Siri ya Mtungi - Imetulia !

Siri ya Mtungi - Imetulia !

Richard Mlangi

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2012
Posts
380
Reaction score
194
Nimeipenda sana hii tamthiliya ya Siri ya Mtungi.

Kwanza ina reflect uhalisia kuanzia jina la tamthiliya, uigizaji, mazingira, lugha mpaka majina ya characters. Majina kama vile Cheche, Mtungi, Tunu n.k. yanapendeza. Na sio kama kina bongo movies utasikia mara clifford, ericson, ford, clara, mark ambayo ni wenzetu wazungu.

Tamthiliya inapendeza inaporeflect uhalisia, na kuzingatia utamaduni wa sehemu husika.
Movie isiporeflect utamaduni inakuwa haina jipya la kuangalia.
Hii ndio siri ya kufanikiwa kwa Movie za ki-Nigeria na Latin America.

Nadhani ni fursa nzuri kwa kina bongo movie kuichukulia muvi hii kama darasa kwao.
 
image002.jpeg

The Shooting of the film
 
siri ya mtungi ni bonge la tamthilia.sio kama 69records
 
Inaoneshwa channel gani,muda gan na siku gani? nataman kuiangalia ila sijui ratiba yake.
 
hiv nani ndo producer wa hy siri ya mtungi na ni vhannel gan na mda gan huonyeshwa?
 
Imetumia gharama nyingi.. Karibu wote katika crew ya production wametoka nje na wamebobea kwenye tasnia ya filamu.
Na wasanii walikuwa wanatunzwa vizuri kuanzia vyakula,usafiri wa kuwatoa majumbani hadi location,kiukweli si tamthilia ya kuacha kuangalia.
 
hii tamthilia inafundisha sana,tena kwa rika zote ukiangalia na mtu yeyote lazma ajifunze kitu tena kinamuhusu kiundani.Duma na steve,nusura wameipamba tamthilia hii,nyingine ni HUKUMU YA TUNU,hii tamthilia ilikua ni funzo mno illionesha jinsi maradhi ya UKIMWI yanavyosambaa toka mjini hadi kijijini Tunu,Riyama,Devi,hidaya njaidi,Isike nao
ba BENCHMARK PRODUCTION watuwekee hii youtube mana kuna episode moja tu.
 
kuna jamaa alikua anakunja tonge la pilau n kurusha mdomoni kma buludoza......halafu anadai anamalaria sasa akiwa mzima v atakula kma kiboko
 
Imetumia gharama nyingi.. Karibu wote katika crew ya production wametoka nje na wamebobea kwenye tasnia ya filamu.
Na wasanii walikuwa wanatunzwa vizuri kuanzia vyakula,usafiri wa kuwatoa majumbani hadi location,kiukweli si tamthilia ya kuacha kuangalia.

Ni kwa msaada wa watu wa Marekani. Ilikuwa ni Mradi.
 
Aaaaargh yaani kumbe kuna watu weupe nyuma ya camera!!!!!

Mbona mnazidi kitupa sababu ya kiwasifia hawa watu, kila kizuri basi wameshiriki.
 
Aaaaargh yaani kumbe kuna watu weupe nyuma ya camera!!!!!

Mbona mnazidi kitupa sababu ya kiwasifia hawa watu, kila kizuri basi wameshiriki.
Wenzetu wako siriazi, kila kitu wanakiangalia kwa jicho la tatu.
 
BADO WAPO KWENYE MAANDALIZI YA MSIMU WA TATU,

KAA MKAO WA KUIONA, AWAMU HII WAMEKWENDA MBALI ZAIDI ,UTAPA PIA KUONA MAENEO KAMA VILE MABWEPANDE ,BUNJU NA PIA TUTAAMIA MAHAKAMANI KWA MUDA
 
Back
Top Bottom