Siri ya mchezo

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,605
696,697
1468079378626.jpg
kichwa cha habari na kwa mtazamo wa haraka utadhani ni michezo ya kuchangamsha mwili, michezo ya kubahatisha au michezo ya kushindana na kupata zawadi
Lakini hapa ni zaidi ya hicho kinachotupeleka kwenye fikra za kawaida..kwenye maisha kuna siri nyingi
Siri za mafanikio
Siri za ndoa
Siri za watu wa kaliba fulani
Siri za serikali nk nk
Siri zote hizi zinaangukia kwenye hali moja tu kwamba kuna jinsi ya kufanya kitu fulani ili uweze kufanikiwa vile inavyotakiwa
Ni kawaida sana kusikia watu wakisema kwa dhihaka kwamba mchezo huu hautaki hasira...! Ni kweli kabisa kwakuwa hata mchezo wa kupigana ukitanguliza tu hasira unadundwa
Wahenga walisema hasira hasara...! Hakuna hata mmoja ambaye alitanguliza hasira kisha akafanikiwa
...! Watu wamepoteza maisha fedha na hata mali kwa sababu tu walitanguliza hasira jabza na kukosa subra, hawa hawakujua siri ya mchezo
Tuna members wenzetu humu wamepigwa ban kwasababu tu ya kuruhusu hasira itawale kuliko hekima, busara na tafakuri
1468080298774.jpg
sekunde chache za kusubiri, dakika chache za kutafakari tena vingeweza kubatilisha maamuzi mengi ambayo yaliishia kwenye majuto
Tunakutana na changamoto nyingi tu za kimaisha, tunakwazwa sana na kuna wakati kwa kiwango kisichovumilika...na kuamua kuchukua hatua za kulipa kisasi bila tafakuri ya kina
Kumbuka hekima ya mtu busara ya mwanadamu huonekana wakati wa shida kubwa wakati wakutatizwa na kukwazwa, wakati wa kuguswa hisia zetu za ndani kabisa kwa namna ya kuumiza sana...maamuzi yako ya busara kwenye kilele cha ghadhabu ndio kipimo cha hekima yako katika maisha..na hii ndio siri kuu ya mchezo
 
Umenena vema Sana Mkuu wangu. Nimebakiwa na kazi ya kuitafakari hiyo picha na kuipatia majibu haswa umemaanisha mini kuiweka ndani ya Uzi huu. Hasira imewakilishwa na hicho kiumbe kinachotisha au huyo binadamu anayenyongwa?
Ndio ni kwakuwa wengi tumetawaliwa na woga wa kutenda wenyewe hasa kwenye mambo ya kulipiza visasi, matokeo yake tunakodi watu wabaya wafanye kwa niaba yetu...ni aina fulani ya ya kutaka kudhuru huku tukijibakisha salama lakini Maranyingi hivi vitu huacha alama
 
kweli kabisa hasira ni hasara wengi wamepoteza mke, mchumba kwasababu ya hasira baadaye unajuta uko pekee yako hata ukimpata mwingine bado yule aliyepita utamuona alikuwa vizuri sana
 
Umenena vema Sana Mkuu wangu. Nimebakiwa na kazi ya kuitafakari hiyo picha na kuipatia majibu haswa umemaanisha mini kuiweka ndani ya Uzi huu. Hasira imewakilishwa na hicho kiumbe kinachotisha au huyo binadamu anayenyongwa?
Mkuu mshana ata aeleze kuhusu mungu, au maisha ya mbinguni, mdada mreeembo, ata aamue siku kuelezea mlimani city au ata kanisa, Uzi wake atauona hauna maana kama asipoweka picha, au maandishi ya kutishatisha tuuu ya kishetani, anahitaji maombi yako mkuu
 
Mkuu mshana ata aeleze kuhusu mungu, au maisha ya mbinguni, mdada mreeembo, ata aamue siku kuelezea mlimani city au ata kanisa, Uzi wake atauona hauna maana kama asipoweka picha, au maandishi ya kutishatisha tuuu ya kishetani, anahitaji maombi yako mkuu
siri ya mchezo. ...!!!
 
Sawa bro pamoja sana naona bado unatukumbusha think beyond na wengi sana wanashindwa hizo hali
 
Bwana nshakambia nyuzi na picha kama hizi ni asubuhi sii Wakati wa kulala.
1468082804300.jpg
itafakari hii kama picha ya vyakula iliyofanyiwa sanaa na mwendawazimu, na si kama kichwa kilichokobolewa ngozi
Cha kujiuliza hapa ni hiki! Je huyu mwendawazimu aliwaza nini?
 

Similar Discussions

17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom