Siri ya mshipa

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,781
Mshiba aka busha ni kitu cha kawaida sana Sehemu za pwani
Japo kuna mishipa mingine ambayo hutokana na kulogwa au ugonjwa lakini kwa watu wa mwambao kuna mishipa ya mapenzi

Yani ukiwa na shipa kubwa basi utawapata sana wanawake, lakini hii fasheni ilikuwa zamani sana, Wakati huo ukiwa na shipa basi mnapokuwa faraghani shipa hulala mapajani mwa mwanamke na kumpa ashki au raha ya ajabu

Wanaume wengi toka bara waliofika pwani wakati huo walirudi kwao na mabusha ya kutengeneza tena waliyanunua kwa bei kubwa, kwakuwa walipokuwa pwani walikosa wapenzi kwa kutokuwa na mshipa

Leo hii mshipa ni ugonjwa unaopigwa vita kwa juhudi kubwa lakini wazee wetu wa zamani hizo mshipa Ulikuwa dili kwenye mahaba

Kumbuka mshipa wa mahaba Ulikuwa haunuki,haupasuki, hautoi harufu mbaya wala haukuwa mzigo

Kama ilivyo leo kwa wanawake wanaotaka kuongeza makalio ili wavutie Wakati huo wanaume walishindana kuwa na mashipa

Imagine leo hii ingekuwaje kama hii fasheni ingerudi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom