Leo kiherehere cha kujifanya msomi civilazed mwenye kupenda haki sawa kimeniisha nilivyompeleka mwanangu wa siku 42 kliniki peke yangu bila kuwa na mama yake ndani ya chumba cha kliniki kwa kumuacha kwenye gari eti alikuwa ana kizunguzungu.
Nimejikuta nimepoteza confidence/kujiamini na aibu, kwenye ile foreni ya kupima Uzito nilikuwa peke yangu mwanaume mwenye ndevu, kati ya wanawake karibia 100, unasikia sauti zao mtoto usimfanye hivi, mbebe vile kila moja anakuangalia wewe loh,
Sasa pale kwenye benchi ya kusubiria chanjo kuna stori zao wanazopiga wanazijua wenyewe mimi nimeshindwa kabisa kuchangia chochochote, nilikuwa ' odd man out' wanacheka mimi natabasamu tu sina hata la kuongea, yale masaa mawili kwangu yamekuwa kama siku nzima.
Hivi kwanini wanaumme wa ki Tanzania hawana utamaduni wa kusindikiza wake zao au ni sababu kama hii ya kwangu, nilidhani nitakutana na wanaumme wenzangu lakini wapi kumbe wale wanaume niliona kwa mbali walikuwa wahudumu wa pale sio wazazi
Nimejikuta nimepoteza confidence/kujiamini na aibu, kwenye ile foreni ya kupima Uzito nilikuwa peke yangu mwanaume mwenye ndevu, kati ya wanawake karibia 100, unasikia sauti zao mtoto usimfanye hivi, mbebe vile kila moja anakuangalia wewe loh,
Sasa pale kwenye benchi ya kusubiria chanjo kuna stori zao wanazopiga wanazijua wenyewe mimi nimeshindwa kabisa kuchangia chochochote, nilikuwa ' odd man out' wanacheka mimi natabasamu tu sina hata la kuongea, yale masaa mawili kwangu yamekuwa kama siku nzima.
Hivi kwanini wanaumme wa ki Tanzania hawana utamaduni wa kusindikiza wake zao au ni sababu kama hii ya kwangu, nilidhani nitakutana na wanaumme wenzangu lakini wapi kumbe wale wanaume niliona kwa mbali walikuwa wahudumu wa pale sio wazazi