Sio sawa kabisa dhifa za taifa kuonyeshwa kwenye tv

TBC inajipotezea mvuto taaaratibu.. Amina Mollel alikuwa anaongea utadhani kameza kanda! Au Charles Hillary anatangaza mechi EPL! State banquet watu walikuwa hawana manners utadhani ni Cocktail Party flani pale Coco Beach?! Aaaaagh!
 
jamani kweli ni aibu..lakini pia mumsamehe angalieni huyo mkuu wetu katokea wapi
ndiyo anajifunza hivyo.kijana wa bwagamoyo na mtoto wa malkia utakaa uone wapi!
Ni bongo tuuu.
 
Mkuu unakumbuka mama salma alitaka kumnyang'anya mmewe kombe la dunia wakati lilipopitishwa hapa bongo?? Na mmewe akataka kumpa....wakamuwahi asimpe.

mkulu mwenyewe ndo wale wale....mguu pande mguu sawa nyuma geuka.
Unajua uko makini sana!

1. Hilo la mtangazaji mbabaishaji lina-apply sana TBC/ Daily News etc. Jana kwenye Jahazi ya Clouds, Kayanda alikuwa anaongea na m-TBC mmoja alieenda London kwenye Miss World. Kwa kuanza Kayanda alijitahidi kuset background kuwa mrembo wetu alijitahidi sana lakini alianguka kutokana na upinzani mkubwa. Alikpopewa m-TBC fursa ya kuongea akaanza kumponda yule mrembo wetu utafikiri wamenyan'ganyana bwana!

2. Kama ni kweli Salva aliongea katikati ya toast za wakubwa, basi amekosea sana.

3. Hilo la kukosa discipline na watu kuzunguka zunguka utaliona kwenye kila tukio kubwa linalowahusu waswahili kama waratibu. Iwe ni uapisho wa waziri, kutoa kombe la mashindano, kote utaikuta hii kitu.
 
Gb, hata kama dhifa itaoneshwa (hii haina tofauti na zile za mengi na walemavu za mwaka mpya), tatizo ni kurusha live! Ingeweza kuwa kipindi maalum na sio kuacha kuonesha taarifa ya habari tuangalie ubwabwa! It was even boring manake hata hawawezi kukata wakati mukulu anaongea na mikono mezani na chakula mdomoni!
Craaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaap hakuna kitu hapa na sio dhifa ya kwanza kuonyeshwa kwenye tv, huu ni wivu wa kike !
 
Lol, table manners mukulu hana kabisaaa! Walau hakuangusha glass manake mweh!
Mkuu unakumbuka mama salma alitaka kumnyang'anya mmewe kombe la dunia wakati lilipopitishwa hapa bongo?? Na mmewe akataka kumpa....wakamuwahi asimpe.

mkulu mwenyewe ndo wale wale....mguu pande mguu sawa nyuma geuka.
 
kudadaddadadeki mimi nilifurahia sana ile dhifa kuoneshwa katika tv, kilichonifurahisha ni kujua kuwa kumbe charles ni mtoto wa mfalme. Hongereni tbc kazeni uzi hapo hapo. Prince charles mwana wa mfalme. Hongera amina mollel ulifanya kazi nzuri sana mpaka ukaishiwa pumzi, wewe kweli uko fiti na unaijua kazi yako hureeeeeeeee tbc, hureeeeeeee amina mollel
unachekesha unavyokenua na mapengo yalivyojaa mdomoni
 
Jana niliona dhifa ya Taifa ,wakubwa wanakunywa michuzi na wine. Sio vibaya kumkirimu mgeni lakini kwa uelewa wangu mdogo ni dharau kwa wavuja jasho, watu wasio na uhakika wa mlo hata mmoja.

Tv zimeenea nchi nzima hata vijijini kule igunga ambapo watu wanakunywa maji na ng'ombe , kule kwetu ambapo mtu akila mara moja anashukuru mungu, anaonyeshwa wanene wanavyofaidi nchi hii.

Swali kwa wenzetu mnaoishi nje hivi rais wetu akifanyiwa dhifa huwa anaonyeshwa live? watanzania tumechoka na dharau hii hatukatai kuleni lakini msitukebehi tunao lala na njaa.

Hapana kamanda toka enzi za nyerere ilikua ikifanyika hivyo labda ulikua hujazaliwa, sema kipindi kile labda hatukua na tv bali tulikua tunasilizia dhifa kwenye RTD,Na tulikua tuna enjoy wenyewe,maana utaelezwa pale meza kuu kuna mchele kutoka mbeya ndizi kutoka kilimanjaro,zbibu kutoka dodoma,kuku wa kienyeji kutoka singida n.k.hiyo ilikua ikiongeza ari ya wakulima kulima kwa bidii kwa kutambua kuwa hata viongozi wa kimataifa wanakula wanachozalisha wao...so kwangu sioni kama tatizo tena nasikitika hapa kati kati kipindi cha mkapa ndio tukaanza kukikosa kipindi cha dhifa ya taifa ambacho nakumbuka kilikua kinaanza kama saatatu usiku live,wakati mchana wake mmesharushiwa live ujio wa mgeni huyo toka ndege inatua airport na muungurumo mnausikia!!!ilikia poa sana.
 
Craaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaap hakuna kitu hapa na sio dhifa ya kwanza kuonyeshwa kwenye tv, huu ni wivu wa kike !

Wivu wa kike cdm utawamaliza, kumbe maneno yako hayo yote ni kwa vile JK , ila angekuwa slaa poa tu, subirini na nyie 3025 mtafanya


mkeo na mama yako wana wivu sana heeeee, unadhani kila mwanamke ni kila kama wanaokuzunguka heshime jinsia wewe
 
Nafurahi kua watu tunamtazamo unaoshabihiana katika kutazama athari ya mambo yanayofanyika ambayo hayana mantiki...sipingani na tukio la kumkirimu mgeni...hasha...ni jambo jema na lenye sifa sana ikikumbukwa kua mgeni mwenyewe ni yule babu zake walikwarubuni babu zetu kwa vioo huku wakijitwalia vito...huu ni upuuzi na dhihaka kwa masikini walipa kodi!
 
Back
Top Bottom