Simulizi ya kweli: Mwanamke jini

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,447
c04c013ba0c3472dc009c3d380c756e7.jpg

SEHEMU YA 1
Sitausahau mwaka 1978. Nina sababu tatu za kutousahau mwaka huo. Sababu ya kwanza ni kuwa kulitokea vita vya Kagera. Majeshi ya Iddi Amin aliyekuwa Rais wa Uganda yalivamia nchi yetu na kusababisha maafa makubwa.
Kaka yangu wa kwanza alikuwa ni miongoni mwa askari waliokuwa mstari wa mbele waliokwenda kuikomboa nchi yetu na aliuawa katika vita hivyo.
Sababu ya pili ya kutousahau mwaka huo ni kuwa ndio mwaka nilioanza kufanya kazi. Niliajiriwa na kampuni ya STC iliyokuwa na maduka ya ushirika nchi nzima. Na mwaka huo pia ndio nilitimiza umri wa miaka ishirini.
Lakini sababu ya tatu na iliyokuwa kubwa zaidi ya kutousahau mwaka huo ni kuwa nilikutana na tukio ambalo lilibadili maisha yangu.
Je lilikuwa tukio gani?
SASA ENDELEA
Ilikuwa februari 18 mwaka 1978. Nilikuwa mmoja wa wafanyakazi wa STC tuliokopeshwa pilipiki. Furaha yangu ikanituma kwenda kuangalia sinema. Wakati huo hakukuwa na video wala televisheni. Kulikuwa na majumba ya sinema. Kwa pale Tanga nilikokuwa naishi kulikuwa na majumba matatu ya sinema.
Kulikuwa na Majestic Sinema, Novelty Sinema na Regal Sinema. Majestic Sinema ndiyo iliyokuwa kubwa na maarufu zaidi na ilikuwa katikati ya jiji.
Mimi nilikuwa mpenzi sana wa filamu za kihindi. Filamu za kihindi zilikuwa zikioneshwa siku ya jumapili tu, yaani mara moja kwa wiki na zinakuwa zinajaza watu kuanzia wahindi wenyewe hadi waswahili.
Tikiti huanza kukatwa tangu asubuhi. Ukienda jioni hupati kitu. Nakumbuka filamu iliyokuwa inaoneshwa siku hiyo iliitwa Dost, ilikuwa filamu ambayo nilishapata sifa zake, hivyo kutokana na furaha ya kupata pikipiki nikaona niende nikaione.
Pikipiki tulikabidhiwa siku ya jumamosi, siku ya jumapili ndio niliamua kwenda kuitazama filamu hiyo ya Dost.
Nilikwenda na pikipiki yangu hadi Majestic Cinema. Nikaiegesha katika eneo la kuegesha na kwenda kupanga foleni. Nilikuta foleni ndefu ya watu waliokuwa wanakata tikiti.
Nilifika hapo saa nne asubuhi. Mpaka nafika kwenye kidirisha cha kukata tikiti ilikuwa saa tano kasorobo. Mbele yangu kulikuwa na watu watatu. Wakimalizika wao kukata tikiti ndio inafika zamu yangu. Akaja msichana mmoja ambaye alikuwa amevaa baibui na hijabu akaniomba nimkatie tikiti.
Ilikuwa ni kawaida mtu kukufata ukiwa kwenye foleni na kukuomba umkatie tikiti. Hivyo sikushngaa msichana huyo ambaye sikumfahamu aliponiomba nimkatie tikiti.
Alikuwa anataka kunipa pesa nikakataa kuchukua pesa yake.
“Nitakukatia kwa pesa yangu kisha utanipa” nikamwambia.
“Asante kaka yangu”
Alikuwa na sauti nzuri ya kusisimua.
Wakati amebaki mtu mmoja mbele yangu, kundi la vijana wakihuni likavamia pale kwenye kidirisha na kuharibu foleni, ikawa vurugu. Mmoja wa vijana hao alinibana na kunikatia vifungo vya shati langu. Nikajaribu kutumia nguvu mpaka nikafanikiwa kukifikia kidirisha, nikakata tikiti mbili za usiku.
Nikazitia mfukoni tikiti hizo kisha nikaanza kumtafuta yule kijana aliyeniumiza. Nikamuona akiuza tikiti yake kwa bei ya juu kwa mhindi mmoja. Nikamkwida ukosi na kumtikisa.
“Wewe mshenzi umenifanya nini pale?” nikamuuliza.
“Hebu niache fala wewe…” akaniambia huku akiukutua mkono wangu.
Nikamtandika ngumi moja tu iliyomtupa chini. Damu ikawa inamtoka mdomoni.
Yule msichana aliyeniomba nimkatie tikiti akanifuata haraka.
“Usipigane” akaniambia huku akinishika bega.
“Angalia jinsi alivyokata vifungo vyangu”
Nikamuonesha yule msichana papi za shati langu ambalo lilichomoka vifungo vitatu.
“Basi muache”
Yule kijana alinyanyuka na kukimbia.
Nilitoa zile tikiti mbili, nikampa tikiti moja yule msichana.
“Asante kaka yangu, ngoja nikupe pesa zako” akaniambia.
Nikaona nimuachie tu.
“Basi usinipe pesa, nimekukatia kwa pesa zangu”
“Kwnini unakataa pesa?” akaniuliza.
“Nimekukatia mimi kama zawadi yako”
“Asante kaka yangu”
“Haya, kwaheri” nikamuaga.
“Basi tutaonana jioni” akakiambia kichogo changu. Nilikuwa nimeelekea kwenye mlango nikitoka.
Nikiwa nje ya jumba hilo nilichukua pikipiki yangu nikaondoka kurudi nyumbani.
Nilikuwa ninaishi eneo la Mabawa kwenye nyumba ya kupanga. Nyumba yenyewe ilikuwa na sehmu mbili. Sehemu moja nilipangisha mimi na sehemu nyingine alipangisha kujana mmoja wa kichaga aliyekuwa akifanya biashara ya duka la nguo barabara ya kumi na tatu.
Nilipofika nyumbani niliingiza ndani pikipiki yangu nikakaa sebuleni kwangu na kutafakari.
Nilikuwa sijaoa, sikuwa na mke wala mtoto. Ndiyo nilikuwa naanza maisha. Wakati huo mzazi wangu aliyebaki alikuwa mmoja, ni mama yangu. Baba yangu alikuwa ameshafariki dunia miaka miwili iliyopita.
Mama yangu alikuwa akiishi barabara ya tisa kwenye nyumba yetu tuliyozaliwa. Kaka yangu wa pili alikuwa akiishi eneo la Chuda na kaka yangu mwingine aliyefuata alikuwa akiishi eneo la Kwaminchi.
Usiku ulipowadia nilitoa pikipiki yangu nikaenda kwenye mkahawa mmoja kula chakula kisha nikaongoza njia kuelekea Majestic.
Nilifika Majestic saa mbili na nusu. Sinema ilikuwa inaanza saa tatu hadi saa sita usiku. Baada ya kuegesha pikipiki yangu niliingia kwenye ukumbi huo nikatafuta siti yenye namba yangu nikakaa. Mpaka imebaki dakika moja kuanza trela, siti ya upande wangu wa kulia ilikuwa tupu. Nilishuku ilikuwa siti ya yule msichana niliyemkatia tikiti kwani siti hizo zilikuwa zikifuatana na namba zilizomo kwenye tikiti.
Ghafla taa zikazimwa na trela ikaanza. Hapo ndipo nilipomuona msichana akiingia na kuja kukaa kwenye kile kiti kilichokuwa kitupu. Alikuwa ni yule msichana niliyemkatia tikiti. Sikujua alijuaje kuwa kiti chake kilikuwa pale. Nikawaza kwamba pengine aliwahi kuingia mapema akakiona kiti chake kisha akatoka.
“Tumekutana tena” akaniambia huku akitabasamu.
“Nilikuwa najiuliza huyu msichana yuko wapi”
“Nilichelewa kidogo, unajua ninaishi mbali”
Sikumuuliza anaishi wapi, akili yangu ilikuwa kwenye ile trela iliyokuwa ikioneshwa.
Sote tukawa kimya. Tuliangalia trela hadi ikaisha. Msichana alitoka, mimi sikutoka. Baada ya muda kidogo alirudi akaketi kwenye kiti chake. Mkononi alikuwa ameshika chupa mbili za soda na pakiti mbili za karanga.
“Chukua soda” akaniambia huku akinipa ile chupa moja.
Nikaipokea.
“Chukua na karanga”
Akanipa na pakiti moja ya karanga.
“Asante’
Hapo hapo taa zikazimwa na filamu ya Dosti ikaanza. Ile filamu ilikuwa ikizungumzia marafiki wawili, mmoja kipofu na mwingine mlemavu wa miguu. Ilikuwa filamu nzuri na ya kusikitisha sana. Ilikuwa na nyimbo nne. Nyimbo tatu ziliimbwa na muimbaji maarufu wa India Mohamed Rafiy ambaye kwa sasa ni marehemu na moja iliimbwa na Usha Mangesh ambaye ni dada wa Lata Mangesh.
Sinema ilipomalizika tuliinuka kwenye viti na kutoka. Kwa vile kulikuwa na watu wengi, nilipotoka sikumuona tena yule msichana, nikaenda kuchukua pikipiki yangu nikaiwasha na kuondoka.
Kutoka Majestic Cinema nilishika barabara ya Eckenford hadi bustani ya Uhuru ambapo nilikata kushoto na kushika barabara ya Pangani. Wakati nalivuka eneo la Tangamano niliona mtu akinipungia mkono mbele yangu. Alikuwa mwanamke na nilihisi likuwa anataka kuniomba lifti.
Kusema kweli muda ule wa usiku nilikuwa sipakii mtu nisiyemfahamu hata kama ni mwanamke. Kwa hiyo nilitaka kumpita lakini pikipiki ikazimika moto ghalfa. Mwanamke huyo akaona nilisimama kwa ajili yake, akanifuata.
Alipofika karibu yangu nikaona alikuwa ni yule msichana niliyekuwa naye sinema. Nikajiuliza alifikaje pale wakati nilimuacha kule Majestic?
MAMBO YAMEANZA. JE NINI KITATOKEA? USIKOSE KUENDELEA NA MKASA HUU WA KUSISIMUA MWANZO HADI MWISHO.
 
yaani hadithi za humu huwa zinaanza kwa mbwembwe tena bila mashsrti kabisa subiri ifike sehem ya 7 na kuendelea mashart yanaanza Mara ohhh ntakuwa naileta baada ya siku3, Mara ohhh natakuwa naruka baadhi ya sehem ili mtafute kitabu. Mara ohhh hsitafika mwisho kwa huku ila kule kwenye group LA WhatsApp Itafika mwisho tafadhali lipia Elf5 na blaa blaa nyingi, kwa nini hayo yote msiwe mnayasema mwanzo wa simulizi??? Mnakera somtym, Shukrani kwa Steve huwa story Inafika mwisho na kama kuna masharti na namna ya kuileta story huwa anasema kabisa toka mwanzo, nimemmis sana LEGE story zake nyingi zilikuwa zinafika mwisho
 
yaani hadithi za humu huwa zinaanza kwa mbwembwe tena bila mashsrti kabisa subiri ifike sehem ya 7 na kuendelea mashart yanaanza Mara ohhh ntakuwa naileta baada ya siku3, Mara ohhh natakuwa naruka baadhi ya sehem ili mtafute kitabu. Mara ohhh hsitafika mwisho kwa huku ila kule kwenye group LA WhatsApp Itafika mwisho tafadhali lipia Elf5 na blaa blaa nyingi, kwa nini hayo yote msiwe mnayasema mwanzo wa simulizi??? Mnakera somtym, Shukrani kwa Steve huwa story Inafika mwisho na kama kuna masharti na namna ya kuileta story huwa anasema kabisa toka mwanzo, nimemmis sana LEGE story zake nyingi zilikuwa zinafika mwisho
mm uwa nasoma nikiwa sha jiandaa kabisa kwamba aita fika mwisho....afu ye mwenyew unakuta ka copy tu sehem
 
SEHEMU YA 02


ILIPOISHIA
Hapo hapo taa zikazimwa na filamu ya Dosti ikaanza. Ile filamu ilikuwa ikizungumzia marafiki wawili, mmoja kipofu na mwingine mlemavu wa miguu. Ilikuwa filamu nzuri na ya kusikitisha sana. Ilikuwa na nyimbo nne. Nyimbo tatu ziliimbwa na muimbaji maarufu wa India Mohamed Rafiy ambaye kwa sasa ni marehemu na moja iliimbwa na Usha Mangesh ambaye ni dada wa Lata Mangesh.
Sinema ilipomalizika tuliinuka kwenye viti na kutoka. Kwa vile kulikuwa na watu wengi, nilipotoka sikumuona tena yule msichana, nikaenda kuchukua pikipiki yangu nikaiwasha na kuondoka.
Kutoka Majestic Cinema nilishika barabara ya Eckenford hadi bustani ya Uhuru ambapo nilikata kushoto na kushika barabara ya Pangani. Wakati nalivuka eneo la Tangamano niliona mtu akinipungia mkono mbele yangu. Alikuwa mwanamke na nilihisi alikuwa anataka kuniomba lifti.
Kusema kweli muda ule wa usiku nilikuwa sipakii mtu nisiyemfahamu hata kama ni mwanamke. Kwa hiyo nilitaka kumpita lakini pikipiki ikazimika moto ghalfa. Mwanamke huyo akaona nilisimama kwa ajili yake, akanifuata.
Alipofika karibu yangu nikaona alikuwa ni yule msichana niliyekuwa naye sinema. Nikajiuliza alifikaje pale wakati nilimuacha kule Majestic?
SASA ENDELEA
Nilipomuona nikatabasamu.
“Ni wewe kumbe?” nikamuuliza.
“Ni mimi, naomba unisaidie lifti”
“Unaishi wapi?” nikamuuliza.
Kabla hajanijibu alikuwa ameshakaa nyuma yangu.
“Unaishi wapi?” nikamuuliza tena.
“Mikanjuni” akanijibu.
Nikaguna lakini bila kutoa sauti. Eneo alilolitaja, wakati huo lilikuwa kama pori la miti ya mikanju. Viwanja vilikuwa vikipimwa sasa na kama kulikuwa na nyumba zilikuwa chache na za kienyeji. Kwenda huko usiku ule ilikuwa ni hatari.
Lakini msichana alikuwa ameshakaa nyuma yangu akijisogeza upande wangu ili akae vizuri.
Nikajikuta nikipiga kiki ya pikipiki ili kuiwasha kwani pikipiki ilikuwa imezima moto. Pikipiki ikawaka, nikatia gea ya kwanza ya kuondokea na kuondoka.
Msichana aliupitisha mkono wake kwenye tumbo langu ili kujizua. Mkono huo uliniletea changamoto na hisia toauti kwenye akili yangu.
“Kama unakaa Mikanjuni kwanini unakwenda sinema za usiku?” nikamuuliza.
“Nimeshazoea” akanijibu. Kidogo aliliminya tumbo langu, pengine ni kwa bahati mbaya, nikashituka.
“Mbona unashituka?” akaniuliza.
“Nilikuwa najiweka sawa”
“Mh!” Msichana akaguna. Sikujua ni kwanini aliguna.
“Ulitegemea ungerudi nyumbani kwa usafiri gani usiku huu?” nikamuuliza.
“Ninaomba lifti tu kwa watu”
“Ukikosa lifti unakwenda kwa miguu?”
“Naweza kukodi teksi lakini sijawahi kukosa lifti hata siku moja”
Baada ya hapo tukabaki kimya.
Nilikwenda hadi Duga kisha nikakata kushoto na kushika barabara ya kuelekea Mikanjuni. Hapo ndipo nilipoanza kupita kwenye eneo la vichaka na miti ya mikanju.
Tulipoingia katika eneo la Mikanjuni nikamuuliza.
“Unaishi sehemu gani?”
“Twende tu, nitakuonesha” akaniambia.
“Una maana hatujafika bado?”
“Bado”
Nikaendelea kwenda mbele. Laiti angekuwa mwanaume mwenzangu, ningemshusha hapo hapo nikarudi kwa hofu ya kutaka kunipora pikipiki.
Sasa tulikuwa tunaingia kwenye pori kamili. Kulikuwa na nyumba moja moja tena zikiwa mbali mbali na hazina taa za umeme . Sehemu nyingi vilikuwa ni viwanja vitupu.
“Simama hapa hapa” Msichana akaniambia tulipokuwa tunaupita mti wa muwembe.
Nikasimamisha pikipki. Msichana akashuka.
“Asante sana kaka” akaniambia.
“Unaishi wapi?” nikamuuliza kwa sababu sikuona nyumba karibu.
“Naishi mtaa wa pili” akaniambia. Mtaa huo pia sikuuona lakini nilimkubalia ili niwahi kurudi.
“Uende salama, mimi nakwenda zangu” nikamwambia huku nikiigeuza pikipiki.
Nikamuona msichana akichapuka kuelekea mtaa huo aliosema. Nikatia gea kwa nguvu na kuingia gea ya pili na kuondoka.
Wakati narudi nilimsikitikia sana msichana yule, alikuwa anaishi pembeni sana na katika mazingira ambayo hayakulingana naye.
Nilipotokea kwenye barabara ya Duga nilikata kulia nikarudi nyumbani kwangu.
Nilifungua mlango nikaingiza pikipiki yangu ukumbini kisha nikaingia chumbani kwangu. Nilivua nguo nikajifunga taulo na kwenda bafuni.
Nilijimwagia maji ya baridi ili kuuosha mwili wangu ulikuwa umetota kwa jasho. Nilipotosheka nilirudi chumbani kwangu na kujiandaa kulala.
Asubuhi kulipokucha nilitoka kwenda kazini kwangu. Baada ya kama wiki moja hivi nilikutana tena na yule msichana. Nilikuwa nimekwenda katika duka moja la vitabu kununua kitabu cha “Mashimo saba ya Mfalme Suleyman”
Mara nyingi niwapo nyumbani hupenda kujisomea vitabu vya hadithi. Katika orodha yangu ya vitabu kitabu hicho hakikuwemo hivyo nikataka nikinunue ili niwe nacho.
Kabla sijaingia kwenye duka hilo nilikiona kitabu hicho kwenye safu ya vitabu vilivyokuwa kwenye kioo. Nilipoingia humo dukani nilimwambia muuzaji kuwa nataka kitabu cha Mashimo Saba ya Malme Suleiman.
“Vimekwisha” akaniambia.
“Kipo kimoja, nimekiona kwenye kioo” nikamwambia.
“Umekiona?” akaniuliza.
“Ndiyo nimekiona”
“Njoja nitazame”
Muuzaji huyo alizunguka nyuma ya kioo akakiona kitabu hicho.
“Ni kweli kipo, kilibaki kimoja tu” akaniambia huku akikifuta vumbi na kunipa.
“Bei gani?”
Akanitajia bei yake nikatoa pesa na kumlipa.
Wakati ninatoka nje ya duka nikakutana na msichana aliyekuwa akiingia dukani humo. Akanishitua aliponiambia.
“Kaka habari ya tangu siku ile?”
Nikaangaza macho yangu kumtazama. Nikamkumbuka. Alikuwa ni yule msichana niliyekutana naye sinema siku ile.
“Oh nzuri! Hujambo?” nilijibu salamu yake.
“Sijambo. Leo tumekutana tena”
“Imekuwa kama bahati. Nilikuwa natoka kununua kitabu”
“Mimi pia nimekuja kununua kitabu. Nilikuwa nahitaji kitabu cha “Mashimo Saba ya Malme Suleiman”
“Vimeisha. Kilikuwa kimebaki kimoja tu nilichonunua mimi” nikamwambia.
“Kumbe wewe pia ulikuja kununua kitabu hicho hicho?”
“Nilikuja kununua kitabu hicho”
Nikakitoa kile kitabu na kumuonesha.
Akakishika na kukitazama.
“Una umuhimu nacho sana kwa leo na kesho?” akaniuliza.
“Ni kwa ajili ya kujisomea tu”
“Basi naomba uniazime kwa siku mbili tu halafu nitakurudishia”
Sikuwa na sababu yoyote ya kukataa. Nilihisi yule msichana alikuwa akikihitaji zaidi.
“Nitakuazima, sasa sijui nitakipata vipi?”
NAAM. MAMBO YANAZIDI KUKOLEA UTAMU. JE NINI KITATOKEA?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom