BlackBerry
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 1,839
- 956
Ndio maana wadada kama sie tunaojua kukamatia huwa tunawalipizia wote wanaoonewa kama huyu wa jamaa. nahakikisha lazima unarudi kunitafuta utake usitake, tena vichwa ngumu mie ndio nawapenda sana hawaPamoja na kwamba issue yenyewe inawakera sana akina mama, lakini hili suala huwatokea sana wanaume. Kwa uzoefu wangu wa kuanzia enzi zile tunajifunza kujenga vijumba vya makuti ...na kujifanya baba na mama....haya mambo ni kawaida sana kutokea. Labda vijana wa dot com kama hawajawahi kusikia!! Ila huo ni ukweli na utabaki kuwa ukweli....
Ushauri wangu ni kwamba Apolinary...kaa mbali sana na huyo binti...ili upate nafasi ya kuona kama hisia kwake zinaweza kurudi. Kama hazitarudi basi usilazimishe kwa sababu utakuja kumuumiza sana huyo dada. Labda kwa sasa jitahidi kumuacha taratibu ili upunguze dozi ya maumivu.
Ukweli wa hili ni kwamba wanaume tunaongozwa na tamaa na ni mara chache sana kumpenda mwanamke...Ila tukipenda basi tena...tunakuwa zaidi ya wehu!