Sio kila muda kulaumu mameneja, kuna wasanii ni kama wadangaji, Hawana uchungu na gharama iliyowekezewa na mameneja, wanajiangalia wao tu

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
Ni kweli kwamba huwa kuna mameneja wanazingua lakini pia tusisahau kuna wasanii nao huwa wanazungua

Lazima tuelewa vizuri mazingira ya wasanii, management na soko kwa jumla.

Wasanii wengi wanapoianza kazi ya miziki wanakuwa hawajiwezi kwa lolote, Hivyo hulazimika kutafuta management itakayoweza kufanikisha kutimiza ndoto zao kwa kulipia gharama.

Msanii na Meneja hujikuta wakiingia mikataba nafuu kwasababu ya ualisia wa biashara yenyewe ya muziki siku zote huwa ya kubahatisha.

Ndio maana mameneja wengi huwa wanasifiwa kwa kumtoa msanii mmoja tu kati ya wengi alionao.

Kazi ya management hiyo kwanza ni kuhakikisha msanii anatunga nyimbo nzuri zitakazoenda kulitingisha soko, Baada ya hapo kulipia gharama za kurekodi audio na video, ikiwa ni pamoja na mavazi kuanzia unyayoni mpaka utosini.

Baada ya hapo kulipia promo kwenye radio na TV station zote ili nyimbo zipigwe kila kukicha, kisha linakuja swala la kum'brand msanii ili kumuongezea thamani angalau naye uonekane ni mtu fulani kati ya watu.
Katika hili ndipo pesa zinapoteketea kwani management ina wajibu wa kuhakikisha msanii anavaa vizuri kuanzia viatu hadi kofia, management pia uhakikisha msanii lazima akae kwenye nyumba nzuri inayoendana na hadhi ya kisanii, gharama za saluni na mahitaji muhimu ya nyumbani zikiwemo samani za nyumba nzima na chakula cha kila siku pamoja na usafiri.

Fahamu kuwa wakati haya yote yanafanyika, ni pesa ya meneja ndio inayoteketea. Promo inapokubali kwenye media, ndipo wanaanza kujitokeza watu wa pembeni na kuanza kumshika masikio msanii, Hapo ndipo maneno ya "unaibiwa wewe yaani nyimbo zimehit bado huna kitu?" Baadhi ya wasanii wengi huwa ni mambumbumbu kwani huwa wanakubali kujaa upepo kirahisi bila kujali gharama ilyotumika imerudi au bado.

Hii husababisha msuguano mkubwa kati ya meneja na msanii. Kwani hasara huwa ni kubwa kuliko faida.

Suala la hili lilikuwa fundisho kwa mameneja kadhaa huko nyuma ndio maana ujinga huo umefanyiwa marekebisho kwenye Lebo ya WBC, ukitaka kusepa lazima uzitapike kachumbari zote ulizokula !!.

Kuna muda wasanii ndio wanazingua !! Tatizo sio mameneja bali akili ya baadhi ya wasanii ni kama ya wadangaji, Hawana uchungu gharama waliyowekezewa, wanajiangalia wao tu.
 
Lazima tuelewa vizuri mazingira ya wasanii, management na soko kwa jumla.

Wasanii wengi wanapoianza kazi ya miziki wanakuwa hawajiwezi kwa lolote, Hivyo hulazimika kutafuta management itakayoweza kufanikisha kutimiza ndoto zao kwa kulipia gharama.

Msanii na Meneja hujikuta wakiingia mikataba nafuu kwasababu ya ualisia wa biashara yenyewe ya muziki siku zote huwa ya kubahatisha.

Ndio maana mameneja wengi huwa wanasifiwa kwa kumtoa msanii mmoja tu kati ya wengi alionao.

Kazi ya management hiyo kwanza ni kuhakikisha msanii anatunga nyimbo nzuri zitakazoenda kulitingisha soko, Baada ya hapo kulipia gharama za kurekodi audio na video, ikiwa ni pamoja na mavazi kuanzia unyayoni mpaka utosini.

Baada ya hapo kulipia promo kwenye radio na TV station zote ili nyimbo zipigwe kila kukicha, kisha linakuja swala la kum'brand msanii ili kumuongezea thamani angalau naye uonekane ni mtu fulani kati ya watu.
Katika hili ndipo pesa zinapoteketea kwani management ina wajibu wa kuhakikisha msanii anavaa vizuri kuanzia viatu hadi kofia, management pia uhakikisha msanii lazima akae kwenye nyumba nzuri inayoendana na hadhi ya kisanii, gharama za saluni na mahitaji muhimu ya nyumbani zikiwemo samani za nyumba nzima na chakula cha kila siku pamoja na usafiri.

Fahamu kuwa wakati haya yote yanafanyika, ni pesa ya meneja ndio inayoteketea. Promo inapokubali kwenye media, ndipo wanaanza kujitokeza watu wa pembeni na kuanza kumshika masikio msanii, Hapo ndipo maneno ya "unaibiwa wewe yaani nyimbo zimehit bado huna kitu?" Baadhi ya wasanii wengi huwa ni mambumbumbu kwani huwa wanakubali kujaa upepo kirahisi bila kujali gharama ilyotumika imerudi au bado.

Hii husababisha msuguano mkubwa kati ya meneja na msanii. Kwani hasara huwa ni kubwa kuliko faida.

Suala la hili lilikuwa fundisho kwa mameneja kadhaa huko nyuma ndio maana ujinga huo umefanyiwa marekebisho kwenye Lebo ya WBC, ukitaka kusepa lazima uzitapike kachumbari zote ulizokula !!.

Kuna muda wasanii ndio wanazingua !! Tatizo sio mameneja bali akili ya baadhi ya wasanii ni kama ya wadangaji, Hawana uchungu gharama waliyowekezewa, wanajiangalia wao tu.
Umeongea ukweli mtupu ,ila tu umeshindwa kutofautisha mabosi na mameneja.

Kuna bosi ,kuna meneja na kuna msanii .

Wasanii wanazingua sana.
 
Mkuu hebu tupe ufafanuzi,Diamond anajiweza kila kitu,kina Babu Tale na Said Fella wamemkuta jamaa tayari ana mpunga na ana chanel nyingi za hela,sasa msaada wao ni nini hasa kwa sasa. Kwa Sallam Sk naweza kusema walianza wote ,ila hao wazee wawili kazi yao pale ni nini hasa?
 
Mkuu hebu tupe ufafanuzi,Diamond anajiweza kila kitu,kina Babu Tale na Said Fella wamemkuta jamaa tayari ana mpunga na ana chanel nyingi za hela,sasa msaada wao ni nini hasa kwa sasa. Kwa Sallam Sk naweza kusema walianza wote ,ila hao wazee wawili kazi yao pale ni nini hasa?
Salaam ana exposure ya nje ya mipaka kumuunga Diamond na dunia ya nje ya Tz

Hao kina babu tale na Fela wana uzoefu na connections kubwa ndani ya mipaka.
 
Bado haujasema, walikuwa na wasanii mbona hawakufika mbali, hakuna kitu pale., Mi naona kampani tu, Simba yupo kamili.
 
Meneja ni mwajiriwa wa msanii.
Executive producer ndiyo mwekezaji.
Producer ndiyo mwenye nyimbo na hakimiliki lakini anaweza kuiuza.
Msanii ni kama dancers tu, huwa analipwa chake anaondoka vilevile waandishi wa nyimbo, sound engineers etc ...
 
Unazungumzia Management au Jina Manager... Bongo hakuna mameneja Kuna masponser au matajiri only.

Kwani meneja ayafanye hayo yote ulioyaorodhesha.? Hapo hapo unasema biashara ya mziki ni kubahatisha kwahiyo msanii abaki Kwa meneja anaesubiria bahati.?

Waambie mameneja wenzako.. muwe mnaandaa mikataba yenyevfaida kotekote.. kama ilivyo Kwa wachezaji wa soka la kulipwa.. msainishen msanii mkataba utakaoonesha mnamlipa shing ngapi Kwa mwezi na nyie mkitumie kipaji chake kurudisha gharama Kwa muda mliokubaliwa Ili hata mkataba ukiisha Kila mtu awe amepata faida.

Leo unaongelea wasanii wanazingua wakati wakitemwa na hizo management wanabaki ombaomba na kuishi Kwa fedheha utazani hawakua na mikataba ya kazi.

Mameneja ndio wanazingua na ushahidi ni huu Utetee ukiweza..
Kwanini msanii akitoka katika management maisha yake yanadrop?

Anzeni kuwalipa Mishahara wasanii muone Kama Kuna atakaezingua. Sio MTU ajitungie wimbo wewe usubiri kumlipia studio wimbo uwe wako.. kweli? Kwahiyo hizi nyimbo tuzisikiazo nyakati hizi ni matokeo ya usimamizi mzuri wa menejiment za Bongo?

Bongo Hakuna Biashara ya Mziki so Meneja ni jina la mtu anaemlipia gharama mbalimbali msanii na sio MTU anaetumia kipaji Cha msanii husika Ili fedha ipatikane wagawane.
 
Meneja ni mwajiriwa wa msanii.
Executive producer ndiyo mwekezaji.
Producer ndiyo mwenye nyimbo na hakimiliki lakini anaweza kuiuza.
Msanii ni kama dancers tu, huwa analipwa chake anaondoka vilevile waandishi wa nyimbo, sound engineers etc ...
Wadau wa mziki wa bongo wanatamani wajione wanauendesha kama Marekani Kwa njia za ki Daslam.
 
Hata mimi nimeshangaa. Yaani meneja ndio anamlipa msanii? Sijawahi kusikia hicho kitu. But this is Bongo, so maybe ...
Hata huko kulipa hakuna anaemlipia msanii... Ukikutana na meneja yeyote muulize mkataba wa msanii wake Una thamani ya shiling ngapi?
 
Wadau wa mziki wa bongo wanatamani wajione wanauendesha kama Marekani Kwa njia za ki Daslam.
Basi hautaenda mbali kwa sababu ili sanaa iende vipaji vingi uhusishwa.

Watu wenye vipaji na elimu au ujuzi wa hali ya juu inabidi uwalipe hela ndefu au uwape mgao/mkataba mzuri.
La siyo, utakuwa unabahatisha.
 
Ni kweli kwamba huwa kuna mameneja wanazingua lakini pia tusisahau kuna wasanii nao huwa wanazungua

Lazima tuelewa vizuri mazingira ya wasanii, management na soko kwa jumla.

Wasanii wengi wanapoianza kazi ya miziki wanakuwa hawajiwezi kwa lolote, Hivyo hulazimika kutafuta management itakayoweza kufanikisha kutimiza ndoto zao kwa kulipia gharama.

Msanii na Meneja hujikuta wakiingia mikataba nafuu kwasababu ya ualisia wa biashara yenyewe ya muziki siku zote huwa ya kubahatisha.

Ndio maana mameneja wengi huwa wanasifiwa kwa kumtoa msanii mmoja tu kati ya wengi alionao.

Kazi ya management hiyo kwanza ni kuhakikisha msanii anatunga nyimbo nzuri zitakazoenda kulitingisha soko, Baada ya hapo kulipia gharama za kurekodi audio na video, ikiwa ni pamoja na mavazi kuanzia unyayoni mpaka utosini.

Baada ya hapo kulipia promo kwenye radio na TV station zote ili nyimbo zipigwe kila kukicha, kisha linakuja swala la kum'brand msanii ili kumuongezea thamani angalau naye uonekane ni mtu fulani kati ya watu.
Katika hili ndipo pesa zinapoteketea kwani management ina wajibu wa kuhakikisha msanii anavaa vizuri kuanzia viatu hadi kofia, management pia uhakikisha msanii lazima akae kwenye nyumba nzuri inayoendana na hadhi ya kisanii, gharama za saluni na mahitaji muhimu ya nyumbani zikiwemo samani za nyumba nzima na chakula cha kila siku pamoja na usafiri.

Fahamu kuwa wakati haya yote yanafanyika, ni pesa ya meneja ndio inayoteketea. Promo inapokubali kwenye media, ndipo wanaanza kujitokeza watu wa pembeni na kuanza kumshika masikio msanii, Hapo ndipo maneno ya "unaibiwa wewe yaani nyimbo zimehit bado huna kitu?" Baadhi ya wasanii wengi huwa ni mambumbumbu kwani huwa wanakubali kujaa upepo kirahisi bila kujali gharama ilyotumika imerudi au bado.

Hii husababisha msuguano mkubwa kati ya meneja na msanii. Kwani hasara huwa ni kubwa kuliko faida.

Suala la hili lilikuwa fundisho kwa mameneja kadhaa huko nyuma ndio maana ujinga huo umefanyiwa marekebisho kwenye Lebo ya WBC, ukitaka kusepa lazima uzitapike kachumbari zote ulizokula !!.

Kuna muda wasanii ndio wanazingua !! Tatizo sio mameneja bali akili ya baadhi ya wasanii ni kama ya wadangaji, Hawana uchungu gharama waliyowekezewa, wanajiangalia wao tu.
Mm naweza sema tatizo kubwa sana sio mamemeja bali ni wale watu wa kati
 
Kwahiyo mond wale mameneja wamefanya hayo yote ya kumlisha kachumbali, au wamemkuta tayari super brand.?
Mfano mzuri, mond kakaa muda na managers wake bila kutengana, but watu wa kati ameshagombana nao sana ndio yakatokea yale yaliyotokea
 
Meneja ni mwajiriwa wa msanii.
Executive producer ndiyo mwekezaji.
Producer ndiyo mwenye nyimbo na hakimiliki lakini anaweza kuiuza.
Msanii ni kama dancers tu, huwa analipwa chake anaondoka vilevile waandishi wa nyimbo, sound engineers etc ...
Hii kwa bongo sio sahihi kivile. Huku manager wapo wengi tu ndio wanaajiri msanii, mifano unayo
 
Unazungumzia Management au Jina Manager... Bongo hakuna mameneja Kuna masponser au matajiri only.

Kwani meneja ayafanye hayo yote ulioyaorodhesha.? Hapo hapo unasema biashara ya mziki ni kubahatisha kwahiyo msanii abaki Kwa meneja anaesubiria bahati.?

Waambie mameneja wenzako.. muwe mnaandaa mikataba yenyevfaida kotekote.. kama ilivyo Kwa wachezaji wa soka la kulipwa.. msainishen msanii mkataba utakaoonesha mnamlipa shing ngapi Kwa mwezi na nyie mkitumie kipaji chake kurudisha gharama Kwa muda mliokubaliwa Ili hata mkataba ukiisha Kila mtu awe amepata faida.

Leo unaongelea wasanii wanazingua wakati wakitemwa na hizo management wanabaki ombaomba na kuishi Kwa fedheha utazani hawakua na mikataba ya kazi.

Mameneja ndio wanazingua na ushahidi ni huu Utetee ukiweza..
Kwanini msanii akitoka katika management maisha yake yanadrop?

Anzeni kuwalipa Mishahara wasanii muone Kama Kuna atakaezingua. Sio MTU ajitungie wimbo wewe usubiri kumlipia studio wimbo uwe wako.. kweli? Kwahiyo hizi nyimbo tuzisikiazo nyakati hizi ni matokeo ya usimamizi mzuri wa menejiment za Bongo?

Bongo Hakuna Biashara ya Mziki so Meneja ni jina la mtu anaemlipia gharama mbalimbali msanii na sio MTU anaetumia kipaji Cha msanii husika Ili fedha ipatikane wagawane.
Unajua bongo hiki ulichozungumza kuna muda huwa ni vice versa. Wapo masponsor na wapo managers pia.

Na pia sii managers wote humlipia msanii kila kitu, wapo managers ambao kazi yao ni kusimamia tu msanii tayari ana pesa yake. Mfano tu Aidan ni meneja wa kiba, hebu niambie Aidan anamlipia nn kiba?

Chopa ni meneja wa harmonize, hebu sema kweli gharama za harmo zinalipwa na Chopa?

Bongo kila kitu kipo pande mbili, hivi na vile
 
Mkuu hebu tupe ufafanuzi,Diamond anajiweza kila kitu,kina Babu Tale na Said Fella wamemkuta jamaa tayari ana mpunga na ana chanel nyingi za hela,sasa msaada wao ni nini hasa kwa sasa. Kwa Sallam Sk naweza kusema walianza wote ,ila hao wazee wawili kazi yao pale ni nini hasa?
Yeye alijua umuhimu wake ndio maana akawatafuta wafanye kazi pamoja.
 
Ni kweli kwamba huwa kuna mameneja wanazingua lakini pia tusisahau kuna wasanii nao huwa wanazungua

Lazima tuelewa vizuri mazingira ya wasanii, management na soko kwa jumla.

Wasanii wengi wanapoianza kazi ya miziki wanakuwa hawajiwezi kwa lolote, Hivyo hulazimika kutafuta management itakayoweza kufanikisha kutimiza ndoto zao kwa kulipia gharama.

Msanii na Meneja hujikuta wakiingia mikataba nafuu kwasababu ya ualisia wa biashara yenyewe ya muziki siku zote huwa ya kubahatisha.

Ndio maana mameneja wengi huwa wanasifiwa kwa kumtoa msanii mmoja tu kati ya wengi alionao.

Kazi ya management hiyo kwanza ni kuhakikisha msanii anatunga nyimbo nzuri zitakazoenda kulitingisha soko, Baada ya hapo kulipia gharama za kurekodi audio na video, ikiwa ni pamoja na mavazi kuanzia unyayoni mpaka utosini.

Baada ya hapo kulipia promo kwenye radio na TV station zote ili nyimbo zipigwe kila kukicha, kisha linakuja swala la kum'brand msanii ili kumuongezea thamani angalau naye uonekane ni mtu fulani kati ya watu.
Katika hili ndipo pesa zinapoteketea kwani management ina wajibu wa kuhakikisha msanii anavaa vizuri kuanzia viatu hadi kofia, management pia uhakikisha msanii lazima akae kwenye nyumba nzuri inayoendana na hadhi ya kisanii, gharama za saluni na mahitaji muhimu ya nyumbani zikiwemo samani za nyumba nzima na chakula cha kila siku pamoja na usafiri.

Fahamu kuwa wakati haya yote yanafanyika, ni pesa ya meneja ndio inayoteketea. Promo inapokubali kwenye media, ndipo wanaanza kujitokeza watu wa pembeni na kuanza kumshika masikio msanii, Hapo ndipo maneno ya "unaibiwa wewe yaani nyimbo zimehit bado huna kitu?" Baadhi ya wasanii wengi huwa ni mambumbumbu kwani huwa wanakubali kujaa upepo kirahisi bila kujali gharama ilyotumika imerudi au bado.

Hii husababisha msuguano mkubwa kati ya meneja na msanii. Kwani hasara huwa ni kubwa kuliko faida.

Suala la hili lilikuwa fundisho kwa mameneja kadhaa huko nyuma ndio maana ujinga huo umefanyiwa marekebisho kwenye Lebo ya WBC, ukitaka kusepa lazima uzitapike kachumbari zote ulizokula !!.

Kuna muda wasanii ndio wanazingua !! Tatizo sio mameneja bali akili ya baadhi ya wasanii ni kama ya wadangaji, Hawana uchungu gharama waliyowekezewa, wanajiangalia wao tu.
Kwani kati ya meneja na msanii nàni boss?
 
Back
Top Bottom