Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 31
Wakati mshindo huo ukipoa ulimkuta Makonko akiwa mbali mitaani, akienda zake; mikononi akiwa na rasilimali zake zote muhimu.
Alikuwa akiumaliza mtaa wake, aingie mtaa wa pili alipogeuka nyuma baada ya kusikia akiitwa. Alilazimika kuirudisha mafichoni bastola yake ambayo alianza kuitayarisha, alipoona akifuatwa na mwanamke. La, msichana. Alikuwa mdogomdogo, mwenye sura nzuri ingawa ilifunikwa na kitu kama huzuni au msiba. Kilichomvutia Makonko si usichana wake tu bali kanga moja tu ambayo aliivaa binti huyo kiasi cha kulifanya umbo lake la ndani kuonekana kama lilivyo; lililojaa na kubonyea panapostahili kwa namna iwezavyo kumletea njaa ya mapenzi mwanaume yeyote. Makonko, akiwa mmoja wao, alijikuta kasahau kuwa ilimpasa kutoweka eneo hilo haraka. Badala yake alisogelea na kuuliza polepole, “Unasemaje shangazi?”
“Samahani kaka,” binti huyo alimjibu hali kamkazia macho. “Nauomba msaada wako. Unisaidie nifike nyumbani tu, tafadhali. Naogopa kuvamiwa na wahuni.”
“Kwani wewe ni nani sista? Na unatoka wapi na kwenda wapi saa hizi?
“Ya Mungu, mengi kaka yangu. Yaliyonikuta hayasemeki.” Sauti yake ilikuwa na huzuni kama uso wake. “Mambo yenu nyie wanaume ya hatari sana. Kanifuata mwenyewe nyumbani, kanibembeleza kwa fedha na hongo hadi nikakubali kwenda naye kwake. Kumbe ana mke. Sijui alikuwa kamficha wapi mke wake. Mara nikaona mke wake akitokea uvunguni. Wakaanza kunipiga. Nimeponea chupuchupu baada ya kukimbia. Tazama nilivyo. “Sina hata nguo, masikini.”
Makonko, ambaye huruma iko mbali na roho yake, alihisi kitu fulani rohoni. “Unaishi wapi? Nitakupeleka.”
“Ahsante sana kaka. Sijui nikushukuru vipi.”
“Usijali. Unaishi wapi?”
“Twende tu. Nitakuonyesha.”
Wakati mshindo huo ukipoa ulimkuta Makonko akiwa mbali mitaani, akienda zake; mikononi akiwa na rasilimali zake zote muhimu.
Alikuwa akiumaliza mtaa wake, aingie mtaa wa pili alipogeuka nyuma baada ya kusikia akiitwa. Alilazimika kuirudisha mafichoni bastola yake ambayo alianza kuitayarisha, alipoona akifuatwa na mwanamke. La, msichana. Alikuwa mdogomdogo, mwenye sura nzuri ingawa ilifunikwa na kitu kama huzuni au msiba. Kilichomvutia Makonko si usichana wake tu bali kanga moja tu ambayo aliivaa binti huyo kiasi cha kulifanya umbo lake la ndani kuonekana kama lilivyo; lililojaa na kubonyea panapostahili kwa namna iwezavyo kumletea njaa ya mapenzi mwanaume yeyote. Makonko, akiwa mmoja wao, alijikuta kasahau kuwa ilimpasa kutoweka eneo hilo haraka. Badala yake alisogelea na kuuliza polepole, “Unasemaje shangazi?”
“Samahani kaka,” binti huyo alimjibu hali kamkazia macho. “Nauomba msaada wako. Unisaidie nifike nyumbani tu, tafadhali. Naogopa kuvamiwa na wahuni.”
“Kwani wewe ni nani sista? Na unatoka wapi na kwenda wapi saa hizi?
“Ya Mungu, mengi kaka yangu. Yaliyonikuta hayasemeki.” Sauti yake ilikuwa na huzuni kama uso wake. “Mambo yenu nyie wanaume ya hatari sana. Kanifuata mwenyewe nyumbani, kanibembeleza kwa fedha na hongo hadi nikakubali kwenda naye kwake. Kumbe ana mke. Sijui alikuwa kamficha wapi mke wake. Mara nikaona mke wake akitokea uvunguni. Wakaanza kunipiga. Nimeponea chupuchupu baada ya kukimbia. Tazama nilivyo. “Sina hata nguo, masikini.”
Makonko, ambaye huruma iko mbali na roho yake, alihisi kitu fulani rohoni. “Unaishi wapi? Nitakupeleka.”
“Ahsante sana kaka. Sijui nikushukuru vipi.”
“Usijali. Unaishi wapi?”
“Twende tu. Nitakuonyesha.”