Simulizi ya maisha na upelelezi: Ishini badala yangu wanangu

gilbert35

JF-Expert Member
Nov 20, 2021
247
474
Simulizi Ya Maisha na Upelelezi; ISHINI BADALA YANGU WANANGU
Mwandishi; GILBERT EVARIST MUSHI
PHONE: 0765824715

Sehemu ya Kwanza

Sauti ya maji ndiyo iliyokuwa ikisikika ndani ya masikio yake mawili, akajaribu kukisogeza kichwa chake karibu zaidi na koki ya bomba inayotiririsha maji bafuni mle lakini bado hakuweza kuuweka sawa ubongo wake uliokuwa ukiwaza mengi. Muda wote akiwa bafuni anaoga akili yake haikuwa bafuni, Alikuwa akiiwaza safari yake ya Kuelekea Dar es Salaam. Tena katika Hospitali kubwa ya Taifa ya Muhimbili.
Macho yake akayaelekeza katika sabuni aliyokuwa akiitumia kuogea. Akapeleka kidole gumba hadi juu ya sabuni ile na kuanza kukita kidole kile, hali iliyopelekea kutokea shimo katikati ya sabuni. Hakuishia hapo tu, akaichukua na kuanza kuimega kidogo kidogo kwa kutumia kucha zake. Ikawa si tena sabuni bali ni vipande vya sabuni.
Akiwa bado Bafuni sauti ya mke wake ilisikika ikimwita.
"Honey simu yako inaita, huko bafuni humalizi kuoga tu mume wangu?"

"Nakuja Kipenzi".. Haraka alitoka bafuni na kuiwahi simu ile. Alihisi mpigaji atakuwa ni Kaka yake aitwaye Abuu.
Hisia zake zilikuwa sahihi haswa, mpigaji alikuwa ni yeye, Abuu Abdallah. Ndugu yake wa damu kabisa.

"Vipi Kinje" Sauti ya Kaka yake ikamsabahi.

"Safi Kaka, kwema huko?"

"Kwema kiasi mdogo wangu. Umekata tiketi ya boti ya saa ngapi kuja huku?" aliuliza Kaka yake
"Safari inatarajia kuanza saa 12 Jioni kaka, nimeshauriana na mke wangu hapa nikaona nikate tiketi ya jioni kabisa ili nifike huko kwenye saa mbili hivi usiku." Kinje Akamjibu kaka yake

"Ohoo. Sawa Mdogo wangu. Ufike salama basi maana Kesho ndio siku yenyewe. Si unalijua hilo?"

"Natambua hilo kaka". Kinje alijibu kisha akavuta pumzi ndefu. Alimaliza kuzungumza na simu ile na kuitupia kitandani. Mke wake muda wote alisimama mbele yake akimtazama kwa macho yenye uchungu mkubwa. Ni kama alitaka kulia lakini alijikaza tu.

"Usijali nitakuwa sawa tu Mke wangu". Kinje alijaribu kumtuliza mkewe. Licha ya Clara kuambiwa vile lakini hakuyajali maneno ya mumewe, alishindwa kujizuia, akamsogelia Kinje na kumkombatia. machozi nayo yakashindwa kujizuia, yakaitafuta njia ya kutokea. Alianza kutokwa machozi

"Kila mara wewe ni wa kusema tu utakuwa sawa. Hujali ni kiasi gani sijapendezwa na hili Honey, hujali pia hisia zangu. Kwa hili siwezi kuwa sawa Kinje." Alilalama Clara huku mdomo wake ukiwa karibu kabisa na sikio la Kinje
"Vipi kama usiporudi? Nitaishije? Huyu mtoto aliyeko tumboni mwangu atapata wapi upendo wa baba kama tu baba yake ananiacha peke yangu na sina imani kama aterejea tena? Tafadhali kipenzi usiniache nakuomba. Mwambie kaka yako atafute hata mtu mwingine mume wangu, sitaki ukae mbali nami, sihitaji kukupoteza Kinje."....
Alizungumza Clara kwa Majonzi makubwa huku akimpigapiga Kinje kwa mkono wake laini kifuani pake.

Kinje akavuta pumzi ndefu na kuiachia taratibu huku akitafakari nini afanye. Alipaswa kwenda Dar es salaam, hakuwa na namna ya kuikwepa safari ile. Kaka yake wa tumbo moja anayeishi Dar es salaam alimhitaji kutokana na matatizo yaliyomkumba mwanaye wa pekee wiki chache zilizopita. Binti yake aitwaye Julieth alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya Figo. Figo moja ilifeli na hivyo ilihitajika figo nyingine.
Julieth mbali na kubakiwa na figo moja, nayo ilishapata maambukizi kutoka katika figo ile ya kwanza kutokana na kucheleweshwa kwenda hospitali, hivyo daktari alishauri mtoto Julieth aondolewe figo zote na kupatiwa figo nyingine. Figo iliyoharibika zaidi ikatolewa na ikabaki ile yenye unafuu kidogo.
Zoezi la kutafuta figo haikuwa kazi rahisi, walipaswa kutafuta namna ya kufanikisha mtoto Julieth aweze kupata figo. Iliwalazimu yeye na kaka yake watafute mtu ambaye vinasaba vyake (DNA) vitaendana na vya Julieth. Mtoto Julieth alihitaji mtu mwenyevina saba vya kufanana naye.
Abuu hakuwa na mtoto mwingine zaidi ya Julieth, alitamani mwanaye aweze kuzinduka tena kutoka kitandani kwani muda wote alikuwa ni mtu wa kitandani tu. Mke wake Abuu alipoteza maisha miaka kadhaa iliyopita baada tu ya kumzaa Julieth hivyo Julieth alibakiwa na mzazi mmoja tu ambaye ni Abuu.
Katika kutafuta mtu, kitu cha ajabu ni kwamba Kinje ndiye aliyeonekana vinasaba vyake kufanana na Julieth kwa asilimia 99.9%. Kinje Hakuwa na hiyana, kwenye kumchangia figo mtoto mdogo tena isitoshe ni mtoto wa kaka yake?
Hilo akaliridhia. Na zilibakia siku mbili tu ili Kinje na Julieth waweze kuingizwa katika chumba maalumu cha upasuaji, figo moja itoke kwake na kwenda kwa Julieth.
Hiki ndicho kilimfanya mke wa Kinje akose raha. Alihofia juu ya usalama wa mumewe endapo atatolewa figo moja na kubakiwa na moja.

"Sikia mke wangu, Mwanadamu akibakiwa na figo moja sio mwisho wa maisha mke wangu, na pia nguvu hazipungui, kazi atapiga kama mwanzoni kabisa. Si unamjua balozi wetu wa hapa Jang'ombe? Mbona Yeye ana figo moja lakini bado anadunda na maisha vizuri mke wangu?, kumchangia mtu figo sio mwisho wa uhai mke wangu nielewe ".
Alizidi kumsihi mkewe huku akimfuta machozi,. Baada ya muda kidogo Mkewe akapoa, Kinje akajiandaa kwa Safari ya kuelekea Bara na hatimaye maandalizi yalikamilika.

Kabla ya kuondoka Mke wake alimlisha chakula kama mtoto mdogo, akamnywesha na juisi ya embe. Muda wote akifanya hivyo hakuwa katika uchangamfu. Hofu yake ilikuwa juu ya mumewe tu. Alitamani kuongozana naye kwenda Jijini Dar es Salaam lakini haikuwezekana kutokana na hakukuwa na mtu wa kusimamia miradi yao biashara na ukijumlisha Clara alikuwa ni mjamzito

Majira ya Saa Kumi na nusu jioni Kinje aliagana na mke wake tayari kwa safari ya kuelekea Jijini Dar es salaam kwa usafiri wa Meli. Mkewe akalikita busu zito katikati ya paji la uso la mumewe huku machozi yakimtoka. Kinje naye akajiandaa kujibu kwa Kumpiga busu katika tumbo lake lililotuna kutokana na ujauzito aliokuwa nalo.

"Pandisha gauni lako mpenzi nimbusu mwanangu, nimwambie ninatoka kidogo sitakawia kurudi". Kinje akamsihi huku akididimiza magoti yake chini taratibu.
Mkewe alikataa.
"Nibusu tu hivyohivyo bwana, hadi nijifunue jamani?" Clara alisema kwa sauti ya madeko. Kinje akakumbuka hii si mara ya kwanza kwa mkewe kumkatalia pindi ahitajipo kubusu tumbo lile bila kuwepo na kizuizi cha nguo. Pia kuna wakati akiligusa tumbo la mkewe, huonekana kushtuka ghafla na kumkatalia.
Akaamua kuliacha lile likapita. Alimbusu mkewe kwa namna alivyotaka.
Wakaagana.

Kinje alifika Bandarini majira ya Saa kumi na moja na nusu jioni, akakamilisha baadhi ya taratibu za msingi kabla ya kupanda meli ndogo ya abiria na mizigo kuelekea Tanzania Bara, na taratibu zilipokamilika safari ilianza rasmi majira ya saa kumi na mbili jioni. Kutokana na umbali wa kutoka Zanzibar hadi Bara, safari ilitarajiwa kuchukua takribani masaa mawili na nusu tu.

Kinje akiwa ndani ya meli, kuna jambo lilimshangaza sana. Katika siti za abiria zilizokuwa mbele yake kulikuwa na wanaume wawili waliokuwa wakimtazama mara kwa mara. Walikuwa wakimtazama huku wakizungumza kama vile wanamjadili. Ilikuwa ni kama vile wamemfananisha ama wanamfahamu kwa jinsi walivyokuwa wakimtazama kwa macho ya udadisi. Kwa upande wa Kinje sura hizi zilikuwa ngeni kabisa kwake kwani hakuwahi kuziona hapo kabla.
Kuna muda Kinje alielekea msalani, akiwa msalani alisikia mazungumzo ya watu wawili wakiteta jambo. Akajaribu kusikiliza mazungumzo yale yaliyokuwa yakifanyika msalani.

"Niamini Edgar. Bosi alinitumia picha yake kabisa, ni yeye huyu jamaa." alisikia sauti ikisema

"Kama ni yeye basi itakuwa bingo kwetu. Hatutakuwa na kazi kubwa sana. Zoezi litafanyika leo leo usiku. Cha kufanya ni kuleta kasoro humu ndani ili meli ikawie kufika Dar,".. Sauti ya pili ilijibu.

Kinje hakuyatilia maanani sana maongezi yale, alifanya kilichompeleka msalani kwa wakati ule kisha akarejea katika siti yake. Kitendo cha kukaa tu, mbele yake akawaona vijana wale wawili waliokuwa wakimtazama mara kwa mara wakitokea upande wa msalani. Akagundua yale maongezi aliyoyasikia kule msalani bila shaka walikuwa ni wao.

"Ni kasoro gani hiyo wanataka kuileta huku ili meli ichelewe kufika bara?." Kinje alijiuliza huku akiwatazama vijana wale, hakupata jibu. Akajionya tabia ya kufwatilia yasiyomuhusu.
Akiwa katika lindi la mawazo akayaelekeza macho yake hadi pale walipoketi vijana wale wawili, macho yake yaligongana na macho yao, kwa haraka vijana wale waliangalia pembeni, Kinje akapata kuhisi kuna jambo halipo sawa. Lakini bado hakutilia maanani kivile.

"Sasa mbona kila muda wananitazama mimi tu? Na kwanini macho yetu kila yakigongana wanaonekana kukwepesha?"..... Kinje aliwaza.
"Ah itakuwa ni mawazo yangu tu. Au labda wamenifananisha," Alijisemea, akaamua kuachana na mawazo yale

Je vijana hawa wana lengo gani na Kinje? Kinje atafanikiwa kufika Tanzania Bara salama? Tuwe wote katika sehemu ijayo ya Simulizi hii itakayokufundisha mengi. Njoo Gilbert akusimulie
IMG-20220106-WA0000.jpg
 
Simulizi Ya Maisha na Upelelezi: ISHINI BADALA YANGU WANANGU
Mwandishi; GILBERT EVARIST MUSHI
PHONE: 0765824715

Sehemu ya Pili
UTANGULIZI
Kinje anamuaga mkewe na kupanda Boti kuelekea Tanzania Bara kwa ajili ya kwenda kumsaidia mtoto wa Kaka yake Figo. Akiwa ndani ya meli anakutana na vijana wawili wanaomfanya akose utulivu kutokana na visa wanavyovifanya.
Tulipoishia.....
"Sasa mbona kila muda wananitazama mimi tu? Na kwanini macho yetu kila yakigongana wanaonekana kukwepesha?"..... Kinje alijiuliza.
"Ah itakuwa ni mawazo yangu tu. Au labda wamenifananisha." Alijisemea, akaamua kuachana na mawazo yale

Songa Nayo....
Akiwa katikati ya safari, Meli aliyopanda ilipata hitilafu ya ghafla. Marubani wakapambana kuweka hali sawa huku spika zilizopo ndani ya meli ile zikiwataka abiria kuwa na amani kwani hali itakaa sawa muda si mrefu. Kwa wakati huo Kinje alijaribu kuyatupa macho yake hadi katika siti za vijana wale wawili, hakuwaona. Akayakumbuka maongezi yale aliyoyasikia chooni. Akajua bila shaka lipo jambo kubwa linalotaraji kutokea. Afanye nini sasa? Alijishauri lakini akili yake haikuwa sawa. Dakika mbili mbele akawaona vijana wale wakirejea zilipo siti zao, aliwaona pia wakitabasamu huku wakionekana kujipa pongezi kwa ishara ya kugongeana mikono. Tukio lile ni Kinje tu aliweza kuliona. Hitilafu ile ilidumu kwa takribani nusu saa na Baada ya hapo hali ikarejea kuwa shwari na meli ikaendelea na safari yake bila changamoto yoyote.

Majira ya Saa tatu na nusu usiku meli ndogo ya abiria na mizigo ilitia nanga katika bandari ya Dar es Salaam. Kinje alimshukuru muumba kwa kufika salama kwani lolote lingeweza kutokea wakiwa ndani ya maji, ila Mungu alikuwa upande wao. Kitu cha kwanza Kinje kufanya alichukua simu yake na kumpigia kaka yake aitwaye Abuu.

"Kaka habari za jioni?....... Nimeshafika bandarini hapa kaka" alisema Kinje baada ya kaka yake kupokea simu

"Salama Kinje, pole na safari. Sasa usiku umekuwa mkubwa tayari, giza limetanda, umechelewa sana kufika mdogo wangu. sasa hivi kupata magari yanayokuja huku Tegeta ni ngumu kidogo, unaonaje ukakodi chumba hoteli yoyote hapo itakayokufaa ili kesho asubuhi uanze safari ya kuja Tegeta huku?." Abuu alimshauri mdogo wake.

Kinje akashauriana na ubongo wake na baada ya sekunde chache aliliafiki jambo hili la yeye kutafuta chumba hotelini apumzike hadi asubuhi ndipo aendelee na safari. Kilichomfanya achelewe kuwasili ni kutokana na hitilafu ile iliyotokea ndani ya meli wakiwa katikati ya safari. Abiria walianza kushuka ndani ya meli, Kinje naye akalikamata begi lake dogo taratibu akateremka.
Akiwa anashuka, wanaume wale waliokuwa wakimtazama mara kwa mara ndani ya meli walikuwa nyuma yake. Alizisikia sauti zao zikisemezana ndipo akageuza shingo yake kuwatazama.
Walikuwa ni wenyewe
Kila alipojaribu kugeuka macho yake na wanaume wale yaligongana, na haraka waliyakwepesha.
Kinje akawapuuza tenakwa mara nyingine.
Alielekea zinapopaki taxi kisha akamtaka dereva ampeleke Royal Hotel. Sifa za hoteli hiyo aliziona kupitia kipeperushi akiwa ndani ya meli. Akaona hoteli hiyo ingemfaa kwa usiku huu mmoja, na uzuri wa hoteli hii ni karibu tu na bandari ya Dar es Salaam. Ipo umbali wa Kilometa mbili tu kutoka bandarini.
Dereva taxi alipoliondoa gari, kupitia kioo cha pembeni Kinje aliwaona wale vijana wawili wakizungumza na dereva taxi mmoja kisha nao wakapanda taxi ile.Taxi ile ikafwata uelekeo uleule inapoelekea Taxi ambayo Kinje ameipanda

Baada ya dakika Tano taxi ilimfikisha Royal Hotel. Akamlipa dereva kiasi chake cha fedha kisha akaelekea upande wa mapokezi.

"Habari', nahitaji chumba kimoja cha kulala kwa usiku huu tu" Kinje alisema pale mapokezi baada ya kufika.

"Sawa, chumba umepata, na karibuni sana katika hoteli yetu ya Royal." Dada wa mapokezi alisema kwa sauti nyororo huku akisogeza vizuri kitabu cha wageni katika mikono yake.

"Sijui niandike nani Kaka?." Muhudumu huyu aliuliza huku akimwangalia usoni Kinje.

"Ninaitwa Kinje, Kinje Abdallah." Kinje alisema huku akigeuka nyuma kutalii mazingira ya hoteli hii.
Baada ya Kinje kuandikisha mambo yote yaliyohitajika katika kile kitabu cha wageni, na kukamilisha malipo, aliambatana na Dada yule yule wa mapokezi hadi mbele ya mlango wa chumba namba 99. Yule muhudumu akautoa funguo mmoja na kufungua mlango ambao kwa juu kuna maandishi meusi yanayosomeka (No. 99).

"Karibu sana Kinje katika hoteli yetu ya Royal.... karibuni sana, hiki ni chumba namba tisini na tisa kama inavyosomeka hapo juu. Ndani kuna choo, bafu, Tv, simu ya mezani pia kama utahitaji huduma unaweza kutupigia tukafika kwa haraka." Muhudumu yule alimwambia huku akimkazia macho.
Kinje akaingia ndani baada ya kukabidhiwa funguo, na muhudumu yule akarejea mapokezi kuendelea na huduma

Ili kupunguza uchovu wa safari, Kinje akaelekea kwanza maliwatoni na huko akaoga. Akarejea chumbani kwake na kubadili nguo nyingine tofauti na zile alizokuja nazo. Tumbo nalo likaanza kudai haki yake. Alitaka apige simu aliyoiona pale mezani aagize chakula lakini akaghairi. akatoka nje ili kwenda kutafuta chakula mwenyewe.
Kabla ya kuondoka alihakikisha kwanza mlango wa chumba chake anaufunga vyema. Ndipo sasa akaelekea nje kutafuta chakula.
Kinje alifwata uelekeo wa korido ndefu hadi mapokezi, akauliza mgahawa ulipo, akaelekezwa. Hakutaka kupiga simu ya kuletewa chakula chumbani kwake, alitaka aagizie nje ili alapo apate kutazama na madhari ya hoteli hii inavyovutia.

Akiwa katikati ya njia inayoelekea katika mgahawa ulipo, kwa mbali alisikia sauti ya mwanamke ikihitaji msaada.

"Nisaidieni nakufaaa, ananibakaaa jamani msaadaa,"
Sauti ya mwanamke anayepiga makelele ilipenya ndani ya masikio yake mawili.
Katika maisha yake hakuna jambo analolichukia kama uonevu, haswa uonevu dhidi ya wanawake. Akaghairi kwanza kuelekea mgahawani, kushoto kwake aliona uchochoro mwembamba unaoelekea sauti inapotokea.
Na muda huo yalikuwa ni majira ya Saa nne usiku.
Hatua kadhaa mbele alifika eneo la tukio, kupitia mwangaza hafifu wa taa inayomulika mbali kidogo akapata kuona Mwanaume mmoja akijitahidi kumpiga mabusu mwanamke anayepiga kelele za kuhitaji msaada.

" Hey!. Acha ujinga." Kinje alisema kwa sauti ya juu kidogo.
Mwanaume yule alimwacha msichana yule kwa haraka baada ya kusikia sauti ile, na alipomuona Kinje alikimbia. Mwanamke yule akaja kwa haraka upande alipo Kinje akihema kwa kasi.

"Nisaidie Wanataka kunibaka."... Alisema huku akitetemeka kwa hofu.
Kinje akajaribu kuangaza macho yake eneo hili, Ghafla kwa mbali aliwaona vijana wale aliokuwa nao kwenye boti. Vijana ambao walimchanganya sana ndani ya boti hadi kuwaza ni kina nani wale. Vijana wale walikuwa wamejificha kwenye kona moja wakichungulia upande alipo Kinje.

"Wale wanafanya nini hapa? kwa nini wananichungulia? kuna kitu gani hapa na kwanini kila mara nawaona?." aliwaza Kinje huku akimtazama mwanamke yule kwa wasiwasi

Vijana wale walipoona Kinje amewaona walirudi nyuma na kujificha vizuri. Kinje akamsogelea yule mwanamke karibu na kumgusa begani.

"Upo sawa?" alimuuliza binti yule. Alionekana ni binti wa miaka takribani ishirini na sita au saba hivi.

"Ndiyo Kaka nipo sawa, hawajanidhuru." Alijibu binti yule kwa sauti ya kudeka.

"Naitwa Kinje,"

"Naitwa Devotha," Binti yule naye alijitambulisha huku aking'ata kucha.

"Ohoo.. Devotha, pole sana kwa hili. Sasa mimi naelekea kupata chakula, nadhani sasa naweza kukuacha, kwaheri". Kinje alimwambia Devotha huku akijiandaa kuondoka.

"Njaa inaniuma kweli, sijala chochote toka asubuhi. Naomba kama hutojali Kaka tunaweza jumuika wote katika chakula?". Devotha alizungumza kwa sauti yenye hisia, yenye kumaanisha asemacho.
Bila kujiuliza Kinje alimkubalia. Wakaongozana hadi katika mgahawa, wakatafuta sehemu iliyojitenga kidogo yenye utulivu. Kinje akaagiza ugali na kuku wa kuchoma huku akimtaka mwanamke yule aliyejitambulisha kama Devotha aagize chochote anachohitaji kula.
Devotha akaagiza chipsi yai. Chakula wapendacho wadada wengi.

Wakati wakila walizungumza mengi huku wakibadilishana mawazo ya hili na lile. Kila muda Devotha alimtazama Kinje kwa macho yenye kila aina ya mtego. Haswa mitego ya kumtoa nyoka pangoni. Kinje akaliacha pango lake wazi ili auone mtego ule ambao kamwe hata wewe usingeweza kuukwepa pindi uonapo. Ni lazima unase tu. Kinje akanasa katika mtego huo na hapo ndipo lilipotokea la kutokea ambalo kamwe hataweza kulisahau hata awapo kaburini

Ni mtego gani huo Devotha ameutega kwa Kinje? Wanaume wale wawili kwanini kila mara wanaonwa na jicho la Kinje? Kuna lipi nyuma ya pazia? Tuwe sote katika sehemu ijayo ya simulizi hii.
 
Simulizi Ya Maisha na Upelelezi; ISHINI BADALA YANGU WANANGU
Mwandishi: GILBERT EVARIST MUSHI
PHONE: 0765824715

Hii ni Sehemu ya Tatu
Tulipoishia....
Wakati wakila walizungumza mengi huku wakibadilishana mawazo ya hili na lile. Kila muda Devotha alimtazama Kinje kwa macho yenye kila aina ya mtego. Haswa mitego ya kumwita nyoka pangoni.

Sasa Endelea...
Devotha akatawala maongezi yale, huku sauti kudeka na kumwita nyoka pangoni ikishamiri.
Kinje akatokea kuvutiwa sana naye.
Kinje alibaki akimtazama Devotha, wakati huo Devotha yeye akizungumza huku akiwa mwenye furaha muda wote.
Kinje akameza mate fundo la kwanza,
akameza tena fundo la pili.
Akamtamani.
Wahenga walinena, tamaa mbele mauti nyuma. Tuiite tamaa ya Kinje ni ile waliyonenaga wahenga? Au hii si ile tamaa iletayo mauti? Ngoja tuone.

"Tunaweza kujumuika wote pamoja usiku wa leo?." Kinje alijaribu kujitetea huku akishika kiganja cha mkono wa Devotha. Devotha akamtazama kwa macho yaliyojaa aibu.
Macho yaliyozidi kumpa wakati mgumu Kinje
Kinje akazidi kunasa kwenye mtego uliotegwa na wawindaji wanaoijua kazi yao

Bila kinyongo Devotha alikubali kujumuika naye pamoja. Wakacheza mziki laini uliokuwa ukiendelea. Walicheza kwa takribani nusu saa hivi. Baada ya hapo wakaelekea katika chumba namba 99, chumba alichopanga Kinje kwa usiku ule.
Wakiwa chumbani wakaoga pamoja, si kuoga tu, na kuogeshana pia. Haikuishia hapo, wakabebana pamoja hadi kitandani.
Huko wakafanya kile walichodhamiria. Ilikuwa ni vita ya tatu ya Dunia ndani ya chumba kile.
Juu ya kitanda kile kisichokuwa na hatia
''''''''''''''''''''''

Baada ya masaa mawili kupita, majira ya saa Sita usiku mlango uligongwa. Hali ya mlango kugongwa majira yale ilimpa wasiwasi Kinje. Muda huo walikuwa bado uwanja wa vita ile iliyofaa kuitwa vita ya tatu ya dunia. Hakukuwa na mtu aliyechoka katika mpambano ule, wote walikuwa katika mashambulizi mazito.
Sauti ya mlango kugongwa ikawafanya walisimamishe pambano lile, na hapo kitanda kikapata ahueni kidogo.

"Ni nani huyu anagonga mlango muda huu?," Kinje aliuliza kwa mashaka huku akijitoa katika mwili wa Devotha"

"Itakuwa ni muhudumu maana kuna muda niliagiza mvinyo watuletee chumbani," Devotha alijibu kwa sauti ya kudeka. Sauti iliyoendana na Mitego pamoja na mashambulizi ya vita walivyovipiga sekunde chache zilizopita kabla ya mlango kugongwa.

."Mh! Mvinyo!". Kinje akauliza kwa mshangao. Akili yake ilimwambia muda wote walipokuwa pamoja hakusikia Devotha akiagiza mvinyo ama kupiga simu. Sasa huo mvinyo unaoletwa ni nani kaagiza?.

"Uliagiza mda gani wakati mda wote tulikuwa pamoja na isitoshe sikukuona ukiongea na mtu yeyote?". Kinje akauliza akiwa na wasiwasi mwingi.

"Mh!" Devotha aliguna.
"Nahisi una mawazo mengi mpenzi. Hukumbuki muda ule tunaongozana kuja chumbani nilimsimamisha mhudumu mmoja aliyekuwa akipishana nasi? Yule muhudumu si ndiye niliyempa oda jamani? Sema labda kwa vile amechelewa sana ndio maana umesahau. Ila hata kama lakini nashangaa unasahau vipi! Kweli una mawazo mengi sana mpenzi."

Kinje akajaribu kukumbuka lakini hakuambulia chochote. Bado akili yake ilikataa katakata kwamba Devotha aliagiza mvinyo...

"itakuwa nilisahau labda. Ngoja nielekee mlangoni mwenyewe nijue ni nani huyu." Kinje aliwaza huku akijiinua pale kitandani.
Akajiinua pale kitandani na kuvaa nguo yake ya ndani na kujitupia shuka jeupe kisha akausogelea mlango. Kwa mwendo wa tahadhari akakinyonga kitasa na kuufungua mlango...
Alikuwa ni muhudumu wa kike. Mkononi alibeba Chupa kubwa ya wine na glasi mbili.

"Samahanini kwa kuchelewa sana kuwaletea hii kitu". Alisema mhudumu yule.
Japo Kinje hakukumbuka kama kinywaji kile kiliagizwa akiwepo lakini alikipokea hivyohivyo. Wakati anajiandaa kuufunga mlango alimwona muhudumu yule akimkonyeza Devotha, Devotha naye akatabasamu na kumfinyia jicho mhudumu yule. Kinje akaufunga mlango, akaubana na ufunguo kabisa, akajongea na wine ile hadi kitandani.

"Unajuana na huyu Mhudumu?." Kinje alimuuliza Devotha

"Hapana. Kwanini umeuliza hivyo?".. Devotha naye aliuliza

"Aa, hamna kitu". Kinje alijibu kwa mkato ili kupotezea mada ile. Nafsi yake ilishaanza kuingia wasiwasi, ilimtaka amalizane na binti huyu kisha kila mtu ashike njia yake.

"Au kwa vile kanikonyeza?, Yule ni mwanamke kama mimi bwana, nadhani alinikonyeza labda akiashiria kunisalimia. Sijui lakini alimaanisha nini tofauti na navyofikiri." Alijitetea Devotha

"Tuachane nayo bwana." Kinje alimsihi. Devotha akatoka kitandani na kuisogelea wine ile iliyoletwa. Akaichukua wine ile kisha akaifungua. Akaitia katika glasi mbili, moja akamkabidhi Kinje.

"Karibu mpenzi wangu. Tunywe tufurahi kisha tuendelee pale tulipoisha." Devotha alisema huku akiupeleka mkono ulioshika glasi mdomoni kwa Kinje.

"Mh! Sio kwa mahaba haya jamani. Huyu mtoto fundi kwa kweli." Kinje alimsifia Devotha bila kutoa sauti. Alikuwa akijiwazia peke yake
Kutokana na hali ya uchovu aliyokuwa nayo, Kinje aliikamata glasi kutoka katika mkono wa Devotha na kuipeleka kinywani mwake, akaigugumia wine ile hadi ikaisha. Akajiinua na kuipeleka glasi ile hadi mezani. Alitaka mambo yaende haraka warudi kwenye vita waliyoisimamisha muda mfupi uliopita.

"Eh! Mbona hivyo jamani? Hutaki tunywe pamoja kwanza unataka tuendelee?". Devotha aliuliza huku akiwa bado ameishikilia glasi yake yenye wine. Hakuwa ameinywa hata tone.

" Ah mimi nakusubiri bwana, nawe umalize tuendelee na mengine." Kinje akasema. Akarejea kilipo kitanda, na awamu hii nguvu zilianza kumwishia taratibu. Kiuchovu Kinje akajitupa kitandani.

"Ngoja ninywe mara moja basi kipenzi, ona sasa umeanza kusinzia jamani. Na ole wako ulale wakati bado nina hamu mie." Devotha alisema huku akijiandaa kupeleka glasi yake kinywani kwani toka amimine hakuitia mdomoni hata tone bado.
Kinje akataka kuongea lakini mdomo ukamsaliti.
Ulimi ukawa mzito kunena,
Akataka kujigeuza kwani alikuwa amelalia mkono lakini mwili uligoma kutii alichotaka
Macho nayo yakawa mazito kutazama. Yakamsaliti

Giza likatanda katika mboni zake. Akaingia katika dimbwi lenye usingizi mzito. Usingizi wa Kifo
Devotha baada ya kuona Kinje amelala, aliirejesha glasi yenye mvinyo mezani. Akachukua simu yake aliyokuwa ameihifadhi katika mfuko wa koti lake dogo alilokuwa amevalia. Akaiwasha na kubofyabofya kwa sekunde kadhaa kisha akaiweka sikioni.

"Kazi yangu uliyonituma imekamilika, mimi naondoka zangu hapa chumba namba 99." Devotha alisema maneno yale na kukata simu. Akaichukua wine ile pamoja na glasi zote mbili, akaelekea mlangoni na kuufungua, akatoka nje na kutokomea.
_______________
ITAENDELEA

Simulizi hii itakujia hapahapa hadi mwisho kabisa. Ila Kama ukiitaka yote kwa haraka utapaswa kulipia kiasi kidogo tu cha pesa. Tshs 1000 nami nitakutumia yote. Lipa kwenda Halopesa namba 0621249611 au Mpesa namba 0765824715 jina Gilbert
 
Simulizi Ya Maisha na Upelelezi; ISHINI BADALA YANGU WANANGU
Mwandishi; GILBERT EVARIST MUSHI
PHONE: 0765824715

Sehemu ya Nne

Tulipoishia...
Devotha baada ya kuona Kinje amelala, aliirejesha glasi yenye mvinyo mezani. Akachukua simu yake aliyokuwa ameihifadhi katika mfuko wa koti lake dogo alilokuwa amevalia. Akaiwasha na kubofyabofya kwa sekunde kadhaa kisha akaiweka sikioni.

"Kazi yangu uliyonituma imekamilika, mimi naondoka zangu hapa chumba namba 99." alisema maneno yale na kukata simu. Akaichukua wine ile pamoja na glasi zote mbili, akaelekea mlangoni na kuufungua, akatoka nje na kutokomea.
_______________
Tuisome Leo....
Asubuhi majira ya saa mbili Kinje alipata kufumbua tena macho yake baada ya usingizi mzito uliomkumba hapo jana. Usingizi ambao bila shaka haukuwa wa kawaida kwake. Macho yake yalikutana na madhari tofauti na ile ya jana ndani ya chumba. Chumba kilikuwa kimevurugika vibaya sana, kama vile kulitokea ugomvi mkubwa hapo jana. Akajaribu kuangaza kushoto na kulia lakini hakumwona Devotha. Akajitahidi kuuinua mwili wake lakini ulikuwa dhaifu sana.
Hakuwa na nguvu kabisa.
Ilikuwa ni kama vile mizigo mzito uliwekwa juu ya kifua chake alipolala. Akajitahidi hivyohivyo kujiinua kiuchovu hadi akafanikiwa kuinuka.
Jambo lililomshangaza zaidi ni kwamba alikuwa uchi wa mnyama, hakuwa na nguo yoyote ile aliyokuwa ameivaa.

"Ah ina maana jana nililala uchi hivi!. Lakini mbona kama nililala na bukta?" Alijaribu kuwaza.
"Halafu yule Mwanamke niliyelala naye jana yuko wapi?" Akajiuliza.

Akiwa anajiuliza hayo Ghafla mlango uligongwa mfululizo. Haraka haraka akaangaza macho yake achukue kipi cha kuusitiri mwili wake kwa wakati huo.
Shuka. Aliliona shuka kitandani
Akalikwapua shuka lile lenye rangi nyeupe lililokuwa pale kitandani ili aweze kujisitiri. Alipovuta shuka lile Ghafla aliliachia kwa haraka baada ya kuona kitu cha kushangaza. Hamu ya kulishika shuka lile ikaishia palepale. Kwa hofu akaanza kurudi kinyumenyume huku akitetemeka

"Ina maana yule binti alikuwa bado ana usichana wake au?" Alijiuliza huku akikisogelea kitanda kwa karibu zaidi. Upande mmoja wa shuka lile palitapakaa damu, tena damu mbichi.

"Looh! Nilimtoa damu nyingi sana mtoto wa watu. Lakini mbona kama nakumbuka hakulalamika kuumia? Na hakuonesha kama ni mgeni kwenye mambo yale, au ni maungo yangu yana michubuko?" Alijiuliza huku akitazama maungo yake. Yalikuwa sawa bila shida yoyote
Akiwaza hayo mlango ulizidi kugongwa. Zoezi la kukitazama kitanda likakoma, taratibu akaelekea hadi mlangoni.

"Nani?". Aliuliza

"Muhudumu hapa. Utahitaji kufanyiwa usafi ndani ya chumba labda?" . Sauti ya kike ilisikika.

"Sihitaji huduma yoyote kwa sasa, labda baadae". Kinje alijibu huku macho yake yakitazama kitandani.

" Sawa. Kukiwa na tatizo lolote usisite kutujulisha." Sauti ya mhudumu ilijibu, kisha kukafuatiwa na vishindo vya miguu, ni kama akiondoka
Kwa mwendo wa taratibu Kinje akajongea kilipo kitanda, akasogea hadi karibu na kitanda. Akalikamata shuka lile na kulivuta kwa nguvu.....

"Mamaaaaa!!"
Alijikuta akitoa ukelele wa ghafla. Yowe zito lilimtoka, hofu ilimzidi mara dufu baada ya kufunua shuka lile. Alichokiona kilitisha kutazama

"Mungu wangu! Damu zote hizi ni za Devotha kweli?. Hapana, labda naota mimi." Akajaribu kujifinya ahakikishe kwamba hakuwa anaota bali anachokiona ni uhalisia.
Haikuwa ni ndoto kweli. Anachokiona ni uhalisia na wala si ndoto
Kitendo cha kufunua shuka lile macho yake yalikutana na damu nyingi sana zilizotapakaa kitandani. Ilikuwa ni kama mtu kaimimina damu mbichi kitandani pale na kuifunika na shuka.
Vitu vitatu vilizidi kumchanganya.
Mwanamke aliyelala naye jana usiku hakuweza kumuona.
Ameamka akiwa mtupu kabisa bila nguo yoyote.
Kitanda kimetapakaa vibaya kwa damu.
"Damu ya nani hii sasa?" Akajiuliza lakini hapakuwa na jibu, wala yeyote wa kumjibu hakuwepo.

"Au kulitokea uvamizi hapa jana usiku wakamdhuru Devotha?" Alitafakari huku akizunguka huku na kule ndani ya chumba. Hatua tatu mbele, kisha nne nyuma. Ni kama alikuwa mwendawazimu.

"Haiwezekani. Kama ilikuwa hivyo kwanini hawakunidhuru na mimi basi?. Na huyu mhudumu aliyenigongea mlango ina maana hajui kinachoendelea kweli? Huu ni mtego nimewekewa bila shaka.".
Maswali yote yalipita katika kichwa chake kwa wakati mmoja. Taratibu akapiga hatua tatu hadi katika ukuta wa chumba chake. Taratibu akauegemea ukuta ule huku akijaribu kutafakari kama atakumbuka chochote kilichotokea jana.

"Aaaaaaah". Alijikuta akitoa ukelele wa maumivu baada ya kuegemea ukuta ule. Chini ya Bega la mkono wa kushoto karibu na mgongo alihisi maumivu makali sana. Yalikuwa ni maumivu makali yasiyoelezeka. Haraka akasogea hatua mbili mbele kutoka pale alipokuwa ameegemea.
Akapatazama pale alipokuwa ameegemea.

"Mmmmh! Damu?" Alitamka kwa mshangao. Pale ukutani palikuwa na damu. Tena damu mbichi kabisa. Akaigusa kwa kutumia kidole chake. Ilikuwa damu mbichi kabisa.

"Sasa damu hii imetoka wapi tena? Au nimeumia? Akajaribu kupeleka mkono wake wa kulia pale alipohisi maumivu.
Maumivu yakazidi kuwa makali.
"Mmh. Sio bure. Ngoja nielekee bafuni kuna kioo nikajitazame". Alijishauri.
Akafika bafuni. Kioo kikubwa kilichokuwa ukutani kilimpa taswira ya mwili wake kuanzia unyayo wa mguu hadi utosini.
Taratibu akageuka kukipa mgongo kioo kile. Akazungusha kichwa chake kutazama ni nini kinamsibu chini ya bega karibu na mgongo wake.

“Oh Mungu wangu. Nini hiki?". Alijikuta akitamka baada ya kuona kitu cha ajabu, taratibu machozi yakaanza kumtoka. Mwili ukaanza kutetemeka kwa ghadhabu

"Devotha umefanya nini hiki katika mwili wangu?. Devotha Devothaaaaa" Alipiga kelele kwa jazba akilia kama mtoto mdogo, alilia kilio kisichotoa ukelele.
Kilio kilikuwa cha mwendo wa kimya kimya.
Ni machozi tu na lawama katika nafsi zilimtawala.
Alichokiona hakuamini kabisa.
Alama ya mshono wa nyuzi uliyaaminisha macho yake ya kuwa alifanyiwa upasuaji eneo hili.
Ni muda gani basi nilifanyiwa huo upasuaji?
Swali hili likabaki katika kichwa chake pasipo hata jibu ama wa kumjibu.
Jeraha lile lenye mshono lilikuwa na urefu wa takribani centimita 12, taratibu maumivu nayo yalianza kupiga hodi hali iliyomfanya azidi kuchanganyikiwa na kupoteza nguvu ya kusimama.
Hapo ndipo akamkumbuka Kaka yake. Abuu. Hapo ndipo akaikumbuka simu yake. Akarejea chumbani kuangalia kama simu yake ipo. Katika kuitafuta simu macho yake yakatua mezani na kukutana na jambo lingine lililomuacha kinywa wazi. Mezani kulikuwa na bahasha kubwa moja pamoja na karatasi mbili. Akaisogelea ile meza, akaishika karatasi ile na kuisoma, ilikuwa ni nakala fupi ya mkataba

"YaH: MAKUBALIANO YA UUZAJI FIGO KUTOKA KWA MR KINJE MWAITIKA"
Kichwa cha habari cha mkataba ule kiliandikwa kwa herufi kubwa, maelezo ya mkataba ule yakieleza kwa mapana yake huku chini kabisa kukiwa na maelezo ya muuza figo kukubaliana na hili. Chini kabisa pakifuatiwa na sahihi yake mwenyewe.
Alichoka.
Je nini kitaendelea?. Una Mengi sana ya kujifunza katika kisa hiki. Usikose sehemu ijayo.

Simulizi hii itakujia hapahapa Japo kwa kuchelewa. Ila Kama ukiitaka yote kwa haraka utapaswa kulipia kiasi kidogo tu cha pesa. Tshs 1500 nami nitakutumia yote. Lipa kwenda Halopesa namba 0621249611 au Mpesa namba 0765824715 jina Gilbert
IMG-20220125-WA0001.jpg
 
ISHINI BADALA YANGU WANANGU
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi

Sehemu ya 05

Tulipoishia....
Kichwa cha habari cha mkataba ule kiliandikwa kwa herufi kubwa, maelezo ya mkataba ule yakieleza kwa mapana yake huku chini kabisa kukiwa na maelezo ya muuza figo kukubaliana na hili. Chini kabisa pakifuatiwa na sahihi yake mwenyewe.
Alichoka.
Songa nayo.....
"Yaani nimeuza figo yangu mimi? Kivipi?"
Akakumbuka maneno ya Kaka yake, mwanaye bado yupo kitandani hospitali ya Muhimbili akisubiri msaada wa figo, msaada ambao mtoaji anapaswa kuwa yeye.
Figo ipi tena atakayoitoa ilihali moja imeshaibiwa kinyamera?. Tamaa zake zimemponza, pendapenda zake kwa wanawake asiowafahamu zimemliza.

"Nimeingizwa choo cha kike, Kweli nimekaribishwa Bongo"... Alikiri Kinje huku machozi yakimtoka pamoja na makamasi membamba

Taratibu mikono yake ikaachia karatasi ile na kukamata bahasha ya kaki iliyotuna vyema. Akapata kuchungulia ndani ya baasha ile, akapata kuona noti nyingi nyekundu za Shilingi elfu Kumi ya Kitanzania.
Pembeni ya baasha ile akapata kuona pia bahasha ndogo, ndani yake akapata kuona vidonge vya aina tatu tofauti vya kumeza, vikimaanisha ni dawa zake anazotakiwa kutumia ili aweze kupona kwa wakati.
"Jamani jamani, yaani waniibie figo na dawa ya kutumia waniachie, dharau gani hizi jamani? Niwatukane tusi gani mbwa nyie?". Aliwaza
"Shenzi sana nyie,"
Tusi zito likamtoka, tusi lisilokuwa na mtu aliye karibu wa kulipokea.
"Mtairejesha wenyewe figo yangu, walai nawabia mtanitafuta wenyewe" alijinasibu kwa uchungu. Eti wamrejeshee wenyewe. Kweli akili zilimruka wasaa ule.
Akaanza kuitafuta simu yake ilipo lakini kwa bahati nzuri kabla hajaiona akapata kusikia ikiita, ilikuwa ikiitia katika mfuko wa suruali yake iliyotundikwa ukutani. Akaisogelea na kuitoa katika mfuko ule, akaitazama mpigaji ni nani.

"Abuu". Jina lilisomeka hivyo. Alipokea

"Mbona napiga simu tangu alfajiri hupokei wewe? Upo wapi?" Abuu aliuliza maswali mfululizo, alionekana kuchukia sana kwani alipiga sana simu ile.

"Kaka. Kaka njoo hapa hotelini sasa hivi nakuomba kaka". Kinje alizungumza huku akigugumia kwa kilio kinachoambatana na maumivu. Maumivu yalikuwa ni makali sana. Mbali na maumivu aliyokuwa akiyasikia, pia akili yake haikutulia sehemu moja.

"Upo sawa kweli wewe? Kimetokea nini?" Abuu aliuliza

"Kaka njoo kwanza utajua kila kitu. Naogopa hata kutoka nje kaka." Kinje alisema

"Duh! Hebu niambie upo hoteli gani ili nije hapo sahivi".
Kinje akamtajia jina la hoteli aliyoifikia kisha akakata simu. Hapo akaweza kuona orodha ya watu waliompigia, Mke Wake Clara alikuwa ni moja ya watu waliompigia pia. alipiga karibu mara tano huku Abuu akipiga zaidi ya Mara kumi. Akaona kwa lililotokea basi ule haukuwa muda sahihi wa kuwasiliana na mke wake kwanza.
______________________
Ni afadhali hakumtafuta mkewe kwa wakati huo kwani hata asingempata simuni. Wakati huohuo yote yakiendelea, katika mtaa wa Jang'ombe mjini Zanzibar, mtaa ambao ndipo ilipo nyumba ya Kinje ilionekana gari ya kubeba mizigo ikipiga honi nje ya geti. Sekunde chache baadae geti lile likafunguliwa, Mke wa Kinje ndiye aliyefungua geti lile. Gari ile ikapita ndani moja kwa moja na kupaki. Wanaume wawili wakateremka chini na kusalimiana na Clara, ambaye ni mke wa Abuu.
Wakati kinje akiagana na Kinje hapo jana, tumbo lake lilikuwa kubwa, ishara ya kuonyesha Clara ni mjamzito. Lakini leo hii hakuwa hivyo. Hakuonyesha kama ana ujauzito. Tumbo lake lilikuwa la kawaida sana. Tisheti nyeusi aliyovalia yenye neno OCAFONA ilimkaa vyema, huku chini akivalia suruali ya Jinsi, yenye rangi ya pinki, nayo ilimbana vyema. Leo Clara alikuwa tofauti sana na alivyokuwa jana na siku zote zilizopita nyuma. Zile dalili za uchovu utokanao na ujauzito hazikuwepo. Usoni alipendeza sana kutokana na vipodozi alivyopaka. Alubadilika mno.
Wanaume wawili waliokuwa ndani ya gari lile walifungua milango na kuteremka huku Clara akiwapokea kwa tabasamu la bashasha mpwitempwite.

"Umefanya Kazi nzuri sana Delila kwa kipindi chote ulichoishi na mwanaume huyu. Sasa ni wakati wa kwenda kuyafurahia matunda ya kile ulichokifanya ndio maana tumefika hapa." alisema mwanaume wa kwanza baada ya kushuka chini.

"Ina maana Delila umedhamiria kuisafisha kabisa nyumba ya bwana wako? Ila wewe bwana hata huridhiki na mshiko uliopatiwa. Haya na kazi ianze ya kupaki vitu harakaharaka." alizungumza mwanaume wa pili ambaye ndiye aliyekuwa dereva wa gari hilo lililoingia katika nyumba ya Kinje

"Bwana! Bwana gani huyo? Hivi kweli naye anajihesabia kwenye kundi la mabwana wa wanawake fulani? Yule mjinga angejua hata nilivyokuwa simpendi khaa. Sema tu nilikuwa kikazi hapa. Ila bahati imeangukia kwangu bila shaka naenda kuwa tajiri mimi, nimewapiku wanawake wengine waliotumwa kazi hii hahahahaha." Clara ambaye wanaume hawa walimwita kwa jina la Delila alisema huku akicheka. Jina lake halisi lilikuwa ni Delila na sio Clara kama mumewe alivyokuwa akimwita.
Kwa nini alitumia jina la Clara katika maisha ya Kinje? Ni kazi gani aliyotumwa kuifanya kwa kinje na sasa kaikamilisha?. Twende sawa.
______

Dae Es Salaam Tanzania

Baada ya lisaa limoja Abuu aliwasili hoteli ya Royal. Moja kwa moja akaelekea chumba namba 99 alichoelekezwa na Kinje. Akagonga mlango

"Kaka." Kinje aliita

"Ni mimi, fungua mlango," Abuu alisema
Kinje baada ya kujiridhisha sauti ni ya Abuu akamfungulia mlango. Abuu alipoingia macho yake yalitua moja kwa moja hadi juu ya kitanda. Wakati huo Kinje hakuwa mtupu tena, alishavaa bukta yake pamoja na shati lake.

"He' he' he'! Mungu Wangu. Kwani umeua au? Damu zote hizi ni za nani?. loooh!". Aliuliza Abuu katika hali ya mshangao. Mikono yote miwili aliipeleka kichwani.

"Sijaua Kaka nisikilize tafadhali". Kinje alijaribu kumtuliza Kaka yake amsikilize kwanza.

"Nikusikilize vipi mjinga wewe wakati umeniitia kwenye matatizo? Mwanangu ndo hivyo yupo hospitali anasubiria msaada wako halafu umeshafanya mauaji huku mbona hii tayari ni jela inatuita? Hiyo maiti ipo wapi. Au umeificha huku?".
Abuu alizungumza kwa jazba huku akichungulia uvunguni mwa kitanda. Uvunguni hakuambulia kitu zadi ya kinga iliyotumika usiku wa jana. Akaitazama kinga ile kwa sekunde chache kisha akanyanyuka.
Alimtazama kwa sekunde chache Kinje huku akitafakari.

"Bila shaka aliyeuwawa ni mwanamke." Abuu aliwaza

"Au umeificha hiyo maiti bafuni?". Abuu aliuliza huku akielekea bafuni.

"Abuu". Kinje aliita. Abuu akasita kuelekea bafuni. Akageuka kumtazama Kinje
Kinje alipoona Abuu kageuka haraka akavua shati lake akabaki kifua wazi.

"Mbona sikuelewi? Unataka kufanya nini?" Abuu aliuliza. Taratibu Kinje akageuka na kumpa mgongo Abuu. Akamtaka atazame eneo lile aliloshonwa.
ITAENDELEA

Je nini kitafuata baada ya hapo? Kwanini Clara ameitwa kwa jina la Delila baada ya kuonana na wanaume wale? Ni kweli hakuwa na ujauzito wa Kinje? Kunani kilichojificha? Tuwe wote katika sehemu ijayo ya Simulizi hii.

Kama unahitaji vipande vyote leo unaweza kuvipata kwa malipo ya Tshs 1000 tu kwa wewe mwanagroup. Hii itakuwa ni ishara ya kusapotiana katika kuandaa vitu vikali zaidi. Namba ya malipo ni HALOPESA NAMBA 0621249611 au Mpesa namba 0765824715
 
Simulizi Ya Maisha na Upelelezi; ISHINI BADALA YANGU WANANGU
Mwandishi; GILBERT EVARIST MUSHI
PHONE: 0765824715

Sehemu ya 06 na 07
"Abuu." Kinje aliita. Abuu akasita kuendelea na hatua anazopiga kuelekea bafuni.
Kinje alipoona Abuu amegeuka, haraka akavua shati lake akabakia kifua wazi..

"Mbona sikuelewi? Unataka kufanya nini?" Abuu aliuliza. Taratibu Kinje akageuka na kumpa mgongo. Akamtaka atazame eneo lile aliloshonwa.

Sura yake Abuu taratibu ikaanza kubadilika na kuleta alama za mikunjo mingi inayoendana na masikitiko, akaanza kumsogelea kwa karibu zaidi.

"Ina maana hizi damu zote kitandani ni zako? Nini kimetokea Kinje?".
Kwa ishara Kinje akanyoosha kidole chake kuelekea mezani ilipo ile baasha pamoja na mkataba ule. Abuu akaziendea na kuzisoma karatasi zile,

"Ilikuwaje hadi likatokea hili?". Abuu akauliza baada ya kuona kila kitu.
Kinje akawaza ajieleze vipi. Aseme aliingia tamaa akalala na mwanamke ndani ya chumba hiki?. Kama ni wewe msomaji ungeanzaje kusema basi au ungejielezaje?..

Akabaki njia panda akitafuta namna ya kumwambia kaka yake lakini ghafla kizunguzungu kilimshika, akaanguka chini na kupoteza fahamu palepale
---------------

Fahamu zilimrejea Kinje akiwa kitanda cha wagonjwa, pembeni ya kitanda kile alisimama Abuu pamoja na Daktari

"Ulipoteza damu nyingi sana kijana. Pole sana". Alizungumza Dokta baada ya kuona Kinje amefumbua macho yake. Kinje akauinua uso wake kutazama chupa ndogo ya damu aliyotundikiwa, damu ile ilikuwa ikikaribia kuisha.
Aibu ikamshika.
Eti figo imechukuliwa kisa okota okota ya visichana asivyovijua. Ni lazima aibu impate

"Unajisikiaje sasa hivi?". Aliuliza Daktari huyu anayefahamika kwa Jina la Dokta Viran. Kabla ya kujibu Kinje akajaribu kuinuka aweze kukaa lakini Dokta Viran akamuwahi na kumzuia.

"Angalau sasa hivi maumivu yamepungua daktari ila nahisi kuchoka sana."

"Muhimu ni kuzingatia maelekezo niliyompa kaka yako hapa, na pia dawa unywe kwa wakati. Tumejaribu kuangalia vidonge vile ulivyoachiwa pale hotelini baada ya tukio tukagundua ni vidonge vizuri sana na ni adimu kuvipata hapa Tanzania. Hivyo vitakusaidia, nakushauri endelea kuvitumia vidonge vile utapona haraka". Dokta Viran alieleza

"Yaani waniibie Figo yangu waniachie madawa yao halafu unaniambia eti nitapona kama nikizitumia hii inaingia akilini? Kwani nyie hamna dawa zinazonifaa mpaka nizitumie za hao washenzi?." Kinje akauliza kwa kufoka kidogo. Binafsi hakupendezwa na kitendo hiki. Aliona ni kama dharau alifanyiwa kwa kitendo cha kuachiwa dawa zile.
Kwa nadharia ni kitendo kibaya ndiyo. Lakini vipi kama Dokta anayeyajua madawa kashasema utampinga?

"Hapana, haipo hivyo kama unavyofikiri. Dawa walizokupatia ni dawa nzuri sana zinazoweza kukausha kidonda chako kwa haraka. Hapa hospitalini zipo dawa nyingi za aina hii lakini hazina nguvu kama hizi ulizopewa, dawa kama hizi ni nadra sana kuziona katika bara la Afrika, ni ghali mno. halafu pia inaonekana ulishazianza kuzitumia hivyo si busara kukubadilishia dozi"... Alieleza Dokta Viran ambaye kichwa chake kilipambwa kwa nywele nyeupe (mvi) zilizomjaa zikiashiria umri umesogea kidogo.

"Sawa, naomba nizungumze kidogo na Kaka yangu Dokta" Kinje akamsihi Dokta Viran kwa upole, bila kupinga daktari yule akatoka nje. Hapo Kinje akaanza kumwelezea Abuu tukio zima la kilichotokea kuanzia alipolala na mwanamke yule aliyejitambulisha kama Devotha hadi kulipokucha asubuhi.

"Duh!, hapo tatizo lishatokea sipaswi kukulaumu sana japo umezidi tamaa mno, kila siku wanawake na wewe. Kwahiyo sijui itakuwaje maana nilipokuleta hapa hospitali walikataa kukupokea hadi niende polisi. Kwa bahati nzuri huyu Dokta Viran alinisaidia sana na kuniunganisha na Inspekta mmoja hivi wa kike na ameshaanza kufwatilia jambo hili." Alizungumza Abuu huku akipiga hatua kadhaa mbele na kurudi nyuma.

"Kama Polisi wameshapata taarifa ni jambo la heri, ila huyu aliyefanya hiki kitendo lazima nimuue kwa mikono yangu. Ama zangu ama zake." Kinje alizungumza kwa jazba. Aliwaza namna ya kumpata kwanza Devotha ,yule mwanamke aliyelala naye. Yule ndiye atakayempa mahali pa kuanzia

Punde mlango ulifunguliwa. Aliingia mwanamke mmoja mrefu, mweupe na mnene kiasi. Kichwani alibana nywele zake vyema, katika mwili wake alivalia sare ya jeshi la Polisi iliyomkaa vyema.

"Naona Mgonjwa wetu amerejewa na fahamu. Vipi unajisikiaje sasa?" Aliuliza mwanamke yule ambaye mawazo ya Kinje yalimwaminisha yule ni Polisi.

"Najisikia nafuu Sasa hivi." Kinje alijibu

"Sawa, naitwa Inspekta Jasmine. Ni Inspekta wa jeshi la polisi na mimi ndiye nitashughulika na swala hili lililotokea hadi nihakikishe nawakamata waliohusika." . Alizungumza Mwanamke yule.

"Ohoo kumbe Inspekta Jasmine ndio wewe! Nilikuwa nikikusoma katika majarida na vitabu vya kijasusi, nikakukubali sana yaani" Kinje alisema kichovu.

"Hahaha' ndiye mimi hapa unaniona sasa. Ulinisoma katika jarida lipi mojawapo?" Aliuliza Inspekta Jasmine

"Kuna mkasa unaitwa Biashara ya Kifo ulitungwa na mwandishi mmoja hivi, nakumbuka niliusoma huo mkasa nikavutiwa sana na uwezo wako Afande"

"Ahaa kumbe. Sawa sasa tuachane na hayo yaliyopita tudili na yaliyokupata. Muhimu ni kwamba ninauhitaji sana ushirikiano wako kwani ushirikiano wako utafanya tuwabaini wahusika wote na kuwakamata. Sawa Kinje?"

"Sawa Inspekta Jasmine". Kinje akajibu kwa ukakamavu. Shughuli ya Inspekta Jasmine anaifahamu si ya Kitoto. Aliwahi kuliona balaa lake alipofwatilia baadhi ya mikasa kama ule uliopewa jina Mtoto wa Rais na mwandishi mmoja. Akajitahidi kujiinua ili akae lakini Inspekta Jasmine akamzuia

"Aaa wewe pumzika bado hujapata nguvu. Cha msingi ni wewe kuzingatia dozi na chakula upate nguvu. Nadhani baadae kidogo nitarejea tuzungumze mawili matatu. Sasa hivi naelekea kule hotelini kwanza kuna vitu nahitaji nivifahamu huko" . Alisema Inspekta Jasmine. Akaaga na kutoka nje.

"Leo ndiyo siku niliyotakiwa kuingia katika chumba cha upasuaji kwa ajili ya kumchangia Julieth Figo, lakini siku inapita hivihivi bila chochote kufanyika. Nitairejesha figo yangu tu, haijalishi nikiwa mfu ama napumua nitapambana. Ole wake yeye aliyefanya haya. Ole wake". Kinje alisema akimtazama Abuu

"Huu si muda wa kuwaza hayo Kinje mdogo wangu, muhimu ni afya yako kwanza. Tumshukuru Mungu maana unapumua. Je wangeuchomoa na huo moyo wako?. Shukuru kwa kila jambo" Abuu alimtuliza

"Nishukuru kwa kuibiwa figo? Kaka nikwambie kitu...' Kitendo cha wao kunifanyia hivi halafu wakaniwekea pesa na mkataba ni dhahiri wamenionyesha dharau kubwa sana. Lazima nami niwaonyeshe dharau kwao. Ni lazima."

"Hiyo dharau uwaonyeshe una ubavu huo? Jali afya yako halafu mengine waachie polisi bwana" Abuu alisisitiza

"We subiri utaona tu" Kinje alijibu huku akijitahidi kunyanyuka, mbali na Abuu kumzuia asijiinue pale kitandani, Kinje alilazimisha kuinuka. Kwa kiasi fulani dawa alizopewa na Dokta Viran zilimpa nguvu. Dripu ile aliyokuwa ametundikiwa ilikwisha damu hivyo bila kujali aliuchomoa mpira ule uliochomekwa katika mshipa wa mkono na kutoka nje.
Abuu akajua labda Kinje ananyoosha viungo vyake.
Hakujua. Hakujua

"Hey unakwenda wapi wakati hujapata ruhusa ya kutoka?" Aliuliza nesi mmoja wa kike baada ya kumwona Kinje akifwata uelekeo wa Geti kuu la Hospitali. Ilikuwa ni hospitali ya Mnazi mmoja, iliyopo karibu na bandari ya Dar es Salaam.

"Najaribu kupunga upepo nje angalau niuchangamshe mwili kidogo Dada yangu" Alimjibu nesi yule lakini mpango wake ulikuwa ni kutoroka pale hospitali. Kuna jambo lilimjia akilini mwake. Alipanga aelekee kwanza hoteli aliyofikia jana aangalie uwezekano wa kumwona Devotha.
Baada ya kuzuga zuga alifanikiwa kutoka pale hospitalini bila kuonekana. Kutoka pale hospitali ya Mnazi mmoja hadi ilipo hoteli ni umbali wa kama kilometa moja hivi.
Alipoingia barabarani alipanda pikipiki ya matairi matatu maarufu kama bajaji na kumtaka dereva ampeleke Royal Hotel.
Baada ya dakika tatu pikipiki ile ikafika nje ya geti kuu la hoteli na taratibu Kinje alianza kushusha mguu wa kushoto chini, akaushusha na wa kulia...

Ile kushusha tu mguu wa kulia akahisi kitu cha ubaridi kikipenya katika nyama za shingo yake. Akajaribu kugeuka atazame kulikoni lakini akashindwa, akaanguka chini kama gunia na hapo aliweza kuona ni nani kafanya lile. Kwa taswira ya mbali akaweza kumwona mwanaume mrefu kiasi amesimama nyuma yake. Alikuwa ni yule mwanaume aliyetaka kumbaka Devotha usiku wa jana kabla ya yeye kuja kutoa msaada.
Mwanaume yule alikuwa akitabasamu na mkononi alishikilia sindano. Sindano ambayo bila shaka ndiyo iliyotumika kumdunga nayo Kinje.
Kinje akajitahidi kukaza macho yake yaliyokuwa yakiikimbia nuru, lakini akashindwa. nguvu zilimwishia palepale.
Akapoteza fahamu palepale.
**********
Wakazi wa Mnazi mmoja walianza kurejea makwao taratibu huku Jua nalo likizidi kutokomea na kuukaribisha usiku. Usiku huo Kinje alikuwa Juu ya Kitanda cha hospitali ya Mnazi mmoja. Kaka yake kwa kushirikiana na Inspekta Jasmine walifanikiwa kumwokota barabarani akiwa hajitambui baada ya kumtafuta kwa takribani masaa manne, ndipo waliposikia habari za mtu kuokotwa barabarani akiwa hajitambui, wakamrejesha hospitali.
Siku ikapita bila Kinje kurejewa na fahamu zake.

Hatimaye ikawa ni siku nyingine mpya kabisa. Majira ya asubuhi kabisa Sauti za ndege waliao pamoja na watu wakizungumza ziliweza kumwamsha tena Kinje baada ya kupoteza fahamu kwa masaa Kumi na Saba. Kinje taratibu alifumbua macho yake kutazama eneo alipo.
Lilikuwa ni eneo geni sana kwake kwa wakati huo. Ni jana tu aliletwa hospitalini hapo lakini leo hii hakuwa anakumbuka kama aliwahi kufika eneo hili hapo kabla. Kila kitu kwake kilikuwa ni Kipya. Watu watatu waliosimama pembeni ya kitanda alicholalia walikuwa wakizungumza kwa pamoja.
Mmoja alikuwa ni Dokta Viran. Mwingine alikuwa ni Inspekta Jasmine, na wa pembeni yake alikuwa ni Abuu

"Sindano aliyodungwa ilikuwa na mchanganyiko wa dawa za usingizi pamoja na sumu iliyokwenda kuathiri ubongo unaohifadhi kumbukumbu zake"... Alizungumza Dokta Viran. Katika mwili wake alivalia koti refu jeupe huku macho yakisitiriwa vyema na miwani mikubwa

Abuu alionekana kushtuka sana baada ya kupewa taarifa ile. Juzi tu mdogo wake alipatwa na tatizo akiwa hotelini, leo tena kadungwa sindano? Mbaya zaidi sindano iliyomletea madhara katika ubongo wake.

"Dokta tafadhali fanya kitu mdogo wangu akae sawa. Kama hatokumbuka kitu chochote mambo yataendaje? Ooh Mungu wangu nini hiki jamani? Kila siku linaibuka jipya Oooh ".. Alilalama Abuu kwa sauti yenye kutia huruma.

"Hili swala litakuwa gumu sana kwangu na kwa jeshi la polisi kiujumla. Nilitegemea anieleze kilichotokea vizuri ili nijue ni wapi pa kuanzia. Ila ndo hivyo tena sijui kumbukumbu zake zitarejea lini" Inspekta Jasmine alimweleza Dokta Viran.
Maongezi yale yakiendelea Kinje alikuwa akiwatazama muda wote. Hakuwa anaelewa wanazungumzia nini na wale ni watu gani na wana lengo gani naye.
Alichokuwa anakielewa kwa wakati huo ni kwamba Njaa ilikuwa imemkamata haswa na si kingine.

Walipomuona Kinje amerejewa na fahamu na anawatazama walimsogelea. Abuu alianza kutokwa na machozi baada ya kumsogelea.
"Kinje unanikumbuka?" Abuu alimuuliza huku akimkazia macho.

"Kinje! Hili jina mbona kama niliwahi kulisikia hapo kabla?" Kinje alijiuliza kabla hajasema lolote, lakini hakupata jibu.

"Kinje ni nani?" Swali hili likawashtua watu wote watatu waliosimama mbele yake. Hakuwa anafahamu Kinje ni nani au ni kitu gani kwa wakati huo. Kuna muda alihisi kama hili jina si geni kwake lakini tatizo ni kwamba hakumbuki alilisikia wapi. Kwa upande wa Abuu machozi yalizidi kumtoka.
Machozi yale hayakubadilisha chochote kwa Kinje. Alimtazama Abuu na hakuwa anaelewa mwanaume huyo ni kitu gani kinamliza.
Inspekta Jasmine aliyevalia sare ya jeshi la polisi alimshika mkono Abuu ambaye muda wote alikuwa anatokwa na machozi, akatoka naye nje. Ndani ya chumba kile akabaki yeye na Dokta Viran.

Pole sana Kinje, kwa sasa umepoteza kumbukumbu zako hivyo hutaweza kukumbuka chochote. Nadhani unapatwa na mshangao kutokana na mazingira unayoyaona, Ila kadri siku zinavyozidi kwenda taratibu utakumbuka kila kitu. Unachopaswa kufahamu kwa sasa ni yule aliyekuwa anatokwa na machozi ni Kaka yako, Abuu. Na yule mwanamke ni Inspekta wa Jeshi la polisi anayechunguza jambo lililokupata,. Anaitwa Inspekta Jasmine. Atakuwa nawe karibu pia ili muweze kufanikisha mambo kadha wa kadha. Mimi ni Dokta Viran. Ni Mganga mkuu wa hapa hospitali ya Mnazi mmoja na nitakuwa nakuangalia hadi pale utakapopona, kwa sasa pumzika". Alisema Dokta Viran. Wakati wote Kinje alikuwa anamtazama tu kama anatazama kitu asichokielewa ama kukijua.

"Kwani mimi ni Mgonjwa? Mbona sijihisi kama naumwa?" Kinje alimuuliza dokta Viran. Dokta Viran akabaki akimtazama kwa masikitiko.

"Ndiyo, kwa sasa wewe ni mgonjwa, unaweza ukajiona upo sawa lakini haupo sawa kabisa".. Alijibu Dokta Viran.

"Kwani mimi naumwa wapi?" aliuliza Kinje.

"Nitakuelezea muda ukifika. Kwa sasa pumzika". Alisisitiza Dokta Viran huku akitoka nje.
Dokta Viran alipotoka tu nje aliingia Abuu akiwa amekunja uso. Akamsogelea Kinje pale kitandani akiwa amefura kwa hasira.
ITAENDELEA

Full vipande vyote vinapatikana inbox hapahapa whatsapp kwa Tshs 1000 tu, ni 1000 tu utaisoma yote leoleo. Lipia kwenda Halopesa namba 0621249611 au Mpesa namba 0765824715 kisha njoo inbox kwa namba 0621249611 nikutumie chapu.
 
Simulizi Ya Maisha na Upelelezi: ISHINI BADALA YANGU WANANGU
Mwandishi; GILBERT EVARIST MUSHI
PHONE: 0765824715

Sehemu ya 08

Dokta Viran alipotoka tu nje aliingia Abuu. Akamsogelea Kinje pale kitandani akiwa amefura hasira.

"Sasa kwanini muda ule ulitoroka hapa hospitalini ingali ulifahamu kabisa bado hujapona? Ona sasa yaliyotokea, unazidi kuongeza matatizo juu ya matatizo Kinje"... Abuu alianza kutoa malalamiko kwa Kinje ambaye hakuwa anatambua lolote kwa wakati ule. Mtu ambaye hata hajui yeye ni nani sembuse ya jana yake ayajue?

"Nilitoroka!!" Kinje aliuliza kwa mshangao.
"Nilitoroka muda gani mbona sikumbuki chochote? Na wewe ni nani mbona sikuelewi?" Kinje aliuliza

"Hivi ni kweli hukumbuki kilichotokea? Hata kilichokupata hukijui? Na mimi pia hunijui?" Aliuliza Abuu akiwa bado haamini. Alihisi Kinje alikuwa yupo katika hali ya Utani.

"Mnazidi kunichanganya jamani, yaani sielewi hili wala lile. Yule mzee mwenye nywele nyeupe kichwani anasema wewe sijui ni Kaka yangu na sina hata uhakika. Kuhusu kutoroka sijui chochote na wala sikumbuki kitu, nashangaa tu naamka hapa mnasema nipo hospitalini naumwa. Kwani mimi naumwa nini?"

"Uuuuuh." Abuu alihema juu juu, maneno ya Kinje ni kama yalimkata maini
"Kazi ipo." alisema Abuu.. "Ok ni Hivi.. Jana uli..." Kabla hajaendelea aliingia Inspekta Jasmine. Alipoingia tu akajikooza kidogo kisha akazungumza

"Abuu.., huu sio wakati wake. Muda ukifika ataambiwa kila kitu na mengine atayakumbuka mwenyewe." Alisema Inspekta Jasmine

"Bila shaka kuna jambo halipo sawa hapa. Wananificha nini haswa hawa? Au ni matapeli hawa? Itanibidi nikimbie hapa." Wakati Inspekta Jasmine akiongea na Abuu, Kinje alikuwa akijishauri huku akiwatazama kwa macho ya udadisi.

"Kila kitu kitakuwa sawa Kinje, usijali kumbukumbu zako zitarejea hivi karibuni. Dokta Viran ameniambia sindano uliyodungwa kwa bahati nzuri sumu yake iliingia kwa kiasi kidogo sana katika ubongo wako, na amenihakikishia utarejea katika hali yako siku si nyingi. Kuna dawa amekupa unywe kila siku kwani itasaidia kumaliza sumu yote".. Alizungumza Inspekta Jasmine akimtazama Kinje. Macho yake yalizungumza kwa hisia.

"Siwaelewi kabisa; Sindano gani nilidungwa kwani? Mbona sikumbuki kama kuna sindano nilidungwa?".. Kinje aliwauliza. Alipowauliza Inspekta Jasmine alitazamana na Abuu. Hii ikampa wasiwasi Kinje ambaye mashaka yalishaanza juu yao.
Wakanong'onezana kisha wakatoa ishara kama ya kukubaliana jambo.

"Jana uliletwa hapa na Kaka yako baada ya wewe kupoteza fahamu, Uliporejewa na Fahamu ulitoroka hapa na kwenda hotelini huko ndipo ulipodungwa sindano hiyo" Alieleza Inspekta Jasmine.
Mbali na kueleza lakini bado Kinje alikuwa njia panda.

"Huko hotelini nilikuwa nafwata nini hadi nikatoroka hapa?". Kinje akauliza tena.
Kabla Inspekta Jasmine hajajibu alitazamana tena na Abuu. Hii ikaongeza wasiwasi zaidi kwa Kinje.

"Kwa mujibu wa maelezo ya Kaka yako ni kwamba, Usiku wa kuamkia Jana ulipanda boti kutoka Zanzibar na kuja Hapa Dar es Salaam. Lengo lako ilikuwa ni kuja kumsaidia mtoto wa Kaka yako figo baada ya yeye kuwa na Uhitaji wa figo. Kabla hujakutana na Kaka yako usiku huo ulifikia Royal Hotel ambapo jana asubuhi ulimpigia simu Kaka yako na kumtaarifu afike hotelini hapo kuna shida. Alipofika alikukuta ukiwa na jeraha dogo la mchano nyuma ya mgongo wako chini ya bega la kushoto. Kilichotokea ni kwamba ulifanyiwa upasuaji na kutolewa figo yako moja. Hivyo kutokana na kupoteza damu nyingi ulipoteza fahamu na kuletwa hapa. Ulipozinduka ndio hivyo kama nilivyokueleza awali".
Alieleza Inspekta Jasmine. Maelezo yale yalikuwa ni kama wimbo wa Taarabu kutoka kwa Mtu wa pwani akimwimbia mtu wa bara. Kwake yalikuwa ni kama makelele tu kwani alikwishapoteza imani nao tangu wakati wananong'onezana. Hakuyaamini maneno yale kutoka kwa Inspekta Jasmine. Badala yake aliitikia kwa ishara ya kutikisa kichwa kuonyesha amemuelewa.
Hakuishia hapo tu. Akawataka wamuonyeshe hilo jeraha la mchano wanalodai kwamba alifanyiwa upasuaji.
Inspekta Jasmine bila kupinga alitoa simu yake na kumtaka avue shati alilovalia , akapiga picha kadhaa katika mgongo wake na kumuonyesha. Ni kweli palikuwa na bandeji nyeupe iliyoficha jeraha hilo, hiyo haikuwa shida sana, Mbali na kuonyeshwa lakini bado hakuamini. Alihisi ni mchezo umechezwa tu. Na hata kama ni kweli ametolewa figo yake basi ni wao wamemtoa.

"Hawa ni watu wabaya sana. Wananichezea mchezo ili wanitoe figo yangu. Nisipokuwa makini hapa nitaangamia. Yule Dokta naye hana hata aibu anathubutu kunidanganya kumbe ametengeneza mbinu chafu na hawa wanifanyie upasuaji. Hapa lazima nitoroke". Kinje alijisemea akiwa ametulia juu ya kitanda.

Kinje akamtazama Mwanaume aliyeelezwa kuwa ni Kaka yake. Hapo akaguna kidogo.
Akamtazama na mwanamke aliyevalia sare ya jeshi la polisi. Aliamini yule hakuwa afisa wa jeshi la polisi. Aliamini walikuwa wakimzuga ili wamfanyie aliyoyahisi kichwani mwake

Ama kweli mwenye macho haambiwi tazama. Ndivyo walivyosema wahenga. Ni kama Wahenga walimsemea Kinje kauli hiyo.

"Hata nikipiga kelele za kuhitaji msaada haitasaidia. Hapa sijui hata nipo wapi. Cha muhimu ni kuwategea nikipata upenyo niweze kutoroka hapa". Aliwaza Kinje.

Muda ulizidi kusogea huku wakizungumza mengi lakini bado Kinje alikuwa njia panda, hakufanikiwa kukumbuka chochote. Kuna muda Abuu alimkabidhi Kinje simu yake akihisi labda ndio njia ya kurahisisha mambo lakini bado haikusaidia, wala hakuamini kama simu ile ni yake na hata kuikumbuka hakuwa anaikumbuka kabisa.
Aliipokea zimu ile na kuiweka katika droo ya meza ndogo iliyo pembeni ya kitanda alicholalia.
Muda wote mawazo yake yalikuwa katika kupanga namna ya kuwatoroka.
-------------

Taratibu jua lilizidi kuzama na kuukaribisha usiku. Abuu muda wote alikuwa pembeni ya kitanda cha Kinje. Baada ya muda kidogo Abuu alipitiwa na usingizi. Usingizi ambao bila shaka Kinje aliushangilia sana.
Wakati huo Inspekta Jasmine hakuwepo. Tabasamu zito likamjia Kinje usoni. Akajinyanyua taratibu na kuvaa viatu alivyoviona sakafuni, akafunga vishikizo vya shati lake, kwa mwendo wa kunyata akausogelea mlango. Akakinyonga kitasa taratibu na mlango ukafunguka. Kabla hajapiga hatua kutoka nje akajiuliza ni wapi anaelekea akitoka hapa, Kumbukumbu zake hazikuwepo kwa wakati huo, hakuwa na imani kwa mtu yeyote kwa wakati huo

"Bora kuelekea popote tu nisipopajua kuliko kukaa hapa maana hawa watu sina imani nao kabisa." Aliwaza.
Akatoka nje, akashuka ngazi taratibu kuelekea chini kisha akajichomeka katikati ya watu waliokuwa wakifwata uelekeo wa geti kuu la Hospitali ya Mnazi Mmoja.

Alitembea kwa muda mrefu bila kufahamu ni wapi anaelekea kwa wakati ule. Njaa nayo ilimtesa huku maumivu nayo ya kidonda nyuma ya mgongo yalianza. Kumbukumbu ya maneno ya Inspekta Jasmine kwamba alifanyiwa upasuaji ilimjia. Akaamini kweli wale ni watu wabaya kwake. Walifanikiwa kumtoa figo halafu wanamuigizia eti wanamuuguza.

"Wale hawana lolote wale, wao ndio wamenipasua halafu wanadai nilipasuliwa, mbaya zaidi sikumbuki hata kwetu ni wapi. Sijui wamenifanyia kitu gani washenzi wale. Sijui nielekee wapi hata" Aliwaza Kinje

Akiwaza hayo mara akasikia sauti ya mlio wa gari ikija kwa kasi alipo. Kabla gari ile haijafika karibu yake ilisimama ghafla umbali wa hatua kama Tano kutoka alipo Kinje. Mara baada ya gari kusimama milango ikafunguliwa na akashuka Mwanaume mmoja mweusi mwenye mwili wa mazoezi, alivalia kaushi nyeupe pamoja na pensi ya kijivu. Pia aliteremka binti mmoja mrefu na mweupe kiasi. Binti yule alipomuona Kinje akamkimbilia huku akiwa na furaha.

"John mpenzi wangu upo hai!. Tumekutafuta sana jamani mume wangu". Alizungumza mwanamke yule huku akimkimbilia Kinje. Akaifungua mikono yake baada ya kumfikia, akamkombatia na kumuachia busu zito shavuni.
Mwanamke yule alikuwa akilia kwa uchungu mkubwa sana. Wakati huo Kinje alikuwa kama amepigwa na shoti ya umeme. Hakuelewa mwanamke huyu ni nani. Mbaya zaidi hakuwa anakumbuka yaliyopita. Mdomo wake ulikuwa ukichezacheza. Alitaka kuzungumza lakini hakupata neno la kusema kwa wakati huo.
Laiti Kinje angejua linalokwenda kutokea basi ni bora angebakia kule hospitalini. Hakujua ni hatari gani inamsogelea
Hakujua.
Je huyu mwanamke aliyemwita Kinje kwa Jina la John ni nani? Ni kweli ni mpenzi wake ama kuna mchezo Kinje anachezewa? Tuwe sote katika sehemu ijayo.

Full story njoo inbox nitakupatia, njoo kwa namba 0621249611 au 0765824715
 
Simulizi Ya Maisha na Upelelezi; ISHINI BADALA YANGU WANANGU
Mwandishi; GILBERT EVARIST MUSHI
PHONE: 0765824715

Sehemu ya 09

"John mpenzi wangu upo hai!. Tumekutafuta sana jamani mume wangu". Alizungumza mwanamke yule huku akimkimbilia Kinje. Akaifungua mikono yake baada ya kumfikia, akamkombatia na kumuachia busu zito shavuni.
Mwanamke yule alikuwa akilia kwa uchungu mkubwa sana. Wakati huo Kinje alikuwa kama amepigwa na shoti ya umeme. Hakuelewa mwanamke huyu ni nani. Mbaya zaidi hakuwa anakumbuka yaliyopita. Mdomo wake ulikuwa ukichezacheza. Alitaka kuzungumza lakini hakupata neno la kusema kwa wakati huo.

Mwanaume aliyekuwa ameambatana naye aliivua miwani yake nyeusi kisha akamtazama Kinje kwa sekunde kadhaa..
"John Upo sawa kweli?". Aliuliza mwanaume yule.

Hili nalo likawa jambo jipya Kwa Kinje. kutoka kuitwa Kinje alipotoka na sasa eti anaitwa John.
"Mbona sielewi kinachoendelea? Nyie ni kina nani?"
Kinje aliuliza kwa kubabaika huku akijitoa mwilini mwa mwanamke yule aliyemkombatia. Kitendo cha Kinje kuuliza vile kiliwapa tabasamu lisiloonekana wawili wale. Walikuwa kwenye harakati za kuthibitisha kama kweli Kinje alipoteza kumbukumbu zake ama Lah. Hii iliwaaminisha kile walichokihisi kwa wakati huo. Kinje hakuwa anakumbuka chochote.

"Hebu acha utani basi John, You are not serious for sure. Inamaana mara hii umeshanisahau? Au ndio mbinu ya kuniacha?" aliuliza mwanamke yule kwa sauti ya kulalamika.
Kinje akajaribu kutuliza akili yake kama ataweza kukumbuka chochote kumhusu mwanamke aliyeko mbele yake lakini Ghafla kichwa chake kilianza kumuuma.

"Aaaah aaaaah Kichwa changu aagh"
Alilalamika huku akishika kichwa chake kwa mikono miwili. Wakati maumivu yakizidi kuwa makali Kuna kumbukumbu ilikuwa ikimjia na kutoweka. Ilikuwa ni kumbukumbu ikimwonyesha mwanamke mwenye ujauzito akilia mbele yake japo sura ya mwanamke huyo hakuifahamu.
Wawili wale walisaidiana kumbeba Kinje na kumwingiza ndani ya gari. Mwanaume yule akawasha gari na kuielekeza katika barabara ya lami na safari ikaanza. Kwa muda wote Kinje alilazwa juu ya mapaja ya mwanamke yule na alionekana kumjali sana huku akimsihi hivi karibuni atakuwa sawa.
"Utakuwa sawa Mume wangu John" Alisema mwanamke yule ambaye muda wote alikuwa akilipapasa sikio la Kinje.
Mwanaume yule aliiendesha Gari kwa mwendo mkali sana. Nusu saa tu iliwatosha kufika Kimara Suka wakitokea Mnazi mmoja alipokuwa Kinje. Gari ilifika katika nyumba moja iliyozungushiwa ukuta mrefu huku Mazingira yakionekana ni ya kishua sana.
Honi ilipigwa na punde geti lilifunguliwa, gari ikaingizwa ndani. Kwa msaada wa yule mwanaume akishirikiana na mwanamke yule Kinje akanyanyuliwa taratibu kutoka ndani ya gari hadi ndani ya jumba lile la kifahari, sebuleni kabisa. Sebule ya nyumba ile ilipambwa kwa maua na rangi nzuri ya kuvutia ikishamirishwa na harufu nzuri ya manukato. Kinje alikuwa akiyapeleka macho yake kila kona ya nyumba ile akiwa bado anaitafakari yamkini kama aliwahi kuishi hapa.
Hakuwa anapafahamu

"Hapa ni wapi?" Alivunja ukimya baada ya kumgeukia yule mwanamke na kumuuliza.

"Hivi John umepatwa na nini mume wangu? Hadi nyumbani hupakumbuki kweli? Nini kimempata jamani?" Mwanamke yule aliuliza huku akijaribu kumsogelea Kinje kwa karibu zaidi. Kinje alipoona vile akasogea mbali zaidi hadi mwisho wa Kochi lile. Bado hakuwa na imani na watu hawa.

"Huyu itakuwa kuna kitu amepewa na wale watu waliomteka. Bila shaka kitu hicho kimemfanya hadi apoteze baadhi ya Kumbukumbu. Hii ni hatari kwake na kwetu pia kama hakumbuki chochote, itabidi tufanye kitu Magreth. Ila ngoja nimwite yule daktari wetu aje amhudumie, ndani ya wiki moja naamini atarudi katika hali yake ya kawaida" Alizungumza mwanaume yule ambaye muda wote alikuwa bize akibonyeza simu yake.

"Japo sikumbuki kama niliwahi kuishi hapa lakini watu hawa wanaonekana ni wenyeji wangu. Ni wakarimu sana na wananionyesha upendo tofauti na wale niliowakimbia kule" Kinje alijisemea baada ya kuwaza kwa sekunde kadhaa.
Yale maumivu ya kichwa yaliyokuwa yakimkabili hayakuwepo tena kwa wakati ule. Akapelekwa hadi ndani ya chumba kimoja kikubwa kilichosheheni kila kitu kinachostahili kukaa chumbani. Juu kabisa ya Ukuta Macho ya Kinje yalitua katika picha moja iliyotengenezewa fremu na kuning'inizwa. Ilikuwa ni picha yake akiwa katika tabasamu zito. Hii ikamfanya aamini pale ni nyumbani na huyo mwanamke aliye pembeni yake ndiye mkewe.

Ndani ya chumba kile walikuwa peke yao wawili tu. Yeye pamoja na mwanamke yule.
Wakati huo yule mwanaume alikuwa sebuleni akizungumza na simu katika harakati za kumwita Dokta. Dokta wa kuja kumhudumia Kinje au tuseme John kama wanavyomwita wao.

"Hivi jina langu ni Kinje au John? Maana sielewi kabisa. Kule wananiita Kinje, mara huku John". Kinje alimuuliza mwanamke yule huku akimtazama machoni.

"John mume wangu wamekufanyaje wale watu? Maana tangu jana usiku ulipotoka hapa nyumbani hukurudi, nikakupigia simu yako hata haukuwa hewani, kilitokea nini Mume wangu jana usiku?" Mwanamke yule aliuliza

"Kumbe mimi naishi hapa!" alijisemea Kinje. alijiaminisha zaidi katika nafsi yake.
"Jana usiku nilipoondoka nilikuaga naelekea wapi?". Kinje akauliza kwa udadisi wa kutaka kufahamu zaidi.

"Ulisema kuna Keki uliweka oda unakwenda kuichukua. Kwani hukumbuki jana ilikuwa ni kumbukizi ya siku yangu ya kuzaliwa?. Jana ulienda kuchukua hiyo keki lakini hukurudi. Hakika siku ya jana ilikuwa ni mbaya sana kwangu. Kwa bahati nzuri uliacha gari lako hukuondoka nalo, hivyo nililazimika kumpigia Moses Shemeji yako nikamwelezea baada ya wewe kukawia kurejea. Tukakupigia simu lakini haukuwa hewani, ikatulazimu tuelekee kituo cha polisi kutoa taarifa ili tuweze kufahamu upo wapi Mume wangu. Leo nikiwa napitapita na Shemeji yako katika harakati za kukutafuta ndipo tukafanikiwa kukuona"
Mwanamke yule alimweleza Kinje huku akiitomasa shingo yake. Maelezo haya kwa kiasi yalimwingia Kinje akilini.
Akayaamini.

"Kumbe yule mwanaume uliyekuja naye kunichukua ni shemeji yangu! Hata yeye simkumbuki kabisa. Mnisamehe bure tu maana huko walipokuwa wameniteka wamenifanyia vitu vingi sana. Kwanza nilizinduka nikajikuta nipo kitandani, mmoja anajifanya analia, eti anadai yeye ni Kaka yangu, mwingine anajitia yeye ni Polisi, huyo mwingine sasa, yeye ni Daktari eti wa kunihudumia. Kumbe wameniondolea kumbukumbu zangu. Halafu kuna kitu nimesahau kukuonyesha. Ona hapa". Kinje alisema huku akifungua vishikizo vya shati alilovaa.
Taratibu akajigeuza na kumpa mgongo mwanamke yule, akamwonyesha sehemu iliyofungwa kwa kitambaa cheupe.

"Oooh. Nini hiki Mume wangu?" aliuliza mwanamke yule kwa shauku ya kutaka kujua kimetokea nini.

"Nilipozinduka nikakutana na sura za watu wale, walinieleza eti nilitekwa sijui mara sijui nililala hotelini nikafanyiwa upasuaji ulionipelekea mimi kuibiwa figo yangu. Kiufupi sikuwaelewa kabisa. Nadhani kuna jambo baya wamenifanyia. Tuwatafute wanaharamu wale ikiwezekana wapelekwe polisi. Halafu hivi jina lako ni nani maana hata sikumbuki pia jina lako mke wangu Utanisamehe bure maana si kwa kupenda kwangu" Alieleza Kinje kisha akauliza kuhusu jina la mwanamke huyu anayedai ni mkewe.

"Usijali John Mume wangu. Mimi ni Magreth bwana. Utakumbuka yote muda ukifika tu. Dokta anafika muda si mrefu". Alijibu mwanamke yule.

"Lakini Magreth kwanini msingenipeleka kabisa hospitali kuliko kumuita dokta hapa nyumbani?" Kinje aliuliza. Kwa mbali ulionekana mshtuko ndani ya mwanamke huyu aliyejitambulisha kwa jina la Magreth, ni kama alihofia kitu fulani, lakini Kinje hakubaini mshtuko huo.

"Kwani John umesahau kwamba huwa hupendi kwenda hospitali kama tatizo si kubwa sana? Umesahau kwamba wewe ndiye uliyemtafuta daktari wa nyumbani awe anakuja kutusaidia pindi tupatapo tatizo? Unamkumbuka Fred? Ndio huyo Shemeji yako amempigia simu na muda si mrefu anakuja kukuangalia. Yeye ndiye atakayehakikisha kumbukumbu zako zinarejea Mme wangu". Alieleza Mwanamke huyu

"Ohoo, sawa ngoja tumsubiri japo simkumbuki huyo Fred". Kinje alijibu

Baada ya dakika chache ilisikika hodi,. Magreth akatoka nje kuangalia ni nani. Punde aliingia akiambatana na Mwanaume mmoja aliyebeba kibegi kidogo mfano wa brufcase, Kinje akayapeleka macho yake kwa mgeni huyo aliyeingia. Alipomuona tu mapigo yake ya moyo yalimuenda kwa kasi sana, naye mgeni yule alipomtazama Kinje aliyakwepesha macho yake kwa haraka.

Full story njoo whatsapp nitakupatia kwa 1000 tu, njoo kwa namba 0621249611
 
Simulizi Ya Maisha na Upelelezi; ISHINI BADALA YANGU WANANGU
Mwandishi; GILBERT EVARIST MUSHI
PHONE: 0765824715

Sehemu ya 10

Baada ya dakika chache ilisikika hodi,. Magreth akatoka nje kuangalia ni nani. Punde aliingia akiambatana na Mwanaume mmoja aliyebeba kibegi kidogo mfano wa brufcase, Kinje akayapeleka macho yake kwa mgeni huyo aliyeingia. Alipomuona tu mapigo yake ya moyo yalimuenda kwa kasi sana, naye mgeni yule alipomtazama Kinje aliyakwepesha macho yake kwa haraka.

"Mbona nakuwa hivi? Nahisi hasira sana baada ya kumtazama sijui kwanini. Huyu mtu bila shaka atakuwa si mwema kwangu". Kinje aliwaza.

"Huyu ndiye yule Dokta Fred niliyekuambia mume wangu". Alisema Magreth huku akimuonyesha mgeni yule ishara ya mahali pa kukaa.

"Vipi kwani Shem. Inamaana amenisahau kabisa hadi unamkumbusha? Yeye si ndiye aliyenitafutaga niwe daktari wa familia yenu?" Aliuliza mwanaume yule aliyetambulishwa kwa jina la Dokta Fred

"Acha tu shemeji yangu. Yaliyomkuta mume wangu hata sielewi, Kaka yangu Moses ndio kwanza kaelekea polisi kufwatilia haya mambo maana inaonekana mume wangu alitekwa, mbaya zaidi hakumbuki chochote kilichopita, hadi mimi alinisahau, nyumbani pia alipasahau kabisa. Hebu fanya mpango kwanza ukague hili jeraha mgongoni mwake limetokana na nini". Alieleza Magreth.
Kinje alibaki tu kuwa msikilizaji na mtazamaji

"Usijali Shem. Hebu John lalia tumbo hapa kitandani niweze kutazama kulikoni. Vua kabisa hili shati" Aliamuru Dokta Fred.
Bila kusita Kinje akafanya kama alivyoambiwa. Alivua shati lake kisha akalalia tumbo pale kitandani.
Bila kuchelewa Dokta Fred akafungua kibegi chake na kutoa baadhi ya vifaa, akavaa na gloves kisha akamsogelea Kinje kwa karibu zaidi. Alianza kufungua kitambaa kile kilichofungwa kwa umakini wa hali ya juu na muda wote kila mtu alikuwa kimya ndani ya chumba kile.

Kwa jinsi alivyokuwa akiigusa ngozi katika mgongo wa Kinje ni kama kuna kumbukumbu zilikuwa zikija na kugoma katika ubongo wa Kinje.
Fred akachukua pamba laini na kuanza kugusagusa taratibu katika jeraha lile dogo lililo katika mgongo wa Kinje.

"Kwa jinsi hali ilivyo, inaonyesha alifanyiwa upasuaji na kutolewa figo yake ya upande wa Kushoto shem"
Alisema Fred huku akizidi kugusagusa eneo lenye jeraha.

Kwa jinsi alivyokuwa akizidi kugusa jeraha lile hisia za Kinje zilienda mbali sana. Alianza kuhisi ni kama yupo kitandani na pembeni yake wamesimama watu wawili wenye visu na mikasi maalum ya kufanyia upasuaji, akahisi kuchanwa chini ya bega lake la kushoto. Mara kumbukumbu ya mwanamke akimpa kinywaji akiwa kitandani ikapita kichwani kwake. Haraka sana kwa kasi kubwa aligeuka na kuikamata shingo ya Dokta Fred aliyekuwa akiligusa jeraha lake. Akili yake ilimtuma kwa wakati huo kuwa Fred ndiye aliyemfanyia upasuaji na kumtoa figo yake.

"Figo yangu uliipeleka wapi? Nataka figo yangu naitakaa.... nitakuuaaaa...."
Kinje aliropoka kwa sauti ya juu huku akimnyonga Fred. Alikuwa akitetemeka kwa ghadhabu wakati huo.
Ghafla kofi zito likatua katika shavu la Kinje

"Paaaaah". Ulisikika Mlio wa kofi kutoka katika mkono wa Magreth. Kwa jinsi kofi lile lilivyopigwa katika shavu la Kinje ilikuwa ni vigumu kuamini kama mpigaji ni Magreth mtoto wa kike. Lakini ndo hivyo mpigaji alikuwa ni yeye.

"Unafanya nini John? Huyu ni Fred acha ujinga unaoufanyaaa" Alizungumza kwa jazba Magreth.
Zile kumbukumbu pamoja na hisia zikatoweka ghafla katika kichwa cha Kinje. Ni mivumo ya upepo alikuwa akiisikia katika sikio lake la kushoto kutokana na kibao kikali alichonaswa. Hapohapo kichwa kikaanza kumuuma sana, hali iliyompelekea aanze kugugumia kwa maumivu.
Ni Sikio moja tu la upande wa kulia ndilo lilikuwa linafanya kazi kwa wakati huo. Na ndilo lililoisikia sauti ya Magreth ikizungumza na yule Daktari aliyetambulishwa kama Dokta Fred

"Huu ndiyo wakati sahihi Fred fanya sasa usimcheleweshe huyo" Alisema Magreth.

Kwa haraka Fred akaitoa sindano na kuichomeka katika kichupa kidogo ambacho kilikuwa na majimaji yenye rangi ya zambarau, akayavuta majimaji yale kwa kutumia sindano aliyoikita kwenye chupa ile.
Magreth akamsogelea Kinje kwa karibu na kumkombatia. Akajifanya kumtuliza Kinje aliyekuwa akiweweseka kwa maumivu makali ya kichwa. Haraka Fred akazunguka hadi nyuma ya Kinje akiwa ameishikilia sindano ile yenye majimaji ya zambarau tayari kwa kumdunga Kinje.
Kinje akahisi Kitu cha ubaridi kikipenya katika shingo yake, hii ikamkumbusha siku mbili zilizopita tukio kama hili la kudungwa sindano katika shingo yake lilifanyika. Akajitahidi kugeuka lakini Magreth alianza kumshambulia kwa mabusu motomoto huku akimtia moyo atapona tu hivi karibuni.

"Tumwache Dokta afanye kazi yake Mume wangu. Utapona tuu" Alisema Magreth huku akipambana kunyonya lipsi za Kinje
Kwa haraka Kinje akamsukuma Magreth, akajitahidi kugeuka. Macho yake yakatua kwa Fred aliyekuwa ameshikilia sindano mkononi.
Labda tuseme Fred alimchoma Kinje sindano ile kwa lengo la kumsaidia apone. Lakini iweje mkono ulioshika sindano utetemeke?. Nini lengo la Fred na Magreth?
Fred alizidi kutetemeka haswa mikono yake miwili alipoona Kinje amegeuka na anamtazama. Alikuwa ni kama mtu mwenye hofu na mashaka. Palepale Kinje aliishiwa nguvu na kumdondokea Magreth kifuani.
--------------------

Siku mbili zlipita. Siku inayofuata Kinje alizinduka kutoka usingizini, ikiwa ni siku mpya kabisa tofauti na siku aliyodungwa sindano. Alipozinduka awamu hii alijihisi tofauti kidogo. Mwili ulikuwa mwepesi sana na maumivu ya kichwa hayakuwepo. Kumbukumbu zake bado hazikurejea pia
Mazingira nayo yalikuwa ni tofauti kabisa. Ilikuwa ni kama yupo katika kitanda cha wagonjwa, chumba nacho kilikuwa na mwonekano kama cha hospitali. Pembeni kulikuwa na stendi ya chuma yenye chupa ndogo ya maji iliyoning'inizwa, mrija mwembamba wa chupa hiyo ulielekea hadi katika mkono wake.
Kumbukumbu zake zinamwambia mara ya mwisho alikuwa na Magreth pamoja na Daktari Fred. Sasa Wapo wapi? Akajaribu kuita.

"Magreth. Magreeeth". Aliita. Alikwisha amini Magreth alikuwa ni mke wake.
Taratibu mlango ukafunguliwa, mguu mmoja ukatangulia ndani, ukafwatiwa na mwingine, Hapo kinje akastaajabu baada ya kumwona aliyeingia ndani.
Alikuwa ni Dokta Viran. Mapigo ya moyo yalianza kumwendea Kinje kwa kasi sana. Mawazo yake yalimwambia aliyeko mbele yake ndiye mbaya wake.

"Nimefikaje hapa wakati nilikuwa nyumbani na Magreth?" Akabaki akijiuliza. Akiwaza hilo Dokta Viran akamsogelea kwa karibu zaidi kisha akaketi jirani naye.

"Kinje". Dokta Viran aliita
Kinje aliamini hilo halikuwa jina Lake halisi.
Yeye anaitwa John. Jina ambalo ni kama lilitumiwa na maadui kumlaghai. Lakini hakulitambua hilo

"Kinje".
Dokta Viran akarudia kuita tena. Awamu hii aliita akimkazia Kinje macho.

"Unamaanisha nini kuniita Kinje? Mimi naitwa John" alisema Kinje. Dokta Viran alibaki akimtazama kwa sura iliyojaa masikitiko.
ITAENDELEA
Kama utahitaji kutumiwa yote nicheki inbox whatsapp, nitakutumia kwa Tshs 1000 tu. Lipa kwenda Halopesa namba 0621249611 au Mpesa namba 0765824715

Naam, Anaitwa John Kinje. Tumwelewe vipi Kinje? Kwa staili hii atarejesha kumbukumbu zake kweli? Usikose sehemu ijayo hapahapa.
 
Simulizi Ya Maisha na Upelelezi; ISHINI BADALA YANGU WANANGU
Mwandishi; GILBERT EVARIST MUSHI
PHONE: 0765824715

Hii ni Sehemu ya 11

"Unamaanisha nini kuniita Kinje? Mimi naitwa John" alisema Kinje. Dokta Viran alibaki akimtazama kwa sura iliyojaa masikitiko.

"Kinje ni Jina Lako. Pole sana kwa yaliyokukuta. Tatizo lako mbali na kupoteza kumbukumbu ni ubishi tu unao. Tulikuambia upumzike muda ukifika kumbukumbu zako zitarudi lakini ukatoroka, hatimaye wamekudunga madawa mengine tena yanayozidi kuharibu ubongo wako. Dawa nilizokupa zilikuwa ni nzuri sana na za uhakika katika kuiondoa sumu ile lakini ulituona sisi ni Mafala siyo? Hata kama umepoteza kumbukumbu zako lakini kwanini ufanye mambo ya hovyo kama mtoto? Huko ulipokuwa umefaidika nini?" Alizungumza Dokta Viran kwa upole wa hali ya juu. Maneno aliyokuwa akiyatoa yalikuwa ni makali sana lakini sauti isemayo maneno hayo ilitoka kwa upole.

"Mmmh! Ina maana Magreth hakuwa mke wangu bali aliniteka? Lakini inawezekana vipi wakati alikuwa akinitafuta na gari? Isitoshe aliponiona alinikimbilia na kunikombatia huku akilia. Kila mtu akiniona anaonyesha kunijua nimwamini nani sasa?" Kinje aliuliza

"Mke wako ulimuacha Zanzibar ulipokuja hapa Bara. Huyo mke mwingine unayemtaja ulimuoa lini? Akili yako inachezewa hovyo san lakini wala hujali. Au huoni faida kuishi? Huna wanaokujali? Huna familia?. Inspekta Jasmine anajitahidi kuutafuta ukweli lakini wewe ndiye unayeuficha ukweli huo. Na huyo mwanamke unayesema ni mkeo pia ni mmoja kati ya watu wanaojitahidi kuuficha ukweli. Ulipaswa kutulia kumbukumbu zako zirejee ndipo Jasmine aweze kuifanya kazi yake kwa usahihi. Kaka yako anapambana kila kukicha urejee katika hali yako lakini kwa unayoyafanya amekata tamaa kabisa juu yako. Kila akisikia jina lako anatokwa na machozi ya uchungu; Kwanini usitulie hadi utakapopona?"
Maneno ya Dokta Viran kwa kiasi fulani yalianza kumwingia Kinje. Akaamini kweli alipo yupo katika mikono salama, japokuwa imani hiyo haikuwa kwa asilimia mia moja..

" Nimeanza kugundua sikuwa sahihi Dokta. Jana nakumbuka kama yule mwanamke alimleta Dokta wa kunihudumia lakini alinichoma sindano na hapo sikujua kilichoendelea". Kinje alisema

"Sio jana. Una takribani siku mbili hapa kitandani baada ya kuokotwa huko Bunju karibu na ule uwanja Wa Timu ya Simba. Kuna mashabiki walikuwa wakienda kutazama mazoezi ya timu yao ndipo wakakuona ukiwa katikati ya barabara umelala ukiwa huna fahamu. Kwa bahati nzuri Inspekta Jasmine alipewa taarifa ndipo akaenda kukuchukua na kukuleta hapa" alisema Dokta Viran

"Uuuh" Kinje alitoa nje pumzi ndefu baada ya kusikia maelezo haya kutoka kwa Dokta Viran. Alijua tukio lilifanyika jana tu lakini ukweli ni kwamba siku mbili zilipita akiwa kitandani hana fahamu. Anapoelezwa hayo na Dokta Viran ilikuwa ndiyo siku ya tatu imeingia. Laiti kama angerejewa na kumbukumbu zake angalau kwa sekunde mbili basi angejilaumu sana kwa ujinga wake anaoufanya. Lakini ndio hivyo hatambui kutokana na kutokukumbuka.

"Ulikuwa ni uzembe wangu Daktari samahani sana kwa kuwasumbua hadi nimejiletea matatizo zaidi" Alisema Kinje kwa upole.

"Huna sababu ya kujilaumu maana hata hivyo huna kumbukumbu kitu ambacho ingekuwa si rahisi kuamini kila kitu". Alisema Dokta Viran
Dokta Viran alikaa ndani ya chumba kile karibu masaa mawili, alikuwa akizungumza na Kinje. alisema naye mambo mengi sana, mambo ambayo ni kama alikuwa akizungumza na mgonjwa wa akili. Kwa asilimia kubwa Kinje akabakia kuwa msikilizaji. Dokta Viran alimjenga kisaikolojia kwa kiasi kikubwa, zile asilimia za uaminifu juu yake zikapanda kutoka chini ya mia moja hadi mia moja yenyewe. Alitakiwa atulie hadi pale atakaporejewa na kumbukumbu zake.
Kinje akaahidi kufuata kile Dokta Viran alichokisema. Akaahidi kutulia hadi pale kumbukumbu zitakaporejea.

Baada ya kuongea kwa muda mrefu Dokta Viran alitoka nje. Akaingia Abuu. Ambaye aliambiwa kuwa ni Kaka yake. Kinje akamwomba radhi kwa yote yaliyotokea. Abuu akamtaka mdogo wake awe tu mtulivu hadi pale atakapokuwa sawa kama zamani.

"Unajua Kinje kuna jambo silielewi kabisa".. Alisema Abuu akiwa sambamba na Kinje ambaye hana kumbukumbu zake bado

"Jambo Gani hilo Kaka?"

"Japo umepoteza kumbukumbu zako lakini ngoja nikuelezee kwa ufupi. Ujue ulipotoka Zanzibar ulimwacha Mkeo akiwa ni Mjamzito, ulikuja huku kwa ajili ya jambo fulani hivi nadhani ukirejewa na kumbukumbu zako utalijua ni jambo gani lililokuleta huku. Sasa ninachoshangaa tokea siku ile ulipofika Dar es Salaam hadi leo Mkeo hajakutafuta kabisa. Yaani hajakupigia simu kabisa hata akujulie hali. Ninaweza kusema labda hakupiga kwa sababu hukumpigia pia, lakini nachojiuliza ni kwamba iweje hadi mimi pia kila nikijaribu kumpigia nimwelezee yaliyotokea lakini naambiwa namba haipatikani?. Na leo ni siku ya nne toka nianze kumtafuta kwenye simu yangu lakini hapatikani" Abuu ulieleza

"Yaani Kaka ukianza kuniambia vitu kama hivyo unanichanganya. Tuyaache haya hadi nikae sawa kumbukumbu zirejee kwanza ndipo nitakumbuka ya nyuma na tutajua tufanye nini". Kinje alimwambia Abuu

"Unachosema Kinje ni sahihi kabisa. Lakini mwenzako hatambui upo katika hali gani, unaweza kukuta kakukalia kimya naye baada ya kuona upo kimya. Ndiyo maana nilimtafuta".

"Sawa. Hivi Inspekta Jasmine yupo wapi?" Kinje alibadili mada.

"Nadhani atakuwa bado mgahawani maana nilimwacha akipata supu. Unamuhitaji?"

"Hapana, nilitaka tu nimsalimie nimwombe na msamaha kwa kumfanya ahangaike kwa ajili yangu"

"Sasa kuhangaika si ndiyo kazi yake?. Ukishakuwa Inspekta wa jeshi la Polisi kuhangaika mbona ni lazima" Alisema Abuu.
Walipiga stori kadhaa hadi pale alipofika Inspekta Jasmine. Leo hii hakuvalia magwanda yake ya kikazi. Alivaa kiraia kabisa. Tisheti nyeusi iliyomkaa vyema na Suruali ya Jeans ilitosha kuusitiri vyema mwili wake.

"Ooh Kinje umeamka. Vipi unajisikiaje?". Aliuliza pindi tu alipoingia ndani.

"Naona nipo sawa Afande, japo Kumbukumbu za nyuma bado"

"Kuhusu hilo usijali. Namwamini Dokta Viran kwa asilimia mia. Siku si nyingi utakumbuka kila kitu. Ila kwa sasa nahitaji kukuuliza baadhi ya mambo nipate kuyajua" Alisema Inspekta Jasmine

"Hivi juzi ulipotoroka hapa hospitali unakumbuka ilikuwaje huko ulipoenda?"

"Ndiyo. Nilipotoka hapa nikiwa barabarani kuna gari ilikuja karibu yangu akashuka mwanaume na mwanamke. Yule mwanamke alidai kuwa yeye ni mke wangu na amesumbuka sana kunitafuta. Tena aliniita kwa jina lingine tofauti na hili mnaloniita sasa. Aliniita kwa jina la John". Kinje akaeleza

"Walikupeleka wapi baada ya hapo?"

"Kwenye nyumba moja kubwa ipo nje ya mji nadhani, huko hapajachangamka sana japo mazingira yake ni ya kishua. Aliita Daktari, lakini huyo daktari nilipomuona tu mapigo yangu ya moyo yalienda kwa kasi sana. Ni kama niliwahi kumwona mahali hivi japo sikuweza kukumbuka nilimwona wapi."

"Unakumbuka huyo daktari aliyeitwa alifanya nini baada ya kufika?

"Ndiyo Nakumbuka. Kila alipokuwa akisafisha jeraha langu ni kama kuna kumbukumbu zilikuwa zikinijia na kuondoka. Halafu pia nilimsikia yule Mwanamke akimsihi Dokta yule afanye kitu. Na nilimwona yule dokta akikamata sindano. Alinidunga shingoni, na mikono yake ilikuwa ikitetemeka haswa. Baada ya hapo sikumbuki kilichofuata ndio leo najikuta nipo hapa". Kinje alieleze

"Unaweza kunielezea mwanamke huyo alikuwa na mwonekano gani?" Inspekta Jasmine alimuuliza

"Ndiyo."
Inspekta Jasmine akatoa simu yake na kuibofya kwa sekunde kadhaa. Akaiweka sikioni kuonyesha anampigia mtu. Akazungumza na simu ile huku akitoa maelekezo kwa mtu aliyepigiwa.
Baada ya dakika ishirini alifika hospitalini pale Askari Kijana anayesifika kwa utanashati pengine kuliko hata Askari vijana wote nchini. Alikuwa ni Adrian Kaanan. Ndiye aliyepigiwa simu ile na Inspekta Jasmine
Adrian alipofika akaingia moja kwa moja hadi katika wodi za watu maalum (Private), na huko akawakuta Inspekta, Kinje na Abuu. Baada ya salamu bila kuchelewa alifungua mkoba wake aliokuja nao na kuchomoa karatasi nyeupe pamoja na penseli ya kuchorea.

"Kinje. Kutana na Adrian Kaanan. Ni Afisa wa Polisi idara ya tehama katika kituo chetu cha Kati hapa Dar es Salaam. Huyu sifa yake kuu ni Askari mtanashati japo kwenye kazi hana utanashati wala utanablauzi. Atakuwa nasi sote katika operesheni hii ya kuwakamata wote waliohusika katika kukufanyia haya yote. Haya tuelezee huyo mwanamke aliyejitambulisha kwako kama Magreth alikuwaje kimwonekano" Alisema Inspekta Jasmine

Bila kuchelewa Kinje akaanza kuuelezea mwonekano wa Magreth. Muda wote akiuelezea mwonekano wa Magreth, Adrian alikuwa bize na karatasi na penseli aliyokuja nayo. Alikuwa akichora.

"Katika kuelezea mwonekano wa mwanamke upo vizuri kweli. Si ajabu ni kwa wanawake tu ndio unajua kuwachambua eti". Inspekta Jasmine aliweka utani kidogo. Kila mtu akajikuta akitoa kicheko
Baada ya kutoa maelezo kwa kina juu ya mwonekano wa Magreth sasa wote walikuwa wakisubiri Askari Kijana amalize kazi yake.
Je baada ya kuongezeka kwa Adrian watafanikiwa kukipata wanachokitafuta? Tukutane Kesho kutwa hapahapa.

Kama utahitaji kutumiwa yote unaweza kunicheki kwa namba 0621249611 au 0765824715 nitakupatia kwa Tshs 1000 tu.
 
Simulizi Ya Maisha na Upelelezi; ISHINI BADALA YANGU WANANGU
Mwandishi; GILBERT EVARIST MUSHI
PHONE: 0765824715

Hii ni Sehemu ya 12

Baada ya kutoa maelezo kwa kina juu ya mwonekano wa Magreth sasa wote walikuwa wakisubiri Askari Kijana amalize kazi yake.

Adrian baada ya dakika 25 alifanikiwa kumaliza kazi yake. akamkabidhi Inspekta Jasmine karatasi ile. Inspekta Jasmine akaitazama kwa sekunde mbili tatu kisha akaisogeza hadi kwa Kinje.
Kinje akaikamata karatasi ile na kuitazama kwa sekunde tatu.

"Loooh. Huyu jamaa anajua kuchora hadi anakera". Kinje alipayuka kwa sauti ya juu iliyomfanya kila mtu atabasamu
Ilikuwa ni taswira ya magreth haswa. Alikiri Adrian alikuwa fundi katika kuchora.
Picha ile ilichukuliwa na kwenda kutiwa rangi. Baada ya kutiwa rangi Ilizidi kuleta taswira halisi ya Magreth

Inspekta Jasmine akawaacha Kinje pamoja na Abuu pale hospitali, akaongozana na Adrian kwenda kumsaka Magreth popote alipo.
**********

Ilipita siku, zikawa siku na hatimaye wiki. Ndani ya wiki yote harakati za kumsaka Magreth hazikuzaa matunda. Inspekta Jasmine kwa Kushirikiana na Adrian walijitahidi kwa kila njia lakini hawakuweza kumtia mikononi mwao Magreth.
Afya ya Kinje nayo ilizidi kuimarika na ule mshono jeraha lilipona kabisa. Dokta Viran akampatia ruhusa kutoka hospitalini arajee nyumbani.
Kwa kuwa kumbukumbu zake bado hazikurejea, Abuu akalazimika kumchukua mdogo wake akaishi naye hadi pale mambo yatakapokuwa sawa.

Nyumba ya Abuu ilikuwa ni ya kisasa na nzuri yenye kuvutia, pia ilikuwa na mfanyakazi wa kike ndani ya nyumba kwa ajili ya usafi na kuandaa chakula.
Tangu afiwe na mkewe miaka michache iliyopita maisha ya Abuu hayakuwa na uchangamfu hata kidogo. Alikuwa ni mtu wa mawazo muda wote. Mawazo ya kumpoteza mkewe pamoja na ya kulazwa kwa mwanaye hospitalini. Mara nyingi hakuwa mtu wa kulala nyumbani kwake, leo alilala kwake na kesho akashinda hospitalini pembeni ya kitanda cha mwanaye Julieth. Abuu alitegemea Kinje angetolewa figo moja na kuwekewa Julieth ili mambo yakae sawa lakini tangu majanga ya kuibiwa figo yamtokee Mdogo wake alizidi kukonda. Hakuwa katika uchangamfu hata kidogo kitu ambacho kilifanya hata biashara zake zianze kufa taratibu. Mara nyingi Abuu alikuwa akiwaona watoto wadogo katika pitapita zake alitokwa na machozi.

"Kaka. Mbona kila mara ukiwaona watoto wadogo unatokwa na machozi? Nini tatizo?." Kinje alimuuliza kaka yake siku moja walipokuwa wakirejea nyumbani majira ya jioni wakitoka Kariakoo katika biashara zao

"Unayafahamu sana tu lakini kwa sasa huwezi kukumbuka hata nikikuelezea. Siku sio nyingi utafahamu kwanini." Alisema Abuu

"Kesho tutaelekea muhimbili kumwona Julieth ". Alisema Abuu wakati wa jioni wakipata chakula.

Ilikuwa ni Jumapili majira ya asubuhi, Dada wa kazi aliandaa chai mapema sana tofauti na siku zote. Ni kutokana na na Safari ya kuelekea Muhimbili ambapo Abuu alimwahidi Kinje wangeongozana pamoja kwenda kumwona Julieth. Wakapata chai ya nguvu kwa pamoja kisha wakatoka Kinje, dada wa kazi pamoja na Abuu kuelekea Muhimbili. Kwa kuwa Abuu alikuwa na gari hivyo suala la usafiri kwao halikuwa changamoto. Na safari ya kwenda Muhimbili ilianza
Wakati wakiwa safarini kuelekea Muhimbili, Gari ikiwa kwenye mwendo mkali kuna jambo ambalo si la kawaida waliloliona

"Kuna gari nilikuwa nikiitilia shaka tulipotoka nyumbani lakini hivi sasa nimeamini kumbe ni kweli inatufwatilia". Abuu akasema huku akipunguza mwendo wa gari

"Watakuwa ni kinanani hao Kaka?" Kinje akauliza kwa hofu

"Hata sifahamu, ngoja tumpigie Inspekta Jasmine tumwambie labda hawa ni wale waliochukua figo yako. Chukua simu yangu, pasword andika neno "JULIETH" kwa herufi kubwa. Mpigie Nimemsevu Inspekta Jasmine. Ukiona inaita weka Loud Speaker".
Alisema Abuu huku akimpatia Kinje simu yake. Haraka Kinje akafanya kama alivyoambiwa. Akampigia Inspekta Jasmine. Kwa bahati nzuri simu yake iliita.
Akapokea

"Inspekta habari yako, nipo na Kinje kwenye gari ila nyuma yetu kuna gari inatufwatilia. Tangu natoka...."
Hakuweza kumaliza sentesi ile Abuu. Lilitokea gari kubwa aina ya scania semitrela na kuwagonga. Gari ile iliyowagonga iligeuza kwa uharaka na kutokomea. Lilikuwa ni jambo la haraka sana.
Wakiwa katika hali ya taharuki na maumivu ya ajali ile ghafla gari iliyokuwa ikiwafwatilia ikafunga breki karibu yao, mara wakateremka garini vijana wawili waliovalia vitambaa vyeusi vilivyoziba nyuso zao. wakaisogelea gari ya kina Abuu. Kijana mmoja akaichomoa bastola kiunoni na kumpiga risasi binti yule wa kazi aliyekuwa akionekana kuwa na fahamu.
Kijana wa pili kwa haraka akamsogelea Abuu na kumkagua. Alipogundua hana fahamu akazunguka upande wa pili alipo Kinje. Wakati yote yakifanyika Kinje alikuwa akiona kila linaloendelea lakini hakuweza kuzungumza kutokana na hofu aliyokuwa nayo. Alipoona Msichana wa Kazi za ndani katika nyumba ya Kaka yake amepigwa risasi, akajua basi naye hana maisha marefu.
Kijana aliyekuwa akija alipo Kinje alimwita mwenzake kwa ishara. Wote kwa pamoja wakamsogelea Kinje kwa tahadhari baada ya kuufungua mlango wa gari. Hawakumdhuru, walitaka kumchukua waondoke naye.
Wakati wakijiandaa kumbeba kinje ili wampeleke katika gari yao kwa mbali ulisikika mlio wa king'ora cha polisi. Vijana wale walivyosikia mlio ule waliachana na Kinje wakakimbilia ilipo gari yao, haraka wakapanda na kuondoka.

"Abuu! Abuu". Kinje alijaribu kuita lakini Abuu hakuitika wala kuonekana kujigusa. Palepale Kinje naye alipoteza fahamu.

Polisi walifika eneo la tukio ilipotokea ajali baada tu ya kuarifiwa na Inspekta Jasmine. Wakati Inspekta Jasmine akizungumza na Abuu aliposikia kishindo na simu ile kukatika kwa ghafla, kwa haraka aliangalia GPS katika simu yake ni wapi alipo Kinje kwakuwa aliwahi kumwekea Chip ndogo eneo lile alilofanyiwa upasuaji. Chip hiyo alimwekea kwa kushirikiana na Dokta Viran ile siku walipomuokota Kinje maeneo ya Bunju akiwa hana fahamu.
Baada ya kugundua ni wapi alipo akawasiliana na askari wa usalama barabarani. Bila kuchelewa askari wakakamata magari yao na kuwahi eneo lenyewe kutokana na kutokuwa na umbali kutoka alipo Kinje na kilipo kituo kidogo cha Askari wa barabarani. Askari wale waliweza kuondoa mwili wa binti aliyeuwawa kwa risasi huku Abuu na Kinje wakiwahishwa hospitali ya Muhimbili.

Majira ya Mchana Kinje aliweza kurejewa na fahamu. Pembeni yake aliweza kumwona Inspekta Jasmine
"Pole sana kwa yaliyowakuta". Alizungumza Inspekta Jasmine.

"Ahsante Sana Afande. Abuu yupo wapi?". Kinje aliuliza. Kumbukumbu ya tukio la mwisho ilimpa wasiwasi.
Inspekta Jasmine alimtazama huku akimkazia macho. "Abuu yu mzima wa Afya, ni mkono tu umeshtuka kidogo hivyo hajadhurika kivile".
Alisema Inspekta. Hapo kinje akavuta pumzi ndefu na kuitoa taratibu huku akimshukuru Mungu.

"Ile ajali ilikuwa ni ya kutengenezwa. Kulingana na mashuhuda wa tukio lile ni wazi walikusudia kuwasababishia ajali. Sijui ni nani hao na wanataka nini haswa". Alisema Inspekta Jasmine akinyanyuka kutoka alipoketi. Akakikuna kichwa chake kisha akamgeukia Kinje na kumtazama.

"Ni kweli Afande ile ajali ilitengenezwa. Tukiwa kwenye gari Abuu aliniambia kuna gari inatufwatilia, tukashauriana tukupigie lakini ghafla wakati Abuu anazungumza nawe kuna gari ilitokea mbele yetu ikatugonga. Tukiwa ndani ya gari baada ya ajali niliwaona vijana wale waliokuwa wakitufwatilia wakishuka katika gari yao na kuja tulipo. Mmoja alichomoa bastola na kumpiga yule mfanyakazi wetu wa ndani, kisha wakaja kwangu na walitaka kunichukua mimi. Ila kwa bahati nzuri waliposikia ving'ora vya polisi walikimbia". Kinje alieleza.

Wakati Kinje akijaribu kueleza jinsi ilivyokuwa Ghafla kichwa kikaanza kumuuma. kuna kumbukumbu ya siku akiwa ndani ya meli ikamjia kichwani, alilamika kwa sekunde tano kisha maumivu yale yakakata.

"Yes nimewakumbuka. Vijana wale niliwaona nikiwa ndani ya meli siku ile natoka Zanzibar kuja Dar es Salaam. Walikuwa wakinitazama kila mara na nilipokuwa nikiwatazama walikuwa wakiyakwepesha macho yao, hii ilinipa wasiwasi siku hiyo".

"Oooh Ahsante Mungu, endelea kukumbuka zaidi Kinje. Halafu ikawaje?" Alisema Inspekta Jasmine huku akichomoa kitabu kidogo na kalamu. Ni kama alitaka kuandika jambo.
Kinje akajaribu kuvuta kumbukumbu apate kujua nini kilitokea baada ya hapo.
Hakuweza.
Inspekta Jasmine akamtazama Kinje kisha akatabasamu

"Nimegundua Njia ya kufanya ili kumbukumbu zako zirejee haraka sana. Inaonekana kumbukumbu zako hazipo mbali" Alisema Inspekta Jasmine akitabasamu zaidi. Njia iliyomjia akilini ilimfanya afurahi.

"Njia gani hiyo Afande?". Kinje akauliza huku akiweka umakini kuisikia njia hiyo

Hebu tujiulize Leo ni njia gani hiyo itamrejeshea Kinje kumbukumbu? Ahante kwa kutufwatilia. Kwa Maoni na ushauri wasiliana nasi kupitia 0621249611 au 0765824715. Namba zote zipo whatsapp pia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom