Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
WANAWAKE NI WAUAJI
Mtunzi/mwandishi HUSSEIN BAKARI
MTOTO WA BECKER
mtotowabecker@gmail.com
0713 46 26 29
_________________
EPS 01
========
********
“Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa pumzi na afya njema hadi leo hii niko hai japo niko tofauti sana na nilivyokuwa awali hata wasionijua wakiniona hii leo watadhani nilizaliwa hivi. La hasha! Ila leo nitawaambia ukweli wa yote yaliyonisibu na yanayowasibu wanaume wengi katika dunia hii ya leo. Nakumbuka zamani babu aliwahi kuniambia niwe makini sana na wanawake pindi nitapokuwa mkubwa.
Na alinisihi ya kwamba niwaelewe wanawake ni watu wa aina gani na jinsi ya kuishi nao. Lakini sikuwahi kuamini maneno yake hadi yalipokuja kunisibu na ndipo nilipokumbuka na kuelewa kwanini babu alinisihi vile. Aaaaagh! Wanawake ni mama zetu na ni pambo la dunia na ndio maana Mungu aliwaumba ili watufariji na watulee, lakini ukweli bado unabaki kuwa wanawake ni watu hatari sana kwetu wanaume.
Hebu tukumbuke hata kwenye hadithi za watu wa kale kwenye vitabu vya dini tukianzia mwanzo kabisa wa dunia enzi za Adam na Hawa/Eva. Adam alitii kila kitu katika mamlaka aliyopewa na Mungu lakini mwishowe alikuja kumkosea Mungu kwa kutenda dhambi aliyoponzwa na mkewe (Hawa/Eve) mara baada ya kushawishiwa na Shetani, Eeeh, amini usiamini shetani ni vigumu sana kumuingia mwanaume hivyo anamtumia mwanamke kama alivyomtumia Hawa/Eve kwenda kumlubuni mwanaume kama alivyolubuniwa Adam na kujikuta mwanaume anaumia kwaajili ya upendo na kumuamini sana mwanamke pasi na kuelewa kiundani udhaifu mkubwa wa mwanake mwenyewe.
Tuachane na Adam, tukumbuke Samson mtu mwenye nguvu aliyewapa tabu sana Wafiristi enzi hizo lakini mwishoe anakuja kukamatwa na kupata mateso makali baada ya kulubuniwa na Delila aliyetumiwa na Wafirist kubaini siri za nguvu za Samsoni. Eee, Samsoni nae aliponzwa kwa ajili ya mwanamke, na si yeye wala Adam tu tukumbuke hata mtu wa kwanza kufa alikuwa ni mwanaume na sababu ya kifo chake kilitokana na mwanamke!!
Eeeh ni wanaume wengi mno wameponzeka kwaajili ya wanawake na mmoja wao ni mimi na ndio maana leo hii nasema wanawake ni wauaji. Najua wengi mtanielewa vibaya hususani wanawake, lakini naomba msizime tv zenu ama radio ili mnielewe vizuri kwanini hasa nimekazania kusema Wanawake ni Wauaji? Hii ni asili iliyoanza toka kwa mwanamke wa kwanza kabisa kuumbwa na bado ipo na itakuwepo na itawaumiza wanaume wengi sana wasiokuwa makini na ndio maana hata Mungu hakuwahi kushusha nabii wa kike.
Wanawake ni wadhaifu wasiokubali udhaifu wao na ndio maana nawaita Wauaji. Achilia mbali vitabu vya dini tukija kwenye maisha yetu ya kila siku lini ulishawahi kusikia mwanaume katupa katoto kachanga? Naamini kama mimba wangekuwa wanabeba wanaume usingesikia neno kutoa mimba.
Hivi ushawahi kujiuliza mwanamke ana moyo wa namna gani hadi anadiliki kukiua kiumbe alichokibeba tumboni miezi tisa na kujifungua kwa uchungu?!! au unadanganywa na maumbile yake na sauti laini unajisahau na unaacha kuwa makini nae? hivi hujui kwamba simba dume ana muungurumo mkubwa sana lakini jike ndiye jasiri wa kuua. Huo ni mfano tu lakini nataka unielewe na uwe makini kwanini nasema WANAWAKE NI WAUAJI..”
Ilikuwa ni sauti ya bwana mmoja mlemavu wa macho na miguu akiongea luningani katika kipindi cha YA WALIMWENGU LIVE kilichokuwa kinarushwa kupitia kituo cha BECKER TV kila siku za jumapili asubuhi na marudio yake ilikuwa jumamosi jioni.
Nilikaa kwenye sofa kwa hamasiko. Macho na masikio niliyatupa luningani huku mkono mmoja nikiwa na kikombe chenye chai na mwengine ukiwa na rimoti nikiongeza sauti ya luninga. Mada ya yule bwana ilinistua na kunigusa sana hali iliyochochea niwe na shauku kubwa ya kumsikiliza ili nimuelewe vizuri kwanini anasema wanawake ni wauaji.
Nilitulia na kujikuta nashindwa hata kupiga funda moja la chai na kubaki nimekishikilia kikombe kwa kumakinika na yule bwana alipokuwa anazungumza ambapo aliendelea kwa kusema......
“Nakumbuka miaka kumi iliyopita nilikuwa na maisha mazuri kabisa ya furaha, mimi na mke wangu kipenzi baada ya kufunga ndoa. Kiukweli nilimpenda sana mke wangu nae alinionesha mapenzi hasa na kunisahaulisha maumivu niliyopata kutoka kwa mke wangu wa kwanza tuliyeachana muda mfupi tu baada ya kukaa kwenye ndoa kwa miaka mitatu na kuanza visa vilivyosababisha nimuache aishi maisha aliyotaka yeye na ndipo baada ya miezi kadhaa nilipompata huyu mwanamke wangu mwengine aliyeonesha kuwa na vigezo vyote nilivyohitaji na mwaka mmoja tu katika mahusiano yetu tuliamua kufunga ndoa kabisa.
Kiukweli mke wangu nilijivunia uzuri aliokuwa nao upole wake na tabia ya kupenda ibada. Na mara nyingi alinibadilisha kwa maneno matamu na kunisihi niache kunywa pombe, na kweli ilifika kipindi niliacha pombe na taratiibu nilipunguza kabisa kuvuta sigara kutoka pakiti moja kwa siku hadi ikafika mahali siku nzima nikavuta sigara mbili tu, hali iliyofanya hadi walionijua kunishangaa na kumsifu sana mke wangu na ndipo nami nilizidisha moyo wa kumpenda na kumpa uhuru wa kila kitu kwani nilimuamini mno…!” Alinyamaza kisha aliendelea…….
“Kila nilichofanya nilihakikisha lazima mke wangu ajue na nilisikiliza sana na kufata ushauri wake kuliko mtu mwengine. Akisema nisifanye kitu fulani nami nilitii, akisema nifanye nami nilitii, hiyo yote nilifanya nikiamini namjenga na kumuonesha kiasi gani namthimini bila kujua kua kuna ugonjwa m baya nilikuwa naufuga.
Awali sikuona tofauti yoyote wala kuhisi kama kuna kitu nakosea zaidi nilianza kusikia minong’ono kutoka kwa majilani na baadhi ya ndugu zangu kuwa napelekeshwa na nimetawaliwa na mke wangu. Kiukweli nilichukizwa na habari zile na kugombana na baadhi ya ndugu zangu waliomsema vibaya mke wangu nikiamini fika wanataka watugombanishe na wananionea wivu kwa kupata mke wa namna ile kwani maisha yetu yalizidi kunyooka siku hadi siku.
Aaaaaagh.. kuna muda huwa nahisi kama ndoto vilee kwani sikujua kabisa kumbe kuna bomu nalitengeneza mwenyewe ambapo baadae litapolipuka litaniletea madhara makubwa na kama si kuniua basi litanipa ulemavu wa kudumu kama ilivyotokea baadae…. Aaaagh, mke wangu!!!...”
Alivyozidi kuongea ndivyo nami nilivyozidi kutulia kumsikiliza kwa umakini huku nikibofya bofya rimoti kuongeza sauti mara kwa mara utafikiri nilikuwa na ubovu wa masikio. Nilimuangalia kwa jicho la shauku ya kujua yaliyomsibu. Uso wake wa jitimai ulitia huruma ukichochewa na ulemavu uliobeba tafsiri ya mazito yaliyomsibu. Kiu ya kujua ilikuwaje ilizidi kuniparua milango yangu ya fahamu. Lakini kabla sijafaidi vizuri hadithi ya yule bwana mara umeme ulikatika na kila kitu kuzimika.
“Aaaagh, Tanesco bwana kama maboya!!!”
Nilinyanyuka kwa hasira kuzima kitufe cha luninga na kuwasha kile cha taa ili umeme utaporudi tu, taa inijulishe mapema.
Wakati huo ile chai kikombeni ilikuwa ya baridi kabisa na sikuambulia kunywa hata chembe. Nilienda imwaga na kurudisha kikombe kabatini na ndipo nilipoikumbuka simu yangu niliyoiacha chumbani kwenye chaji. Haraka niliiendea na kukuta ikiwa na ‘missed calls’ tisa ‘sms’ nne. Nilipofungua zote zilitoka kwa mtu mmoja. Mtu ambae alikuwa zaidi ya uwaridi moyoni mwangu. Mwanamke wa ndoto zangu ambaye tulikuwa na miadi ya kukutana wikiendi hiyo ili tufurahi pamoja. Huyo alikuwa MARIAM ama MAMU kama nilivyopenda kumwita.
Nilizisoma zile ‘sms’ ambapo mojawapo iliandikwa hivi…
MBONA HUPOKEI SIMU WALA HUJIBU MSG ZANGU? KAMA UPO NA MALAYA WAKO SI UNAMBIE TU NISIJE..!!
“hahaa Mamu bwana..”
Nilijisemea moyoni na kuingia sehemu ya ujumbe kujibu lakini kabla sijabonyeza kitufe cha kutuma ujumbe, mara mlango wa sebuleni uligongwa kwa rabsha. Nilipouendea kabla sijaufikia, ulifunguliwa na mgongaji aliyeingia akiwa kashiba ununo. Alikuwa ni Mamu kipenzi changu. Nilifurahi nilipomuona nilimkumbatia na kum-busu lakini aliitoa mikono yangu kiunoni mwake na kunisukuma pembeni huku akiingia na kunipita bila kusema chochote na kwenda kukaa sebuleni.
Nilibaini kuwa amekasilishwa kutokana na kutopokea simu yake na nilijua sasa nina wajibu wa kum-bembeleza ili nimuweke sawa. Nilimjua kipenzi changu ni chakudeka, nami kwa huba nilimdekeza.
“Unakunywa nini bebi” nilimuuliza kwa sauti ya mahaba.
“Sitaki kunywa chochote niache.” Alijibu kwa hasira huku akipandisha miguu sofani na kubetua midomo huku uso wake akiuelekezea pembeni.
Hali ile ilizidi kunihakikishia kuwa nina shughuli pevu ya kubembeleza mtu mzima sasa. Lakini kabla sijafanya hivyo mara taa ya sebuleni iliwaka na ndipo nilipokumbuka kuwasha luninga kwanza niendelee na kile kipindi huku moyoni nikiwa na shauku Mamu nae amsikie yule bwana juu ya hadithi yake iliyowatuhumu kuwa wanawake ni wauaji.
Lakini lol! Mada ya yule bwana hasa kauli yake ya kuwa wanawake ni wauaji ilimchukiza zaidi Mamu na kuamua kuzima luninga kwa hasira.
“Aaag! Wee vipi?” nilitahayuri.
“Vipi nini!!?” Alinijibu kwa kuniswalika.
“Si uache tuangalie sasa unazimia nini?!”
“Hivi Hussein kwa akili zako timamu unaona hiki kitu anachokizungumza huyu mpuuzi ni sahihi!!”
“Kitu gani..?”
“Kusema wanawake ni wauaji.!!”
“Mh! hapo kumjaji moja kwa moja itakuwa ngumu, sasa nitamjaji vipi wakati hata hadithi yenyewe sijaisikia!! anaweza kuwa sahihi au si sahihi inategemea na point zake mwenyewe.”
”Hee! hivi nyinyi wanaume mpoje!!!” Aliwaka Mamu kwa sauti ya juu na kusimama huku akinitazama kwa hasira. Alihema juu juu na kuzidisha povu akinguruma kama moto wa kifuu.
“Hivi mnatuchukuliaje sisi wanawake eeh!!?”
“Kivipi baby.. mbona tunawakiana sasa.”
“Sio Nawakaa.. ila nakwambia ukweli acha kuwa na mitazamo ya kijinga au ndio kashakulisha ujinga huyo mpuuzi mwenzio…! Kwa hiyo na mimi muuaji si ndio, au unanionaje!!”
“Hapana baby sijamaanisha hivyo..”
“kumbe unanionaje..!”
“Unaweza kuwa muuaji au si muuaji inategemea tuu.”
“Aahaa.. kwa hiyo hadi mamaako aliyekuzaa muuaji, dada zako wauaji, shangazi zakoo si ndio..!”
“Sasa Mamu hayo matusi..”
“Matusi nini.. si wanawake ni wauaji! We vipi..?! Hebu nipishe huko nisije nikakuua buree..”
Alichukua mkoba wake kishari pale sofani kwa hasira Mamu alielekea mlango wa kutokea ulipo na kutoka huku akiubamiza kwa nguvu.
“Aaagh!! Sasa huo mlango umekukosea nini..!”
Nilibaki nimebumbazika pale kwenye kiti huku nikiwa nimechanganyikiwa kwa jinsi Mamu alivyonibadilikia siku hiyo kuliko siku zote. Hakuwa cha kudedee tena bali alikuwa mbogo. Nilijilaumu kidogo kwa kubishana nae punde alipozima luninga na kumsababishia mpenzi wangu kuwa na hasira mara tatu zaidi alivyoingia. Niliuendea mlango na kuokota funguo zilizodondoka pindi ulipobamizwa kisha nilirudi na kujitupa kwenye sofa huku akili yangu ikiwa imecheza makida.
Niliiwasha tena luninga safari hii nikiwa sina shauku kabisa wa kuangalia kile kipindi ambacho ndio kilikuwa kinaishia lakini kuna maneno ya mwishoni ya yule bwana yalipenya vizuri masikioni mwangu na kukistua kichwa changu kidogo pindi aliposema.
“Najua wanawake wengi wataobahatika kunisikiliza na kunitazama watanichukia na kuona nimewadhalilisha na kuwatusi. Nami sitoshangaa wala kuogopa hilo kwa sababu najua kuwa wanawake tayari wana ulemavu wa asili ambao Mungu aliwaumba nao kwa dhumuni la kuwa wasaidizi na wafariji kwa wanaume tu.
Mwanaume hajaumbwa kwaajili ya mwanamke ila mwanamke aliumbwa kwaajili ya mwanaume na ndio maana tunaambiwa kuwa mwanamke ametoka ubavuni kwa mwanaume. Lakini udhaifu wao ndio unafanya tuone mpaka leo hii wanawake wakitaka kushindana na wanaume wakisahau kuwa mwanaume ni wa kwanza tu kiasili.
Na hii inatokana na kuwa mwanamke ni rafiki mkubwa wa shetani anayetumiwa katika kuiharibu dunia na hata baadhi ya wasomi wa dini kiimani wanatwambia wanawake wengi sana wataingia motoni.
Mungu ameweka mifano mingi sana ya wazi kuwakumbusha wanawake kuwa mwanaume ni kiongozi na anapaswa kunyenyekewa na mwanamke japo kwa akili mbovu za wanawake wengi wanaona kufanya hivyo ni ujinga kwani hata wao wanaweza kufanya wanayofanya wanaume. Ha ha haa yaani hata mifano ya wanyama hawaioni!! Wazee waliosema Wanawake mwalimu wao kipofu walikuwa na maana kubwa sana ambayo sasa imepuuzwa.
Cha mwisho nakukumbusha wewe mwanaume unayenitazama hususani wewe uliegombana na mkeo au mpenzi wako hivi punde chanzo kikiwa hiki kipindi na hii mada yangu. Nataka ujue kwamba uko katika wakati mgumu sana na huyo mwanamke tena nakusihi uwe makini nae sana.
Ukipuuza siku moja yanaweza kukukuta kama yaliyonikuta mimi hata kama hautakuwa na ulemavu wa viungo kama mimi. Kuweni makini sana na wanawake wanaume wenzangu kwani hata mwenyezi Mungu ametwambia tuishi nao kwa akili.”
Nilistuka kwa maneno yale na kuhisi kama naambiwa mimi moja kwa moja. Muda mfupi baada ya kile kipindi kuisha nikiwa nimemezwa mawazoni nikijiuliza mwenyewe nishike yapi niache yapi haswa nikiambatanisha na kauli za Mchumbaangu kipenzi.
Mara ujumbe uliingia kwenye simu yangu na nilipoichukua kuufungua alikuwa ni Mariam.
Ujumbe ulisomeka hivi…
“Hussein nashukuru sana kwa matusi yako ya kuwa eti mimi ni muuaji haina shida ila kama ulikuwa hunitaki na ulikuwa unatafutia sababu ungenambia mapema tuu kuliko kunipoteza muda wangu.. Nashukuru sana, usinitafute nakutakia maisha Mema..”
Sio siri ujumbe wa Mamu ulinishangaza. Sikutaraji kabisa kama kile kipindi kinaweza kusababisha yote yale. Niliisoma mara mbili mbili ile 'sms' na kuamua kumpigia Mamu lakini simu yake iliita bila kupokelewa.
Sikuchoka niliendelea kupiga lakini bado haikupokelewa na mara nyengine ilikatwa na mwishoe nikawa nasikia sauti ya huduma kwa wateja wakinambia kuwa namba ninayopiga inatumika.
Niliachana na simu na kuingia bafuni kuoga niliporejea chumbani nikatupia pamba kama kawaida yangu.
Eeeh.. kupendeza ilikuwa kawaida kwangu kutokana na jinsi nilivyojua kupangilia mavazi hadi watu wengi kitaani wakawa wananita bitozi, si unajua tena uswahilini kila 'chocho' unayokata ukiwa 'umejitupia' sana watu macho kodoo.
Nilirejea sebuleni baada ya kujiridhisha kwa nguo nilizovaa siku hiyo na kabla sijatoka nilipiga tena simu ya Mamu lakini jibu lilikuwa lile lile kwamba namba ninayopiga ipo bize.
Sikuwa na jinsi ilibidi nitoke na kuchukua bodaboda kuelekea kwa kina Mariam nikiwa na nia na madhumuni ya kwenda kuomba msamaha ili mapenzi yetu yaendelee kwani nilimpenda sana na nilijua kama nisingeenda muda huo basi ingebidi nisubiri hadi wiki ijayo kwani nisingepata nafasi kutokana na kuwa kazini muda mwingi.
Baada ya mwendo wa dakika kumi tulifika maeneo ya kina Mam na kumlipa ujira wake yule dogo aliyenileta nami moja kwa moja nikaanza kuongoza njia ya kwa kina Mamu huku nikiwazia jinsi ya kuanza.
_________________ITAENDELEA..
Mtunzi/mwandishi HUSSEIN BAKARI
MTOTO WA BECKER
mtotowabecker@gmail.com
0713 46 26 29
_________________
EPS 01
========
********
“Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa pumzi na afya njema hadi leo hii niko hai japo niko tofauti sana na nilivyokuwa awali hata wasionijua wakiniona hii leo watadhani nilizaliwa hivi. La hasha! Ila leo nitawaambia ukweli wa yote yaliyonisibu na yanayowasibu wanaume wengi katika dunia hii ya leo. Nakumbuka zamani babu aliwahi kuniambia niwe makini sana na wanawake pindi nitapokuwa mkubwa.
Na alinisihi ya kwamba niwaelewe wanawake ni watu wa aina gani na jinsi ya kuishi nao. Lakini sikuwahi kuamini maneno yake hadi yalipokuja kunisibu na ndipo nilipokumbuka na kuelewa kwanini babu alinisihi vile. Aaaaagh! Wanawake ni mama zetu na ni pambo la dunia na ndio maana Mungu aliwaumba ili watufariji na watulee, lakini ukweli bado unabaki kuwa wanawake ni watu hatari sana kwetu wanaume.
Hebu tukumbuke hata kwenye hadithi za watu wa kale kwenye vitabu vya dini tukianzia mwanzo kabisa wa dunia enzi za Adam na Hawa/Eva. Adam alitii kila kitu katika mamlaka aliyopewa na Mungu lakini mwishowe alikuja kumkosea Mungu kwa kutenda dhambi aliyoponzwa na mkewe (Hawa/Eve) mara baada ya kushawishiwa na Shetani, Eeeh, amini usiamini shetani ni vigumu sana kumuingia mwanaume hivyo anamtumia mwanamke kama alivyomtumia Hawa/Eve kwenda kumlubuni mwanaume kama alivyolubuniwa Adam na kujikuta mwanaume anaumia kwaajili ya upendo na kumuamini sana mwanamke pasi na kuelewa kiundani udhaifu mkubwa wa mwanake mwenyewe.
Tuachane na Adam, tukumbuke Samson mtu mwenye nguvu aliyewapa tabu sana Wafiristi enzi hizo lakini mwishoe anakuja kukamatwa na kupata mateso makali baada ya kulubuniwa na Delila aliyetumiwa na Wafirist kubaini siri za nguvu za Samsoni. Eee, Samsoni nae aliponzwa kwa ajili ya mwanamke, na si yeye wala Adam tu tukumbuke hata mtu wa kwanza kufa alikuwa ni mwanaume na sababu ya kifo chake kilitokana na mwanamke!!
Eeeh ni wanaume wengi mno wameponzeka kwaajili ya wanawake na mmoja wao ni mimi na ndio maana leo hii nasema wanawake ni wauaji. Najua wengi mtanielewa vibaya hususani wanawake, lakini naomba msizime tv zenu ama radio ili mnielewe vizuri kwanini hasa nimekazania kusema Wanawake ni Wauaji? Hii ni asili iliyoanza toka kwa mwanamke wa kwanza kabisa kuumbwa na bado ipo na itakuwepo na itawaumiza wanaume wengi sana wasiokuwa makini na ndio maana hata Mungu hakuwahi kushusha nabii wa kike.
Wanawake ni wadhaifu wasiokubali udhaifu wao na ndio maana nawaita Wauaji. Achilia mbali vitabu vya dini tukija kwenye maisha yetu ya kila siku lini ulishawahi kusikia mwanaume katupa katoto kachanga? Naamini kama mimba wangekuwa wanabeba wanaume usingesikia neno kutoa mimba.
Hivi ushawahi kujiuliza mwanamke ana moyo wa namna gani hadi anadiliki kukiua kiumbe alichokibeba tumboni miezi tisa na kujifungua kwa uchungu?!! au unadanganywa na maumbile yake na sauti laini unajisahau na unaacha kuwa makini nae? hivi hujui kwamba simba dume ana muungurumo mkubwa sana lakini jike ndiye jasiri wa kuua. Huo ni mfano tu lakini nataka unielewe na uwe makini kwanini nasema WANAWAKE NI WAUAJI..”
Ilikuwa ni sauti ya bwana mmoja mlemavu wa macho na miguu akiongea luningani katika kipindi cha YA WALIMWENGU LIVE kilichokuwa kinarushwa kupitia kituo cha BECKER TV kila siku za jumapili asubuhi na marudio yake ilikuwa jumamosi jioni.
Nilikaa kwenye sofa kwa hamasiko. Macho na masikio niliyatupa luningani huku mkono mmoja nikiwa na kikombe chenye chai na mwengine ukiwa na rimoti nikiongeza sauti ya luninga. Mada ya yule bwana ilinistua na kunigusa sana hali iliyochochea niwe na shauku kubwa ya kumsikiliza ili nimuelewe vizuri kwanini anasema wanawake ni wauaji.
Nilitulia na kujikuta nashindwa hata kupiga funda moja la chai na kubaki nimekishikilia kikombe kwa kumakinika na yule bwana alipokuwa anazungumza ambapo aliendelea kwa kusema......
“Nakumbuka miaka kumi iliyopita nilikuwa na maisha mazuri kabisa ya furaha, mimi na mke wangu kipenzi baada ya kufunga ndoa. Kiukweli nilimpenda sana mke wangu nae alinionesha mapenzi hasa na kunisahaulisha maumivu niliyopata kutoka kwa mke wangu wa kwanza tuliyeachana muda mfupi tu baada ya kukaa kwenye ndoa kwa miaka mitatu na kuanza visa vilivyosababisha nimuache aishi maisha aliyotaka yeye na ndipo baada ya miezi kadhaa nilipompata huyu mwanamke wangu mwengine aliyeonesha kuwa na vigezo vyote nilivyohitaji na mwaka mmoja tu katika mahusiano yetu tuliamua kufunga ndoa kabisa.
Kiukweli mke wangu nilijivunia uzuri aliokuwa nao upole wake na tabia ya kupenda ibada. Na mara nyingi alinibadilisha kwa maneno matamu na kunisihi niache kunywa pombe, na kweli ilifika kipindi niliacha pombe na taratiibu nilipunguza kabisa kuvuta sigara kutoka pakiti moja kwa siku hadi ikafika mahali siku nzima nikavuta sigara mbili tu, hali iliyofanya hadi walionijua kunishangaa na kumsifu sana mke wangu na ndipo nami nilizidisha moyo wa kumpenda na kumpa uhuru wa kila kitu kwani nilimuamini mno…!” Alinyamaza kisha aliendelea…….
“Kila nilichofanya nilihakikisha lazima mke wangu ajue na nilisikiliza sana na kufata ushauri wake kuliko mtu mwengine. Akisema nisifanye kitu fulani nami nilitii, akisema nifanye nami nilitii, hiyo yote nilifanya nikiamini namjenga na kumuonesha kiasi gani namthimini bila kujua kua kuna ugonjwa m baya nilikuwa naufuga.
Awali sikuona tofauti yoyote wala kuhisi kama kuna kitu nakosea zaidi nilianza kusikia minong’ono kutoka kwa majilani na baadhi ya ndugu zangu kuwa napelekeshwa na nimetawaliwa na mke wangu. Kiukweli nilichukizwa na habari zile na kugombana na baadhi ya ndugu zangu waliomsema vibaya mke wangu nikiamini fika wanataka watugombanishe na wananionea wivu kwa kupata mke wa namna ile kwani maisha yetu yalizidi kunyooka siku hadi siku.
Aaaaaagh.. kuna muda huwa nahisi kama ndoto vilee kwani sikujua kabisa kumbe kuna bomu nalitengeneza mwenyewe ambapo baadae litapolipuka litaniletea madhara makubwa na kama si kuniua basi litanipa ulemavu wa kudumu kama ilivyotokea baadae…. Aaaagh, mke wangu!!!...”
Alivyozidi kuongea ndivyo nami nilivyozidi kutulia kumsikiliza kwa umakini huku nikibofya bofya rimoti kuongeza sauti mara kwa mara utafikiri nilikuwa na ubovu wa masikio. Nilimuangalia kwa jicho la shauku ya kujua yaliyomsibu. Uso wake wa jitimai ulitia huruma ukichochewa na ulemavu uliobeba tafsiri ya mazito yaliyomsibu. Kiu ya kujua ilikuwaje ilizidi kuniparua milango yangu ya fahamu. Lakini kabla sijafaidi vizuri hadithi ya yule bwana mara umeme ulikatika na kila kitu kuzimika.
“Aaaagh, Tanesco bwana kama maboya!!!”
Nilinyanyuka kwa hasira kuzima kitufe cha luninga na kuwasha kile cha taa ili umeme utaporudi tu, taa inijulishe mapema.
Wakati huo ile chai kikombeni ilikuwa ya baridi kabisa na sikuambulia kunywa hata chembe. Nilienda imwaga na kurudisha kikombe kabatini na ndipo nilipoikumbuka simu yangu niliyoiacha chumbani kwenye chaji. Haraka niliiendea na kukuta ikiwa na ‘missed calls’ tisa ‘sms’ nne. Nilipofungua zote zilitoka kwa mtu mmoja. Mtu ambae alikuwa zaidi ya uwaridi moyoni mwangu. Mwanamke wa ndoto zangu ambaye tulikuwa na miadi ya kukutana wikiendi hiyo ili tufurahi pamoja. Huyo alikuwa MARIAM ama MAMU kama nilivyopenda kumwita.
Nilizisoma zile ‘sms’ ambapo mojawapo iliandikwa hivi…
MBONA HUPOKEI SIMU WALA HUJIBU MSG ZANGU? KAMA UPO NA MALAYA WAKO SI UNAMBIE TU NISIJE..!!
“hahaa Mamu bwana..”
Nilijisemea moyoni na kuingia sehemu ya ujumbe kujibu lakini kabla sijabonyeza kitufe cha kutuma ujumbe, mara mlango wa sebuleni uligongwa kwa rabsha. Nilipouendea kabla sijaufikia, ulifunguliwa na mgongaji aliyeingia akiwa kashiba ununo. Alikuwa ni Mamu kipenzi changu. Nilifurahi nilipomuona nilimkumbatia na kum-busu lakini aliitoa mikono yangu kiunoni mwake na kunisukuma pembeni huku akiingia na kunipita bila kusema chochote na kwenda kukaa sebuleni.
Nilibaini kuwa amekasilishwa kutokana na kutopokea simu yake na nilijua sasa nina wajibu wa kum-bembeleza ili nimuweke sawa. Nilimjua kipenzi changu ni chakudeka, nami kwa huba nilimdekeza.
“Unakunywa nini bebi” nilimuuliza kwa sauti ya mahaba.
“Sitaki kunywa chochote niache.” Alijibu kwa hasira huku akipandisha miguu sofani na kubetua midomo huku uso wake akiuelekezea pembeni.
Hali ile ilizidi kunihakikishia kuwa nina shughuli pevu ya kubembeleza mtu mzima sasa. Lakini kabla sijafanya hivyo mara taa ya sebuleni iliwaka na ndipo nilipokumbuka kuwasha luninga kwanza niendelee na kile kipindi huku moyoni nikiwa na shauku Mamu nae amsikie yule bwana juu ya hadithi yake iliyowatuhumu kuwa wanawake ni wauaji.
Lakini lol! Mada ya yule bwana hasa kauli yake ya kuwa wanawake ni wauaji ilimchukiza zaidi Mamu na kuamua kuzima luninga kwa hasira.
“Aaag! Wee vipi?” nilitahayuri.
“Vipi nini!!?” Alinijibu kwa kuniswalika.
“Si uache tuangalie sasa unazimia nini?!”
“Hivi Hussein kwa akili zako timamu unaona hiki kitu anachokizungumza huyu mpuuzi ni sahihi!!”
“Kitu gani..?”
“Kusema wanawake ni wauaji.!!”
“Mh! hapo kumjaji moja kwa moja itakuwa ngumu, sasa nitamjaji vipi wakati hata hadithi yenyewe sijaisikia!! anaweza kuwa sahihi au si sahihi inategemea na point zake mwenyewe.”
”Hee! hivi nyinyi wanaume mpoje!!!” Aliwaka Mamu kwa sauti ya juu na kusimama huku akinitazama kwa hasira. Alihema juu juu na kuzidisha povu akinguruma kama moto wa kifuu.
“Hivi mnatuchukuliaje sisi wanawake eeh!!?”
“Kivipi baby.. mbona tunawakiana sasa.”
“Sio Nawakaa.. ila nakwambia ukweli acha kuwa na mitazamo ya kijinga au ndio kashakulisha ujinga huyo mpuuzi mwenzio…! Kwa hiyo na mimi muuaji si ndio, au unanionaje!!”
“Hapana baby sijamaanisha hivyo..”
“kumbe unanionaje..!”
“Unaweza kuwa muuaji au si muuaji inategemea tuu.”
“Aahaa.. kwa hiyo hadi mamaako aliyekuzaa muuaji, dada zako wauaji, shangazi zakoo si ndio..!”
“Sasa Mamu hayo matusi..”
“Matusi nini.. si wanawake ni wauaji! We vipi..?! Hebu nipishe huko nisije nikakuua buree..”
Alichukua mkoba wake kishari pale sofani kwa hasira Mamu alielekea mlango wa kutokea ulipo na kutoka huku akiubamiza kwa nguvu.
“Aaagh!! Sasa huo mlango umekukosea nini..!”
Nilibaki nimebumbazika pale kwenye kiti huku nikiwa nimechanganyikiwa kwa jinsi Mamu alivyonibadilikia siku hiyo kuliko siku zote. Hakuwa cha kudedee tena bali alikuwa mbogo. Nilijilaumu kidogo kwa kubishana nae punde alipozima luninga na kumsababishia mpenzi wangu kuwa na hasira mara tatu zaidi alivyoingia. Niliuendea mlango na kuokota funguo zilizodondoka pindi ulipobamizwa kisha nilirudi na kujitupa kwenye sofa huku akili yangu ikiwa imecheza makida.
Niliiwasha tena luninga safari hii nikiwa sina shauku kabisa wa kuangalia kile kipindi ambacho ndio kilikuwa kinaishia lakini kuna maneno ya mwishoni ya yule bwana yalipenya vizuri masikioni mwangu na kukistua kichwa changu kidogo pindi aliposema.
“Najua wanawake wengi wataobahatika kunisikiliza na kunitazama watanichukia na kuona nimewadhalilisha na kuwatusi. Nami sitoshangaa wala kuogopa hilo kwa sababu najua kuwa wanawake tayari wana ulemavu wa asili ambao Mungu aliwaumba nao kwa dhumuni la kuwa wasaidizi na wafariji kwa wanaume tu.
Mwanaume hajaumbwa kwaajili ya mwanamke ila mwanamke aliumbwa kwaajili ya mwanaume na ndio maana tunaambiwa kuwa mwanamke ametoka ubavuni kwa mwanaume. Lakini udhaifu wao ndio unafanya tuone mpaka leo hii wanawake wakitaka kushindana na wanaume wakisahau kuwa mwanaume ni wa kwanza tu kiasili.
Na hii inatokana na kuwa mwanamke ni rafiki mkubwa wa shetani anayetumiwa katika kuiharibu dunia na hata baadhi ya wasomi wa dini kiimani wanatwambia wanawake wengi sana wataingia motoni.
Mungu ameweka mifano mingi sana ya wazi kuwakumbusha wanawake kuwa mwanaume ni kiongozi na anapaswa kunyenyekewa na mwanamke japo kwa akili mbovu za wanawake wengi wanaona kufanya hivyo ni ujinga kwani hata wao wanaweza kufanya wanayofanya wanaume. Ha ha haa yaani hata mifano ya wanyama hawaioni!! Wazee waliosema Wanawake mwalimu wao kipofu walikuwa na maana kubwa sana ambayo sasa imepuuzwa.
Cha mwisho nakukumbusha wewe mwanaume unayenitazama hususani wewe uliegombana na mkeo au mpenzi wako hivi punde chanzo kikiwa hiki kipindi na hii mada yangu. Nataka ujue kwamba uko katika wakati mgumu sana na huyo mwanamke tena nakusihi uwe makini nae sana.
Ukipuuza siku moja yanaweza kukukuta kama yaliyonikuta mimi hata kama hautakuwa na ulemavu wa viungo kama mimi. Kuweni makini sana na wanawake wanaume wenzangu kwani hata mwenyezi Mungu ametwambia tuishi nao kwa akili.”
Nilistuka kwa maneno yale na kuhisi kama naambiwa mimi moja kwa moja. Muda mfupi baada ya kile kipindi kuisha nikiwa nimemezwa mawazoni nikijiuliza mwenyewe nishike yapi niache yapi haswa nikiambatanisha na kauli za Mchumbaangu kipenzi.
Mara ujumbe uliingia kwenye simu yangu na nilipoichukua kuufungua alikuwa ni Mariam.
Ujumbe ulisomeka hivi…
“Hussein nashukuru sana kwa matusi yako ya kuwa eti mimi ni muuaji haina shida ila kama ulikuwa hunitaki na ulikuwa unatafutia sababu ungenambia mapema tuu kuliko kunipoteza muda wangu.. Nashukuru sana, usinitafute nakutakia maisha Mema..”
Sio siri ujumbe wa Mamu ulinishangaza. Sikutaraji kabisa kama kile kipindi kinaweza kusababisha yote yale. Niliisoma mara mbili mbili ile 'sms' na kuamua kumpigia Mamu lakini simu yake iliita bila kupokelewa.
Sikuchoka niliendelea kupiga lakini bado haikupokelewa na mara nyengine ilikatwa na mwishoe nikawa nasikia sauti ya huduma kwa wateja wakinambia kuwa namba ninayopiga inatumika.
Niliachana na simu na kuingia bafuni kuoga niliporejea chumbani nikatupia pamba kama kawaida yangu.
Eeeh.. kupendeza ilikuwa kawaida kwangu kutokana na jinsi nilivyojua kupangilia mavazi hadi watu wengi kitaani wakawa wananita bitozi, si unajua tena uswahilini kila 'chocho' unayokata ukiwa 'umejitupia' sana watu macho kodoo.
Nilirejea sebuleni baada ya kujiridhisha kwa nguo nilizovaa siku hiyo na kabla sijatoka nilipiga tena simu ya Mamu lakini jibu lilikuwa lile lile kwamba namba ninayopiga ipo bize.
Sikuwa na jinsi ilibidi nitoke na kuchukua bodaboda kuelekea kwa kina Mariam nikiwa na nia na madhumuni ya kwenda kuomba msamaha ili mapenzi yetu yaendelee kwani nilimpenda sana na nilijua kama nisingeenda muda huo basi ingebidi nisubiri hadi wiki ijayo kwani nisingepata nafasi kutokana na kuwa kazini muda mwingi.
Baada ya mwendo wa dakika kumi tulifika maeneo ya kina Mam na kumlipa ujira wake yule dogo aliyenileta nami moja kwa moja nikaanza kuongoza njia ya kwa kina Mamu huku nikiwazia jinsi ya kuanza.
_________________ITAENDELEA..