Siri kubwa ya Ruge Mutahaba

sangujoseph

Senior Member
Nov 30, 2015
164
183
.

By Sangu J

Wakati taifa hususani sisi vijana tukiwa kwenye huzuni kubwa kupotelewa kwa ndugu yetu #Ruge Mutahaba mimi napendelea kumuita ( KING OF YOUTH) kwa uhodari wa kuhakikisha anajitoa kwa ajili ya sisi vijana wa kitanzania ili tuweze kuleta mabadiliko chanya kwenye Taifa letu.

Inawezekana nimechelewa kwa sababu wakati naandika haya Boss Ruge hatunaye tena kwenye uso wa dunia na hawezi kujibu chochote kwa sababu tunayemsimulia ni mwili ambao mzee wangu Mengi aliuita jina la Kasha.

Nilibahatika kukutana naye mara chache lakini nilishuhudia kupokelewa kwa mwili wake na kikubwa nilichokigundua Boss Ruge aliwekeza zaidi kwa vijana, karibia 85% walikuwa ni vijana ambao ndiyo idadi kubwa ya watu tulijitokeza kumlaki Boss Ruge.

Somo pekee alilothibitisha na ametufunza Boss Ruge ukihitaji kufanikiwa kwenye jambo wahamasishe kwa kugusa maisha ya vijana na kuwajaza uzalendo juu ya TZ na ndiyo jambo kubwa lilimfanya Boss Ruge kutuunganisha vijana na kutambua thamani ya nchi, kulinda raslimali, kujua vijana ndiyo tunaotegemewa na kuivusha nchi hii kutoka tulipo ili kufikia uchumi wa kati.
.
#KijanaMzalendo #IloveTz #PumzikaRuge #SanguJoseph

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niko nasoma kwa sauti ili mama watoto naye asikie nini kipo kwenye hii thread,, ila umenipa kazi kubwa sana ya kusoma bila kutaja neno boss,, kumbuka Ruge hakuwa boss wa kila mtu,,
 
We jamaa bana.

Hebu nitajie vijana watano tu aliowasaidia Marehemu na sasa wana maisha ya kupigiwa mfano.

Tatizo mnapenda kukuza mambo na kutia machumvi.

Amezunguka nchi nzima kwa Fiesta na Semina za Fursa, nioneshe watu 10 waliopiga hatua kwa hizo semina.

Ni hivi, huwezi kufanya baadhi ya shughuli na ukafanikiwa kama hukumnufaisha ama hunufaishi watu Fulani - nadhani umenielewa.
 
Mimi pia nilikuwa sijui kama jamaa hakuwa na mke lakini alikuwa na watoto wengi hivi, kuna mdau kaomba kuonyeshwa watu 10 aliyowasaidia yeye ila mimi bila unafiki naomba mmoja tu


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niko nasoma kwa sauti ili mama watoto naye asikie nini kipo kwenye hii thread,, ila umenipa kazi kubwa sana ya kusoma bila kutaja neno boss,, kumbuka Ruge hakuwa boss wa kila mtu,,

kivumishi hicho

hata nyerere hakuwa mwalimu wa kila mtu
 
.

By Sangu J

Wakati taifa hususani sisi vijana tukiwa kwenye huzuni kubwa kupotelewa kwa ndugu yetu #Ruge Mutahaba mimi napendelea kumuita ( KING OF YOUTH) kwa uhodari wa kuhakikisha anajitoa kwa ajili ya sisi vijana wa kitanzania ili tuweze kuleta mabadiliko chanya kwenye Taifa letu.

Inawezekana nimechelewa kwa sababu wakati naandika haya Boss Ruge hatunaye tena kwenye uso wa dunia na hawezi kujibu chochote kwa sababu tunayemsimulia ni mwili ambao mzee wangu Mengi aliuita jina la Kasha.

Nilibahatika kukutana naye mara chache lakini nilishuhudia kupokelewa kwa mwili wake na kikubwa nilichokigundua Boss Ruge aliwekeza zaidi kwa vijana, karibia 85% walikuwa ni vijana ambao ndiyo idadi kubwa ya watu tulijitokeza kumlaki Boss Ruge.

Somo pekee alilothibitisha na ametufunza Boss Ruge ukihitaji kufanikiwa kwenye jambo wahamasishe kwa kugusa maisha ya vijana na kuwajaza uzalendo juu ya TZ na ndiyo jambo kubwa lilimfanya Boss Ruge kutuunganisha vijana na kutambua thamani ya nchi, kulinda raslimali, kujua vijana ndiyo tunaotegemewa na kuivusha nchi hii kutoka tulipo ili kufikia uchumi wa kati.
.
#KijanaMzalendo #IloveTz #PumzikaRuge #SanguJoseph

Sent using Jamii Forums mobile app
Na aliwatumia kweli kupata ''vicopy copy''
 
Back
Top Bottom