Sioni usafi wa Lowassa

Sioni usafi wa Lowassa

Luther3

Member
Joined
Nov 9, 2011
Posts
41
Reaction score
7
hivi inawezekanaje lowasa akasema kua yeye hausiki kwenye richmond?kwakuzingatia yeye ndo alikua waziri mkuu. Je iweje sasa anaanza kusema anataka kuwasaidia vijana wakati alikuepo madarakani na hakuonesha juhudi mufilisi kama anavyofanya sasa?

Ameshika nafasi mbalimbali kwenye serikali lakini hatukuona utendaji mzuri anaojinasibu kua nao. Angalau hata unaofanana na huu wa akina Mwakyembe na Magufuli.

Kwanini kasi ya kufanya viharambee imeshika kasi sasa kuliko wakati mwingine wowote ambapo alikuepo?na ukizingatia wakati wa uchaguzi umekaribia.
Watanzania tunahitaji kujiuliza maswali haya ya msingi tusisubiri kuambiwa sijui na viongozi wa dini au wa vyama tutumie akili zetu kutafakari siasa zao.

Watatumaliza hawa mafisadi.
 
Ati wanaCCM Lowassa wanadai ni Jembe Lao lkn wakati wakipiga deal na JM sijui kwanini hakukataa kama aliona ni ufisadi.
Lowasssa TAPELI, JM TAPELI,CCM TAPELI
 
Ati wanaCCM Lowassa wanadai ni Jembe Lao lkn wakati wakipiga deal na JM sijui kwanini hakukataa kama aliona ni ufisadi.
Lowasssa TAPELI, JM TAPELI,CCM TAPELI

Jembe kwa lipi alilofanya au hizo shule za kata zinazotoa ziro kila siku?. Lowasa ataendelkea kuota kamwe hawezi kuwa Rais
 
Nakuunga mkono 100% watanzania wepesi sana wa kusahau! Na zaidi Kikwete mwenyewe anakiri kwamba watu wanatumia pesa kununua uongozi na bado wao hawahoji zinatoka wapi.
 
Nakuunga mkono 100% watanzania wepesi sana wa kusahau! Na zaidi Kikwete mwenyewe anakiri kwamba watu wanatumia pesa kununua uongozi na bado wao hawahoji zinatoka wapi.

Inamaana na yeye alinunua?
 
Lowasa anataka uraisi ili amalizie yale aliyoyaacha akiwa PM. Tulimuondoa kwenye uPM mapema mno. Hebu tumpe jamani ili aweke rekodi ya kukumbukwa milele. Yaani mtu kapiga kadili kamoja tu tunamng'oa! Tumpe hata miaka mitano bac arudishe hata hela zake za harambee.
 
Lowasa anataka uraisi ili amalizie yale aliyoyaacha akiwa PM. Tulimuondoa kwenye uPM mapema mno. Hebu tumpe jamani ili aweke rekodi ya kukumbukwa milele. Yaani mtu kapiga kadili kamoja tu tunamng'oa! Tumpe hata miaka mitano bac arudishe hata hela zake za harambee.

Ndio akili za wapiga kura ziko hivi! Eti "tumuachie amalizie", "yaani kapiga kadiki kamoja tu"..Hivi unamjua ENL wewe?

Katika nchi ukijumlisha pesa za ubadhirifu kwa jina la "tumuache tu amalizie" kwa ngazi ya chini hadi uraisi, tunaweza kutengeneza bajeti!
 
Back
Top Bottom