sipendi masimu haya jamani.

sipendi masimu haya jamani.

Mphamvu

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2011
Posts
10,702
Reaction score
3,345
haya masimu ya kisasa yenye sijui wifi na skype na windows 6, pamoja na ma iphone sijui siyapendi kabisa! ingawa yana features za kisasa zote, mengi ni aidha smartphones au touchscreen., kwanza ni vilaini, ukikaangusha tu kwishney, pili zimepotesa clasic identity yake, mfano, mi ni mpenzi wa samsung, tangu zamani nikiona menyu ya simu hata kwa mbali najua kama ile ni samsung, sasa hv kuna mchezo wa os za simu, zote zinafanana hata kama brand tofauti. halafu imagine simu ya touch inawekewa screen keypad za qwerty, sijui text unaandika vipi kwa raha! keyboard ya kawaida imeundwa kutoshana na fleksibility za vidole zetu, sasa zinawekwa kwa kablakberi au simu ya touch! mwenzenu candybar mpango mzima, kama samsung yangu sgh-d780!
 
And we needed to know because.....? Peleka kwnye Complaints and Congrats Forum...
 
And we needed to know because.....? Peleka kwnye Complaints and Congrats Forum...

Tulia kinega, kama unahisi huwezi kuchangia potelea kule. hilo jukwaa ulilolisema ni kwa ajili ya malalamiko yanayohusu forums na member wake. sasa hili la simu za android na 4g ni la jf?
 
Mkuu huna tofauti na babu yangu, hadi leo anaamini gari bora kabisa ni Landrover 109
Watu wanasonga mbele wewe unapika makitaimu
 
Usiogope hata samsung wana simu nzuri zenye os za kisamsung samsung badilika wewe.
 
Tupo kwenye dunia ambayo the only thing people are thinking is about money. That's why Business men believes ''money makes the world go round''.
 
hahaha yani umenifurahisha sana. jaribu kutumia smart phone uizoee ndiyo utajua utamu wake. wajua ukizoea tumia simu zenye os za ukweli kama ios au android au wm hutatamani tena simu zenye embemed os kama hizo unazozisema. dunia inabadirika mkuu na inabidi uende nayo sambamba ni sawa mtu aje aseme daa mimi sipendi windows 7 yani windows 98 ya ukweli mimi naona windows 7 haina dili. test you will find out what i mean mkuu.
 
Sawa huzipendi, kwani simu za tochi hazipatikani siku hizi? Ndo uzuri wa kuwa na choice.
 
Mkuu huna tofauti na babu yangu, hadi leo anaamini gari bora kabisa ni Landrover 109
Watu wanasonga mbele wewe unapika makitaimu

hapana kaka, hata hii simu ninayotumia sio outdated sana, ni moja kati ya javaphones bora kabisa.
 
hahaha yani umenifurahisha sana. jaribu kutumia smart phone uizoee ndiyo utajua utamu wake. wajua ukizoea tumia simu zenye os za ukweli kama ios au android au wm hutatamani tena simu zenye embemed os kama hizo unazozisema. dunia inabadirika mkuu na inabidi uende nayo sambamba ni sawa mtu aje aseme daa mimi sipendi windows 7 yani windows 98 ya ukweli mimi naona windows 7 haina dili. test you will find out what i mean mkuu.

nay, nimeshatumia symbians, galaxy na iphone kipindi fulani, ila zimenishinda kwa kweli! nabaki kuwa mpenzi wa candybar phones!
 
haya masimu ya kisasa yenye sijui wifi na skype na windows 6, pamoja na ma iphone sijui siyapendi kabisa! ingawa yana features za kisasa zote, mengi ni aidha smartphones au touchscreen., kwanza ni vilaini, ukikaangusha tu kwishney, pili zimepotesa clasic identity yake, mfano, mi ni mpenzi wa samsung, tangu zamani nikiona menyu ya simu hata kwa mbali najua kama ile ni samsung, sasa hv kuna mchezo wa os za simu, zote zinafanana hata kama brand tofauti. halafu imagine simu ya touch inawekewa screen keypad za qwerty, sijui text unaandika vipi kwa raha! keyboard ya kawaida imeundwa kutoshana na fleksibility za vidole zetu, sasa zinawekwa kwa kablakberi au simu ya touch! mwenzenu candybar mpango mzima, kama samsung yangu sgh-d780!
hata mimi natumia sgh-d780, lakini mpaka sasa nashindwa namna ya ku-attach picha. ebu nisaidie
 
Sawa huzipendi, kwani simu za tochi hazipatikani siku hizi? Ndo uzuri wa kuwa na choice.

sijasema kuwa napenda tochi jameni. mi napenda candybar phones, tatizo langu ni kwanini feature latest zimewekwa kwa androids na windows mobile wakati choice lazma iwe na updates?
 
karbu katika ulimwengu wa tech.

via HTC Incredible S .. hehe
 
hata mimi natumia sgh-d780, lakini mpaka sasa nashindwa namna ya ku-attach picha. ebu nisaidie

kama ni jf tumia pc mode ambayo katika opera haipatikani, jaribu kudownload uc browser version 9.7, itasaidia. kama ni facebook hakuna shida kabisa!
 
Mimi naona simu ambazo ni latest zinafaida nyingi sana, kwanza zin sensitive camera kuanzia 5MP - 8MP, pili zina uwezo wa kuchukua video movie bila shida yoyote hadi MP4 (1280 -780) ambayo highest quality. Net ndiyo usiseme kabisa, kwa vifu hivyo vitatu kwangu mimi ndiyo msingi wa maamuzi, vinginevyo kama nataka kupokea na kukata Nokia tochi ni simu poa. Kinachokuja hapa ni gharama ya simu hizo, mfano simu ya chini nzuri touch samsung wave II utaipata kuanzia 660,000.00 na kuendelea, ukija kwenye Iphone ndiyo balaa hadi 1.3ml! Kutokana na ughali huo ndiyo maana zinawashinda wengu lakini otherwise ni best phones ever in the world for the time being.
 
Back
Top Bottom