Sitosahau: Tuliowahi kukimbia kazi za kubeba beseni na kuzitembeza mitaani tukutane hapa

Dah imebidi nisome visa vya wenzangu nicheke. Ilikuta miaka kadhaa iliyopita wakati nimemaliza six nimetafuta sana tempo shule za sekondari nikakosa nikaamua kutulia kitaa nawaza ntatokaje huku nikisubiri matokeo ya mitihani. Ndipo nikakuta tangazo classified (matangazo madogo madogo, yanakuwa mengi kwenye page 1) kwenye gazeti sikumbuki jina.

Nikapiga simu ikapokelewa nikaambiwa kesho niende ofisini Magomeni kati ya Mapipa au Usalama ila ni maeneo hayo hayo karibu na Magomeni Mikumi. Mimi huwa sikeep bad memories in details. Kufika nikaonana na vijana wenzangu wakaka na wadada. Picha linaanza unapewa mtihani wa interview vimaswali na hesabu za kiboya wakati mi ndo nimetoka kupiga EGM yangu a few days ago.

After kama nusu saa hivi majibu yakatoka. Tukawa tunaitwa mmoja mmoja....mtu akiingia huko ndani ofisini kwa boss harudi. Zamu yangu ikafika. Lakini wakati wote nilikua nasikia kelele za watu kama vile wanapasha misuli au wanacheza karate nyuma ya nyumba huko. Nikajiuliza maswali bila majibu, watu hao wanafanya nini.

Nilipofika ndani kwa boss akaniambia hongera sana umefaulu kwa 95% na hivyo kazi umepata. Pembeni kuja jamaa kachoka choka....shati limepauka, kiatu kimelika soli kinyama na suruali yake nyeusi na bonge la tai. Akaambiwa utaenda naye huyu (mimi) umpe maelekezo leo siku nzima nami nikaambiwa niwe msikivu kwa mkufunzi wangu. Tukatoka, hapo sijahoji chochote zaidi ya kuitikia maelekezo. Jamaa akanitoa kupitia mlango mwingine nikakuta majagi, mabeseni, viti vya kukaa watoto ku poop, makontena na vikorokoro vingine vya plastic. Jamaa akabeba kadhaa akanipa namimi nibebe viti vile vya watoto...safari ikaanza. Akaniambia tunaenda Mabibo.

Tukapanda daladala mpaka Mabibo. Tulivyoshuka tukaanza kuingia mtaani, nakumbuka ni maeneo yale ya chuo cha NIT. Tukazunguka hukoo mitaani tunauza, tukiona watu wamekaa hasa wamama tunawaface. Moyoni nlikua nawaza tu nsije kutana na mtu anayenifahamu....aibu yake ingekuwa kubwa sana. Sijui ningeificha wapi sura yangu. Maana nimechoka, nna njaa, nimeloa jasho, kiatu kina vumbi balaa. Yule jamaa alinitembeza kutwa hatukula kitu. Tuliuza vitu vichache tu.

Tukapanda daladala tukarudi ofisini jioni saa 11. Wakaniambia hongera sana mmefanya kazi nzuri na mwanzo mzuri. Inabidi uende nyumbani uje kesho, ila kesho uje na tai.

Nilivyotoka pale nikasepa home nikaapa kutorudia tena. Kuna mwana tulikua naye, tuliexchange namba wakati tunasubiri majibu ya usaili yeye walienda Kinondoni huko. Jioni tulivyopigiana simu tukacheka sana. Jamaa alicheka sana kwenye simu dah.

Mwaka jana nikiwa na majukumu yangu kikazi nikapita ile mitaa ya NIT mtaa ule ule tulioanza kutembeza vile vitu, nilivyopark tu na kushuka niliduwaa kama sekunde 30 hivi nikasikitika peke yangu.

Mungu ni mwema, maisha yanasonga.
 
Dah imebidi nisome visa vya wenzangu nicheke. Ilikuta miaka kadhaa iliyopita wakati nimemaliza six nimetafuta sana tempo shule za sekondari nikakosa nikaamua kutulia kitaa nawaza ntatokaje huku nikisubiri matokeo ya mitihani. Ndipo nikakuta tangazo classified (matangazo madogo madogo, yanakuwa mengi kwenye page 1) kwenye gazeti sikumbuki jina...
Nmecheka sana namimi vile vile naingia tu nasikia watu nwakipayuka mala heeeeee hoooooo awa vipi awa kumbe ndo wapo kwenye tizi
 
Nimecheka balaa hapo makumbusho nimewahi kwenda ila nilishtuka baada ya kuona watu wanatoka na vyombo nikarudi zangu nyumbani, sehemu ya pili nilipata wale wa kuuza dawa za alovera dah nilitembea ubungo maziwa na vichochoro vingine hata sivijui vizuri afu nilivaa viatu virefu niliumwa siku mbili miguu sitasahau hizo kazi
 
Nimesoma yote, hii dunia tuishi tuu. Hakika tuko tofauti.

Hadithi yangu mm si sawa na hizi za waungwana humu, binafsi nilikataa mshahara wa laki sabiini ililikuwa hotel visiwani. P.O ni kimama flani hivi cha kikenya mara tu baada ya kumkabidhi CV na vyeti vyangu akaita wenzake, nikaambiwa nijieleze niko na potential gani ndani yangu ya kuwashawishi wanikubali niwe kwenye team yao pale hotel, mzee nikajimwaga niwezavyo. Ilikuwa ni non official interview panel ambayo kila mmoja aliniuliza masuala kadhaa apendavyo.

Baada ya kumaliza mm nikaamuriwa kutoka nje ya chumba cha ofisi, baadae nikaambiwa nirudi ndani na nikajibiwa kulingana na taaluma yako hapa hatuna kazi ya kukupa ila tuna nafasi moja ya mhuduma yaani waiter ambae anatakiwa ahudumie restaurent, basi kwa kuwa nina njaa nikasema sawa hiyo hiyo inafawa kwangu. Nikafanya haraka kuuliza mshahara yule mama ananiambia laki sabiini, aaaaa nilichoka nikajiuliza ina maana hawa watu ninaowaona wanajiremba na kujimwambafai ndio mshahara wanaolipwa huu, sikupata jibu hadi leo. Basi nilichofanya nikumuaomba yule P.O anipatie karatasi zangu na kusepa zangu kwetu kutafakari nn cha kufanya. Hizi kazi za kuajiriwa sizitamani hata kidogo ila basi tuu.

Ila wakati natoka kuna dada mmoja alinifata akanambia hukupaswa kukataa, yule alikuwa anakuangalia tuu utakavyo respond kwa kima kile, ila tayari tulishajadiliana wapi pakukuweka na ungetusaidia kwa fani na ujuzi ulo nao.

Mzee nilishakata shauri, hata nyuma sikugeuka. Nilihisi nimedharauliwa pakubwa. Ila kwa umri nilo nao na mafunzo niliyopitia hivi sasa nina ustahamilivu na ukomavu wa hali ya juu kuhimili dharau na majaribu makubwa kiasi ya watu kunishangaa na kustaajabu kwa nn niko nilivyo.

KISICHOKUUA KINAKUKOMAZA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo ya Chang'ombe hata mimi imeshanikuta, mwaka 2012. Baada ya kumaliza degree yangu Mlimani mwaka 2011 niliamua kutorudi kijijini kwetu ili nibaki dar kutafuta mishe ya kufanya. nikawa nakaa kwa binamu yangu maeneo ya kawe kwa bahati nzuri nilikuwa napatana sana na shemaeji yangu(mke wa huyo binamu yangu) basi nikawa napata msosi hapo na vihela vidogo vidogo sana kwa ajili ya vocha na vinauli vya daladala kwa ruti fupi fupi za hapa na pale kutembeza vyeti kwenye maofisi.

Siku moja kama zari vile, kweney gazeti kama sio Alasiri ni Mwanaspot nikaona kipande cha Tangazo la kazi mshahara 300,000/= Elimu kuanzia drs la saba hadi degree(wale jamaa wana ujasiri), basi nikachukua namba ya simu nikaipiga, wakanielekeza kwamba kesho yake niende Chang'ombe Maduka mawili. nikamshtua na jamaa yangu ambaye tulikuwa tumemaliza naye chuo na jirani zetu wawili wa darasa la saba tukatia timu pale Chang'ombe(sifa zote tunazo kuanzia wa darasa ala saba hadi sisi wa chuo kikuu).

Tulipofika pale tukakuta kuna watu wengine wengi wengi tu wa kiume na wa kike, tukaambiwa tusubiri interview basi baada ya muda tukaitwa kila mmoja kwa zamu yake kwenda kwa boss, ukifika kule huombwi vyeti wala nini unahojiwa tu vimaswali vya kitoto viwili vitatu unaambiwa ukasubiri majibu. Baada ya interview tukaambiwa wote tumefaulu hivyo kesho yake tuje kuripoti kazini, tuje tukiwa nadhifu na tuwe tumevaa tai. tukaagiziwa pia na barua za wadhamini na ya mwenyekiti wa mtaa. Shemeji yangu akanisapoti hela ya kuclear hayo mahitaji yote nikayapata.

Asubuhi na mapema kesho yake tukawasili pale ofisini, bwanaweee kikafunguliwa chumba kina beseni za kufa mtu,majag, sahani na kila aina ya plastic products unayoijua. Tunajiuliza hiki ni nini kinaendelea hapa?, mara tukagawanywa watatu watatu tukapewa viongozi wa kutupeleka field(Kumbuka hapo tunaajiriwa kama field oficcers, hahahaaaa!! maisha haya), tukabebeshwa mabeseni tuakaambiwa mazungumzo mengine ni hapo tutakaporudi kutoka field, sitokaa niisahau hii siku. Mwili ulipata baridi, miguu ikatetemeka hapo nje ya geti tu nikamrudishia yule kiongozi mabeseni yake nikamwabia hii sio field officer niliyokuwa naitaka mimi akajaribu kuwa mbishi hapo na kunishawishi lkn sikutaka katu kumsikiliza nikapiga chini huo mpango na wale jamaa zangu wote nao kila mmoja alikataa tukarudi zetu home tukiwa hatutazamani machoni. Daaaaah! maisha ni safari hadi sasa tunasonga. Sitaisahau Chang'ombe
 
Nikisoma michango ya waungwana humu, huwa siwezi kujizuia kucheka. Kweli dunia shujaa. Yaani mtu na degree yako unabebeshwa mabeseni na huku unajengwa ari kuwa ndio maisha, hupaswi kuyaogopa ilhal mabeseni hayo sio ya kwako kabisa.

Mifumo ya utawala na uchumi isiyosimamiwa vyema ndio mara zote huleta matatizo haya kwa vijana wanaohitaji ajira.

Mungu katuumba tofauti kwa maana na sababu zake, kutuweka tofauti ana hekma yake, sio kweli sote tutakuwa matajiri lakini sio poa kuwa na degree halafu ubebeshwe mabeseni ambayo pia sio ya kwako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah imebidi nisome visa vya wenzangu nicheke. Ilikuta miaka kadhaa iliyopita wakati nimemaliza six nimetafuta sana tempo shule za sekondari nikakosa nikaamua kutulia kitaa nawaza ntatokaje huku nikisubiri matokeo ya mitihani. Ndipo nikakuta tangazo classified (matangazo madogo madogo, yanakuwa mengi kwenye page 1) kwenye gazeti sikumbuki jina.

Nikapiga simu ikapokelewa nikaambiwa kesho niende ofisini Magomeni kati ya Mapipa au Usalama ila ni maeneo hayo hayo karibu na Magomeni Mikumi. Mimi huwa sikeep bad memories in details. Kufika nikaonana na vijana wenzangu wakaka na wadada. Picha linaanza unapewa mtihani wa interview vimaswali na hesabu za kiboya wakati mi ndo nimetoka kupiga EGM yangu a few days ago.

After kama nusu saa hivi majibu yakatoka. Tukawa tunaitwa mmoja mmoja....mtu akiingia huko ndani ofisini kwa boss harudi. Zamu yangu ikafika. Lakini wakati wote nilikua nasikia kelele za watu kama vile wanapasha misuli au wanacheza karate nyuma ya nyumba huko. Nikajiuliza maswali bila majibu, watu hao wanafanya nini.

Nilipofika ndani kwa boss akaniambia hongera sana umefaulu kwa 95% na hivyo kazi umepata. Pembeni kuja jamaa kachoka choka....shati limepauka, kiatu kimelika soli kinyama na suruali yake nyeusi na bonge la tai. Akaambiwa utaenda naye huyu (mimi) umpe maelekezo leo siku nzima nami nikaambiwa niwe msikivu kwa mkufunzi wangu. Tukatoka, hapo sijahoji chochote zaidi ya kuitikia maelekezo. Jamaa akanitoa kupitia mlango mwingine nikakuta majagi, mabeseni, viti vya kukaa watoto ku poop, makontena na vikorokoro vingine vya plastic. Jamaa akabeba kadhaa akanipa namimi nibebe viti vile vya watoto...safari ikaanza. Akaniambia tunaenda Mabibo.

Tukapanda daladala mpaka Mabibo. Tulivyoshuka tukaanza kuingia mtaani, nakumbuka ni maeneo yale ya chuo cha NIT. Tukazunguka hukoo mitaani tunauza, tukiona watu wamekaa hasa wamama tunawaface. Moyoni nlikua nawaza tu nsije kutana na mtu anayenifahamu....aibu yake ingekuwa kubwa sana. Sijui ningeificha wapi sura yangu. Maana nimechoka, nna njaa, nimeloa jasho, kiatu kina vumbi balaa. Yule jamaa alinitembeza kutwa hatukula kitu. Tuliuza vitu vichache tu.

Tukapanda daladala tukarudi ofisini jioni saa 11. Wakaniambia hongera sana mmefanya kazi nzuri na mwanzo mzuri. Inabidi uende nyumbani uje kesho, ila kesho uje na tai.

Nilivyotoka pale nikasepa home nikaapa kutorudia tena. Kuna mwana tulikua naye, tuliexchange namba wakati tunasubiri majibu ya usaili yeye walienda Kinondoni huko. Jioni tulivyopigiana simu tukacheka sana. Jamaa alicheka sana kwenye simu dah.

Mwaka jana nikiwa na majukumu yangu kikazi nikapita ile mitaa ya NIT mtaa ule ule tulioanza kutembeza vile vitu, nilivyopark tu na kushuka niliduwaa kama sekunde 30 hivi nikasikitika peke yangu.

Mungu ni mwema, maisha yanasonga.
Lakini wakati wote nilikua nasikia kelele za watu kama vile wanapasha misuli au wanacheza karate nyuma ya nyumba huko. Nikajiuliza maswali bila majibu, watu hao wanafanya nin.......hapa pamenichekesha sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakumbuka mwaka flan nlitoka kijijini na kuja Dar kutafuta mishe nlipofika nikawa natafuta pa kuanzia mala nikaona tangazo AJIRA MSIMU WA SABASABA nikachukua namba kupiga nikaambiwa nitafute barua za wadhamini mbili nipeleke maeneo ya waires


Siku iliyofata nikapanda gari hadi waires secondary mala nikacimama na kupiga cm mala upande wa pili mtu kasimama barazani akinijta njoo nikavuka na kuingia ndani nikawakuta wadada na vijana wakiimba na kupayuka kama machizi mala yule kiongozi akaniita na kukagua zile barua then akaniambia unataka ajira ya muda mfupi or mlefu nikamjibu mlefu basi akasema hupo tayali kwa interview nikasema ndiyo akanambia basi nakupa kiongozi punde ikatolewa michupa ya chai maglass mala tukapangwa makundi watu watatu watatu

Nikasema ngoja nisiondoke nibaki nione mala yule kiongozi akatuambia jana walikwenda ubungo asubuhi hadi jioni wameuza chupa moja tu so mmoja akasema twende pugu mnadani basi tukawa tunaelekea huko tukapanda gari tandika za gongolamboto mala tukashuka gongolamboto na kupanda daradara za pugu mnadani punde tukafika nakumbuka ilikuwa mwezi huu maana waislam walikuwa kweny mfungo tulitembea tulizunguka humo mnadani jamaa yule kiongozi mbishi mtu anamwambia sinunui anaenda then anarudi tena pale pale matusi mnakuta watu toka mwanza washauza ng'ombe wanakunywa pombe wanawaita awanunui wanawamwagia matusi
Kufika mishale ya saa kumi me hapo njaa inauma nina nauli tu mala bi mkubwa akanipigia cm vip mwanangu nikamwambia kumbe kazi yenyew kuzunguka na vyombo kuuza nilitaka niondoke zangu ila nimeona nije nizunguke nao na nijue maisha na nipate cha kusimulia akanambia basi nakutumia elfu kumi toa ununue ata soda

Ilipofika saa 11 tulifanikiwa kuuza vtu vyote chupa za chai glass hotpot kila kitu yule jamaa kiongozi wetu ndo anashika hera tukarudi kituoni gongolamboto yule jamaa akatununulia machungwa tukapanda gari za tandika tukarudi mala yule bosi akaja wakaingia ofisini na yule kiongozi wakaongea then wakaniita jamaa akaanza kunisifia kuwa nachapa kazi uenda mda si mlefu watanipa umenejaa akanipa mkono akanipongeza akasema ananitakia usiku mwema kesho niwahi

Hapo ndo nkawatolea uvivu yaani nikakuuzie mavyombo alafu usinipe ata nauli nikawasha moto mle ofisini kuna vibinti vilikuwa vinafutulu vikasema leo mmeyakanyaga nikaanza kuongea jamaaa akatoa buku mbili nikasema thubutuuu ndo wakatoa elfu nane wakanipa wakaniambia kesho nisirudi nlipotoka nje nikarudi kudai barua zangu za wadhamin wakanipa nikapanda gari za buza sikurudi tena
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Back
Top Bottom