Minjingu Jingu
Senior Member
- Nov 2, 2023
- 116
- 480
Hili suala nilikuwa naambiwa lakini jana nimeshuhudia. Kwa masikio yangu nimemsikia jamaa akiniponda. Sijamkosea lolote maskini. Mimi nimekaa ofisini kwao nikimsubiri Boss wao. Akaja dada mmoja akauliza kama nimesikilizwa, nikamjibu ndiyo lakini ni kama hakuridhika akaona kuwa nilipaswa kuwa attended kwa uharaka sana.
Akaenda kuuliza akifoka kwa wafanyakazi wengine kuwa mbona sijawa attended sijawekewa na kinywaji. (Huyu dada ananifahamu nina shughuli gani na boss wao, mimi nikifika huwa nakaa tu sehemu wanayokaa watanzania wenzangu na kiuhalisia napaswa niwe nakaa VIP) so akawa anawasema kwa nini hawajanipeleka VIP ndo secretary akasema nilimwambia tu hata pale panatosha asiwe na shaka.
Yule dada alinifuata this time akiomba kwa unyenyekevu sana kuwa nihamie kule VIP si vyema mimi kusubiri hapa nilipo. Nikajisikia vibaya kumkatalia kutokana na lugha aliyotumia. Basi nikaamka kwenda. Nikiwa kule kumbe wale jamaa ofisi ya pembeni hawakujua kama nitapita pale kwao ndo nikamsikia jamaa anasema.
"Boss anatulalamikia sababu ya yule Jamaa bitozi white kama demu" nikakohoa ili asiendelee kuongea maneno mengine ajue napita, alishtuka.
Sikuelewa why aniite white kama demu. Mimi sijichubui, sipaki lotion au cream. Napaka tu vaselline au mafuta ya nani. Why ameonesha chuki kwangu na hali sijamtukana, sijamdharau wala nini? Nikakumbuka niliwahi kuwa na demu mmoja alikuwa ananiambia ananipenda sana isipokuwa anakosa amani kutembea nami sababu namfunika..... Sikuwa naelewa. Baadaye akaja akasema anamaanisha hii rangi yangu ya mtume inampa shida, tulikuja achana. Cha ajabu aliolewa na baadaye akawa ananifuata nimpatie mtoto. Ili apate mtoto mweupe. Sikuona kama ni jambo jema kwa kweli.
Hili tatizo sielewi nini chanzo, binafsi mimi napenda mwanamke rangi yoyote ile huwa rangi si tatizo kwangu awe tu mzuri na mwenye kuvutia. sibagui sana rangi. nadhani tusifikie hatua ya kubaguana kwa sababu ya rangi. si wanaume wala wanawake. Mungu anajua mwenyewe why alitupa rangi tofaut tofaut.
Rangi nyeupe ni ya wote tu, angalia wazungu, wachina, waarabu, wahindi n.k na kuwa mweusi siyo ndo kuwa mwanaume au mwafrika sana.
Akaenda kuuliza akifoka kwa wafanyakazi wengine kuwa mbona sijawa attended sijawekewa na kinywaji. (Huyu dada ananifahamu nina shughuli gani na boss wao, mimi nikifika huwa nakaa tu sehemu wanayokaa watanzania wenzangu na kiuhalisia napaswa niwe nakaa VIP) so akawa anawasema kwa nini hawajanipeleka VIP ndo secretary akasema nilimwambia tu hata pale panatosha asiwe na shaka.
Yule dada alinifuata this time akiomba kwa unyenyekevu sana kuwa nihamie kule VIP si vyema mimi kusubiri hapa nilipo. Nikajisikia vibaya kumkatalia kutokana na lugha aliyotumia. Basi nikaamka kwenda. Nikiwa kule kumbe wale jamaa ofisi ya pembeni hawakujua kama nitapita pale kwao ndo nikamsikia jamaa anasema.
"Boss anatulalamikia sababu ya yule Jamaa bitozi white kama demu" nikakohoa ili asiendelee kuongea maneno mengine ajue napita, alishtuka.
Sikuelewa why aniite white kama demu. Mimi sijichubui, sipaki lotion au cream. Napaka tu vaselline au mafuta ya nani. Why ameonesha chuki kwangu na hali sijamtukana, sijamdharau wala nini? Nikakumbuka niliwahi kuwa na demu mmoja alikuwa ananiambia ananipenda sana isipokuwa anakosa amani kutembea nami sababu namfunika..... Sikuwa naelewa. Baadaye akaja akasema anamaanisha hii rangi yangu ya mtume inampa shida, tulikuja achana. Cha ajabu aliolewa na baadaye akawa ananifuata nimpatie mtoto. Ili apate mtoto mweupe. Sikuona kama ni jambo jema kwa kweli.
Hili tatizo sielewi nini chanzo, binafsi mimi napenda mwanamke rangi yoyote ile huwa rangi si tatizo kwangu awe tu mzuri na mwenye kuvutia. sibagui sana rangi. nadhani tusifikie hatua ya kubaguana kwa sababu ya rangi. si wanaume wala wanawake. Mungu anajua mwenyewe why alitupa rangi tofaut tofaut.
Rangi nyeupe ni ya wote tu, angalia wazungu, wachina, waarabu, wahindi n.k na kuwa mweusi siyo ndo kuwa mwanaume au mwafrika sana.