Singida Mashariki, Kazi anazofanya Miraji Mtaturu, Lissu tafuta jimbo lingine

Mwanahabari wa Taifa

JF-Expert Member
May 27, 2020
1,450
799
====
Pamoja na kuwa Jimbo la Singida Mashariki lilisalia mikononi Mwachadema kwa zaidi ya mwongo mmoja ajabu ni kwamba baadhi ya maeneo ya jimbo hilo kwenye karne hii ya Sayansi na tekinologia watu walikuwa bado wakiwasiliana kwa kutumia "Barua " kwani hawakuwa na minara ya simu,

Ujio wa Mhe Miraji Mataturu Singida Mashariki umebadili kabisa mitazamo na utendaji wa wananchi wa jimbo hilo lililokuwa taabani karibu katika kila idara ya maendeleo ya watu na vitu,

Hivi majuzi Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Tekinolojia ya Habari Mhe Eng Kundo Andrew alifanya ziara kwenye kata ya Misughaa wilaya ya Ikungi,

Lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa mnara wa simu unaojengwa na Kampuni ya TTCL kwa Usimamizi wa Mbunge Miraji Mtaturu,

Kukamilika kwa mnara huo kutatatua changamoto ya muda mrefu ya mawasiliano kwenye kata za Misughaa, Kikio na Ntuntu zote zilizokuwa chini ya CHADEMA kwa miaka nenda rudi uje,

Naibu Waziri aliwaeleza wananchi wazi kuwa Maombi ya kujenga Mnara huo yaliwasilishwa Wizarani na Mhe Miraji Mtaturu Mbunge wa Singida Mashariki mwaka 2019.

"Leo mnafaidika na Umahiri na Uwajibikaji wa Mbunge wenu,"

"Nimemsikia Mbunge wenu amewaeleza lengo la Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe Samia Suluhu Hassan ni kumaliza miradi yote iliyoanzishwa na serikali ya awamu ya tano ukiwemo mradi huu " alisema Naibu Waziri

Kwa upande wake Mbunge wa Singida Mashariki Mhe Miraji Mtaturu amemshukuru Naibu Waziri kwa kufanya ziara jimboni kwake na kuwaeleza wazi wananchi juhudi zake katika kuwaletea maendeleo endelevu,

Alitumia fursa hiyo kumshukuru pia Rais Samia Suluhu Hassan kwa kukubali fedha ziletwe kukamilisha mradi huu muhimu kwa maendeleo ya wananchi kwani itarahisha na kuharakisha mawasiliano na biashara sambamba na usalama wa WanaSingida Mashariki.


HUYU MBUNGE MIRAJI MTATURU NI HAZINA KWA MKOA WAKE NA TAIFA,
 
Matako yako mleta mada na Mtatulu wako, Mtatulu alipewa ubunge n Magufuli Tundu Lissu alichakuliwa na wapiga kura wa jimboSingida mashariki
 
Naona unapiga misele...



1646533994598.png



1646533874055.png
 
Nimeisha elewa kumbe washikaji wanalilia mnara wa simu wakati simu zenyewe hawana mna propaganda za kitoto sana
 
Zungumzia majimbo yaliyokaliwa na CCM tangu uhuru na ni maskini ya kutupwa
 
Tuambie singida Magharibi inamawasiliano??
Hii ndio haijawahi hata kuwa na mwenyekiti wa Kijiji asiekuwa ccm
 
Matako yako mleta mada na Mtatulu wako, Mtatulu alipewa ubunge n Magufuli Tundu Lissu alichakuliwa na wapiga kura wa jimboSingida mashariki
Kumbe Tundu Lissu 2020 aligombea Urais na Ubunge wakati mmoja? Maana kabla ya hapo Mtatulu alikuta Jimbo likiwa wazi baada ya Ndugai kufanya mambo yake.
 
====
Pamoja na kuwa Jimbo la Singida Mashariki lilisalia mikononi Mwachadema kwa zaidi ya mwongo mmoja ajabu ni kwamba baadhi ya maeneo ya jimbo hilo kwenye karne hii ya Sayansi na tekinologia watu walikuwa bado wakiwasiliana kwa kutumia "Barua " kwani hawakuwa na minara ya simu,

Ujio wa Mhe Miraji Mataturu Singida Mashariki umebadili kabisa mitazamo na utendaji wa wananchi wa jimbo hilo lililokuwa taabani karibu katika kila idara ya maendeleo ya watu na vitu,

Hivi majuzi Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Tekinolojia ya Habari Mhe Eng Kundo Andrew alifanya ziara kwenye kata ya Misughaa wilaya ya Ikungi,

Lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa mnara wa simu unaojengwa na Kampuni ya TTCL kwa Usimamizi wa Mbunge Miraji Mtaturu,

Kukamilika kwa mnara huo kutatatua changamoto ya muda mrefu ya mawasiliano kwenye kata za Misughaa, Kikio na Ntuntu zote zilizokuwa chini ya CHADEMA kwa miaka nenda rudi uje,

Naibu Waziri aliwaeleza wananchi wazi kuwa Maombi ya kujenga Mnara huo yaliwasilishwa Wizarani na Mhe Miraji Mtaturu Mbunge wa Singida Mashariki mwaka 2019.

"Leo mnafaidika na Umahiri na Uwajibikaji wa Mbunge wenu,"

"Nimemsikia Mbunge wenu amewaeleza lengo la Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe Samia Suluhu Hassan ni kumaliza miradi yote iliyoanzishwa na serikali ya awamu ya tano ukiwemo mradi huu " alisema Naibu Waziri

Kwa upande wake Mbunge wa Singida Mashariki Mhe Miraji Mtaturu amemshukuru Naibu Waziri kwa kufanya ziara jimboni kwake na kuwaeleza wazi wananchi juhudi zake katika kuwaletea maendeleo endelevu,

Alitumia fursa hiyo kumshukuru pia Rais Samia Suluhu Hassan kwa kukubali fedha ziletwe kukamilisha mradi huu muhimu kwa maendeleo ya wananchi kwani itarahisha na kuharakisha mawasiliano na biashara sambamba na usalama wa WanaSingida Mashariki.

View attachment 2140473
HUYU MBUNGE MIRAJI MTATURU NI HAZINA KWA MKOA WAKE NA TAIFA,
Anajihami kwa propaganda ....pumbaf zake
 
Back
Top Bottom