Sipendi kabisa mwanamke anayesuka

Sipendi kabisa mwanamke anayesuka

BILGERT

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2015
Posts
6,532
Reaction score
11,027
Habarini za asubuhi wanajukwaa pendwa la MMU.

Bila kupoteza muda niende moja kwa moja kwenye mada husika,baada ya kuhangaika kwa muda mrefu bila kumpata mwanamke tunayeendana naye, hatimaye nimebahatika kumpata mdada mmoja hivi wa kibosho...kwa hakika namuelewa saaana nami ananielewa haswaaa....ila shida iliyopo ni kwamba mimi binafsi sipendi kabisa mwanamke anaye suka..

Napenda sana mwanamke anayenyoa kawaida,na kipindi namtokea nilimkuta anasuka, bali niliamini kuwa naweza kumbadilisha.....hivi karibuni nmemgusia suala la kuacha mara moja suala la kusuka na hatimaye aanze kunyoa, tumegombana saaana.Mpaka muda huu, hali bado sio shwariii baina yetu...

Naombeni mnishauri jamani, nitumie mbinu zipi za kumuelewesha aweze kuacha kusuka bila kuathiri mahusiano yetu? Natanguliza shukrani zangu za dhati kwenu nyote

NB: Sisi ni wachumba...hatujaoana bado
 
vazi la mwanamke la kwanza ni nywele.. sina maana nywele bandia nywele zake asili...naamini na wewe kuna mapungufu unayo anayachukulia jitahidi umchukulie mwenzio
sawa mkuu,lakini cjamaanisha anyoe kipara ujue ila abaki na nywele fupi
 
Dunia sasa inaelekea kubaya... Hivi sasa mmeanza kupendea nywele??

Wenzako wanakuambia mwanamke nywele, Kijana angalia sana usije ukaanza kutamani wanaume wenzio.

Sote tusimame kumwombea mleta mada asiingie kwenye ukameruni
 
Dunia sasa inaelekea kubaya... Hivi sasa mmeanza kupendea nywele??

Wenzako wanakuambia mwanamke nywele, Kijana angalia sana usije ukaanza kutamani wanaume wenzio.

Sote tusimame kumwombea mleta mada asiingie kwenye ukameruni

hahaahaa,co poa mkuu
 
Mkuu wewe ni kama mimi.
Mwanamke akiwa simple..nywele fupi kama namba 1 au kama zipo nyingi basi azifunge kwa nyuma kikorea fulani hivi na ziwe safiii.

Aseeh hapo chochote anachukua kwangu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom