Sina hamu na tra uwiiii

Sina hamu na tra uwiiii

mdache

Member
Joined
Jan 10, 2014
Posts
21
Reaction score
1
Nimekusanya vsenti vyangu nikaagiza gari japani, sijakaa sawa uchakavu ukawa miaka nane ikabidi nijichange tena ili gari lisije likaozea bandarini, documets zimekuja TRA wame uplift CIF ina maana kodi inazidi kuwa kubwa zaidi. Jamani hii tanzania tunaenda wapi jaman, TRA SINA HAMU NA NYINYI
 
pole sana mkuu....hii ndiyo tanzaniaaa mnyonge ananyongwa na haki yake hapewi anaishiaaaa kudhulumiwa...
 
yaani mtu unatafuta hela kwa malengo lakini kinachofanyika unajikuta umechoka yaani sina hamu
 
Ingezidi miaka 10 ndio ungefilisika mkuu.
 
ni kawaida, masikini azid kua masikini na Tajiri zaidi kua Tajiri.
siku zote masikini ndo wanaolipa zaidi Kodi hapa tanzania. mnakumbuka issue ya kukwepa Kodi ya home shopping cetre imeishaje? ile ya dhandho kukwepa Kodi alipokua anatoa vichwa vyake vya malori, aliyoisimamia Mwakyembe?
Nakumbuka wale mabinti walimjibu Waziri "tumetumwa na wakubwa, sisi tunatimiza wajibu wetu"
 
Tanzania ni nchi pekee duniani ambayo mwananchi anaagiza kitu nje bila kujua ushuru wake itakuwa ni kiasi gani,ndio maana biashara ya Import/ Export inakuwa ngumu sana zaidi kama wewe ni mgeni hujui njia za wale 'wazoefu' wanazotumia pale bandarini.Gari zinauzwa bei rahisi kwenye nchi zisizo na bandari [Rwanda,Burundi,Uganda nk]kuliko zinavyouzwa hapa kwetu,kuna Toyota Harrier ya mwaka 2007 ilitolewa juzi ushuru pekee ulikuwa 14ML na bado unazungushwa ili jamaa zao wapate pesa ya storage.
 
Hivi kwanini serikali mambo mengine inawekaga sheria bila kutafakari kwanza? nchi zingine zimeweka kodi kubwa ya uchakavu kwa nia kwamba watu wanunue magari mapya yanayotengenezwa nchini mwao ili kukuza uchumi wa nchi usika. sasa nyie TRA mnaweka mikodi mikubwa kwa vigezo gani? sana sana mnasema eti magari yamekuwa mengi, mi naona uo ni mtazamo (-), mnadanganywa na vibala bala vidogo vya magufuri mdo mnaona magari ni mengi?

kabla hamjatupandishia mikodi mikubwa ya uchakavu, angalia uchumi wa wananchi wenu, mimi nafikiri mwanzilishi wa kuwepo kwa sheria duniani alikosea, isingekuwepo sheria yaani mimi TRA wote ningewachapa makofi kabisa.
 
Nimekusanya vsenti vyangu nikaagiza gari japani, sijakaa sawa uchakavu ukawa miaka nane ikabidi nijichange tena ili gari lisije likaozea bandarini, documets zimekuja TRA wame uplift CIF ina maana kodi inazidi kuwa kubwa zaidi. Jamani hii tanzania tunaenda wapi jaman, TRA SINA HAMU NA NYINYI

Pole mkuu. CIF ilikuwa dollar ngapi na hapa wakapandisha kiasi gani?
 
mkuu umeagiza gari gani.. mimi leo nimefanya assessment ya kigari changu nimeshukuru cif hawaja uplift japokuwa uchakavu nimepigwa kodi kama kawa..

tatizo huu uchakavu kwa gari za 2005 umekuja kwa kushtukiza
 
Back
Top Bottom