Simulizi: Wimbo wa ajabu

Simulizi: Wimbo wa ajabu

bioto

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2017
Posts
1,261
Reaction score
2,099
..WIMBO WA AJABU ..
SEHEMU YA KWANZA.
¶¶¶Wanakandia,Wanapondea wanadhani
watafanikiwa¶¶¶. ¶¶¶Nimeshajua,Janet wangu,Ni
bora tufunge ndoa¶¶¶. ¶¶¶Sema basi laazizii,Sema
mpenzi, Nikilala usingizi,Nakuota kipenzi¶¶¶.
¶¶¶Lazizii,Sema basi kipenzi, nikilala isingizi
Nakuota mpenzi¶¶¶.
Chorus. ¶¶¶Janet nampenda,Janet wangu sana, Kuna
watu wanabana, Ni siishi na huyu kimwana,Na bado
nawaambia,Milele hatutaachana, Hatuta tengana iwe
kufa na kuzikana¶¶ Usingizi uliniishia huku nikiwa
nimeiota tena nyimbo hii ya ajabu ambayo
sikuitunga bali kila nikilala inanijia na kuiota
namuimbia mrembo nisiyemjua ndotoni.
Mara nyingi nilikuwa namkimbiza huyo mrembo
ndotoni huku nikimuimbia huyu mrembo hiyo
nyimbo ambaye nilikuwa simtambui ninani na
anatokea wapi. Basi niliamka na nikaipuuza hii
ndoto tena licha ya kujirudia zaidi ya mara tatu.
Nikachukua mswaki wangu na kupiga fasta kisha
kujiandaa kwenda shule.
Kilikuwa ni kipindi karibia na mitihani ya kidato cha
sita huku nami nikiwa ni miongoni wa watahiniwa
wa hiyo mitihani Ila ghafla nimejikuta naiogopa sana
mitihani hii inayokuja ya kidato cha sita kutokana na
majibu ya kukatisha tamaa ya mock. Nisiwafiche
wadau mock nilipata zero hili jambo linanitisha sana
kwasababu kidato cha sita PCM sio sawa na kidato
cha nne kwani mpaka nimefika hapa wadau kidato
cha nne nilipata one ya point Saba lakini hapa
mambo yananiendea vibaya.
Basi siku hiyo ilibidi niwahi shule ili nikajisomee
zaidi na zaidi walau kujinusuru na hili janga. Nilifika
shuleni nikakutana na rafiki yangu anaitwa Salehe
nilitamani tukajadili naye kidogo maana jamaa
mock alipiga two. "Salehe vipi mshkaji"
Nilimsalimia Saleh ambaye alionekana kashika
daftari na peni anaelekea maktaba kujisomea. "Poa
,Vip Musa".
"Safi ,unaelekea wapi". "Library (Maktaba)". "Jana si
uliahidi tutadiscus(Tutajadili) physics Leo".
"Tutadiscus au mnataka niwafundishe mbona mi
sioni mtu wa kudiscus naye kwenye group letu wote
ni maziro tu nyi mnataka niwavute mpaka kwenye
four mpate vyeti alafu mi nipolomoke mpaka
kwenye three nikose mkopo". Saleh aliongea kwa
dharau sana.
"Mmh,Saleh mambo gani hayo , ukidiscuss ndo
unagain zaidi". "Ukidiscuss na watu wenye akili sio
na vilaza kama nyie mtanipumzikia tu" Basi Saleh
alisema maneno hayo kisha kuondoka na kuniacha
nimeduwaa tu. Basi hakuna noma kwakuwa group
letu tuko sita na Salehe peke yake ndo hayupo basi
acha niende kudiscus na washkaji wengine. Basi
nikapandisha mpaka kwenye darasa tuliopanga
kukutana. "Afadhari Musa umefika" John mmoja wa
washkaji zangu alinipokea na kuniingiza moja Kwa
moja kwenye ubishi waliokuwa wakibishana na
mwenzake Nashon. "Eti ,Messi na Ronaldo nani
mkali".
John alinipa mada ya ubishi moja kwa moja mara tu
baada ya kufika . "Mi naona Messi ni mkali".
Nilijibu. "Mkali wapi mtu mwenyewe ahami timu sio
kama fighter Ronaldo". "Kuhama timu sio hoja
Messi kwenye magoli anashindana na
Ronaldo,Suarez na Rwewandoski, Assist
anashindana na Ozil na Di Maria, Dribble
anashindana na Neymar na hazard kwahiyo Messi
anavitu vingi tofauti na Ronaldo".
"Vitu vingi wapi niambie Mesi anataji gani timu ya
Taifa" Alisema Nashon nami nikaona ubishi utakuwa
hauishi hapa ikabidi nivunje mada. "Hoya washkaji
tuacheni maswala ya Ronaldo na Messi vipi kuhusu
discussion Leo". "Tutadiscus nini wakati Saleh
hayupo" Aliongea Nashon "Sasa kama hayupo si
tunadiscus wenyewe"Nilijaribu kuwashauri washkaji
lakini washkaji hawakunielewa wakaendelea
kusisitiza discussion haiwezi kuwepo kwasababu
Saleh hayupo na tuliopo hapo wote ni vilaza hivyo
hatuna cha kudiscuss sanasana tutapotezeana muda
kama vipi kila mtu ajisomee peke yake .
Hii rai ya kila mtu ajisomee peke yake ndo ilipita
hivyo kila mtu akawa anajisomea peke yake lakini
bado Nashon na John waliendelea kubishana
kuhusu Ronaldo na Messi mimi nikaona hilo eneo
sio sahihi Kwa kujisomea Basi ikabidi nitoke
darasani na kwenda kutafuta mahali patulivu zaidi
kwaajili ya kujisomea, Sikutamani kwenda library
(Maktaba) maana kule kuna washkaji wengine
wakikuona wanaanza kuongea maneno ya ajabu
"Eehee mpaka Musa Library Leo kulikoni au ziro
imemnyoosha?".
Basi ikabidi nielekee sehemu ya uwanja wa shule
ambapo kulikuwa na mbuyu mkubwa pia kulikuwa
na utulivu wa kutosha kwani shule nzima tuko sisi
kidato cha sita,Kidato cha tano wamefunga
kutupisha sisi kwaajili ya mitihani kwani ni wiki
moja tu mitihani inaanza na shule yetu haina oleval
(1-4) . Hivyo eneo la uwanjani lilikuwa tulivu zaidi
kwasababu hakuna hata mwanafunzi mmoja
maeneo hayo. Basi mi nikasogelea eneo la mbuyu
pale uwanjani ili kupata kivuli jua lisinipige wakati
najisomea.
Nilifika eneo lile na nikaanza kujisomea mara ghafla
nikaanza kusikia ule wimbo ukiimbwa tena. ¶¶¶
Sauti nzuri,Kama ya gita, hiyo inakuita, Taratibu uje
kwangu,Uje bila kusita¶¶¶. ¶¶¶Sema basi lazizi,Sema
basi kipenzi, Nikilala usigizi nakuota kipenzi ,lazizi
sema basi kipenzi,Nikilala usingizi nakuota
kipenzi¶¶¶. Nilishtuka Kwasababu wimbo huo huwa
nausikia ndotoni iweje uimbwe live ,Nani anauimba
huu wimbo live wakati sio wa msanii yeyote
ninayemjua mimi. Nilishtuka sana nakuanza
kuogopa ikabidi ninyanyuke kuelekea eneo
linaloimbwa hiyo nyimbo. ***...
 
(2-----5)
#02
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA PILI. Niliogopa
sana kusikia wimbo huo ukiimbwa maeneo
hayo.Hasa ukizingatia kuwa shule yetu ipo maeneo
ya polini yahaani imezungukwa na poli ikiwa na uzio
wa senyenge tu. Pamoja na woga niliokuwa nao ila
sikusita kuendelea kuifata ile sauti inapotokea ilibidi
nipite kwenye tobo moja la senyenge ili kuelekea
kule polini ambapo nasikia sauti nzuri ya msichana
ikiimba ule wimbo. Ni kweli nikafanikiwa kumuona
msichana mweupe mithili ya muarabu akiwa kavaa
Shela huku kanipa kichogo kama vile
ninavyomuonaga kwenye ndoto. Basi nikaanza
kumfata pale alipo huku nikitetemeka nikiwa nahofia
huwenda atakuwa si binadamu wa kawaida. "Za saa
hizi dada" Nilimpa salamu mara tu nilipomfikia.
"Nzuri"Dada aliitikia kwa tabasamu pana na kugeuka
kunitazama alikuwa ni mdada mzuri mithili ya
muarabu pia alikuwa na umri kama wangu yahaani
tunaendana. Nikajikuta namshangaa kwa dakika
kadhaa huku nikisahau kabisa kilichonileta hapo
mpaka akanishtua. "Sema Musa" "Eehee!" Nilishtuka
na kumuuliza. "Umejuaje jina langu?". "Mmh mi
nisikujue wewe tena wakati wewe ni maarufu Tabora
nzima". "Mmh maarufu,Kivipi". "We si ulikuwa
mfungaji bora kwenye umishumita uliopita".
"Eehee,Kweli" Nilijikuta naitikia maana mashindano
ya umitashumita yaliisha hivi karibuni nami ndo
nikawa mfungaji bora.Ila nikajiuliza huyu amejuaje
kama mimi nilikuwa mfungaji bora kwasababu
anavyooneka hafananii na mwanafunzi kwani
amevaa shela kama la harusi kitu ambacho si rahisi
kwa mwanafunzi kuvaa shela nikataka nimuulizi
kama na yeye ni mwanafunzi lakini ghafla akanijibu
pasina mimi kumuuliza. "Ndio ,Mimi ni mwanafunzi
usinione nimevaa shela la harusi ukajua labda mimi
si mwanafunzi ni mwanafunzi mie". Jibu lake
lilinitisha ila sikutaka kuonyesha hali ya kuogopa
"Mmh asije akawa jini huyu?" Niliwaza kimoyomoyo.
"Mi sio jini bwana,Mimi nimwanafunzi kama wewe".
Basi nilizidi kuogopa ila nikajikaza. "Unasoma shule
gani?". "Nasoma vilambo girl". Mimi nasoma
Vilambo boys shule zetu zipo karibu karibu tu
zimetenganishwa na msitu mdogo tu "Combi gani?".
"Nasoma ,PCM kama wewe". "Eehee "Nilishtuka.
"Umejuaje wewe ?". "Si nimekuona umeshika kitabu
cha Physics na Mathematics ". Duh ni kweli kabisa
nilikuwa nimeshika kitabu cha Physics na
Mathematics inamaana aliniona wakati nakuja
kujisomea ,sasa mbona nilimkuta mbali huyu.
"Nilikuwa karibu nilipokuona unakuja ndipo
nikasogea mbali kidogo" Alijibu swali langu la
kichwani bila mimi kumuuliza. "Naitwa Janet nipo
Form six PCM Vilambo girl ,nimefurahi kuonana na
wewe bwana Musa nadhani tutasaidiana sana
kwenye kipindi hiki cha mwisho". Jina lake
liliniduwaza nakuniacha midomo wazi maana hilo
jina lipo kwenye ule wimbo nami kila siku nauota
namuimbia mrembo aliyevaa shela huku
akikimbia,Wakati nawaza hayo basi naye alikimbia
eneo la tukio huku akiimba ule wimbo nakuniacha
namshangaa tu. ¶¶¶Sauti nzuri,kama ya gita, Hiyo
inakuita, Taratibu uje kwangu, uje bila kusita, Yale
mapenzi yautata,. Sipendi kuyapata,. Kimapenzi
nimedata
Siwezi kutafuta¶¶¶. ¶¶¶Sema basi lazizi,Sema basi
mpenzi nikilala usingizi, nakuota mpenzi,Lazizi sema
basi kipenzi nikilala usingizi nakuota mpenzi¶¶¶
Basi niliendelea kuganda huku nikimtazama jinsi
anavyokimbia mithili ya Ile ndoto,Na wimbo
anaoimba upo kwenye Ile ndoto na mbaya zaidi
hata jina lake pia lipo kwenye Ile ndoto. Shela
alilovaa lipo ndotoni. Basi nikawa nimeshindwa hata
kumuuliza huu wimbo yeye ameujuaje maana hilo
ndo lilikuwa lengo langu la kufika hapo,Nilishindwa
kumuuliza pia hiyo kusaidiana tutasaidianaje maana
mtihani unaanza wiki ijayo jumatatu na Leo
jumatatu,Pia nilishindwa kumuuliza tutaonanaje tena
maana shuleni huruhusiwi kumiliki simu.Pia Swali
lingine la msingi nilishindwa kumuuliza anafanya
nini peke yake polini haogopi kwani peke yake
***
#03
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA TATU Toka
nimemuona yule mrembo nilijikuta nimempenda
sana ingawa nilikuwa na maswali mengi kichwani
kwamba huyo ni jini au laa lakini nilijikuta
nayapuuza hayo maswali huku nikitamani kuonana
naye tena. Hivyo siku nilijikuta naenda uwanjani
kujisomea walau atokea tena nimuone lakini wapi.
Hisia za mapenzi zilinitesa sana kwenye hiyo wiki ya
mwisho karibia na mtihani na mara nyingi
nikijisomea pale chini ya mbuyu ambacho ndicho
kijiwe changu kipya cha kujisomea nilikuwa
namuwaza yule mrembo. Nilikuwa nawaza macho
mazuri makubwa yaliyolegea mithili yanataka
kudondoka ya yule mrembo.Shepu yake bomba na
uzuri wake kama muarabu ulinitatiza. Pamoja
nilikuwa najisomea chini ya ule mbuyu ili nimuone
akija Ila nikiwaza sifa zake tu basi nilikuwa nafunga
vitabu vyangu mara moja na kuzama msituni
kumtafuta huyu mrembo. Lakini wapi nimuonee
wapi huyu mrembo ,hivyo nikajikuta nasogea mpaka
eneo la shule ya Vilambo girl. Nakumbuka siku ya
jumamosi penzi lilinizidia moyoni nikafanya ujinga
nikaenda hadi Vilambo girl na kupita kwenye
senyenge zao nikakutana na baadhi ya mabinti wa
form six "Eehee ,We Kaka unafanyanini hapa"
Wadada walinishangaa mara tu baada ya kupenya
kwenye senyenge zao maana hilo ni kosa kisheria
unaweza ukafukuzwa hadi shule. "Samahanini,Jam
ani namuulizia dada mmoja anasoma form six PCM
anaitwa Janet". "Mmh,Janet huyo hatumjui". Basi
nikahisi kama vile alinidanganya jina ikabidi
niwaelezee kidogo jinsi alivyo. "Ni mweupe kama
muarabu na ana macho makubwa hivi".
"Mmh,Kusema kweli kakaangu sisi ndo PCM tupo
40 tu shule nzima huyo dada wa aina hiyo sisi
hatumfahamu alafu tunaomba uondoke maana isije
ikawa kesi hapa". Maneno yale ya wale mabinti
yalininyong'onyeza nikajikuta narudi shuleni kwetu
kwa majonzi sana. Nilijilaumu sana na kumlaumu
Janet kwani alisema yeye ni PCM kama mimi hivyo
tutasaidiana kwenye mitihani na Leo ni Jumamosi
kesho Jumapili, Jumatatu mitihani inaanza. Pamoja
na kujilaumu na kumtupia lawama Janet ,Lawama
zangu zikawa hazina maana kwasababu Jumatatu ni
mtihani nami maandalizi kwaajili ya mtihani
sikufanya vya kutosha. Nikajikuta nikama mtu
niliyekata tamaa siku hiyo yahaani penzi nimekosa
na mitihani inayokuja hivi karibuni naenda kufeli.
Basi nilikosa mzuka kabisa wakujisomea siku hiyo
nikaenda zangu kujilaza kitandani huku nikiwaacha
wenzangu wakikesha siku hiyo maana Jumatatu
mtihani wa kwanza ni Physics hivyo wengi
walikomaa kujisomea huku wakishukuru Mungu
afadhari imeanza Physics maana ndo ngumu watu
wapate muda mrefu wa kujiandaa mimi wakati huo
nipo zangu kitandani nauchapa usingizi sijali
chochote kije tu. Nililala mpaka asubuhi washkaji
wakanishangaa. Ilipofika asubuhi ya Jumapili
kulipambazuka na tetesi mpya kulipambazuka na
tetesi za kuvuja Kwa mtihani wa taifa wengi
walishangilia mimi nikiwa bado kitandani nikiwa
sijui linaloendelea. Mara mida ya saa nne alikuja
Nashon bwenini kwetu na makelele kibao. "Woyo,
We Musa vipi unalalala mambo yamevuja huko".
"Nini ?". "Pepa ya physic imevuja huko hapa
tunaelekea darasa la form five hkl kusolve pepa,
Kuna Saleh,Gerald na Jabir vichwa vyote
vimejikusana sisi vilaza twende tukachukue hata
majibu tupasue". Nashon alitoka fasta mara baada
ya kunishtua akiwa na daftari lake na peni kwaajili
ya kuchukua majibu. Nami nilivyosikia pepa
limevuja ikabidi ninawe uso haraka kisha
nikachukua karatasi zangu nyeupe kadhaa kwaajili
ya kuandika majibu. Nilifika darasani nikawakuta
Saleh, Gerald na Jabir wamezungukwa na darasa
zima wanasolve pepa wakiwa navitabu kadhaa vya
physics kwaajili ya uhakika zaidi. Sikuweza kupata
nafasi ya kuchungulia mtihani kwasababu watu
walikuwa wengi sana wamezunguka na swali moja
likimalizwa kusoviwa watu ndo wanakopi. Mara
ghafla nikausikia ule wimbo ukiimbwa Kwa nguvu
¶¶¶Jama kosa lipi ambalo tumewakosea,. Ebu mje
mtukanye ili tusijerudia. Wanasema haufai
changudoa,
Tena Malaya, Tukiachana moyo wao nadhani
watafurahiya,. Wanakandiya, wanapondea wanadhani
watafanikiwa, Nimeshajua Janet wangu ni bora
tufunge ndoa¶¶¶. Nilisikia huo wimbo Kwa nguvu
sana ni kama kuna mtu kaweka spika kwa nje
mpaka nikaziba masikio ila ajabu wenzangu
walikuwa kawaida tu. Ikabidi niwaulize "Nashon
husikii nyimbo ikiimbwa we". "Wimbo!Wimbo
gani?" Nashon alionyesha mshangao kwa mimi
kumuuliza swali kama lile. Nikawaangalia watu
wengine bado walikuwa wako bize na pepa hapo
ndo nikajua ule wimbo nausikia peke yangu. Basi
nikajikuta napata shauku ya kuufata ule wimbo
unapotokea na kutembea nikahisi kama sitafika
haraka ikanibidi nikimbie ili kujua huo wimbo
unatokea wapi. ¶¶¶Sauti nzuri kama ya gita,. Hiyo
inakuita,. Taratibu uje kwangu ,uje bila kusita,. Yale
mapenzi ya utata,. Sipendi kuyapata,. Kimapenzi
nimedata,. Siwezi kutafuta,. Sema basi lazizi, Sema
basi mpenzi , nikilala usingizi , nakuota mpenzi,
kipenzi. ¶¶¶ ***
#04
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA NNE Basi nilijikuta
nikikimbia kama mtu aliyechanganyikiwa au aliye na
hamu kubwa ya kuona Jambo kubwa. Ule wimbo
ulikuwa unaimba kwa nguvu lakini cha ajabu kadri
nilivyokuwa naelekea sauti ile inapotokea ndivyo
sauti ya wimbo ilivyozidi kupungua. Sauti ilikuwa
inatokea maeneo yaleyale ya uwanjani karibu na ule
mbuyu ambao nimekuwa nikiutumia kujisomea hivi
karibuni. Basi ilinibidi nielekee mpaka uwanjani
huku na kimbia wakati huo wimbo ukakata ghafla
nikawa siusikii tena ila kwa mbali nikamuona tena
yule msichana akiwa kavaa tena shela lake jeupe
amesimama kwenye mbuyu kunipa kisogo.
Nikaanza kujongea taratibu kuelekea maeneo alipo
huku nikiwa na uwoga kidogo kwasababu imekuwaje
nilivyomuona huyu msichana kwa mbali ya uwanja
ndo ghafla tu wimbo ukaacha kulia, Pia hii ni mara
ya pili wimbo kukata ghafla maana hata
nilivyomuona kwa mara ya kwanza wimbo ulikata
ghafla. Swali la pili la kuogopesha juu ya ule wimbo
ni kwamba unasikia sauti kubwa ukiwa mbali tu ila
kadri unavyoukaribia wimbo ulipo ndipo wimbo
unapozidi kupunguza sauti. Pamoja na maswali yote
hayo ya kuogopesha bado upendo niliokuwa nao juu
ya msichana Janet ulinizidia na kunisahaulisha
habari zote kuhusu ule wimbo. Nilijikuta nimemiss
sana hivyo nikajikuta nimemkimbilia harakaharaka
na kumkumbatia Kwa nyuma huku yeye akinipa
kichogo. "Musa mpenzi". Aliniita kitu ambacho
kilinishtua alinijuaje kama ni mimi wakati
nimemkumbatia kwa nyuma na hajageuka? Lakini
lile neno la mpenzi ndilo lililonizuzua na kujikuta
najisahaulisha swali langu la awali. "Naam Janet".
"Mmh,mbona uniiti vizuri jamani?". "Nikuiteje?".
"Niite mpenzi" Maneno yake yalinifanya nipagawe
maana huyu mrembo ni mzuri haswa sasa anataka
kunitunuku pendo bila mimi kutumia nguvu yeyote
nilijikuta nimesita tu na kubaki mdomo wazi huku
nikijiuliza maswali moyoni ni kweli anamaanisha
tuwe wapenzi au anatania? "Sinaga utani Musa"
Nilishangaa maana nilichojiuliza ndicho alichokijibu.
"Musa unanipenda bwana unashindwa kuniambia
nami sitaki tuchelewe kuwa wapenzi hata mimi
nakupenda". Nilijikuta namshangaa amejuaje
kwamba nampenda wakati hiyo ni mara ya pili tu
tumeonana. "Nilikuona unavyonikimbilia kwa kasi ni
wazi unanipenda hutakiwi kujiuliza maswali ya
kijinga". Jibu la swali langu nililokuwa najiuliza
moyoni lilinishtua sana. Lakini Janet akaondoa
mshtuko wangu kwa kunikumbatia nami nikajikuta
nimezama kwenye mahaba na kusahau maswali
yote. "Janet hili ni eneo la shule tukikutwa hapa ni
msala". "Usijali hatukuti mtu". Bado nilihofia
kukutwa hivyo nikawa natafuta sababu kichwani
namna ya kumuacha Janet pale kwenye mbuyu.
"Janet , mtihani Jumatatu umejiandaaje ?". "Mimi
nimejiandaa vizuri tu naamini nitafaulu". "Janet
mwenzako siko vizuri ila inapaswa nikajiandae".
Janet alicheka "Aahaa" Alafu akasema "Ng'ombe
hanenepi siku ya mnada". "Najua lakini uzuri Leo
washkaji wamebahatika kupata feki ya physics hivyo
niache kidogo nikasolve hiyopepa huwenda ikawa
ndo yenyewe". "Mmmh ,ushasema feki alafu
unaenda kusolve si utapoteza muda hiyo pepa
haiwezi kutoka". "Mmh ,umejuaje kwamba haiwezi
kutoka ?". "Nimejua tu kwani nimeiona hiyo feki
ikisolviwa shuleni". "Sasa wewe una uhakika gani
kwamba haiwezi kutoka". Janet akacheka "Aahaaa"
kisha akasema. "Nauhakika kwamba haiwezi kutoka
kwasababu nimeuona mtihani original". "Mmh
muongo una uhakika gani kama huo ulio uona ndio
original". "Mimi naitwa Janet George Rwezalila".
Nilishtuka kwasababu jina lake la baba ni la waziri
wa elimu Tanzania. "Eehee kumbe baba yako ni
waziri ". "Ndio,Ndo maana nimejua Kuwa ule
mtihani sio wenyewe". "Kwa hiyo original unayo
wewe" niliongea kwa shauku. "Ndio ninazo pepa
zote na majibu yake ila sharti nikikupa
usimuonyeshe mtu yeyote isije ikagundulika baba
yangu kavujisha mitihani akavuliwa uwaziri". "Nipe".
"Niahidi kwanza kuwa hutomuonyesha mtu yeyote
hiyo pepa". "Nakuahidi ,Simuonyeshi yeyote"
#05
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA TANO. "Ni ahidi
hautamuonyesha mtu huu mtihani". Kwasababu
nilikuwa na shauku ya kuuona huo mtihani nilijibu
harakaharaka. "Sitamuonyesha mtu". "Je
ukimuonyesha?". "Nichinje". "Unasema mwenyewe
nikuchinje nitakuchinja kweli mimi sina masihara".
Nikajikuta nacheka tu kimoyomoyo. "Aahaa ,hata
nikimuonyesha mtu atajuaje kwani huyu". "We cheka
tu Ila ukimuonyesha mtu utanitambua" Aliongea kwa
hasira sana kiasi cha kunitisha maana muda ule
nilijichekea moyoni na maswali nilijiuliza moyoni
sasa amejuaje huyu kama mimi niliwaza hivyo?
"Acha kujiuliza maswali ya ajabu nimejua tu maana
wewe unaonekana kutaka kumuonyesha mtu". Bado
nikawa natetemeka namuhofia sana na kujiuliza
moyoni "Ni jini nini huyu mbona anayajua ya moyoni
mwangu?". "Sio jini bwana ,ebu acha kujiuliza ujinga
ujinga" Alisema hayo kisha akanikumbatia. "Unajua
Musa mi nakupenda sana, Sipendi kukupoteza
naomba niahidi hutoniacha utanipenda mimi tu
maishani". Alinikumbatia Kwa nguvu huku akinibusu
shingoni na kunifanya nipagawe kidogo na kujikuta
nasahau maswali niliyokuwa najiuliza juu yake.
"Hata mimi nakupenda pia". Nilijibu kauli yake kisha
akanitoa kwenye kumbatio laki akiwa kashika
mtihani na booklet la majibu nilishtuka. "Eehee hizi
karatasi zimefikajefikaje". "Mmmh ,kwani hukuniona
nikiwa nimezishika mkononi muda mrefu" Alijibu
fasta ambapo jibu lake mi sikuliridhia haraka.
"Mbona sikukuona nazo". "Ulivyonikumbatia Kwa
nyuma nikazificha Kwa mbele ulivyonikumbatia kwa
mbele nikazificha Kwa nyuma". "Aahaa"Nikajikuta
naitikia hivyohivyo tu maana huyu binti nilivyomkuta
sikumkuta na karatasi hata moja sasa hii ni miujiza
nilijikuta napata hofu kidogo. "Mbona unahofu na
mimi mpenzi?" Aliniuliza swali ambalo nalo lilizidi
kunichanganya ni kwanini amejua nina hofu. "Sina
hofu na wewe" ikabidi nimjibu tu hivyohivyo.
"Mtihani wenyewe wa Physics ndo huu" Alinionyesha
ule mtihani nami nikaanza kuusoma harakaharaka
na kujisemea "Mama yangu kwa pepa hii hatoki
mtu Si Saleh wala Gerald" Mtihani ulikuwa ni
mgumu sana. "Vipi umeuonaje mwepesi eehee?"
Alisema huku anacheka. "Huu mtihani Janet ni
mgumu sana aise kama utatoka huu watu wengi
watafeli". "Ndo huo huo utakaotoka usiseme kama
utatoka,Huo ndo unaotoka". Janet alitoa booklet ya
majibu. "Haya majibu yake haya,Kuna lingine la
ziada unahitaji?"Janet aliuliza. "Umesema
nisimuonyeshe mtu huu mtihani, Sasa hapa kuna
calculation zingine ni ngumu zinahitaji mtu
uelekezwe kidogo". "Usijali nitakusaidia" Basi ikabidi
tukae na Janet akaanza kufanya Yale maswali yote
magumu ili kunisaidia kuelewa hata kwenye kukalili
iwe rahisi. Nakumbuka siku hiyo wakati Janet
ananisaidia yale maswali alipita John mbio mbio na
kidaftari chake akaniona nimekaa kwenye mbuyu.
"Hoya Musa vipi wewe mbona umekaa hapo peke
yako wakati mambo yashavuja huko". Nikajikuta
nimepigwa na butwaa maana sijui cha kujibu maana
sikutegemea kama John ataona nimekaa peke
yangu ,Lakini John aliondoka harakaharaka maana ni
kama alikuwa amenishtua tu kuhusu kuvuja kwa
mtihani alafu akaondoka hakujali kitu tena.
Akaniacha nikiwa na maswali moyoni Inamaana
John hakumuona Janet au. Nikamuangalia Janet
nikamuona naye ananiangalia kwa kunikazia macho
mpaka nikajikuta nahogopa nikarudisha macho
kwenye mtihani haraka. Basi tuliendelea kusolve ule
mtihani huku Janet akipiga story mbalimbali ili
kujaribu kuniondoa hofu na kuna wakati nilikuwa
nawaza vitu na akawa hayasomi mawazo yangu.
Basi ile hofu ya kuwa Janet sio binadamu wa
kawaida ilianza kunipotea na kuanza kuhisi ni
mawazo yangu tu. Tulimaliza kusolve ule mtihani na
Janet akanipa ile pepa. "Vip we uhitaji
kujikumbushia?" Nilimuuliza Janet ambaye alikuwa
anaondoka bila kuchukua hata mtihani ili
akajisomee. "Mi nipo fiti" Janet alijifanya kukaza
mikono kama baunsa ili kuonyesha ufiti wake hali
ambayo nikajikuta nacheka tu. "Basi Musa mpenzi ,
Tafadhari usimuonyeshe mtu,Alafu kumbuka kesho
tukutane hapa kwaajili ya Mathematics" Alisema
huyo huku anaondoka. Mi nikajikuta natabasamu tu
yahaani hata siamini nimepata mtoto mkali namna
hii tena ni kichwa kwelikweli anafanya maswali ya
physics bila kubabaika. Furaha niliyonayo siku hiyo
ilikuwa kubwa mno kiasi cha kusahau kabisa
kumuuliza Janet kuhusu ule wimbo "Kwanini
ukiimbwa ndio yeye anatokea?" Pia nilijikuta
navisahau vituko vyote vya Janet na kuanza kuhisi
huwenda Janet ana karoho fulani kabaya kwani
hataki watu wote tufaulu nami roho mbaya siwezi,
Moyoni moja kwa moja nilipanga kumshirikisha
mshikaji wangu Nashon kwasababu yeye ndiye
alinishtua kama kuna fake hivyo amenipa mzuka wa
kusoma nami nilitamani kulipa fadhila mshikaji
wangu asije akadhalilika kwenye pepa
 
6------10 )*
#06
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA SITA. Nilirejea
kwenye darasa ambalo watu wote walikuwa
wakisolve ile pepa nikiwa na shauku kubwa ya
kumwambia Nashon kuhusu ile pepa lakini kabla
sijafanya hivyo nikasikia sauti ya ukali. "We acha"
Nilishtuka kusikia hivyo nikageuka niangalie kama
kunamtu yeyote kasema lile neno maana nilihisi
kama naambiwa mimi lakini sikumuona
mtu.Nikawaangalia washkaji wengine kama
wamesikia ile sauti lakini jamaa walikuwa bize na
wala hawajashtuka chochote hii ilionyesha wazi ni
kuwa hawajasikia chochote. Basi nami nikapuuza Ile
sauti na kumfata Nashon. "Hoya Nashon ,njoo
chemba mara moja". "Nije kufanya nini bwana
baadaye, Maswali yakitupita hapa hakutakuwa na
mtu wa kutuelezea" Nashon alijibu huku akiendelea
na ubize kufatilia kila hatua ya maswali
yanavyosoviwa. "Njoo bwana mara moja ni muhimu
sana" Nilimsisitizia Nashon ambaye awali
alionyesha kupuuza wito wangu. "Poa ,iwe muhimu
kweli" Nashon aliitikia na kuacha shughuli zake
kisha kunifata kunisikiliza. "Nashon unajua Ile pepa
inayosoviwa sio yenyewe". Nashon akacheka "Aahaa
,Umejuaje kama sio yenyewe wakati hata kuiona
hujaiona" Nikabaki mdomo wazi maana ni kweli
pepa sijaiona. "Sijaiona ndio lakini ,mimi ninayo
pepa yenyewe" Nashon akajikuta anacheka tena
"Aahaa,Sasa pepa yenyewe we umeipata wapi
wakati ulikuwa umelala muda wote" "Nimeipata
tu,kuna msi......" Nilitamani kusema kuna msichana
mmoja wa Vilambo girl ndio kanionyesha hiyo pepa
lakini nikajikuta nimekwama ghafla na sauti aitoki
tena. "Vipi mzee umekuwa bubu ,Ebu tusipotezeane
muda ,unaujua mziki wa physics lakini we" Nashon
aliongea hayo kisha kurudi kwenye solving huku
akiniacha mimi nikiwa midomo wazi mara ghafla
nikasikia tena. "We si nimekwambia uache"
Nikageuka kwa hofu kuangalia anaye nisemesha
sikumuona hivyo nami nikaona ni bora tu kuitunza
ahadi ya Janet tulioahidiana. Ikanibidi nitafute
darasa kwaajili ya kujikumbushia yale maswali.
Niliyasoma yote na kujikumbushia kama mara mbili
hivi hapo nikajikuta napata wazo lingine maana
waswahili wanakwambia wasiwasi ndio akili. "Vipi
itakuwaje kama haya maswali hayatatoka yatatoka
yale mengine inamaana shule nzima nitafeli peke
yangu?" Nilikikuta nawaza lakini nikashangaa sauti
ya msichana ikinisemesha. "Naona huniamini na
hauna Siri sasa hivi nakuja kuchukua mtihani wangu"
Nilishtuka kusikia sauti hiyo mahali pale hasa
ukizingatia nilikuwa peke yangu. Basi morali wote
wa kusoma ukaniishia na kujikuta na kusanya vitu
vyangu harakaharaka na kuondoka eneo lile.Nilikuwa
na karatasi fulani kubwa kubwa ambazo nilikuwa
nazitumia kusovia maswali. Nikauchukua ule
mtihani na kuuweka katika yale makaratasi kisha
kuondoka haraka. Nilikuwa na uwoga sana hivyo
sikuweza kwenda tena sehemu ya peke yangu
kukaa, Ilibidi nirudi kwa wanafunzi wenzangu
waliokuwa wanajisolve pepa nikakaa pembeni huku
nikiwa natetemeka. Nilivyofika Jamaa walikuwa ndo
wamemaliza walivyoniona tu wakacheka. "Musa
tupe hiyo feki uliyokuwa nayo tusolve maana nasikia
unayofake". Kumbe Nashon alishawaambia kila kitu.
"Musa,Ebu jionee huruma,Yahaani tangu pepa ianze
kusolviwa hujaonekana zaidi ya kuja na kusimama
na kutoka hivi shule nzima ikifaulu ukafeli peke
yako si itakuwa aibu?" Salehe aliongea maneno ya
kuniumbua kidogo maana huyu jamaa Salehe
hujifanya ni mjuaji sana na mtoa ushauri. Mara John
akaja mpaka nilipo na kusema. "Eti anayofeki
anayoitegemea wakati Nashon kasema muda wote
jamaa alikuwa kalala sasa sijui hiyo feki kaitolea
wapi? Ebu tuone"
Alisema hayo kisha akanipora karatasi zangu
nilizozishika mimi nikataka nimnyang'anye Lakini
John alishazipasisha karatasi zangu Kwa watu
wengine hatimaye nikazikosa kabisa.Na mara ghafla
nikajikuta nawaza ile kauli ya Janet baada ya mimi
kusema kama nitazionyesha pepa basi anichinje.
"Je ukimuonyesha?". "Nichinje". "Unasema
mwenyewe nikuchinje nitakuchinja kweli mimi sina
masihara
***Share
#07
WIMBO WA AJABU SEHEMU 7 Mawazo juu ya
maneno ya Janet yalinijia kichwani.Na kila
nikikumbuka vituko vya ajabu ajabu ambavyo
vishaanza kunitokea ni wazi kuwa Janet ni
Jini.Ukijumlisha na ile ahadi ya kuchinjana nilijikuta
napata hofu zaidi na kujikuta nafanya vurugu nyingi
ili nirudishiwe karatasi zangu lakini bahati mbaya
wenzangu walikuwa wengi hivyo nikadhibitiwa na
karatasi ikasomwa. Msomaji alikuwa ni Gerald
maana ndiye wanayemuaminia kuwa ni kichwa.
Alichokutana nacho alijikuta akicheka tu.
"Aaahaa,Huyu Musa kachanganyikiwa" Kicheko
chake kilinishtua hata Mimi ni kitu gani amekiona.
Karatasi alimpasia Salehe naye alivyoona tu
akacheka kisha akawaambia wale jamaa waliokuwa
wananizuia nisichukue karatasi zangu. "Muachieni
huyo mpuuzi achukue vikatuni vyake".Kauli hiyo
ilinishangaza ingawa niliachiwa ili nikachukue
karatasi zangu ila sikufanya vurugu tena zaidi ya
kubaki mdomo wazi.Salehe kwa dharau zake
akanitupia zile karatasi zangu usoni. "Mjinga we
acha utoto umechanganyikiwa au vipi? Kesho ndo
pepa ila inashangaza wewe hujihurumii
unachorachora vikatuni hovyo" Basi niliokota zile
karatasi ,Sikuamini nilichokiona nilikutana na
vikatuni vitupu vya kina Tom and Jerry na vikatuni
vya kina masudi kipanya. Watu wote waliamini kuwa
mimi nilivichora vile vikatuni kwasababu mbali na
kipaji cha mpira wa miguu pia mimi ni mtaalamu
wa kuchora katuni hivyo ikawafanya waamini
huwenda nilishakata tamaa ya mtihani nikaamua
nijichoree katuni tu. Wengi wakawa wananicheka
ingawa mimi nilikuwa sijali vicheko vyao bali
nilikuwa nawaza hivi vikatuni vimetoka wapi katika
haya makaratasi na pepa yenyewe iko wapi? Ila
ghafla nikajikuta nakumbuka ile kauli niliyoiwaza
nikiwa peke yangu
"Naona huniamini na hauna Siri sasa hivi nakuja
kuchukua mtihani wangu" Mmh atakuwa amekuja
kuchukua mtihani wake nini? Nilijikuta najiuliza
lakini nikasikia sauti kwa nyuma ikijibu "Ndio"
niligeuka nyuma hamna mtu basi nikajikuta napata
hofu zaidi na kuanza kutetemeka ingawa kukimbia
nilishindwa kwasababu nilihofia upweke wa peke
yangu na kama Janet ni jini kweli ameahidi
atanichinja hivyo nisingeweza kukaa peke yangu
ikanibidi ni baki palepale kwa washkaji ingawa
walinidhihaki sana lakini sikujali bali niliendelea
kubaki kwani nilikuwa naogopa sana kuwa
mwenyewe asije akatokea Janet. Siku hiyo sikuweza
tena kujisomea kwani kichwa changu kilitawaliwa na
mawazo ya kuchinjwa kama kweli Janet ni
jini.Wengi walijisomea barabara maswali ya feki
huku wengine wakibaki kunihurumia na wengine
wakibaki kunicheka tu. ******************************
********* Jumatatu ikapambazuka na bado mimi
sikuwa na mzuka wa kujisomea kabisa zaidi ya
kuomba kuwa pepa niliyoisolve isiwe yenyewe ?
Unajua kwanini niliomba hivyo niliomba hivyo
kwasababu sikutaka kuamini kama Janet ni jini
hivyo bora pepa isiwe yenyewe. Muda wa mtihani
uliwadia na wanafunzi wengi walionyesha kujiamini
zaidi kwani walikuwa na uhakika wa asilimia karibia
mia moja kwamba mtihani ndio wenyewe. Tuliingia
kwenye chumba cha mtihani na wote tutakabidhiwa
pepa ikafunikwa kwenye meza zetu kabla
msimamizi hajatuambia tugeuze karatasi zetu.
Wengi walikuwa na nyuso za tabasamu huku
wengine wakiniangalia mimi huku wakinisikitikia ila
nyuso zao zilikuja kubadilika ghafla pale msimamizi
aliposema. "Sasa mnaweza kusoma maswali" Hapo
nikamsikia Nashon akisema. "Mamaa" Watu wote
wakamgeukia yeye na kuhisi ni dalili mbaya maana
wengine walikuwa bado hawajaanza kusoma
maswali ,wakafungua haraka haraka hawakuamini
walichokutana nacho hakuna hata swali moja
waliosolve jana alafu mtihani ni mgumu balaa. Mimi
baada ya kuona kila mtu anaguna kivyake nikaanza
kupata hofu huku nikijisemea "Kama mtihani ni
wenyewe basi Janet ni jini". Nikawa naufungua ule
mtihani huku natetemeka huku nikiomba usiwe
wenyewe
**
#08
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA NANE Nilitetemeka
sana wakati naufungua ule mtihani mpaka nikaamua
nifumbe macho alafu nikaufungua ule mtihani na
kuwa mweupe kisha nikafungua macho ghafla.
Huwezi amini mtihani ulikuwa ndo wenyewe
maswali yote kila kitu nikajiuliza Inamaana Janet ni
kweli Jini? nikajikuta najijibu hapana ni mtoto wa
waziri. Je na ile sauti yake niliyokuwa naisikia
nikikaa peke yangu? Jibu yale yalikuwa ni mawazo
tu. Nilijiulizangi kuhusu Janet na kujiridhisha kuwa
ni mtoto wa Waziri na sio Jini. Sikujua ni kitu gani
kilinifanya nijiridhishe kuwa ni mtoto wa Waziri na
sio jini maana maswali ya msingi kama kupotea
mtihani hali ya kuwa niliwaza kuwa Janet anautaka
mtihani wake sikujiuliza. Pia sikujiuliza kuwa kuhusu
wimbo nilijikuta naamini tu moja Kwa moja kuwa
Janet ni mtoto wa Waziri. Basi niliendelea kusonga
mbele Kwa kusolve ule mtihani na mtihani kwangu
ulikuwa mwepesi mno. Na haikupita muda
nikanyoosha mkono,watu wakanishangaa na
msimamizi akaja. "Nikusaidie nini?". "Naomba
booklet la lingine". Darasa zima walinitazama kwa
mshangao kwani mtihani kwa upande wao
umewawia vigumu na wanakwamakwama
tu.Msimamizi akanipa bocklet lingine nami
nikaendelea na mtihani.
Basi niliucharaza mtihani fastafasta huku karibia
watu wote darasani walikuwa wakiniangalia mimi
kwani walipata nafasi ya kufanya hivyo maana
mtihani ulikuwa ni mgumu mno hivyo wengi
walijikuta wakifanya maswali mawili tu au matatu
tena kwa mbinde hali ambayo ilisababisha muda
wote watu wageuke huku na huku mpaka kufikia
hatua watu kunitazama mimi kama video kwani
hawakuamini kama kwa mtihani ule kuna kiumbe
chochote kitaomba booklet la pili. "Hoya Musa
naomba weka booklet lako vizuri nichungulie" hiyo
ilikuwa ni sauti ya Nashon baada ya kuona darasa
zima likiwa doro huku watu wakiwa wanagalagala
kama wamemwagiwa maji baridi ndipo akatumia
nafasi hiyo kuniomba majibu nami sikuwa na hiyana
nilimuachia booklet wazi upande mmoja nikampisha
agelezee atakavyo. Nashon aligelezea harakaharaka
lakini haikupita hata nusu saa msimamizi
alishausoma mchezo. "Wewe ebu njoo mbele"
Msimamizi alininyanyua kwenye Ile siti akaniweka
siti ya mbele kabisa na kumuacha Nashon akiwa
hana msaada tena. Mimi nikaendelea kuucharaga
ule mtihani bila wasiwasi nikaumaliza na kuukabidhi
na kutoka nje nikawaacha watu wanaangaika tu.
Sikutaka kupoteza muda moja kwa moja nilielekea
kwenye ule mbuyu ili kumsubiri Janet maana
tuliahidiana tutakutana hapo kwaajili ya mtihani wa
hesabu. Lakini ajabu wakati naenda nikamkuta
Janet tayari ameshafika kwenye ule mbuyu na kama
kawaida yake alikuwa amevaa shela jeupe huku
akiwa kanipa kisogo. Nilijikuta nashangaa kidogo
maana kutoka shule Yao mpaka ya kwetu inaweza
ikamchukua mtu dakika 20 au 30 lakini Janet tayari
alishafika kwenye ule mbuyu tena kwakutokea
shuleni kwao. Maswali ni mengi niliyojiuliza ni kuwa
ule mtihani ni wa masaa matatu na kutokana mi
nayajua maswali yote kila kitu ndo maana
nimeufanya saa moja na dakika kumi binafsi
niliamini mimi ndo mtu niliyewahi kumaliza mtihani
mapema zaidi si tu hapa shuleni tu bali Tanzania
nzima ila Janet ananitisha kidogo maana ukitoa
muda wa mimi kumaliza mtihani na umbali wa
shuleni kwao utapata dakika 40 na bado Janet
anaonekana alimaliza mtihani akaenda bwenini
kubadilisha nguo hali hii inaonyesha huwenda huyu
kafanya mtihani chini ya nusu saa kitu ambacho
hakiwezekani pia hata sheria za mtihani haziruhusu
mtu kutoka kwenye chumba cha mtihani chini ya
nusu saa hali hiyo ili nitisha kidogo wakati na
msogelea huku na tetemeka nikajiuliza. "Huwenda
ni jini kweli" Nikasikia sauti inanijibu "Acha kujihami
,niwe jini au ni siwe jini Leo utaniambua kwanini
ulitaka kuonyesha mtihani"
***Share
#09
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA TISA
Jibu lile lilinishtua nikataka kukimbia lakini nikasikia
sauti ya Janet ikicheka "Aahaa ,unakimbia unafikiri
unaweza kunikimbia?" Nilisikia hiyo sauti huku Janet
akiwa bado amenipa kisogo.Aise nilishindwa
kuvumilia ikanibidi nianze kukimbia lakini ghafla
nikahisi miguu yangu inaisha nguvu na nashindwa
tena kunyanyua mguu wangu kupiga hatua hata
moja. Hapo ndipo nikaanza kuhisi mtu
ananisogelea,Alikuwa ni nani mwingine zaidi ya
Janet alinisogelea mpaka mbele ambapo nilikuwa
nimedondoka kwa kutaka kukimbia alafu
akaninyanyua pale chini nilipokuwa nimeanguka
wakati najaribu kukimbia. "Vipi mbona unataka
kunikimbia?" Aliniuliza swali la ukali mno.
"Aaahaa,nilikuwa sikimbii". Nilijikuta napata
kigugumizi katika kujibu lile swali. "Unanikimbia
kwasababu unajua ulichokifanya" Neno lake
lilinitetemesha kidogo kwasababu ni kipi
nilichokifanya zaidi ya kutaka kuonyesha mtihani.
"Tafadhari nisamehee"Nilijikuta naomba msamaha
mwenyewe kabla sijahukumiwa kutokana na kosa
langu. "Hivi kwanini umekuwa huna siri Musa
unataka baba yangu afukuzwe kazi" Janet aliuliza
kwa ukali kidogo Ila mimi sikutoa jibu kwa muda
nikaanza kutafakari ile kauli yake aliyoitoa kwani
inaonyesha huyu anahofia mtihani usivuje
kwasababu baba yake atafukuzwa kazi na kama
anahofia baba yake kufukuzwa kazi basi inaelekea
huyu ni mtoto wa waziri kweli na sio jini,Sasa
amejuaje kama nilitaka kuvujisha mtihani? au ni
jini?Nilijikuta najiuliza maswali mengi moyoni kabla
sijajibu swali lake lakini akanijibu hapohapo.
"Nimejua tu kwasababu ulitaka kukimbia ulivyoniona
na pili umejifanya kwa kuomba msamaha". Kauli
yake ilinishtua kidogo nikajikuta nawaza "Mmh
mbona kama anajua ya moyoni mwangu huyu sio
jini kweli". "Mimi najua namna ya kumsoma mtu
moyoni Ila sio jini ebu futa hayo mawazo yako ya
kuwa mimi ni jini au sio jini". "Sasa unajuaje ya
moyoni kwangu bila kuambiwa kitu wewe" Nilijikuta
namuuliza swali waziwazi huku nikitetemeka maana
niliona hakuna haja ya kujiuliza moyoni maana
nikama anayasoma mawazo yangu "Hayo yote
utayajua baadaye kikubwa hutakiwi kutoa siri yangu
ya aina yeyote Kwa mtu yeyote ila pia sitaki
uniambie kuwa mimi ni jini hilo neno lako la kuwa
mimi ni jini linanihudhi muda wote". Basi nikabaki
nimeduwaa tu huku namtazama Janet nikajiuliza
tena. Sasa kama sio jini ni nani?
Safari hii nilimuhudhi sana Janet. "We nimekwambia
nini saa hivi na unafanya nini muda huu kumbuka
nilipaswa nikuadhibu ukaomba msamaha alafu bado
unanihudhi" Basi ikabidi niwe mpole na kujaribu
kubadilisha mada. "Mtihani wa hesabu unao". "Ndio
ninao ila safari hii naomba ujitahidi asione mtu
yeyote sawa". "Sawa". "We endelea kuitikia sawa tu
alafu umuonyeshe mtu safari hii sitakusamehee".
Basi Janet akatoa mtihani wa hesabu na tukaanza
kuusolve. ***************************************
Masaa matatu ya mtihani yaliisha huku watu wakiwa
hoi wakati wanatoka kwenye chumba cha mtihani
kwani kwenye mtihani wa maswali 10 kuna
waliofanya maswali 3 wengine 2 Ila wapo baadhi ya
vichwa vilivyofanya maswali matano akiwemo
Gerald na Salehe lakini katika orodha ya waliofanya
maswali mengi Nashon pia naye alifanya maswali
mengi kwani aligerezea maswali kama manne
kutoka kwangu Kwa harakaharaka na kufanya baadhi
ya maswali kama mawili kwa uwezo wake binafsi.
Wengi walibeza kitendo cha mimi kuchukua booklet
mbili Kwa harakaharaka hasa Gerald na Salehe
walitoka huku wakiulizana mtihani Kwa upande wao
ulikuwaje. "Vipi Salehe lile swali la nne limeenda
kweli".Gerald alimuuliza Salehe swali moja ambalo
hana uhakika nalo. "Aahaa lile ni swali la necta
mwaka 93 limerudiwa" Salehe alitoa kitabu cha
mitihani iliyopita ya Taifa Nakuonyesha lile swali
kumbe wakati huo Nashon naye akachungulia
akajikuta anafurahi "Dah nimepata hilo" Ila Salehe na
Gerald hawakumjali waliendelea kufungua vitabu
mbalimbali ili kuhakikisha maswali yaliyojirudia
kama wamepata au lahaa na kila walipopita Nashon
alikuwa anashangilia sana mpaka kwenye swali
moja ambalo waliliona Kwa bahati mbaya kwenye
kitabu Fulani Kwa bahati mbaya au nzuri wakati
wanatafuta swali lingine. "Eehee,kumbe hiki kitabu
kizuri hata ili swali lipo humuhumu alafu tumekosa"
Nashon alivyoliona lile swali akafurahi zaidi. "Dah
nimepata Yule Musa atakuwa alikuwa na feki Yule
maana kila swali kapata" kauli hiyo ya Nashon
iliwashtua Gerald na Salehe na baadhi ya wanafunzi
waliopo karibu
***Share
#10
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA KUMI Baada ya
kumaliza kufanya mtihani Janet alisema. "Musa
unajua mimi nakupenda sana" "Hata mimi
nakupenda" Nikamjibu. "Musa mi sitaki nikupoteze
hivyo jitahidi kutunza siri" Nilishtuka kidogo maana
ni kauli ya kitisho kidogo. "Sipendi utishike ila
napenda uzingatie kile ninachokisema maana mimi
sio binadamu wa kawaida". Nilimuangalia kwa
woga sana. "Pia sipendi uniogope naomba unizoee
kwani mimi nina uwezo mkubwa sana wakusoma
mawazo ya mtu hivyo uwezo wangu wa kusoma
mawazo yako usikutishe naomba uuzoee". "Sasa
wewe ni binadamu wa aina gani mwenye uwezo
mkubwa kama huo kama sio jini" Nilijikuta
namuuliza hilo swali licha ya mara kadhaa kunionya
nisimuite jini wala nisimdhanie kuwa yeye ni jini.
"Musa mpenzi unajua mimi kila kitu nafanya kwaajili
yako ndo maana unaona nimekuibia mtihani" Alivuta
pumzi kisha kuendelea. "Mimi sipendi unavyoniita
jini kwani hapa ni lipo ni nusu jini ni nusu binadamu
hivyo nisingependa uniite jini kwani mimi natamani
kuishi kama binadamu hivyo unavyoniita jini
unanirudisha kwenye hali ya ujini". Nilishtuka kidogo
na kutaka kukimbia. "Usinikimbie wala usiniogope
kwani mimi siwezi kukudhuru na binadamu kama
wewe". Maneno yake yaliniondoa hofu kidogo lakini
nikawaza "Kwanini sasa anang'angania kuwa yeye ni
binadamu". "Ndio mimi ni binadamu ndo maana
hapo awali nilikueleza kuwa mimi sio jini na sipendi
uniite jini". "Sasa kama sio jini kwanini umejiita
wewe ni nusu jini nusu binadamu". "Mimi naitwa
Janet George Rwezalila ni mtoto wa Waziri wa
elimu". Janet alinichanganya maana muda mfupi
alisema yeye ni nusu jini nusu binadamu na sasa
anajitambulisha kuwa ni mtoto wa waziri. "Ndio
mimi ni nusu jini nusu binadamu pia ni mtoto wa
waziri wa Elimu ,Baba yangu ni George Rwezalila na
mama yangu anaitwa Zulekha umul subiha". Janet
akavuta mate kidogo kisha kuendelea na story yake
ilinistaabisha. "Mama yangu anatokea katika ukoo
wa majini ya kisubihani yahaani majini ambayo
yanaweza kuwa na mahusiano na wanadamu".
Nikabaki nimeshangaa tu nakujiuliza maswali
yahaani kumbe majini nao wana koo zao. "Ndio
majini wana koo zao kama ruhani wao ni watu wa
kichwani pia kuna koo nyingi za majini nisingependa
kuyazungumzia hayo maana hapa tulipo wapo
wanatusikiliza". Nilishtuka kusikia majini
yanatusikiliza. "Usishtuke ni kuwa wanatusikiliza tu
Ila hawawezi kutudhuru wao kazi yao ni umbea tu
hivyo muda wote huongozana na wanadamu
kusikiliza habari zao". "Kwa hiyo wewe umesema
Baba yako ni waziri na mama yako ni jini kivipi sasa
hiyo ikawa hivyo". "Ndio Baba yangu ni waziri
George Rwezalila na mama yangu ni Zulekha umul
Subiani yeye ni jini" Alivuta mate kisha kuendelea.
"Mama yangu ndiye aliyempenda baba yangu hivyo
akaanza ukaribu naye bila baba yangu kujua".
Alinyamaza kidogo kisha kuendelea. "Mara nyingi
mama yangu alimjia baba nyakati za usiku na
kufanya naye tendo la ndoa bila baba kujua Ila
alimpa ishara ya ndoto tu juu ya ujio wake". Nilikuta
nimeganda tu kwa mshangao "Mama yangu
alitamani kujitokeza kwa baba yangu ana kwa ana
lakini alishindwa kutokana na pingamizi kutoka kwa
wazazi wake kuwa hatakiwi kuoana na binadamu
hivyo aliamua afanye Kwa siri sana mpaka kipindi
mama yangu alivyopata ujauzito hivyo akaamua
kujificha mbali mno maeneo ya milimani mbali
kabisa na familia yake inapoishi mpaka aliponizaa
mimi". "Na aliponizaa alitegemea atazaa mtoto jini
kamili Ila kwa bahati mbaya amenizaa nikiwa nusu
jini nusu binadamu". Story ya Janet ilinivutia kiasi
fulani licha ya mwanzo nilikuwa namuogopa Ila
nikajikuta simuogopi tena nikajikuta namuuliza.
"Kuna tofauti gani Kati ya jini kamili na nusu jini
nusu binadamu". "Tofauti zipo nyingi Ila moja wapo
ya harakaharaka ni kuwa jini ana kwato na mimi
sina kwato"
 
(16-----20)
#16
WIMBO WA AJABU SEHEMU 16. Nilijikuta naanza
kujiogopa nilivyozisikia sauti za rafiki zangu kwani
siku tarajia kabisa hapo ndipo nikajilazimisha
kukumbuka yale maneno yalisemwa saa ngapi kuwa
mimi nimekuwa thumuni jini na ujini wa Janet
umepungua kwa thumuni Inamaana Janet sasa ujini
wake sio nusu tena kwasababu amechanganya
damu na binadamu nami tena sio binadamu kamili
kwasababu nishachanganya damu na jini basi
nilijaribu kuwaza ni wakati gani huo nilichanganya
damu na Janet ila sikupata jibu mpaka kichwa
kikaniuma ikabidi niende kujipumzisha tu.Nikapitiwa
na usingizi ,Kwenye usingizi nikaota jinsi ilivyokuwa
jana mara baada ya kukubali kutokutoa siri mama
yake Janet alinishika kichwani kisha kuniambia
maneno Fulani nisiyoyajua nikajikuta nimekuwa
kama zezeta.Kisha mama yake Janet akatoa mkeka
aina ya mswala akakaa kisha akatuita mimi na
Janet pia tukakaa kwenye ule mkeka huku mimi
nikiwa bado sijitambui ni kama zezeta vile. Mama
Janet aliongea maneno Fulani ambayo yakaifanya ile
sehemu kubadilika ghafla na kuwa ni kama sehemu
juu ya maji. Yahaani niliona ule mkeka umetandikwa
juu ya maji nasi tumekaa juu yake . "Huyu
anapaswa kuwa thumuni jini walau ili ikisaidie usije
ukamuua katika kipindi ambacho unafanya maombi
uwe binadamu kamili si unajua hupaswi kuua
kiumbe chochote chenye damu inayoweza kuzidi
nusu Lita". "Najua hilo,Ndo maana nimemleta
kwako ili utuozeshe". Basi mama Janet nikama
alimuita mtu asiyekuwepo pale kwa lugha fulani
nisiyoielewa na ghafla akaja mjakazi fulani wa kijini
akiwa amemshika mbuzi mwepe asiye na doa na
bakuli moja kubwa. Yule mbuzi aliwekwa kwenye
mkao wa kuchinjwa na mama Janet pasipo kuwa na
Kisu na mara ghafla Meno marefu yakamtoka mama
Janet akarukia mbuzi kwenye shingo kisha kutoboa
shingo ya mbuzi kwa kutumia meno yake na mbuzi
akaanza kupapalika kwa kukata roho huku damu
ikimtoka wakati huo mama Janet alikinga ile damu
kupitia lile bakuli la dhahabu alilolishika. Wakati huo
Janet alikuwa akiweweseka sana na manyoya
yakaanza kumtoka huku Meno pamoja na makucha
marefu yalianza kumtoka mama akachukua mkono
wangu na kumkabidhi mwanaye mdomoni
akaning'ata kisha kuanza kuninyonya damu huku
akiwa kaning'ang'ania Barabara lakini mama yake
akautoa mkono wangu kwa nguvu kisha kumyosha
Janet damu ya mbuzi hapo nikamuona Janet akiwa
katulia. Baada ya hapo mama Janet alimng'ata
mwanae mkononi kisha kukinga damu kidogo
kupitia lile bakuli ambalo lilikuwa na damu ya
mbuzi,kisha kuninywesha ile damu. Baada ya
kunywa ile damu mama Janet aligusisha vidonda
vyetu ambavyo vilikuwa na majeraha ya kung'atwa
kisha akasema yale maneno ya kuwa mimi
nimekuwa thumuni jini .Maneno ambayo
sikuyaelewa toka Jana kuwa yalitamkwa wakati
gani. **************************************** "We
Musa vipi mbona umelala mpaka saa hivi mtihani
bado nusu saa tu uanze"Nilijikuta nakurupuka haraka
usingizini dah kumbe nilipitiwa na usingizi mzito wa
masaa mengi na kulala toka saa tatu mpaka saa
moja asubuhi. Basi ilinibidi nijiandae haraka kisha
kuelekea kwenye chumba cha mtihani lakini wakati
naelekea nilikuwa najiuliza maswali mengi kuwa ni
kweli nimekuwa thumuni jini au laa. Basi ikabidi
niangalie mkono wangu kama unajeraha lolote
maana niling'atwa kwenye mkono katika ile
ndoto,Kwakweli sikukuta jeraha lolote basi ikanibidi
nijipe moyo tu kuwa ile ni ndoto tu. Nilifika kwenye
chumba cha mtihani nikamkuta msimamizi ndo
anasema. "Start"(Anza). Mimi nilipita moja kwa
moja ili nikakae kwenye siti yangu lakini msimamizi
akanizuia Kwanza. "Huruhusiwi kufanya mtihani
kwasababu umechelewa" Msimamizi alijikuta
anaropoka tu kinyume na taratibu za mtihani maana
taratibu za mtihani huruhusiwi kuingia kwenye
chumba kama zishapita dakika 30 lakini mimi
nilifika muda ambao watu ndo wameambiwa waanze
hivyo na haki ya kupewa mtihani na kufanya. Basi
nilijikuta namuangalia msimamizi kwa hasira
nikajikuta nasoma mpaka mawazo yake hali
ambayo ilinitisha sana. "Ngoja nimbanie huyu dogo
ili nionekane sina masihara kwenye kazi"
#17
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA 17. Nilimuangalia
yule msimamizi kwa hasira sana kwani niliona
kabisa katika moyo wake alikuwa anatafuta sifa tu
na si kutenda haki. "Lakini nusu saa bado haijatimia
ninavyojua mimi sheria za mitihani unatakiwa
usichelewe zaidi ya nusu saa ". "Dogo acha kuleta
sheria zako za mid term huu ni mtihani wa taifa
unapaswa kuingia kabla ya nusu saa" Basi nikawa
namuangalia tu maana cha kufanya nilikuwa sina
nilitamani japo nimsukume kwa nguvu nimbamize
ukutani,lakini kwa ghafla nikajishangaa nikama
nimemvamia na kumsukuma kwa nguvu lakini
ukweli nilikuwa nimesimama tu ila nikama mawazo
yangu yalijenga fikra zile kutokana na hasira
nilizokuwa nazo. Lakini ghafla nikasikia wanafunzi
wameshtuka. "Eehee" Nami ikabidi nigeuke maana
baada ya maneno yake ya kutafuta sifa niliamua
nigeuke kutaka kuondoka ili nikamshtaki walau kwa
wasimamizi wengine haki itendeke. Nilipogeuka
kuangalia wale wanafunzi walikuwa wameshtushwa
na kitu gani ndipo nikamuona yule msimamizi
alikuwa ameanguka kwenye meza na kuvuja damu
puani na masikioni huku akiwa anatweta kwa
kupumua. Ikabidi nibaki kushangaa tu na kujiuliza
maswali hivi ni kweli nilimsukuma huyu msimamizi
au kitu gani kilitokea. Gabriel aliacha kufanya
mtihani na kutoka nje maana yeye ndiye monitor wa
darasa akaenda kuwaita wasimamizi wengine
ambao walikuja mkuku mkuku na kuuliza. "Nini
kimetokea" Msimamizi ambaye ni mwanamama
aliuliza huku anatweta maana alikimbizwa na Gabriel
mkukumkuku aje kuona kuna dharura
imetokea.Mimi wakati huo nilikuwa bado sijielewi
kama lile tukio nimelifanya mimi au ameanguka
kivyakevyake maana nilijiona kabisa namsukuma
yule msimamizi kwa nguvu na kumbamiza ukutani
lakini cha ajabu nilijiona tena nimesimama
nikijiuliza itakuwa ni mawazo tu Ila ajabu
msimamizi kweli ameenda chini na damu zinatoka.
"Hata sisi hatujui ,tumeshangaa msimamizi
ameanguka ghafla" "Wewe,Wewe na wewe naomba
mnisaidie kumtoa nje" Yule msimamizi wa kike
alituchagua watu kadhaa tukamtoa msimamizi nje
mpaka ofisini kisha akateuliwa msimamizi
mwingine kuja kutusimamia. Tuliporudi
nilimwambia Yule msimamizi."Mi sikupata mtihani"
Nikapewa na mtihani ukaendelea. Mtihani kwa kweli
ulikuwa ndo wenyewe kila mtu aliufurahia mimi
nilikuwa nafanya mtihani huku nikiangalia watu jinsi
walivyokuwa wanafanya mtihani kwa furaha ila
bahati mbaya au nzuri macho yangu yakakutana na
Salehe. Salehe alikuwa kama ananiangalia kwa
macho mabaya hivi hali hiyo ikanifanya nitamani
kujua anachowaza "Huyu mjinga bora angetolewa tu
kwenye pepa" Hapo ndipo nikagundua binadamu si
watu wakuwaamini maana Salehe ni rafiki yangu
kitambo ila sikutarajia kama atafurahia mi kukosa
mtihani. ***************************************
Mtihani huu wa hesabu wote tulishausolve hivyo
kwenye kuwahi kumaliza mimi sikuwa wa Kwanza
hasa ukizingatia kunamuda kama wa nusu saa mimi
na baadhi ya wanafunzi tuliupoteza mara baada ya
kumsaidia yule msimamizi hivyo nilijikuta namaliza
wa mwishomwisho. Na mara baada ya kumaliza
mtihani niliukusanya mtihani na kutoka nje.
Nilivyotoka nje tu nikasikia ule wimbo ukiimbwa
nikajua moja kwa moja atakuwa ni Janet. Ikabidi ni
pite tu kwa washkaji bila kuwauliza chochote
kuhusu mtihani au kujadili jambo lolote kwani
nilikuwa na hamu kubwa ya kumuuliza Janet
maswali mengi kuhusu mimi mwenyewe binafsi
nimekuwaje tena. Nilitoka harakaharaka ingawa
nilikuwa mbali Ila nikasikia washkaji wakisema.
"Atakuwa anaenda kufata mtihani wa Chemistry
yule". "Na alivyomchoyo yule anaweza akauficha
mtihani wa Chemistry tusiuone". Mimi sikuwajali
nilikuwa naenda kwa kasi kwa Janet ili kumuuliza
maswali mengi kuhusu huu ujini walionipandikiza.
Sikumkuta Janet kwenye mti nikapitiliza moja kwa
moja kwenye msitu kwani sauti ilikuwa inatokea
huo. Nilimkuta Janet akiwa amekaa msituni peke
yake tena akiwa juu ya kitanda cha mbao,Sikujiuliza
amekitoa wapi au kimefikaje pale kwasababu
niliamini kwa uwezo wa majini lile ni jambo dogo
mno. "Janet nimekuja nataka nikuulize" Kabla
sijauliza nilichotaka kuuliza Janet alijibu."Nadhani
unauliza kuhusu mabadiliko yako uliyokuwa nayo
sasa, Usihofu wewe bado ni mwanadamu ila hayo
mabadiliko unayoyaona ni ishara ndoa yetu
imekubalika mbinguni na ndo maana umeniona
nimekuja na hiki kitanda hapa". "Kitanda tena cha
kufanya nini?". "Cha kufanya kile ambacho mke na
mume hukifanya wanapokuwa chumbani,Tena hilo
tendo yapaswa lifanyike ni kiwa na umbo langu
halisi la kijini na si umbo la kibinadamu". Palepale
uso wa Janet ulianza kubadilika na kuota manyoya,
makucha yakamtoka na Meno yakarefuka.Macho
yake yakawa ni macho ya kusimama si kulala tena
kama binadamu na masikio yake yakawa marefu.
Wakati huo yale yakiendelea msituni kumbe John
alipata wazo kuwa baada ya mimi kupata mtihani
wa Chemistry ningeuficha kutokana na tabia yangu
ya uchoyo hivyo aliamua kunifatilia wapi naenda
kuchukua huo mtihani ili nikiuficha auone
...
#18
WIMBO WA AJABU 18. Palepale Janet akaanza
kubadilika meno na kucha zake zilivyokuwa ndefu
zilitosha kunitisha nikajikuta namuogopa ghafla na
kutaka kukimbia lakini Janet alijitokeza kwa mbele
na kurudi katika umbo la kawaida. "Vipi mpenzi
mbona unakimbia". Janet aliniuliza kwa upole na
sikuwa jibu la kumjibu zaidi ya kuzidi kumuogopa
na nikatafuta nafasi niweze kukimbia lakini sikuweza
kunyanyua mguu wangu pale ulipo kupiga hatua
yeyote. "Huwezi kwenda sehemu yeyote bila mimi
na wewe kufanya tendo la ndoa kwani mimi na
wewe ni wanandoa sasa inabidi tuthibitishe kwa
kufanya tendo la ndoa" Janet aliongea kwa upole
sana na ufasahaa mwingi. "Nikikataa je" Nilimuuliza.
Janet akacheka. "Aahaa huwezi kukataa" "Siwezi
kukataa wakati ndo nimekataa". "Sitakuruhusu
ukatae bora nikuuwe ili niwe shetani kabisa kuliko
kukuruhusu ukatae,Utakapokataa nami nikakuruhusu
uende wewe na mimi tutakuwa robo jini na tukiwa
robo jini tutaishi ujinini kwa manyanyaso na mateso
nami sitakubali hilo ukikataa hapahapa nakuuwa ili
niwe shetani kabisa kuliko kuwa robo jini". Palepale
nikafikiria mara mbili hivi ni kweli nifanye mapenzi
na jini kisa kuogopa ataniua ,nikaona bora nife tu
kuliko kuruhusu kufanya mapenzi na jini tena akiwa
katika hali ile ya kutisha. Pamoja nilikuwa
nampango wakuja kuchukua mtihani wa chemistry
Ila nikaona acha nisamehe kila kitu basi nikapiga
hatua ili niweze kuondoka na moyo wangu ukiwa
unaruhusu kabisa kuuliwa na Janet. Hapo
nikamuona Janet atumii ubabe tena bali yupo kama
mtu aliyechanganyikiwa hivi ,Machozi ya kutoka
yalimtoka machoni huku akinizuia nisiondoke kwa
mikono miwili. "Tafadhari Musa usinifanyie hivi hujui
ni kiasi gani nimehangaika mpaka kukupata
wewe"Sikujali kilio chake bali nilikuwa nimechukia
kwasababu alinigeuza kuwa thumuni jini bila
kunishirikisha. "Musa Sikukushirikisha kwasababu
siku ile mama yangu alikasirika sana alipoona
mtihani umevuja hivyo alitaka kukuuwa ndipo
nikamwambia kuwa umekubali kunioa hivyo uwe
thumuni jini hivyo nimesaidia maisha yako" Alijibu
mawazo yangu ya kichwani nami sikushtuka
kwasababu nilishamzoea mambo yake ya kusoma
mawazo yangu ,pia sikuujali utetezi wake kwani
bado sikuwa tayari kufanya naye mapenzi hakiwa
katika hali kama ile hali ya mnyama si mnyama
mdudu si mdudu ni hali mbaya ya kutisha hivyo ni
bora nife tu kuliko kufanya mapenzi na kiumbe cha
ajabu kama kile. "Musa tafadhari nisikilize unajua
mi nakupenda sana nahofia nitashindwa kukuuwa
hivyo tutakuwa robo jini wote na tutateseka mno"
Janet alisema hayo lakini bado niliendelea
kumpuuza kwani sikutaka kabisa kusikia utetezi
wake lakin ghafla tukasikia mchakacho wa majani
wote tukageuka kujua mchakacho unatokea wapi
,Kumbe alikuwa ni John alipoona tumemkaribia
akataka kukimbia lakini akatereza kwenye majani
hali iliyotustua mimi na Janet. Janet alikimbia kwa
Kasi kama kimbunga akasimama mbele ya John
nami nikageuka nakuishangaa ile kasi ya Janet
maana ni kitendo cha sekunde tu yupo mbele ya
John. "Haya niambie mwanadamu umeona nini"
Janet alisema hayo kwa hasira huku ngozi yake
ikianza kubadilika na kuota manyoya,Makucha
yakamtoka na kuanza kumsogelea John. John
aliogopa sana akajikuta anarudi nyuma kwa hofu
kubwa huku akitetemeka.
"Sijaona kitu"John alijibu kwa woga mkubwa .Janet
akacheka. "Aaahaa,Wanadamu ni waongo sana
wewe John" John akashtuka kusikia anaitwa jina na
Janet. "Eehee". "Leo ndo siku yako ya kufa kwani
siwezi kukuruhusu uwende ukatoe siri zangu".
"Sitasema chochote tafadhari naomba unisamehee".
"Binadamu si mtu wa kumuamini hivyo inapaswa
niondoke na roho yako ili niwe na uhakika kuwa siri
yangu itakuwa iko salama" Baada ya kusema hayo
Janet alimrukia John
#19
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA 19. Janet
akamrukia John nami nikapata hofu moja kubwa
kama Janet atamuua John huwenda kesi itakuwa
upande wangu licha ya kuwa kesi inaweza kuwa
upande wangu pia John ni rafiki yangu nisingependa
afe huku nikishuhudia kwa macho yangu mawili
basi wakati nawaza hayo huku nikitamani kumsaidia
John nikajikuta ghafla nimeruka mpaka sehemu
alipo John na Janet . Sijajua niliwezaje kuruka kwa
kasi namna ile mpaka kulifikia lile eneo kabla Janet
hajamshambulia John. Nilipofika eneo lile nikajikuta
najua ghafla kuwa namna ya kumtuliza Janet ni
kufanya naye mapenzi la sivyo atamuua
John.Sikuelewa nilijulia wapi hilo jambo lakini
nilijihisi ni kuwa nalielewa hilo jambo siku nyingi tu
huwenda ikawa ni zaidi ya miaka miwili au mitatu
hivi kumbe hilo jambo nililijulia hapohapo. Basi
nikampa Janet mate na nikamuona ameachana tena
na John na kunigeukia mimi tukabingilita mpaka
chini huku Janet akinitoa nguo zangu wa haraka
mno kitendo ambacho sikukihisi kabisa kama
nilivuajevuaje nguo. Janet alikuwa na umbo la
kutisha sana lakini nilijikaza kuwa naye kwa kuhofia
John asije akauwawa. Wakati nafanya mapenzi na
Janet nilijishangaa nami naanza kugeuka kiumbe
cha ajabu manyoya na makucha yaliniota ghafla.
Wakati huo John alikuwa haamini anachokiona
maana mwanzo alijikuta akitweta kama mtu
aliyekimbia umbali mrefu hiyo ni kutokana na
kuogopa kifo.Akajikuta anashindwa kuondoka eneo
la tukio kwasababu ni kama akili yake iliduwaa
kidogo. Na akaja akapata mshangao mkubwa
alivyoniona na mimi nabadilika na kuwa umbo la
ajabu. John alishindwa kuvumilia kukaa pale ilibidi
akimbie na kuniacha mimi na Janet tukiwa
tumezama katika bahari nzito ya mapenzi. Baada ya
nusu saa tulimaliza mambo yetu ndipo maumbo
yetu ya kibinadamu halisia yalipo rejea nikajikuta
napata hofu kubwa maana John aliniona
nilivyobadilika kama mnyama na amekimbia hivyo
anaweza watu kuwaelezea yaliyotokea huku porini.
Janet yeye alifurahi sana "Aaahaa umenifurahisha
sana" Nikajikuta nimejua bila kujulishwa kuwa
baada ya kufanya mapenzi na Janet kunabaadhi ya
vitu vimepungua katika ujini wa Janet nami kuna vitu
vimeongezeka kwenye ujini wangu hivyo
ameshindwa kuyasoma mawazo yangu.Maana
nilikuwa nawaza kuhusu kutoroka kwa John lakini
yeye alikuwa na furaha na mada yake sio John tena.
"Sasa ndoa yetu imetimia" Janet aliongea hayo
kisha akanipa mtihani wa Chemistry na majibu
yake. Niliupitia haraka haraka nikajikuta nimeuelewa
haraka Ila bado nikataka niuchukue niondoke nao
lakini Janet akanikataza kwa kuniambia. "Kwa sasa
unauwezo mkubwa wa kushika vitu uchane tu huu
mtihani wasikusumbue". Basi niliuchana ule mtihani
kisha kuondoka. ******************************
**************John alirudi bwenini akiwa ni mtu
mwenye hofu tele akawa anatetemeka muda wote
kwa woga.Watu walitamani kimuuliza nini
kimetokea kuhusu yeye kunifatilia mimi lakini
hakuonekana ni mtu mwenye kujitambua sawasawa
kwani muda wote alikuwa akitetemeka huku
akishtukashtuka. Mara nami nikarejea bwenini huku
nikiwa bado nahofu kubwa kuwa kama John
ataimwaga siri yangu itakuwaje mimi si nitakuwa
uchi kuwa ni mnyama na sio binadamu wa kawaida
niliwaza hivyo ila nikapuuza na kurejea bwenini
ambapo nilipofika tu watu walianza kunigombania
kunidai mtihani. Watu waliambizana shule nzima
kuwa Musa amerejea kutoka huko anapochukuaga
pepa hivyo waje kuchukua pepa na kusolve. Taarifa
za kurejea kwangu zilimfikia kila mtu mpaka John
ambaye tangu amerudi aliamua kuingia bwenini
kwao na kujifunika mashuka huku anatetemeka.
John alivyopata habari hizo kuwa mimi nimerejea
aliogopa sana lakini akajikuta anajiuliza maswali
yaliyompa ujasiri wa kuinuka kitandani ili kuwazuia
watu wasije wakanigusa. "Musa ni jini yule
,Tunavyoendelea kumgasi anaweza akatuua wote,
Washkaji wengi hawajui kuwa Musa ni jini hivyo
watamgasi Musa acha nikawazuie ikiwezekana
niwaambie ukweli kuhusu Musa" Baada ya mawazo
hayo John alijikokota huku anatetemeka mpaka
bwenini kwangu ambapo nilishazingirwa na watu
wote wanataka mtihani...
#20
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA 20 John alijikokota
mpaka bwenini kwangu ambapo alinikuta nikiwa
nimezingirwa na washkaji wanataka mtihani kwa
nguvu.Wakati washkaji wakinipekuwa mtihani huku
na huku mara ghafla tukasikia sauti ya John sauti
ambayo iliwashtua wote. "Jamani naombeni
mnisikilize kuhusu Musa ana siri kubwa nataka
niwaambie msije mka...." Watu wote waligeuka
nyuma ili kumsikiliza John nami niligeuka ili
kumsikiliza lakini nilikuwa na hofu sana kuwa huyu
jamaa anaweza kusema mimi nilifanya mapenzi na
kiumbe cha ajabu nikajikuta ghafla najutia kuhusu
John bora ningemuacha tu afe kule polini .Lakini
kabla hajamaliza kusema sentensi yake ghafla
akanyamaza akawa anayatafuta maneno ya kuongea
lakini hayapati yahaani ni kama mtu aliyekumbwa
na ububu wa ghafla. Watu wote walimshangaa John
maana nikama mtu aliyetaka kuongea lakini ghafla
amenyamaza na kuanza kutoa ishara ya kidole huku
akiongea kibububu kisha akaanguka chini. Watu
wote walimkimbilia kumuangalia nini kimemkuta
kasoro mimi nilikuwa naangalia kile kidole alikuwa
amenyooshewa nani? Kumbe alikuwa ni Janet
alikuwa ndo anaondoka akaniangalia akatabasamu
alafu akacheka. Nilipata hofu kubwa sana huku
nikiogopa isije ikawa Janet amekuja kumuua John
ikabidi nami nielekee eneo alipo John lakini
nikashangaa Nashon ananisukumiza kwa nguvu.
"Toka mchawi mkubwa "Nashon alinisukuma kwa
hasira na nguvu nyingi nikaanguka chini. "Nashon
vipi umechanganyikiwa?" Niliuliza kwa mshangao na
watu walikuwa hawanijali tena wakambeba John na
kumpeleka hospitali huku mi nikifata nyuma kwa
nyuma lakini njia nzima walikuwa wakiniongelea
mimi. "John alimfatilia Musa polini sijui alikutana
na nini huko akarudi anatetemeka,Na bado akaamua
aje kutueleza yaliyojiri huko ndo yamemkuta ya
kumkuta mimi nikiunganisha matukio haya mawili
napata picha kuwa kuna nguvu za giza hapa".
Alisema mshkaji mmoja alafu Nashon akadakia
"Ndo maana mimi nimesema Musa ni mchawi" Basi
kutokana na yale mazungumzo mimi nikaachana na
ule msafara na kurudi bwenini Ila Janet alinihudhi
sana siku hiyo maana nilihisi kabisa amenitafutia
matatizo mazito. ******************************
********** John alichukuliwa na kupelekwa kwenye
hospitali iliyopo karibu daktari alielezewa hilo tatizo
jinsi lilovyompata alafu akachukua vipimo vyake ili
kujiridhisha mgonjwa anaumwa nini baada ya
majibu Daktari alipigilia msumali kwenye point ya
Nashon. "Kwa maelezo yenu mliyonipa nilitarajia
itakuwa ni presha ya kushuka lakini nimempima
presha inaonekana hiko normal hii imenitisha mimi
kama Daktari mtu awe katika hali hii alafu presha
yake iwe normal hilo ni jambo la kushangaza mno
kwa upande wangu.Kutokana na taaluma za
kidaktari napaswa niwape transfer muende hospital
ya mkoa lakini mimi natoa ushauri binafsi nikiwa
kama binadamu wa kawaida na sio Daktari" Daktari
alisita kidogo alafu akasema. "Huu ushauri
hauhusiani na udaktari mjue msije mkasema docta
Clifton ametushauri hichi na hichi Bali mnapaswa
kusema kuwa mlikutana na mwananchi wa kawaida
anaitwa Clifton akatushauri hichi kitu". "Daktari
tuambie" Alisema Mwalimu Ana ambaye ndiye
aliongozana na baadhi ya wanafunzi kumpeleka
John hospitali. "Jaribuni na mambo ya Kiswahili
kidogo msije mkampoteza huyu mtoto". "Mmmh
"Mwalimu Ana aliguna maana hakutarajia kuwa
Daktari anaweza kuwashauri kitu kama kile Ila
Nashon akadakia. "Kweli mwalimu,John amerogwa
kwani kuna kitu muhimu alitaka azungumze lakini
ghafla akajikuta anashindwa kuzungumza kwani
kuna kitu kimemkumba na alionyesha ishara ya
kidole kabisa kuhusu hicho kitu". Mwalimu
alisikiliza kwa umakini akasema. "Sawa Ila
inapaswa kuwashilikisha wazazi wake kwanza
maana mimi sina pesa muda huu". "Usijali hapa
karibu na hospital kuna mganga anatibu bure
malipo ukishapona" Docta alijazilizia point yake ili
kutia urahisi katika utekelezaji wa swala hilo. "Sawa
Ila inabidi tuwashilikishe wazazi wake tusije
tukajichukulia tu Sheria ya kumpeleka mtoto wao
kwa mganga bila idhini Yao". Basi mwalimu Ana
alipiga simu kwa wazazi wa John na wakatoa
ruhusa afanye awezavyo mwanao apone nao kesho
wanakuja shule. Basi safari ya kwenda kwa mganga
ikaanza kutokea pale hospitali huku Nashon
akijisemea kimoyomoyo. "Napenda mganga awe wa
ukweli ili amuumbue Musa kwa uchawi wake"
JE MUSA ATAUMBUKA ? ****
 
(21-----22)
MWISHO...
#21
WIMBO WA AJABU SEHEMU 21. Basi wakaenda
kwa mganga wa karibu na ile hospitali ,Mganga
anaitwa Zemweni kilingoni ni maarufu sana hapo
Tabora licha ya kuwa sisi tulikuwa hatumfahamu
lakini kwa watu wanaoamini mambo ya waganga
huyu ni Mganga kiboko. "Tatizo lipo shuleni
kwenu,Itabidi turudi shuleni kwenu tukaliondoe
tatizo" Mganga alitoa maoni ambapo hakuna
aliyempinga zaidi ya kufata maelekezo kila kitu.
Walifika shuleni wakiwa na Mganga mimi
nilipowaona tu nikashtuka nikijua wazi kuwa
nimeumbuka. Sikutaka kukaa mahali alipo Mganga
nikaamua kujufungia ndani ambapo wanafunzi
karibia wote na walimu walibaki kumzingira Mganga
ili wajionee miujiza. Mganga alianza mambo yake
ya manyanga nami nikaanza kuona kama navutwa
upande wa yale manyanga bila kupenda na kila
nikijitahidi kujizuia Siwezi.Nilikuwa nimekaa bwenini
kitandani Ila nikajikuta naenda mlangoni ili
kuufungua mlango nitoke lakini ghafla akaja Janet
na mama yake wakanizuia nisitoke. "Inabidi tumtoe
uthumuni jini huyu laa sivyo atavutwa huyu".
"Hapana mama tumzuie tu" Janet alisema kwa
majonzi kidogo. "Hatuwezi kumzuia muda huu ukoo
wa makata utafika hapa ili kutulazimisha wote
twende kwenye kilinge cha Mganga ili kumponyesha
John na huyu ataitwa pia akiwa anaonekana kwa
wenzake japo sisi hatutaonekana, huyu atatakiwa
awape maelezo na hapo atakutaja utadhurika na
kufa" Mama yake Janet alimwambia Janet madhara
yapi yatajitokeza iwapo mimi sitarudishwa kwenye
ubinadamu was kawaida. Basi Janet huku akilia
akanipiga na utambi fulani ambao ni kama wa
kiganga nikajukuta mwili wangu unagawanyika mara
mbili.Mwili mmoja ulibaki umelala fofofo na mwili
mmoja ukiwa macho basi wakanishika mkono kisha
tukakimbia kwa kasi ya ajabu ,yahaani ni kitendo
kama cha sekunde mbili niliona tunatoka Tabora
kwa haraka na kuvuka mikoa kadhaa mpaka Dar es
salaam hao tukaingia kwenye bahari. "Dah afadhari
tumefika nyumbani Salama kabla kina makata
hawajafika" Mama Janet alishukuru. Ila dakika mbili
nyingi niliona majini saba ambao wapo kama
binadamu lakini wana vichwa vya ng'ombe. Sisi
tulipoingia kwenye himaya ya subiani kila mtu
alikuwa anaendelea na mambo yake lakini ghafla
walipokuja hao mabwana saba kila mtu aliacha
shughuli zake na kusogea eneo la tukio. "Nyinyi
makata mmefata nini hapa" Aliuliza mwanaume
mmoja mwenye kifua kipana kutoka ukoo wa
subiani. "Sisi tumemfata huyu nusu jini na binadamu
,hatujaja kwa Shari". "Hawa hawawezi kutoka"
Mama Janet aliongea kwa kupaniki kidogo huku
akijiweka tayari kwa mapambano. "We mwanamke
Mzee ,Sisi hatukuja kwa mapambano ebu tuitieni
kwanza kiongozi wenu hapa maana tukiamua
kumchukua kwa nguvu tunaweza ila tumeamua
tutumie busara tu". "We nenda kamuite sultan"
Mwanaume mmoja mwenye miraba mnne kutoka
subiani alimtuma kijana mmoja wa kijini naye
akapotea kabla hata yule mwanaume hajamaliza
sentensi yake na kabla hata hatujapepesa macho
alikuja mwanaume mmoja mfupi na Mzee akiwa
amevaa mavazi ya kifalme. Nguo zake zilikuwa ni
majoho ya halili na kichwa chake kilipambwa na
kofia ya kifalme ambayo imetapakaa dhahabu.Yule
mtu alibebwa na wanaume sita ambao nikama
mabaunsa hivi au wanaume wenye miraba minne
walikuwa wako vifua wazi huku kila mmoja akiwa
amebeba jambia. Wale wanaume walivyofika pale
wakamshusha yule mtu niliyemdhania kuwa ni
sultan na majini yote yakainama kumuheshimu
Sultan pamoja na mimi niliinama maana Janet
alinishika kichwa changu na kunipa ishara ya
kuinama kama heshima kwa kiongozi wao lakini
wale kina makata. "Nyinyi viburi kwanini
hamkuinama mnatamani mbakize shingo zenu
kwenye ardhi ya subiani". "Sio kiongozi wetu Lakini".
"Hata kama sio kiongozi wenu hapa mmekuja
kwenye ardhi ya subiani msipoinamisha vichwa
vyenu chini tutawachinja mara moja"
#22
WIMBO WA AJABU SEHEMU YA 22. Basi wale
makata wakainamisha vichwa vyao chini kama
ishara ya kumtukuza kiongozi. "Eehee,niambieni
mnashida gani makata" Sultan aliuliza. "Shida yetu
ni kuja kumchukua huyu nusu jini pamoja na
binaadamu kuna uhalifu wamefanya". Makata mmoja
akajibu.Mara nikasikia minong'ono kutoka kwa
majini wengine wa subihani. "Mmh hawa makata
hujipendekeza sana kwa wanadamu". "Sisi
hatujipendekezi bali tunawazuia majini waarifu
wasifanye uharifu kwa wanadamu kwa hiyo mtukufu
Sultan tupe huyu nusu jini na binaadamu tuondoke
naye" Sultan alimgeukia mama Janet na kumuuliza.
"Huyu mwanao ameshafunga ndoa na huyu
mwanadamu kwani?". "Ndio mkuu". "Mi
siniliwakataza msifunge ndoa na wanadamu sasa
imekuwaje tena mnaweza mkatuletea matatizo
hapa". "Ye mwenyewe alisisitiza sana Sultan
nikashindwa kumzuia kwani lengo lake lilikuwa awe
binaadamu". Sultan akabaki anasikitika tu kisha
kusema. "Mnajua kabisa hilo haliwezekani zaidi
zaidi atakuwa shetani wa kutisha,na akiwa shetani
wa kutisha nani unafikiri wakumdhibiti hapo".
"Samahani mkuu" Mama Janet aliomba msamaha
huku mimi na Janet tukiwa hatuna la kuchangia.
"Basi nendeni mkaivunje hiyo ndoa alafu mje hapa".
Sultan alitoa agizo. "Lakini tutakosa ushaidi" Makata
walisema kwa mshangao. "Shida yenu si yule kijana
apone au mnashida ya ushahidi". Makata waliona
kitendo cha kuvunja ndoa maana yake watakosa
ushahidi wa kunipeleka kwa yule mganga hivyo
walitamani ndoa isivunjwe. "Kijana apone". "Basi
hakuna kutulazimisha jambo ambalo subihani wote
hatutakubaliana nalo,kwani hamjui sababu ya vita ya
mwaka jana Kati ya Subihani na makata?". Sultan
aliwauliza makata ambao ilibidi wakae kimya maana
mwaka jana katika kulazimisha ushahidi jini mmoja
wa kisubihani akageuka kuwa Shetani wa kutisha
ambaye aliwasumbua sana wakazi wa Subihani kwa
kula watoto wao lakini baadaye wakafanikiwa
kumuua hivyo ikabidi waingie vitani na makata
lakini mwisho wa siku wakakaa kwenye meza moja
ya mazungumzo na kuambizana hakuna kulazimisha
ushahidi eti kwa kutafuta sifa kwa wanadamu. Mimi
na Janet tulichukuliwa na mama yake Janet mpaka
kwenye vilindi vya mbali kabisa vya maji,mimi
nikakumbuka vilindi hivyo ndipo ndoa yetu
ilipofungwa. Basi tulifika hapo na kukalishwa chini
kisha mama yake Janet akachukua kisu na kusema
baadhi ya maneno fulani kisha kunitoboa kwenye
kiganja cha mkono alafu akakinga damu ,Ilikuwa
inatoka damu ya blue kumbe yale maneno yalikuwa
kwaajili ya kuvuta damu ya kijini inayotembea
mwilini mwangu. Baada ya kutolewa damu ile
nilijikuta naanguka chini na kupoteza fahamu mpaka
nikaja kuzinduka nikiwa bwenini sikuelewa tena
kama Janet naye alitolewa damu au laa pia sikujua
tena wale makata ilikuwaje tena Ila nilivyoamka
nilishtuliwa na Nashon akiniomba msamaha kwa
kuniita mchawi na akasema kuwa John alizimia
Jana kwa kuona kiumbe cha ajabu ambacho
kimedhibitiwa na mganga kisifike shuleni tena.
Nilikubali msamahaa wake Ila maneno Yale ya
Nashon yalinipa wasiwasi kuwa Janet atakuwa
amedhibitiwa na mganga. ***************
************************** Basi baada ya hapo pepa
ziliendelea kama kawaida ni pepa ya chemistry tu
ndo ilikuwa feki yangu ya mwisho niliyopewa na
Janet mitihani mingine yote nilifanya kwaakili yangu
kwani Janet hakuweza tena kutokea licha ya mimi
kwenda kukaa mbuyuni walau kumgonja lakini wapi.
Baada ya mitihani kuisha ilibidi kuondoka pale
shuleni ndipo nikakutana na kiboksi cha zawadi
nilifungua nikakuta donge nono la Alamasi likiwa
linakaratasi ya ujumbe mfupi. "Dear mpenzi Musa
hiyo ndo zawadi yangu ya mwisho kwako wale
makata wamenidhibiti kwasasa sina uwezo
wakumfikia mwanadamu yeyote wako kipenzi
Janet". MWISHO
 
Shukrani Sana mkuu kwa burudani hii murua kabisa.
Kazi nzuri sana
 
Back
Top Bottom