Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Klabu ya Singida Black Stars imewasilisha rasmi malalamiko kwa mamlaka za soka nchini, ikiwemo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), baada ya kutoridhishwa na mwenendo wa mchezo wao dhidi ya Simba SC uliochezwa jana Mei 28 kwenye Uwanja wa KMC Complex.
Katika mchezo huo, Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0, bao pekee likifungwa na mshambuliaji Steven Mukwala dakika ya 42. Ushindi huo umeiwezesha Simba kufikisha alama 72 na kuendelea kushika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC, ikiwa pointi moja nyuma ya vinara Yanga SC walio na pointi 73. Timu zote zimecheza michezo 27.
Kwa upande wao, Singida Black Stars wamesalia katika nafasi ya nne wakiwa na pointi 53 baada ya mechi 28.
Afisa Habari wa klabu hiyo, Hussein Massanza, amethibitisha kuwa wamechukua hatua hiyo ili kutafuta haki kufuatia kile walichokieleza kuwa ni vitendo vilivyoathiri ushindani wa haki katika mchezo huo.
Katika mchezo huo, Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0, bao pekee likifungwa na mshambuliaji Steven Mukwala dakika ya 42. Ushindi huo umeiwezesha Simba kufikisha alama 72 na kuendelea kushika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC, ikiwa pointi moja nyuma ya vinara Yanga SC walio na pointi 73. Timu zote zimecheza michezo 27.
Kwa upande wao, Singida Black Stars wamesalia katika nafasi ya nne wakiwa na pointi 53 baada ya mechi 28.
Afisa Habari wa klabu hiyo, Hussein Massanza, amethibitisha kuwa wamechukua hatua hiyo ili kutafuta haki kufuatia kile walichokieleza kuwa ni vitendo vilivyoathiri ushindani wa haki katika mchezo huo.