Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,896
Wananchi wa Kata ya Sirari Jimbo la Tarime vijijini amekusanyika katika kituo cha polisi cha Sirari, Baada ya Jeshi la polisi kudaiwa Kumuua Mdogo wa Mbunge wa Tarime vijijini Mhe. John Heche akiwa chini ya ulinzi, anaejulikana kwa jina la Suguta Chacha.
---
UPDATES..
Mbunge John Heche ameithibitishia JamiiForums kutokea kwa tukio hili..
Ameeleza kuwa;
1. Tukio ni la kweli
2. Kijana Suguta Chacha ameuawa kwa kuchomwa kisu na Polisi waliomkamata jana usiku akiwa Bar.
3. Polisi walijaribu kumtupa baada ya kumuua lakini eneo hilo kulikuwa na mlinzi ambaye aliwafukuza hivyo ikashindikana na kuwalazimu kumpeleka Mochwari.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Polisi Tarime Rorya Henry Mwaibambe amethibitisha kuuawa kwa Bwana Chacha Heche Suguta ambaye ni mdogo wa Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche, kwa kuchomwa kisu na Polisi.
“Tukio ni la kweli limetokea na huyo askari tunamshikilia, huyo kijana alikamatwa usiku sasa wakati wapo kwenye gari wakielekea kituo cha polisi, ukatokea mzozo kati ya huyu askari na huyu marehemu, mzozo kama wanataka kupigana, mwenzake akaingilia kuamua, lakini ni kweli askari amemjeruhi huyu mgongoni, mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi leo saa 6 mbele ya ndugu zake, kweli umekutwa na jeraha la hicho kisu mgongoni na mtuhumiwa alikuwa hajavalishwa pingu, ila hatujui nini waliambiana mpaka kufikia hivyo”, amesema Kamanda Mwaibambe.
Pia Kamanda Mwaibambe amewataka watu kutochukulia tukio hilo kisiasa, isipokuwa ni kama tukio lingine la mauaji, ingawa sio jambo zuri kwa mtu yeyote.
---
UPDATES..
Mbunge John Heche ameithibitishia JamiiForums kutokea kwa tukio hili..
Ameeleza kuwa;
1. Tukio ni la kweli
2. Kijana Suguta Chacha ameuawa kwa kuchomwa kisu na Polisi waliomkamata jana usiku akiwa Bar.
3. Polisi walijaribu kumtupa baada ya kumuua lakini eneo hilo kulikuwa na mlinzi ambaye aliwafukuza hivyo ikashindikana na kuwalazimu kumpeleka Mochwari.
-------------- Jeshi la Polisi lathibitisha askari wake kuhusika----------------
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Polisi Tarime Rorya Henry Mwaibambe amethibitisha kuuawa kwa Bwana Chacha Heche Suguta ambaye ni mdogo wa Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche, kwa kuchomwa kisu na Polisi.
“Tukio ni la kweli limetokea na huyo askari tunamshikilia, huyo kijana alikamatwa usiku sasa wakati wapo kwenye gari wakielekea kituo cha polisi, ukatokea mzozo kati ya huyu askari na huyu marehemu, mzozo kama wanataka kupigana, mwenzake akaingilia kuamua, lakini ni kweli askari amemjeruhi huyu mgongoni, mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi leo saa 6 mbele ya ndugu zake, kweli umekutwa na jeraha la hicho kisu mgongoni na mtuhumiwa alikuwa hajavalishwa pingu, ila hatujui nini waliambiana mpaka kufikia hivyo”, amesema Kamanda Mwaibambe.
Pia Kamanda Mwaibambe amewataka watu kutochukulia tukio hilo kisiasa, isipokuwa ni kama tukio lingine la mauaji, ingawa sio jambo zuri kwa mtu yeyote.