata kama hawajui?
yeye SITTA kwanini hawataji,Anataka nani awataje?Hebu awe mzalendo bana
Mh Sita acha uoga, source zako zinawajua na hata wewe umekua Waziri tangu awamu ya Kwanza, lazima unawajua. Tanzania haitajengwa na waoga kama wewe, wapenda vyeo
Haitoshi...lazima wahusika wachezee mvua za kutosha vingivevyo hili tatizo sugu la mafisadi ndani ya Serikali kamwe halitakwisha. Wale wa EPA, Kigoda, Meremeta, Rada n.k. mpaka kesho kutwa bado wanapeta na mabilioni yao.
Usiwe mvivu wa kufikiri, hakuna mnafiki kama Sitta. Unakumbuka alipokuwa Spika? Alitoa kauli gani orodha ya Mwembeyanga ilipowekwa hadharani? Alitoa kauli gani list ya wezi wa EPA ilipoanikwa hadharani? Je unakumbuka siku mkewe alipotajwa kushiriki katika kitendo cha rushwa alivyong'aka?Kwa hiyo unataka awataje hata kama hawajui?
Utafiti uliofanywa na Shirika la Kimataifa la Fedha la Global Financial Integrity, unaonyesha kuwa tatizo la utoroshaji wa fedha nchini limekuwapo katika awamu zote za Serikali zilizoiongoza Tanzania, lakini Awamu hii ya Nne imetia fora.
Utafiti huo uliofanywa kuanzia mwaka 1970 hadi 2009, unaonyesha kuwa katika utawala wa Rais Jakaya Kikwete, fedha zilizofichwa nje ya nchi ni Dola za Marekani 7,967.4 milioni (sawa Sh12.7 trilioni).