Siri ya kushindwa CCM Arumeru Mashariki

ikiona pamoja na kutumia polisi,NEC,wezi na wauwaji bado unashindwa ujue watu hawakutaki sasa ccm wajifunze wananchi hatuwapendi wametuchosha tupo tayari kuthubutu na kujaribu vyama vingine.
 
Wacha kujifariji na kusingizia kambi zenu...

..wananchi wameelimishwa wakaelimika, endeleeni kutafuta wachawi..

..wanaume wanajipanga..
habari za kuaminika kutoka chanzo cha uhakika ni kuwa ccm imeshindwa uchaguzi wa arumeru mashariki,ni kutokana na mvutano mkubwa unaoendelea katika kile kinachoitwa kujivua gamba.Kubwa ni kumkomoa Lowasa na jeuri yake ya pesa na ubishi wake wa kulazimisha mkwewe sioi sumari awe mgombea wa ccm,japo kamati kuu ilimkataa.Taarifa ni kuwa baadhi ya viongozi wa juu wa ccm wamefurahi kuanguka kwa ccm huko arumeru,wakidai ni anguko la Lowasa na matumizi ya fedha nyingi kuelekea uchaguzi 2015
 
Umenena mkuu! Sijui ni kwa nini watu wanashindwa kuona ukweli kuwa ccm imeshachokwa na muhimu zaidi ni kuwa inaboronga kwa kila jambo la maana!
Nakubaliana na wewe kwa 100%.Madhara ya utawala wa ccm hasa baada ya Nyerere kwa nchi hii ni makubwa sana na itachukua muda mrefu sana kuyarekebisha.
CCM wameua mfumo wa elimu wa Taifa hili ili hali viongozi na makada wake wakisomesha watoto wao nje kwa kutambua ubora wa elimu wanayoisimamia haukidhi viwango vya Kimataifa,Wameweka uchumi wa Taifa hili mikononi mwa Wageni na kuacha Watanzania kuwa watumwa wa wageni kwa kufanya kazi ambazo haziwapi fursa ya kupata kipato endelevu kwa vizazi vyao,wamewafanya Watanzania kuwa watu omba omba wakati raslimali zao zikineemesha wageni.
Yako mengi ya kuelezea ambayo nanyi mnaweza kuyaendeleza.
 
Wangekuwa na makundi wasingekwenda kuporomoshea wenzao matusi badala ya kuuza sera kwani tuliwaona wakiwa pamoja na walisema watashinda kwa wingi wa kura! CCM hayooooooooooooooooooooooooooooo!
 
CCM wakubali kwamba wameshindwa kihalali na ni kwa sababu wamepoteza mvuto. Kuna mengi sana ambayo yanakatisha tamaa wananchi kwa kuwa wanaona wabunge wao mambo wanayoyafanya Bungeni ambayo ni ya aibu.

Wanamkomoa Lowassa, kwani aliwalazimisha CC wampitishe Sioi? Wakati Sioi anapitishwa, Lowassa alikuwa Ujerumani.

Kama walikuwa wanamkomoa Lowassa ilikuwaje, Secretariat ya NEC ihamie Arumeru? Ambaye sikumuona huko ni Chiligati na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar. Lakini wengine wote walikuwa huko kuanzia Mukama, Makamba, Nape, Yule mama Mzanzibari (Asha Abdallah) na Mwigulu. Bado Msekwa naye alikuwa huko.

Mawaziri Wasira, Nagu, na Medeye walikuwa huko. Wabunge kibao wa CCM walikuwa huko. UVCCM uongozi wa Taifa, Mkoa, na Wilaya karibu zote za Arusha na Kilimanjaro walikuwa huko. UWT Taifa nao walikuwa huko na ahadi za kuwapa mikopo akina mama.

Sasa kama CCM ilikuwa inamkomoa Lowassa ilikuwaje itume jeshi lote hilo la Jumuiya zote za chama, uongozi wa Taifa wa CCM, na mawaziri juu.
 
Ungefanya some editting kwa heading ungeandika siri ya kushindwa CCM uchaguzi wa mbunge Arumeru na chaguzi za madiwani.
Kwa kifupi ni testimony ya anguko la CCM towards 2015
 
Kuanza kutafuta mchawi ni kushindwa kuon ambali. Ni kisingizio kisicho na mashiko. Tatizo siyo Siori vile vile. Ufumbuzi ni CCM kutafakari kama sera zake na ahadi zake pamoja na utekelezaji wake vinaleta tija kwa wananchi. Tukifuata njia hiyo tutaona mwanga. Hivi sasa giza inaanza kunyemela CCM;tuanze safari ya 'kujirudi' kwa ukombozi awamu ya pili bada ya kupata uhuru
 
Je, kwa CCM kupoteza jimbo la Arumeru Mashariki in wakati mwafaka sasa wa CCM kuwavua gamba Lowassa na Chenge kwa sababu hata 2015 kwa pesa yao hawawezi tena kuisaidia CCM dhidi ya nguvu ya vijana wapenda mabadiliko????????
 
Kirumba, Kiwira na Lisbon wamemkmoa nani? CCM kimeshindwa na wala si kwa sababu ya Lowassa.

Ni kweli mwisho wa Chukua Chako Mapema umewadia. Anguko kubwa zaidi laja 2015. Wanachezea nguvu ya umma eeh...?? Aibu yao magambaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!:smile-big::smile-big:
 
Si kweli, maneno hayo ni sawa na mtu asiyeamini kuwa kumekucha kwa kujifunika shuka usoni ili asione nuru ya mchana, kimsingi imani hiyo ni nzuri kwetu kwani inawaweka pabaya zaidi!!
 
Arumeru ni ushindi mkubwa sana kwa CCM kwa mwenye uelewa!

kweli wewe ni zomba, uelewa upi huo mkubwa? mmeshindwa nyamaza kimya na kutafakari nini cha kufanya sio kujifariji ei ni ushindi mkubwa. acha utoto wa kufikiri na ulevi wa fikra. mmewatumia watu wenu maarufu bado kipigo kimewkuta, sijajua tu hao viongozi wa serikali ( waliopo na wastaafu) walilipwa posho na chama au serikali, maana kwenu nyiee hamna tofauti kati ya serikali na chama
 
Back
Top Bottom