Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Kisa kitamu saana hiki mkuu! Ni vyema ungeandika full halafu ukawa unaachia vipande au yoote kwa pamoja, ingeprndeza zaidi kuliko hivi kuandika ukipata nafasi, wakati mwingine nahisi kabisa hukuwa na mood ya kuandika ila kwa hofu ya wasomaji unajikuta unaandika kwa ufupi! Matumaini yangu kuna mengi umeyaacha! Kuna sehemu nasoma naona kabisa hapa muandishi kaufosi mkono, mengine unataka kuandika unasema tuache hayo! Umekuwa unaandika kwa ufupi na vipande vifupi. Bossless

Sikuwa na wewe ila naamini kuna visa vingi umeacha kusimulia.
Hilo hata mimi nimelioma jamaa angeachwa amgeansika story nzur lakini sasa analipua ili iishe kama wanavyotaka wenye haraka
 
Habari zenu wakubwa kwa wadogo.

Kwanza napenda kutoa pole na shughuli za kutwa kwa wale wahangaikaji wote kama mimi ambao kila siku lazima tutoke ili tuweze kujipatia riziki halali kila siku iendayo kwa mungu. Tuseme wote asante mungu.

Nisiwachoshe niende moja kwa moja kwenye mada,mdaa huu wakati naandika huu ushuhuda wangu binafsi ambayo nimeishuhudia kwa macho yangu mawili nchini rwanda wakati wa vita ya kikabila ,wenyewe hupenda kuiita mauji ya halaiki.

Stori inaanza wakati ndo nimemaliza masomo yangu ya uhasibu ngazi ya stashahada mwaka 1989 (sintotaja chuo hicho) nikajaribu kuomba kazi wizara ya mambo ya njee mungu si Athumani nikapata kazi ubalozi lakini nikapaangiwa kituo changu cha kazi kigali-Rwanda, kama sijasahau ubalozi Tanzania ulikuwa maeneo yanaitwa KICHUKIRO ,kwa sasa sijui kama bado upo palepale au vipi sina uhakika.

basi mwezi wa sita baada ya kukamilisha taratibu zote nikaanza safari ya kwenda Rwanda kituo changu cha kazi kipya,ajira mpya na mara ya kwanza kusafiri nje ya Tanzania... Safari ikaanza kwenda kuanza maisha mapya nchi ya watu ,mbali na ndugu jamaa na marafiki nikiwa sijui chochote kuhusu nchi hiyo..

Angalizo. naomba tuvulimiliane ni long stori kidogo na yanaweza jitokeza makosa ya kiundishi na kifasihi.... Ntaelezea mambo mengi sana ya kutisha ambayo niliyashuhudia kwa macho yangu mwenyewe ambayo hadi leo nimejitahidi kuyasahau lakini imeshindika kabisa.

Safari inaanza pale Mnazi moja nakumbuka enzi zile kulikuwa hakuna mambo ya Booking. unawahi alfajiri na mapema unatafuta basi lako unapanda tu unasubiri safari ianze.

Basi nikiwa na mabegi yangu na shilingi za kitanzania 60 elfu(nilipewa kwa ajili safari na kujikimu na passport ) tu ,naianza safari ya kwenda Kahama, safari ikaanza midaa ya kama saa moja kamili asubuhi (jina la basi lile nimelisahau ila nakumbuka lilikuwa rayland) kipindi hicho barabara ni vumbi tupu changarawe la vumbi hadi linaingia kupitia madirishani, baada ya safari ya uchovu mwingi hatimae saa nane usiku tunaingia singida stand. Mimi mgeni sijui niende uelekeo gani ikumbukwe miaka ile nyumba za wageni zilikuwa za kuhesabu basi ikabidi tushuke pale stand tukawa tunakula mikate na chai na wengine chai na kahawa.

Basi mimi nikarudi kulala kwenye gari,alfajiri na mapema gari likaanza safari tena nakumbuka tulifika stand kuu Kahama kana saa tatu usiku hivi. yani tulitumia kama siku mbili hivi Dar-kahama .leo hii dar - Kahama unatumia siku moja umefika halafu utasikia mtu anasema nchini hii bwana hakuna maendeleo kabisa daa!!!

Tumefika Kahama stand tumepokelewa na wapiga debe enzi hizo wao ndo walikuwa kama mawakala wa magari makubwa anakubebea mzigo hadi kwenye gari unalipa nauli yeye anachukua chake mnaachana hapo hapo hapo ni usiku inabidi kupata gari ya kwenda boda ya Rwanda na Tanzania Rusumo hapo unavuka Mpaka, kuna mto mkubwa unaitwa mto Rusumo unapita kwenye daraja la chuma kama lile lile liloejengwa na wanajeshi pale njia panda Kawe unavuka ng'ambo ukagonga passport ,cha kuchekesha pale kulikuwa hakuna magari ya abiria makubwa.

Magari ya abiria kutoka boda hadi kigali mjini yalikuwa hakuna, ilikuwa inakubidi upande roli la mizigo au abiria mjichange kwa makundi mkodi magari madogo kama tax ila mnabananishwa humo hatari na mizigo juu, kutoka boda hadi kigali ilikuwa kama mwendo wa masaa nane hivi kuingia kigali mjini.
Hatimae baada ya kubadilisha fedha zetu kuwa mafaranga tukapata usafiri wa kutufikisha kigali nakumbuka kundi langu kwenye gari tulilokodi nilipanda na wazaire watupu hivyo kelele zilikuwa nyingi hadi tunaingia kigali wanaimba nakuongea sanaa ubishi mwingi mara mpira mara siasa ili mradi makelele tu.

Saa tisa mchana nikawa tumewasili kigali town enzi hizo sijui lolote kuhusu mji huo zaidi ya address na namba za simu ikabidi niangaze angalau kupata simu lakini wapi,aise kinyarwanda sijui na wao kiswahili kigumu kila nae mujliza ila kupata mawasiliano sikupata msaada ikabidi nikasogolea kwenye stand ya mabus madogo nikamuulize konda kuwa nataka kwenda ubalozi wa Tanzania akaishia kucheka tu niligundua hakunielewa lugha .

Nakumbuka nilikaa stand pale hadi saa kumi na mbili bila bila ikabidi niulizie sehemu pakulala hapo nikaeleweka nikaambiwa lazima upande bus nipelekwe sehemu inaitwa NYAMIRAMBO na nikaambiwa pia kuwa kuna waswahili wengi nikapanda bus hadi nyamirambo nikashushwa tu stand konda akanionyesha kuna hoteli moja ilikuwa imeandikwa nakumbuka inaitwa kama sijasahau ilikuwa inaitwa IMHALA ila nyamirambo ilichanganya kigodo naweza fananisha Magomeni enzi zile.


Nikaenda nikalipia chumba nikaomba kuelekezwa eneo la kula nikaelekezwa, nikaenda nikala halafu nikarudi kujilaza nikipanga namna ya kuingia kesho u abalozi wa Tanzania kuanza majukumu mapya .

Itaendelea...........





Sent using Jamii Forums mobile app
Inaendelea.........

Wandugu habari mchana sasa tuendelee tulipoishia, ubalozini. Sasa maisha yakawa yamehamia ubalozini maisha yakawa changanyikeni maisha yakawa hayana thamani tena, wanaume wajasiri wakajitolea kukaa zamu kulinda geti la ubalozi, maji yakakata watu wanalala njee kwenye nyasi hakuna cha mume wala mke wa mtu kama una mkeka mnalala chini familia mbili, ile mandhari ya ubalozi ikageuka kuwa kama kambi ya wakimbizi majani ya kukauka yote, maua yakafaa vyoo vikaanza kuzidiwa maji hamna daaahhh watoto vilio usiku kucha, ukichanganya na milio ya risasi ya mara kwa mara ikawa ni kusubiri siku ifike tuone nini kitakachotokea .

Sasa kuna mambo yalikuwa yanaendelea huku tanzania, kulikuwa sijui kuna vikao vya mazungumzo sijui ya amani kati ya serikali ya rwanda na waasi kama sijakosea alikuja habyarimana mwenyewe na baadhi ya mawaziri wake na wakati tunasikiliza redio bbc jioni anatoka kwenye kikao kuna maneno Aliyatamka hakika kuanzia siku hiyo niliwachukia Wanyarwanda wote, mungu anisamehe.

Alisema hivi watanzania na wageni wote nchini rwanda wako salama wala hakuna lolote linaloendelea baya kwao na serikali inaendelea kuwalinda, na maneno kuwa nchi imeingiwa na machafuko ni propaganda za waasi wa Kagame kujaribu kuishawishi dunia ili imuunge mkono katika hatua yake ya kuivamia rwanda na apuuzwe. Na siku hiyo ndo ilikuwa mwisho wa kusikiliza redio maishani mwangu, utamaduni ambao nimeendelea nao hadi sasa huwa sisikilizi redio kabisa,yani nikija kwako kukutembelea ukitaka kunifukuza kwako washa redio naondoka hapo hapo.

Watu wakawa wengi chakula kikawa kimeisha.tukafanya mawasiliano na balozi,sasa kuna kitu kilikuwa kinaendelea ambacho tulikuwa hatujui. unawakumbuka wale jamaa saba alikuwepo moja kama mpemba hivi siku hiyo alikuja na balozi, pale akaangalia hali halisi wakaingia ndani walichoengea na balozi hatujui ila wakatoka wakaondoka hapo wote tukabaki tunatazamana hakuna anaejua nini kinaendelea.

Sasa ipo hivi hakuna watu wabaya kama wafanyabiashara lakini walikuwa na msaada mkubwa unajua kama sio wafanyabishara wa maroli tungekuwa tumeondoka mda mrefu ila kukawa na zuio kuwa maroli yote ya watanzania ambayo yalikuwa bandari kavu eneo la MAGERWA (tamka majerwa) lazima yarudi na madereva wake wote sasa ikawa kuna mengine yalikuwa hayajapakua ililazimu yapakue na, ndo walipokuwa wale manjemba saba waliokuja na defender nilikuja kuambiwa baadae na dereva moja hivi lakini nae alikuwa anawaona tu wanazungukazunguka mle ndani ya bandari ila wakiwa makini kweli kweli na mabegi yao.

Siku zikayoyoma ikawa kila siku lazima balozi awashe gari lake aende Majerwa( bandari kavu) Peke yake anapakia tambi, majani ya chai maziwa ya kopo, na mazagazaga mengine waliyokuwa wanashusha kwenye maroli ya watanzania analeta tunakula siku imeisha mlo moja tu hakuna cha mama anayenyonyesha wala wala mtoto ni mlo moja tu basiii.siku zikawa zinakwenda ikawa sasa inakaribia siku yenyewe sasa ambayo iliweka historia nchini rwanda....................

Mwanzo wa safari ya mateso, kutembea katika njia ya mauti, kushuhudia maiti zimezaga barabarani kama nzige ,unyama mbaya kuwahi kuushudia maishani mwangu.....

Itaendelea............. Leo leo.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii imekuwa fupi, unatuacha na uraibu
Inaendelea.........

Wandugu habari mchana sasa tuendelee tulipoishia, ubalozini. Sasa maisha yakawa yamehamia ubalozini maisha yakawa changanyikeni maisha yakawa hayana thamani tena, wanaume wajasiri wakajitolea kukaa zamu kulinda geti la ubalozi, maji yakakata watu wanalala njee kwenye nyasi hakuna cha mume wala mke wa mtu kama una mkeka mnalala chini familia mbili, ile mandhari ya ubalozi ikageuka kuwa kama kambi ya wakimbizi majani ya kukauka yote, maua yakafaa vyoo vikaanza kuzidiwa maji hamna daaahhh watoto vilio usiku kucha, ukichanganya na milio ya risasi ya mara kwa mara ikawa ni kusubiri siku ifike tuone nini kitakachotokea .

Sasa kuna mambo yalikuwa yanaendelea huku tanzania, kulikuwa sijui kuna vikao vya mazungumzo sijui ya amani kati ya serikali ya rwanda na waasi kama sijakosea alikuja habyarimana mwenyewe na baadhi ya mawaziri wake na wakati tunasikiliza redio bbc jioni anatoka kwenye kikao kuna maneno Aliyatamka hakika kuanzia siku hiyo niliwachukia Wanyarwanda wote, mungu anisamehe.

Alisema hivi watanzania na wageni wote nchini rwanda wako salama wala hakuna lolote linaloendelea baya kwao na serikali inaendelea kuwalinda, na maneno kuwa nchi imeingiwa na machafuko ni propaganda za waasi wa Kagame kujaribu kuishawishi dunia ili imuunge mkono katika hatua yake ya kuivamia rwanda na apuuzwe. Na siku hiyo ndo ilikuwa mwisho wa kusikiliza redio maishani mwangu, utamaduni ambao nimeendelea nao hadi sasa huwa sisikilizi redio kabisa,yani nikija kwako kukutembelea ukitaka kunifukuza kwako washa redio naondoka hapo hapo.

Watu wakawa wengi chakula kikawa kimeisha.tukafanya mawasiliano na balozi,sasa kuna kitu kilikuwa kinaendelea ambacho tulikuwa hatujui. unawakumbuka wale jamaa saba alikuwepo moja kama mpemba hivi siku hiyo alikuja na balozi, pale akaangalia hali halisi wakaingia ndani walichoengea na balozi hatujui ila wakatoka wakaondoka hapo wote tukabaki tunatazamana hakuna anaejua nini kinaendelea.

Sasa ipo hivi hakuna watu wabaya kama wafanyabiashara lakini walikuwa na msaada mkubwa unajua kama sio wafanyabishara wa maroli tungekuwa tumeondoka mda mrefu ila kukawa na zuio kuwa maroli yote ya watanzania ambayo yalikuwa bandari kavu eneo la MAGERWA (tamka majerwa) lazima yarudi na madereva wake wote sasa ikawa kuna mengine yalikuwa hayajapakua ililazimu yapakue na, ndo walipokuwa wale manjemba saba waliokuja na defender nilikuja kuambiwa baadae na dereva moja hivi lakini nae alikuwa anawaona tu wanazungukazunguka mle ndani ya bandari ila wakiwa makini kweli kweli na mabegi yao.

Siku zikayoyoma ikawa kila siku lazima balozi awashe gari lake aende Majerwa( bandari kavu) Peke yake anapakia tambi, majani ya chai maziwa ya kopo, na mazagazaga mengine waliyokuwa wanashusha kwenye maroli ya watanzania analeta tunakula siku imeisha mlo moja tu hakuna cha mama anayenyonyesha wala wala mtoto ni mlo moja tu basiii.siku zikawa zinakwenda ikawa sasa inakaribia siku yenyewe sasa ambayo iliweka historia nchini rwanda....................

Mwanzo wa safari ya mateso, kutembea katika njia ya mauti, kushuhudia maiti zimezaga barabarani kama nzige ,unyama mbaya kuwahi kuushudia maishani mwangu.....

Itaendelea............. Leo leo.



Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa heshima na tahadhima mkuu naomba usitumie kingereza, kiache tu kipumzike, ni hayo tu.
Inaendelea.........

Habari za mchana wandugu ,sasa tuendelee leo ntajikita kuelezea matukio mbalimbali ya unyanyasaji, uonevu, mauji, uporaji ulianza kujitokeza . nitajitahidi kuelezea niliyoyashuhudia kwa macho yangu ya yaliyotutokea sisi kama sisi maoneo ya kazi... (ubalozini). Haya matukio yamejaa kichwani kwangu kwa kipindi cha mda wa miaka mingi hadi huwa yananikoseha raha wakati mwingine naota kabisa hadi na weweseka vibaya ndugu zangu msiombe vita narudia tena usiombe vita ( utasikia kijana humu anasema bora kinuke aise tema mate chini).

Tukio la kwanza -: hii ilikuwa kipindi hicho hicho mwaka 1992 kama sijasahau mwezi wa nne hivi kama unavyojua mpaka hapo tayari nimeshakuwa na Demu mweupe mfupi kiasi ila alikuwa mzuri ( hapo naona vijana wa mambo yetu wanaanza kutabasamu hhhhaaaa ...) nikiwa nae kwenye mahusiano kama miezi minne hivi sasa kukawa kuna sehemu moja hivi town kulikuwa linapigwa disco kama lile lilokuwa linapigwa pale mikocheni (blue palm eneo dogo lakini weekend wanakaa watu nyomi hatari mziki unapigwa balaa,kwaa taarifa tu eneo lile lilikuwa haliguswi na Askali yeyote yule au interahamwe au kwenda pale kuanzisha vurugu unajua kwanini? Eneo lile ni la Kada wa eneo lile mtemi na msumbufu aliitwa Nyihibilazi (balozi) na disko la kwake sasa mnanza aje? Kwanza mlangoni ukiingia unakuta Askali wake wana AK 47 na magrouneti yapo nje nje.

Basi disko likapigwa kufika mida kama saa kumi hivi nikamwambia demu wangu tuondoke enzi hizo tunakula Mai hatari (pombe) kwa kwenda mbele mzee unakula primus hadi unazima watu wanakubeba kukurudisha nyumbani, basi mtu mzima nikashika chombo( demu) yangu kiuno nikawa nashuka nayo lami kutokea ukumbini kama kuna kilima unashika unaenda lami kuu ndo unasimamisha texi ya kurudi home ,ile namalizia tu kilima kile kwa mbele kidogo nikaona Toyota hilux inakuja wamejaa interahamwe tupu na mabunduki i yao .
Kufika tu mbele wakasimama wakawa wanarudi nyuma aise asikwambie mtu pombe inaleta ujasiri,nikamwambia demu wangu hakuna kuongea chochote hata akiuliza jina lako labda aulizwe kwa kiingereza au kiswahili ndo ajibu, siku hiyo alivaa tisheti yangu zile za watalii zimeandikwa HAKUNA MATATA zilikuwa sinatengenezwa kenya kama sijasahau, basi majama yakawa yamefika pale kwanza wakaanza kukoki mibhnduki yao ebwaanae nikasema sasa tumekwisha lakini niwaambie mwanaume kama una mapenzi na demu wako aise hata itokee hatari gani lazima unamtetea tu hata kama kuna hatari kiasi gani basi swala la kwanza wakatuuliza tulipitokea niliwajibu disko wakasikia refudhi yangu ya kiswahili wakasema nyinyi ni waswahili? Nikamjibu ndio wakauliza watz yani watanzania wanafupisha nane tz nikasema ndo kumbuka nilimwambia demu asiongie hata akipigwa kibao, moja anaiuliza na huyu mugole? (Mugole-ni mwanamke nikamjibu mke wangu) kumbuka hapo kinyarwanda nimeshaanza kukipata pata ila kuongea ikawa shida kidogo, sasa ikatokea ubishi miongoni mwao baadhi yao wakawa wanahisi yule si mtz ni mnyarwanda wengine wakawa wanananiamini mimi hapo sasa ndo kimbembe kilipoanza

Vuta ni kuvute kumlazimisha demu aongee demu anasem na mimi nawaambieni huyu hawaelewi nyinyi huyu ni mtz kwanza haelewi mnaongea nini wakaomba ID ninatoa passport jina moja wakaomba ID ya demu ikiwaambia ipo ubalozini kama vipi twende nikawaonyeshe wakagoma ,demu waNgu yupo kimyaa, sasa ipo hivi yule demu naweza mfananisha na kama msanii Menina ya ni mweupe ana sifa zote za kitusi ila pua lake tu ni pana kidogo kama unavyomuona Menina ,sasa wakawa wanashindwa wafanye nini kumchukua hawawezi wanahisi ni mtz sasa mimi wakati huo nachapa kiswahili hatari na vijimaneno vya hapa na pale ghafla ukaingia ujumbe kwenye redio call yao nikasikia maneno flani nikaona wanaitana wakapakiana kwenye gari na kuondoka pale pale nikawahi texi tukarudi nyumbani na sikumpeleka kwao nilienda kulala( ikawa furaha tosha kwetu kwa usiku huo naona vijana wanatabasamu hapa hhhaaaaa.....) hakika yule demu alinipenda sanaa kwa lile tukio akaja akawa anawahadithia ndugu zake pale mtaani tukawa vile mke na mume aise anakuja nyumbani anytime mungu amsaidie huko aliko kwani tulipoteana tu uenda simu zingekuwepo au mitandao tungetafutana ( jina kapuni) ntaalezea baadae tulivyopoteana vita.. vita ...vita ..baba mbaya sanaa sasa sijui yuko hai au alishakufa ? Maisha yakaendelea...

Tukio la pili-: nilishuhudia saa nane mchana eneo la birjogo( tamka bijogo) hiace nzima ya abiria watu wakashushwa wanapigwa fimbo wakachambuliwa wakatolewa INYEZI ( inyezi maanake mende yani Watusi) wakatandikwa virungu vya kufaa mtu sasa hapo niliona kada (balozi )hilo analisimamia mwenyewe, sasa utamtambuaje balozi katikati ya interahamwe? Yeye anakuwa amevaa belleti nyekundu na shati la chama aisee wale watu walipigwa walikatwakatwa na mapanga huku watusi wakipata mateso makali sanaa ,unajua kwanini ?nilikuja kugundua baadae sanaa kwanini Watusi wanateswa. Sasa ipo hivi wakati Rpf wanaanza chokochoko walikuwa wanapewa taarifa na Watusi wa ndani n baadhi ya ndugu zao wanaume walikuwa wanaenda kwa siri kupata mafunzo maeneo mbali mbali karibu na walipokuwa waasi sasa taarifa hizo zikawa zinawafikia mabalozi mbalimbali nao wanazisambaza kwa interahamwe sasa usiku unashangaa unavamiwa na hao jamaa wanakula kisago halafu wanaondoka na wewe ni ndo imetoka hakuna anaejali basi wakawakatakata mapanga wale Watusi pale shell kituoni cha mafuta hadi leo picha hii huwa hainitoki akilini kuua kwa mapanga zaidi ya watu 12 wanauawa machoni mwangu kweupe pakavu jua la saa saba mchana then nobody care .

Nimesema hapa leo naweka matukio....ya kinyama.

Itaendelea jioni hii......................... Msichoke.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu na wewe ulikuwepo huko?
Hapana Mkuu, jamaa zangu ndiyo walikutana na mkasa huo mbaya,
Avatar yangu inaelezea mengi Mkuu,hapo ni makumbusho yalipowekwa mafuvu ya wahanga wa lile tukio baya kuwahi kutokea.

Mwenyezi Mungu awarehemu,wapumzike kwa amani Ameen..
 
Hapana Mkuu, jamaa zangu ndiyo walikutana na mkasa huo mbaya,
Avatar yangu inaelezea mengi Mkuu,hapo ni makumbusho yalipowekwa mafuvu ya wahanga wa lile tukio baya kuwahi kutokea.

Mwenyezi Mungu awarehemu,wapumzike kwa amani Ameen..
Dah pole ni wabongo au warwanda ?
 
Hapana Mkuu, jamaa zangu ndiyo walikutana na mkasa huo mbaya,
Avatar yangu inaelezea mengi Mkuu,hapo ni makumbusho yalipowekwa mafuvu ya wahanga wa lile tukio baya kuwahi kutokea.

Mwenyezi Mungu awarehemu,wapumzike kwa amani Ameen..
Na hakuna alorudi salama akakupa mkasa?
 
Back
Top Bottom