mama kubwa
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 5,413
- 8,398
Jana niliona dhifa ya Taifa ,wakubwa wanakunywa michuzi na wine. Sio vibaya kumkirimu mgeni lakini kwa uelewa wangu mdogo ni dharau kwa wavuja jasho, watu wasio na uhakika wa mlo hata mmoja.
Tv zimeenea nchi nzima hata vijijini kule igunga ambapo watu wanakunywa maji na ng'ombe , kule kwetu ambapo mtu akila mara moja anashukuru mungu, anaonyeshwa wanene wanavyofaidi nchi hii.
Swali kwa wenzetu mnaoishi nje hivi rais wetu akifanyiwa dhifa huwa anaonyeshwa live? watanzania tumechoka na dharau hii hatukatai kuleni lakini msitukebehi tunao lala na njaa.
Tv zimeenea nchi nzima hata vijijini kule igunga ambapo watu wanakunywa maji na ng'ombe , kule kwetu ambapo mtu akila mara moja anashukuru mungu, anaonyeshwa wanene wanavyofaidi nchi hii.
Swali kwa wenzetu mnaoishi nje hivi rais wetu akifanyiwa dhifa huwa anaonyeshwa live? watanzania tumechoka na dharau hii hatukatai kuleni lakini msitukebehi tunao lala na njaa.