mireille
JF-Expert Member
- Mar 4, 2020
- 606
- 665
- Thread starter
- #61
USINIACHE 4:
Sura ya 151
Alissa alisimama tu na kumuangalia Kendrick akitokomea. Alissa alijiona yuko salama.
Kendrick alikuwa anamuunga mkono, hivyo angeweza kusonga mbele bila wasiwasi wowote.
Alissa aliingia ndani ya gari baada ya kumuona Kendrick akitokomea mbali.
“Twendeni.” Alisema Alissa kwa upole.
Nora alifikiri kuna kitu kibaya kwa Alissa na Kendrick na kuuliza tena. “Kuna nini nyie?”
“Hakuna kitu. Nitakuambia baadaye.” Alissa akatikisa kichwa. “Hebu twende nyumbani kwanza.”
Nora hakuuliza zaidi, akamuomba dereva aendeshe gari.
Ndani ya gari, hatimaye Alissa alipumzika.
“Alissa, wacha kuniweka roho juu. Nina hamu ya kujua unachotaka kiniambia.” Alissa alimpeleka Doris.
Doris alikuwa mtulivu, na Nora alikuwa amempa simu yake acheze gemu. Akili yake yote ilikuwaimeishia kwenye simu.
Nora alikuwa dukuduku moyoni na Alissa alikuwa hana haraka.
“Una usingizi?”
"Hapana." Alissa alikaa kitako huku akihisi mtupu kidogo.
“Ulifanya muda gani jana usiku?” Nora hakuweza kuzuia udadisi wake. “Kendrick yuko sawa?”
“Jamani, unazungumza nini?” Alissa aliona haya kwa maneno ya Nora, “Sijafanya chochote naye.”
"Unataka kumdanganya nani Alissa? Kwa kumbato lile bado unadiriki kusema hukufanya?" Nora alishangaa, lakini Alissa aliitikia kwa nguvu.
Alimtazama Alissa kuanzia kichwani hadi miguuni na kurudi kwa macho mazito.
Hatimaye macho yake yakatua kwenye uso wa Alissa na kukunja uso. "Haipaswi kuwa hivyo."
"Nini?" Alissa alijiuliza huku akiwa amemtumbulia macho yake.
“Mwanaume gani hawezi kuvutiwa na umbo na sura yako? Mwanaume angekurukia na kulala nawe mara tu unapoingia naye chumbani. Bwana Kendrick na wewe ni mume na mke. Ni sawa kufanya ngono. Kwa nini hamjafanya lolote?” Nora alichanganua. "Mnasubiri nini? Au ni mgonjwa?"
"Ni sawa na hakuna chochote kibaya kwake." Alissa alikunywa maji, na ubaridi tulivu ukaenea kati ya meno yake.
“Umejaribu? Unathubutu kusema yuko sawa? Ikiwa yuko sawa, hakuwezaje kulala na wewe jana?" Nora alimtolea Alissa macho.
“Bila shaka nime…” Alissa nusura amwage ukweli, lakini mara moja akajirekebisha, “Amekuwa akifanya mazoezi kila siku. Nina hakika hana tatizo. Na sisi ni mume na mke, lakini sasa tuko kwenye uhusiano. Alisema ataniheshimu na nikisema tu ndio tutafanya hivyo.”
"Bwana Kendrick ni muungwana, sivyo? Ndiyo, anaonekana kuwa na nguvu.” Nora alikunywa maji yake. “Oh, sawa. Kwa nini alikuleta kwangu na kisha kuondoka peke yake? Kwanini asingekupeleka kwa Maziku?”
"Hapana, anarudi Geita." Mwanga wa nyota ukaangaza machoni mwa Alissa.
Nora alishika mng'ao wa macho yake. “Kwa hiyo huwa anakuja na kuondoka? Je, kuna kitu kibaya katika familia yao? Mbona umeondoka kwa haraka hivyo?”
"Hapana." Alissa alikanusha huku usoni akiwa na utamu mdogo wa kike. "Alitaka tu kuwa nami na kunirudisha salama Mwanza."
Hatimaye Nora alielewa, “Vema. Jinsi wewe ni mtamu.”
Alissa alikunywa maji mara mbili zaidi kwa kuridhika.
"Wale ambao wako tayari kutumia pesa na wewe wanaweza kuwa sio wale wanaokupenda, lakini wale ambao wako tayari kutumia muda adimu na wewe lazima wakupende.
"Kwa hivyo, mtu wa thamani zaidi ulimwenguni ni yule ambaye yuko tayari kutumia wakati na wewe. Mthamini mwanaume huyo, haswa anapokuwa mtu mwenye shughuli nyingi, na yuko tayari kubana muda wa kuwa na wewe."
Alissa aliguswa na maneno ya Nora.
Baada ya kuwa mbali na Kendrick kwa zaidi ya saa moja, alianza kumkumbuka, kum'miss kuwa kando yake, kumkosa kumshika mikononi mwake, kuimiss sauti yake, na kumiss busu lake.
"Itakuwa tamu zaidi katika siku zijazo." Alissa alijibu.
Nora alimpa dole gumba. “Ni vizuri kukuona hivi. Ni kama unakuwa wewe tena.”
“Ndiyo. Ninahisi kutaka kujipata tena.” Alissa aliwaza hivyo. “Wewe unaweza pia. Umepotea tu sasa hivi.”
"Ni juu yangu tena." Nora akahema. "Sio kila mtu ana bahati kama wewe kupata ubinafsi wako uliopotea. Sijisikii nimepotea tu, nahisi nimekufa.”
"Bila shaka huwezi kujikuta na mawazo hayo." Alissa alimfikiria ghafla mtu aliyemwona katika Dar es Salaam, na baada ya kusita kwa muda mrefu, alisema, “Nora, namaanisha nini ikiwa… Je, ikiwa hajafa?”
Nora alimtazama, akiwa na chupa ya maji mkononi, katika mkao wa kifahari.
"Uliniuliza swali kama hilo mara ya mwisho." Nora alidhani Alissa aliuliza mara mbili. “Kuna kitu unanificha?”
Alissa aliuma midomo yake, lakini aliamua kumwambia yote aliyoyajua. "Nora, utanisikiliza kwa utulivu?"
Nora akaitikia kwa kichwa.
“Siku moja tukiwa Dar, mimi na Jane tulikuwa tunakula chakula cha jioni, na mtu fulani alitulipia. Nilipotoka mbio, yule jamaa alikuwa tayari kwenye gari, na niliona uso wake kidogo kupitia dirisha lililoinuliwa. Nilifikiri anafanana sana naye… Bila shaka, kuna watu wengi duniani wanaofanana. Unajua, kuna kaka au dada mapacha waliopoteana, kwa hiyo nadhani ninaweza kuwa nimekosea.”
Nora, hata hivyo, alikuwa mtulivu sana na akasema, “Nadhani ulikosea. Au labda unaamini ni yeye, kwa hiyo ulifikiri kwamba mtu huyo ni kama yeye.”
Na kisha akaongeza, "Amekufa. Hatutakuwa tena naye.”
"Sawa, tuachane na hii." Alissa alijisikia faraja kusema, lakini haikumsaidia Nora.
Nora alikuwa mtulivu juujuu, lakini moyoni alijua kuliko mtu yeyote jinsi alivyokuwa anamtaka huyo mtu awe hai.
Alisema hivyo kwa sababu hakuthubutu kujipa mwanga wa matumaini, kwa kuhofia kwamba angemkosa zaidi, kwa kuhofia kwamba angepoteza hata ile furaha iliyojificha, na kuhofia ndoa hiyo isingeweza kumnasa.
“Niambie wewe na bwana Kendrick. Kwa nini ulimtazama sana wakati anaondoka?" Nora alibadilisha mada kwa haraka, “Ulisema utaniambia baadaye.”
“Hiyo ni kwa sababu tunamtafuta mtu aliurtufremu…” Alissa alimpa Nora maelezo mafupi ya kilichotokea, pamoja na mpango aliokuwa akiufikiria.
Sura ya 152
Baada ya safari ya karibu saa nzima barabarani kutokana na foleni, hatimaye Alissa alirudi kwenye makazi ya familia ya Maziku na Doris.
Giza lilikuwa likiingia na jumba hilo la kifahari lilikuwa na mwanga mkali.
Waliporudi, bibi Jenifer alikuwa tayari alikuwa ameenda kulala. Merry pekee ndiye aliyekuwa sebuleni. Alipomwona Alissa, alikuwa na shauku zaidi kuliko hapo awali, “Alissa na Doris, habari za jioni. Mmekula?”
“Ndiyo.” Alissa alimshika Doris na kukaribia kuondoka.
Merry akamuuliza tena, “Nimesikia kuwa ulienda Geita kikazi.”
“Ndiyo.”
"Umekutana na Bwana Kendrick?" Merry alikuwa na wasiwasi juu ya uhusiano wao sasa.
“Ndiyo.” Alissa alijua wazi anachomaanisha Merry,
“Hata aliachana na kazi zake kwanza na kuandamana pamoja nami. Tulikuwa na wakati mzuri.”
"Inapendeza." Merry alicheka, “
Usiku umeenda. Nenda ghorofani ukapumzike sasa. Usiku mwema." Alissa kisha akatulia na kumpeleka Doris juu.
Merry alisimama na kuwatazama wakipanda juu huku akikunja uso kwa kuchanganyikiwa.
Ilionekana kuwa kuna kitu kibaya. Melissa alisema kwamba alimwomba mtu aende kwa familia ya Mayala ili kufichua ukweli kwamba Alissa alikuwa hawara wa Kendrick. Familia ya Mayala ilikuwa ya kifahari sana kwamba mwanamke ambaye angeweza kuolewa naye anapaswa pia kuwa msichana wa kuvutia na alikuwa na historia ya nguvu. Kwa hivyo, familia ya Mayala ingeshughulikia. Mbali na hilo, Merry alisikia kutoka kwa Melissa kwamba mwanamume huyo alimwambia kwamba ingawa bwana wa familia ya Mayala hakukasirika sana, alikosa furaha kidogo.
Kwa hivyo, Alissa hakupaswa kuandamana na Kendrick kwa furaha.
Au Melissa alidanganywa na mtu huyo?
Wakati huo, Alex, ambaye alikuwa amerudi kutoka kwenye karamu ya chakula cha jioni, aliingia na kumpiga kiwiko Merry ambaye aliganda, "Unaangalia nini?"
“Hakuna kitu.” Merry hakuthubutu kumwambia Alex juu ya kile Melissa alichokifanya. Kwa sababu aliogopa kwamba Alex angeharibu mpango wao.
Hakukubaliana na Melissa. Lakini pia hakutaka Alissa awe na kiburi kwa sababu ya Kendrick katika familia ya Maziku. Kwa hivyo, alifumbia macho kile Melissa alikuwa amefanya.
***
Alissa ilimbidi akamilishe mradi wa FarmCom baada ya wiki mbili. Kwa hiyo, ilimbidi kuwa bize na kazi yake. Muda ulikimbia.
Yeye na Kendrick hawakuwa na mawasiliano ya ana kwa ana. Lakini wangezungumza kwenye simu.
Kendrick alimtumia hii saa sita mchana: [Hata kama uko busy na kazi, unapaswa kula.]
Alissa alijibu kwa njia ya kucheza na kufurahisha: [Sina shughuli nyingi kama Bwana Kendrick. Mimi ndiye ninayepaswa kuwa na wasiwasi iwapo Bwana
Kendrick ana mlo mzuri.]
Kendrick kisha akainuka na kuiendea meza ya duara karibu na sofa. Kulikuwa na vyakula kadhaa mezani, vyote hivyo vilikuwa ni chakula cha mchana ambacho Chale alimuagizia kila siku.
Kendrick: [Je, ungependa kuungana nami?]
Alissa alituma emoji: Mlo wa mchana wa bwana mkubwa ni wa gharama sana! Najihisi mimi ni maskini sana.]
Kendrick aliketi kwenye sofa: [Unataka kula? Ni haki tu kwamba unatoa kitu kwa kubadilishana, sivyo? Bi. Mayala.]
Alissa alituma emoji ya busu ili kumhonga Kendrick.
Kendrick alitabasamu: [Nitakumbuka kwamba Bi. Mayala anadaiwa kunibusu. Subiri.]
Subiri? Angojee nini?
Alissa aliinamisha kichwa, akakunja uso na kuwaza. Anapaswa kwenda kwenye kantini ya kampuni sasa.
Aliweka kalamu yake chini, akainuka na kwenda kwenye mgahawa.
Wakati anaandaa chakula chake, alimuona Emmy akimpungia mkono.
Alissa kisha akaenda kwake.
Emmy ndiye mfanyakazi mwenzake pekee ambaye alikuwa na shauku zaidi kwake katika kampuni na alimsaidia kila wakati.
Mathew pia alimsaidia. Lakini hata hivyo alikuwa bosi wake. Sasa Alissa alikuwa ameolewa. Kwa hivyo, wanapaswa kuepuka kukutana mara kwa mara kuibua tuhuma.
"Hii nyama ni kwa ajili yako." Emmy alichukua nyama kutoka kwenye sahani yake na kumpa Alissa.
“Kisha nitashiriki nawe baadhi ya vipande hivi vitamu vya nyama choma?” Alissa alisema.
"Hapana. Kulikuwa na vipande viwili tu vilivyobaki. Nikifikiria kwamba unapenda nyama choma pia, hivyo nilichukua moja kwa ajili yako.”
Emmy alipenda nyama choma zaidi. “Tulia. tunapaswa kusaidiana kama wafanyakazi wa kampuni moja.”
Alissa alihisi kwamba Emmy alikuwa mwenye usawaziko na alikumbuka fadhili zake kwa siri.
“Hebu tufurahie.”
Walipoanza kula tu, mwanamume mmoja aliyevalia nguo za sare za Mgahawa wa City Star Restaurant alikuja na kontena maalum la chakula kutoka kwenye mgahawa huo.
Mkahawa wa City Star ulikuwa msururu wa kitaifa wa migahawa maarufu ya hali ya juu. Watu waliotaka kula chakula hapo lazima wawe wanachama wao. Wanachama walihitaji kulipa ada ya kila mwaka. Wapishi wao walikuwa mahiri katika vyakula vinane. Chakula walichopika kilikuwa kizuri sana.
Kontena lilifunguliwa. Kila mtu alikaza macho yake kwenye chombo kizuri cha chakula cha na hakuweza kujizuia kumeza mate ya uchu.
Mhudumu huyo alisimama mbele ya meza ya Alissa na kumchunguza. Alipoona kitambulisho chake cha kazi shingoni, alisema, “Je, wewe ni Bibi Alissa?”
“Ndiyo.” Alissa akaweka chini uma uliokuwa mkononi mwake.
"Tafadhali saini hapa." Mhudumu alimkabidhi barua ya kupokelea mzigo.
Alissa alisaini na kumrudishia mhudumu yule. Mwanamume huyo akaiweka, akafungua chombo cha chakula, akatoa sahani kadhaa, ikiwa ni pamoja na samaki watamu sato, wakukaanga katika mchuzi wa moto na nyama ya kukaanga na pilipili, Chipsi moto, kuku wa kuoka, na madikodiko mengine kibao.
Vyakula hivi vilikuwa sawa kabisa na vile kwenye picha aliyomtumia Kendrick.
Kwa hivyo, hivi ndivyo Kendrick alimaanisha kwa kungoja. Alimuagizia chakula sawa. Alissa aliguswa na wema wake.
Alikuwa ameushika moyo wake na kumuacha apendezwe naye kwa namna ambayo hakuitarajia.
Baada ya mhudumu yule kuondoka, Emmy alitazama sahani tajiri kwenye meza. Ilikuwa na harufu nzuri ambayo ilimfanya apate njaa sasa.
Watu wengine pia walikitazama chakula kilichokuwa mezani, wakasikia harufu yake na kukionea wivu.
Lily tu na rafiki yake wa karibu walikuwa na wivu sana.
"Alissa, mumeo alikutumia haya yote?" Emmy angeweza kufikiria tu jambo hili.
"Nadhani." Alissa alitabasamu tu.
"Alissa, mume wako anakupenda sana." Emmy alionekana mwenye wivu, “Sijawahi kula chakula katika Mkahawa wa City Star. Nilisikia kwamba ni ghali sana. Bei ya baadhi ya sahani ni sawa na mshahara wangu wa kila mwezi.”
Alissa alichukua samaki mtamu na kumweka kwa Emmy, "Basi jaribu leo."
"Alissa, wewe ni mkarimu sana." Emmy aliguswa, “Lakini hii ni sawa? Hii ni zawadi kutoka kwa mumeo.”
"Mambo mazuri yanapaswa kushirikiwa na marafiki. Jisaidie tu.” Alissa alidhani Emmy alikuwa mzuri sana.
“Sawa, asante.”
Lily kwenye meza iliyofuata alitazama hili na alikuwa na hasira sana kwamba hakuwa na hamu ya kula kabisa.
"Lily, Alissa hawezi kupata chakula kutoka kwa Mgahawa wa City Star hata kama ana pesa. Mume wake ana nguvu sana?” Rafiki wa Lily aliuliza kwa kuchanganyikiwa.
"Hivi kweli ana mume anaposema ana mume?" Lily alionekana kukasirika na kusema kwa jeuri, "Labda yeye ni hawara tu wa mtu."
“Ndiyo. Anaonekana kukata tamaa. Hawara anayeharibu familia za watu hatafikia mwisho mwema.”
Sura ya 153
Emmy alikasirika sana kusikia Lily na marafiki zake wakimtukana Alissa. Alimwambia Lily, “Lily, huo ni wivu tu. Unafikiri wewe ni bora kuliko wengine?"
“Wivu? Ni utani ulioje.” Lily alikoroma kwa ubaridi, “Kama ana mume, kwa nini asimlete hapa tumuone? Anakataa kwa kila aina ya visingizio. Hata kama mumewe anamletea vyakula na maua, ili iweje? Je, anathubutu kumleta mume wake hapa? Ninaogopa mume wake ataaibika sana kutuona, sawa?”
“Ndiyo. Angalau, Lily na bwana mdogo wa Vortex Company wako juu na hawaogopi mtu yeyote anayewasema vibaya. Ni Neema, rafiki wa Lily, alimzungumza, “Mara ya mwisho, mpenzi wa Lily alitualika Villa Park Club. Huwezi kusahau jinsi alivyokuwa mkarimu kwa Lily, sivyo?
“Emmy, unafikiri wewe ni mtu mzuri? Alissa anaendesha gari aina ya Range Rover na kukupa baadhi ya vyakula kutoka kwenye Mkahawa wa City Star. Basi, wewe ni kama mbwa anayejikombakomba kwa bwana wake. Natumaini kwamba yote hayatakuwa bure, au utakuwa na huzuni.”
Neema kweli alikuwa na ulimi wa fedha.
Emmy alikuwa na hasira na wasiwasi baada ya kuzomewa na Neema. Pia alihuzunika sana, "Nyinyi ... ninyi ndio mbwa wanaouma watu kila mahali."
"Wewe ni nzi anayefuata mzoga." Walijibu kwa karipio la kejeli, na kumfanya Emmy karibu kulia kwa hasira, “Nyinyi watu …
nitamwambia Bw. Matthew nyinyi watu mnaenda mbali sana.”
“Jipange. Sasa ni mapumziko ya chakula cha mchana. Bwana Mathew hatajali sana.” Jamila, rafiki mwingine wa Lily, alijibu.
Walionekana kuwa na kiburi na kufanya wapendavyo.
Alissa hakuwa na nia ya kujiletea matatizo. Lakini walichosema na kufanya kilikuwa kinaenda mbali sana.
Hawakumpenda na kumdhulumu. Lakini kwa sababu tu Emmy alikuwa karibu naye, walimdhalilisha Emmy hivi. Ilikuwa ni chukizo sana.
Ikiwa angevumilia kila wakati, angechukuliwa kama dhaifu.
"Mbona nyie watu ni wakali sana? Lily, unasahau kwamba umekatwa miezi sita ya bonasi na Bw. Matthew?” Alissa aliwakumbusha kwa mtazamo mzuri.
“Alissa, unathubutuje kutaja hili? Kama si wewe, ningekatwa miezi sita ya bonasi? Ninajua kwamba Bw.
Mathew alikuwa na upendeleo kwako. Siamini kwamba hakuna chochote kati yako na Bw. Mathew.” Akifikiria bonasi yake, Lily alihisi kufadhaika.
Alissa alikuwa karibu kusema kitu alipoona mtu anayemfahamu anakuja. Kumtazama mtu anayekuja, alishtuka na kisha kushangaa.
“Lily?” yule mtu mzuri alisimama mbele ya Lily na kutazama kadi yake ya kazi.
“Mimi…..” Lily alimtazama mwanamume mrembo mbele yake. Ingawa mwanamume huyo alionekana mpole na mtaratibu, Lily aliogopa kidogo na kuingiwa na hofu, “Wewe ni nani?”
“Mimi ndiye kiongozi wa ofisi kuu ya Universal Group. Tafadhali rudia ulichosema hivi punde.” Sauti ya mtu huyo ilikuwa baridi, “Kama ni kweli kama ulivyosema kuna uhusiano usiofaa kati ya wasaidizi na bosi, nitaomba makao makuu yamfukuze kazi.”
“Kweli?” Lily alishangaa.
"Lily." Hata hivyo, Neema alimvuta Lily na kumwambia atulie. “Tunawezaje kuamini kwamba wewe ndiye bosi mkuu kutoka makao makuu? Wewe ni nani?"
Mtu huyo alitoa kadi yake ya kazi, ambayo ilisoma Nilesh Kumar kutoka makao makuu ya Universal Group, na nafasi yake ilikuwa Mkurugenzi wa Miradi.
Lily, Neema na Jamila, na wengine katika mgahawa wote walishangaa.
Mtu huyo alikuwa mkurugenzi wa miradi wa wa kampuni! Alionekana mzuri na mpole. Sauti yake ilikuwa ya kupendeza na laini. Pia alikuwa kipaji bora ambaye alihitimu kutoka taasisi bora ya biashara na kurudi kutoka nje ya nchi. Alimshangaza kila mtu hapa.
Nilesh kila mara aliweka hadhi ya chini maishani na kazini. Ingawa alikuwa amechukua miradi mingi mikubwa na kuishughulikia kikamilifu, hakuwahi kufanya mahojiano na hakujali kamwe ofisi ya tawi. Kwa hiyo, watu wachache walikuwa wamemwona kuwa mtu halisi.
Sasa alifika kwenye ofisi ya tawi ya Mwanza, ambayo ilikuwa fursa adimu kwa Lily.
"Bwana Nilesh?” Lily alitabasamu kwa kutaniana.
"Unaweza kuzungumza nami chochote unachotaka kusema." Nilesh alitabasamu kwa upole.
"Mimi ..." Lily alikuwa karibu kusema kitu. Lakini alisimama na kumtazama Alissa, “Mr. Nilesh na Alissa wanajuana, sawa?”
Alissa alikuwa akifanya kazi katika idara ya Nilesh huko makao makuu, Dar. Kwa kawaida alikuwa amefanya kazi na Nilesh, mkurugenzi wa miradi.
“Tulikuwa tukifanya kazi pamoja katika makao makuu. Kwa hiyo, bila shaka tunafahamiana.” Nilesh alikuwa na busara na hekima wakati akitaja uhusiano wao.
"Bwana Nikesh, huu ni mkutano wangu wa kwanza na wewe. Je, utaamini nilichosema?” Lily hakuwa mjinga kiasi hicho.
"Ninaamini tu katika ushahidi." Nilesh alikuwa mwenye usawaziko, “Nipe ushahidi nami nitashughulika naye kulingana na ushahidi.”
“Tumeona kwa macho yetu kwamba wakati Alissa anahamia hapa, amechukuliwa gari la Bw. Matthew mara chache kwenda na kushuka kazini. Hivi karibuni, aliendesha gariaina ya Range Rover. Hawezi kumudu kununua gari kama hilo lenye thamani ya mamilioni kwa kiwango chake cha mshahara. Ikiwa hakuwa na historia, angewezaje kupata nafasi ya meneja wa miradi baada ya kuja hapa?" Jamila alifurahi na kusema.
“Kila mtu anaweza kuzungumza. Ninachotaka ni ushahidi.” Nilesh aliwakumbusha tena.
“Sikuwaza sana wakati huo. Kwa hiyo, sikupiga picha.” Jamila sasa alijuta sana.
“Huna ushahidi. Ina maana unabahatisha na kumtilia shaka bosi wako!” Nilesh akawa baridi na hasira.
Jamila aliogopa. Aliinamisha kichwa chini na hakuthubutu kumwangalia, "Mimi ... sidhani hivyo."
“Si ulisema hivyo?” Macho ya Nilesh yalitiririka kutoka uso kwa uso, “Kila mtu anaweza kushuhudia kwamba sikukosea, sivyo?”
Jamila aliuma mdomo wake na kumtazama Lily kwa woga fulani, akimwomba Lily msaada.
"Lily anafikiria nini kifanyike kuhusu tabia ya aina hii?" Nilesh, hata hivyo, aliuliza kabla Lily hajazungumza chochote.
Lily alikuwa katika hali ngumu, akifikiri kwamba Jamila ni mjinga kweli.
"Bwana Nilesh, yeye ni mnyoofu kidogo na hana ubaya wowote. Kwa nini tusisahau tu?” Lily alimtetea Jamila kwa sababu Jamila alikuwa amemsaidia sana.
"Tusahau? Halafu sheria na kanuni za kampuni ni za kuonyesha tu!” Nilesh alikoroma kwa upole, “Anaweza kumshuku Alissa na Bw.
Matthew wana uhusiano wa kimapenzi leo. Halafu atashuku kuwa nina uhusiano wa kimapenzi na Alissa kesho, sawa?"
“Hapana, hapana. Bwana Nilesh, sithubutu.” Jamila akatikisa kichwa.
Sura ya 154
"Hujathubutu?” Nilesh alicheka na uso wake mzuri ulikuwa baridi, “Ulichosema bado kinasikika masikioni mwangu! Siwezi kustahimili watu kama wewe wanaochochea uadui kati ya bosi na wafanyakazi.”
"Kwa hivyo, haupaswi kukatwa tu bonasi ya nusu mwaka kwa kumsingizia bosi wako. Unastahili kufukuzwa kazi.”
Jamila aliposikia kwamba atafukuzwa kazi, alipigwa na butwaa. Alikuwa ametoka tu kuwa mgeni na kuwa mfanyakazi mkongwe na alifurahia matibabu mazuri katika kampuni hiyo kuliko makampuni mengine aliyofanya kazi. Hakutaka kuachishwa kazi.
Mara tu atakapofukuzwa kazi, hataweza kusimama katika jiji hili. Hakuwa mrembo kama Lily kupata mchumba tajiri. Hakuwa na asili dhabiti ya familia na alikuwa mtu wa kawaida kutoka familia ya kawaida. Hakutaka kurudi huko.
"Bwana Nilesh, hii si adhabu kali sana?” Lily bado alitaka kumtetea Jamila. Baada ya yote, Jamila alikuwa msaidizi wake mwenye uwezo na hangeweza kumpoteza.
“Sifikirii hivyo. Adhabu hii ni ya haki sana.” Emmy alijitokeza kwa wakati ufaao, “Hatupaswi kutoa matamshi ya kutowajibika.
Kashfa kama hii pia inaweza kusababisha mashambulizi ya kibinafsi."
“Na si mara ya kwanza nyie kuongea hivi. Bado nakumbuka kwamba kuna msichana mgeni aliacha kazi yake akilia kwa sababu ya mashambulizi yenu ya maneno na udhalilishaji. ”
“Nyie mmefanya mambo mengi mabaya. Je, hampaswi kuadhibiwa?”
"Acha kuongea ujinga." Uso wa Lily ulikuwa wa rangi.
Neema hakuthubutu kuongea na Jamila alionekana kuwa na wasiwasi.
“Ninasema ukweli. Ikiwa kuna uwongo, nitapigwa na radi na kugawanyika sehemu mbili." Emmy alikuwa imara na akaapa.
Wakati huu, umati wa watu ulianza kunong'ona. Kwa kuwa Lily alikuwa na tajiriba na alikuwa na mpenzi tajiri kama msaidizi wake, watu wachache katika kampuni hiyo walithubutu kumkasirisha.
Sasa kwa kuwa mtu fulani angemwadhibu, wote walikuwa wachangamfu.
“Emmy yuko sahihi. Sisi pia tunajua mambo haya.” Kuna mtu alimuunga mkono Emmy.
"Mradi tu mtu hamtii Lily katika kampuni, watamkemea na kumdhulumu. Ni kweli haiwezi kuvumilika.”
"Bwana Nilesh, tafadhali washughulikie.”
Nilesh alitikisa kichwa huku akisikiliza umati, "Kwa hivyo, Jamila lazima aache kazi sasa hivi."
“Hapana, Bw. Nilesh. Tafadhali usinifukuze kazi.” Jamila alisonga mbele na kusihi, "Nahitaji kazi hii."
"Inaonekana hauthamini kazi hii hata kidogo." Nilesh hakuonyesha huruma yoyote, "Baada ya chakula cha mchana, nenda kwa ofisi ya fedha ili ulipwe mshahara wa mwezi huu na mshahara wa miezi mitatu kama fidia."
Wakati huu, Mathew pia alikuja. Alisikia kutoka kwa msaidizi kwamba kuna kitu kilitokea kwenye mgahawa wa kampuni na kukimbilia hapa.
"Bwana Nilesh.” Mathew angeenda kwenye makao makuu kwa mkutano kila robo mwaka. Kwa hivyo, kwa kawaida alimjua Nilesh.
Nilesh alitikisa kichwa, “Nadhani unajua kilichotokea. Unafikiri ninaishughulikia ipasavyo?”
Jamila aliweka matumaini yake kwa Mathew na kusihi, “Bw. Mathew, wewe ndiye unayesimamia tawi hili. Uamuzi wa Bw. Nilesh hauwezi kuwa sawa na wako. Maadamu haukubali kunifuta kazi, bwana Nilesh hawezi kufanya lolote kuhusu hilo. Bw. Matthew, kwa ajili ya miaka yangu katika kampuni, tafadhali nipe nafasi.”
“Nafasi imehifadhiwa kwa wale wanaoithamini. Ni dhahiri kwamba wewe si mtu wa namna hiyo. Nadhani uamuzi wa Bw. Nilesh unafaa. Hata asipofanya, nitafanya hivyo. Kutekeleza moja kama onyo kwa mia moja ndiyo njia bora ya kuwajulisha watu zaidi sheria ni nini! Mathew alikuwa akikazia na kumuunga mkono Nilesh.
Kuona kwamba Mathew alisema hivi, Jamila hakuwa na matumaini hata kidogo.
Mwili wake ukaishiwa nguvu na akaanguka chini.
Kuona hivyo, Lily alijaribu kumsaidia. Kwani, Jamila alikuwa amemsaidia sana na alijua jambo fulani kumhusu.
Lakini Jamila alimvuta kwa nguvu na kukataa kuachia mkono wake, “Lily, nisaidie. Tafadhali nizungumzie jambo mbele ya Bw.
Matthew na Bw. Nilesh…”
“Jamila, hizi ni sheria za kampuni na uamuzi wa Bw. Matthew na Bw. Nilesh. Samahani. Siwezi kufanya lolote kuhusu hilo.” Lily alimtazama Alissa, akimaanisha kuwa Alissa ndiye angeweza kumsaidia Jamila.
Jamila alijua kwamba jambo hili lilitokea kwa sababu ya Alissa. Kwa hiyo, angeweza tu kumwomba Alissa msaada wake.
Lakini kumwomba Alissa msaada ilimaanisha kwamba alipaswa kukiri kwamba alikosea.
Isitoshe, kwa kawaida Alissa hangeweza kumsaidia. Aliogopa kuwa Alissa atamcheka tu. Hata angefedheheshwa na Alissa, alishindwa kuendelea na kazi hiyo na angewachekesha watu wengi zaidi.
“Lilly, inabidi unisaidie. Nilifanya yote kwa ajili yako. Nimesema maneno hayo kwa niaba yako.” Mtu pekee ambaye Jamila angeweza kuomba msaada alikuwa Lily.
Lily alikasirika, “Sikukuuliza useme hivyo. Kwa nini unanipanga?”
“Mimi … hufikiri hivyo? Ulisema Alissa alikuwa mpenzi wa Bwana Mathew…”
“Unaongea ujinga gani? Sikusema lolote!” Lily aliona kwamba Jamila alianza kuongea bila maneno ya uangalifu na aliogopa kwamba Jamila angesema zaidi dhidi yake, “Upuuzi wako una faida gani kwako? Ukipoteza kazi hii, unaweza kupata nyingine. Kwa nini unafuata kisasi dhidi yangu?”
“Ndiyo, Jamila.” Neema alisogea mbele ili kumsaidia Jamila na kuchukua nafasi hiyo kupunguza sauti yake, “Haitakufaa kusema zaidi. Acha kusema nitamwomba Lily amshawishi Bwana Ernest akutafutie kazi. Acha ujinga sasa."
Jamila hakuwa na budi ila kufanya hivyo. Vinginevyo, ikiwa kweli angemchukiza Lily, hangeweza kuwa na kazi nzuri.
Hivyo, Lily, Neema na Jamila waliondoka kwanza, na watu katika mgahawa pia waliondoka mmoja baada ya mwingine.
Nilesh na Alissa pekee ndio walikuwa wamebaki kwenye mgahawa huo.
"Alissa, sikukuona kwa muda mrefu." Sauti ya kupendeza ya Nilesh ilisikika katika mkahawa huo tulivu, na kuwafanya watu wajisikie vizuri.
"Ndio, hatujaonana kwa muda mrefu." Alissa alipumua muda huo akaruka.
Alissa alimtazama Nilesh ambaye alikuwa hajamuona kwa muda mrefu. Ilikuwa kana kwamba alikuwa amerudi nyuma katika miaka ambayo walikuwa wakifanya kazi pamoja.
Nilesh alikuwa amerimbikiza kazi fulani kutokana na kulazwa hospitalini. Ilibidi atumie wakati mwingi kuzishughulikia. Kwa hivyo, alipata tu wakati wa kuja kumuona Alissa katika Jiji la Mwanza baada ya siku hizi.
"Ulisisitiza kuhamia Mwanza. Je, haya ndiyo uliyoyataka?" Nilesh alipofika tu, aliona watu walivyokuwa wanamnyanyasa, wakimpa hasira na kufadhaika.
"Bwana Nilesh, unatawala sana wakati huu." Alissa alionyesha kumshukuru. Hajawahi kumuona Nilesh asiye na huruma kama huyo, "Karibu nilifikiri wewe sio Nilesh niliyemjua."
"Kuna ubaya gani kuwa mtu mbaya kwa ajili yako?" Nilesh hakujali watu walimfikiria nini. Alitaka tu kumlinda mpenzi wake.
Alissa alikutana na macho ya joto ya Nilesh. Lakini hakustahili utunzaji aliompa. Kwa sababu hakuweza kujibu upendo wake. Hilo lilikuwa jambo baya zaidi kwake.
"Sistahili." Alissa akamkumbusha kwa mara nyingine.
“Nilisema ni kazi yangu iwe unastahili au hustahili. Huhitaji kuhisi kulemewa.” Nilesh alitaka tu kuwa mzuri kwake.
"Nilesh, lazima nikuambie kitu."
Sura ya 155
Alissa alimtazama Nilesh kwa umakini huku akiwa na mwanga machoni mwake. Alionekana mgumu na thabiti.
"Nisikilize kabla ya kusema, sawa?" Nilesh alisema kwa upole.
“Sawa. Wewe sema kwanza." Alissa akaminya midomo yake, akimpa nafasi na kuonyesha heshima.
Nilesh alikaa mkabala na Alissa. Nje ya dirisha, miale michache ya mwanga wa jua ilimwangukia uso wake mzuri, na kumfanya aonekane mpole na mrembo kiasi kwamba watu hawakuthubutu kumkufuru.
"Kwanini usiniulize sababu iliyonifanya nije Mwanza?" Nilesh aliuliza kwa kejeli.
"Safari ya kibiashara? Ili kuhudhuria mkutano? Au kuniona?” Alissa alikisia.
“Jambo la kwanza ni kukuona. Pia ni safari ya biashara. Isitoshe, niko hapa kuhudhuria karamu.” Nilesh alibadilisha mpangilio wa mambo aliyosema.
“Basi utakuwa hapa kwa siku chache. Je, kuna mahali popote unapotaka kwenda? Naweza kuwa kiongozi wako.” Alissa alitaka kutekeleza majukumu ya mwenyeji. Hii pia ilikuwa malipo madogo kwa utunzaji wa Nilesh kwa miaka mingi.
“Nilikuwa nakuja Mwanza. Lakini kila mara nilikuja na kuondoka kwa haraka. Wakati huu, nataka kutazama vizuri na kuona jiji hili ambalo ulikulia." Nilesh alitaka kujua zaidi kuhusu maisha yake ya zamani na hata alitaka kuhudhuria maisha yake ya baadaye, “Bila shaka unapaswa kunitunza. Hili ni eneo lako.”
"Hakuna shida." Alissa alisema.
“Alissa, nitakaa Mwanza kwa wiki moja. Mwezi mmoja baadaye, nitakuwa mwenzako tena.” Hoja ya Nilesh ilikuwa hii.
Alissa alichanganyikiwa kidogo, “Sisi si wenza sasa pia. Hatuko mahali pamoja.”
“Hicho sicho ninachomaanisha. Nimewasilisha ombi la uhamisho. Ninataka kuja Mwanza niwe upande wako." Nilesh alitabasamu, “Alissa, tafadhali nipe ushauri wako wakati huo.”
“Nilesh, usifanye hivyo. Familia yako, marafiki na watu unaowasiliana nao wote wako Dar. Utapata maisha bora ukiwa Dar. Usimwachie mwanamke kila kitu ulicho nacho. Ni kweli si thamani yake. Sitajisikia furaha kwa wakati utafanya hivyo, lakini huzuni, unajua?"
Alissa alijua vyema kwamba Nilesh angeshushwa cheo tu ikiwa angeondoka makao makuu ya Universal Group na kuja Mwanza. Kwani, Matthew alikuwa meneja mkuu katika tawi la Mwanza. Ikiwa Nilesh alngehamishwa, hangeweza kumshusha Matthew, vinginevyo labda Matthew angehamishwa. Hata kama bado angekuwa meneja wa tawi hilo baada ya kuhamishwa, bado haikuwa nzuri kama nafasi ya mkurugenzi wa miradi aliyokuwa nayo katika makao makuu.
“Alissa, sikuweza kukushikilia ulipoamua kuondoka hapo awali. sasa, nitakuja kuambatana nawe. Hii ni dhamira yangu.
Sikufurahi hata kidogo baada ya wewe kuondoka. Kuangalia mtu mwingine ameketi kwenye kiti chako cha zamani, nilifikiri nifanye jambo fulani. Hivyo ndivyo mwanaume anapaswa kufanya.” Nilesh alikuwa ameamua.
"Alissa, hata nikiangalia sura yako na tabasamu lako kila siku, najisikia mchangamfu. Unaelewa?"
“Nilesh, ninaelewa. Lakini tafadhali acha kuwa mzuri kwangu. Usiwe mjinga sana kuacha kila kitu ulicho nacho kwa ajili yangu… samahani. Ninakuchukulia kama rafiki tu." Alissa akashusha pumzi ndefu na kudhibiti sauti na hisia zake.
Hakutaka kumuumiza Nilesh. Lakini ilimbidi aseme maneno haya na hakuweza kuepuka kumuumiza. Hata ikiwa ilikuwa ngumu kusema, ilibidi aseme. La sivyo, ingelemea dhamiri yake na ingemwangamiza pia Nilesh.
Hata kama angemchukia, alikuwa mwadilifu.
"Alissa, naweza kukusubiri." Wakati wake ulikuwa kwake tu, “Nimengoja kwa miaka minne na sijali kuhusu miaka minne ijayo…”
“Huwezi.” Macho ya Alissa yalikuwa mekundu, “Mimi … nimeolewa.”
Sauti yake ilikuwa nyororo sana, ambayo ilikuwa kama kipepeo anayeruka. Lakini ilifika masikioni mwa Nilesh na kumshtua.
Alikaa tu. Kulikuwa na jua. Lakini hakuweza kuhisi hata chembe ya joto.
Ni wazi ilikuwa siku ya jua. Lakini alihuzunika sana hivi kwamba ilikuwa kana kwamba mvua ingenyesha sekunde inayofuata.
Alissa naye hakusogea. Wawili hao walikuwa kama jozi ya sanamu. Muda ulikuwa umeganda na alionekana kuwa ameanguka katika ulimwengu wa barafu na theluji. Nilesh alitetemeka kwa baridi.
Baada ya kungoja kwa muda mrefu, Alissa alishindwa kustahimili mazingira yaliyowazunguka na akasema kidogo, "Nilesh, uko sawa?"
"Alissa, unanidanganya, sivyo?" Nilesh alilazimisha tabasamu kwa kutoamini, “Hutaki nicheleweshe kazi yangu na kuwaacha wazazi na marafiki zangu. Kwa hiyo, unasema mambo kama hayo ili kunidanganya, sivyo?
“Niambie unasema uongo na hujaolewa. Hutaki nikusumbue hivi, sivyo?”
"Hapana." Alissa alikuwa na hisia tofauti, “Nimeolewa kweli. Sikudanganyi, na sitaki kukudanganya.
“Usiseme hivyo kukuhusu pia. Hukunisumbua. Ni kwamba sistahili upendo na utunzaji wako. Nilesh, katika maisha haya, wewe ni rafiki yangu na mshauri wangu. Lakini yeye ndiye ninayetaka kutumia maisha yangu na ninampenda."
Nilesh akanyamaza tena. Macho yake yakawa yamefifia kabisa. Alionekana mwenye uchungu sana hivi kwamba alikuwa tofauti kabisa na hapo awali.
"Nilesh, samahani."
Hata milioni moja ya msamaha isingeweza kuponya majeraha yake.
Nilesh akatulia taratibu na kutabasamu kidogo. Alionekana baridi na mwenye huzuni, “Hakuna haja ya kusema samahani. Labda hii ndiyo hatima." Ni Mungu ambaye hakutaka wawe pamoja. Aliweza tu kujisikia vizuri kwa kufikiria hivyo.
"Ni kosa langu kukufanya ubebe shinikizo hili." Alissa hakujua la kusema. Nilesh alikuwa hivyo kila wakati. Hata alipoumizwa, hakutaka ajilaumu kwa hilo.
“Hakuna shinikizo. Ni heshima.” Ilikuwa heshima kwamba mtu bora kama huyo alimpenda.
“Yeye ni nani?” Nilesh alikunja ngumi, akijizuia.
"Ni mtu unayemfahamu." Alissa alisema, "Kendrick."
“Kendrick?” Nilesh alishtuka, kisha akatoa tabasamu la utulivu, “Ni jambo lisilotarajiwa na la busara. Mimi sikutegemea kabisa.”
Alikaa na Alissa kwa miaka minne na Alissa alimchukulia kama rafiki tu. Alissa na Kendrick walikuwa wamefahamiana kwa muda usiozidi miezi mitatu tu, lakini wangeweza kuoana na kutumia maisha yao pamoja.
Je, asingewezaje kuwa na wivu na huzuni?
"Kwa kweli, tumefahamiana kwa muda mrefu." Alissa alijua kile Nilesh alikuwa akifikiria na polepole alizungumza juu ya siku za nyuma, "Miaka mitatu iliyopita ... Kwa hivyo, tumeanzisha uhusiano hivi majuzi. Nilesh, najua nilipaswa kukuambia kuhusu uhusiano wangu naye. Lakini sikuweza kwa sababu ya vikwazo vya mkataba. Sikutarajia kwamba mambo yangetokea hivi … nilimpenda, na pia alikuwa na hisia kwangu.”
"Haya ndiyo matokeo bora zaidi. La sivyo, ningempiku.” Nilesh alihisi kitulizo baada ya kusikiliza alichosema, “Ninaweza kuja lini kwenye harusi yako?”
“Bado hatujaamua. Lakini urasmi haujalishi. Kilicho muhimu ni dhamira ya kuwa pamoja.”
"Uko sahihi. Lakini akikutendea vibaya, nitakuondoa na sitampa nafasi tena.”
Sura ya 156
Alissa alijisikia raha baada ya kumwambia Nilesh kila kitu. Walifaa zaidi kuwa marafiki kuliko wapenzi.
“Sijamwona Doris kwa muda mrefu. Vipi nimchukue na wewe kutoka shuleni baada ya kazi na kwenda kula chakula cha jioni?" Nilesh alipendekeza.
Alikuwa akimpenda sana Doris zaidi ya Kendrick. Lakini Kendrick alikuwa baba yake Doris. Hapa ndipo mahali ambapo Kendrick alikuwa na faida zaidi ya Nilesh. Kwa hivyo, Doris alihisi Kendrick alikuwa mkarimu mara ya kwanza walipokutana.
"Sawa." Alissa alikubali.
Nilesh, ambaye alikuja tu Mwanza, alikuwa mgeni, na Alissa alikuwa mwenyeji. Kwa hivyo, kwa kawaida angepaswa kutekeleza majukumu ya mwenyeji.
Mbali na hilo, Nilesh hakuwa bosi wake tu, bali pia rafiki yake. Alikuwa amemtunza kwa miaka mingi na alikuwa na deni kubwa kwake. Alipaswa kumlipa. Chakula kinaweza kuonyesha fadhili zake.
Kwa njia hiyo, Alissa na Nilesh walifanya mipango. Nilesh aliondoka na kwenda kwa Mathew kuzungumza juu ya mambo kadhaa.
Baada ya kumaliza kuongea, Nilesh hakutoka akakaa kwenye sofa ofisini kwa Mathew akinywa chai.
"Bwana Nilesh na Alissa wanafahamiana sana.” Mathew alichukua birika na kumimina chai kwenye kikombe chake.
“Ndiyo.” Nilesh hakuwa na haya, "Nilifikiri alikuwa wa pekee sana tangu alipojiunga na kampuni. Ana mawazo maalum na talanta katika kazi. Kwa kuthamini talanta yake, nilimpa nafasi na aliitumia vizuri sana.
"Kwa kweli Alissa ni mchanga na ana talanta." Mathew naye alifikiri hivyo.
"Sikutarajia angerudi Mwanza. Kwa hivyo, tafadhali umtunze katika siku zijazo, Bw. Matthew." Nilesh alifikiri kwamba angeweza kumhifadhi Alissa kwa maisha yake yote. Hakutarajia kumwacha.
” Usiseme hivyo, bwana Nilesh. Alissa ni mzuri sana na ana uwezo. Hahitaji matunzo ya wengine hata kidogo.” Matthew alikuwa akisema ukweli, “Bila shaka, nitamtendea kwa fadhili talanta kama yeye.”
Kama msimamizi, bila shaka alitaka kuweka wafanyikazi wake bora. Wakati kama mfanyakazi mwenza, kwa kawaida alipaswa kujiweka mbali na Alissa.
Baada ya yote, Kendrick na Alissa walikuwa na utata kwa kiasi fulani. Hakutaka kuwa mwiba kwa Kendrick.
“Samahani kumsumbua Bwana Matthew kuanzia sasa.” Nilesh akanyanyua chai yake kama zawadi.
Mathew naye aliinua chai yake kwa malipo. Baada ya kunywa chai hiyo tamu, aliinuka, “Jisikie nyumani bwana Nilesh. Naenda kazini sasa hivi.”
"Sawa." Nilesh aliitikia kwa kichwa na kunywa chai yake, akisubiri hadi Alissa atakapotoka kazini.
Nilesh aliona kuwa muda ulikuwa umekaribia. Mathew naye alikuwa tayari anafungasha vitu vyake.
"Alissa anaenda kumchukua binti yake baada ya kazi. Bwana Nilesh itaambatana naye?” Mathew alichukua koti la suti nyuma ya kiti na kuivaa.
“Ndiyo. Sijamuona Doris kwa muda mrefu.” Nilesh alikuwa mpole zaidi huku akimtaja Doris.
Mathew alienda kwa Nilesh. Kwa kawaida alisafisha pingu za shati lake jeupe na sehemu ya ziada ya pingu za suti na kuonekana mpole.
“Mwanangu yuko darasa moja na binti wa Alissa. Kwa nini tusiende pamoja huko?” Mathew alisema.
“Twende zetu.” Nilesh alitoka na Mathew akafuata.
Walienda kumtafuta Alissa mara tu Alissa alipotoka. Matthew alitabasamu na kusema, “Tunaenda hukohuko. Kwa hiyo, twende tukawachukue watoto pamoja.”
Alissa akaitikia kwa kichwa. Wote watatu walichukua lifti hadi kwenye maegesho ya chini, ambapo Alissa aliiendea Range Rover yake nyekundu na kubonyeza ufunguo wa kufungua milango.
Nilesh kwa kawaida alivutiwa na gari lake la kupendeza la kisasa. Akausogelea na kuuvuta mlango na kukaa ndani yake.
“Jifunge mkanda wako wa kiti.” Alissa alimkumbusha.
Mathew aliendesha gari lake kwanza, na kisha Alissa akafuata.
"Inaonekana anakupenda na mkarimu sana." Nilesh alidhani gari hilo ni zawadi kutoka kwa Kendrick kwa Alissa.
Alissa alitunza pesa na hangepoteza pesa zake kwa usafiri wa gharama kubwa kama huo. Pili, mapato yake hayakumtosha kununua gari la gharama kubwa kama hilo. Kwa hivyo, hakuweza kufikiria sababu yoyote kwa nini angekuwa na gari la kifahari muda mfupi tu baada ya kurudi Mwanza na aliweza kumfikiria Kendrick tu.
Alissa alijivunia sana na hakuwahi kupokea zawadi kutoka kwa mtu yeyote bila sababu. Hakutaka kuwa na deni kwa mtu yeyote, ikiwa ni pamoja na yeye.
Ila alikubali gari la Kendrick kumaanisha alimkubali sana Kendrick na hakumchukulia Kendrick kama mtu wa nje.
Nilesh alihisi kuwa mgumu na mwenye uchungu. Alikuwa amechelewa sana baada ya yote.
"Hakuninunulia yeye." Alissa alijua angeelewa vibaya na akaeleza, “Nilifika nyumbani na kukuta dada yangu alikuwa na gari zuri sana. Kwa hiyo, nilimwomba baba yangu aninunulie pia. Hiyo ilikuwa haki.”
Nilesh alishtuka, hakutarajia baba yake Alissa angekuwa tajiri kiasi hicho, “Baba yako ni nani?”
“Haijalishi yeye ni nani hata kidogo. Kilicho muhimu ni kwamba anipe kile ninachostahili.” Alissa hakutaka kumtaja baba yake ni nani. Lakini, hakukuwa na uhusiano wa kifamilia kati yao. Ingefanya watu wacheke tu.
Nilesh hakuuliza maswali zaidi. Kwa kuwa hakutaka kusema hivyo, hakuuliza.
Alissa hakuendelea na mada. Muda si mrefu, walifika katika shule ya chekechea.
Gari lake lilikuwa limeegeshwa nyuma ya lile la Mathew. Walishuka kwenye gari na kuingia chekechea wakiwa na cheti. Kisha, wakaenda darasani na kuwachukua Doris na Walter na kuachana kwenye lango.
Walter alichukia kuachana na Doris. Alissa aliwaalika, “Mr. Mathew, kwa nini usiende kula chakula cha jioni pamoja nasi?”
“Sahau muda huu. Bw. Nilesh huja Mwanza mara chache. Ni lazima nyie muwe na mengi ya kusema, sitawasumbua. Kutakuwa na fursa kwangu kumualika Bw. Nilesh na wewe kwenye chakula cha jioni.” Mathew alikuwa na busara na hakutaka kujisumbua na kuharibu uhusiano kati yao.
"Walter, sema kwaheri." Mathew alimvuta mwanae.
Walter akamwambia Doris, "Kwaheri."
Pamoja na hayo, waliondoka. Alissa alimpeleka Doris kwenye gari.
"Unataka kula nini?" Alissa alimuuliza Nilesh.
"Mgeni anapaswa kuendana na urahisi wa mwenyeji. Chochote unachotaka, nitakula.” Nilesh hakuwa mchaguzi. Alitaka tu kutumia muda zaidi pamoja naye.
Alissa kisha akaendesha gari hadi kwenye mgahawa mzuri wenye mpangilio mpana na rahisi, ambao uliwafanya watu wajisikie vizuri.
Ghorofa ya kwanza ilikuwa ukumbi. Ghorofa ya pili, ya tatu na ya nne vilikuwa vyumba vya watu binafsi.
Waliketi sebuleni na walikuwa karibu na dirisha la ua wa ndani. Nje, kulikuwa na mianzi ya kijani na mtazamo hapa ulikuwa mzuri.
Alissa alimwomba Nilesh aagize, lakini alimruhusu afanye uamuzi.
Alissa kisha akaagiza sato watatu wakukaangwa na chips, ambayo iliwafaa.
Aliagiza vinywaji na kuzungumza na Nilesh huku akisubiri vyakula.
Hawakugundua kuwa kuna mtu alikuwa akiwatazama kwa muda kwenye ngazi na alikuwa ametoa simu yake ya mkononi kutafuta pembe za hila za kupiga picha.
Alissa na wale wengine wawili hawakuliona kabisa. Kisha, vyakula vilitolewa.
Sura ya 157
Doris, kula zaidi samaki, hawa samaki ndiyo unaowapenda zaidi." Alissa akampa Doris mnofu.
“Sawa.” Doris alikula kimya kimya.
Alissa alimkaribisha Nilesh, “Furahia. Huwezi kufika Mwanza na usile sato. Ikiwa huzipendi, agiza nyingine.”
"Zote zinaonekana vizuri sana." Nilesh alifikiri kwamba vyakula hivyo vilikuwa vya kupendeza na chakula kilikuwa kitamu, jambo ambalo liliamsha hamu yake ya kula.
Nilesh alikula samaki hiyo na akafikiri ilikuwa tamu.
Alissa alikuwa ametoka kula chakula mara ujumbe ukaingia kwenye simu yake kutoka kwa Kendrick.
Kendrick: [uko wapi?]
Alissa alikuwa na hofu kidogo. Lakini hakuthubutu kufikiria sana. Kwa hivyo, alijibu: [Natoka kazini. Wewe uko wapi?]
Kendrick akajibu haraka haraka: Niko kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza.
Mkono wa Alissa ulikuwa dhaifu na nusura adondoshe simu: [Unakuja Mwanza tena? Mbona hukuniambia mapema?]
Kendrick: [Nilitaka nikupe surprise tu.]
'Siyo mshangao, lakini mshtuko, sawa?' Alissa alijiwazia na kujaribu kutulia.
"Nini tatizo?" Nilesh alimuona Alissa akiitazama simu yake. Kitu kilionekana kuwa kibaya.
“Hakuna kitu.” Alissa alimtazama Nilesh na kuendelea kumjibu Kendrick: [Hakika ni mshangao.]
Kendrick alisema tena: Ndo nimeshuka tu na sikupanga gari kuja kunichukua. Njoo unichukue, sawa?
Angewezaje kuondoka sasa? Hangeweza kumwacha Nilesh tu na kwenda zake.
Vinginevyo, Nilesh angefikiria nini kuhusu hilo? Angekuwa mwanamke ambaye alipendezwa zaidi na mumewe kuliko marafiki.
Alissa alijibu huku akitegemea Kendrick asingesisitiza: [Siwezi kuondoka sasa hivi. Unaweza kuchukua teksi hadi hoteli. Nitakuja kwako baadaye.]
Kendrick "alihuzunishwa" sana kama alivyotarajia: [Ni nini muhimu zaidi kuliko mume wako? Bi. Mayala, unataka kukataa kutekekeza jukumu lako?]
Alissa akashusha pumzi kidogo, akimtazama Nilesh upande wake. Ilionekana kwamba angeweza tu kusema ukweli. Isitoshe, yeye na Nilesh walikuwa marafiki wasio na hatia. Ilikuwa kawaida kwa marafiki kula chakula cha jioni pamoja.
Alissa alipima maneno yake: ,[Nilesh amekuja hapa Mwanza kikazi. Ningependa kutekeleza majukumu ya mwenyeji na kumshukuru kwa kunitunza miaka hii yote.]
Sekunde kumi, nusu dakika, dakika…zilipita dakika mbili na Kendrick hakujibu.
Alissa alihisi kuwa muda wa kusubiri ulikuwa ukiongezeka na alikuwa na wasiwasi kidogo.
Alituma ujumbe: [Je! una hasira? Bw. Nilesh anakuja Mwanza kwa mara ya kwanza. Yeye ni rafiki yangu na bosi wa zamani. Ninapaswa kukutana naye na kumwalika kwenye chakula cha jioni. Hata hivyo, sikufanya chochote kibaya. Ikiwa una hasira, sina la kusema.]
Alissa hakukubali, lakini alizungumza mawazo yake vyema.
Kendrick bado hakujibu. Alissa hakumsubiri. Katika chakula cha jioni na marafiki, ilikuwa ni kukosa heshima kuendelea kuzungumza kwenye simu.
Nilesh pia aliweka uma chini na kumtazama Alissa ambaye alikuwa akitazama simu na hakula, "Alissa, ikiwa kuna chochote, sema tu."
Nilesh aliweza kusema kutoka kwa uso wake kwamba alikuwa na wasiwasi juu ya jambo fulani.
“Mimi…” Alissa alipokuwa karibu kuongea wakati ujumbe ukaingia kwenye simu yake, “Subiri kidogo.”
Akabonyeza ujumbe kutoka kwa Kendrick. Ilikuwa na picha chache zake na Nilesh katika mgahawa huu.
Pembe ya picha ilikuwa ngumu. Kwa hiyo, ilionekana kana kwamba walikuwa na utata kidogo.
Alissa alikunja uso. Ilionekana kuwa kuna watu ambao hawakumpenda katika mgahawa huu waliwaona, au mtu alikuwa akimfuatilia.
Ikiwa ilikuwa ya kwanza, basi mtu nyuma ya hii alikuwa anatisha sana. Mtu huyo lazima atake kumfanya Kendrick amuue.
Haishangazi Kendrick alituma ujumbe kama huo akiuliza yuko wapi wakati huu. Ilionekana kuwa alipokea picha hizo mapema.
Kendrick: [Nilifikiri hungeniambia kuwa Nilesh alikuwa na wewe. Lakini kwa vile uliniambia, sina hasira na wewe. Ana bahati sana kwamba Bi Mayala anaweza kula chakula cha jioni pamoja naye. Isitoshe, sikuja Mwanza, nilikuwa nakuzingua tu.
Kendrick alikuwa anamjaribu tu kama atasema ukweli.
Alissa akajibu: [lini umeanza tabia mbaya hivyo? Hata ulinidanganya hivi?]
Kendrick: [Unadhani sijui Nilesh anawaza nini? Je, ni lazima niwe mtu wa kutojali na mkarimu ninapomwona anamfukuzia mke wangu?]
Alissa aliweza kufikiria kuwa Kendrick alikuwa akiinua nyusi zake kwa dharau pale.
Alissa: [Ni chakula tu. Nina deni kubwa kwake na lazima nimrudishie fadhila. Mbali na hilo, Doris pia yuko pamoja nasi. Una wasiwasi gani? Bila Nilesh, hakungekuwa naye sasa.]
Kendrick akajibu: [Niko kwenye ulinzi dhidi yake, sio wewe. Nitamlipa kwa ajili yako kama mume wako. Unaruhusiwa kujitolea kufanya tena. Hata ikibidi ufanye, lazima niwepo pia.]
Alissa: [Nitaripoti kwako mapema, sawa? Lakini ulinidanganya. Unafikiri nifanye na wewe?]
Kendrick: [Nitaoga na nilale kitandani upendavyo.]
Alissa alikunja pua yake nzuri. Yeye hakujali, sawa?
Hatimaye Alissa akajibu: [Lazima nile vya kutosha ili nipate nguvu. Usisumbue chakula changu cha jioni. Wacha tuzungumze juu yake baada ya kurudi nyumbani. Kwaheri.]
Alissa kisha akaiweka simu yake pembeni na wala hakujishughulisha kusoma meseji zozote.
Nilesh bado alikuwa akisubiri majibu yake.
“Alijua uko Mwanza na tunakula chakula cha jioni pamoja. Kwa hiyo, aliniruhusu nikutendee mema.” Alissa alikuwa anasema uwongo tu.
Nilesh alitabasamu, "Ninaogopa hii sio kutoka kwa Bwana Kendrick, lakini kutoka kwako kwa ajili yake."
Alimfahamu vyema Kendrick. Kendrick hatawahi kusema maneno ya upole kama haya. Lilikuwa neno la fadhili kutoka kwa Alissa ambaye alitaka 'waelewane'.
Alissa aliendelea kutabasamu, “Alisema mengi. Lakini ndivyo alivyomaanisha kwa ufupi.”
“Alijua ninakula chakula cha jioni na wewe hapa. Hajakuaibisha?” Nilesh hakutaka kumsumbua, "Naweza kumuelewa."
"Hakuna haja. Nimeweka wazi, na hakuniaibisha.” Alissa hakutaka kusema kwa Kendrick nia ya wao kula chakula cha jioni pamoja.
"Alissa, ikiwa anakutendea vibaya, mimi ..."
Alissa akamkatisha, "Hebu tuharakishe na tule chakula chetu, au kitakuwa baridi na kuathiri ladha." Alibadilisha mada na kumpa Nilesh msisitizo wa kula.
Nilesh alisisitiza kumaliza maneno yake, “Alissa, nitafurahi ikiwa utaishi maisha ya furaha. Ikiwa sivyo, sitaki mtu yoyote akudhuru, hata kama mtu huyo ni Kendrick.”
“Sidhani kama mimi ndiye nitajiumiza. Nilesh, usijali. Najua ninachopaswa kufanya. Haijalishi nini kitatokea kwangu na Kendrick mwishowe, sitawahi kukudurika. Unaelewa?" Alissa aliogopa tu kwamba Nilesh angebaki hivi kila wakati. Ikiwa ndivyo, angehisi hatia.
“Hupaswi kuyatoa maisha yako kwa ajili yangu. Nilesh, tazama mbele. Furaha inakungoja sio mbali."
"Wacha tuwe marafiki maishani, sawa?"
Sura ya 158
Alissa alitoa maoni yake kwa dhati na kwa uthabiti. Alitaka tu Nilesh aache wazo la kumngoja milele.
Maisha yalikuwa mafupi kama miongo ya miaka. Aina hii ya dhabihu ilikuwa tu kupoteza muda na maisha, ambayo kwa kweli haikuwa ya haki kwake.
Mtu anapaswa kuishi maisha kwa busara zaidi. Kupenda kwa kila nyuzi ya nafsi yake wakati kuna mtu wa kupenda, na kujipenda mwenyewe wakati hakuna.
Nilesh alijua kwamba Alissa alikosa amani kwa sababu alitaja hilo tena, “Alissa, samahani. Nilisema hivyo kwa kukata tamaa kabisa. Ni sawa tuwe marafiki kwa maisha yote, lakini usitilie umuhimu zaidi kwa mpenzi wako kuliko rafiki."
"Bila shaka hapana." Alissa alitabasamu kwa utulivu, na aliamini Nilesh angetimiza ahadi yake.
"Vizuri." Nilesh akachukua glasi ya kinywaji kutoka mezani.
Alissa naye akachukua glasi na kugonganisha naye. Walisema kwa mtiririko huo.
"Uwe na furaha."
"Urafiki wetu na udumu milele."
Baada ya kuongea walikunywa na kula, wakitazamana huku wakitabasamu.
Baada ya chakula, Nilesh alikuwa karibu kulipa bili wakati Alissa alipomsimamisha, “Hii ni Mwanza, ninapoishi, na mimi ndiye mwenyeji. Ukilipa bili, nitakasirika na hatuwezi hata kuwa marafiki katika siku zijazo.”
Kwa hivyo, Nilesh alikubali. Alissa alilipa bili na kujisikia furaha sana, akihisi kwamba amepunguza mzigo wa fadhila ambazo Nilesh alimdai.
Alissa alimrudisha Nilesh kwenye Hoteli aliyofikia, na akaendesha gari kurejea nyumbani pamoja na Doris.
Alissa na Doris walisoma vitabu kwa muda. Kisha Alissa akamuogesha Doris, akambembeleza hadi akalala na kwenda kumuona bibi kama kawaida yake...
Ilikuwa karibu saa 10:00 usiku alipopanda ghorofani kwenda kulala. Kendrick akampigia simu.
“Mbona hujanijibu kwa muda mrefu hivyo?” Kendrick aliuliza.
“Unataka kuanzisha ugomvi?” Alissa alisimama kwenye kibaraza cha ghorofa ya pili.
Kendrick alipigwa na butwaa, na kuwaza kwa sekunde chache, “Unataka kufanya nini?”
“Mimi na yeye ni marafiki tu. Tumekula tu pamoja. Je, unanitilia shaka sasa? Nimeacha mambo mengi kwa ajili yako. Huniamini?” Alissa alihisi huzuni na hasira kidogo.
Ikiwa Kendrick bado hakujua ni nini kilikuwa kimetokea kusikia hivyo, basi alikuwa mjinga sana.
"Bi. Mayala alicheza mchezo mzuri sana." Kendrick alitabasamu kidogo, "Ninahitaji kujibu nini ili kukusaidia kucheza vizuri zaidi?"
"Unamaanisha nini?" Alissa aliuliza huku akishtuka sana, “Utanitelekeza? Kwa nini? Si ulisema ingawa huwezi kunitajia jina la mke wako, utanitendea mema kama mkeo na kamwe hutaniacha?”
"Hapana, tuachane." Kendrick alishirikiana naye, baada ya kuelewa kile Alissa alimaanisha.
“Sitaki kuachana, na sihitaji kujua jina la mkeo. Nataka tu kubaki na wewe.” Alissa alimsumbua, "Sitaogopa hata kama anajua."
"Nilichosema hakitabadilika kamwe, na hatuna uhusiano katika siku zijazo."
"Nini? Vipi kuhusu ujana wangu wa miaka mingi? Je, utarudi upande wake? Ungewezaje kunidanganya? Sitakubali kamwe…”
"Matokeo yake ni sawa ikiwa unakubali au la."
“Siwezi kukupoteza… Usikate simu… wewe…” Alissa alishusha earphone masikioni na kuitazama huku akisema kwa meno ya kusaga, “Mwanaharamu!”
Alissa alikasirika sana hadi akahisi kuishiwa nguvu, mikono ikiwa kwenye uzio, na macho yake yakawa mekundu.
Mtu mwembamba alitembea karibu polepole, hadi akasimama mbele ya Alissa.
“Alissa, uko sawa?” Melissa alikuwa na wasiwasi juu yake.
“Hakuna kitu.” Alissa alijizuia kutokwa na machozi, akarudi kwenye sura yake ya baridi.
“Nimesikia unaonekana umegombana na mtu. Lakini Alissa, usifikirie sana. Nilishuka tu kunywa maji nikasikia sauti yako kali, nikaja kutazama. sijaelewa chochote.” Melissa alijieleza.
"Ni wewe unayehangaika sana. Sasa nina furaha sana kila siku. Nitagombana na nani?" Alissa alihamisha nywele zake kutoka mbele hadi nyuma ya bega kwa umaridadi, akionyesha shingo yake nzuri na maridadi, "Umesikia vibaya."
“Labda nimesikia vibaya. Sisikii vizuri kwa sababu ya kuwa mjamzito. Alissa pia umezaa na Doris nadhani umenielewa, au sivyo? Utakuwa na hasira na mimi?" Melissa akampa glasi, "Unataka kunywa maji?"
“Melissa, huoni ni uchafu? Kwanini unafanya hivyo.” Alissa alitazama juu kwa kidevu kilichoinuliwa kidogo, “Nenda tu kulala mapema. Ikiwa mwanamke hatapata usingizi wa kutosha akiwa mjamzito, ni rahisi sana kupata mikunjo na kuonekana mzee.”
"Mbali na hilo, ni rahisi kupata siasma na kunenepa… Mwanamke atashushwa hadhi mara tu akiwa mjamzito, na atakuwa na ugonjwa wa siasma mbaya, na ngozi iliyolegea baada ya kuzaa… Inachukiza sana.”
"Ingawa wewe ni mrembo wa kuzaliwa, ninaogopa huwezi kukwepa sheria ya asili. Wanaume ni wanyama wenye hisia, na watatoa macho zaidi kwa wanawake wachanga na warembo wenye umbo la kuvutia la mwili. Afadhali uzingatie zaidi mumeo. Unakuwa mzito siku baada ya siku. Katika siku za upweke… Mume wako angefanya nini? Unapaswa kuwa mwangalifu ili usimruhusu kutongoza mwanamke mwingine. Ikiwa ndivyo, juhudi zako zote zitabatilika.”
Alichokisema Alissa kiliufanya uso wa Melissa kubadilika rangi. Alissa alimkumbusha Melissa kwamba Melissa alimnyang'anya Seidrick, na ingetokea pia kwa Melissa.
“Alissa, una wasiwasi sana. Haitatokea kamwe.” Melissa alijiamini sana, lakini alisema kwa ngumi zilizofungwa kwa nguvu, "Ninataka kupendekeza uweke nafasi yako."
“Sina busara kama wewe. Nimechoka na ninaenda kulala.” Alissa aliondoka kwa hatua za kifahari na zisizo na wasiwasi. Umbo lake jembamba na refu lililopungua bado lilikuwa la kuvutia sana.
Lakini nini? Labda alikosana na Kendrick. Kumpoteza Kendrick kama mlinzi, angeridhika hadi lini?
Anachopaswa kufanya Melissa sasa ni kuweka kipaumbele zaidi kwa Seidrick. Hakuweza kumruhusu Alissa kumnyang'anya Seidrick kwa sababu alikuwa mjamzito.
Ilibidi atafute nafasi ya kumfanya Alissa awe na sifa mbaya kama miaka 5 iliyopita, na hivyo kumfanya Alissa asiinuke tena.
Alissa alipoingia tu chumbani, akampigia tena Kendrick, Kendrick akaitikia haraka.
"Melissa alikuwa karibu nami sasa hivi."
"Kwa hivyo uliigiza kuachwa na mimi ili kumchanganya?"
“Ndiyo. Ikiwa amefanya kitu kwenye zile picha, basi matokeo haya yatamfanya kupata kile anachotaka." Alissa aliketi kwenye kiti cha mkono, akisema kwa miguu iliyovuka, "Basi nitamsaidia."
"Niamini. Tutajua kama ni yeye au la hivi karibuni." Kendrick akasema, “Dada yako ana hila sana. Lazima kuwe na mtu anayemfundisha somo zuri."
"Unafikiria sawa na mimi." Alissa aliweka kidevu chake kidogo kwenye miguu yake, kwa macho ya baridi kidogo. Angemrudishia kile ambacho Melissa alikuwa anadaiwa kidogo kidogo.
"Melissa, ngoja tu uone." Ilikuwa kawaida kwamba mtu alipe deni lake. Alissa hangeweza kamwe kuwa laini na asiye na msimamo.
Sura ya 159
Wikendi hii, kungekuwa na karamu ya biashara katika Hoteli ya Kimataifa ya Garden, na watu wengi mashuhuri na wafanyabishara mashuhuri wangehudhuria, ambayo ilikuwa fursa adimu.
Nilesh na Matthew pia wangehudhuria karamu hiyo. Nilesh alikuwa tayari amemuomba Alissa ahudhurie pamoja naye. Baada ya yote, Nilesh alikuwa muungwana mseja, mchanga na mwenye kuahidi, hivyo alihitaji mwenzi wa kike.
Ikiwa Nilesh angewaomba wanawake wengine katika kampuni hiyo waandamane naye, bila shaka wangeanza kumsogelea, ambayo ingesababisha shida nyingi.
Lakini Alissa hakutaka. asingetaka hata kama angemtaka. Alikuwa mtu bora kuwakilisha kampuni.
Saa 7:00 jioni, taa zenye kung'aa katika hoteli hiyo zilikuwa nzuri sana. Wengi wa watu wa ndani walikusanyika hapa, wenye kelele sana.
Nilesh na Alissa waliingia katika jumba la karamu la hoteli hiyo. Baada ya kuingia ndani, walisababisha msukosuko na umakini.
Nilesh alivaa suti nyeupe, tai nyeusi, na uso mzuri, umbo refu na jembamba na tabia nyororo, kama Prince Charming.
Alissa alimshika mkono Nilesh. Macho yake mazuri yalikuwa yakiangaza chini ya taa, na midomo yake myekundu na nywele ndefu nyeusi zilivutia sana. Alivaa vazi refu la rangi ya champagne lililotengenezwa kwa chachi laini ya tabaka nyingi, mrembo sana kama mrembo aliyeanguka kutoka ulimwengu mwingine.
Mtu aliyemfahamu Nilesh akasogea mbele kuwasalimia, na Nilesh akajibu kwa upole. Alissa naye alitajwa katika mazungumzo yao.
"Mwanamke aliye karibu na Bw. Nilesh ni mrembo sana, na amemvutia kila mtu aliyepo."
“Asante.”
“Nashangaa ni lini ninaweza kuhudhuria harusi ya Bw. Nilesh?”
“Siku moja. Subiri."
Nilesh hakukataa wala kukiri, akajibu tu swali. Hakusema kuwa yeye na Alissa walikuwa marafiki na wafanyakazi wenza tu ili kumlinda Alissa asinyanyaswe na wengine.
Kwa kawaida Alissa alijua kwamba Nilesh alikuwa akimlinda kimakusudi. Hakupenda wengine wamuulize juu yake, na kwa njia hii angeweza kuepuka matatizo mengi.
Nilesh pia hakutaka Alissa aangaliwe juu chini na wale wanaume waliokuwa wakivutiwa na urembo wa Alissa, lakini alipata kisingizio cha kumuacha Alissa aondoke kwenye umati wa watu, na yeye angeshughulika na watu hawa peke yake.
Kulikuwa na kila aina ya vitafunwa na vinywaji, matunda na divai kwenye meza ya buffet ya ukumbi wa karamu.
Alissa alijificha hapa na kuchukua matunda ili ale.
Kwa wakati huu, mhudumu alienda mbele, akiwa na glasi ya divai kwenye trei juu ya mkono wake wa kulia, "Bi Alissa, Bwana Nilesh aliniomba nikupe."
"Vizuri. Asante.” Alissa aliichukua kwa tabasamu, akiishika kwa ncha za vidole vyake.
Alitazama chini na kutikisa. Divai ilionekana kwenye kioevu giza nyekundu, nzuri sana.
Yeye hakunywa, lakini akaiweka kwenye meza.
Katika miaka hii, Alissa alikuwa na uzoefu mwingi na kuona mengi sana. Hakuwa msichana asiye na hatia na rahisi tena, na alikuwa macho zaidi kuliko hapo awali.
Hakunywa vinywaji vya ajabu, ambayo ilikuwa msingi wa kujilinda.
Alichukua chupa ya maji safi kutoka kwenye meza, na mhudumu aliyekuja kuchukua divai akauliza, “Bi, unahitaji bilauri yoyote tupu?”
“Asante.” Kwa kweli haikuwa kifahari kwake kunywa maji na chupa katika hafla kama hiyo.
Baada ya kutuma divai, mhudumu alileta glasi tupu, "Haya, bibiye."
Alissa aliichukua ile glasi na kuiangalia. Hakuona ubaya wowote, akamimina maji kwenye glasi.
Kwa wakati huu, Nilesh alikuwa amemaliza salamu na toast, na akachukua champagne ya dhahabu nyepesi kutoka mezani, na kugundua kuwa Alissa alikuwa ameshika maji mkononi mwake.
"Je, nidhamu ya familia ni kali sana? Hakuna champagne?" Nilesh alisema kwa mzaha.
"Hapana, sitaki tu kunywa pombe." Alissa alichukua maji kwenye glasi, "Unajua kwamba sipendi tukio la aina hii, ambapo lazima nijifurahishe na wengine."
"Lakini lazima uwe na mazoea." Nilesh alichukua shampeni, "Umemchagua, na itabidi uhudhurie karamu nyingi. Huwezi kukataa zote. Lazima uhudhurie karamu muhimu zinazohitaji mahudhurio ya wanandoa."
"Sijafikiria sana." Alissa hakufikiria sana, “Wacha tuijadili baadaye.”
Hapo awali walifunga ndoa kwa siri, ambayo haikutangazwa kwa umma. Kendrick alikuwa bado hajaoa machoni pa umma, kwa hivyo hakuhitaji kuandamana naye.
Lakini, sasa ndoa yao ilitangazwa kwa umma. Kwa kweli kungekuwa na hafla muhimu ambazo zilihitaji kuonekana kwao wote wawili. Anapaswa kutoa ushirikiano kwa ajili yake.
Wakati Alissa na Nilesh walipokuwa wakizungumza, Mathew alienda, “Bw. Nilesh, kampuni yetu pia ni mmoja wa wazabuni wa mradi wa FarmCom unaoshirikiana na kampuni ya Kilimo Kwanza na Kilimo Hai. Twende tuzungumze nao.”
"Sawa." Nilesh alitikisa kichwa, na kumwambia Alissa, "Njoo pamoja nasi, kwa sababu wewe pia unashiriki katika mradi huu."
Mradi huu ulikuwa mojawapo ya miradi muhimu zaidi ya Universal Group katika nusu ya pili ya mwaka. Kama mkurugenzi wa miradi wa ofisi kuu, Nilesh alipaswa kuchukua jukumu hilo.
“Sawa.” Alissa alihisi ni biashara tu, na hakukataa.
Matthew aliwachukua Nilesh na Alissa kwa umati, na wakakutana na Alex, Merry, Sam na Maira, Seidrick na Melissa. Ambao nao walikuwa wamealikwa kupitia kampuni za familia zao.
Ingawa Sam na Maira walisikia kwamba Alissa alikuwa tayari amerudi kwa familia ya Maziku, ilikuwa mara ya kwanza kwao kukutana naye baada ya miaka 5.
Baada ya miaka 5, Alissa hakuwa na hatia na mchanga kama hapo awali. Wakati huo ulimpa ukomavu na haiba, na alikuwa akivutia sana sasa, ambayo ilikuwa wakati wa dhahabu kwa mwanamke.
Kumwona Alissa, Sam alionyesha uso wa baridi kidogo, lakini Maira alionyesha tabasamu hafifu, la neema.
Alissa aliwatambulisha wao kwa wao.
Nilesh aliwasalimia familia ya Maziku na familia ya Masolwa. Alex na Sam walimsifu kwa kuwa mchanga na mwenye kuahidi.
Kisha Alissa akasema, “Bw. Masolwa, Bibi Masolwa.”
Sam alimpuuza Alissa, na Maira pekee aliitikia kwa kichwa.
Sam aliweka uso ulionyooka kama hapo awali, na hata akakunja kipaji kidogo.
Melissa, ambaye alishika mkono wa Sam, alisema kwa upole, “Alissa, ni mshangao ulioje! Kwa nini uko hapa? Nakumbuka kuwa hupendi tukio la aina hii.”
Alissa?
Nilesh na Mathew walishangaa. Hawakuwahi kufikiria kwamba Alissa alikuwa binti wa thamani wa familia ya Maziku.
Familia ya Maziku ilikuwa na ushawishi mkubwa katika Jiji la Mwanza, na baada ya kuunganishwa kwa ndoa na familia ya Masolwa, ilianza kushirikiana na familia ya Masolwa kibiashara. Thamani yao iliongezeka sana.
“Ninahudhuria tafrija hii kwa niaba ya kampuni. Unaweza kuniita Miss Maziku au Meneja Maziku.” Alissa aliweka umbali na Melissa kwa nje.
Melissa aliaibishwa ghafla na maneno ya Alissa, kana kwamba Melissa alijipendekeza kwa Alissa kwa makusudi.
"Alissa, mbona hujali?" Melissa alitabasamu ili kupunguza hali ya hila kati yao, "Sisi ni dada na tulikua pamoja."
"Afadhali tuweke wazi juu ya jambo fulani." Mtazamo wa Alissa ulimzunguka Seidrick karibu na Melissa, "Ingawa sisi ni dada, kuna kitu ambacho hatuwezi kushiriki na kila mmoja."
Sura ya 160
Kwa hakika, kidokezo cha Alissa kilimfanya Melissa kuwa na wasiwasi kwamba alishindwa kujizuia kushika mikono ya Seidrick kwa nguvu.
Seidrick pia alihisi wazi mabadiliko ya Melissa, hivyo alinyoosha mkono wake kimya kwenye mkono wake, ambao ulimshikilia kwa nguvu, na kumfariji.
"Alissa yuko sawa. Baadhi ya mambo ni wazi hayawezi kushirikiwa, kwa hivyo ni bora kutotamani vitu ambavyo si vyako.”
Seidrick akimlinda, Melissa alijiamini zaidi. Aling'ang'ania Seidrick kwa ukaribu zaidi, akionyesha kwamba Seidrick alikuwa wake.
Alissa hakujali hata kidogo, lakini sasa ilimbidi aigize nafasi ya mwanamke ambaye aliachwa na Kendrick na alitaka kumlenga Seidrick… Hii ilihitaji uigizaji stadi.
"Ndio, hata kama mtu alitamani na kupata alichotaka, hawakufanya kwa haki, hivyo mwishowe, wanaweza kuachwa ..." Alissa alipumua sana, kana kwamba alikuwa akijiongelea mwenyewe huku akimshutumu Melissa.
Melissa kwa kawaida alifikiria kuwa Alissa ameachwa na Kendrick. Alifurahi na tabasamu kidogo likajijenga usoni mwake.
“Uko sahihi,” Melissa alikubali.
Watu ambao hawakuwaelewa walihisi kwamba mazungumzo yao yalikuwa ya kutatanisha kidogo, lakini uadui wa maneno yao ulikuwa dhahiri.
"Bwana Alex, sikutarajia Alissa angekuwa binti yako. Yeye ni mtu hodari sana na mkarimu, na kazi yake ni bora. Kampuni inamthamini sana.” Nilesh alibadili mada na kumsifia Alissa.
“Asante, Bw. Nilesh.” Alex alitikisa kichwa na kutabasamu. "Ni kwa sababu kampuni ilimpa fursa."
Nilesh alileta mada za kikazi na akafanikiwa kupunguza hali hiyo.
Alissa alihisi kwamba kulikuwa na watu wengi hapa na kulikuwa na mtiririko mdogo wa hewa. Alikuwa na shida kidogo ya kupumua. "Samahani."
Baada ya kuongea aligeuka na kuondoka. Nilesh alimtazama kwa wasiwasi kidogo. Hakuonekana vizuri. Je, alikuwa anajisikia vibaya?
Lakini alianza mazungumzo hapa na Alex na Sam, kwa hivyo hakuweza kuondoka naye.
Alissa akatoka kwenye mlango wa nyuma wa jumba la karamu. Ilikuwa ni bustani ndogo isiyokuwa na mtu ndani, hivyo palikuwa kimya sana. Mimea ilikuwa imestawi vyema. Kulikuwa na upepo usiku. Hatimaye alijisikia raha, isipokuwa bado alipata upungufu wa pumzi ambao ulikuwa bado haujaisha.
Alissa aliona benchi karibu na kichaka cha maua, hivyo akasogea na kuketi.
Baada ya muda, sura ilionekana machoni pake.
“Bi Maziku, uko peke yako?" Sauti hii ilikuwa ya Timothy.
Alissa aligeuza kichwa chake na kumuona akiwa amesimama kwenye kivuli huku akiwa na tabasamu usoni ambalo lilionekana kuwa mbaya sana kwa wakati huu.
“Kuna nini bwana Timothy?” Alissa aligeuza uso wake kidogo na kumtazama.
“Vipi wewe na bwana Kendrick?” Timothy aliuliza kwa uwazi.
"Vizuri sana." Alissa alitabasamu sana, macho yake safi kama nyota zinazong'aa usiku.
"Bwana Kendrick huja kuambatana nawe mara kwa mara, lakini hajafika hapa kwa muda mrefu hivi majuzi. Atakuwa kwenye safari ya kikazi?” Timothy akasogea karibu zaidi, kivuli chake kikirefuka kwa miondoko yake.
“Hayuko katika safari ya kikazi, na hana shughuli nyingi sana kazini. Yeye huenda tu nyumbani kwa wakati kila siku kula chakula na mke wake.”
Kidokezo katika maneno yake kilikuwa dhahiri sana. Kendrick bado alimjali mke wake, na alikuwa tu mchezo wake wa pupa.
Sasa kwa kuwa alicheza naye na kupoteza hamu, alikuwa karibu au alikuwa tayari ameachwa.
"Kwa hiyo?" Alissa hakujali.
Kendrick alisasisha hali yake kwenye mtandao wake wa facebook, na zote zilihusu yeye kutoka kazini kwa wakati na kwenda nyumbani kuandamana na mke wake.
Kisha pia alichapisha baadhi ya picha za chakula hicho na nukuu zikisema kwamba alipenda watu wa familia yake zaidi na milo iliyopikwa nyumbani zaidi. Ingawa hakutaja wazi ni nani aliyeitengeneza, aliaminisha umma kwamba chakula kiliandaliwa na Bi. Mayala.
Ingawa Kendrick hakukubali wala kukanusha, aliwafanya wengine wamuamini.
Hata hivyo ni Alissa pekee ndiye aliyejua kuwa huo ni mpango ambao Kendrick na yeye waliutengeneza ili kuwachanganya adui.
"Bwana Kendrick amerudi kwa familia yake. Mbona unasubiri hapa kwa ujinga?" Timothy naye akaketi kando yake.
Alissa alisogea pembeni kidogo, hakutaka kujiweka karibu naye. "Hapana, hataniacha hivi."
“Kama msemo unavyosema, usipendane na mwanamume mwenye familia. Utaachwa tu.” Timothy alipomwona hivyo alitabasamu badala ya kukasirika huku akitazama kando ya uso wake maridadi. “Bi Maziku ni mwerevu sana, kwa hivyo hawezije kuelewa sababu? Isitoshe, Bwana Kendrick si mtu wa kawaida, na ndoa yake haiwezi kulinganishwa. Yeye ni mwenye nguvu na mtukufu. Ulijihusisha naye, lakini unaweza kumshinda? Wanaume wakimaliza kurukaruka nje watarudi kwa familia zao. Afadhali kuwa mke wa mtu kuliko kuwa hawara wa mtu.”
Alissa alishusha kope zake kidogo, macho yake yakionekana kulegalega. "Bwana Timothyuko sahihi. Mimi ni mjinga sana hata kumwamini…”
Aliruhusu machozi yajae machoni mwake na kuinua mkono wake kufuta chozi lililokuwa likimtoka. Sura yake ya kusikitisha iliwafanya watu wahisi huzuni.
“Bi Maziku, ikiwa haujali, naweza kukukopesha bega langu." Timothy akatoa kitambaa mfukoni na kumkabidhi.
Alissa akatingisha kichwa huku akijifanya ana nguvu. “Sijambo. Asante.
Sitaki tu kukubali. Sijali kama ameoa na ana mke. Nilimpa mwili na roho yangu. Alisema wazi atanilinda maisha yangu yote. Angewezaje kuvunja ahadi yake na kuniacha peke yangu?”
Timothy aliposikiliza maneno ya Alissa, alitabasamu kwa siri. Ilionekana kuwa alichokisikia Melissa kuhusu Kendrick na Alissa wakigombana kilikuwa kweli. Uhusiano wao ulikuwa tayari umevunjika. Sasa alijua kutokana na maneno ya Alissa kuwa Kendrick alikuwa ameachana naye.
Timothy alifurahi. Juhudi za pamoja za yeye na Melissa hazikuwa bure.
Walikuwa wakitarajia Alissa na Kendrick kuachana ili Alissa apoteze msaada wake. Hapo ndipo wangeweza kumwadhibu.
Alimdanganya kwa makusudi na kumtia aibu mbele ya Kendrick. Angewezaje kumsamehe na kumwacha aondoke kirahisi?
“Usiwe na huzuni. Tunaweza kuanza tena ukitaka.” Timothy alichukua mbinu ya upole, akijaribu kuvunja ulinzi wa Alissa wakati alikuwa 'amejeruhiwa' zaidi. “Sijali uhusiano kati yako na bwana Kendrick. Baada ya yote, hakuna mwanamke Bwana Kendrick hawezi kupata na uwezo wake.
“Sitaki kumzungumzia. Nataka kumsahau na kuanza upya.” Alissa alisema kwa upole. “Nataka kuingia ndani.” Alissa akainuka, na Timothy akamfuata.
Alissa aliporudi kwenye jumba la karamu, alisikia tu vurugu kubwa. Alimwona Kendrick, mtu mwenye mvuto zaidi mle chumbani, akiwa amesimama kati ya umati wa watu waliokuwa wakiongezeka.
Bado alikuwa kwenye shati jeupe la kawaida na suti nyeusi. Alikuwa mrefu na mwembamba, akilinganishwa na wanamitindo wa kiume, na alionekana mtanashati na maridadi kuliko wanaume wengine. Alikuwa amekomaa na ametungwa.
Macho yake ya kina yalikuwa makali na tulivu kutokana na uzoefu wa miaka mingi kuwa katika nyadhifa za mamlaka ambazo hakuna aliyethubutu kumvunjia heshima.
Sura ya 151
Alissa alisimama tu na kumuangalia Kendrick akitokomea. Alissa alijiona yuko salama.
Kendrick alikuwa anamuunga mkono, hivyo angeweza kusonga mbele bila wasiwasi wowote.
Alissa aliingia ndani ya gari baada ya kumuona Kendrick akitokomea mbali.
“Twendeni.” Alisema Alissa kwa upole.
Nora alifikiri kuna kitu kibaya kwa Alissa na Kendrick na kuuliza tena. “Kuna nini nyie?”
“Hakuna kitu. Nitakuambia baadaye.” Alissa akatikisa kichwa. “Hebu twende nyumbani kwanza.”
Nora hakuuliza zaidi, akamuomba dereva aendeshe gari.
Ndani ya gari, hatimaye Alissa alipumzika.
“Alissa, wacha kuniweka roho juu. Nina hamu ya kujua unachotaka kiniambia.” Alissa alimpeleka Doris.
Doris alikuwa mtulivu, na Nora alikuwa amempa simu yake acheze gemu. Akili yake yote ilikuwaimeishia kwenye simu.
Nora alikuwa dukuduku moyoni na Alissa alikuwa hana haraka.
“Una usingizi?”
"Hapana." Alissa alikaa kitako huku akihisi mtupu kidogo.
“Ulifanya muda gani jana usiku?” Nora hakuweza kuzuia udadisi wake. “Kendrick yuko sawa?”
“Jamani, unazungumza nini?” Alissa aliona haya kwa maneno ya Nora, “Sijafanya chochote naye.”
"Unataka kumdanganya nani Alissa? Kwa kumbato lile bado unadiriki kusema hukufanya?" Nora alishangaa, lakini Alissa aliitikia kwa nguvu.
Alimtazama Alissa kuanzia kichwani hadi miguuni na kurudi kwa macho mazito.
Hatimaye macho yake yakatua kwenye uso wa Alissa na kukunja uso. "Haipaswi kuwa hivyo."
"Nini?" Alissa alijiuliza huku akiwa amemtumbulia macho yake.
“Mwanaume gani hawezi kuvutiwa na umbo na sura yako? Mwanaume angekurukia na kulala nawe mara tu unapoingia naye chumbani. Bwana Kendrick na wewe ni mume na mke. Ni sawa kufanya ngono. Kwa nini hamjafanya lolote?” Nora alichanganua. "Mnasubiri nini? Au ni mgonjwa?"
"Ni sawa na hakuna chochote kibaya kwake." Alissa alikunywa maji, na ubaridi tulivu ukaenea kati ya meno yake.
“Umejaribu? Unathubutu kusema yuko sawa? Ikiwa yuko sawa, hakuwezaje kulala na wewe jana?" Nora alimtolea Alissa macho.
“Bila shaka nime…” Alissa nusura amwage ukweli, lakini mara moja akajirekebisha, “Amekuwa akifanya mazoezi kila siku. Nina hakika hana tatizo. Na sisi ni mume na mke, lakini sasa tuko kwenye uhusiano. Alisema ataniheshimu na nikisema tu ndio tutafanya hivyo.”
"Bwana Kendrick ni muungwana, sivyo? Ndiyo, anaonekana kuwa na nguvu.” Nora alikunywa maji yake. “Oh, sawa. Kwa nini alikuleta kwangu na kisha kuondoka peke yake? Kwanini asingekupeleka kwa Maziku?”
"Hapana, anarudi Geita." Mwanga wa nyota ukaangaza machoni mwa Alissa.
Nora alishika mng'ao wa macho yake. “Kwa hiyo huwa anakuja na kuondoka? Je, kuna kitu kibaya katika familia yao? Mbona umeondoka kwa haraka hivyo?”
"Hapana." Alissa alikanusha huku usoni akiwa na utamu mdogo wa kike. "Alitaka tu kuwa nami na kunirudisha salama Mwanza."
Hatimaye Nora alielewa, “Vema. Jinsi wewe ni mtamu.”
Alissa alikunywa maji mara mbili zaidi kwa kuridhika.
"Wale ambao wako tayari kutumia pesa na wewe wanaweza kuwa sio wale wanaokupenda, lakini wale ambao wako tayari kutumia muda adimu na wewe lazima wakupende.
"Kwa hivyo, mtu wa thamani zaidi ulimwenguni ni yule ambaye yuko tayari kutumia wakati na wewe. Mthamini mwanaume huyo, haswa anapokuwa mtu mwenye shughuli nyingi, na yuko tayari kubana muda wa kuwa na wewe."
Alissa aliguswa na maneno ya Nora.
Baada ya kuwa mbali na Kendrick kwa zaidi ya saa moja, alianza kumkumbuka, kum'miss kuwa kando yake, kumkosa kumshika mikononi mwake, kuimiss sauti yake, na kumiss busu lake.
"Itakuwa tamu zaidi katika siku zijazo." Alissa alijibu.
Nora alimpa dole gumba. “Ni vizuri kukuona hivi. Ni kama unakuwa wewe tena.”
“Ndiyo. Ninahisi kutaka kujipata tena.” Alissa aliwaza hivyo. “Wewe unaweza pia. Umepotea tu sasa hivi.”
"Ni juu yangu tena." Nora akahema. "Sio kila mtu ana bahati kama wewe kupata ubinafsi wako uliopotea. Sijisikii nimepotea tu, nahisi nimekufa.”
"Bila shaka huwezi kujikuta na mawazo hayo." Alissa alimfikiria ghafla mtu aliyemwona katika Dar es Salaam, na baada ya kusita kwa muda mrefu, alisema, “Nora, namaanisha nini ikiwa… Je, ikiwa hajafa?”
Nora alimtazama, akiwa na chupa ya maji mkononi, katika mkao wa kifahari.
"Uliniuliza swali kama hilo mara ya mwisho." Nora alidhani Alissa aliuliza mara mbili. “Kuna kitu unanificha?”
Alissa aliuma midomo yake, lakini aliamua kumwambia yote aliyoyajua. "Nora, utanisikiliza kwa utulivu?"
Nora akaitikia kwa kichwa.
“Siku moja tukiwa Dar, mimi na Jane tulikuwa tunakula chakula cha jioni, na mtu fulani alitulipia. Nilipotoka mbio, yule jamaa alikuwa tayari kwenye gari, na niliona uso wake kidogo kupitia dirisha lililoinuliwa. Nilifikiri anafanana sana naye… Bila shaka, kuna watu wengi duniani wanaofanana. Unajua, kuna kaka au dada mapacha waliopoteana, kwa hiyo nadhani ninaweza kuwa nimekosea.”
Nora, hata hivyo, alikuwa mtulivu sana na akasema, “Nadhani ulikosea. Au labda unaamini ni yeye, kwa hiyo ulifikiri kwamba mtu huyo ni kama yeye.”
Na kisha akaongeza, "Amekufa. Hatutakuwa tena naye.”
"Sawa, tuachane na hii." Alissa alijisikia faraja kusema, lakini haikumsaidia Nora.
Nora alikuwa mtulivu juujuu, lakini moyoni alijua kuliko mtu yeyote jinsi alivyokuwa anamtaka huyo mtu awe hai.
Alisema hivyo kwa sababu hakuthubutu kujipa mwanga wa matumaini, kwa kuhofia kwamba angemkosa zaidi, kwa kuhofia kwamba angepoteza hata ile furaha iliyojificha, na kuhofia ndoa hiyo isingeweza kumnasa.
“Niambie wewe na bwana Kendrick. Kwa nini ulimtazama sana wakati anaondoka?" Nora alibadilisha mada kwa haraka, “Ulisema utaniambia baadaye.”
“Hiyo ni kwa sababu tunamtafuta mtu aliurtufremu…” Alissa alimpa Nora maelezo mafupi ya kilichotokea, pamoja na mpango aliokuwa akiufikiria.
Sura ya 152
Baada ya safari ya karibu saa nzima barabarani kutokana na foleni, hatimaye Alissa alirudi kwenye makazi ya familia ya Maziku na Doris.
Giza lilikuwa likiingia na jumba hilo la kifahari lilikuwa na mwanga mkali.
Waliporudi, bibi Jenifer alikuwa tayari alikuwa ameenda kulala. Merry pekee ndiye aliyekuwa sebuleni. Alipomwona Alissa, alikuwa na shauku zaidi kuliko hapo awali, “Alissa na Doris, habari za jioni. Mmekula?”
“Ndiyo.” Alissa alimshika Doris na kukaribia kuondoka.
Merry akamuuliza tena, “Nimesikia kuwa ulienda Geita kikazi.”
“Ndiyo.”
"Umekutana na Bwana Kendrick?" Merry alikuwa na wasiwasi juu ya uhusiano wao sasa.
“Ndiyo.” Alissa alijua wazi anachomaanisha Merry,
“Hata aliachana na kazi zake kwanza na kuandamana pamoja nami. Tulikuwa na wakati mzuri.”
"Inapendeza." Merry alicheka, “
Usiku umeenda. Nenda ghorofani ukapumzike sasa. Usiku mwema." Alissa kisha akatulia na kumpeleka Doris juu.
Merry alisimama na kuwatazama wakipanda juu huku akikunja uso kwa kuchanganyikiwa.
Ilionekana kuwa kuna kitu kibaya. Melissa alisema kwamba alimwomba mtu aende kwa familia ya Mayala ili kufichua ukweli kwamba Alissa alikuwa hawara wa Kendrick. Familia ya Mayala ilikuwa ya kifahari sana kwamba mwanamke ambaye angeweza kuolewa naye anapaswa pia kuwa msichana wa kuvutia na alikuwa na historia ya nguvu. Kwa hivyo, familia ya Mayala ingeshughulikia. Mbali na hilo, Merry alisikia kutoka kwa Melissa kwamba mwanamume huyo alimwambia kwamba ingawa bwana wa familia ya Mayala hakukasirika sana, alikosa furaha kidogo.
Kwa hivyo, Alissa hakupaswa kuandamana na Kendrick kwa furaha.
Au Melissa alidanganywa na mtu huyo?
Wakati huo, Alex, ambaye alikuwa amerudi kutoka kwenye karamu ya chakula cha jioni, aliingia na kumpiga kiwiko Merry ambaye aliganda, "Unaangalia nini?"
“Hakuna kitu.” Merry hakuthubutu kumwambia Alex juu ya kile Melissa alichokifanya. Kwa sababu aliogopa kwamba Alex angeharibu mpango wao.
Hakukubaliana na Melissa. Lakini pia hakutaka Alissa awe na kiburi kwa sababu ya Kendrick katika familia ya Maziku. Kwa hivyo, alifumbia macho kile Melissa alikuwa amefanya.
***
Alissa ilimbidi akamilishe mradi wa FarmCom baada ya wiki mbili. Kwa hiyo, ilimbidi kuwa bize na kazi yake. Muda ulikimbia.
Yeye na Kendrick hawakuwa na mawasiliano ya ana kwa ana. Lakini wangezungumza kwenye simu.
Kendrick alimtumia hii saa sita mchana: [Hata kama uko busy na kazi, unapaswa kula.]
Alissa alijibu kwa njia ya kucheza na kufurahisha: [Sina shughuli nyingi kama Bwana Kendrick. Mimi ndiye ninayepaswa kuwa na wasiwasi iwapo Bwana
Kendrick ana mlo mzuri.]
Kendrick kisha akainuka na kuiendea meza ya duara karibu na sofa. Kulikuwa na vyakula kadhaa mezani, vyote hivyo vilikuwa ni chakula cha mchana ambacho Chale alimuagizia kila siku.
Kendrick: [Je, ungependa kuungana nami?]
Alissa alituma emoji: Mlo wa mchana wa bwana mkubwa ni wa gharama sana! Najihisi mimi ni maskini sana.]
Kendrick aliketi kwenye sofa: [Unataka kula? Ni haki tu kwamba unatoa kitu kwa kubadilishana, sivyo? Bi. Mayala.]
Alissa alituma emoji ya busu ili kumhonga Kendrick.
Kendrick alitabasamu: [Nitakumbuka kwamba Bi. Mayala anadaiwa kunibusu. Subiri.]
Subiri? Angojee nini?
Alissa aliinamisha kichwa, akakunja uso na kuwaza. Anapaswa kwenda kwenye kantini ya kampuni sasa.
Aliweka kalamu yake chini, akainuka na kwenda kwenye mgahawa.
Wakati anaandaa chakula chake, alimuona Emmy akimpungia mkono.
Alissa kisha akaenda kwake.
Emmy ndiye mfanyakazi mwenzake pekee ambaye alikuwa na shauku zaidi kwake katika kampuni na alimsaidia kila wakati.
Mathew pia alimsaidia. Lakini hata hivyo alikuwa bosi wake. Sasa Alissa alikuwa ameolewa. Kwa hivyo, wanapaswa kuepuka kukutana mara kwa mara kuibua tuhuma.
"Hii nyama ni kwa ajili yako." Emmy alichukua nyama kutoka kwenye sahani yake na kumpa Alissa.
“Kisha nitashiriki nawe baadhi ya vipande hivi vitamu vya nyama choma?” Alissa alisema.
"Hapana. Kulikuwa na vipande viwili tu vilivyobaki. Nikifikiria kwamba unapenda nyama choma pia, hivyo nilichukua moja kwa ajili yako.”
Emmy alipenda nyama choma zaidi. “Tulia. tunapaswa kusaidiana kama wafanyakazi wa kampuni moja.”
Alissa alihisi kwamba Emmy alikuwa mwenye usawaziko na alikumbuka fadhili zake kwa siri.
“Hebu tufurahie.”
Walipoanza kula tu, mwanamume mmoja aliyevalia nguo za sare za Mgahawa wa City Star Restaurant alikuja na kontena maalum la chakula kutoka kwenye mgahawa huo.
Mkahawa wa City Star ulikuwa msururu wa kitaifa wa migahawa maarufu ya hali ya juu. Watu waliotaka kula chakula hapo lazima wawe wanachama wao. Wanachama walihitaji kulipa ada ya kila mwaka. Wapishi wao walikuwa mahiri katika vyakula vinane. Chakula walichopika kilikuwa kizuri sana.
Kontena lilifunguliwa. Kila mtu alikaza macho yake kwenye chombo kizuri cha chakula cha na hakuweza kujizuia kumeza mate ya uchu.
Mhudumu huyo alisimama mbele ya meza ya Alissa na kumchunguza. Alipoona kitambulisho chake cha kazi shingoni, alisema, “Je, wewe ni Bibi Alissa?”
“Ndiyo.” Alissa akaweka chini uma uliokuwa mkononi mwake.
"Tafadhali saini hapa." Mhudumu alimkabidhi barua ya kupokelea mzigo.
Alissa alisaini na kumrudishia mhudumu yule. Mwanamume huyo akaiweka, akafungua chombo cha chakula, akatoa sahani kadhaa, ikiwa ni pamoja na samaki watamu sato, wakukaanga katika mchuzi wa moto na nyama ya kukaanga na pilipili, Chipsi moto, kuku wa kuoka, na madikodiko mengine kibao.
Vyakula hivi vilikuwa sawa kabisa na vile kwenye picha aliyomtumia Kendrick.
Kwa hivyo, hivi ndivyo Kendrick alimaanisha kwa kungoja. Alimuagizia chakula sawa. Alissa aliguswa na wema wake.
Alikuwa ameushika moyo wake na kumuacha apendezwe naye kwa namna ambayo hakuitarajia.
Baada ya mhudumu yule kuondoka, Emmy alitazama sahani tajiri kwenye meza. Ilikuwa na harufu nzuri ambayo ilimfanya apate njaa sasa.
Watu wengine pia walikitazama chakula kilichokuwa mezani, wakasikia harufu yake na kukionea wivu.
Lily tu na rafiki yake wa karibu walikuwa na wivu sana.
"Alissa, mumeo alikutumia haya yote?" Emmy angeweza kufikiria tu jambo hili.
"Nadhani." Alissa alitabasamu tu.
"Alissa, mume wako anakupenda sana." Emmy alionekana mwenye wivu, “Sijawahi kula chakula katika Mkahawa wa City Star. Nilisikia kwamba ni ghali sana. Bei ya baadhi ya sahani ni sawa na mshahara wangu wa kila mwezi.”
Alissa alichukua samaki mtamu na kumweka kwa Emmy, "Basi jaribu leo."
"Alissa, wewe ni mkarimu sana." Emmy aliguswa, “Lakini hii ni sawa? Hii ni zawadi kutoka kwa mumeo.”
"Mambo mazuri yanapaswa kushirikiwa na marafiki. Jisaidie tu.” Alissa alidhani Emmy alikuwa mzuri sana.
“Sawa, asante.”
Lily kwenye meza iliyofuata alitazama hili na alikuwa na hasira sana kwamba hakuwa na hamu ya kula kabisa.
"Lily, Alissa hawezi kupata chakula kutoka kwa Mgahawa wa City Star hata kama ana pesa. Mume wake ana nguvu sana?” Rafiki wa Lily aliuliza kwa kuchanganyikiwa.
"Hivi kweli ana mume anaposema ana mume?" Lily alionekana kukasirika na kusema kwa jeuri, "Labda yeye ni hawara tu wa mtu."
“Ndiyo. Anaonekana kukata tamaa. Hawara anayeharibu familia za watu hatafikia mwisho mwema.”
Sura ya 153
Emmy alikasirika sana kusikia Lily na marafiki zake wakimtukana Alissa. Alimwambia Lily, “Lily, huo ni wivu tu. Unafikiri wewe ni bora kuliko wengine?"
“Wivu? Ni utani ulioje.” Lily alikoroma kwa ubaridi, “Kama ana mume, kwa nini asimlete hapa tumuone? Anakataa kwa kila aina ya visingizio. Hata kama mumewe anamletea vyakula na maua, ili iweje? Je, anathubutu kumleta mume wake hapa? Ninaogopa mume wake ataaibika sana kutuona, sawa?”
“Ndiyo. Angalau, Lily na bwana mdogo wa Vortex Company wako juu na hawaogopi mtu yeyote anayewasema vibaya. Ni Neema, rafiki wa Lily, alimzungumza, “Mara ya mwisho, mpenzi wa Lily alitualika Villa Park Club. Huwezi kusahau jinsi alivyokuwa mkarimu kwa Lily, sivyo?
“Emmy, unafikiri wewe ni mtu mzuri? Alissa anaendesha gari aina ya Range Rover na kukupa baadhi ya vyakula kutoka kwenye Mkahawa wa City Star. Basi, wewe ni kama mbwa anayejikombakomba kwa bwana wake. Natumaini kwamba yote hayatakuwa bure, au utakuwa na huzuni.”
Neema kweli alikuwa na ulimi wa fedha.
Emmy alikuwa na hasira na wasiwasi baada ya kuzomewa na Neema. Pia alihuzunika sana, "Nyinyi ... ninyi ndio mbwa wanaouma watu kila mahali."
"Wewe ni nzi anayefuata mzoga." Walijibu kwa karipio la kejeli, na kumfanya Emmy karibu kulia kwa hasira, “Nyinyi watu …
nitamwambia Bw. Matthew nyinyi watu mnaenda mbali sana.”
“Jipange. Sasa ni mapumziko ya chakula cha mchana. Bwana Mathew hatajali sana.” Jamila, rafiki mwingine wa Lily, alijibu.
Walionekana kuwa na kiburi na kufanya wapendavyo.
Alissa hakuwa na nia ya kujiletea matatizo. Lakini walichosema na kufanya kilikuwa kinaenda mbali sana.
Hawakumpenda na kumdhulumu. Lakini kwa sababu tu Emmy alikuwa karibu naye, walimdhalilisha Emmy hivi. Ilikuwa ni chukizo sana.
Ikiwa angevumilia kila wakati, angechukuliwa kama dhaifu.
"Mbona nyie watu ni wakali sana? Lily, unasahau kwamba umekatwa miezi sita ya bonasi na Bw. Matthew?” Alissa aliwakumbusha kwa mtazamo mzuri.
“Alissa, unathubutuje kutaja hili? Kama si wewe, ningekatwa miezi sita ya bonasi? Ninajua kwamba Bw.
Mathew alikuwa na upendeleo kwako. Siamini kwamba hakuna chochote kati yako na Bw. Mathew.” Akifikiria bonasi yake, Lily alihisi kufadhaika.
Alissa alikuwa karibu kusema kitu alipoona mtu anayemfahamu anakuja. Kumtazama mtu anayekuja, alishtuka na kisha kushangaa.
“Lily?” yule mtu mzuri alisimama mbele ya Lily na kutazama kadi yake ya kazi.
“Mimi…..” Lily alimtazama mwanamume mrembo mbele yake. Ingawa mwanamume huyo alionekana mpole na mtaratibu, Lily aliogopa kidogo na kuingiwa na hofu, “Wewe ni nani?”
“Mimi ndiye kiongozi wa ofisi kuu ya Universal Group. Tafadhali rudia ulichosema hivi punde.” Sauti ya mtu huyo ilikuwa baridi, “Kama ni kweli kama ulivyosema kuna uhusiano usiofaa kati ya wasaidizi na bosi, nitaomba makao makuu yamfukuze kazi.”
“Kweli?” Lily alishangaa.
"Lily." Hata hivyo, Neema alimvuta Lily na kumwambia atulie. “Tunawezaje kuamini kwamba wewe ndiye bosi mkuu kutoka makao makuu? Wewe ni nani?"
Mtu huyo alitoa kadi yake ya kazi, ambayo ilisoma Nilesh Kumar kutoka makao makuu ya Universal Group, na nafasi yake ilikuwa Mkurugenzi wa Miradi.
Lily, Neema na Jamila, na wengine katika mgahawa wote walishangaa.
Mtu huyo alikuwa mkurugenzi wa miradi wa wa kampuni! Alionekana mzuri na mpole. Sauti yake ilikuwa ya kupendeza na laini. Pia alikuwa kipaji bora ambaye alihitimu kutoka taasisi bora ya biashara na kurudi kutoka nje ya nchi. Alimshangaza kila mtu hapa.
Nilesh kila mara aliweka hadhi ya chini maishani na kazini. Ingawa alikuwa amechukua miradi mingi mikubwa na kuishughulikia kikamilifu, hakuwahi kufanya mahojiano na hakujali kamwe ofisi ya tawi. Kwa hiyo, watu wachache walikuwa wamemwona kuwa mtu halisi.
Sasa alifika kwenye ofisi ya tawi ya Mwanza, ambayo ilikuwa fursa adimu kwa Lily.
"Bwana Nilesh?” Lily alitabasamu kwa kutaniana.
"Unaweza kuzungumza nami chochote unachotaka kusema." Nilesh alitabasamu kwa upole.
"Mimi ..." Lily alikuwa karibu kusema kitu. Lakini alisimama na kumtazama Alissa, “Mr. Nilesh na Alissa wanajuana, sawa?”
Alissa alikuwa akifanya kazi katika idara ya Nilesh huko makao makuu, Dar. Kwa kawaida alikuwa amefanya kazi na Nilesh, mkurugenzi wa miradi.
“Tulikuwa tukifanya kazi pamoja katika makao makuu. Kwa hiyo, bila shaka tunafahamiana.” Nilesh alikuwa na busara na hekima wakati akitaja uhusiano wao.
"Bwana Nikesh, huu ni mkutano wangu wa kwanza na wewe. Je, utaamini nilichosema?” Lily hakuwa mjinga kiasi hicho.
"Ninaamini tu katika ushahidi." Nilesh alikuwa mwenye usawaziko, “Nipe ushahidi nami nitashughulika naye kulingana na ushahidi.”
“Tumeona kwa macho yetu kwamba wakati Alissa anahamia hapa, amechukuliwa gari la Bw. Matthew mara chache kwenda na kushuka kazini. Hivi karibuni, aliendesha gariaina ya Range Rover. Hawezi kumudu kununua gari kama hilo lenye thamani ya mamilioni kwa kiwango chake cha mshahara. Ikiwa hakuwa na historia, angewezaje kupata nafasi ya meneja wa miradi baada ya kuja hapa?" Jamila alifurahi na kusema.
“Kila mtu anaweza kuzungumza. Ninachotaka ni ushahidi.” Nilesh aliwakumbusha tena.
“Sikuwaza sana wakati huo. Kwa hiyo, sikupiga picha.” Jamila sasa alijuta sana.
“Huna ushahidi. Ina maana unabahatisha na kumtilia shaka bosi wako!” Nilesh akawa baridi na hasira.
Jamila aliogopa. Aliinamisha kichwa chini na hakuthubutu kumwangalia, "Mimi ... sidhani hivyo."
“Si ulisema hivyo?” Macho ya Nilesh yalitiririka kutoka uso kwa uso, “Kila mtu anaweza kushuhudia kwamba sikukosea, sivyo?”
Jamila aliuma mdomo wake na kumtazama Lily kwa woga fulani, akimwomba Lily msaada.
"Lily anafikiria nini kifanyike kuhusu tabia ya aina hii?" Nilesh, hata hivyo, aliuliza kabla Lily hajazungumza chochote.
Lily alikuwa katika hali ngumu, akifikiri kwamba Jamila ni mjinga kweli.
"Bwana Nilesh, yeye ni mnyoofu kidogo na hana ubaya wowote. Kwa nini tusisahau tu?” Lily alimtetea Jamila kwa sababu Jamila alikuwa amemsaidia sana.
"Tusahau? Halafu sheria na kanuni za kampuni ni za kuonyesha tu!” Nilesh alikoroma kwa upole, “Anaweza kumshuku Alissa na Bw.
Matthew wana uhusiano wa kimapenzi leo. Halafu atashuku kuwa nina uhusiano wa kimapenzi na Alissa kesho, sawa?"
“Hapana, hapana. Bwana Nilesh, sithubutu.” Jamila akatikisa kichwa.
Sura ya 154
"Hujathubutu?” Nilesh alicheka na uso wake mzuri ulikuwa baridi, “Ulichosema bado kinasikika masikioni mwangu! Siwezi kustahimili watu kama wewe wanaochochea uadui kati ya bosi na wafanyakazi.”
"Kwa hivyo, haupaswi kukatwa tu bonasi ya nusu mwaka kwa kumsingizia bosi wako. Unastahili kufukuzwa kazi.”
Jamila aliposikia kwamba atafukuzwa kazi, alipigwa na butwaa. Alikuwa ametoka tu kuwa mgeni na kuwa mfanyakazi mkongwe na alifurahia matibabu mazuri katika kampuni hiyo kuliko makampuni mengine aliyofanya kazi. Hakutaka kuachishwa kazi.
Mara tu atakapofukuzwa kazi, hataweza kusimama katika jiji hili. Hakuwa mrembo kama Lily kupata mchumba tajiri. Hakuwa na asili dhabiti ya familia na alikuwa mtu wa kawaida kutoka familia ya kawaida. Hakutaka kurudi huko.
"Bwana Nilesh, hii si adhabu kali sana?” Lily bado alitaka kumtetea Jamila. Baada ya yote, Jamila alikuwa msaidizi wake mwenye uwezo na hangeweza kumpoteza.
“Sifikirii hivyo. Adhabu hii ni ya haki sana.” Emmy alijitokeza kwa wakati ufaao, “Hatupaswi kutoa matamshi ya kutowajibika.
Kashfa kama hii pia inaweza kusababisha mashambulizi ya kibinafsi."
“Na si mara ya kwanza nyie kuongea hivi. Bado nakumbuka kwamba kuna msichana mgeni aliacha kazi yake akilia kwa sababu ya mashambulizi yenu ya maneno na udhalilishaji. ”
“Nyie mmefanya mambo mengi mabaya. Je, hampaswi kuadhibiwa?”
"Acha kuongea ujinga." Uso wa Lily ulikuwa wa rangi.
Neema hakuthubutu kuongea na Jamila alionekana kuwa na wasiwasi.
“Ninasema ukweli. Ikiwa kuna uwongo, nitapigwa na radi na kugawanyika sehemu mbili." Emmy alikuwa imara na akaapa.
Wakati huu, umati wa watu ulianza kunong'ona. Kwa kuwa Lily alikuwa na tajiriba na alikuwa na mpenzi tajiri kama msaidizi wake, watu wachache katika kampuni hiyo walithubutu kumkasirisha.
Sasa kwa kuwa mtu fulani angemwadhibu, wote walikuwa wachangamfu.
“Emmy yuko sahihi. Sisi pia tunajua mambo haya.” Kuna mtu alimuunga mkono Emmy.
"Mradi tu mtu hamtii Lily katika kampuni, watamkemea na kumdhulumu. Ni kweli haiwezi kuvumilika.”
"Bwana Nilesh, tafadhali washughulikie.”
Nilesh alitikisa kichwa huku akisikiliza umati, "Kwa hivyo, Jamila lazima aache kazi sasa hivi."
“Hapana, Bw. Nilesh. Tafadhali usinifukuze kazi.” Jamila alisonga mbele na kusihi, "Nahitaji kazi hii."
"Inaonekana hauthamini kazi hii hata kidogo." Nilesh hakuonyesha huruma yoyote, "Baada ya chakula cha mchana, nenda kwa ofisi ya fedha ili ulipwe mshahara wa mwezi huu na mshahara wa miezi mitatu kama fidia."
Wakati huu, Mathew pia alikuja. Alisikia kutoka kwa msaidizi kwamba kuna kitu kilitokea kwenye mgahawa wa kampuni na kukimbilia hapa.
"Bwana Nilesh.” Mathew angeenda kwenye makao makuu kwa mkutano kila robo mwaka. Kwa hivyo, kwa kawaida alimjua Nilesh.
Nilesh alitikisa kichwa, “Nadhani unajua kilichotokea. Unafikiri ninaishughulikia ipasavyo?”
Jamila aliweka matumaini yake kwa Mathew na kusihi, “Bw. Mathew, wewe ndiye unayesimamia tawi hili. Uamuzi wa Bw. Nilesh hauwezi kuwa sawa na wako. Maadamu haukubali kunifuta kazi, bwana Nilesh hawezi kufanya lolote kuhusu hilo. Bw. Matthew, kwa ajili ya miaka yangu katika kampuni, tafadhali nipe nafasi.”
“Nafasi imehifadhiwa kwa wale wanaoithamini. Ni dhahiri kwamba wewe si mtu wa namna hiyo. Nadhani uamuzi wa Bw. Nilesh unafaa. Hata asipofanya, nitafanya hivyo. Kutekeleza moja kama onyo kwa mia moja ndiyo njia bora ya kuwajulisha watu zaidi sheria ni nini! Mathew alikuwa akikazia na kumuunga mkono Nilesh.
Kuona kwamba Mathew alisema hivi, Jamila hakuwa na matumaini hata kidogo.
Mwili wake ukaishiwa nguvu na akaanguka chini.
Kuona hivyo, Lily alijaribu kumsaidia. Kwani, Jamila alikuwa amemsaidia sana na alijua jambo fulani kumhusu.
Lakini Jamila alimvuta kwa nguvu na kukataa kuachia mkono wake, “Lily, nisaidie. Tafadhali nizungumzie jambo mbele ya Bw.
Matthew na Bw. Nilesh…”
“Jamila, hizi ni sheria za kampuni na uamuzi wa Bw. Matthew na Bw. Nilesh. Samahani. Siwezi kufanya lolote kuhusu hilo.” Lily alimtazama Alissa, akimaanisha kuwa Alissa ndiye angeweza kumsaidia Jamila.
Jamila alijua kwamba jambo hili lilitokea kwa sababu ya Alissa. Kwa hiyo, angeweza tu kumwomba Alissa msaada wake.
Lakini kumwomba Alissa msaada ilimaanisha kwamba alipaswa kukiri kwamba alikosea.
Isitoshe, kwa kawaida Alissa hangeweza kumsaidia. Aliogopa kuwa Alissa atamcheka tu. Hata angefedheheshwa na Alissa, alishindwa kuendelea na kazi hiyo na angewachekesha watu wengi zaidi.
“Lilly, inabidi unisaidie. Nilifanya yote kwa ajili yako. Nimesema maneno hayo kwa niaba yako.” Mtu pekee ambaye Jamila angeweza kuomba msaada alikuwa Lily.
Lily alikasirika, “Sikukuuliza useme hivyo. Kwa nini unanipanga?”
“Mimi … hufikiri hivyo? Ulisema Alissa alikuwa mpenzi wa Bwana Mathew…”
“Unaongea ujinga gani? Sikusema lolote!” Lily aliona kwamba Jamila alianza kuongea bila maneno ya uangalifu na aliogopa kwamba Jamila angesema zaidi dhidi yake, “Upuuzi wako una faida gani kwako? Ukipoteza kazi hii, unaweza kupata nyingine. Kwa nini unafuata kisasi dhidi yangu?”
“Ndiyo, Jamila.” Neema alisogea mbele ili kumsaidia Jamila na kuchukua nafasi hiyo kupunguza sauti yake, “Haitakufaa kusema zaidi. Acha kusema nitamwomba Lily amshawishi Bwana Ernest akutafutie kazi. Acha ujinga sasa."
Jamila hakuwa na budi ila kufanya hivyo. Vinginevyo, ikiwa kweli angemchukiza Lily, hangeweza kuwa na kazi nzuri.
Hivyo, Lily, Neema na Jamila waliondoka kwanza, na watu katika mgahawa pia waliondoka mmoja baada ya mwingine.
Nilesh na Alissa pekee ndio walikuwa wamebaki kwenye mgahawa huo.
"Alissa, sikukuona kwa muda mrefu." Sauti ya kupendeza ya Nilesh ilisikika katika mkahawa huo tulivu, na kuwafanya watu wajisikie vizuri.
"Ndio, hatujaonana kwa muda mrefu." Alissa alipumua muda huo akaruka.
Alissa alimtazama Nilesh ambaye alikuwa hajamuona kwa muda mrefu. Ilikuwa kana kwamba alikuwa amerudi nyuma katika miaka ambayo walikuwa wakifanya kazi pamoja.
Nilesh alikuwa amerimbikiza kazi fulani kutokana na kulazwa hospitalini. Ilibidi atumie wakati mwingi kuzishughulikia. Kwa hivyo, alipata tu wakati wa kuja kumuona Alissa katika Jiji la Mwanza baada ya siku hizi.
"Ulisisitiza kuhamia Mwanza. Je, haya ndiyo uliyoyataka?" Nilesh alipofika tu, aliona watu walivyokuwa wanamnyanyasa, wakimpa hasira na kufadhaika.
"Bwana Nilesh, unatawala sana wakati huu." Alissa alionyesha kumshukuru. Hajawahi kumuona Nilesh asiye na huruma kama huyo, "Karibu nilifikiri wewe sio Nilesh niliyemjua."
"Kuna ubaya gani kuwa mtu mbaya kwa ajili yako?" Nilesh hakujali watu walimfikiria nini. Alitaka tu kumlinda mpenzi wake.
Alissa alikutana na macho ya joto ya Nilesh. Lakini hakustahili utunzaji aliompa. Kwa sababu hakuweza kujibu upendo wake. Hilo lilikuwa jambo baya zaidi kwake.
"Sistahili." Alissa akamkumbusha kwa mara nyingine.
“Nilisema ni kazi yangu iwe unastahili au hustahili. Huhitaji kuhisi kulemewa.” Nilesh alitaka tu kuwa mzuri kwake.
"Nilesh, lazima nikuambie kitu."
Sura ya 155
Alissa alimtazama Nilesh kwa umakini huku akiwa na mwanga machoni mwake. Alionekana mgumu na thabiti.
"Nisikilize kabla ya kusema, sawa?" Nilesh alisema kwa upole.
“Sawa. Wewe sema kwanza." Alissa akaminya midomo yake, akimpa nafasi na kuonyesha heshima.
Nilesh alikaa mkabala na Alissa. Nje ya dirisha, miale michache ya mwanga wa jua ilimwangukia uso wake mzuri, na kumfanya aonekane mpole na mrembo kiasi kwamba watu hawakuthubutu kumkufuru.
"Kwanini usiniulize sababu iliyonifanya nije Mwanza?" Nilesh aliuliza kwa kejeli.
"Safari ya kibiashara? Ili kuhudhuria mkutano? Au kuniona?” Alissa alikisia.
“Jambo la kwanza ni kukuona. Pia ni safari ya biashara. Isitoshe, niko hapa kuhudhuria karamu.” Nilesh alibadilisha mpangilio wa mambo aliyosema.
“Basi utakuwa hapa kwa siku chache. Je, kuna mahali popote unapotaka kwenda? Naweza kuwa kiongozi wako.” Alissa alitaka kutekeleza majukumu ya mwenyeji. Hii pia ilikuwa malipo madogo kwa utunzaji wa Nilesh kwa miaka mingi.
“Nilikuwa nakuja Mwanza. Lakini kila mara nilikuja na kuondoka kwa haraka. Wakati huu, nataka kutazama vizuri na kuona jiji hili ambalo ulikulia." Nilesh alitaka kujua zaidi kuhusu maisha yake ya zamani na hata alitaka kuhudhuria maisha yake ya baadaye, “Bila shaka unapaswa kunitunza. Hili ni eneo lako.”
"Hakuna shida." Alissa alisema.
“Alissa, nitakaa Mwanza kwa wiki moja. Mwezi mmoja baadaye, nitakuwa mwenzako tena.” Hoja ya Nilesh ilikuwa hii.
Alissa alichanganyikiwa kidogo, “Sisi si wenza sasa pia. Hatuko mahali pamoja.”
“Hicho sicho ninachomaanisha. Nimewasilisha ombi la uhamisho. Ninataka kuja Mwanza niwe upande wako." Nilesh alitabasamu, “Alissa, tafadhali nipe ushauri wako wakati huo.”
“Nilesh, usifanye hivyo. Familia yako, marafiki na watu unaowasiliana nao wote wako Dar. Utapata maisha bora ukiwa Dar. Usimwachie mwanamke kila kitu ulicho nacho. Ni kweli si thamani yake. Sitajisikia furaha kwa wakati utafanya hivyo, lakini huzuni, unajua?"
Alissa alijua vyema kwamba Nilesh angeshushwa cheo tu ikiwa angeondoka makao makuu ya Universal Group na kuja Mwanza. Kwani, Matthew alikuwa meneja mkuu katika tawi la Mwanza. Ikiwa Nilesh alngehamishwa, hangeweza kumshusha Matthew, vinginevyo labda Matthew angehamishwa. Hata kama bado angekuwa meneja wa tawi hilo baada ya kuhamishwa, bado haikuwa nzuri kama nafasi ya mkurugenzi wa miradi aliyokuwa nayo katika makao makuu.
“Alissa, sikuweza kukushikilia ulipoamua kuondoka hapo awali. sasa, nitakuja kuambatana nawe. Hii ni dhamira yangu.
Sikufurahi hata kidogo baada ya wewe kuondoka. Kuangalia mtu mwingine ameketi kwenye kiti chako cha zamani, nilifikiri nifanye jambo fulani. Hivyo ndivyo mwanaume anapaswa kufanya.” Nilesh alikuwa ameamua.
"Alissa, hata nikiangalia sura yako na tabasamu lako kila siku, najisikia mchangamfu. Unaelewa?"
“Nilesh, ninaelewa. Lakini tafadhali acha kuwa mzuri kwangu. Usiwe mjinga sana kuacha kila kitu ulicho nacho kwa ajili yangu… samahani. Ninakuchukulia kama rafiki tu." Alissa akashusha pumzi ndefu na kudhibiti sauti na hisia zake.
Hakutaka kumuumiza Nilesh. Lakini ilimbidi aseme maneno haya na hakuweza kuepuka kumuumiza. Hata ikiwa ilikuwa ngumu kusema, ilibidi aseme. La sivyo, ingelemea dhamiri yake na ingemwangamiza pia Nilesh.
Hata kama angemchukia, alikuwa mwadilifu.
"Alissa, naweza kukusubiri." Wakati wake ulikuwa kwake tu, “Nimengoja kwa miaka minne na sijali kuhusu miaka minne ijayo…”
“Huwezi.” Macho ya Alissa yalikuwa mekundu, “Mimi … nimeolewa.”
Sauti yake ilikuwa nyororo sana, ambayo ilikuwa kama kipepeo anayeruka. Lakini ilifika masikioni mwa Nilesh na kumshtua.
Alikaa tu. Kulikuwa na jua. Lakini hakuweza kuhisi hata chembe ya joto.
Ni wazi ilikuwa siku ya jua. Lakini alihuzunika sana hivi kwamba ilikuwa kana kwamba mvua ingenyesha sekunde inayofuata.
Alissa naye hakusogea. Wawili hao walikuwa kama jozi ya sanamu. Muda ulikuwa umeganda na alionekana kuwa ameanguka katika ulimwengu wa barafu na theluji. Nilesh alitetemeka kwa baridi.
Baada ya kungoja kwa muda mrefu, Alissa alishindwa kustahimili mazingira yaliyowazunguka na akasema kidogo, "Nilesh, uko sawa?"
"Alissa, unanidanganya, sivyo?" Nilesh alilazimisha tabasamu kwa kutoamini, “Hutaki nicheleweshe kazi yangu na kuwaacha wazazi na marafiki zangu. Kwa hiyo, unasema mambo kama hayo ili kunidanganya, sivyo?
“Niambie unasema uongo na hujaolewa. Hutaki nikusumbue hivi, sivyo?”
"Hapana." Alissa alikuwa na hisia tofauti, “Nimeolewa kweli. Sikudanganyi, na sitaki kukudanganya.
“Usiseme hivyo kukuhusu pia. Hukunisumbua. Ni kwamba sistahili upendo na utunzaji wako. Nilesh, katika maisha haya, wewe ni rafiki yangu na mshauri wangu. Lakini yeye ndiye ninayetaka kutumia maisha yangu na ninampenda."
Nilesh akanyamaza tena. Macho yake yakawa yamefifia kabisa. Alionekana mwenye uchungu sana hivi kwamba alikuwa tofauti kabisa na hapo awali.
"Nilesh, samahani."
Hata milioni moja ya msamaha isingeweza kuponya majeraha yake.
Nilesh akatulia taratibu na kutabasamu kidogo. Alionekana baridi na mwenye huzuni, “Hakuna haja ya kusema samahani. Labda hii ndiyo hatima." Ni Mungu ambaye hakutaka wawe pamoja. Aliweza tu kujisikia vizuri kwa kufikiria hivyo.
"Ni kosa langu kukufanya ubebe shinikizo hili." Alissa hakujua la kusema. Nilesh alikuwa hivyo kila wakati. Hata alipoumizwa, hakutaka ajilaumu kwa hilo.
“Hakuna shinikizo. Ni heshima.” Ilikuwa heshima kwamba mtu bora kama huyo alimpenda.
“Yeye ni nani?” Nilesh alikunja ngumi, akijizuia.
"Ni mtu unayemfahamu." Alissa alisema, "Kendrick."
“Kendrick?” Nilesh alishtuka, kisha akatoa tabasamu la utulivu, “Ni jambo lisilotarajiwa na la busara. Mimi sikutegemea kabisa.”
Alikaa na Alissa kwa miaka minne na Alissa alimchukulia kama rafiki tu. Alissa na Kendrick walikuwa wamefahamiana kwa muda usiozidi miezi mitatu tu, lakini wangeweza kuoana na kutumia maisha yao pamoja.
Je, asingewezaje kuwa na wivu na huzuni?
"Kwa kweli, tumefahamiana kwa muda mrefu." Alissa alijua kile Nilesh alikuwa akifikiria na polepole alizungumza juu ya siku za nyuma, "Miaka mitatu iliyopita ... Kwa hivyo, tumeanzisha uhusiano hivi majuzi. Nilesh, najua nilipaswa kukuambia kuhusu uhusiano wangu naye. Lakini sikuweza kwa sababu ya vikwazo vya mkataba. Sikutarajia kwamba mambo yangetokea hivi … nilimpenda, na pia alikuwa na hisia kwangu.”
"Haya ndiyo matokeo bora zaidi. La sivyo, ningempiku.” Nilesh alihisi kitulizo baada ya kusikiliza alichosema, “Ninaweza kuja lini kwenye harusi yako?”
“Bado hatujaamua. Lakini urasmi haujalishi. Kilicho muhimu ni dhamira ya kuwa pamoja.”
"Uko sahihi. Lakini akikutendea vibaya, nitakuondoa na sitampa nafasi tena.”
Sura ya 156
Alissa alijisikia raha baada ya kumwambia Nilesh kila kitu. Walifaa zaidi kuwa marafiki kuliko wapenzi.
“Sijamwona Doris kwa muda mrefu. Vipi nimchukue na wewe kutoka shuleni baada ya kazi na kwenda kula chakula cha jioni?" Nilesh alipendekeza.
Alikuwa akimpenda sana Doris zaidi ya Kendrick. Lakini Kendrick alikuwa baba yake Doris. Hapa ndipo mahali ambapo Kendrick alikuwa na faida zaidi ya Nilesh. Kwa hivyo, Doris alihisi Kendrick alikuwa mkarimu mara ya kwanza walipokutana.
"Sawa." Alissa alikubali.
Nilesh, ambaye alikuja tu Mwanza, alikuwa mgeni, na Alissa alikuwa mwenyeji. Kwa hivyo, kwa kawaida angepaswa kutekeleza majukumu ya mwenyeji.
Mbali na hilo, Nilesh hakuwa bosi wake tu, bali pia rafiki yake. Alikuwa amemtunza kwa miaka mingi na alikuwa na deni kubwa kwake. Alipaswa kumlipa. Chakula kinaweza kuonyesha fadhili zake.
Kwa njia hiyo, Alissa na Nilesh walifanya mipango. Nilesh aliondoka na kwenda kwa Mathew kuzungumza juu ya mambo kadhaa.
Baada ya kumaliza kuongea, Nilesh hakutoka akakaa kwenye sofa ofisini kwa Mathew akinywa chai.
"Bwana Nilesh na Alissa wanafahamiana sana.” Mathew alichukua birika na kumimina chai kwenye kikombe chake.
“Ndiyo.” Nilesh hakuwa na haya, "Nilifikiri alikuwa wa pekee sana tangu alipojiunga na kampuni. Ana mawazo maalum na talanta katika kazi. Kwa kuthamini talanta yake, nilimpa nafasi na aliitumia vizuri sana.
"Kwa kweli Alissa ni mchanga na ana talanta." Mathew naye alifikiri hivyo.
"Sikutarajia angerudi Mwanza. Kwa hivyo, tafadhali umtunze katika siku zijazo, Bw. Matthew." Nilesh alifikiri kwamba angeweza kumhifadhi Alissa kwa maisha yake yote. Hakutarajia kumwacha.
” Usiseme hivyo, bwana Nilesh. Alissa ni mzuri sana na ana uwezo. Hahitaji matunzo ya wengine hata kidogo.” Matthew alikuwa akisema ukweli, “Bila shaka, nitamtendea kwa fadhili talanta kama yeye.”
Kama msimamizi, bila shaka alitaka kuweka wafanyikazi wake bora. Wakati kama mfanyakazi mwenza, kwa kawaida alipaswa kujiweka mbali na Alissa.
Baada ya yote, Kendrick na Alissa walikuwa na utata kwa kiasi fulani. Hakutaka kuwa mwiba kwa Kendrick.
“Samahani kumsumbua Bwana Matthew kuanzia sasa.” Nilesh akanyanyua chai yake kama zawadi.
Mathew naye aliinua chai yake kwa malipo. Baada ya kunywa chai hiyo tamu, aliinuka, “Jisikie nyumani bwana Nilesh. Naenda kazini sasa hivi.”
"Sawa." Nilesh aliitikia kwa kichwa na kunywa chai yake, akisubiri hadi Alissa atakapotoka kazini.
Nilesh aliona kuwa muda ulikuwa umekaribia. Mathew naye alikuwa tayari anafungasha vitu vyake.
"Alissa anaenda kumchukua binti yake baada ya kazi. Bwana Nilesh itaambatana naye?” Mathew alichukua koti la suti nyuma ya kiti na kuivaa.
“Ndiyo. Sijamuona Doris kwa muda mrefu.” Nilesh alikuwa mpole zaidi huku akimtaja Doris.
Mathew alienda kwa Nilesh. Kwa kawaida alisafisha pingu za shati lake jeupe na sehemu ya ziada ya pingu za suti na kuonekana mpole.
“Mwanangu yuko darasa moja na binti wa Alissa. Kwa nini tusiende pamoja huko?” Mathew alisema.
“Twende zetu.” Nilesh alitoka na Mathew akafuata.
Walienda kumtafuta Alissa mara tu Alissa alipotoka. Matthew alitabasamu na kusema, “Tunaenda hukohuko. Kwa hiyo, twende tukawachukue watoto pamoja.”
Alissa akaitikia kwa kichwa. Wote watatu walichukua lifti hadi kwenye maegesho ya chini, ambapo Alissa aliiendea Range Rover yake nyekundu na kubonyeza ufunguo wa kufungua milango.
Nilesh kwa kawaida alivutiwa na gari lake la kupendeza la kisasa. Akausogelea na kuuvuta mlango na kukaa ndani yake.
“Jifunge mkanda wako wa kiti.” Alissa alimkumbusha.
Mathew aliendesha gari lake kwanza, na kisha Alissa akafuata.
"Inaonekana anakupenda na mkarimu sana." Nilesh alidhani gari hilo ni zawadi kutoka kwa Kendrick kwa Alissa.
Alissa alitunza pesa na hangepoteza pesa zake kwa usafiri wa gharama kubwa kama huo. Pili, mapato yake hayakumtosha kununua gari la gharama kubwa kama hilo. Kwa hivyo, hakuweza kufikiria sababu yoyote kwa nini angekuwa na gari la kifahari muda mfupi tu baada ya kurudi Mwanza na aliweza kumfikiria Kendrick tu.
Alissa alijivunia sana na hakuwahi kupokea zawadi kutoka kwa mtu yeyote bila sababu. Hakutaka kuwa na deni kwa mtu yeyote, ikiwa ni pamoja na yeye.
Ila alikubali gari la Kendrick kumaanisha alimkubali sana Kendrick na hakumchukulia Kendrick kama mtu wa nje.
Nilesh alihisi kuwa mgumu na mwenye uchungu. Alikuwa amechelewa sana baada ya yote.
"Hakuninunulia yeye." Alissa alijua angeelewa vibaya na akaeleza, “Nilifika nyumbani na kukuta dada yangu alikuwa na gari zuri sana. Kwa hiyo, nilimwomba baba yangu aninunulie pia. Hiyo ilikuwa haki.”
Nilesh alishtuka, hakutarajia baba yake Alissa angekuwa tajiri kiasi hicho, “Baba yako ni nani?”
“Haijalishi yeye ni nani hata kidogo. Kilicho muhimu ni kwamba anipe kile ninachostahili.” Alissa hakutaka kumtaja baba yake ni nani. Lakini, hakukuwa na uhusiano wa kifamilia kati yao. Ingefanya watu wacheke tu.
Nilesh hakuuliza maswali zaidi. Kwa kuwa hakutaka kusema hivyo, hakuuliza.
Alissa hakuendelea na mada. Muda si mrefu, walifika katika shule ya chekechea.
Gari lake lilikuwa limeegeshwa nyuma ya lile la Mathew. Walishuka kwenye gari na kuingia chekechea wakiwa na cheti. Kisha, wakaenda darasani na kuwachukua Doris na Walter na kuachana kwenye lango.
Walter alichukia kuachana na Doris. Alissa aliwaalika, “Mr. Mathew, kwa nini usiende kula chakula cha jioni pamoja nasi?”
“Sahau muda huu. Bw. Nilesh huja Mwanza mara chache. Ni lazima nyie muwe na mengi ya kusema, sitawasumbua. Kutakuwa na fursa kwangu kumualika Bw. Nilesh na wewe kwenye chakula cha jioni.” Mathew alikuwa na busara na hakutaka kujisumbua na kuharibu uhusiano kati yao.
"Walter, sema kwaheri." Mathew alimvuta mwanae.
Walter akamwambia Doris, "Kwaheri."
Pamoja na hayo, waliondoka. Alissa alimpeleka Doris kwenye gari.
"Unataka kula nini?" Alissa alimuuliza Nilesh.
"Mgeni anapaswa kuendana na urahisi wa mwenyeji. Chochote unachotaka, nitakula.” Nilesh hakuwa mchaguzi. Alitaka tu kutumia muda zaidi pamoja naye.
Alissa kisha akaendesha gari hadi kwenye mgahawa mzuri wenye mpangilio mpana na rahisi, ambao uliwafanya watu wajisikie vizuri.
Ghorofa ya kwanza ilikuwa ukumbi. Ghorofa ya pili, ya tatu na ya nne vilikuwa vyumba vya watu binafsi.
Waliketi sebuleni na walikuwa karibu na dirisha la ua wa ndani. Nje, kulikuwa na mianzi ya kijani na mtazamo hapa ulikuwa mzuri.
Alissa alimwomba Nilesh aagize, lakini alimruhusu afanye uamuzi.
Alissa kisha akaagiza sato watatu wakukaangwa na chips, ambayo iliwafaa.
Aliagiza vinywaji na kuzungumza na Nilesh huku akisubiri vyakula.
Hawakugundua kuwa kuna mtu alikuwa akiwatazama kwa muda kwenye ngazi na alikuwa ametoa simu yake ya mkononi kutafuta pembe za hila za kupiga picha.
Alissa na wale wengine wawili hawakuliona kabisa. Kisha, vyakula vilitolewa.
Sura ya 157
Doris, kula zaidi samaki, hawa samaki ndiyo unaowapenda zaidi." Alissa akampa Doris mnofu.
“Sawa.” Doris alikula kimya kimya.
Alissa alimkaribisha Nilesh, “Furahia. Huwezi kufika Mwanza na usile sato. Ikiwa huzipendi, agiza nyingine.”
"Zote zinaonekana vizuri sana." Nilesh alifikiri kwamba vyakula hivyo vilikuwa vya kupendeza na chakula kilikuwa kitamu, jambo ambalo liliamsha hamu yake ya kula.
Nilesh alikula samaki hiyo na akafikiri ilikuwa tamu.
Alissa alikuwa ametoka kula chakula mara ujumbe ukaingia kwenye simu yake kutoka kwa Kendrick.
Kendrick: [uko wapi?]
Alissa alikuwa na hofu kidogo. Lakini hakuthubutu kufikiria sana. Kwa hivyo, alijibu: [Natoka kazini. Wewe uko wapi?]
Kendrick akajibu haraka haraka: Niko kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza.
Mkono wa Alissa ulikuwa dhaifu na nusura adondoshe simu: [Unakuja Mwanza tena? Mbona hukuniambia mapema?]
Kendrick: [Nilitaka nikupe surprise tu.]
'Siyo mshangao, lakini mshtuko, sawa?' Alissa alijiwazia na kujaribu kutulia.
"Nini tatizo?" Nilesh alimuona Alissa akiitazama simu yake. Kitu kilionekana kuwa kibaya.
“Hakuna kitu.” Alissa alimtazama Nilesh na kuendelea kumjibu Kendrick: [Hakika ni mshangao.]
Kendrick alisema tena: Ndo nimeshuka tu na sikupanga gari kuja kunichukua. Njoo unichukue, sawa?
Angewezaje kuondoka sasa? Hangeweza kumwacha Nilesh tu na kwenda zake.
Vinginevyo, Nilesh angefikiria nini kuhusu hilo? Angekuwa mwanamke ambaye alipendezwa zaidi na mumewe kuliko marafiki.
Alissa alijibu huku akitegemea Kendrick asingesisitiza: [Siwezi kuondoka sasa hivi. Unaweza kuchukua teksi hadi hoteli. Nitakuja kwako baadaye.]
Kendrick "alihuzunishwa" sana kama alivyotarajia: [Ni nini muhimu zaidi kuliko mume wako? Bi. Mayala, unataka kukataa kutekekeza jukumu lako?]
Alissa akashusha pumzi kidogo, akimtazama Nilesh upande wake. Ilionekana kwamba angeweza tu kusema ukweli. Isitoshe, yeye na Nilesh walikuwa marafiki wasio na hatia. Ilikuwa kawaida kwa marafiki kula chakula cha jioni pamoja.
Alissa alipima maneno yake: ,[Nilesh amekuja hapa Mwanza kikazi. Ningependa kutekeleza majukumu ya mwenyeji na kumshukuru kwa kunitunza miaka hii yote.]
Sekunde kumi, nusu dakika, dakika…zilipita dakika mbili na Kendrick hakujibu.
Alissa alihisi kuwa muda wa kusubiri ulikuwa ukiongezeka na alikuwa na wasiwasi kidogo.
Alituma ujumbe: [Je! una hasira? Bw. Nilesh anakuja Mwanza kwa mara ya kwanza. Yeye ni rafiki yangu na bosi wa zamani. Ninapaswa kukutana naye na kumwalika kwenye chakula cha jioni. Hata hivyo, sikufanya chochote kibaya. Ikiwa una hasira, sina la kusema.]
Alissa hakukubali, lakini alizungumza mawazo yake vyema.
Kendrick bado hakujibu. Alissa hakumsubiri. Katika chakula cha jioni na marafiki, ilikuwa ni kukosa heshima kuendelea kuzungumza kwenye simu.
Nilesh pia aliweka uma chini na kumtazama Alissa ambaye alikuwa akitazama simu na hakula, "Alissa, ikiwa kuna chochote, sema tu."
Nilesh aliweza kusema kutoka kwa uso wake kwamba alikuwa na wasiwasi juu ya jambo fulani.
“Mimi…” Alissa alipokuwa karibu kuongea wakati ujumbe ukaingia kwenye simu yake, “Subiri kidogo.”
Akabonyeza ujumbe kutoka kwa Kendrick. Ilikuwa na picha chache zake na Nilesh katika mgahawa huu.
Pembe ya picha ilikuwa ngumu. Kwa hiyo, ilionekana kana kwamba walikuwa na utata kidogo.
Alissa alikunja uso. Ilionekana kuwa kuna watu ambao hawakumpenda katika mgahawa huu waliwaona, au mtu alikuwa akimfuatilia.
Ikiwa ilikuwa ya kwanza, basi mtu nyuma ya hii alikuwa anatisha sana. Mtu huyo lazima atake kumfanya Kendrick amuue.
Haishangazi Kendrick alituma ujumbe kama huo akiuliza yuko wapi wakati huu. Ilionekana kuwa alipokea picha hizo mapema.
Kendrick: [Nilifikiri hungeniambia kuwa Nilesh alikuwa na wewe. Lakini kwa vile uliniambia, sina hasira na wewe. Ana bahati sana kwamba Bi Mayala anaweza kula chakula cha jioni pamoja naye. Isitoshe, sikuja Mwanza, nilikuwa nakuzingua tu.
Kendrick alikuwa anamjaribu tu kama atasema ukweli.
Alissa akajibu: [lini umeanza tabia mbaya hivyo? Hata ulinidanganya hivi?]
Kendrick: [Unadhani sijui Nilesh anawaza nini? Je, ni lazima niwe mtu wa kutojali na mkarimu ninapomwona anamfukuzia mke wangu?]
Alissa aliweza kufikiria kuwa Kendrick alikuwa akiinua nyusi zake kwa dharau pale.
Alissa: [Ni chakula tu. Nina deni kubwa kwake na lazima nimrudishie fadhila. Mbali na hilo, Doris pia yuko pamoja nasi. Una wasiwasi gani? Bila Nilesh, hakungekuwa naye sasa.]
Kendrick akajibu: [Niko kwenye ulinzi dhidi yake, sio wewe. Nitamlipa kwa ajili yako kama mume wako. Unaruhusiwa kujitolea kufanya tena. Hata ikibidi ufanye, lazima niwepo pia.]
Alissa: [Nitaripoti kwako mapema, sawa? Lakini ulinidanganya. Unafikiri nifanye na wewe?]
Kendrick: [Nitaoga na nilale kitandani upendavyo.]
Alissa alikunja pua yake nzuri. Yeye hakujali, sawa?
Hatimaye Alissa akajibu: [Lazima nile vya kutosha ili nipate nguvu. Usisumbue chakula changu cha jioni. Wacha tuzungumze juu yake baada ya kurudi nyumbani. Kwaheri.]
Alissa kisha akaiweka simu yake pembeni na wala hakujishughulisha kusoma meseji zozote.
Nilesh bado alikuwa akisubiri majibu yake.
“Alijua uko Mwanza na tunakula chakula cha jioni pamoja. Kwa hiyo, aliniruhusu nikutendee mema.” Alissa alikuwa anasema uwongo tu.
Nilesh alitabasamu, "Ninaogopa hii sio kutoka kwa Bwana Kendrick, lakini kutoka kwako kwa ajili yake."
Alimfahamu vyema Kendrick. Kendrick hatawahi kusema maneno ya upole kama haya. Lilikuwa neno la fadhili kutoka kwa Alissa ambaye alitaka 'waelewane'.
Alissa aliendelea kutabasamu, “Alisema mengi. Lakini ndivyo alivyomaanisha kwa ufupi.”
“Alijua ninakula chakula cha jioni na wewe hapa. Hajakuaibisha?” Nilesh hakutaka kumsumbua, "Naweza kumuelewa."
"Hakuna haja. Nimeweka wazi, na hakuniaibisha.” Alissa hakutaka kusema kwa Kendrick nia ya wao kula chakula cha jioni pamoja.
"Alissa, ikiwa anakutendea vibaya, mimi ..."
Alissa akamkatisha, "Hebu tuharakishe na tule chakula chetu, au kitakuwa baridi na kuathiri ladha." Alibadilisha mada na kumpa Nilesh msisitizo wa kula.
Nilesh alisisitiza kumaliza maneno yake, “Alissa, nitafurahi ikiwa utaishi maisha ya furaha. Ikiwa sivyo, sitaki mtu yoyote akudhuru, hata kama mtu huyo ni Kendrick.”
“Sidhani kama mimi ndiye nitajiumiza. Nilesh, usijali. Najua ninachopaswa kufanya. Haijalishi nini kitatokea kwangu na Kendrick mwishowe, sitawahi kukudurika. Unaelewa?" Alissa aliogopa tu kwamba Nilesh angebaki hivi kila wakati. Ikiwa ndivyo, angehisi hatia.
“Hupaswi kuyatoa maisha yako kwa ajili yangu. Nilesh, tazama mbele. Furaha inakungoja sio mbali."
"Wacha tuwe marafiki maishani, sawa?"
Sura ya 158
Alissa alitoa maoni yake kwa dhati na kwa uthabiti. Alitaka tu Nilesh aache wazo la kumngoja milele.
Maisha yalikuwa mafupi kama miongo ya miaka. Aina hii ya dhabihu ilikuwa tu kupoteza muda na maisha, ambayo kwa kweli haikuwa ya haki kwake.
Mtu anapaswa kuishi maisha kwa busara zaidi. Kupenda kwa kila nyuzi ya nafsi yake wakati kuna mtu wa kupenda, na kujipenda mwenyewe wakati hakuna.
Nilesh alijua kwamba Alissa alikosa amani kwa sababu alitaja hilo tena, “Alissa, samahani. Nilisema hivyo kwa kukata tamaa kabisa. Ni sawa tuwe marafiki kwa maisha yote, lakini usitilie umuhimu zaidi kwa mpenzi wako kuliko rafiki."
"Bila shaka hapana." Alissa alitabasamu kwa utulivu, na aliamini Nilesh angetimiza ahadi yake.
"Vizuri." Nilesh akachukua glasi ya kinywaji kutoka mezani.
Alissa naye akachukua glasi na kugonganisha naye. Walisema kwa mtiririko huo.
"Uwe na furaha."
"Urafiki wetu na udumu milele."
Baada ya kuongea walikunywa na kula, wakitazamana huku wakitabasamu.
Baada ya chakula, Nilesh alikuwa karibu kulipa bili wakati Alissa alipomsimamisha, “Hii ni Mwanza, ninapoishi, na mimi ndiye mwenyeji. Ukilipa bili, nitakasirika na hatuwezi hata kuwa marafiki katika siku zijazo.”
Kwa hivyo, Nilesh alikubali. Alissa alilipa bili na kujisikia furaha sana, akihisi kwamba amepunguza mzigo wa fadhila ambazo Nilesh alimdai.
Alissa alimrudisha Nilesh kwenye Hoteli aliyofikia, na akaendesha gari kurejea nyumbani pamoja na Doris.
Alissa na Doris walisoma vitabu kwa muda. Kisha Alissa akamuogesha Doris, akambembeleza hadi akalala na kwenda kumuona bibi kama kawaida yake...
Ilikuwa karibu saa 10:00 usiku alipopanda ghorofani kwenda kulala. Kendrick akampigia simu.
“Mbona hujanijibu kwa muda mrefu hivyo?” Kendrick aliuliza.
“Unataka kuanzisha ugomvi?” Alissa alisimama kwenye kibaraza cha ghorofa ya pili.
Kendrick alipigwa na butwaa, na kuwaza kwa sekunde chache, “Unataka kufanya nini?”
“Mimi na yeye ni marafiki tu. Tumekula tu pamoja. Je, unanitilia shaka sasa? Nimeacha mambo mengi kwa ajili yako. Huniamini?” Alissa alihisi huzuni na hasira kidogo.
Ikiwa Kendrick bado hakujua ni nini kilikuwa kimetokea kusikia hivyo, basi alikuwa mjinga sana.
"Bi. Mayala alicheza mchezo mzuri sana." Kendrick alitabasamu kidogo, "Ninahitaji kujibu nini ili kukusaidia kucheza vizuri zaidi?"
"Unamaanisha nini?" Alissa aliuliza huku akishtuka sana, “Utanitelekeza? Kwa nini? Si ulisema ingawa huwezi kunitajia jina la mke wako, utanitendea mema kama mkeo na kamwe hutaniacha?”
"Hapana, tuachane." Kendrick alishirikiana naye, baada ya kuelewa kile Alissa alimaanisha.
“Sitaki kuachana, na sihitaji kujua jina la mkeo. Nataka tu kubaki na wewe.” Alissa alimsumbua, "Sitaogopa hata kama anajua."
"Nilichosema hakitabadilika kamwe, na hatuna uhusiano katika siku zijazo."
"Nini? Vipi kuhusu ujana wangu wa miaka mingi? Je, utarudi upande wake? Ungewezaje kunidanganya? Sitakubali kamwe…”
"Matokeo yake ni sawa ikiwa unakubali au la."
“Siwezi kukupoteza… Usikate simu… wewe…” Alissa alishusha earphone masikioni na kuitazama huku akisema kwa meno ya kusaga, “Mwanaharamu!”
Alissa alikasirika sana hadi akahisi kuishiwa nguvu, mikono ikiwa kwenye uzio, na macho yake yakawa mekundu.
Mtu mwembamba alitembea karibu polepole, hadi akasimama mbele ya Alissa.
“Alissa, uko sawa?” Melissa alikuwa na wasiwasi juu yake.
“Hakuna kitu.” Alissa alijizuia kutokwa na machozi, akarudi kwenye sura yake ya baridi.
“Nimesikia unaonekana umegombana na mtu. Lakini Alissa, usifikirie sana. Nilishuka tu kunywa maji nikasikia sauti yako kali, nikaja kutazama. sijaelewa chochote.” Melissa alijieleza.
"Ni wewe unayehangaika sana. Sasa nina furaha sana kila siku. Nitagombana na nani?" Alissa alihamisha nywele zake kutoka mbele hadi nyuma ya bega kwa umaridadi, akionyesha shingo yake nzuri na maridadi, "Umesikia vibaya."
“Labda nimesikia vibaya. Sisikii vizuri kwa sababu ya kuwa mjamzito. Alissa pia umezaa na Doris nadhani umenielewa, au sivyo? Utakuwa na hasira na mimi?" Melissa akampa glasi, "Unataka kunywa maji?"
“Melissa, huoni ni uchafu? Kwanini unafanya hivyo.” Alissa alitazama juu kwa kidevu kilichoinuliwa kidogo, “Nenda tu kulala mapema. Ikiwa mwanamke hatapata usingizi wa kutosha akiwa mjamzito, ni rahisi sana kupata mikunjo na kuonekana mzee.”
"Mbali na hilo, ni rahisi kupata siasma na kunenepa… Mwanamke atashushwa hadhi mara tu akiwa mjamzito, na atakuwa na ugonjwa wa siasma mbaya, na ngozi iliyolegea baada ya kuzaa… Inachukiza sana.”
"Ingawa wewe ni mrembo wa kuzaliwa, ninaogopa huwezi kukwepa sheria ya asili. Wanaume ni wanyama wenye hisia, na watatoa macho zaidi kwa wanawake wachanga na warembo wenye umbo la kuvutia la mwili. Afadhali uzingatie zaidi mumeo. Unakuwa mzito siku baada ya siku. Katika siku za upweke… Mume wako angefanya nini? Unapaswa kuwa mwangalifu ili usimruhusu kutongoza mwanamke mwingine. Ikiwa ndivyo, juhudi zako zote zitabatilika.”
Alichokisema Alissa kiliufanya uso wa Melissa kubadilika rangi. Alissa alimkumbusha Melissa kwamba Melissa alimnyang'anya Seidrick, na ingetokea pia kwa Melissa.
“Alissa, una wasiwasi sana. Haitatokea kamwe.” Melissa alijiamini sana, lakini alisema kwa ngumi zilizofungwa kwa nguvu, "Ninataka kupendekeza uweke nafasi yako."
“Sina busara kama wewe. Nimechoka na ninaenda kulala.” Alissa aliondoka kwa hatua za kifahari na zisizo na wasiwasi. Umbo lake jembamba na refu lililopungua bado lilikuwa la kuvutia sana.
Lakini nini? Labda alikosana na Kendrick. Kumpoteza Kendrick kama mlinzi, angeridhika hadi lini?
Anachopaswa kufanya Melissa sasa ni kuweka kipaumbele zaidi kwa Seidrick. Hakuweza kumruhusu Alissa kumnyang'anya Seidrick kwa sababu alikuwa mjamzito.
Ilibidi atafute nafasi ya kumfanya Alissa awe na sifa mbaya kama miaka 5 iliyopita, na hivyo kumfanya Alissa asiinuke tena.
Alissa alipoingia tu chumbani, akampigia tena Kendrick, Kendrick akaitikia haraka.
"Melissa alikuwa karibu nami sasa hivi."
"Kwa hivyo uliigiza kuachwa na mimi ili kumchanganya?"
“Ndiyo. Ikiwa amefanya kitu kwenye zile picha, basi matokeo haya yatamfanya kupata kile anachotaka." Alissa aliketi kwenye kiti cha mkono, akisema kwa miguu iliyovuka, "Basi nitamsaidia."
"Niamini. Tutajua kama ni yeye au la hivi karibuni." Kendrick akasema, “Dada yako ana hila sana. Lazima kuwe na mtu anayemfundisha somo zuri."
"Unafikiria sawa na mimi." Alissa aliweka kidevu chake kidogo kwenye miguu yake, kwa macho ya baridi kidogo. Angemrudishia kile ambacho Melissa alikuwa anadaiwa kidogo kidogo.
"Melissa, ngoja tu uone." Ilikuwa kawaida kwamba mtu alipe deni lake. Alissa hangeweza kamwe kuwa laini na asiye na msimamo.
Sura ya 159
Wikendi hii, kungekuwa na karamu ya biashara katika Hoteli ya Kimataifa ya Garden, na watu wengi mashuhuri na wafanyabishara mashuhuri wangehudhuria, ambayo ilikuwa fursa adimu.
Nilesh na Matthew pia wangehudhuria karamu hiyo. Nilesh alikuwa tayari amemuomba Alissa ahudhurie pamoja naye. Baada ya yote, Nilesh alikuwa muungwana mseja, mchanga na mwenye kuahidi, hivyo alihitaji mwenzi wa kike.
Ikiwa Nilesh angewaomba wanawake wengine katika kampuni hiyo waandamane naye, bila shaka wangeanza kumsogelea, ambayo ingesababisha shida nyingi.
Lakini Alissa hakutaka. asingetaka hata kama angemtaka. Alikuwa mtu bora kuwakilisha kampuni.
Saa 7:00 jioni, taa zenye kung'aa katika hoteli hiyo zilikuwa nzuri sana. Wengi wa watu wa ndani walikusanyika hapa, wenye kelele sana.
Nilesh na Alissa waliingia katika jumba la karamu la hoteli hiyo. Baada ya kuingia ndani, walisababisha msukosuko na umakini.
Nilesh alivaa suti nyeupe, tai nyeusi, na uso mzuri, umbo refu na jembamba na tabia nyororo, kama Prince Charming.
Alissa alimshika mkono Nilesh. Macho yake mazuri yalikuwa yakiangaza chini ya taa, na midomo yake myekundu na nywele ndefu nyeusi zilivutia sana. Alivaa vazi refu la rangi ya champagne lililotengenezwa kwa chachi laini ya tabaka nyingi, mrembo sana kama mrembo aliyeanguka kutoka ulimwengu mwingine.
Mtu aliyemfahamu Nilesh akasogea mbele kuwasalimia, na Nilesh akajibu kwa upole. Alissa naye alitajwa katika mazungumzo yao.
"Mwanamke aliye karibu na Bw. Nilesh ni mrembo sana, na amemvutia kila mtu aliyepo."
“Asante.”
“Nashangaa ni lini ninaweza kuhudhuria harusi ya Bw. Nilesh?”
“Siku moja. Subiri."
Nilesh hakukataa wala kukiri, akajibu tu swali. Hakusema kuwa yeye na Alissa walikuwa marafiki na wafanyakazi wenza tu ili kumlinda Alissa asinyanyaswe na wengine.
Kwa kawaida Alissa alijua kwamba Nilesh alikuwa akimlinda kimakusudi. Hakupenda wengine wamuulize juu yake, na kwa njia hii angeweza kuepuka matatizo mengi.
Nilesh pia hakutaka Alissa aangaliwe juu chini na wale wanaume waliokuwa wakivutiwa na urembo wa Alissa, lakini alipata kisingizio cha kumuacha Alissa aondoke kwenye umati wa watu, na yeye angeshughulika na watu hawa peke yake.
Kulikuwa na kila aina ya vitafunwa na vinywaji, matunda na divai kwenye meza ya buffet ya ukumbi wa karamu.
Alissa alijificha hapa na kuchukua matunda ili ale.
Kwa wakati huu, mhudumu alienda mbele, akiwa na glasi ya divai kwenye trei juu ya mkono wake wa kulia, "Bi Alissa, Bwana Nilesh aliniomba nikupe."
"Vizuri. Asante.” Alissa aliichukua kwa tabasamu, akiishika kwa ncha za vidole vyake.
Alitazama chini na kutikisa. Divai ilionekana kwenye kioevu giza nyekundu, nzuri sana.
Yeye hakunywa, lakini akaiweka kwenye meza.
Katika miaka hii, Alissa alikuwa na uzoefu mwingi na kuona mengi sana. Hakuwa msichana asiye na hatia na rahisi tena, na alikuwa macho zaidi kuliko hapo awali.
Hakunywa vinywaji vya ajabu, ambayo ilikuwa msingi wa kujilinda.
Alichukua chupa ya maji safi kutoka kwenye meza, na mhudumu aliyekuja kuchukua divai akauliza, “Bi, unahitaji bilauri yoyote tupu?”
“Asante.” Kwa kweli haikuwa kifahari kwake kunywa maji na chupa katika hafla kama hiyo.
Baada ya kutuma divai, mhudumu alileta glasi tupu, "Haya, bibiye."
Alissa aliichukua ile glasi na kuiangalia. Hakuona ubaya wowote, akamimina maji kwenye glasi.
Kwa wakati huu, Nilesh alikuwa amemaliza salamu na toast, na akachukua champagne ya dhahabu nyepesi kutoka mezani, na kugundua kuwa Alissa alikuwa ameshika maji mkononi mwake.
"Je, nidhamu ya familia ni kali sana? Hakuna champagne?" Nilesh alisema kwa mzaha.
"Hapana, sitaki tu kunywa pombe." Alissa alichukua maji kwenye glasi, "Unajua kwamba sipendi tukio la aina hii, ambapo lazima nijifurahishe na wengine."
"Lakini lazima uwe na mazoea." Nilesh alichukua shampeni, "Umemchagua, na itabidi uhudhurie karamu nyingi. Huwezi kukataa zote. Lazima uhudhurie karamu muhimu zinazohitaji mahudhurio ya wanandoa."
"Sijafikiria sana." Alissa hakufikiria sana, “Wacha tuijadili baadaye.”
Hapo awali walifunga ndoa kwa siri, ambayo haikutangazwa kwa umma. Kendrick alikuwa bado hajaoa machoni pa umma, kwa hivyo hakuhitaji kuandamana naye.
Lakini, sasa ndoa yao ilitangazwa kwa umma. Kwa kweli kungekuwa na hafla muhimu ambazo zilihitaji kuonekana kwao wote wawili. Anapaswa kutoa ushirikiano kwa ajili yake.
Wakati Alissa na Nilesh walipokuwa wakizungumza, Mathew alienda, “Bw. Nilesh, kampuni yetu pia ni mmoja wa wazabuni wa mradi wa FarmCom unaoshirikiana na kampuni ya Kilimo Kwanza na Kilimo Hai. Twende tuzungumze nao.”
"Sawa." Nilesh alitikisa kichwa, na kumwambia Alissa, "Njoo pamoja nasi, kwa sababu wewe pia unashiriki katika mradi huu."
Mradi huu ulikuwa mojawapo ya miradi muhimu zaidi ya Universal Group katika nusu ya pili ya mwaka. Kama mkurugenzi wa miradi wa ofisi kuu, Nilesh alipaswa kuchukua jukumu hilo.
“Sawa.” Alissa alihisi ni biashara tu, na hakukataa.
Matthew aliwachukua Nilesh na Alissa kwa umati, na wakakutana na Alex, Merry, Sam na Maira, Seidrick na Melissa. Ambao nao walikuwa wamealikwa kupitia kampuni za familia zao.
Ingawa Sam na Maira walisikia kwamba Alissa alikuwa tayari amerudi kwa familia ya Maziku, ilikuwa mara ya kwanza kwao kukutana naye baada ya miaka 5.
Baada ya miaka 5, Alissa hakuwa na hatia na mchanga kama hapo awali. Wakati huo ulimpa ukomavu na haiba, na alikuwa akivutia sana sasa, ambayo ilikuwa wakati wa dhahabu kwa mwanamke.
Kumwona Alissa, Sam alionyesha uso wa baridi kidogo, lakini Maira alionyesha tabasamu hafifu, la neema.
Alissa aliwatambulisha wao kwa wao.
Nilesh aliwasalimia familia ya Maziku na familia ya Masolwa. Alex na Sam walimsifu kwa kuwa mchanga na mwenye kuahidi.
Kisha Alissa akasema, “Bw. Masolwa, Bibi Masolwa.”
Sam alimpuuza Alissa, na Maira pekee aliitikia kwa kichwa.
Sam aliweka uso ulionyooka kama hapo awali, na hata akakunja kipaji kidogo.
Melissa, ambaye alishika mkono wa Sam, alisema kwa upole, “Alissa, ni mshangao ulioje! Kwa nini uko hapa? Nakumbuka kuwa hupendi tukio la aina hii.”
Alissa?
Nilesh na Mathew walishangaa. Hawakuwahi kufikiria kwamba Alissa alikuwa binti wa thamani wa familia ya Maziku.
Familia ya Maziku ilikuwa na ushawishi mkubwa katika Jiji la Mwanza, na baada ya kuunganishwa kwa ndoa na familia ya Masolwa, ilianza kushirikiana na familia ya Masolwa kibiashara. Thamani yao iliongezeka sana.
“Ninahudhuria tafrija hii kwa niaba ya kampuni. Unaweza kuniita Miss Maziku au Meneja Maziku.” Alissa aliweka umbali na Melissa kwa nje.
Melissa aliaibishwa ghafla na maneno ya Alissa, kana kwamba Melissa alijipendekeza kwa Alissa kwa makusudi.
"Alissa, mbona hujali?" Melissa alitabasamu ili kupunguza hali ya hila kati yao, "Sisi ni dada na tulikua pamoja."
"Afadhali tuweke wazi juu ya jambo fulani." Mtazamo wa Alissa ulimzunguka Seidrick karibu na Melissa, "Ingawa sisi ni dada, kuna kitu ambacho hatuwezi kushiriki na kila mmoja."
Sura ya 160
Kwa hakika, kidokezo cha Alissa kilimfanya Melissa kuwa na wasiwasi kwamba alishindwa kujizuia kushika mikono ya Seidrick kwa nguvu.
Seidrick pia alihisi wazi mabadiliko ya Melissa, hivyo alinyoosha mkono wake kimya kwenye mkono wake, ambao ulimshikilia kwa nguvu, na kumfariji.
"Alissa yuko sawa. Baadhi ya mambo ni wazi hayawezi kushirikiwa, kwa hivyo ni bora kutotamani vitu ambavyo si vyako.”
Seidrick akimlinda, Melissa alijiamini zaidi. Aling'ang'ania Seidrick kwa ukaribu zaidi, akionyesha kwamba Seidrick alikuwa wake.
Alissa hakujali hata kidogo, lakini sasa ilimbidi aigize nafasi ya mwanamke ambaye aliachwa na Kendrick na alitaka kumlenga Seidrick… Hii ilihitaji uigizaji stadi.
"Ndio, hata kama mtu alitamani na kupata alichotaka, hawakufanya kwa haki, hivyo mwishowe, wanaweza kuachwa ..." Alissa alipumua sana, kana kwamba alikuwa akijiongelea mwenyewe huku akimshutumu Melissa.
Melissa kwa kawaida alifikiria kuwa Alissa ameachwa na Kendrick. Alifurahi na tabasamu kidogo likajijenga usoni mwake.
“Uko sahihi,” Melissa alikubali.
Watu ambao hawakuwaelewa walihisi kwamba mazungumzo yao yalikuwa ya kutatanisha kidogo, lakini uadui wa maneno yao ulikuwa dhahiri.
"Bwana Alex, sikutarajia Alissa angekuwa binti yako. Yeye ni mtu hodari sana na mkarimu, na kazi yake ni bora. Kampuni inamthamini sana.” Nilesh alibadili mada na kumsifia Alissa.
“Asante, Bw. Nilesh.” Alex alitikisa kichwa na kutabasamu. "Ni kwa sababu kampuni ilimpa fursa."
Nilesh alileta mada za kikazi na akafanikiwa kupunguza hali hiyo.
Alissa alihisi kwamba kulikuwa na watu wengi hapa na kulikuwa na mtiririko mdogo wa hewa. Alikuwa na shida kidogo ya kupumua. "Samahani."
Baada ya kuongea aligeuka na kuondoka. Nilesh alimtazama kwa wasiwasi kidogo. Hakuonekana vizuri. Je, alikuwa anajisikia vibaya?
Lakini alianza mazungumzo hapa na Alex na Sam, kwa hivyo hakuweza kuondoka naye.
Alissa akatoka kwenye mlango wa nyuma wa jumba la karamu. Ilikuwa ni bustani ndogo isiyokuwa na mtu ndani, hivyo palikuwa kimya sana. Mimea ilikuwa imestawi vyema. Kulikuwa na upepo usiku. Hatimaye alijisikia raha, isipokuwa bado alipata upungufu wa pumzi ambao ulikuwa bado haujaisha.
Alissa aliona benchi karibu na kichaka cha maua, hivyo akasogea na kuketi.
Baada ya muda, sura ilionekana machoni pake.
“Bi Maziku, uko peke yako?" Sauti hii ilikuwa ya Timothy.
Alissa aligeuza kichwa chake na kumuona akiwa amesimama kwenye kivuli huku akiwa na tabasamu usoni ambalo lilionekana kuwa mbaya sana kwa wakati huu.
“Kuna nini bwana Timothy?” Alissa aligeuza uso wake kidogo na kumtazama.
“Vipi wewe na bwana Kendrick?” Timothy aliuliza kwa uwazi.
"Vizuri sana." Alissa alitabasamu sana, macho yake safi kama nyota zinazong'aa usiku.
"Bwana Kendrick huja kuambatana nawe mara kwa mara, lakini hajafika hapa kwa muda mrefu hivi majuzi. Atakuwa kwenye safari ya kikazi?” Timothy akasogea karibu zaidi, kivuli chake kikirefuka kwa miondoko yake.
“Hayuko katika safari ya kikazi, na hana shughuli nyingi sana kazini. Yeye huenda tu nyumbani kwa wakati kila siku kula chakula na mke wake.”
Kidokezo katika maneno yake kilikuwa dhahiri sana. Kendrick bado alimjali mke wake, na alikuwa tu mchezo wake wa pupa.
Sasa kwa kuwa alicheza naye na kupoteza hamu, alikuwa karibu au alikuwa tayari ameachwa.
"Kwa hiyo?" Alissa hakujali.
Kendrick alisasisha hali yake kwenye mtandao wake wa facebook, na zote zilihusu yeye kutoka kazini kwa wakati na kwenda nyumbani kuandamana na mke wake.
Kisha pia alichapisha baadhi ya picha za chakula hicho na nukuu zikisema kwamba alipenda watu wa familia yake zaidi na milo iliyopikwa nyumbani zaidi. Ingawa hakutaja wazi ni nani aliyeitengeneza, aliaminisha umma kwamba chakula kiliandaliwa na Bi. Mayala.
Ingawa Kendrick hakukubali wala kukanusha, aliwafanya wengine wamuamini.
Hata hivyo ni Alissa pekee ndiye aliyejua kuwa huo ni mpango ambao Kendrick na yeye waliutengeneza ili kuwachanganya adui.
"Bwana Kendrick amerudi kwa familia yake. Mbona unasubiri hapa kwa ujinga?" Timothy naye akaketi kando yake.
Alissa alisogea pembeni kidogo, hakutaka kujiweka karibu naye. "Hapana, hataniacha hivi."
“Kama msemo unavyosema, usipendane na mwanamume mwenye familia. Utaachwa tu.” Timothy alipomwona hivyo alitabasamu badala ya kukasirika huku akitazama kando ya uso wake maridadi. “Bi Maziku ni mwerevu sana, kwa hivyo hawezije kuelewa sababu? Isitoshe, Bwana Kendrick si mtu wa kawaida, na ndoa yake haiwezi kulinganishwa. Yeye ni mwenye nguvu na mtukufu. Ulijihusisha naye, lakini unaweza kumshinda? Wanaume wakimaliza kurukaruka nje watarudi kwa familia zao. Afadhali kuwa mke wa mtu kuliko kuwa hawara wa mtu.”
Alissa alishusha kope zake kidogo, macho yake yakionekana kulegalega. "Bwana Timothyuko sahihi. Mimi ni mjinga sana hata kumwamini…”
Aliruhusu machozi yajae machoni mwake na kuinua mkono wake kufuta chozi lililokuwa likimtoka. Sura yake ya kusikitisha iliwafanya watu wahisi huzuni.
“Bi Maziku, ikiwa haujali, naweza kukukopesha bega langu." Timothy akatoa kitambaa mfukoni na kumkabidhi.
Alissa akatingisha kichwa huku akijifanya ana nguvu. “Sijambo. Asante.
Sitaki tu kukubali. Sijali kama ameoa na ana mke. Nilimpa mwili na roho yangu. Alisema wazi atanilinda maisha yangu yote. Angewezaje kuvunja ahadi yake na kuniacha peke yangu?”
Timothy aliposikiliza maneno ya Alissa, alitabasamu kwa siri. Ilionekana kuwa alichokisikia Melissa kuhusu Kendrick na Alissa wakigombana kilikuwa kweli. Uhusiano wao ulikuwa tayari umevunjika. Sasa alijua kutokana na maneno ya Alissa kuwa Kendrick alikuwa ameachana naye.
Timothy alifurahi. Juhudi za pamoja za yeye na Melissa hazikuwa bure.
Walikuwa wakitarajia Alissa na Kendrick kuachana ili Alissa apoteze msaada wake. Hapo ndipo wangeweza kumwadhibu.
Alimdanganya kwa makusudi na kumtia aibu mbele ya Kendrick. Angewezaje kumsamehe na kumwacha aondoke kirahisi?
“Usiwe na huzuni. Tunaweza kuanza tena ukitaka.” Timothy alichukua mbinu ya upole, akijaribu kuvunja ulinzi wa Alissa wakati alikuwa 'amejeruhiwa' zaidi. “Sijali uhusiano kati yako na bwana Kendrick. Baada ya yote, hakuna mwanamke Bwana Kendrick hawezi kupata na uwezo wake.
“Sitaki kumzungumzia. Nataka kumsahau na kuanza upya.” Alissa alisema kwa upole. “Nataka kuingia ndani.” Alissa akainuka, na Timothy akamfuata.
Alissa aliporudi kwenye jumba la karamu, alisikia tu vurugu kubwa. Alimwona Kendrick, mtu mwenye mvuto zaidi mle chumbani, akiwa amesimama kati ya umati wa watu waliokuwa wakiongezeka.
Bado alikuwa kwenye shati jeupe la kawaida na suti nyeusi. Alikuwa mrefu na mwembamba, akilinganishwa na wanamitindo wa kiume, na alionekana mtanashati na maridadi kuliko wanaume wengine. Alikuwa amekomaa na ametungwa.
Macho yake ya kina yalikuwa makali na tulivu kutokana na uzoefu wa miaka mingi kuwa katika nyadhifa za mamlaka ambazo hakuna aliyethubutu kumvunjia heshima.