TAECOLTD
JF-Expert Member
- Mar 2, 2013
- 1,051
- 1,844
Story : ZAFEERA
Mwandishi : Gerald Mtenga
Mawasiliano : 0625600802
Barua pepe : gmtenga@gmail.com
UTANGULIZI :
Bila shaka hakuna binadamu anayependa kuishi maisha ya kimasikini na ya kujidhalilisha mbele ya jamii lakini tukatae au kukubaliana na ukweli kuwa uwezo wa watu umetofautiana sana. Umasikini uliokithiri ndiyo chanzo cha matatizo mengi katika jamii zetu kama ujambazi, ukahaba, utapeli, uchawi n.k na vijana wanahangaika usiku na mchana kuweza kujikomboa na mkono wa jinamizi wa umasikini anayewakaba koo ,na wengine wakikimbia maisha ya mjini na kuelekea vijijini na kuishia kwenye tufani la umasikini mkubwa. Hii ndiyo sababu kubwa iliyomfanya kijana Gerald anayetokea katika maisha ya kimasikini kujiapiza kwamba atahakikisha anaukamata utajiri kwa nyanja yoyote na kufanikiwa kupindua historia ya ukoo wao ambao haujawahi kuwa na msomi wala tajiri yeyote. Katika kitabu hiki utaona namna Zafeera anavyomsababishia kijana Gerald kuharibu njia zake hapa ulimwenguni na kuishia kwenye majuto makubwa.
Ilikuwa vipi mpaka akafanikiwa kufikia ndoto zake na hatimaye kuziharibu mwenyewe? Fuatana na mimi katika kitabu hiki mwanzo hadi mwisho ili uweze kuburudika na kujifunza mambo mengi ambayo yatakusaidia wewe kuweza kutambua mambo ambayo yalikuwa kama ukungu mzito uliokuwa umetanda katika mboni za macho yako. Ikumbukwe majina yote yaliyotumika katika kitabu hiki ni ya kusadikika na kumrathi kwa yeyote atakayekuta jina lake hapa, atambue ya kwamba sijamlenga yeyote katika stori hii.
SEHEMU YA 1:
Ilikuwa ni siku ya jumamosi tulivu kabisa ya mwaka 2006 nikiwa nimepumzika pembezoni mwa ufukwe wa bahari ya Hindi jijini Dar es salaam, na kutafakari mahala maisha yangu yalipotoka mpaka hapa nilipo na kujaribu kupanga na kutafakari mambo yangu ya maisha tangu awali hadi huko siku za usoni. Nikiwa nimezama katika wimbi la mawazo ghafla lilinijia wazo zuri ambalo ilinibidi kulitekeleza ipasavyo, kutokana na hali ya maisha yangu kuwa ya kawaida sana hivyo wazo langu ilikuwa ni kuanzisha banda la kuuza nguo na mashuka ya mtumba.
Nilitafakari kwa muda mrefu na jua lilikuwa limekwishapata usingizi na kufumba macho yake barabara, hivyo ilinilazimu kujinyanyua mahala pale kwani hata wasimamizi wa ufukwe ule walikuwa wakiwaondoa watu eneo la ufukwe kwa muda ule hivyo kuamua kutafuta usafiri wa kurudi nyumbani. Kwa kuwa nilikuwa ufukwe wa koko maeneo ya msasani na maskani yangu yalikuwa ni pande za manzese, niliamua kupanda gari za masaki-kariakoo na gari ilipofika magomeni hospitali niliteremka na kuanza kutembea kuelekea kituo cha usalama ili nipande gari za ubungo.
ITAENDELEA...
SEHEMU YA 2:
Ilikuwa ni mida ya saa moja usiku nikiwa natembea taratibu kuelekea kituo cha basi ambapo ningepanda gari na kufika nyumbani. Nilikuwa na shauku ya kufika mtaani ili niende kwa rafiki yangu Regan ambaye alikuwa ni rafiki na pia kaka yangu mkubwa, nilitaka nimdokeze wazo langu ambalo kwa wakati huo niliamini lilikuwa wazo zuri kupita mawazo yangu ya awali. Nikiwa nakunja kona ya magomeni kwenye ukuta wa hospitali ya magomeni niliona kitu ardhini kikiwa kinang’aa sana.
Nilipiga hatua kadhaa za haraka haraka na kukiinamia kile kitu na kukiokota haraka sana kisha nikaanza kutazama kushoto na kulia kama mwizi aliyetoka kuvunja nyumba na kuiba vito vya thamani. Simu yangu ya kichina iliyokuwa na tochi kali ilinisaidia barabara kuweza kukitazama kile kitu nilichokiokota na maneno yakawa wazi yakisomeka "Zafeera" na maneno mengine ya kilugha ambacho sijawahi kukiona labda sababu sikuwa na elimu kubwa hivyo lugha ile ilinipiga chenga. Kichuma chenyewe kilikuwa na rangi ya dhahabu huku kikiwa kinang’aa sana kikiwa na muonekano wa tofauti na vyuma nilivyowahi kuviona iwe kwenye televusheni au magazetini.
ITAENDELEA...
SEHEMU YA 3:
Baada ya kujirithisha kwamba kile kichuma nilichokiokota kilikuwa na uashiria wa asilimia kubwa kuwa ni dhahabu niliangalia tena pande zote safari hii nikiwa na mashaka kama kuna mtu yeyote aliniona wakati nikikiokota kitu kile. Nilipojiridhisha ya kwamba hakuna aliyeniona niliamua kukihifadhi vizuri kwenye mfuko wa ndani ya suruali yangu (si unajua sisi masikini nguo zetu zinakuwa na mifuko mingi hadi ya ndani ya nguo ili kuhifadhi akiba zetu zisipotee kirahisi).
Baada ya kuhakikisha nimekihifadhi vyema mfukoni nilianza kutembea kwa madaha huku nikiachia tabasamu la ushindi na kuamini kuwa ndio mwanzo wa mafanikio yangu. Niliamini kuwa iwapo ningeenda kukiuza basi ningepata fedha nyingi ambazo zingeniwezesha kufanya biashara kubwa, niliamua kumpigia simu mshikaji wangu Regan kwa migoko mikubwa ili kujua kama yupo chumbani kwake ama kijiweni tunapopenda kukaa jioni baada ya shughuli za kutwa nzima.
“Oyoo, niaje mwanangu mwenyewe?”
“Freshii tu kaka Gerald, vipi?”
“Poa poa mwana, umejiachia pande zipi wewe?”
“Nipo geto tu nimejinyosha kitandani maana najisikia hovyo sana kaka na ndio maana leo maskani nimeshindwa kupanda”
“Aaaah unaumwa wapi wewe, utakuwa umeshapata dawa zako ndio maana umeamua kuvutia stimu magetoni kama kawaida yako”
“Unanirushia njiwa mwana, leo sijapata dawa kabisa maana sijapanda maskani na kama nilivyokuambia najihsi mwili mzima naumwa.”
“Hah hah hah hah hah hah wewe huyo siku ipite hujapata dawa? Labda unataka kuanza kuniuzia chai kama sikujui vile”
ITAENDELEA...
SEHEMU YA 4:
“Hah hah hah hah haya bwana, tuachane na hayo nipe habari zingine”
“Poa poa mimi nipo magomeni hapa nakuja maskani hapo maana nina bonge la dili na wazo la msingi mtu wangu”
“Aaah we Gerald nimeshakuzoea siasa kibao mshkaji wangu, unanirushia stimu tu”
“Mwana we ngoja nije dakika kama kumi hivi nitakuwa hapo, maana hata salio lenyewe linakata sasa hivi”
“Haina kwere kaka, nakusubiria”
Nilivuka barabara na kuelekea upande wa kituo cha magari ya ubungo na kusimama maeneo yale kungojea usafiri. Kama ilivyo kawaida ya usafiri wetu wa jijini ulivyo mgumu, kila basi lililokuja kituoni pale lilikuwa limeshiba abiria mpaka pomoni. Usafiri unapokuwa mgumu ni kawaida kwa wenye magari yao binafsi kusimamisha magari yao kituoni na kutangaza kwa uchu mkubwa bei zao wanazopendezwa nazo. Kwakuwa nilikwishasimama pale kituoni zaidi ya nusu saa hivyo nilikata shauri na kuamua kupanda gari za watu binafsi kwa bei mara tatu zaidi ya nauli za mabasi ya kawaida.
Gari ilikata vituo kadhaa kwa mwendo wa wastani kuashiria kwamba dereva alikuwa mstaarabu na mjuzi, ilipofika tip-top niliomba kushushwa na dereva bila hiyana alisimamisha gari na nilimlipa haki yake kisha nikateremka na kuanza kuelekea nyumbani. Nilinyoosha na ile barabara moja kwa moja mpaka kuifikia njia ya mabibo kisha nikakunja kona na kupiga hatua kama ishirini nikawa nimefika maeneo anayoishi mshakaji wangu Regan. Nilibisha hodi pale mlangoni na nilisikia sauti kwa ndani ikiniashiria niingie ndani, niliingia ndani na kumkuta jamaa akiwa amejilaza kitandani huku akitazama luninga.
“Yani jamaa yangu tangu saa moja umenipigia simu na kuniambia dakika kumi utakuwepo lakini hapa saa zima limepita ndio dakika kumi za siku hizi?”
“Aaah usafiri mizinguo kinoma noma yani magari yameshona mbaya, si unajua leo wikiendi watu kibao wametoka kula bata”
“(Akinicheka) na wewe mmoja wao umetoka kula bata au siyo?”
ITAENDELEA...
SEHEMU YA 5:
“Aaaaaah hilo sio la kuuliza, nimetoka kujiachia mbele mbele kula bata kama vigogo wanavyofanya vile”
“(Akiendelea kucheka kwa nguvu zaidi)”
“Sasa kinachokuchekesha ni kitu gani haswa, kwani kipi kigeni hapo?” “Unanichekesha sana, umetoka kula bata au umetoka kutangaza shida zako huko na umasikini wako”
“Kwa sasa kweli ni masikini lakini nakuapia mbele za Mungu lazima niwe tajiri mkubwa sana hapa nchini na duniani lazima wanitambue”
“Wapi wewee, mwenye nacho ataendelea kuongezewa na yule asiye nacho hata kile kidogo alicho nacho kitaondolewa”
“Hayo unasema wewe ila sio mimi na napozidi kupata adha ya usafiri wanazidi kuntia hasira za kupambana na maisha mpaka na mimi nifike juu sana zaidi yao”
“Freshi ndio maisha hayo si unajua jiji lenyewe limeshona watu kibao mpaka kero”
“Tuachane na hayo, duuuh kweli mwana utakuwa unaumwa maana madudu yako hujayaleta leo? Maana daily unaleta mwanamke na unabadili kama nguo, utakufa na mizoga yako kaka”
“Ushaanza porojo zako, wanawake wamewekwa ili watumike sio kama wewe mzinguaji. Halafu jamaa yangu sijui kama wewe ni mzima au rijali kweli maana tangu umeachana na Patricia miaka kibao iliyopita sijawahi kusikia hata shemeji wa kusingiziwa?”
“Hivi kaka unaona maisha tunayoishi yanavyotuzingua na ndio maana jamaa yangu hupigi hatua, kila siku ni wanawake, pombe na ganja zako Jirekebishe ushakuwa mtu mzima wewe”
“Ndio maana huwa nakuambia wewe Gerald siasa nyingi, yani unaongeeeea kama upo kwenye kampeni bwana. Enhee nipe michongo ya maana achana na siasa zako”
“Sio siasa bali nakuchana uhalisia wenyewe hivyo, tatizo lako hupendi kuambiwa ukweli hata siku moja”
“Tuachane na hayo nipe habari uliyosema utaniambia ukifika hapa, maana naona unamwaga sera sijui ili nichague chama gani cha siasa mshkaji wangu”
ITAENDELEA...
SEHEMU YA 6:
“Poa haina noma kaka mkubwa, Sasa leo nimepata wazo zuri sana, unaona pande hizi zote za mabibo na manzese? Wakitaka kununua nguo au mashuka hawaendi kariakoo au posta bali kwakuwa maisha yao ni ya chini kama ya kwetu hulazimika kwenda mahakama ya ndizi au karume kupata mahitaji yao”
“Naelewa hilo we nenda kwenye point husika acha kuzunguka mbuyu”
“Hata hivyo ndiyo nilikuwa naenda kwenye point, nimekueleza hayo ili uweze kunielewa barabara. Si unajua kuwa mimi napenda sana kumuelezea mtu hadi anielewe?”
“Sawa ndio nakusikiliza hivyo”
“Sasa mimi nimekuja na wazo la kufungua biashara ya duka la nguo na mashuka ya mitumba kaka”
“Ahah hah hah hah hah hah hah hah hah hah (kicheko cha nguvu)”
“Sasa mbona unanicheka kabla hata sijamaliza? (nikikunja sura kuashiria nimekasirishwa na kitendo kile)”
“Mwana umeongea siriazi nikajua booonge moja la wazo kumbe ni suala la kuwa “machinga”?!”
“Umetafakari ndivyo s..............(akanikatisha)”
“Haina haja ya kuendelea kunipa elimu nimeshakupata vizuri kabisa, unataka tufanye biashara ya machinga wa nguo za mitumba. Hah hah hah hah hah hah hah hah masuala ya ‘za leo leo bei nzuri, bei poa anabeba anabeba mia tano, mia tano, mia tano’ hahahaha basi kaka hilo wazo sijaliafiki kabisa.”
Nilipata ghadhabu sana hadi sura ikabadilika kwa maana sikutegemea jamaa angelipuuza wazo langu kiurahisi vile tena kwa dharau kama aliyekuwa anaongea ni mtoto mdogo. Lakini nilifanikiwa kutuliza hasira zangu kisha kwa upole nikamuuliza. “Poa nimekuelewa kaka mkubwa kwa maelezo yako, sasa basi nipe wewe wazo unaloona ni zuri na imara kuliko nililolisema mimi basi”
“Nilishakuambia tukikaza kwenye fani hii ya muziki lazima tutoke yaani wewe kama kawaida unachana na kutengeneza midundo ya ukweli na mimi naimba mwanzo mwisho, lazima tung’ae maana one day yes”
“Lakini kaka huu ni mwaka wa ngapi tunajihusisha na muziki bila mafanikio na hata kwenye kata yetu hatujulikani?”
“Wee tambua hata mbuyu ulianza kama mchicha, tukikaza one day lazima uwe zaidi ya wana profesa Jay na mimi bongo fleva watangoja sana si unajua ninavyojua kuipanga sauti yangu ya ukweli”
“Aaaahah hah hah hah hah hah hah hah unajidanganya sana ndugu yangu, huu mwaka wa sita unajidanganya tu hivyo. Yani kama usingekuwa pusha na kucheza kwako kamari basi ungeshauliwa kwa wizi, maana huo muziki hauna manufaa yoyote kwako”
“Sawa upusha wangu na kamari vinaniingizia sana hela lakini suala la kuwa machinga hapana kaka. Nilijua unaniletea wazo la maana kwamba umepata dili la kusukuma kete za poda (madawa ya kulevya) ambalo ndilo dili ninaloliwinda badala yake unaniletea ishu za kuuza mashuka bwana”
“Ila nimeshakuzoea jamaa yangu, ukiendelea kuwa na mawazo yako mgando utakuja kuishia mahali pabaya sana na ukipona pona utakuja kujutia njia zako za sasa unazozipitia”
“Utaishia na ushauri wako hivyo hivyo huku wenzio wanapiga mtonyo. Ila mwana nikitoka sitakusahau ili uwe unanipa mahubiri na ushauri wako vizuri hah hah hah hah hah hah”
“Hah hah hah hah hah endelea kujidanganya hivyo hivyo. Poa bwana haina noma namna gani vipi naenda kuegesha mwili kitandani si unaona mida nayo imesogea saa nne sasa hivi Kwahiyo usiku mwema kaka nitakucheki kesho basi”
“Haina noma askari wangu nimekuelewa vizuri kabisa, usiku mwema pia ila leo nalala mpweke sana shemeji yako hajaja bwana”
“Haha hah hah hah hah kumbatia mto. Poa bwana kesho”
Baada ya kumaliza kuzungumza na Regan nilimuaga kisha nikaondoka nikiwa na mawazo tele na nilijiamini sana kwani nikikumbuka nina dhahabu mfukoni basi niliona tayari ulimwengu ni wangu na nilitamani kukuche haraka niweze kwenda kwa sonara nikachukue hela yangu na nikaanza kupanga mipango mingi.
ITAENDELEA...
Mwandishi : Gerald Mtenga
Mawasiliano : 0625600802
Barua pepe : gmtenga@gmail.com
UTANGULIZI :
Bila shaka hakuna binadamu anayependa kuishi maisha ya kimasikini na ya kujidhalilisha mbele ya jamii lakini tukatae au kukubaliana na ukweli kuwa uwezo wa watu umetofautiana sana. Umasikini uliokithiri ndiyo chanzo cha matatizo mengi katika jamii zetu kama ujambazi, ukahaba, utapeli, uchawi n.k na vijana wanahangaika usiku na mchana kuweza kujikomboa na mkono wa jinamizi wa umasikini anayewakaba koo ,na wengine wakikimbia maisha ya mjini na kuelekea vijijini na kuishia kwenye tufani la umasikini mkubwa. Hii ndiyo sababu kubwa iliyomfanya kijana Gerald anayetokea katika maisha ya kimasikini kujiapiza kwamba atahakikisha anaukamata utajiri kwa nyanja yoyote na kufanikiwa kupindua historia ya ukoo wao ambao haujawahi kuwa na msomi wala tajiri yeyote. Katika kitabu hiki utaona namna Zafeera anavyomsababishia kijana Gerald kuharibu njia zake hapa ulimwenguni na kuishia kwenye majuto makubwa.
Ilikuwa vipi mpaka akafanikiwa kufikia ndoto zake na hatimaye kuziharibu mwenyewe? Fuatana na mimi katika kitabu hiki mwanzo hadi mwisho ili uweze kuburudika na kujifunza mambo mengi ambayo yatakusaidia wewe kuweza kutambua mambo ambayo yalikuwa kama ukungu mzito uliokuwa umetanda katika mboni za macho yako. Ikumbukwe majina yote yaliyotumika katika kitabu hiki ni ya kusadikika na kumrathi kwa yeyote atakayekuta jina lake hapa, atambue ya kwamba sijamlenga yeyote katika stori hii.
SEHEMU YA 1:
Ilikuwa ni siku ya jumamosi tulivu kabisa ya mwaka 2006 nikiwa nimepumzika pembezoni mwa ufukwe wa bahari ya Hindi jijini Dar es salaam, na kutafakari mahala maisha yangu yalipotoka mpaka hapa nilipo na kujaribu kupanga na kutafakari mambo yangu ya maisha tangu awali hadi huko siku za usoni. Nikiwa nimezama katika wimbi la mawazo ghafla lilinijia wazo zuri ambalo ilinibidi kulitekeleza ipasavyo, kutokana na hali ya maisha yangu kuwa ya kawaida sana hivyo wazo langu ilikuwa ni kuanzisha banda la kuuza nguo na mashuka ya mtumba.
Nilitafakari kwa muda mrefu na jua lilikuwa limekwishapata usingizi na kufumba macho yake barabara, hivyo ilinilazimu kujinyanyua mahala pale kwani hata wasimamizi wa ufukwe ule walikuwa wakiwaondoa watu eneo la ufukwe kwa muda ule hivyo kuamua kutafuta usafiri wa kurudi nyumbani. Kwa kuwa nilikuwa ufukwe wa koko maeneo ya msasani na maskani yangu yalikuwa ni pande za manzese, niliamua kupanda gari za masaki-kariakoo na gari ilipofika magomeni hospitali niliteremka na kuanza kutembea kuelekea kituo cha usalama ili nipande gari za ubungo.
ITAENDELEA...
SEHEMU YA 2:
Ilikuwa ni mida ya saa moja usiku nikiwa natembea taratibu kuelekea kituo cha basi ambapo ningepanda gari na kufika nyumbani. Nilikuwa na shauku ya kufika mtaani ili niende kwa rafiki yangu Regan ambaye alikuwa ni rafiki na pia kaka yangu mkubwa, nilitaka nimdokeze wazo langu ambalo kwa wakati huo niliamini lilikuwa wazo zuri kupita mawazo yangu ya awali. Nikiwa nakunja kona ya magomeni kwenye ukuta wa hospitali ya magomeni niliona kitu ardhini kikiwa kinang’aa sana.
Nilipiga hatua kadhaa za haraka haraka na kukiinamia kile kitu na kukiokota haraka sana kisha nikaanza kutazama kushoto na kulia kama mwizi aliyetoka kuvunja nyumba na kuiba vito vya thamani. Simu yangu ya kichina iliyokuwa na tochi kali ilinisaidia barabara kuweza kukitazama kile kitu nilichokiokota na maneno yakawa wazi yakisomeka "Zafeera" na maneno mengine ya kilugha ambacho sijawahi kukiona labda sababu sikuwa na elimu kubwa hivyo lugha ile ilinipiga chenga. Kichuma chenyewe kilikuwa na rangi ya dhahabu huku kikiwa kinang’aa sana kikiwa na muonekano wa tofauti na vyuma nilivyowahi kuviona iwe kwenye televusheni au magazetini.
ITAENDELEA...
SEHEMU YA 3:
Baada ya kujirithisha kwamba kile kichuma nilichokiokota kilikuwa na uashiria wa asilimia kubwa kuwa ni dhahabu niliangalia tena pande zote safari hii nikiwa na mashaka kama kuna mtu yeyote aliniona wakati nikikiokota kitu kile. Nilipojiridhisha ya kwamba hakuna aliyeniona niliamua kukihifadhi vizuri kwenye mfuko wa ndani ya suruali yangu (si unajua sisi masikini nguo zetu zinakuwa na mifuko mingi hadi ya ndani ya nguo ili kuhifadhi akiba zetu zisipotee kirahisi).
Baada ya kuhakikisha nimekihifadhi vyema mfukoni nilianza kutembea kwa madaha huku nikiachia tabasamu la ushindi na kuamini kuwa ndio mwanzo wa mafanikio yangu. Niliamini kuwa iwapo ningeenda kukiuza basi ningepata fedha nyingi ambazo zingeniwezesha kufanya biashara kubwa, niliamua kumpigia simu mshikaji wangu Regan kwa migoko mikubwa ili kujua kama yupo chumbani kwake ama kijiweni tunapopenda kukaa jioni baada ya shughuli za kutwa nzima.
“Oyoo, niaje mwanangu mwenyewe?”
“Freshii tu kaka Gerald, vipi?”
“Poa poa mwana, umejiachia pande zipi wewe?”
“Nipo geto tu nimejinyosha kitandani maana najisikia hovyo sana kaka na ndio maana leo maskani nimeshindwa kupanda”
“Aaaah unaumwa wapi wewe, utakuwa umeshapata dawa zako ndio maana umeamua kuvutia stimu magetoni kama kawaida yako”
“Unanirushia njiwa mwana, leo sijapata dawa kabisa maana sijapanda maskani na kama nilivyokuambia najihsi mwili mzima naumwa.”
“Hah hah hah hah hah hah wewe huyo siku ipite hujapata dawa? Labda unataka kuanza kuniuzia chai kama sikujui vile”
ITAENDELEA...
SEHEMU YA 4:
“Hah hah hah hah haya bwana, tuachane na hayo nipe habari zingine”
“Poa poa mimi nipo magomeni hapa nakuja maskani hapo maana nina bonge la dili na wazo la msingi mtu wangu”
“Aaah we Gerald nimeshakuzoea siasa kibao mshkaji wangu, unanirushia stimu tu”
“Mwana we ngoja nije dakika kama kumi hivi nitakuwa hapo, maana hata salio lenyewe linakata sasa hivi”
“Haina kwere kaka, nakusubiria”
Nilivuka barabara na kuelekea upande wa kituo cha magari ya ubungo na kusimama maeneo yale kungojea usafiri. Kama ilivyo kawaida ya usafiri wetu wa jijini ulivyo mgumu, kila basi lililokuja kituoni pale lilikuwa limeshiba abiria mpaka pomoni. Usafiri unapokuwa mgumu ni kawaida kwa wenye magari yao binafsi kusimamisha magari yao kituoni na kutangaza kwa uchu mkubwa bei zao wanazopendezwa nazo. Kwakuwa nilikwishasimama pale kituoni zaidi ya nusu saa hivyo nilikata shauri na kuamua kupanda gari za watu binafsi kwa bei mara tatu zaidi ya nauli za mabasi ya kawaida.
Gari ilikata vituo kadhaa kwa mwendo wa wastani kuashiria kwamba dereva alikuwa mstaarabu na mjuzi, ilipofika tip-top niliomba kushushwa na dereva bila hiyana alisimamisha gari na nilimlipa haki yake kisha nikateremka na kuanza kuelekea nyumbani. Nilinyoosha na ile barabara moja kwa moja mpaka kuifikia njia ya mabibo kisha nikakunja kona na kupiga hatua kama ishirini nikawa nimefika maeneo anayoishi mshakaji wangu Regan. Nilibisha hodi pale mlangoni na nilisikia sauti kwa ndani ikiniashiria niingie ndani, niliingia ndani na kumkuta jamaa akiwa amejilaza kitandani huku akitazama luninga.
“Yani jamaa yangu tangu saa moja umenipigia simu na kuniambia dakika kumi utakuwepo lakini hapa saa zima limepita ndio dakika kumi za siku hizi?”
“Aaah usafiri mizinguo kinoma noma yani magari yameshona mbaya, si unajua leo wikiendi watu kibao wametoka kula bata”
“(Akinicheka) na wewe mmoja wao umetoka kula bata au siyo?”
ITAENDELEA...
SEHEMU YA 5:
“Aaaaaah hilo sio la kuuliza, nimetoka kujiachia mbele mbele kula bata kama vigogo wanavyofanya vile”
“(Akiendelea kucheka kwa nguvu zaidi)”
“Sasa kinachokuchekesha ni kitu gani haswa, kwani kipi kigeni hapo?” “Unanichekesha sana, umetoka kula bata au umetoka kutangaza shida zako huko na umasikini wako”
“Kwa sasa kweli ni masikini lakini nakuapia mbele za Mungu lazima niwe tajiri mkubwa sana hapa nchini na duniani lazima wanitambue”
“Wapi wewee, mwenye nacho ataendelea kuongezewa na yule asiye nacho hata kile kidogo alicho nacho kitaondolewa”
“Hayo unasema wewe ila sio mimi na napozidi kupata adha ya usafiri wanazidi kuntia hasira za kupambana na maisha mpaka na mimi nifike juu sana zaidi yao”
“Freshi ndio maisha hayo si unajua jiji lenyewe limeshona watu kibao mpaka kero”
“Tuachane na hayo, duuuh kweli mwana utakuwa unaumwa maana madudu yako hujayaleta leo? Maana daily unaleta mwanamke na unabadili kama nguo, utakufa na mizoga yako kaka”
“Ushaanza porojo zako, wanawake wamewekwa ili watumike sio kama wewe mzinguaji. Halafu jamaa yangu sijui kama wewe ni mzima au rijali kweli maana tangu umeachana na Patricia miaka kibao iliyopita sijawahi kusikia hata shemeji wa kusingiziwa?”
“Hivi kaka unaona maisha tunayoishi yanavyotuzingua na ndio maana jamaa yangu hupigi hatua, kila siku ni wanawake, pombe na ganja zako Jirekebishe ushakuwa mtu mzima wewe”
“Ndio maana huwa nakuambia wewe Gerald siasa nyingi, yani unaongeeeea kama upo kwenye kampeni bwana. Enhee nipe michongo ya maana achana na siasa zako”
“Sio siasa bali nakuchana uhalisia wenyewe hivyo, tatizo lako hupendi kuambiwa ukweli hata siku moja”
“Tuachane na hayo nipe habari uliyosema utaniambia ukifika hapa, maana naona unamwaga sera sijui ili nichague chama gani cha siasa mshkaji wangu”
ITAENDELEA...
SEHEMU YA 6:
“Poa haina noma kaka mkubwa, Sasa leo nimepata wazo zuri sana, unaona pande hizi zote za mabibo na manzese? Wakitaka kununua nguo au mashuka hawaendi kariakoo au posta bali kwakuwa maisha yao ni ya chini kama ya kwetu hulazimika kwenda mahakama ya ndizi au karume kupata mahitaji yao”
“Naelewa hilo we nenda kwenye point husika acha kuzunguka mbuyu”
“Hata hivyo ndiyo nilikuwa naenda kwenye point, nimekueleza hayo ili uweze kunielewa barabara. Si unajua kuwa mimi napenda sana kumuelezea mtu hadi anielewe?”
“Sawa ndio nakusikiliza hivyo”
“Sasa mimi nimekuja na wazo la kufungua biashara ya duka la nguo na mashuka ya mitumba kaka”
“Ahah hah hah hah hah hah hah hah hah hah (kicheko cha nguvu)”
“Sasa mbona unanicheka kabla hata sijamaliza? (nikikunja sura kuashiria nimekasirishwa na kitendo kile)”
“Mwana umeongea siriazi nikajua booonge moja la wazo kumbe ni suala la kuwa “machinga”?!”
“Umetafakari ndivyo s..............(akanikatisha)”
“Haina haja ya kuendelea kunipa elimu nimeshakupata vizuri kabisa, unataka tufanye biashara ya machinga wa nguo za mitumba. Hah hah hah hah hah hah hah hah masuala ya ‘za leo leo bei nzuri, bei poa anabeba anabeba mia tano, mia tano, mia tano’ hahahaha basi kaka hilo wazo sijaliafiki kabisa.”
Nilipata ghadhabu sana hadi sura ikabadilika kwa maana sikutegemea jamaa angelipuuza wazo langu kiurahisi vile tena kwa dharau kama aliyekuwa anaongea ni mtoto mdogo. Lakini nilifanikiwa kutuliza hasira zangu kisha kwa upole nikamuuliza. “Poa nimekuelewa kaka mkubwa kwa maelezo yako, sasa basi nipe wewe wazo unaloona ni zuri na imara kuliko nililolisema mimi basi”
“Nilishakuambia tukikaza kwenye fani hii ya muziki lazima tutoke yaani wewe kama kawaida unachana na kutengeneza midundo ya ukweli na mimi naimba mwanzo mwisho, lazima tung’ae maana one day yes”
“Lakini kaka huu ni mwaka wa ngapi tunajihusisha na muziki bila mafanikio na hata kwenye kata yetu hatujulikani?”
“Wee tambua hata mbuyu ulianza kama mchicha, tukikaza one day lazima uwe zaidi ya wana profesa Jay na mimi bongo fleva watangoja sana si unajua ninavyojua kuipanga sauti yangu ya ukweli”
“Aaaahah hah hah hah hah hah hah hah unajidanganya sana ndugu yangu, huu mwaka wa sita unajidanganya tu hivyo. Yani kama usingekuwa pusha na kucheza kwako kamari basi ungeshauliwa kwa wizi, maana huo muziki hauna manufaa yoyote kwako”
“Sawa upusha wangu na kamari vinaniingizia sana hela lakini suala la kuwa machinga hapana kaka. Nilijua unaniletea wazo la maana kwamba umepata dili la kusukuma kete za poda (madawa ya kulevya) ambalo ndilo dili ninaloliwinda badala yake unaniletea ishu za kuuza mashuka bwana”
“Ila nimeshakuzoea jamaa yangu, ukiendelea kuwa na mawazo yako mgando utakuja kuishia mahali pabaya sana na ukipona pona utakuja kujutia njia zako za sasa unazozipitia”
“Utaishia na ushauri wako hivyo hivyo huku wenzio wanapiga mtonyo. Ila mwana nikitoka sitakusahau ili uwe unanipa mahubiri na ushauri wako vizuri hah hah hah hah hah hah”
“Hah hah hah hah hah endelea kujidanganya hivyo hivyo. Poa bwana haina noma namna gani vipi naenda kuegesha mwili kitandani si unaona mida nayo imesogea saa nne sasa hivi Kwahiyo usiku mwema kaka nitakucheki kesho basi”
“Haina noma askari wangu nimekuelewa vizuri kabisa, usiku mwema pia ila leo nalala mpweke sana shemeji yako hajaja bwana”
“Haha hah hah hah hah kumbatia mto. Poa bwana kesho”
Baada ya kumaliza kuzungumza na Regan nilimuaga kisha nikaondoka nikiwa na mawazo tele na nilijiamini sana kwani nikikumbuka nina dhahabu mfukoni basi niliona tayari ulimwengu ni wangu na nilitamani kukuche haraka niweze kwenda kwa sonara nikachukue hela yangu na nikaanza kupanga mipango mingi.
ITAENDELEA...