Habari zenu,
Poleni na majukumu pamoja na pilika za siasa. Mimi ni mama mwenye mume na familia kiumri ni miaka 38. Ni mfatiliaji mzuri wa habari za huku leo nami nineona niwape ya kwangu. Kifupi nimechoshwa na mapenzi, sitamani mapenzi, nimekinai sitaki hata kusikia habari zake.
Mbaya zaidi siku zinavozidi kwenda sitaki hata kuhudhuria harusi au ndoa. Nikiona tukio hilo huwa linanitesa sana na hii ni baada ya kuona ndoa nyingi hazina amani, wanandoa wengi wanaishi maisha yasio na amani.
Nilibahatika kuchaguliwa nafasi ya malezi kanisani ambapo ndoa nyingi zilizokuwa zikija kuleta malalamiko kanisan nikiitwa na mch kutoa ushauri. Kwakweli nilikua naumia sana. Sikutamani hayo yanikute nilijua iwapo yatanitokea yatanitesa sana.
Sasa yamenikuta na yananitesa sana, nashindwa kujishauri japo kwa wengine nilifanikiwa kiasi fulan. Ama kweli mganga hajigangi. Kupitia kusikiliza ndoa nyingi zenye maumivu nilijitahidi sana kutimiza wajibu wangu kama mama, nilimpenda mume wangu, nilimjali sana, mara nyingi nilimsisitiza awe mwaminifu nami nilijitahi pia kuwa mwaminifu mume wangu si mlevi wa pombe ila ana kaulevi kake.
Jaman sikuamini kilichotokea, alitembea na mtoto wa kaka angu bila mimi kujua akatembea na hg na kumpa mimba. Siku niliyomfuma housegirl akakiri na kuniambia hata mtoto wa kaka yangu ametembea na baba ndio maana walikua hawapendani. Housegirl alirudi kwao na amejifungua. Mtoto wa kaka nae alirudi kwa mama ake nilimchukua baada ya baba ake kufariki. Ni zaidi ya miezi sita imepita nashindwa kumsamehe huyu mume, simtaman kabisa.
Nipo kwa kulea watoto ila ameniumiza sana. Sitaki kabisa kushiriki nae tendo la ndoa silitaman kabisa. Mara nyingi nilisikia taarifa mbaya za mume wangu nilipuuza hata nilipojaribu kumuuliza alikua mkali sana. Baada ya fumanizi hili yote niliowahi kusikia kumbe yalikua yana ukweli kabisa.
Nimeumia sana, sana. Nimemwambia na kumpa uhuru andelee tu na wao anaona wanamfaa mimi tena basi. Yaan ndoa hizi zina mambo. Polen wanandoa wote mnaopita katika kipindi kigumu. Mwenzenu nimeinua mikono.
Sijui kwanini ndoa badala ziwe na amani zinakua jehanam ya dunia. Mh!!
Poleni na majukumu pamoja na pilika za siasa. Mimi ni mama mwenye mume na familia kiumri ni miaka 38. Ni mfatiliaji mzuri wa habari za huku leo nami nineona niwape ya kwangu. Kifupi nimechoshwa na mapenzi, sitamani mapenzi, nimekinai sitaki hata kusikia habari zake.
Mbaya zaidi siku zinavozidi kwenda sitaki hata kuhudhuria harusi au ndoa. Nikiona tukio hilo huwa linanitesa sana na hii ni baada ya kuona ndoa nyingi hazina amani, wanandoa wengi wanaishi maisha yasio na amani.
Nilibahatika kuchaguliwa nafasi ya malezi kanisani ambapo ndoa nyingi zilizokuwa zikija kuleta malalamiko kanisan nikiitwa na mch kutoa ushauri. Kwakweli nilikua naumia sana. Sikutamani hayo yanikute nilijua iwapo yatanitokea yatanitesa sana.
Sasa yamenikuta na yananitesa sana, nashindwa kujishauri japo kwa wengine nilifanikiwa kiasi fulan. Ama kweli mganga hajigangi. Kupitia kusikiliza ndoa nyingi zenye maumivu nilijitahidi sana kutimiza wajibu wangu kama mama, nilimpenda mume wangu, nilimjali sana, mara nyingi nilimsisitiza awe mwaminifu nami nilijitahi pia kuwa mwaminifu mume wangu si mlevi wa pombe ila ana kaulevi kake.
Jaman sikuamini kilichotokea, alitembea na mtoto wa kaka angu bila mimi kujua akatembea na hg na kumpa mimba. Siku niliyomfuma housegirl akakiri na kuniambia hata mtoto wa kaka yangu ametembea na baba ndio maana walikua hawapendani. Housegirl alirudi kwao na amejifungua. Mtoto wa kaka nae alirudi kwa mama ake nilimchukua baada ya baba ake kufariki. Ni zaidi ya miezi sita imepita nashindwa kumsamehe huyu mume, simtaman kabisa.
Nipo kwa kulea watoto ila ameniumiza sana. Sitaki kabisa kushiriki nae tendo la ndoa silitaman kabisa. Mara nyingi nilisikia taarifa mbaya za mume wangu nilipuuza hata nilipojaribu kumuuliza alikua mkali sana. Baada ya fumanizi hili yote niliowahi kusikia kumbe yalikua yana ukweli kabisa.
Nimeumia sana, sana. Nimemwambia na kumpa uhuru andelee tu na wao anaona wanamfaa mimi tena basi. Yaan ndoa hizi zina mambo. Polen wanandoa wote mnaopita katika kipindi kigumu. Mwenzenu nimeinua mikono.
Sijui kwanini ndoa badala ziwe na amani zinakua jehanam ya dunia. Mh!!