Sithaminiwi....

Sithaminiwi....

BG baba

Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
42
Reaction score
4
Niliposhindwa kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano dada yangu (mwalimu) na kakangu (businessman kimataifa) walinitafutia chuo cha MIFUGO NA KILIMO Iringa,nilipata nafasi hiyo na wakanipeleka. Lakin tangu nifike huko mwezi wa kumi 2012,ndugu zangu hawanipigii hata simu mpaka kuna wakati niliugua niliwajuza kwa sms sikuona hata missed call,nikaamua kupiga kwa dada matokeo yake simu ilipokelewa na rafii yake akaniambia ""usimsumbue dada yako ana majukumu nengi''.

Nikasaidiwa na wanafunzi wenzangu. Mwez wa 12 tukafunga tarehe 12, ikiwa niliwajuza pia kwa hili wiki mbili kabla,nikaamza kuomba nauli hawakupiga tena mpaka siku ya kufunga tukafukuzwa shuleni twende makwetu nikaondoka.

Mpaka sasa sijaona simu yao kupigiwa na nina wiki moja sijaenda shulenI nikipiga na kuuma sms hawajibu.

Nifanyeje jamani INANIUMA SANA, naomben ushauri
 
kuna mahali umeharibu hasa ulipofeli ndipo ulipoharibu kabisa,walichokitegemea kwako sicho walichokipata sasa wamekata tamaa hata huko mifugo walipokupeleka shukuru mungu.
angalia huyu mwenzako hapa nae alifeli mpaka veta tukampeleka chuo cha ualimu matokeo yake ni hay je!utamthamini mtu huyu kama ni wewe,kumbuka dada yako ,kaka yako wanamajukumu kukusomesha its just extra will .
https://www.jamiiforums.com/mahusia...liki-ndio-kitendawili-kingine.html?highlight=
 
kuna mahali umeharibu hasa ulipofeli ndipo ulipoharibu kabisa,walichokitegemea kwako sicho walichokipata sasa wamekata tamaa hata huko mifugo walipokupeleka shukuru mungu.

Mkuu hata kama kufail shule siyo mwisho na isiwe sababu ya kumu ignore mtu na kumfanyia hivyo anavyofanyiwa unless kuna kitu cha ziada kaficha. Wangapi wamefail shule tena zaidi ya mara moja lakini kwa msaada na back up ya ndugu na jamaa leo hii watu wakubwa serikalini.
Tatizo watu uwa tuna tabia ya kuweka expectations sana katika mtu na zikienda ndivyo sivyo basi tunakuwa discouraged naye lakini kumbuka kama wewe ulisoma na masomo yakawa tambalale si lazima na mwingine awe kama wewe kwakuwa binadamu hatufanani ndiyo maana kuna maji ya kunde, kuna mweusi kuna mnene, kuna mwembamba, kuna anayefaulu kwa kusoma kidogo na kuna anayesoma sana na hafaulu.
Ndugu yangu kama huna ulilowakosea zaidi ya kufail, basi omba Mungu kazana sana siku moja ipo milango itafunguliwa.
 
Ndugu yangu,yawezekana,lakini nina dvn 3 ya 25,na ilivyokuwa nilipata nafasi ya kwenda jesh na nyingine kwenda ualimu wakanikataza na wakadai niwaskilze je ni kwel m ninakosa?
 
ndugu yangu,yawezekana,lakini nina dvn 3 ya 25,na ilivyokuwa nilipata nafasi ya kwenda jesh na nyingine kwenda ualimu wakanikataza na wakadai niwaskilze je ni kwel m ninakosa?

tungesikiliza na upande wa pili tungejua tatizo lilipo pia.ninachoweza sema ni kwamba u didint meet thier expectation,mfano walitaka either upate angalau div 1,2 upate mkopo usiwategemee nahisi hilo ila kumbuka wanakupenda sana majukumu na utafutaji wa pesa ulivyomguu na umaskini na tegemezi kuwa wengi ndio tatizo .umaskini tu ndio uliochangia
 
Hebu kuwa muwazi! Dada&kaka hawawezi kukutenga bila tatizo lazima kuna ki2 umefanya, labda umebadilika kitabia, KUWA MUWAZI UPATE MSAADA ZAIDI!
 
Wewe nahisi una matatizo na hao ndugu zako umewasumbua sana kama wameweza kukutafutia chun Kwanini wasikujali kwahayo mengine?hebu jirekebishe nawewe ufanye sehemu yako na ujitambue unawajibika kwa maisha yako mwenyewe siyo kupenda tu lawama kwa ndugu wala hawawajibiki kukaa wanakusukuma kusoma kumbuka nao wana watoto wao hebu uache na lawama zako hazına msingi unatia aibu tu hapa.jithamini kwanza wewe mwenyewe ndıo nawengine watafanya
 
Hayatuhusu. Peleka umbeya wako kwa ndugu zako. Toa mada zenye kueleweka. Sasa ndio umeandika nini hapo juu? umenikera sana.
 
kuna mahali umeharibu hasa ulipofeli ndipo ulipoharibu kabisa,walichokitegemea kwako sicho walichokipata sasa wamekata tamaa hata huko mifugo walipokupeleka shukuru mungu.
angalia huyu mwenzako hapa nae alifeli mpaka veta tukampeleka chuo cha ualimu matokeo yake ni hay je!utamthamini mtu huyu kama ni wewe,kumbuka dada yako ,kaka yako wanamajukumu kukusomesha its just extra will .
https://www.jamiiforums.com/mahusia...liki-ndio-kitendawili-kingine.html?highlight=

Hapa rafiki inabidi tutofautiane tu...
Kufeli shule si ndio kufeli maisha...Ndugu bado wana haki ya kumsaidia huyu rafiki,huyu ndugu kafeli lakini bado kaona kuna umuhimu wa kuendelea na shule hata kama ni ya mifugo.
Kwa namna aliyoelezea ni kama vile nduguze wamemsusa, ingawa hatujaelezwa sababu gani haswa imepelekea yote hayo.

Binafsi ninahisi yafuatayo;
1. Nduguze wanamuona ni kama mzigo usiobebeka na ndio maana wakaamua kwenda kumtupa mbali na nyumbani. Hii ni kawaida kwa familia zetu, mtoto akiwa mtukutu wazazi au ndugu husikika wakisema, "Mpelekeni shule ya bweni au mbali na nyumbani atanyooka tu".

2. Kuna uwezekano ni kweli dada yako hana kipato cha kutosheleza zaidi ya karo ya shule. Ualimu haulipi sana hapa nchini sote twafahamu mshahara wao.

Ushauri:
1. Jitahidi hali iliyopo isiathiri maendeleo yako ya kitaaluma maana kwa hali ilivyo elimu unayoipata ndio urithi wako pekee mwema.

2. Nyakati za likizo hakikisha unatafuta kazi ndogo ndogo hata vibarua vya kumenya viazi vya chips.

3. Jaribu kuongea na ndugu wengine ili wakusaidie mawazo na mengineyo.
 
Pole mwaya, haya mambo yapo ktika families...

Elimu yako ndo mkombozi wako, jitahidi usome tu mambo yatakuwa poa...

Lakini pia uchunguze tatizo lililopo!!!
 
Kwa ulivyoiweka unaonekana huna MAKOSA...Lakini kama wameweza kukutafutia shule i mean chuo nashindwa kuelewa kwa nini wasikujali?..by the way hebu kama itawezekana fanya mpango ukaonane nao 'physically'...na ukipata majibu yao 'mdomo kwa mdomo' basi rudi hapa jamvini tujadili...however, i still believe there's something wrong on your side rather than theirs.....
 
ndugu mtoa mada naomba ufungue masikio yako ya ndani usikie haya toka kwangu.

Nikuite mwanangu, sema ukweli je huna kosa ulilowafanyia ndugu zako???.....................lkn pia kosa lako halibadili hadhi yako ya kuwa mtu na binadamu wala halikufanyi thamani yako ya kuwa mtu ishuke.

yawezekana pi kuna mgogoro wa kifamilia ulio wa kimaslahi zaidi juu ya kuhudumiwa wewe hasa kielimu. mara nyingi sana hali hii itokeapo ndugu hugombana na kushindwa kufikia compromise matokeo yake ni haya ugomvi wa simba ziumiazo ni nyasi.

istoshe kwenye maisha kuna muda wa kupita pagumu, hii hata uwe tajiri ama maskini lazima upitie ugumu fulani na ugumu huu hauangallii wewe ni nani ingawa hutofautian kati ya mtu mmoja na mwingine. yawezekana kabisa wewe unapaona pagumu hapo unapopita ila kuna mwingine ukimwambia ataona kama ni rahisi sana kwani anapita pagumu kuliko wewe.

labda nikupe mfano huu:..............kuna mwanafunzi wangu mmoja alikuwa anaish mwanza anasoma mkoa mwingine. siku moja akiwa shule pasipo sisi kujua wazazi wake wote walifariki pamoja na wadogo zake kwa kuingiliwa na kijiji kizima kwa tuhuma za wizi mikoa hiyo ya kanda ya ziwa. wote waliuwawa na nyumba ikachomwa moto. kiasi kwamba hata nguo zake hazikubakia.

jambo la ajabu hakuna aliyemtafuta huku shule alikokuwa anasoma so baada ya wiki licha ya kwamba kwenye tv tuliona ila ndipo tulipojua kwamba amepata msiba mzito sana tena kwa simu ilyopigwa na Dc wao shulen. imagine huyu kijana amepitishwa pagumu kiasi gani. na je wafikiri yeye na wewe yupi ambaye anatumani japo dogo.

sisemi kwamba lako siyo tatizo ila kiukweli ni dogo sana sana, kama wamesitisha kukusomesha just nenda shule andika barua omba shule ikudhamini usome kwa kipengele kwamba nitakuwa natafuta ada nilipe.

kuliko kufikiri kwann huthaminiwi ungefikiri nitapata wapi ada ya chuo nimalize. leta bandiko uombe msada wa ada hapa jf uone kama hutalipiwa tena hadi umalize shule. usiendelee kulalamika jipange kiume mwanangu.

MAISHA YANA CHANGAMTO NYINGI ILA NI AKILI NA NIDHAMU TU YA KUFIKIRI KWA UTASHI ITAKAYO KUSAIDIA, HATA ULALAMIKE MABANDIKO MIA HUNA NIDHAM YA UTASH WA KUFIKIRI HUWEZ KUTOKA ULIPO.

wasalaam,
Mwl @gfsnwin!!!
 
kabla ya kwenda chuo ulikua unaishi na nani, na baada ya kufunga chuo umeenda wapi, vumilia ushukuru maana vyuo vya hivyo ni ajira , after gud two years utaanza pokea matunda, maisha magumu usiwalaumu sana shukuru wamekulipia ada
 
tungesikiliza na upande wa pili tungejua tatizo lilipo pia.ninachoweza sema ni kwamba u didint meet thier expectation,mfano walitaka either upate angalau div 1,2 upate mkopo usiwategemee nahisi hilo ila kumbuka wanakupenda sana majukumu na utafutaji wa pesa ulivyomguu na umaskini na tegemezi kuwa wengi ndio tatizo .umaskini tu ndio uliochangia
lakini wao sio mungu
 
kuna mahali umeharibu hasa ulipofeli ndipo ulipoharibu kabisa,walichokitegemea kwako sicho walichokipata sasa wamekata tamaa hata huko mifugo walipokupeleka shukuru mungu.

Mkuu hata kama kufail shule siyo mwisho na isiwe sababu ya kumu ignore mtu na kumfanyia hivyo anavyofanyiwa unless kuna kitu cha ziada kaficha. Wangapi wamefail shule tena zaidi ya mara moja lakini kwa msaada na back up ya ndugu na jamaa leo hii watu wakubwa serikalini.
Tatizo watu uwa tuna tabia ya kuweka expectations sana katika mtu na zikienda ndivyo sivyo basi tunakuwa discouraged naye lakini kumbuka kama wewe ulisoma na masomo yakawa tambalale si lazima na mwingine awe kama wewe kwakuwa binadamu hatufanani ndiyo maana kuna maji ya kunde, kuna mweusi kuna mnene, kuna mwembamba, kuna anayefaulu kwa kusoma kidogo na kuna anayesoma sana na hafaulu.
Ndugu yangu kama huna ulilowakosea zaidi ya kufail, basi omba Mungu kazana sana siku moja ipo milango itafunguliwa.
 
Niliposhindwa kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano dada yangu (mwalimu) na kakangu (businessman kimataifa) walinitafutia chuo cha MIFUGO NA KILIMO Iringa,nilipata nafasi hiyo na wakanipeleka. Lakin tangu nifike huko mwezi wa kumi 2012,ndugu zangu hawanipigii hata simu mpaka kuna wakati niliugua niliwajuza kwa sms sikuona hata missed call,nikaamua kupiga kwa dada matokeo yake simu ilipokelewa na rafii yake akaniambia ""usimsumbue dada yako ana majukumu nengi''.

Nikasaidiwa na wanafunzi wenzangu. Mwez wa 12 tukafunga tarehe 12, ikiwa niliwajuza pia kwa hili wiki mbili kabla,nikaamza kuomba nauli hawakupiga tena mpaka siku ya kufunga tukafukuzwa shuleni twende makwetu nikaondoka.

Mpaka sasa sijaona simu yao kupigiwa na nina wiki moja sijaenda shulenI nikipiga na kuuma sms hawajibu.

Nifanyeje jamani INANIUMA SANA, naomben ushauri

Usiwe na wasiwasi ndo hali ya Dunia. Kutesa kwa zamu,


Sent from my Nokia 8310 using Tapatalk
 
Ningekuwa mimi ningeichukkulia hio kama changamoto na namna ya kuwa na maisha yangu binafsi, as far as wanakulipia ada the rest ni anasa tu...soma kwa hasira sana ndipo utawashinda, we have the same background na leo hii unaonekana mtu akti ya watu
 
Back
Top Bottom