Simulizi: Usiniache

Simulizi: Usiniache

USINIACHE 4:
Sura ya 151


Alissa alisimama tu na kumuangalia Kendrick akitokomea. Alissa alijiona yuko salama.

Kendrick alikuwa anamuunga mkono, hivyo angeweza kusonga mbele bila wasiwasi wowote.

Alissa aliingia ndani ya gari baada ya kumuona Kendrick akitokomea mbali.

“Twendeni.” Alisema Alissa kwa upole.

Nora alifikiri kuna kitu kibaya kwa Alissa na Kendrick na kuuliza tena. “Kuna nini nyie?”

“Hakuna kitu. Nitakuambia baadaye.” Alissa akatikisa kichwa. “Hebu twende nyumbani kwanza.”

Nora hakuuliza zaidi, akamuomba dereva aendeshe gari.

Ndani ya gari, hatimaye Alissa alipumzika.

“Alissa, wacha kuniweka roho juu. Nina hamu ya kujua unachotaka kiniambia.” Alissa alimpeleka Doris.

Doris alikuwa mtulivu, na Nora alikuwa amempa simu yake acheze gemu. Akili yake yote ilikuwaimeishia kwenye simu.

Nora alikuwa dukuduku moyoni na Alissa alikuwa hana haraka.

“Una usingizi?”

"Hapana." Alissa alikaa kitako huku akihisi mtupu kidogo.

“Ulifanya muda gani jana usiku?” Nora hakuweza kuzuia udadisi wake. “Kendrick yuko sawa?”

“Jamani, unazungumza nini?” Alissa aliona haya kwa maneno ya Nora, “Sijafanya chochote naye.”

"Unataka kumdanganya nani Alissa? Kwa kumbato lile bado unadiriki kusema hukufanya?" Nora alishangaa, lakini Alissa aliitikia kwa nguvu.

Alimtazama Alissa kuanzia kichwani hadi miguuni na kurudi kwa macho mazito.

Hatimaye macho yake yakatua kwenye uso wa Alissa na kukunja uso. "Haipaswi kuwa hivyo."

"Nini?" Alissa alijiuliza huku akiwa amemtumbulia macho yake.

“Mwanaume gani hawezi kuvutiwa na umbo na sura yako? Mwanaume angekurukia na kulala nawe mara tu unapoingia naye chumbani. Bwana Kendrick na wewe ni mume na mke. Ni sawa kufanya ngono. Kwa nini hamjafanya lolote?” Nora alichanganua. "Mnasubiri nini? Au ni mgonjwa?"

"Ni sawa na hakuna chochote kibaya kwake." Alissa alikunywa maji, na ubaridi tulivu ukaenea kati ya meno yake.

“Umejaribu? Unathubutu kusema yuko sawa? Ikiwa yuko sawa, hakuwezaje kulala na wewe jana?" Nora alimtolea Alissa macho.

“Bila shaka nime…” Alissa nusura amwage ukweli, lakini mara moja akajirekebisha, “Amekuwa akifanya mazoezi kila siku. Nina hakika hana tatizo. Na sisi ni mume na mke, lakini sasa tuko kwenye uhusiano. Alisema ataniheshimu na nikisema tu ndio tutafanya hivyo.”

"Bwana Kendrick ni muungwana, sivyo? Ndiyo, anaonekana kuwa na nguvu.” Nora alikunywa maji yake. “Oh, sawa. Kwa nini alikuleta kwangu na kisha kuondoka peke yake? Kwanini asingekupeleka kwa Maziku?”

"Hapana, anarudi Geita." Mwanga wa nyota ukaangaza machoni mwa Alissa.

Nora alishika mng'ao wa macho yake. “Kwa hiyo huwa anakuja na kuondoka? Je, kuna kitu kibaya katika familia yao? Mbona umeondoka kwa haraka hivyo?”

"Hapana." Alissa alikanusha huku usoni akiwa na utamu mdogo wa kike. "Alitaka tu kuwa nami na kunirudisha salama Mwanza."

Hatimaye Nora alielewa, “Vema. Jinsi wewe ni mtamu.”

Alissa alikunywa maji mara mbili zaidi kwa kuridhika.

"Wale ambao wako tayari kutumia pesa na wewe wanaweza kuwa sio wale wanaokupenda, lakini wale ambao wako tayari kutumia muda adimu na wewe lazima wakupende.

"Kwa hivyo, mtu wa thamani zaidi ulimwenguni ni yule ambaye yuko tayari kutumia wakati na wewe. Mthamini mwanaume huyo, haswa anapokuwa mtu mwenye shughuli nyingi, na yuko tayari kubana muda wa kuwa na wewe."

Alissa aliguswa na maneno ya Nora.

Baada ya kuwa mbali na Kendrick kwa zaidi ya saa moja, alianza kumkumbuka, kum'miss kuwa kando yake, kumkosa kumshika mikononi mwake, kuimiss sauti yake, na kumiss busu lake.

"Itakuwa tamu zaidi katika siku zijazo." Alissa alijibu.

Nora alimpa dole gumba. “Ni vizuri kukuona hivi. Ni kama unakuwa wewe tena.”

“Ndiyo. Ninahisi kutaka kujipata tena.” Alissa aliwaza hivyo. “Wewe unaweza pia. Umepotea tu sasa hivi.”

"Ni juu yangu tena." Nora akahema. "Sio kila mtu ana bahati kama wewe kupata ubinafsi wako uliopotea. Sijisikii nimepotea tu, nahisi nimekufa.”

"Bila shaka huwezi kujikuta na mawazo hayo." Alissa alimfikiria ghafla mtu aliyemwona katika Dar es Salaam, na baada ya kusita kwa muda mrefu, alisema, “Nora, namaanisha nini ikiwa… Je, ikiwa hajafa?”

Nora alimtazama, akiwa na chupa ya maji mkononi, katika mkao wa kifahari.

"Uliniuliza swali kama hilo mara ya mwisho." Nora alidhani Alissa aliuliza mara mbili. “Kuna kitu unanificha?”

Alissa aliuma midomo yake, lakini aliamua kumwambia yote aliyoyajua. "Nora, utanisikiliza kwa utulivu?"

Nora akaitikia kwa kichwa.

“Siku moja tukiwa Dar, mimi na Jane tulikuwa tunakula chakula cha jioni, na mtu fulani alitulipia. Nilipotoka mbio, yule jamaa alikuwa tayari kwenye gari, na niliona uso wake kidogo kupitia dirisha lililoinuliwa. Nilifikiri anafanana sana naye… Bila shaka, kuna watu wengi duniani wanaofanana. Unajua, kuna kaka au dada mapacha waliopoteana, kwa hiyo nadhani ninaweza kuwa nimekosea.”

Nora, hata hivyo, alikuwa mtulivu sana na akasema, “Nadhani ulikosea. Au labda unaamini ni yeye, kwa hiyo ulifikiri kwamba mtu huyo ni kama yeye.”

Na kisha akaongeza, "Amekufa. Hatutakuwa tena naye.”

"Sawa, tuachane na hii." Alissa alijisikia faraja kusema, lakini haikumsaidia Nora.

Nora alikuwa mtulivu juujuu, lakini moyoni alijua kuliko mtu yeyote jinsi alivyokuwa anamtaka huyo mtu awe hai.

Alisema hivyo kwa sababu hakuthubutu kujipa mwanga wa matumaini, kwa kuhofia kwamba angemkosa zaidi, kwa kuhofia kwamba angepoteza hata ile furaha iliyojificha, na kuhofia ndoa hiyo isingeweza kumnasa.

“Niambie wewe na bwana Kendrick. Kwa nini ulimtazama sana wakati anaondoka?" Nora alibadilisha mada kwa haraka, “Ulisema utaniambia baadaye.”

“Hiyo ni kwa sababu tunamtafuta mtu aliurtufremu…” Alissa alimpa Nora maelezo mafupi ya kilichotokea, pamoja na mpango aliokuwa akiufikiria.

Sura ya 152

Baada ya safari ya karibu saa nzima barabarani kutokana na foleni, hatimaye Alissa alirudi kwenye makazi ya familia ya Maziku na Doris.

Giza lilikuwa likiingia na jumba hilo la kifahari lilikuwa na mwanga mkali.

Waliporudi, bibi Jenifer alikuwa tayari alikuwa ameenda kulala. Merry pekee ndiye aliyekuwa sebuleni. Alipomwona Alissa, alikuwa na shauku zaidi kuliko hapo awali, “Alissa na Doris, habari za jioni. Mmekula?”

“Ndiyo.” Alissa alimshika Doris na kukaribia kuondoka.

Merry akamuuliza tena, “Nimesikia kuwa ulienda Geita kikazi.”

“Ndiyo.”

"Umekutana na Bwana Kendrick?" Merry alikuwa na wasiwasi juu ya uhusiano wao sasa.

“Ndiyo.” Alissa alijua wazi anachomaanisha Merry,
“Hata aliachana na kazi zake kwanza na kuandamana pamoja nami. Tulikuwa na wakati mzuri.”

"Inapendeza." Merry alicheka, “

Usiku umeenda. Nenda ghorofani ukapumzike sasa. Usiku mwema." Alissa kisha akatulia na kumpeleka Doris juu.

Merry alisimama na kuwatazama wakipanda juu huku akikunja uso kwa kuchanganyikiwa.

Ilionekana kuwa kuna kitu kibaya. Melissa alisema kwamba alimwomba mtu aende kwa familia ya Mayala ili kufichua ukweli kwamba Alissa alikuwa hawara wa Kendrick. Familia ya Mayala ilikuwa ya kifahari sana kwamba mwanamke ambaye angeweza kuolewa naye anapaswa pia kuwa msichana wa kuvutia na alikuwa na historia ya nguvu. Kwa hivyo, familia ya Mayala ingeshughulikia. Mbali na hilo, Merry alisikia kutoka kwa Melissa kwamba mwanamume huyo alimwambia kwamba ingawa bwana wa familia ya Mayala hakukasirika sana, alikosa furaha kidogo.

Kwa hivyo, Alissa hakupaswa kuandamana na Kendrick kwa furaha.
Au Melissa alidanganywa na mtu huyo?

Wakati huo, Alex, ambaye alikuwa amerudi kutoka kwenye karamu ya chakula cha jioni, aliingia na kumpiga kiwiko Merry ambaye aliganda, "Unaangalia nini?"

“Hakuna kitu.” Merry hakuthubutu kumwambia Alex juu ya kile Melissa alichokifanya. Kwa sababu aliogopa kwamba Alex angeharibu mpango wao.

Hakukubaliana na Melissa. Lakini pia hakutaka Alissa awe na kiburi kwa sababu ya Kendrick katika familia ya Maziku. Kwa hivyo, alifumbia macho kile Melissa alikuwa amefanya.
***
Alissa ilimbidi akamilishe mradi wa FarmCom baada ya wiki mbili. Kwa hiyo, ilimbidi kuwa bize na kazi yake. Muda ulikimbia.

Yeye na Kendrick hawakuwa na mawasiliano ya ana kwa ana. Lakini wangezungumza kwenye simu.

Kendrick alimtumia hii saa sita mchana: [Hata kama uko busy na kazi, unapaswa kula.]

Alissa alijibu kwa njia ya kucheza na kufurahisha: [Sina shughuli nyingi kama Bwana Kendrick. Mimi ndiye ninayepaswa kuwa na wasiwasi iwapo Bwana
Kendrick ana mlo mzuri.]

Kendrick kisha akainuka na kuiendea meza ya duara karibu na sofa. Kulikuwa na vyakula kadhaa mezani, vyote hivyo vilikuwa ni chakula cha mchana ambacho Chale alimuagizia kila siku.

Kendrick: [Je, ungependa kuungana nami?]

Alissa alituma emoji: Mlo wa mchana wa bwana mkubwa ni wa gharama sana! Najihisi mimi ni maskini sana.]

Kendrick aliketi kwenye sofa: [Unataka kula? Ni haki tu kwamba unatoa kitu kwa kubadilishana, sivyo? Bi. Mayala.]

Alissa alituma emoji ya busu ili kumhonga Kendrick.

Kendrick alitabasamu: [Nitakumbuka kwamba Bi. Mayala anadaiwa kunibusu. Subiri.]

Subiri? Angojee nini?

Alissa aliinamisha kichwa, akakunja uso na kuwaza. Anapaswa kwenda kwenye kantini ya kampuni sasa.

Aliweka kalamu yake chini, akainuka na kwenda kwenye mgahawa.

Wakati anaandaa chakula chake, alimuona Emmy akimpungia mkono.
Alissa kisha akaenda kwake.

Emmy ndiye mfanyakazi mwenzake pekee ambaye alikuwa na shauku zaidi kwake katika kampuni na alimsaidia kila wakati.

Mathew pia alimsaidia. Lakini hata hivyo alikuwa bosi wake. Sasa Alissa alikuwa ameolewa. Kwa hivyo, wanapaswa kuepuka kukutana mara kwa mara kuibua tuhuma.

"Hii nyama ni kwa ajili yako." Emmy alichukua nyama kutoka kwenye sahani yake na kumpa Alissa.

“Kisha nitashiriki nawe baadhi ya vipande hivi vitamu vya nyama choma?” Alissa alisema.

"Hapana. Kulikuwa na vipande viwili tu vilivyobaki. Nikifikiria kwamba unapenda nyama choma pia, hivyo nilichukua moja kwa ajili yako.”

Emmy alipenda nyama choma zaidi. “Tulia. tunapaswa kusaidiana kama wafanyakazi wa kampuni moja.”

Alissa alihisi kwamba Emmy alikuwa mwenye usawaziko na alikumbuka fadhili zake kwa siri.
“Hebu tufurahie.”

Walipoanza kula tu, mwanamume mmoja aliyevalia nguo za sare za Mgahawa wa City Star Restaurant alikuja na kontena maalum la chakula kutoka kwenye mgahawa huo.

Mkahawa wa City Star ulikuwa msururu wa kitaifa wa migahawa maarufu ya hali ya juu. Watu waliotaka kula chakula hapo lazima wawe wanachama wao. Wanachama walihitaji kulipa ada ya kila mwaka. Wapishi wao walikuwa mahiri katika vyakula vinane. Chakula walichopika kilikuwa kizuri sana.

Kontena lilifunguliwa. Kila mtu alikaza macho yake kwenye chombo kizuri cha chakula cha na hakuweza kujizuia kumeza mate ya uchu.

Mhudumu huyo alisimama mbele ya meza ya Alissa na kumchunguza. Alipoona kitambulisho chake cha kazi shingoni, alisema, “Je, wewe ni Bibi Alissa?”

“Ndiyo.” Alissa akaweka chini uma uliokuwa mkononi mwake.

"Tafadhali saini hapa." Mhudumu alimkabidhi barua ya kupokelea mzigo.

Alissa alisaini na kumrudishia mhudumu yule. Mwanamume huyo akaiweka, akafungua chombo cha chakula, akatoa sahani kadhaa, ikiwa ni pamoja na samaki watamu sato, wakukaanga katika mchuzi wa moto na nyama ya kukaanga na pilipili, Chipsi moto, kuku wa kuoka, na madikodiko mengine kibao.

Vyakula hivi vilikuwa sawa kabisa na vile kwenye picha aliyomtumia Kendrick.

Kwa hivyo, hivi ndivyo Kendrick alimaanisha kwa kungoja. Alimuagizia chakula sawa. Alissa aliguswa na wema wake.

Alikuwa ameushika moyo wake na kumuacha apendezwe naye kwa namna ambayo hakuitarajia.

Baada ya mhudumu yule kuondoka, Emmy alitazama sahani tajiri kwenye meza. Ilikuwa na harufu nzuri ambayo ilimfanya apate njaa sasa.

Watu wengine pia walikitazama chakula kilichokuwa mezani, wakasikia harufu yake na kukionea wivu.

Lily tu na rafiki yake wa karibu walikuwa na wivu sana.

"Alissa, mumeo alikutumia haya yote?" Emmy angeweza kufikiria tu jambo hili.

"Nadhani." Alissa alitabasamu tu.

"Alissa, mume wako anakupenda sana." Emmy alionekana mwenye wivu, “Sijawahi kula chakula katika Mkahawa wa City Star. Nilisikia kwamba ni ghali sana. Bei ya baadhi ya sahani ni sawa na mshahara wangu wa kila mwezi.”

Alissa alichukua samaki mtamu na kumweka kwa Emmy, "Basi jaribu leo."

"Alissa, wewe ni mkarimu sana." Emmy aliguswa, “Lakini hii ni sawa? Hii ni zawadi kutoka kwa mumeo.”

"Mambo mazuri yanapaswa kushirikiwa na marafiki. Jisaidie tu.” Alissa alidhani Emmy alikuwa mzuri sana.

“Sawa, asante.”

Lily kwenye meza iliyofuata alitazama hili na alikuwa na hasira sana kwamba hakuwa na hamu ya kula kabisa.

"Lily, Alissa hawezi kupata chakula kutoka kwa Mgahawa wa City Star hata kama ana pesa. Mume wake ana nguvu sana?” Rafiki wa Lily aliuliza kwa kuchanganyikiwa.

"Hivi kweli ana mume anaposema ana mume?" Lily alionekana kukasirika na kusema kwa jeuri, "Labda yeye ni hawara tu wa mtu."

“Ndiyo. Anaonekana kukata tamaa. Hawara anayeharibu familia za watu hatafikia mwisho mwema.”

Sura ya 153

Emmy alikasirika sana kusikia Lily na marafiki zake wakimtukana Alissa. Alimwambia Lily, “Lily, huo ni wivu tu. Unafikiri wewe ni bora kuliko wengine?"

“Wivu? Ni utani ulioje.” Lily alikoroma kwa ubaridi, “Kama ana mume, kwa nini asimlete hapa tumuone? Anakataa kwa kila aina ya visingizio. Hata kama mumewe anamletea vyakula na maua, ili iweje? Je, anathubutu kumleta mume wake hapa? Ninaogopa mume wake ataaibika sana kutuona, sawa?”

“Ndiyo. Angalau, Lily na bwana mdogo wa Vortex Company wako juu na hawaogopi mtu yeyote anayewasema vibaya. Ni Neema, rafiki wa Lily, alimzungumza, “Mara ya mwisho, mpenzi wa Lily alitualika Villa Park Club. Huwezi kusahau jinsi alivyokuwa mkarimu kwa Lily, sivyo?

“Emmy, unafikiri wewe ni mtu mzuri? Alissa anaendesha gari aina ya Range Rover na kukupa baadhi ya vyakula kutoka kwenye Mkahawa wa City Star. Basi, wewe ni kama mbwa anayejikombakomba kwa bwana wake. Natumaini kwamba yote hayatakuwa bure, au utakuwa na huzuni.”

Neema kweli alikuwa na ulimi wa fedha.

Emmy alikuwa na hasira na wasiwasi baada ya kuzomewa na Neema. Pia alihuzunika sana, "Nyinyi ... ninyi ndio mbwa wanaouma watu kila mahali."

"Wewe ni nzi anayefuata mzoga." Walijibu kwa karipio la kejeli, na kumfanya Emmy karibu kulia kwa hasira, “Nyinyi watu …
nitamwambia Bw. Matthew nyinyi watu mnaenda mbali sana.”

“Jipange. Sasa ni mapumziko ya chakula cha mchana. Bwana Mathew hatajali sana.” Jamila, rafiki mwingine wa Lily, alijibu.

Walionekana kuwa na kiburi na kufanya wapendavyo.

Alissa hakuwa na nia ya kujiletea matatizo. Lakini walichosema na kufanya kilikuwa kinaenda mbali sana.

Hawakumpenda na kumdhulumu. Lakini kwa sababu tu Emmy alikuwa karibu naye, walimdhalilisha Emmy hivi. Ilikuwa ni chukizo sana.

Ikiwa angevumilia kila wakati, angechukuliwa kama dhaifu.

"Mbona nyie watu ni wakali sana? Lily, unasahau kwamba umekatwa miezi sita ya bonasi na Bw. Matthew?” Alissa aliwakumbusha kwa mtazamo mzuri.

“Alissa, unathubutuje kutaja hili? Kama si wewe, ningekatwa miezi sita ya bonasi? Ninajua kwamba Bw.
Mathew alikuwa na upendeleo kwako. Siamini kwamba hakuna chochote kati yako na Bw. Mathew.” Akifikiria bonasi yake, Lily alihisi kufadhaika.

Alissa alikuwa karibu kusema kitu alipoona mtu anayemfahamu anakuja. Kumtazama mtu anayekuja, alishtuka na kisha kushangaa.

“Lily?” yule mtu mzuri alisimama mbele ya Lily na kutazama kadi yake ya kazi.

“Mimi…..” Lily alimtazama mwanamume mrembo mbele yake. Ingawa mwanamume huyo alionekana mpole na mtaratibu, Lily aliogopa kidogo na kuingiwa na hofu, “Wewe ni nani?”

“Mimi ndiye kiongozi wa ofisi kuu ya Universal Group. Tafadhali rudia ulichosema hivi punde.” Sauti ya mtu huyo ilikuwa baridi, “Kama ni kweli kama ulivyosema kuna uhusiano usiofaa kati ya wasaidizi na bosi, nitaomba makao makuu yamfukuze kazi.”

“Kweli?” Lily alishangaa.

"Lily." Hata hivyo, Neema alimvuta Lily na kumwambia atulie. “Tunawezaje kuamini kwamba wewe ndiye bosi mkuu kutoka makao makuu? Wewe ni nani?"

Mtu huyo alitoa kadi yake ya kazi, ambayo ilisoma Nilesh Kumar kutoka makao makuu ya Universal Group, na nafasi yake ilikuwa Mkurugenzi wa Miradi.

Lily, Neema na Jamila, na wengine katika mgahawa wote walishangaa.

Mtu huyo alikuwa mkurugenzi wa miradi wa wa kampuni! Alionekana mzuri na mpole. Sauti yake ilikuwa ya kupendeza na laini. Pia alikuwa kipaji bora ambaye alihitimu kutoka taasisi bora ya biashara na kurudi kutoka nje ya nchi. Alimshangaza kila mtu hapa.

Nilesh kila mara aliweka hadhi ya chini maishani na kazini. Ingawa alikuwa amechukua miradi mingi mikubwa na kuishughulikia kikamilifu, hakuwahi kufanya mahojiano na hakujali kamwe ofisi ya tawi. Kwa hiyo, watu wachache walikuwa wamemwona kuwa mtu halisi.

Sasa alifika kwenye ofisi ya tawi ya Mwanza, ambayo ilikuwa fursa adimu kwa Lily.

"Bwana Nilesh?” Lily alitabasamu kwa kutaniana.

"Unaweza kuzungumza nami chochote unachotaka kusema." Nilesh alitabasamu kwa upole.

"Mimi ..." Lily alikuwa karibu kusema kitu. Lakini alisimama na kumtazama Alissa, “Mr. Nilesh na Alissa wanajuana, sawa?”

Alissa alikuwa akifanya kazi katika idara ya Nilesh huko makao makuu, Dar. Kwa kawaida alikuwa amefanya kazi na Nilesh, mkurugenzi wa miradi.

“Tulikuwa tukifanya kazi pamoja katika makao makuu. Kwa hiyo, bila shaka tunafahamiana.” Nilesh alikuwa na busara na hekima wakati akitaja uhusiano wao.

"Bwana Nikesh, huu ni mkutano wangu wa kwanza na wewe. Je, utaamini nilichosema?” Lily hakuwa mjinga kiasi hicho.

"Ninaamini tu katika ushahidi." Nilesh alikuwa mwenye usawaziko, “Nipe ushahidi nami nitashughulika naye kulingana na ushahidi.”

“Tumeona kwa macho yetu kwamba wakati Alissa anahamia hapa, amechukuliwa gari la Bw. Matthew mara chache kwenda na kushuka kazini. Hivi karibuni, aliendesha gariaina ya Range Rover. Hawezi kumudu kununua gari kama hilo lenye thamani ya mamilioni kwa kiwango chake cha mshahara. Ikiwa hakuwa na historia, angewezaje kupata nafasi ya meneja wa miradi baada ya kuja hapa?" Jamila alifurahi na kusema.

“Kila mtu anaweza kuzungumza. Ninachotaka ni ushahidi.” Nilesh aliwakumbusha tena.

“Sikuwaza sana wakati huo. Kwa hiyo, sikupiga picha.” Jamila sasa alijuta sana.

“Huna ushahidi. Ina maana unabahatisha na kumtilia shaka bosi wako!” Nilesh akawa baridi na hasira.

Jamila aliogopa. Aliinamisha kichwa chini na hakuthubutu kumwangalia, "Mimi ... sidhani hivyo."

“Si ulisema hivyo?” Macho ya Nilesh yalitiririka kutoka uso kwa uso, “Kila mtu anaweza kushuhudia kwamba sikukosea, sivyo?”

Jamila aliuma mdomo wake na kumtazama Lily kwa woga fulani, akimwomba Lily msaada.

"Lily anafikiria nini kifanyike kuhusu tabia ya aina hii?" Nilesh, hata hivyo, aliuliza kabla Lily hajazungumza chochote.

Lily alikuwa katika hali ngumu, akifikiri kwamba Jamila ni mjinga kweli.

"Bwana Nilesh, yeye ni mnyoofu kidogo na hana ubaya wowote. Kwa nini tusisahau tu?” Lily alimtetea Jamila kwa sababu Jamila alikuwa amemsaidia sana.

"Tusahau? Halafu sheria na kanuni za kampuni ni za kuonyesha tu!” Nilesh alikoroma kwa upole, “Anaweza kumshuku Alissa na Bw.
Matthew wana uhusiano wa kimapenzi leo. Halafu atashuku kuwa nina uhusiano wa kimapenzi na Alissa kesho, sawa?"

“Hapana, hapana. Bwana Nilesh, sithubutu.” Jamila akatikisa kichwa.

Sura ya 154

"Hujathubutu?” Nilesh alicheka na uso wake mzuri ulikuwa baridi, “Ulichosema bado kinasikika masikioni mwangu! Siwezi kustahimili watu kama wewe wanaochochea uadui kati ya bosi na wafanyakazi.”

"Kwa hivyo, haupaswi kukatwa tu bonasi ya nusu mwaka kwa kumsingizia bosi wako. Unastahili kufukuzwa kazi.”

Jamila aliposikia kwamba atafukuzwa kazi, alipigwa na butwaa. Alikuwa ametoka tu kuwa mgeni na kuwa mfanyakazi mkongwe na alifurahia matibabu mazuri katika kampuni hiyo kuliko makampuni mengine aliyofanya kazi. Hakutaka kuachishwa kazi.

Mara tu atakapofukuzwa kazi, hataweza kusimama katika jiji hili. Hakuwa mrembo kama Lily kupata mchumba tajiri. Hakuwa na asili dhabiti ya familia na alikuwa mtu wa kawaida kutoka familia ya kawaida. Hakutaka kurudi huko.

"Bwana Nilesh, hii si adhabu kali sana?” Lily bado alitaka kumtetea Jamila. Baada ya yote, Jamila alikuwa msaidizi wake mwenye uwezo na hangeweza kumpoteza.

“Sifikirii hivyo. Adhabu hii ni ya haki sana.” Emmy alijitokeza kwa wakati ufaao, “Hatupaswi kutoa matamshi ya kutowajibika.
Kashfa kama hii pia inaweza kusababisha mashambulizi ya kibinafsi."

“Na si mara ya kwanza nyie kuongea hivi. Bado nakumbuka kwamba kuna msichana mgeni aliacha kazi yake akilia kwa sababu ya mashambulizi yenu ya maneno na udhalilishaji. ”

“Nyie mmefanya mambo mengi mabaya. Je, hampaswi kuadhibiwa?”

"Acha kuongea ujinga." Uso wa Lily ulikuwa wa rangi.

Neema hakuthubutu kuongea na Jamila alionekana kuwa na wasiwasi.

“Ninasema ukweli. Ikiwa kuna uwongo, nitapigwa na radi na kugawanyika sehemu mbili." Emmy alikuwa imara na akaapa.

Wakati huu, umati wa watu ulianza kunong'ona. Kwa kuwa Lily alikuwa na tajiriba na alikuwa na mpenzi tajiri kama msaidizi wake, watu wachache katika kampuni hiyo walithubutu kumkasirisha.

Sasa kwa kuwa mtu fulani angemwadhibu, wote walikuwa wachangamfu.

“Emmy yuko sahihi. Sisi pia tunajua mambo haya.” Kuna mtu alimuunga mkono Emmy.

"Mradi tu mtu hamtii Lily katika kampuni, watamkemea na kumdhulumu. Ni kweli haiwezi kuvumilika.”

"Bwana Nilesh, tafadhali washughulikie.”

Nilesh alitikisa kichwa huku akisikiliza umati, "Kwa hivyo, Jamila lazima aache kazi sasa hivi."

“Hapana, Bw. Nilesh. Tafadhali usinifukuze kazi.” Jamila alisonga mbele na kusihi, "Nahitaji kazi hii."

"Inaonekana hauthamini kazi hii hata kidogo." Nilesh hakuonyesha huruma yoyote, "Baada ya chakula cha mchana, nenda kwa ofisi ya fedha ili ulipwe mshahara wa mwezi huu na mshahara wa miezi mitatu kama fidia."

Wakati huu, Mathew pia alikuja. Alisikia kutoka kwa msaidizi kwamba kuna kitu kilitokea kwenye mgahawa wa kampuni na kukimbilia hapa.

"Bwana Nilesh.” Mathew angeenda kwenye makao makuu kwa mkutano kila robo mwaka. Kwa hivyo, kwa kawaida alimjua Nilesh.

Nilesh alitikisa kichwa, “Nadhani unajua kilichotokea. Unafikiri ninaishughulikia ipasavyo?”

Jamila aliweka matumaini yake kwa Mathew na kusihi, “Bw. Mathew, wewe ndiye unayesimamia tawi hili. Uamuzi wa Bw. Nilesh hauwezi kuwa sawa na wako. Maadamu haukubali kunifuta kazi, bwana Nilesh hawezi kufanya lolote kuhusu hilo. Bw. Matthew, kwa ajili ya miaka yangu katika kampuni, tafadhali nipe nafasi.”

“Nafasi imehifadhiwa kwa wale wanaoithamini. Ni dhahiri kwamba wewe si mtu wa namna hiyo. Nadhani uamuzi wa Bw. Nilesh unafaa. Hata asipofanya, nitafanya hivyo. Kutekeleza moja kama onyo kwa mia moja ndiyo njia bora ya kuwajulisha watu zaidi sheria ni nini! Mathew alikuwa akikazia na kumuunga mkono Nilesh.

Kuona kwamba Mathew alisema hivi, Jamila hakuwa na matumaini hata kidogo.

Mwili wake ukaishiwa nguvu na akaanguka chini.

Kuona hivyo, Lily alijaribu kumsaidia. Kwani, Jamila alikuwa amemsaidia sana na alijua jambo fulani kumhusu.

Lakini Jamila alimvuta kwa nguvu na kukataa kuachia mkono wake, “Lily, nisaidie. Tafadhali nizungumzie jambo mbele ya Bw.
Matthew na Bw. Nilesh…”

“Jamila, hizi ni sheria za kampuni na uamuzi wa Bw. Matthew na Bw. Nilesh. Samahani. Siwezi kufanya lolote kuhusu hilo.” Lily alimtazama Alissa, akimaanisha kuwa Alissa ndiye angeweza kumsaidia Jamila.

Jamila alijua kwamba jambo hili lilitokea kwa sababu ya Alissa. Kwa hiyo, angeweza tu kumwomba Alissa msaada wake.
Lakini kumwomba Alissa msaada ilimaanisha kwamba alipaswa kukiri kwamba alikosea.

Isitoshe, kwa kawaida Alissa hangeweza kumsaidia. Aliogopa kuwa Alissa atamcheka tu. Hata angefedheheshwa na Alissa, alishindwa kuendelea na kazi hiyo na angewachekesha watu wengi zaidi.

“Lilly, inabidi unisaidie. Nilifanya yote kwa ajili yako. Nimesema maneno hayo kwa niaba yako.” Mtu pekee ambaye Jamila angeweza kuomba msaada alikuwa Lily.

Lily alikasirika, “Sikukuuliza useme hivyo. Kwa nini unanipanga?”

“Mimi … hufikiri hivyo? Ulisema Alissa alikuwa mpenzi wa Bwana Mathew…”

“Unaongea ujinga gani? Sikusema lolote!” Lily aliona kwamba Jamila alianza kuongea bila maneno ya uangalifu na aliogopa kwamba Jamila angesema zaidi dhidi yake, “Upuuzi wako una faida gani kwako? Ukipoteza kazi hii, unaweza kupata nyingine. Kwa nini unafuata kisasi dhidi yangu?”

“Ndiyo, Jamila.” Neema alisogea mbele ili kumsaidia Jamila na kuchukua nafasi hiyo kupunguza sauti yake, “Haitakufaa kusema zaidi. Acha kusema nitamwomba Lily amshawishi Bwana Ernest akutafutie kazi. Acha ujinga sasa."

Jamila hakuwa na budi ila kufanya hivyo. Vinginevyo, ikiwa kweli angemchukiza Lily, hangeweza kuwa na kazi nzuri.

Hivyo, Lily, Neema na Jamila waliondoka kwanza, na watu katika mgahawa pia waliondoka mmoja baada ya mwingine.

Nilesh na Alissa pekee ndio walikuwa wamebaki kwenye mgahawa huo.

"Alissa, sikukuona kwa muda mrefu." Sauti ya kupendeza ya Nilesh ilisikika katika mkahawa huo tulivu, na kuwafanya watu wajisikie vizuri.

"Ndio, hatujaonana kwa muda mrefu." Alissa alipumua muda huo akaruka.

Alissa alimtazama Nilesh ambaye alikuwa hajamuona kwa muda mrefu. Ilikuwa kana kwamba alikuwa amerudi nyuma katika miaka ambayo walikuwa wakifanya kazi pamoja.

Nilesh alikuwa amerimbikiza kazi fulani kutokana na kulazwa hospitalini. Ilibidi atumie wakati mwingi kuzishughulikia. Kwa hivyo, alipata tu wakati wa kuja kumuona Alissa katika Jiji la Mwanza baada ya siku hizi.

"Ulisisitiza kuhamia Mwanza. Je, haya ndiyo uliyoyataka?" Nilesh alipofika tu, aliona watu walivyokuwa wanamnyanyasa, wakimpa hasira na kufadhaika.

"Bwana Nilesh, unatawala sana wakati huu." Alissa alionyesha kumshukuru. Hajawahi kumuona Nilesh asiye na huruma kama huyo, "Karibu nilifikiri wewe sio Nilesh niliyemjua."

"Kuna ubaya gani kuwa mtu mbaya kwa ajili yako?" Nilesh hakujali watu walimfikiria nini. Alitaka tu kumlinda mpenzi wake.

Alissa alikutana na macho ya joto ya Nilesh. Lakini hakustahili utunzaji aliompa. Kwa sababu hakuweza kujibu upendo wake. Hilo lilikuwa jambo baya zaidi kwake.

"Sistahili." Alissa akamkumbusha kwa mara nyingine.

“Nilisema ni kazi yangu iwe unastahili au hustahili. Huhitaji kuhisi kulemewa.” Nilesh alitaka tu kuwa mzuri kwake.

"Nilesh, lazima nikuambie kitu."

Sura ya 155

Alissa alimtazama Nilesh kwa umakini huku akiwa na mwanga machoni mwake. Alionekana mgumu na thabiti.

"Nisikilize kabla ya kusema, sawa?" Nilesh alisema kwa upole.

“Sawa. Wewe sema kwanza." Alissa akaminya midomo yake, akimpa nafasi na kuonyesha heshima.

Nilesh alikaa mkabala na Alissa. Nje ya dirisha, miale michache ya mwanga wa jua ilimwangukia uso wake mzuri, na kumfanya aonekane mpole na mrembo kiasi kwamba watu hawakuthubutu kumkufuru.

"Kwanini usiniulize sababu iliyonifanya nije Mwanza?" Nilesh aliuliza kwa kejeli.

"Safari ya kibiashara? Ili kuhudhuria mkutano? Au kuniona?” Alissa alikisia.

“Jambo la kwanza ni kukuona. Pia ni safari ya biashara. Isitoshe, niko hapa kuhudhuria karamu.” Nilesh alibadilisha mpangilio wa mambo aliyosema.

“Basi utakuwa hapa kwa siku chache. Je, kuna mahali popote unapotaka kwenda? Naweza kuwa kiongozi wako.” Alissa alitaka kutekeleza majukumu ya mwenyeji. Hii pia ilikuwa malipo madogo kwa utunzaji wa Nilesh kwa miaka mingi.

“Nilikuwa nakuja Mwanza. Lakini kila mara nilikuja na kuondoka kwa haraka. Wakati huu, nataka kutazama vizuri na kuona jiji hili ambalo ulikulia." Nilesh alitaka kujua zaidi kuhusu maisha yake ya zamani na hata alitaka kuhudhuria maisha yake ya baadaye, “Bila shaka unapaswa kunitunza. Hili ni eneo lako.”

"Hakuna shida." Alissa alisema.

“Alissa, nitakaa Mwanza kwa wiki moja. Mwezi mmoja baadaye, nitakuwa mwenzako tena.” Hoja ya Nilesh ilikuwa hii.

Alissa alichanganyikiwa kidogo, “Sisi si wenza sasa pia. Hatuko mahali pamoja.”

“Hicho sicho ninachomaanisha. Nimewasilisha ombi la uhamisho. Ninataka kuja Mwanza niwe upande wako." Nilesh alitabasamu, “Alissa, tafadhali nipe ushauri wako wakati huo.”

“Nilesh, usifanye hivyo. Familia yako, marafiki na watu unaowasiliana nao wote wako Dar. Utapata maisha bora ukiwa Dar. Usimwachie mwanamke kila kitu ulicho nacho. Ni kweli si thamani yake. Sitajisikia furaha kwa wakati utafanya hivyo, lakini huzuni, unajua?"

Alissa alijua vyema kwamba Nilesh angeshushwa cheo tu ikiwa angeondoka makao makuu ya Universal Group na kuja Mwanza. Kwani, Matthew alikuwa meneja mkuu katika tawi la Mwanza. Ikiwa Nilesh alngehamishwa, hangeweza kumshusha Matthew, vinginevyo labda Matthew angehamishwa. Hata kama bado angekuwa meneja wa tawi hilo baada ya kuhamishwa, bado haikuwa nzuri kama nafasi ya mkurugenzi wa miradi aliyokuwa nayo katika makao makuu.

“Alissa, sikuweza kukushikilia ulipoamua kuondoka hapo awali. sasa, nitakuja kuambatana nawe. Hii ni dhamira yangu.
Sikufurahi hata kidogo baada ya wewe kuondoka. Kuangalia mtu mwingine ameketi kwenye kiti chako cha zamani, nilifikiri nifanye jambo fulani. Hivyo ndivyo mwanaume anapaswa kufanya.” Nilesh alikuwa ameamua.

"Alissa, hata nikiangalia sura yako na tabasamu lako kila siku, najisikia mchangamfu. Unaelewa?"

“Nilesh, ninaelewa. Lakini tafadhali acha kuwa mzuri kwangu. Usiwe mjinga sana kuacha kila kitu ulicho nacho kwa ajili yangu… samahani. Ninakuchukulia kama rafiki tu." Alissa akashusha pumzi ndefu na kudhibiti sauti na hisia zake.

Hakutaka kumuumiza Nilesh. Lakini ilimbidi aseme maneno haya na hakuweza kuepuka kumuumiza. Hata ikiwa ilikuwa ngumu kusema, ilibidi aseme. La sivyo, ingelemea dhamiri yake na ingemwangamiza pia Nilesh.

Hata kama angemchukia, alikuwa mwadilifu.

"Alissa, naweza kukusubiri." Wakati wake ulikuwa kwake tu, “Nimengoja kwa miaka minne na sijali kuhusu miaka minne ijayo…”

“Huwezi.” Macho ya Alissa yalikuwa mekundu, “Mimi … nimeolewa.”

Sauti yake ilikuwa nyororo sana, ambayo ilikuwa kama kipepeo anayeruka. Lakini ilifika masikioni mwa Nilesh na kumshtua.

Alikaa tu. Kulikuwa na jua. Lakini hakuweza kuhisi hata chembe ya joto.

Ni wazi ilikuwa siku ya jua. Lakini alihuzunika sana hivi kwamba ilikuwa kana kwamba mvua ingenyesha sekunde inayofuata.

Alissa naye hakusogea. Wawili hao walikuwa kama jozi ya sanamu. Muda ulikuwa umeganda na alionekana kuwa ameanguka katika ulimwengu wa barafu na theluji. Nilesh alitetemeka kwa baridi.

Baada ya kungoja kwa muda mrefu, Alissa alishindwa kustahimili mazingira yaliyowazunguka na akasema kidogo, "Nilesh, uko sawa?"

"Alissa, unanidanganya, sivyo?" Nilesh alilazimisha tabasamu kwa kutoamini, “Hutaki nicheleweshe kazi yangu na kuwaacha wazazi na marafiki zangu. Kwa hiyo, unasema mambo kama hayo ili kunidanganya, sivyo?

“Niambie unasema uongo na hujaolewa. Hutaki nikusumbue hivi, sivyo?”

"Hapana." Alissa alikuwa na hisia tofauti, “Nimeolewa kweli. Sikudanganyi, na sitaki kukudanganya.

“Usiseme hivyo kukuhusu pia. Hukunisumbua. Ni kwamba sistahili upendo na utunzaji wako. Nilesh, katika maisha haya, wewe ni rafiki yangu na mshauri wangu. Lakini yeye ndiye ninayetaka kutumia maisha yangu na ninampenda."

Nilesh akanyamaza tena. Macho yake yakawa yamefifia kabisa. Alionekana mwenye uchungu sana hivi kwamba alikuwa tofauti kabisa na hapo awali.

"Nilesh, samahani."

Hata milioni moja ya msamaha isingeweza kuponya majeraha yake.

Nilesh akatulia taratibu na kutabasamu kidogo. Alionekana baridi na mwenye huzuni, “Hakuna haja ya kusema samahani. Labda hii ndiyo hatima." Ni Mungu ambaye hakutaka wawe pamoja. Aliweza tu kujisikia vizuri kwa kufikiria hivyo.

"Ni kosa langu kukufanya ubebe shinikizo hili." Alissa hakujua la kusema. Nilesh alikuwa hivyo kila wakati. Hata alipoumizwa, hakutaka ajilaumu kwa hilo.

“Hakuna shinikizo. Ni heshima.” Ilikuwa heshima kwamba mtu bora kama huyo alimpenda.

“Yeye ni nani?” Nilesh alikunja ngumi, akijizuia.

"Ni mtu unayemfahamu." Alissa alisema, "Kendrick."

“Kendrick?” Nilesh alishtuka, kisha akatoa tabasamu la utulivu, “Ni jambo lisilotarajiwa na la busara. Mimi sikutegemea kabisa.”

Alikaa na Alissa kwa miaka minne na Alissa alimchukulia kama rafiki tu. Alissa na Kendrick walikuwa wamefahamiana kwa muda usiozidi miezi mitatu tu, lakini wangeweza kuoana na kutumia maisha yao pamoja.

Je, asingewezaje kuwa na wivu na huzuni?

"Kwa kweli, tumefahamiana kwa muda mrefu." Alissa alijua kile Nilesh alikuwa akifikiria na polepole alizungumza juu ya siku za nyuma, "Miaka mitatu iliyopita ... Kwa hivyo, tumeanzisha uhusiano hivi majuzi. Nilesh, najua nilipaswa kukuambia kuhusu uhusiano wangu naye. Lakini sikuweza kwa sababu ya vikwazo vya mkataba. Sikutarajia kwamba mambo yangetokea hivi … nilimpenda, na pia alikuwa na hisia kwangu.”

"Haya ndiyo matokeo bora zaidi. La sivyo, ningempiku.” Nilesh alihisi kitulizo baada ya kusikiliza alichosema, “Ninaweza kuja lini kwenye harusi yako?”

“Bado hatujaamua. Lakini urasmi haujalishi. Kilicho muhimu ni dhamira ya kuwa pamoja.”

"Uko sahihi. Lakini akikutendea vibaya, nitakuondoa na sitampa nafasi tena.”

Sura ya 156

Alissa alijisikia raha baada ya kumwambia Nilesh kila kitu. Walifaa zaidi kuwa marafiki kuliko wapenzi.

“Sijamwona Doris kwa muda mrefu. Vipi nimchukue na wewe kutoka shuleni baada ya kazi na kwenda kula chakula cha jioni?" Nilesh alipendekeza.

Alikuwa akimpenda sana Doris zaidi ya Kendrick. Lakini Kendrick alikuwa baba yake Doris. Hapa ndipo mahali ambapo Kendrick alikuwa na faida zaidi ya Nilesh. Kwa hivyo, Doris alihisi Kendrick alikuwa mkarimu mara ya kwanza walipokutana.

"Sawa." Alissa alikubali.

Nilesh, ambaye alikuja tu Mwanza, alikuwa mgeni, na Alissa alikuwa mwenyeji. Kwa hivyo, kwa kawaida angepaswa kutekeleza majukumu ya mwenyeji.

Mbali na hilo, Nilesh hakuwa bosi wake tu, bali pia rafiki yake. Alikuwa amemtunza kwa miaka mingi na alikuwa na deni kubwa kwake. Alipaswa kumlipa. Chakula kinaweza kuonyesha fadhili zake.

Kwa njia hiyo, Alissa na Nilesh walifanya mipango. Nilesh aliondoka na kwenda kwa Mathew kuzungumza juu ya mambo kadhaa.

Baada ya kumaliza kuongea, Nilesh hakutoka akakaa kwenye sofa ofisini kwa Mathew akinywa chai.
"Bwana Nilesh na Alissa wanafahamiana sana.” Mathew alichukua birika na kumimina chai kwenye kikombe chake.

“Ndiyo.” Nilesh hakuwa na haya, "Nilifikiri alikuwa wa pekee sana tangu alipojiunga na kampuni. Ana mawazo maalum na talanta katika kazi. Kwa kuthamini talanta yake, nilimpa nafasi na aliitumia vizuri sana.

"Kwa kweli Alissa ni mchanga na ana talanta." Mathew naye alifikiri hivyo.

"Sikutarajia angerudi Mwanza. Kwa hivyo, tafadhali umtunze katika siku zijazo, Bw. Matthew." Nilesh alifikiri kwamba angeweza kumhifadhi Alissa kwa maisha yake yote. Hakutarajia kumwacha.

” Usiseme hivyo, bwana Nilesh. Alissa ni mzuri sana na ana uwezo. Hahitaji matunzo ya wengine hata kidogo.” Matthew alikuwa akisema ukweli, “Bila shaka, nitamtendea kwa fadhili talanta kama yeye.”

Kama msimamizi, bila shaka alitaka kuweka wafanyikazi wake bora. Wakati kama mfanyakazi mwenza, kwa kawaida alipaswa kujiweka mbali na Alissa.

Baada ya yote, Kendrick na Alissa walikuwa na utata kwa kiasi fulani. Hakutaka kuwa mwiba kwa Kendrick.

“Samahani kumsumbua Bwana Matthew kuanzia sasa.” Nilesh akanyanyua chai yake kama zawadi.

Mathew naye aliinua chai yake kwa malipo. Baada ya kunywa chai hiyo tamu, aliinuka, “Jisikie nyumani bwana Nilesh. Naenda kazini sasa hivi.”

"Sawa." Nilesh aliitikia kwa kichwa na kunywa chai yake, akisubiri hadi Alissa atakapotoka kazini.

Nilesh aliona kuwa muda ulikuwa umekaribia. Mathew naye alikuwa tayari anafungasha vitu vyake.

"Alissa anaenda kumchukua binti yake baada ya kazi. Bwana Nilesh itaambatana naye?” Mathew alichukua koti la suti nyuma ya kiti na kuivaa.

“Ndiyo. Sijamuona Doris kwa muda mrefu.” Nilesh alikuwa mpole zaidi huku akimtaja Doris.

Mathew alienda kwa Nilesh. Kwa kawaida alisafisha pingu za shati lake jeupe na sehemu ya ziada ya pingu za suti na kuonekana mpole.
“Mwanangu yuko darasa moja na binti wa Alissa. Kwa nini tusiende pamoja huko?” Mathew alisema.

“Twende zetu.” Nilesh alitoka na Mathew akafuata.

Walienda kumtafuta Alissa mara tu Alissa alipotoka. Matthew alitabasamu na kusema, “Tunaenda hukohuko. Kwa hiyo, twende tukawachukue watoto pamoja.”

Alissa akaitikia kwa kichwa. Wote watatu walichukua lifti hadi kwenye maegesho ya chini, ambapo Alissa aliiendea Range Rover yake nyekundu na kubonyeza ufunguo wa kufungua milango.

Nilesh kwa kawaida alivutiwa na gari lake la kupendeza la kisasa. Akausogelea na kuuvuta mlango na kukaa ndani yake.
“Jifunge mkanda wako wa kiti.” Alissa alimkumbusha.

Mathew aliendesha gari lake kwanza, na kisha Alissa akafuata.

"Inaonekana anakupenda na mkarimu sana." Nilesh alidhani gari hilo ni zawadi kutoka kwa Kendrick kwa Alissa.

Alissa alitunza pesa na hangepoteza pesa zake kwa usafiri wa gharama kubwa kama huo. Pili, mapato yake hayakumtosha kununua gari la gharama kubwa kama hilo. Kwa hivyo, hakuweza kufikiria sababu yoyote kwa nini angekuwa na gari la kifahari muda mfupi tu baada ya kurudi Mwanza na aliweza kumfikiria Kendrick tu.

Alissa alijivunia sana na hakuwahi kupokea zawadi kutoka kwa mtu yeyote bila sababu. Hakutaka kuwa na deni kwa mtu yeyote, ikiwa ni pamoja na yeye.
Ila alikubali gari la Kendrick kumaanisha alimkubali sana Kendrick na hakumchukulia Kendrick kama mtu wa nje.

Nilesh alihisi kuwa mgumu na mwenye uchungu. Alikuwa amechelewa sana baada ya yote.

"Hakuninunulia yeye." Alissa alijua angeelewa vibaya na akaeleza, “Nilifika nyumbani na kukuta dada yangu alikuwa na gari zuri sana. Kwa hiyo, nilimwomba baba yangu aninunulie pia. Hiyo ilikuwa haki.”

Nilesh alishtuka, hakutarajia baba yake Alissa angekuwa tajiri kiasi hicho, “Baba yako ni nani?”

“Haijalishi yeye ni nani hata kidogo. Kilicho muhimu ni kwamba anipe kile ninachostahili.” Alissa hakutaka kumtaja baba yake ni nani. Lakini, hakukuwa na uhusiano wa kifamilia kati yao. Ingefanya watu wacheke tu.

Nilesh hakuuliza maswali zaidi. Kwa kuwa hakutaka kusema hivyo, hakuuliza.

Alissa hakuendelea na mada. Muda si mrefu, walifika katika shule ya chekechea.

Gari lake lilikuwa limeegeshwa nyuma ya lile la Mathew. Walishuka kwenye gari na kuingia chekechea wakiwa na cheti. Kisha, wakaenda darasani na kuwachukua Doris na Walter na kuachana kwenye lango.

Walter alichukia kuachana na Doris. Alissa aliwaalika, “Mr. Mathew, kwa nini usiende kula chakula cha jioni pamoja nasi?”

“Sahau muda huu. Bw. Nilesh huja Mwanza mara chache. Ni lazima nyie muwe na mengi ya kusema, sitawasumbua. Kutakuwa na fursa kwangu kumualika Bw. Nilesh na wewe kwenye chakula cha jioni.” Mathew alikuwa na busara na hakutaka kujisumbua na kuharibu uhusiano kati yao.

"Walter, sema kwaheri." Mathew alimvuta mwanae.

Walter akamwambia Doris, "Kwaheri."

Pamoja na hayo, waliondoka. Alissa alimpeleka Doris kwenye gari.

"Unataka kula nini?" Alissa alimuuliza Nilesh.

"Mgeni anapaswa kuendana na urahisi wa mwenyeji. Chochote unachotaka, nitakula.” Nilesh hakuwa mchaguzi. Alitaka tu kutumia muda zaidi pamoja naye.

Alissa kisha akaendesha gari hadi kwenye mgahawa mzuri wenye mpangilio mpana na rahisi, ambao uliwafanya watu wajisikie vizuri.

Ghorofa ya kwanza ilikuwa ukumbi. Ghorofa ya pili, ya tatu na ya nne vilikuwa vyumba vya watu binafsi.

Waliketi sebuleni na walikuwa karibu na dirisha la ua wa ndani. Nje, kulikuwa na mianzi ya kijani na mtazamo hapa ulikuwa mzuri.

Alissa alimwomba Nilesh aagize, lakini alimruhusu afanye uamuzi.

Alissa kisha akaagiza sato watatu wakukaangwa na chips, ambayo iliwafaa.

Aliagiza vinywaji na kuzungumza na Nilesh huku akisubiri vyakula.

Hawakugundua kuwa kuna mtu alikuwa akiwatazama kwa muda kwenye ngazi na alikuwa ametoa simu yake ya mkononi kutafuta pembe za hila za kupiga picha.

Alissa na wale wengine wawili hawakuliona kabisa. Kisha, vyakula vilitolewa.

Sura ya 157

Doris, kula zaidi samaki, hawa samaki ndiyo unaowapenda zaidi." Alissa akampa Doris mnofu.

“Sawa.” Doris alikula kimya kimya.

Alissa alimkaribisha Nilesh, “Furahia. Huwezi kufika Mwanza na usile sato. Ikiwa huzipendi, agiza nyingine.”

"Zote zinaonekana vizuri sana." Nilesh alifikiri kwamba vyakula hivyo vilikuwa vya kupendeza na chakula kilikuwa kitamu, jambo ambalo liliamsha hamu yake ya kula.

Nilesh alikula samaki hiyo na akafikiri ilikuwa tamu.

Alissa alikuwa ametoka kula chakula mara ujumbe ukaingia kwenye simu yake kutoka kwa Kendrick.

Kendrick: [uko wapi?]

Alissa alikuwa na hofu kidogo. Lakini hakuthubutu kufikiria sana. Kwa hivyo, alijibu: [Natoka kazini. Wewe uko wapi?]

Kendrick akajibu haraka haraka: Niko kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza.

Mkono wa Alissa ulikuwa dhaifu na nusura adondoshe simu: [Unakuja Mwanza tena? Mbona hukuniambia mapema?]

Kendrick: [Nilitaka nikupe surprise tu.]

'Siyo mshangao, lakini mshtuko, sawa?' Alissa alijiwazia na kujaribu kutulia.

"Nini tatizo?" Nilesh alimuona Alissa akiitazama simu yake. Kitu kilionekana kuwa kibaya.

“Hakuna kitu.” Alissa alimtazama Nilesh na kuendelea kumjibu Kendrick: [Hakika ni mshangao.]

Kendrick alisema tena: Ndo nimeshuka tu na sikupanga gari kuja kunichukua. Njoo unichukue, sawa?

Angewezaje kuondoka sasa? Hangeweza kumwacha Nilesh tu na kwenda zake.
Vinginevyo, Nilesh angefikiria nini kuhusu hilo? Angekuwa mwanamke ambaye alipendezwa zaidi na mumewe kuliko marafiki.

Alissa alijibu huku akitegemea Kendrick asingesisitiza: [Siwezi kuondoka sasa hivi. Unaweza kuchukua teksi hadi hoteli. Nitakuja kwako baadaye.]

Kendrick "alihuzunishwa" sana kama alivyotarajia: [Ni nini muhimu zaidi kuliko mume wako? Bi. Mayala, unataka kukataa kutekekeza jukumu lako?]

Alissa akashusha pumzi kidogo, akimtazama Nilesh upande wake. Ilionekana kwamba angeweza tu kusema ukweli. Isitoshe, yeye na Nilesh walikuwa marafiki wasio na hatia. Ilikuwa kawaida kwa marafiki kula chakula cha jioni pamoja.

Alissa alipima maneno yake: ,[Nilesh amekuja hapa Mwanza kikazi. Ningependa kutekeleza majukumu ya mwenyeji na kumshukuru kwa kunitunza miaka hii yote.]

Sekunde kumi, nusu dakika, dakika…zilipita dakika mbili na Kendrick hakujibu.

Alissa alihisi kuwa muda wa kusubiri ulikuwa ukiongezeka na alikuwa na wasiwasi kidogo.

Alituma ujumbe: [Je! una hasira? Bw. Nilesh anakuja Mwanza kwa mara ya kwanza. Yeye ni rafiki yangu na bosi wa zamani. Ninapaswa kukutana naye na kumwalika kwenye chakula cha jioni. Hata hivyo, sikufanya chochote kibaya. Ikiwa una hasira, sina la kusema.]

Alissa hakukubali, lakini alizungumza mawazo yake vyema.

Kendrick bado hakujibu. Alissa hakumsubiri. Katika chakula cha jioni na marafiki, ilikuwa ni kukosa heshima kuendelea kuzungumza kwenye simu.

Nilesh pia aliweka uma chini na kumtazama Alissa ambaye alikuwa akitazama simu na hakula, "Alissa, ikiwa kuna chochote, sema tu."

Nilesh aliweza kusema kutoka kwa uso wake kwamba alikuwa na wasiwasi juu ya jambo fulani.

“Mimi…” Alissa alipokuwa karibu kuongea wakati ujumbe ukaingia kwenye simu yake, “Subiri kidogo.”

Akabonyeza ujumbe kutoka kwa Kendrick. Ilikuwa na picha chache zake na Nilesh katika mgahawa huu.

Pembe ya picha ilikuwa ngumu. Kwa hiyo, ilionekana kana kwamba walikuwa na utata kidogo.

Alissa alikunja uso. Ilionekana kuwa kuna watu ambao hawakumpenda katika mgahawa huu waliwaona, au mtu alikuwa akimfuatilia.
Ikiwa ilikuwa ya kwanza, basi mtu nyuma ya hii alikuwa anatisha sana. Mtu huyo lazima atake kumfanya Kendrick amuue.

Haishangazi Kendrick alituma ujumbe kama huo akiuliza yuko wapi wakati huu. Ilionekana kuwa alipokea picha hizo mapema.

Kendrick: [Nilifikiri hungeniambia kuwa Nilesh alikuwa na wewe. Lakini kwa vile uliniambia, sina hasira na wewe. Ana bahati sana kwamba Bi Mayala anaweza kula chakula cha jioni pamoja naye. Isitoshe, sikuja Mwanza, nilikuwa nakuzingua tu.

Kendrick alikuwa anamjaribu tu kama atasema ukweli.

Alissa akajibu: [lini umeanza tabia mbaya hivyo? Hata ulinidanganya hivi?]

Kendrick: [Unadhani sijui Nilesh anawaza nini? Je, ni lazima niwe mtu wa kutojali na mkarimu ninapomwona anamfukuzia mke wangu?]

Alissa aliweza kufikiria kuwa Kendrick alikuwa akiinua nyusi zake kwa dharau pale.

Alissa: [Ni chakula tu. Nina deni kubwa kwake na lazima nimrudishie fadhila. Mbali na hilo, Doris pia yuko pamoja nasi. Una wasiwasi gani? Bila Nilesh, hakungekuwa naye sasa.]

Kendrick akajibu: [Niko kwenye ulinzi dhidi yake, sio wewe. Nitamlipa kwa ajili yako kama mume wako. Unaruhusiwa kujitolea kufanya tena. Hata ikibidi ufanye, lazima niwepo pia.]

Alissa: [Nitaripoti kwako mapema, sawa? Lakini ulinidanganya. Unafikiri nifanye na wewe?]

Kendrick: [Nitaoga na nilale kitandani upendavyo.]

Alissa alikunja pua yake nzuri. Yeye hakujali, sawa?

Hatimaye Alissa akajibu: [Lazima nile vya kutosha ili nipate nguvu. Usisumbue chakula changu cha jioni. Wacha tuzungumze juu yake baada ya kurudi nyumbani. Kwaheri.]

Alissa kisha akaiweka simu yake pembeni na wala hakujishughulisha kusoma meseji zozote.

Nilesh bado alikuwa akisubiri majibu yake.

“Alijua uko Mwanza na tunakula chakula cha jioni pamoja. Kwa hiyo, aliniruhusu nikutendee mema.” Alissa alikuwa anasema uwongo tu.

Nilesh alitabasamu, "Ninaogopa hii sio kutoka kwa Bwana Kendrick, lakini kutoka kwako kwa ajili yake."

Alimfahamu vyema Kendrick. Kendrick hatawahi kusema maneno ya upole kama haya. Lilikuwa neno la fadhili kutoka kwa Alissa ambaye alitaka 'waelewane'.

Alissa aliendelea kutabasamu, “Alisema mengi. Lakini ndivyo alivyomaanisha kwa ufupi.”

“Alijua ninakula chakula cha jioni na wewe hapa. Hajakuaibisha?” Nilesh hakutaka kumsumbua, "Naweza kumuelewa."

"Hakuna haja. Nimeweka wazi, na hakuniaibisha.” Alissa hakutaka kusema kwa Kendrick nia ya wao kula chakula cha jioni pamoja.

"Alissa, ikiwa anakutendea vibaya, mimi ..."

Alissa akamkatisha, "Hebu tuharakishe na tule chakula chetu, au kitakuwa baridi na kuathiri ladha." Alibadilisha mada na kumpa Nilesh msisitizo wa kula.

Nilesh alisisitiza kumaliza maneno yake, “Alissa, nitafurahi ikiwa utaishi maisha ya furaha. Ikiwa sivyo, sitaki mtu yoyote akudhuru, hata kama mtu huyo ni Kendrick.”

“Sidhani kama mimi ndiye nitajiumiza. Nilesh, usijali. Najua ninachopaswa kufanya. Haijalishi nini kitatokea kwangu na Kendrick mwishowe, sitawahi kukudurika. Unaelewa?" Alissa aliogopa tu kwamba Nilesh angebaki hivi kila wakati. Ikiwa ndivyo, angehisi hatia.
“Hupaswi kuyatoa maisha yako kwa ajili yangu. Nilesh, tazama mbele. Furaha inakungoja sio mbali."

"Wacha tuwe marafiki maishani, sawa?"

Sura ya 158

Alissa alitoa maoni yake kwa dhati na kwa uthabiti. Alitaka tu Nilesh aache wazo la kumngoja milele.

Maisha yalikuwa mafupi kama miongo ya miaka. Aina hii ya dhabihu ilikuwa tu kupoteza muda na maisha, ambayo kwa kweli haikuwa ya haki kwake.

Mtu anapaswa kuishi maisha kwa busara zaidi. Kupenda kwa kila nyuzi ya nafsi yake wakati kuna mtu wa kupenda, na kujipenda mwenyewe wakati hakuna.

Nilesh alijua kwamba Alissa alikosa amani kwa sababu alitaja hilo tena, “Alissa, samahani. Nilisema hivyo kwa kukata tamaa kabisa. Ni sawa tuwe marafiki kwa maisha yote, lakini usitilie umuhimu zaidi kwa mpenzi wako kuliko rafiki."

"Bila shaka hapana." Alissa alitabasamu kwa utulivu, na aliamini Nilesh angetimiza ahadi yake.

"Vizuri." Nilesh akachukua glasi ya kinywaji kutoka mezani.

Alissa naye akachukua glasi na kugonganisha naye. Walisema kwa mtiririko huo.

"Uwe na furaha."

"Urafiki wetu na udumu milele."

Baada ya kuongea walikunywa na kula, wakitazamana huku wakitabasamu.

Baada ya chakula, Nilesh alikuwa karibu kulipa bili wakati Alissa alipomsimamisha, “Hii ni Mwanza, ninapoishi, na mimi ndiye mwenyeji. Ukilipa bili, nitakasirika na hatuwezi hata kuwa marafiki katika siku zijazo.”

Kwa hivyo, Nilesh alikubali. Alissa alilipa bili na kujisikia furaha sana, akihisi kwamba amepunguza mzigo wa fadhila ambazo Nilesh alimdai.

Alissa alimrudisha Nilesh kwenye Hoteli aliyofikia, na akaendesha gari kurejea nyumbani pamoja na Doris.

Alissa na Doris walisoma vitabu kwa muda. Kisha Alissa akamuogesha Doris, akambembeleza hadi akalala na kwenda kumuona bibi kama kawaida yake...

Ilikuwa karibu saa 10:00 usiku alipopanda ghorofani kwenda kulala. Kendrick akampigia simu.

“Mbona hujanijibu kwa muda mrefu hivyo?” Kendrick aliuliza.

“Unataka kuanzisha ugomvi?” Alissa alisimama kwenye kibaraza cha ghorofa ya pili.

Kendrick alipigwa na butwaa, na kuwaza kwa sekunde chache, “Unataka kufanya nini?”

“Mimi na yeye ni marafiki tu. Tumekula tu pamoja. Je, unanitilia shaka sasa? Nimeacha mambo mengi kwa ajili yako. Huniamini?” Alissa alihisi huzuni na hasira kidogo.

Ikiwa Kendrick bado hakujua ni nini kilikuwa kimetokea kusikia hivyo, basi alikuwa mjinga sana.

"Bi. Mayala alicheza mchezo mzuri sana." Kendrick alitabasamu kidogo, "Ninahitaji kujibu nini ili kukusaidia kucheza vizuri zaidi?"

"Unamaanisha nini?" Alissa aliuliza huku akishtuka sana, “Utanitelekeza? Kwa nini? Si ulisema ingawa huwezi kunitajia jina la mke wako, utanitendea mema kama mkeo na kamwe hutaniacha?”

"Hapana, tuachane." Kendrick alishirikiana naye, baada ya kuelewa kile Alissa alimaanisha.

“Sitaki kuachana, na sihitaji kujua jina la mkeo. Nataka tu kubaki na wewe.” Alissa alimsumbua, "Sitaogopa hata kama anajua."

"Nilichosema hakitabadilika kamwe, na hatuna uhusiano katika siku zijazo."

"Nini? Vipi kuhusu ujana wangu wa miaka mingi? Je, utarudi upande wake? Ungewezaje kunidanganya? Sitakubali kamwe…”

"Matokeo yake ni sawa ikiwa unakubali au la."

“Siwezi kukupoteza… Usikate simu… wewe…” Alissa alishusha earphone masikioni na kuitazama huku akisema kwa meno ya kusaga, “Mwanaharamu!”

Alissa alikasirika sana hadi akahisi kuishiwa nguvu, mikono ikiwa kwenye uzio, na macho yake yakawa mekundu.

Mtu mwembamba alitembea karibu polepole, hadi akasimama mbele ya Alissa.

“Alissa, uko sawa?” Melissa alikuwa na wasiwasi juu yake.

“Hakuna kitu.” Alissa alijizuia kutokwa na machozi, akarudi kwenye sura yake ya baridi.

“Nimesikia unaonekana umegombana na mtu. Lakini Alissa, usifikirie sana. Nilishuka tu kunywa maji nikasikia sauti yako kali, nikaja kutazama. sijaelewa chochote.” Melissa alijieleza.

"Ni wewe unayehangaika sana. Sasa nina furaha sana kila siku. Nitagombana na nani?" Alissa alihamisha nywele zake kutoka mbele hadi nyuma ya bega kwa umaridadi, akionyesha shingo yake nzuri na maridadi, "Umesikia vibaya."

“Labda nimesikia vibaya. Sisikii vizuri kwa sababu ya kuwa mjamzito. Alissa pia umezaa na Doris nadhani umenielewa, au sivyo? Utakuwa na hasira na mimi?" Melissa akampa glasi, "Unataka kunywa maji?"

“Melissa, huoni ni uchafu? Kwanini unafanya hivyo.” Alissa alitazama juu kwa kidevu kilichoinuliwa kidogo, “Nenda tu kulala mapema. Ikiwa mwanamke hatapata usingizi wa kutosha akiwa mjamzito, ni rahisi sana kupata mikunjo na kuonekana mzee.”

"Mbali na hilo, ni rahisi kupata siasma na kunenepa… Mwanamke atashushwa hadhi mara tu akiwa mjamzito, na atakuwa na ugonjwa wa siasma mbaya, na ngozi iliyolegea baada ya kuzaa… Inachukiza sana.”

"Ingawa wewe ni mrembo wa kuzaliwa, ninaogopa huwezi kukwepa sheria ya asili. Wanaume ni wanyama wenye hisia, na watatoa macho zaidi kwa wanawake wachanga na warembo wenye umbo la kuvutia la mwili. Afadhali uzingatie zaidi mumeo. Unakuwa mzito siku baada ya siku. Katika siku za upweke… Mume wako angefanya nini? Unapaswa kuwa mwangalifu ili usimruhusu kutongoza mwanamke mwingine. Ikiwa ndivyo, juhudi zako zote zitabatilika.”

Alichokisema Alissa kiliufanya uso wa Melissa kubadilika rangi. Alissa alimkumbusha Melissa kwamba Melissa alimnyang'anya Seidrick, na ingetokea pia kwa Melissa.

“Alissa, una wasiwasi sana. Haitatokea kamwe.” Melissa alijiamini sana, lakini alisema kwa ngumi zilizofungwa kwa nguvu, "Ninataka kupendekeza uweke nafasi yako."

“Sina busara kama wewe. Nimechoka na ninaenda kulala.” Alissa aliondoka kwa hatua za kifahari na zisizo na wasiwasi. Umbo lake jembamba na refu lililopungua bado lilikuwa la kuvutia sana.
Lakini nini? Labda alikosana na Kendrick. Kumpoteza Kendrick kama mlinzi, angeridhika hadi lini?

Anachopaswa kufanya Melissa sasa ni kuweka kipaumbele zaidi kwa Seidrick. Hakuweza kumruhusu Alissa kumnyang'anya Seidrick kwa sababu alikuwa mjamzito.

Ilibidi atafute nafasi ya kumfanya Alissa awe na sifa mbaya kama miaka 5 iliyopita, na hivyo kumfanya Alissa asiinuke tena.

Alissa alipoingia tu chumbani, akampigia tena Kendrick, Kendrick akaitikia haraka.

"Melissa alikuwa karibu nami sasa hivi."

"Kwa hivyo uliigiza kuachwa na mimi ili kumchanganya?"

“Ndiyo. Ikiwa amefanya kitu kwenye zile picha, basi matokeo haya yatamfanya kupata kile anachotaka." Alissa aliketi kwenye kiti cha mkono, akisema kwa miguu iliyovuka, "Basi nitamsaidia."

"Niamini. Tutajua kama ni yeye au la hivi karibuni." Kendrick akasema, “Dada yako ana hila sana. Lazima kuwe na mtu anayemfundisha somo zuri."

"Unafikiria sawa na mimi." Alissa aliweka kidevu chake kidogo kwenye miguu yake, kwa macho ya baridi kidogo. Angemrudishia kile ambacho Melissa alikuwa anadaiwa kidogo kidogo.

"Melissa, ngoja tu uone." Ilikuwa kawaida kwamba mtu alipe deni lake. Alissa hangeweza kamwe kuwa laini na asiye na msimamo.

Sura ya 159

Wikendi hii, kungekuwa na karamu ya biashara katika Hoteli ya Kimataifa ya Garden, na watu wengi mashuhuri na wafanyabishara mashuhuri wangehudhuria, ambayo ilikuwa fursa adimu.

Nilesh na Matthew pia wangehudhuria karamu hiyo. Nilesh alikuwa tayari amemuomba Alissa ahudhurie pamoja naye. Baada ya yote, Nilesh alikuwa muungwana mseja, mchanga na mwenye kuahidi, hivyo alihitaji mwenzi wa kike.

Ikiwa Nilesh angewaomba wanawake wengine katika kampuni hiyo waandamane naye, bila shaka wangeanza kumsogelea, ambayo ingesababisha shida nyingi.

Lakini Alissa hakutaka. asingetaka hata kama angemtaka. Alikuwa mtu bora kuwakilisha kampuni.

Saa 7:00 jioni, taa zenye kung'aa katika hoteli hiyo zilikuwa nzuri sana. Wengi wa watu wa ndani walikusanyika hapa, wenye kelele sana.

Nilesh na Alissa waliingia katika jumba la karamu la hoteli hiyo. Baada ya kuingia ndani, walisababisha msukosuko na umakini.

Nilesh alivaa suti nyeupe, tai nyeusi, na uso mzuri, umbo refu na jembamba na tabia nyororo, kama Prince Charming.

Alissa alimshika mkono Nilesh. Macho yake mazuri yalikuwa yakiangaza chini ya taa, na midomo yake myekundu na nywele ndefu nyeusi zilivutia sana. Alivaa vazi refu la rangi ya champagne lililotengenezwa kwa chachi laini ya tabaka nyingi, mrembo sana kama mrembo aliyeanguka kutoka ulimwengu mwingine.

Mtu aliyemfahamu Nilesh akasogea mbele kuwasalimia, na Nilesh akajibu kwa upole. Alissa naye alitajwa katika mazungumzo yao.

"Mwanamke aliye karibu na Bw. Nilesh ni mrembo sana, na amemvutia kila mtu aliyepo."

“Asante.”

“Nashangaa ni lini ninaweza kuhudhuria harusi ya Bw. Nilesh?”

“Siku moja. Subiri."

Nilesh hakukataa wala kukiri, akajibu tu swali. Hakusema kuwa yeye na Alissa walikuwa marafiki na wafanyakazi wenza tu ili kumlinda Alissa asinyanyaswe na wengine.

Kwa kawaida Alissa alijua kwamba Nilesh alikuwa akimlinda kimakusudi. Hakupenda wengine wamuulize juu yake, na kwa njia hii angeweza kuepuka matatizo mengi.

Nilesh pia hakutaka Alissa aangaliwe juu chini na wale wanaume waliokuwa wakivutiwa na urembo wa Alissa, lakini alipata kisingizio cha kumuacha Alissa aondoke kwenye umati wa watu, na yeye angeshughulika na watu hawa peke yake.

Kulikuwa na kila aina ya vitafunwa na vinywaji, matunda na divai kwenye meza ya buffet ya ukumbi wa karamu.
Alissa alijificha hapa na kuchukua matunda ili ale.

Kwa wakati huu, mhudumu alienda mbele, akiwa na glasi ya divai kwenye trei juu ya mkono wake wa kulia, "Bi Alissa, Bwana Nilesh aliniomba nikupe."

"Vizuri. Asante.” Alissa aliichukua kwa tabasamu, akiishika kwa ncha za vidole vyake.

Alitazama chini na kutikisa. Divai ilionekana kwenye kioevu giza nyekundu, nzuri sana.
Yeye hakunywa, lakini akaiweka kwenye meza.

Katika miaka hii, Alissa alikuwa na uzoefu mwingi na kuona mengi sana. Hakuwa msichana asiye na hatia na rahisi tena, na alikuwa macho zaidi kuliko hapo awali.

Hakunywa vinywaji vya ajabu, ambayo ilikuwa msingi wa kujilinda.

Alichukua chupa ya maji safi kutoka kwenye meza, na mhudumu aliyekuja kuchukua divai akauliza, “Bi, unahitaji bilauri yoyote tupu?”

“Asante.” Kwa kweli haikuwa kifahari kwake kunywa maji na chupa katika hafla kama hiyo.

Baada ya kutuma divai, mhudumu alileta glasi tupu, "Haya, bibiye."

Alissa aliichukua ile glasi na kuiangalia. Hakuona ubaya wowote, akamimina maji kwenye glasi.

Kwa wakati huu, Nilesh alikuwa amemaliza salamu na toast, na akachukua champagne ya dhahabu nyepesi kutoka mezani, na kugundua kuwa Alissa alikuwa ameshika maji mkononi mwake.

"Je, nidhamu ya familia ni kali sana? Hakuna champagne?" Nilesh alisema kwa mzaha.

"Hapana, sitaki tu kunywa pombe." Alissa alichukua maji kwenye glasi, "Unajua kwamba sipendi tukio la aina hii, ambapo lazima nijifurahishe na wengine."

"Lakini lazima uwe na mazoea." Nilesh alichukua shampeni, "Umemchagua, na itabidi uhudhurie karamu nyingi. Huwezi kukataa zote. Lazima uhudhurie karamu muhimu zinazohitaji mahudhurio ya wanandoa."

"Sijafikiria sana." Alissa hakufikiria sana, “Wacha tuijadili baadaye.”

Hapo awali walifunga ndoa kwa siri, ambayo haikutangazwa kwa umma. Kendrick alikuwa bado hajaoa machoni pa umma, kwa hivyo hakuhitaji kuandamana naye.

Lakini, sasa ndoa yao ilitangazwa kwa umma. Kwa kweli kungekuwa na hafla muhimu ambazo zilihitaji kuonekana kwao wote wawili. Anapaswa kutoa ushirikiano kwa ajili yake.

Wakati Alissa na Nilesh walipokuwa wakizungumza, Mathew alienda, “Bw. Nilesh, kampuni yetu pia ni mmoja wa wazabuni wa mradi wa FarmCom unaoshirikiana na kampuni ya Kilimo Kwanza na Kilimo Hai. Twende tuzungumze nao.”

"Sawa." Nilesh alitikisa kichwa, na kumwambia Alissa, "Njoo pamoja nasi, kwa sababu wewe pia unashiriki katika mradi huu."

Mradi huu ulikuwa mojawapo ya miradi muhimu zaidi ya Universal Group katika nusu ya pili ya mwaka. Kama mkurugenzi wa miradi wa ofisi kuu, Nilesh alipaswa kuchukua jukumu hilo.

“Sawa.” Alissa alihisi ni biashara tu, na hakukataa.

Matthew aliwachukua Nilesh na Alissa kwa umati, na wakakutana na Alex, Merry, Sam na Maira, Seidrick na Melissa. Ambao nao walikuwa wamealikwa kupitia kampuni za familia zao.

Ingawa Sam na Maira walisikia kwamba Alissa alikuwa tayari amerudi kwa familia ya Maziku, ilikuwa mara ya kwanza kwao kukutana naye baada ya miaka 5.

Baada ya miaka 5, Alissa hakuwa na hatia na mchanga kama hapo awali. Wakati huo ulimpa ukomavu na haiba, na alikuwa akivutia sana sasa, ambayo ilikuwa wakati wa dhahabu kwa mwanamke.

Kumwona Alissa, Sam alionyesha uso wa baridi kidogo, lakini Maira alionyesha tabasamu hafifu, la neema.

Alissa aliwatambulisha wao kwa wao.

Nilesh aliwasalimia familia ya Maziku na familia ya Masolwa. Alex na Sam walimsifu kwa kuwa mchanga na mwenye kuahidi.

Kisha Alissa akasema, “Bw. Masolwa, Bibi Masolwa.”

Sam alimpuuza Alissa, na Maira pekee aliitikia kwa kichwa.

Sam aliweka uso ulionyooka kama hapo awali, na hata akakunja kipaji kidogo.

Melissa, ambaye alishika mkono wa Sam, alisema kwa upole, “Alissa, ni mshangao ulioje! Kwa nini uko hapa? Nakumbuka kuwa hupendi tukio la aina hii.”

Alissa?

Nilesh na Mathew walishangaa. Hawakuwahi kufikiria kwamba Alissa alikuwa binti wa thamani wa familia ya Maziku.

Familia ya Maziku ilikuwa na ushawishi mkubwa katika Jiji la Mwanza, na baada ya kuunganishwa kwa ndoa na familia ya Masolwa, ilianza kushirikiana na familia ya Masolwa kibiashara. Thamani yao iliongezeka sana.

“Ninahudhuria tafrija hii kwa niaba ya kampuni. Unaweza kuniita Miss Maziku au Meneja Maziku.” Alissa aliweka umbali na Melissa kwa nje.

Melissa aliaibishwa ghafla na maneno ya Alissa, kana kwamba Melissa alijipendekeza kwa Alissa kwa makusudi.

"Alissa, mbona hujali?" Melissa alitabasamu ili kupunguza hali ya hila kati yao, "Sisi ni dada na tulikua pamoja."

"Afadhali tuweke wazi juu ya jambo fulani." Mtazamo wa Alissa ulimzunguka Seidrick karibu na Melissa, "Ingawa sisi ni dada, kuna kitu ambacho hatuwezi kushiriki na kila mmoja."

Sura ya 160
Kwa hakika, kidokezo cha Alissa kilimfanya Melissa kuwa na wasiwasi kwamba alishindwa kujizuia kushika mikono ya Seidrick kwa nguvu.

Seidrick pia alihisi wazi mabadiliko ya Melissa, hivyo alinyoosha mkono wake kimya kwenye mkono wake, ambao ulimshikilia kwa nguvu, na kumfariji.

"Alissa yuko sawa. Baadhi ya mambo ni wazi hayawezi kushirikiwa, kwa hivyo ni bora kutotamani vitu ambavyo si vyako.”

Seidrick akimlinda, Melissa alijiamini zaidi. Aling'ang'ania Seidrick kwa ukaribu zaidi, akionyesha kwamba Seidrick alikuwa wake.

Alissa hakujali hata kidogo, lakini sasa ilimbidi aigize nafasi ya mwanamke ambaye aliachwa na Kendrick na alitaka kumlenga Seidrick… Hii ilihitaji uigizaji stadi.

"Ndio, hata kama mtu alitamani na kupata alichotaka, hawakufanya kwa haki, hivyo mwishowe, wanaweza kuachwa ..." Alissa alipumua sana, kana kwamba alikuwa akijiongelea mwenyewe huku akimshutumu Melissa.

Melissa kwa kawaida alifikiria kuwa Alissa ameachwa na Kendrick. Alifurahi na tabasamu kidogo likajijenga usoni mwake.
“Uko sahihi,” Melissa alikubali.

Watu ambao hawakuwaelewa walihisi kwamba mazungumzo yao yalikuwa ya kutatanisha kidogo, lakini uadui wa maneno yao ulikuwa dhahiri.

"Bwana Alex, sikutarajia Alissa angekuwa binti yako. Yeye ni mtu hodari sana na mkarimu, na kazi yake ni bora. Kampuni inamthamini sana.” Nilesh alibadili mada na kumsifia Alissa.

“Asante, Bw. Nilesh.” Alex alitikisa kichwa na kutabasamu. "Ni kwa sababu kampuni ilimpa fursa."

Nilesh alileta mada za kikazi na akafanikiwa kupunguza hali hiyo.

Alissa alihisi kwamba kulikuwa na watu wengi hapa na kulikuwa na mtiririko mdogo wa hewa. Alikuwa na shida kidogo ya kupumua. "Samahani."

Baada ya kuongea aligeuka na kuondoka. Nilesh alimtazama kwa wasiwasi kidogo. Hakuonekana vizuri. Je, alikuwa anajisikia vibaya?

Lakini alianza mazungumzo hapa na Alex na Sam, kwa hivyo hakuweza kuondoka naye.

Alissa akatoka kwenye mlango wa nyuma wa jumba la karamu. Ilikuwa ni bustani ndogo isiyokuwa na mtu ndani, hivyo palikuwa kimya sana. Mimea ilikuwa imestawi vyema. Kulikuwa na upepo usiku. Hatimaye alijisikia raha, isipokuwa bado alipata upungufu wa pumzi ambao ulikuwa bado haujaisha.

Alissa aliona benchi karibu na kichaka cha maua, hivyo akasogea na kuketi.

Baada ya muda, sura ilionekana machoni pake.

“Bi Maziku, uko peke yako?" Sauti hii ilikuwa ya Timothy.

Alissa aligeuza kichwa chake na kumuona akiwa amesimama kwenye kivuli huku akiwa na tabasamu usoni ambalo lilionekana kuwa mbaya sana kwa wakati huu.

“Kuna nini bwana Timothy?” Alissa aligeuza uso wake kidogo na kumtazama.

“Vipi wewe na bwana Kendrick?” Timothy aliuliza kwa uwazi.

"Vizuri sana." Alissa alitabasamu sana, macho yake safi kama nyota zinazong'aa usiku.

"Bwana Kendrick huja kuambatana nawe mara kwa mara, lakini hajafika hapa kwa muda mrefu hivi majuzi. Atakuwa kwenye safari ya kikazi?” Timothy akasogea karibu zaidi, kivuli chake kikirefuka kwa miondoko yake.

“Hayuko katika safari ya kikazi, na hana shughuli nyingi sana kazini. Yeye huenda tu nyumbani kwa wakati kila siku kula chakula na mke wake.”

Kidokezo katika maneno yake kilikuwa dhahiri sana. Kendrick bado alimjali mke wake, na alikuwa tu mchezo wake wa pupa.

Sasa kwa kuwa alicheza naye na kupoteza hamu, alikuwa karibu au alikuwa tayari ameachwa.
"Kwa hiyo?" Alissa hakujali.

Kendrick alisasisha hali yake kwenye mtandao wake wa facebook, na zote zilihusu yeye kutoka kazini kwa wakati na kwenda nyumbani kuandamana na mke wake.

Kisha pia alichapisha baadhi ya picha za chakula hicho na nukuu zikisema kwamba alipenda watu wa familia yake zaidi na milo iliyopikwa nyumbani zaidi. Ingawa hakutaja wazi ni nani aliyeitengeneza, aliaminisha umma kwamba chakula kiliandaliwa na Bi. Mayala.

Ingawa Kendrick hakukubali wala kukanusha, aliwafanya wengine wamuamini.

Hata hivyo ni Alissa pekee ndiye aliyejua kuwa huo ni mpango ambao Kendrick na yeye waliutengeneza ili kuwachanganya adui.

"Bwana Kendrick amerudi kwa familia yake. Mbona unasubiri hapa kwa ujinga?" Timothy naye akaketi kando yake.

Alissa alisogea pembeni kidogo, hakutaka kujiweka karibu naye. "Hapana, hataniacha hivi."

“Kama msemo unavyosema, usipendane na mwanamume mwenye familia. Utaachwa tu.” Timothy alipomwona hivyo alitabasamu badala ya kukasirika huku akitazama kando ya uso wake maridadi. “Bi Maziku ni mwerevu sana, kwa hivyo hawezije kuelewa sababu? Isitoshe, Bwana Kendrick si mtu wa kawaida, na ndoa yake haiwezi kulinganishwa. Yeye ni mwenye nguvu na mtukufu. Ulijihusisha naye, lakini unaweza kumshinda? Wanaume wakimaliza kurukaruka nje watarudi kwa familia zao. Afadhali kuwa mke wa mtu kuliko kuwa hawara wa mtu.”

Alissa alishusha kope zake kidogo, macho yake yakionekana kulegalega. "Bwana Timothyuko sahihi. Mimi ni mjinga sana hata kumwamini…”

Aliruhusu machozi yajae machoni mwake na kuinua mkono wake kufuta chozi lililokuwa likimtoka. Sura yake ya kusikitisha iliwafanya watu wahisi huzuni.

“Bi Maziku, ikiwa haujali, naweza kukukopesha bega langu." Timothy akatoa kitambaa mfukoni na kumkabidhi.

Alissa akatingisha kichwa huku akijifanya ana nguvu. “Sijambo. Asante.
Sitaki tu kukubali. Sijali kama ameoa na ana mke. Nilimpa mwili na roho yangu. Alisema wazi atanilinda maisha yangu yote. Angewezaje kuvunja ahadi yake na kuniacha peke yangu?”

Timothy aliposikiliza maneno ya Alissa, alitabasamu kwa siri. Ilionekana kuwa alichokisikia Melissa kuhusu Kendrick na Alissa wakigombana kilikuwa kweli. Uhusiano wao ulikuwa tayari umevunjika. Sasa alijua kutokana na maneno ya Alissa kuwa Kendrick alikuwa ameachana naye.

Timothy alifurahi. Juhudi za pamoja za yeye na Melissa hazikuwa bure.

Walikuwa wakitarajia Alissa na Kendrick kuachana ili Alissa apoteze msaada wake. Hapo ndipo wangeweza kumwadhibu.

Alimdanganya kwa makusudi na kumtia aibu mbele ya Kendrick. Angewezaje kumsamehe na kumwacha aondoke kirahisi?

“Usiwe na huzuni. Tunaweza kuanza tena ukitaka.” Timothy alichukua mbinu ya upole, akijaribu kuvunja ulinzi wa Alissa wakati alikuwa 'amejeruhiwa' zaidi. “Sijali uhusiano kati yako na bwana Kendrick. Baada ya yote, hakuna mwanamke Bwana Kendrick hawezi kupata na uwezo wake.

“Sitaki kumzungumzia. Nataka kumsahau na kuanza upya.” Alissa alisema kwa upole. “Nataka kuingia ndani.” Alissa akainuka, na Timothy akamfuata.

Alissa aliporudi kwenye jumba la karamu, alisikia tu vurugu kubwa. Alimwona Kendrick, mtu mwenye mvuto zaidi mle chumbani, akiwa amesimama kati ya umati wa watu waliokuwa wakiongezeka.

Bado alikuwa kwenye shati jeupe la kawaida na suti nyeusi. Alikuwa mrefu na mwembamba, akilinganishwa na wanamitindo wa kiume, na alionekana mtanashati na maridadi kuliko wanaume wengine. Alikuwa amekomaa na ametungwa.

Macho yake ya kina yalikuwa makali na tulivu kutokana na uzoefu wa miaka mingi kuwa katika nyadhifa za mamlaka ambazo hakuna aliyethubutu kumvunjia heshima.
 
USINIACHE 4:
Sura ya 161

Kendrick bila shaka alikuwa mgeni mashuhuri katika hafla kama hiyo. Watu wa tabaka mbalimbali walitaka kupendezwa naye, wakijivunia nafasi hiyo ya kuzungumza naye.

Aliitikia kwa kichwa kama salamu kwa mtu yeyote kisha akatembea moja kwa moja hadi sehemu ambayo Alex na wengine walikuwa kwenye umati wa watu.
Wale waliomfuata macho walishangaa kwamba angechukua hatua ya kutafuta mtu.

"Bwana. Kendrick yuko hapa pia. Jinsi ya kupendeza." Timothy alisimama nyuma ya Alissa. “Unataka kwenda juu?”

"Sitaki kwenda huko." Alissa akatikisa kichwa huku akionyesha huzuni.

Kwa kweli Alissa alikuwa anashangaa kwanini Kendrick alikuja. Hakumwambia kwamba atakuja kwenye karamu hii leo.

Alikuwa hapa kwa ajili ya nini? Je, alikuwa na wasiwasi kuhusu Nilesh au alikuja kuigiza naye?

“Unaogopa kukutana naye?” Timothy alidhani hii ndiyo hali aliyokuwa nayo Alissa, hivyo akazungumza ili kumtia moyo. "Siku zote nitasimama nyuma yako na kukuunga mkono. Ingawa kuna pengo kati yangu na Bwana Kendrick, upendo wangu kwako ni wa kweli. Kwa kuwa yuko hapa, basi unapaswa kukabiliana naye kwa ujasiri ili kumjulisha kwamba unaweza pia kuwa na urahisi bila yeye. Nakuunga mkono ukijidhihirisha.”

Alissa alisita, “Mimi…”

"Hatua ya kwanza ni ngumu, lakini mradi tu unapiga hatua moja kwa mguu wako wa kushoto, mguu wako wa kulia utaendelea. Hutaki kwenda kumsikiliza mjomba Alex anachotaka kumwambia?”

Hatimaye Alissa alijipa ujasiri. “Twende zetu.”

Alissa akasonga mbele. Hapo awali, kulikuwa na watu sita, wanandoa wa Maziku na wanandoa wawili wa Masolwa. Sasa Kendrick alijiunga, pamoja na Nilesh na Matthew, ilikuwa ya kusisimua sana na pia ilikuwa katikati na lengo la ukumbi mzima wa karamu.

Walisalimiana na Kendrick, lakini ghafla Maira alizimia na kumuegemea Sam.

"Mama Seidrick, una shida gani?" Sam alimshika mkono mkewe, ambaye miguu yake ilikuwa dhaifu.

“Sijambo. Ni anemia tu. Hili ni tatizo la zamani.” Maira alichukua fursa ya nguvu za Sam kusimama kwa utulivu.

"Seidrick, mwambie dereva ampeleke mama yako nyumbani akapumzike." Sam aliona uso wake wa rangi na alikuwa na wasiwasi.

Maira akatikisa kichwa na kusisitiza kubaki. “Sijambo. Nitapumzika kidogo tu.”

"Basi nitamsaidia mama yangu kukaa chini." Seidrick ilimsaidia Maira hadi eneo la mapumziko.

Maira alichukua nafasi hiyo kumtazama kwa makini Kendrick alipompita.

"Naomba unisamehe mke wangu," Sam alisema.

"Ni sawa." Kila mtu alikuwa anaelewa.

Alissa alitembea taratibu huku akificha hisia zake na kubadilika na kuwa katika hali nzuri. Akiwa na tabasamu usoni mwake, alionekana kama mnyama ambaye alikuwa ameingia kwenye jumba la karamu, akionekana kung'aa.

Ni kwamba Kendrick hakumwangalia mwanzo mwisho, achilia mbali kumtazama.

"Kendrick na Alissa hawapaswi kuzoeana hivi," walifikiria watu waliojua uhusiano wao.

Hasa Alex alipoona Kendrick na Alissa hawakuwa wamejibizana hata kidogo au hata kutazamana machoni, aliingiwa na wasiwasi kidogo juu ya nini kilikuwa kibaya kati yao.

Lakini uhusiano wao unaweza kuwa wa siri tu, kwa hivyo Alex hakuweza kuuliza juu yake hadharani.

"Uko salama?" Nilesh alimuona Alissa akiondoka kwa muda na kukuta macho yake yalikuwa mekundu kidogo.

“Sijambo. Kulikuwa na mambo mengi humu ndani, nikaenda kutembea kidogo,” alisema Alissa huku akitabasamu. "Mimi niko vizuri sasa."

Nilesh kwa kawaida alihisi kuna kitu hakikuwa sawa kati ya Alissa na Kendrick, kana kwamba hawakuonana.

Lakini Alissa alisema ni watu wachache sana wanaofahamu uhusiano wao wakiwa mke na mume, hivyo akamtaka afanye siri na asiseme chochote hadharani. Vinginevyo, bila shaka angeuliza hadithi nzima.

"Bwana Kendrick ni mara chache sana kufika nyumbani siku hizi. Je, ni kwa sababu kazi ni nyingi sana?” aliuliza Melissa.

"Kwa kweli si shughuli nyingi. Ni kwamba mke wangu amekuwa akipenda kupika hivi karibuni. Alitengeneza vitu mbalimbali kila siku na akaniomba nirudi mapema na kuonja mwenyewe.” Kendrick alipokuwa akiongea kuhusu mke wake, macho yake makali yakawa ya upole. "Siwezi kupingana naye na siwezi kufanya chochote juu yake ..."

Ni wazi alisikika kama anamharibia Alissa na kumkemea au kumzodoa. Alikuwa akionyesha uhusiano wao kwa hila.

Nilesh alikunja uso aliposikia na alikasirika kidogo. Ilikuwa dhahiri kuwa Alissa alikuwa hapa, kwa nini Kendrick alisema kuwa Bi Mayala alikuwa nyumbani? Aliifanya isikike kana kwamba Alissa hakuwa Bi Mayala.

Je, Alissa alikuwa anamdanganya? Hapana, hakuwahi kumdanganya tangu alipomfahamu.

Nini hasa kilikuwa kikiendelea?

Nilesh alimtazama Alissa kwa mashaka, na yule wa pili akapepesa macho yake mara mbili mbili. Mwangaza ukamulika na kumtaka asiongee bali aendelee kutazama.

Hakuwa na la kufanya zaidi ya kuzuia hasira yake na kutazama kwa siri. Alissa hakuwa na wasiwasi, hivyo yeye alikuwa na wasiwasi wa nini?

Ikiwa Bi Mayala angekuwa mtu mwingine, haingekuwa mbaya ikiwa Alissa alimdanganya kweli. Angalau ilimaanisha kuwa alikuwa peke yake, na bado alikuwa na nafasi.

Ingawa walikubaliana kwamba wangekuwa marafiki, bado alitaka zaidi.

"Bwana. Kendrick anampenda sana Bi Mayala. Wewe ni mume mzuri sana,” alisifia Sam ambaye hakujua undani wake.

“Asante bwana Sam.” Sauti ya Kendrick ilikuwa baridi na ya kupendeza. “Wanawake ni wasumbufu. Ikiwa sitamsikiliza, basi angefadhaika, na hakutakuwa na amani tena. Kwa hiyo, ikiwa unataka kuwa na siku yenye amani nyumbani, ni lazima umsikilize mke wako.”

“Umesema kweli bwana Kendrick. Ni muhimu kuwa muungwana na kuwatendea wanawake mema, achilia mbali mkeo.” Sam pia alijulikana sana kwa kumtendea mema mkewe. Alikuwa na uhusiano wa upendo na mke wake.

Alex na Marry hawakuweza hata kuongea, wala hawakuthubutu kujibu. Baada ya yote, binti yao, Alissa, alikuwa mwanamke wa pembeni. Hawakuweza kulizungumzia hadharani.

Waliweza kucheka tu kwa aibu, lakini kadiri walivyozidi kulifikiria, ndivyo walivyozidi kuchanganyikiwa.

"Bwana Kendrick alikuja peke yake? Kwa nini hukumleta mkeo kwenye karamu? Nilisikia kuwa Bi. Mayala pia anatoka Mwanza, kwa hivyo ingekuwa fursa nzuri kwetu kukutana naye na kujua ni familia gani anatoka,” alisema Sam.

"Ni kweli anatoka Mwanza, na alikuja nami wakati huu. Ni kwamba hajisikii vizuri, hivyo anapumzika hotelini.”

Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Kendrick kuongea juu ya mkewe hadharani. Jinsi alivyozungumza juu yake aliwafanya wanawake waone wivu.

Melissa alimsikia Kendrick akiongea kuhusu Bi. Mayala na alishangaa na kushtuka. Ikiwa Bi Mayala angemjua yule mwanamke mwingine na kumkabili Alissa, basi kungekuwa na jambo la kutazamia.

"Bwana Kendrick anampenda Bi. Mayala kupita kiasi na hataki tukutane, sivyo?” Melissa, ambaye alikuwa akitazama, alipata fursa sahihi ya kujiunga na mazungumzo. "Sote tunamwonea wivu Bi. Mayala kwa kuwa na mapenzi ya Bw. Kendrick."

“Je, Bw. Seidrick hampendi Bi. Masolwa?” Kendrick alimtazama ambaye uso wake ulilegea kidogo baada ya kusikia swali lake la balagha.

Baada ya Seidrick kumsaidia mama yake, haya ndiyo maneno aliyoyasikia na kumfanya mwonekano wake kuwa baridi kidogo.

Sura ya 162

Macho ya Kendrick na Seidrick yakagongana, yule wa kwanza akapumzika na yule wa pili akiwa mzito.

Melissa alishika mkono wa Seidrick haraka baada ya kuona hali hiyo. "Bila shaka hapana. Mume wangu ananipenda sana.”

“Basi Bibi Masolwa hatakiwi kumuonea wivu mke wangu. Vinginevyo, nitafikiri Bibi Masolwa anataka kitu kingine.”

Mapendekezo ya maneno ya Kendrick yalikuwa sawa. Mtu yeyote angeweza kujua maana, lakini hakuna aliyethubutu kufikiria zaidi kuhusu Kendrick.

"Sisi ni wanandoa wenye upendo ambao wanaaminiana na ni waaminifu kwa kila mmoja. Kwa kawaida hatutakuwa na mawazo yoyote ambayo Bw. Kendrick alisema hivi punde,” Seidrick alisema kumsaidia Melissa. "Sisi sote ni watu wenye maadili. Hatufanyi mambo yanayovuka mipaka.”

Maana yake ni kwamba japo Kendrick alikuwa anavutia, hakutosha kumvutia mkewe.
Lakini sio wale ambao hawakuwa na maadili. Kuhusu ni nani ambaye hakuwa na maadili - ilikuwa ni Alissa, "mwanamke wa pembeni wa Kendrick", machoni pa Seidrick.

"Bwana Seidrick alisema vizuri sana. Maadili ni muhimu, la sivyo, wewe ni mpotovu.” Tabasamu la Alissa likazidi kuongezeka, hakujali tabia ya Seidrick ya chuki dhidi yake.

“Haha… Kwa nini mazungumzo haya ni mazito?” Alex hakupenda alichokisikia na aliona aibu. "Bwana Mayala, tupumzike kidogo.”

"Ndio, zungumza kuhusu jambo la kawaida." Mtu anayeitwa Bwana Jax pia aliingia ili kupunguza hali hiyo. "Bwana.
Kendrick na Mr. Seidrick wote ni vijana na wamefanikiwa katika uhusiano na kazi zao. Tofauti na mwanangu ambaye amekuwa akijificha nje ya nchi miaka yote na harudi tena. Nina wasiwasi sana ikizingatiwa anakaribia miaka 30 na hana rafiki wa kike bado.”

"Siku hizi, vijana wanachelewa kuoa, tofauti na zamani ambazo tulikuwa tunafunga ndoa punde tu umri wetu ukitosha kufanya hivyo."

"Bwana Jax, Binti mdogo wa Alex ameolewa na Bw. Seidrick. Tuna wivu sana kwa kuwa una mkwe mzuri hivi."

“Ndiyo, binti mdogo wa Bw. Alex ameolewa. Ninatamani kujua binti yako mkubwa aliolewa katika familia gani ya daraja la juu?”

“Yeye…” Alex alimtazama Alissa lakini hakuweza kuendelea na maneno yake.

Kendrick alikuwepo. Ijapokuwa wawili hao hawakutangamana, hakuthubutu kuongea upuuzi.

"Bwana Jax, dada yangu bado hajaolewa,” alisema Melissa. Alissa alikuwa ameachwa na Kendrick, hivyo haikujalisha alichosema.
Isitoshe, alisema ukweli.

“Yeye hajaolewa?” Bwana Jax alimtazama Alissa na kutikisa kichwa kumsifu. "Binti mkubwa wa Alex ni mrembo sana. Ninaogopa kwamba kuna wachumba wengi sana kwamba hakuna nafasi tena katika jumba la kifahari la familia ya Maziku, huh?

"Hehe… Hapana, yeye ni msichana wa kawaida tu," Alex alisema kwa unyenyekevu.

Ingawa Marry hakuongea kwa shida, hakumpenda Alissa kutoka ndani ya moyo wake kama Alex. Alichokifanya miaka mitano iliyopita kiliharibu sifa ya familia ya Maziku. Ikiwa si familia ya Maziku na jitihada za familia ya Masolwa kuficha kila kitu na kumbukumbu mbaya ambazo watu siku hizi walikuwa nazo, basi kila mtu angeicheka familia ya Maziku.

"Ikiwa Bw. Alex hajali, basi vipi kuhusu kuanzisha uchumba kwa ajili ya mvulana wangu na Miss. Maziku kuwa na chakula pamoja?" Bwana
Jax alitaka ndoa iliyopangwa kimakusudi na familia ya Maziku.

"Asante, Bwana Jax." Alex alikuwa na msongo wa mawazo haswa kwa sababu Kendrick alikuwa bado yupo hivyo hakuthubutu kumfanyia maamuzi Alissa.

"Bwana Jax, siku hizi ndoa za vijana si juu ya wazazi wao. Wanataka kuwa na ndoa ya upendo… Labda ingekuwa bora kwako kumuuliza wewe mwenyewe kwenye mlo kwa ajili yake na mwanao. Kitu pekee tunachoweza kufanya kama wazazi ni kutokuwa na hasira." Kutoridhika kwa Marry na Alissa ilionekana wazi kwa maneno yake, lakini aliificha iwezekanavyo.

"Binti Maziku anafikiria nini?" Bwana Jax alimgeukia Alissa na kumuuliza. "Kwa kuwa Bi Maziku na mwanangu wote hawana wachumba, kwa nini usijaribu?"

Alissa alitabasamu kidogo lakini hakujibu, alisikiliza kwa adabu tu.

“Bi Maziku hataki? Aliuliza Bw. Jax.

“Siyo kwamba sitaki. Siwezi kusema ndiyo.” Alissa alikumbuka kuwa yeye ni mwanamke aliyeolewa, kwa hiyo angewezaje kuwa mchumba wa mtu mwingine?

"Nini maana ya Miss Maziku? Unamdharau mwanangu? Labda Bi Maziku aliweka upau juu sana." Bwana Jax alichukizwa kidogo na jinsi Alissa alivyokataa pendekezo lake kwa uwazi.

Melissa aliendelea na mazungumzo. "Bwana Jax, unaweza kuwa hujasikia, lakini Bw. Timothy anampenda dada yangu na kumchumbia, lakini hakukubali. Kweli, yeye ni mrembo sana. ”…

Kile Melissa alitaka kumaanisha kilikuwa dhahiri, na Bw. Jax pia alielewa. "Kwa hivyo Bi. Maziku ana matarajio makubwa na hafikirii mtu yeyote tu?"

“Nafikiri hakuna ubaya kuwa na matarajio makubwa,” Alissa alikiri waziwazi. "Hata inabidi uchague wakati unanunua kabichi kwenye duka la mboga. Hili ni suala la furaha yangu katika maisha yangu yote, kwa hivyo hakuna ubaya kuwa mchaguzi.”

Uso wa Bwana Jax ulikuwa umekunjamana, na alihisi kudhalilishwa.

"Labda Bi. Maziku anatuona kama kabichi za bei rahisi?" Timothy alidhihaki.

“Kwani bwana Timothy hujui sifa yako ni mbaya? Nadhani kumlinganisha bwana Timothy na kabichi ni tusi kwa kabichi. Nafikiri tikitimaji lililooza ni ulinganisho unaofaa zaidi kwa Bw. Timothy.” Alissa alimtazama Timothy bila kujieleza. Macho yake yalikuwa baridi, na maneno yake yalikuwa mabaya.

Alissa, ambaye sasa alikuwa na uwepo wa nguvu, alikuwa tofauti kabisa na Alissa dhaifu na mwenye huzuni katika bustani ndogo sasa hivi.

Maneno ya Alissa yalifanikiwa kumkasirisha Timothy. Alikuwa na sura ya kutisha usoni mwake, na macho yake yalijawa na hasira. Alikoroma kwa ubaridi, “Alissa, nina sifa mbaya? Halafu wewe ni mtu wa aina gani?"

"Usijali kuwa na talaka na mtoto. Unataka kujihusisha na mtu wa nafasi ya juu ya kijamii. Angalau sina mtoto na sina maadili, sawa! Wewe je uliyekuwa Hawara wa mtu? Kando na wewe kuwa mrembo, una nguvu gani za kutisha? Unastahili kuachwa!”

Timothey alikuwa mtu ambaye kichwa chake kilijawa na tamaa ya wanawake. Akawa mwenye midomo mikubwa kirahisi kwa sababu alikuwa akikasirika kila anapopatwa na tatizo.

Alipozungumza tu, kila mtu alikuwa katika ghasia. Hakuna aliyetarajia Alissa, ambaye alionekana kuwa msafi na asiye na hatia, kuwa mwanamke mwingine, yaani hawara.

Nilesh na Mathew hawakuamini kwamba Alissa alikuwa mtu kama huyo, lakini wengine hawakufikiri hivyo. Baadhi ya watu “wenye haki” walianza kumkosoa na kumshambulia Alissa kwa maneno, na akawa adui wa umma.

Hasa, Bw. Jax, ambaye alikuwa amekasirishwa tu na Alissa, alidhihaki, “Bi. Maziku hakika ina ladha ya kipekee. Afadhali kuwa mwanamke mwingine kuliko kuwa mke? Sasa najua kutokuwa na aibu kunaonekanaje!"

"Nashangaa ni nani ambaye hana bahati ya kulaghaiwa kwa sababu yake!"

Hata hivyo, Kendrick alisimama na kutazama pembeni bila kusema neno lolote. Jambo hilo lilizidi kuwaaminisha Timothy na Melissa kuwa Kendrick na Alissa walikuwa wameachana.

“Niliachwa na nani? Una ushahidi wowote?" Alissa bado alikuwa mtulivu, hakuwa na wasiwasi wala hasira.

“Kwa nini nizungumze mambo ambayo sina ushahidi nayo? nitakujulisha.” Timothy alicheka kwa ushindi

Sura ya 163

"Basi onyesha ushahidi wako mbele ya kila mtu." Alissa alitulia bila woga huku akitabasamu.
Timothy alichukua simu yake na kucheza rekodi ya sauti.

[Nimekuwa nyumbani kwa mtu huyo. Wazazi wake walipojua kwamba Alissa alikuwa hawara wa mwanawe, walikasirika sana… inaonekana kwamba Alissa amefikia kikomo. Wanawake wanaoharibu familia wafe. ..]

“Mtu huyu ni nani? Hebu aje hapa na kunikabili.” Utulivu wa Alissa ulimfanya Timothy ajione kuwa ni mnene sana.

Timothy alisema, "Ili kulinda usalama wa mtu anayehusika, siwezi kukuambia yeye ni nani."

"Zaidi ya hayo, ulinilalamikia kwenye bustani ndogo nje sasa hivi. Ulisema umeachwa.” Timothy alicheza sehemu ya mazungumzo aliyokuwa nayo na Alissa hivi sasa.

Kwa kuzingatia maudhui ya mazungumzo, sauti hii ilishawishi zaidi. Baada ya yote, alichosema Alissa kilimfanya asikike kama ameachwa.

Naye Timothy alikuwa hapa kama shahidi.

“Basi bwana Timothy, kwa kuwa huna shida na maisha yangu ya nyuma, tunaweza kuanza upya kadri nitakavyo,” Alissa alisema maneno ambayo aliyakata. “Hata nikithubutu kukukubali, unathubutu kunioa?”

Alikuwa ni mke wa Kendrick. Nani angethubutu kumuoa?

Na watu hawa walikuwa wajinga sana. Waliamini katika kile kinachoitwa ushahidi ambao Timothy aliwasilisha ingawa mtoa habari hakuthubutu kuuthibitisha.

Kwa kawaida Timothy hangekubali kwamba hilo lilikuwa kweli. “Nani atataka kuoa mwanamke kama wewe! Usizungumze ujinga. Mwanaume zaidi angefanya ni kukutumia kama kitu cha starehe. Nani angeoa bibi? Isipokuwa kuna kitu kibaya kichwani mwake."

Waliotazama tanthilia hiyo wote walikubaliana na Timothy na kumkosoa Alissa kwa kukosa aibu na kujiamini.

“Unawezaje kumwambia hivyo dada yangu. Si rahisi kwake kuwa single mama na mtoto. Hakuwa na chaguo kwa sababu ya maisha.
Usimlaumu.” Maneno ya Melissa yaliwafanya watu wahisi kuwa Alissa alijitoa ili asiishi maisha magumu.

Nilesh hasa hakuelewa ni nini kilikuwa kikiendelea kati ya Kendrick na Alissa. "Alissa, nini kinaendelea?"

"Kuna mtu ananipanga." Alissa alimtazama Nilesh aliyekuwa na wasiwasi. "
“Sikilizeni nyote. Mimi, Alissa, sitakuwa hawara wa mtu yeyote! Ikiwa ninataka kuolewa na mtu, bila shaka nitakuwa mke wake."

“Mh! Hakuna atakayekuoa hata ukitaka kuolewa,” alikoroma Timothy kwa dharau.
Aliwatazama watu waliokuwa karibu naye kisha akachagua wanaume wachache waliooa bila mpangilio na kuwauliza, “Je, unataka kumuoa?”

Takriban watu wote waliokuwa kwenye karamu hiyo walikuwa watu mashuhuri katika Jiji la Mwanza. Sasa Alissa alipojulikana kama mwanamke hawara, sifa yake iliharibiwa, na hakuna mtu aliyethubutu kumuoa.

Kwa sababu hiyo, watu ambao Timothy aliwauliza walitikisa vichwa vyao kwa wasiwasi kwa kuhofia sifa yao.

Timothy aliona kila mtu aliharakisha kumkwepa Alissa na kutabasamu kama mshindi. "Angalia, nani atakuoa?"

"Ningemuoa, mradi tu akubali." Nilesh ndiye aliyeongea. Hakuweza tena kuwatazama watu wanavyomtusi Alissa na kukasirika zaidi wakati Kendrick hakusema neno.

Hivyo alihitimisha kuwa kweli Alissa alimdanganya. Alikuwa akimtumia Kendrick kama kisingizio cha kumkataa.

Ingawa hakuna aliyempenda Alissa sasa, bado alimuunga mkono. Hakuamini kuwa angeharibu ndoa na familia ya mtu mwingine.

"Bwana Nilesh, sio jambo lako.” Wakati kila mtu karibu kusahau uwepo wake, Kendrick, alizungumza kwa njia ya kutawala.

"Kendrick anataka kumuoa Alissa kama mimi?" Nilesh alimtazama Kendrick kwa macho ya kumtoboa na kuuliza bila woga.

"Kisha unapaswa kuuliza kwanza ikiwa anataka kuolewa nawe." Kendrick alikuwa amevalia shati na suruali za bei ghali. Alikuwa charismatic na alikuwa na uwepo wa nguvu.

Nilesh alimtazama Alissa kwa hisia tofauti. Alijua kabisa Alissa hatataka kuolewa naye. Ikiwa angetaka, asingemkataa mara nyingi na hata kufikia hatua ya kumdanganya kuhusu kuolewa na Kendrick.

"Bwana Kendrick, usisahau kuwa wewe ni mtu aliyeoa. Si jambo lako pia.” Nilesh hakumuuliza Alissa badala yake alitoa maoni yake.

“Sihitaji bwana Nilesh kuhangaikia biashara yangu,” alisema Kendrick kwa kujigamba. "Mimi ndiye mtu anayestahili kusema hivi."

Nilesh alikunja uso, akifikiria maneno yake. "Bwana Kendrick, tafadhali nifafanulie.”

“Tayari ameshaolewa, kwa hiyo usimfikirie tena, Bw. Nilesh.” Midomo myembamba ya Kendrick ilisogea kidogo alipokuwa akisema maneno haya.

"Ameolewa?"

Kila mtu aliposikia maneno ya Kendrick, wote walichanganyikiwa na kuanza kuzungumza wao kwa wao.

Walisikia tu kwamba Alissa ndiye mwanamke mwingine aliyeharibu familia ya mtu mwingine, lakini sasa akawa mwanamke aliyeolewa? Iliwafanya watazamaji kuchanganyikiwa sana.

Hasa Alex, Marry, Sam, Seidrick, Melissa, na wengine walishangaa zaidi.

Melissa hakushangaa tu bali pia alichukia. Mwanamke kama Alissa anapaswa kuharibu sifa yake na kuondoka katika familia ya Maziku na Mwanza kwa mara nyingine tena, lakini alikuwa ameolewa?

Isitoshe, ni Kendrick ndiye aliyezungumza. Je, hawakuachana tayari? Kwanini Kendrick bado aliongea kwa ajili ya Alissa?

"Bwana Kendrick inaonekana unamfahamu sana dada yangu kulingana na maneno yako. Halafu bwana Kendrick anaweza kuniambia dada yangu ameolewa na nani?” Melissa alisita kukubali kuwa Kendrick bado anamlinda Alissa.

Alijisikia furaha mara baada ya kufikiria uhusiano kati ya Kendrick na Alissa kuwa wazi, huku Alissa akiwa mchimba dhahabu na mwanamke mwingine.

Kendrick akasogea mbele na kuelekea upande wa Alissa kwa hatua kadhaa. Macho yao yalikutana. Macho ya Alissa yalionyesha chembe za furaha, na macho ya Kendrick yalikuwa mazito na meusi. Walidhamiria kushinda chochote.

Akaunyoosha mkono wake mrefu kwenye kiuno cha Alissa na kukiweka kiganja chake vyema kwenye kiuno chake laini.

Tangazo kama hilo lilikuwa la kusadikisha na kuathiri zaidi kuliko maneno.

Kila mtu alipoona, alitazama kwa makini, kana kwamba wote walikuwa wamepigwa na butwaa. Chumba kilikuwa kimya kana kwamba ulimwengu umeingia wakati wa baridi.

"Bwana. ... Bwana Kendrick, unamaanisha nini?” Baada ya muda, Melissa alizinduka na kulazimisha tabasamu gumu.

Kulikuwa na sauti moyoni mwake ikipiga kelele, ikikanusha kuwa Alissa na Kendrick walikuwa wamefunga ndoa kihalali...

Hata kama Kendrick angetumia vitendo kuonyesha haki zake, hangeamini kuwa ni kweli.

Urafiki kama huo kati ya mwanamume na mwanamke haukumaanisha kuwa walikuwa mume na mke, kwa hivyo hangeamini.

“Basi nitatumia fursa hii kutangaza jambo moja. Alissa ni mke wangu halali, Bibi Mayala wangu.” Kendrick alitabasamu na kumtazama Melissa kwa macho makali, na kumpa pigo la mwisho na la nguvu.

Sura ya 164

Alichosema Kendrick kilikuwa kama wavu mkubwa, ulionasa Melissa, Timothy, Mr. Jax, Sam, Seidrick, Alex na Marry ... na wengine wote ndani yake.
Alipoushika wavu, ukawasonga.

Melissa, ambaye bado alikuwa na matumaini dhidi ya tumaini, hakuwa na udanganyifu zaidi juu yake. Alionekana kupigwa na butwaa.

Alikuwa amejitahidi sana kumshinda Alissa. Lakini hakutarajia kwamba alichokifanya kingemdhuru yeye mwenyewe.

Timothy alikuwa katika hofu. Bado alikumbuka alichosema kumdhalilisha Alissa sasa hivi. Sasa kwa kuwa "hawars" alikua Bi.
Mayala halisi, ambayo ilimshika machoni, na Kendrick alikuwepo wakati wote, Timothy alihisi kwamba hivi karibuni angekuwa mnyonge.

Isitoshe, Bwana Jax ambaye alisikiza tu maneno ya wengine na kusema kwa jeuri na kumdharau Alissa, sasa alikuwa anakula maneno yake.

“Samahani kwa kushindwa kumtambua Bi. Mayala na kuwa mpole kuamini matamshi ya upande mmoja ya wengine. Tafadhali nisamehe kutokuheshimu kwangu sasa hivi, Bw. Kendrick na Bi. Mayala.”

"Bi. Mayala ni mkarimu. Kwa hivyo, sidhani kama utafanya fujo kuhusu mambo madogo madogo na sisi.”

Kwa hivyo, ikiwa Alissa atafanya fujo, atakuwa mbaya?

Wapenda raha wengine wote walitazama chini, hawakuthubutu kutazama macho ya Kendrick. Walikuwa kimya sana, kana kwamba ndimi zao zilitolewa nje.

Nilesh akakunja uso. Alipowaona wamesimama pamoja kwa ukaribu sana, aligundua kuwa Alissa hakutafuta visingizio vya kumsingizia. Ni yeye ambaye hakuwa tayari kukiri ukweli na kupata visingizio vya kujidanganya.

Mathew alikuwa amewaza kuwa Kendrick na Alissa bado walikuwa katika hali ya kutatanisha. Hakutarajia kuwa tayari walikuwa wamefunga ndoa na wanandoa. Kwa bahati nzuri, hakuwa na upendo kwa Alissa, lakini alimthamini tu kama talanta na uwezo wake bora.

"Halo, hakuna mtu anataka kutupongeza?" Kendrick alitazama juu na kutabasamu.

Baada ya Kendrick kuwakumbusha, watu wale walionekana kurejewa na fahamu zao na kusema kwa dhati huku tabasamu zikiwa kwenye nyuso zao, “Hongera sana Bwana Kendrick na Bi Mayala!”

Walikuwa na hekima ya kidunia na wenye uwezo mkubwa sana wa kubembeleza.

Kendrick alijua kuwa wote wanajuta na walikuwa wakijiuliza iwapo atalipiza kisasi kwao kwa kile kilichotokea sasa hivi.

Melissa alipoona alichokifanya ni bure, bado hakuamini, “Kwa hadhi ya Bwana Kendrick, unawezaje kumpenda mama asiye na mume mwenye mtoto?”

“Ngoja nikuambie jambo moja zaidi. Mtoto ni binti yangu mwenyewe. Hakuna mtu anayeruhusiwa kutoa matamshi ya kutowajibika kwa mtoto wa familia ya Mayala. Tafadhali kumbuka, Bi Maziku!"

Kendrick alikuwa akimlinda sana Doris na hakuruhusu mtu yeyote kumtia kiwewe na kumdhuru.

"Bwana. Kendrick, hausemi uwongo kwetu, sivyo?" Melissa alijua fika kuwa Kendrick hakujua kuwa yeye ndiye baba wa mtoto, na Alissa asingeweza kumwambia. Alissa na Kendrick walikuwa wanandoa. Lakini nani angeamini mtoto anaweza kuwa wake?

Iwapo Kendrick ndiye baba halisi wa mtoto, ingekuwaje Alissa angeishia mbali na nyumbani enzi hizo na asingerudi Mwanza kwa miaka mingi?

Alitaka kutumia hoja hiyo kumweka Alissa kwenye wakati mgumu.

“Nilikudanganya nini? Upendo wako, moyo wako au mwili wako?" Kendrick alidhihaki ujinga wake, "Zaidi ya mke wangu, mwili wa watu wengine na upendo hauna maana kwangu."

Alichokisema Kendrick kilimaanisha kuwa Melissa hakuwa kitu kwake! Hakumjali hata kidogo.

Melissa alikunja ngumi. Kukabiliana na mabadiliko haya ya kushangaza, hatimaye hakuweza kuyakubali.

Seidrick alimshika Melissa ambaye hakuweza kujizuia kutetemeka, “Bw. Kendrick, hata ukimjali mkeo, hutakiwi kuwadharau wengine.
Bi. Mayala ni hazina kwako. Melissa ni mke wangu na pia hazina yangu. Ninamheshimu Bw. Kendrick na ninatumaini kwamba Bw. Kendrick pia anaweza kuniheshimu.”

"Je, Bwana Seidrick bado hanijui?" Kendrick akawa mzito, “Siku zote mimi ni baridi na mkatili, mkatili … mwenye ulinzi na asiye na akili.
Lakini nategemea uwezo wangu. Bwana Seidrick, unaonaje??”

Seidrick hakuwa na la kusema kujibu. Kwa utambulisho wa Kendrick, kwa kawaida hakuweza kufikiria chochote juu ya mtu yeyote.

"Natumai tu kwamba kile Bw. Kendrick alimfanyia Bi. Mayala leo kinastahili." Seidrick alimtazama Alissa akidhani ni mwerevu sana. Angeweza kuwa Bi Mayala?
Seidrick alimshangaa sana Alissa.

"Pia ninatumai kuwa juhudi za Bw. Seidrick zinastahili na hutajuta kamwe katika maisha haya." Alissa ndiye aliyejibu.

Melissa aliingiwa na woga na kushika nguo za Seidrick kwa ukali. Alitokwa na jasho kwenye paji la uso wake na kusema, "Seidrick, sijisikii vizuri ... Twende nyumbani."

"Sawa." Seidrick kisha akamnyanyua Melissa na kuondoka.

Sam naye alichukua nafasi hiyo kwenda sebuleni kumtafuta Maira na kuondoka naye, hakutaka kukutana na fujo zaidi hapo.

Umati pia ulionyesha baraka zao na kuondoka, bila kuthubutu kukaa tena. Ikiwa wangekuwa wazembe na kuchukiwa na Kendrick, wangekuwa duni.

Umati ulitawanyika. Ukweli kwamba Alissa alikuwa Bi Mayala ulikuwa umepoa kidogo.

Alex na Marry hawakuhisi chochote zaidi ya mshtuko.

Ilibainika kuwa binti yao hakuwa hawara, lakini aliweza kuolewa katika familia ya Mayala.

Kuanzia sasa, Alissa atakuwa mmoja wa watu wenye nguvu zaidi. Kama wazazi wake, walipaswa pia kumheshimu.

Walikuwa na hisia mchanganyiko sasa. Binti yao, ambaye walikuwa na matumaini makubwa naye tangu utotoni, walimwacha kabisa kwa sababu ya kuzaa bila kuolewa miaka mitano iliyopita, sasa alikuwa Bibi Mayala.

"Bwana Kendrick, hivi wewe na Alissa mmeoana kweli?” Alex bado alihisi kuwa jambo hili lilionekana kuwa sio kweli.

“Wakati mwingine nikija, nitakuletea cheti cha ndoa, ili baba apate nafuu, sawa?” Kendrick alibadilisha anwani yake kwa Alex kutoka kwa Bwana Maziku hadi kwa Baba, na kumkumbusha Alex kwamba huo ndio ukweli.

“Mlifunga ndoa lini?” Alex aliuliza. Alikuwa na maswali mengi sasa.

"Miaka mitatu iliyopita."

“Miaka mitatu iliyopita?” Ilikuwa ni muda mrefu sana. Marry naye alishtuka. Walificha uhusiano wao wa kweli vizuri, “Basi kwa nini hukutuambia ulipokuwa nyumbani kwetu mara ya mwisho? Ulisema hata Alissa ni hawara yako…”

“Nimesema mimi mwenyewe?” Kendrick pia hakutarajia kuwa wazazi wa Alissa wangedhani binti yao angekuwa bibi yake.

Alex na Marry walitikisa vichwa vyao. Kendrick hakusema hivyo mwenyewe. Lakini walimdharau Alissa na kubahatisha.

“Kama wazazi wa Alissa, mnapaswa kumfahamu vyema. Ikiwa mngemwamini vya kutosha, naamini haungemwelewa vibaya." Kendrick alimtazama Alissa kwa upole, "Bila shaka, nitamtunza na kumwamini kabisa katika siku zijazo."

Sura ya 165

Alissa alihisi joto alipoona mapenzi machoni mwa Kendrick. Hakuweza kujizuia kusukumwa.

Alikuwa ni mama asiye na mume ambaye hakupendwa na wengine. Kwenye macho ya Kendrick, alionekana kuwa bora zaidi.

Pia alimwamini kama alivyosema. Ingawa angekuwa na hasira kidogo, hangekuwa asiye na akili au kufanya fujo bure au kama mtawala jeuri.

Angempa uaminifu na uhuru wa kutosha, akimfanya ahisi kwamba anaheshimiwa.

Hata hivyo, kwa sababu ya ubaguzi wao, wazazi wake siku zote walikuwa wakimchukia na hata kumdharau, wakifikiri kwamba yeye ni mtu mpotovu. Walimchukulia kuwa yeye ndiye hawara wa Kendrick. Hawakuwahi kufikiria kwamba angekuwa Bi Mayala halisi.

Walimtazama chini kutoka ndani ya mioyo yao na kuhisi kwamba bahati na utukufu haupaswi kuwa wake.

Alikuwa amekatishwa tamaa na wazazi wake miaka mitano iliyopita. Kwa wakati huu, alihisi kuwa mbali na ukoo wa damu, walikuwa wageni wanaojulikana zaidi ulimwenguni.

"Alichosema bwana Kendrick ni sawa." Alex aliona aibu na kutokwa na jasho kwenye paji la uso wake.

Ingawa Kendrick alimwita Alex 'baba' na kukiri utambulisho wa Alex, Alex alijua wazi kuwa Kendrick alikuwa na adabu tu. Hakuthubutu kulitaja jina lake ovyo.

Alipojua Kendrick ni mume wa Alissa, alishtuka, akafurahi na pia aliogopa kidogo.

Asili na mbinu za Kendrick, pamoja na kasi yake, zilimfanya ahisi shinikizo zaidi.

Marry naye alikunja uso bila kuongea. Akiwaza walichokifanya kwa Alissa, alijiuliza Alissa atawachukuliaje sasa akiwa Bi Mayala?

“Nitawaita Mama na Baba kama Alissa anavyowaita. Kuanzia sasa mnaweza kuniita Kendrick.” Kendrick alisema ana kwa ana.

Alex na Marry hawakuwa na budi ila kuitikia kwa kichwa.
"Kisha ... Kendrick, kuanzia sasa na kuendelea, tafadhali mtunze Alissa." Alex akamwambia kama baba anayependa.

"Bila shaka nitafanya. Hakika nitamwona kuwa wa thamani. Maadamu niko hapa, hakuna anayeweza kumdhulumu. Msijali, Baba na Mama.” Kendrick aliuweka mkono wake begani kwa Alissa na kumuunga mkono.

“Tumefarijika…” Alex alimtazama Marry ambaye hakuzungumza naye na kulazimisha tabasamu lisilofaa.

Lakini alikuwa na wasiwasi ndani, bila kujua jinsi ya kukabiliana na binti yake.

“Baba, Mama, msijisumbue kunipangia siku ya kutoonana naye siku zijazo. Nadhani mnatakiwa kuridhishwa na mimi kuolewa na Kendrick.” Alissa alisema kwa kejeli nzito.

Familia nyingi maarufu zilitaka kuunganishwa na familia ya Mayala kwa ndoa. Watu wengi walitaka kujipendekeza kwa Kendrick.
Sasa, familia ya Maziku ikawa mshindi.

“Hatukujua ulikuwa umeolewa hapo awali na tulihisi huzuni kwamba ulimlea mtoto peke yako. Kwa hiyo, tulitaka kukupatia mume ili mshiriki mzigo huo. Sasa kwa vile tunajua, hakika hatutafanya hivyo tena.” Alex aliongea kwa kujiamini sana na hakuwa na haya hata kidogo.

“Baba, Timothy ni mwanaume sahihi?” Alissa alijibu kwa kejeli.

Maneno yalishindikana kwa Alex na hakuweza kusema chochote.

“Alissa, Mama na Baba walikuwa na makosa. Hebu tusahau, sawa? Ishi maisha mazuri na Kendrick. Mama na Baba wanakutakia.” Marry ambaye siku zote alikuwa na kiburi mbele ya Alissa aliongea kuwa makini sasa.

“Alissa, ni kosa la Baba. Usijisumbue na mimi.” Alex pia alikiri kosa lake.

Alissa aliwatazama Alex na mkewe ambao walikuwa wamefadhaika na kuogopa. Alijua kwamba kwa kutegemea utambulisho wa Bi Mayala, angelipiza kisasi kwa wale waliomdharau na kumfukuza.

Alissa hakuwa na nia ya kumtegemea Kendrick. Vinginevyo, hangeweza kuweka ukweli kwamba alikuwa ameolewa naye kuwa siri.
Na hakuwahi kutarajia kwamba angeweza kumtegemea mtu kama huyo. Angeweza kumwachia kila kitu na kumwamini bila masharti.

Alissa aligeuka na kukutana na macho ya Kendrick tulivu na kutabasamu sana.

Kuona tabasamu lake kama mtoto mwenye furaha, Kendrick alilainika, akiinua mkono wake kumpiga paji la uso.

“Twende zetu.”

Sauti yake ilikuwa ya upole na ya joto.

Akamnyooshea mkono. Kwa hivyo, Alissa alinyoosha mkono na kuunganisha vidole vyake na vyake, "Sawa."

Kendrick aliwaitikia kwa kichwa Alex na Marry kabla ya kuondoka, “Baba na Mama, nitamrudisha Alissa sasa hivi.”

"Sawa. Kuwa mwangalifu. "Alex alitikisa kichwa mara kwa mara,

"Alissa, ungemleta Kendrick kwa familia ya Maziku kwanza. Kwa kuwa ninyi mmeoana, ni bora mkae nyumbani kwetu. Usiende kukaa hotelini. Kwani, hoteli si nzuri kama nyumba yetu, sivyo?”

“Asante kwa wema wako, baba. Namsikiliza Alissa na nitakaa naye.” Kendrick alitenda kama mtu mzuri ambaye alimpenda sana mke wake.

"Mama na baba, kwaheri." Alissa kisha akaondoka huku akiwa ameshika mkono Kendrick.

Watu waliokuwa ukumbini waliwatazama wakishikana mikono na kuondoka.

Baada ya kutoweka, wale waliotawanyika walikusanyika tena karibu na Alex.

“Hongera sana Bwana Maziku na Bibi Maziku. Hongera…”

"Bwana. Maziku, kuanzia sasa, Bwana Kendrick itabidi akuite Baba. Unastahili kupongezwa.”

Alex alilazimisha tabasamu alipopata pongezi za wengine. Anaweza kuwa Baba wa kutisha zaidi.

Alissa na Kendrick wakatoka nje ya hoteli ile. Dereva aliendesha gari hadi kwenye mlango wa hoteli. Kendrick aliufungua mlango kwa ajili ya Alissa na kumruhusu aingie kwanza. Kisha, akaenda upande wa pili na kuingia ndani.

Dereva alipotoka nje ya hoteli hiyo, Alissa aliuliza, “Unakaa wapi usiku huu?”

"Bi. Mayala, ungependa kukaa nami hotelini? Au nikupeleke kwenye jumba langu la kifahari? Au kwa familia ya Maziku?” Kendrick alimpa chaguzi tatu.

Alissa aliegemea bega lake kwa upole, "Kwa kuwa umekubali uhusiano wetu hadharani, basi nitakukaribisha kwetu."

“Hupendi twende kwangu?” Kendrick alitazama chini, “Unanigeuka baada ya kunitumia?”

"Hapana." Alissa alikanusha, "Ninaogopa kuwa hautataka kwenda kwenye kwa familia ya Maziku na hutazoea."

"Bi. Mayala ni mtu wa kufikiria na mkarimu sana, akinifikiria. Kendrick alitania kwa sauti ya chini.

"Kuanzia sasa na kuendelea, utakuwa msaada wangu mkubwa." Alissa alimshika mkono, “Bila shaka sina budi kukufikiria. Hukuona sura za wazazi wangu walipogundua kuwa wewe ni mume wangu. Inashangaza sana.”

"Hata hivyo walikutendea vibaya hapo awali, hawatathubutu tena kukudharau." Vidole vyake vilibembeleza nyuma ya mkono wake, “Nitakuunga mkono chochote utakachofanya. Usijali.”

“Kwa nini umekuja kwenye karamu leo? Hukuniambia mapema. Ulitaka kunishangaza?” Alikuwa akimwambia kila mara alipofika Mwanza. Wakati huu, ilikuwa ni mshangao.

Sura ya 66

"Uko hapa kunisaidia? Au unaogopa kwamba siwezi kufanya hivyo peke yangu?" Aliuliza swali moja baada ya jingine.

Kendrick alitabasamu kidogo, sauti yake ikitetemeka, "Una maswali mengi."

“Ndiyo au hapana?” alitikisa mkono wake kwa urahisi na kujifanya kama mtoto a mb ayedeka.

Ikiwa ni wengine ambao walimsumbua, Kendrick angewatupa nje. Lakini alikuwa Alissa. Kendrick alijisikia mcheshi tu. Hasa Alissa, siku zote alikuwa baridi, ghafla alijifanya kama mtoto, jambo ambalo lilimfanya ashindwe kuvumilia.

"Nini unadhani; unafikiria nini?" Kendrick alimuuliza kwa kejeli na taratibu akawa serious, “Wewe ni mke wangu. Kwa kawaida sitaki kukuacha ukabiliane nayo peke yako.”

Alissa alipiga kelele, akatabasamu kwa furaha, kisha akampiga busu shavuni, “Mr. Kendrick, asante. Ni vizuri kuwa na wewe hapa.” Macho yake mazuri yalikuwa yakiangaza kama nyota, ambayo ilionekana kupendeza sana.

"Ni hayo tu?" aliinua nyusi zake kwa upole, akidhani kwamba busu hili halitoshi.

“Basi unataka nini?” Aliuma mdomo na kuuliza kwa kunong'ona.

Kendrick alichukua kifundo cha mkono wake kwa mkono mmoja, akakikandamiza nyuma ya kiti, na kuvuta sehemu ya kati ili kutenga nafasi hiyo.
Kisha, akageuka na kumuinamia kumbusu Alissa.

Aliposhangaa, alichukua nafasi hiyo kunyonya midomo yake. Alikuwa na nguvu na mtawala, na kumfanya Alissa ashindwe kupumua.

Walibusiana sana na hawakuweza kutengana, wakitaka kuwa pamoja milele…

Kendrick alichukua hatua ya kumuachia huku akiwa amemshika uso kwa mikono miwili. Aliegemeza paji la uso wake dhidi yake, akipumua sana.
Inaweza kuonekana jinsi busu lilivyokuwa kali.

Alissa alihisi pumzi yake inayowaka, huruma yake na utawala, na pumzi yake ilikuwa imechanganyikiwa.

Sasa hivi wote walikuwa wamezama katika nafsi ya kila mmoja.

“Hicho ndicho ninachotaka. Nataka hata zaidi. Unaogopa?" Sauti ya Kendrick ilisikika.

Alissa akatikisa kichwa bila kusita, "Hapana."

“Kweli?” Kendrick aliogopa akashindwa kujizuia kumgusa tena.

Ikiwa hawakuwa kwenye gari wakati huu, hangeweza kudhibiti hamu yake kwake.

“Siogopi. Umesema kwamba sihitaji kuogopa chochote nikiwa na wewe kando yangu. Nakuamini." Alissa naye alihisi angeweza kufunguka na kumkubalia.

Kendrick alifunga macho yake na kukunja uso wake kwa nguvu, akibaki na paji la uso wake dhidi yake.

Alissa kwa umakini aliinua mikono yake na kuizungusha kiunoni taratibu.

Kwa wakati huu, ukimya ulikuwa bora kuliko hotuba.

Dereva aliwapeleka kwenye jumba la Maziku na kuondoka.

Kendrick na Alissa waliingia chumbani na kumuona bibi na Doris wakicheza mchezo wa kitoto.

Walikuwa wakicheza kwa umakini sana hata hawakugundua kuwa Kendrick na Alissa walikuwa wameingia sebuleni.

“Bibi mkubwa, wewe ni mzuri. Sijashinda mchezo hata mmoja.” Doris alikata tamaa kidogo. Alikuwa mwerevu sana, lakini bado hakuweza kumshinda bibi yake mkubwa.

"Hiyo inamaanisha kuwa wazee wana uwezo kuliko watoto." Jennifer aliweka kipande kwa urahisi.

Kendrick na Alissa wakaja nyuma ya Doris. Kendrick aliweka moja chini kabla Doris hajakaribia kuchukua vipande, "Iweke hapa au bibi yako mkubwa atashinda."

Doris aliwageukia Kendrick na Alissa baada ya kusikia sauti aliyoifahamu, “Baba, Mama….”

Kisha, akaushika mguu wa Kendrick, “Nilikukumbuka sana. Hujakaa hapa kwa miaka mingi.”

“Baba pia anakukumbuka sana. Lakini kuna mambo muhimu sana katika kazi. Kwa hiyo, samahani. Sitakuwa hivi tena.” Kendrick alichuchumaa na kumbusu uso wa Doris ili kumfariji.

"Doris, umemwita nini?" Jennifer aliuliza akidhani hajasikia vizuri.
"Bibi mkubwa, nilimwita baba." Doris alisema kwa sauti safi na ya kiburi.

“Ulimwita Kendrick Daddy?” Jennifer alikunja uso na kumrekebisha Doris, “Doris, unamkosea Baba yako. Ni mjomba Kendrick.”

"Bibi, Doris hakunikosea." Kendrick alimshika mabega Doris, “Mimi ni Baba yake.”

Jennifer alichanganyikiwa zaidi na kumtazama Alissa, “Alissa, nini kinaendelea? Kwani Kendrick hajaoa?”

"Bibi, yule aliyemwoa ni mimi." Alissa alichukua hatua ya kumsogelea Kendrick na kumshika mkono.

Walisimama pamoja na kuonekana kama familia ya watu watatu.

Jennifer aliwatazama kwa butwaa kwa muda mrefu kabla ya kusema polepole, “Nyinyi watu … mmeoana?”

“Ndiyo. Bibi, una furaha?" Sauti ya Kendrick ilikuwa kubwa na safi kiasi cha kumsikia Jennifer.

Jennifer bado alikuwa amechanganyikiwa kidogo huku akiwatazama wakiwa wameshikana mikono na macho ya Doris yaliyokuwa yamemetameta.

“Nipe muda.” Jennifer alitulia na kufikiria kwa muda, “Kendrick alikuoa baada ya kuachana naye?”

Mara ya mwisho Jennifer kumuona Kendrick, Kendrick na Alissa hawakuwa na uhusiano wowote kati yao. Lakini wakati huu walipokutana, Jennifer alipata habari hizo za kushtua. Ilikuwa ni ghafla kwamba alishikwa na tahadhari.

"Bibi, samahani nilikudanganya." Alissa alijitokeza na kuketi kando ya Jennifer, “Hatukuachana. Aliyeolewa naye ni mimi. Hatukuweka hadharani kwa sababu yangu.”

"Kwa hiyo hata ulimficha bibi yako mwenyewe?" ijapokuwa Jennifer alisema hana hasira, bado alihisi kuudhika kidogo, “Unashindwaje kuniambia jambo kubwa kuhusu ndoa yako? Pia nina wasiwasi kuwa wewe ni mpweke sana peke yako. Ndio sababu mimi hupanga miadi ya uchumba kwako kila wakati. Si ajabu umekuwa ukipata kila aina ya visingizio vya kukataa.”

"Bibi, nilikosea." Alissa alikuwa mtiifu kama mtoto wa shule.

Kendrick pia alisema, “Bibi, ninawajibika pia. Ikiwa unataka kumlaumu mtu, tafadhali nilaumu mimi.”

"Kuna maana gani ya kuwalaumu nyinyi katika hali kama hizi?" Jennifer alipumua kidogo na kuushika mkono wa Alissa na kusema kwa uzito, “Kwa kweli, nilikuwa na matumaini kuhusu ndoa yako. Lakini Kendrick alikuwa ametangaza kuwa alikuwa ameoa wakati huo. Kwa hivyo, sikuthubutu kufikiria juu yake tena na nikapata majuto. Sasa kwa kuwa nyinyi mko pamoja, kwa kawaida nina furaha na sina majuto tena. Lakini lazima uwe na furaha maisha yako yote, la sivyo sitakusamehe kwa kunidanganya.”

Jennifer hatimaye "aliwatishia". Hili pia lilikuwa hamu yake kuu.

“Bibi, usijali. Tutakuwa sawa.” Kendrick alimhakikishia.

“Safi.” Jennifer alitabasamu kwa furaha na kumtazama Kendrick, “Kendrick, kumbuka ulichoniambia leo. Ukimdhulumu Alissa, nitafanya kila niwezalo kupata haki yake.”

"Bibi, sitakupa nafasi hiyo." Kendrick alijiamini na kumtazama Alissa, “Kama Alissa ndiye anayenionea, basi Bibi atanifanyia mimi pia?”

Sura ya 67

Jennifer alimtazama Alissa pembeni yake, huku Alissa akimtazama Kendrick kwa mshangao, “Nakuonea? nitakuoneaje?" Aliuliza maswali mawili kwa kuchanganyikiwa.

Je, Kendrick, mtu mwenye nguvu, angewezaje kusema maneno kama haya?

"Utajua baadaye." Kendrick hakujilaza na kuweka tabasamu ambalo lilimfanya Alissa kuwa mpole.

"Kwa nini huwezi kuniambia sasa?" Alissa aliuliza kwa udadisi.

“Naweza kukuambia. Lakini tunapaswa kusema kwa faragha." Kendrick alimkonyeza Alissa na kumshtua.

Alissa alikuwa na aibu na haya, akijaribu kujiweka poa.

Jennifer alijisikia mcheshi alipotazama jinsi walivyopatana, “Sawa. Nakuahidi. Ikiwa ni kosa la Alissa, nitamfundisha somo zuri kwako.”

Pamoja na Jennifer kumuunga mkono, Kendrick alijiamini zaidi.

“Umeolewa kwa muda gani?” akifikiria kuhusu ndoa yao, Jennifer bado alihisi kuwa ni ndoto.

“Si muda mrefu hivyo.” Alissa alikwepa jambo hilo muhimu na aliogopa kidogo kusema ukweli.

"Miaka mitatu." Kendrick alijibu wazi. Lakini alichosema kilimfanya Jennifer kukunja uso.

Alinyoosha mkono na kuupapasa mkono wa Alissa, “Wewe! Miaka mitatu imepita na unaniambia sasa hivi? Ni nini kinaendelea na nyinyi wawili?"

Alissa alibana midomo na hakuthubutu kujibu huku Kendrick akisema, “Bibi, ingawa mimi na Alissa tulipata cheti cha ndoa miaka mitatu iliyopita, tuliishi sehemu mbili tofauti. Isitoshe, tulioana kwanza kabla ya kupendana. Lazima tuwe na uhakika wa hisia zetu za kweli kabla ya kukuambia."

Ikiwa nyinyi hamjapendana, je, ndoa ingekuwa batili?” Jennifer hakukubaliana nao, “Kufunga ndoa kabla ya kupendana ni kutowajibika kwa ndoa, na kwenu pia. Ingawa Bibi anataka muwe pamoja, kwa hakika si kwa namna hiyo kutowajibika kwenu wenyewe."

“Bibi, tunajua tulikosea. Kwa bahati nzuri, tuna mwisho mwema sasa, sivyo?” Alissa alijua kuwa Jennifer alikuwa na hasira sana wakati huu.

Jennifer alikuwa serious na hakujibu.

“Bibi, usikasirike. Si vizuri kwa afya yako kuwa na hasira.” Alissa alimpa mkono Jennifer kwa urahisi, “Tulifunga ndoa baada ya kufikiria kwa uzito. Hatukuwa na hisia kwa kila mmoja.”

Alissa aliweza kusema uwongo mtupu. Hakuweza kumwambia Jennifer sababu halisi, ambayo ingemkasirisha Jennifer na kurudia ugonjwa wake wa zamani.

“Bibi, tulikuwa hatuelewani zamani. Kwa hiyo, tulitengana kwa miaka mitatu.” Kendrick alichukua hatua ya kuchukua jukumu hilo, “Kama mwanaume, lilikuwa kosa langu kumfanya Alissa ateseke. Lakini sasa kwa kuwa kutoelewana kumetatuliwa, nitatumia muda wangu kumlipia wakati ujao. Natumai bibi anaweza kunipa nafasi.”

Jennifer alijua kuwa Kendrick alikuwa mkweli. Angeweza kutambua kutoka kwa macho yake na baadhi ya maneno madogo-madogo kwamba alimpenda Alissa sana.

Zaidi ya hayo, aliamini kuwa Kendrick alikuwa mtu wa kuwajibika sana.

“Sawa, nitakupa nafasi. Usifanye hivi tena. Bibi anatumai kwamba nyinyi watu mnaweza kuwa na furaha milele.” Jennifer alipumua, “Usiwe kama mimi na babu yako, ambaye hatimaye aliaga dunia kwanza.”

"Tutafanya." Walisema kwa pamoja.

“Nimefarijika kukupata wewe.” Jennifer alitaka Kendrick awe mume wa Alissa. Hata hivyo, hakutarajia kwamba alikuwa ameolewa. Ilikuwa ni jambo jema kwamba hatimaye Kendrick akawa mume wa Alissa kimakosa.

Jennifer alipokuwa akisema hivyo, macho yake yalikuwa yamelowa machozi.

“Bibi, nadhani huna hasira, sivyo? Tumekubali kosa letu. Kwa nini unalia?" Kichwa cha Alissa kilikuwa karibu na cha Jennifer na alihisi kufadhaika.

"Nina furaha sana." Jennifer alinyoosha mkono na kumpapasa Alissa usoni kwa upole, “Una mume mzuri kama Kendrick. Naweza kumwambia babu yako baada ya kufa kwangu.”

“Bibi…” Alissa alilia.

Babu zake walimpenda zaidi katika ulimwengu huu. Babu yake alifariki. Sasa, bibi alikuwa na afya mbaya. Alissa aliogopa sana kwamba siku moja nyanya yake, ambaye alimpenda sana, pia ... Kama ni hivyo, hangekuwa na hisia tena kwa familia hii.

Kendrick aliona kingo za macho yao kuwa mekundu na wote walionekana kuwa na huzuni kana kwamba wangeachana milele.

Alimsukuma Doris taratibu mbele yake huku akimpa ishara ya kuwafariji.

"Bibi mkubwa, Mama, ni aibu kwamba unalia katika umri wako." Maneno ya kitoto ya Doris yalikuwa ya kufurahisha haswa.

Kwa hakika, Jennifer na Alissa mara moja wakageuza machozi kuwa tabasamu. Alissa alinyoosha mkono kumkandamiza Doris mashavu laini.
Jennifer alitulia, “Mimi pia nimechoka. Ningependa kwenda kulala sasa.”

“Basi nitakusaidia kurudi chumbani kwako.” Alissa alimsaidia Jennifer kunyanyuka kwenye sofa.

“Nitakusaidia pia.” Doris akasimama upande wa pili wa Jennifer na kumshika mkono Jennifer.

Ingawa alikuwa mdogo sana na hakusaidia sana, alisifiwa kwa uchaji wake wa kimwana.

Alissa alipomsaidia Jennifer na kumpita Kendrick, alimpa ishara kwa macho aache kusimama na kukaa kwa muda.

"Usiku mwema, bibi." Kendrick alisema.
Alitazama migongo yao kwa muda kabla ya kukaa kwenye sofa moja.

Punde, Alex na Marry walifika nyumbani na kumuona Kendrick akiwa amekaa peke yake sebuleni. Walishangaa kwamba Kendrick alikuwa amechagua kukaa kwenye jumba la familia yao.

“Kendrick, mbona uko peke yako hapa? Alissa yuko wapi?" Alex hakuthubutu kumpuuza akamwendea kwa haraka.

"Alimsaidia bibi kwenda chumbani kwake kupumzika." Kendrick aliketi kwa uzuri na kwa kawaida, kana kwamba alikuwa nyumbani kwake, na hakuwa na wasiwasi hata kidogo.

“Naona.” Alex alikaa kwenye sofa na kugundua kuwa hakuna maji mbele ya Kendrick, achilia mbali chai.

Marry pia aliiona na akaharakisha kusema, “Nitapika chai.”

“Usijisumbue, Mama. Sipendi kunywa chai jioni." Kendrick alikuwa ametulia kiasi kwamba alikuwa kama bwana wa familia kuliko wanandoa wenye wasiwasi na hofu.

"Basi ungependa kunywa nini?" Marry aliuliza.

"Maji tu." Kendrick alisema kikawaida, sio kwamba lazima anywe.

"Kisha nitapata glasi mpya." Marry alizingatia maelezo. Baada ya yote, wote walikuwa na vikombe vyao vya kipekee. Mtu kama Kendrick hawezi kamwe kutumia kikombe ambacho mtu mwingine ametumia.

"Asante." Kendrick alikuwa na adabu na kujitenga.

"Unakaribishwa." Marry kisha akageuka kwenda jikoni, akiwa ametulia kidogo.

Alex alikaa pale huku mikono yake ikiwa imepiga magoti, vidole vyake vikisogea, “Kendrick, kwani umekuja hapa? Jisaidie tu. Hii ni nyumba yako. Unaweza kutuambia chochote unachohitaji.”

"Asante." Miguu mirefu ya Kendrick ilipishana, “Mahali popote alipo Alissa panaweza kuwa nyumbani kwangu.”

Sura ya 68
Waliweza kujua alichokisema Kendrick kwa Alissa kilikuwa na maana kubwa kwake.

Mahali popote alipokuwa Alissa pangeweza kuwa nyumbani kwake. Kinyume chake, mahali pasipo yeye hapakuwa nyumbani kwake.

Ikiwa Alissa aliacha familia ya Maziku au hakukubaliwa na familia ya Maziku, basi Kendrick kwa kawaida hangechukua familia ya Maziku kama nyumba yake.

Alex na Marry waliheshimiwa naye tu kwa sababu walikuwa wazazi wa Alissa. Ikiwa hawakuwa wazazi wa Alissa, wangekuwa wageni kwake.

Kwa kawaida walielewa Kendrick alimaanisha nini na walijua hili vizuri.

“Unachosema ni kweli.” Alex hakuwa na chaguo ila kuinamia ukweli.

Binti yao sasa alikuwa mwanamke mwenye nguvu. Hawakuweza kumkosea kwa urahisi, au familia ya Maziku ingekuwa na wakati mbaya.

“Nyie ni wazazi wa Alissa. Anawaheshimu, na ninawaheshimu kwa asili. Ikiwa yeyote katika familia hii atamfanya ateseke, sitakaa na kutazama tu." Kendrick alisema kwa kumaanisha, akimrejelea Melissa ambaye alikuwa na kinyongo dhidi ya Alissa, "Lakini kwa kuwa Alissa ameolewa nami, hataishi katika nyumba ya familia ya Maziku kwa muda mrefu na kwa kawaida ataenda kwa familia ya Mayala huko Geita pamoja nami."

“Kwa Mayala?” Alex alishangaa kisha akacheka, “Umesema kweli. Mwanamke anapaswa kuridhika na mwanamume aliyeolewa naye. Alissa anaweza kukutunza vizuri akiwa kando yako.”

"Ni mimi ninayeweza kumtunza vizuri." Ikiwa angekaa karibu naye, angeweza kumlinda.

Alex alikunja uso. Kendrick alimweka Alissa katika nafasi ya kwanza katika kila sentensi. Aliweza kuona jinsi Kendrick alivyomthamini Alissa.

Tangu mwanzo Marry alikuwa amepanga mambo mengi ya kumuacha Alissa aolewe, ikabidi Alissa aiache familia ya akina Maziku haraka iwezekanavyo.

Lakini sasa, wakati Alissa angeenda Geits na Kendrick, Alex alisita kidogo kumruhusu kuondoka.

Alikuwa na wasiwasi juu ya ndoa hii.

Kendrick alioana na Alissa na familia ya Maziku na familia ya Mayala walikuwa na uhusiano wa ndoa. Ingawa familia ya Maziku ilionekana kuwa maarufu sasa, Alex alijua wazi jinsi Alissa alivyowachukia familia ya Maziku na wao. Aliogopa kwamba mara baada ya Alissa kuondoka familia ya Maziku, hatarudi tena.

Kisha familia ya Maziku na familia ya Mayala hawangekuwa karibu na bado wangekuwa wa ajabu kama walivyokuwa.

Isitoshe, Alissa alikuwa mke wa Kendrick. Iwapo walitaka kuwa na ushirikiano wowote na Nyanza Group ya familia ya Mayala… Alex aliogopa kwamba haingekuwa laini. Kwani Alissa asingewasaidia.

Alikuwa amewekeza katika miradi kadhaa. Sasa, uchumi pia ulikuwa katika hali duni. Ikiwa angeendelea hivi, ingekuwa ngumu kwa kampuni yake kuishi.

Ikiwa Kendrick angeweza kusaidia hilo, ingekuwa tofauti.
Lakini, Kendrick alimthamini Alissa, akisema kwamba alimsikiliza Alissa kwa kila kitu.
Hii ilimfanya Alex ashindwe kuomba msaada.

Marry ambaye alikuwa ameenda jikoni kuchukua glasi, akarudi sebuleni, akammiminia Kendrick glasi ya maji, akaiweka mbele yake, kisha akaketi karibu na Alex.

"Kendrick, kama wazazi, tunafurahi sana kwamba unamthamini Alissa. Kumpenda mkeo ni jukumu la mwanaume. Lakini utamharibu ikiwa utaendelea kufanya hivi. Unaweza kufanya nini katika siku zijazo?" Alex alionekana kuonyesha upendeleo kwa Kendrick.

"Ndio, familia ya Mayala ni familia ya zamani na inayojulikana sana. Ni bora kwake kuwa na tabia. Ikiwa atavunja sheria, vyombo vya habari vinaweza kufanya jambo kubwa kutoka kwake. Marry aliunga mkono.

“Usijali. Ikiwa ataharibiwa na hakuna mtu anayeweza kustahimili hasira yake mbaya, hataweza kuniacha." Macho meusi ya Kendrick yalijawa na mapenzi kwa Alissa.

Alex na Marry wote walikuwa na woga na kutokwa na jasho baridi kwenye vipaji vya nyuso zao, “Hilo ni wazo la riwaya kabisa. Lakini inasikika vizuri. ”…

Walilazimisha tabasamu.
“Unazungumzia nini?” Alissa aliyekuwa amemsaidia Jennifer kitandani aliingia sebuleni na kusikia hivyo.

Kendrick akamtazama Doris aliyekuwa amemshika Alissa mkono. Alimpa ishara Alissa amruhusu Doris apande ghorofani kwanza. Kuna baadhi ya mambo hawakuweza kuyazungumza mbele ya Doris.

Alissa aliinama chini na kumwambia Doris, “Baby, nenda ghorofani kwanza umsaidie mama kuniandalia nguo zangu za kulalia. Subiri mama na baba, sawa?"

“Sawa.” Doris alikuwa mwenye busara na mzuri sana.

Alijua kwamba watu wazima siku zote waliwaepuka watoto wanapozungumza. Kwa hiyo, alikuwa mtiifu.

Baada ya Doris kupanda ghorofani, Alissa alitembea na kumuuliza Kendrick kilichotokea.

"Nilisema kwamba ikiwa umeharibiwa na hakuna mtu anayeweza kuvumilia hasira yako mbaya, hautaweza kuniacha." Kendrick alirudia alichokisema sasa hivi.

“Wazo ni zuri. Lakini nina nia thabiti na sitaharibiwa na wewe kirahisi.” Alissa alijiamini.

"Basi tujaribu."

“Hakika.”

"Lakini ni wakati wa kupumzika sasa." Kendrick aliinua mkono wake, shati jeupe lenye urefu wa ziada kwenye pingu ya suti yake nyeusi iliyoagizwa nje ya nchi, na saa ya kifahari ya almasi iking'aa kwa mwanga wa kioo, "Wilaga" Kendrick alisema Kisukuma akimaanisha 'usiku mwema'.

"Basi usiku mwema." Alipoona Kendrick anaenda kupumzika, Alex alihisi faraja na kumwambia Alissa, “Alissa, mtunze Kendrick vizuri. Ndiyo kwanza anaishi hapa.”

"Sawa." Alissa akaitikia kwa kichwa.

Kendrick akanyanyuka na kuinyoosha suti yake.

Alikuwa mrefu na mzuri katika suti yake.

“Unaangalia nini? Twende zetu.” Alipoona Alissa hasogei, Kendrick akahimiza.

Alissa kisha akarudi kwenye fahamu zake na kwenda mbele.

Kendrick aliwaitikia kwa upole Alex na Marry. Kisha Bwana na Bibi Maziku nao wakasimama kuwaona wakiondoka.

Walipofika juu na kufika kwenye kona ya ngazi, Kendrick alinyoosha mkono na kumshika mkono Alissa. Alissa alimtazama na wakatembea kimya hadi chumbani.

Alissa alinyoosha mkono na kufungua mlango. Kendrick aliingia naye.

Doris alikuwa ameweka nguo za kulalia za Alissa kitandani.
Alipowaona wazazi wake wakiingia, Doris alikimbilia kwao, “Je, baba haondoki leo?”

“Ndiyo. Na Doris anataka baba abaki hapa?" Kendrick alimnyanyua binti yake na kukaa kwenye sofa.

“Hakika. Nina furaha hasa leo. "Doris alikuwa mzuri.

“Kwa nini?” Kendrick aliuliza.

“Watoto wengine wote wanalala na wazazi wao. Leo, naweza kulala na wazazi wangu pia.” Haya ndiyo yalikuwa matakwa ya Doris ya muda mrefu. Leo, hatimaye ingekuwa kweli.

"Basi fanya haraka kuoga." Alissa alimvuta Doris taratibu mapajani mwa Kendrick.

"Sawa. Nitaoga vizuri.” Doris kisha akapelekwa bafuni na Alissa.

Alissa alitoka baada ya kumuandalia maji ya kuoga Doris. Kendrick alikuwa akiangalia mtindo wa urembo wa chumba chake cha kulala, “Hii ni mara ya kwanza kuwa katika chumba cha kulala cha mwanamke.”

"Hujawahi kuingia kwenye chumba cha dada yako?" Alissa alisitasita kidogo.

"Hapana." Kendrick akajibu, “Mbali na hilo, kwa nini niingie chumbani kwake?”

“Wewe si kaka na dada? Ni kawaida kwenda kwenye vyumba vya kulala vya kila mmoja.”

"Kuna jambo moja nahitaji kukuambia."

“Ni nini?”

Sura ya 169

Alissa alimkazia macho Kendrick. Je, alikuwa hajamwambia mambo mangapi? Je, alikuwa na siri ngapi au vitu vingapi asivyovijua?

Alijiona kuwa muwazi mbele yake bila usiri, ilhali hakuweza kumwona na hakumuelewa hata kidogo.

"Kabula sio dada yangu." Hiki ndicho Kendrick alitaka kumwambia.

Alissa alitoa macho yake mazuri na akastaajabu kwa muda…

“Yeye si dada yako? Vipi asiwe dada yako? Hata kama una baba mmoja lakini mama tofauti, yeye pia ni dada yako." Alissa alikunja uso na kutafakari.

Alikuwa amemwona Kabula mara mbili. Lakini hakujua jambo hili.

Kwanino Kendrick hakuwa na shauku na familia yake isipokuwa kaka yake? Yeye na Francis hata walipambans 'tit for tat' na hakuna aliyekuwa tayari kukubali kushindwa.

Labda hakuona tofauti yoyote katika mtazamo wa Kendrick kuelekea Kabula. Kwa hiyo, yeye hakufikiria.

“Ni binti wa Salome tu, lakini si wa Baba yangu, maana yake hana uhusiano na mimi. Sisi ni kaka na dada kwa jina tu." Kendrick alimwambia Alissa sababu.

"Yeye si binti wa baba?" Alissa alionekana kutokuamini sana.

“Ndiyo. Aliletwa kwa familia ya Mayala baada ya Salome na Baba kuoana. Kwa hivyo, jina lake la ukoo ni Ndallo. Ninawezaje kuingia kwenye chumba chake?"

Akimaanisha hawakuwa na uhusiano wa damu na alipaswa kuwa na umbali naye.

“Vipi kuhusu Stefano? Anapaswa kuwa mtoto wa baba, sawa?" Alissa alimtazama kama mtoto mwenye hamu ya kutaka kujua.

Kendrick alitazama chini macho yake safi, "Stefano ni mtoto wa Salome na Baba."

"Nimefikiria Kabula ana jina la mwisho la mama yake na Stefano ana jina la baba yake. Kwa hiyo, wewe huna uhusiano na Kabula.” Alissa alimulika ghafla, “Si ajabu yuko hivyo. Yote yana maana.”

“Ana shida gani? Nini kinaleta maana?” ikawa zamu ya Kendrick kuuliza swali.

Alissa alitabasamu kwa fahari, “Kwa hiyo kuna jambo hujui?”

“Mimi si Mungu. Mimi ni mtu wa kawaida tu. Hilo si jambo pekee ambalo sijui.” Kendrick alivuka miguu yake mirefu kidogo na kuhamia kwenye nafasi nzuri zaidi, “Usinifikirie kuwa muweza wa yote. Nina nyama na damu pamoja na hisia na tamaa.”

Alimkazia macho usoni huku akisema. Macho yake laini yakatangatanga juu ya uso wake, pua yake, na kusimamishwa katika midomo yake ya pink.

Aliona haya kidogo kwa macho yake ya shauku, "Mbona unanitazama hivyo?"

"Nasubiri unijibu swali langu." Alikuwa akimngoja kwa subira.

"Ninahisi kuwa Kabula hanipendi na ana hasira kidogo kwangu. Lakini yeye anakujali hasa. Mara ya mwisho tulipoenda kukaa kwa familia ya Mayala kwa usiku mmoja, alikuwa na furaha sana wakati huo. Pia alionekana kuumia ulipokuwa baridi.” Alissa alikumbuka nyakati mbili alizomwona Kabula, na maelezo yalipita akilini mwake.

"Ndio hivyo?" Kendrick hakujali.

“Je, hukuona?” Alissa alionekana kuwa serious.

"Anaishi Geita na mimi ninaishi hapa Mwanza muda mwingi. Tunaonana tu kwenye chakula cha jioni cha familia mara moja moja. Unafikiri nitazingatia kila mtu?" Kendrick alijibu kwa upole.

Ilisemekana kuwa Kendrick hakuwa na moyo. Inaweza kuonekana kutokana na kile alichosema sasa hivi kwamba kwa kweli hakuwa na moyo.

Hata kama Kabula hakuwa dada yake halisi na alikuwa dada yake wa kambo tu, alipaswa kuwa na adabu juu ya uso. Lakini bado alikuwa baridi sana.

Lakini, Kabula alimjali sana. Ni wazi alikuwa na wasiwasi juu ya kila kitu kumhusu. Angekuwa na furaha kwa ajili yake na kuwa na huzuni kwa ajili yake. Lakini hakuweza kupata athari ya joto kutoka kwake.

"Kweli yeye ni dada yangu wa kambo juu juu. Lakini kwa kweli, yeye hana uhusiano na mimi na hana tofauti na wanawake wengine kwangu. Lazima niwe mbali na kumfanya aelewe wazi kwamba hatutakaribia." Kendrick aliona mawazo yake na kueleza.

"Bado sijauliza na umenijibu." Alissa alikasirishwa kuwa bado alikuwa muwazi mbele yake.

"Ninaogopa kuwa utachoka baada ya kuzungumza zaidi." Kendrick alishika chupa ya maji na kumimina glasi ya maji, akamkabidhi, "Kunywa maji ili ujirudishe."

Alissa alichukua maji na kumkazia macho, “Kwa hiyo sina budi kumshukuru Bwana Kendrick kwa mawazo yake.”

"Karibu." Kendrick hakuweza kujizuia alitabasamu kwa upole.

Sura ya 170

Alissa alimtoa Doris bafuni. Akiwa amevalia vazi la kulalia la katuni la pinki, nywele zake ndefu zikiwa zimelowa, Doris alikuwa mrembo sana huku uso wake ukiwa na rangi nyekundu.

Alissa alichukua taulo kumsaidia Doris kukausha nywele zake zilizolowa maji. Kendrick aliuliza, “Kikaushia nywele kiko wapi?”

"Katika droo ya chini ya kifua cha droo." Alissa alisema.

Kendrick alienda kwenye droo, akachuchumaa, akafungua droo na kuchukua dryer ya nywele.

Kendrick akasogea mpaka kwenye kitanda kikubwa, kisha Alissa akaweka taulo na kukifikia kifaa cha kukaushia nywele, lakini akakiweka kitandani.
“Nenda kuoga na nitamkausha Doris nywele zake.” Kendrick alisema huku akifikia kuvua suti yake.

Baada ya kusikia hivyo, Doris alipiga makofi kwa furaha. "Baba ni mzuri!"

Kendrick alinyoosha mkono na kugusa sehemu ya juu ya nywele za Doris, huku akitabasamu kuharibika.

Alissa alimtazama Kendrick kwa mashaka, “Una uhakika?”

"Bila shaka." Kendrick akavua suti yake na kumkabidhi. "Ikatae kwa ajili yangu."

"Je, unaweza kukausha nywele?" Alissa akaichukua ile suti huku akiuliza kwa wasiwasi.

Machoni mwa Alissa, Bwana Mayala alionekana kujua mambo ya kidunia. Je, kweli angeweza kujua jinsi ya kutumia dryer?

"Mimi sio mjinga, sawa?" Kendrick kisha akafungua vifungo vya shati lake na kukunja mikono yake. “Nenda ukaoge.”

"Mama, unapaswa kumwamini baba." Doris naye akawa upande wa Kendrick. “Sio mapenzi ya kweli kwako kumtilia shaka Baba kiasi hicho. Baba atakuwa na huzuni."

Alissa aliinua mabega yake na kumkumbusha Kendrick kabla hajaondoka, “Kama una maswali yoyote, nijulishe.

Kendrick alitabasamu vibaya, kisha akainama mbele na kumnong’oneza sikioni, “Utakuwa uchi wakati unaoga. Je, utatoka tu nikikupigia simu?”

"Kendrick, unawezaje kuwa mpotofu hivyo?" Alissa alinyoosha mkono na kumpiga ngumi begani.

Kendrick alikuwa sawa, lakini alikuwa akiumiza mikono yake kwa sababu ya misuli yake migumu. Alikuwa akitafuta shida tu alipompiga.

Alissa alipeleka suti yake kwenye chumba cha nguo kisha akaoga.

Kendrick alimkalisha Doris pembeni ya kitanda laini huku akisimama na kupeperusha nywele zake zilizolowa.

Aliinua kifaa cha kukaushia nywele na kupitisha vidole vyake kwenye nywele ndefu za Doris kwa mkono wake mwingine. Aligusa nywele zake kwa upole na kwa hila, kwa kuogopa kuvuta nywele za Doris na kumuumiza.

"Baby, ilikuumiza?" Kendrick alimuuliza.

Doris alikuwa amekaa vizuri. "Hapana, baba ni mzuri."

Tabasamu la upole likainua pembe za mdomo wa Kendrick. Aliridhika kusifiwa na bintiye.

"Doris, baba anaweza kukuuliza kitu?" Kendrick alibembeleza nywele zake ndefu kwa upole.

"Endelea."

“Unataka kwenda kwa baba pamoja na baba?”

"Nyumba ya baba iko wapi?"

"Si mbali."

"Mama ataenda nasi?"

"Bado sijamuuliza mama, lakini kama Doris anataka kwenda, basi fanya kazi na baba kumshawishi mama, ili sisi watatu turudi kwangu pamoja. Hapo ndipo nyumbani kwetu halisi.” Kendrick alikuwa akijaribu kumuweka Doris upande wake.

“Nyumbani kwetu?” Doris alikunja uso kidogo. "Nyumbani na mama, mimi na Daddy?"

“Ndiyo. Ikiwa tunaishi pamoja, hatutawahi kutengana." Kendrick aliendelea, “Hii ni familia yetu ndogo, na babu na babu yako wanapokuwa hapa, sisi ni familia kubwa. Bado hujaonana na babu na babu yako, sawa?”

"Je, bibi na babu watanipenda?"

"Bila shaka, wewe ni mrembo sana."

"Vema, Doris huenda popote mama na baba wanakwenda."

“Ndio mpango huo.”

“Ndiyo.”

Baada ya Kendrick kukausha nywele za Doris, Alissa alitoka bafuni na kumkuta Doris akiwa amejilaza katikati ya kitanda kikubwa na Kendrick akimvutia mto Doris.

Alissa akaja, "Unataka kuoga?"

“Una nguo za kulalia?” Kendrick hakuleta chochote. Hakuweza kununua nguo yoyote usiku huo.

"Nilijiandaa tu kwa taulo na mswaki, lakini hakuna pajama." Alissa hakuwahi kufikiria kuwa Kendrick angejinyenyekeza kwa familia ya Maziku hata siku moja.

Kendrick alioga kila siku, sio tu kwa sababu alikuwa akizingatia usafi, lakini pia kwa sababu inaweza kumsaidia kupumzika. Lakini leo, ilionekana hakuweza kuoga ...

Wakati huu, mlango uligongwa na wote wawili wakatazama mlango wa chumba cha kulala.

"Nitakwenda kuona." Alissa akaupita mlango. "Nani huyo?"

"Alissa, ni mimi." Alikuwa Marry.

Alissa aliufungua mlango, lakini ulikuwa mpana tu kama vile mtu angeweza kupita, “Kuna nini?”

“Hatujatayarisha nguo za kulalia kwa Kendrick. Nilinunua pajama mpya za baba yako. Ikiwa Kendrick yuko sawa nayo, basi ichukue." Mtazamo wa Marry kwa Alissa ulikuwa umebadilika sana.

Ilikuwa ni shukrani kwa utambulisho wake kuwa Bi. Mayala.

“Asante kwa ajili yake.” Alissa alisema huku akichukua nguo za kulalia ambazo hazijafunguliwa.

"Sisi ni familia. Usinichukulie kama mtu wa nje. ” Marry akatabasamu, “basi sitakusumbua. Pumzika."

Marry aliondoka, na Alissa akafunga mlango. Alichukua pajama kwa Kendrick. "Inaweza isikufae, lakini ni bora kuliko kutokuwa na kitu. Ichukue tu kwa usiku mmoja."

Kendrick alizitazama nguo za kulalia ambazo hazijafunguliwa na kuzifikia. "Ninazikubali kwa ajili ya Bi. Mayala," alisema.
Akaenda bafuni.

Alissa akalala huku akiwa amelala upande wa kushoto wa Doris.

"Mama atakusomea hadithi." Alissa alikifikia kitabu cha hadithi kitandani.

“Mama, naweza kumwomba baba anisomee leo?” Doris aliomba huku macho yake yakiwa wazi.

"Baba alienda kuoga, na baba alikuwa amechoka baada ya siku nyingi kazini." Alissa alijua kuwa Kendrick alikuja hapa kwa haraka siku hiyo.
“Wakati ujao, sawa?”

“Mama, baba anarudi kwake kesho. Wakati mwingine utakuja lini?" Doris alihisi kwamba baba alipaswa kutumia wakati pamoja naye kila siku.

Alissa hakuweza kujibu, na Doris akasema tena, "Mama, hamia kwa baba pamoja nami, basi tunaweza kukutana kila siku."

"Unataka kwenda kuishi na Baba?" Alissa hakutarajia ombi kama hilo kutoka kwa binti yake.

"Utakuwa uwongo nikikataa, lakini ikiwa hutaki kwenda nasi, nitakaa na mama na sitaenda popote." Doris aliweka wazo la mama yake mbele.

"Nipe muda wa kufikiria juu yake." Alissa alijua wakitengana Kendrick ataenda huku na huko kuwaona na atakuwa amechoka.

Alifikiria kuishi na Kendrick, lakini haikuwa sasa. Alitaka kwenda kwa familia ya Mayala mpaka wamzoee, ili ajiamini zaidi.

Sura ya 171

Alissa kisha akamsomea Doris hadithi kabla ya kulala. Doris alimshika mdoli wake mkubwa wa panda na kumsikiliza mama yake akisoma hadithi hiyo kimya kimya. Sauti nyororo na ya kupendeza ya mama yake ilimfanya Doris ahisi amani.

Hadi katikati ya stori, Kendrick alitoka bafuni huku akijifuta nywele zake zilizolowa huku akielekea kitandani.

Alissa alimtazama Kendrick. Alikuwa amevaa pajama zake za hariri za kijivu. Zilikuwa na kiasi kwake, kwani Kendrick alikuwa na urefu wa sentimeta kumi kuliko Alex, hivyo vifundo vya mikono na vifundo vya Kendrick vilikuwa wazi zaidi ndani ya vazi la kulalia na hilo lilimfanya Kendrick huyo mrefu na mwenye sura nzuri aonekane mcheshi kidogo.

Alissa alitaka kucheka, lakini hakuweza.

Kwa jinsi Alissa alivyomtazama, Kendrick akajua kuwa nguo za kulalia hazikumtosha.

"Cheka ukipenda." Kendrick akasogea upande wa pili wa kitanda.

Kusikia hivyo Alissa hakuzuia kicheko chake na kucheka mithili ya mtukutu.
Hata Doris ambaye alikuwa hajalala alikaa chini na kutabasamu.

Kendrick alifika na kugusa paji la uso la Doris. "Umemdhihaki baba pia?"

“Baba wewe ni kama mwizi mkubwa anayevaa nguo za watoto. Kwa kweli siwezi kujizuia.” Doris alimshtua Kendrick kwa mkono. "Lakini baba ndiye mwanaume mzuri zaidi machoni pangu."

"Msichana mwenye busara." Kendrick aligusa daraja la pua yake.

“Sawa, nenda kalale. Usichelewe kufika shuleni kesho asubuhi.” Alissa aliupapasa mto laini kumkumbusha Doris.

Doris akachukua kitabu cha hadithi kutoka kwa Alissa na kukiweka mkononi mwa Kendrick, “Baba utanisomea leo. Ni mama ambaye amekuwa akinisomea, lakini kwa kuwa upo hapa leo ni zamu yako.”

Alikodoa macho yake ya pande zote kwa Kendrick, akitumaini angekubali ombi lake.

“Baba amechoka.” Alissa alimkumbusha Doris kuwa mzuri.

Kendrick alikuwa na shughuli nyingi kiasi kwamba Alissa hakutaka bintiye amuongezee mzigo.

“Ina maana gani? Binti yangu anataka kunisikia nikisoma.” Kendrick alichukua kitabu cha hadithi kutoka kwa Doris na kusugua nywele zake kwa upendo.
“Baba atakusomea hadithi hiyo kila siku na kufidia wakati ambao sikukaa nawe hapo awali, sawa?”

“Kweli?” Doris alimtazama Kendrick kwa furaha.

Kendrick aliitikia kwa umakini. “Bila shaka ni kweli. Baba amewahi kukudanganya lini?”

Doris alitikisa kichwa bila kusita. “Hiyo ni nzuri sana! Baba ndiye bora zaidi."

Kuangalia uso wa furaha wa Doris, Alissa alihisi kutengwa.

"Baba ndiye bora, lakini mama sivyo? Una baba yako sasa na umsahau mama yako." Alissa alimtania Doris.

Doris alimkumbatia Alissa na kusema, “Mama ana nafasi pia katika moyo wangu.”

Mtoto mdogo mwenye busara alikuwa mzuri sana.

"Sawa, lala chini." Alissa alimweka Doris kwenye mto kisha akamlaza kitandani.

Kendrick alimshikia kitabu cha hadithi na kuendelea kusoma hadithi.

Labda Doris alisisimka sana usiku huo hivi kwamba alikesha hadi hadithi hiyo ilipomalizika.

“Una shida gani leo?” Alissa alimtazama Doris. “Hujambo?”

"Hapana, nadhani nimefurahi sana hadi nashindwa kulala." Doris alitazama huku na huko. “Mama, baba, mtalala hapa wote wawili? Lala na mimi.”

Alissa na Kendrick walitazamana kisha wakalala.

Doris alilala katikati, na mama yake akiwa upande wake wa kushoto na baba upande wake wa kulia, kama tu binti wa kifalme waliyemlinda katikati, akiwa salama na mwenye furaha.

Akaunyoosha mkono wake laini wa kushoto kuushika mkono wa mama yake, akaunyoosha mkono wake wa kulia kuushika wa baba yake.

Walikuwa familia ya watu watatu kwa wakati huu, wachangamfu sana na wa kupendeza.

Doris alisema, “Inapendeza kuwa na Mama na Baba pamoja nami.”

"Nitakuwa na wewe kila wakati." Kendrick alimuahidi Doris.

"Funga macho yako na ulale." Alissa alimpapasa kidogo ili alale.

Doris alifunga macho yake kwa utii, kope zake nene zilizopinda zikionekana kama mbawa ndogo.

Doris alishika mikono ya wazazi wake kwa nguvu na kulala chini ya kubembelezwa kwa upole na Alissa.

Baada ya bintiye kusinzia kwa upole, Alissa alijaribu kuurudisha mkono wake nyuma, lakini mtoto aliushikilia kwa nguvu sana hata asiuache hata akiwa usingizini.

“Baba, usiende…” Doris alikuwa akinong’ona ndotoni.

Kendrick alimpapasa mtoto kwa upole na kusema, “Baba hataondoka. Unaweza kuwa na uhakika. Mama na baba wako hapa pamoja.” Kisha Doris akalala tena na hakuzungumza usingizini.

Inaweza kuonekana kwamba mtoto alikuwa na hamu ya upendo wa baba. Alitumai mama na baba yake kuwa pamoja na kutamani kuwa na familia kamili.

Alissa aliutazama uso mzuri wa Doris uliolala, na moyo wake ukajawa na msisimko.
Alimhurumia mtoto huyo kwani alikuwa akipuuza hisia zake.

"Sawa, usijilaumu mwenyewe." Kendrick alimuona Alissa akishusha kope zake, macho yakiwa mekundu. “Ni silika kwamba watoto hutamani kupendwa na wazazi wao. Umekuwa ukifanya kazi kwa bidii kumtunza peke yako miaka hii, na umefanya kazi nzuri.

“Kwa hiyo, usilitie moyoni sana. Nikiwa hapa, nitakutunza vizuri. Ningemtunza na kumfanya asijisikie tena kuwa yeye ni mtoto asiye na baba.”

Kendrick alimsogelea na kumshika mkono wa kulia na kumtuliza.

Alissa alihisi joto la mkono wake wa moto likimfunga kwa nguvu, na kumpa nguvu na usalama.

Alissa akaitikia kwa kichwa. "Baada ya kukabidhi uchambuzi wa mradi wa FarmCom, mimi na Doris tutahamia kwako."

Hakuwa akimfanyia Doris tu, bali alikuwa akifanya kwa ajili yake na kwa Kendrick.

Kwa kuwa alikuwa ameamua kuwa naye, yeye, akiwa mke, anapaswa kumjali mume wake.

Ilikuwa tu kwamba alibadilisha mahali pa makazi, ili aweze kumuepusha Kendrick kuishi miji miwili kwa wakati mmoja na kuepusha uchovu wake wa kufanya kazi.

"Kwa kweli, ikiwa hutaki kuondoka hapa, nitaheshimu uamuzi wako." Kendrick hakutaka kumlazimisha. “Kwa vile huwezi kuja kwangu, nitakaa hapa na wewe, na nitaenda kazini na kurudi kila siku. Mimi ni mwanaume na ninapaswa kuwajibika zaidi.”

Alissa akatikisa kichwa na kumshika mkono. “Sikujilazimisha kufanya uamuzi huu, niko serious. Sisi ni familia. Tunapaswa kulinda nyumba yetu. Familia ya Maziku haijawahi kuwa familia yangu. Ni kwa sababu ya bibi kwamba ninakaa hapa.

“Bibi pia alisema tangu niolewe, nilipaswa kutunza familia yangu. Na ninapaswa kusawazisha kazi na familia."
 
USINIACHE 4:
Sura ya 172

"Bibi yuko sahihi, kwa hivyo nimeamua kuhama na Doris kuja kwako ili kuishi nawe na kutunza familia yetu vizuri."

Baada ya Alissa na bibi yake kuwa na mazungumzo ya kina, bibi alimuunga mkono sana kwenda kwa Kendrick.

Kendrick akaona ameamua na akafurahi sana. “Sawa, nitakusubiri.”

Baada ya maongezi Alissa na Kendrick walienda kulala, wakashikana mikono kumlinda Doris kati yao.

Usiku huo, familia ililala kwa utamu zaidi kuliko hapo awali.

Kendrick hakuamka saa 6,30 asubuhi kwenda kukimbia. Badala yake, alijilaza kitandani na kuwatazama Alissa na Doris wakiwa wamelala.

Bado walikuwa kwenye usingizi mzito. Kendrick hakuwasumbua. Aliachilia tu mikono yake na Alissa na kupiga nywele zake usoni mwake, akaziweka nyuma ya masikio yake kwa upole.

Vidole vya mikono yake vilimsisimua na akakunja nyusi zake, lakini hakufungua macho yake.

Chini ya mwanga hafifu, kope zake ndefu huweka vivuli kwenye ngozi yake nyeupe, kama picha, nzuri sana na inayogusa.
Kendrick aliwatazama kwa muda. Hadi saa moja ndipo aliinuka kirahisi.

Baada ya kuvaa, alitoka chumbani na kushuka chini.

Hakukuwa na mtu katika chumba cha kulia, kwa hiyo alitembea kuzunguka nyumba, akipumua hewa safi. Harufu safi ya nyasi na maua ilimburudisha sana.

Alizunguka kwa muda na kisha akarudi ndani. Wakati huo Alex na Marry nao wakashuka na kumuona Kendrick akiingia sebuleni.

"Kendrick, ulilala vizuri jana usiku?" Alex alikuwa na wasiwasi sana, akiogopa kwamba hakumtendea vizuri mgeni wake.

Kendrick hakuwa mgeni wa kawaida tu kwa familia ya Maziku. Kama mkwe, alikuwa mgeni wa heshima.

"Nzuri sana, asante." Kendrick alikuwa ametulia. "Ulikuwa ni usingizi wa kustarehesha na wa kufurahisha zaidi kuwahi kupata."

Akiwa na mkewe na bintiye…hakukuwa na usiku mzuri zaidi ya huu.

“Vipi kuhusu Alissa na Doris?” aliuliza Marry.

“Nilinyanyuka kwanza na kwenda kupunga hewa bustanini. Wanapaswa kuwa bado juu. Nitakwenda kuwaona.” Kendrick alitaka wapate usingizi zaidi.

“Ni wakati wa kifungua kinywa. Tutakusubiri kwenye chumba cha kulia chakula.” Alex alimkumbusha.

Kendrick aliitikia kwa kichwa na kwenda juu.

Ilikuwa saa moja na nusu, wakati ambao Alissa na Doris huwa wanaamka.

Kendrick alipanda ghorofani na kukuta wameamka. Doris alikuwa anavaa mwenyewe.

Alissa alioga kisha akabadilisha, Kendrick akampeleka Doris bafuni kuoga.

Baada ya Alissa na Doris kuwa tayari, walishuka kupata kifungua kinywa na Kendrick.

Kulikuwa na vyakula vya Kisukuma pia na vya kiswahili kwenye meza. Kwa sababu Marry hakujua tabia ya Kendrick ya kula, alikuwa ameandaa vyakula tofauti.

Wakati wa kifungua kinywa, Kendrick hakuzungumza kabisa, na alikuwa mzuri sana wakati wa kula. Kila mtu alijua kuwa alizaliwa kwa familia yenye heshima kwa njia yake ya kula. Heshima na utulivu bora vilionekana kuzaliwa pamoja naye.

Alex na Marry hawakuweza kujizuia kumtazama Kendrick, lakini hakuguswa na kitu chochote na wala hakuongea chochote tangu mwanzo hadi mwisho wa chakula.

Baada ya Kendrick kumaliza kula, alisogeza vyombo pembeni na kusema, “Nimemaliza. Kifungua kinywa ni kitamu. Asanteni sana.” Upole wake ulikuwa ishara ya umbali wake kutoka kwa familia ya Maziku.

“Asante pia.” Alex alitabasamu.

"Mimi pia." Doris akaweka kijiko chake chini na kuchukua kitambaa kufuta mdomo wake.

Kendrick akamshika mkono Doris na kusema, “Unafurahi kwamba Baba atakupeleka shuleni leo?”

“Ndiyo.” Doris alisisimka.

“Twende basi.” Kendrick akachukua begi dogo la pinki lililokuwa nyuma ya kiti na kumshika mkono Doris.

Alissa alishika mkono mwingine wa Doris, na Alex na Marry walitazama kwa muda wakati wote watatu wakiondoka.

Jennifer kisha akasema, “Alex, huthubutu hata kuongea na Kendrick karibu? Na Marry, hukusema lolote.” Sauti ya Jennifer ilijaa kejeli, jambo lililowatia aibu Alex na Marry.

"Kendrick ni mgeni katika Familia hii, kwa hivyo lazima tumtendee vizuri." Alex aliepuka aibu.

“Ndiyo. Hata ikibidi kugombana, hatuwezi kufanya hivyo mbele ya Kendrick. Haifai sana, sawa?” Marry alisema kwa tabasamu, "Kama mama mkwe, ninapaswa kuzingatia tabia yangu."

“Mnaogopa tu labda mmemkosea Kendrick. Hakika nimefarijika kumuacha Kendrick amtunze Alissa, hivyo nitaondoka wiki ijayo na sitarudi tena.” Jennifer alifanya uamuzi wake.

Kukaa kwake hapa kungemfanya Alissa kuwa na wasiwasi juu yake na kumsumbua mpango wake wa kumfuata Kendrick kwake. Alissa angefarijika tu ikiwa angeondoka na kupata huduma bora zaidi.

"Unakwenda wapi?" Alex aliuliza kwa mshangao.

"Kwa mwanangu Sindano, Arusha."

“Mama unafanya nini? Sindano hataweza kukuhudumia vizuri.” Alex alisema, “Kaa hapa, nami nitakutafutia wahudumu bora zaidi wa kulea wazee. Tunaweza kukuona kila wakati.”

"Hapana. Nataka kuishi kwa amani.” Jennifer alikataa, akila vyakula vyake kimya kimya. “Kabla sijaondoka, kuna mambo machache ninayohitaji kusema.”

Jenifer alifuta midomo na kuendelea.

“Alex, Marry, hamna sifa ya kuwa wazazi! Hamkutaka kuwa mwema kwa Alissa, na sasa mtu anapompenda na kumtunza vizuri, mnataka kuwa wema kwake. Lakini haihitajiki kwa sasa.”

“Mama, tunajua tumekosea. Tutamsaidia Alissa kuanzia sasa.” Alex alijuta sasa.

"Mama, hatujachelewa sana kufanya hivyo, sivyo?" Marry pia alijuta.

Jennifer alipumua tu, “Kuna faida gani kujaribu kumlipia? Hawezi kukuambia kuwa huo unaoitwa wema ulitokana na ukweli kwamba aliolewa na Kendrick? Alex, Marry, watu hawathamini chochote hadi wanapokipoteza… Kwa hivyo, msijutie mlichofanya.”

“Mama tufanye nini? Alissa anakusikiliza wewe tu.”

“Siwezi kukusaidia.”

Alex na Marry walipomtazama Jennifer akinyanyuka na kuondoka, walikuwa na hisia tofauti.
Hawakuwahi kufikiria kuwa Alissa angekuwa mke wa Kendrick, na hawakuwahi kufikiria kuwa msichana waliyeachana naye angesimama kwenye kilele cha maisha hata siku moja.

Lakini wao wangeweza tu kusimama chini ya mlima na kutazama juu yake juu.

Badiliko kama hilo liliwashtua sana na kuwafanya wakasirike.

Sura ya 173

Kendrick na Alissa walimpeleka Doris chekechea pamoja huku mwalimu akiwatumia taarifa.

"Ijumaa ijayo, tutafanya shughuli ya mzazi na mtoto kwa muhula huu. Tunatumaini wazazi wote wanaweza kutumia wakati huu wenye kufurahisha na wenye maana wa mzazi na mtoto pamoja na watoto wao.” Mwalimu aliwakumbusha wazazi.

“Nzuri.” Alissa alichukua taarifa.

Wakati huohuo, Matthew, ambaye alikuwa amemwacha Walter shuleni, alipokea notisi hiyo na kukunja nyusi zake.

Sio tu kwamba hakuwa na wakati, lakini mtoto hakuwa na mama wa kuongozana naye.

Walter alionekana kukasirika. Doris akavuta shati lake. "Una tatizo gani?"

“Sipendi shughuli za mzazi na mtoto. Kila mtoto mwingine ana baba na mama. Lakini mimi sina mama.” Walter alinong'ona.
Na kisha akainamisha kichwa chake, akionekana kupotea.

"Naelewa. Sikuwa napenda shughuli za mzazi na mtoto hapo awali, kwa sababu sikuwa na baba.” Doris alimuelewa Walter. “Lakini ina maana gani? Muhimu ni kwamba tufurahie.”

“Doris, mimi sina mama na wewe huna baba, kwa nini tusitengeneze familia halafu tuwe na mama na baba sawa?” Walter alimtazama Doris kwa maombi machoni pake, akitumaini angekubali.

"Walter, samahani, nina baba sasa." Doris alimnyooshea kidole Kendrick na kusema kwa majivuno, “Huyo ni Baba yangu. Yeye ni mzuri?"

Walter alimtambua Kendrick. Alikuwa mjomba mwenye barafu ambaye alimuona mara ya mwisho kwenye kisiwa cha Saa Nane.

"Si mzuri kama wangu," Walter alisema huku akiwa amekunja uso.

"Baba yangu ndiye mzuri zaidi machoni pangu." Doris alitoa mguno kidogo.

Walter alimvuta, akishangaa, “Yule mjomba akawa baba yako lini?”

“Ni hadithi ndefu. Wacha tuzungumze juu yake wakati tunatembea…”

Na Doris na Walter wakaingia kwenye darasa la chekechea wakiwa wameshikana mikono.

Mathew akatoa macho yake kwa Doris, akachukua taarifa na kumtazama Kendrick. "Bwana Mayala, pongezi kwako na Bi Alissa.

Jana usiku Mathew alipojua kuwa Kendrick na Alissa walikuwa mume na mke, alishtuka sana. Na wakati huo, kulikuwa na watu wengi ambao waliwapongeza kwamba hakupata nafasi ya kufanya kitu kizuri kwao.

“Asante, Bw. Matthew.” Kendrick alitabasamu kidogo.

Walipoondoka chekechea. Kendrick alimshusha Alissa ofisini kwake na kuondoka.
Kendrick aliingia kwenye Mercedes. Chale aliketi mbele yake.

“Timothy yuko wapi wakati huu?” Baada ya kuachana na Alissa, upole wa Kendrick ulitoweka, ukiacha ubaridi tu, na alikuwa amerudi kuwa mtu mwenye moyo baridi kama uvumi ulivyosema.

"Bado yuko Golden Hotel." Chale aliripoti.

"Ikiwa hatanijia, nitaenda kwake." Kendrick alikuja kibinafsi.

Timothy alithubutu kumpanga mke wake. Ulifika wakati wa yeye kulipa maovu yake.

Kendri akamwomba dereva ampeleke huko.

Walipofika Golden Hotel, Kendrick alipanga chumba kwenye ghorofa moja mkabala na ile ya Timothy na kwenda moja kwa moja.

Timothy alikuwa katika chumba namba 1605 na Chale akaenda na kugonga kengele ya mlango wake.

Alibonyeza kengele mara tatu, lakini hakuna aliyejibu mlango. Aliendelea kubonyeza mpaka laana ikatoka mle ndani, “Ni mpuuzi gani anajaribu kuharibu ndoto yangu asubuhi na mapema…”

Timothy alipofungua mlango na kumuona Chale amesimama pale, alikasirika zaidi. “Wewe ni nani jamani? Ondoka au nitakupiga!”

Chale aliporudi nyuma kwa heshima na Kendrick akatokea, Timothy alikutana na macho makali na kuhisi miguu yake ikiwa laini na kutetemeka.

“Bwana…Bwana Kendrick…” Timothy hakuweza hata kusema sentensi kamili, “Asubuhi…”

"Bwana Timothy, hutanikaribisha ndani?” Kendrick alikuwa amevalia shati jeupe na suti nyeusi, akionekana mzuri na mrefu na alikuwa tofauti kabisa na Timothy ambaye alikuwa amevalia fulana na bukta tu.

Walikuwa kama chaki na jibini.

"Bwana Kendrick, tafadhali subiri kidogo. Nitabadilisha nguo zangu." Timothy alivuta vazi lake ili kufunika mikwaruzo kwenye ngozi yake.

"Hakuna haja ya kubadilisha..." Kendrick aliweka mikono yake kwenye mifuko ya suruali. Alikuwa mkali sana hivi kwamba Timothy hakuweza kutoroka.

Timothy hakuthubutu kumuudhi Kendrick, akauachia mlango na kurudi chumbani.

Kendrick aliingia ndani, alipofika sebuleni hakukaa mara moja. Badala yake, alikunja uso.

Chale akapiga hatua na kuvuta mapazia na kusukuma dirisha la chumba ili kuruhusu hewa safi.

"Timothy, ni nani huyo? Ni asubuhi sana na hatujapata wakati mzuri…” Sauti kubwa ya kike ilisikika.

"Inaonekana ninaharibu wakati wako mzuri." Kendrick alifikiria kuhusu mikwaruzo kwenye uso wa Timothy.

Timothy hakuchukua hatua ya kumwomba Alissa msamaha tu, bali hata alipata mwanamke wa kukaa hotelini kwa usiku wenye furaha?

Mwanamke aliyetoka chumbani alikuwa amevalia nguo za kulalia za lace nyekundu, huku bega lake likiwa wazi nusu na nywele ndefu zikidondoka upande wa kushoto. Ilikuwa ya kuvutia sana… Lakini aliganda alipomwona Kendrick.

Mungu wangu, mtu huyu alikuwa mzuri sana! Ilikuwa mara chache sana kumuona mtu mwenye haiba kama hiyo duniani!

Yule mwanamke alimkazia macho moja kwa moja na kutaka kumwangukia.

“Usiwe mkorofi. Usimkazie macho bwana Kendrick.” Timothy alisema.

"Bwana Kendrick…” Mwanamke huyo alipouona uso mweupe wa Timothy kwa woga, alitambua kwamba mtu huyu alikuwa bora mara nyingi kuliko Timothy.

Ikiwa angeweza kuungana na mwanamume huyu, je, maisha yake yangebadilikaje?

Alizungusha nyonga na kwenda mbele bila viatu kwa Kendrick kisha akanyoosha mkono wake na kujaribu kuuweka begani kwa Kendrick.

Kutokana na hali hiyo, Kendrick aligeuka na kumkazia macho kwa kasi na kumfanya mwanamke huyo asipate chochote.

Mwanamke huyo alitetemeka kidogo, kisha akarudisha tabasamu, na kusema kwa ucheshi, “Bw. Kendrick, mbona una hasira sana asubuhi na mapema. Vipi kuhusu kupumzika…”

“Ondoka nje.” Kendrick alisema kwa upole, neno kwa neno.

"Bwana Kendrick, usiwe mkali sana. Ninaogopa…” Mwanamke huyo, hata hivyo, bado alitaka kuwa karibu naye tena.

"Chale..." Kendrick hakutaka kupoteza muda na mwanamke huyu.

Baada ya Chake kuitwa, wale wanaume wawili waliokuwa nao nje ya mlango waliingia na kumtoa nje.

Mwanamke huyo alitambua kwamba alikuwa amemkosea mtu ambaye hakupaswa kumkosea. "Bwana. Kendrick… Tafadhali niache...”

"Bwana. Kendrick, naomba nibadilishe nguo kabla hujanitupa nje...”

"Bwana Kendrick… Ah…”

Mwanamke huyo alitupwa nje na mlango ukafungwa.

Timothy aliinamisha kichwa chini na hakusema chochote.

Kendrick alimkazia macho Timothy aliyekuwa na jasho kwenye paji la uso. “Unajua kwanini ninakutafuta?”

Sura ya 174

Timothy aliogopa sana sura kali ya Kendrick hivi kwamba hakuthubutu kutazama juu. Alikuwa mnyonge sana kiasi kwamba alikuwa amebakiwa na nguvu za mwisho tu za kumzuia asianguke.

Alihisi ameshindwa kujizuia, akatingisha kichwa kisha akaitikia kwa kichwa. Kwa kweli, hakujua alichokuwa akifanya.

Kendrick alimtazama Timothy chini, “Unaijua au hujui?”

“Sijui… Unaweza kuniambia tafadhali…?” Timothy aliogopa sana.

Kendrick alikuwa amesimama pale. Mwanga wa jua nje ya dirisha ulikuwa ukimuangukia. Hewa ilikuwa safi sana, lakini haikuweza kupunguza hasira yake.

Macho yake yalikuwa makali na baridi.
Aliongea huku akikodoa macho.

Hali ilikuwa bado ya kutisha, na kumfanya Timothy ajisikie mgonjwa.

Timothy aliuma meno na hatimaye akakubali. “Mr. Kendrick, nilikosea. Sikupaswa kumfanyia njama Bi Mayala… Lakini sikujua yeye ni Bi Mayala... Kama ningalijua, nisingemkaribia. Bwana Kendrick, naomba unisamehe. Sithubutu kufanya hivyo katika siku zijazo. Hapana… sitafanya hivyo tena. Tafadhali.”

"Nikusamehe? Nitakusamehe vipi?" Macho ya Kendrick yalizidi kuwa makali.

Kendrick alisema kwa sauti nyepesi, lakini masikioni mwa Timothy ilisikika kama sauti kutoka kuzimu ambayo ilimfanya atetemeke.

"Bwana. Kendrick, najua kweli nimekosea.” Timothy aliomba, “Nitakaa mbali na Bi. Mayala…”

"Nini?" Kendrick aliuliza kwa sauti ya mashaka.

"Hapana, hapana, hapana. Ambapo kuna Bi. Mayala, hakutakuwa na mimi. Nitaondoka mbali.” Thimothy alieleza.

"Ulipaswa kufahamu hilo mapema kabla hujafanya ujinga wako!" Kendrick aliketi kwenye kochi moja karibu na meza ya mbao ya mviringo ikiwa na waridi jekundu kwenye vesi nyeupe juu yake.

"Wewe sio mjinga, huna woga. Hata kama ulikuwa hujui Alissa ni mke wangu, ulijua ni mwanamke wangu! Na, ulimsema vibaya na kumharibia sifa yake kwenye karamu ya chakula!”

"Nilikuwa nimelewa na kupoteza akili…” Hicho ndicho kilikuwa kisingizio pekee ambacho Timothy angeweza kupata.

"Ulifanya makusudi." Macho ya Kendrick yalikuwa baridi. "Ulimtuma mtu kwa familia ya Mayala?"

"Hapana, sio mimi!" Timothy alitikisa kichwa mara kwa mara kukataa.

"Ingekuwa nani kama si wewe?" Kendrick ghafla alionekana mwenye huzuni.

“Kwa kweli sikuwa mimi. Hata simfahamu.” Timothy alikanusha.

Kendrick aligeuza midomo yake na kumtazama Chale, ambaye alikuwa akimsubiri.

Chale alikuwa na Kendrick kama msaidizi wake kwa miaka mingi, na alijua kabisa kile Bosi wake alimaanisha.

Chale alipiga simu, "Je, huyo yupo bado? Mleteni ndani.”

Alipokata tu simu, mlinzi mmoja aliyekuwa amevalia nguo nyeusi alimchukua mwanaume mmoja na kuondoka zake.

Mtu huyo alikubali na kuanguka miguuni pa Chale, “Bw. Kendrick, sijui chochote. Sio mimi, sio mimi."

"Tazama ni nani aliye mbele yako." Chale alirudi nyuma ili Kalunde aweze kumtazama vyema Kendrick nyuma.

Kendrick aliinamisha kichwa chake kidogo, akitazama vidole vyake virefu, vilivyo laini na vya kupendeza. Alikaa pale vizuri kabisa kama sanamu ya baridi.

Kalunde alitazama juu kwa makini, akamtazama Kendrick, kisha akainamisha macho yake, “Bw. Kendrick…”

Alikuwa mjinga sana hata alimkosea Bwana Kendrick halisi.

“Kwa kuwa Timohty hakukutuma, utamwambia Bwana Kendrick ni nani aliyefanya hivyo?” Chale aliongea badala ya Kendrick.

Kalunde alimwonyesha Timothy bila kusita, “Ni yeye. Aliniomba nifanye hivyo.”

“Unazungumzia nini jamani? Mara Timothy akakana akisema, “Hata siwajui ninyi. Ningewezaje kukuomba ufanye kitu kama hiki?"

"Bwana. Timothy, ulinipa 200,000 kwenda kwa familia ya Mayala na ukamshtaki Bi Mayala kuwa hawala wa Bwana Kendrick, na ulisema kwamba utanilinda." Kendrick akamjibu Timothy kisha akamtazama Kendrick, “Bw. Kendrick, kama huniamini, unaweza kuangalia akaunti yangu. Nilipokea 200,000 siku mbili kabla ya kwenda kwa familia ya Mayala.

"Ninaapa kwa maisha yangu kwamba nikisema uwongo, nitakufa!"

Ili kuthibitisha kwamba alikuwa akisema kweli, Kalunde alijiapiza kikatili sana hivi kwamba alihatarisha maisha yake.

Kendrick alikosa subira sana kusikiliza mabishano yao.

“Inatosha.” Chale alipiga kelele. "Bwana Kendrick atakuwa na uamuzi wake mwenyewe. Amekupa nafasi ya kusema ukweli na anaweza kumuacha yule anayesema ukweli, lakini usimlaumu Bwana Kendrick kwa kuwa mkatili kwa anayesema uwongo."

Macho ya Kendrick yalikuwa makali kama mishale iliyomchoma Timothy kifuani.

Timothy akatetemeka, magoti yakalegea na kuanguka chini.

"Bwana Kendrick, ubongo wangu haukuwa ukifanya kazi wakati huo…” Hatimaye Timothy alikiri, “Sikuwa na nia ya kufanya hivi.”

“Halafu ni nani aliyekuambia ufanye hivyo? Kwa nini usiniambie huyo ni nani, nami nitakuacha?” Kendrick alitabasamu kwa hatari.

Timothy aliuma meno na asijue la kujibu.

"Nini? Je! ni lazima ufikirie kuhusu mtu huyo?" Kendrick alivuka miguu yake kwa uzuri, "Kwa kuwa wewe ni mwaminifu sana, natumai mtu huyo hatakusaliti."

“Timothy, hii ni nafasi ya mwisho kukupa bwana Kendrick. Kuwa mwaminifu." Chale alimwonya asifikiri kwamba anaweza kuondoka bila kusema chochote.

"Ningeweza kukuambia, lakini natumai Bwana Kendrick atakubali sharti moja." Timothy alithubutu kufanya ombi.

"Je, unafikiri una sifa ya kumpa masharti Bwana Kendrick?" Chale alidhihaki.

“Sawa, niambie.” Kendrick alitaka kuona anachotaka kufanya.

"Bwana Kendrick, usimwambie huyo mtu kuwa ni mimi niliyekwambia, na unisamehe.” Timothy bado alitaka kuendelea kuwa hai.

Kendrick alikuwa mkatili na mkatili… Kila mtu alijua hilo.

Hakuweza kujizuia kukumbuka kilichowapata wale waliomkosea Kendrick.

Hakutaka kuharibu maisha yake yote ya furaha kwa ajili ya mwanamke.

"Unaomba sana." Chale alimuonea aibu. “Unataka kuomba zaidi?”

Sura ya 175

Chale alitabasamu, akijifanya kuwa mkarimu.
Timothy akatikisa kichwa na hakuwa na ujasiri wa kujadili, "Hapana, bwana."

"Kweli, wewe sio mchoyo, sivyo?" Chale alidhihaki.

Timothy hakuwa na budi ila kuvumilia fedheha hiyo. Sasa kipaumbele chake kikuu kilikuwa kujiweka salama, “Bw. Kendrick, kwa hivyo ... unafikiria nini?"

Isingekuwa kwamba alimwambia Kendrick kwamba Melissa ndiye aliyekuwa nyuma ya haya yote, angehukumiwa.

Baada ya yote, Melissa alikuwa mwanachama wa familia ya Maziku, pia dada ya Alissa, mke wa Kendrick. Yaani Melissa alikuwa shemeji wa Kendrick. Kwa sababu hiyo, pengine Kendrick hangefanya lolote zito kumuadhibu bali angemkemea tu.

Hata hivyo, Timothy mwenyewe alikuwa mgeni tu kwake. Hakuweza kumudu kumkosea Kendrick. Kwa hiyo hakuwa na budi ila kuungama ukweli.

“Sawa…” Kendrick alinyanyua waridi jekundu kwenye vesi na kulainisha petali, “Lazima huyo atakuwa Melissa Maziku!”

Timothy alipigwa na butwaa huku macho yakiwa yamemtoka. Ilionekana kuwa hakuwahi kutarajia Kendrick kuujua ukweli mapema.

"Kwa kweli, Alissa amekuwa mke wangu halali badala ya hawara. Nilishampelekaga kwa familia yangu kukutana na wazazi wangu. Hata kama mlimfanya Kalunde aende kwa familia yangu, hakufanya kazi kamwe. Na si ndiyo sababu baba yangu alikasirika.” Kendrick alifungua midomo yake myembamba na kusema kwa sauti ya baridi kawaida.

"Nilidanganya kuachana na Alissa kwa sababu tu wakati yeye yuko upande dhaifu ndipo wahalifu hao wataonekana. Ndio maana wewe na Melissa mlijidhihirisha wakati wa sherehe."

Kendrick aling'oa shina moja baada ya nyingine na kuyaangusha chini, "Kwa hiyo sihitaji ukiri kwa sababu nimekuwa nikifahamu ukweli.

“Kwa kweli, nyinyi wawili mnapaswa kulaumiwa. Mna hamu sana ya kulipiza kisasi kwa Alissa na ndio maana mnajichanganya.”

Aliposikia hivyo, Timothy alimeza mate kwa woga na kusema, “Mr. Kendrick, huo sio ukweli. Tafadhali nisikilize!”

"Bwana. Kendrick hana muda wa kupoteza kusikiliza maneno yako!” Chale alimkatiza.

Kwa kuwa kila kitu kilikuwa wazi, Kendrick hakutaka kusikia neno lolote kutoka kwake.

Zaidi ya hayo, Kendrick alithamini wakati wake na ilimbidi kufanya haraka.

Alidondosha upara wa waridi mezani na kusimama kama bwana.

Alifunga kifungo cha suti yake na kusema kwa umaridadi, “Chale, ni kwako sasa hivi.”

“Usijali bwana Kendrick. Nitaifanya kikamilifu." Chale aliinama kwake kwa heshima kubwa.

Kwa kawaida, Kendrick hakulazimika kufika hapa ana kwa ana kwa tapeli kama hiyo. Ilikuwa ni kazi ya Chale kumalizana naye. Ila kwa sababu mhusika alikuwa ni Alissa, Kendrick alifika yeye mwenyewe!

Wakati Kendrick anakaribia kupiga hatua, Timothy aliharakisha kupiga magoti mbele yake na kuwa karibu kuushika mguu wa Kendrick kuomba rehema. Lakini Chale alimzuia mapema kwa kumfukuza.

“Usiichafue suruali ya bwana Kendrick! Bwana Jabo, ninaogopa kwamba hutakuwa na mikono ya kukumbatia wasichana wowote warembo.” Chale alisema bila huruma.

"Bwana. Kendrick, tafadhali nisamehe! Ninaweza kukufanyia chochote mradi tu utanihurumia!” Timothy aliingiwa na hofu kabisa.

“Ninachohitaji ufanye ni rahisi sana. Lakini umefanya kila kitu mara moja! Hicho ndicho unachostahili.” Kendrick aliitazama ile love bite iliyokuwa kwenye shingo ya Timothy. Ilionekana kumkumbusha Timothy juu ya ulafi wake jana usiku.

"Bwana Kendrick, naomba msamaha wako? Sina akili sana kukuelewa ulimaanisha nini?" Timothy alichanganyikiwa.

“Acha nikuambie,” Chale alisema, “Hujamwomba Bi. Mayala msamaha mara tu baada ya kumkosea kwenye karamu jana usiku. Hukufanya lolote usiku mzima hadi sasa. Na hata ulimfanya Bwana Kendrick aje kwako ana kwa ana!”

“Hukuomba msamaha. Mbaya zaidi hata ulijiingiza kwenye tafrija pale hotelini. Je, hukuwa na muda wa kumuomba msamaha Bi
Mayala? Vipi wewe! Unamdhalilisha Bwana Kendrick kwa kufanya hivyo?”

Hiyo ndiyo sababu iliyomfanya Kendrick asione huruma.

"Bwana. Kendrick, ni…Nitamuomba msamaha Bi. Mayala sasa hivi!” Timothy aliruka na kukaribia kukimbia ili avae.

“Umechelewa!”

“Sijachelewa maadamu niko tayari kuomba msamaha kwa unyoofu wangu mkuu!” Timothy alisema kwa woga.

“Haitasaidia!”

"Itafanya kazi! Nitaendelea kuomba msamaha hadi anisamehe!” Timothy alijaribu kila njia na kusisitiza, “Niko tayari kupiga magoti mbele yake. Sitasimama hadi anisamehe!”

“Utamtishia?” Kendrick aliinua nyuso zake, akionekana kuwa hatari.

"Hapana, hapana, hapana!" Timothy akatikisa kichwa.

“Huna nafasi!” Kendrick alichukua shina la ua kutoka kwenye meza tena.

Alipepesa macho na kulinyakua lile shina na kulidondosha chini. Alisema bila kujali, "Siku ya mwisho ya familia ya Jabo inakuja!"

Siku ya mwisho ya familia ya Jano?! Ni kisasi kibaya kama nini!

Timothy alishindwa kupumua aliposikia hivyo.

Akashtuka, “Hapana! Bwana Kendrick, tafadhali hapana, usifanye hivyo!”

Kendrick hakuwa na mood ya kukaa. Akasonga mbele kuondoka.

Chale alimzuia Timothy, “Bw. Kendrick hatarudi nyuma ya maneno yake! Usipoteze muda wako! Unastahili! Hakuna anayeweza kukuokoa! Hata familia yako lazima itaangamizwa kwa sababu yako!”

Chale akageuka na kuondoka. Ni Timothy pekee aliyeachwa nyuma, na akaanguka chini na tabasamu la uchungu. Machozi yalitiririka usoni mwake.

Angeweza kusema jinsi maisha yake yangekuwa duni bila chelezo ya familia yake. Bila shaka, hakuna mtu angeweza kumudu kumkosea Kendrick.

Timothy alimtazama Kalunde, ambaye aliganda pale pale huku akiwa na hofu kubwa.

Timothy alimkokota mbele na kumpiga ngumi kwenye taya yake, “Kalunde! Ngoja nikuonye! Usijaribu kutoroka hata kama familia yangu imeenda!”

Kalunde pia alipigana kwa kuwa hakuwa na njia ya kujiokoa, "Timothy! Unastahili! Haina uhusiano wowote nami!”

“Kama si usaliti wako, nisingeishia hivyo! Lazima nikuue! Sina chochote sasa!” Timothy alipatwa na kichaa.

Alimkaba kwa nguvu Kalunde kwa mikono yake miwili kwa macho yake yenye damu.

Kalunde alikuwa mzee na mwembamba kuliko yeye. Hakuweza kumpinga Timothy, ambaye alikuwa mrefu na mwenye nguvu zaidi. Uso wake ulikuwa unawaka hasira na alikuwa amekosa hewa. Uso wake ulibadilika rangi huku akikaribia kuzimia.

Alijaribu kushika mikono ya Timothy ili kumtoa, lakini alishindwa, “…acha tu…niache niende… nipate wazo la kukusaidia…”

Aliposikia hivyo, mara Timothy alipunguza mshiko wake, “Usidanganye kwangu! Au nitakuua!”

Kalunde alijitahidi kutikisa kichwa. Ndipo Timothy akamwachia, “Sema!”

Sura ya 176

Kalunde bado alishtuka. Bado hakuweza kutamka kwa muda.

Aliponyongwa tu, aliogopa sana kwa sababu ya kifo. Lakini ghafla alikuja na wazo la kujiweka hai.

“Sema! Nakusikia!” Timothy alimhimiza kwani alikuwa na wasiwasi sana alipomwona bado anahema.

“Tu…subiri kidogo!” Kalunde alikuwa mzee wa miaka hamsini. Alihitaji muda zaidi wa kupumua vizuri tena.

"Unanidanganya?!" Timothy alimshika bega kwa nguvu huku akionyesha ukali.

Alifanya tofauti kabisa na wakati uliopita alipokabiliana na Kendrick, ambapo alitetemeka kwa hofu.

Sheria ya msitu inatumika kila wakati ulimwenguni bila ubaguzi.

“Bila shaka sithubutu kukudanganya!” Kalunde alishusha pumzi ndefu kisha akaendelea, “Tulia tu na unisikilize. Siwezi kukuhakikishia kuwa unaweza kujiokoa. Lakini bado inawezekana kwa 50%. Na kila kitu kinategemea wewe sasa."

“Zaidi ya hayo, jifanye masikini na unanyanyaswa. Na acha kiburi chako na kujistahi ili kupata huruma kadri uwezavyo! "Haijalishi matokeo yatakuwaje, natumai unaweza kuniruhusu niende."

Kalunde alitishwa sana kwani alikaribia kunyongwa hadi kufa na huyu mwendawazimu. Hakuweza kumudu kuangamia pamoja naye.

“Sawa, nitakuruhusu uende mradi tu nadhani itafanya kazi. Zaidi ya hayo, ikiwa itafanya kazi kweli, utapata tuzo yangu!

Timothy aliiona kuwa ni bahati ya kutosha hata ikiwa ni 50% tu ya mafanikio, "Basi niambie tu!"

Kalunde alimwambia kila kitu ambacho alikuja nacho. Aliposikia, macho ya Timothy yalionekana kung'aa kwa tumaini tena.

“Sawa, hilo ndilo tu ningeweza kufanya. Na sasa kila kitu kinategemea wewe!" Kalunde aliiba shingo yake iliyokuwa inauma kwa woga wa kudumu.

“Sawa!” Timothy akaitikia kwa kichwa, “Sawa, unaweza kuondoka sasa.”

Kalunde alifurahi sana kusikia hivyo. Mara moja akatoka nje ya chumba kile.

Timothy alikaa kwenye sofa ili kujipumzisha kidogo. Kisha akaingia bafuni kujisafisha.

Baadae, alivaa na kurudi kuwa muungwana.

Alitoka nje ya hoteli hiyo kisha akaendesha gari hadi kwenye Kampuni ya Tawi ya Universal Group katikati ya Jiji la Mwanza.

Timothy aliegesha gari na kuingia ndani ya ukumbi wa jengo hilo. Kisha akaja kwenye dawati la mapokezi, “Samahani, mimi ni Mark Jabo. Je, Miss Alissa Maziku yuko huru sasa? Ningependa kuwa na miadi naye.”

Timothy alichagua kutaja jina la Mark kuhofia Alissa angekataa kukutana naye.

“Sawa, tafadhali subiri kidogo.” Mwanamke wa mapokezi alimpigia Alissa, “Bi Alissa, bwana mmoja anayeitwa Mark Jabo anataka kuwa na miadi nawe. Naomba ratiba yako?”

Alissa ambaye alikuwa akifanya kazi ya kuandaa rasimu yake pale ofisini, alishangaa sana kusikia jina la Mark.

Ingawa mara moja bibi yake alimwomba awe na uchumba na Mark, hata walikuwa hawajaonana. Bibi yake alipokaribia kupanga upya miadi naye, ndipo alipopewa taarifa kuwa Alissa ameolewa na Kendrick. Kwa hivyo, kwa kawaida, bibi yake hangepanga miadi yake tena.

Labda bibi yake alisahau kumjulisha Mark kwamba miadi hiyo ilighairiwa. Na aliendesha gari kukutana naye siku hiyo?

Alissa aliinua mkono wake kuitazama saa yake, Ilikuwa ni saa 10:10 sasa.

"Bi Alissa, upo?" Mwanamke wa Mapokezi aliuliza huku Alissa akiwa bado kimya.

“Ndiyo. Acha tu asubiri hapa. Nitakuwa hapo chini dakika tano baadaye.” Alissa alifikiria kwa muda. Bado aliona ni muhimu kumweleza iwapo kungekuwa na kutoelewana. Hakutaka kumiashiria Mark vibaya kwa bibi yake kwa kuvunja miadi. Wala hakutaka Kendrick awe na wivu nayo.

Kwa kuwaza kwa sura ya Kendrick mwenye huzuni na wivu, Alissa alishindwa kujizuia kucheka.

Alissa akaweka simu chini. Akashusha pumzi ndefu na kuinama. Alilainisha nguo zake na kutoka nje ya ofisi.

Aliangalia hata sura yake kwenye kioo kwenye lifti.

Alissa alipotoka kwenye lifti, alitembea kuelekeaapokezi, "Mark yuko wapi?"

Mwanamke wa mapokezi alielekeza kwa yule aliyesimama nje ya mlango, "Yule pale."

Alissa aliitazama sura yake, akihisi kuifahamu kabisa. Kisha akasonga mbele. Na yule mtu akageuka polepole.

Alissa alipokutana naye uso kwa uso, alimuona wazi kuwa ni Timothy, sio Mark. Mara akageuka na kuondoka na uso wa baridi.

Ingawa hakuwa amekutana na Mark hapo awali, alijua sura yake kutokana na picha aliyoonyeshwa na bibi yake.

"Bi Alissa, subiri!" Timothy alisonga mbele kumzuia alipomwona akiondoka.

“Unafanya nini Timothy!” Alissa alipiga hatua mbili nyuma ili kukaa mbali naye, “Hapa ni kazini kwangu! Usifanye fujo!”

"Bi Alissa, sina nia mbaya na niko hapa kukuomba msamaha." Timothy alimsujudia kwa heshima, “Nasikitika sana kwa yale niliyokutendea. Tafadhali naomba unisamehe!"

Alissa alikosa la kusema na kupigwa na butwaa kwa hatua yake, “Nini…unafanya nini? Bwana Timothy, nahitaji kufanya kazi. Na sina muda wa kucheza na wewe.”

Alissa kwa umakini alimpita na kuwa karibu kuondoka. Lakini Timothy alimzuia na bado akainama kuomba msamaha.

Mwanamke wa mapokezi na wafanyakazi wengine wote waliwatazama kwa udadisi. Baadhi yao hata walianza kusengenya.

Alissa hakuwa na la kufanya ila kuwaomba walinzi msaada, “Security, tafadhali mnaweza kumtoa Bw. Timothy hapa?”

Walinzi walimfahamu Alissa. Kwa hiyo walitembea kwa Timothy na kusema, “Bw. Mkubwa, tafadhali ondoka hapa. Au ninaogopa tunahitaji kukutoa kwa nguvu."

“Nipo hapa kuomba msamaha. Niamini, sina nia mbaya.” Timothy aliona kuwa sio lazima kufukuzwa kwani hakukusudia kumnyanyasa.

Ilibidi walinzi wamtoe nje kwa nguvu.

Timothy bado alijikaza, “Bi Alissa, sitaondoka mpaka leo unisamehe!”

Timothy alitolewa nje na hakuweza kuingia kwani walinzi bado walikuwa wamesimama mbele ya mlango. Angeweza tu kukaa nje ya jengo.

"Kaa tu kama unataka!" Alissa aligeuka kwa ubaridi, akimuacha peke yake na porojo za wengine.

“Bi Alissa, usiondoke tafadhali! Huwezi kuniona nikifa!” Timothy alipiga goti moja.

Hakuwa na la kufanya zaidi ya kupiga magoti mbele ya jengo hilo, akijaribu kupata huruma zaidi.

Alitaka kumshinikiza Alissa na watazamaji hao. Hiyo ndiyo ilikuwa njia pekee ya yeye kupata msamaha.

Alikuwa na matumaini tu ilimradi Alissa amsamehe.

Baada ya yote, Kendrick alimthamini sana. Alissa pekee ndiye angeweza kumuepushia hasira za Kendrick.

Sura ya 177

Timothy alimuogopa kabisa Kendrick. Hakutaka familia yake iangamizwe. Bado alilazimika kutegemea familia yake kwa utajiri na msaada. Ilimbidi aache kiburi chake na kumpigia magoti mwanamke hata akidhihakiwa. Kila gharama ilikuwa muhimu mradi tu angekuwa na nafasi ya kuishi.

Alissa alichanganyikiwa sana alipomuona amepiga magoti nje ya mlango.

Alimdhihaki vikali kwenye karamu jana yake usiku. Ingewezekanaje kuwa yuko tayari kupiga magoti kuomba msamaha kesho yake?

Kila mpita njia aliona tukio la ajabu. Wote walikuwa wakikisia kilichotokea kati ya Alissa na mwanaume huyu.

"Unafikiri kama Bi Alissa angemwacha mtu huyu ..."

"Hapana! Bibi Alissa ameolewa, kwa hivyo mtu huyu anaweza kuwa mume wake. Unaona, anaendelea kuomba msamaha. Labda alimcheat na Bi Alissa alifahamu hilo.

"Hapana! Anamtaja kama Miss Alissa, sio babe au honey! Kwa hiyo yeye si mume wake!”

"Pengine Miss Alissa aliharibu mpango wake au alikuwa na kitu juu yake. Ndio maana hata muungwana kama yeye hupiga magoti kuomba msamaha.”

“Singefanya hivyo kama singekuwa yeye. Ikinilazimu, ningefanya nyumbani wakati hakuna mtu.” "Kwa hivyo ni nini kinachomfanya ampigie magoti!"

“Acha kubahatisha! Tutajua hivi karibuni ikiwa tutaendelea kutazama."

Alissa alikunja uso baada ya kuwaona wale wasengenyaji. Kisha akamtazama Timothy.

Aliona bora amwache. Kisha akageuka na kuwaacha kila mtu akiendelea kupiga porojo, akimuacha Timothy akicheza hila yake.

Alifikiri watazamaji hao pia wangeondoka ikiwa wangepoteza hamu baada ya yeye kuondoka.

Timothy alifadhaika sana alipomwona akiondoka. Kisha akapiga kelele, "Bi Alissa, nitaendelea kupiga magoti hapa hadi unisamehe kwa kichwa"

Jinsi alivyothubutu kumtishia!

Alissa alitabasamu kwa ubaridi na kusema bila kujali, “Bw. Timothy, unaweza tu kupiga magoti hapa kwa siku nzima ikiwa unasisitiza.

“Nina kazi nyingi ya kushughulikia. Ninaogopa sina muda wa kukupotezea.” Kisha Alissa akawaambia walinzi, “Mwangalieni! Msimruhusu aingie ndani ili kunisumbua!” Alissa hakuwa na chaguo.

Kisha akageuka kuelekea kwenye lifti bila kuangalia nyuma.

Timothy alimwona akiingia kwenye lifti na kubonyeza kitufe. Alitaka kukimbilia ndani kwa wasiwasi. Lakini walinzi walimzuia kama ilivyotakiwa.

"Bwana Mkubwa, samahani. Huruhusiwi kuingia.” Timothy alikuwa na wasiwasi na wazimu alipomwona Alissa akipanda juu.

Baadhi ya watazamaji bado walisimama na kutazama. Ikiwa angeondoka, juhudi zake zote zingetoweka.

Zaidi ya hayo, alikuwa ameahidi tu. Kwa hiyo ilimbidi aendelee kupiga goti moja mbele ya jengo hilo.

Alitegemea tu Alissa angeweza kumuonea huruma kwa kuendelea kwake.

Timothy aliendelea kupiga magoti. Hata hivyo, akiwa mwanamume anayeishi kwa ukwasi, alihisi maumivu ya kiuno na mgongo baada ya kupiga magoti kwa muda. Goti lake liliumia pia kwa sababu ya ardhi ngumu.

Ukweli wake ulibadilika rangi na shati lake lililowa jasho ambalo lilimkakamaa mwilini na kumfanya akose raha kabisa.

Ilipofika saa sita mchana, Timothy alianguka chini. Akavua koti lake la suti na pia tai yake.

Nywele zake zililowa jasho kana kwamba alikimbia maili kadhaa kufika hapa.

Wakati watu walipita kula chakula cha mchana, Timothy aliwaambia, “Tafadhali mwambieni Bi Alissa nahitaji kukutana naye. Ikiwa bado anakataa, nitakuwa nimekufa ... "

Timothy alijiona karibu kufa ikiwa Alissa bado alikataa kukutana naye.

Mmoja wa wapiga porojo alienda kupeleka ujumbe wa Timothy mbele ya Alissa.

Alissa alimtazama kwa ubaridi tu yule ambaye wakati fulani alikuwa karibu na Lily, “Kama uko huru sasa, chukua faili hizo kwa nakala. Jumla ya faili hizi ni 100."

Mtu huyo alionekana kutoridhika kabisa alipoona faili hizo, “Bi Alissa, unapaswa kuwafanya wasichana hao kufikia malengo haya. Hiyo si kazi yangu.”

"Kwa hiyo unaona kuwasilisha ujumbe wa Bw. Timothy kama kazi yako?" Alissa aliacha kazi yake na bado akamkazia macho mtu huyo, “Kwa kuwa kazi yako ni kuingilia mambo madogo madogo, kwa nini nisikuruhusu kushughulikia nakala hizo?”

"Niko hapa kuwasilisha ujumbe."

"Na ninakuomba tu uchukue na nakala." Kisha Alissa akaendelea kusema kwa uzito, “Ikiwa unahisi kuudhika, twende
ofisini kwa Bw. Matthew tumruhusu aamue kuhusu jambo hili.”

Aliposikia hivyo, mtu huyo alifadhaika, “Bi Alissa, sifikiri kwamba tunapaswa kumsumbua Bw. Matthew kwa sababu tu ya mambo madogo madogo kama haya.”

Pia aliogopa kufukuzwa kazi kama Jamila ikiwa Mathew angejua.

Ingawa mtu huyo alikasirishwa sana na ukweli kwamba Alissa angeweza kumtishia uhusiano wake na Mathew na William, hakuwa na chaguo ila kuficha malalamiko yake na kuchukua faili kwa nakala.

Alissa alimdharau sana mchongezi kama yeye. Ni mtu wa ajabu na wa kuchukiza jinsi gani!

Mara simu yake ikaita. Ilikuwa ni simu kutoka kwa Kendrick.

Alichukua simu, ingawa alikasirika, "Kwa nini unanipigia?"

"Habari kwamba Timothy anapiga magoti mbele ya eneo lako la kazi imekuwa mada yenye joto kwenye Mtandao." Kendrick bado alizingatia hatua inayofuata ya Timothy.

“Nina hamu ya kutaka kujua. Kwa nini alikuja kwangu kwa ajili msamaha? Ulimtisha , sawa?" Alissa alionekana kujua sababu aliposikia maneno yake.

"Kalunde alimwambia baba yangu katika Hoteli ya Intercontinental Garden kwamba ina uhusiano fulani na Timothy uliporipotiwa kuwa Hawara yangu. Lakini mpangaji alikuwa Melissa." Kendrick alieleza na kisha akaendelea, “Pamoja na kile kilichotokea jana usiku kwenye karamu…
Ingawa walikuumiza, waliniudhi tangu wakati huo.”

Kendrick asingesimama tu na kutazama wakati Alissa anahusika. Ilimbidi kuwafanya walipe gharama.

Na alianza tu mpango wake wa kulipiza kisasi dhidi ya Melissa huku akianzia kwa Timothy.

Alissa aliposikia hivyo alitabasamu. Alihisi joto moyoni mwake na machozi yakilowanisha macho yake.

Alikaa kimya kwa muda lakini bado alishindwa kutamka kwani alihisi joto kabisa moyoni mwake.

"Nini? Je, umehamasika?” Kendrick alionekana kusoma mawazo yake.

“Asante mpenzi.” Alimwita kama 'mpenzi' kwa ukaribu sana.

"Usiseme, mpenzi." Kendrick alifurahi sana kusikia hivyo, “Ngoja nishughulikie haya yote. Na unahitaji tu kuzingatia kazi yako tu."

“Sawa. Lakini sikutarajia kwamba Timothy angeshirikiana na Melissa.” Alissa alijisikia raha wakati akizungumza. Kwa Kendrick, hiyo itakuwa chelezo bora zaidi.

"Bado ninaweza kuwavunja kirahisi hata wakiungana." Kendrick alidhihaki.

Sura ya 178

Hata kama familia ya Maziku ilijihusisha na familia ya Jabo, haingehitaji Kendrick mapambano yoyote kuishughulikia. Baada ya yote, alikuwa na nguvu zaidi.

"Usiwe na moyo mpole." Kendrick alionekana kumwona, "Najua Melissa ni dada yako."

“Dada? Kwa hiyo? Udada wetu ulikufa miaka mitano iliyopita. Hatuendani sasa! Alikuwa amepanga njama dhidi yangu tena na tena! Kwa nini niwe mpole!” Alissa alikuwa na chuki.

Isingekuwa njama ya Melissa miaka mitano iliyopita, hangekimbia vibaya na hangerudi kulipiza kisasi.

Bado alikumbuka siku ambayo dada yake na mpenzi wake walimsaliti. Iliuma sana.

Alissa alikunja ngumi, viganja vyake vilimuuma huku ukucha ukiwa umevikandamiza kwa nguvu.

"Nina furaha kujua kwamba hatimaye unafahamu." Kendrick aliinua nyusi zake na kutazama saa yake, “Je, ulikula chakula cha mchana?”

"Oh, karibu nisahau." Alissa alijishughulisha sana na kazi yake hadi akasahau kula chakula cha mchana.

"Lazima upate chakula cha mchana bila kujali una shughuli nyingi kiasi gani. Lazima ujitunze.” Kendrick alimkumbusha, ingawa alijua kuwa yeye ni mchapa kazi.

Kendrick alimuunga mkono na kumwachia nafasi ya kutosha kwa kazi yake. Alimfahamu vyema. Alissa hatataka tu kuwa mama wa nyumbani.

Bado alimruhusu kufanya kazi baada ya ndoa. Alijua njia nzuri ya kumpenda ni kumkomboa na nafasi ya kutosha badala ya kumzuia nyumbani.

“Sitaki msichana wangu awe mgonjwa kwa sababu ya kazi nzito. Au ni lazima nikufungie nyumbani.” Kendrick alijaribu kumkumbusha kujitunza kwa kutoa vitisho tu.

“Ninajitunza. Lakini leo imetokea tu.” Alissa aliweza kujua jinsi alivyokuwa serious. Kisha akaendelea, “Sasa nitakula chakula cha mchana.”

“Sawa.” Kendrick aliitikia kwa kichwa.

Baada ya simu hiyo Kendrick alikazia macho kwenye laptop ili aendelee na project zake.

Chale alikuja na kusema kwa heshima, “Bw. Kendrick, tumefuatilia mali zote za familia ya Jabo. Na hii ndio orodha ya washirika wakuu wa familia ya Jabo. Nimewaona na wote wako tayari kusitisha ushirikiano na familia ya Jabo. Hivi karibuni wataanguka katika shida ya uzalishaji."

“Sawa.” Kendrick alishika kikombe maridadi cha kahawa kando yake kwa umaridadi. Alichukua sip na kutabasamu kwa ushindi.
Kila kitu kiliendelea kama ilivyotarajiwa ikijumuisha upunguzaji wa wazi kutoka kwa washirika wote wakuu wa familia ya Jabo. Hakuna aliyethubutu kumkosea Kendrick.

Chale alimchukulia bosi wake kama kituko cha mke wake, ambaye alikuwa tayari kuharibu biashara yenye matumaini kama vile biashara za familia ya Jabo kwa ajili ya mke wake tu. Uzuri wa hatari kama nini!

Bila shaka, Chale angeweza tu kuzika maneno yake katika akili yake.

"Agiza baadhi ya vitafunwa kwa ajili yake. Na uwape wafanyakazi wenzake wote wa kampuni yake chai nzuri ya juu na viburudisho.” Kendrick kisha akaendelea kuagiza, "Mbali na hilo, mpe seti ya chakula cha mchana kinachotayarishwa na Mgahawa wa City Star kila siku kuanzia kesho na kuendelea."

Alimtaka apate chakula cha mchana kwa wakati na pia afurahie tasnifu akiwa na njaa.

“Ndiyo, bwana!” Chale aliitikia kwa kichwa lakini bado alisimama.

Kendrick aliinua nyusi zake, "Unataka kusema nini tena?"

"Bwana. Kendrick, bado hatujapata chakula chochote…” Chale alikuwa akifanya kazi kwa agizo la Kendrick na wafanyakazi wengine kuanzia asubuhi hadi saa nane mchana.
Wote walikuwa njaa.

"Lakini sina njaa hata kama ni saa nane mchana." Kendrick alisema.

"Hiyo ni kwa sababu umelishwa na mapenzi ..." Chale alinung'unika, "Lakini sisi sote hatujaoa na hatuna mapenzi ya kutulisha ..."

"Ulisema nini?" Kendrick aliangaza macho.

"Hapana ... hakuna." Chale aliinamisha kichwa chake baada ya kuona macho yake, “Nilisema nitakuwa sahihi kumuagizia Bi Mayala tasnifu. Lakini, je, tunaweza kuagiza chakula na sisi?”

"Mke wangu bado ana njaa." Kendrick alisema kawaida. Lakini alionekana kumuonya Chale amlishe Alissa kwanza.

"Nitaweka kipaumbele agizo la Bi. Mayala." Chale aligeuka na kuondoka huku akijaribu kutomsumbua Kendrick.

"Utapata bonasi yako ya mwisho wa mwaka mara mbili mwaka huu." Punde, sauti nzito ya Kendrick ilitoka nyuma.

Macho ya Chale yalikuwa yakimeta kwa furaha. Ilionekana kuwa hakuwa na huzuni tena kama muda mfupi uliopita. Aligeuka kwa mshangao, “Asante sana, Bwana Kendrick!”

Akiwa msaidizi wake maalum, Chale Kisendi alikuwa amefurahia kiasi kikubwa cha bonasi ya mwisho wa mwaka. Ikiwa angeongezewa bonasi maradufu, angekuwa tayari hata kufa njaa kwa siku nzima!

Nusu saa baadaye, Alissa alipokea pakiti mbili kubwa zilizojazwa vitafunwa pamoja na chai ya juu, ambayo iliwachukua wanaume watano kupeleka.

“Mungu wangu! Una vitafunwa vingi sana?" Emmy alishangaa huku akiona pakiti kubwa za tasnifu na pia seti maalum ya chakula cha mchana kwa ajili ya Alissa haswa. Kisha akaendelea, “Bi Alissa, mume wako ni nani? Yule tajiri zaidi duniani?”

Alissa alisaini risiti huku akitikisa kichwa, “Hata mimi sikutarajia. Lazima anataka kunifanya niwe na uzito wa tani nyingi.”

Emmy alichukua kikombe cha kahawa kutoka kwenye pakiti na kusema, "Bi Alissa, mume wako lazima atake kukulisha kwa upendo ikiwa unaweza kutafuta upendo kutoka kwa mtu mwingine."

Kisha Emmy akachukua baa ya chokoleti iliyotengenezwa na chapa maarufu duniani. Akaipiga na kuiweka mdomoni. Aliinua uso wake na kutabasamu mbele ya Alissa kwa utata huku mdomo wake ukiwa umetawaliwa na utamu.

Alissa alinyoosha paji la uso wake kwa kidole kwa upole, "Ninajua unachofikiria."

"Alissa, ninakuonea wivu sana kwa ajili ya mume wako mpendwa!" Emmy alihisi upendo kutoka kwa mtu huyo asiyejulikana, "Nitampenda sana mvulana kama yeye ikiwa ningekuwa naye."

“Kweli? Una uhakika mume wangu ni mpenzi? Hujawahi hata kumuona kabla. Pakiti ya disserts itatosha kukushinda?" Alissa alimwona kuwa rahisi sana na asiye na hatia.

"Ingawa pesa sio kiwango pekee cha kuthamini upendo, bado inachukuliwa kuwa muhimu. Ninaweza kujua ni kiasi gani yuko tayari kukulipa. Bado unakumbuka chakula cha Mkahawa wa City Star ulichopokea mara ya mwisho, sivyo? Wakati huu imekuja kila aina ya kahawa maarufu, vinywaji, chokoleti, mikate, skonzi, maandazi, burger... Alitayarisha seti kwa kila mtu hapa.

Baada ya kufikiria kwa muda, Emmy aliendelea, “Niliweza kusema ni lazima iwe ghali sana kwani pakiti zote hapa zina tasnifu na vinywaji vyote kwa kila mfanyakazi katika kampuni. Ni wanaume wachache tu watakuwa tayari kulipa bili.”

Alissa hakujibu bali alitabasamu tu.

"Bi Alissa, mumeo ni mtu wa kuvutia?" Emmy aliuliza kwa udadisi huku akishika shavu lake.

“Ni mzee mwenye umri wa miaka hamsini. Yeye si mrefu. Wala havutii. Yeye ni tajiri sana." Alissa alisema kinyume na Kendrick.
“Siamini.” Emmy akatikisa kichwa.

"Kwa nini isiwe hivyo?" Alissa alitabasamu hata zaidi, “Labda mimi ni mchimba dhahabu ambaye ningethamini pesa kuliko ndoa yenyewe.”

Sura ya 179

Alissa alisema hivyo bila kujali, kana kwamba hakujali kujichafua.

"Siamini kwamba Miss Alissa ni mtu kama huyo." Emmy alisema kwa hisia, “Bi Alissa, wanakupaka matope kwa sababu tu wanakuonea wivu maisha yako ya furaha. Huwezi kujichafua namna hii.”

"Emmy, huna hatia sana." Akiutazama uso mzuri wa Emmy, Alissa alihisi kwamba Emmy alikuwa kama yeye hapo awali.

Kwa macho ya watu wasio na hatia, kulikuwa na mambo mengi safi na mazuri duniani, kwa hiyo waliishi kwa furaha zaidi kuliko mtu mwingine, lakini ilikuwa rahisi kwao kuumia.

"Bi Alissa, ingawa nimekujua kwa muda mfupi tu, nadhani wewe sio mfuasi wa mali. Ninaamini uadilifu wako binafsi, pamoja na macho yangu.” Emmy alifikiri mtu mzuri kama Alissa ni mrembo sana na hakuwa mtu wa aina hiyo.

Alissa alitabasamu tu. Hakika alikuwa mfuasi wa mali.
Miaka mitatu iliyopita, aliuza ndoa yake kwa Kendrick kwa pesa tu.

Alitaka kumwambia Emmy, lakini alifikiri kwamba Emmy hangeamini, kwa sababu hakufikiri kwamba siku moja angejisaliti.

Lakini, kwa bahati nzuri, Kendrick alitokea kuwa ndiye baba wa mtoto wake. Na alipokutana naye akampenda na kumfanya apate upendo wa kweli na furaha.

"Endelea na kazi yako ukimaliza kula." Alissa akabadili mada, akageuka na kuingia ofisini kwake.

Wakati Alissa alipokuwa akielekea ofisini, bado kulikuwa na watu wengi waliotoa shukrani zao kwake, “Asante, Bi Alissa.”

"Karibu." Alissa alijibu.
Lakini bado kulikuwa na mtu asiyeridhika, kama vile adui ya Alissa, Lily, na mtu wa karibu naye.

Akiwatazama wale watu waliojaribu kumfurahisha Alissa, Lily alihisi kuchukizwa sana hivi kwamba alisukuma mfuko wa zawadi ya chai ya mchana kutoka kwenye dawati la ofisi.

Mfuko ulianguka tu kwenye mguu wake. Ulikuwa mzito sana hadi mguu wake ukaumia, hivyo alikasirika na kuupiga teke.
“Ni baadhi tu ya vitafunio. Mtu yeyote anaweza kumudu…”

Rafiki mkubwa wa Lily, Neema, alisema kwa dharau, na kumfariji Lily, “Lily, usiwe na wasiwasi na
hasira na mwanamke huyo ambaye ameolewa na mzee wa zaidi ya miaka 50. Siku moja mlete mpenzi wako ili kumuaibisha.”

"Sawa, Lily, wakati ujao acha Alissa aangalie kile kinachoitwa utajiri wa kweli. Jonathan ndiye handsome wa kweli mwenye haiba.”

“Lily, kama huwezi kustahimili hilo, muombe Jonathan akusaidie. Baada ya yote, utaolewa na familia yake tajiri na mashuhuri."

"Lily, siku yako ya kuzaliwa inakuja. Jonathan hakika atakuandalia karamu. Uliza tu kila mtu kuleta waume zao au marafiki wa kiume. Ngoja tuone kama Alissa atathubutu au la! Akithubutu, onyesha tu mapenzi na Jonathan ili kuwafanya waone wivu.”

“Mwache ajue kwamba mwanamume utakayefunga naye ndoa ni mwanamume halisi!”

"Haki! Kwa njia, Alissa ni mdogo sana, na mzee anaweza kumridhisha? Je, atapata mwanaume mwingine nje?”

"Naam, itakuwa mtu huyo ambaye amepiga magoti chini?"

“Ha, ha, ha…”

Walichosema watatu hao hakivumiliki!

Timothy, ambaye alizungumziwa nao, hakuweza kustahimili aibu hiyo tena. Alivutia umakini wa kila mtu, na kulikuwa na watu wengi waliokusanyika kwenye lango la jengo la ofisi.

Lakini ilileta ushawishi mkubwa kwa taswira ya kampuni. Mara Mathew alipojua, mara moja akashuka, lakini hakwenda kwa Alissa.

Huenda ni Mathew pekee katika kampuni hiyo aliyejua kuwa Alissa ni mke wa Kendrick.

Ni heshima kubwa kuwa na Bi. Mayala anayefanya kazi katika Universal Group. Kwa kweli hakuthubutu kumsumbua Alissa.

Mathew alishuka chini ili kukabiliana na Timothy. Alikunja uso alipoona watu wengi sana.

"Bwana. Mathew… Bwana Mathew…”

Mathew alimwendea Timothy. Mathew alijua kuhusu watu hawa mashuhuri kwenye mduara wao wa kibiashara.

"Bwana Timothy, kwa nini unasujudu mbele ya kampuni yetu?” Kwa kawaida Mathew alijua kwamba kulikuwa na kitu cha kufanya na Alissa, lakini alijifanya kana kwamba hajui lolote, “Inasemekana umepiga magoti hapa kwa muda mrefu. Hujapata maji wala chakula, sivyo?
Sasa niko huru, vipi nikupeleke ukanywe maji na chakula?”

"Bwana. Mathew, nataka kumuona Bi Maziku. Nitaondoka maadamu nitamuona.” Timothy alihisi kuishiwa nguvu kidogo alipokuwa anazungumza.

“Kwa hiyo, kwa nini unataka kumuona? Hiyo ni kwa sababu ya maneno ya aibu uliyomwambia Bi Maziku jana?" Mathew alichukua hatua ili kwamba Timothy angesema jambo lenye kumuumiza Alissa.

“Ndiyo.” Timothy alisema huku akiwa ameuma meno, “Nilikuja kumwomba msamaha na msaada wake.”

"Utamletea shida sana Miss Maziku kwa kuomba msamaha kwa njia hii. Kama ningekuwa yeye, nisifurahi kukuona katika hali kama hii.” Matthew alisema kile Alissa alitaka kusema, akisimama katika mtazamo wake, "Ikiwa Bw. Timothy unataka kuomba msamaha, unapaswa kufanya mkutano na waandishi wa habari na kuomba msamaha mbele ya umma wa jiji zima, au kutembelea familia ya Maziku ili kuomba msamaha, badala ya kusababisha shida hapa kwa kazi ya Miss Maziku.

"Mimi ... nilisisitiza muda, na sina chaguo lingine." Timothy aliweka matumaini yake yote kwa Alissa.

Alikuwa amepokea simu ya wazazi wake sasa hivi, ambao walisema kwamba kuna jambo zito lilitokea katika familia yao, na kumwambia arudi nyumbani.

Alijua kwamba Kendrick alikuwa ameanzisha mashambulizi, na hangeacha mara tu atakapoanza. Aliyeweza kumzuia Kendrick alikuwa ni Alissa.

Baada ya yote, ilikuwa bora kwa mtendaji kufuta kile alichokifanya. Ilimradi Alissa alimwambia Kendrick asimame, iliwezekana Kendrick asimame.

"Miss Maziku ameondoka kwenye kampuni kupitia maegesho ya chini. Atakuwa kwenye safari ya kikazi siku hizi, na hatakuja kwenye kampuni.” Mathew alisema uwongo.

Simu ya mkononi ya Timothy iliita tena, na mama yake akapiga simu, “Timothy, rudi. Baba yako amepoteza fahamu, na amepelekwa hospitali… Familia yetu imemkosea nani?”

Kusikia kilio cha huzuni cha mama yake na kwamba baba yake alikuwa amepelekwa hospitali, Timothy alipata pigo na hakuweza kujisimamia tena. Alizimia mbele ya jengo la Universal Group, akiwa hana mwendo.

Mhudumu wa mapokezi alimwita Alissa, “Bi Alissa, Bw. Timothy alizimia mbele ya kampuni.”

“Kwa nini unaniita? Piga simu ya dharura na umpeleke hospitali." Alissa alisema bila kusita.

"Sawa."

Mathew alimuona Timothy akiwa amezimia huku jasho likimtoka hata alionekana kama ametoka majini.

“Piga 911. Haraka!”

Ingawa Timotheo hakuwa na ushirikiano nao, ingeleta ushawishi mbaya kwao ikiwa kitu kingempata mbele ya ofisi zao.

Ilichukua dakika 8 kwa gari la wagonjwa kufika, na Timothy akapelekwa hospitali.

Mathew alimwomba mfanyakazi aongozane naye, na akawajulisha familia ya Timothy.

Baada ya Timothy kupelekwa hospitalini, Matthew aliuambia umati, “Rudini kazini.”

Kama matokeo, Universal Group Mwanza Bruch, na Timothy ikawa mada inayovuma.

Universal Group ilikuwa na umaarufu ulioenea zaidi, ambao ungeokoa mamilioni ya gharama za utangazaji kwao.

Lakini hawakujua ikiwa ilikuwa ni bahati au bahati mbaya kuwa mada inayovuma kwa njia hii kwa sababu ya Timothy!

Sura ya 180

Ni utani na utani ulioje!

Alissa alipoona taarifa za Timothy kupelekwa hospitalini, aliinua midomo yake kwa unyonge. Ingawa alimuonea huruma kidogo, haikutosha kwake kusamehe alichokifanya.

Alifikia mwisho huo, kwa sababu tu alivuna matunda ya matendo yake mwenyewe.

Ingawa bado kungekuwa na mtu ambaye angejadili na kumtetea Timothy dhidi ya udhalimu huo, lakini pia kulikuwa na watu ambao walisimama upande wa Alissa. Uvumi ulienea nje.

Hata hivyo, Alissa aliendelea na kazi yake kana kwamba hakuna kilichompata, bila kuathiriwa.

Mhudumu wa mapokezi alimpigia simu Alissa tena, kwa kigugumizi, “Bi… Bi Alissa, safari hii mwanamume anayeitwa Mark Jabo alisema anataka kukuona…”

Alissa alikunja uso kidogo akiwa na simu mkononi, na mawazo yake yakapotea.
Timothy alipelekwa hospitalini. Labda aliyekuja kumtafuta alikuwa Mark wa ukweli.

"Mwambie kwamba nina shughuli nyingi leo, na umwombe arudi." Alissa bado alikataa.

Alikataa kuonana na Timothy, na kwa kawaida sawa na Mark. Wote walikuwa watu wa familia ya Jabo, na hakupaswa kuwatendea kila mmoja wao kwa njia tofauti.

Ingawa bibi yake alisifu utu wa Mark, alikataa kwa sababu sasa haukuwa wakati mzuri wa wao kukutana.

Alissa alipuuza na bado alijishughulisha na kazi hiyo. Zabuni ilikuwa inakuja hivi karibuni na hakuweza kulegea. Baada ya kushinda mradi huu, basi angeweza kuondoka Mwanza kwenda Geita akiwa na Kendrick.

Anapaswa kufurahia furaha ya familia. Hakuna kilichokuwa cha kuridhisha zaidi kuliko kuwa na mtoto mzuri na mume anayempenda.

Alissa alitoka kazini kwenda kumchukua Doris, kisha akarudi kwa akina Maziku.

Aliegesha gari uani, na kumpeleka Doris ndani ya jumba lile.

Walipobadili viatu pale ukumbini, walisikia sauti ya bibi ikitoka sebuleni, pamoja na sauti changa na ya ajabu.

Alissa na Doris waliingia sebuleni wakiwa na slippers laini, “Bibi, kuna mgeni yeyote?”

Sauti safi na nyororo ya Alissa ilivutia umakini wa bibi na mgeni, ambao walimkazia macho.

Macho ya Alissa yakagongana na yule mgeni, wote wawili wakashtuka kidogo.

Alikuwa ni Mark? Kwa nini alikuja nyumbani kwao?

Kilichomshtua Mark ni uzuri wa ajabu wa Alissa kwa mara ya kwanza.

Baada ya sekunde chache, Mark alisimama kutoka kwenye sofa, kwa heshima na kifahari, "Halo, Bi Maziku, mimi ni Mark Jabo."

"Habari, Bwana Mark, mimi ni Alissa Maziku." Alissa alirudi kama alivyokuwa na kujitambulisha kwa uzuri,

"Tafadhali kaa." Alissa akasogea mbele na kuketi, na Mark naye akaketi.

"Mama, nitapanda ghorofani kupumzika." Doris alipanda juu baada ya kuzungumza.

Mark alimtazama Doris, “Je, ni binti yako?”

Alissa alionekana kuwa na umri wa miaka ishirini na tano tu. Je, alikuwa na binti? Bi Jabo alipomwambia bibi yake wawatambulishe, Bi Maziku hakusema kuwa ana mtoto wa kike!

“Ndiyo.” Alissa aliona shaka machoni pa Mark, “Kwa sababu fulani, bibi yangu hakujua kuhusu hilo, pia. Sio kosa lake, lakini ni shida yangu. Sikukusudia kumdanganya bibi yangu, na Bwana Mark.”

Mark aliitikia kwa kichwa kidogo na kukubali maelezo yake.

Ijapokuwa leo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kwake kumuona Alissa, utumbo wake ulimwambia kuwa yeye si mwanamke wa aina hiyo ambaye alikuwa akipanga vitimbi na kuficha makusudi.

“Bibi Maziku, ninasikitika sana kuja Universal Group kukutafuta na kuleta usumbufu mkubwa kwako, lakini ni suala zito, na siwezi kupata muda mwafaka wa kukutafuta. Kwa hiyo, sikuwa na la kufanya ila kuja kumtafuta Bi. Maziku na kukuona.”

Kwa kuwa macho ya watu hayakudanganya, hakukuwa na hisia ya kuchukiza machoni pake ikilinganishwa na ile ya Timothy.

"Kweli, Mark amenunua zawadi nyingi." Bi. Maziku alielekeza kwenye vifurushi vya zawadi kwenye meza, "Yeye ni mpole sana."

"Hicho ndicho ninachopaswa kufanya." Mark alisema kwa upole.

“Je, Bw. Mark ana jambo la haraka la kunitafuta?” Alissa hakuwa kipofu, lakini aliona kabisa alikuja kumtafuta kwa sababu ya jambo la Timothy.

"Bi Maziku, tunahitaji msaada wako." Baada ya kuongea, Mark alikunja uso kwa nguvu, na huzuni ikaibuka kwenye uso wake mzuri.

"Lakini hakuna chochote cha kufanya na mimi." Alissa alihisi kuchanganyikiwa.

“Jana kaka yangu Timothy alikukera kwenye sherehe. Naomba msamaha wako kama ndugu yake. Alichokifanya kimemkasirisha bwana
Kendrick ambaye aliishambulia familia yetu kwa ajili yako, na familia ya Jabo sasa inafilisika. Nakubali kuwa Timothy alifanya jambo baya. Simuonei huruma na sitamuombea. Ila nipo hapa kwa ajili ya familia

“Kampuni yetu si ya kaka yangu pekee. Imeundwa na kuendeshwa na wazazi wangu, ambao wamefariki, bibi yangu, na mimi, pamoja na wafanyakazi wote wa kampuni. Bw. Kendrick anataka kuteketeza kampuni yetu kama onyo kwa wengine, ambayo, kusema kweli, ni kwa sababu tu anataka kulipiza kisasi kwako… Kwa njia hii, ikiwa kampuni yetu itafilisika, kutakuwa na watu wengi wasio na kazi. Je, wanaweza kufanya nini? Hawakufanya kosa lolote. Je, wanapaswa kubeba matokeo yaliyosababishwa na kosa la Timothy, ambalo hawastahili?

“Bi Maziku, ninavutiwa na upendo anaoonyeshwa na Bw. Kendrick kwako, lakini nashukuru kama Bi Maziku anaweza kumshawishi Bw. Kendrick kuwaachilia wasio na hatia. Mtu anapaswa kujibu kwa kile anachofanya mwenyewe. Haijalishi jinsi Bwana Kendrick anataka kumwadhibu Timothy, ni sawa. Ikiwa anahisi haitoshi, anaweza kuniadhibu pia.”

Ili kudumisha bidii ya baba yake, Marko angechukua jukumu hilo. Kwa kweli alikuwa mtu asiyekata tamaa, ambaye alikuwa mwaminifu na mwenye kuwajibika.

"Bi Maziku, maneno yako rahisi yanaweza kuacha familia ya Jabo, na kuokoa maelfu ya watu wa kawaida."

"Bwana. Timothy, mimi si mkuu kama unavyosema.” Alissa hakutaka kubeba mzigo huo.

“Kwa hiyo, Bi Maziku anamaanisha…” Mark alifikiri Alissa hangesaidia, “Ninaelewa. Sasa kwa kuwa Bi Maziku hayuko tayari kusaidia, sitakulazimisha. Lakini hata hivyo, nitafanya niwezavyo kuokoa kampuni yetu. Bi Maziku, Bibi Maziku, samahani kwa kuwasumbua. Kwaherini."

“Sijamaliza maneno yangu. Unaelewa nini?” Alissa alimzuia Mark, ambaye alikuwa amesimama, “Ninatambua kwamba ulichosema ni sawa. Mtu anapaswa kujibu kwa kile anachofanya mwenyewe."

Nuru ya matumaini ilimulika kidogo machoni mwa Mark.

“Alissa, nimemfahamu bibi wa Mark kwa miongo kadhaa, na nimemshuhudia Mark akikua. Ninasikitika kwamba ajali kama hiyo ilitokea kwa familia ya Jabo. Kama bibi, haifai mimi kuingilia biashara ya Kendrick, lakini kama mke wake, unaweza kujaribu kumshawishi." Bibi. Maziku alitaka sana kuisaidia familia ya Jabo, “Bibi. Jabo alikasirika sana hadi akazimia na kupelekwa hospitalini. Alikuwa katika umri huo na hakuweza kustahimili mgomo huo. Natumai unaweza kuwasaidia.”

"Bibi, naona." Alissa alitabasamu na kumtazama Bibi Maziku na kumtaka asiwe na wasiwasi. Angeweza kushughulikia vizuri.

"Asante, Bi Maziku. Sitasahau wema wako mkuu. Ikiwa una jambo ambalo linahitaji msaada wangu katika siku zijazo, niambie tu, na sitakataa kamwe." Mark alisimama na kumuinamia Alissa kutoa shukrani zake.

Sura ya
181
"Bwana Mark, tafadhali, usifanye hivyo.” Alissa aliogopa kuwa hakustahili, “Naweza kujaribu. Lakini Bw. Kendrick ndiye mwenye uamuzi wa mwisho. Isitoshe, hajawahi kurudisha nyuma maneno yake. Sina hakika kama naweza kumshawishi au la. Kwa hiyo, Bw. Mark, usinishukuru sasa, mimi si mtu wa kutegemewa hivyo.”

Alissa alitania kumfanya Mark atulie.

“Samahani kwa kukuaibisha Bi Alissa. Lakini ikiwa inafaa kwa Bwana Kendrick, kwa nini usinitambulishe kwake, ili niweze kuzungumza moja kwa moja na Bwana Kendrick? Kwa njia hii, haitakuathiri wewe na Bwana Kendrick.” Mark alihisi kwamba angeweza kufanya jaribio na hakupaswa kumuaibisha Alissa.

"Nitamuuliza kwanza nione kama ni rahisi kwake kukutana nawe." Alissa angeweza tu kufanya yote awezayo, “Kwa nini usirudi ukasubiri simu yangu?”

"Mark, kwa kuwa Alissa alisema hivyo, huna haja ya kuwa na wasiwasi." Jennifer alimfariji Mark, “Bibi yako bado yuko hospitali. Nenda kamuone kwanza.”

Mark alikuwa na wasiwasi. Aliogopa sana. Kwa asili ya Kendrick, hadi kesho asubuhi akijaaliwa kuamka, familia ya Jabo ingekuwa imefilisika.

Lakini hakuweza kumlazimisha Alissa tena. Alibahatika kupata msaada wake, ilitosha.

"Sawa. Samahani kwa kuwaletea shida sana nyie." Mark alitikisa kichwa na kuondoka kwenye jumba la familia ya Maziku.

Alipomwona Mark akiondoka kwa huzuni, Jennifer pia alikuwa na wasiwasi, “Alissa, nini kinaendelea? Kendrick angewezaje kulenga familia ya Jabo?”

Alissa alichukua mkono wa Jennifer na kisha kumweleza hadithi nzima, “Kwa hiyo, Kendrick alinifanyia hivyo na alitaka kumfundisha Timothy somo.”

"Inaonekana Kendrick ana uhusiano mtamu na wewe." Jennifer alishusha pumzi, “Alifanya yote hayo kwa ajili yako? Ukiiombea familia ya Jabo msamaha, hatakasirika? Acha niwe mtu mbaya."

“Bibi, Kendrick ana akili timamu. Nikizungumza naye ataelewa.” Alissa alishajua kuwa Kendrick sivyo kama alivyovumishwa. Alikuwa hivyo kwa sababu.

Sababu kwanini wengine walisema kwamba alikuwa katili na hana huruma ni kwamba watu hao hawakumwelewa, au wale walioadhibiwa naye walistahili.

Hatawahi kumuumiza mtu bila sababu.

Jennifer aliupapasa mkono wa Alissa, “Uko sawa.”

Kisha, Alissa akampigia Kendrick, “Ulirudi Geita?”

"Hapana. Bado nina mambo kadhaa ya kushughulikia." Kendrick alijibu, vidole vyake vikiteleza kidogo juu ya padi ya kugusa ya kompyuta yake ndogo, "Umenimiss tayari?".

“Ndiyo nimekukumbuka. Nataka kukuona. Uko wapi? nitakuja kwako.” Alissa alidhani Kendrick anajiamini sana. Kila alipompigia simu, alifikiri kwamba amem'miss.

"Bi. Mayala ni mkweli na amekunywa asali leo?" Kendrick aliinua nyusi zake kwa mshangao.
"Hiyo ni kwa sababu Bw. Kendrick alinituma vitindamlo vingi sana mchana wa leo." Alissa alijibu kwa ucheshi.

Kendrick aliangua kicheko, “Kwa hivyo nitaweza kusikia maneno matamu ya Bi. Mayala kila siku?”

"Nitasema ikiwa unataka kusikia." Alissa alikuwa mnene wa ngozi kumuona.

"Niko Capripoint, katika eneo la makazi la 'Lake City'." Kendrick akamwambia anwani, “Nitamwomba dereva akuchukue.”

Je, Lake City halikuwa eneo lenye majumba bora katika Jiji la Mwanza? Lilijulikana pia kama eneo la Watu wazito? Ni matajiri wa hali ya juu tu ndiyo wangeweza kumudu kuishi huko. Lilikuwa kandokando ya ziwa, likizungukwa na maji kwa asilimia 70, kama pete, ambapo kila kipande cha ardhi kilikuwa cha thamani kubwa sana.

Japo Kendrick angeweza kumiliki jumba katika eneo hilo, Alissa hakuwahi kusikia kutoka kwake. Alihisi huenda alikuwa kwa rafiki yake. Baada ya yote, kwa hali yake, haikuwa ajabu kwamba alikuwa na marafiki kila mahali.

“Naweza kuendesha mwenyewe. Itachukua muda mrefu kwa dereva kuja kunichukua.” Alissa alisema.

“Inaonekana Bi. Mayala anatamani sana kuniona. Je, unadhani nifanye nini ili nikutunuku kwa shauku yako nitakapokuona baadaye?” Kendrick alitania jambo lililomfanya Alissa aone haya.

"Tunaweza kuzungumza juu yake nikifika huko." Alissa alisema kwa utulivu.

"Ukifika langoni, Chale atakuwa pale akikusubiri akuongoze ndani." Kendrick alisema. Baada ya yote, ilikuwa eneo bora la makazi ya matajiri na ufikiaji wake ulikuwa mkali sana.

“Sawa.” Alissa alimwacha Doris kwa Jennifer na akaondoka kwenye jumba la kifahari la familia ya Maziku kwenye Range yake nyekundu hadi Capripoint.

Alifika chini ya nusu saa. Alipofika langoni, alimuona Chale.

Chale alimuonyesha mlinzi kitambulisho chake kabla mlinzi huyo hajamruhusu Alissa ndani. Kisha, Chale akaingia kwenye gari na kumpa Alissa maelekezo.

Waliendesha gari ndani ya ua mkubwa. Ua ulikuwa umeezekwa kwa matofali ya duara ya kijivu na bluu, ambayo yalikuwa mazuri kama maua.

Baada ya kuegesha gari, Alissa alimfuata Chale ndani ya jumba namba 68. Walivuka ukumbi, wakaingia sebuleni, kisha wakaenda upande wa kushoto wa ghorofa ya pili. Wakausukuma mlango wa chumba cha kusomea na kumuona Kendrick.

Alissa aliingia ndani na kulitazama ile maktaba kubwa. Rangi yake ilikuwa hasa ya mwanga, ambayo ilikuwa ya kifahari na ya joto.

Rafu ya vitabu iliyokuwa ukutani ilikuwa juu sana, ikiwa na vitabu vingi, ambavyo vilimshangaza Alissa.

Kendrick alipomuona alitabasamu na kumnyooshea kidole.

Alissa akasogea na kusimama kando ya dawati, mikono yake ikiwa imeegemea kidogo ukingo wa dawati, “Bado una shughuli?”

Kendrick alinyoosha mkono na kumshika kifundo cha mkono, akamshusha chini ili aketi kwenye mapaja yake.

Alissa alishikwa na butwaa. Kabla hajapata nafuu kutokana na mshangao huo, tayari mkono wake mmoja aliuweka kiunoni mwake laini na kumkandamiza na mwingine nyuma ya kichwa chake na kumsogeza karibu yake. Kisha, akambusu.

Busu lake lilikuwa la uchokozi, shauku, na hamu. Alissa alichukua busu lake moto, kufuatia mdundo wake.
Kendrick alitawala zaidi na kwa nguvu, akinyonya midomo yake.

Alissa hakuweza kupinga shauku yake. Mwili wake ulikuwa dhaifu. Mikono yake ilining'inia shingoni mwake na kuuegemea mwili wake wenye nguvu, akimruhusu afanye anachotaka.

Kendrick alimuachia, muda huo alishindwa kupumua. Alissa alijihisi kuishiwa nguvu mwili mzima.

"Je, unafikiri inafaa kama thawabu kwa shauku yako ya kuniona?" Kendrick alimtazama Alissa aliyekuwa amejiegemeza begani mwake huku akihema.

Alissa alihisi kudhulumiwa. Alikuwa na hamu lini?

“Una haya… Una aibu?” Kendrick aliona alishtuka na hakujibu.

“Ninahisi joto kidogo…” Alissa hakukubali.

"Vua nguo zako ikiwa unahisi joto." Mkono wa Kendrick kiunoni ukateleza chini.

Alissa alimshika mkono na kubadilisha mada, “Umekuwa ukifanya kazi hapa muda mrefu. Umekula chakula cha jioni au bado?"

"Bado." Kendrick alikuwa amechelewa kula chakula cha mchana. Kwa hiyo, hakuwa na njaa sasa.

“Mimi pia sijala. Vipi nikutengenezee mlo?” Macho ya Alissa yalikuwa yanaangaza na midomo yake ilikuwa imevimba na kuwa myekundu.

Kendrick, hata hivyo, alinyoosha mkono, akakibana kidevu chake kwa kidole gumba na cha shahada, na kukiinua. Kisha, akatabasamu, “Nataka kukula wewe zaidi ya mlo wako…”

Sura ya 182


Sauti ya Kendrick ilikuwa ya mvuto na ya kuvutia…

Alissa alihisi kuwa sauti hiyo ilikuwa ya kupendeza sana hadi akapata haya.

"Nina njaa." Alissa aliinua midomo yake na kumtazama kwa macho yasiyo na hatia na ya huruma.

Kendrick hakuogopa kitu chochote zaidi ya ukarimu wa Bi Mayala na kutokuwa na hatia.

Alikuwa safi na alikuwa na sifa nzuri, ambazo zilikuwa kama mchoro. Alipokuwa hana hatia, angekuwa kama sungura mweupe laini na wa kupendeza, jambo ambalo lilifanya watu washindwe kumkataa.

Kendrick angeweza tu kukubaliana naye, “Sawa. Hebu pika kwanza.”

Alissa alitabasamu kwa furaha, “Kisha nitakutengenezea mlo mtamu na kukuletea ukiwa tayari.”

"Unajua jikoni iko wapi?" Kendrick aliisugua pua yake nzuri kwa vidole vyake.

Alissa akatingisha kichwa kuashiria hajui lolote.

"Ngoja nikuonyeshe." Kendrick pia akaamua kuwa na mapumziko.

Wakainuka. Kendrick aliushika mkono wa Alissa bila kujijua. Jinsi walivyopatana ilikuwa ya kawaida kama wanandoa, kana kwamba walikuwa wamefanya mazoezi mara nyingi.

Kendrick akamchukua kwa mkono mmoja, na mkono mwingine katika mfuko wake wa suruali. Akampeleka chini jikoni.

Jikoni lilikuwa kubwa na lilikuwa na kila kitu ambacho watu wangehitaji.

Jumba hili lilikuwa bora zaidi kuliko jumba la familia ya Maziku na lile la Kendrick la Igoma yakiwekwa pamoja. Lilistahili kuwa jumba la gharama kubwa zaidi katika jiji.

"Je, unaipenda?" Kendrick bado alikuwa makini kiasi cha kushika ishara ya mshangao machoni mwake.

Alissa alifikiria hata kama aliipenda, ilikuwa mahali pa rafiki yake.

"Ikiwa hupapendi, tutahamia mahali pengine." Kendrick alisema kawaida.

Hili lilikuwa jumba la kifahari ambalo watu wa kawaida hawakuweza kumudu maishani mwao.

Lakini Kendrick, ambaye alikuwa na hadhi ya juu ya kijamii, hakujali hata kidogo. Kwa hivyo, kuwa na mume tajiri ilikuwa ajabu sana.

"Ikiwa unapapenda, tutakaa hapa." Kendrick alizungusha mikono yake kiunoni kwa nyuma yake.

“Hii ni nyumba ya rafiki yako, sivyo? Si wazo zuri kwetu kubaki hapa, sivyo?” Alissa aliuvuta mkono wake chini.

“Nyumba ya rafiki yangu?” Kendrick alikunja paji la uso na kugusa vidole vyake kwenye paji la uso wake, “Tunapaswa kuwa na nyumba yetu wenyewe tunaporudi Mwanza. Hapa ndipo nilipochagua kwa wiki mbili na kununua. Katika siku zijazo, tunaweza kuishi katika nyumba yetu wenyewe tunaporudi Mwanza. Si lazima tukae katika jumba la kifahari la familia ya Maziku.”

"Ulinunua jumba hili?" Alissa alishangaa kuwa angenunua nyumba ya bei ghali sana na alikuwa na nyumba nyingine. "Na kule Igoma?" Alissa alishangaa.

"Kule ni kama kwa Peter na Megan. Ni Watu wazima wale. Siwezi kuwahamisha na wala hatuwezi kuishi nao. Si vyema wakajua kila kitu tunachofanya."

“Nilikuahidi kwenda Geita. Ni mara chache tutakaa Mwanza. Kwa hiyo, hakuna haja ya wewe kununua nyumba.”

“Nimekuoa. Siwezi kukuacha uteseke vibaya. Kukupa nyumba ni jukumu la msingi zaidi kwangu mimi mumeo.” Kendrick alizipapasa nywele zake ndefu nyeusi, “Usichukie kutumia pesa zangu. Ninaweza kuchuma mabilioni kwa dakika moja. Lakini nina mke mmoja tu. Kwa hiyo, nitahitaji kukutunza.”

Alissa alichukua hatua ya kumwegemea mikononi mwake, akizungusha mikono yake kiunoni, “Asante.”

“Usiseme, Bi Mayala. Ikiwa kweli unataka kunishukuru, sijali kunishukuru kwa njia nyingine.” Kendrick alicheka vibaya.

Alissa akatazama juu uso wake mzuri mikononi mwake, “Hiyo ni dili. Kendrick, wewe kaa tu hapa na usubiri kidogo.” Alitoa tabasamu la ujanja, kama mbweha mdogo mzuri.

Kisha, akamuacha. Alissa akaanza kazi yake. Alivaa apron na kofia ya jikoni, na kuliendea friji.

Alifungua friji, ambayo pia ilikuwa imejaa. Kwa kweli ilimfanya ajisikie yuko nyumbani.

Alissa alichukua mazagazaga na kuanza kuandaa mlo. Wakati huo huo, Kendrick alijaribu kusaidia, lakini alikataa.

Aliandaa sato watatu, maana Kendrick aliwaoenda sana hao samaki, kisha akaendelea kutayarisha viungo, kitunguu saumu kilichosagwa, limao…

"Unapenda chakula cha pilipili?" alimuuliza huku akikaribia kuweka unga wa pilipili.

"Ningependa kula chochote unachotengeneza."

Hata hivyo, Alissa alimdhihaki, “Ikiwa nilichoweka ni sumu, nawe utaila?”

"Ikiwa ni sumu, nachagua kufa na wewe." Hata kama angekufa, ilimbidi amchukue ili afe pamoja naye, ili asiwe mpweke, “Lakini najua hutafanya hivyo.”

“Inaonekana unanifahamu vizuri. Hujasikia msemo kwamba wanawake ndio wanyonge zaidi?" Alissa alimimina samaki kwenye mafuta yaliyokuwa yakichemka kwenye kikaangio, ambayo yalitoa sauti na harufu ya utamu ikaelea.

"Pia kuna msemo kwamba ukatili ni alama ya mtu mkweli!” Alissa alikatakata mbogamboga kwenye sufuria ili kuzipika wakati samaki wakiiva kwenye mafuta.

Baada ya samaki kuiva, alizichukua na kuziweka kwenye sinia la viungo. Kisha, aliweka kachumbali na mbogamboga jikoni. Pembeni aliweka sufuria la ugali. Kendrick alipenda sana ugali.

Samaki zilinukia vizuri na zilionekana vizuri.

Alissa alipeleka samaki kwenye baa ya pembeni kisha akaenda kuchukua mwiko wa ugali.

Kendrick alichukua vikombe viwili na jagi la mtindi. Ugali ulipowiva, wakajumuika pamoja jikoni

Walikaa uso kwa uso kwenye viti virefu. Kendrick akamwaga mtindi kwenye glasi mbili.

“Asante, Bi. Mayalq, kwa kunipikia mlo mnono.” Kendrick alinyanyua glasi yake ili kugonganisha na Alissa.

Alissa pia aliinua kikombe chake na kukigonganisha na chake kwa upole, “Asante, Bw. Kendrick, kwa kutupatia nyumba katika Jiji la Mwanza.”

Waliinua glasi kwenye midomo yao na kunywa ….

"Kula ushibe." Alissa alichukua ugali na kumlisha.

Kendrick naye akaanza kula. Hakuna hata mmoja wao aliyesema chochote wakati wa chakula. Lakini wangetazamana mara kwa mara, jambo ambalo lingewaridhisha.

Baada ya chakula, Alissa alivuta kipande cha tishu na kumpa Kendrick, “Je, kilikuwa kitamu?”

“Ndiyo.” Kendrick alichukua sip nyingine ya mtindi na kuonekana wa kifahari na mwenye raha.

"Basi nimelipia ulichonifanyia." Alissa alipitisha mikono yake na kuiweka juu ya meza.
Kendrick aliinua nyusi zake, akimtaka ampe maelezo.

"Umekula chakula changu, ambayo inamaanisha kuwa umekula mpishi." Alissa alisema kwa umakini.

Kendrick aliendelea kutabasamu, bila kutarajia kuwa Alissa alikuwa mwerevu na mtukutu kiasi kile.

Chini ya mwanga wa joto na laini, Kendrick alionekana mpole sana sasa.

Alissa naye alihisi Kendrick alikuwa mzuri sana. Alikuwa na uso uliowekwa wazi, ambao ulikuwa ni kazi kuu ya Mungu.

Kendrick akachukua mvinyo mwekundu na kumiminia Alissa na yeye kwenye glasi.

"Bwana. Kendrick, naweza kujadili jambo moja na wewe?” Alissa alikilaza kidevu chake mikononi mwake.

"Hutatetea familia ya Jabo, sivyo?" Kendrick alijua anachofikiria na kusema moja kwa moja.

“Unajuaje?” Alissa alifikiri kwamba hakuwa ametoa taarifa yoyote kabisa.

"Mtu fulani kutoka kwa familia ya Jabo alikuwa ametembelea nyumba ya familia ya Maziku. Kisha, ulikuja kwangu.” Hakukuwa na kitu ambacho hakujua, "Je, kweli unataka nimwachie Timothy?"

“Sijaribu kukuuliza umruhusu Timothy aondoke. Nadhani tu kwamba haina uhusiano wowote na wengine. Anapaswa kubeba matokeo ya matendo yake mwenyewe. Kwa nini tusimfundishe tu yeye mwenyewe somo?” Alissa alizungumza kwa uangalifu, akiogopa kwamba hukumu yoyote isiyofaa ingeumiza hisia zao, “Watu wengine hawana hatia, sivyo?”
 
USINIACHE 4:
Sura ya 183

Kendrick alitazama macho yake meusi na kuinua nyusi zake kidogo. Hakuna mtu aliyeweza kutambua kutoka kwa uso wake kile alichokuwa akifikiria.

“Kwa hiyo, Bi. Mayala ananilaumu kwa kuwafanya wasio na hatia wateseke?” Macho yake ya upole taratibu yakawa baridi.

Hakika, hakumwelewa. Kwa nini alifanya kazi ngumu hivyo lakini isiyo na shukrani? Ni nini hasa kilikuwa kibaya kwake?

Alichokifanya Kendrick ni kumlinda. Mtu kama Timothy alistahili kukosa chochote. Lakini Alissa hakutaka kuwaumiza wasio na hatia.

Dhamiri yake haikumruhusu kukimbia.

"Unajua sivyo ninavyofikiria." Alissa alihisi kufadhaika alipoona kwamba alikuwa na hasira.

Kendrick alisimama kwenye kiti chake na kugeuka kutoka jikoni.

Kendrick alivaa tu shati jeupe na suruali nyeusi, ambayo ilimletea umbo lake jembamba na lililo wima.
Alissa alikunja uso na kuharakisha kumfuata, “Kwa kweli sikumaanisha hivyo.”

Alieleza nyuma yake, akitumaini kwamba hatamuelewa vibaya.

Lakini Kendrick hakugeuka akaondoka tu.

Alissa alitazama mgongo wake na kufikiria kuwa alikuwa hajasafisha jikoni.

Alisafisha vyombo, kisha akaosha baadhi ya matunda na kukata vipande vipande na kuweka kwenye bakuli. Kulikuwa na tufaha, ndizi, papai, chungwa, nanasi…. Kulikuwa na aina mbalimbali za matunda.

Akiwa amekaa kwenye sofa laini la pale sebuleni, Kendrick aliweka mkono mmoja kwenye sehemu ya kuegemea mkono ya sofa na kupitisha miguu yake mirefu. Alikuwa kifahari kama bwana mdogo.

Alissa akatembea. Alikuwa baridi katika kuangalia kwake. Alifumba macho tu, kana kwamba alikuwa amechoka sana.

“Una hasira kweli?” Alissa alitania kwa sauti laini.

Aliweka tunda mkononi mwake juu ya meza ya chai na kumtazama uso wake mzuri.

Baada ya kusubiri kwa muda mrefu, Kendrick alizungumza, “Una uhusiano gani na Mark? Mara tu alipokuomba msaada, ulikuja kwangu mbio ili kumwombea.”

"Sina uhusiano wowote naye." Alissa alionekana kuchanganyikiwa.

Kendrick aliweka tabasamu hafifu na hakujibu.

“Tumewahi kusikiana tu hapo awali. Lakini leo ni mara ya kwanza kukutana.” Alissa aligawanya kipande cha tufaha kwa uma kidogo na kukiinua hadi kwenye midomo ya Kendrick. Lakini aligeuka na hakula.

Alissa alikutana na kukataliwa. Hakuwa na budi ila kula yeye mwenyewe na akaeleza, “Bi. Jabo na Bibi wamekuwa marafiki wazuri kwa zaidi ya miaka kumi. Mark ndiye mjukuu kipenzi cha Bibi yake. Timothy alipoingiza familia yao kwenye matatizo, Bi Jabo alikasirika sana hadi akazimia na kulazwa hospitalini. Kwa hiyo, Mark alikuja kuniona na Bibi ili kuomba msaada. Kama haingekuwa kwa miongo kadhaa ya urafiki kati ya Bi. Jabo na Bibi, nisingeingilia kati.”

Alissa alimtaja Jennifer, akitumaini kwamba Kendrick angemhurumia Jennifer.

Kendrick aliegemeza kichwa chake na kusugua paji la uso kwa vidole vyake, bado hakujali.

"Nilichosema ni kweli." Alissa alikuwa mzito sana na aliogopa kwamba hakumwamini, “Tangu unioe, wewe ni kizazi kidogo kuliko Bibi. Kwa hivyo, ni kawaida kwa Bibi Jabo kumwomba Mark aje kwa Bibi.”

“Hutambui jinsi ulivyo na nguvu! Kila mtu anakuogopa na kukuheshimu. Ni vigumu kwao kukuona. Kwa hivyo, Bibi alinipa jukumu hilo na kuniruhusu niiombee familia ya Jabo isipokuwa Timothy."

"Bi. Jabo na Mark, Timothy na wazazi wake, ni wa ulimwengu tofauti."

Alissa alisema mengi. Kendrick alisikiliza kwa muda, akainuka kwenye sofa na kugeuka kwenda ghorofani.

Ilibidi Alissa amfuate chumbani. Baada ya kuingia bafuni, Kendrick alisimama ghafla na Alissa akapiga mgongo wake mgumu.

Kendrick anyoosha mkono kufungua vifungo vya shati lake, “Nitaoga. Bi Mayala, unataka kubaki hapa kutazama au kuoga nami?”

... nitakusubiri nje." Alissa aliona aibu na kugeuka ili kuondoka.

Kendrick, hata hivyo, alimshika kifundo cha mkono na kumvuta, akimkandamiza kwenye vigae vya baridi kwa mikono yake mirefu.
"Bi. Mayala, kwa kuwa sasa uko hapa, huwezi kuondoka.” Kendrick akawa serious na kumvutia.

Alissa alijikaza. Sasa, alikuwa na woga zaidi kuliko alivyokuwa wakati alipokabiliwa na mitihani yake ya kuingia.

Hakujua la kusema na aliogopa kwamba hakuna kitu ambacho kingefaa.

Alimeza mate huku akiwaza sana la kusema ambalo lisingemtia hasira zaidi.

Kendrick alikuwa amenyoosha mkono kufungua valve ya kudhibiti ya kuoga. Maji baridi yakamwagika ghafla juu ya uso wa Alissa uliokuwa ukiwaka moto.

Lakini maji mengi yalidondoka kwenye mgongo wa Kendrick pia . Shati lake jeupe lililowa mara moja na kung'ang'ania mwili wake wenye nguvu, likionyesha misuli ya kifua chake.

Maji yalidondoka kwenye nywele zake zilizolowa. Alionekana mtanashati sana wakati huo, na kufanya moyo wa Alissa udunde.

Alissa alikuwa na hakika kwamba alivutiwa naye, "Kendrick ...."

Macho yake yakawa meusi zaidi, kana kwamba kila kitu kilikuwa kinazama.

Alissa aliweza kuona tamaa machoni pake. Kendrick aliuma meno na kujizuia. Kisha, akamgeuzia mgongo na kuruhusu maji ya joto yamwagike juu yake.

Alissa alichukua hatua ya kumshika nyuma yake, na kumsindikiza kwenda kumwaga maji, “Mimi… ningependa kuwa mke wako halisi.”

Kwa wakati huu, Alissa hakujali ikiwa alikuwa na msukumo sana na alipoteza akili. Kwa sababu alitaka sana kuwa mke wake halisi sasa.

Kendrick alitetemeka kidogo kwa sababu ya maneno yake, “Bi. Mayala, unajaribu kutumia mtego wa asali?"

"Bila shaka hapana." Alissa alizungumza kwa uthabiti na kwa sauti kubwa, "Niko serious."

Alissa akamwachia na kuja kwake. Macho yake yalikuwa yameng'aa sana na kujawa na uthabiti na ujasiri ambao haujawahi kutokea.

Aliweka mikono yake juu ya mabega yake, akasimama juu ya njongwanjongwa, na kumbusu midomo yake myembamba.

Mpango wake ulishinda uvumilivu wake na kuwasha hamu yake.

Midomo yake ilikuwa moto. Alimbusu midomo yake kwa upole na kwa jeuri.

Kisha, Kendrick akauweka mkono wake kwenye kiuno laini cha Alissa na kumtoa bafuni kuelekea kwenye kitanda kikubwa kilichokuwa ndani ya chumba hicho, huku wakivua nguo zao.

Shati nyeupe, suruali ya suti nyeusi, sidiria ya waridi, sketi nyeupe, soksi tupu … Vyote vilitolewa…

Chumba cha kulala kilikuwa kimya. Taa ya laini ilisaidia kuunda hali ya utata, ambayo iliwafanya wasisimke.

Alissa alikuwa active na Kendrick alikuwa na shauku. Walifanya ngono, wote wawili wakitamani kila mmoja ajaze miili na roho zao zilizo pweke kwa upendo na uchangamfu.

Sura ya 184

Alissa alihisi sana jinsi Kendrick alivyokuwa na nguvu.

Pia alikumbuka usiku wake wa kwanza na Kendrick ulikuwa katika Hoteli ya Full Kipupwe. Alikuwa na nia ya kufanya mapenzi na Kendrick ili kumuokoa Seidrick.

Muda huo alimpa dawa Kendrick ili alale naye. Kendrick, ambaye alidhibitiwa na wadawa hayo, alimtesa. Lakini pia alipata furaha kubwa na kuridhika.

Wakati huu, alichukua hatua ya kumshawishi. Kendrick alikuwa na kiasi, lakini alikuwa bora kuliko wakati alikuwa na madawa ya kulevya. Alissa alichoka sana hadi akaanguka kitandani. Alihisi uchungu hata aliposogeza kidole chake.

Kendrick pia hakutarajia kuwa japo haukuwa usiku wa kwanza kwa Alissa, lakini bado alikuwa na aibu na kumfanya awe wazimu na kusisimka.
Hakujua kwanini hakujali hata kidogo kuwa Alissa hakuwa bikra na hata kwa hiari yake alizama kwa ajili yake.

Alihisi kuwa alikuwa anamfahamu kidogo, kana kwamba haikuwa mara ya kwanza kufanya naye ngono. Lakini kwa wakati huu, hakuweza kufikiria sana.

Baada ya hapo, Kendrick ndiye aliyembeba hadi kuoga, kisha wakajilaza kitandani.

Kendrick alimchukua mikononi mwake na kumbusu kwenye paji la uso, "Lala ikiwa umechoka."

"Sitaki kulala bado." Alissa alizika kichwa chake shingoni.

Alikuwa amechoka, lakini akili yake ilikuwa sawa. Alisisimka tu kidogo.

“Una nguvu sana. Kwa nini tusifanye hivyo tena?” Kendrick alipendekeza.

Alissa, hata hivyo, alirudi nyuma, “Bw. Kendrick, tafadhali niruhusu niondoke.”

Kendrick alimshika bega kwa viganja vyake vikubwa na kuinamisha kichwa chake. Lakini alipofika karibu, alimbusu tu machoni na kurudi nyuma.

Alissa naye aliona tabasamu zito machoni mwake.

“Ulifanya makusudi tu! Mtu mbaya!" Alissa alihisi anachezewa na yeye na kufikia kumpiga kifua chake imara kwa ngumi.

Kendrick alimshika kwa nguvu zaidi, “Ni kawaida kwa Bw. Kendrick kuwa mtu mbaya kwa Bi. Mayala. Nitakufanyia mambo mabaya tu milele.”

Kulikuwa na msemo kwamba kitu cha kufurahisha zaidi katika ulimwengu huu ni kwamba kuna mtu ambaye alikufanyia kitu milele.
Ilimaanisha kuwa mwanaume huyu alimpenda sana na hakupendezwa na wanawake wengine.

“Mbali na hilo, nimekuwa mpweke kwa muda mrefu sana. Ni wakati wa mimi kuwa na joto baada ya kukutana nawe.”

Ingawa Kendrick alikuwa maarufu kwa wanawake, alidumisha uadilifu wake na hakuwahi kujihusisha na wanawake na faida zake za asili.

Kwa hiyo, Alissa alipochukua hatua hiyo, alikuwa akijitesa. Hakuwa ametoa tamaa yake kwa miaka mingi na alikuwa na nguvu zaidi ya kulala naye.

Japokuwa alijua kuwa bwana Kendrick ana ulimi wa kubweteka, na hakupaswa kuamini maneno matamu ya wanaume, lakini bado Alissa aliguswa na maneno yake.

Hata kama alikuwa amesalitiwa na kuumizwa na Seidrick, bado alikuwa tayari kumwamini Kendrick na kuishi naye maishani.

"Utasikia joto wakati wote kuanzia sasa na kuendelea." Alissa hakuwa na haya tena.

Kendrick alitabasamu kwa furaha, “Kwa hiyo, furaha yangu itahusiana na Bi Mayala. Tuelewane vizuri siku zijazo.”

“Hakika.” Alissa naye akaizungusha mikono yake kwenye kiuno chake.

Alissa alipata nafasi nzuri mikononi mwake na akafumba macho yake kidogo. Alisikia harufu mpya ya chumvi ya bahari na joto la kiume, ambayo pia ilionekana kumfanya alale kwa utulivu zaidi.

Kendrick alipoona amefumba macho alizima taa na kumkumbatia Alissa kwa nguvu ili alale.

Asubuhi, ndege waliimba nje ya dirisha. Jua liliwaka kutoka angani.

Alissa alipozinduka, hakukuwa na mtu zaidi yake. Lakini bado kulikuwa na harufu ya Kendrick, ikimkumbusha kuwa kilichotokea jana usiku haikuwa ndoto.

Alilala kwenye mto Kendrick aliotumia jana usiku na kunusa kwa mahaba.

Baada ya Alissa kuamka na kunawa alikuta zile nguo alizovaa jana zimetoweka. Alikuwa na aibu.

Wakati huo, Kendrick alirudi kutoka kwenye mazoezi yake ya asubuhi. Akausukuma mlango na kuona kuwa Alissa anashida, “Nguo zako zimepelekwa kwa dobi. Kuna nguo kwenye chumba cha dressing."

Alissa alienda kwenye chumba kikubwa cha mavazi. Kulikuwa na nguo za kiume upande wa kushoto na za kike upande wa kulia kwenye chumba cha hicho.
Kulikuwa na kila aina ya nguo, ambazo zilipatikana mwaka mzima, hata kofia na viatu.

Alissa akasogea na kunyoosha mkono kugusa safu za nguo. Nguo hizi zote zilikuwa bidhaa mpya za kifahari bila kukata lebo. Bei zazo pia ilikuwa ya kushangaza.

“Umenunua nyingi sana. Je, ni saizi inayofaa?" Alissa akageuka kumtazama, “Mr. Kendrick, hata kama una pesa, usipoteze hivi. Kwa nini usitumie pesa hizo kufanya hisani na kupata sifa nzuri?”

“Kumtumia mke wangu si upotevu. Zaidi ya hayo, ni wakati tu wanawake wanaweza kutumia, wanaume wanaweza kupata.” Kendrick alichagua moja kutoka kwenye safu ya nguo na kumkabidhi, “Nyanza Group na mimi tunatumia pesa nyingi kwa hisani kila mwaka. Wakati watu wa nchi wanakabiliwa na maafa au watoto katika maeneo ya mbali ya milimani wanahitaji misaada, tutatoa pesa… Hadi sasa, Nyanza Group imejenga zaidi ya shule mia moja za msingi za watoto katika maeneo ya vijijini na mwaka huu zinaweza kufikia 200.”

Alissa alizichukua zile nguo alizochagua Kendrick, akijua kuwa mtu huyu mbele yake ni mkarimu na mwenye huruma.

Mtazamo wa ulimwengu juu yake ulikuwa wa juu juu.

Alissa alienda kubadilisha nguo. Jasho la Kendrick lilikuwa karibu kuyeyuka. Kwa hiyo, akaenda kuoga.

Alissa alikuwa mwanamke wa ofisi na kwa kawaida alivaa suti au shati na overskirt kazini.

Kendrick alichomchagulia ni suti ya rangi ya chungwa na sweta iliyosokotwa ya shingo ya kijivu nyepesi, ambayo ilionekana ya joto, angavu na yenye heshima. Hereni zilizo na lulu tano ndogo zilikuwa za kifahari na za kipekee, zinaonyesha hali ya joto.

Mbali na hilo, Alissa alikuwa mrembo wa kuzaliwa mwenye midomo myekundu na macho angavu. Alikuwa thabiti na mwenye kujiamini na sura yenye nguvu. Alikuwa mrembo mahali pa kazi, na angeshangaza wengine kwa mtazamo.

Kendrick pia ilimbidi akiri kwamba alionyesha busara kubwa katika uchaguzi wake wa mke. Alissa alikuwa mwanamke sahihi kwake.

“Mrembo.” Kendrick mara chache alimsifu mwanamke. Lakini huyu alikuwa mke wake, ambaye anapaswa kumsifu, "Je, ni saizi inayofaa?"

“Ndiyo.” Zote zilikuwa saizi ya Alissa, "Umejuaje saizi yangu?"

"Nilipima kwa mikono yangu." Kendrick alichezesha vidole vyake na kumuonyesha Alissa.

Alissa alimkazia macho, "Jitunze."

"Ikiwa watu wote wangekuwa na tabia kama yako, mwanadamu angekuwa ametoweka." Kendrick alielekea upande wa kushoto na kuanza kuchagua nguo ambazo atavaa leo.

Nguo zake nyingi zilikuwa nyeusi. Pia alikuwa na mashati mengi meupe na baadhi ya mashati ya rangi nyingine.

Bado alikuwa amevaa shati jeupe na suti nyeusi leo. Ingawa nguo hizo zilikuwa nyeusi na nyeupe tu, alipozivaa, bado aliwashangaza wengine. Muda wote alipokuwa hapa, hakuna mtu ambaye angeweza kumtolea macho na angekamatwa na sura yake.

Pia alikuwa mwanamume wa kuvutia zaidi kuwahi kumuona akiwa amevalia shati jeupe na suruali ya suti.

Kwa kawaida Kendrick alivua vazi lake jeupe na kubadilisha shati na suruali ya suti.

Mwili wake wa misuli haukuwa na selulosi. Alikuwa na tumbo la eight pack, ambalo lilikuwa la kushangaza sana ambalo lilivutia watu.

"Njoo hapa."

Sura ya 185

Japokuwa Alissa alikuwa ametulia, alipoona sura ya Kendrick inayofanana na ya mwanamitindo wa kiume, akawaza kuwa wamelala jana usiku, hakuweza kujizuia.

Kendrick alimwita. Lakini hakujibu. Kisha, akamwita tena kabla hajarudi kwenye fahamu zake.
Akamsogelea, “Kuna nini?”

"Bi. Mayala, mumeo yuko hapa na bado unajishughulisha? Je, sivutii sana? Au sikukuridhisha?” Kendrick alinyoosha mikono yake mirefu na kumnasa Alissa kati ya chumbani na yeye, “Unadhani nifanye nini ili nikuadhibu kwa kutokuwa makini kwako?”

Alissa akawa na wasiwasi. Alijaribu kuwa mtulivu na kuweka tabasamu lake, “Nitakufungulia.” Aliweka tabasamu tamu na kupiga vifungo kwenye shati lake jeupe kwa vidole vyake, "kwa uangalifu" kumpendeza.

“Kwa nini huwa unavaa mashati meupe na suti nyeusi? Hujawahi kufikiria kujaribu rangi zingine?" Alissa alifunga shati lake huku akibadilisha mada.

"Ladha ya kibinafsi." Kendrick alidhani kuwa nyeusi na nyeupe ni rangi za classic, ambazo zilikuwa na rangi nyingi na rangi yoyote. Hakuhitaji kufikiria sana na angeweza kuokoa muda.

Ingemchukua muda zaidi wakati alipaswa kulinganisha rangi nyingine na tai na viatu.
Mbali na hilo, alifikiri kwamba anaonekana mzuri na mwenye utulivu wakati anavaa hivi.

Alissa akamfungulia, "Vipi kuhusu tai?"

“Nyeusi.” Kendrick bado alichagua nyeusi na alionekana kuwa anapenda rangi hii.

Kendrick akafungua droo aliyoiweka ile tai. Alissa alizitazama zile tai mle ndani na kuchukua tai nyeusi yenye michirizi ya fedha badala ya nyeusi tupu.

“Kuna michirizi. Bwana Kendrick, hutajali, sivyo?” Alissa akafungua tai.

"Ni heshima yangu kuhudumiwa kibinafsi na Bi. Mayala." Kendrick akatikisa kichwa.

Alijisikia furaha sana wakati kulikuwa na mtu ambaye alimtunza kibinafsi.

Kendrick alikuwa mrefu kiasi kwamba ilimbidi Alissa anyanyue kichwa ili kuifunga tai shingoni mwake. Alivuta kola ya shati jeupe, akaweka tai mahali pake, kisha akamfunga kwa ustadi na kulainisha.

"Wewe ni mtaalamu." Kendrick aliitazama ile tai, “Inaonekana umefanya mazoezi mara nyingi.”

"Nimemfanyia baba yangu hapo awali." Alissa alijua kuwa Kendrick anamaanisha nini. Alitaka kujua alikuwa amefunga mahusiano kwa ajili ya nani.
Alissa akachukua tena koti la suti na kumvisha. Sasa, Kendrick alikuwa mzuri.

“Twende zetu.” Walishuka chini.

Kifungua kinywa kilikuwa tayari. Baada ya kifungua kinywa, Kendrick alitoka na Alissa.

"Unarudi Geita?" Alissa aliuliza. Vinginevyo, kwa nini alivaa rasmi?

Ikiwa angeondoka Mwanza, kungekuwa na ahueni kwa familia ya Jabo?

Lakini Alissa aliweza kuliweka hilo akilini mwake na hakuthubutu kumuuliza.

“Bibi amekuomba uwasemee. Nisipokubali, namuaibisha bibi.” Kendrick alinyoosha mkono na kusugua pua yake, "Najua unafikiria nini."

Alissa aliunganisha ncha za vidole vyake na kukunja midomo yake huku akitabasamu.

“Haya. Nitakupeleka kazini kwanza.” Kendrick akaliendea gari, huku mkono wake ukizunguka begani mwake.

"Nitaenda kazini mwenyewe." Lilikuwa jambo dogo angeweza kulisimamia peke yake.

Tayari dereva alifungua mlango wa gari na kusubiri.

Kendrick alimshika mkono na kumtaka aingie ndani,

“Hakuna haja. Nitamtaka Chale aendeshe gari lako hadi kwenye kampuni yako.”

Baada ya kuketi, dereva akawasha gari.

Kendrick alimshika mkono Alissa na hakuuachia njia yote.

Alissa hakutaka kutambulika, alimtaka Kendrick kuegesha kando ya barabara kisha akaendesha gari lake hadi kwenye maegesho ya kampuni.

Kendrick alimwambia dereva kwa upole, "Nenda kwa kampuni ya familia ya Jabo."

Walipofika huko, Kendrick alitangulia mbele. Chale na wengine wakamfuata nyuma. Walikuwa na hadhi ya juu na walionekana wanyenyekevu.

Ambapo alienda, kila mtu aliacha na hakuthubutu kumkosea.

"Bwana Kendrick anataka kumuona Mark, bosi wako.” Chale alikwenda mbele kuzungumza na mhudumu wa mapokezi.

Msichana huyo alipiga simu mara moja ofisi ya bosi. Dakika sifuri tu, Mark alikuja kukutana na Kendrick kibinafsi.

Mark alishangaa na kufurahi kumuona Kendrick akija hapo ana kwa ana. Alijaribu kuwa mtulivu.

“Bw. Kendrick, habari za asubuhi."

"Hebu tuache salamu za heshima na twende juu tuzungumze." Kendrick alisema.

Mark alifanya ishara ya mwaliko na kuchukua lifti ya kipekee na Kendrick.

“Twende kwenye chumba cha mikutano.” Baada ya kutoka kwenye lifti, mahali alipokuwa Kendrick alikuwa wazi.

Kampuni ya Jabo Cotton Mills, mali ya familia ya Jabo, ambayo ilihusika na kuchambua pamba na kusindika mafuta ya pamba, ilikuwa na kikao cha dharura cha bodi siku hiyo. Mark alikuwa akikutana na wakurugenzi sasa hivi.

Kendrick alipoingia kwenye chumba cha mkutano, hali ilizidi kuwa kali. Wakurugenzi wote wenye wasiwasi na hofu walisimama, “Bw.
Kendrick.”

Kendrick akawaashiria wakae chini. Kisha, yeye pia akaketi na Chale akasimama nyuma yake wima.

"Nitaongea kifupi." Kendrick alimpa Chale ishara nyuma yake.

Chale akasonga mbele. Akiwa msemaji wa Kendrick, alisema, “Maadamu Bw. Timothy, Makamu wa Mkurugenzi wa JCM Ltd (Jabo Cotton Mills), na wazazi wake wanaondoka kwenye nyadhifa zote za kampuni, na kamwe hawatoshiriki katika usimamizi wowote wa Kampuni, na hawashiki nyadhifa zozote, na Kampuni ya JCM inachukuliwa na Bw. Mark, basi mgogoro wa Kampuni hiyo utaondolewa.”

Hilo ndilo lilikuwa sharti la Kendrick. Alimradi washiriki Timothy na wazazi wake wangelipia gharama kwa kung'atuka, Kampuni ingeweza kuokolewa.

Kwa kweli, hali hii haikuwa ngumu. JCM na maslahi ya wakurugenzi hayakuharibiwa.

Yeyote ambaye alikuwa na kichwa wazi angechagua kumtoa Timothy ili kuokoa kampuni.

Mark pia alifikiri kwamba Kendrick alikuwa mpole na Timothy alistahili. Alipaswa kuongoza katika kukubali pendekezo hilo.

Mark alipokuwa anaenda kuzungumza, mlango wa chumba cha mkutano ulisukumwa na Bi Jabo akasaidiwa kuingia.

Mark aliharakisha kwenda mbele ili kumsaidia, “Bibi, mbona uko hapa? Kwanini usikae hospitalini? Wewe….”

"Sijambo na sitakufa bado." Bi. Jabo alisimama mbele ya meza ya mkutano kwa kutazama kwa umakini, “Sasa, sote tunaweza kuona mgogoro wa Kampuni yetu. Tunapaswa pia kuelewa ni nani anayeweza kuongoza Kampuni kwenye njia sahihi. Napendekeza kumwondoa Timothy kwenye wadhifa wake wa Makamu wa Mkurugenzi na wazazi wake kwenye bodi ya wakurugenzi na kuwataka wajiondoe kwenye bodi. Pia ninapendekeza kwamba Mark awe Mwenyekiti wa Bodi. Tupigie kura.”

Kama mbia muhimu wa Kampuni, na Timothy alikuwa mjukuu wake mwenyewe, Bi. Jabo alikuwa mtu bora zaidi kutoa pendekezo.

Kwa hivyo, bodi ilipiga kura kwa kunyoosha mkono na kura ya kauli moja ikapigwa.
Hili lilitarajiwa na Kendrick na aliridhika sana.

Kendrick alipoona matokeo, aliinuka kwenye kiti na kubandika suti yake kidogo kwa mkono mmoja, “Bi. Jabo, basi nitaondoka.”

"Bwana. Kendrick, nitakuona binafsi.” Bi Jabo alisisitiza kuonana naye.

Kendrick hakuweza kukataa na kumheshimu mwanamke mzee.

Mark alimsaidia Bi Jabo na kuchukua lifti chini na Kendrick.

"Bwana Kendrick, asante." Bi Jabo alisema.

Kendrick aliweka tabasamu hafifu, “Unamaanisha nini Bibi Jabo? sielewi.”

Sura ya 186

Kendrick alishughulika na familia ya Jabo kwa sababu tu Timothy alimdhulumu Alissa. La sivyo, asingemjali Timothy.

“Timothy ni mjukuu wangu mdogo. Baba yake ndiye mwanangu wa mwisho. Yeye na wazazi wake ni mizigo tu katika familia na Kampuni. Lakini ana nguvu kubwa ndani ya Kampuni na akafanikiwa kumkandamiza Mark. Kwa hakika, kwa sababu ya kazi ngumu ya mume wangu ana mwana wangu mkubwa waliokufa, pamoja na binti-mkwe wangu, kampuni hii imefikia kiwango na mafanikio yake ya sasa.”

Bi Jabo alihuzunika alipokuwa akizungumza, “Kampuni inabidi irithiwe na Mark. Lakini mwanangu mdogo hana dhamiri. Ili kujinyakulia mamlaka kwa ajili yake mwenyewe na mwanawe, anamfanya Mark kuwa kielelezo tu. Sasa, bado niko hai. Nikifa, sijui watamfanyia nini Mark.”

"Hawawezi kushikilia Kampuni kwa miaka michache. Kwa kuwa sasa mmeweka kampuni hii hatarini, naweza kuchukua nafasi hiyo kuwalazimisha wakurugenzi wakubali kuwatimua Timothy na wazazi wake. Kisha, Kampuni hatimaye inaweza kuwa na utulivu."

"Bwana Kendrick, unatupa njia ya kutoka. Kwa hivyo, ninataka kukushukuru sana kwa kunisaidia kumpatia Mark nafasi hii. Tutachukua wema wako kwa moyo. Ikiwa kuna jambo lolote tunaloweza kusaidia katika siku zijazo, tuambie tu na tutajitahidi tuwezavyo.”

"Bi. Jabo, usitaje. Unapaswa kujua kwamba ninafanya hivi ili mke wangu apate haki.” Kendrick hakuwa na nia ya kuwasaidia. Lakini ilikuwa sahihi zaidi kwake kumwacha Mark apate nafasi hiyo.

Na Mark alikuwa mtu wa tabia bora. Kendrick aliamini kwamba hatamhukumu vibaya Mark. Ikiwa Mark alikuwa anasimamia Kampuni ya Jabo, isingemletea matatizo zaidi.

Ingawa Kendrick hakuogopa kufanya maadui katika biashara, rafiki mmoja zaidi alikuwa bora kuliko adui mmoja zaidi.

"Ingawa unapata matokeo chanya bila kukusudia, bado wewe ni mfadhili wangu na Mark." Bibi Jabo alishukuru.

"Sasa, inaonekana kuwa mwisho bora." Kendrick alisema.

Bi Jabo alimtazama Mark, mjukuu wake. Macho yake yalijawa na upendo na matarajio, “Ninahisi kutulia kwa kuwa Mark ndiye anayesimamia Kampuni. Ninapokufa, ninaweza kumwona mume wangu na mtoto wangu mkubwa. Mark, kumbuka wema huu na uongoze Kampuni vyema."

“Bibi … siogopi chochote watanifanyia. Utaishi maisha marefu. Inatosha mimi kuwa na wewe kando yangu.” Mark alikuwa na tamaa. Lakini ikilinganishwa na tamaa, alimpenda bibi yake na familia ya Jabo zaidi. Hakutaka kumweka Bibi Jabo katika hali ya kutatanisha, “Itakuwa sawa hata nikiacha kweli Kampuni na kuwa mfanyakazi wa kawaida wa ofisi. Labda basi tutakuwa na furaha zaidi."

“Kijana mjinga. Hii ni kampuni ambayo babu yako na wazazi wako waliokufa wamejitahidi kuianzisha. Ukiruhusu baba yako mdogo na Timothy wachukue nafasi hiyo, kampuni itaangamizwa siku moja. Unawezaje kukabiliana na babu yako na wazazi wako?" Bibi Jabo alinyoosha mkono na kumpigapiga begani, “Kuanzia sasa, utawajibika kwa familia na Kampuni. Unahisi shinikizo?"

“Ndiyo.” Mark alitikisa kichwa, “Hakuna motisha bila shinikizo. Nitajitahidi."

“Nzuri.” Bi Jabo alifarijika na kutabasamu, “Mark, ukiwa na jambo ambalo huelewi mbeleni, muulize bwana Kendrick akupe ushauri. Ingawa Bwana Kendrick ni mdogo kwako, ana uzoefu na uwezo zaidi kuliko wewe.”

"Tafadhali nikubalie kwa maagizo yako, Bwana Kendrick." Mark alikuwa mwenye kiasi.

“Usiseme, Bwana Mark. Ninaamini kuwa umekandamizwa na pande zote kwa miaka mingi kwenye Kampuni na haujaweza kutoa uwezo kamili kwa nguvu zako. Unapoingia madarakani, bila shaka utaweza kufanya makubwa na kupata kile unachotaka.” Maneno ya Kendrick pia yalikuwa ni kukataa kwa kishindo. “Mbali na hilo, bado kuna Bibi Jabo ambaye anampa Mr. Mark ushauri. Haitakuwa zamu yangu kukupa ushauri.”

Kendrick hakuwa tayari kutoa ushauri. Lakini Mark hakuwa Timothy, mpotovu. Mark alikuwa na uwezo wa kutosha. Alichokosa ni nafasi tu.

Sasa kwa kuwa alipata nafasi hiyo, Mark, ambaye amekuwa akisitasita kwa miongo kadhaa, bila shaka angeweza kuwa na njia nyingi.

"Asante Bwana Kendrick hata hivyo." Bi Jabo hakumlazimisha.

"Bi. Jabo, Bwana Mark, basi nitaondoka sasa hivi.” Kendrick aligeuka kuondoka.

Chale alimfuata nyuma na alikuwa msaidizi wake hodari.

Bi Jabo alipoona Kendrick anaingia kwenye gari, akamwambia Mark, “Kwa bahati nzuri, miadi yako ya uchumba na Alissa iliharibiwa. Vinginevyo, ninaogopa kwamba tusingeweza kuendelea na Kampuni hii leo.

“Bibi, Alissa anastahili kupendwa sana na bwana Kendrick. Tusitaje tena kilichotokea kati yangu na Alissa.” Mark aliona ni bora kwao kusahau kuhusu hilo.

“Ndiyo.” Bibi Jabo alifarijika, “Mark, miaka hii, kwa sababu ya biashara ya kampuni, hujafunga ndoa katika miaka ya thelathini. Sasa kwa kuwa utachukua Kampuni, unaweza kuwa na utulivu katika siku zijazo."

"Bibi, hali kwa ujumla haijulikani. Siwezi kuzama katika mapenzi.” Mark alimtuliza Bi. Jabo, "Tutalizungumza baadaye tukipata nafasi."

Kendrick aliondoka kwenye Kampuni ya JCM na kumtaka dereva aendeshe hadi uwanja wa ndege.

Hakupaswa kuja Mwanza, lakini alikuja kwa ajili ya Alissa. Ilikuwa ni wakati wa yeye kurudi.

Ilikuwa ya kuchoka kusafiri kati ya maeneo hayo mawili. Lakini alikuwa na furaha.

Kendrick alikaa kwenye sebule ya watu mashuhuri na alikuwa anataka kumpigia simu Alissa mara Alissa akampigia kwanza.

“Mark aliniambia kuhusu Kampuni yao. Asante mpenzi.” Alissa alishukuru, “Alisema angekualika kwenye chakula cha jioni wakati ujao ikiwa kuna nafasi.”

"Hakuna haja." Kendrick alikataa moja kwa moja.

“Basi nitakupikia usiku wa leo. Ungependa kula nini? Nitanunua nikitoka kazini.” Alissa alifikiri angeweza kupika mwenyewe.

“Nilikuwa naenda kukuambia kuwa nipo uwanja wa ndege. Lazima nirudi Geita leo."

Kendrick alikusudia kukutana naye kabla hajaondoka. Lakini alipofikiria kuwa yuko bize na kazi, hakutaka kumsumbua.

“Unarudi?” Alissa alishangaa kisha akahisi kukata tamaa.

“Unachukia kuachana nami?” Kendrick alisikia dokezo la kukatishwa tamaa kwa sauti yake.

"Wewe fanya kazi kwa amani." Alissa aliifanya sauti yake kuwa angavu zaidi, “Pia nitafanya kazi vizuri. Usijali kuhusu mimi.”

Kendrick alitabasamu kidogo, “Bi. Mayala anajali sana. Lakini unajua umefanya kosa gani?"

Alissa hakujua alichokuwa amefanya au kusema vibaya, “Sielewi.”

"Je, kweli huna uhusiano wowote na Mark?" Kendrick aliitaja tena.

“Ndiyo.” Alissa alikuwa na uhakika.

"Bibi alikuwa amewakutanisha nyie wawili." Kendrick alijua kuhusu hilo. Hakuiweka wazi mara ya mwisho.

Alissa aliuma mdomo wake kwa upole, "Lakini hatukukutana."

“Ndiyo. Anapaswa kufurahi kwamba Timothy alichukua nafasi hiyo mbali naye. Vinginevyo...” Kendrick hakumaliza alichotaka kukisema. Lakini alichomaanisha kilikuwa dhahiri.

“Imekuwa muda mrefu. Bwana Kendrick usiwe mkali sana.” Alissa alipiga kelele.

"Nisingeenda kwenye Kampuni yao leo kama ningekuwa mbaya." Kendrick alihisi kwamba alikuwa mkarimu sana kumsaidia “mpinzani” wake kutwaa mamlaka. “Lakini ninapofikiria kwamba ulikaribia kupatana naye uchumba, mimi bado sina furaha.”

Sura ya 187

Alissa alihisi kuwa Kendrick ni mtoto sana wakati akiongea haya.
"Bwana Kendrick, mimi tayari ni wako. Kwa nini huna furaha?” Alissa alijaribu kutokuwa na haya sana na kusema.

"Bi. Mayala ana mdomo wa asali." Kendrick aliridhika sana na maneno yake na hakumwaibisha tena, "Nitapanda ndege."

"Sawa. Nitakupikia wakati mwingine ukirudi.” Alissa naye akajisikia raha sasa.

Ikiwa wangeendelea na mada ya uchumba wake na Mark, angefadhaika.

"Wakati mwingine nitakaporudi, nataka kula wewe kwanza, kisha chakula cha jioni." Kendrick alitabasamu vibaya na alichokiongea kilimfanya Alissa aone aibu.

"Nipigie ukifika Geita. Bye." Alissa alikata simu kwa haraka.

Alijikaza kifuani na kuhisi moyo wake ukidunda kwa nguvu.

Kendrick alikuwa busy sana na kazi. Alikuwa amechelewa pale Mwanza. Je, angekuja lini tena?

Japo alikuwa na biashara nyingine kubwa hapo Mwanza, biashara ya dhahabu huko Geita ndiyo aliisimamia kwa karibu zaidi. Isitoshe, ikiwa angeendelea kuiacha kampuni hiyo na kuja Jiji Mwanza kila saa, ingechukuliwa kuwa janga na watu wa Nyanza Gold.

Mungu! Afadhali amalize kazi yake hapa haraka iwezekanavyo na kumpeleka Doris hadi Geita. Kisha, si tu kwamba angeweza kumtunza, lakini pia ingemruhusu kufanya kazi kwa urahisi.

Alissa alifanya uamuzi wake tena.

Shule hiyo ya chekechea ilifungwa saa moja mapema siku hiyo mchana. Alissa alimuomba Nora amchukue Doris kisha wapate chakula cha jioni pamoja.

Alissa alienda kwenye Mgahawa wa Nearby baada ya kazi kulingana na anwani ambayo Nora aliyotuma. Mgahawa huu ulikuwa wa Nora.

Mgahawa ulikuwa katika mtindo wa kifahari, na mapambo ya kipekee na tani za retro. Ulilipewa kipaumbele kikubwa kwa mpangilio wa nafasi. Kwa hivyo, ilionekana kung'aa na inaweza kuwafanya watu wastarehe.

Alissa alifika pale na kusema ni rafiki wa Nora. Kisha, mhudumu akamchukua kuwatafuta.

Nora alikuwa tayari amemuagizia Doris viazi vilivyokaangwa.

“Mama.” Doris aliuliza baada ya kumuona Alissa amekaa, “Baba yuko wapi?”

"Amerudi Geita kwa kazi." Alissa alinyoosha mkono na kukipapasa kichwa cha bintiye, “Baba yuko bize sana na kazi. Kwa hiyo, tujaribu kutomkatisha kazini, sawa?”

“Nimefikiri Baba angeweza kukaa nami wakati wote mara wewe na Baba mtakapooana ..." Doris alikata tamaa. Alikuwa na furaha kwa siku mbili tu!

"Baada ya mama kumaliza kazi, tunaweza kuhamia Geita ili kuwa na Daddy. Kisha, Baba anaweza kuja nyumbani ili kuwa nawe mara tu anapotoka kazini, sawa?” Alissa alimweleza Doris kuhusu uamuzi wake, akitumaini kwamba Doris angeweza kuwa na furaha.

"Basi hatutatengana tena, sawa?" Macho ya Doris yaliangaza sana.

“Ndiyo.” Alissa alitabasamu kidogo.

“Sawa.” Doris alipiga mkono mdogo wake kwa furaha.

Kumtazama binti yake mwenye furaha na msisimko, Alissa alihisi kwamba hayo yalikuwa maisha mazuri.

Alichoagiza Nora hapo awali kilitolewa. Doris alikula mboga zaidi na minofu ya samaki kabla ya kwenda kucheza kwenye uwanja wa michezo wa watoto kwenye mgahawa huo, ambapo kulikuwa na mtu wa kuwatunza watoto.

“Unataka sana kwenda Geita na Doris?” baada ya Doris kuondoka, Nora alithibitisha tena.

“Ndiyo.” Alissa alichukua juisi yake, “Kwa kuwa tumeamua kuchukulia ndoa yetu kwa uzito, si wazo zuri kwetu kuishi mbalimbali. Pia si nzuri kwa Doris.

“Ndoa nzuri ni ile ya watu wawili kuvumiliana na kujaliana. Mmoja wetu anapaswa kufanya makubaliano. Tayari amenilipa pesa nyingi. Kwa hiyo, ni zamu yangu kutoa wakati huu.” Alissa alikuwa tayari na amedhamiria.

“Nyinyi wawili…” Nora aliweka vidole vyake viwili vya shahada pamoja na kutabasamu kwa utata.

“Wacha tule.” Alissa aliona haya na kukwepa mada, akihofia Nora angejihisi mpweke sana na kumuonea husuda.

"Inaonekana Bwana Kendrick amepata anachotaka." Nora alijua kutokana na usemi wa Alissa kwamba wawili hao walikuwa wamelala pamoja, “Hongera sana.”

“Sawa.” Alissa alimkazia macho kwa upole, “Unaongea sana.”

"Nina furaha tu kwa ajili yako." Simu ya mkononi ya Nora iliita, "Lazima nipokee simu." Nora aliinuka kwa umaridadi.

Alissa alimtazama. Nora alivalia sketi ya kukunja iliyomwaga. Miguu yake mirefu ilikuwa myeupe na ya kupendeza. Alikuwa na umbo la ajabu na alikuwa mrembo sana. Alikuwa mzuri kama waridi jekundu lililochanua kabisa.

Kwa wakati huu, mwanamke mmoja alikaribia na kumtazama Alissa kwa muda kabla ya kusema, "Alissa?"

Alissa alitazama pembeni na kugeuka kumwangalia yule mgeni. Alikuwa mama wa Seidrick, Maira.

Alissa hakutarajia kukutana na Maira hapo. Yeye mara chache alikula nje. Ni sadfa iliyoje!

Alissa aliganda kwa sekunde moja tu kabla hajaweka tabasamu zuri, “Bi. Masolwa, habari yako?"

Maira alishangaa sana baada ya kusikia anwani ya Alissa. Alissa alikuwa akimwita Maira kwa upendo.

“Naweza kuzungumza nawe?” Sauti ya Maira ilikuwa ya upole kama zamani.

"Kaa chini ikiwa haujali." Alissa hakuweza kukataa.

“Sawa.” Maira aliketi na kutazama uso wa Alissa kwa makini kwa muda, “Je, unakula chakula cha jioni na marafiki zako?”

“Ndiyo.” Alissa akaitikia kwa kichwa, “Anapokea simu.”

“Naona.” Maira aliinua midomo yake na kuonekana mwenye haya, “Marafiki zako ni na nani? Ni mwanaume au mwanamke? Nina hamu tu. Unaweza kukataa kujibu.”

"Nora Mabala," Alissa alisema waziwazi, "mwanamke mchanga wa familia ya Mabala. Bibi Masolwa anapaswa kujua.”

"Kwa hivyo ni Miss Mabala? Najua ni rafiki yako mkubwa.” Maira alikunja ngumi na alikuwa na woga kidogo. Kulikuwa na ladha ya kupotea kimawazo katika macho yake.

"Bi. Masolwa, uko sawa?" Alissa aliuliza.

“Sijambo.” May akashusha pumzi ndefu, “Alissa, kama huna shida, bado unaweza kuniita Maira kama hapo awali. Unaponiita Bibi Masolwa ... inaonekana sisi ni wa ajabu sana.”

“Lakini nadhani inafaa zaidi mimi kukuita Bibi Masolwa sasa. Baada ya yote, Melissa ni binti-mkwe wako sasa. Na mwanao… Hawatataka kunisikia nikikuita Maira,” Alissa alisema, akifikiri ingefaa wawe mbali watakapokutana tena baada ya miaka mitano.

"Alissa, samahani." Maira alihisi kufadhaika alipomtazama msichana huyo mjinga ambaye alikuwa amekomaa na thabiti baada ya kuwa na wakati mgumu, “Hapo zamani, ni mimi niliyekusihi umuokoe Seidrick. Lazima ulikuwa unatafuta njia. Iliwezekanaje ulikuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume wengine?"

"Kwa hivyo, sikuamini kuwa utamsaliti Seidrick. Sielewi kwanini ulijifungua mtoto kwa siri. Unaweza kuniambia nini kilitokea wakati huo?”

Sura ya 188

Alissa alishangaa na kutulia mara aliposikia Maira akichukua hatua ya kutaja kilichotokea miaka mitano iliyopita.

Maira alisema kwamba alimwamini. Alissa alijua kuwa Maira alikuwa mkweli. Aliweza kuona hatia na aibu machoni pake.

“Si lazima uombe msamaha. Kila kitu kilikuwa kimeenda na niko sawa sasa.” Alissa hakutaka kutaja yaliyopita, “Na ninashukuru uliniamini.”

Lilikuwa ni kovu. Kila alipokuwa akiyataja, ilikuwa ni kana kwamba alikuwa akipasua tena majeraha yake.

Na hata kama alisema, ilikuwa muhimu? Bila ushahidi, nani angemwamini? Sasa kwa kuwa Maira alikuwa mama mkwe wa Melissa, ikiwa kweli alisema, ingeonekana kuwa alikuwa akimtenga Maira kutoka kwa Melissa.

"Nimefurahi kusikia kuwa haujambo." Alipoona kwamba Alissa hakutaka kuzungumzia mambo yaliyopita, Maira alibadili mada na kuzungumzia jambo lingine, “Je, umeolewa sasa?”

Siku ya karamu Maira alienda kwenye chumba cha watu mashuhuri kwa sababu alikuwa na kizunguzungu. Kwa hivyo, hakujua kilichotokea nje.

“Ndiyo.” Alissa alisema kwa uwazi.

“Yeye ni mwanaume wa aina gani? Lazima anakupenda sana, sawa?" Uso wa Maira ulikuwa na wasiwasi, kana kwamba Alissa alikuwa binti yake mwenyewe.

Maira alikuwa akimchukulia Alissa kama binti yake. Lakini, hakutarajia kitu kama kile kilichotokea miaka mitano iliyopita kuharibu uhusiano wao.

"Hajali maisha yangu ya zamani na kwamba nina mtoto wa kike. Pia anamchukulia binti yangu kana kwamba ni mtoto wake mwenyewe. Anatoa zaidi tunapokuwa pamoja. Lakini halalamiki kamwe.” Alissa alipomzungumza Kendrick, uso wake ulikuwa na furaha.

Aliposikia hivyo, Maira alifurahi kwa ajili yake, “Kwa kweli huyo ni mtu mzuri.”

"Kwa hiyo, nataka tu kushikilia furaha niliyo nayo sasa. Hakuna kitu kingine muhimu kwangu." Alissa alihisi maumivu yote aliyoyapata hapo awali yametulizwa kwa upole na Kendrick.

“Alissa, nimefarijika kukuona ukiwa na furaha. Ni Seidrick ambaye hakustahili wewe. Ni familia ya Masolwa ambayo inakuomba radhi.” Maira alijihisi kuwa na hatia, “Natumai hutuchukii.”

"Bi. Masolwa, si ni vizuri kwamba Seidrick yuko na Melissa sasa? Melissa alipata ujauzito wa mtoto wa Seidrick. Wana furaha pia.” Alissa alibaki akitabasamu kana kwamba anatamani kwa dhati.

Maira hakujibu akaitikia kwa upole tu.

“Mume wako yuko wapi? Si alikusindikiza leo?” Maira alimtaja tena mume wa Alissa.

"Alirudi Geita mchana huu kwa ajili ya kazi." Alissa alikuwa amekauka mdomo na akanywa maji machache ya ili kulainisha koo lake lililokauka, “Anatoka Geita”

“Geita?” Maira alikunja uso aliposikia Geita, “Anatoka Geita? Basi, lazima amfahamu Bw. Kendrick. Nimesikia kuwa wewe na bwana Kendrick mnafahamiana kwa sababu ya kazi zenu.”

“Mume wangu si mwingine bali ni Kendrick.” Alissa hakuficha chochote.

Maira, hata hivyo, aligeuka rangi na kugonga glasi ya maji mbele ya Alissa. Maji yalishuka kwenye meza na kudondoka kwenye sketi yake. Lakini alionekana kutoliona hilo na akabaki kimya.

"Bi. Masolwa.” Alissa alipoona hivyo alimuita mara mbili mbili na kuchukua kitambaa kujifuta maji.

Maira alirudi kwenye fahamu zake. Lakini uso wake ulikuwa bado umepauka na hata kupumua kwake kulikuwa na uzito kidogo.

"Uko salama?" Katika kumbukumbu ya Alissa, Maira daima alikuwa wa kifahari na mtulivu. Hakuwahi kupoteza utulivu kama alivyofanya.
"Samahani. Ninahisi mgonjwa kidogo." Maira aliona kwamba pembe za paji la uso wake zikiuma tena.

Alissa alimuangalia Maira, akakumbuka kuwa pale mapokezi siku hiyo Maira alikuwa na kizunguzungu na kujisikia vibaya aliposikia jina la Kendrick. Hata alijikwaa na karibu kuanguka.

Kwa nini Maira alijisikia vibaya sana aliposikia jina la Kendrick? Je, kulikuwa na uhusiano au tatizo lolote kati yake na Kendrick? Binafsi hakuona uwezekano. Familia ya Masolwa haikuwahi kuingiliana na familia ya Mayala ya Geita kwa miaka mingi sana.

“Unamfahamu Kendrick?” Alissa alimuuliza Maira.

"Familia ya Mayala ya Geita ni maarufu sana. Nimesikia tu habari zake… lakini simjui.” Maira alinyoosha mkono kusugua pembe za paji la uso wake ili kupunguza maumivu huku akivuta pumzi ndefu ili atulie, “Labda nitakuomba uwe mtambulishaji baadaye, Alissa.”

Kadiri alivyozidi kusema ndivyo alivyozidi kushtuka. Midomo yake ilikuwa imepauka.

“Huonekani vizuri sana. Afadhali nikupeleke hospitali.” Alissa alinyanyuka na kumshika Maira kwa kuhofia ajali.

“Hapana … hakuna haja…” Maira alipomaliza kusema tu alizirai, akiegemea mikononi mwa Alissa.

Alissa alikuwa na wasiwasi Nora aliporudi. Nora alishtuka kumuona Maira,

“Mbona yuko hapa? Nini kinaendelea?”

"Alizimia." Alissa alikunja uso, “Nora, nenda ukaendeshe gari. Tumpeleke hospitali.”

“Alissa, ni mama yake Seidrick. Seidrick na Melissa walikufanyia nini? Yeye pia anatoka kwa familia ya Masolwa ... usiwe na moyo laini na mtu mwenye shughuli nyingi. Wengine wanaweza kufikiri kwamba una nia mbaya.” Nora hakupenda watu wote wa familia ya Masolwa na pia alikasirika kuwa Alissa alikuwa na moyo laini.

"Maira amekuwa na afya mbaya kila wakati. Maisha ya mwanadamu yana thamani kubwa kuliko kila kitu. Nenda haraka, sawa?" Alissa alimsihi na kumsihi Nora.

Nora alisitasita sana kugeuka ili kuchukua gari. Alissa alimuomba mhudumu amwite Doris, kisha akamsaidia kumbeba Maira hadi kwenye gari la Nora.

Hospitali ya karibu ilikuwa umbali wa dakika kumi tu. Muda si mrefu, walifika na Maira akapelekwa kwenye chumba cha dharura.

Nora alimaliza taratibu za kuingia hospitali akaja huku akiinua bili mkononi mwake, “Nimekushangaa sana! Msichana mjinga!”

"Mairs amekuwa mzuri kwangu kila wakati. Lakini yeye ana utambulisho wake mwenyewe na msimamo. Kuna baadhi ya mambo hawezi kufanya uamuzi. Nitakuhamishia hizo pesa.” Alissa alifikia bili wakati Nora alipomkabudhi.

“Kila deni lina mdaiwa wake. Sio pesa nyingi, lakini haipaswi kulipwa na sisi." Nora alimkataa, ikiwa tu Alissa angefanya jambo la kijinga.

Walisubiri kwa muda kabla ya Sam na Seidrick kufika kwenye chumba cha dharura. Walishangaa walipowaona Alissa na Nora.

Sam alikunja uso na Seidrick akaminya midomo yake.

Kabla hawajazungumza chochote, pazia la kitanda cha dharura lilifunguliwa. Waliharakisha kwenda mbele na kumuuliza daktari, "Daktari, vipi mke wangu (mama)?"

"Yuko sawa. Alizimia kwa sababu alikuwa dhaifu na alishindwa kudhibiti hisia zake. Mwacheni apumzike vizuri, na umapate lishe bora na mazoezi.” Daktari alishauri, "Anaweza kwenda nyumbani wakati IV yake imekamilika."

“Asante daktari.” Sam na Seidrick walisema.

Maira alihamishiwa kwenye chumba cha kuwekea dawa na nesi na Sam na Seidrick walikuwa karibu kufuata.

Nora alisonga mbele na kuwazuia njia, “Bw. Sam na Bwana Seidrick hata hamuonyeshi shukrani zenu?”

"Asante, Bi Nora." Wawili hao walisema.

"Siko tayari kupokea shukurani za mtu mwingine. Ukitaka kumshukuru mtu, mshukuru Alissa tu.” Ilikuwa dhahiri kwamba Nora alikuwa akijaribu kusababisha matatizo.

Sura ya 189

Nora alifanya hivyo kwa sababu alitaka kumtetea Alissa. Alikuwa akijaribu kuwaaibisha wanafamilia ya Masolwa, haswa Seidrick, ambaye alikuwa mchafu machoni pake.

Kwa vile Nora alikuwa amesema hivyo, Alissa hakumzuia. Alimuokoa Maira. Sam na Seidrick walipaswa kumshukuru.

Kusikia alichosema Nora, sura za Sam na Seidrick zilibadilika kana kwamba wamemeza nzi.
“Asante Bi Alissa.” Hawakuwa na chaguo ila kutoa shukrani zao, hata kama hawakutaka kukabiliana na hali halisi.

Lilikuwa jambo dogo kwao kutoa shukrani zao. Kilichokuwa muhimu ni kwamba wana deni la upendeleo kwa Alissa. Madeni yanayohusisha pesa yalikuwa rahisi kulipa ilhali madeni ya shukrani yalikuwa magumu kuyalipa.

Sasa, walikuwa na deni kwa yule ambaye hawakumpenda zaidi. Kwa hiyo, walikasirika kidogo.

“Inaonekana Bw. Sam na Bw. Seidrick si waaminifu. Kwa kuwa nyinyi watu mnasitasita kunishukuru, basi msifanye hivyo.” Alissa alidhihaki.

Hakuwa na nia ya kujisumbua kubishana na watu kama Sam na Seidrick na kuwalazimisha kumshukuru. Lakini alikuwa mfadhili wa Maira hata hivyo. Hata kama hawakumpenda, hawapaswi kuwa katika mtazamo kama huo kwa mtu aliyeokoa familia yao.

"Nani alisema kuwa watu kutoka kwa familia ya Masolwa ni wakarimu? Inaonekana kutiliwa chumvi.” Nora alisema kwa kejeli.

Sam alikunja uso. Kwa kuwa walikuwa hospitalini, hakusema chochote.

Seidrick pia aliweka uso wa baridi, "Bi. Alissa, ningependa kukushukuru kwa ajili ya mama yangu. Asante kwa kumuokoa. Tuna deni kwako. Kadiri tunavyoweza kufanya hivyo, tutatimiza ahadi yetu.”

“Sawa. Nitakumbuka ahadi yako na kwa hakika sitairuhusu iwe ya midomo, Bwana Seidrick.” Alissa alikubali kwa furaha, “Tafadhali usisahau ulichosema leo.”

Alissa alijua Seidrick alitaka tu kurudisha fadhila. Hakutaka kumdai wala kujihusisha naye.

“Mimi ni shahidi.” Nora alinyoosha mkono na kuweka mkono wake kwenye bega la Alissa, "Nitakumbuka kwa Bwana Seidrick."

"Mimi ni mtu wa neno langu." Seodrick alikuwa baridi na shwari. Hakuwa mpole tena kama ilivyokuwa awali, alitengwa na Alissa.

"Kisha tafadhali ulipe ada ya mashauriano ya matibabu kwanza, Bw. Seidrick." Nora akasonga mbele na kutoa bili alizokuwa amemaliza kulipa.

Seidrick alinyoosha mkono na kuchukua bili, akitazama kiasi, "Nitahamisha pesa kwenye akaunti ya Bi Nora baadaye."

“Siyo pesa nyingi. Unaweza kunihamishia tu kwenye mpesa.” Nora akatoa simu yake.

Seidrick kisha akatoa simu yake ili kumuongezea akaunti, kisha akamkabidhi pesa hizo.

“Sawa, hatuna la kufanya zaidi. Twende sasa.” Nora kwa umaridadi aliweka simu na kuchukua mkono wa Alissa.

Alissa kisha akatoka hospitali na Nora. Seidrick aliwaandalia maumbo yao yakitoweka.

Nora na Alissa walikwenda kwenye maegesho, “Chakula chetu kilikuwa kinasumbua. Bado sijashiba. Kwa nini tusije kula nyama choma na kunywa bia?”

“Hutaki kuweka sura yako nzuri? Ni kuchelewa sana. Bado unataka kulewa?" Alissa alishangaa.

Baada ya yote, Nora alikuwa mwenye nidhamu na hakula chochote isipokuwa milo mitatu kwa siku.

“Niko katika hali nzuri sana. Ni sawa kujifurahisha mara moja moja.” Nora aliingia ndani ya gari na kufunga mkanda wake wa usalama, akisema, “Hata hivyo, tayari ulikuwa na mtu kumrudisha Doris kwenye kwa familia ya Maziku kwanza. Kwa hiyo, huhitaji kuwa na haraka ya kwenda nyumbani.”

“Sihitaji kuwa na haraka kwenda nyumbani. Lakini nashangaa kwa nini ghafla unataka kunywa pombe.” Alissa akainama nyuma na kuegemeza paji la uso wake kwa mkono mmoja.

Nora alicheka kwa furaha, “Nyuso za Sam na Seidrick sasa hivi zilikuwa na huzuni sana. Je, hatupaswi kusherehekea?”

Alissa alitabasamu kwa unyonge, “Je, hili ni jambo la kusherehekea?”

Alichungulia dirishani na kuwaza kama Seidrick angejua ukweli miaka mitano iliyopita na alijua kwamba ana deni lake la maisha, uhai wake…
Kwa tabia yake, angempa maisha yake?

“Njoo.” Ingawa Nora alikuwa akimshauri Alissa, alikuwa ameendesha gari kuelekea baa moja karibu na mgahawa wake.

Gari la Nora jekundu la Porsche 911 la michezo linaloweza kubadilishwa lilivutia umati mara tu alipoegesha mbele ya baa hiyo.

"Je! tunahitaji kuwa wastaarabu sana hadi baa?" Alissa alihisi woga kidogo alipoona umati wote ukiwatazama.

Hakutaka kuwa wa juu sana. Alihisi kuwa watu walikuwa wanawashangaa tu.

“Waache wafanye wanavyotaka. Tunajifurahisha wenyewe.” Nora moja kwa moja akausukuma mlango wa gari na kushuka kwenye gari. Alichukua mkoba wake na kuelekea kwenye meza iliyokuwa mlangoni.

Alissa pia alikuwa ametulia na hakujali kuhusu kutazamwa kwa udadisi au kushangaza.

Walikuwa katika hali ya kutamanika na ya urembo na gari la kifahari. Umati ulikuwa na hamu ya kuchukua hatua.

“Bi. Nora, huwa unaleta msisimko unapokuja hapa.” Mwanamke aliyekuwa na kibanda cha chakula alijitokeza na kucheka.

“Bibi, una mdomo wa asali. Haishangazi kuwa una biashara bora zaidi katika mtaa huu." Nora alichukua menyu na kuchagua nyama choma alizopenda.

"Ni kwa sababu Bi. Nora hutufadhili kila wakati na hutupendekeza kwa marafiki zako kwamba tunaweza kujikimu." Mwanamke huyo alishangaa alipomtazama Alissa, “Bi. Alissa?”

"Bibiye, sijakuona muda mrefu." Alissa hakutarajia kuwa mwanamke huyo bado anamkumbuka.

Alissa na Nora mara nyingi walikuwa na nyama choma hapo walipokuwa katika shule ya upili. Hata walipohitimu, waliwaalika wanafunzi wenzao kula chakula hapo.

Lakini kumbukumbu hizo za ujana zilikuwa ndefu sana hivi kwamba alihisi hayo yalikuwa mambo ya maisha yake ya mwisho ...

"Nimefurahi kumuona Bi Alissa tena." Mwanamke huyo alipumua kwa hisia, kisha akanong'ona, "Agiza zaidi kama ukaribisho kwa Bi. Alissa, nami nitakupa punguzo la 50%.

“Bibi, asante. Lakini hakuna haja." Alissa akatikisa kichwa, “Hatuwezi kumaliza ikiwa tutaagiza sana.”

“Kama huwezi kuimaliza, unaweza kupakia. Ni mpango. Furahia tu.” Mwanamke huyo alisema waziwazi, “Mimi na mume wangu hatuwezi kamwe kulipa deni tunalodaiwa na Bi. Nora.”

“Unafanya biashara. Hatuwezi kukubali.” Nora hakuwa mwanamke ambaye alichukua fursa ya watu, na hakuhitaji, "Ni sawa kutupa punguzo la 20% kama kawaida."

"Punguzo la 30%."

Baada ya uamuzi huo mzuri, mwanamke huyo alichukua menyu za Nora na Alissa na kuandaa chakula.

Nora alifurahia huduma ya VIP hapa. Hakuhitaji kupata vyakula yeye mwenyewe na alikaa tu na kuhudumiwa.

Baadhi ya sahani zao na bia zilitolewa kwanza. Nora alifungua bia na kujaza glasi yake, akimsihi Alissa, "Njoo."

“Mbona una furaha sana leo?” Alissa naye akajaza glasi yake.

Sura ya 190

Alinyanyua glasi kwenye midomo yake na kunywa huku akimwangalia Nora akinywa glasi ya bia kwa mkupuo mmoja.

Nora alijimimina glasi nyingine ya pombe na kunywa, "Alissa, unakumbuka enzi za shule?"

“Ndiyo.” Alissa akatazama juu. Ingawa kuna kitu kilikuwa kimebadilika, bado alikuwa anafahamika kidogo.

"Unakumbuka? Siku ya kwanza tulipokuja chuoni pamoja, wale wanaume wawili waliotuchukua walitupenda na kuapa kutufukuzia. Hata hivyo, sisi sote tulikiwa na watu ambao tuliwapenda wakati huo. Kwa hivyo, tungewezaje kuwapenda?" Nora alicheka aliposema hivyo.

Alissa alikumbuka wazi kwamba Seidrick, ambaye alisoma shule miaka miwili mbele yake, pia alienda shule ya jirani yake wakati huo. Alissa alisoma Ngaza na Seidrick Nsumba. Kwa hivyo, walionana mara kwa mara. Alipomaliza kidato cha sita Seidrick alijiunga na JKT kwa mujibu wa sheria. Alipomwona tena, alikuwa na uzoefu wa mwezi wa mafunzo ya kijeshi. Alikuwa amekonda na alikuwa mweusi kidogo kuliko hapo awali.

Aliwaalika wenzake kula chakula cha jioni pamoja. Nora alipendekeza kula hapo. Seidrick ambaye alikuwa amekunywa pombe alikiri kwa Alissa na kumtaka awe mpenzi wake.

Alisema kwamba ni wakati tu alipokubali kuwa mpenzi wake, ndipo angeweza kwenda chuo kikuu huko UDSM alikokuwa amechaguliwa kwa urahisi. Vinginevyo, angetafuta njia ya kuhamia chuo kikuu cha SAUT hapo Mwanza au kufanya mtihani tena.

Haikuwa rahisi kuingia katika chuo kikuu enzi hizo. Alissa hakutaka amfanyie mzaha kuhusu masomo yake na pia alikuwa na mapenzi na Seidrick. Kwa hivyo, kwa shangwe za wenzake, alikubali.

Usiku huo, alimshika mkono na wakazunguka shuleni, wakiangalia shule ambayo alikuwa karibu kuishi kwa miaka minne.
Kisha akampeleka kantini na kumbusu.

Wakati huo, alikuwa na miaka kumi na sita tu na yeye alikuwa na kumi na tisa. Walikuwa wachanga na walikuwa na hamu ya kupendana…
Ingawa haikuchukua muda kabla ya kurasimisha uhusiano wao, walikuwa wamependana kwa ujana mzima.

Wote wawili walidhani kwamba wanaweza kuwa na furaha katika upendo kama huo na kuoana vizuri baada ya kuhitimu. Lakini, ilikuwa hatima iliyowafanya wapenzi kuwa maadui.

Alissa aliinua glasi juu ya bia na kunywa. Alihisi kufadhaika na huzuni kidogo.

"Alissa, njoo, kula!" Nora alichukua mshikaki wa nyama ya ng’ombe na kumkabidhi, “Najua unafikiria nini. Lakini unapaswa kujua kwamba ikiwa alikupenda kweli, alipaswa kuwa na imani na wewe. Hata kama hakuweza kukubali, lazima akupe nafasi ya kujieleza. Hakukuamini wala hakusikiliza maelezo yako. Badala yake, alipendekeza kwa Melissa hadharani ... Yeye ni takataka na hastahili kuzingatiwa nawe."

"Bwana Kendrick ni mkarimu zaidi kuliko Seidrick. Haijalishi zamani zako, au kwamba Doris sio binti yake mwenyewe. Yeye ndiye unapaswa kumwamini. Unapofikiria jinsi alivyo mzuri, utajua jinsi Seidrick alivyo mbaya!

“Simwazii. Ninawaza tu kuhusu ujana wangu… ” Alissa akainua glasi yake, “Usiku wa leo, ninaaga ujana wangu na maisha yangu ya zamani!”

Ndio, tangu sasa, alitaka kusema kwaheri kwa maisha yake ya zamani na hatakumbuka tena. Anachopaswa kufanya ni kuthamini alichokuwa nacho sasa na kutazamia.

“Ndiyo. Wacha tuyaage yaliyopita!” Nora alikunywa bia yake na akahuzunika kidogo, “Nitauaga pia.”

“Ni wakati wa kusema kwaheri. Tuwe wazuri kuanzia sasa.” Alissa aliushika mkono wa Nora pale mezani na kuushika kwa nguvu.

Macho ya Nora yalikuwa yakiangaza kwa machozi, lakini aliitikia kwa tabasamu.

Ni kwa kusahau yaliyopita tu ndipo wangeweza kupata tena maisha mapya.

Nora na Alissa walikuwa na wakati mzuri pamoja. Kila mmoja alikunywa chupa nne za bia kwa muda mfupi. Wote wawili walikuwa wamelewa kidogo.

"Halo, wasichana, mko peke yenu?" Mwanamume aliyevaa nguo za kifahari alikuja na glasi ya bia, “Mimi na rafiki yangu pia hatujaoa. Tunaweza kuwasaidia kupunguza upweke.”

Aliweka mkono mmoja begani mwa mtu mrefu na mwembamba karibu yake. Walibadilishana tabasamu la maana.

Nora alijiegemeza kwenye kiwiko cha mkono mmoja, akaweka taya yake ya chini kwenye mkono wake, akageuka kidogo kuwatazama wale wageni, “Nyie ni nani? Siwajui. Toka nje! Msitusumbue!”

"Utakuwa na wakati mzuri ikiwa utakunywa na mwanaume." Mwanamume huyo hata alikaa chini bila aibu, akitabasamu, "Utaridhika, miss."

Kusikia hivyo, Nora ghafla aligeuka kuwa adui. Alipiga meza, akasimama, na alikuwa akitetemeka kidogo,

"Nilisema toka nje. Ondoka mbali iwezekanavyo. Je, wewe ni kiziwi? Hunisikii?”

“Nora.” Alissa alihisi kuwa wawili hao walikuwa na nia mbaya. Kwa hivyo, alimwonyesha Nora kwa ishara asiwe na msukumo.

Alijitahidi kuinuka, akasonga mbele na kuchukua mkono wa Nora, "Twende."

“Mnawezaje kuondoka baada ya kututukana?” Wanaume hao wawili walizuia njia yao.

Nora alikuwa karibu kwenda mbele. Lakini Alissa alimvuta nyuma na kusimama mbele yake,

“Basi kwa nini mnakuja huku bila kualikwa?”

"Hata hivyo, kwa kuwa mnatukemea, hamuwezi kuondoka!" Yule mtu alisema kwa ukali.

“Kwa hiyo, unataka nini?” Alissa alitaka kujua hali zao.

Mtu huyo alikunja midomo yake na kusema, "Niombe msamaha hadharani."

"Nini? Acha kuota ndoto za mchana!” Nora aliweka mikono yake mbele ya kifua chake na kujigamba, “Unapaswa kushukuru kwamba sikushtaki kwa unyanyasaji.”

“Nilikugusa au kukubusu? Unyanyasaji gani?” wanaume wawili wakacheka sana.

Wakakaribia zaidi. Mmoja wao alimvuta Alissa, huku mwingine akimshika Nora mkono.

"Grey, hao ni wageni wa mara kwa mara kwenye baa yangu. Tafadhali waache waende zao, nami nitaondoa bili yako yote leo.” Mwanamke huyo alijitokeza mbele kumtetea Nora.

“Niwaache waende zao?”wanamume anayeitwa Grey alikoroma, “Ikiwa bado unataka kufanya biashara hapa, jali mambo yako mwenyewe!”

"Grey, ni marafiki zangu. Tafadhali waache waende na nitaondoa bili yako yote kwa mwezi mmoja, sawa?” Mwanamke aliweka viganja vyake pamoja na kutoa masharti ya kuvutia zaidi.

Lakini Grey hakutetereka hata kidogo. Alipiga teke meza yao, “Ukisema neno moja zaidi la kukasirisha, nitavunja kibanda chako!”

"Bibiye, usijali kuhusu sisi." Alissa hakutaka kumhusisha mwanamke huyo, “Tunaweza kulishughulikia.”

Mwanamke huyo alitaka kuwasaidia lakini hakuweza kufanya lolote. Macho yake yalikuwa yamejaa wasiwasi.

“Niache!” Nora alisema.

"Afadhali utuache, au huwezi kumudu matokeo." Alissa alikumbusha.

“Haya, usiniogopeshe!” Grey aliinua nyusi zake, "Hatuogopi."

“Ukithubutu kunigusa, nitaukata mkono wako!” Nora alijitahidi. Lakini miguu yake ilikuwa dhaifu kutokana na pombe. Hakuweza kushindana na mwanaume mwenye nguvu.

"Ni mwanamke mwenye kiburi kama nini!" Grey alijifanya kuwa na hofu, lakini hakuweza kuficha tabasamu la ucheshi usoni mwake, "Ninapenda tabia yako kali!"

Nora alimtemea mate usoni, akimtazama kwa macho yake mazuri.

Grey alifunga macho yake na kukasirika. Aliinua mkono wake kufuta uso wake, "Bitch, huna shukrani sana!"

Aliinua mkono wake mkubwa na alikuwa karibu kumpiga Nora uso mzuri. Alissa akapiga kelele, “Acha! Acha!"

Sura ya 191

Alissa aliangaza macho yake huku akitazama kwamba Grey karibu ampige kofi usoni Nora.

Katika wakati muhimu, umbo la mtu liliruka kutoka mahali fulani. Alikuwa mwepesi kama chui, na akashika kifundo cha mkono cha Grey kumzuia asimpige Nora.

Grey aligeuka baada ya kusimamishwa na kusema kwa hasira, "Nani jamani... Ah!"

Kisha mtu huyo akampiga uso wa Grey kwa ngumi kali. Wengine waliweza kusikia meno ya Grey yakigongana huku uso wake ukipepesuka na akatema damu iliyojaa mdomoni.

Nora alikuwa mbele yake na kuangaza macho kwa mshtuko. Mtu huyu alikuwa na nguvu kweli!

Grey alitokwa na jasho kwenye paji la uso wake na uso wake ulikuwa umepinda kwa maumivu. Akalegeza kuushika mkono wa Nora kisha akaanguka chini moja kwa moja.

Yule mtu aliyekuwa akimvuta Alissa aliona hivyo akakasirika sana na kushika kiti na kujaribu kumpiga mtu aliyemuokoa Nora. Hata hivyo, mtu huyo aligeuka na kumpiga teke na kiti kokamtoka mkononi. Alianguka chini na akajichubua paji la uso wake.

Alissa, ambaye aliachiliwa, alikimbia mbele na kumshika Nora, “Nora, uko sawa?”

“Niko sawa.” Nora aliweka mkono mmoja kifuani mwake na bado alikuwa anasumbuliwa na mshtuko huo.

Ilifanyika haraka sana kwamba hakuwa na wakati wa kujibu. Lakini pia aliweza kuhisi jinsi mwanaume huyo alivyokuwa na nguvu. Ikiwa angepigwa, aliogopa kwamba angekuwa amevunjika.

“Vizuri.” Alissa alikuwa macho zaidi ya muda mfupi uliopita, “Kaka, asante kwa kutuokoa. Naweza kujua jina lako?”

"Bosi wangu ndiye anayeniomba niwaokoe.nakaribishwa." Yule mtu akaitikia kwa kichwa, “Bosi wangu amewaita polisi, na polisi watakuja hivi karibuni. Mko salama sasa. Kwaherini.”

Baada ya kusema hivyo aligeuka na kuondoka.

“Bosi wako ni nani? Tafadhali unaweza kuturuhusu kumshukuru ana kwa ana?” Alissa alimwambia mtu huyo mwokozi wao.

Mtu huyo hakugeuka, “Bosi wangu hataki kuonana na mtu yeyote.”

Alissa na Nora walimwona mtu huyo akitembea kuvuka barabara. Chini ya safu ya miti upande wa pili wa barabara yenye njia nne tu, kulikuwa na gari nyeusi aina ya Maybach S. Ilisimama gizani, kama duma akingojea hatua.

Wasifu wa mtu ulionekana hafifu kwenye madirisha yaliyoshushwa kwa theluthi moja.

"Bosi wake aliyemsema lazima atakuwa ndani ya gari." Nora alilitazama gari hilo, “Nataka kujua ni nani. Mimi, Nora, sitaki kuwa na deni kwa mtu yeyote. Sidhani hata wewe kama unataka, sivyo?”

“Ndiyo.” Alissa akatabasamu kwake.
Kisha Nora alilegeza mkono wa Alissa na kumfuata mtu huyo kwa hatua zisizo imara.

Alikaribia kuanguka alipotoka kwenye ukingo. Alissa alijaribu kumsaidia, lakini alikimbia haraka. Alipofika karibu na gari, gari ilianza kuondoka.

Nora alikuwa na wasiwasi, “Subiri! Nyinyi…"

Lakini gari halikusimama na kuondoka. Dirisha likakunjwa taratibu na uso wa mtu aliyekuwa amekaa kimya gizani nao ukafichwa.

Lakini kwa kutazama tu kwa mbali ndani ya sekunde chache, Nora alionekana kushtuka. Uso wake ulikuwa umepauka na macho yalikuwa wazi. Alilitazama gari moja kwa moja. Macho yake yalikuwa yamepigwa na butwaa kidogo, kana kwamba ameona mzimu.

"Nora, una shida gani?" Alissa aliyesogea baadae kidogo alimuona Nora akiwa ameganda.

"Alissa, nilimwona ... alikuwa ndani ya gari." Nora aliongea bila kujitambua na kuonekana mnyonge.

"Yeye ... ni nani?" Alissa alichanganyikiwa.

"Lakini sina uhakika kama ni yeye." Nora aliushika mkono wa Alissa na mkono wake ulikuwa ukitetemeka, “Kuna giza sana ndani ya gari. Mimi pia nilikuwa mbali nalo. Sikuona waziwazi. Lakini wasifu wa mtu huyo unajulikana na kama wake. Hata hivyo ... Sura ya mtu huyo ni tofauti na yake. Mtu huyo ni baridi, wakati yeye ni mpole na joto. Kwa hivyo, sio lazima awe yeye ... "

"Sasa unataka kwenda wapi?"

"Alissa, nataka kujua kama yeye ni Oscar au la!" Kwa hayo, Nora alimtikisa Alissa na kukimbilia garini kabla ya Alissa kusema chochote.

Lakini haikuwa rahisi kwa sababu alikuwa amevaa viatu virefu. Moja kwa moja alivua viatu virefu, akakimbia bila viatu baada ya gari kuwa limepita umbali fulani, na alikuwa kama mwendawazimu.

Alionekana kurudi kwenye ile ajali ya moto alipokuwa na umri wa miaka 19. Wakati huo, pia alikuwa na wazimu na alitaka kuharakisha ili kumtafuta. Baada ya kusimamishwa, aliita jina lake mpaka machozi yakakoma na sauti yake ilikuwa ya kishindo.

“Nora!” Alissa alimuita nyuma yake akijaribu kumsimamisha.

Nora hakuweza kumsikia Alissa sasa. Oscar Steven alikuwa mtu ambaye hawezi kamwe kumsahau kwenye maisha yake.

Alissa alikuwa na wasiwasi kuhusu Nora. Lakini gari la polisi lilifika.

Alikuwa mmoja wa wahusika waliohusika. Polisi walimtaka atoe maelezo. Ilibidi afanye hivyo kwanza. Kwani alijua kuwa Nora hangekuwa mbali na asingeweza kulishika gari lile.

Labda ingekuwa bora kumuacha Nora apate jambo hilo, ili aweze kukata tamaa kabisa baada ya kuhakikisha kuwa mwanaume huyo si Oscar.
Lakini kama angekuwa Oscar… nini kingetokea?

Alissa aliwaeleza polisi na mara akamaliza kutoa taarifa. Kisha, akapata dereva, akachukua mikoba yao, na kuliendesha gari la Nora kumtafuta Nora.

Kwa wakati huu, Nora alikuwa kwenye taa ya pili ya trafiki kwenye barabara hii. Alikuwa ameketi chini. Ingawa hakulia, alionekana kuwa mbaya kana kwamba ameachwa.

Kumtazama Nora vile, Alissa alihisi huzuni. Alimwomba dereva aingie kando ya barabara na kusubiri kwa muda.

Alishuka kwenye gari na kukimbilia kwa Nora, akachuchumaa.

Miguu ya Nora nyeupe ilikuwa imefunikwa na vumbi na vidole vyake vilikuwa vichafu. Hakuwa kama yule mwanamke mchanga wa familia ya Mabala hata sasa.

Alissa alinyoosha mkono na kumpigapiga mgongoni, “Nora, usilie.”

"Alissa, sikulifikia gari kuthibitisha kama ni yeye." Nora alijitupa kwenye mikono ya Alissa, akimkumbatia Alissa kwa nguvu na kujaribu kupata faraja.

"Kuna watu wengi katika ulimwengu huu ambao wanafanana. Labda kweli umekosea. Na kama angekuwa yeye, angesimama.
Isitoshe, kwa kazi yake, hapaswi kuwa anaendesha gari la bei kubwa namna hiyo.” Alissa alijifuta jasho usoni mwake, "Angalia, unapolia, vipodozi vyako vinatoka na hata huonekani mrembo."

“Alissa, nimemkumbuka. Namkumbuka sana.” Nora alisema maneno ambayo alikuwa ameyakandamiza moyoni mwake kwa miaka mitano wakati huu, "Sijawahi kumsahau hata siku moja."

Alissa aliweza kuhisi jinsi Nora alivyompenda Oscar. Kwa sababu yeye ndiye aliyewatazama wakiwa pamoja, wakishikana mikono na kupendana. Alimtazama Oscar akimtazama Nora, na kwamba Nora alikuwa kama mtoto mwenye furaha na macho yake yaling'aa kwa furaha.

Lakini furaha ilikuwa daima kitu cha kupita. Ndani ya mwaka mmoja, Oscar alipata ajali ya moto, akateketea. Kufikia sasa, walikuwa wametengana kwa miaka mitano.

"Ninajua kwamba lazima pia anafikiria juu yako katika ulimwengu mwingine na hajawahi kukusahau hata siku moja." Alissa alijisikia huzuni huku machozi yakimtoka.

Sura ya 192

Alissa alimkumbatia Nora kwa nguvu zaidi, huku Nora akiuzika uso wake zaidi mikononi mwake.
Walikumbatiana tu barabarani ambapo magari yalikuja na kwenda. Upepo wa usiku ulipeperusha nywele zao taratibu...

“Bi. Alissa, Bi. Alissa…” Alipowaona wamenyamaza, ikabidi dereva awasihi, “Si salama kukaa hapa. Hebu tuingie ndani ya gari."

Mbali na hilo, pia walichelewesha kazi yake.

Alissa kisha akapata nafuu kutoka kwa huzuni. Alikuwa amekusudia kuja kumshawishi Nora. Lakini sasa, yeye pia alikuwa amezama katika huzuni hiyo.

“Nora, inuka. Twende nyumbani.” Alissa alisimama kwanza, kisha akamsaidia Nora kuinuka.

Nora alisimama na kumng’ang’ania Alissa, akamuacha Alissa amsaidie kuingia kwenye gari.

Ndani ya gari, Nora aliendelea kumkumbatia Alissa. Hakusema chochote wala kulia na alikuwa mtulivu wa kutisha.

Alissa alijua kwamba Nora alihitaji muda wa kujizuia na kurekebisha hisia zake. Kwa hiyo, aliendelea kupiga mgongo wake, akijaribu kumwondolea wasiwasi na maumivu hayo kwa ajili yake.

Baada ya kufika kwenye jumba alilokuwa akiishi kando ya ziwa, ambako Nora aliishi, dereva aliegesha gari na kuondoka. Alissa alimshukuru, kisha akagonga mlango.

"Freya, njoo unisaidie." Bado kulikuwa na taa sebuleni. Kwa hivyo, Freya, mlinzi wa nyumba wa Nora bado alipaswa kuwa macho.

Freya aliharakisha kufungua mlango na kuona ni Alissa, “Bi. Alissa, kuna nini? Bi Nora hayupo nyumbani.”

“Amelewa na yupo ndani ya gari. Tafadhali njoo umsaidie kuingia nyumbani.” Alissa akageuka na Freya akafuata.

Walimsaidia Nora kwa uangalifu kutoka kwenye gari na kuingia ndani ya nyumba. Kisha, wakapanda juu na kumweka Nora kwenye sofa chumbani kwake.

“Bi. Alissa, nini kinaendelea kwa Bi Nora? Kuna kitu kibaya?" Freya alimtazama Nora, ambaye hakuwa na hisia na mchafu, na alikuwa na wasiwasi.

"Freya, Nora alilewa tu na akaanguka. Hakuna kitu kibaya." Alissa alieleza kwa ufupi, “Unaweza kwenda kupumzika. Nitamtunza hapa.”

"Nitamuandalia Bi. Nora supu ili atulie, la sivyo ataumwa na kichwa kesho." Freya kisha akaondoka.

Alissa alienda bafuni na kuchukua maji ya joto. Aliloweka kitambaa kwenye maji na kukikunja. Kisha, akaketi, akaiweka miguu ya Nora kwenye magoti yake, kisha akafuta vumbi na uchafu kwenye miguu ya Nora kwa taulo, hasa vidole vyake vilivyochakaa kwa vumbi na kuvuja damu kutokana na kujikwaa kwa kukimbia peku.

Kuangalia hii, Alissa alihisi kufadhaika na akamsafisha Nora kwa uangalifu. Hata kama ilimuuma, Nora alikunja uso na kujichosha.

Baada ya kumsafisha miguu, Alissa alileta sanduku la matibabu na kuchukua pamba na spirit ili kuua viini kwenye michubuko ya viganja vya mikono na vidole vya Nora. Nora bado alikaa kimya.

Aliweza kumuelewa Nora. Maumivu ya akili kwa wakati huo yalikuwa mazito mara elfu zaidi ya maumivu ya mwili. Kwa hiyo, maumivu ya kimwili yalikuwa kitu kidogo.

Baada ya kumaliza matibabu, Alissa alirudisha beseni la maji, taulo na sanduku la dawa.

Freya pia alileta supu, "Bi. Alissa, Bi Nora, tafadhali kumbuka kunywa supu.”

“Asante Freya,” Alissa alimtazama Nora aliyekuwa amelala kwenye sofa huku akiwa amefumba macho.

“Nipigie kama unahitaji chochote. Nitaondoka kwanza.”
Alissa alichukua blanketi jembamba na kumfunika Nora,

“Sawa."

"Usijidhuru hivi tena, sawa?”

Kope za Nora zilitetemeka kidogo kabla hajafungua macho yake polepole, "Nilikuwa na msukumo sana leo. Yeye ni mzimu ama nini?... Nilimuona akichomwa moto kwa macho yangu na nilijua wazi kuwa amekufa. Nilijua pia kuwa nitakuwa na wakati mgumu kama huu. Lakini bado naendelea…Alissa, mimi ni mjinga sana.”

"Wewe sio mjinga, lakini umependezwa na hauwezi kutazama mbele. Kwa hiyo, ni jambo lisiloepukika kwamba utajinasa ndani yako mwenyewe.” Alissa aliushika mkono wake na kuupungia, “Siku zote umenishauri niweke yaliyopita kando nisonge mbele. Lakini wewe umewahi kufanya hivyo? Unapaswa kujifunza kutoka kwangu sasa.”

“Una bwana Kendrick ambaye anakupenda. Lakini nina nani?" Nora alitazama juu na kucheka, "Niko peke yangu."

“Nora, kwa kuwa ulimchagua Alan miongoni mwa watu waliokuchumbia, lazima atakuwa na kitu unachokipenda. Umeolewa naye kwa miaka mitano. Kwa nini usijaribu kuanzisha familia yenye uchangamfu na yenye furaha?” Alissa alishauri, “Mimi na Kendrick hatukuwahi kufikiria kwamba tunaweza kupendana hata siku moja. Lakini sasa, tunaenda katika mwelekeo mzuri zaidi. Ninaamini unaweza kufanya pia, mradi tu unatazamia."

“Hebu niambie, Alan ana sifa gani? Alinioa tu kwa sababu tuliweka miadi ambayo hatukuweza kuwekeana vikwazo baada ya kufunga ndoa. Hadharani, sisi ni wanandoa. Kwa faragha, sisi ni wageni. Vinginevyo, unafikiri angenioa?” Nora alitazama kuzunguka chumba kikubwa, “Ingawa tunaishi pamoja, tunalala katika vyumba tofauti. Kwa kweli haiwezekani mimi na yeye kuwa pamoja.”

“Unajua pia kwamba Alan ana rafiki wa kike. Ninawezaje kuvunja makubaliano yetu ya siri? Mbali na hilo, tumefanya makubaliano. Hata hivyo, tumekuwa hivi kwa miaka mitano. Hakuna ubaya wowote.”

Alissa hakusema chochote zaidi, lakini akakumbusha, “Nora, inabidi ufikirie jambo hilo kwa uwazi. Oscar amekufa. Unataka kuzika maisha yako kwa ajili yake hivi?"

“Niliwahi kumwambia kuwa mimi ni mwanamke wake awe hai au amekufa. Kwa hivyo, wakati alipokufa, nilikufa pamoja naye. Mimi ni maiti inayotembea sasa hivi.” Nora aliketi na kurejesha tabasamu lake la kupendeza, “Usiku umeenda sana. Kwa nini usilale hapa? Tunaweza kulala pamoja kama tulivyozoea.”

“Sawa.” Alissa alikuwa amelewa na hakuweza kuendesha gari kurudi mwenyewe. Isitoshe, alikuwa na wasiwasi kuhusu Nora.

Usiku huo, alitaka kuwa na Nora.

“Basi nenda kaoge kwanza. Kuna pajama mpya kwenye chumba cha kubadilishia nguo."

"sawa."

Alissa akachukua nguo zake za kulalia na kwenda bafuni kuoga.

Nora alimsubiri Alissa huku chumba kikifunguliwa kutoka nje.

Alan aliingia haraka na kumwendea Nora huku uso wake ukiwa na wasiwasi, “Nilisikia kutoka kwa Freya kwamba ulianguka chini. Umeumia? Kwa nini usiende hospitali kujiangalia?”

“Sijambo.” Nora alikaa sawa, “Mbona umeingia bila kubisha hodi? Toka nje!”

"Niliogopa kwamba umeumia." Alan alitazama miguu ya Nora iliyofunikwa na blanketi, "Hebu nione jeraha lako."

"Hakuna haja. Toka nje.” Nora aliinuka na kujaribu kumtoa nje.

Kisha Alan aliona jeraha kwenye vidole vya miguu vya Nora na kumshika mkono, “Umeumia. Usihangaike.”

"Mradi hunisumbui, sitahangaika." Nora alijikaza na kujaribu kuurudisha mkono wake nyuma.

Hata hivyo, Alan alimnyanyua na kupiga hatua hadi kwenye kitanda kikubwa, “Nitaondoka baada ya kulala.”

Muda huo Alissa alitoka akiwa amevalia nguo za kulalia na kuona hivi. Nora alipiga bega la Alan kwa mkono wake, “Nishushe.”

Sura ya 193

Alan pia alimwona Alissa na akamsalimia kwa tabasamu, "Habari, Bi. Alissa."

"Njema Bwana Alan. Habari za jioni?" Alissa alimsalimia pia.

"Salama kabisa."

Alan alimbeba Nora hadi kitandani na kumweka chini, akamfunika blanketi, na kusema kwa wasiwasi, “Pumzika vizuri. Nijulishe ikiwa unajisikia vibaya. Nitamwita daktari.”

"Hakuna haja, sijambo.” Nora alifikiri kwamba Alan alifanya fujo. Ilikuwa ni jeraha dogo tu. "Mimi sio dhaifu sana."

"Kama mke wangu, lazima nikutunze vizuri."

Alan alikuwa tofauti sana.

Huyu wa sasa alikuwa tofauti kabisa na yule aliyekuwa akicheka na kumtania kila mara, jambo ambalo lilimfanya Nora ajione kuwa hajamzoea.

"Wewe kaa mbali nami." Nora aliweza kuhisi pumzi yake ya moto.

Ukaribu huo ulimfanya akose raha. Baada ya yote, isipokuwa kwa busu nyepesi kwenye harusi wakati wa ndoa, hawakuwa wameshikana hata mikono tena.

"Sisi ni wanandoa. Bi Alissa anaweza kuelewa.” Alan alitabasamu kwa upole.

Nora alimtazama na kuonekana kuashiria kwamba hawakupaswa kujifanya wanapendana mbele ya rafiki yake wa karibu.

Mara ya mwisho katika mgahawa wa vyakula vya haraka, Alissa alikuwa amemwona akiwa na mpenzi wake.

"Leo hutumii wakati na mpenzi wako?" Nora alibadilisha mada ili kumjulisha kuwa hakuna siri kati yake na Alissa.

"Sina rafiki wa kike." Alan alikuwa mkweli vya kutosha kukiri.

Mara ya mwisho walifanya fujo katika mgahawa wa vyakula vya haraka na akaachana na mpenzi wake.

"Alan, kwa hiyo wale ninaokukutaga nao ni dada zako, sivyo?" Nora alikuwa amekutana na marafiki zake kadhaa wa kike.

"Mke wangu, kweli, sipendi kucheza tena maishani. Nataka kurudi kwa familia yangu na kuwa mume mwema.” Alan aliendelea kutabasamu na hakuna aliyejua kama maneno yake yalikuwa ya kweli au ya uongo.

Lakini machoni pa Nora, hakika yalikuwa ya uwongo,

“Sawa, tutaona."

“Sawa mke wangu, tusubiri tuone.” Alan aliinuka kutoka kwenye ukingo wa kitanda na kuweka mikono yake mfukoni, “Nyinyi ongeeni. Naenda kuoga."

Alan alimgeukia Alissa ambaye alikuwa amesimama si mbali, “Bi. Alissa, tafadhali mtunze Nora usiku wa leo. Nipigie ikiwa unahitaji chochote.
Nitalala chumba cha kingine.”

"Bwana. Njia, usijali. Nitamtunza vizuri Nora.” Alissa akaitikia kwa kichwa.

Alan akamtazama tena Nora kisha akaondoka.

Baada ya mlango kufungwa, Nora alishusha pumzi. Alissa pia alitembea, "Alan ana wasiwasi sana juu yako. Ni jeraha dogo tu, lakini ana wasiwasi sana. Labda anakupenda?"

“Ananipenda mimi?” Nora alikoroma bila kuamini, “Alissa, unawaza nini? Yeye, mwanamume wa kucheza, atanipenda? Ananipenda ilhali anawaza wanawake wengine wengi? Upendo wa aina hii ni nafuu sana. Je, unataka?”

Alissa alinyamazishwa na Nora na kuhisi kuwa alichosema Nora kilikuwa cha busara.

“Sawa. Ni wakati wa kulala.” Nora alikuwa karibu kubadili nguo zake za kulalia.

Alissa aliinua blanketi na kwenda kulala. Miaka mingi iliyopita walilala kitanda kimoja.
Sasa kwa kuwa walikuwa wamelala pamoja, siku hizo za shule zikawarudia akilini.

Wote wawili walikuwa na bahati ya kuwa watu wa kuaminiana zaidi wa kila mmoja, na kwamba walipendana kila wakati.

"Alissa, asante kwa kuwa nawe."

"Nora, asante kwa kuwa nawe."

Usiku huu, walishikana mikono na kukaa na kila mmoja.

Katikati ya usiku, Nora aliamshwa na ndoto mbaya. Alipiga kelele na kuketi kwa nguvu kwa jasho baridi, akihema sana.

"Nora, ulikuwa na ndoto mbaya?" Alissa aliamka na kukaa ili kumpigapiga mgongoni.

“Niliota tena ule moto. Wakati huu, ni kweli zaidi kuliko hapo awali. Nilihisi moto ukichoma ngozi yangu…” Nora aliufikia mwili wake kana kwamba unaunguza ngozi yake, “Unafikiri angekuwa na uchungu kiasi gani… Lakini sikuweza kumuokoa, nikimtazama tu akichomwa hadi majivu. ”

Alimshika Alissa kwa nguvu, “Alissa, lazima asinisamehe. Ndiyo maana ni vigumu kwangu kusahau moto. Mimi huota juu yake tena na tena, jambo ambalo hunikumbusha jinsi nilivyo mbinafsi!”

“Sio hivyo. Moto huo ni kiwewe tu kwako. Kwa kweli, mimi pia nitaota siku hiyo." Alissa alimshika mabega, “Yote ni majaliwa tu. Usijilaumu sana.”

“Safari hii, nilimsikia akisema katika ndoto yangu kwamba hatanisamehe kamwe. Hangenisamehe kamwe…” Nora alitazama chini na kuuzika uso wake kwenye viganja vya mikono yake.

"Alikuwa mzuri sana kwako. Angewezaje kukuambia maneno kama haya? Lazima umesikia vibaya.” Alissa alimsaidia Nora kurudi kitandani, “Wewe acha kumfikiria sana. Achana na ndoto. Hebu tuhesabu kondoo pamoja... Kondoo mmoja, kondoo wawili…”

Nora alimng'ang'ania Alissa, akisikiliza sauti yake ya upole, na akajituliza taratibu ...

Kwa bahati nzuri, siku hiyo ilikuwa wikendi. Alissa alifikiri kwamba angeweza kulala na Nora kwa muda mrefu zaidi. Lakini Nora aliamka saa kumi na mbili na kwenda kwenye mazoezi kukimbia.

Alissa alifarijika kumuona Nora akisikiliza muziki na kukimbia kwenye mashine ya kukanyaga. Kwa hiyo, alienda jikoni kumsaidia Freya kuandaa kifungua kinywa.

“Bi. Alissa, huwezi kufanya hivyo.” Freya hakuthubutu kumwacha Alissa afanye hivi, “Bi. Nora atanikosoa akikuona.”

"Basi nitatoa kifungua kinywa, sawa?" Alissa akatoa uji nje.

Nora na Alan walifika kwenye chumba cha kulia chakula kwa wakati ufaao.

Alan alimtazama Nora, “Uko sawa?”

"Sijambo." Nora hakuwa amelala vizuri jana usiku. Kwa hiyo, uso wake ulikuwa umepauka kidogo. Lakini alikuwa na roho nzuri.

Huyo alikuwa ni Nora. Angeweza kujificha vizuri wakati wa mchana. Lakini usiku, alipokuwa peke yake, upweke wote uliongezeka na hakuweza kutulia tena. Kwa hivyo, alianguka na kujiondoa.

Baada ya kujituliza, angekuwa mwanamke mchanga wa familia ya Cooper Mabala ambaye aliwashangaza wengine tena wakati wa mchana.

Alissa akawapa uji. Alan akasema, “Asante, Bi. Alissa.”

“Usiseme, Bwana Masele. Hata mimi hukaa na kupata kifungua kinywa hapa bure." Alissa akaweka tabasamu la kujidharau.

“Wewe ni rafiki mkubwa wa Nora. Jisikie tu uko nyumbani. Ningependa sana uje hapa mara kwa mara katika siku zijazo.
Nora atatabasamu zaidi anapokuwa na wewe.” Alan alipata hii, na akamtazama Nora kwa upole, “Mpenzi, unapaswa kutabasamu zaidi. Wewe ni mrembo wakati ukitabasamu.”

Nora alichukua uji kwa mdomo na kupaliwa kwa kile alichosema Alan.

Alan alivuta kitambaa haraka na kumpa huku akimpigapiga mgongoni, “Kunywa polepole.”

"Mbona unaongea ujinga?" Nora alimkazia macho, “Hutaki nifurahie kifungua kinywa changu, sivyo?”

“Sikuongea upuuzi. Wewe ni mke wangu, na mpenzi wangu.” Alan alionekana kuhuzunika, “Bi. Alissa, tafadhali shuhudia kwa niaba yangu.”

"Alan, una shida gani?" Nora alichanganyikiwa. Mbali na kumwita 'mke' au 'mpenzi' hadharani, kila mara alimuita Nora faraghani.
 
USINIACHE 4:
Sura ya 195

Alan alionja uji wake, kisha akasema, “Mpenzi, ni makosa kwako kufanya hivi. Ninakuwa mwema kwako na kukujali.”

Nora alijisikia vibaya sana, “Asante kwa wasiwasi wako. Lakini tafadhali waache rafiki zako wa kike kabla ya kuniita mimi mke. Sistahili.”

“Nilisema sina rafiki wa kike sasa. Nitakutunza vyema siku zijazo.” Alan hakuwa na hasira hata kidogo akamtazama kwa macho laini.

“Nyoo!” Nora naye alikunywa uji ule, “Siuhitaji. Alan, bora tubaki na uhusiano wa awali."

"Je, uhusiano wetu umewahi kubadilika? Siku zote tumekuwa wanandoa,” Alan alisema huku akitabasamu, meno yake yakiwa nadhifu na meupe.

Nora aliweka kijiko chake chini na kumtazama kwa tabasamu, “Sikujali wewe.”

Pia aliacha kupata kifungua kinywa, akachukua begi lake na kumwambia Alissa, “Alissa, nitakupeleka nyumbani.”

“Ni wikendi. Wewe pumzika nyumbani na mimi nitarudi mwenyewe.” Alissa alitaka Nora apumzike vizuri nyumbani.

“Siku zote mimi hujifurahisha kwa karamu na burudani nyinginezo. Ulimwengu wa nje unanifaa zaidi.” Nora alishika mkono wa Alissa,

Alissa alivutwa na Nora kuondoka naye. Alimgeukia Alan ambaye bado alikuwa anakula kifungua kinywa, “Mr. Masele, kwaheri.”

“Bi. Alissa, asante. Karibu tena baadaye.” Alan aliinua mkono wake na kumpungia Alissa huku akitabasamu.

Walipotoka nje ya nyumba na kuingia kwenye gari, Alissa alimuuliza Nora, “Unafanya nini? Hata hukupata kifungua kinywa.”

"Siwezi kufurahia kifungua kinywa changu pamoja naye." Nora akawasha gari na kuondoka na Alissa.

“Basi unaenda wapi?” Alissa alikuwa na wasiwasi kwani alikuwa anataka kutoka peke yake.

“Naweza kwenda kununua vitu na kurekebisha urembo wangu saluni. Nitafanya lolote ili kumwepuka. Sitaki kubaki nyumbani nikabiliane naye.” Nora alikuwa akiishi kama alivyotaka. Maadamu alikuwa na jambo la kufanya, hangefikiria mambo mengine.

Akiwa mtu mzima, ilimbidi ajishawishi kuishi vizuri na kuwa na furaha.

Alissa alimtazama Nora ambaye alikuwa akitabasamu na mwenye roho ya juu, na kuweka tabasamu hafifu. "Inaonekana nina wasiwasi sana."

"Nilikunywa sana jana. Lakini sasa niko sawa.” Nora alimtabasamu kwa furaha, kana kwamba si yeye aliyepata shida jana usiku, "Kujifurahisha kidogo mara moja moja kunaweza kuzuia shida za endocrine."

Alissa alifurahishwa na ucheshi wake wakati huu.

Nora alimpeleka Alissa kwenye makazi ya familia ya Maziku na kuondoka.

Alissa alipofika nyumbani, Doris alijitupa mikononi mwake, “Mama, ulikuwa wapi jana usiku? Niliogopa sana kuwa peke yangu.”

"Unaweza kulala na Bibi Mkubws." Alissa alimpapasa paji la uso na kusema.

"Bibi mkubwa ni mzee. Sikutaka kumsumbua. Lakini Bibi alilala nami na kunisimulia hadithi.” Doris alizungusha midomo yake kidogo. Pia hakutarajia bibi yake, ambaye hajawahi kumpenda, angekuwa na urafiki kiasi hicho.

Alissa aliposikia hivyo alinyamaza na kumtazama Marry. Ingawa hakuweza kuwasamehe wazazi wake kwa walichokifanya, lakini alipaswa kumshukuru Marry kwa kusaidia kumtunza Doris.

“Asante, Mama.” Alissa alisema kwa mbali.

"Sisi ni familia. Usiseme, Alissa. Unapokuwa na kitu cha kufanya, nitakuhudumia Doris. Usijali.” Marry haikuwa tena mkali na mbaya kama hapo awali. Alitabasamu na kuwa kama mtu tofauti.

“Ndiyo. Alissa, Doris ni mjukuu wetu. Unaweza kufanya kazi au kutumia wakati na Kendrick unavyotaka. Mimi na mama yako tutamtunza vizuri Doris. Ni kile tunachopaswa kufanya kama babu na babu." Alex naye aliweka tabasamu la kubembeleza na alikuwa katika mtazamo tofauti kabisa.

Alissa alijua kuwa wazazi wake wamebadilika hivi kwa sababu ya Kendrick. Alikuwa mke wake. Kwa hivyo, alikuwa akichukua mamlaka yake.

“Asante kwa wema wanu. Lakini hakuna haja. Kendrick alisema tutamchukua Doris popote tuendapo siku za usoni. Jana usiku, jambo fulani lilimtokea Nora. Ilikuwa hali maalum. Nitajaribu kutowasumbua nyie katika siku zijazo." Alissa hakutaka kuwategemea sana.

Walikuwa tu wakijaribu kutafuta upendeleo zaidi kwa Kendrick kupitia yeye ili wapate faida zaidi katika biashara.

Alitaka kuwaambia wasipoteze juhudi zao. Hangeweza kuwasaidia, hata kama angeweza.

“Kuhusu Kendrick, mimi na yeye tumekubaliana kuweka pembeni mambo ya umma na ya kibinafsi. Sitawahi kumuuliza kuhusu kazi yake. Na sihitaji anisaidie katika kazi yangu.”

Alex alilazimisha tabasamu tu.

"Ikiwa ni sawa, mimi na Doris tunapanda juu." Alissa alimnyanyua Doris na kupanda ghorofani, akamuuliza Doris, “Unataka kwenda wapi leo? Mama atakuridhisha.”

“Sawa.”

Akiwatazama Alissa na Doris wakitoweka pembeni, Marry akamwambia Alex, “Umesikia alichosema hivi punde? Yeye hatakusaidia wewe na familia yetu. Je, hatukupoteza muda wetu jana usiku? Hata sikulala vizuri.”

"Bado ana kinyongo na kile tulichofanya hapo awali. Hakiwezi kuondolewa kwa muda mfupi. Lakini maadamu tumekuwa wema kwake na Doris, tunaweza kumlainisha polepole. Hata hivyo, sisi ni wazazi wake wa kumzaa.” Alex alipiga goti lake kidogo, “Na yeye pia ni mshiriki wa familia ya Maziku. Nani mwingine anaweza kusaidia isipokuwa familia ya Maziku? Je, familia ya Mayala inahitaji msaada wake?"

"Mbali na hilo, mradi tu tuko vizuri kwake, Kendrick ataona kwa macho yake na kuiweka akilini. Kisha, atatufanyia upendeleo hata hivyo. Sasa, sisi ni baba na mama wa mkewe. Atatuheshimu na hatakwenda kinyume nasi hadharani angalau, sawa?

“Kwa hiyo, afadhali tumsaidie Alissa. Usilalamike. Ikiwa tutaondoa chuki moyoni mwake ya miaka yote hii, je, hatuwezi kupata manufaa kutoka kwa Kendrick?”

Marry aliitikia kwa kichwa kukubaliana na uchambuzi wa Alex, “Uko sahihi.”

"Ndio maana inasemekana kuwa wanawake huwa hawaoni mbali." Alex alimwonyesha Marry, kana kwamba alikuwa akisema kwamba Marry ni mjinga sana.

“Unamzungumzia nani?” Marry alimchukia sana Alex kwa kuthubutu kusema hivyo kumhusu, “Kwa hivyo mimi ni mjinga sivyo? Kwa vile unafikiri mimi sina maana, basi usiku huu utalala kwenye kochi!”

Alipoona kwamba Marry alikuwa na hasira, Alex alilazimika kuomba msamaha, “Mpenzi, samahani. Ni kosa langu kwamba nilisema kitu kibaya. Tafadhali usilitie moyoni.”

Marry alikoroma, akageuka na kumpuuza.

“Njoo.” Alex alitazama huku na huku, “Ikiwa una hasira kweli, unaweza kunilaani au kunipiga upendavyo baada ya kupanda ghorofani na kufunga mlango. Doris bado yuko hapa. Kama babu yake, tafadhali epuka hisia zangu, sawa?"

Marry bado alimpuuza na kuweka uso mrefu.

Alissa ambaye alikuwa amebadili nguo alishuka na Doris. Walipopita sebuleni, Doris akawapungia mkono, “Babu, Bibi, natoka na mama, kwaheri.”

"Kwaheri, Doris." Mara moja, nyuso nzito za Marry na Alex zikalainishwa na kuwa tabasamu.

Sura ya 195

Alissa alitoka nje na Doris Dorisalifurahi sana.

Kwanza alimpeleka Doris kwenye Mbuga ya Burudani ya Kassa Zoo, ambapo hawakuweza tu kutazama na kuvutiwa na maua mengi, bali pia walilisha wanyama wazuri, kama vile kobe, sungura, twiga n.k.

Doris alipenda kulisha wanyama, lakini pia aliogopa.
Pia walienda kwenye slaidi ya maji, wakiteleza chini ya mkondo wa vilima.

Kwa chakula cha mchana, walikula pizza, pasta na samaki, na mishikaki ya ng'ombe.

Doris alifurahi sana. Alissa alichukua kitambaa na kufuta pembe za midomo yake iliyokuwa na mchuzi, "Angalia, unakula kama paka mdogo."

"Nimefurahi sana mama." Doris alisema huku akikunja tambi kwa uma na kula kwa kuridhika.

Baada ya chakula cha mchana, Alissa alimpeleka Doris katika Hospitali ya Kamanga na kununua kikapu cha matunda kutoka dukani mbele ya hospitali na rundo la maua kutoka kwa mtunza maua.

"Mama, tunafanya nini hospitali?" Doris aliuliza.

"Tunakuja kumtembelea mwanamke." Alissa alimruhusu Doris kuyashika yale maua huku akiwa amebeba kikapu cha matunda na kumpeleka Doris hospitali.

Familia ya Masolwa ilikuwa imemwomba daktari amruhusu Maira aende nyumbani baada ya kudungwa sindano. Lakini Maira alikuwa na maumivu makali ya kichwa. Kwa hivyo, alilazwa hospitalini kwa uchunguzi.

Alissa aligonga mlango wa wodi ya Maira na kuingia huku Maira akiwa peke yake.

Alissa alitembea na Doris. Macho ya Maira yalijawa na furaha na mshangao alipomuona Alissa.

"Bi. Masolwa, habari yako?" Alissa aliweka kikapu cha matunda na maua chini.

Kwa kuwa Alissa alikuwa amemtendea wema, Maira alishukuru kwa kwenda kumtembelea.

“Alissa, asante kwa kuja kunitembelea. Maira aliguswa, “Asante kwa kuniokoa jana.”

"Ni silika tu. Unakaribishwa." Alissa alimleta Doris mbele yake na kumtambulisha, “Doris, huyu ni Bi Masolwa.” “Habari, Bibi Masolwa.” Doris alisema kwa upole.

“Habari, Doris. Wewe ni mrembo sana na unafanana na mama yako alipokuwa mtoto.” Maira alimsoma Doris, ambaye alikuwa mrembo na alionekana kupendeza zaidi na mwenye uso usio na hatia.

Maira aliondoa macho yake kwa Doris hadi kwa Alissa, "Je, yeye ndiye mtoto wa miaka mitano iliyopita?"

“Ndiyo. Ni mtoto wangu.” Alissa alimshika Doris mabega kwa mikono miwili na kujivunia, “Yeye ndiye anayenifariji. Vinginevyo, sijui ningeendeleaje.”

"Sisi ndio tunasikitika." Maira alijilaumu.

"Bi. Masolwa, haina uhusiano wowote na wewe. Ni chaguo langu.” Alissa alikuwa na nguvu baada ya mabadiliko hayo.

Maira bado alijisikia hatia kwa Alissa. Lakini angeiweka akilini mwake na pengine angeweza kupata nafasi ya kuisuluhisha baadaye.
Na sasa alikuwa karibu na Alissa.

“Wewe na Kendrick mlifunga ndoa na bado sijakupongeza.” Maira akavua bangili nyeupe ya jadi mkononi mwake, “Sijui ni zawadi gani ya harusi inakufaa. Hii ni zawadi yangu ndogo.”

Alikuwa amekusudia kumpa Alissa bangili ya jadi aliyokuwa amevaa baada ya Seidrick na Alissa kufunga ndoa. Lakini watu hawakujua kilikachotokea. Alissa hakuolewa na Seidrick. Lakini, Melissa alikua mke wa Seidrick.

Sio kwamba hakumpenda Melissa. Alimpendelea Alissa bila fahamu.

Alissa alimwambia Doris aende kucheza kwenye kochi, kisha akakataa bangili ya Maira, “Bi. Masolwa, asante kwa wema wako, lakini siwezi kukubali."

"Alissa, usikatae." Maira alisisitiza, “Nisikilize tu na uichukue, ili nijisikie vizuri. Hutaki kuichukua kwa sababu hutaki kunisamehe? Lakini ni jambo jema kunisamehe.”

"Hapana, Maira." Alissa alibadilisha anwani yake kuonyesha ukweli wake.
Hakuelewana na Melissa. Ikiwa Melissa angejua kuhusu hilo, Alissa hakujua ni shida gani ambayo Melissa angefanya.

Bila shaka si kwamba alikuwa anamuogopa Melissa. Ilikuwa tu kwamba alifikiria shida kidogo na kuepuka migogoro isiyo na lazima. Hakutaka kugombana na Melissa.

"Kwa kuwa bado uko tayari kuniita Maira, basi pokea." Maira alimsihi Alissa kwa macho laini, “Hii ni zawadi kwa ndoa yako.
Zaidi ya hayo, ninaweza kutoa vitu vyangu kwa yeyote ninayemtaka. Unapaswa kuichukua.”

Macho yake yalikuwa thabiti na yenye kuendelea. Alissa alijua kwamba asipoipokea, Maira hatauachia mkono wake.

"Naweza, basi asante." Ilimbidi Alissa aiweke kando kwa uangalifu, akifikiri kwamba angeirudisha kwa Maira baadaye wakati kungekuwa na nafasi, “Lakini sielewi unamaanisha nini kwamba niichukue.”

"Utaelewa baadaye." Maira hakusema zaidi.

Maira alipoona anaipokea, alimpa mkono kwa kuridhika.

Je, Maira bado alikuwa akimchukulia kama binti-mkwe wake? Je, Maira bado alifikiri kwamba yeye na Seidrick wataweza kupatanishwa siku moja?

Hili liliwezekanaje? Waliachsna na tayari walikuwa wamefunga ndoa na Watu wachumba wengine. Hawangeweza kurudi zamani.

"Kisha Maira, nitakumenya tufaha." Alissa alichukua tufaha na kuziosha, kisha akamenya tufaha mbili na kuzigawa, moja kwa Maira na moja kwa Doris.

"Wewe pia unayo?" Maira akachukua kipande kwa ajili yake na toothpick na kumkabidhi.

“Asante.” Alissa alichukua toothpick na kula tufaha.

Maira alimtazama Alissa na kutabasamu, na Alissa naye akatabasamu. Walionekana wamerudi enzi walipokuwa karibu sana.

"Alissa, mbona uko hapa!" Muonekano wa Melissa aliyetokea ghafla ulivunja amani.

Alissa aliweka bakuli la kioo kwenye meza ya kando ya kitanda, akamtazama Melissa ambaye alikuwa akimsogelea kwa hasira na uhasama machoni pake, na kuuliza kwa kejeli, “Kwa nini nisiwe hapa? Wewe ndiye unayesimamia hospitali hii?"

“Wewe…” Melissa alikabwa, kisha akamtazama Maira, “Mama, umesahau alichomfanya Seidrick miaka mitano iliyopita? Sio tu kwamba hakumuokoa Seidrick kutoka kwa kifo, lakini alimsaliti na akazaa mwana haramu ... "

Ghafla, Alissa alimpiga Melissa kofi kali usoni na kumfanya anyamaze.

Uso wake ulikuwa umepinda na mwili wake umeinama.

Melissa alihisi uso wake ukiwaka vibaya. Ilimuuma sana hata mzizi wa ulimi ulikuwa umekufa ganzi kidogo.

“Unawezaje kunipiga?” Melissa alikuwa anaenda kuwaka hasira. Lakini kumuona Maira hapa, angeweza tu kuzuia hasira yake.
Daima alikuwa mzuri na mtulivu mbele ya Maira. Kwa hivyo, hakuweza kukasirika kumwacha Maira hisia mbaya.

Melissa mara moja alijifanya mwanamke mwenye huruma na mpole, kana kwamba alikuwa na malalamiko yasiyo na mwisho na kuwafanya watu waone huruma.

“Mama, Alissa ananipiga. Nimembeba mtoto wa familia ya Masolwa tumboni mwangu. Yeye pia ni mjukuu wako.” Macho ya Melissa yalijawa na machozi huku akilia, “Mama, tafadhali upate haki kwa ajili yangu.”

Sura ya 196

Melissa angeweza tu kuruhusu Maira kupata haki kwa ajili yake. Vinginevyo, hangeweza kuiruhusu iende kwa urahisi.

“Kukupiga kwangu hakuna uhusiano wowote na Maira. Ni kati yetu. Sisi sote ni watu wazima na tunaweza kulitatua sisi wenyewe.” Alissa alikuwa na sura yenye nguvu na alikuwa makini.

“Alissa, si unatumia tu uwezo wa bwana Kendrick? Kwa nini usijitegemee?” Melissa alimwonea wivu Alissa kwa kuwa na bahati sana. Hakuwahi kufikiria kuwa baada ya kuachana na Seidrick, Alissa angeweza kuolewa na Kendrick.

Ilikuwa ni kuudhi sana kwamba Alissa alikuwa na sifa mbaya na mtoto na bado aliweza kuwa Bi Mayala.

“Ni mume wangu. Kuna ubaya gani mimi kutumia nguvu za mume wangu? Sijali kutumia uwezo wa mumeo, kama unaweza kufanya hivyo.” Alissa aliweka tabasamu zuri, lakini macho yake yalikuwa baridi na makali, “Melissa, nakuambia, sijali unataka kunifanyia nini. Lakini binti yangu ndiye msingi wangu. Ukithubutu kupima kikomo changu, sitakuacha uende kamwe!”

“Nilichosema ni ukweli tu!” Melissa bado alikuwa mkaidi na kusitasita kukiri makosa, “Je, nilisema jambo baya?”

“Acheni!” Maira alikunja kipaji na hakuweza kusikiliza maneno ya Melissa tena, “Melissa, ni ufidhuli kwako kuzungumza hivi. Alissa ni dada yako na Doris ni sawa na binti yako. Wewe pia utakuwa mama hivi karibuni. Je, huwezi kuwa mwadilifu kwa mtoto wako?”

Melissa alipepesa macho kwa wepesi na machozi yalitiririka kwenye mashavu yake mazuri, “Tangu alipoondoka na kumsaliti Seidrick nyuma, hakuwa dada yangu tena. Sitakubali kuwa mtu ambaye hana dhamiri bila kujali usalama wa Seidrick. Ni dada yangu. Seidrick ndiye aliyeokoa maisha yake wakati huo. Lakini yeye alifanya nini?

“Mama vipi bado unamlinda hivyo? Najua umempendelea Alissa kila wakati. Kwa hiyo unataka achukue nafasi yangu kama mkwe wako?"

Maira alidhihaki.,“acha kuwaza hayo matamanio. Ameolewa na Bwana Kendrick, mtu mwenye nguvu na tajiri. Unafikiri bado atakuwa tayari kuolewa katika familia ya Masolwa?"

"Mimi ndiye pekee ninayempenda Seidrick. Alissa hastahili hata kidogo!”

“Ndiyo sikatai kuwa nampendelea Alissa. Ingawa hawezi kuwa binti-mkwe wangu, ninaweza kumchukulia kama binti yangu. Je, hivyo pia ni shida?

“Na tangu uolewe na Seidrick, nimekutambua kutoka moyoni mwangu kama binti-mkwe wangu. Pia nilifanya wajibu wangu kama mama mkwe. Sikukuacha uteseke katika familia ya Masolwa na siku zote niliomba Seidrick akujali zaidi na kuongozana nawe.

"Naona jinsi ulivyo mzuri kwa Seidrick. Na sasa una mimba ya mtoto wa Seidrick. Baba yako, dada yako, Seidrick na mimi sote tunakushukuru kwa dhati. Tunajaribu tuwezavyo kukuridhisha. Chunguza dhamiri yako mwenyewe. Je, nimewahi kukutendea vibaya katika kipindi cha miaka mitano hivi hivi?”

Melissa alijua kuwa familia ya Masolwa ilikuwa nzuri na alikuwa na bahati ya kuolewa na Seidrick. Lakini Alissa alipotokea, Melissa alihisi angeachwa na kubadilishwa.

Alipoingia tu na kuona kwamba walikuwa karibu kama familia, alishtuka.
Hakuweza kumruhusu Alissa amchukue mtu yeyote kutoka kwake. Hangeruhusu!

“Mama, hamjanitendea vibaya. Lakini Alissa aliwahi kuwa mchumba wa Seidrick, na mimi ni mke halali wa Seidrick sasa. Unanifanya nijisikie vipi wakati uko karibu naye? Je, unaweza kuzuia hisia zangu?” Melissa alilipapasa tumbo lake bapa, “Hata kama ni kwa ajili ya mjukuu wako.”

“Nilizimia jana na Alissa akanipeleka hospitali. Yeye ndiye mfadhili wangu. Kama binti-mkwe wangu, baada ya kuingia, haukumshukuru tu, bali pia ulipiga kelele na kuzungumza kwa jeuri. Umefikiria juu ya mtoto wako?" Maira ilikuwa mbaya sana.

"Mama, kwa neno moja, hunipendi tena kwa sababu amerudi, sawa?" Melissa aliuma midomo yake, macho yake yakiwa yamejaa machozi na chuki.

"Hapana." Maira akatikisa kichwa, “Nyinyi ni dada. Kwa nini hamuelewani?”

"Kuelewana?" Melissa alidhihaki, “Unaweza kumuuliza ikiwa anataka kuishi pamoja nami vizuri! Bado anampenda Seidrick."

“Alissa ameolewa na Kendrick. Haifai kwako kusema maneno kama haya. Huku si tu kuwatukana Alissa na Seidrick, bali pia kujidhalilisha wewe mwenyewe!” Maira alifikiri kwamba Melissa alikuwa mkaidi sana, “Wewe ni mke wa Seidrick. Humwamini hata kidogo? Basi kwa nini mnaweza kuwa pamoja? Jambo la msingi sana kumpenda mtu ni uaminifu na heshima. Ikiwa huwezi hata kufanya hivyo, unampenda Seidrick kweli?

Melissa alinyamazishwa tena na swali la Maira, “Mama, unatilia shaka mapenzi yangu kwa Seidrick? Ikiwa sikumpenda, nisingekubali pendekezo lake muda mfupi tu baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini. Hata sikujali kama ningeweza kupata watoto naye… nilijitolea sana kwa ajili yake. Lakini sasa, bado unadhani simpendi…

“Halafu unadhani Alissa anampenda Seidrick? Ikiwa ni hivyo, angekuwa amefanya kitu kumsaliti Seidrick!” Melissa alimnyooshea kidole Alissa kwa hasira.

Hakukata tamaa kwa kuwa siku zote kuna watu wanamlinda na kumsaidia Alissa, huku yeye mwenyewe akitegemea juhudi zake za kupigania kila kitu, “Kwa kuwa unaniona hivi mama, basi bora nitoe mimba ya huyu mtoto tumboni mwangu…”

Melissa alifumba macho taratibu kwa maumivu na kugeuka kuondoka. Maira alimwita, “Melissa, huyu ni mtoto wako na wa Seidrick. Unawezaje kuwa mtu asiye na maana sana?”

"Mimi si kitu katika familia ya Masolwa, achilia mbali yeye. Hata akizaliwa hatathaminiwa.” Melissa hakukaa tena akaondoka bila kuangalia nyuma.

Maira alikunja uso, akafumba macho na kushika shuka kwa nguvu.

Kisha akainua shuka na kutoka kitandani. Wakati Melissa akivuta mpini wa mlango, aliushika mkono wa Melissa, “Melissa, huwezi kufanya hivi. Mtoto hana hatia.”

Huyu alikuwa mtoto oekee wa Seidrick. Seidrick alikuwa naye kwa shida. Asingeweza tu kumtazama Melissa akimtoa mtoto.

“Basi mimi nina hatia?” Melissa aliuliza kwa kejeli.

Kwa kweli, Melissa alijivunia ndani. Alikuwa akiweka dau kwamba Maira alimjali mtoto na hangemruhusu atoe mimba kwa urahisi.

“Alissa ameolewa na Kendrick. Hana sababu ya kuwa na uhusiano wowote na Seidrick. Hakuwezi kuwa na chochote kati yao! Niamini." Maira alimsihi kwa uhakika, macho yake yalijazwa na usafi.

“Kwa nini nikuamini?” Melissa alimtazama pembeni Alissa aliyekuwa amesimama pale.

"Melissa, usiwe na akili mbovu!" Alipoona Maira akiongea kwa unyenyekevu kwa ajili ya hili, Alissa alishindwa kuvumilia, “Usijali, sawa? Ninawezaje kuachana na Kendrick na kuwa na uhusiano na Bwana Seidrick? Mimi, Alissa, najua kabisa ninachotaka!”

"Hii ni biashara ya familia yetu. Haina uhusiano wowote na wewe!” Melissa alimtenga Alissa.

“Kwa hiyo unataka nini?” Maira alijua Melissa alikuwa na masharti.

Sura ya 197

Maira angeweza tu kufanya maelewano kwa ajili ya mtoto, wakati Melissa alitegemea mtoto huyu na alikuwa na kiburi.

Alissa kwa upande wake alikuwa mtulivu sana akiwaza tu kwamba Seidrick hapaswi kumuona Melissa namna hii. Ikiwa Seidrick angejua kwamba Melissa alikuwa akimdharau mama yake mpendwa, ingekuwaje?

“Mama niahidi kuwa hutakutana na Alissa siku zijazo. Hata ikiwa utakutana naye, unapaswa kuondoka mara moja na ukae mbali naye iwezekanavyo. Vinginevyo, sitakuwa mzuri kama nilivyo leo. Melissa alicheka baada ya kusema masharti yake, "Mama, nadhani unaweza kufanya hivyo kwa ajili ya mjukuu wako."

"Pia, Hii inaweza tu kujulikana na sisi katika wodi hii. Ikiwa mtu mwingine yeyote atajua kuhusu hilo, ninaweza kufanya lolote nikiwa sina furaha.” Akautazama mkono wake uliokuwa ukilipapasa tumbo lake.

Ilikuwa dhahiri kwamba Melissa alikuwa akimtishia Maira. Lakini Maira hakuweza kufanya lolote kwa sababu alitishiwa.

Kuona Melissa akienda mbali, Alissa alihuzunika kwa Maira.

Alissa alichukua hatua chache mbele, akapuuza sura ya Melissa ya uvivu, na kumwambia Maira, “Maira…”

"Huo ni mwito wa upendo sana. Alissa, unawezaje kumwita mama yangu hivi?” Melissa alikoroma, akitafuta shida kwa makusudi.

“Maira, nadhani kwa kweli haifai sisi kuonana tena. Kwa hivyo, sitakusumbua tena katika siku zijazo. Jitunze tu. Natumai utapona hivi karibuni.” Alissa alichukua hatua ya kuweka mawazo yake wazi mbele ya Melissa, na hakutaka kumuaibisha Maira.

Maira pia alielewa nia ya Alissa. Alissa alikuwa akichukua hatua ya kumweka waziwazi ili afanye uamuzi.

"Doris, twende." Alissa alimpungia mkono Doris aje.

Doris alinyanyuka na kuushika mkono wa Alissa.

“Huwezi kwenda sasa hivi.” Melissa alizuia njia yake, "Ulichosema sio kile alichosema. Kwa hivyo, lazima aseme mara moja."

"Melissa, usiende mbali sana." Alissa alikunja uso.

“Naenda mbali sana? Ninafanya hivi kwa manufaa ya mama.” Melissa alisema kwa kujiamini sana, “Itakuwaje awe karibu na mwanamke ambaye amemsaliti na kumuumiza mwanae? Je, amewahi kufikiria kuhusu mwanawe mwenyewe? Hawezi kutofautisha kati ya adui na watu walio upande wake! Alissa, hii ni biashara ya familia yetu. Unaingilia kati kwa uwezo gani?"

Kwa kweli Alissa hakuwa katika nafasi ya kuingilia masuala ya familia ya Masolwa, "Inaonekana kwamba baadhi ya mambo yanaweza tu kuamuliwa mbele ya wazazi wetu unaporudi nyumbani kwa Maziku."

"Unamaanisha nini?" Macho ya Melissa kisha yakaangaza kwa woga.

Timothy alikuwa ameshughulikiwa na Kendrick. Melissa hakuwa amerudi kwa familia ya Maziku katika kipindi hiki cha wakati na alikuwa akikaa katika familia ya Masolwa, ili asikutane na Alissa.

Alifikiri angekuwa salama ikiwa angejificha. Bila kutarajia, bado alikutana na Alissa hapa.
Popote alipokuwa Alissa, Melissa alihisi woga na hasira.

Maira akashusha pumzi ndefu, “Sawa. Acha kuongea. Ninakuahidi kuwa sitakutana tena na Alissa na nitaondoka mara moja nitakapomuona. Je, ni sawa?”

Maira alikunja uso, hakutaka Melissa awe mkaidi na asimwandame Alissa.

Leo, Maira aliona wazi kwamba tabia zote mbovu za Melissa zilifichwa. Lakini Seidrick bado iliwekwa gizani.

"Mama, tafadhali kumbuka ulichosema leo na ufanye, au kutakuwa na malipo." Melissa alimtazama Alissa kwa sura ya ushindi.

“Melissa, wewe bado ni binadamu? Unawezaje kuwatendea wazee wako hivi? Hata ni mama wa mwanaume unayempenda! Je! Seidrick anafahamu sura yako halisi?" Alissa alimtazama Maira ambaye alikuwa mgonjwa na mwenye huzuni, na hakuweza kujizuia tu kutaka kuingiza pua yake kwenye biashara yao.

“Mimi ni binti-mkwe wa familia ya Masolwa na mwokozi wa Seidrick. Wote wanapaswa kunishukuru.” Melissa alidhani alikuwa shujaa wa familia ya Masolwa, na kwamba walikuwa na deni kubwa la shukrani kwake.

Alissa alitikisa kichwa kwa tabasamu baridi, “Melissa, unadai kuwa ulikuwa mwokozi wa Seidrick. Kwa hiyo una ushahidi gani?"

“Nilimpa daktari damu ya kitovu na ikaokoa maisha ya Seidrick. Huo ndio uthibitisho.” Melissa alidanganya kwa uso ulionyooka.

Alikuwa amechukua mchango wa Alissa kwa Seidrick miaka mitano iliyopita. Angewezaje kukiri kwamba alikuwa akidanganya?

“Daktari yuko wapi?” Alissa aliendelea kumuuliza.

"Sijui." Melissa alionekana kukosa subira kidogo.

"Mpigieni na tutamuuliza ana kwa ana ili kuthibitisha damu ya kitovu ni ya nani." Alissa alitabasamu kwa utulivu na kumtazama Melissa, ambaye alikuwa na hatia kidogo.

"Hata hivyo sio yako." Melissa aliuma meno na kukana.

"Hiyo si lazima iwe kweli." Alissa alimtazama Doris kwa macho laini.

"Acha kuongea ujinga hapa." Melissa alimkazia macho Alissa ambaye alikuwa akimtafutia shida.

Akisikiliza mazungumzo yao, Maira alifikiri kuna kitu kibaya. Kwa hiyo, aliuliza, “Melissa, je, damu ya kitovu ni ya nani? Uliipata wapi?"

Wakati huo, Seidrick alikuwa mgonjwa na afya yake ilikuwa mbaya zaidi. Hawakuweza kupata mechi ya uboho. Daktari alisema kwamba wangeweza tu kusubiri.

Lakini wakati Seidrick alikuwa katika hatari kubwa, Melissa aliwapa matumaini, akisema kwamba amepata damu ya kitovu. Kila mtu alikuwa amezama katika furaha ya wokovu wa Seidrick na hawakuingia ndani ya kile kilichotokea.

Walitaka kumshukuru mfadhili. Lakini Melissa alikataa kwa madai kuwa mfadhili huyo hakutaka wengine wamjue yeye ni nani.
Kisha wakampa Melissa milioni 2 ili ampe mfadhili huyo kumshukuru.

Kisha wangejitayarisha kwa ajili ya zawadi na kumwomba Melissa ampe mtoaji kila mwaka kama ishara ya uthamini wao.

Hadi sasa, walikuwa hawajawahi kukutana na mtu huyo. Kila walipotaja suala la mfadhili, Melissa alikuwa akibadilisha mada ya mazungumzo.
Sasa baada ya Alissa kutaja, Maira alihisi mashaka.

"Mama, haijalishi nimeipata wapi, ni sawa kwamba Seidrick ni mzima sasa." Melissa akanyamaza na kuongeza, “Mama, unamwamini yeye au mimi? Tafadhali kumbuka kuwa mimi ni mke wa Seidrick! Hata hivyo sitamuumiza Seidrick.”

“Lakini…” Maira hakuwa na shaka na hisia za Melissa kwa Seidrick, lakini tabia yake.

“Hapana, lakini Kila kitu ninachofanya ni kwa manufaa ya Seidrick.” Melissa alikatiza harakati za Maira, “Mama, jitunze. Nitakuona wakati ujao.
Na wewe Alissa, fanya haraka uondoke hapa!”

Hakutaka kushikwa na Maira hapa. Alissa akiwa karibu, Melissa aliogopa sana.

Melissa kisha akaufungua mlango na kuondoka kwa haraka.

Maira alisimama pale, akili yake ikiwa katika msukosuko.

"Maira, usifikirie sana. Afya yako ni muhimu zaidi." Alissa alimshikilia Maira, “Nitakusaidia kulala kitandani.” Maira alilala juu ya kitanda. Uso wake ulikuwa wa rangi na wenye huzuni sana.

"Maira, nitaondoka sasa. Jitunze vizuri.”

Lakini Maira akamshika mkono, “Alissa, unajua nini kuhusu mfadhili?”

Sura ya 198

Alissa aliweka mkono wake mwingine nyuma ya mkono wa Maira na kuupapasa kidogo, akimtuliza, “Maira, mambo fulani lazima yasemwe kwa wakati ufaao. Chochote ninachojua, si wakati mwafaka sasa.”

"Hiyo inamaanisha unajua hadithi ya ndani." Macho ya Maira yaliangaza na akasema kwa matumaini.

"Sijui." Alissa alikanusha.

Maira alikuwa mama yake Seidrick. Ikiwa Maira angezungumza na Seidrick kuhusu kile kilichotokea siku hiyo, Alissa aliogopa tu kwamba Seidrick angemshuku kuwa na nia mbaya.

Na hakuwa amepata ushahidi bora na wa moja kwa moja wa kuthibitisha hilo kwa wakati huo.

Ilibidi Alissa atafute ushahidi wa chuma ili kumfanya Melissa ashindwe kusema na kushindwa kugeuka. Vinginevyo, ikiwa Melissa angerejea, angemshambulia kwa kulipiza kisasi.

Macho ya Maira, ambayo yalikuwa na mng'aro wa furaha, yakawa na huzuni.
Alissa hakutaka kusema lolote baya kuhusu Melissa. Baada ya yote, hakukuwa na watu wengi ambao walimwamini sasa.

Hakutaka kujiingiza katika jambo fulani. Hasa, Seidrick alikuwa ikimlinda sana Melissa. Zaidi ya hayo, Melissa sasa alikuwa na ujauzito wa mtoto wa Seidrick na akawa muhimu kwake.

Huu haukuwa wakati mzuri wa kumwangusha Melissa.

Alissa sasa alikuwa kama mwindaji ambaye alikuwa akingojea fursa ya kutoa pigo mbaya wakati mawindo yalikuwa yamepumzika zaidi na kujisahau.

Kwa wakati huu, mlango wa wodi ulisukumwa wazi kutoka nje. Walikuwa ni Seidrick, Alaya na Jasmin walioingia pamoja.

Walishangaa kidogo kumuona Maira akiwa amemshika Alissa mkono.

Alissa alirudisha mkono wake, “Bi. Masolwa, kwaheri."

Alissa alimchukua Doris na kuwa karibu kuondoka. Maira alimwambia Seidrick ambaye aliganda, "Seidrick, muone Alissa."

Seidrick hakusogea, akifikiri kwamba aepuke mashaka kwa sababu ya hali kati yao. Alisita kidogo kumuona Alissa.

Alaya na Seidrick walikuwa karibu zaidi na waliweza kuona kile ambacho kaka yake alikuwa akiwaza. Kwa hivyo, alitabasamu na kuweka maua mikononi mwake, "Mama, niruhusu nifanye. Nina kitu cha kuzungumza na Alissa tu.”

Kwa hayo, Alaya alitoka wodini na Alissa na kumpeleka kwenye maegesho.

"Alissa, asante kwa kumuokoa mama yangu. Sijali ulichomfanyia Seidrick hapo awali. Lakini natumai hutakuja karibu na mama yangu tena.
Baada ya yote, Melissa na Seidrick tayari wameoana na wewe pia umeolewa. Kwa hiyo, jihadhari.” Alaya alifikiria kwa muda ikabidi aseme alichokuwa anakiwaza.

“Alaya, umesema kweli. Najua la kufanya.” Alissa alielewa mara tu aliposikia, "Sitamsumbua Maira katika siku zijazo."

"Asante." Alaya aligeuka ili kurudi wodi, "Jihadhari."

Alissa aliitikia kwa kichwa na kumpeleka Doris kwenye gari ili kuondoka.

Walipokuwa wakielekea kwenye gari, Doris alimvuta mkono Alissa, “Mama, usihuzunike.”

"Kwa nini niwe na huzuni?" Alissa alimtazama mtoto wake mdogo.

“Wote hawakupendi. Lakini ninakupenda, na Baba, Nora, na Jane wote wanakupenda. hiyo inatosha. Wengine wote ni watu wasio na umuhimu.
Kwa hiyo, usifadhaike kwa sababu ya wale wasiyo muhimu.” Doris alisema kwa njia ya busara.

Alissa alichuchumaa na kuweka mikono yake kwenye mabega ya Doris, “Umesema kweli. Lakini mama hajakasirika hata kidogo. Kwa sababu mama hawapendi pia."

Doris alifunika mdomo wake kwa mikono yake na kutabasamu, akitoa ishara ya dole gumba.

“Turudi.”

Alissa alipokuwa anakaribia kuinuka, aliona watu wawili waliowafahamu wakikwepa kwenye lango la usalama.

Alifungua mlango wa gari, akamwomba Doris aketi ndani, na kusema, “Doris, msubiri mama kwa dakika chache kwenye gari. Msichana mzuri, usiseme chochote. Narudi muda si mrefu."

"Sawa." Doris hakuuliza kwa nini na alishirikiana kwa utii.

Alijua kwamba lazima mama yake awe na jambo fulani muhimu la kufanya. Ndio maana alimuacha hapa.

Alichopaswa kufanya ni kumngoja mama yake kwa utiifu na sio kufanya fujo.

Alissa alifunga gari kisha akajipenyeza hadi kwenye mlango wa usalama.

Alijibanza ukutani na taratibu akalisogelea lile jopo baridi la mlango wa chuma kigumu huku akilibana sikio lake kwa nguvu ili kujaribu kusikiliza mazungumzo ya mle ndani.

Hakika ilisikika sauti ya mazungumzo kati ya watu wawili.

“Timothy, unaweza kutulia na kunisikiliza?” ilikuwa ni sauti ya Melissa yenye sauti ya kuomba. Alikuwa tofauti kabisa na mwanamke mwenye kiburi katika wodi ya Maira hivi sasa.

"Melissa, ikiwa ungekuwa kama hivi nilivyo sasa, ungeweza kutulia?" Timothy alikasirika, “Kwa kuwa nimemkosea Kendrick, sasa nimefukuzwa nyadhifa zote na wakurugenzi. Wananilazimisha hata kutoa hisa zangu. Sasa sina chochote!

"Na hii yote ni kwa sababu yako! Usingeweka habari za uongo kuwa Alissa ni hawara kwenye ndoa ya Kendrick, nisingeomba mtu apekeke zile picha Geita. Ulisema Kendrick alimchoka Alissa na kumtelekeza. Lakini nini kilifanyika basi? Alissa ndiye Bi Mayala halisi!”

"Kwa kweli lazima ule maneno yako!" Timothy alijinyooshea uso wake mwenyewe, “Jitazame wewe kisha unitazame. Kama shemeji ya Kendrick, bado wewe ni mrembo. Lakini mimi ni kama panya! Kwa nini?”

Kusikia hivyo, Alissa alikuwa na uhakika kabisa kwamba Timothy na Melissa walikuwa katika makundi dhidi yake. Lakini wawili hao walikuwa hawajawahi kukutana. Jinsi gani walikusanyika na kula njama dhidi yake?

“Mimi … sikutarajia mambo yangekuwa hivi pia! Sisi ni washirika katika mashua moja. Ningewezaje kukudhuru? Ni yule bwege Alissa ambaye alikuwa ametuzuga na kutupotosha. Bila kutarajia, Kendrick angeshirikiana naye kikamilifu.” Melissa alishika nguo zake kwa woga kwa vidole vyake, "Namchukia Alissa zaidi kuliko wewe."

“Kuna maana gani ya kuzungumza juu yake sasa!” Timothy hakusikiliza maneno yake na kutomwamini kama hapo awali, “Je, ninaweza kurudi katika siku za zamani hata kama unasema hivi? Unaniruhusu niwe hivi hata hivyo. Kwa vile umeniumiza sana, unawezaje kutua kwa miguu yako? Tufe pamoja!”

Timothy akasogea mbele na kumshika bega kwa nguvu kiasi kwamba bega lilimuuma. Melissa alivumilia maumivu na aliogopa.

Sasa, Timothy hakuwa na kitu. Kwa hiyo, yeye pia hakuwa na cha kupoteza. Hakuweza kumhurumia.

“Unaongea upuuzi gani? Je, tunawezaje kulipiza kisasi kwa Alissa tukifa? Unataka kuiacha iende kwa urahisi hivyo?" Melissa alisema huku uso wake ukiwa laini.

“Sijui. Lakini je, inajalisha? Mpinzani ni mkali. Kumi kati yenu na mimi hatulingani na mtu mwenye nguvu kama hizo. Au bado unataka kunitumia? “Timothy alikaza macho, akawa na hekima zaidi baada ya kupata hasara.

“Si utakufa? Kwa nini tusilipize kisasi kabla ya kufa, ili wote wasiweze kuachwa. Tunapaswa kubaki hai sasa na kusubiri nafasi yetu. Tutapata nafasi.”

“Kwa nini nikuamini?” Hakuwa mjinga kama hapo awali.

Sura ya 199

Melissa alijua kwamba kulikuwa na pengo la uaminifu kati yake na Timothy. Ilibidi amfanye Timothy kumwamini tena.
"Nipe muda nitakuthibitishia." Melissa alisema kwa upole, akauvuta mkono wake ulioushika begani mwake, na akatabasamu kwa unyonge.

“Sawa, nitakupa muda unavyotaka. Ukithubutu kucheza hila, basi sitakuacha kirahisi.” Timothy aliweka tabasamu baya, kisha akainama na kuinamisha kichwa chake kumbusu Melissa.

Kichefuchefu kilimpanda Melissa huku akisikia harufu yake. Alishusha pumzi kwa siri ili kuvumiliq.
Alitabasamu kwa kujifurahisha na kuweka kidole chake cha shahada kwenye midomo yake, “Usifanye hivyo. Hii ni njia ya usalama.”

“Hakuna mtu mwingine hapa. Kwa nini huwezi kunibusu? Usisahau kwamba mara ya mwisho ulishindwa kumtumia dawa Alissa. Badala yake, ulitiwa wewe dawa. Nilikusaidia. Uliniomba nilale na wewe wakati huo. Ulifurahia kiasi gani! Kwa nini usiweze! hata kukubusu sasa?

"Melissa, unafikiri siwezi kukubusu kwa vile nimepoteza nafasi yangu, sawa?" Timothy alisema kwa ukali na kumfedhehesha Melissa.

Melissa alikuwa tayari hana raha. Isitoshe, alikuwa mjamzito na alikuwa na ugonjwa wa asubuhi. Sasa, hakuweza kujizuia kujirudisha nyuma kwa ukali.

Kuona kuwa Melissa alikuwa amechukizwa naye hata akatapika, Timothy alikasirika na kuweka sura ngumu.

“Melissa, bado ninazo picha zako za uchi. Inaonekana unataka nimtumie hizi picha na video Seidrick, ili aone jinsi mke wake anavyofurahi anapolala na mwanaume mwingine.”

Timothy alisema na kugeuka kuondoka. Melissa alimshika mkono, akizuia ugonjwa wake na kumsihi, “Timothy, si kwamba sikupendi.
Nina maumivu ya tumbo tu. Ndio maana nilikuja hospitalini. Niamini. Tazama, hii ndiyo ripoti yangu ya uchunguzi.”

Ilikuwa ni kweli kwamba hakuweza kula katika kipindi hiki cha wakati. Kwa hivyo, alienda hospitali kuchunguzwa na hakutarajia kwamba angeweza kumpumbaza Timothy na ripoti hii ya uchunguzi sasa.

Alichukua ripoti kutoka kwenye begi lake na kumpa Timothy, "Angalia, sikukudanganya."

Timothy alikodoa macho yake na kuichomoa ile ripoti kutoka mkononi mwake ili kuitazama. Baada ya kuiangalia, hasira yake iliondolewa.

“Na nimekuwa nje kwa muda mrefu sana. Ninaogopa Seidrick atakuwa na shaka. Kwa hivyo, hatuwezi kufanya wakati huu. Tufanye miadi nyingine.” Melissa aliutazama uso wake kwa makini, akisema kitu kizuri ambacho Timothy angesikiliza.

Kabla ya kupata picha hizo kutoka kwa Timothy na kushughulika na Timothy, Melissa angeweza tu kuwa mpole na mtiifu ili kumtuliza. Sasa, yeye ndiye pekee ambaye angeweza kumtegemea. Bado alikuwa na thamani fulani kwa Timothy katika kumrekebisha Alissa.

Kabla ya kumwondolea thamani yake, lazima akubaliane na matakwa yake kadiri awezavyo.

Timothy alisugua pua yake vibaya, “Chukua chumba cha hoteli siku nyingine na nitakuja kukuona. Usiniruhusu ningojee kwa muda mrefu sana.
Ninaonyeshwa unyenyekevu sasa. Wanawake wote hujificha wanaponiona. Siwezi hata kuachilia tamaa yangu. Inabidi unifariji ipasavyo.”

Aliinua mkono wake na kushika kidevu cha Melissa, akatabasamu vibaya, na kumpiga busu kali kwenye midomo.

"Na ninahitaji pesa!" Timothy alikuwa amebakiwa na pesa kidogo katika siku hizi chache.

"Nitumie nambari ya kadi yako na nitahamisha 100,000 kwako." Melissa alibaki akitabasamu na kutii.

Timothy akakaza mkono wake na kumbana kidevu, “100,000? Unadhani mimi ni mtoto wa shule? Nipe milioni kwanza.”

"Milioni moja?" Melissa alitoa macho yake kwa mshtuko, bila kutarajia kwamba atakuwa na tamaa na kutaka mara kumi ya kile alichompa, “Nawezaje kupata kiasi hicho?”

Timothy alimpandisha Melissa juu na kutembeza vidole vyake kutoka kwenye kidevu chake hadi kwenye hereni za almasi masikioni mwake, na akateleza kwenye shingo yake nyembamba hadi kwenye mkufu wa almasi uliofanana na hereni zilizo kifuani mwake. Kisha, alizunguka juu ya bega lake na chini ya mkono wake ili kumshika mkono wake wa kulia, ambapo pete ya harusi ya almasi ilikuwa inaangaza. Zote zilikuwa bidhaa za kifahari.

“Thamani ya nguo na vito unavyovaa inakaribia milioni kumi. Wewe ni binti-mkwe wa familia ya Masolwa na mwanamke wa familia ya Maziku. Je, hali yako iko vipi katika Jiji hili? Unataka kuniambia kuwa huna pesa? Unafikiri mimi ni mjinga?" Timothy alipapasa almasi laini na nzuri kwenye kidole chake, "Ni sawa ikiwa hutaki kunipa. Basi nipe tu pete yako ya ndoa.”

Melissa mara moja alikunja ngumi ili kumzuia asiiondoe, “Siwezi kukupa hii. Ikiwa Seidrick atagundua ahadi ya ndoa yangu imetoweka, ninawezaje kuelezea?"

"Hiyo ni biashara yako." Timothy alisema bila haya, “Au fanya kama nisemavyo.”

“Milioni moja ni nyingi sana. Sina pesa nyingi sana mkononi mwangu. Kwa hiyo, nipe muda wa kufikiria namna ya kupata pesa.” Akiwa amekabiliwa na bei kubwa ya Timothy, Melissa hakuwa na lingine ila kuafikiana.

"Siku moja. Lazima nipokee pesa kwenye akaunti yangu kufikia wakati huu kesho." Timothy alinyoosha mkono kwa kidole kimoja na kutoa tarehe ya mwisho.

"Milioni moja sio pesa ndogo. Kwa kweli siwezi kuipata hata siku moja.” Melissa alikosa raha na akamwomba ampe muda wa ziada, "Nipe siku tatu."

"Siku mbili. Haijadiliwi.” Hiki kilikuwa kibali cha mwisho cha Timothy.

Hakuwa na pesa nyingi sasa. Alihitaji pesa kwa ajili ya chakula, maisha, na usafiri. Isitoshe, alizoea kutumia pesa kupita kiasi. Ilikaribia kumtia wazimu kwamba sasa alikuwa na shida ya kupata pesa.

Hakuweza tena kustahimili siku za umaskini wakati hakuweza kupata chochote alichotaka.

Ilibidi awe na pesa. Vinginevyo, angewezaje kuishi?

Na Melissa ndiye alikuwa chanzo cha bora cha matatizo yake, hivyo ingebidi awe pia chanzo chake cha pesa.

“Sawa.” Melissa angeweza tu kutikisa kichwa na kusema, “Kisha nitaenda kwanza kukuletea pesa.”

“Melissa, afadhali ukumbuke kuwa sina kitu sasa. Sikuogopi wewe kucheza maujanja! Ikiwa mbaya zaidi itatokea, tutakufa pamoja!

Kwa hayo, Timothy alishusha kofia nyeusi ya besiboli kichwani mwake na kuondoka kupitia hatua ya kituo cha usalama.

Melissa kisha akashusha pumzi ya raha. Lakini alikasirika sana baada ya kuonewa na Timothy kwa wakati huu hadi akaupiga mkoba uliokuwa mkononi mwake ukutani ili kutoa hasira yake.

Alissa hakukaa sana akageuka na kuondoka kimya kimya.
Aliingia kwenye gari lake na kuondoka hospitalini kwa haraka.

Hakuwahi kufikiria kuwa Melissa angekuwa na uhusiano kama huo na Timothy. Ilimshangaza sana. Lakini hiyo ilieleza kwa nini walijuana.

Ilisemekana kuwa ukifanya madhara, utapata madhara. Mtu mwovu atanyanyaswa na mtu mwingine wa kufanana naye.

Akifikiria kuhusu mwisho wa Melissa , Alissa alikuwa katika hali nzuri zaidi.

Hakuweza kulegea na pia ilimbidi ampe Melissa zawadi. Alikasirika sana kuona Melissa akiwa na kiburi sana.

Sura ya 200

Baada ya kumfukuza Alissa, Alaya alirudi katika wodi ya Maira na kuona kwamba Maira alikuwa na huzuni.

Seidrick alikuwa akimuuliza Maira, “Mama, una tatizo gani?”

"Seidrick, sijisikii vizuri ndani." Maira akaugua. Akifikiria kile ambacho Melissa alikuwa ametoka tu kufanya katika wodi hiyo, alikuwa amepoa na kuogopa.

Melissa alikuwa daima laini na dhaifu juu ya uso. Lakini Maira hakuwahi kufikiria kwamba angekuwa mkali sana ndani.

Na mwanamke wa aina hii alikuwa mke wa mtoto wake. Kujificha kwa Melissa kulitisha sana.

"Nitakwenda kumwita daktari akuchunguze." Seidrick ilikuwa karibu kugeuka, lakini Maira akamzuia, “Ninasumbuliwa na wasiwasi wangu.
Daktari hawezi kuuponya.”

"Mama, unaweza kuona daktari wa magonjwa ya akili kwa wasiwasi wako. Nitakutafuta daktari mzuri.” Seidrick alikaa chini na kumtazama Maira.

"Wasiwasi wangu hauwezi kuponywa na daktari wa magonjwa ya akili." Maira alikuwa katika hali mbaya.

Alaya pia alikuja mbele na kutulia, “Mama, kuwa na amani. Unaweza kuzungumza nasi kuhusu hilo. Tutajaribu tuwezavyo kufanya chochote unachotaka kufanya.”

“Ndiyo hivyo mama. Tuambie tu unachotaka. Pia tuna wasiwasi tunapokuona hivi.” Seidrick alisema.

“Sijui kama niseme. Hata nikisema, naogopa kwamba hamtaamini nyote.” Maira alitazama chini na kusitasita sana.

“Mama, wewe ni wa ajabu sana leo. Je, yeye alikuambia kitu? Usimwamini na nitashughulikia kila kitu.” Seidrick aliinua mikono yake magotini na kukunja uso.

“Yeye?” Maira alimuuliza mwanawe kwa kejeli, “Unamrejelea nani?”

"Alissa." Seidrick alikutana na macho ya mama yake yenye maswali, “Yeye ndiye aliyekuleta hospitali jana. Lakini nilirudisha fadhila zote ambazo nilipaswa kurudisha. Kwa hivyo, usijisikie kama una deni kwake."

“Seidrick , haukumuelewa Alissa. Hakuja kuniomba nimrudishie kibali. Alinijali tu na alikuja kuniona.” Maira alihisi kwamba Seidrick ilikuwa na chuki kubwa dhidi ya Alissa, "Una chuki dhidi yake?"

“Sina chuki na mtu yeyote. Lakini yeye si Alissa tena tuliyemjua zamani.” Seidrick pia ilihisi kwamba Maira alikuwa mkaidi sana, "Mama, unaweza kuwa na akili timamu?"

"Wewe ndiye unapaswa kuwa na akili timamu." Maira alikandamiza hasira yake iliyokuwa ikipanda.

“Mama, alikuambia nini hasa? Inaonekana ulivurugwa na yeye.” Seidrick alikuwa na uchungu kwa kukosolewa na Maira, “Je, hujui alifanya nini wakati huo? Sasa, unamtetea. Bado wewe ni mama yangu? Hukuona kwamba mimi mwanao niliachwa naye kama mpumbavu?”

Kadri Seidrick alivyosema, uso wake uligeuka kuwa kama majivu kwa hasira. Aliuma meno na kukunja ngumi kwenye magoti yake.

“Sedrick, tulia. Usiharibu uhusiano wako na Maira.” Alaya alipiga bega la Seidrick.

“Alaya, asante kwa kuja kuniona leo. Lakini inabidi nizungumze vizuri na Seidrick sasa. Samahani." Maira hakutaka Alaya amkosee na akaeleza.

"Mama, najua. Ninaweza kukaa hapa kwa muda tu na lazima nimchukue Jasmin. Anajifunza Kiingereza." Alaya alimwambia Seidrick tena, “Seidrick, zungumza na Maira. Nitatangulia.”

Seidrick aliitikia kwa kichwa, na Alaya kisha akaondoka akiwa ametulia.

Wodi ilikuwa kimya. Sio Maira wala Seidrick aliyezungumza kwanza wakati huu. Walikuwa wakijaribu kutulia.

"Seidrick, unajua kuwa Melissa pia yuko hapa leo?" Maira alitulia kabla ya kuzungumza polepole.

“Kweli?” Seidrick bila shaka hakujua kuhusu hilo, "Alisema alitaka kurudi kwenye nyumba ya familia ya Maziku. Labda alikuja kukuona kwa muda.”

Kwa sababu Melissa alikuwa mjamzito, familia ya Masolwa ilimthamini sana. Alikuwa amejitolea kuja kumuona Maira. Lakini kila mtu alisema kuwa kulikuwa na watu wengi hospitalini. Haikufaa kwa mwanamke mjamzito. Pia haikuwa nzuri kwake na kwa mtoto. Kwa hiyo, wakamwomba abaki nyumbani.

“Alipokuja, Alissa pia alikuwa hapa…” Maira alimwambia Seidrick kilichokuwa kimetokea hivi punde, “Seidrick, je, hatukumwelewa Alissa? Kwa asili yake, hangeweza kamwe kufanya chochote kukuumiza na kukusaliti hivyo. Kwa nini alijifungua mtoto ghafla? ...
Lazima alikumbana na mambo ambayo hangeweza kushughulika nayo, au anaweza kuwa na matatizo yake mwenyewe...

"Na Melissa, nadhani ana kitu cha kutuficha. Haya ni machale yangu. Sitakudhuru kamwe. Wewe ni mwanangu. Kwa hivyo, Seidrick, lazima uwe mwangalifu zaidi."

"Mama, Alissa anaweza kuwa alipata shida gani, hata akazaa mtoto wa mtu mwingine nyuma yangu?" Wakati Alissa alipotajwa, Seidrick alikumbuka tukio hilo miaka mitano iliyopita wakati Alissa alipotoka hospitalini akiwa amemkumbatia mtoto wake, jambo ambalo liliufanya moyo wake kutetemeka kwa maumivu, “Ni yeye ndiye aliniacha nilipokuwa nikimhitaji zaidi. Wakati huo ndipo nilipoona rangi zake halisi.”

"Kuhusu Melissa, yeye ni mzuri kwangu. Sasa, ana mimba ya mtoto wangu. Ikilinganishwa na Alissa, ni wazi kuwa yeye ni bora zaidi. Mama, labda mfadhili hataki kutuona. Si jambo kubwa.”

“Siamini.” Maira alijua jinsi pigo kubwa aliloleta Alissa kwa Seidrick wakati huo.

"Mama, ninamwamini Melissa. Ninaamini tu katika kile nilichokiona. Sitamsamehe Alissa wala kumuamini.” Seidrick alinyoosha mkono na kufungua kidogo kifungo kimoja cha shati lake. Alihisi kukosa pumzi kidogo, “Mama, nitarudi kwanza.”

Hakutaka kuongea na Maira kuhusu Alissa na hakutaka hata kusikia jina lake.

"Seidrick, mama hatawahi kukudanganya. Melissa sio mpole na mstaarabu kama unavyomwona." Maira alimkumbusha tena, “Seidrick, unapingana na Alissa kwa sababu bado huwezi kumwacha aende zake, sivyo? Huwezi kuamini kwamba alikuacha ulipokuwa hatarini na akakusaliti?

"Seidrick, bado unampenda ndani."

“Namchukia!” kwa hayo, Seidrick alipiga hatua kuondoka bila kuangalia nyuma.

Alikuwa na haraka. Alipofika kwenye maegesho ya magari na kuingia kwenye gari lake, hakuendesha gari mara moja. Badala yake, aliegemea kiti chake na kufumba macho yake ili kuweka mambo hayo ya kuudhi nyuma yake.

Alijiambia asifikirie chochote wala kuathiriwa na mtu yeyote.
Lakini kadiri alivyokuwa akijaribu kujituliza ndivyo alivyokuwa akikereka.

Aliugonga kwa nguvu usukani na kuudhika kwamba bado hawezi kumkabili kwa utulivu mwanamke aliyemuumiza baada ya miaka mingi!

Hakika hakuwa kama mama yake alivyosema kwamba hangeweza kumuacha kwa sababu bado anampenda.
Hakuweza kujiachia kwa sababu alitaka kujikumbusha ili asisahau kirahisi usaliti wake na kuumia kwake.

Lakini kwa nini kulikuwa na sauti nyingine moyoni mwake ikisema kwamba haikuwa hivyo?
 
USINIACHE 4:
Sura ya 196

Melissa angeweza tu kuruhusu Maira kupata haki kwa ajili yake. Vinginevyo, hangeweza kuiruhusu iende kwa urahisi.

“Kukupiga kwangu hakuna uhusiano wowote na Maira. Ni kati yetu. Sisi sote ni watu wazima na tunaweza kulitatua sisi wenyewe.” Alissa alikuwa na sura yenye nguvu na alikuwa makini.

“Alissa, si unatumia tu uwezo wa bwana Kendrick? Kwa nini usijitegemee?” Melissa alimwonea wivu Alissa kwa kuwa na bahati sana. Hakuwahi kufikiria kuwa baada ya kuachana na Seidrick, Alissa angeweza kuolewa na Kendrick.

Ilikuwa ni kuudhi sana kwamba Alissa alikuwa na sifa mbaya na mtoto na bado aliweza kuwa Bi Mayala.

“Ni mume wangu. Kuna ubaya gani mimi kutumia nguvu za mume wangu? Sijali kutumia uwezo wa mumeo, kama unaweza kufanya hivyo.” Alissa aliweka tabasamu zuri, lakini macho yake yalikuwa baridi na makali, “Melissa, nakuambia, sijali unataka kunifanyia nini. Lakini binti yangu ndiye msingi wangu. Ukithubutu kupima kikomo changu, sitakuacha uende kamwe!”

“Nilichosema ni ukweli tu!” Melissa bado alikuwa mkaidi na kusitasita kukiri makosa, “Je, nilisema jambo baya?”

“Acheni!” Maira alikunja kipaji na hakuweza kusikiliza maneno ya Melissa tena, “Melissa, ni ufidhuli kwako kuzungumza hivi. Alissa ni dada yako na Doris ni sawa na binti yako. Wewe pia utakuwa mama hivi karibuni. Je, huwezi kuwa mwadilifu kwa mtoto wako?”

Melissa alipepesa macho kwa wepesi na machozi yalitiririka kwenye mashavu yake mazuri, “Tangu alipoondoka na kumsaliti Seidrick nyuma, hakuwa dada yangu tena. Sitakubali kuwa mtu ambaye hana dhamiri bila kujali usalama wa Seidrick. Ni dada yangu. Seidrick ndiye aliyeokoa maisha yake wakati huo. Lakini yeye alifanya nini?

“Mama vipi bado unamlinda hivyo? Najua umempendelea Alissa kila wakati. Kwa hiyo unataka achukue nafasi yangu kama mkwe wako?"

Maira alidhihaki.,“acha kuwaza hayo matamanio. Ameolewa na Bwana Kendrick, mtu mwenye nguvu na tajiri. Unafikiri bado atakuwa tayari kuolewa katika familia ya Masolwa?"

"Mimi ndiye pekee ninayempenda Seidrick. Alissa hastahili hata kidogo!”

“Ndiyo sikatai kuwa nampendelea Alissa. Ingawa hawezi kuwa binti-mkwe wangu, ninaweza kumchukulia kama binti yangu. Je, hivyo pia ni shida?

“Na tangu uolewe na Seidrick, nimekutambua kutoka moyoni mwangu kama binti-mkwe wangu. Pia nilifanya wajibu wangu kama mama mkwe. Sikukuacha uteseke katika familia ya Masolwa na siku zote niliomba Seidrick akujali zaidi na kuongozana nawe.

"Naona jinsi ulivyo mzuri kwa Seidrick. Na sasa una mimba ya mtoto wa Seidrick. Baba yako, dada yako, Seidrick na mimi sote tunakushukuru kwa dhati. Tunajaribu tuwezavyo kukuridhisha. Chunguza dhamiri yako mwenyewe. Je, nimewahi kukutendea vibaya katika kipindi cha miaka mitano hivi hivi?”

Melissa alijua kuwa familia ya Masolwa ilikuwa nzuri na alikuwa na bahati ya kuolewa na Seidrick. Lakini Alissa alipotokea, Melissa alihisi angeachwa na kubadilishwa.

Alipoingia tu na kuona kwamba walikuwa karibu kama familia, alishtuka.
Hakuweza kumruhusu Alissa amchukue mtu yeyote kutoka kwake. Hangeruhusu!

“Mama, hamjanitendea vibaya. Lakini Alissa aliwahi kuwa mchumba wa Seidrick, na mimi ni mke halali wa Seidrick sasa. Unanifanya nijisikie vipi wakati uko karibu naye? Je, unaweza kuzuia hisia zangu?” Melissa alilipapasa tumbo lake bapa, “Hata kama ni kwa ajili ya mjukuu wako.”

“Nilizimia jana na Alissa akanipeleka hospitali. Yeye ndiye mfadhili wangu. Kama binti-mkwe wangu, baada ya kuingia, haukumshukuru tu, bali pia ulipiga kelele na kuzungumza kwa jeuri. Umefikiria juu ya mtoto wako?" Maira ilikuwa mbaya sana.

"Mama, kwa neno moja, hunipendi tena kwa sababu amerudi, sawa?" Melissa aliuma midomo yake, macho yake yakiwa yamejaa machozi na chuki.

"Hapana." Maira akatikisa kichwa, “Nyinyi ni dada. Kwa nini hamuelewani?”

"Kuelewana?" Melissa alidhihaki, “Unaweza kumuuliza ikiwa anataka kuishi pamoja nami vizuri! Bado anampenda Seidrick."

“Alissa ameolewa na Kendrick. Haifai kwako kusema maneno kama haya. Huku si tu kuwatukana Alissa na Seidrick, bali pia kujidhalilisha wewe mwenyewe!” Maira alifikiri kwamba Melissa alikuwa mkaidi sana, “Wewe ni mke wa Seidrick. Humwamini hata kidogo? Basi kwa nini mnaweza kuwa pamoja? Jambo la msingi sana kumpenda mtu ni uaminifu na heshima. Ikiwa huwezi hata kufanya hivyo, unampenda Seidrick kweli?

Melissa alinyamazishwa tena na swali la Maira, “Mama, unatilia shaka mapenzi yangu kwa Seidrick? Ikiwa sikumpenda, nisingekubali pendekezo lake muda mfupi tu baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini. Hata sikujali kama ningeweza kupata watoto naye… nilijitolea sana kwa ajili yake. Lakini sasa, bado unadhani simpendi…

“Halafu unadhani Alissa anampenda Seidrick? Ikiwa ni hivyo, angekuwa amefanya kitu kumsaliti Seidrick!” Melissa alimnyooshea kidole Alissa kwa hasira.

Hakukata tamaa kwa kuwa siku zote kuna watu wanamlinda na kumsaidia Alissa, huku yeye mwenyewe akitegemea juhudi zake za kupigania kila kitu, “Kwa kuwa unaniona hivi mama, basi bora nitoe mimba ya huyu mtoto tumboni mwangu…”

Melissa alifumba macho taratibu kwa maumivu na kugeuka kuondoka. Maira alimwita, “Melissa, huyu ni mtoto wako na wa Seidrick. Unawezaje kuwa mtu asiye na maana sana?”

"Mimi si kitu katika familia ya Masolwa, achilia mbali yeye. Hata akizaliwa hatathaminiwa.” Melissa hakukaa tena akaondoka bila kuangalia nyuma.

Maira alikunja uso, akafumba macho na kushika shuka kwa nguvu.

Kisha akainua shuka na kutoka kitandani. Wakati Melissa akivuta mpini wa mlango, aliushika mkono wa Melissa, “Melissa, huwezi kufanya hivi. Mtoto hana hatia.”

Huyu alikuwa mtoto oekee wa Seidrick. Seidrick alikuwa naye kwa shida. Asingeweza tu kumtazama Melissa akimtoa mtoto.

“Basi mimi nina hatia?” Melissa aliuliza kwa kejeli.

Kwa kweli, Melissa alijivunia ndani. Alikuwa akiweka dau kwamba Maira alimjali mtoto na hangemruhusu atoe mimba kwa urahisi.

“Alissa ameolewa na Kendrick. Hana sababu ya kuwa na uhusiano wowote na Seidrick. Hakuwezi kuwa na chochote kati yao! Niamini." Maira alimsihi kwa uhakika, macho yake yalijazwa na usafi.

“Kwa nini nikuamini?” Melissa alimtazama pembeni Alissa aliyekuwa amesimama pale.

"Melissa, usiwe na akili mbovu!" Alipoona Maira akiongea kwa unyenyekevu kwa ajili ya hili, Alissa alishindwa kuvumilia, “Usijali, sawa? Ninawezaje kuachana na Kendrick na kuwa na uhusiano na Bwana Seidrick? Mimi, Alissa, najua kabisa ninachotaka!”

"Hii ni biashara ya familia yetu. Haina uhusiano wowote na wewe!” Melissa alimtenga Alissa.

“Kwa hiyo unataka nini?” Maira alijua Melissa alikuwa na masharti.

Sura ya 197

Maira angeweza tu kufanya maelewano kwa ajili ya mtoto, wakati Melissa alitegemea mtoto huyu na alikuwa na kiburi.

Alissa kwa upande wake alikuwa mtulivu sana akiwaza tu kwamba Seidrick hapaswi kumuona Melissa namna hii. Ikiwa Seidrick angejua kwamba Melissa alikuwa akimdharau mama yake mpendwa, ingekuwaje?

“Mama niahidi kuwa hutakutana na Alissa siku zijazo. Hata ikiwa utakutana naye, unapaswa kuondoka mara moja na ukae mbali naye iwezekanavyo. Vinginevyo, sitakuwa mzuri kama nilivyo leo. Melissa alicheka baada ya kusema masharti yake, "Mama, nadhani unaweza kufanya hivyo kwa ajili ya mjukuu wako."

"Pia, Hii inaweza tu kujulikana na sisi katika wodi hii. Ikiwa mtu mwingine yeyote atajua kuhusu hilo, ninaweza kufanya lolote nikiwa sina furaha.” Akautazama mkono wake uliokuwa ukilipapasa tumbo lake.

Ilikuwa dhahiri kwamba Melissa alikuwa akimtishia Maira. Lakini Maira hakuweza kufanya lolote kwa sababu alitishiwa.

Kuona Melissa akienda mbali, Alissa alihuzunika kwa Maira.

Alissa alichukua hatua chache mbele, akapuuza sura ya Melissa ya uvivu, na kumwambia Maira, “Maira…”

"Huo ni mwito wa upendo sana. Alissa, unawezaje kumwita mama yangu hivi?” Melissa alikoroma, akitafuta shida kwa makusudi.

“Maira, nadhani kwa kweli haifai sisi kuonana tena. Kwa hivyo, sitakusumbua tena katika siku zijazo. Jitunze tu. Natumai utapona hivi karibuni.” Alissa alichukua hatua ya kuweka mawazo yake wazi mbele ya Melissa, na hakutaka kumuaibisha Maira.

Maira pia alielewa nia ya Alissa. Alissa alikuwa akichukua hatua ya kumweka waziwazi ili afanye uamuzi.

"Doris, twende." Alissa alimpungia mkono Doris aje.

Doris alinyanyuka na kuushika mkono wa Alissa.

“Huwezi kwenda sasa hivi.” Melissa alizuia njia yake, "Ulichosema sio kile alichosema. Kwa hivyo, lazima aseme mara moja."

"Melissa, usiende mbali sana." Alissa alikunja uso.

“Naenda mbali sana? Ninafanya hivi kwa manufaa ya mama.” Melissa alisema kwa kujiamini sana, “Itakuwaje awe karibu na mwanamke ambaye amemsaliti na kumuumiza mwanae? Je, amewahi kufikiria kuhusu mwanawe mwenyewe? Hawezi kutofautisha kati ya adui na watu walio upande wake! Alissa, hii ni biashara ya familia yetu. Unaingilia kati kwa uwezo gani?"

Kwa kweli Alissa hakuwa katika nafasi ya kuingilia masuala ya familia ya Masolwa, "Inaonekana kwamba baadhi ya mambo yanaweza tu kuamuliwa mbele ya wazazi wetu unaporudi nyumbani kwa Maziku."

"Unamaanisha nini?" Macho ya Melissa kisha yakaangaza kwa woga.

Timothy alikuwa ameshughulikiwa na Kendrick. Melissa hakuwa amerudi kwa familia ya Maziku katika kipindi hiki cha wakati na alikuwa akikaa katika familia ya Masolwa, ili asikutane na Alissa.

Alifikiri angekuwa salama ikiwa angejificha. Bila kutarajia, bado alikutana na Alissa hapa.
Popote alipokuwa Alissa, Melissa alihisi woga na hasira.

Maira akashusha pumzi ndefu, “Sawa. Acha kuongea. Ninakuahidi kuwa sitakutana tena na Alissa na nitaondoka mara moja nitakapomuona. Je, ni sawa?”

Maira alikunja uso, hakutaka Melissa awe mkaidi na asimwandame Alissa.

Leo, Maira aliona wazi kwamba tabia zote mbovu za Melissa zilifichwa. Lakini Seidrick bado iliwekwa gizani.

"Mama, tafadhali kumbuka ulichosema leo na ufanye, au kutakuwa na malipo." Melissa alimtazama Alissa kwa sura ya ushindi.

“Melissa, wewe bado ni binadamu? Unawezaje kuwatendea wazee wako hivi? Hata ni mama wa mwanaume unayempenda! Je! Seidrick anafahamu sura yako halisi?" Alissa alimtazama Maira ambaye alikuwa mgonjwa na mwenye huzuni, na hakuweza kujizuia tu kutaka kuingiza pua yake kwenye biashara yao.

“Mimi ni binti-mkwe wa familia ya Masolwa na mwokozi wa Seidrick. Wote wanapaswa kunishukuru.” Melissa alidhani alikuwa shujaa wa familia ya Masolwa, na kwamba walikuwa na deni kubwa la shukrani kwake.

Alissa alitikisa kichwa kwa tabasamu baridi, “Melissa, unadai kuwa ulikuwa mwokozi wa Seidrick. Kwa hiyo una ushahidi gani?"

“Nilimpa daktari damu ya kitovu na ikaokoa maisha ya Seidrick. Huo ndio uthibitisho.” Melissa alidanganya kwa uso ulionyooka.

Alikuwa amechukua mchango wa Alissa kwa Seidrick miaka mitano iliyopita. Angewezaje kukiri kwamba alikuwa akidanganya?

“Daktari yuko wapi?” Alissa aliendelea kumuuliza.

"Sijui." Melissa alionekana kukosa subira kidogo.

"Mpigieni na tutamuuliza ana kwa ana ili kuthibitisha damu ya kitovu ni ya nani." Alissa alitabasamu kwa utulivu na kumtazama Melissa, ambaye alikuwa na hatia kidogo.

"Hata hivyo sio yako." Melissa aliuma meno na kukana.

"Hiyo si lazima iwe kweli." Alissa alimtazama Doris kwa macho laini.

"Acha kuongea ujinga hapa." Melissa alimkazia macho Alissa ambaye alikuwa akimtafutia shida.

Akisikiliza mazungumzo yao, Maira alifikiri kuna kitu kibaya. Kwa hiyo, aliuliza, “Melissa, je, damu ya kitovu ni ya nani? Uliipata wapi?"

Wakati huo, Seidrick alikuwa mgonjwa na afya yake ilikuwa mbaya zaidi. Hawakuweza kupata mechi ya uboho. Daktari alisema kwamba wangeweza tu kusubiri.

Lakini wakati Seidrick alikuwa katika hatari kubwa, Melissa aliwapa matumaini, akisema kwamba amepata damu ya kitovu. Kila mtu alikuwa amezama katika furaha ya wokovu wa Seidrick na hawakuingia ndani ya kile kilichotokea.

Walitaka kumshukuru mfadhili. Lakini Melissa alikataa kwa madai kuwa mfadhili huyo hakutaka wengine wamjue yeye ni nani.
Kisha wakampa Melissa milioni 2 ili ampe mfadhili huyo kumshukuru.

Kisha wangejitayarisha kwa ajili ya zawadi na kumwomba Melissa ampe mtoaji kila mwaka kama ishara ya uthamini wao.

Hadi sasa, walikuwa hawajawahi kukutana na mtu huyo. Kila walipotaja suala la mfadhili, Melissa alikuwa akibadilisha mada ya mazungumzo.
Sasa baada ya Alissa kutaja, Maira alihisi mashaka.

"Mama, haijalishi nimeipata wapi, ni sawa kwamba Seidrick ni mzima sasa." Melissa akanyamaza na kuongeza, “Mama, unamwamini yeye au mimi? Tafadhali kumbuka kuwa mimi ni mke wa Seidrick! Hata hivyo sitamuumiza Seidrick.”

“Lakini…” Maira hakuwa na shaka na hisia za Melissa kwa Seidrick, lakini tabia yake.

“Hapana, lakini Kila kitu ninachofanya ni kwa manufaa ya Seidrick.” Melissa alikatiza harakati za Maira, “Mama, jitunze. Nitakuona wakati ujao.
Na wewe Alissa, fanya haraka uondoke hapa!”

Hakutaka kushikwa na Maira hapa. Alissa akiwa karibu, Melissa aliogopa sana.

Melissa kisha akaufungua mlango na kuondoka kwa haraka.

Maira alisimama pale, akili yake ikiwa katika msukosuko.

"Maira, usifikirie sana. Afya yako ni muhimu zaidi." Alissa alimshikilia Maira, “Nitakusaidia kulala kitandani.” Maira alilala juu ya kitanda. Uso wake ulikuwa wa rangi na wenye huzuni sana.

"Maira, nitaondoka sasa. Jitunze vizuri.”

Lakini Maira akamshika mkono, “Alissa, unajua nini kuhusu mfadhili?”

Sura ya 198

Alissa aliweka mkono wake mwingine nyuma ya mkono wa Maira na kuupapasa kidogo, akimtuliza, “Maira, mambo fulani lazima yasemwe kwa wakati ufaao. Chochote ninachojua, si wakati mwafaka sasa.”

"Hiyo inamaanisha unajua hadithi ya ndani." Macho ya Maira yaliangaza na akasema kwa matumaini.

"Sijui." Alissa alikanusha.

Maira alikuwa mama yake Seidrick. Ikiwa Maira angezungumza na Seidrick kuhusu kile kilichotokea siku hiyo, Alissa aliogopa tu kwamba Seidrick angemshuku kuwa na nia mbaya.

Na hakuwa amepata ushahidi bora na wa moja kwa moja wa kuthibitisha hilo kwa wakati huo.

Ilibidi Alissa atafute ushahidi wa chuma ili kumfanya Melissa ashindwe kusema na kushindwa kugeuka. Vinginevyo, ikiwa Melissa angerejea, angemshambulia kwa kulipiza kisasi.

Macho ya Maira, ambayo yalikuwa na mng'aro wa furaha, yakawa na huzuni.
Alissa hakutaka kusema lolote baya kuhusu Melissa. Baada ya yote, hakukuwa na watu wengi ambao walimwamini sasa.

Hakutaka kujiingiza katika jambo fulani. Hasa, Seidrick alikuwa ikimlinda sana Melissa. Zaidi ya hayo, Melissa sasa alikuwa na ujauzito wa mtoto wa Seidrick na akawa muhimu kwake.

Huu haukuwa wakati mzuri wa kumwangusha Melissa.

Alissa sasa alikuwa kama mwindaji ambaye alikuwa akingojea fursa ya kutoa pigo mbaya wakati mawindo yalikuwa yamepumzika zaidi na kujisahau.

Kwa wakati huu, mlango wa wodi ulisukumwa wazi kutoka nje. Walikuwa ni Seidrick, Alaya na Jasmin walioingia pamoja.

Walishangaa kidogo kumuona Maira akiwa amemshika Alissa mkono.

Alissa alirudisha mkono wake, “Bi. Masolwa, kwaheri."

Alissa alimchukua Doris na kuwa karibu kuondoka. Maira alimwambia Seidrick ambaye aliganda, "Seidrick, muone Alissa."

Seidrick hakusogea, akifikiri kwamba aepuke mashaka kwa sababu ya hali kati yao. Alisita kidogo kumuona Alissa.

Alaya na Seidrick walikuwa karibu zaidi na waliweza kuona kile ambacho kaka yake alikuwa akiwaza. Kwa hivyo, alitabasamu na kuweka maua mikononi mwake, "Mama, niruhusu nifanye. Nina kitu cha kuzungumza na Alissa tu.”

Kwa hayo, Alaya alitoka wodini na Alissa na kumpeleka kwenye maegesho.

"Alissa, asante kwa kumuokoa mama yangu. Sijali ulichomfanyia Seidrick hapo awali. Lakini natumai hutakuja karibu na mama yangu tena.
Baada ya yote, Melissa na Seidrick tayari wameoana na wewe pia umeolewa. Kwa hiyo, jihadhari.” Alaya alifikiria kwa muda ikabidi aseme alichokuwa anakiwaza.

“Alaya, umesema kweli. Najua la kufanya.” Alissa alielewa mara tu aliposikia, "Sitamsumbua Maira katika siku zijazo."

"Asante." Alaya aligeuka ili kurudi wodi, "Jihadhari."

Alissa aliitikia kwa kichwa na kumpeleka Doris kwenye gari ili kuondoka.

Walipokuwa wakielekea kwenye gari, Doris alimvuta mkono Alissa, “Mama, usihuzunike.”

"Kwa nini niwe na huzuni?" Alissa alimtazama mtoto wake mdogo.

“Wote hawakupendi. Lakini ninakupenda, na Baba, Nora, na Jane wote wanakupenda. hiyo inatosha. Wengine wote ni watu wasio na umuhimu.
Kwa hiyo, usifadhaike kwa sababu ya wale wasiyo muhimu.” Doris alisema kwa njia ya busara.

Alissa alichuchumaa na kuweka mikono yake kwenye mabega ya Doris, “Umesema kweli. Lakini mama hajakasirika hata kidogo. Kwa sababu mama hawapendi pia."

Doris alifunika mdomo wake kwa mikono yake na kutabasamu, akitoa ishara ya dole gumba.

“Turudi.”

Alissa alipokuwa anakaribia kuinuka, aliona watu wawili waliowafahamu wakikwepa kwenye lango la usalama.

Alifungua mlango wa gari, akamwomba Doris aketi ndani, na kusema, “Doris, msubiri mama kwa dakika chache kwenye gari. Msichana mzuri, usiseme chochote. Narudi muda si mrefu."

"Sawa." Doris hakuuliza kwa nini na alishirikiana kwa utii.

Alijua kwamba lazima mama yake awe na jambo fulani muhimu la kufanya. Ndio maana alimuacha hapa.

Alichopaswa kufanya ni kumngoja mama yake kwa utiifu na sio kufanya fujo.

Alissa alifunga gari kisha akajipenyeza hadi kwenye mlango wa usalama.

Alijibanza ukutani na taratibu akalisogelea lile jopo baridi la mlango wa chuma kigumu huku akilibana sikio lake kwa nguvu ili kujaribu kusikiliza mazungumzo ya mle ndani.

Hakika ilisikika sauti ya mazungumzo kati ya watu wawili.

“Timothy, unaweza kutulia na kunisikiliza?” ilikuwa ni sauti ya Melissa yenye sauti ya kuomba. Alikuwa tofauti kabisa na mwanamke mwenye kiburi katika wodi ya Maira hivi sasa.

"Melissa, ikiwa ungekuwa kama hivi nilivyo sasa, ungeweza kutulia?" Timothy alikasirika, “Kwa kuwa nimemkosea Kendrick, sasa nimefukuzwa nyadhifa zote na wakurugenzi. Wananilazimisha hata kutoa hisa zangu. Sasa sina chochote!

"Na hii yote ni kwa sababu yako! Usingeweka habari za uongo kuwa Alissa ni hawara kwenye ndoa ya Kendrick, nisingeomba mtu apekeke zile picha Geita. Ulisema Kendrick alimchoka Alissa na kumtelekeza. Lakini nini kilifanyika basi? Alissa ndiye Bi Mayala halisi!”

"Kwa kweli lazima ule maneno yako!" Timothy alijinyooshea uso wake mwenyewe, “Jitazame wewe kisha unitazame. Kama shemeji ya Kendrick, bado wewe ni mrembo. Lakini mimi ni kama panya! Kwa nini?”

Kusikia hivyo, Alissa alikuwa na uhakika kabisa kwamba Timothy na Melissa walikuwa katika makundi dhidi yake. Lakini wawili hao walikuwa hawajawahi kukutana. Jinsi gani walikusanyika na kula njama dhidi yake?

“Mimi … sikutarajia mambo yangekuwa hivi pia! Sisi ni washirika katika mashua moja. Ningewezaje kukudhuru? Ni yule bwege Alissa ambaye alikuwa ametuzuga na kutupotosha. Bila kutarajia, Kendrick angeshirikiana naye kikamilifu.” Melissa alishika nguo zake kwa woga kwa vidole vyake, "Namchukia Alissa zaidi kuliko wewe."

“Kuna maana gani ya kuzungumza juu yake sasa!” Timothy hakusikiliza maneno yake na kutomwamini kama hapo awali, “Je, ninaweza kurudi katika siku za zamani hata kama unasema hivi? Unaniruhusu niwe hivi hata hivyo. Kwa vile umeniumiza sana, unawezaje kutua kwa miguu yako? Tufe pamoja!”

Timothy akasogea mbele na kumshika bega kwa nguvu kiasi kwamba bega lilimuuma. Melissa alivumilia maumivu na aliogopa.

Sasa, Timothy hakuwa na kitu. Kwa hiyo, yeye pia hakuwa na cha kupoteza. Hakuweza kumhurumia.

“Unaongea upuuzi gani? Je, tunawezaje kulipiza kisasi kwa Alissa tukifa? Unataka kuiacha iende kwa urahisi hivyo?" Melissa alisema huku uso wake ukiwa laini.

“Sijui. Lakini je, inajalisha? Mpinzani ni mkali. Kumi kati yenu na mimi hatulingani na mtu mwenye nguvu kama hizo. Au bado unataka kunitumia? “Timothy alikaza macho, akawa na hekima zaidi baada ya kupata hasara.

“Si utakufa? Kwa nini tusilipize kisasi kabla ya kufa, ili wote wasiweze kuachwa. Tunapaswa kubaki hai sasa na kusubiri nafasi yetu. Tutapata nafasi.”

“Kwa nini nikuamini?” Hakuwa mjinga kama hapo awali.

Sura ya 199

Melissa alijua kwamba kulikuwa na pengo la uaminifu kati yake na Timothy. Ilibidi amfanye Timothy kumwamini tena.
"Nipe muda nitakuthibitishia." Melissa alisema kwa upole, akauvuta mkono wake ulioushika begani mwake, na akatabasamu kwa unyonge.

“Sawa, nitakupa muda unavyotaka. Ukithubutu kucheza hila, basi sitakuacha kirahisi.” Timothy aliweka tabasamu baya, kisha akainama na kuinamisha kichwa chake kumbusu Melissa.

Kichefuchefu kilimpanda Melissa huku akisikia harufu yake. Alishusha pumzi kwa siri ili kuvumiliq.
Alitabasamu kwa kujifurahisha na kuweka kidole chake cha shahada kwenye midomo yake, “Usifanye hivyo. Hii ni njia ya usalama.”

“Hakuna mtu mwingine hapa. Kwa nini huwezi kunibusu? Usisahau kwamba mara ya mwisho ulishindwa kumtumia dawa Alissa. Badala yake, ulitiwa wewe dawa. Nilikusaidia. Uliniomba nilale na wewe wakati huo. Ulifurahia kiasi gani! Kwa nini usiweze! hata kukubusu sasa?

"Melissa, unafikiri siwezi kukubusu kwa vile nimepoteza nafasi yangu, sawa?" Timothy alisema kwa ukali na kumfedhehesha Melissa.

Melissa alikuwa tayari hana raha. Isitoshe, alikuwa mjamzito na alikuwa na ugonjwa wa asubuhi. Sasa, hakuweza kujizuia kujirudisha nyuma kwa ukali.

Kuona kuwa Melissa alikuwa amechukizwa naye hata akatapika, Timothy alikasirika na kuweka sura ngumu.

“Melissa, bado ninazo picha zako za uchi. Inaonekana unataka nimtumie hizi picha na video Seidrick, ili aone jinsi mke wake anavyofurahi anapolala na mwanaume mwingine.”

Timothy alisema na kugeuka kuondoka. Melissa alimshika mkono, akizuia ugonjwa wake na kumsihi, “Timothy, si kwamba sikupendi.
Nina maumivu ya tumbo tu. Ndio maana nilikuja hospitalini. Niamini. Tazama, hii ndiyo ripoti yangu ya uchunguzi.”

Ilikuwa ni kweli kwamba hakuweza kula katika kipindi hiki cha wakati. Kwa hivyo, alienda hospitali kuchunguzwa na hakutarajia kwamba angeweza kumpumbaza Timothy na ripoti hii ya uchunguzi sasa.

Alichukua ripoti kutoka kwenye begi lake na kumpa Timothy, "Angalia, sikukudanganya."

Timothy alikodoa macho yake na kuichomoa ile ripoti kutoka mkononi mwake ili kuitazama. Baada ya kuiangalia, hasira yake iliondolewa.

“Na nimekuwa nje kwa muda mrefu sana. Ninaogopa Seidrick atakuwa na shaka. Kwa hivyo, hatuwezi kufanya wakati huu. Tufanye miadi nyingine.” Melissa aliutazama uso wake kwa makini, akisema kitu kizuri ambacho Timothy angesikiliza.

Kabla ya kupata picha hizo kutoka kwa Timothy na kushughulika na Timothy, Melissa angeweza tu kuwa mpole na mtiifu ili kumtuliza. Sasa, yeye ndiye pekee ambaye angeweza kumtegemea. Bado alikuwa na thamani fulani kwa Timothy katika kumrekebisha Alissa.

Kabla ya kumwondolea thamani yake, lazima akubaliane na matakwa yake kadiri awezavyo.

Timothy alisugua pua yake vibaya, “Chukua chumba cha hoteli siku nyingine na nitakuja kukuona. Usiniruhusu ningojee kwa muda mrefu sana.
Ninaonyeshwa unyenyekevu sasa. Wanawake wote hujificha wanaponiona. Siwezi hata kuachilia tamaa yangu. Inabidi unifariji ipasavyo.”

Aliinua mkono wake na kushika kidevu cha Melissa, akatabasamu vibaya, na kumpiga busu kali kwenye midomo.

"Na ninahitaji pesa!" Timothy alikuwa amebakiwa na pesa kidogo katika siku hizi chache.

"Nitumie nambari ya kadi yako na nitahamisha 100,000 kwako." Melissa alibaki akitabasamu na kutii.

Timothy akakaza mkono wake na kumbana kidevu, “100,000? Unadhani mimi ni mtoto wa shule? Nipe milioni kwanza.”

"Milioni moja?" Melissa alitoa macho yake kwa mshtuko, bila kutarajia kwamba atakuwa na tamaa na kutaka mara kumi ya kile alichompa, “Nawezaje kupata kiasi hicho?”

Timothy alimpandisha Melissa juu na kutembeza vidole vyake kutoka kwenye kidevu chake hadi kwenye hereni za almasi masikioni mwake, na akateleza kwenye shingo yake nyembamba hadi kwenye mkufu wa almasi uliofanana na hereni zilizo kifuani mwake. Kisha, alizunguka juu ya bega lake na chini ya mkono wake ili kumshika mkono wake wa kulia, ambapo pete ya harusi ya almasi ilikuwa inaangaza. Zote zilikuwa bidhaa za kifahari.

“Thamani ya nguo na vito unavyovaa inakaribia milioni kumi. Wewe ni binti-mkwe wa familia ya Masolwa na mwanamke wa familia ya Maziku. Je, hali yako iko vipi katika Jiji hili? Unataka kuniambia kuwa huna pesa? Unafikiri mimi ni mjinga?" Timothy alipapasa almasi laini na nzuri kwenye kidole chake, "Ni sawa ikiwa hutaki kunipa. Basi nipe tu pete yako ya ndoa.”

Melissa mara moja alikunja ngumi ili kumzuia asiiondoe, “Siwezi kukupa hii. Ikiwa Seidrick atagundua ahadi ya ndoa yangu imetoweka, ninawezaje kuelezea?"

"Hiyo ni biashara yako." Timothy alisema bila haya, “Au fanya kama nisemavyo.”

“Milioni moja ni nyingi sana. Sina pesa nyingi sana mkononi mwangu. Kwa hiyo, nipe muda wa kufikiria namna ya kupata pesa.” Akiwa amekabiliwa na bei kubwa ya Timothy, Melissa hakuwa na lingine ila kuafikiana.

"Siku moja. Lazima nipokee pesa kwenye akaunti yangu kufikia wakati huu kesho." Timothy alinyoosha mkono kwa kidole kimoja na kutoa tarehe ya mwisho.

"Milioni moja sio pesa ndogo. Kwa kweli siwezi kuipata hata siku moja.” Melissa alikosa raha na akamwomba ampe muda wa ziada, "Nipe siku tatu."

"Siku mbili. Haijadiliwi.” Hiki kilikuwa kibali cha mwisho cha Timothy.

Hakuwa na pesa nyingi sasa. Alihitaji pesa kwa ajili ya chakula, maisha, na usafiri. Isitoshe, alizoea kutumia pesa kupita kiasi. Ilikaribia kumtia wazimu kwamba sasa alikuwa na shida ya kupata pesa.

Hakuweza tena kustahimili siku za umaskini wakati hakuweza kupata chochote alichotaka.

Ilibidi awe na pesa. Vinginevyo, angewezaje kuishi?

Na Melissa ndiye alikuwa chanzo cha bora cha matatizo yake, hivyo ingebidi awe pia chanzo chake cha pesa.

“Sawa.” Melissa angeweza tu kutikisa kichwa na kusema, “Kisha nitaenda kwanza kukuletea pesa.”

“Melissa, afadhali ukumbuke kuwa sina kitu sasa. Sikuogopi wewe kucheza maujanja! Ikiwa mbaya zaidi itatokea, tutakufa pamoja!

Kwa hayo, Timothy alishusha kofia nyeusi ya besiboli kichwani mwake na kuondoka kupitia hatua ya kituo cha usalama.

Melissa kisha akashusha pumzi ya raha. Lakini alikasirika sana baada ya kuonewa na Timothy kwa wakati huu hadi akaupiga mkoba uliokuwa mkononi mwake ukutani ili kutoa hasira yake.

Alissa hakukaa sana akageuka na kuondoka kimya kimya.
Aliingia kwenye gari lake na kuondoka hospitalini kwa haraka.

Hakuwahi kufikiria kuwa Melissa angekuwa na uhusiano kama huo na Timothy. Ilimshangaza sana. Lakini hiyo ilieleza kwa nini walijuana.

Ilisemekana kuwa ukifanya madhara, utapata madhara. Mtu mwovu atanyanyaswa na mtu mwingine wa kufanana naye.

Akifikiria kuhusu mwisho wa Melissa , Alissa alikuwa katika hali nzuri zaidi.

Hakuweza kulegea na pia ilimbidi ampe Melissa zawadi. Alikasirika sana kuona Melissa akiwa na kiburi sana.

Sura ya 200

Baada ya kumfukuza Alissa, Alaya alirudi katika wodi ya Maira na kuona kwamba Maira alikuwa na huzuni.

Seidrick alikuwa akimuuliza Maira, “Mama, una tatizo gani?”

"Seidrick, sijisikii vizuri ndani." Maira akaugua. Akifikiria kile ambacho Melissa alikuwa ametoka tu kufanya katika wodi hiyo, alikuwa amepoa na kuogopa.

Melissa alikuwa daima laini na dhaifu juu ya uso. Lakini Maira hakuwahi kufikiria kwamba angekuwa mkali sana ndani.

Na mwanamke wa aina hii alikuwa mke wa mtoto wake. Kujificha kwa Melissa kulitisha sana.

"Nitakwenda kumwita daktari akuchunguze." Seidrick ilikuwa karibu kugeuka, lakini Maira akamzuia, “Ninasumbuliwa na wasiwasi wangu.
Daktari hawezi kuuponya.”

"Mama, unaweza kuona daktari wa magonjwa ya akili kwa wasiwasi wako. Nitakutafuta daktari mzuri.” Seidrick alikaa chini na kumtazama Maira.

"Wasiwasi wangu hauwezi kuponywa na daktari wa magonjwa ya akili." Maira alikuwa katika hali mbaya.

Alaya pia alikuja mbele na kutulia, “Mama, kuwa na amani. Unaweza kuzungumza nasi kuhusu hilo. Tutajaribu tuwezavyo kufanya chochote unachotaka kufanya.”

“Ndiyo hivyo mama. Tuambie tu unachotaka. Pia tuna wasiwasi tunapokuona hivi.” Seidrick alisema.

“Sijui kama niseme. Hata nikisema, naogopa kwamba hamtaamini nyote.” Maira alitazama chini na kusitasita sana.

“Mama, wewe ni wa ajabu sana leo. Je, yeye alikuambia kitu? Usimwamini na nitashughulikia kila kitu.” Seidrick aliinua mikono yake magotini na kukunja uso.

“Yeye?” Maira alimuuliza mwanawe kwa kejeli, “Unamrejelea nani?”

"Alissa." Seidrick alikutana na macho ya mama yake yenye maswali, “Yeye ndiye aliyekuleta hospitali jana. Lakini nilirudisha fadhila zote ambazo nilipaswa kurudisha. Kwa hivyo, usijisikie kama una deni kwake."

“Seidrick , haukumuelewa Alissa. Hakuja kuniomba nimrudishie kibali. Alinijali tu na alikuja kuniona.” Maira alihisi kwamba Seidrick ilikuwa na chuki kubwa dhidi ya Alissa, "Una chuki dhidi yake?"

“Sina chuki na mtu yeyote. Lakini yeye si Alissa tena tuliyemjua zamani.” Seidrick pia ilihisi kwamba Maira alikuwa mkaidi sana, "Mama, unaweza kuwa na akili timamu?"

"Wewe ndiye unapaswa kuwa na akili timamu." Maira alikandamiza hasira yake iliyokuwa ikipanda.

“Mama, alikuambia nini hasa? Inaonekana ulivurugwa na yeye.” Seidrick alikuwa na uchungu kwa kukosolewa na Maira, “Je, hujui alifanya nini wakati huo? Sasa, unamtetea. Bado wewe ni mama yangu? Hukuona kwamba mimi mwanao niliachwa naye kama mpumbavu?”

Kadri Seidrick alivyosema, uso wake uligeuka kuwa kama majivu kwa hasira. Aliuma meno na kukunja ngumi kwenye magoti yake.

“Sedrick, tulia. Usiharibu uhusiano wako na Maira.” Alaya alipiga bega la Seidrick.

“Alaya, asante kwa kuja kuniona leo. Lakini inabidi nizungumze vizuri na Seidrick sasa. Samahani." Maira hakutaka Alaya amkosee na akaeleza.

"Mama, najua. Ninaweza kukaa hapa kwa muda tu na lazima nimchukue Jasmin. Anajifunza Kiingereza." Alaya alimwambia Seidrick tena, “Seidrick, zungumza na Maira. Nitatangulia.”

Seidrick aliitikia kwa kichwa, na Alaya kisha akaondoka akiwa ametulia.

Wodi ilikuwa kimya. Sio Maira wala Seidrick aliyezungumza kwanza wakati huu. Walikuwa wakijaribu kutulia.

"Seidrick, unajua kuwa Melissa pia yuko hapa leo?" Maira alitulia kabla ya kuzungumza polepole.

“Kweli?” Seidrick bila shaka hakujua kuhusu hilo, "Alisema alitaka kurudi kwenye nyumba ya familia ya Maziku. Labda alikuja kukuona kwa muda.”

Kwa sababu Melissa alikuwa mjamzito, familia ya Masolwa ilimthamini sana. Alikuwa amejitolea kuja kumuona Maira. Lakini kila mtu alisema kuwa kulikuwa na watu wengi hospitalini. Haikufaa kwa mwanamke mjamzito. Pia haikuwa nzuri kwake na kwa mtoto. Kwa hiyo, wakamwomba abaki nyumbani.

“Alipokuja, Alissa pia alikuwa hapa…” Maira alimwambia Seidrick kilichokuwa kimetokea hivi punde, “Seidrick, je, hatukumwelewa Alissa? Kwa asili yake, hangeweza kamwe kufanya chochote kukuumiza na kukusaliti hivyo. Kwa nini alijifungua mtoto ghafla? ...
Lazima alikumbana na mambo ambayo hangeweza kushughulika nayo, au anaweza kuwa na matatizo yake mwenyewe...

"Na Melissa, nadhani ana kitu cha kutuficha. Haya ni machale yangu. Sitakudhuru kamwe. Wewe ni mwanangu. Kwa hivyo, Seidrick, lazima uwe mwangalifu zaidi."

"Mama, Alissa anaweza kuwa alipata shida gani, hata akazaa mtoto wa mtu mwingine nyuma yangu?" Wakati Alissa alipotajwa, Seidrick alikumbuka tukio hilo miaka mitano iliyopita wakati Alissa alipotoka hospitalini akiwa amemkumbatia mtoto wake, jambo ambalo liliufanya moyo wake kutetemeka kwa maumivu, “Ni yeye ndiye aliniacha nilipokuwa nikimhitaji zaidi. Wakati huo ndipo nilipoona rangi zake halisi.”

"Kuhusu Melissa, yeye ni mzuri kwangu. Sasa, ana mimba ya mtoto wangu. Ikilinganishwa na Alissa, ni wazi kuwa yeye ni bora zaidi. Mama, labda mfadhili hataki kutuona. Si jambo kubwa.”

“Siamini.” Maira alijua jinsi pigo kubwa aliloleta Alissa kwa Seidrick wakati huo.

"Mama, ninamwamini Melissa. Ninaamini tu katika kile nilichokiona. Sitamsamehe Alissa wala kumuamini.” Seidrick alinyoosha mkono na kufungua kidogo kifungo kimoja cha shati lake. Alihisi kukosa pumzi kidogo, “Mama, nitarudi kwanza.”

Hakutaka kuongea na Maira kuhusu Alissa na hakutaka hata kusikia jina lake.

"Seidrick, mama hatawahi kukudanganya. Melissa sio mpole na mstaarabu kama unavyomwona." Maira alimkumbusha tena, “Seidrick, unapingana na Alissa kwa sababu bado huwezi kumwacha aende zake, sivyo? Huwezi kuamini kwamba alikuacha ulipokuwa hatarini na akakusaliti?

"Seidrick, bado unampenda ndani."

“Namchukia!” kwa hayo, Seidrick alipiga hatua kuondoka bila kuangalia nyuma.

Alikuwa na haraka. Alipofika kwenye maegesho ya magari na kuingia kwenye gari lake, hakuendesha gari mara moja. Badala yake, aliegemea kiti chake na kufumba macho yake ili kuweka mambo hayo ya kuudhi nyuma yake.

Alijiambia asifikirie chochote wala kuathiriwa na mtu yeyote.
Lakini kadiri alivyokuwa akijaribu kujituliza ndivyo alivyokuwa akikereka.

Aliugonga kwa nguvu usukani na kuudhika kwamba bado hawezi kumkabili kwa utulivu mwanamke aliyemuumiza baada ya miaka mingi!

Hakika hakuwa kama mama yake alivyosema kwamba hangeweza kumuacha kwa sababu bado anampenda.
Hakuweza kujiachia kwa sababu alitaka kujikumbusha ili asisahau kirahisi usaliti wake na kuumia kwake.

Lakini kwa nini kulikuwa na sauti nyingine moyoni mwake ikisema kwamba haikuwa hivyo?
 
USINIACHE 5:
Sura ya 201

Seidrick aliupapasa uso wake kwa mikono yake, hakutaka kukiri kuwa chuki yake kwa Alissa haikuwa safi, bali ilichanganyika na hisia nyingi ngumu.

Seidrick alijitahidi sana kujituliza, kisha akatoa gari nje ya hospitali na kumpigia simu msaidizi wake, “Tafuta ni nani aliyetoa damu ya kitovu na nani alichukua hundi hiyo ya milioni mbili miaka mitano iliyopita."

Kwa sababu fulani, alishuku na alitaka kujua ukweli. Bado alitaka kujipa sababu ya kutomchukia.
Alikuwa amechoka katika miaka hii mitano.

Seidrick ilirudi kwa familia ya Masolwa. Melissa hakuwepo nyumbani.

Baba yake, Sam, alikuwa na jambo muhimu la kufanya na akaenda kucheza gofu na mtu mwenye nguvu.

Kisha, Seidrick akapanda ghorofani na kwenda kwenye maktaba ya familia ili kufanya jambo fulani, kama vile kusoma vitabu ili awe katika hali ya utulivu.

Muda si mrefu, msaidizi akamuita, “Bw. Seidrick, niligundua kuwa hakuna mtu anayepokea hundi ya milioni mbili kila mwaka hadi sasa.”

“Sawa, nimeipata.” Seidrick aliweka kitabu mkononi mwake kwenye kishikilia kitabu na akazama katika mawazo.

Ilionekana kana kwamba mambo hayakuwa vile alivyokuwa akifikiria. Lakini hakutaka kuwa na shaka na Melissa, mke wake. Melissa alikuwa naye kila wakati katika wakati wake mgumu zaidi. Isitoshe, alikuwa mjamzito sasa.

Lakini kwa nini hakuna mtu yeyote aliyechukua hundi hii kwa miaka mitano? Je, mfadhili hakujali pesa au hakuhitaji pesa?

Seidrick hakuweza kubaini. Alikasirika sana akachukua tena kitabu na kuendelea kusoma, akitumaini angeweza kutulia.

Kwa ghafula, mtu fulani akabisha hodi kwenye mlango wa maktaba.

"Ni nani huyo?"

"Mpenzi, ni mimi." Ilikuwa ni sauti ya Melissa.

Melissa kisha akausukuma mlango ndani, akiwa ameshikilia trei yenye bakuli la supu juu yake.

“Mpenzi, nilirudi na kusikia kutoka kwa mtumishi kwamba ulikuwa kwenye maktava. Kwa hiyo, nimekuja kukuona.” Melissa alitabasamu bila madhara na kwa utamu, “Supu imetengenezwa hivi punde. Kunywa ili bado na joto.”

"Leo ulienda hospitali kumuona mama?" Seidrick aliuliza moja kwa moja na kumtazama usoni kutazamia majibu yake.

Melissa aliganda kwa sekunde. Kisha, akamwendea, akamshika mkono, na kwa kawaida akaepuka kumtazama, “Nilikuwa na tumbo lililofadhaika. Kwa hiyo, nilienda hospitali na kumuona daktari kabla ya kwenda kumsalimia Mama...

“Lakini kilichoniudhi ni kukutana na Alissa. Sijui alisema nini. Mama alikuwa mwema kwake kuliko mimi, binti-mkwe wake. Nilikuwa na wivu na katika hali mbaya. Kwa hiyo, nilisema maneno ya kuudhi. Lakini nilikuwa namlenga Alissa, sio mama."

Melissa hakukiri tu kwamba alikuwa ameenda hospitalini, lakini pia alichukua hatua ya kumtaja Alissa. Alijifanya hata aonekane mwenye huzuni na kumlaumu Alissa.

"Pia nilisikia kwamba ulikuwa kama mtu tofauti." Seidrick aliuvuta mkono wake kutoka kwake na kisha akaketi kwenye kiti cha kuzunguka cha ngozi kilichokuwa nyuma yake, “Unajua, haifai kuwa na hasira juu ya mtu mwingine. Isitoshe, huyo ni mama yangu. Hupaswi kuongea mbele naye hivyo hata hivyo.”

“Mpenzi, najua nilikosea. Kwa hivyo, mara tu niliporudi, nimekuja kukurekebisha kwa supu. Nilisikia kuwa wanawake hawana msimamo wanapokuwa wajawazito. Pia sijui nina tatizo gani.” Melissa alichukua tena mkono wa Seidrick na kuutikisa kwa upole, akimwangalia.

Alionekana mwenye huzuni sana hivi kwamba hakuna mtu aliyeweza kuvumilia kumlaumu.

Njia ya Melissa ilikuwa imeonekana kuwa nzuri kila wakati. Alijua kwamba wanaume wote walipenda wanawake wapole na wazuri na hawakuweza kupinga wanawake ambao walitenda kama mtoto anayedeka.

Seidrick pia alikuwa amesikia kwamba wanawake hawakuwa thabiti walipokuwa wajawazito na wanaweza kuwa watu tofauti.

Kwa kweli hii ilitosha kumshawishi.

“Leo nikiwa nachambua hesabu, nimegundua milioni mbili ulizopewa kila mwaka kwa miaka mitano iliyopita kumpatia mfadhili wangu hazijawahi kutolewa. Unaelezaje hilo?” Seidrick alimuuliza.

Mara tu kitu kikianza, haikuweza kusimamishwa.

Seidrick sasa ilikuwa akijaribu na kumshuku Melissa.

“Mpenzi, pesa alipewa mfadhili. Ni haki yake kuipokea au la, au kuitumia au kutoitumia. Je, inanihusu nini? Je, ikiwa mpokeaji hataki kutumia pesa hizo?” Melissa alikasirika kidogo na kutikisa mkono wake, "Je, unanitilia shaka?"

"Nataka kujua yeye ni nani." Basi asingekuwa na mashaka naye.

"Imekuwa miaka mitano. Sina mawasiliano yake na sijui ameenda wapi.” Melissa aliuma midomo yake na kukasirishwa na Seidrick kwa kuuliza maswali kama hayo, "Mpenzi, una shida gani?"

Alifikiri Maira lazima alizungumza na Seidrick kuhusu kile kilichotokea siku hiyo. Ndiyo maana Seidrick alikuwa akimuuliza kuhusu mambo haya.

"Melissa, tumekuwa pamoja kwa muda mrefu. Tayari unanifahamu vizuri. Natumai hutanidanganya. Niambie kwanza ikiwa kuna chochote. Sisi ni wanandoa na hakuna jambo ambalo hatuwezi kuzungumzia.” Seidrick hakutaka tena maelezo marefu ya Melissa.

Lakini wakati huu, angeweza kweli kumwamini Melissa? “Mpenzi, najua.” Melissa akatabasamu tena.

"Jambo muhimu zaidi kwako sasa ni kujilinda wewe na mtoto."

“Nitafanya.” Melissa alimchukia Alissa zaidi.

Alissa ambaye alikuwa amerudi kwenye familia ya akina Maziku alipiga chafya mara kadhaa mfululizo akidhani labda kuna mtu anamkunbuka au anamlaani.

Akiwaza tu, Kendrick alimpigia, “Unanimiss?”

"Nadhani wewe ndio umenimiss." Alissa alijilaza kwenye sofa huku miguu yake miembamba akiwa ameikunja kwenye vifundo vya miguu.

“Unaweza kusoma mawazo yangu?” Kendrick alitabasamu, “Nina habari njema kwa ajili yako.”

"Kwa kweli, pia nina habari njema kwako." Alissa akaweka tabasamu hafifu.

"Inaonekana tuna konsonanti." Kendrick alitabasamu kwa kina zaidi, “Bodi ya wakurugenzi ya Nyanza Group imepitisha miradi wa ujenzi wa meli kubwa ya uvuvi. Kwa hiyo, nitakuja Mwanza kufanya kazi kwa muda na unaweza kuishi pamoja nami.
Hiyo ni nzuri?"
Kendrick pia alikuwa akimiliki kiwanda cha kusindika samaki, TanFish."

"Unatumia kampuni kwa faida ya kibinafsi." Ingawa Alissa alisema hivyo, aliguswa na Kendrick.

"Siku zote nimekuwa mwangalifu katika kutenganisha kazi na masilahi ya kibinafsi. Ni muhimu sana kwa maendeleo ya Kampuni." Kendrick alikuwa serious.

"Mwongo.” Alissa akacheka.

“Safari hii, ninaweza kuandamana na Doris kwenye shughuli za shile. Zaidi ya hayo, baba yangu pia anakuja Mwanza." Kendrick alifichua kwanza ili Alissa ajiandae, “Atawaalika wazazi wako kwenye chakula cha jioni. Chakula cha jioni hiki ni cha lazima. Huwezi kukataa tena.”

“Kwa nini nitakataa?”

“Una habari gani njema? ”

“Nimegundua leo kuwa Timothy na Melissa hawakujuana tu, bali walilala pamoja. Wakati alijaribu kutumia dawa za kulevya ili alale na mimi, njama hizo zilimgeukia Melissa mwenyewe."

Sura ya 202

Kendrick alimsikiliza Alissa kwa utulivu akiongea kuhusu mazungumzo kati ya Timothy na Melissa ambayo aliyasikia kwenye maegesho ya hospitali hiyo leo.

“Unasikiliza?” Alissa hakusikia majibu yoyote kutoka kwa Kendrick baada ya kusema mengi.

“Ndiyo. Sitaki tu kukukatisha...” Msimamo wa Kendrick ulibadilika, "Kwa nini hukuniambia kwamba Melissa alipanga njama dhidi yako?"

"Tulikuwa hatuna uhusiano wakati huo. Ningewezaje kukuambia?” wakati huo, Alissa na Kendrick walikuwa na mkataba tu, hakukuwa na hisia hata kidogo. Ingekuwa ajabu ikiwa angemwaga shida zake kwa Kendrick.

“Haina uhusiano? Halafu cheti cha ndoa ni feki?” Kendrick alipapasa uso wake kwa upole, akiwa na hofu kidogo baada ya tukio, "Kwa bahati nzuri, wewe ni mwerevu."

“Ndiyo. Hata walipanga njama na kunisakazia uchumba na mtu mwenye sifa mbaya kama Timothy. Kwa hakika ningekuwa makini zaidi hata hivyo.” Akisifiwa na Kendrick, Alissa alifurahi na kujivunia.

"Ni kweli wewe sio mjinga sana." Kendrick alicheka.

Alissa alikasirika kidogo, "Je, hiyo ni pongezi au kejeli?"

"Bila shaka ni pongezi." Kendrick alifadhaika katika sifa zake, “Bi. Mayala ni mrembo, mwerevu, mkarimu, mpole, na mwema. Kwa kweli nakupenda."

"Waoo, usiwe na sifa sana." Alissa hakuamini maneno yake, "Nitahakikisha kwamba Melissa anapata kile anachostahili."

Miaka mitano iliyopita, Melissa alipanga njama za Alissa kumsaliti na kuachana na Seidrick. Sasa, Alissa angeshughulika na Melissa kama Melissa alivyomfanyia.

“Alissa, kwanini unamchukia sana Melissa? Kwa sababu ya Seidrick?” Kendrick alimuuliza.

Alissa alikanusha haraka, “Hapana. Ni kwa sababu aliwahi kunizunguka na kuharibu maisha yangu.”

“Basi kwa nini alifanya hivyo? Alifanya hivyo kwa sababu ya Seidrick, sivyo?” Kendrick alimkumbusha Alissa kuwa maadamu wanaizungumzia hii mada, ingemhusu Seidrick.

Alissa akanyamaza kwa muda, kisha akaitikia kwa kichwa, “Ndiyo. Alimpenda Seidrick. Lakini wakati huo, Seidrick alikuwa na uchumba nami. Kwa hivyo, Melissa alifanya kila alichoweza kunizunguka na kuniumiza. Nilikuwa na umri wa miaka ishirini tu mwaka huo. Lakini kila mtu aliniacha. Nikiwa nimetengwa na kutokuwa na msaada, nilihisi kwamba kila kitu kilionekana kuwa sawa juu yangu wakati huo ... kwa hivyo, siwezi kumwacha aende zake tu.

“Sisemi hivi ili unihurumie. Nataka nikuambie tu hata ukinipinga sitaacha. Hiki ndicho anachostahili Melissa na lazima akipate.”

“Kwa nini nipinge hilo?” Kendrick alikunja uso kidogo, "Je, ndivyo nilivyo machoni pako?"

Kwa kweli, alikuwa mtu kama huyo. Muda wote akiwaza hayo hisia zote za Alissa zilikuwa zinahusiana na Seidrick, alisikitika sana.
Lakini hakuweza kuonyesha mawazo yake mbele yake.

“Hupingi?” Alissa alidhani amesikia vibaya.

“Unajua ningependa kufanya nini sasa hivi?” Kendrick alitazama juu ya anga la bluu angavu.

"Nini?" Alissa aliuliza.

"Nataka kukushika mikononi mwangu, sasa." Sauti ya Kendrick ilikuwa laini, “Katika siku zijazo, ukiwa na mimi karibu, hakuna mtu anayeweza kukudhulumu. Yeyote anayekudhulumu atalipizwa kisasi nami mara elfu.”

"Utashughulika na Melissa? Chuki kati yenu huanza na Seidrick na inapaswa kuishia na Seidrick. Fanya tu chochote unavyotaka. Nitakutengenezea njia na kukusafishia sitaha.”

Alichelewa sana kushiriki katika maisha yake ya zamani. Lakini angemthamini na kumpenda sasa na katika siku zijazo.

“Kendrick…” Alissa alinong’ona jina lake kwa upendo.

Mapenzi yake kwake yalimchangamsha na kumsogeza.

"Ikiwa unataka kunishukuru, shuka tu." Kendrick alipenda kusikia akiita jina lake.

“Uko wapi?” Mara Alissa akakaa kwenye kochi huku mapigo ya moyo yakienda kasi.

"Mlangoni kwenu. Fanya haraka kuja kuniona.” Kendrick alicheka kwa sauti ya unyonge.

"Subiri kidogo na usimame." Alissa akaweka simu yake chini na kuharakisha kwenda chumba cha kubadilishia nguo ili kuweka nguo zake vizuri.

Aliangalia vipodozi na nywele zake kwa uangalifu ili kuona kama kulikuwa na kosa lolote kwavyo. Baada ya kujiweka sawa, alitoka chumbani na kuteremka chini.

Alissa aliondoka kwenye jumba hilo na kuelekea uani. Kupitia lango lililochongwa, aliweza kumuona yule mtu aliyenyooka wima akiwa amesimama nje.

Alitabasamu na kutembea kwa kasi. Lakini alipunguza mwendo alipokuwa karibu kuufikia mlango.

Alifungua mlango na kutoka nje taratibu. Kendrick alikuwa anakaribia kusonga mbele wakati Alissa alimsimamisha. “Nimekuambia usimame tuli.”

Kendrick aliinua nyusi zake kidogo, akatoa miguu yake mirefu na kusimama kwenye kivuli. Mwangaza wa jua ulianguka na mahali pa nuru ilionekana kati ya majani. Kendrick alionekana maridadi sana.

Alissa akasogea mbele na kumkumbatia bila kuficha huku akiufunika uso wake mikononi mwake na kunusa harufu yake ya kipekee iliyomfanya atulie.

Hewa ilikuwa na harufu ya majani…

"Kwa nini unakuja kimyakimya kila wakati?" Alissa akatazama juu mikononi mwake, “Unataka kunichunguza?”

"Unafikiria nini?" Kendrick hakuchukizwa na kutokuelewana kwake, “Nilitaka tu kukusuprise.”

"Itakuwaje ikiwa hautapata kiwango sawa na suprise u
Onageuka kuwa mshtuko?" Alissa alinyoosha mkono wake na kugusa kidevu chake, "Mimi ni dhaifu sana."

"Basi unawezaje kuthubutu kunikumbatia kwa nguvu hadharani?" Kendrick alihisi joto na nguvu ya kiganja chake.

“Wewe ni mume wangu. Unataka nikumbatie mtu mwingine?” Alissa aliinamisha kichwa chake kwa kucheza, macho yake angavu yaking'aa, "Mradi tu huna shida."

“Itakuwa ajabu kama sitajali… ” Kendrick alitazama chini na kumkaribia.

Alissa alitabasamu kidogo na kushikwa na kiganja chake. Aliweza kuhisi joto la kiganja chake kikavu kupitia kitambaa cha nguo yake.
Na pumzi yake ilinyunyizia uso wake maridadi, na kufanya masikio yake yafurahi.

“Mbona unajificha?” Kendrick alihisi mgongo wake unakandamiza kiganja chake.

"Sijifichi." Alissa hakukubali.

Kendrick kisha akabusu midomo yake kwa urahisi, ambayo ilikuwa mitamu na yenye harufu nzuri kama alivyokumbuka. Alissa alifumba macho yake kwa wepesi, akihisi joto kwenye midomo yake kwa sababu yake.

Busu lake lilikuwa laini lakini kali. Alikuwa anakawia kwenye midomo yake na kuonja manukato yake.

Kendrick alikuwa na nia ya kumpa Alissa busu la upole. Lakini kadiri alivyobusu ndivyo alivyokuwa mraibu zaidi. Alitaka hata kumsugua kwenye mifupa yake na alikuwa na wazimu juu yake.

Sura ya 203

Katika mchana huu, kwanza, Alissa alikuwa na wasiwasi kidogo na kumbusu Kendrick kwa tahadhari. Hakuweza kupumzika kabisa na kujitolea kwa busu. Lakini, Kendrick alikataa kumwachilia na kumshinda kwa ustadi wake wa hali ya juu wa kumbusu, na hivyo kumfanya ahisi kuwa wao ndio pekee waliosalia ulimwenguni.

"Si ajabu mama alinyanyuka ghafla kwenda kumuona baba. Kwa hivyo unataka kumbusu baba tu." Wakati wanabusu tu, Doris alitokea mahali fulani na kuwatazama kwa tabasamu la kihuni.

Alissa alimsukuma Kendrick pale aliposikia sauti ya Doris na kuona aibu kidogo. Alinyoosha mkono kuinua nywele kwenye mashavu yake nyuma ya masikio yake yaliyokuwa yanawaka.

"Mama, unaona haya?" Doris alimtazama Alissa ambaye aliona haya, “Baba, endelea. Sitakutazama.”

Doris akafumba macho mara moja, akafunika uso wake mdogo kwa mikono yake na kugeuka.

"Unaongea ujinga gani?" Alissa alimkaripia bintiye kwa upole.

Kendrick akamvuta kidogo, kisha akamsogelea Doris na kushusha mikono yake midogo, “Umemkumbuka baba? ”

“Ndiyo.” Doris aliitikia kwa nguvu.

“Unanimissije?” Kendrick alisugua pua yake kwa kidole chake.

"Hapa, hapa, na hapa wote wanakumiss ..." Doris alielekeza kichwa chake, macho yake na kifua chake.

"Unaweza kuni'miss kwa macho yako pia?" Kendrick alichanganyikiwa.

“Sijamwona baba kwa muda mrefu. Kwa hiyo, nataka kumuona baba.” Doris alikuwa mzuri sana na aliweza kusema maneno ya kufurahisha.

“Naona.” Kendrick alinyoosha mkono na kumchukua Doris mikononi mwake, “Baba ana habari njema kwako. Baba hataondoka sasa hivi. Nitakaa na wewe hadi kazi ya mama hapa itakapomalizika. Twende pamoja nyumbani kwa Baba.”

“Kweli?” Doris alifurahi sana na kuizungushia mikono yake myembamba shingoni mwa Kendrick.

Kendrick alimkonyeza Alissa, “fikiria unachotakiwa kufungasha. Kisha tutampeleka Doris nyumbani.”

“Sawa.” Alissa alirudi kwenye jumba la familia ya Maziku kuchukua begi lake, akachukua nguo za Doris, na kuondoka.

Alissa na Doris waliingia kwenye gari la Kendrick na kwenda pamoja hadi Lake City Capripoint.

Mara tu Doris alipoingia mlangoni, alikimbia kupitia ukumbi hadi sebuleni na kuwatazama mama na baba yake, akidhani hii ndiyo nyumba aliyoitaka.

"Baba, hii ni nyumba yako?" Doris alitazama huku na kule na kujijulisha na nyumba hii mpya.

"Hii ni nyumba yetu." Kendrick akasahihisha, “Tutakaa hapa kwa muda kabla hatujahamia huko Geita. Hii pia ni nyumba yako kuanzia sasa na kuendelea.

Kendrick alitaka sana Doris ahamie Geita kwa sababu huko kuna shule nzuri ya kisasa ambayo angesimama, 'Nyanza Gold International School.'

Doris alielewa huku Kendrick akimshika mkono, “Haya. Baba atakuonyesha chumba chako."

“Sawa baba!” Doris alimfuata Kendrick kuelekea kwenye ngazi huku akimgeukia Alissa, "Mama, njoo."

Kuona Doris alikuwa na furaha sana, Alissa naye alifurahi.

Wakapanda juu na kutembea hadi chumba cha pili. Kendrick alimtia moyo Doris, “Baby, nenda kafungue chumba chako mwenyewe.”

Doris alimtazama Alissa nyuma yake, ambaye alitoa tabasamu la kumtia moyo.

Doris akasokota kitasa cha mlango kwa uangalifu na kuufungua mlango taratibu. Ulimwengu wa rangi ya pink na nyeupe ulionekana mbele yake.
"Wow, ni nzuri sana." Doris alifungua mlango na kuingia ndani.

Akaanza kukitazama kile chumba kwa macho yake makubwa mazuri. Vigae vya sakafu nyeupe vilikuwa vinang'aa. Kuta zilipakwa rangi ya pinki. Sakafu ilifunikwa na zulia kubwa la waridi, lenye viti vya waridi juu yake.

Kilichomshangaza zaidi Doris ni kwamba kitanda chake kilikuwa ni kitanda cha kasri kikiwa kimeegemea ukutani. Upande wa kulia, kulikuwa na ngazi ya kupanda juu. Upande wa kushoto, kulikuwa na slaidi ambapo angeweza kuteleza chini. Alikuwa binti wa kifalme ambaye angeishi kwenye ngome.

Mbali na hilo, meza yake, kabati la vitabu, na kabati la nguo pia vilikuwa vya mtindo wa ngome, ambavyo vilikuwa vyema sana na kumshtua.

Dirisha la ghuba liliundwa kama tatami na mito ya waridi na nyeupe juu yake. Doris angeweza kuketi juu yake na kusoma au kulala juu yake. Skrini za madirisha ya pink na nyeupe ziliinuka na kuanguka kwa upole na upepo.

Pembe ya chumba iliundwa kama makao ya midori yake, yenye wanasesere wa waridi na mwanasesere wake anayependa sana wa panda. Panda nyeusi na nyeupe ilikuwa ya kuvutia macho katika wanasesere hawa wa waridi.

Chumba hiki kilikuwa kikubwa na kizuri sana.

"Unakipenda? Nijulishe ikiwa hupendi chochote, na nitaleta fundi akibadilishe." Kendrick alimuuliza.

“Ndiyo, nakipenda. Ni kikubwa mara kadhaa kuliko chumba changu huko Dar. Ni kizuri sana, ninahisi kama binti wa kifalme.” Doris alipenda hasa kitanda ambacho kilikuwa kama ngome.

Angeweza kuamka katika kitanda hiki kila siku. Ilikuwa kama ndoto.

"Wewe ni binti yetu mdogo." Kendrick alichuchumaa chini.

Doris alimkumbatia na kumbusu usoni, macho yake yaking’aa sana, “Nnajisikia vizuri kuwa na baba!”

"Pia najisikia vizuri kuwa na binti kuniita baba." Kendrick alihisi kuwa Doris alikuwa kama binti yake. Hakukuwa na kizuizi kati yao.

Doris alikimbia kuelekea kitanda cha ngome kisha akaketi juu yake.
Kendrick akasimama taratibu. Alissa alisogea mbele na kwa kawaida akamshika mkono, “Asante kwa kumpenda sana.”

“Ni binti yangu. Ni nani mwingine ninayeweza kumpenda zaidi yake?" Kendrick alimtazama chini.

Alissa alitabasamu na kutikisa kichwa, “Doris ana furaha sana kwa sababu yako. Nilikuwa nikifikiria kwamba ikiwa ningeweza kumpa upendo wangu wote, basi asingetaka baba. Lakini nilithibitishwa kuwa si sahihi. Ningeweza kumpa kile ambacho ningeweza kumpa. Lakini alichotaka si lazima nimpe. Sasa kwa kuwa umempa alichokuwa akitaka, nataka tu kusema ni vizuri kukutana nawe.”

Kendrick akamshika mkono na kusema, "Yote ni siku za nyuma. Nitakuwa kimbilio lako kuanzia sasa na kuendelea.”

Doris alianza kupanda ngazi za upande wa kulia na kushuka tena upande wa kushoto.

“Baba, hiki ni kitanda cha kulala. Je, nilale kwenye gorofa ya juu au ya chini?” Doris akamkimbilia Kendrick.
"Fanya upendavyo." Kendrick alipiga kichwa chake.

“Sasa mimi ni mtoto pekee katika nyumba hii, basi nitalala kwenye chumba cha chini sasa. Nikiwa na kaka au dada baadaye, nitalala kwenye chumba cha juu na kumwacha kaka au dada yangu alale kwenye chumba cha chini.” Doris alifanya uamuzi.

"Utakuwaje na kaka au dada mdogo?" Alissa alikunja uso.

“Kwa kuwa Baba na Mama wamefunga ndoa, bila shaka watapata watoto.” Doris alikumbatia kiuno cha Alissa na kuuminya uso wake kwenye tumbo lake.

“Usijali. Nakubali kwamba mna mtoto mdogo. Lakini nataka dada kwanza. Ni juu yenu wawili kama mnataka kupata mtoto wa kiume au la.”

Sura ya 204

Alissa alimwangalia msichana mrembo ambaye alikuwa amebembelezwa mikononi mwake. Doris alikuwa serious. Ingawa alikuwa mdogo, alikuwa mwerevu.

Alissa alinyoosha kidole chake cha shahada cha kulia na kusukuma kidogo kwenye paji la uso la Doris, “Mtoto mdogo anajua nini?”

“Mama, mimi si mdogo. Nina umri wa miaka mitano na nitasoma shule ya msingi mwaka ujao. Najua mengi.” Doris aliinua nyusi zake, akionekana anajua kila kitu.

“Ndiyo, unajua mengi. Lakini hii kitu...” Alissa alikatishwa na Kendrick.

Alinyoosha mkono na kumshika Alissa mkono, “tutamsikiliza binti yetu katika suala hili.”

Alissa akakipiga kiwiko kiuno cha Kendrick, “Unasemaje? Yeye ni mtoto tu.”

“Mimi ni mtoto. Lakini pia unapaswa kumheshimu mtoto. Kwa sababu mimi ni mtu wa familia hii.” Doris alihisi kupuuzwa, “Mimi pia nina haki.”

“Nataka dada hata hivyo. Kwa nini tusiwe na mkutano wa familia na kupiga kura kwa kunyoosha mkono?” Doris alinyoosha mkono kumvuta Kendrick koti, “Baba, unapaswa kuwa mwadilifu. Huwezi kumsikiliza Mama kwa sababu tu unampenda. Si haki kwangu.”

“Msichana mjinga. Unaongea ujinga gani?" Kendrick alimwangalia Doris aliyekasirika, “Nampenda mama zaidi. Lakini mama anampenda Doris zaidi. Kwa hiyo, nakupenda zaidi pia.”

"Unaweza kumwambia baba kwa nini unapenda dada tu?"

"Kwa sababu dada yangu atakuwa mzuri na mwerevu kama mimi. Pia atakuwa msichana. Lakini kaka wadogo wengi wao ni wakaidi na ni watukutu sana. Sitaki kuwa na wasiwasi juu yake.” Doris alisema mawazo yake.

“Basi tutapiga kura sasa."

"Nataka dada.” Doris alikuwa wa kwanza kuinua mkono wake na kupiga kura.

"Ninampigia kura Doris." Kendrick akashika upande wa Doris.

Alissa aliwatazama wale watu wawili ambao waliungana, “Doris, sikiliza, hili si jambo linaloweza kuamuliwa kwa pupa. Mvulana au msichana wote ni watoto. Mtoto si rahisi kama kununua kabichi sokoni...

"Tunapaswa kuwajibika kwa maisha haya. Kwa hivyo, tunapaswa kufikiria kwa uangalifu kabla ya kuamua. Nitalijadili jambo hili na baba yako baadaye.”

Doris hakuelewa kabisa, lakini alitikisa kichwa kwa utii.

"Sawa, basi unacheza hapa. Nitaenda kuzungumza na Baba kuhusu jambo fulani.” Alissa kisha akampa macho Kendrick na kumwambia amfuate nje.

Kendrick kisha akatoka katika chumba cha watoto na Alissa na kuelekea chumbani kwao.

Alissa akashusha pumzi ndefu, “Unataka mtoto?”

“Wewe hutaki?” Kendrick aliuliza kujibu.

"Sidhani kama huu ndio wakati mzuri wa kupata mtoto mwingine. Nina mambo mengi ya kufanya.” Alissa alitoa udhuru, “Na sina nia ya kuwa na mtoto mwingine sasa hivi. Kwangu mimi, Doris inatosha." Hakutaka kumdanganya. Kwa hiyo, alizungumza kwa uwazi.

Alikuwa mbinafsi na hakuweza kumwambia Kendrick kuwa Doris ni mtoto wake pia ilitosha kuwa naye.

"Ikiwa huwezi kukubali hilo, unaweza kufikiria upya uhusiano wetu. Kwani, bado kuna muda kabla ya ndoa yetu kuisha. Mkataba bado ni halali kwa sasa." Alissa alivumilia maumivu ya mle ndani na kusema maneno kama hayo.

"Kwa nini unasema kitu kama hiki?" Kendrick alihisi Alissa hajamuelewa, “Mimi si mtu wa kusema jambo moja na kufanya lingine. Ninampenda Doris kama binti yangu mwenyewe. Vinginevyo, nisingekubali mara ya mwisho kule kwa Mzee Mayala kwamba Doris alikuwa mtoto wangu...

"Kusema kweli, nataka mtoto. Kwa sababu nilimuahidi baba yangu kuwa nitampa mjukuu, ili asiniruhusu kufanya uchunguzi wa ubaba na Doris. Unajua pia kuhusu hilo.” Koo la Kendrick lilicheza, "Na kikomo cha muda kilikuwa miezi sita."

“Na najua una mambo mengi ya kufanya. Mimi siwezi kuku-force. Ikiwa hutaki mtoto sasa, hatuwezi kufanya mipango yake sasa. Ninaweza kutafuta njia nyingine ya kuzungumza na baba yangu. Ikiwa hutaki kamwe mtoto, basi tunaweza kukubaliana pia. Lakini natumai utanielewa na usiseme maneno makali kama haya. Sio tu itakuumiza, itaniumiza pia."

Alissa alitazama chini tu, hakuthubutu kumwangalia Kendrick.

Kendrick alinyoosha mkono kumuunga mkono, "Alissa, isipokuwa ukifa, sitakuacha uende."

Kope za Alissa zilitetemeka kidogo mara kadhaa, "Kendrick, mimi sikustahili wewe."

Alimdanganya na kumficha kitu… Lakini alikuwa akimlinda sana na kumjali. Angewezaje kukabiliana naye? Alihisi kuwa mapenzi yake kwa Kendrick yalikuwa chini sana kuliko vile anavyompenda, na kwamba hakuwa amempa karibu kama vile alivyokuwa amempa.

“Nitaamua kama unastahili au laa. Ikiwa nadhani unastahili, basi unastahili." Kendrick akamshika mikononi mwake, akiegemeza kidevu chake kidogo juu ya kichwa chake, “Kumbuka tu kwamba chochote utakachofanya, una mimi, mumeo, nyuma yako. Kwa hiyo, nenda mbele kwa ujasiri. Fanya unachopaswa kufanya na usiwe na moyo laini. Warudishie titi kwa tat."

"Sawa." Alissa alinyoosha mkono na kumkumbatia kwa nguvu, "Kendrick, ikiwa ... namaanisha ukigundua siku moja kwamba nimekudanganya, utafanya nini?"

"Unidanganye?" Kendrick aligusa nyusi zake maridadi, “Alissa, bora usinidanganye. Sijui nitafanya nini. Ikiwa umenidanganya, basi nitakupa nafasi ya kuniambia sasa na ninaweza kuyaacha."

Alissa alibaki kimya, akionekana mwenye wasiwasi.

“Kwa hiyo umenidanganya? Unaonekana kuwa na hatia sasa.”

"Sina hatia." Alissa alijaribu kujituliza, “Ni wewe uliyenidanganya. Tulikubali kuachana na kila mtu awe kivyake baada ya miaka mitatu. Bila kutarajia, tunaishi maisha ya ndoa sasa. Unafikiri ni nani mwongo?”

"Sawa, nilikudanganya." Kendrick aliitikia kwa kichwa kuafiki, “Kwa hiyo unataka kuniadhibu vipi? Ni bora kuwa adhabu ya viboko. Nitakubali kwa hiari.”

Macho yake, hata hivyo, yakatua kwenye kitanda kikubwa kisichokuwa mbali. Alichomaanisha kilikuwa wazi sana.

Alissa alijifanya hajui lolote na kuinua mkono wake kuangalia muda, “Inakaribia saa kumi na mbili hivi. Nitaenda kufanya chakula cha jioni."

“Nimeajiri mfanyakazi wa muda aandae chakula cha jioni. Kwa hiyo, huna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu hilo.” Kendrick alimrudisha nyuma Alissa ambaye alikuwa anaharakisha kuondoka.

"Basi nitaenda kuona ikiwa kiko tayari..." Alissa aliuvuta mkono wake chini, “Ni wakati wa Doris kuwa na chakula cha jioni pia. Tafadhali acha nimwandali chakula cha jioni.”

"Ndiyo mpenzi." Kendrick alimvuta mikononi mwake na kumbusu kabla ya kumwachilia alivyotaka.

Alissa, ambaye alikuwa na haya, alimkodolea macho Kendrick ambaye alikuwa amemfanyia fujo, “Hauko makini.”

"Tunaweza kupata mtoto ikiwa niko serious?" Kendrick alijibu na alikuwa uso wa mzaha.

"Ongea na mkono." Alissa kisha akakimbia.

Sura ya 205

Ilikuwa ni siku ambayo Shule ya Chekechea aliyosoma Doris ilifanya shughuli za mzazi na mtoto.
Doris alifurahi sana. Aliamka saa 6:00 asubuhi.

Kendrick naye aliamka mapema maana alihitaji kufanya mazoezi asubuhi. Hata hivyo, Alissa aliamka saa 7:00 asubuhi kwa sababu bado alikuwa na usingizi.

Doris na Alissa waliandaa nguo zinazotumika kwa shughuli za mzazi na mtoto na wakazivaa.

Kendrick alishuka chini baada ya kuoga. Alivaa fulana nyeupe na koti jeusi la kawaida. Ingawa hakuvaa suti, alionekana mtulivu na mwenye mtindo.

Hata hivyo, alipoenda jikoni na kuona kwamba Doris na Alissa, waliokuwa wakipata kifungua kinywa, walikuwa wamevaa nguo zilezile za mzazi-mtoto, alihisi kwamba alikuwa tofauti nao.

“Baba, unaonekana mzuri sana. Lakini kwa nini huvai nguo sawa na zetu?” Doris alimtazama na kumuuliza, huku akiwa amekata tamaa machoni pake, “Sidhani kama tutaonekana kama familia ya kweli ikiwa hatutavaa nguo zinazofanana.

Kendrick alikaa chini na kumwambia Alissa, “Wewe hikuniambia nivae nguo za mzazi. Unataka kunifanya mjinga mbele ya binti yangu?"

“Hapana, sikujua.” Alissa alisikitika na kusema, “Ni kwa sababu…”

“Nipe nguo zile zile za mzazi na mtoto.” Kendrick alimuamuru.

Alissa aliacha kula. Alisikitika na hakuthubutu kumuangalia. Alisema, “Hizi ni nguo za mzazi na mtoto tulizonunua hapo awali. Nilinunua kwa ajili yangu na Doris tu wakati huo, kwa hivyo hakuna kwa ajili yako…”

Alissa hakuthubutu kumuangalia, maana alihisi ana hasira yake.

Kendrick hakusema chochote tena. Aliketi mezani na kuanza kupata kifungua kinywa.

Alijua kwamba alikuwa na hasira, lakini hakujua jinsi ya kumfariji.

Ikiwa angekutana na hali hii, pia angekasirika.

Haikuwa wikendi siku hiyo, na aliacha kazi yake kwa ajili ya kumsapoti Doris. Kwa maendeleo zaidi ya Nyanza Group, alikuwa na shinikizo jingi na kazi nyingi.

Hata hivyo, alishughulikia kazi zote muhimu kwanza, akaweka kando kazi nyingine, na kubadilisha ratiba kwa ajili ya shughuli ya mzazi na mtoto leo.

Alifurahi kwa sababu angeweza kujiunga na shughuli ya mzazi na mtoto kwa Doris na kumfanya ahisi furaha zaidi.
Hata hivyo, hakufikiri kwamba hangemwandalia nguo za mzazi na mtoto. Kwa hiyo alijisikia vibaya.

Alissa alikuwa akishughulika na mradi wa FarmCom katika kipindi hiki. Pia alisahau kumnunulia nguo za mzazi na mtoto. Kwa kweli hili lilikuwa kosa lake.

“Doris, kwa nini hukunikumbusha kumnunulia baba yako nguo za mzazi na mtoto?” Alissa alimuuliza Doris.

Doris alisema, “Baba hakuwahi kushiriki nami katika shughuli ya mzazi na mtoto, kwa hiyo niliisahau pia.”

Alikuwa akishiriki shughuli ya mzazi na mtoto pamoja na mama yake hapo awali, kwa hivyo hakutambua kwamba walihitaji kumnunulia baba yake nguo mpya za mzazi na mtoto wakati huu.

“Isitoshe, si wewe ndiyo huwa unatayarisha nguo? Unawezaje kunilaumu kwa hili?” Doris alisema na kuuma kijiko.

Baba hakuwahi kujiunga naye katika shughuli ya mzazi na mtoto, kwa hiyo kwa hakika hangeweza kufikiria kwamba wanapaswa kumnunulia nguo mpya za mzazi na mtoto.

Alissa hakujua la kusema, akamtazama Kendrick kwa siri.

Kendrick alikuwa anapata kifungua kinywa, na ni wazi alionekana kuwa na hasira.

Alissa alimnong’oneza Doris, “Baba yako amekasirika.”

Doris akasema, “Najua.”

“Basi unapaswa kumfariji. Wewe ni mtoto wake, na anakupenda sana. Nadhani atakusikiliza.” Alissa alimuomba Doris amfariji Kendrick.

Alihisi kweli Kendrick alikuwa na hasira, jambo ambalo lilimfanya aogope kidogo. Hivyo hakuthubutu kuongea naye ikabidi amuombe Doris amfariji.

Maana Kendrick asingemkasirikia Doris japo alikuwa na hasira.

"Kwanini mimi? Mama, ni mume wako, unapaswa kumfariji kama mke wake.” Doris alimtazama Kendrick kwa siri na kusema, “Wewe ni mke wake, kwa hiyo nadhani unapaswa kumfariji.”

Doris alimaliza kifungua kinywa na kusema, “Baba, mama, nimeshiba. Nitakusubiri sebuleni.” Naye akateleza kutoka kwenye kiti kwa urahisi na kukimbia.

Alissa alimtazama na hakuweza kusema chochote.

Hakuthubutu kuondoka, ikabidi abaki hapa na kujifanya anaendelea kupata kifungua kinywa.
"Vipi kuhusu kumenya yai kwa ajili yako?" Alissa akachukua yai kisha akalimenya.

Kendrick hakumjibu akaendelea kupata kifungua kinywa.

Alissa alipotaka kuweka yai kwenye sahani yake, alisimama na kusema, “Nimeshiba.”

"Je, hutaki kula yai?" Alissa naye alisimama na kumzuia asiondoke.

“Hapana, asante.” Kendrick alimtazama Alissa na kusema, "Wewe ni mwembamba sana, kwa hivyo unapaswa kula zaidi."

"Najua una hasira." Alissa hakumruhusu aende zake. Aliliweka yai chini kisha akashika pembe ya nguo yake kwa mikono yake na kusema, “Ni kosa langu. Nikumbuke kukununulia nguo zilezile za mzazi na mtoto. Lakini nimekuwa na shughuli nyingi siku hizi, kwa hivyo nilisahau.
Tafadhali naomba unisamehe."

Kendrick alimshika mikono na kumtazama kwa umakini, “Tunahitaji kujiunga na shughuli ya mzazi na mtoto leo, na shule ya chekechea inatuhitaji kuvaa nguo za mzazi na mtoto. Doris na wewe mmevaa sawa. Lakini, kama baba yake, sina nguo sawa. Sidhani kama ni sawa...

“Wakinijua mimi ni nani watafikiri nafanya makusudi, na sitaki kabisa kujiunga na shughuli hiyo. Hakika, sijali kuhusu hilo. Hata hivyo, ni muhimu kwa Doris. Akisikia jambo baya kutoka kwa wengine, anaweza kuwa na huzuni.”

"Alissa, unapaswa kujua ni mbaya."

Alissa hakujua ajibu nini tena.

"Ndiyo, najua ni mbaya. Lakini tufanye nini sasa? Bado ni mapema kwamba maduka ya nguo bado hayajafunguliwa. Sote tuna mashati meupe na suruali nyeusi. Nadhani tunaweza kuvaa mashati meupe na suruali nyeusi sare. Nini unadhani; unafikiria nini?" Hii ndiyo njia pekee ambayo angeweza kujua.

Simu yake ya mkononi iliita wakati huo, na aliposikia maneno kutoka upande wa pili wa simu, aliunganisha uso wake kidogo na kusema, "Sawa, nitakuwa hapo."

Alikata simu na kuwa tayari kuondoka. Alissa alimfuata na kumuuliza, “Unaenda wapi?”

Sura ya 206

Kendrick hakugeuka nyuma. Alikuwa na haraka na akajibu, "Lazima nishughulikie jambo la dharura sasa."

“Kendrick, vipi kuhusu shughuli? Umemuahidi Doris na kusema kwamba utajiunga naye kwenye shughuli hiyo. Hii ni mara ya kwanza unajiunga naye katika shughuli ya mzazi na mtoto. Huwezi kurudi nyuma kwa maneno yako kwa sababu una hasira na mimi.” Alissa hakutaka kumkatisha tamaa Doris.

Doris alifurahi sana kwa sababu baba yake angeweza kujiunga na shughuli hiyo pamoja naye. Alitumaini kwamba angeweza pia kuwa na baba kama watoto wengine wowote; alitumaini kwamba angeweza kuwa na baba ambaye alimpenda sana. Kwa hiyo Alissa hakutaka kumhuzunisha kwa sababu baba yake hakuweza kujiunga na shughuli hiyo kwa sababu ya kazi.

"Ni kosa langu. Tafadhali usimkasirikie Doris.” Akamwambia.

Kendrick alisaini alipoona kwamba macho yake yamebadilika kuwa mekundu. Aligusa macho yake na kusema, “Hakika nitaungana na Doris kwenye shughuli hiyo. Ninahitaji tu kufanya jambo la haraka sasa. Na nitajiunga na shughuli mara tu nitakapomaliza. Sawa?"

“Usilie. Doris atafikiri kuwa nakuonea. Unataka kumfanya anichukie?”

Alissa alisema haraka, "Simaanishi hivyo."

"Kisha nionyeshe tabasamu." Kendrick akamwambia huku akitabasamu.

Na Alissa naye akatabasamu.

“Hiyo ni nzuri. Usilie mbele ya Doris.” Kendrick alimshika mikono na kusema, “Unapaswa kwenda kumchukua Doris sasa hivi.”

"Itachukua muda gani kushughulikia kazi yako?" Alissa alikuwa na wasiwasi kwamba hangeweza kujiunga na shughuli hiyo kwa wakati.

Kendrick aliangalia saa kwenye saa yake na kusema, “Hadi saa mbili. Nitakuja haraka iwezekanavyo. Usijali.”

“Ni nini kilitokea kazini? Kwa nini unahitaji kuishughulikia sasa hivi?” Alissa aliendelea kumuuliza.

"Ni haraka sana, kwa hivyo sina budi kuishughulikia sasa hivi." Kendrick hakuwa na chaguo, "Lazima niende sasa..."

“Sawa, nimeipata. Tafadhali kumbuka kujiunga na shughuli haraka iwezekanavyo.” Alissa alifikiria zaidi hisia za mtoto, “Au atakuwa na huzuni.”

“Najua.” Kendrick aliitikia kwa kichwa kisha akaenda sebuleni pamoja na Alissa.

Doris alisimama kutoka kwenye sofa alipowaona na kusema, “Baba, mama, twende sasa?”

“Ndiyo.” Alissa alisema.

"Twende, mpenzi." Kendrick alimshika mikononi na kutoka nje ya nyumba.

Baada ya kuingia kwenye gari, Kendrick aliwapeleka kwenye chekechea peke yake.

Walihitaji kukusanyika katika shule ya chekechea saa mbili, na kisha wakachukua basi kwenda Sehemu iyoandaliwa kwa shughuli ya mzazi na mtoto. Kwa watoto, hii ilikuwa mchakato wa kujifunza na kukua. Pia iliruhusu wazazi kupata fursa ya kuandamana na watoto wao kufurahia wakati na kujifunza maarifa, na kufanya uhusiano wao wa mzazi na mtoto kuwa wa karibu zaidi.

Alissa alishuka kwenye gari na Doris, lakini Kendrick hakushuka kwenye gari. Doris alimtazama Kendrick kwa mshangao na kumuuliza, “Baba, kwa nini usiende nasi?”

"Mpendwa, tafadhali tangulia na mama yako kwa kuchukua basi kwanza. Nitaenda kutununulia nguo za mzazi na mtoto sasa. Na nitakujai ili kujumuika nawe kwenye shughuli mara tu nitakaponunua nguo. Sawa?" Kendrick ikabidi amdanganye ili asikate tamaa wala kuhuzunika.

"Sawa, tutakusubiri kwenye shughuli." Doris hakumtilia shaka, “Baba, lazima uzingatie usalama unapoendesha gari.”

"Sawa. Na pia unahitaji kufuata agizo la mama yako." Kendrick akawapungia mkono kisha akaendesha gari.

Baada ya kuondoka, Alissa aliingia shule ya chekechea akiwa na Doris.

Walipoingia katika Shule ya Chekechea, mwalimu aliwaambia wazazi, “Tafadhali wapeleke watoto wenu kwenye uwanja wa michezo ili kupanga mstari kulingana na madarasa yao. Tunakaribia kuanza safari.”

"Darasa letu lipo huku." Doris alikimbilia darasani pamoja na Alissa na kusema, “Namwona Walter!”

Walijiunga na darasa kisha wakapanga mstari. Walter na baba yake walisimama mbele yao.

Walter alipomwona Doris, mara moja aliachia mkono wa Matthew na kumwendea Doris na kumwambia, “Doris, Aunty Alissa. Tumewasubiri kwa muda mrefu. Niliogopa sana kwamba hamtojiunga na shughuli hii.”

“Wewe ni mpumbavu sana. Inachekesha sana katika shughuli ya mzazi na mtoto, kwa hivyo hakika nitajiunga nayo." Doris aligonga kidogo paji la uso wake.

Na Walter akagusa paji la uso wake na kutabasamu, "Hiyo ni nzuri."

"Hakika nitajiunga nayo." Doris alisema tena.

“Si unaye baba wa kushiriki shughuli pamoja na wewe? Kwa nini haji hapa?” Walter aligundua kuwa Doris alikuja kwa Chekechea na mama yake tu walipofika kwenye uwanja wa michezo.

"Sio kazi yako." Doris alisema, "Baba yangu atajiunga na shughuli hiyo baadaye."

"Vizuri." Walter alitikisa kichwa kisha akamwambia Mathew, “Baba, unaweza kuja nami? Nataka kujipanga nyuma ya Doris, ili nizungumze naye.”

Mathew ikabidi amfuate na kujipanga nyuma ya Doris na Alissa.

"Halo, Matthew." Alissa alimsalimia kwanza. Japokuwa alikuwa ni mke wa Kendrick, ilimbidi amheshimu kwa sababu alikuwa ni mtu wake wa juu kazini.

Mathew aliitikia kwa kichwa na kusema, “Kwa nini Bw. Kendrick hashiriki shughuli pamoja nawe?”

“Ana jambo la dharura, hivyo anatakiwa kulishughulikia kwanza. Na atajiunga na shughuli hiyo baadaye.” Alissa alimwambia ukweli.

"Vizuri." Matthew na Walter walivaa shati nyeupe na mikono ya kijani na suruali ya kijani, na mapambo ya kijani kwenye shati na suruali.

Walter alipenda dinosaur, kwa hivyo alikuwa na nguo nyingi za dinosaur.

Kisha, chini ya uongozi wa walimu, wazazi na watoto wa kila darasa walipanda basi mmoja baada ya mwingine.

Gari hilo liliendeshwa kiulaini hadi kwenye mandhari yaliyoandaliwa.

Ilichukua dakika hamsini njiani. Walipofika eneo husika walipumzika. Shughuli ya mzazi na mtoto ingeanza saa 9:30.

Shughuli ilipokaribia kuanza, Doris alihisi woga kidogo. Alimshika mkono Alissa na kusema, “Mama, baba atakuja?”

“Ndiyo atafanya hivyo. Atatimiza ahadi yake. Atafanya hivyo kwa sababu amekuahidi. Tunapaswa kumwamini.” Naye alikuwa na wasiwasi kidogo, lakini ilimbidi atulie na kumfariji Doris.

Doris alimwamini na kusema, “Sawa, tunapaswa kumwamini baba.”

Saa 9:20, walimu walitaka kuchagua viongozi wawili wa kikundi kati ya watoto. Mmoja alikuwa msichana na mwingine mvulana.

Doris aliinua mkono wake kwanza na kutaka kuwa kiongozi wa kikundi.
Na kisha walimu wakamwomba awe kiongozi wa kikundi.

Walter hakuthubutu kuinua mkono wake, lakini alijisikia furaha sana kwa sababu Doris alikuwa amechaguliwa kuwa mmoja wa viongozi wa kikundi.

Doris alikuwa kiongozi wa kikundi cha wasichana. Baada ya kupanga foleni, shughuli ya mzazi na mtoto ilianza saa 9:30.

Mchezo wa kwanza ulikuwa wa kuvuta kamba. Watoto waliwekwa katika makundi mawili yenye wastani wa idadi ya watoto. Baada ya walimu kuhesabu hadi tatu, wangeanza kuvuta kamba kwa nguvu zao zote. Hapo awali, nguvu ya vikundi hivi viwili ni sawa ...

Sura ya 207

Hatimaye, kundi la Doris lilishindwa katika raundi ya kwanza.

Lakini kulikuwa na raundi tatu kwa jumla, kwa hivyo walipata nafasi mbili baadaye. Alissa alimfariji Doris, “Sawa mpenzi. Tunaweza kufanya vizuri zaidi baadaye.”

"Vizuri."

Hatimaye, kundi la Doris lilishinda raundi moja tu, hivyo wakashindwa. Kikundi kingine kilishinda, na kila mtoto kwenye kikundi alipata bendera nyekundu.
Doris alikata tamaa kidogo. Alissa, Walter na Matthew walimfariji.

Ilikuwa kawaida kushinda au kushindwa katika michezo, na walikuwa na nafasi ya kupata bendera nyekundu baadaye katika michezo mingine.

Doris aliisahau hivi karibuni.

Kwa wakati huu, walimu waliwapeleka kutembelea msingi wa mboga shambani, na kuwaruhusu watoto kujifunza kuhusu kila aina ya chakula na mboga maishani.

Walimu waliwapa kitabu na wakawataka watafute mboga kulingana na kitabu, kisha wakapiga picha na kutuma picha hizo kwa kikundi cha WhatsApp. Ikiwa wangemaliza kazi hiyo, wangeweza kupata bendera mbili ndogo nyekundu; Vinginevyo, wangeweza tu kupata bendera moja ndogo nyekundu.

Na kisha Doris na Walter wakaenda kutafuta mboga, na Alissa na Mathew wakawafuata.

Ya kwanza ilikuwa ya nyanya chungu. Wangeweza kuitambua kwa urahisi. Na kisha walihitaji kupata mbilinganya, nyanya na kadhalika.

“Mama, nilijifunza mboga nyingi sana. Na ninazipenda zote." Doris alihisi njaa alipoona nyanya.

"Mama, hatimaye ninatofautisha kati ya vitunguu maji na vitunguu swaumu." Doris alihisi kuridhika.

"Pia nilijifunza tangawizi na Karoti huzaliana chini ya udongo." Walter pia alisema.

"Angalia, mboga hizi hupandwa na wakulima kwa bidii, kwa hivyo tusipoteze nafaka na mboga katika siku zijazo."

"Sawa. Sitazipoteza katika siku zijazo.”

Walichukua dakika 40 kumaliza kazi ya kutafuta mboga kulingana na kitabu na kupiga picha.
Doris alifurahi sana alipopata bendera mbili nyekundu.

Walimu waliwataka wacheze kwa uhuru kwa dakika kumi kisha wakusanyike kujiandaa na mchezo unaofuata. Ulikuwa mchezo ulioshirikisha baba na mama.

Doris na Walter walihisi kuchoka, kwa sababu Doris hakuwa na baba na Walter hakuwa na mama wakati wa kucheza mchezo huu.

Walipoishi Dar es Salaam hapo awali, Mamdogo wske Jane angewasaidia kucheza mchezo huu. Sasa, Jane hakuwepo, kwa hivyo Doris hakujua jinsi ya kucheza mchezo huu.

Alissa alimimina maji kutoka kwenye birika kwenye kifuniko, kisha akampa Doris, “Kunywa maji.”

Doris alichukua kifuniko chenye maji na kusema, "Mama, nahitaji kwenda."

“Mimi pia.” Walter kila mara alimfuata Doris bila kujali alitaka kufanya nini.

Mathew na Alissa walikaa pale.

Matthew alichukua chupa ya maji na kumpa Alissa, “Kunywa maji.”

“Hapana, asante. Nina maji.” Alissa akatoa chupa ya maji yaliyosafishwa kutoka kwa mkoba wake na kusema, "Unaweza kuiweka kwa ajili ya Walter na wewe mwenyewe."

Mathew alichukua maji na kunywa peke yake, kisha akamtazama tena Alissa.

Alissa alijua kwamba alikuwa na jambo la kuzungumza naye, hivyo akasema, “Kuna nini Mathew?

"Kendrick atakuja hapa baadaye?" Mathew alimuuliza kuhusu hilo tena na kumtazama, “Itakuwa vyema ikiwa anaweza kuja kujiunga na shughuli hiyo. Ikiwa hawezi kujiunga na shughuli kwa wakati, nadhani tunaweza kucheza mchezo huu wa watu watatu pamoja. Kwa sababu kila familia inahitaji watu watatu kwa mchezo huu, tunaweza kusaidiana kucheza mchezo huu. Hakika, tunafanya hivyo ili kuwafurahisha watoto wetu. Sitaki kuwakatisha tamaa.”

"Naelewa." Alissa aliangalia muda na hakua na uhakika kama Kendrick atakuja kujiunga na shughuli hiyo au la, hivyo akajibu, “Sawa hata mimi nadhani tusaidiane kuchezesha mchezo huu kwa kuchelewa, watoto wetu wasije kukata tamaa.”

Doris alipotoka chooni, alizungukwa na watoto kadhaa. Watoto wakasema, “Doris, si ulisema kwamba baba yako atakuja kujiunga nawe katika shughuli hii? Kwa nini haji hapa leo?”

"Baba yangu ana jambo la kufanya kwa sasa, na atakuja hapa baadaye."

“Ni karibu saa sita mchana. Sidhani kama atakuja baadaye.”

"Nimesikia kuwa huna baba kabisa."

“Upuuzi! Nina baba. Walter anamfahamu.”

Walter alikubali kwa kichwa na kusema, "Nilimwona baba yake hapo awali, na alionekana kuwa mzuri sana."

"Walter, lazima akudanganye. Hana baba hata kidogo.”

“Ndiyo. Doris, umesema uwongo. Unawezaje kumfanya Walter kusema uwongo, pia?"

“Hatusemi uwongo kwenu. Tunakuambia ukweli tu.”

“Wewe ni mwongo!”

"Hapana."

"Doris, huna baba, na Walter hana mama. Vipi kuhusu kumwomba mama yako na baba yake kucheza mchezo wa watu watatu pamoja?”

"Wewe ni mbaya sana."
Doris alikasirika sana na kuelekea kumsukuma mtoto aliyekuwa na jeuri zaidi.

Ndipo mtoto akaanguka chini na kuanza kulia, “Doris kanipiga! Doris alinipiga!”

Alipiga kelele huku akilia, na mara akavutia watu wengi.

Watoto wengine walikwenda kumwambia Alissa kuhusu hilo.

"Nini?" Kwa haraka Alissa akasimama na kumfuata mtoto ili kuona kinachoendelea.

Mathew naye akawafuata kwa haraka. Alipofika chooni, aliona msichana mnene kidogo ameketi chini na kulia kwa sauti.
“Oh, mpenzi wangu. Umeumia??"

Mmoja wa walimu alifika pale na kujua kilichotokea. Na kisha akamwambia Doris, “Doris, ni kukosa adabu kumsukuma mwanafunzi mwenzako. Unapaswa kumwambia Erica samahani."

“Ninakubali kwamba nilimsukuma, lakini sifikirii ningeweza kumsukuma kwa nguvu zangu sasa hivi. Alianguka chini kwa makusudi. Kwa hiyo sitamuomba msamaha.” Doris alisema kwa uthabiti.

“Madam, tazama, hana adabu! Alimsukuma Erica na hata kubishana na wewe. Anawezaje kufanya hivyo?” Mama Erica alikasirika sana, akamlaumu Doris.

Mwalimu naye hakuridhika Doris aliposema hivyo. Akamwambia tena Doris, “Doris, ni kosa lako kwa sababu unamsukuma kwanza.
Kwa hiyo ni lazima umuombe msamaha.”

“Alisema kwamba sina baba, na kwamba mimi ni mwongo. Lakini nina baba yangu." Doris aliendelea kubishana naye.

"Kama inavyotarajiwa, hakuna baba anayekufanya kuwa mzazi mbaya. Madam, kama tunavyojua, familia yetu imetoa pesa nyingi sana kwa Shule ya Chekechea. Nafikiri unapaswa kumfukuza mtoto kama yeye, au atakuwa na matokeo mabaya kwa watoto wengine.” Mama Erica alisema kwa majigambo.

"Sawa, sidhani kama unapaswa kuzungumza sana hivyo." Baba Erica alimshika Erica mikononi mwake.

Mama Erica alijipamba kwa kujitia, na hata alivaa pete yenye rubi kubwa kwenye kidole chake kimoja. Ilionekana kuwa alijionyesha kwa makusudi.

Baada ya kusikia hivyo, Alissa alisonga mbele kumlinda Doris na kusema, “Mimi ni mama yake. Tafadhali tuwe na uvumilivu kwa watoto.”

“Kwa nini? Binti yako alimsukuma Erica juu kwanza. Kwa nini tuwe na wanyonge kwako?” Mama Erica aligombana naye.

Nina baba. Baba yangu atakuja hapa baadaye kwa sababu ameniahidi.” Doris alisema tena.

"Ndio, nitakuja hapa kwa sababu nimekuahidi." Katika umati huo, Alissa alisikia sauti aliyoijua. Na kisha akamuona Kendrick akitembea chini ya jua alipotazama nyuma.

Sura ya 208

Kila mtu, kutia ndani Doris, Alissa, Walter na Matthew, walimtazama Kendrick. Wakati huo, watu wengi walishangaa kwa sababu alionekana kuwa na nguvu sana.

“Baba.” Doris aliachana na mkono wa Alissa na kumkimbilia Kendrick kwa furaha, kisha akaingia mikononi mwake, “Hatimaye umefika.”

Kendrick alimshika mikononi mwake na kumwambia kwa upole, “Mpenzi wangu, samahani sana, nimechelewa na kukufanya usieleweke na wanafunzi wenzako. Ni kosa langu. Kwa kuwa nipo hapa, sitaruhusu mtu yeyote akuonee bila sababu.”

“Baba najua uko busy. Naweza kukuelewa. Lakini usinidharau. Sitamruhusu mtu yeyote kunidhulumu.” Doris alisema kwa nguvu kwa sababu hakutaka wazazi wake wawe na wasiwasi juu yake.

"Mpenzi wangu, wewe ni mgumu sana." Kendrick alimshika mkono na kuelekea kwenye umati wa watu pamoja naye.

Alivaa nguo nyeupe za mzazi na mtoto na muundo wa panda na mikono nyeusi na suruali nyeusi. Ilikuwa ni sura ya panda mbele na nyuma ya nguo. Ilionekana kupendeza sana na Kendrick bado alionekana mzuri na mwenye nguvu kwa kuivaa.

Kwa kuwa alionekana mwenye nguvu nyingi, hakuna aliyethubutu kumwangalia moja kwa moja.

"Bwana Kendrick...” Mathew alimsalimia kwa heshima.

Watu wengine hawakuwa na utulivu tena walipoona Mathew anamheshimu sana. Kwa kuwa ilikuwa ni shule ya chekechea ya kibinafsi kwa waheshimiwa, watu wengi walimjua Mathew. Hivyo ilibidi wafikirie ni nani Kendrick.

"Nani alisema binti yangu hana baba sasa hivi?" Kendrick alitazama huku na huko kisha akaitazama familia ya Gaba.

Ilimfanya mama Erica atetemeke.

"Binti yako alimsukuma binti yangu juu." Mama Erica alisema.

“Kwa nini alimsukuma binti yako? Sidhani kama angemsukuma binti yako bila sababu yoyote ile. Kwa hiyo nataka kujua sababu iliyomfanya kumsukuma.” Kendrick alisema kwa sauti ya chini, lakini ilisikika sana.

“Mjomba, Doris alimsukuma kwa sababu Erica alisema kuwa Doris hana baba, na hata alisema mimi na Doris ni waongo. Alisema tunapaswa kumwomba baba yangu na mamake Doris kucheza mchezo wa watu watatu kwa sababu sina mama na Doris hana baba…” Walter alimweleza Kendrick kwa urahisi.

Baada ya Walter kueleza, watu wengi walishangaa. Mathew pia alikasirika, akasema, “Bw. Gaba na Bi. Gaba, unawezaje kumtia adabu mtoto wako kwa njia hii? Sidhani yeye ni bora kuliko kijana wangu, ingawa ana mama na baba.

"Bwana. Mathew, lilikuwa kosa.” Bwana Gaba alisema na kisha akamuuliza binti yake, aliyekuwa akilia mikononi mwake, “Erica, ulisema hivyo?”

Erica alikunja uso kisha akalia tena kwa nguvu.

“Upuuzi! Sidhani binti yangu angesema hivyo.” Bi Gaba alihuzunika alipomwona binti yake akilia, “Unawezaje kumdhulumu mtoto namna hii?”

“Unazungumzia nini?” Kendrick alikasirika zaidi aliposikia hivyo, "Hao ni mke wangu na binti yangu, mimi, Kendrick Mayala, sitamruhusu mtu yeyote kuwadhulumu."

Kendrick Mayala? Je, ilikuwa familia ya Mayala wale matajiri wa dhahabu?

Baada ya kusikia jina la Kendrick, Bwana Gaba alishtuka.

Kendrick Mayala alikuwa maarufu katika mzunguko wa biashara, hivyo kila mtu alimjua, isipokuwa alikuwa mtu asiyemjua kwa sura.

Na Bi Gaba alikuwa mtu wa namna hiyo ambaye alikuwa mjinga. Alisema, "Siruhusu mtu yeyote kumdhulumu binti yangu, pia."

"Nyamaza." Bwana Gaba alimlaumu kisha akamtazama Kendrick huku akitabasamu, “Mr. Kendrick, binti yangu hakuwa na adabu sasa hivi. Nitamtia adabu baadaye. Tafadhali msamehe.”

“Kwa nini? Kwa nini binti yangu aonewe hivyo?” Kendrick alimtazama Doris kwa upole.

“Samahani sana kwa hilo. Nitamwomba Erica aombe msamaha kwa binti yako sasa hivi.” Bwana Gaba alisema kwa haraka.

Ndipo akamweka binti yake chini na kusema, “Mpenzi, hukupaswa kuzungumza naye namna hiyo. Kwa hiyo unapaswa kumuomba msamaha.”

Erica akatikisa kichwa na kujificha nyuma ya mama yake, "Hapana, sitamwomba msamaha ... Mama, sitaki kumwomba msamaha."

“Binti yake alimsukuma kwanza. Kwa nini tunahitaji kuwaomba msamaha?” Bi Gaba aligombana nao kwa ajili ya bintiye.

“Ni kwa sababu binti yetu aliwadhihaki hivyo. Kwa hiyo lazima aombe msamaha.” Bwana Gaba alikuwa na wasiwasi sana.

"Kwa hiyo? Angalau binti yangu hakuwapiga. Yeye ni mbaya zaidi kwa sababu alimsukuma binti yangu." Bi Gaba hakukubaliana na mumewe, hivyo akabishana naye.

“Doris hakumpiga. Alisukuma tu bega lake kidogo, na kisha Erica akaanguka chini peke yake." Walter alielezea tena.

"Wewe ni mtoto tu, sidhani unachosema ni cha kuaminika." Bi Gaba alikoroma kidogo.

“Binti yako pia ni mtoto. Sidhani anachosema pia ni cha kuaminika.” Mathew alidhihaki na kusema, “Bi. Gaba, huwezi kwenda mbali sana.”

"Nadhani nyinyi mnaenda mbali sana." Bi Gaba alibishana nao tena huku akiwatazama Mathew na Kendrick.

"Kwa kuwa unafikiria hivyo, naweza kushinikiza zaidi." Kendrick alionekana kupoa, “Ni jukumu lako kumsomesha mtoto wako mwenyewe kama mzazi. Sitamlaumu mtoto, lakini, kama wazazi wake, mnapaswa kuchukua jukumu hili.

"Bwana Gaba, nadhani pia unapaswa kuwajibika kwa hili, vinginevyo, hutajua jinsi ya kumlea mtoto wako vizuri." Mathew hakuweza kumvumilia tena, kwa sababu alikuwa na kiburi sana. Kwa hiyo alihitaji kumpa somo.

"Unataka kufanya nini?" Bi Gaba aliogopa kidogo sasa.

"Hebu tuwasikilize watoto kwanza." Alissa alitaka kujua ukweli kwanza, “Madam, unaweza kuwauliza watoto ikiwa Walter alisema uwongo sasa hivi?”

"Sawa." Mwalimu aliogopa kwa sababu ya Kendrick na Mathew, hakuthubutu kuwaudhi.

“Watoto, nisikilizeni. Mnaweza kujua kama Walter alituambia ukweli sasa hivi? Tafadhali kuweni jasiri na mniambie ukweli, nitawalinda.” Mwalimu aliuliza watoto.

"Ndio, Walter alisema ukweli tu. Ni kweli Erica anamzomea Doris kwanza.” Mtoto mmoja aliinua mkono wake na kusema. Na kisha watoto wengine walikubaliana naye.

“Tangu Doris aje katika Shule yetu ya Chekechea, wengi wetu tulipenda kucheza naye. Erica alifikiri kwamba hatupendi kucheza naye kwa sababu ya Doris, kwa hiyo hatukumpenda.”

“Doris alipokuja katika Shule yetu ya Chekechea, alitupa picha zilizotiwa sahihi za Jerome Wa Rising Boys. Hata hivyo, Erica alisema kwamba picha hizo zilikuwa za uwongo, na hata alizitupa."

Sura ya 209

"Erica alianguka chini kwa makusudi sasa hivi. Doris hakuwahi kumdhulumu mtu yeyote katika Shule yetu ya Chekechea.”

"Erica hakuturuhusu kucheza na Doris, vinginevyo, angekasirika na kutulaani."

“Mara nyingi Erica huwadhulumu wanafunzi wenzetu. Na alisema baba yake alikuwa tajiri sana. "
Kwa hivyo wengi wetu hatukupenda kucheza naye."

Watoto wengi walianza kusema ukweli.

Baada ya watoto kulalamika, Bwana Gaba na Bi Gaba walijisikia vibaya na kuaibika. Hata hivyo, Bi Gaba hakufikiri kuwa ni kosa la binti yake.

“Nyie… Nyinyi nyote mlizungumza upuuzi! Je, Doris na Walter waliwaambia mseme hivyo?” Bi Gaba alikasirika sana na kuwalaumu watoto.

"Bi. Gaba, tafadhali tulia. Utawatisha watoto.” Mwalimu hakuridhika.

"Bi. Gaba, unawezaje kumshtaki mtoto wangu?Watoto wengi walisema kwamba ni kosa la binti yako. Unafikiri wote walisema uongo? Sidhani hivyo.”

“Wewe… Wewe…” Bi. Gaba alikasirika sana asiseme chochote, “Nyinyi ni wabaya sana!”

"Nyamaza!" Bwana Gaba alikasirika na kutikisa kichwa kwa kujiuzulu.

"Wanamnyanyasa binti yetu sasa!" Bi Gaba alitaka kumlinda binti yake mwenyewe.

"Nyamaza!" Bwana Gaba alimkatisha kwa hasira.

“Kama…” Bw. Gaba alimuonya, “Ukithubutu kusema chochote tena, nitakupa talaka!”

Bi Gaba alishtuka kwa muda kisha akasema, “Unawezaje kusema hivyo? Kwa nini usijaribu uwezavyo kumlinda binti yetu? Unawezaje kunitaliki? Mwanaharamu wewe!”

“Ndiyo, mimi ni mwanaharamu! Lakini sitaki kuwa maskini kama Timothy Jabo!” Kairo Gaba hakutaka kumuudhi Kendrick, kwa sababu hakutaka kupata kushindwa kabisa kama Timothy.

Bibi Gaba aliacha kulia mara moja na alishtuka sana, "Nini ... Unazungumza nini?"

Bwana Gaba hakumjibu. Akasogea karibu na Kendrick na kusimama mbele ya Kendrick. Hata hivyo hakuthubutu kumwangalia Kendrick akahisi hofu kwani Kendrick alionekana baridi kweli.

"Bwana Kendrick, nina… samahani sana. Ni kosa letu. Tafadhali tusamehe.” Bw. Gaba alisema kwa heshima, “Binti yangu hajui lolote, hana hatia. Kama baba, nadhani unaweza kunielewa. Tafadhali usimlaumu.”

"Nadhani ni jukumu lako kwa sababu haukumlea mtoto wako vizuri." Kendrick bado alikuwa na hasira na kusema, “Yeye ni mtoto mdogo, lakini amekuwa mkorofi sana. Nadhani itakuwa na athari mbaya kwa watoto wengine. Kwa kuwa unampenda binti yako sana, naona afadhali umpeleke katika shule nyingine bora ya chekechea.”

Lakini, hii ilikuwa shule ya chekechea bora zaidi katika jiji hili. Ikiwa binti yao angeacha shule hii ya chekechea kwa sababu ya jambo hili, waliogopa kwamba asingekubaliwa kwa chekechea nyingine yoyote.

Lakini kama hawakufanya hivyo, Kendrick hangewaacha waende zao.
Kwa hiyo, ilimbidi Bw. Gaba akubali, “Sawa, tutaondoka hapa.”

"Sitaki kwenda shule nyingine ya chekechea." Erica alikataa kwa minong'ono.

Bi Gaba aligundua kuwa Kendrick labda alikuwa mtu wa ajabu sana, ikabidi amwambie Erica, “Jamani kama hutaki kwenda uombe msamaha kwa Doris na umuombe msamaha mama yake. Kisha unaweza kumwomba amshawishi baba yake.”

Erica alimtazama Doris. Alisema kwamba hatawahi kumwomba Doris msaada. Ikiwa angemwomba msamaha mbele ya wanafunzi wenzake, angeaibika, na hakuna mtu ambaye angemsikiliza wakati ujao.

"Ni kwa kufanya hivi tu unaweza kukaa hapa."

Erica akajishika mdomo kisha akaelekea kwa Doris. Hatimaye, alibana vidole vyake na kichwa chake chini na kusema, “Doris, samahani.
Tafadhali naomba unisamehe. Unaweza kumwomba baba yako aniruhusu nibaki hapa?”

Doris alishuka kutoka mikononi mwa baba yake na kumtazama Erica aliyekuwa amesimama mbele yake na kusema, “Erica, naweza kukusamehe kwa ulichofanya. Lakini unapaswa kuwauliza wanafunzi wenzetu kama wanaweza kukusamehe.”

“Siwezi kumsamehe. Kwa sababu alininyanyasa mimi na Doris.” Walter alisema kwanza.

“Siwezi kumsamehe pia. Alininyanyasa hapo awali.”

"Hatutaki kumsamehe."

"Bwana Kendrick, tafadhali mpeleke.”

"Ndio, anapaswa kwenda katika shule nyingine ya chekechea, au atawanyanyasa watoto wetu."

Hatimaye, wazazi wote walikubaliana na Kendrick na kumwomba ahamishie shule nyingine ya chekechea.

Ni wazi kwamba Erica hakupendwa darasani. Na watoto wengi hawakuwa tayari kumsamehe au kumkubali.
Ndipo Erica akaanza kulia tena.

"Bwana Gaba, kama unavyoona, watoto na wazazi wao hawataki kumsamehe. Sidhani kama binti yako anafaa kukaa hapa tena. Kwa hivyo ni bora umpeleke kwa shule nyingine ya chekechea, na itakuwa nzuri kwake. Ikiwa atabaki, hatafurahi.

"Nadhani utajua la kufanya." Walijua kwamba hata wangesema nini, Kendrick hangewaruhusu kubaki hapa. Kendrick aliendelea, “Mr. Gaba, tafadhali tafakari mara mbili."

Bwana Gaba aliinamisha kichwa chini, na Bi Gaba akamshika Erica mikononi mwake na kujihisi kufedheheka.
Kila mtu aliridhika sana na matokeo haya.

"Madam, ni wakati wa kucheza michezo."

"Ndio, tukutane pamoja."

Kendrick akavua begi la mgongoni na kumpa Alissa na kusema, “Kuna nguo za wewe na Doris ndani. Badilisheni."

Alissa akauchukua lile begi na kumshika mkono Doris, “Jamani twende tukabadili nguo zetu”.

"Je, ni sawa na ile ya baba yangu?" Doris aliuliza huku akipepesa macho yake mazuri.

“Bila shaka. Sisi ni familia, sawa?" Kendrick aligusa kichwa chake kwa upole, na alionekana mzuri sasa.

Kwa neno moja hakuna aliyethubutu kumuudhi Kendrick kwa sababu alikuwa mwema kwa familia yake huku akiwa hana huruma na maadui zake.

"Baba nakupenda." Doris alimshika mkono na kumtaka achuchumae kisha akambusu usoni.

Kendrick alitabasamu kwa upole, kana kwamba anaogeshwa na jua kali.

Wazazi wengine na familia ya Gaba hatimaye walijua kwamba Doris alikuwa na baba na baba yake alikuwa na uwezo mkubwa, na baba yake angeweza kumfanyia kila kitu na hangeruhusu mtu yeyote kumdhulumu.

Wale waliokuwa wamemdharau Doris au kumdhulumu wote waliona aibu.

“Doris, samahani. Kwa sababu ya Erica, mara nyingi nilikudhulumu hapo awali. Lakini sitafanya hivyo tena. Je, uko tayari kufanya urafiki nami?”

Mtoto mmoja alimwomba Doris msamaha kwa dhati.

"Doris, nataka pia kukuomba msamaha."

“Doris ni rafiki yangu mkubwa. Nyinyi mnaweza tu kuwa marafiki zake wa kawaida.” Walter alisimama mbele yao na kusema.

"Ndio, wewe ni rafiki yangu mkubwa." Doris akacheka.

Kisha Doris na Alissa wakaenda kubadilisha nguo. Baada ya kubadilisha nguo walisimama pamoja na Kendrick. Na Doris alipenda zaidi kwenye nguo zenye mifumo ya panda.

Walionekana wazuri sana.

Sura ya 210


Baada ya mzozo huo sasa hivi, watoto walikusanyika tena na kuanza kucheza michezo.

Watoto waligawanywa katika makundi mawili kwa ajili ya mchezo wa watu watatu, na wangeweza kupata bendera nyekundu kwa kila mtu katika kundi lao ikiwa wangeshinda.

Baada ya watoto kujipanga, mwalimu alisema, “Tayari!” Na ndipo timu za kwanza za vikundi viwili zilianza mara tu mwalimu alipopiga filimbi.

Kendrick, Alissa na Doris walikuwa kwenye timu ya mwisho. Kendrick aliwasaidia kufunga kamba za miguu na kuzitunza vizuri.

Watu wengi walimstaajabia Alissa kwa sababu walifikiri kwamba mume wake anampenda sana, japo alikuwa mfanyabiashara mkubwa.

Ilisikika kuwa alikuwa mtu mgumu katika biashara. Bila kutarajia, alikuwa mpole sana faraghani.

Ilikuwa zamu ya Matthew na Walter kucheza mchezo huu, lakini, hawakuwa na njia ya kucheza mchezo huu kwa sababu kulikuwa na Matthew na Walter pekee. Walipaswa kumwomba mtu msaada, vinginevyo, walipaswa kuacha.

“Baba, tufanye nini?” Walter alikuwa na wasiwasi. Ilikuwa ngumu kwake kucheza mchezo huu kila wakati, lakini alitaka sana kujiunga nao.

"Nadhani tunaweza kujiunga na mchezo mwingine baadaye." Mathew hakutaka kuwasumbua watu wengine, kwa hivyo hakutaka kuuliza mtu yeyote msaada wa kucheza mchezo huu.

“Lakini nataka kujiunga nayo. Kwa kweli, nilitaka sana kujiunga nayo kila wakati.” Walter alijisikia huzuni.

"Tumecheza mchezo huu hapo awali. Walter, wakati mwingine utajifunza kukata tamaa. Mathew aligusa kichwa chake kwa upole.

“Ndiyo, baba.” Walter alilazimika kukata tamaa.

Doris alipoona kwamba Walter amekasirika, alishika mikono ya wazazi wake na kusema, “Baba, mama, tunaweza kumsaidia Walter? Alinisaidia sasa hivi, kwa hiyo nafikiri nimsaidie.”

Alissa aliwatazama Matthew na Walter na pia akawahurumia. Alisema, "Mpendwa, tunaweza kuwasaidia?"

“Unataka kuwasaidia?” Kendrick alimuuliza huku mikono yake ikiwa kifuani.

“Nadhani tunapaswa kuwasaidia. Ikiwa hutaki kuifanya, naweza kuifanya peke yangu." Alissa alisema huku akitabasamu.

“Unadhani mimi ni mbaya? Unafikiri siko tayari kuwasaidia?” Kendrick alisema kwa kutoridhika.

“Hapana, sifikirii hivyo. Nafikiri ninaweza kufanya peke yangu.” Alissa hakutaka kuonyesha mawazo yake halisi.

“Najua unafikiri hivyo.” Kendrick alisema.

Alissa alitabasamu kwa hatia. Haijalishi alikuwa akifikiria nini, Kendrick angeweza kukisia.

"Hapana, sidhani kama hivyo." Alissa hakukubali, “Nitawasaidia sasa hivi.”

Wakati huo, Kendrick alimshika mkono na kuutazama mguu wake ambao ulikuwa umefungwa pamoja na mguu mmoja wa Doris wenye kamba za mguu na kusema, “Mguu wako mmoja umefungwa kwa kamba za miguu. Nadhani naweza kuwasaidia pia.”

"Una uhakika?" Alissa alifikiri kwamba haikuwezekana, “Tafadhali kuwa muungwana, sawa?”

“Mimi ni mbaya kweli?” Kendrick alihisi kutoridhika, “Doris, unafikiri mimi pia ni mbaya?”

"Hapana. Nadhani wewe ni superman." Doris alimtazama kwa mshangao.

Kendrick alimgeukia Alissa na kumnong’oneza, “Unaona? Doris alisema mimi ni superman."

Na kisha akamtazama Alissa kwa kiburi jambo ambalo lilimfanya Alissa aone aibu.

"Vema, unapaswa kuwa muungwana mbele ya binti yetu." Alimsukuma kwa wepesi na kusema, “Kama hutaki kuwasaidia, kwa kweli naweza kufanya hivyo peke yangu. Vinginevyo, hawawezi kujiunga na mchezo."

"Hakika ninaweza kufanya." Kendrick alisema, “Kaa hapa unisubiri.”

“Haya baba! Lazima ushinde.” Doris akamwambia.

Na kisha akatembea kuelekea Mathew na Walter.

Matthew na Walter walikuwa wakizungumza na mwalimu, “Madam, tunataka kuondoka...”

“Sawa…” Kabla mwalimu hajamaliza kuzungumza, Kendrick aliwaambia, “Madam, ninaweza kuwasaidia. Kisha hawana haja ya kuondoka.”

"Bwana Kendrick?” Mathew alishangaa kidogo aliposikia hivyo.

“Mjomba upo tayari kutusaidia kweli? Walter alijisikia furaha tena.

“Hakika.” Kendrick alikubali kwa kichwa, “Asante kwa kumsaidia Doris sasa hivi. Wewe ni mwema sana. Kwa hiyo nataka kukusaidia pia.”

“Hiyo ni nzuri. Asante mjomba Kendrick.” Walter alimpigia magoti.

"Asante sana. Natumai haitakuchukua muda mwingi.” Mathew aliwatazama Alissa na Doris walipokuwa wakizungumza.

“Sisi ndio timu ya mwisho katika kundi letu. Kwa hiyo nina muda wa kutosha kukusaidia kujiunga na mchezo kwanza.” Kendrick alikuwa na muda wa kutosha kwa sababu haikuwa zamu yao kujiunga na mchezo huo.

"Asante, Bwana Kendrick." Mathew alionyesha uthamini wake kwake.

"Walter ni jasiri sana, ningependa kuonyesha shukrani zangu kwake." Kendrick alimthamini sana Walter, "Na, yeye ni rafiki mkubwa wa Doris."

Na kisha, Matthew na Walter waliweza kujiunga na mchezo tena. Kendrick na Matthew walijiunga na mchezo pamoja na Walter, jambo ambalo lilimfurahisha sana Walter na hata kusisimka. Hakuonekana kujali matokeo, kwa sababu ilikuwa muhimu zaidi kwamba angeweza kujiunga nayo.

Doris alimshangilia Walter kwa sauti kubwa.


Baada ya muda, Kendrick alilazimika kujiunga na mchezo pamoja na Alissa na Doris.

Walishirikiana wakati wa kucheza mchezo huu. Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Kendrick kujiunga na mchezo huu, lakini alifanya hivyo kwa urahisi na hatimaye wakashinda.

Chini ya uongozi wake, walitembea kwa kasi zaidi kuliko timu nyingine na kufika mahali walipoenda vizuri. Hatimaye, walishinda na kupata bendera nyekundu.

Saa sita mchana, walipata chakula cha mchana, ambacho kilikuwa kimetayarishwa shambani, na walichukua milo na mboga zao wenyewe.
Mboga zilichukuliwa kutoka shambani, ambazo zilikuwa na afya na lishe.

Hakika, ilikuwa mara ya kwanza kwa Kendrick kufurahia aina hiyo ya chakula.

Alissa hakufikiri kwamba angependa aina hii ya chakula, kwa hiyo alisema, “Ikiwa hupendi vyakula hivi, ninaweza kukupa mkate na biskuti.

"Hapana. Kama wazazi, tunapaswa kufanya vizuri zaidi. Kwa hiyo siwezi kupoteza chakula.” Ingawa hakupenda vyakula hivi, alitaka kuonyesha kuwa ni mlaji mzuri.

Alissa bado alikuwa na wasiwasi naye.
Lakini, Kendrick alionekana mwenye furaha sana ingawa alikuwa akila chakula cha mchana na aina hii ya chakula katika mazingira kama haya.

Baada ya chakula cha mchana, walipumzika kwa zaidi ya saa moja. Saa 2:00 nchana walianza kulisha baadhi ya mifugo shambani kama kuku, bata, kondoo, ng'ombe na sungura na kadhalika.

Kisha, walienda kwenye jumba la sanaa kuchora na kupaka rangi, kupiga ngoma, kuruka sarakasi, kuimba na kucheza na hatimaye wakaenda kucheza mpira na kukimbia…

Hatimaye, wangeweza kupewa zawadi kulingana na idadi ya bendera nyekundu walizopata.

Na kisha shughuli ya mzazi na mtoto iliisha kwa mafanikio.
 
USINIACHE 5:
Sura ya 211

Baada ya shughuli ya wazazi na watoto, Alissa na Kendrick walijikita tena kwa kazi zao wenyewe.

Tarehe ya zabuni ya mradi wa FarmCom ilikuwa inakaribia.

Lakini, Alissa hakuhitaji tu kutekeleza kazi yake mwenyewe, lakini pia alihitaji kumzingatia Melissa ambaye alishirikiana na Timothy kumfanyia figusufigisu. Bila shaka, hangeweza kuwaacha.

Seidrick ndiye ambaye Melissa alimjali zaidi. Njia bora ya kulipiza kisasi kwake ilikuwa kuruhusu Seidrick aone upande wake wa kihuni na kumfanya awe mchungu kama Alissa alivyokuwa.

Haijalishi alikuwa na shughuli nyingi kiasi gani, aliendelea kumpeleka na kumrudisha bintiye shuleni peke yake, na bila hali maalum, Kendrick angeenda naye.

Kuhusu kazi za nyumbani, walikuwa wameajiri mfanyakazi wa kila siku kuwasaidia kupika na kufanya usafi, jambo ambalo pia lilipunguza mizigo yao.

Baada ya chakula cha jioni, walienda kutembea na Doris.

Sio mpaka walipomlaza mtoto, walioga na kulala kitandani kwa raha.

Akiwa amewashwa na taa yenye rangi ya manjano hafifu, Kendrick alimshika Alissa mikononi mwake na kumuuliza, “unawaza nini?”

“Hakuna kitu.” Alissa akatingisha kichwa, hakutaka kumjulisha mpango wake.

"Kuhusu Timothy na Melissa?" Kendrick alikuwa anamfahamu sana.

Alissa aliganda baada ya kusikia hivyo. Alikuwa muwazi sana mbele yake.

“Haya! Unawezaje kujua kila kitu?" Alissa hakuridhika na akaelekeza uso wake kwa Kendrick, "Unaweza kuniacha sehemu fulani kwa faragha?"

“Mwili wako tayari umekuwa wangu. Unahitaji faragha gani?" Kendrick alitabasamu, huku macho yake yakiangaza kama nyota gizani.

“Jamani!” Alissa alikuwa tayari kugeuza mgongo, “Nimechoka sana. Usiku mwema."

Hata hivyo, Kendrick alimzuia asigeuke na kusema, “Kama ulivyosema awali, Melissa na Timothy wangekutana tena. Na kama tutashika mkia baada yake wakati huu, ni lazima tukusanye ushahidi wa ukafiri wake. Sivyo?"

"Inaonekana kuwa njia bora zaidi kwa sasa." Ilibidi Alissa akubali.

“Ngoja nifanye! Wewe zingatia tu kazi yako." Kendrick alimshika zaidi.

“Wewe?” Nyusi za Alissa zililegea.

"Nini? Huniamini? Au unaogopa kuwa nina madhumuni mengine?" Kendrick alimtazama usoni kwa umakini.

"Hapana. Wewe pia huna kazi?” Aliuliza Alissa.

"Haijalishi nina shughuli nyingi kiasi gani, biashara yako ni biashara yangu tu." Kendrick alibadilika na kulala kitandani na kusema, “Siku hizi kuna mtu anayemchunguza Melissa. Akishachukua hatua nyingine, nitaweza kukuonyesha ushahidi. Kuhusu jinsi utakavyoishughulikia, inategemea wewe.”

"Najua unanijali, lakini huu ni ugomvi wangu na Melissa. Nataka kulitatua peke yangu bila msaada wako.” Alissa alielewa kuwa alifanya hivyo kutokana na wema wa moyo wake, lakini hakutaka kukubali.

“Sitaki niwe tegemezi kwako kupita kiasi kwa sababu ulinzi wako utanizuia kuwa na nguvu zaidi. Nilikuwa mjinga hadi Melissa akaweza kuniumiza. Katika miaka hii mitano, nimepata uzoefu mwingi hivi kwamba nimekua na kuwa na nguvu zaidi kuliko hapo awali…

“Naogopa kwa ulinzi wako nitakuwa laini tena na nitajidharau hivyo. Nguvu ya kweli inatokana na ukuaji wa kibinafsi. Natumai utanielewa.”

Nyusi zake taratibu zikaunganishwa kwa kukunja uso. Aliogopa kwamba siku moja angeanguka bila msaada wake. Mara tu atakapokutana na msiba kama huo tena, asiweza kusimama tena.

Kwa hivyo, hakutaka kuwa tegemezi kamili kwa Kendrick na kwa njia hiyo tu angeweza kujilinda.

“Sawa.” Kendrick aliweza kumuelewa.

Aligeuka kumwangalia macho yake, akibembeleza nywele zake kwa hisia za uchungu na huruma.

"Sijafanya vya kutosha ili usijisikie salama 100% na kuweka chini uchungu akilini mwako." Alitabasamu, “Itanifanya nijisikie siwezi.”

Kendrick angeweza kushughulikia chochote isipokuwa hali ya usalama aliyohitaji. Ilimfadhaisha sana kwamba hakuruhusiwa kuingia katika ulimwengu wake.

“Usijali.” Alissa alimshika mkono na kuwa na wasiwasi, “Wewe ni bora vya kutosha. Usijilaumu. Ni mimi ambaye sitaki kuwategemea wengine sana.”

"Mimi ni tofauti na wengine na nimekuwa nikithibitisha ukweli kama huo." Kendrick alipumua kwa kujiuzulu.

"Najua wewe ni tofauti na sijawahi kufikiria kuwa haukufanya vizuri, lakini nahitaji muda zaidi." Alissa alikiri kwamba bado alikuwa dhaifu na alihitaji muda wake pale ilipobidi.
“Hakuna haraka. Tuna muda wa kutosha."

"Muda haujawahi kumtosha mtu yoyote." Kendrick alipapasa nyusi zake zilizokunjamana kwa ncha ya kidole, akijaribu kumwondolea matatizo. Aliendelea kusema, "kwa hiyo nafasi inapopatikana, itumie vizuri."

“Sawa!” Alissa alichukua hatua ya kushika kiuno chake na kutikisa kichwa kwa hisia na kushukuru.

Kendrick alitabasamu na kumbusu kwenye paji la uso wake, "Usiku mwema, mpenzi."

Alissa alifumba macho mikononi mwake na Kendrick akazima taa. Hatimaye, chumba cha kulala kikaingia gizani.

Kendrick alimkabidhi Alissa kuhusu upelelezi wa kibinafsi wa Melissa siku iliyofuata alipoenda kazini na kumuacha ajipange na kufanya maamuzi peke yake.

“Kama unahitaji msaada wangu zaidi. Jisikie huru kuniambia tu.” Kendrick pia alikumbusha, “Usalama ndio kipaumbele. Ukikabiliwa na hatari yoyote, usifanye mwenyewe, vinginevyo sitakusamehe.”

“Sawa. Nimeelewa." Alissa alitenda kwa upole.

Hadi saa 2 asubuhi, Alissa alipata maandishi kutoka kwa mpelelezi huyo 'Habari Bi Mayala, Melissa tayari ametoka.'

'Mfuate na usimpoteze au ukigunduliwa, au itakuwa ngumu zaidi katika siku zijazo. Hili ni jambo langu binafsi na ninaamini uwezo wako.' Alissa alijibu mara moja.

Alikuwa amesubiri kwa muda mrefu, akitumaini kwamba hatua zaidi ya Melissa inaweza kumpa ushahidi wenye nguvu zaidi.
'Nitafanya vizuri."

"Asante kwa bidii yako."

Gari nyeusi ilitoka taratibu kutoka kwenye jumba la kifahari la familia ya Masolwa na mpelelezi akaifuata akiwa kwenye gari lake. Gari hiyo ilisimama ilipofika hospitali maarufu ya uzazi.

Melissa alishuka kutoka kwenye gari, akiwa amevaa miwani ya jua, kofia na jozi ya viatu vya gorofa. Ingekuwa ngumu sana kumtambua ikiwa mtu hakumtazama kwa makini.

Gari iliondoka baada ya Melissa kumwambia kitu dereva.

Alionekana akitembea moja kwa moja hadi kwenye kliniki ya uzazi ya VIP na aliingia kuangalia.

Hospitalini alitumia saa moja kumaliza ukaguzi wa uzazi, kisha akaondoka hospitalini na kuchukua teksi peke yake.

Askari wa upelelezi wa Alissa bado alikuwa akimfuata na baadaye Melissa alichagua kuteremka kando ya barabara.

Alishusha kofia yake na kwenda haraka akiwa ameinamisha kichwa chake chini. Kupitia pembe kadhaa, aliingia kwenye kichochoro cha mbali, ambapo kulikuwa na hoteli nyingi za bei rahisi.

Aliingia kwenye hoteli iitwayo Luck Hotel. Mlinzi wa hoteli alimsimamisha na kumtazama Melissa juu na chini na kumuuliza, "Unamtafuta nani?"

Moja kwa moja alichukua noti ya elfu kumi na kuiweka kwenye dawati na kusema, "Nitapanda tu ghorofani na kuzungumza na rafiki kwa muda."

“O… sawa.” Mlinzi wa hoteli alivutiwa kabisa na pesa, ambayo ilitosha kumtoa arosto ya pombe kali alizokunywa usiku. “Lakini tafadhali fanya haraka.”

Kwa sababu kitambulisho chake hakikurekodiwa, mfanyakazi wa hoteli aliogopa kwamba polisi wangempa shida ikiwa wangepita kwa ukaguzi. Lakini, kwa kweli polisi walikuja hapo mara chache.

"Sawa," alisema Melissa. "Mtu akikuuliza juu yangu, usimwambie chochote."

“Nimeelewa. Nitasema sijawahi kuona mtu kama huyo." Mlinzi wa hoteli alikuwa mwerevu sana.

“Asante.” Kisha Melissa akapanda juu.

Mlinzi wa hoteli alitazama pesa mkononi, akaiweka kama feni na kuipepesa kwa nyuma ya mkono wake. Haraka akaochomoka kwenda kaunta ya pombe.

Mtu mwingine alikuja wakati mlinzi wa hoteli alificha pesa. Alitupa bahasha juu ya dawati na kusema, "Usiulize na kusema."

Kisha mtu huyo alifuatilia kwa karibu njia ya Melissa. Mlinzi wa hoteli mara moja alifungua bahasha mara tu mtu huyo alipotoweka machoni pake. Alishangaa na kufurahi kwamba kulikuwa na pesa zaidi ya kiasi alichopata kutoka kwa Melissa.

Alifikiri amekutana na Mungu wa Utajiri na akaelekea kufurahia kwa muda.
Haraka akaomba na kumshukuru mungu.

Melissa alifika chumba namba 303, na kugonga mlango mara mbili kila wakati, tatu kwa jumla.

Baadaye, mtu fulani ndani akauliza kwa sauti ya chini, “Ni nani hapo?”

“Ni mimi,” Melissa alisema, huku sauti yake ikibadilika kimakusudi.

Kisha mlango ukafunguliwa kidogo. Mtu wa upande wa pili alikuwa na tahadhari sana kwamba ni jicho tu na sehemu ndogo ya uso inaweza kuonekana. Haikuwezekana kumtambua yeye ni nani.

Kisha mlango ulifunguliwa nusu wakati Melissa alipotambuliwa. Alipoingia tu chumbani, mlango ukafungwa.

Baada ya kuchukua hatua kadhaa, Melissa alichukia sehemu hii ndogo hadi kufa kwa sababu haikuwa kubwa kama bafu yake.

Lakini, Timothy alisogea mbele na kumshika mikononi mwake. Alimbusu sana shingoni mwake na kusema, "Nimekukumbuka sana."

Melissa hakuchukizwa tu na harufu yake, lakini pia alichukia kuwasiliana naye kimwili, lakini hakuwa na chaguo ila kuvumilia.

“Niache. Nina jambo la kukuambia,” Melissa alijaribu kumshika mkono ili kukwepa kuguswa kwake.

"Haijalishi utasema nini, tufanye ngono kwanza." Timothy alikuwa na upwiru sana hivi kwamba hakuwa tayari kumwacha aende zake.
“Wow! Hakuna mwenye harufu nzuri kuliko wewe.”

Muda si muda akambusu shingoni. Melissa alitatizika huku uso wake ukijikunja-kunja, “Usijisumbue.”

"Nini?" Timothy hakuridhika na kukwepa kwake na akasema, “Tayari umefanya mapenzi na mimi. Na sasa unajifanya mwanamke asiye na hatia hapa? Kumbe!”

"Hapana." Melissa alikasirika lakini hakuthubutu kutawaliwa na hasira. “Unasukuma sana. Siwezi kumuelezea nikirudi. Itakuwa kama kumuonyesha picha na video hizo. Kwa hiyo unajaribu kuniua au kujiua? Ukafiri wangu ukigunduliwa, nawe utateseka. Nisikilize tu ikiwa unataka kupata vitu kutoka kwangu."

Timothy alikubaliana naye. Alikuwa mbaya sana kwamba sasa angeweza tu kupata pesa kutoka kwake. Bila yeye, hakuweza kupata riziki.

Alimwachilia, huku Sehemu yake ya kiume ikiwa imetuna vibaya. “Ona. nakumiss sana tu.”

“Lazima niweke wazi kuwa huu ni mkutano wetu wa mwisho. Kwa sababu familia ya Masolwa inanisimamia sana, ni vigumu kwangu kutoka nje.” Melissa hakuwa tayari kumuona tena, kwa hivyo alitoa udhuru kama huo.

“Kweli? Usinidanganye.” Timothy hakuamini, alimtazama kwa mashaka.

“Sina sababu ya kukudanganya. Kwa kweli hii ni nzuri kwetu, kwani tuko kwenye mashua moja. Mara ya mwisho nimehamisha milioni moja kwenye akaunti yako na itatosha kutumia kwa muda. Ikiwa una lolote la kuniambia, nipigie tu na nitafanya lolote niwezalo kukusaidia,” alisema Melissa.

Timothy akakaribia tena, “Nahitaji mwanamke sasa. Wacha tufanye ngono! Ninaahidi sitasukuma sana.”

"Sina uwezo leo," Melissa alisema, akiketi kitandani.

Timothy aliketi chini na kumkandamiza Melissa alipokuwa hana ulinzi. Alizuia mwanga juu yake, na kivuli juu ya uso wake.

"Ngoja nijaribu nitajua kama unaweza au huwezi." Kwa kawaida Timothy alifikiri alikuwa akitoa udhuru na haikuwa rahisi kudanganya.

Melissa alipoona mkono wake ukienda chini, uso wake ulibadilika rangi na kusema kwa sauti, “Usinishike!” Melissa hakuwa na mwelekeo wa kumwambia kuwa kutoweza kwake kulitokana na ujauzito lakini sio hedhi.

“Mbwembwe! Je, hutaki kuchezewa tu na mimi? Usipokubali, naweza tu kufichua siri yetu. Tunaona." Timothy alihisi kutotaka kwake na akakasirika.

"Unahitaji mwanamke tu, sivyo? Nitakutafutia mtu yeyote upendavyo. Kuhusu uhusiano wetu, umefikia kikomo.” Melissa akashusha pumzi ndefu, akijaribu kutulia.

“Anhaa!” Timothy aliachia mikono yake na kusimama, “Basi usinilaumu kwa kutuma picha hizi kwa Seidrick ili afurahie sura yako chafu.”

"Endelea." Melissa alikaa kitako taratibu na kusugua viganja vyake vya mikono, “Kama Seidrick atajua kashfa yetu, mbaya zaidi sitakuwa mke wake tena, lakini mimi bado ni binti wa familia ya Maziku ambayo inaweza kuhakikisha kwamba ninalishwa na kuvikwa nguo kwa maisha yangu yote...

"Na wewe je? Uliachwa tu bila kitu na Kendrick halafu utarekebishwa na Seidrick na wazazi wangu, ambayo itakuwa mbaya zaidi kuliko sasa. Endelea tu ikiwa unataka kuonja matokeo kama haya," Melissa alisema.

Melissa alisema kwa urahisi huku pembeni ya midomo yake ikinyanyua hali iliyoonyesha kuwa haogopi kutishiwa na Timothy.

Sura ya 213

Ingawa Melissa alijifanya kutojali, lakini kwa kweli alikuwa na hofu kuu kwa sababu alikuwa bado anabebwa na Timothy.

Kufanya hivyo ilikuwa ni kubeti tu ikiwa Timothy angemburuta naye chini au angeogopa kifo.
Ikiwa bado alikuwa na uchu wa maisha na pesa, angekuwa na nafasi ndogo ya kushinda kwa sababu alikuwa tegemeo lake pekee.

Kusikia hivyo, Timothy alichukizwa moyoni, lakini alikuwa akijaribu kutulia ili kupima faida na madhara ambayo angeyapata.

Ilibidi akubali kwamba Melissa alikuwa amepata kitu sawa. Ingawa asingekuwa tena mke wa Seidrick, bado alikuwa binti wa familia ya Maziku. Kama yeye mwenyewe, angempoteza Melissa kama ng'ombe wake wa pesa, angekuwa mnyonge zaidi.

Kufikia wakati huo, hangekuwa na chochote, na hata kupoteza maisha yake.

Ingawa alikuwa ameanguka sasa, bado angeweza kupata pesa kutoka kwa Melissa na kufurahia maisha yake.

Alikuwa mdogo sana hata hakuwa tayari kwenda kuzimu bila kufurahia vya kutosha, lakini ilibidi akubali ofa ya Melissa.

“Unanitisha?” Timothy alijua kwamba hakuwa na njia ya kurudi, lakini bado alitaka kuhangaika kwa muda.

“Sikutishi. Ninasema ukweli tu, ambayo yatakuwa matokeo mabaya zaidi kwetu." Melissa alisema kwa dhati, "Namaanisha, tunaweza kuwa washirika sasa lakini sio maadui wanaopanga kuharibu maisha ya kila mmoja. Alissa ni adui yetu wa kawaida. Ikiwa sio kwa sababu yake, tusingekuwa hapa. Alitufanya sote kama hivi.”

Timothy akashika ngumi, “Ni wewe uliyenishawishi nifanye hivyo, vinginevyo nisingekuwa hivi. Niliangamizwa na wewe, kwa hivyo lazima unifidie, la sivyo sitakuacha kamwe"

Sasa hangekuwa mjinga kama hapo awali na kuhusisha mambo yote mabaya kwa Alissa kulingana na kile Melissa alisema.

Kwa hakika Melissa alishindwa kujinasua, lakini sasa angewezaje kupigana na Alissa au hata kulipiza kisasi kwake? Alikuwa na bahati ya kuwa na maisha yake kushoto.

"Pia nilidanganywa na yeye." Melissa alikasirika sana wakati fulani akifikiria jambo hili, lakini kwa wakati huu ilimbidi kumtuliza Timothy kwa kuhofia kwamba angemchafua, “Pole sana kwa hali yako, lakini nimefanya niwezavyo kukusaidia. Ulisema unahitaji milioni moja na nikatafuta kiasi hicho cha pesa kwa njia zote mara moja. Kwa ajili yako, nimefanya chochote ninachoweza. Kama kweli ulinipenda kama ulivyosema, hukupaswa kunitendea hivyo.”

Melissa alionekana kuwa dhaifu na maskini, macho yake yakiwa mekundu na machozi yakitiririka, ambayo inaweza kushusha kwa urahisi ulinzi wa kiume.

Kama ilivyotazamiwa, Timothy aliguswa moyo na kuacha hasira na uadui wake. “Nimekuambia kuwa nimekukumbuka sana.
Ingawa nakupenda, bado unakaa na Seidrick na kulala mikononi mwake, lakini mimi siwezi kukugusa. Ningewezaje kutulia?”

Hakushawishika, “Kama usingesababisha mimi kuishia hivi, nisingeomba hiyo milioni moja. Hata hivyo, una deni kwangu, unapaswa kulipa kwa mwili wako."

"Kwa hivyo hukubaliani juu ya ushirikiano wetu na unataka tufe pamoja, sawa?" Melissa angeweza kufanya chochote ili kumfariji isipokuwa kwa mwili wake mwenyewe, "Ikiwa una hamu ya mwanamke, ninaweza kumpata mwanamke na kumwambia akutumikie."

Timothy hakufanya makubaliano yoyote, akifikiri kwamba hangeweza kuachwa kwa urahisi, “Hebu tufanye biashara. Leo nakutaka tu na ninaahidi hii itakuwa mara ya mwisho.”

Melissa alikunja ngumi na kubisha, "Nitajuaje kama unanidanganya?"

Timothy aliapa, "Ninaahidi na unaweza kuniamini tu."

Melissa hakuwa na chaguo na alijua kwamba kufanya biashara na mnyama kama huyo kunaweza kumvuta gizani na hangeweza kuona jua tena.

Alipoona Melissa amenyamaza, Timothy akamkumbatia tena, “Usijali. Sitafanya kama mara ya mwisho."

Timothy alimbusu uso wake laini, huku Melissa akiweza kukunja ngumi tu na kufumba macho, akibeba maumivu tena.

Timothy aliridhika na utii wake na kumkandamiza kitandani.

Melissa alijikaza kwa matarajio kuwa baada ya hapo atakuwa huru na hahitaji kutishiwa na kulala naye tena.

Wakati huo, Melissa alikuwa kama ua linaloshambuliwa na dhoruba.

Hali katika chumba ikawa ya furaha na ya kimwili.

Baada ya ngono kadhaa za kupendeza kuisha, Timothy alikuwa bado hajatosheka na kufurahia wakati huo mzuri.

Kinyume chake, Melissa alikuwa ameanza kuchukua na kuvaa nguo zake.

Ghafla, mtu alikuwa akigonga mlango, "Fungua mlango! Sisi ni polisi. Mmeripotiwa kuwa wazinzi.”

"Nani yuko hapo?" Timothy alikuwa ameganda.

Melissa alikuwa macho zaidi na alikuwa karibu kujificha bafuni mara moja bila kuvaa kikamilifu. Hata hivyo, polisi hawakuwa na subira hivyo kwa kushirikiana na meneja wa hoteli, wakafungua mlango kwa kadi ya akiba. Kwa bahati mbaya, Melissa na Timothy walishikwa na hatia.

Timothy alikuwa amelala kitandani huku sehemu yake ya juu ikiwa wazi na ile ya chini ikiwa imefunikwa na shuka tu. Melissa alikuwa amevaa nguo zake za ndani pekee
na nywele zake zilikuwa zimetimka. Juu ya sakafu kulikuwa na tishu zilizotumika na hewa ilikuwa imejaa harufu mbichi ya shahawa baada ya ngono ambayo ilikuwa ya kibabe kabisa.

Kukabiliana na polisi, sura zao zilibadilika kabisa. Walinyang'anyana shuka ili kujifunika kwa haraka.

Polisi walipoona hali kama hiyo, wakawa makini, “Vaeni nguo zenu na mje pamoja nasi.”

Melissa alikimbilia bafuni na kuvaa nguo zake na kofia kwa haraka.

Vivyo hivyo, Timothy alivaa nguo zake kwa kuangaza. Wakati huo, ilikuwa aibu zaidi.

“Sawa. Twende zetu,” alisema polisi huyo.

Kwa sababu ya kukamatwa, Melissa karibu aanguke kwa hofu.

Alijua kwamba hangeweza kuruhusu kukamatwa. Ikiwa ndivyo, maisha yake yangeharibiwa kabisa bila Timothy kufichua picha hizo.

“Bwana…” Melissa hakujua pa kuweka vidole vyake.
Yule polisi alimtazama kwa ubaridi, “Kaa kimya. Ikiwa una lolote la kusema, lihifadhi hadi utakapofika kituo cha polisi."

Alikuwa akijaribu kumpa rushwa polisi, “Bwana, unaweza tafadhali tuache twende wakati huu? Ikiwa una mahitaji yoyote, nitafanya niwezavyo ili kukidhi..."

Yule polisi akawa makini zaidi, “Mahitaji? Kuwa mwaminifu tu na usifanye hila. Harakisha."

Chini ya hali hiyo, Melissa alilazimika kuchukua hatari, "Unataka kutuachia tuende kwa kiasi gani? Naahidi sitamwambia mtu yeyote.”

Sura ya 214

Unajua unachofanya sasa hivi?” polisi huyo aliendelea kusema, “Ukitoa fedha kwa watendaji wa serikali kwa maslahi yasiyo halali, unaweza kuhukumiwa kwa rushwa. Unafikiri kukushtaki tu kwa uasherati haitoshi? Unataka malipo mashtaka zaidi?"

Maneno ya yule polisi yalimgusa sana kichwani. Alikuwa mwadilifu sana hivi kwamba Melissa aligeuka rangi kwa woga.

Melissa alijifanya maskini kwa matumaini kwamba angeweza kuonewa huruma na polisi, “Sikuwa na maana hiyo. Nakuomba tu uniruhusu niende na ninaahidi hakutakuwa na wakati mwingine. Tafadhali…”

Polisi hakujali, “Kila mtu ni sawa mbele ya sheria na hutakuwa juu ya sheria. Ukikosa kwenda, nitaita mtu akulete huko.”

“Hapana…” Melissa alirudi nyuma kwa silika, akatikisa kichwa na kukataa kukamatwa, “Niache niende tafadhali. Tafadhali…”

Melissa aliogopa kuhusu Seidrick, kwa hivyo angeweza tu kuomba rehema hapa.

"Hapana." Polisi alizungumza na wenzake nyuma yake, "Mwondoe."

Walikuja kwake. Melissa bado alikuwa akiomba na alikuwa karibu na machozi.


Lakini, hata angepinga vipi, angekamatwa mwishowe. Jambo lisilotarajiwa ni kwamba alipiga magoti na kupiga magoti kwa polisi lakini wapi. Alisema, “Nakuomba. Nililazimishwa kufanya hivyo na sikutaka. Nikikamatwa na mume wangu akijua hilo na hatanisamehe na kunitaliki. Bila yeye afadhali nife… Kwa hiyo tafadhali niruhusu niende kwa ajili ya familia yangu na nitashukuru kwa hilo.”

“Mjinga wewe!” alipiga kelele Timothy.

Polisi alisisitiza, "Hata kama hukuwa tayari au ulilazimishwa, utatoa maelezo yako katika kituo cha polisi." Bado hakuwa tayari kumpa nafasi moja zaidi, "Mwondoe."

Kwa kweli polisi walikuwa na huruma. Walikuwa wamekutana na hali kama hiyo ya kutosha. Baadhi walikuwa wakweli, wakati wengine walikuwa waongo. Lakini hata hivyo, inapaswa kueleweka kuwa ikiwa ungejua matokeo kama haya, kwa nini bado ungefanya hivyo?

Melissa alivunjika moyo kuona kwamba polisi alikuwa na uamuzi wa kumkamata.
Alisukuma polisi na kuokota kikombe mezani ili kumponda nacho polisi. Kwa bahati mbaya kilimponyoka na kushuka sakafuni, kikombe kilivunjika.

Polisi waligundua lakini hata hivyo, Melissa aliokota kipande na kukibandika kwenye kwenye shingo yake.

Aliwakodolea macho polisi hao kwa hasira, “Kama hamtaniacha, nitakufa tu hapa. Hata hivyo, sitakuwa na chaguo ila kufa mara tu mume wangu atakapojua hilo. Kwa nini isiishie hapa?”

Watu wote walipigwa na butwaa. Kiongozi wa polisi alisema, “tulia. Usijidhuru. Weka kipande chini na tuzungumze juu yake! Ingawa uasherati ni kinyume cha sheria, adhabu yake si sawa na kifo. Hatutaki kuona maafa yakitokea.”

"Isipokuwa utaniruhusu niende, sitakubali. Bora nife." Hii ndiyo ilikuwa hali yake pekee.
Mkuu wa polisi alichanganyikiwa na kubishana, “Sawa. Tafadhali iweke chini kwanza.”

"Ondoka njiani. Niruhusu nitoke!” Melissa kila mara alishika kipande hicho na kukiweka shingoni mwake. Alijua kwamba maisha yake ndiyo nafasi pekee ya kutoroka.

“Afande. Huyu mwanamke ni mjanja sana. Ikiwa anataka kufa, acha tu afe. Kuwepo kwake kutachafua hali ya hewa tu!” alipiga kelele Timothy. Hakuweza kufikiria kwamba angekamatwa peke yake kama Melissa aliachiliwa.

"Nyamaza!" Yule polisi alimuonya Timothy kwa macho yake ya ukali.

Kwa kuogopa onyo hilo, Timothy aliinamisha kichwa chake.

"Tulia. Fikiri tena. Ukipoteza maisha yako, utapoteza kila kitu.” Yule polisi alikuwa bado anajaribu kumshawishi Melissa.

“Kata ujinga. Ondoka tu njiani.” Kitu pekee ambacho Melissa alikuwa akifikiria ni jinsi ya kutoroka. Kuhusu kile polisi alisema, ilikuwa ni ujinga kabisa kwake. Alipaza sauti, “Ikiwa hutafanya kama nilivyokuambia, niangalie nikifa!”

Ghafla, Melissa alitoboa kipande hicho kwenye ngozi yake na damu ilikuwa ikitoka.

Hakukuwa na njia katika hali. Yule polisi akasema, “Sawa. Tumekuacha uende.”

Melissa akawatazama kwa kujitetea. Kisha akasonga mbele polepole na kwa uangalifu. Akageuka hatua kadhaa, akatoka mlangoni kinyumenyume.

Alipotoka tu, aliteremka chini.
“Afande. Je, tukamkamate?” aliuliza msaidizi wake.

"Haijalishi." Kiongozi wa polisi alimtazama Timothy, “Tumempata. Hakuweza kutoroka pia. Mwondoe.”

Kwa sasa, Timothy hakuwa na jambo la kujali. Bila uso na pesa, alijua kwamba jinsi alivyokuwa mtiifu, ndivyo adhabu ingekuwa nyepesi.

Aliwafuata polisi hadi kituoni bila mabishano yoyote na alikuwa tayari kurekodi ungamo lake.

Yule polisi akatoa daftari lililotayarishwa, “Jitambulishe kwanza.”

"Jina langu ni Timothy Jabo, na nina umri wa miaka 35..." Timothy alikiri kila kitu hotelini, isipokuwa kwamba alimlazimisha Melissa lakini hakutaka.

Yule polisi alimtazama kwa kichwa na kumuuliza, “Anaitwa Melissa Maziku, sivyo? Anatoka wapi na anaishi wapi?"

"Anatoka hapa hapa Mwanza, anaishi Nyakato. Yeye ni binti wa familia ya Maziku na mke wa Seidrick.Masolwa." Timothy alikiri kila kitu kuhusu Melissa, "Nimekuambia kila kitu ninachojua."

Yule polisi akauliza tena, “Je, nyote wawili mlifanya kwa hiari?”

“Bila shaka…” Timothy alitabasamu isivyo kawaida, “afande, hakukuwa na kubadilishana pesa kati yetu, kwa hivyo haipaswi kuwa uasherati, sawa?

Polisi huyo alimtazama na kuendelea kurekodi, “Hatuwezi kuhukumu kulingana na maungamo yako tu. Ni wakati tu maungamo ya mwanamke huyo yatakuwa sawa na yako, utakuwa hauna hatia."

"Swali moja zaidi, afande. Sitaingia kwenye hatia ikiwa atasema uwongo kwamba alilazimishwa?" Timothy aliogopa kwamba Melissa angeenda kinyume
naye. Kufikia wakati huo, angepatikana na hatia ya ubakaji badala ya uasherati.

Ikiwa angepatikana na hatia ya ubakaji, ingemlazimu kuwa gerezani maisha yake yote, ambayo yangekuwa mabaya mara nyingi zaidi kuliko sasa.

Uso wake ulikunjamana, akipinga kufungwa.

“Mara nyingi zaidi, katika hali kama hiyo mwanamke atakuwa mwathirika. Yule polisi akatingisha kichwa bila kupenda akifikiria ni mtu wa aina gani.

Polisi akamkabidhi Timothy taarifa iliyokamilika, “Nimemaliza. Tafadhali iangalie. Ikiwa hakuna shida, saini hapa."

Timothy alichukua karatasi na kuangalia ndani yake. Hakupata shida, lakini alisita kwa muda alipoona maneno 'waliamua kufanya mapenzi kwa hiari'.

Hata hivyo, alitia saini taarifa hiyo kwa uthabiti, akidhani kwamba itamsaidia vyema kukwepa shtaka la ubakaji.

"Utakaa ndani hadi mtu atakapokuwekea dhamana," polisi alisema.

“Asante.” Timothy alikuwa tayari ameomba msaada kwa mtu fulani, lakini hakuwa na uhakika kama mtu huyo angekuja.

Sura ya 215

Timothy aliangalia muda na kusubiri kwa wasiwasi.

Dakika kumi baadaye, mwanamume mmoja mwenye umbo la wima aliingia ndani ya kituo cha polisi na kuwauliza wafanyakazi ambao walimpa mwelekeo.
Mwanamume huyo alimtazama Timothy, ambaye alikuwa akimpungia mkono.

"Mark, hapa." Timothy alifarijika kumwona Mark akija.

Mark pia alimwona Timothy na akamwendea kwa mguu, "Umefanya nini? Kwa nini ulikamatwa katika kituo cha polisi?”

“Mimi … sijambo. Niliandaliwa tu." Timothy alikunja mdomo, “Mark, asante kwa kuja hapa, la sivyo ningelazimika kulala kwenye kituo cha polisi.”

Timothy alimsihi Mark. Mbali na Mark, hakuweza kupata mtu mwingine wa kumsaidia kwa wakati huo. Tangu ajali yake, marafiki zake na wanawake ambao kwa kawaida walicheza naye walikuwa wamemweka mbali kama virusi. Hakuweza kuwategemea hata kidogo.

Lakini Marko alikuwa binamu yake hata hivyo. Walikuwa ndugu. Kwa ajili ya babu yao, Mark angekuja.

“Umetengenezewa njama?” Uso mpole wa Mark ulikuwa baridi, “Hujui ni mambo mangapi mabaya umefanya?”

"Mark, kwa kweli sikufanya chochote kibaya." Timothy alisikitika, akiogopa kwamba Mark asingemdhamini na kumwacha hapa, “Tafadhali fanya haraka na upitie taratibu.”

Mark alipumua kisha akapitia taratibu na polisi. Aliuliza pia nini kilitokea, na kugundua kuwa Timothy na Melissa walikamatwa wakifanya uasherati kwenye hoteli hapo hapo.

Mark alikosa la kusema. Lakini alikuwa amekuja hapa na hatimaye kumdhamini Timothy.

Ingawa Timothy hakuwa na chochote, alikuwa mwanachama wa familia ya Jabo. Ilibidi Mark amsaidie kwa ajili ya mababu wa familia ya Jabo. Lakini hakutarajia Timothy angefanya tena ujinga kama huo.

Baada ya kutoka kituo cha polisi, Mark alimwambia Timothy, “Ni nini kilitokea kati yako na Melissa?”

“Amelala na mimi kwa sababu alikuwa mpweke. Unajua mume wake alikuwa karibu kufa alipokuwa mgonjwa wakati huo? Hata ikiwa sasa ni mzima wa afya, ni dhaifu sana kumridhisha.” Timothy aliongea upuuzi.

“Husemi ukweli, sivyo?” Mark hakuwa mtu wa kudanganywa kirahisi, “Hebu niambie, nimekuja hapa leo kwa ajili ya babu, lakini mara moja tu. Ikiwa una chochote baadaye, usinipigie simu. Pia nitakuingiza kwenye blacklist!”

“Mark, sisi ni ndugu. Kweli utanifanyia ukatili kiasi hiki?” Timothy alikasirika.

"Sihitaji kukukumbusha kile ambacho familia yako ilinifanyia mimi na Bibi mara moja, sivyo?" Mark hakutaka kueleza yaliyopita. Lakini kwa kuwa Timothy alisema alikuwa mkatili, angesema ukweli.

Uso wa Timothy ulibadilika isivyo kawaida, “Mark, najua nimekosea. Tusiyalete tena yaliyopita.”

Mark alikasirishwa na kushindwa kwa Timothy kufanya wema alipomtazama Timothy ambaye hakuwa na kiburi tena kama hapo awali.

“Timothy, ni muda mfupi tu umepita. Unasahau maumivu baada ya kupona?" Mark bado aliweza kukumbuka njia za kikatili za Kendrick.
Alipowaza sasa, akatoka jasho la baridi.

Kwa kweli, maadamu Timothy hakusababisha matatizo tena na kuishi maisha ya kiasi, Mark hangepuuza kabisa familia yake. Angalau, angeweza kuhakikisha kwamba wangeweza kuwa na chakula cha kutosha, mavazi na mahali pa kuishi. Lakini, Mark hakutarajia kwamba Timothy alikuwa ameishia katika hali kama hiyo, lakini bado hakujifunza somo na akawa mwanaharamu mbaya zaidi.

"Huna ujuzi mwingine ila kucheza na wanawake. Sasa, una uhusiano wa kimapenzi na Melissa, mke wa Seidrick. Unathubutu vipi?”

“Usifikiri kwamba familia ya Masolwa ni ya kuchezewa. Familia ya Masolwa na Maziku ni mojawapo ya familia kumi bora katika jiji la Mwanza. Je, umewahi kufikiria kuhusu madhara ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Melissa? Je, Seidrick atakuruhusu uende wakati anajua? Je, familia ya Maziku itakuruhusu uende wakati wanajua? Unabipu kifo tu!”

Akisikiliza uchambuzi wa Mark, Timothy aliogopa sana hivi kwamba uso wake ulibadilika rangi. Akasema kwa kigugumizi, “Mark, wewe … inabidi usaidie mimi…

“Umefanya ujinga kama huo. Nikusaidie vipi? Je! unataka nikusaidie kwa gharama ya familia nzima ya Jabo? Ninakuambia, haifai kwako! Mark alikatishwa tamaa kabisa na Timothy, “Kwa hiyo siwezi kukusaidia!”

Timothy alihisi miguu inaishiwa nguvu na kupiga magoti mbele ya Mark, akashika suruali yake, “Mark, tafadhali nisaidie. Mimi ni ndugu yako. Ikiwa babu angali hai, asingekuruhusu kusimama hivi. Ukinisaidia wakati huu, sitafanya chochote kibaya tena. Nitafanya kila utakalosema. Tafadhali! La sivyo, nitakuwa nimekufa!”

Sasa, Timothy alitambua hali aliyokuwa nayo na angekabili nini. Aliogopa sana. Bado alitaka kuhifadhi maisha yake na kuwa na furaha hadi atakapozeeka.

“Nimesema siwezi kukusaidia. Siwezi kuruhusu familia ya Jabo kuwa hatarini tena kwa sababu yako.” Mark bila kujali alimtazama Timothy ambaye alikuwa akilia kwa uchungu, “Sasa kuna njia moja tu. Unapaswa kuchukua hatua ya kukubali makosa yako na kuruhusu familia ya Masolwa ikuruhusu uende, au itabidi ujitoe mwenyewe kwa hatima yako. Ndivyo ninavyoweza kusema."

Mark alirudisha miguu yake nyuma, akapanda gari lake na kuondoka bila kuangalia nyuma.

Timothy alilitazama lile gari kisha akasimama taratibu huku macho yake yakiwa yamejaa chuki.

Je, si alikuwa akijihukumu kifo ikiwa alichukua hatua ya kukiri kosa lake? Je, angeweza kuishi? Sasa, Jambo pekee alilopaswa kufanya lilikuwa kujificha ili mtu yeyote asiweze kumpata.

Timothy akavua koti lake, akatazama chini na kuondoka kituo cha polisi.

Jioni, polisi walifuata maelezo ambayo Timothy alikuwa amewapa na kupata nyumba ya familia ya Masolwa katika Nambari 66 mtaa wa Uzunguni huko Nyakato.

Polisi walipoingia ndani, familia ya Masolwa ilichanganyikiwa na kusimama tuli.

“Naweza kukuuliza mnataka nini?” Sam aliuliza.

"Samahani, Melissa anaishi hapa?" polisi aliuliza.

"Ndio, ni mke wangu." Seidrick akasonga mbele, "Naweza kuuliza nini kilitokea?"

"Leo, mtu aliripoti kwamba kulikuwa na biashara haramu ya ngono kati ya mwanamume na mwanamke katika Hoteli ya Luck kwenye Barabara ya Makongoro.
Tulipoenda huko, tulimkuta mwanamume na mwanamke waliokuwa wametoka kufanya ngono. Mwanamke huyo alikuwa Melissa, mke wa Bwana Seidrick,” polisi walitoa maelezo mafupi.

Familia ya Masolwa iliposikia habari hii, wote walishtuka na hawakuweza kusema neno lolote kwa muda mrefu.

"Afande, umekosea?" Seidrick alipata mshtuko kwanza, “Mke wangu ni mpole na mwema. Amekuwa akikaa nyumbani wakati huu wote. Lazima kuna kutokuelewana."

“Pia tunaogopa kwamba tutafanya makosa. Ndiyo maana tumekuja hapa kuuliza.” Polisi walitoa picha, “Hii ndiyo picha tuliyopiga papo hapo. Tafadhali angalia kama huyu ni Melissa, mke wako.”

Seidrick alichukua picha na aliweza kuona vizuri uso wa mwanamke huyo. Ilikuwa ni Melissa, mke wake, bila shaka.

Sam, Maira, na Alaya pia walisogea mbele kuitazama picha hiyo na wakakubali kuwa ni Melissa.

Kwa kweli hawakuamini kuwa kashfa kama hiyo ilitokea kwa familia ya Masolwa na kwa Melissa.

Machoni mwao, Melissa alikuwa msichana mpole na mzuri. Vinginevyo, wangekubali vipi ndoa yake na Seidrick? Lakini sasa… kwa nini alikosa haya?

Mbali na hilo, alishikwa papo hapo, jambo ambalo lilileta fedheha kwa familia ya Masolwa.

Sam alifumba macho, akahisi Melissa amemwangusha. Lakini Maira alitazama pembeni na kuketi kwenye sofa tena.

Hakuwa na huzuni haswa, kwa sababu alikuwa ameona sura halisi ya Melissa hapo awali. Alifikiri kwamba hii inapaswa kuwa sura halisi zaidi ya Melissa. Tabia yake nzuri ilifichwa.

Alaya pia alihisi kwamba alikuwa amemuunga mkono mtu asiyefaa. Almuunga mkono Melissa na Seidrick. Lakini, alipata tu matokeo kama hayo.

Seidrick ndiye aliyeumia zaidi. Melissa alikuwa naye kwa miaka mingi na walikuwa wameoana miaka michache. Alimwamini kwa moyo wake wote.

Aliamini kwamba Melissa hangekuwa mtu kama Alissa, na kwamba Melissa alielewa uchungu wake na asingemdhuru na kumsaliti tena. Lakini mwishowe, alimchoma kisu cha moyoni, ambacho hata kilimpata bila tahadhari.

Seidrick akashusha pumzi kwa siri ili atulie. Ikilinganishwa na jeraha lililomletea Alissa, alihisi kwamba wakati huu alikuwa na uwezo wa kushangaza wa kuzoea haraka.

"Bwana. Seidrick, naomba kuuliza kama huyo mwanamke kwenye picha ni mkeo?” ingawa polisi walihisi huzuni ya familia, ilibidi aendelee.

“Hapana, yeye sivyo.” Sam alikanusha.

Hakuweza kukubali kuwa mwanamke huyo alikuwa Melissa. Ikiwa angekubali, sifa ya familia ya Masolwa ingeharibiwa na pia ingewafanya wengine wawacheke.

Maira, Alaya na Seidrick wote walimtazama Sam kwa mshangao, bila kutarajia angejibu hili.

Lakini Seidrick alipuuza maneno ya baba yake na kukiri, "Ndiyo, ni mke wangu."

“Nani anasema ukweli? Tuko kazini hapa, acheni utani. Kwa hiyo, tafadhali tafakarini kwa makini kabla ya kujibu.” Polisi walichukizwa kidogo.

Sam alikuwa karibu kusema kitu ndipo Seidrick alipomshika mkono na kumsimamisha, “Bwana, ni mke wangu. Baba yangu ni mzee na ana macho hafifu. Tafadhali msamehe.”

Seidrick alikubali kwa mara nyingine tena. Kwa hiyo, Sam hakuweza kusema kitu kingine chochote akaketi kwenye sofa.

Polisi walitikisa kichwa na kuiweka kando picha hiyo, “Basi tafadhali umruhusu mke wako atoke nje, Bwana Seidrick. Tunataka kumwomba atoe maelezo.”

"Hayupo nyumbani kwa sasa." Seidrick alikuwa amepanda juu baada ya kazi kumtafuta Melissa. Lakini Melissa hakuwepo nyumbani.

"Basi unajua yuko wapi?" polisi waliongeza.

"Anapaswa kuwa katika makazi ya familia yao, kwa Maziku." Kwa ujumla, ikiwa Melissa hangekuwa katika familia ya Masolwa, angekuwa katika familia ya Maziku.
Kwa hivyo, Seidrick hakuwa na shaka kuhusu aliko.

“Basi tafadhali tupeleke kwake.”

“Sawa. Lakini nina maswali kadhaa." Seidrick alikuwa na maswali mengi sana.

Baada ya polisi kutikisa kichwa, aliuliza, “Ulisema alikamatwa hapohapo. Sasa kwanini hakupelekwa kituo cha polisi kutoa taarifa? Badala yake, ulilazimika kuja nyumbani kwetu ili kumtafuta. Isitoshe, mwanamume aliyekuwa naye alikuwa nani? Nafikiri nina haki ya kujua kama mume wa Melissa.”

“Tulikusudia kumpeleka katika kituo cha polisi ili kutoa taarifa. Lakini alitutisha kwa kifo ili tumwachie aende zake. Hakuna kitu muhimu zaidi kuliko maisha. Kwa hiyo, ilitubidi tukubaliane na kumwacha aende kwa sasa.” Afisa huyo wa polisi alisema hali ilikuwa mbaya zaidi mara milioni moja, “Tumempeleka mtu huyo kituo cha polisi kutoa taarifa. Jina lake lilikuwa Timothy.”

"Nini? Yeye ni nani?” Sam aliyekuwa ameketi tu akasimama tena.

“Ni Timothy. Anatoka katika familia ya Jabo na ana umri wa miaka thelathini na mitano...”

Timothy huyu kwa kawaida ndiye alikuwa katika maoni ya familia ya Masolwa. Kwa hiyo, alikuwa mwanaharamu huyo!

“Kwa kuwa ni Timothy, basi lazima kuna kitu kibaya kwenye hiki kitu! Siamini kwamba Melissa angefanya jambo kama hilo.” Sam alifikiri kwamba yote yalikuwa makosa ya Timothy, “Lazima Timothy anajaribu kudhuru familia yetu!”

Seidrick hakusema neno akakunja uso.

Polisi walisema tena, “Bw. Seidrick, ni lini tunaweza kuondoka kwenda kwa nyumba ya familia ya Maziku kumtafuta mke wako?"

“Afande, naomba unisubiri nje kidogo. Nina jambo la kuzungumza na wazazi wangu.” Seidrick hakutaka watu wa nje wawe hapa.
Polisi nao wakaelewa wakatoka nje.

“Kwanini ulikubali kuwa ni Melissa? Je, umezingatia sifa ya familia ya Masolwa?” Sam alimkaripia Seidrick.

“Baba, hatuwezi kusema uongo mbele ya polisi. Ukweli ni ukweli. Hata kama unaweza kuficha sasa, huwezi kuificha milele. Na ni kinyume cha sheria kusema uwongo kwa polisi. Hatuwezi kujua sheria na kuivunja!” Seidrick iliweka maoni yake wazi.

“Seidrick, huyu Timothy ni mpuuzi. Sote tunaweza kuona hisia za Melissa kwa ajili yako. Hatuamini kwamba angefanya hivi. Lazima alilazimishwa na Timothy!” Sam bado alimtetea Melissa mpaka sasa.

“Baba, najua. Pia nataka mambo yaende vizuri. Lakini lazima uwe tayari kwa mabaya." Seidrick kisha akageuka na kuondoka katika nyumba ya familia ya Masolwa.

Seidrick alisonga mbele na kuongoza njia kuwapeleka polisi hadi kwenye jumba la kifahari la familia ya Maziku.

Wakati Seidrick na polisi waliponekana kwenye makazi ya familia ya Maziku, familia ya Maziku ilikuwa ikijumuika kwa chakula cha jioni. Lakini Melissa hakuwepo.

"Seidrick, nini kinaendelea?" Alex aliwatazama polisi na kuchanganyikiwa.

"Baba, mama, Melissa yuko nyumbani?" Seidrick akawauliza.

"Melissa hajisikii vizuri. Yuko juu.” Marry akajibu, “Ni nini kilitokea?”

“Hakuna kitu. Nitapanda juu na kumchukua.” Seidrick kisha akapanda ghorofani na kufika chumbani kwa Melissa.

Alisimama mlangoni na kujizuia kutokana na mihemko iliyochanganyika kabla hajabisha hodi, “Melissa, upo hapo? Ni Seidrick.”

Melissa aliposikia sauti ya Seidrick, alihuzunika sana. Kamasi zikamtoka na kuanza kulia.
Kuona kwamba hakujibu, Seidrick alisema tena, "Basi nitaingia."

Kisha akausukuma mlango ndani na kumuona Melissa akiwa ameketi kando ya kitanda. Aliinamisha miguu yake, akavuka mikono yake karibu na magoti yake, na akatazama juu kidogo.

Alipomuona Seidrick, machozi yalitiririka mashavuni mwake na uso wake ukalowa haraka.
“Seidrick…” alilia kwa kwikwi, sauti yake ikijaa huzuni na huruma.

“Nitakupeleka nyumbani. Njoo nami.” Seidrick akaenda kwake, lakini hakuketi chini.

Alimtazama Melissa ambaye machozi yalikuwa yakimtoka wala hakumfariji. Hakukuwa na joto machoni pake tena, bali baridi tu.

"Twende nyumbani?" Melissa, hata hivyo, hakuona mabadiliko ya Seidrick.

“Ndiyo.” Seidrick alisema, akinyoosha mkono kumshika mkono, "Twende."

Melissa alishikilia mkono wake kwa nguvu, kama mtu anayezama akishika majani ya mwisho na kuwa na hamu ya kuishi.

Wakati Seidrick ilipomleta Melissa chini, aliwaona polisi. Alijificha nyuma ya Seidrick na uso wake ulibadilika sana.

Alikuwa amefikiria tu kwamba angekuwa sawa ikiwa angekimbia. Lakini hakutarajia polisi wangeweza kumfuata nyumba kwao.

Angewezaje kusahau kwamba Timothy alikuwa amepelekwa kwenye kituo cha polisi? Timothy lazima alisema kitu.

Melissa alijihisi mgonjwa alipomfikiria Timothy, yule mtu mjinga.
Alikuwa ametoroka. Lakini kwa hakika Timothy angemsaliti kwa ajili yake mwenyewe na hata angesema maneno yasiyo ya kweli.

Sasa alikuwa na wasiwasi juu ya kile Timothy alikuwa amesema, na alikuwa na hofu.

Polisi na Seidrick walikuwa hapa. Aliogopa kwamba kashfa kati yake na Timothy haiwezi kufichwa tena. Alikuwa akitetemeka vibaya kwani alikuwa kwenye kuvunjika kwa mara nyingine tena.

"Bi. Masolwa, tuko hapa kukuona kwa taarifa.” Polisi walikuja moja kwa moja kwa uhakika.

“Ondokeni! Ondokeni nyie!” Melissa alifura sana.

Aliogopa kuwatazama polisi waliovalia sare na kujificha nyuma ya Seidrick, akikimbia ukweli.

"Melissa, una shida gani?" Alex alihisi huzuni huku akimwangalia binti yake ambaye alikuwa na hofu.

“Melissa, usiogope. Wao ni maafisa wa polisi, si watu wabaya.” Marry pia alimtuliza binti yake.

“Baba, mama, waache waondoke nyumbani kwetu. Sitaki kuwaona!” Melissa aliendelea kutikisa kichwa na kushika mkono wa Seidrick, “Seidrick, si ulisema utanipeleka nyumbani? Fanya haraka unichukue sasa hivi!”

Seidrick alimtazama kwa utulivu na kuuvuta mkono wake chini, "Melissa, unaogopa nini?"

"Sina hofu. Sina hofu!" Melissa alitoa macho yake na kusema kwa sauti kubwa, kana kwamba kuna kitu anaficha.

“Kweli? Sasa mbona unawaogopa sana polisi!” Seidrick alikunja kipaji kidogo.

"Sina hofu. Sitaki tu kuonana na polisi.” Melissa alikanusha.
"Bi. Masolwa, tafadhali ushirikiane nasi kutoa taarifa!” polisi nao wakawa wakali.

“Sikufanya lolote. Kwa nini ninahitaji kutoa taarifa? Nikisema nimelazimishwa! Kwa nini nyie hamwezi kuniruhusu niende? Ikiwa mnahitaji kutoa taarifa, mnaweza kwenda kutafuta wengine. Usije kwangu!” Melissa alifadhaika sana hata akashindwa kutulia hata kidogo.

Aliogopa sana kuwatazama polisi, alibaki kichwa chini, na hofu.

“Timothy ametoa kauli, na wewe pia utafanya hivyo. Tutaangalia kama taarifa zako zinalingana na kuona kama kuna yeyote kati yenu anadanganya." Polisi wakamwambia.

“Timothy? Ni nini kinaendelea?" Alex na Marry walichanganyikiwa kusikia jina hili. Na kauli…Hawakuweza kuieleza hata kidogo.

“Simjui mtu huyu!” Melissa alikana kabisa.

"Bi. Masolwa, tafadhali usifanye mapambano yasiyo na maana. Leo, wewe na Timothy mlipatikana papo hapo kwenye Hoteli ya Luck kwenye barabara ya Makongoro Road. Isingekuwa wewe kuwatishia polisi, ungetoa taarifa na kwenda nyumbani sasa hivi.” Polisi walimkodolea macho Melissa, “Hata kama utakanusha vipi, huwezi kubadilisha kilichotokea. Kwa hiyo, unapaswa kushirikiana nasi kumaliza mapema, ili tuondoke mapema.”

"Afande, unaweza kutuambia nini kinaendelea?" Alex alichanganyikiwa wakati akisikiliza hii na alitaka tu kujua ukweli.

“Ndiyo. Binti yangu amefanya nini? Na ina uhusiano gani na Timothy?” Marry alimtazama Melissa kwa huzuni. Ni nini kilimpata Melissa na kumfanya aonekane hivi?

“Sawa…” Melissa aliwakatiza polisi kabla hawajamaliza maneno yake, “Huwezi kulizungumzia! Acha!”

Melissa aliwarukia, akipunga mikono yote miwili kama simba jike aliyejeruhiwa, akijaribu kuwapiga polisi.

Kuona hivyo, Alex na Marry wakamvuta, “Melissa, huwezi kupigana na polisi. Ni kinyume cha sheria kuwashambulia polisi!”

“Baba, Mom, ni wao… Wanataka kuniharibia kila kitu…” Melissa alikuwa katika maumivu makali. Machozi yalimjaa na kuonekana mwenye huruma.

"Bi. Masolwa, tafadhali usiwe na akili mbovu!” polisi wakasema kwa ukali, “Unawezaje kutulaumu kwa ulichofanya? Tunatekeleza sheria bila upendeleo!”

“Upuuzi! Nyinyi mnanilenga kimakusudi!” Melissa alishindwa kujizuia kulia kana kwamba alikuwa amekosewa sana.

Seidrick aliendelea kumwangalia Melissa kwa ubaridi, akihisi kana kwamba mwanamke huyu hakuwa tena Melissa anayemfahamu, bali ni mwanamke wa ajabu na wa kutisha.

"Baba, ngoja niseme." Seidrick akawatazama polisi na kuwasihi.

“Sawa.” Polisi walitikisa kichwa.

Seidrick aliwatazama Bw. na Bi. Maziku waliokuwa wamemshikilia Melissa aliyekuwa analia, “Mama na Baba, leo Melissa na Timothy walinaswa papo hapo kwa biashara haramu kati ya wanaume na wanawake katika Hoteli ya Luck kwenye Barabara ya Makongoro… kwa hivyo, unapaswa kuelewa sasa.”

Alimueleza mzee huyo yote kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na polisi.

Melissa hakuthubutu kuangalia juu na kukabiliana na Seidrick. Aliendelea kulia tu, lakini hakuweza kumsogelea Seidrick hata kidogo.

"Nini!" Alex alikasirika baada ya kuisikiliza na akamtazama Melissa karibu naye, "Melissa, umefanya jambo gani?"

Marry pia alihisi kwamba habari hiyo ilikuwa kama radi kutoka angani. Ingawa alijua kwamba Melissa alikuwa amelala na Timothy mara moja, ilikuwa ajali tu, kwa sababu Melissa alikuwa amelewa dawa.

Lakini wakati huu, hakuweza kutoa udhuru wowote kwa Melissa. Kwa sababu mbele ya ushahidi wa uhakika, sababu yoyote itakuwa haina nguvu.

"Melissa, unawezaje kuwa mjinga hivyo!" Marry alihuzunika, “Ninawezaje kusema kukuhusu?”

Alex akauachia mkono wake na Marry naye akajiachia. Melissa alihisi miguu inaishiwa nguvu na kuanguka chini. Nywele zake ndefu zilifunika uso wake, na hakuna mtu aliyeweza kumuona waziwazi.

"Bi. Masolwa, tutakupa nafasi moja zaidi ya kutoa taarifa.” Polisi wakamuuliza, “Bw. Timothy alisema kwamba ulifanya hivyo kwa hiari. Ikiwa ndivyo, si shtaka la ukahaba.”

“Nililazimika kufanya hivyo. Sikufanya hivyo kwa kupenda!” Melissa alijibu kwa msisimko aliposikia "kwa hiari".

"Ikiwa ulilazimishwa, basi alikubaka na una haki ya kumshtaki." Polisi walimkumbusha.

“Nitamshtaki!” Melissa aliuma mdomo wake, macho yake yakiwa yamejaa chuki, “Nitamfanya alipe!”

Kwa hilo, Melissa alishirikiana na polisi kutoa taarifa katika utafiti huo, huku wengine wakisubiri nje.

Polisi walipoondoka baada ya kauli hiyo kutolewa, Melissa alikuja taratibu pale Seidrick aliposimama huku macho yake yakiwa yamejaa machozi, “Mpenzi, naomba unisamehe. Kwa kweli nililazimishwa kufanya hivyo. Tafadhali niamini…”

Aliinua midomo yake na karibu kulia. Lakini alijaribu kuzuia machozi yake na kumtazama tu Seidrick kwa huzuni. Macho yake yalikuwa yamejaa kuomba.

Seidrick alimtazama tu uso wake mtamu na mzuri kimya kimya, kana kwamba alikuwa akijaribu kumwona kwa uwazi, lakini akagundua kuwa alikuwa
hajawahi kuona kupitia kwake.

“Melissa, ningependa kukuamini. Lakini mambo yamefikia hatua hii. Kwa nini nikuamini?” Seidrick alitabasamu, lakini macho yake yalikuwa baridi.

Sura ya 218

Seidrick alitoa tabasamu baridi. Hakuwa tena mpole na mtaratibu kwa Melissa.
Ulimwengu wao ulionekana kuwa na theluji nyingi wakati huu, ikigandisha mioyo yao.

"Hapana, Seidrick, nililazimishwa sana. Mimi ni mke wako. Je! ungependa kuamini wengine kuliko mimi?” Akiwa ameketi chini, Melissa alimtazama juu Seidrick ambaye alikuwa kama mgeni.

"Melissa, inaonekana umesahau kuwa Bwana Seidrick aliwahi kusema kwamba kile unachosikia kinaweza kuwa cha uwongo na unachokiona ni kweli. Anaamini tu katika ukweli anaoona kwa macho yake. Hakuna ubaya katika hilo.” Alissa aliingia sebuleni kutoka nje.

Alissa alikuwa amevaa shati la rangi nyeusi ya mandhari nyuma yenye kola nyeusi na tai yenye mistari wima, suruali nyeusi ya penseli yenye pointi tisa, na jozi ya visigino virefu. Nguo zilikuwa rahisi na nzuri. Akiwa na vipodozi maridadi vya mwanga, alionekana kifahari, mwenye ujasiri na mtu mzima.

Katika miaka hii mitano, Alissa alikuwa amekua sana. Sasa alikuwa na familia yenye furaha na kazi yenye mafanikio. Kuona kwamba uso wa kweli wa Melissa ungefichuliwa, alichangamka sana.

"Seidrick, usimsikilize!" Melissa alikumbuka kawaida kwamba Seidrick aliwahi amesema hivi.

Miaka mitano iliyopita, Alissa alipotoka hospitalini akiwa na mtoto mikononi mwake, Seidrick alimwona. Bila kumpa nafasi Alissa kueleza alisema anaamini alichokiona kwa macho tu.

Sasa, ilikuwa zamu ya Melissa kupata kashfa. Alissa aliyataja maneno haya kumkumbusha Seidrick kutokula maneno yake!

"Seidrick, bado ana kumbukumbu ndefu kwa kile kilichotokea miaka mitano iliyopita. Kwa hivyo, anachukia sisi kupendana sisi kwa sisi kama wanandoa na anajaribu kwa makusudi kuleta mifarakano.” Melissa aliogopa kwamba Seidrick angeamini maneno ya Alissa.

“Nilisema hivyo. Ina uhusiano gani naye?" Seidrick alikunja uso, "Melissa, umetandika kitanda chako, acha ulale humo."

Melissa aliinua midomo yake, bila kuthubutu kudhihirisha hasira yake kwa Seidrick, na aliweza tu kumgeukia Alissa, "Alissa, uko hapa kunicheka?" Melissa alikasirika sana alipomtazama Alissa, ambaye alikuwa akitabasamu, na kufikiria hali yake ya sasa ya aibu.

“Nimerudi kuwaona Bibi na Mama na Baba.” Alissa aliweka sanduku la matunda na zawadi mkononi mwake kwenye meza ya kahawa, “Nilijuaje kuwa ulikuwa hapa?”

“Upuuzi!” Melissa hakuamini hata kidogo alichokisema Alissa.

"Amini usiamini." Alissa alitoa mabega yake.

"Alissa, kwa nini unaleta zawadi nyumbani kwako?" Uso wa Alex ukalainika na kuwa tabasamu.

Marry pia alimbembeleza, "Alissa, umepata chakula cha jioni?"

Sasa, Alissa alikuwa katika kupanda. Baada ya kuwa Bi Mayala, hata wazazi wake walipaswa kumheshimu.

Hata kama Melissa angeolewa na Seidrick, hangetendewa hivi. Kwa sababu familia ya Masolwa haikuwa na nguvu kama familia ya Mayala.

Alissa aliwaambia Alex na Marry, “Baba, hivi ndivyo wazazi wa Kendrick walivyosema niwaletee. Lishe ni kwa Bibi.
Chai na divai ni kwa ajili yako, na vito hivyo ni vya Mama."

Alex na Marry waliposikia kwamba ni kutoka kwa wazazi wa Kendrick, walifurahi. Baada ya yote, walikuwa na bahati ya kuwa jamaa na familia ya Mayala kwa ndoa.

“Nipe salamu zangu kwa wazazi wa Kendrick na kuwashukuru.” Alex alichojali sio zawadi, lakini utambuzi na umakini wa familia ya Mayala.

“Kendrick hakuja na wewe?” Marry alikuwa na wasiwasi juu ya Kendrick.

"Ana shughuli nyingi kuliko mimi." Alissa alikaa kwenye sofa na hakuwa na nia ya kuondoka, “Mama, bado sijapata chakula cha jioni. Ningependa kula ugali wa muhogo na samaki mchemsho."

"Sawa. Nitamruhusu mpishi afanye hivyo.” Kumsikiliza Alissa akimwita Mama, Marry aliendelea kutabasamu na kusahau kuwa ana mtoto mwingine wa kike, Melissa.

Alipoona kwamba mtazamo wa Alex na Marry kwa Alissa ulikuwa umebadilika kutoka kwa karaha hadi kubembeleza, Melissa alichukizwa na hasira. Sasa, Alissa alikuwa amechukua mahali pake na akawa muhimu katika mioyo ya wazazi wake.

Kwa macho ya wazazi wake, alionekana kuwa mtu asiye na umuhimu wowote. Hawakuwajali yeye na Seidrick tena.

"Mama na Baba, Melissa atakaa kwenu kuanzia wakati huu. Tafadhali mtunzeni. nitaondoka sasa hivi.” Seidrick hakutaka kula maneno yake mbele ya Alissa. Kwa hiyo, alikuwa anaenda kuondoka kwanza.

"Seidrick, usiende!" Melissa alikumbatia mguu wa Seidrick na kumvuta, “Hata kama unataka kuondoka, nipeleke nyumbani kwako. Ulisema unakuja kunipeleka nyumbani. Unawezaje kuniacha peke yangu hapa?"

"Melissa, unawezaje kuthubutu kurudi kwa familia ya Masolwa sasa?" Seidrick alisimama wima na kumgeuzia mgongo Melissa, “Huna haya wala soni!”

“Seidrick, huwezi kunifanyia hivi… mimi ni mke wako. Bado nina mimba ya mtoto wako. Yeye pia ni mjukuu mkubwa wa familia ya Masolwa. Katika miaka hii mitano, nimekuwa na wewe. Ninapaswa kupewa sifa kwa kufanya kazi kwa bidii, ikiwa si kwa sifa…” Melissa alimshika, akiogopa kwamba ikiwa angemwachilia, Seidrick angetoweka.

“Mtoto? Una uhakika mtoto aliye tumboni mwako ni wangu?" Seidrick alidhihaki na kuanza kutilia shaka ujauzito huo.

“Bila shaka ni wako. Ni mjukuu wa Masolwa. Naapa!" Melissa aliinua vidole vitatu vya mkono wake wa kulia.

Seidrick alichukua nafasi hiyo kuurudisha mguu wake nyuma, kisha akapiga hatua mbili nyuma ili kujiweka mbali na Melissa, “Melissa, siwezi kukuamini tena. Kweli ulilala na Timothy mara moja tu?”

"Unakumbuka? Wakati huo, tulifanya miadi ya kufanya uchunguzi wa kimwili pamoja, lakini ulitoweka kwa muda mrefu. Nilikukuta hotelini na Timothy pia alikuwepo… Kama hukuwa na mawasiliano naye, kwa nini ulikuwa naye hotelini? Kwa kuangalia nyuma, nadhani ulikuwa na hatia badala ya kukosa raha wakati huo. Ninaogopa kuwa umelala naye zaidi ya mara moja! Kwa hivyo, anaweza kukulazimisha kwa sababu ana bidhaa kwako, sivyo?

“Hapana, hapana…” Melissa akatikisa kichwa na kujaribu kwenda mbele kueleza.

Lakini Seidrick alimkwepa, “Melissa, ni sawa usipokubali. Nitapata ushahidi wa kukushawishi.”

"Hapana, Seidrick. Nimekosea…” Melissa alikuwa na wasiwasi hata akapiga magoti mbele yake, “Nilitishwa naye, sikudanganya...

“Baba, mama, tafadhali nisaidie. Nisaidieni kuzungumza na Seidrick na kumfanya aniamini.” Melissa hatimaye aliweka matumaini yake kwa wazazi wake.

“Ukweli upo mbele yetu. Hata polisi walikuja nyumbani na kuonyesha ushahidi. Unataka tuseme nini?” Uso wa Alex ulikuwa na huzuni, “Umeaibisha familia yetu, wewe mwenye dhambi!”

“Hapana, Baba. Yote ni kwa sababu ya Alissa. Yote ni kwa sababu yake kwamba nilitishwa na Timothy!”

Kofi kali likasikika.



Sura ya 219

Melissa alihisi kizunguzungu na hisia inayowaka usoni mwake. Hata meno yake yalikuwa yanauma. Inaweza kuonekana jinsi Alex alivyompiga kofi kali.

"Ni wewe ambae hauna aibu kufanya kitu kama hicho ili kuaibisha familia ya Masolwa na familia yetu. Lakini bado unajaribu kumlaumu dada yako? Alissa ni dada yako mwenyewe. Unawezaje kusema maneno kama haya ili kumkashifu? Unataka kunikasirisha na kuniua?” Alex alimshutumu Melissa na karibu alitaka kumnyonga hadi afe.

“Melissa, unafikiri Alissa ni nani sasa? Si lazima awe kinyume nawe, sivyo? Kwa kuongeza, unapaswa kuchukua jukumu kwa makosa yako mwenyewe. Unawezaje kumlaumu Alissa? Tumekatishwa tamaa na wewe!” Marry pia alikuwa mbele sawa na Alex, akimkosoa Melissa.

"Baba, mama, msikasirike." Alissa alikuwa mtulivu. Hakuchukulia kashfa za Melissa kwa uzito, “Mwenye busara anajua hajui chochote, mpumbavu anadhani anajua yote. Haijalishi jinsi ninavyoielezea, watu ambao hawaniamini hawataamini. Kwa hiyo, mradi nyinyi wawili mnaniamini, nitafurahi sana.”

Alichosema Alissa sio tu kiliwatuliza Bwana na Bi Maziku, bali pia kiliwaweka katika nafasi muhimu, na kuwafurahisha sana.

Mbali na hilo, pia alimuaibisha Seidrick. Alijaribu kuelezea wakati huo. Lakini Seidrick hakumsikiliza hata kidogo na kwa ukaidi aliamini kile alichokiona kwa macho yake.

Seidrick kawaida alielewa nini Alissa alimaanisha. Uso wake ulibadilika kidogo na kumtazama Alissa aliyekaa kwenye sofa, huku akiminya midomo yake myembamba kwa nguvu.

"Angalia, jinsi Alissa alivyo mkarimu na mrembo! Wewe sio tu umetutia aibu, lakini pia ni mbaya kumwandama dada yako. Wewe ni msichana mbaya sana!” Alex alikoroma. Alikasirika sana hivi kwamba alihisi shinikizo kubwa kwenye kifua chake.

Alissa alitazama chini, akatabasamu na kusikiliza karipio lao.

“Baba, Melissa ameniandama mara nyingi. Ingawa sijui anafanya kwa ajili gani, sitafanya fujo kuhusu hilo. Baada ya yote, mimi ni dada yake mkubwa na lazima nimchukulie kama mdogo wangu.” Alissa aliiga jinsi Melissa alivyozungumza miaka mitano iliyopita, jambo ambalo lingeweza kuwakasirisha zaidi wazazi wake.

Alissa alitaka Melissa apatwe na maumivu aliyoyapata.

"Ikilinganishwa na Alissa, wewe ni mbaya zaidi kuliko nguruwe na mbwa!" Alex alisema maneno yasiyo na moyo, pigo baya kwa kujistahi kwa Melissa.

“Baba mimi ni mtoto wako na wa Mama. Ikiwa mimi ni mbaya kuliko nguruwe au mbwa, basi vipi kuhusu nyinyi na dada yangu mpendwa?” Melissa alitabasamu zaidi. Aliwatazama wazazi wake waliokata tamaa ya kuwa na binti asiyefaa, akahuzunika sana.

“Wewe!” Melissa alinyamazishwa na maneno ya kuumwa ya Alex.

“Haya binti, unathubutuje kutusema hivi? Tunakulea na dada yako pia anakupenda. Je! una dhamiri?" Marry alichukua maneno na kumpiga Melissa mara mbili zaidi.

“Baba, Mama, Melissa hakukusudia. Ana wazimu tu na anaongea upuuzi. Msimlaumu. Isitoshe, ni mjamzito.” Alissa akainua jagi na kujimiminia glasi ya maji huku akiishika bilauri.

Seidrick ambaye alikuwa ametulia alibadilika rangi aliposikia alichosema Alissa. Akatoa macho yake na kumtazama Alissa ambaye aliendelea kutabasamu kidogo kana kwamba ni mtazamaji tu.

Alihisi kuwa tukio hili lilifanana sana na wakati Alissa alipomsaliti miaka mitano iliyopita.

Tofauti ni kwamba Alissa alikuwa amejifungua mtoto, wakati Melissa alikuwa bado mjamzito.

Yeye, Seidrick, "alipendwa" sana na Mungu hivi kwamba mchumba wake wa zamani na mke wake walikuwa wamemsaliti na hakuna watoto wao aliyekuwa wake.
Miaka mitano iliyopita, Melissa alikuwa mwenye kujali. Lakini sasa, alikuwa na chuki sana.

Miaka mitano iliyopita, Alissa alikuwa na chuki. Lakini sasa, alikuwa mwenye kujali sana.

Historia ilikuwa inafanana kila wakati. Seidrick akaweka tabasamu la kujidharau. Ilionekana kuwa kweli hakustahili kupata furaha.
Aligeuka na uso wa huzuni na kwenda nje ya sebule ya familia ya Maziku.

__
Melissa alimtazama Seidrick aliyekuwa anaondoka na kujaribu kumfata. Lakini alijikwaa na kuanguka chini. Magoti yalimuuma sana hata akashindwa kusimama. Kwa hiyo, alilala tu chini na kupiga kelele kwa uchungu mgongoni mwa Seidrick, “Seidrick, usiende! Usiniache mimi na mtoto wetu! Seidrick…”

Seidrick alipuuza maneno yake na kuondoka bila kuangalia nyuma, na kutoweka.

Melissa alinyoosha mkono tu, akijaribu kupata sura ya Seidrick. Lakini alishindwa na hakupata chochote.
Melissa alikunja mikono yake na kulia chini ...

Kwa wakati huu, yeye pia alionja hisia ya kukata tamaa.

Alissa alimtazama Melissa aliyekuwa akilia kwa uchungu na kutabasamu kwa ubaridi.

"Aibu kwako! Ni aibu iliyoje!” Alex alikasirika, "familia ya Masolwa haitamuacha!"

“Tunaweza kufanya nini?” Marry alikuwa na wasiwasi, “Je, watakuja nyumbani kwetu kuleta matatizo?”

“Mama, vyakula viko tayari? Nina njaa sana.” Alissa alimuuliza Marry.

“Oh, nitaenda kutazama sasa hivi.” Marry akatoka kwa wasiwasi.

“Baba mbona huendi na mama? Nina jambo la kuzungumza na dada yangu.” Alissa akawaondoa kwa kisingizio.

“Sawa. Nitawaacha peke yenu.” Bwana na Bi Maziku kisha wakaenda jikoni pamoja, bila kumjali Melissa hata kidogo.

Baada ya kuondoka kwa muda, huzuni ya Melissa ilikuwa karibu kutolewa na kilio chake kilinyamaza polepole.

Hapo ndipo Alissa akasema, “Melissa, gurudumu la bahati litazunguka tena. Unajisikiaje sasa?”

"Alissa, ni wewe unayecheza hila, sivyo? Umenifanya nifikie mwisho mbele ya Seidrick na Mama na Baba hawakunitilia maanani tena! Yote ni kwa sababu yako!” Melissa alijiinua huku macho yake yakiwa yamejaa chuki kwa Alissa.

"Melissa, unastahili! Ulipaswa kujua haya miaka mitano iliyopita kabla hujanizunguka!” Alissa alisimama taratibu na kumtazama Melissa chini, kana kwamba anatazama fuko mnyenyekevu chini ya miguu yake, “Ikiwa hukuwahi kukusudia kuwadhuru wengine, haungekuwa hivi sasa!Umeniumiza tena na tena kwa ajili yako. Nisipopigana, utafikiri mimi ni punchbag, sawa?”

Alissa alitabasamu kwa upole na alikuwa mwenye neema, “Ulinitia dawa ili kunifanya nipoteze usafi wangu kwa Timothy, lakini ulipoteza wewe. Ulitaka kunifanya niachwe na Kendrick, lakini ni wewe utakayeondoka kwa familia ya Masolwa. Ulijaribu kuonyesha kutokuwa na hatia mbele ya Seidrick, lakini huna uhakika hata baba wa mtoto wako ni nani, sivyo? Ulitaka kuwa na Seidrick, na sasa, umempoteza…

"Ulidhani jambo moja sawa. Mimi ndiye niliyemwomba mtu akupeleleze wewe na Timothy. Nilitaka wewe pia uonje hisia ya kupoteza sifa yako na kuachwa na yule umpendaye. Je, unajisikia huzuni au furaha sana? Kisha hongera kwa kuteseka kwa uchungu niliokuwa nao wakati huo.”

Sura ya 220

Macho ya Alissa yalikuwa safi na ya ukali, hayakuwa tena rahisi na yasiyo na hatia kama hapo awali.
Katika miaka hii mitano, alikuwa amejawa na magumu na kukua.
Hangenaswa tena na Melissa na kupoteza kila kitu. Badala yake, angeruhusu Melissa azame kwenye kaburi alilojichimbia mwenyewe.

Sasa, baada ya kuona kwamba Melissa alipatwa na maumivu na kuachwa na Seidrick, ambaye aliondoka bila kuangalia nyuma, na kujaribu kupigana lakini hakuweza kufanya chochote, Alissa alifurahi sana.

Alijua alikuwa amebadilika. Lakini badiliko kama hilo lilikuwa tu kumfanya awe bora.

“Alissa, nitakuua! Nitakuua!" Melissa alikasirika zaidi na alionekana kuwa mkali aliposikia Alissa akikiri kwamba yeye ndiye aliyetoa taarifa hiyo, “Nitakuua!”

Melissa alivumilia maumivu ya magoti yake, akakenua meno yake na kuinuka. Alikuwa kama ng'ombe aliyekimbia na kumrukia Alissa.
Alissa kwa silika alijaribu kukwepa, lakini alishindwa. Aliangushwa chini na Melissa.

Melissa akanyoosha mikono yake, akafungua vidole vyake kumi, na kuibana shingo ya Alissa kwa ukali.

Alissa alikabwa koo naye akashindwa kupumua. Uso wake uligeuka mwekundu.

Alinyoosha mkono ili kujifungua. Lakini hakujua kwa nini Melissa, ambaye kwa kawaida alikuwa mpole na dhaifu, alikuwa na nguvu sana sasa.
Hakuweza kujinasua hata kidogo.

“Alissa, umenifanyia hivi. Siwezi kuishi, na wewe pia huwezi kuishi! Tutakufa pamoja!” Melissa alionekana kupoteza akili na macho yake yalikuwa mekundu.

Alissa alikuwa bado anahangaika, akijaribu kuachana na Melissa. Silika ya kutamani kuishi ilimfanya asikate tamaa hadi mwisho.
Zaidi ya hayo, alikuwa ameokoka siku hizo ambapo maisha yalikuwa mabaya zaidi kuliko kifo. Sasa, hakuwa na mtoto mzuri tu, bali pia mume aliyempenda, kazi iliyositawi, na familia yenye furaha. Haya yote yalikuwa motisha kwake kuishi.

Alissa akakitazama kikombe kilichokuwa kwenye meza ya chai. Melissa, ambaye alikuwa karibu na wazimu, hakuliona kabisa, aliendelea kukaza vidole vyake.

Alissa alinyoosha mkono kwenye kikombe. Alishusha pumzi na kukipiga chini kwenye kichwa cha Melissa kwa nguvu zake zote. Kikombe kilivunjika vipande vipande.

Kichwa cha Melissa kiligongwa sana. Kilimuuma sana hata nguvu mikononi mwake ikaisha. Alissa alichukua nafasi hiyo kumsukuma.

Melissa alisukumwa hadi sakafuni. Alissa, ambaye aliachana na Melissa, alishusha pumzi ndefu na kujiegemeza kwenye meza ya chai.

"Alissa, mbwa!" Melissa alikipapasa kichwa chake ambacho kilikuwa kimevunjika na kuhisi damu.

Alizidi kumchukia Alissa. Alichukua vipande vya kikombe sakafuni, akijaribu kumrudia Alissa kwa mara nyingine tena.

Alissa alimtazama usoni na kusema, “Melissa, una damu usoni!

Melissa alinyoosha mkono kumgusa uso wake. Hakika kulikuwa na damu kwenye vidole vyake.

Hakuwa mzuri kama Alissa. Lakini alikuwa mtamu na mrembo. Sasa, uso wake uliharibiwa, na akapoteza faida yake pekee.

Melissa alihisi kukata tamaa. Alishika vipande vya kikombe katika mkono wake wa kulia huku akimuelekezea Alissa moja kwa moja, “Kwa kuwa unaniharibu uso wangu, basi nitaharibu uso wako pia! Baada ya kuwa mbaya, ngoja nione kama Kendrick bado atakutaka!”

Melissa alimkimbilia tena Alissa. Alissa alikwepa. Lakini hatimaye, Alissa alikamatwa.

Melissa alivikandamiza vile vipande mkononi mwake kuelekea usoni mwa Alissa, huku Alissa akimshika Melissa kifundo cha mkono na kupinga kwa nguvu. Hawakuweza kusonga kila mmoja ...

Kwa wakati huu, Alex na Marry walitoka jikoni na kuona tukio kama hilo la kusisimua.

“Melissa, wewe mwenye dhambi! Acha!" Alex alishtuka.

"Melissa, acha!" Marry alimshauri hivi kwa wasiwasi, “Si vyema kufanya hivyo!” Iwapo Kendrick angelijua hili, au ukimuumiza Alissa, tutamwambiaje Kendrick?

“Hata hivyo, sina kitu, siogopi chochote! Kendrick anaweza kufanya nini? Hata kama atajua kuhusu hilo?" Melissa hakujali matokeo, na alifanya vile alivyopenda wakati huo.

Lakini, Kendrick alitokea kwenye sebule ya familia ya Maziku. Kuona hali hii ya kushangaza, alikunja uso, akasonga mbele, na kumshika mkono Melissa, akamtupa nje.

Melissa alikuwa na maumivu kwenye goti lake. Alitupwa kwa nguvu hadi akajikwaa na kuanguka chini.

Kendrick alimshika Alissa bega, macho yake yakiwa yamejaa wasiwasi, “Uko sawa?”

“Sijambo.” Alissa akatikisa kichwa.

Lakini Kendrick aliona pete ya alama nyekundu kwenye shingo yake-nyeupe-theluji, "Hii ni nini?"

Alissa alimtazama Melissa, “Mimi si dhaifu kiasi hicho.”

Kendrick alijua kuwa ilisababishwa na Melissa. Macho yake yalikuwa baridi na kujawa na hasira, "Melissa, hebu niambie, ungetaka kujua matokeo yake?"

Melissa, hata hivyo, alicheka kwa sauti kubwa kwa kutojali. Alikuwa akicheka sana na alionekana kutokuwa na hofu hata kidogo.

Alitazama macho ya wino ya Kendrick ya kuua na kusema kwa utulivu, "Ni kwamba sitakuwa na chochote. Ninaweza kupoteza nini sasa? Unaweza kunifanya chochote, au kunaniua! Lakini, ni mbaya zaidi kuliko kufa ikiwa ninaishi hivi. Kwa hiyo, unaweza kuniua au kuniacha niende!”

“Nikuue? Huo utakuwa upendeleo mkubwa sana kwako. Nitafanya maisha yako kuwa mabaya zaidi kuliko kifo! Lakini katika jumuiya ya kisheria, nitakuadhibu kwa sheria.
Melissa, subiri tu.”

Melissa bado alikuwa akicheka, bila kuchukulia maneno ya Kendrick kwa uzito hata kidogo, "Ndio, nitasubiri."

Alex na Marry wote walihisi woga walipomwona Melissa akiongea bila heshima na Kendrick na kumkasirisha.
Melissa alikuwa akitamani kifo! Ilikuwa sawa ikiwa alitaka kufa. Lakini yeye hapaswi kuwahusisha.

Alex na Marry waliutazama uso wa baridi wa Kendrick, na kutokwa na jasho migongoni mwao.

“Twende zetu.” Alissa alikuwa ametimiza lengo lake na hakutaka kubaki hapo tena.

“Sawa.” Kendrick alimtii, macho yake yakiwa yamejaa mahaba.

Jeraha kwenye shingo yake pia lilihitaji kutibiwa, lakini, kushughulika na Melissa hakukuwa na haraka.

“Alissa, chakula kiko tayari.…” Marry alisema huku akimtazama Kendrick akimsaidia Alissa kuondoka.

“Mwachie binti yako mdogo unayempenda zaidi.” Alissa alisema bila kujali.

Melissa bado alicheka na kusema, “Kendrick, una nguvu na wengine wote wanakuheshimu. Lakini machoni pangu, wewe ni mjinga! Unamlinda Alissa sana na kumchukulia kama hazina. Lakini Alissa si mtu mzuri!”
 
USINIACHE 5:
Sura ya 221

Maneno ya Melissa yalimfanya Kendrick aliyekuwa anatoka asimame. Alissa alimtazama Kendrick pembeni yake huku Kendrick akielekeza macho yake kwa Melissa.

“Najua mke wangu ni mtu wa aina gani. Sihitaji unikumbushe! Unafikiri nitaamini unachosema?” Kendrick kwa kawaida hangeamini maneno ya Melissa kwa urahisi hivyo, “Unajaribu tu kuweka kabari kati yetu. Ninawezaje kukupatia unachotaka?”

Melissa alicheka, kana kwamba alikuwa ametoka tu kusikia mzaha, "Kendrick, najua kwamba sina uwezo wa kuendesha kabari kati yenu. Lakini bado nina kitu cha kusema. Unaweza tu kuchukua kile utakachosikia baadaye kama hadithi.

Alissa aliganda na kukamata nguo za Kendrick, “Kendrick, twende nyumbani. Usimsikilize upuuzi wake.”

"Kendrick, mke wako mzuri anaogopa na ana hatia." Melissa alimtazama Alissa ambaye alitaka kuondoka.

“Huna la kusema? Nitakupa nafasi ya kusema leo. Usifikiri nitakuacha uende kwa sababu tu umesema hivyo. Unachohitaji kuwa wazi ni kwamba hakuna chochote utakachosema kitakachosaidia." Kendrick aliuzungusha mkono wake begani kwa Alissa huku akimpa nguvu na kumwambia asiogope na atakuwa naye.

Alissa alijaribu kujituliza, hakuguswa na maneno ya Melissa.

“Sikutarajia ungeniacha niende kirahisi hata kidogo. Nataka tu kujua mtazamo wako. Nitakuambia vizuri kuhusu huyo Alissa mwingine usiyemjua. Baada ya kuisikiliza, sidhani kama utakuwa katika hali ya kunishughulikia kwanza.”

Melissa aliridhika na mtazamo wa Kendrick.
Lakini macho yake yalikuwa na kinyongo na matata alipomtazama Alissa, “Alissa hajawahi kuolewa na mtu yeyote. Kwa hiyo, Doris alitoka wapi? Hutaki kujua?”

Alex litetemeka kwa woga aliposikia hivyo, na Marry naye alikuwa akitokwa na jasho.

Alissa alionekana kuwa mtulivu juujuu. Lakini uso wake uligeuka rangi kidogo.

Kupumua kwake pia bila kujua kukawa kuzito, na vidole vyake vilipishana pamoja.

“Melissa, inatosha! Alissa na Kendrick wanapendana sana. Huithamini ndoa yako na unaongea upuuzi tu hapa?” Alex alitaka Melissa kuacha. Hakupaswa kamwe kumjulisha Kendrick kuhusu kuzaliwa kwa Doris.

“Melissa, tafadhali. Wewe ni mwanamke wa familia ya Maziku. Acha kufanya hivi, sawa?" Marry pia alikuwa na wasiwasi.

Sasa, Melissa hangeweza kurudi kwenye familia ya Masolwa. Bila shaka kungekuwa na mpasuko au hata chuki kati yao na familia ya Masolwa.

Baada ya yote, binti wawili wa familia ya Maziku walikuwa wamemkosea Seidrick. Bila shaka wangeanzisha ugomvi.

Melissa alikuwa ameanguka katika fedheha. Wazazi wao hawangeweza kumruhusu Alissa, ambaye aliolewa na familia ya Mayala, ateseke vile vile. Ilibidi wamlinde Alissa. Vinginevyo, familia ya Maziku ingekabiliwa na maafa ya karibu.

"Baba, Mama, mnajali tu masilahi ya familia ya Maziku na utukufu wenu. Hivi kweli mnanipenda mimi na Alissa? Sisi ni vibaraka tu kwenu kupata faida kwa familia ya Maziku. Hamjawahi kuwa waaminifu kwangu! Kwa nini niwasikilize?

“Mlinipenda hapo mwanzo kwa kuwa nilikuwa mke wa Seidrick, na sasa mnamlinda Alissa sasa kwa sababu aliolewa na familia ya Mayala na kuolewa na Kendrick. Ikiwa yeye pia angeachwa na Kendrick, hamtampenda mtu yeyote. Sivyo?

“Nataka tu kufanya jambo zuri sasa. Alissa hastahili kuolewa na mwanaume mzuri kama Kendrick!” Melissa alisema, kana kwamba alikuwa akimtetea Kendrick dhidi ya ukosefu wa haki wa Alissa.

“Kendrick… Melissa amerukwa na akili na anaongea upuuzi. Kwa hiyo, usijisumbue naye.” Alex alijaribu kumsihi Kendrick aondoke, “Ondoka na Alissa sasa. Tutamfundisha Melissa vizuri.”

"Ndio ndio ndio. Nyie tangulieni mbele.” Marry aliunga mkono, akijaribu kuwaruhusu waondoke.

“Sijapoteza akili na kuzungumza upuuzi. Niko macho zaidi sasa kuliko hapo awali na ninajua nitafanya nini na kuongea nini.” Melissa aliwakodolea macho wazazi wake, “Badala yake, mnajaribu kunizuia nisiseme ukweli kuhusu Doris. Mnataka kuficha kashfa ya Alissa miaka mitano iliyopita? Mnataka Kendrick awe mpumbavu asiyejua chochote?”

"Bwana Kendrick, tafadhali nisikilize nikueleze hadithi nzima. Nadhani hutaki kutendewa kama mjinga na Alissa, sivyo?”
Kendrick alitazama kwa ubaridi kwa Bwana na Bi Maziku. Waliweza tu kubana midomo yao na hawakuthubutu kusema chochote.

Alipoona kwamba Melissa alikuwa karibu kusema kilichotokea miaka mitano iliyopita, Alissa alikaribia kuvunjika. Mbaya zaidi alilotarajia lilikuja mwishowe.

Hakutaka Kendrick ajue kuwa aliwahi kulala naye mara moja na kumzaa Doris kwa ajili ya maisha ya Seidrick. Kendrick alijivunia sana. Je, angewezaje kuwa tayari kutumiwa kama kibaraka ili kumuokoa mwanamume mwingine?

Isitoshe, Doris alikuwa binti yake halisi. Alikuwa amemficha. Kendrick alikuwa amempa imani yake kamili. Lakini alimdanganya.

Hakuweza kumfahamisha Kendrick haya yote. Hakutaka kumpoteza yeye na familia hii.

"Kendrick, huwezi kuamini maneno yake na kumsikiliza." Alissa alishika mkono wake kwa mikono miwili, “Twende nyumbani. Doris bado anatusubiri nyumbani.”

Kendrick alihisi ubaridi kutoka kwenye vidole vyake. Hata uso wake ulikuwa mweupe. Alimkazia macho, kana kwamba anajaribu kusema kile anachohisi sasa.

“Unaogopa nini?” Kendrick alihisi kuwa Alissa sasa alikuwa si wa kawaida na mwenye wasiwasi.

"Nitakuambia unachotaka kujua, sio yeye." Alissa angeweza tu kukubaliana. Angeweza kumwambia Kendrick kuhusu jambo hili mwenyewe, ili aweze kusema ukweli nusu na nusu ya uwongo ili kuepuka kuvuja taarifa muhimu.

"Bwana Kendrick, huwezi kumwamini. Atachosema Alissa hakiwezi kuwa ukweli kabisa.” Melissa alikuwa amesimama mita mbili tu kutoka kwao, na alijisikia raha kutazama hali ya Alissa iliyojawa na hofu.

“Najua baba wa mtoto ni nani. Huna haja ya kusema zaidi.” Kendrick alidhani kuwa Doris ni binti wa Seidrick.

"Labda huwezi kujua." Melissa alikuwa na hakika.

"Sitaki kujua pia." Kendrick alimtazama Alissa ambaye macho yake yalikuwa mekundu na alikusudia kumpa nafasi.

Kwa hayo, Kendrick alimuongoza Alissa kutoka kwenye sebule ya akina Maziku. Alissa alikuwa ametulia kidogo. Sasa hivi, alikuwa na wasiwasi sana na machozi yake yalikuwa karibu kumwagika. Kwa bahati nzuri, Kendrick alichagua kumheshimu na kumpa nafasi ya kusema mwenyewe.

Kabla hawajaenda kwenye lango, Melissa alimkimbilia na kusema, "Bw. Kendrick, miaka mitano iliyopita, Alissa na Seidrick walikuwa wachumba. Lakini Alissa alijifungua mtoto wa nje y nyuma ya mgongo wa Seidrick. Kwa nini?”

"Kwa sababu Seidrick alikuwa mgonjwa sana na hakuweza kupata mechi ya uboho. Asingeweza kuishi. Alissa alitafuta mtu ambaye angeweza kuendana na uboho wa Seidrick na akalala naye. Kisha, alikuwa mjamzito. Mtoto alikuwa Doris. Kwa bahati nzuri, Doris angeweza kuendana na uboho wa Seidrick na kumuokoa.”

Sura ya 222

Kendrick alisimama baada ya kusikia maneno haya, akiwa ameshikwa na udadisi.

Alissa aliyekuwa amemshikilia hakuwa na jinsi zaidi ya kusimama. Hata angefanya nini, asingeweza kumzuia Melissa asieleze kilichotokea wakati huo.

Watu hawakuweza kufunika moto kwenye karatasi hata hivyo. Moto ungeunguza kila kitu.

Alissa alifumba macho kwa kukata tamaa na aliweza tu kumsikiliza Melissa kwa utulivu huku Melissa akiendelea.
Lakini kwa bahati nzuri, Melissa hakujua kuwa mtu huyo alikuwa Kendrick. Alissa bado angeweza kutunza siri hii.

“Huyo mtu ni kibaraka. Doris pia ni chombo cha kumuokoa Seidrick na alizaliwa kwa bahati mbaya. Kuhusu baba Doris, Alissa hakuwahi kuniambia. Kwa hiyo, sijui. Lakini kwa uwezo wa Bw. Kendrick, ni rahisi kujua mtu huyo ni nani.

"Bwana Kendrick, Alissa sio rahisi na mrembo kama unavyoona. Yeye pia ni mbinafsi. Ili kuokoa mtu wake mpendwa, alijitolea na kumdanganya mwanamume mwingine. Alimzaa Doris, lakini hakuweza kumpa baba na familia.

"Bwana. Kendrick, alikuambia mambo haya yote? Je, anakupenda kweli? Ninaweza kukuambia kwa hakika kwamba mtu anayempenda ni Seidrick. Nilimuiba Seidrick kutoka kwake wakati huo. Kwa hiyo, aliporudi kuniona mimi na Seidrick tukiwa katika upendo, alifanya haya yote ili kulipiza kisasi. Je, hana ubinafsi?

“Kama alikuwa hampendi Seidrick, kwa nini angekuwa mgumu sana kwangu? Alikubali umuoe ili tu kutumia utambulisho wako kulipiza kisasi. Lakini ni kosa langu tu kwamba Seidrick alimwacha?

"Ilikuwa kwa sababu Seidrick hakumwamini. Seidrick ndiye aliyemuumiza zaidi. Kwa nini hakulipiza kisasi kwa Seidrick? Bwana Kendrick una akili sana. Nadhani sihitaji kusema zaidi na unapaswa kujua pia. Bwana Kendrick, nasema hivi ili kukujulisha kuwa Alissa sio mzuri kama unavyofikiria. Sitaki akudanganye na kukutumia kwa kutegemea uso wake usio na madhara!

"Bwana Kendrick, usinishukuru. Nataka tu kufanya jambo jema…”

"Nyamaza!" Kendrick akasogea na kumshika Melissa shingoni kwa mkono wake wa kulia.

Melissa alikaribia kunyongwa papo hapo na kuonja hisia alizopata Alissa hivi sasa.

“Maneno haya yanaweza tu kuwekwa akilini mwako kuanzia sasa na kuendelea. Ukithubutu kufichua neno, usinilaumu kwa kuukata ulimi wako!” Kendrick alimtishia vikali, "Unaelewa?"

Kendrick alikuwa baridi na kama Shetani. Melissa aliganda.
Melissa hakuthubutu kusema tena na aliweza tu kutii kwa kichwa.

Kendrick alipoona anaitikia kwa kichwa kisha akamuachia huku macho yake yakiwa yamejawa na karaha.

Melissa akamgusa shingo, akainama na kukohoa mara kadhaa. Alijisikia vibaya sana. Sasa hivi, alifikiri kweli kwamba angekufa.

Ingawa alihisi kuwa hana chochote na haogopi kifo, alifadhaika wakati alipata aliponyongwa na Kendrick wakati huu.
Alijitahidi sana kuishi.

Kendrick aligeuka na kumvuta Alissa ili aingie kwenye gari, akalitoa gari nje ya nyumba ya familia ya akina Maziku.

Baada tu ya kusikia gari likiondoka ndipo Alex na Marry walitoka nje ya jumba lile, wakamwona Melissa akiwa amesimama peke yake gizani.

"Ulizungumza na Kendrick kuhusu kile kilichotokea miaka mitano iliyopita?" Alex aliuliza kwa wasiwasi.

Walikaa ndani ya nyumba hiyo na hawakuthubutu kutoka. Kwa hiyo, hawakusikia ukweli.

“Ndiyo. Kwa kuwa Alissa ananifanya niwe na wakati mgumu, nampa tit kwa tat. Hata kama Kendrick hatamuacha sasa, kutakuwa na mpasuko katika akili yake, ambao utamchoma kila dakika. Siku moja, hataweza kuvumilia! Wakati huo, Alissa atapoteza kila kitu kama mimi leo.” Hili ndilo lilikuwa kusudi la Melissa.

“Melissa, una wazimu? Unaongea ujinga gani?" Marry alimkaripia Melissa, “Nilikuambia usimchokoze. Lakini ulifanya upendavyo. Sasa, umejiingiza ndani yake. Ni nini kizuri kwako kupoteza Seidrick?"

“Mama, siwezi kuishi bila Seidrick. Kwa kuwa siwezi kuishi, basi Alissa pia hawezi kuishi.” Melissa alikuwa akiwajeruhi wengine na kujiharibu sasa.

“Huoni Alissa atafikia mwisho mzuri, kwa hiyo utaweza? Wewe ndiye utashughulikiwa na Kendrick atakapotulia!” Marry bado alimpenda binti yake mdogo, “Nina wazo. Nenda kuwaomba msamaha kwa dhati. Hata wakikuuliza upige magoti, unapaswa pia kufanya! Baada ya yote, sisi bado ni familia. Maadamu una mtazamo mzuri, inaweza kutatuliwa. Je, ni lazima ujiweke katika hali kama hiyo?”

“Kuomba msamaha?” Melissa alidhihaki, “Msamaha ungefanya kazi, kungekuwa na watu wengi wanaomuogopa Kendrick!”

"Hata kama hujifikirii wewe, unapaswa kufikiria juu ya mtoto aliye tumboni mwako. Je, hutaki kuungana na Seidrick? Maadamu una mtoto wake, atafanya jambo kwa kumjali mtoto.” Marry alipumua na kumshawishi Melissa.

"Mama, mimi na Seidrick tunaweza kutengeneza?" Macho yenye huzuni ya Melissa yaliwaka.

"Ikiwa utamtunza mtoto, kutakuwa na matumaini. Seidrick ndiye mwana pekee wa kiume wa familia ya Masolwa. Kwa afya yake, ni bahati sana kwake kupata mtoto huyu. Familia ya Masolwa haimtaki mtoto huyu?” Marry aliendelea kumtuliza Melissa. Alitaka pia kupatana na familia ya Masolwa. Ilikuwa bora kuwa marafiki kuliko maadui. Mbali na hilo, familia ya Masolwa ilikuwa na nguvu.

Kulikuwa na miradi waliyokuwa wanafanya, pamoja, kama Hoteli ya Beach. Kwa hakika hawakuweza kwenda vibaya kwa wakati huu.

“Umefanya vile. Mwanaume hakika atahisi aibu na kukasirika. Seidrick ana hasira, ambayo ina maana kwamba yeye hujali kuhusu wewe. Yuko kwenye hasira. Akipoa atakusamehe. Tutafuatana nawe kwa familia ya Masolwa ili kuomba msamaha na kukubali makosa. Mtoto huyu ndiye ufunguo wa wewe na Seidrick kuwa pamoja, na pia ndiye mpango wetu wa kufanya mazungumzo na familia ya Masolwa. Unachotakiwa kufanya sasa ni kujiweka katika hali nzuri ya akili na kumtunza mtoto.” Hatua kwa hatua, Marry aliweka matumaini kwa Melissa.

"Mama, nitafanya chochote utakachosema." Melissa alichangamka alipofikiria kwamba alitarajia kuwa na Seidrick.

Alex aliingilia kati, "Melissa, niambie kwa uaminifu ikiwa mtoto huyu ni wa Seidrick au Timothy!"

“Wa Seidrick.” Melissa alikuwa na hakika.

"Huwezi kutudanganya." Alex alikunja uso, “Ikiwa tu ni wa Seidrick, ndipo kunaweza kuwa na nafasi kidogo ya mabadiliko. Vinginevyo, sio tu kwamba hakutakuwa na nafasi, utafukuzwa kutoka kwa familia ya Masolwa na Seidrick hatakupa nafasi nyingine.

“Najua. Ni mtoto wangu na wa Seidrick. Ni wetu.” Melissa alinyoosha mkono kugusa tumbo lake, macho yake yakibubujikwa na machozi. Alitazama chini na kumwambia mtoto, “Mtoto, twende kwa Baba pamoja na kumfanya amsamehe mama. Tunaweza kufanya hivyo. Njoo.”

"Afadhali ufikirie hivyo." Marry alisema, “Ingia ndani ujisafishe. Pumzika kidogo twende kwa familia ya Masolwa kuomba msamaha kesho.”

Sura ya 223

Kendrick alikuwa kimya baada ya kuendesha gari nje ya nyumba ya familia ya Maziku. Hakusema neno, na hata uso wake ulikuwa wa baridi na huzuni.

Alissa aliyeketi karibu naye alihisi msongo wa mawazo na kushindwa kupumua.

Alissa aliitazama sura ya baridi ya Kendrick, akafungua mdomo wake kwa upole na kujaribu kusema kitu. Lakini maneno yaliishia midomoni mwake kwani hakujua la kusema.

Alichosema Melissa kilikuwa kweli. Alissa alimdanganya Kendrick. Kwa hivyo, yeye ndiye alikuwa na hatia na hakuweza kukataa.

Alissa akatazama pembeni na kuinamisha kichwa chini.
Alipitisha mikono yake kwa hisia mchanganyiko.

Ufinyu wa nafasi ndani ya gari ulifanya ukimya kati yao uzidi kuwa mkali.

Kendrick alirudi Lake City. Baada ya kuegesha gari, hakushuka mara moja. Kuona hashuki, Alissa naye hakushtuka alionekana kumsubiri aongee.

Kendrick alikaa kwa dakika chache kisha akasema, "Shuka kwenye gari na uende nyumbani."

“Huna lolote la kuniambia?” Alissa akajipa ujasiri wa kuongea kwanza.

"Tunaweza kuzungumza juu yake baada ya kwenda nyumbani." Kendrick akafungua mkanda wake na kushuka kwenye gari.

Alissa alimfuata. Alipomuona Kendrick akielekea nyumbani, alimfuata kwa kasi.

Lakini alikuwa na wasiwasi na haraka sana kwamba hakujali miguu yake na akakunja kifundo cha mguu wake, “Ah…”

Kwa Silika alipiga kelele nje. Kendrick aliyekuwa akitembea mbele yake aliisikia sauti yake, akageuka kumwangalia na mara akageuka nyuma kumsaidia.

“Mbona unakuwa mzembe sana? Unafikiria nini?" Kendrick alimkaripia kwa uzembe wake.

"Mimi ... niko sawa." Alissa alijaribu kusimama na kuhisi hakuna kitu kibaya.

Kendrick alipoona yuko sawa akakaribia kulegeza kamba na kumuacha aende zake. Alissa alimshika mkono kwa haraka huku akiuliza hivi, “nimekukera?”

"Hapana." Kendrick alisema kwa upole.

"Lakini ninahisi wazi kuwa una hasira." Alissa aliweza kuhisi, “Hukuzungumza nami njia nzima, na hukutabasamu tulipofika nyumbani. Ikiwa una kitu cha kuniambia, sema tu na ninakusikiliza."

Kendrick, hata hivyo, alimtazama kwa muda tu, "Hebu tuingie ndani kwanza, sawa?"

Kendrick alitoa mkono wake na kuingia ndani.

Alissa aliutazama mkono wake mtupu, akahisi baridi ya ziada bila Kendrick karibu.

Yeye pia aliingia ndani ya nyumba. Kendrick alikuwa amebadilisha viatu na kwenda juu. Akaenda chumbani kwa Doris kwanza.

Akausukuma mlango, akawasha taa ya ukutani na kuelekea kwenye kitanda cha Doris. Akiwa anautazama uso wake uliokuwa umelala kwa amani kwa muda, Kendrick akamweka ndani, akambusu kwenye paji la uso, kisha akaondoka.

Alissa aliona alichokifanya. Lakini, Kendrick hakujua kuwa ni baba wa Doris, lakini bado alimjali sana.

Alissa alihisi joto na kumfuata Kendrick kurudi chumbani kwao.

Kendrick alikaa kimya, akachukua nguo na kwenda bafuni kuoga. Alissa alikaa tu. Alikuwa katika hali mbaya sana na amekasirika sasa.

Ilibainika kuwa aliogopa sana kumpoteza Kendrick. Kendrick alipokasirika, alihisi akili yake imevurugika.

Kendrick alipotoka baada ya kuoga, Alissa alisimama na kumwambia, “Nina jambo la kukuambia.

“Nimechoka leo. Sitaki kusema wala kusikia chochote, nataka kupumzika tu.” Kendrick akakitupa kile kitambaa pembeni.

Alikuwa baridi sana, jambo ambalo lilimkera Alissa.

Lakini mwanamume yeyote ambaye alijua kwamba mke wake alikuwa na historia ya nyuma kama hiyo hangeweza kukubali, sivyo?

“Kendrick, najua ni makosa kwangu kuficha yaliyopita. Lakini hiyo ni wakati uliopita. Hatukujua hata wakati huo. Siwezi kubadilisha yaliyopita. Ikiwa una hasira kwa sababu ya maisha yangu ya zamani, naweza kusema samahani kwa kutokujua mapema.” Alissa akainua midomo yake na kuleta jambo kwanza.

Kendrick alikaa pembeni ya kitanda na kukaa kimya.

“Ni kweli nililala na mtu ili nimzalie mtoto ili kumokoa Seidrick. Haikuwa tu kwa sababu alikuwa mchumba wangu wakati huo, lakini pia kwa sababu alikuwa ameokoa maisha yangu. Kwa hiyo, alipopata ajali, sikuweza kusimama na kumtazama akifa. Sikujua nilipataje ujasiri wa kufanya uamuzi huo na kuzaa mtoto ili kumuokoa. Lakini sasa, sijutii uamuzi huo. Nilisema kwamba nisingeweza kubadili yaliyopita.

"Ninaweza tu kuchukua yaliyopita kama somo kwa ukuaji wangu na kila mara nijikumbushe kutofanya makosa yaleyale tena. Lakini sikutarajia kukutana na wewe na kuwa na wewe sasa. Lakini naapa sijawahi kufikiria kukutumia. Nakumbuka jinsi ulivyo mzuri kwangu. Pia najitahidi niwezavyo kukutendea wema kama mkeo. Hii ni mara yangu ya kwanza kuwa mke wa mtu, lakini sikufanya vizuri hatimaye…
Pole.

“Nimesema yote yanayopaswa kusemwa. Iwapo huna kuridhika yoyote au utafanya uamuzi wowote, ikiwa ni pamoja na mpango wetu… Sina malalamiko… Baada ya yote, ni kosa langu kukuficha sana. ” Alissa alishindwa kujizuia kubaki na maneno ya mwisho.

Kisha akashusha pumzi ndefu ili atulie. Lakini macho yake yalikuwa bado mekundu kidogo.

Kendrick alimtazama Alissa na kuhisi huzuni. Lakini hakutaka kumsamehe haraka hivyo.

“Unafikiri nina hasira kwa sababu nilimsikiliza Melissa, au ninajali kuhusu maisha yako ya zamani?”

Alissa alimtazama kwa upole asielewe anamaanisha nini.

“Unadhani mimi ni mtu wa juujuu tu? Nitaathirika kwa maneno machache tu? Au huniamini sana?”

“Huna hasira hata kidogo? Maisha yangu ya nyuma kwa kweli ni mabaya na ni ngumu kuongea. Kama Melissa alisema, mimi si mkamilifu sana. Mimi pia ni mbinafsi.
Kwa hivyo, nilimdhuru Doris na kumwacha azaliwe na hatima isiyo ya haki.

"Si lazima watu wengine wafanye vizuri zaidi yako wanapokutana na kitu kama hiki. Kwa hiyo, umefanya vizuri.” Kendrick alimtuliza.

“Kweli?” Alissa alifurahi kupata sifa kama hizo kutoka kwa Kendrick.

Kendrick alionyesha mtazamo na msimamo wake, “Hata aseme nini, sitamwamini. Kwa sababu wewe ni mke wangu. Ikiwa hata sina imani na wewe, basi mimi si mwanaume na sistahili hata kidogo kuwa mume wako.”

Alissa alisikiliza kwa makini alichosema, na taratibu akatulia. Maneno ya Kendrick yalimpa moyo wa usalama.
“Asante kwa kuniamini.” Alissa alihisi kuwa amemuelewa vibaya Kendrick.

"Lakini Alissa, unaniamini?" Kendrick alibadili mazungumzo na kuyaelekeza kwenye mada nyingine, na macho yake yakawa baridi, “Usifikiri uko sawa kwa sababu nakuamini. Hakika nina hasira sana. Fanya hivyo utakavyo.”

Sura ya 224

Alissa aliuma midomo yake na kukunja uso kwa mawazo. Kwa kuwa hakuwa na hasira juu ya maisha yake ya zamani, au uchochezi wa Melissa, je, alikasirika kwamba hakumwamini kama yeye?

Alimtazama Kendrick na kumuuliza, “Nina imani nawe. Lakini sijiamini.”

"Unamaanisha nini?" Kendrick alikunja uso.

Alissa alisita kusema. Aliogopa kwamba angemkasirisha tena kwa kusema.

“Si unataka kusema kitu? Kwa nini usiendelee?” Kendrick aliuliza tena.


"Huwezi kukasirika tena nikisema?" Alissa alinong'ona.

“Kwa hiyo, unajua hayo unayosema yataniudhi? Basi kwa nini huwezi kusema jambo ambalo halitaniudhi na kunifurahisha?” Macho ya baridi ya Kendrick yalitua kwenye uso wa Alissa na kukutana na macho yake, “Je, ni vigumu kwako kusema kitu kizuri, Alissa? Au sistahili?”

Au labda Alissa alimpenda Seidrick kila wakati. Kwa hivyo, kama Melissa alivyosema, ingawa Seidrick ndiye aliyemuumiza zaidi Alissa, Alissa hata hakumjibu.

Kendrick hakuweza kuuliza swali kama hilo. Alikuwa na kiburi chake na aliogopa kwamba angepata jibu ambalo lingevunja moyo wake.

Alikunja ngumi kwa hisia tofauti.

Alichojali sana ni iwapo kweli Alissa anampenda.

"Hapana, sitaki tu kukudanganya." Alissa alijaribu kutomdanganya sasa. Baada ya yote, alikuwa amemdanganya kuhusu mambo mengi sana.

“Sasa, unasema hutaki kunidanganya. Kisha umefanya nini hapo awali?" Kendrick alikuwa na huzuni.

Kiukweli alijitahidi sana kujiaminisha kumuamini Alissa ili waidumishe ndoa yao.

Lakini aligundua kuwa hangeweza kufanya hivyo. Baada ya yote, ilihusiana na uhusiano wao. Hakutaka kupuuza. Ikiwa angetaka tu kupuuza, hangekuza ndoa yao kwa uzito.

Hakujali maisha yake ya nyuma. Kama alivyosema, hakuweza kubadilisha siku za nyuma. Lakini alikuwa akimfikiria nani sasa?

“Baada ya tukio hilo Melissa alilosema lilitokea miaka mitano iliyopita, nilifukuzwa na wazazi wangu wapendwa na kusalitiwa na Seidrick. Seidrick alipendekeza kumuoa Melissa bila hata kunisikiliza. Nilifukuzwa kutoka kwa familia ya Maziku na kutoweka hadi Dar. Lilikuwa jeraha langu. Sikuweza kusahau kwa miaka hii yote na nilitaka kulipiza kisasi.”

“Miaka hiyo yote, sikuthubutu kamwe kufungua moyo wangu kumkubali mtu yeyote. Baada ya kuwa na wewe, huwa ninahisi kama ninaota. Je, mtu bora kama wewe atanitendeaje? Unanijali na kunilinda. Kisha, taratibu najikuta nakutegemea zaidi…

"Lakini ninaogopa nitafanya tena kosa lile lile na kupoteza kila kitu ... Kwa hivyo, sithubutu kujaribu kufungua moyo wangu wote na kukupenda kabisa ..."

"Inatoshaaa!" Kendrick hakuwa na ujasiri wa kuendelea kumsikiliza.

Uso wake ulibadilika bila kujua. Alishusha pumzi ndefu kwa siri na kuikandamiza hasira yake, akihofia kwamba angefanya jambo lisilo na akili baada ya kukasirika.

Alissa aliogopa kwa maneno yake.
Alijua kuwa Kendrick alikuwa na hasira kweli, hapana, alikuwa na wazimu.

“Kendrick, nisikilize. Baada ya kusikiliza ninachosema, bila shaka utanielewa.” Alissa alikuwa na wasiwasi na kujaribu kuendelea.

“Sitaki kusikia sasa hivi. Nadhani sote tunahitaji kutulia.” Kendrick akainuka, “Nitalala kwenye chumba cha wageni leo.”

Kwa kuwa alitaka kumdanganya, basi aliendelea kusema uwongo, au labda alitaka kujidanganya na hakutaka kuwa na kiasi ili kukabiliana na ukweli.

Kendrick alitoka chumbani kwao.

“Kendrick!” Alissa alitazama nyuma yake.

Lakini jibu pekee kwake lilikuwa ni sauti tu ya kufungua na kufunga mlango. Aliachwa peke yake katika chumba chao cha kulala.

Alissa alikasirika kidogo, akifunika uso wake kwa mikono yake…
Usiku huo, wote hawakulala kwa amani.

Asubuhi Kendrick alikaa kimya aliporudi kutoka mbio zake za asubuhi na kuelekea chumbani kuoga na kubadilisha nguo. Alissa alihisi kana kwamba alikuwa hewa machoni pake.

Usiku, walionekana kutengwa kutoka kwa kila mmoja.

Hakumsumbua. Kwa hiyo, alienda kumnyanyua Doris na kumshusha chini kwa ajili ya kifungua kinywa.

Kendrick alifika baadaye. Doris alimsalimia kwa furaha, “Shikamoo, Baba.”

"Marahabaa, mtoto." Kendrick alinyoosha mkono na kuzisugua nywele za Doris taratibu.

Kendrick hakuonyesha chuki yoyote kwa Doris, lakini bado alimjali kama hapo awali.

Baada ya kifungua kinywa, Kendrick na Alissa walimpeleka Doris shuleni pamoja. Kisha, Kendrick akampeleka Alissa kwenye kampuni yake.

Wakiwa njiani kuelekea kwenye kampuni, Alissa alitaka kumwambia kitu. Akiwa anataka kuongea, Kendrick akapokea simu fulani.

Alissa hakujua ni nani anayempigia simu, na hakuthubutu kuuliza, "Asante kwa kuwa bado unamjali Doris."

"Doris hana hatia. mimi sio mbaya sana." Kendrick aliweka simu, na kuchungulia kwenye dirisha la gari.

"Hiyo sio ninamaanisha." Hakika Alissa alijua kuwa hakuwa mwanaume wa namna hiyo.

Upendo na chuki katika ulimwengu wa watu wazima haukuwa na uhusiano wowote na watoto. Haijalishi alikuwa mpole kiasi gani kwa Alissa, Kendrick bado alikuwa mzuri kwa Doris.

“Jana usiku…” Alissa alitaka kuendelea na mazungumzo ya jana, lakini akakatishwa na Kendrick, “Kwa nini hukuniambia kwamba baba halisi wa Doris hakuwa Seidrick? Kwa nini ulinificha?”

Kendrick alikuwa amemuuliza Alissa kama baba yake Doris alikuwa Seidrick enzi hizo. Alissa alikuwa amekubali.
Sasa, Melissa alisema baba wa Doris alikuwa mtu mwingine.

“Mimi…” Alissa hakujua jinsi ya kujibu kwa muda.

“Usiongee.” Kendrick aliinua kiwiko chake, akakunja mkono wake na kuunyanyua kwenye midomo yake.

Kulikuwa na maana gani ya kuuliza swali sasa? Ndiyo au hapana, haikuwa kazi yake tena.

Au labda bila kujua alitaka babake Doris awe Seidrick?

Wakanyamaza tena. Alissa alihisi kuchanganyikiwa. Alitaka kuongea na Kendrick, lakini alishindwa kujieleza vizuri.

Alissa alishuka kwenye gari walipofika kwenye ofisi za kampuni yake.

"Furahia chakula chako cha mchana." Alissa alimpungia mkono baada ya kusema hivyo.

"Wewe pia." Kendrick kisha akamuagiza dereva aondoke.

Alihisi amekuwa akijidanganya. Alifikiri angeweza kumfanya Alissa apendezwe naye kwa kuwa mzuri kwake. Lakini alisahau kuwa haikuhusiana moja kwa moja na mapenzi.

Alimpa upendo usio na masharti… kwanini bado hakuweza kuushnda moyo wake?

Ni lini yeye, Kendrick, amekuwa msumbufu sana!

Sura ya 225

Katika familia ya Masolwa.

Saa 7:30 asubuhi, Marry alimpeleka Melissa kwa familia ya Masolwa. Alex hakwenda nao. Alijisikia kudhalilishwa sana. Zaidi ya hayo, hakuweza kukabiliana na Sam na Maira. Baada ya yote, binti zake wawili walikuwa wamuumiza Seidrick na kuiangusha familia ya Masolwa.

Lakini Alissa hakuolewa na Seidrick wakati huo hata hivyo. Wakati huu, Melissa alikuwa amekwenda mbali sana. Kama binti-mkwe wa familia ya Masolwa, alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Timothy na hata alikamatwa na polisi papo hapo na kurekodiwa. Ikiwa haikuwa ni urafiki wao na familia ya Masolwa kwa miaka mingi na hakutaka kuharibu uhusiano wao, Alex hakutaka kabisa kumsaidia Melissa, binti yake.

Marry alimpendelea Melissa tangu utoto. Melissa pia alimsikiliza. Kwa hivyo, alipomwona Melissa hivi, Marry alitaka kumsaidia.

"Mama, unadhani ninaonekana mzuri hivi?" Melissa alinyoosha nguo zake na kuangalia vipodozi na nywele zake tena.

Marry alimtazama na kusema.“Umeniuliza mara nyingi. Hiyo inatosha.”

“Nitaonekana mvivu kwa vipodozi vyepesi hivi. Na uso wangu bado una mkwaruzo ya jana ... Ni mbaya sana. Je, Seidrick hatanipenda?”

Mkwaruzo usoni mwa Melissa ulikuwa mwembamba sana, haukutosha kumharibu. Lakini kama mwanamke, hakuweza kustahimili kuwa na doa kidogo, haswa usoni.

"Utaomba msamaha kwa kufanya kitu kibaya. Kwa nini ni lazima upendeze? Kadiri unavyoonekana kuwa na huruma, ndivyo itakuwa bora zaidi. Kwa njia hii, unaweza kupata huruma yao.” Marry alinyoosha mkono na kusukuma paji la uso wake, "Sio wakati sahihi wa kufikiria kuwa mrembo."

Melissa aliitikia kwa kichwa, akihisi kwamba mama yake alikuwa sahihi. Kwa hiyo, aliweka mfuko wa poda kando na alikuwa na wasiwasi, “Mama, unafikiri Seidrick atanisamehe? Jana, alisema sikustahili kurejea kwa familia ya Masolwa tena … ninaogopa hatakubali.”

Ikiwa hangeweza hata kumuona Seidrick, basi angeweza kufanya nini?

"Hapana. Usijali. Mama atakuwa na wewe. Familia ya Masolwa haitakutendea vibaya kwa kunijali. Mbali na hilo, usiku mmoja wa upendo una thamani ya siku mia za urafiki. Una mimba ya mtoto wa Seidrick. Ilimradi una tabia nzuri na uonekane mwenye huruma wakati wa kuomba msamaha kwa dhati, watakusamehe. Baada ya yote, hawawezi kuruhusu mtoto kuzaliwa bila baba au mama. Hakuna awezaye kuvumilia.” Kila neno Marry alisema liligonga msumari kichwani.

“Mama, hakika nitajirekebisha baadaye, sitakuangusha.” Melissa akaamua.

Mlinzi alipoona ni gari la akina Maziku akawaruhusu kuingia ndani.

Dereva akaegesha gari uani. Marry na Melissa walishuka kwenye gari, kisha kuchukua zawadi walizokuja nazo, wakatembea hadi ndani.

Familia ya Masolwa ilikuwa imemaliza kupata kifungua kinywa. Sam na Seidrick walikuwa karibu kwenda kazini. Alaya alikuwa anaenda kumpeleka mtoto wake shule.
Na Maira alikuwa akiwaona kwa mbali.

Marry na Melissa kisha wakaingia ndani ya nyumba. Marry alisema kwa tabasamu, "Habari za asubuhi. Pole kwa kuwasumbua." Tabasamu kwenye nyuso zote za familia ya Masolwa zilitoweka walipomwona Melissa, na wote wakawa baridi.

Marry na Melissa kwa kawaida walihisi kwamba walichukuliwa kama wavamizi wasiokubalika na familia ya Masolwa. Lakini kwa vile walikuwa hapa na walikuwa wamejipanga kiakili, hawakuwa na jinsi zaidi ya kuendelea.

Marry alimkonyeza Melissa, ambaye alisogea mbele na kuweka sanduku la zawadi kwenye meza ya kahawa. Seidrick alimtazama, "Nani alimruhusu aingie?"

“Seidrick…” Melissa alimwita kwa unyonge.

“Seidrick, hapa pia ni nyumbani kwa Melissa. Ni kawaida kwake kurudi nyumbani.” Marry alitabasamu na kusema.

"Niliweka wazi jana usiku katika familia ya Maziku kwamba hakustahili kurudi kwenye familia ya Masolwa. Kwa hivyo, yeye si binti-mkwe tena wa familia ya Masolwa. Tafadhali toka nje.” Seidrick hakuwa na mzaha.

"Seidrick, Melissa ni mke wako na amekuokoa. Hata kama haujali uhusiano wako, unapaswa kukumbuka kuwa yeye ndiye mwokozi wako. Isitoshe, ana mimba ya mtoto wako. Je, huwezi kumsamehe hata mara moja?” Marry alimuombea Melissa na kumsukuma kwa siri.

Melissa pia alijibu na kusema kwa uso wa huzuni, “Baba, Mama, Alaya, Seidrick, najua nilikosea. Lakini nililazimishwa na Timothy! Na.penda sana Seidrick. Ninaapa kwamba sitawahi kuleta aibu kwa familia ya Masolwa tena. Kwa ajili ya mtoto ambaye hajazaliwa, tafadhali nipeni nafasi!”

“Melissa, usitukane mapenzi. Hustahili kuzungumza juu ya mapenzi!” Seidrick tayari hakuweza kuvumilia usaliti huo.

Ikiwa angemsamehe Melissa wakati huu, basi alistahili kumsamehe Alissa wakati huo! "Melissa, umeiletea aibu familia yetu na kumkasirisha Seidrick. Unathubutuje kuja hapa kutuomba tukusamehe na tutoe nafasi nyingine? Unafikiri sisi ni nini? Shimo la taka?” Alaya alisimama na Seidrick na kuwasemea wazazi wake ambao hawakuwa wazuri wa kusema maneno makali.

“Baada ya kashfa hii kati yako na Timothy, unawezaje kuhakikisha kwamba mtoto aliye tumboni mwako ni wa Seidrick? Usituchukulie sisi sote kama wajinga!”

“Mtoto aliye tumboni mwangu ni wa Seidrick. Yeye ni mjukuu wa familia ya Masolwa.” Melissa alieleza kwa haraka, akinyoosha mkono na kulipapasa tumbo lake tambarare, “Hutaki hata mtoto wako mwenyewe? Huu ni mjukuu wa familia ya Masolwa!"

"Melissa, umesema uongo sana. Hatutakuamini tena.” Maira alikuwa ameona uso wa kweli wa Melissa. Baada ya kashfa hii, asingemkubali Melissa tena.

“Melissa, hujawahi kunyanyaswa katika familia yetu. Je, Seidrick amekukosea? Kwa nini ufanye jambo lisilo na aibu hivyo!” Sam alimkumbuka Alissa na kumwangalia Melissa mbele yake, huku akipandwa na hasira zaidi, “Tuna deni la familia ya Maziku? Mbona mnatuletea aibu tena na tena?

“Hebu nikuambie, familia yetu haitamkubali mwanamke asiye na haya! Melissa, hutawahi kusamehewa na sisi! Hata kama Seidrick atakusamehe, sisi hatutakusamehe kama wazazi wake!"

“Baba, mama, sitakuwa mjinga kiasi hicho.” Seidrick sasa ilikuwa na utulivu zaidi kuliko hapo awali. Alimtazama Melissa ambaye machozi yalikuwa yakimtoka, “Melissa, kwa vile unadai mtoto ni wangu, basi sawa. Tutaachana baada ya wewe kumzaa mtoto.

"Wakati huo, tutafanya vipimo vya unasaba. Ikiwa mtoto ni wangu, sitakwepa jukumu langu na nitamlea mtoto. Ikiwa sivyo, basi tafadhali utamchukua mtoto wako na hutakuwa na uhusiano wowote na familia yangu!”

Maneno ya Seidrick yalivunja tumaini la mwisho la Melissa. Alianguka katika kukata tamaa.

“Hapana, hapana! sikubali!” Melissa aliumia moyoni na kuumia, “Seidrick, huwezi kufanya hivi. Mtoto wetu hawezi kuwa na baba mwingine.”

Sura ya 226

Melissa alijisikia uchungu na kulia kwa mawazo ya kutengwa na Seidrick na mawazo ya mtoto wake kuzaliwa bila baba.

“Seidrick, mimi ni mkeo. Huwezi kunifanyia ukatili sana. Mimi ndiye nimekuwa kando yako na nimekaa nawe ili kuinua miguu yako na kupata nafuu…” Melissa alishindwa kujizuia kulia, “Sasa, nina mimba ya mtoto wako. Huwezi kumuacha mtoto bila baba. Hatuwezi kuachana!”

“Mtoto hajazaliwa. Sina hakika ni mtoto wa nani hadi akapime vipimo vya ubaba. Unafikiri mimi ni mjinga kweli?" Hakukuwa na huruma au ulaini kwenye uso mzuri wa Seidrick hata kidogo, "Kama si kwa ajili ya siku za nyuma, nisingesubiri hadi mtoto azaliwe ili kukupa talaka."

"Kuanzia sasa, huruhusiwi kurudi kwa familia ya Masolwa na kusumbua maisha yetu. Utaishi katika nyumba ya familia ya Maziku. Pesa unazohitaji kutumia kwa chakula, mavazi na uchunguzi wa kimwili zitatumwa kwenye akaunti yako tarehe 1 ya kila mwezi hadi utakapojifungua. Hilo ndilo ninaloweza kukufanyia.”

“Hapana, sitaki talaka. Sitaki kuiacha familia ya Masolwa. Sitaki kukuacha!” Melissa alipiga kelele na kuomba. Lakini Seidrick alimpuuza.

“Melissa, huu ni uamuzi wangu. Si juu yako!” Seidrick alikuwa baridi sana na uamuzi aliofanya haungebadilishwa kwa urahisi, "Ondoka sasa na usichafue siku yangu."

“Baba, Mama, Alaya, tafadhali nisaidieni kumshawishi Seidrick. Sitaki kuachana naye. Sitaki kuiacha familia yetu … Tafadhali. Sasa, Seidrick atawasikiliza nyinyi tu…” Kuona kwamba Seidrick alikuwa haijatikiswa, Melissa angeweza tu kuweka tumaini lake kwa washiriki wengine wa familia ya Masolwa.

Alipiga magoti chini na kuwainamia Sam na Maira ili kuonyesha uaminifu wake.

"Sam, Maira, Alaya, Seidrick, angalieni. Melissa tayari amejua kuwa alikosea. Tafadhali msameheni kwa mara moja. Hakika atawasikiliza nyinyi siku za usoni na hatawahi kufanya jambo lolote la kijinga tena.” Kuona hivyo, Marry pia alikuwa hoi na alijaribu kufanya amani, "Seidrick, kama msemo unavyosema, usiku mmoja wa upendo una thamani ya mia moja ya urafiki. Msamehe tu wakati huu, sawa?"

“Amefanya vile. Tunawezaje kumsamehe?” Sam aliuliza kwa kejeli, “Hakuwa na haya hata akapelekwa kituo cha polisi! Familia yetu sio jalala la kuhifadhi uchafu! Hatuwezi kumsamehe.”

"Sote tunaheshimu uamuzi wa Seidrick!" Maira na Alaya pia walikubaliana na Seidrick, “Hatuwezi kumsamehe.”

"Ikiwa naweza kusamehe kitu kama hiki, basi miaka mitano iliyopita, ningemsamehe Alissa na nisingekuwa na uhusiano wowote na Melissa!" Seidrick alisikitika na akafumba macho yake taratibu.

Mara aliposikia Seidrick akimtaja Alissa, hasira ilimuwaka Melissa.

“Alissa?” Melissa alisimama kutoka chini na kumkabili Seidrick, “Seidrick, si unajua jinsi mimi, Melissa, nilivyokutendea kwa miaka mingi? Nilionewa na Timothy. Ukiwa mume wangu hukunitafutia haki, na hata ukampuuza mtoto tumboni mwangu na sasa unataka kunitaliki?

“Wewe huna moyo sana. Najua hujamsahau Alissa! Unasema kila mara kuwa unamchukia. Lakini bado unampenda ndani yake...

“Nilifumbia macho na kujifanya sijui ukweli kwamba ulikuwa unampenda mwanamke mwingine moyoni mwako. Nililazimishwa na Timothy. Ulinidanganya kiakili na mimi nilidanganya kimwili. Tuko sawa! Sitakuacha!”

"Melissa, huna aibu?" Maira alikasirika sana hadi akatetemeka.

"Mama, usiwe na hasira. Haifai kukasirika na mtu wa aina hii.” Alaya alimuunga mkono May na kumpigapiga mgongoni ili kumtuliza.

Seidrick alifungua macho yake polepole. Hakuwa mpole tena na akamtazama Melissa kwa macho ya baridi, “Ondoka!”

“Kwa nini niondoke?” Melissa alitabasamu kwa ubaridi, “Umenioa. Mimi ni binti-mkwe wa familia ya Masolwa. Nina haki ya kuishi hapa kabla ya talaka yetu! Hapa pia ni nyumbani kwangu!”

Aliyatoa macho yake ambayo yalikuwa yamejaa machozi. Lakini aliendelea kuwa mkaidi, “Maadamu mimi ni mshiriki wa familia ya Masolwa, sitamruhusu Alissa kuingia katika nyumba hii na kuchukua nafasi yangu! Seidrick, hapana!

“Oh … nilisahau kwamba Alissa ameolewa na Bwana Kendrick. Yeye ndiye Bi Kendrick sasa hivi. Hata ukitaka aolewe katika familia ya Masolwa, atakudharau tu. Mimi ndiye mpumbavu pekee duniani ambaye nitakuwa kando yako daima!” Kifua cha Melissa kilimtoka kwa nguvu. Kulikuwa na mchanganyiko wa hisia za uadui na chuki, “Kwa nini huwezi kunitazama tu? Mimi ndiye ninayekupenda sana.”

"Melissa, unasema unampenda Seidrick. Umefanya nini kinachoweza kuonyesha kuwa unampenda Seidrick?" Alaya alikunja uso, “Timothy alikulazimisha? Alikulazimisha vipi? Ikiwa huna chochote juu yake, angewezaje kukulazimisha kulala naye?"

"Nilikuwa nadhani wewe ni msichana mzuri, mpole na mtamu. Lakini jiangalie sasa. Wewe ndiye uliyemkosea Seidrick na familia ya Masolwa. Unawezaje bado kuongea kwa ujasiri mkubwa hivyo?"

“Nina tatizo gani kwangu? Nimelazimishwa kuwa hivi na nyinyi!” Macho ya Melissa yalikuwa mekundu, na alimchukulia kila mtu kama adui.

Seidrick hakusema chochote zaidi kwake, lakini alisema tu kwa walinzi wa kaya, “Jamani, mwondoeni hapa. Msimruhusu aingie tena. Yeyote atakayemruhusu atafukuzwa kazi na familia ya Masolwa.”

“Ndiyo, bwana.”

Kisha watu wawili wakasogea mbele na kumwambia Melissa, “Bi. Masolwa…”

"Yeye si Bi Masolwa tena wa familia ya Masolwa." Seidrick ilirekebisha maneno yao.

“Bi. Maziku, tafadhali ondoka sasa, la sivyo tutakukosea adabu.” Wanaume hao wawili walijaribu njia za haki kabla ya kutumia nguvu.

“Nyie ni akina nani? U
Mkithubutu kunigusa, nitawaua!” Melissa aliwatazama watu wale wawili na bado alikuwa na kiburi.

“Baba twende kazini. Waachie hawa.” Seidrick alimuita Sam.

Sam alikunja uso huku akimtazama Melissa ambaye sasa alikuwa kichaa na kugeuka na kuondoka.

“Seidrick, usiende. Usiniache.” Kuona Seidrick anaondoka, Melissa aliharakisha kumfuata na kumzuia njia.

Seidrick hakutaka kumwangalia hata kidogo akawaambia tu wale watu wawili kwa ubaridi, “Mbona bado mmesimama pale? Hakuna haja ya kuwa na adabu kwake. Mtoeni tu hapa.”

“Ndiyo.” Wanaume hao wawili walisonga mbele na kumshika Melissa, huku Melissa akilaani, “Nyinyi wawili ni walinzi tu wa familia ya Masolwa.
Mnathubutuje kunigusa? Niacheni!”

Wale watu wawili walipuuza laana zake na kumkokota Melissa kuelekea nje ya sebule.

Sura ya 227

Marry alimtazama Melissa akiburutwa moja kwa moja na watu hao wawili na aliweza kujua kwamba familia ya Masolwa ilikuwa imedhamiria kutomkubali Melissa tena. Yeye pia alikuwa amechoka.

Bado alimshawishi Seidrick kwa matumaini, “Seidrick, tulia. Melissa ni mjamzito sasa na yuko katika hali mbaya, akiongea upuuzi. Tafadhali usimlaumu kwa alichokifanya. Hakika nitamfundisha somo.”

"Sina la kumwambia zaidi." Seidrick ilitazama vitu kwenye meza ya kahawa, "Tafadhali chukua ulichokuja nacho." Kwa hayo, Seidrick na Sam kisha wakatoka nje.

Alaya alimsaidia Maira kupanda ghorofani, akimuacha Marry peke yake pale sebuleni.

"Bi. Maziku, nitakupeleka nje.” Lauren, mtumishi wa familia ya Masolwa, alikuja na kusema.

Marry alipumua na alikuwa na aibu sana kukaa katika familia ya Masolwa. Kwa hivyo, aligeuka kuondoka bila msaada.

Lauren alichukua masanduku ya zawadi kwenye meza ya kahawa na kumfuata Marry ili ampeleke nje.

Melissa alishikwa na watu hao wawili. Hakuweza kujiachia na aliweza kumtazama tu Seidrick akiingia kwenye gari, asingeweza kumkaribia.

“Seidrick, huwezi kunifanyia hivi!” Melissa alirudia tu maneno haya, hakitaka kuwa mwanamke wa kawaida tu kwa Seidrick.

Alikuwa amejitahidi sana kumpiku Alissa miaka mitano iliyopita na akaaminiwa na Seidrick. Lakini baada ya miaka mitano tu, hakuwa na chochote kilichobaki.

Alichokuwa ametoa na hisia zake kwa Seidrick ni kweli. Hata alimpa Seidrick moyo wake. Lakini sasa, bado aliachwa na Seidrick.
Melissa angewezaje kuzowea? Ilikuwa ngumu sana kumeza!

Lakini hakuna mtu aliyemjali Melissa, kana kwamba ndiye hewa. Haijalishi alichosema au kulaani au kupiga kelele, walimpuuza tu.

Dereva alitoa gari nje ya lango la kuchonga la familia ya Masolwa. Melissa alitolewa nje ya lango la familia ya Masolwa na watu hao wawili.

Mara baada ya Melissa kuwa huru, alikimbiza gari jeusi ambalo Seidrick na baba yake walikuwa wameketi.

“Seidrick, nisubiri. Seidrick, umesahau ulichosema miaka mitano iliyopita? Umesahau kuwa tulipooana ulisema utanitunza maisha yako yote na hutaniacha peke yangu? Seidrick … huwezi kunifanyia hivi…” Melissa alilifuata gari hilo kwa huzuni na kuendelea kulia.

Lakini Seidrick hakuguswa na vitendo vya Melissa. Alikaa ndani ya gari na kufumba macho taratibu, hakutaka kuutazama uso wa ajabu wa Melissa kupitia kioo cha kuakisi nyuma.

"Seidrick, uko sawa?" Sam alimtazama Seidrick, ambaye alikunja uso, na kuhisi huzuni.

“Baba, mimi sijambo.” Seidrick alitikisa kichwa chake, lakini hakufungua macho yake.

"Familia ya Maziku imekwenda mbali sana. Usijali. Baba hatakuacha uteseke sana tena na tena.” Sam alipiga bega la Seidrick, "Kuanzia sasa na kuendelea, hatutakuwa na ushirikiano wowote na familia ya Maziku tena."

"Kwa mwanamke kama Melissa, usimwonee huruma. Alitandika kitanda chake, mwache alale mwenyewe. Hawezi kumlaumu mtu yeyote!”

“Baba, najua. Usijali. Naweza kuishughulikia.” Seidrick alifungua macho yake na kutabasamu mbele ya Sam.

Melissa bado alikuwa akilikimbiza gari. Seidrick ilimwambia dereva, "Endesha haraka zaidi."

“Ndiyo.” Dereva aliitikia kwa kichwa na kukanyaga kichapuzi kwa nguvu zaidi ili aendeshe kwa kasi na kumtikisa Melissa.

Gari lililokuwa likienda kasi liliongeza umbali kati yake na Melissa. Lilipotea hatua kwa hatua kwenye kona. Melissa, ambaye alikuwa mvivu, hakukimbia mbali kabla ya kuishiwa nguvu na kuanguka chini.

Aliinua mikono yake chini, akivuta hewa. Jasho lilitiririka chini. Lakini aliendelea kutazama upande gari lilipotoweka na hakuwa tayari kutazama pembeni.

“Seidrick… kwa nini unanitendea ukatili…” Melissa alikunja ngumi zake taratibu na alikuwa na uchungu. Mabega yake yalitetemeka. Aliuma midomo yake na mwishowe akalia.

Katika siku hizi mbili, alitokwa na machozi zaidi kuliko miaka mitano aliyokuwa na Seidrick.

Wakati huo, alitokea machozi kwa sababu ya furaha. Sasa, ilikuwa ni kwa sababu ya kukata tamaa.

Gari la familia ya Maziku lilisimama karibu na Melissa. Marry alikuwa amekaa ndani yake.

Dirisha lilivingirishwa chini. Marry alimuangalia Melissa aliyekuwa amekaa magotini katikati ya barabara akilia, “Kulia kuna faida gani sasa! Kama ungejua ingekuja hivi, ungetenda tofauti!"

“Kama usingewaruhusu Timothy na Alissa kwenda miadi ya uchumba, ningewekwa na kulazimishwa naye? Je, huna mchango wowote kwangu kwa hapa nilipo leo?” Melissa alicheka kwa uchungu.

Marry aliposikia hivyo, uso wake ulizama na hakuwa na furaha sana.

“Melissa, kama mama yako, nimefanya ninachoweza kukufanyia. Familia ya Masolwa haiwezi kukusamehe na siwezi kukusaidia. Nina aibu sana kuja kwa familia ya Masolwa tena. Kwa hiyo, unaweza kukaa hapa kama unavyotaka.” Kwa hayo, Marry akamwambia dereva, “Twende.”

Dirisha lilikunjwa taratibu na kuziba uso maridadi wa Marry. Wakati huu, Marry alikuwa tofauti.

Gari lilipita karibu na Melissa na kuondoka. Vumbi kutoka nyuma ya gari lilimwagika usoni mwa Melissa, na kumfanya asongwe na kukohoa.

Melissa alilitazama lile gari kwa mbali lakini hakusogea hata kidogo. Hangeiacha tu familia ya Masolwa bila chochote.

Ilibidi amsubiri hapa Seidrick. Hakuamini kwamba alikuwa mkatili kiasi hicho kwake. Lazima atakuwa na hasira na hangeweza kumsamehe mara moja. Anapaswa kumngoja hapa hadi apoe. Kisha, angeweza kwenda nyumbani na bado wangeweza kupendana kama hapo awali.

Melissa alithamini udanganyifu, akasimama, na kwenda kwenye mlango wa mbele wa familia ya Masolwa. Aligonga kengele ya mlango, lakini wengine wa familia ya Masolwa hawakuthubutu kumruhusu aingie.

Haijalishi alichosema au kufanya, walimpuuza.

Melissa alilazimika kungoja nje ya mlango na kukaa chini dhidi ya nguzo wakati hakuweza kujikimu tena.
Sebuleni, Maira alikuwa akinywa chai na Alaya,

"Ameondoka?"

"Bado." Alaya akatikisa kichwa.

"Huyu mwanamke hana aibu sana!" Maira alikasirika sana hivi kwamba aliweka kikombe maridadi cha chai cha mtindo wa Uropa kwenye sahani akiwa na uso wa kuchukizwa, “Je, ikiwa ataonwa na wengine huku akiendelea kukaa mlangoni? Ameidhalilisha familia yetu. Sasa anataka hata kutuburuta hadi kuzimu. Kwa kweli ana nia potofu!”

"Mama, usiwe na hasira. Haifai kuharibu afya yako.” Alaya alikunywa chai yake kwa raha, “Hakika hajakata tamaa sasa.
Puuza tu. Atakata tamaa baada ya siku mbili au tatu.”

"Na yeye ndiye aliyefanya kitu kibaya. Ikiwa ataendelea kuwa mkaidi, tunaweza kufanya mkutano na waandishi wa habari ili kuiweka wazi. Watu ambao hawajui chochote wataelewa jinsi tunavyoumizwa."

"Kisha tutachekwa na wengine!" Maira hakufikiri ni wazo zuri.

“Familia ya Maziku itafedheheshwa pia! Kwa hivyo, nitaiweka wazi kwa familia ya Maziku. Labda sisi sote tutadhihakiwa, au wamrudishe binti yao mpendwa na kukaa mbali na familia yetu.” Alaya alisema.

Maira aliitikia kwa kichwa na kustarehe kidogo, "Lakini kwa kweli inampa Seidrick wakati mgumu."

Alaya alishika kikombe mkononi na kushikanisha midomo yake bila kusema neno lolote.

Sura ya 228

Seidrick alifika ofisini na baba yake. Familia ya Masolwa ilimiliki Kampuni ya Tanganyika Ferries, iliyoendesha vivuko kwenye visiwa mbalimbali ndani ya ziwa Victoria.

Alipoingia ofisi ya Meneja Mkuu, msaidizi wake, Ruben Samike, akamfuata, “Bw. Seidrick, nikufanyie nini?"

Seidrick aliketi kwenye kiti cha kuzunguka cha ngozi na kusema, “Nisaidie kujua Alissa alikuwa anafanya nini nilipolazwa hospitalini miaka mitano iliyopita, alikuwa anamfahamu mwanaume yupi na baba wa mtoto wake ni nani. Na ninataka kujua mfadhili wangu alikuwa nani. Tafuta majibu haraka iwezekanavyo.”

"Ndiyo, Bwana Seidrick." Ruben aliahidi kisha akaondoka.

Baada ya kuondoka, Seidrick aliweka viwiko vyake juu ya dawati, akiwa ameshikanisha vidole vyake na nyusi zake zikiwa zimekunjamana.

Baada ya kukaa pale kwa muda, alisimama kisha akachuchumaa na kufungua droo ya mwisho ya dawati lile, kisha akatoa picha nyeupe ya mbao iliyofunikwa na vitabu vingi.

Akaweka sura ya picha kwenye dawati. Kioo cha fremu kilivunjwa, lakini picha ya ndani ilikuwa bado shwari. Alimpapasa mtu huyo kwenye picha kwa vidole vyake kupitia kioo.

Msichana kwenye picha alikuwa ni Alissa. Alikuwa na umri wa miaka 18 hivi kwenye picha; alikuwa amesimama chini ya mti wa cherry, na nywele ndefu zilimwagika kichwani mwake.

Katika picha, Alissa alitabasamu kwa furaha na alionekana kama ua katika bustani na mavazi meupe na petals kuanguka chini karibu yake.

Kila mara aliweka picha hii kwenye kichwa cha kitanda chake; baadaye akaipeleka ofisini kwake alipokuwa na mafunzo ya kazi; na kisha akaipeleka hospitalini alipokuwa mgonjwa, kwa sababu alitaka kukaa naye kila dakika. Lakini, alitoweka alipokuwa mgonjwa na alikuwa karibu kufa ...

Alipotokea akiwa na mtoto mikononi mwake, alihisi kuumia na huzuni. Afadhali asingefanyiwa upasuaji au kupona, afadhali angekufa.

Baada ya kumuoa Melissa, alimsukuma kumsahau Alissa. Na alikuwa amemsahau kwa miaka mitano. Hata hivyo, hakuweza kumsahau mpaka sasa hivi, na bado alimkumbuka.

Hakumpa nafasi ya kueleza, ikabidi apate jibu peke yake sasa.

***
Wakati huo huo, Kendrick alikuwa amekaa ofisini na kusikiliza ripoti ya Chale Kisendi, msaidizi wake.

"Bwana Kendrick, ni unawaza nimi?" Chale aliona kwamba bosi wake hakuweza kuzingatia kazi siku hiyo.

Kendrick alifikiria jambo fulani kwa muda kisha akasema, “Chale, ninahitaji usaidizi wako.”

"Nikusaidie nini Bwana Kendrick?" Chale aliuliza.

“Nataka kujua ni nini kilitokea miaka mitano iliyopita…”

Kendrick alipozungumza kuhusu hilo, Chale aliogopa na kumkatisha, “Je, unataka kumchunguza mwanamke ambaye alilala nawe na kutoweka miaka mitano iliyopita?”

Alimchunguza mwanamke huyo kwa muda mrefu kipindi hicho, lakini hakuweza kupata habari yoyote kumhusu. Hatimaye Kendrick akakata tamaa ya kumchunguza.
Kwa nini alimtaja tena?

Kendrick alimkazia macho na kusema, “Asante kwa kunikumbusha kwamba hukuweza hata kupata taarifa zozote kuhusu mwanamke huyo.”

"Bwana Kendrick, nadhani mwanamke huyo alikuwa amejipanga vizuri kabla hajatimiza lengo lake. Alikuwa mjanja sana. ”

Chale alitiliwa shaka na Kendrick kuhusu uwezo wake kwa sababu ya mwanamke huyu, hata akatishiwa kufukuzwa kazi. Hivyo pia hakuridhika na mwanamke huyu.

“Hakuna udhuru!” Kendrick aliegemea nyuma ya kiti chake na kumlaumu.

Chale alithubutu kutosema lolote akiwa ameinamisha kichwa chini.

"Safari hii, ningependa kukupa nafasi moja zaidi. Lakini safari hii unahitaji kumchunguza Alissa.” Kendrick hakuwa na jinsi zaidi ya kufanya hivyo maana hakujua zaidi kuhusu Alissa.

Hapo awali akidhani Seidrick ndiye baba wa Doris, lakini alikosea kwani Doris hakuwa binti yake. Kwanini Alissa hakumwambia mtu yoyote ni nani ambaye alikuwa baba mzazi wa Doris? Kusudi lake lilikuwa nini?

“Nisaidie kuchunguza kilichotokea wakati Alissa alipomzaa Doris miaka 5 iliyopita. Nataka kujua zaidi juu yake kwa undani. Na la muhimu zaidi ni kuchunguza baba mzazi wa Doris ni nani.”

“Ndiyo bwana Kendrick. Sitakuangusha wakati huu. ” Kisha Chale akaondoka.

Sura ya 229

Alissa naye alikuwa na siku mbaya kazini.

Baada ya kazi, dereva alikuwa akimsubiri kwenye mlango wa kampuni. Dereva alimfungulia mlango wa gari, kisha akaingia ndani ya gari.

Wakiwa njiani kuelekea shule ya chekechea, Nora alimpigia, “Alissa, twende tukanywe pombe leo usiku.”

"Lazima nimchukue Doris." Alissa akajibu, “Na ni lazima nimtunze usiku wa leo.”

“Muombe Bwana Kendrick akusaidie.” Nora alitenda kama mtoto.

“Amerudi Geita leo…” Alissa alikasirika alipozungumza kuhusu Kendrick.

“Si analala hukohuko? Hiyo ni nzuri! Ni lazima utoke nami.” Nora alicheka kwa furaha na kusema, “Na unaweza kumpeleka Doris nyumbani kwangu, na Freya atamtunza vizuri.”

Alissa alikaa kimya kwa muda akawaza mara mbilimbili.

“Kwa kuwa Bwana Kendrick amerudi Geita, ni nafasi nzuri kwetu kwenda nje na kujiburudisha. Jayden pia ana wakati leo, na hatujaungana kwa muda mrefu. Haya, twende zetu.” Nora alijaribu kila awezalo kumshawishi.

“Sawa.” Alissa alikuwa amemuahidi, kwa sababu pia alitaka kumuona Jayden.

"Basi nitakusubiri wewe na Doris nyumbani." Nora alisema kwa furaha.

Alissa alipofika shule ya chekechea na kumchukua Doris, Doris hakumuona Kendrick, akauliza, “Mama baba yuko wapi?”

"Alirudi Geita kushughulikia kazi zake." Alissa alimshika mikono na kujibu, “Tutaenda kumtembelea shangazi Nora.”

“Hiyo ni nzuri! Pia namkumbuka shangazi Nora. ” Doris alifurahi kidogo, “Nitafurahi kumuona.”

Alissa alimshika kichwa chake taratibu kwa mkono na kumshika mikononi mwake. Alijiona hajali chochote ilimradi tu Doris aendelee kuwa pamoja naye.

Walipofika nyumbani kwa Nora, Freya tayari alikuwa amewaandalia chakula. Aliwasalimia kwa furaha, “Habari, Bibi Alissa. Habari, Doris.

"Halo, Freya." Alissa na Doris walimjibu kwa pamoja.

Nora alisogea mbele na kuinama kugonga pua ya Doris kwa upole kwa kidole chake na kusema, “Unanimiss?”

“Bila shaka.” Doris alimbusu usoni huku akiongea.

"Twende kwa chakula cha jioni." Nora alimshika mkono na kumpeleka kwenye chumba cha kulia chakula.

Alissa aliweka mkoba na begi lake na kisha akatembea hadi chumba cha kulia pia.

Nora alipenda kula vyakula vya mafuta huku Alissa alipenda kula mboga mboga na matunda na kunywa mtindi.

"Kula kidogo, tafadhali." Nora akamwambia Alissa, “Tutakunywa mvinyo baadaye.”

Kati ya milo mitatu kwa siku, Alissa alikula chakula chepesi jioni. Lakini Doris alihitaji lishe, hivyo angetayarisha chakula chenye lishe ambacho kilimfaa.

Baada ya chakula cha usiku walicheza pamoja na Doris kwa muda, kisha Jayden akaja kuwachukua.

Walimwomba Freya amtunzie Doris, na Doris alikuwa na tabia nzuri, “Mama, kila siku unachoka sana kutoka kazini, ni vizuri utoke nje kwenda kuburudika. Na huna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu mimi.”

Alissa aliguswa moyo sana na kuthaminiwa sana kwa sababu binti yake alikuwa na akili timamu na mwenye kujali.

Dereva ndiye aliyekuwa na jukumu la kuendesha gari. Jayden alikaa kwenye siti ya abiria, Alissa na Nora nyuma.

Walienda kwenye Baa ya Las Vegas, ambayo ilikuwa miongoni mwa baa kubwa na bora zaidi katika Jiji la Mwanza. Na wafanyakazi hao kwenye baa walichangamka tena na tena.

Walipanda ghorofa ya pili na kukuta meza iliyokuwa na vigawanyiko na kuketi, wakiikabili sakafu ya kucheza dansi chini ili waweze kuwaona live band wakicheza.

Jayden alimuomba mhudumu awape dazeni mbili za mvinyo, jambo ambalo lilimshangaza Alissa, “Jayden, una uhakika tunaweza kunywa mvinyo wote huo?"


“Tukilinganishwa na wengine, sisi ni dhaifu sana. Nadhani tunapaswa kunywa zaidi." Nora alisema kwa dharau.

“Umesahau kuwa ulilia mtaani baada ya kulewa mara ya mwisho? Usinywe pombe kupita kiasi.” Alissa akamjibu.

“Mnawezaje kwenda kunywa pombe bila kunialika?” Jayden akajiegemeza kwenye sofa, huku miguu yake ikiwa imepishana.

"Je, ungeweza kwenda kwenye kibanda cha chakula kwenye mlango wa shule yetu kunywa? Haya, haikufai kwani wewe ni mtukufu.” Nora alidhihaki.

Jayden daima alifuata maisha mazuri, na alihitaji ubora wa juu kwa kila kitu maishani mwake. Kwa hiyo asingeenda kwenye kibanda cha chakula kunywa kinywaji.

"Fungua viriba vya divai, tunywe." Jayden akamwambia mhudumu.
Alissa, Nora na Jayden wakachukua chupa na kushangilia kwa pamoja.

"Nilisikia kwamba umepata mchumba." Nora alimuuliza Jayden kwa kucheza, “Yule msichana alikuwa nani? Nilisikia kwamba alikuwa binti wa familia ya Kamote?”

"Je, ni Lilah Kamote?" Alissa alisikia kwamba Lilah Kamote alikuwa bora sana hivyo angeweza kuendana na Jayden. Na mara chache wasichana wangeweza kulinganishwa naye. Kwa hivyo alisema, "Nadhani anaweza kukidhi mahitaji yako ya juu."

Jayden alikunywa mvinyo kisha akajibu, "Hapana."

"Alikuwa wa familia gani?" Nora aliuliza tena, kwa sababu alikuwa na hamu zaidi juu yake.

"Familia ya Mageni?" Jayden alisema bila kujali.

Lakini hawakujua kuwa familia ya Mageni ilikuwa na binti. Walisikia kwamba Bw. Mageni alikuwa na wake watatu na kulikuwa na wavulana wote katika familia zake

Kinyume chake, familia ya Mabeyo ilikuwa na mvulana mmoja tu, ambaye alikuwa Jayden. Na alikuwa mtoto wa mwisho katika familia yake.
Kwa hivyo ilikuwa tofauti na familia ya Mageni.

“Inasemekana kuwa mke wake wa kwanza alijifungua mapacha, na pacha mmoja ambaye ni binti aliibiwa hospitalini wakati huo. Lakini sasa wamempata.” Jayden akasimama na kutazama mbele.

"Nadhani familia ya Mabeyo ina nguvu sana. Baada ya babu yako kusema hadharani kuwa anataka kukusaidia kupata msichana wa kuoa, kila mtu alijaribu kila awezalo kuwatambulisha mabinti zake kwako. Nadhani una bahati sana.” Nora alicheka sana.

"Haijabainika ikiwa msichana aliyepatikana na familia ya Mageni alizaa na mke wake wa kwanza au alitolewa tu kimchongo na mwanamke mwingine wa Bw.
Mageni. Sitaki kutapeliwa nao.” Jayden alisema kwa kejeli.

"Jambo muhimu zaidi ni kwamba, unampenda yupi kati ya hao?" Alissa alimuuliza.

"Kwa maoni yangu, lazima ampende msichana wa familia ya Kamote, kwa sababu ana mahitaji ya juu na ladha nzuri." Nora alisema.

"Sitapenda msichana kirahisi." Jayden alisema, “Zaidi ya hayo, nina umri wa miaka 27 tu na sitaki kabisa kuoa. Nataka kufurahia maisha yangu kwa sababu mimi ni mdogo sana.”

" Alissa na Nora walimtazama na kusema, "Huwezi kuamua kuoa au kutooa, kwa sababu babu yako atakufanyia uamuzi. Niambie babu yako anampenda yupi?"

Jayden alikunja uso kisha akajibu, "Haijalishi ni yupi anampenda, inategemea mimi."

"Nafikiri ni lazima ni kwa sababu babu yako alifikiri kwamba msichana wa familia ya Mageni angeweza kuzaa watoto wa kiume, kwa hiyo angeahidi kukuomba uchumbiane naye." Alissa alisema, “Kwa hiyo nadhani atakuomba umuoe.”

“Lakini nadhani inawezekana zaidi atamwomba Jayden amuoe msichana wa familia ya Kamote, kwa sababu binti yao amesoma vizuri. Kinyume chake, msichana wa familia ya Mageni hakukulia katika familia ya Mageni, hivyo anaweza kuwa mbaya zaidi kuliko msichana wa familia ya Kamote. katika kila nyanja.” Nora alitoa maoni yake mwenyewe,

“Isipokuwa…” Hakuendelea kwa makusudi.

“Unataka kusema nini?” Alissa alimuuliza.

Na Jayden naye akamtazama na kusubiri jibu lake.

Sura ya 230

Nora alitabasamu kwa kushangaza, "Isipokuwa Jayden alimpenda mara ya kwanza na kumchagus yeye..."

Jayden alipaliwa vibaya na kutema mvinyo kwa uzembe sana.

Kwa bahati nzuri, walikaa katika eneo la VIP kwenye ghorofa ya pili, kwa hiyo hapakuwa na watu wengi waliokuwa makini nao.

Nora na Alissa walikuwa wamechelewa sana kukwepa, na baadhi ya madoa ya mvinyo yalinyunyiziwa kwenye nguo zao.

"Jayden, tafadhali zingatia picha yako mwenyewe." Nora alichukua vipande vichache vya tishu ili kufuta madoa ya mvinyo kwenye mikono yake.

"Ninaapa sitampenda." Jayden akafuta midomo yake kwa kipande cha tishu.

"Inamaanisha kuwa haumpendi, sawa?" Nora alimgeukia Alissa aliyekuwa ameketi kando yake na kusema, “Alissa, nadhani ni sawa.
Anampenda Lilah.”

"Naam, umeshinda." Na kisha Alissa akachukua chupa ya divai na kusema, “Nitakunywa.”

Alissa alifumba macho kisha akainywa ile wine. Na Jayden alisema baada ya kujisafisha, “Kweli nimemchagua Lilah, lakini babu yangu anapenda Sia Mageni. Kwa hiyo…”


“Kwa hiyo nini kilitokea?” Nora alikuwa na wasiwasi, “Je, babu yako alikuomba uwaoe Lilah na Sia ili upate wake wawili kama Bwana Mageni?”

Jayden alimtazama Nora. Ukimya wake uliashiria kukubali.

"Lakini nadhani inapendeza, kwa sababu unaweza kuwa na wake wawili, na wanaweza kuzaa watoto wengi kwa ajili yako." Nora alimcheka.

“Unasemaje? Nani anathubutu kufanya hivi?” Jayden hakukubaliana naye, “Hata kama mwanaume anaweza kuwa na wake wengi, sitafanya hivyo.”

"Kwa kuwa una jeni nzuri kama hii, inasikitisha sana kutokuwa na watoto zaidi." Nora alipenda kubishana na Jayden.

“Kwa nini basi huna watoto wengi na Alan?” Jayden alimuuliza.

"Kama unavyoona, simpendi, kwa hivyo sitazaa naye mtoto." Nora aliinua mabega yake kidogo.

Alivaa gauni jekundu la mabega na shingo iliyokatika na nywele ndefu za mawimbi zilizotawanyika mabegani mwake, jambo ambalo lilimfanya aonekane wa kike sana.

"Hata mimi siwapendi." Jayden alimtazama Nora kisha akacheka ghafla, “Nora kwa vile humpendi Alan unaweza kuachana naye.
Kwa kweli, napenda msichana kama wewe. Usingeolewa nikiwa ughaibuni, ningerudi na kukuoa, halafu akakosa nafasi ya kukuoa.”

"Ikiwa hautajali ikiwa nitaachana, babu yako atakuruhusu?" Nora aliunga mkono kidevu chake kwa mikono yake na kujikanusha yeye mwenyewe. "Sahau. sitaki kukuumiza.”

Nora aliitikisa chupa ya mvinyo mkononi mwake na kusema, “Na nimekuwa nikielewana naye miaka hii. Alifanya alichoniahidi tulipooana. Isitoshe, sitapenda watu wengine nikiolewa.”

Jayden na Alissa walishangilia kisha wakanywa.

“Mnamaanisha nini jamani?” Nora alisema kwa kutoridhishwa, "Wacha tunywe pamoja. Alissa, kunywa pamoja nami."

Nora akafungua chupa mpya ya beti kisha akamkabidhi Alissa.

Kisha wakanywa tena pamoja.

Kulikuwa na chupa tupu zaidi na zaidi kwenye meza, Nora akamwambia kwa upole, "Jayden, utafanya nini?"

"Sina chaguo ila kuchagua mmoja." Jayden alisema bila kujali na alionekana kutokuwa na wasiwasi juu ya ndoa yake mwenyewe.

“Jayden, kama rafiki yako mkubwa, natumai unaweza kuoa msichana ambaye unampenda sana, vinginevyo haina maana kuoa. Na utakuwa na furaha tu baada ya kuoa yule umpendaye.” Alissa alimwambia


“Furaha? Unafikiri tuna furaha?” Jayden alihisi kuwa ni ujinga, “Sitaki kuzungumzia jambo hilo. Ninataka tu kufurahiya na kufurahiya maisha yangu. Huna haja ya kuwa na wasiwasi juu yangu, kwa sababu najua cha kufanya.”

Na kisha akasimama na kuelekea kwenye stage ya dansi, akiwa na chupa moja ya mvinyo katika mkono wake mmoja na mkono mwingine kwenye mfuko wake wa suruali. Aliutikisa mwili wake kwa muziki huo huku akiwatazama wale watu waliokuwa wakicheza.

Akatazama huku na huko kisha akatazama kaunta ya baa. Hakuwa mbali na baa iliyokuwa upande wake wa kushoto, na baa hiyo ndiyo ilikuwa sehemu yenye mwangaza zaidi.

Alimwona mtu ameketi juu ya kiti kirefu na kunywa peke yake. Alihisi kuwa mtu huyo anaonekana kumfahamu.

Wakati huu, mwanamke mrembo aliyevalia nguo za chini alikuwa akimsogelea na ilionekana kuwa anataka kumtongoza.
Jayden alitabasamu kisha akawaambia Nora na Alissa, “Unajua ninamuona nani?”

"Nani? Msichana mzuri?" Nora alicheka.

“Mwanaume. Na tunamfahamu.” Jayden alimtazama Alissa na kusema, “Na tulielewana naye hapo awali…”

“Seidrick?” Nora alisema.
Alissa naye alijua kuwa ni Seidrick, lakini hakutaka kujibu. Alichukua chupa ya mvinyo kisha akanywa.

“Kwa nini asibaki nyumbani na mkewe huku akinywa pombe peke yake hapa? Ni nadra kufika mahali kama baa.” Nora alifikiri kwamba kulikuwa na tatizo kwake.

"Ningependa kumwalika anywe pamoja nasi." Jayden alisema.

"Jayden, kwa nini unataka kufanya hivyo?" Alissa alikasirika kidogo akiwa na chupa ya mvinyo mikononi mwake, “Nitaondoka kama atakuja hapa.”

“Nataka kulipiza kisasi kwake kwa sababu alikuumiza hivyo hapo awali. Nitamlevya usiku wa leo.” Jayden akamwambia anachotaka kufanya.

“Sitaki kumuona.” Alissa alichukua chupa ya mvinyo na kunywa haraka, hivyo akapaliwa.

"Basi ningependa kushuka chini na kunywa pamoja naye." Na kisha Jayden akaondoka.

"Usifikiri sana." Nora alipiga mgongo wake kwa upole, “Jayden alitaka tu kukusaidia. Usimlaumu.”

“Sitaki kumlaumu. Sijui jinsi ya kukabiliana naye nikimwona.” Alissa alijaribu kutolia kisha akainywa tena ile wine.

Nora alifikiri kwamba kulikuwa na tatizo kwake, “Una tatizo gani?”

"Melissa aliwaambia kila mtu kwamba nilimzaa Doris ili kumuokoa Seidrick." Alissa alimweleza Nora kilichotokea jana yake.

Nora alishtuka na kusema, “Kwa hiyo Bw. Kendrick amekuwa na hasira baada ya kujua jambo hilo, sivyo?”

“Alisema hatakasirika. Lakini nilihisi kwamba alikuwa na hasira.” Alissa alisema.

"Hakukuambia alichofikiria hasw" Nora alipumua, "ikiwa ni mimi, ningehuzunika pia. Baada ya yote, ulijifungua mtoto ili kumsaidia mpenzi wako wa zamani. Ilimaanisha kwamba ulimpenda kweli, hivyo ungekuwa jasiri sana kumwokoa. Sidhani kama alikuwa na hasira. Nadhani alikuwa na wivu."

Sura ya 231

Alissa alihisi haiaminiki na kushangaa, kisha akakunja uso na kufikiria tena. Hakuamini kuwa Kendrick alikuwa na wivu.

Alissa aligundua hilo ghafla baada ya Nora kumwambia.
"Nora, alikuwa na wivu kweli?" Alissa hakuamini.

"Kama sivyo, kwa nini afanye hivyo?" Nora alisema kwa tabasamu, “Nadhani anajali sana kuhusu wewe.”

“Simpendi Seidrick hata kidogo. Kwa nini anakuwa na wivu?” Alissa alifikiri ni jambo la ajabu, “Sitampenda Seidrick kwani aliniumiza sana hapo awali.
Mbona haelewi?”

“Anajua kuwa humpendi Seidrick tena? Umemwambia wazi kuwa unampenda?" Nora alimuuliza.

Alissa alifikiria jambo hilo kisha akasema, “Inaonekana sikuwahi kumwambia.”

"Kwa hivyo hawezi kuhakikisha kama unampenda yeye au Seidrick kwa sababu haujawahi kumwambia kuhusu hilo." Nora aliugusa moyo wake na kusema, “Na, ulimwambia kuwa hukumpenda kwa mapenzi yako yote. Umemuumiza sana hivi.”

“Alinikatiza kabla sijamaliza kuzungumza muda huo. Kwa kweli nilisema kwamba sikumpenda kwa mapenzi yangu yote wakati huo.
Lakini ni kwa sababu alikuwa bora sana, na sikujiamini, kwa hivyo niliogopa kuumizwa ikiwa ningempenda kwa mapenzi yangu yote…” Alissa aliuma mdomo wake.

Aliogopa kwamba angeumizwa tena, kwa hivyo hakuthubutu kumpenda kwa mapenzi yake yote. Baada ya yote, hakuweza kuvumilia maumivu ya kihisia tena.

"Mara ya kwanza kukosea ni sawa, mara ya pili lazima ujihami." Nora alimshika mabega yake kwa upole na kusema kwa upendo, “Ninaweza kukuelewa. Hata hivyo, Bw. Kendrick ni mwanamume. Wanaume daima ni wamiliki. Na wewe ni mke wake, hivyo ana matumaini kwamba unaweza kuwa wake. Nadhani hakukosea...

“Alissa, unahitaji kuwasiliana naye zaidi. Na unahitaji kumwambia jinsi unavyofikiri vizuri, ili ajue kwamba unampenda.” Nora alimtazama na kusema, “Kama wanawake, tunahitaji hali ya usalama, vivyo hivyo mwanamume. Na nadhani unapaswa kufanya zaidi kwa Bwana Kendrick."

“Yeye ni bora sana. Kwa nini yeye pia hana hali ya usalama?” Alissa hakuelewa.

“Hata awe bora kiasi gani, anapopenda mtu, atakosa usalama. Inamaanisha kwamba anajali sana na anakupenda sana.” Nora alimwambia.

Alissa alishangaa, lakini bado alihisi ni jambo lisilowezekana.

Ingawa alijua kuwa Kendrick alikuwa mzuri kwake, alimpenda na alijitahidi kumlinda, lakini hakuthubutu kuamini kuwa anampenda.

“Kwa jinsi alivyo mtukufu, hatamuonea wivu mwanamke kirahisi. Kwa hivyo, ikiwa ana wivu kwa sababu yako, lazima akupende sana.
Niamini mimi, Alissa." Nora alipiga mabega yake kwa upole na kumtia moyo, "Baada ya kurudi, unapaswa kuzungumza naye na kumwambia kile unachofikiri."

Alissa alikubali kwa kichwa, kisha Nora akachukua chupa ya mvinyo na kumwambia, "Njoo, tulewe."

"Lakini nitafadhaika zaidi baada ya kuamka." Ingawa alisema hivyo, alikunywa pamoja na Nora.

Siku iliyofuata ilimbidi Alissa aende kazini, hivyo alikusudia kurudi nyumbani baada ya kuangalia muda.

Nora aliondoka pamoja naye. Waliposhuka wakakutana na Jayden ambaye alikuwa ana nia ya kupanda ghorofani.

"Mnafanya nini?" Jayden aliwatazama na kuwauliza huku akiwa na chupa ya mvinyo mkononi mwake.

"Lazima nirudi nyumbani kwa sababu lazima niende kazini kesho." Alissa alivuta mnyororo wa chuma wa mkoba wake kisha akakusudia kuondoka.

Nora alimfuata. Alissa angerudi nyumbani kwake usiku huo, kwa hiyo arudi nyumbani pamoja naye.

"Hakuna mtu anayebaki pamoja nami ikiwa mtaondoka." Jayden akawaona wanaondoka.

Alimaliza kunywa mvinyo mkononi mwake, kisha akaweka chupa chini. Hatimaye, alihisi kuchoka, hivyo ikambidi aondoke.

Jayden akawafuata na kutoka nje ya baa. Kulikuwa na sehemu ya maegesho mbele ya mlango wa baa hiyo. Walipoelekea kwenye gari la Jayden, wakamuona mtu mmoja akitapika kwa kuinama huku akiwa ameshikilia gari lake kwa mkono mmoja.

“Seidrick?” Ingawa kulikuwa na giza, Nora alimtambua mara ya kwanza. Na kisha akamwambia kwa kejeli, “Bw. Seidrick kwanini usikae na mkeo nyumbani na ukaja kulewa huku?”

Seidrick aliposikia sauti yake, alijifuta mdomo kwa mikono yake kisha akasimama na kuwageukia.
Alimtazama Alissa na kukuta anaonekana kutojali wala kumjali hata kidogo.

Seidrick alikunja uso na alionekana kuwa mgumu machoni pake, lakini aligeuka nyuma na kuondoka bila kusema chochote.

Ingawa alikuwa amelewa na hakuweza kutembea kwa kasi, alijaribu kila awezalo kuondoka.

“Ulimlewesha hivyo?” Nora alimtazama Jayden na kumuuliza, “Alikunywa mvinyo kiasi gani?”

“Nilimsaidia tu kwa sababu alitaka kulewa. Sikumbuki alikunywa mvinyo kiasi gani.” Jayden hakumtaka anywe pombe nyingi. Badala yake, Seidrick ilimtaka anywe kila wakati.

“Twende zetu.” Alissa akageuka nyuma.

Walipoingia kwenye gari, dereva aliliondoa gari kutoka kwenye baa.

Seidrick aliingia kwenye gari lake na kuwatazama wakiondoka. Aligusa paji la uso kwa sababu alikuwa na maumivu ya kichwa. Na kisha akamwambia dereva wake, "Twende nyumbani."

Na kisha dereva akamkimbiza nyumbani. Njiani kuelekea nyumbani, Seidrick haikusema chochote. Alijiegemeza tu nyuma ya siti na kufumba macho ili apumzike. Ilionekana kuwa alilala.

Walipofika kwenye mlango wa kuingilia nyumbani kwake, aliamshwa kwa sababu dereva alisimamisha gari ghafla.
Alijitegemeza kwa kushika nyuma ya kiti na kuuliza, “Ni nini kimetokea?”

"Bwana. Seidrick, samahani sana. Kuna mtu alitoka ghafla kisha akasimama mbele ya gari.” Dereva aliogopa kidogo, "Nitashuka kwenye gari ili kuangalia ni nani."

Dereva alijifuta jasho kwenye paji la uso kisha akafungua mlango na kutoka nje ya gari. Kwa mwanga hafifu, aligundua kuwa alikuwa Melissa.

Alisimama mbele ya gari na kusimamisha gari kwa mikono yake.

Akiwa na nguo zilizochafuka, zilizokunjamana na uso uliopauka, alionekana mnyonge sana, bila mwanga wowote katika macho yake mazuri kama hapo awali. Ilikuwa ni siku moja tu, hakuwa tena Bi Seidrick mtamu na mrembo.

"Bwana…. Bi Maziku, unafanya nini hapa? Ni hatari sana.” Driver karibu amwite Bw. Seidrick kwa sababu alikuwa na hofu, "Ikiwa utajeruhiwa, nitalaumiwa na familia ya Maziku."

Dereva aliogopa. Hakutarajia kwamba angetoka ghafla na kutaka kusimamisha gari. Ikiwa hangesimamisha gari haraka iwezekanavyo, angejeruhiwa.

Melissa hakumjibu dereva. Alifika karibu na gari na kupapasa dirishani na kusema, “Seidrick, najua umeketi kwenye gari sasa hivi. Unaweza kuzungumza nami?”

Seidrick alihisi mbaya zaidi na maumivu ya kichwa aliposikia sauti yake.

"Parry, mpeleke nyumbani." Ikabidi Seidrick amuombe dereva nirudishe nyumbani.

Sura ya 232

Dereva akajibu ndio kisha akakusudia kupanda gari. Hata hivyo, Melissa alisimama mbele ya gari tena na kusema, “Ikiwa hutazungumza nami, sitakuacha uende, isipokuwa uendeshe gari hilo na kunishinda.”

Dereva alimtazama Melissa na asithubutu kuendesha gari. Ilibidi aombe msaada wa Seidrick, “Bw. Seidrick, Bi Maziku haondoki… Tufanye nini?”

Seidrick alihema na kumchukia sana Melissa.

Alijipapasa paji la uso wake kwa mikono yake na kukaa kimya kwa muda. Na kisha akafungua mlango na kutoka nje ya gari huku akiongea na dereva, "Nitarudi nyumbani peke yangu."

Melissa alifikiri kwamba Seidrick aliahidi kuzungumza naye alipomwona akishuka kwenye gari.

Hata hivyo, Seidrick alitembea moja kwa moja hadi kwenye geti la nyumba hiyo lakini hakumtilia maanani hata kidogo.

Seidrick alijaribu kila awezalo kutembea kwa utulivu, ili Melissa asimuone kuwa alikuwa dhaifu.

Melissa aliuma mdomo na kumfuata. Alimshika mkono kwa mkono na kusema, "Seidrick ..."

Seidrick alimsukuma mbali kwa kuchukizwa na kusema, “Usinishike! Nadhani wewe ni mchafu sana na unanifanya niwe mgonjwa.”

"Seidrick, unajua nini? Unanifanya nijisikie vibaya. Nililazimishwa na Timothy kufanya naye mapenzi kwa sababu ya Alissa. Aliweka mvinyo wangu dawa na kisha Timothy akanibaka! Yote ni kwa sababu yake! Mimi ni mke wako. Unapaswa kulipiza kisasi kwa ajili yangu kwa sababu aliniumiza hivyo.” Melissa akamwambia.

"Melissa, ni kosa lako mwenyewe. Kwa nini unaweza kukwepa wajibu wako mwenyewe? Usidhani huna hatia.” Seidrick alimtazama usoni na kusema, “Kama nisingejua ukweli, ungenidanganya milele. Kwa nini unanidanganya kila wakati?”

"Miaka mitano iliyopita, tulitoa kadi ya benki iliyokuwa na milioni mbili ndani kwa mfadhili wangu, na hakuna mtu aliyetoa pesa hizo katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Hata hivyo, fedha hizo zilitolewa muda si mrefu uliopita. Kwa nini? Melissa, niambie mtoaji ni nani?"

"Mfadhili ana haki ya kutoa pesa muda wowote anaotaka. Si jambo langu. Huwezi kunishuku kwa hilo.” Melissa alikataa kukiri alichofanya.
Kwa sababu alikuwa ametoa milioni moja na kumpa Timothy. Alihitaji pesa, kwa hivyo ilimbidi atoe pesa kutoka kwa
kadi ya benki.”

"Unanidanganya kila wakati, kwa hivyo sitaki kuongea na wewe tena." Seidrick alisema, “Usije hapa tena. Sitaki kukuona. Ondoka kwangu.”

“Seidrick, mimi ni mke wako, hivyo nina haki ya kukaa na familia ya Masolwa. Huwezi kuniambia nitoke nje.” Melissa hakutaka kuondoka.

"Ikiwa utaendelea kufanya hivi, nitakutumia hati ya makubaliano ya talaka kesho." Seidrick awali alitaka kumpa talaka baada ya mtoto kuzaliwa. Lakini, hakuweza kumvumilia tena kwa sababu alikuwa kama tapeli.

“Sitatia saini hati. Isitoshe, nina mimba sasa, hivyo huwezi kunitaliki.” Melissa hakuwa na aibu kweli, “Baada ya kumzaa mtoto, nitapata kipindi cha kunyonyesha. Na huwezi kunitaliki katika kipindi hicho. Seidrick, kwa nini unasisitiza talaka?

“Najua nilipaswa kujaribu kumuondoa Timothy kwa njia yoyote ile. Ilikuwa ni kosa langu. Unaweza kunisamehe?”

"Hapana!" Seidrick akajibu kwa uthabiti na bila kujali.
Ikiwa angeweza kumsamehe kirahisi hivyo, kwa nini hakumsamehe Alissa hapo awali?

Seidrick alifungua mlango mdogo wa upande wa kushoto wa geti wenye michoro ya kuchonga na kuingia ndani ya nyumba hiyo. Melissa alitaka kumfuata, lakini alizuiwa na wanaume wawili waliokuwa wamesimama getini.

“Ondoka kwangu! Mimi ni Bi Seidrick. Hunijui mimi ni nani?” Melissa akawaambia kwa kiburi.

Wale watu wawili hawakumjibu kisha wakafunga mlango.

Wakati huo huo, dereva aliendesha gari ndani ya familia ya Masolwa. Melissa alitaka kuingia ndani ya nyumba kupitia lango, lakini alishindwa. Hakuweza kulizuia lango lisifungwe, kwa hiyo aliweza tu kusimama pale nje.

Melissa aligonga lango na kupiga kelele kwa Seidrick, "Seidrick, ilikuwa kosa langu. Sijala chochote kwa siku nzima. Je, unaweza kuniruhusu ninywe maji na kula chakula cha jioni? Ijapokuwa hunijali, unapaswa kumjali mtoto wetu. Seidrick…”

Melissa alijifanya maskini na kumsihi. Lakini Seidrick hakumjibu.

“Seidrick…” Melissa alihisi kutokuwa na tumaini na alikuwa na huzuni sana hivi kwamba alitaka kulia.

Aliegemea geti kisha akapiga magoti. Alilia kwa machozi.

Lakini, hakutaka kuondoka, kwa sababu alitaka kupata huruma kutoka kwa Seidrick.

Baada ya dakika kumi, mtu mmoja alifungua geti na kuweka mfuko kando yake.

Aliuliza, "Ni nini?"

"Bi Maziku, kuna vyakula na vinywaji kwenye mfuko." Yule mtu alisema.

"Je! Seidrick amekutuma unipe?" Melissa alifurahi kidogo. Je, alisikia alichosema sasa hivi?

"Hapana." Mwanaume huyo alikana.

Seidrick alimwomba asimwambie ukweli, vinginevyo, angefikiri kwamba bado anampenda.

“Hapana, unadanganya. Ni lazima ni yeye. Najua ananijali. Ananikasirikia tu na hajui jinsi ya kujishawishi
mwenyewe kunisamehe sasa hivi.” Melissa alimwambia mwanamume huyo huku akijigusa tumbo la chini kwa mikono yake, na ilionekana kuwa hana raha, “Tafadhali mwambie ninampenda sana.”

“Bi. Maziku, nadhani bora uiache familia ya Masolwa.” Mtu huyo aliondoka baada ya kuzungumza.

Melissa alihisi kuwa tumbo lake la chini lilimuuma sana, hivyo akasema, “Subiri…”

“Kitu kingine?” Mwanaume huyo alisimama na kumuuliza.

“Tumbo langu la chini linauma.” Melissa alihisi uchungu sana, “Nataka kumuona Seidrick. Tafadhali nisaidie."

“Bi Maziku, Bwana Seidrick hatakuona tena. Afadhali uondoke sasa. Usipoteze muda wako hapa.” Yule mtu akatikisa kichwa na kuhema.

Melissa alianguka chini kabla hajamaliza kuzungumza.

Na kisha mtu huyo aliona kwamba Melissa amelala chini wakati aligeuka nyuma. Alishtuka na kumkaribia kwa haraka, “Bi.
Maziku, kuna nini?”

Melissa hakumjibu. Akamwambia tena, “Bi. Maziku, hata ukijifanya umekufa, Bwana Seidrick hatakuona tena. Afadhali uache kufanya hivyo.”

Chini ya mwanga hafifu, aliona kwamba uso wake ulikuwa umepauka na kulikuwa na jasho kwenye paji la uso wake…

Alimsukuma mabega yake kidogo na kugundua kuwa kweli alianguka kwa kuzirai.

Ikiwa kweli angekufa mbele ya nyumba ya familia ya Masolwa, wangekuwa na shida.
Kwa hiyo akamwita Seidrick haraka, “Bw. Seidrick, Bi Maziku alianguka na kuzirai. Nifanye nini?"

“Pigia simu namba 120 kisha umpeleke hospitalini,” Seidrick alikuwa mtulivu na akasema, “kisha uwajulishe familia ya Maziku.”

Sura ya 233

Haraka akapiga simu 120. Punde, ambulensi ilifika pale na wahudumu wa afya wakamshikilia ili aingie kwenye gari la wagonjwa.

“Ana tatizo gani?” Nesi aliuliza.

"Alianguka ghafla na kuzirai sasa hivi." Yule mtu alisema.

“Wewe ni familia yake?”

“Hapana, mimi si. Lakini nitawapigia simu familia yake mara moja na kuwaomba waende hospitali.” Yule mtu akasema tena.

“Basi utufuate twende hospitali kwanza. Kisha unaweza kuondoka baada ya familia yake kufika hospitalini.”

Basi yule mtu akapanda gari la wagonjwa na kwenda naye hospitali. Alijiandikisha kwa malipo kisha akasubiri nje ya chumba cha dharura.

Baada ya muda, washiriki wa familia ya Maziku walifika hospitalini, akiwemo Alex na Marry.

"Bwana. na Bi Maziku, sasa mko hapa, nitaondoka wakati huo.” Mwanamume huyo akawakabidhi bili.

Marry alichukua bili na kuuliza, "Je, Seidrick anajua kuwa Melissa yuko hospitalini sasa?"

"Bwana Seidrick aliniomba niwataarifu baada ya kumpeleka Bi Maziku hospitalini.” Yule mtu akawaambia kisha akaondoka.

Alex alikunja uso kisha akaketi kwenye kiti nje ya chumba cha dharura, "Inaonekana Seidrick ameamua kumruhusu atoke nje ya familia ya Masolwa."

"Tunapaswa kufanya nini?" Marry pia alikuwa na wasiwasi.

“Sijui pia. Kwa kweli alinitia aibu. Anastahili.” Alex pia alikatishwa tamaa na Melissa, "Tulikuwa na matumaini kwa sababu alikuwa mjamzito. Hata hivyo, mtoto huyu hawezi kuwa wa familia ya Masolwa.

“Kwa kuwa hana haya, sidhani kama familia ya Masolwa itamlea mtoto. Ni bora kwake ikiwa anaweza kuishi."

Marry akauliza, “Unamaanisha nini?”

“Hatuwezi kumsaidia. Anapaswa kuishi peke yake.” Alex alisema.

Ikiwa mtoto huyu ni wa familia ya Masolwa? Marry alitumaini hivyo.

"Ikiwa mtoto huyu ni wa familia ya Masolwa, hatuhitaji kufanya chochote, kwa sababu familia ya Masolwa itamlea mtoto." Alex akamwambia, "Na hauitaji kumjali katika siku zijazo."

Walipokuwa wakiongea, daktari alifungua mlango kisha akaingia, Alex na Marry wakasonga mbele na kumuuliza daktari, “Binti yangu ana tatizo gani?

“Amekuwa mjamzito kwa karibu miezi mitatu, lakini ni dhaifu sana na ana utapiamlo kutokana na upungufu wa damu na hypoglycemia, na anakabiliwa na hatari ya kutoa mimba. Kama mwanamke mjamzito, kwa nini anaweza kuwa mahali mbaya hivi? Mnamtunzaje kama wazazi wake? Kwa nini mume wake hajali sana mke wake na mtoto wake?” Daktari aliwalaumu, “Kama hamkuwa tayari, msingemruhush kupata mimba kirahisi!”

“Ndiyo upo sahihi. Ni kosa letu.” Marry aliendelea kuitikia kwa kichwa, “Tutamtunza vizuri baadaye.”

"Lazima akae hospitalini kwa siku mbili kwa uchunguzi. Na anahitaji lishe zaidi baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini.” Na kisha daktari akaondoka.

Melissa alihamishiwa kwenye chumba cha faragha. Marry na Alex walimfuata.

Marry alijihisi mgumu alipoona uso wake umepauka.
Alikuwa amejishawishi kutomjali, lakini hakuweza kufanya hivyo.

"Amekuwa bora zaidi. Tunaweza kuajiri mfanyakazi wa uuguzi kumtunza. Turudi nyumbani.” Alex alikagua saa na kugundua kuwa tayari ilikuwa 00:00, "Lazima tuende kazini kesho."

Marry alilipa ada zote kisha akaondoka pamoja na Alex.

Siku iliyofuata, Melissa aligundua kuwa alikuwa hospitalini baada ya kuamka.

Melissa akanyanyua shuka na kuinuka. Hata hivyo, alikuwa dhaifu sana hivi kwamba alipiga magoti.

Yule mfanyakazi wa uuguzi aliona kwamba alipiga magoti alipofungua mlango, kwa hiyo akamsaidia kuinuka haraka na kusema, “Bi Maziku, hata ufanye nini, unaweza kuniomba msaada.”

"Wewe ni nani?" Alishika kitanda ili asimame.

"Mimi ni mfanyakazi wa uuguzi aliyeajiriwa na Bi. Maziku." Mama huyo wa makamo alimsaidia kumrudisha kitandani kisha akampa mto auegemee ili ajisikie vizuri.

“Nataka kumuona mama yangu.” Melissa alisema.

Wakati huu, Marry alifungua mlango na kuingia ndani akiwa na hotpot mikononi mwake kisha akakaa kitandani na kusema, “Nilimwomba mpishi akupikie supu ya kuku. Unapaswa kunywa supu zaidi baadaye."

"Bi. Maziku, ngoja nikusaidie.” Mfanyikazi wa uuguzi alichukua hotpot.

"Mama, nakumbuka kwamba nilikuwa nikimngojea Seidrick mbele ya nyumba yao. Nani alinileta hospitali jana usiku? Alikuwa Seidrick?" Melissa alimtazama Marry kwa matarajio.

"Mtumishi wa familia ya Masolwa alifanya hivyo." Marry akamjibu.

Melissa alikasirika na mikono yake ikashikilia kitako kwa nguvu, “Kwa nini hakunitembelea? Kwani hajui kuwa nilikuwa hospitalini? Kwa nini yeye ni mkatili sana?”

"Daktari alisema unahitaji kupumzika vizuri. Usifikirie juu yake.” Marry alimuona yule mfanyakazi wa uuguzi akimwendea akiwa na bakuli la supu ya kuku mikononi mwake, hivyo akachukua bakuli na kumlisha Melissa.

Melissa alikataa kunywa supu ya kuku.
Marry akaweka bakuli chini ya meza kisha akasema, “Daktari alisema uliugua kutokana na lishe mbovu na kuhatarisha kutoa mimba. Kwa kuwa Seidrick hataki kuwa na wewe tena, unaweza kumtoa mtoto huyu kwa kula au kunywa chochote, ili mtoto huyu asije kuwa mzigo wako siku za usoni.”

Melissa alimgeukia na kusema huku akitokwa na machozi, “Mama, huyu mtoto ni wa Seidrick na mimi, sitakata tamaa. Ni lazima nimzalie mtoto huyu na kumwomba mtoto amwite Seidrick kama baba."

“Bado unataka kuwa naye?” Marry alimuona mkaidi sana, “Melissa hata ukizaa huyu mtoto na Seidrick akawa ndio baba mzazi wa mtoto, hawatakukubali tena. Wewe sio muhimu kwao hata kidogo. Unapaswa kutambua hilo...

“Wewe bado kijana. Ikiwa huna mtoto, unaweza kuolewa na mwanamume ambaye ni bora kuliko Seidrick. Na kisha unaweza kuishi kwa furaha zaidi. Kwa nini unajitesa namna hii? Usifanye hivyo tena!”

"Mama, nampenda Seidrick tu." Melissa alisema huku akitokwa na machozi, “Siwezi kuishi bila yeye. Ninahisi kama ninakaribia kufa sasa.”

"Lakini yeye anaishi vizuri bila wewe. Unaweza kuwa na nguvu?" Marry alikasirika, "Yeye hakupendi tena."

"Hapana, ananikasirikia tu." Melissa alibishana naye huku akitokwa na machozi, "Itakuwa sawa ikiwa hana hasira."

"Kweli, nadhani unapaswa kufikiria mara mbili." Marry alikasirika sana asiweze kuongea naye tena.

Melissa alilia.

Alichukua simu yake kisha akampigia Seidrick. Lakini hakujibu…

Aliendelea kumpigia simu lakini hakupokea hata kidogo. Hatimaye akaitupa simu yake kisha akalia kwa sauti.

Alipohisi uchovu wa kulia, akanywa supu ya kuku kisha akataka kuondoka hospitalini.

Mfanyakazi wa uuguzi alimsimamisha, “Bi. Maziku, wewe ni dhaifu sasa. Huwezi kwenda nje.”

"Niache peke yangu." Na kisha Melissa akaondoka hospitalini.

Alichukua teksi hadi kwenye ofisi za Tanganyika Ferries, lakini alisimamishwa kwenye ukumbi kwenye ghorofa ya kwanza.

“Mimi ni Bi Masolwa. Nataka kumuona mume wangu. Kwa nini mnaweza kunizuia?”

"Bwana Masolwa ametuomba tukuzuie, kwa sababu hataki kukuona.”

Sura ya 234

Melissa aliona aibu, “Najua yuko bize, kwa hiyo hana muda wa kuniona. Lakini lazima nipande ghorofani kumuona. Niache niende!”

“Bi. Maziku, tafadhali usituingize kwenye matatizo. Ni kazi yetu.” Yule mlinzi na yule msichana anayefanya kazi pale mapokezi walimshawishi.

Wale watu waliokusanyika karibu walikuwa wakizungumza juu yake.

“Sasa mmejiingiza kwenye matatizo, kwa sababu huniruhusu kwenda ghorofani kumuona mume wangu.” Melissa alibishana nao.

“Bi. Maziku, tafadhali ondoka sasa. Vinginevyo, tutalazimika kukulazimisha kuondoka." Usalama walisema.

"Sitaondoka ikiwa siwezi kumuona Seidrick leo." Melissa aliendelea kulazimisha kumuona Seidrick, "Ninataka pia kuona jinsi mtakavyonilazimisha kuondoka."

"Basi ningependa kukuomba msamaha kwanza." Na kisha kiongozi wa usalama aliuliza washiriki wawili wa timu yake kuwa karibu na Melissa.

Melissa hakusogea na akasema kwa umakini, "Ikiwa utathubutu kunigusa, nitakushtaki kwa shambulio la aibu."

Kwa wakati huu, mtu mmoja aliingia kwenye kampuni na kusema, "Tafadhali niruhusu niingie."

Wale watu walitazama huku na kule wakaondoka kisha wakawaruhusu kuingia ndani. Na hapo kulikuwa na watu wachache wakiingia ndani ya kampuni hiyo, akiwemo Alissa.

Kampuni ya Tanganyika Ferries ilitaka kuagiza vipuri vya vivuko vyao vya majini je ya nchi, na safari hii waliamua kutumia kampuni ya Universal Machines Group. Alissa na wenzake walifika hapo kuwasilisha zabuni yao kwa mabosi wa kampuni hiyo.

Melissa alipomuona Alissa, alikasirika zaidi.

Alissa alishangaa kidogo alipomuona Melissa hapa. Lakini alitulia tena kwa haraka, kisha akaiendea lifti kana kwamba hajamwona Melissa.

"Bi Maziku, kwa njia hii, tafadhali." Wafanyakazi walikuwa na adabu.

Alipoona wafanyakazi hao walikuwa wakimstahi sana Alissa na hata kumuonyesha njia, Melissa alikasirika sana.
Hata alitetemeka.

"Alissa, simama!" Melissa akapiga kelele.

Hata hivyo, Alissa alitembea moja kwa moja hadi kwenye lifti kana kwamba hajamsikia.

“Alissa, huna aibu sana? Mimi ni Bi Masolwa, si wewe. Unathubutuje kuja hapa kumtongoza mume wangu?” Alissa alimkashifu Alissa alipompuuza.

Melissa aliposema hivyo, watu waliokuwa wakitazama huku na huku walianza kujadiliana tena. Na wote wakamtazama Alissa.

Alissa alihisi msongo wa mawazo chini ya macho ya watu wengi sana, lakini hakuwa na hofu hata kidogo.

"Melissa, una ushahidi wowote kuthibitisha kwamba nilimtongoza Seidrick?" Alissa alisimama na kusema bila kujali, “Kama huna ushahidi, usinisingizie hapa. Vinginevyo, ninaweza kukushtaki kwa kashfa."

"Ushahidi ni kwamba unathubutu kuja kwa ofisi ya mume wangu leo." Melissa alidhihaki, “Kama mke wake, sikuweza kuingia kwenye kampuni na sikuweza kumuona. Kwa nini wewe unaweza kuingia kwenye kampuni kumuona?”

Mfanyakazi alifafanua, “Bi. Maziku, Miss Alissa yupo hapa kikazi, na anakuja kwa kampuni yetu kwa mambo ya kiofisi. Natumai unaweza kuacha kumkashifu Miss Alissa. Na wewe unakuja hapa kwa mambo ya kibinafsi, kwa hiyo bwana Seidrick hana muda wa kukuona kwa sababu yuko bize na kazi sasa. Natumai unaweza kutulia na usilete shida hapa. Tafadhali ondoka sasa hivi.”

“Hivi kweli anakuja hapa kufanya kazi? Kama tunavyojua, alikuwa mchumba wake hapo awali. Sasa anataka tu kufanya naye mapenzi kwa jina la kazi. Unafikiri sisi ni wajinga?" Melissa alisema huku akitokwa na machozi. Alijifanya dhaifu ili apate huruma kutoka kwa wengine.

“Bi. Maziku, tafadhali acha kuongea hivyo.” Wafanyakazi hawakuridhika.

“Kwa nini? Ninajisaidia tu kupigana na adui yangu, kwa sababu sitaki mtoto wangu asiwe na baba siku zijazo. Kwa hivyo nadhani sina makosa.” Melissa alisema huku machozi yakimtoka, na kweli alionekana maskini namna hii. Aliendelea, "Anakataa kuniona na mtoto wetu kwa sababu unamtongoza."

"Nadhani wewe ni mjinga." Alissa alifikiri kwamba itakuwa sawa ikiwa angempuuza sasa hivi. Bila kutarajia, Melissa alimkashifu hivi. Lazima alikuwa kichaa.

Alissa alipotaka kuondoka, ghafla Melissa alipiga magoti chini huku akilia kwa machozi.

“Alissa, naomba usinidhuru tena. Mimi na mtoto wangu hatuwezi kuishi bila Seidrick. Najua hunipendi, lakini naomba ufikirie hilo mara mbili kwa ajili ya mtoto wangu. Yeye ni mpwa wako. Alissa, tafadhali mwache…” Melissa alimsihi huku akilia, na hata akainama chini kwa Alissa.

Alimsujudia Alissa kwenye vigae vya sakafu ngumu na baridi, na kila mtu karibu nao alishtuka.

Watu daima waliwahurumia wanyonge, kwa hiyo wote walimuhurumia Melissa wakati huu. Na walikuwa na mashaka zaidi juu ya Alissa ambaye walimwona kuwa mwanamke mwenye tamaa.

Wote wakamkazia macho Alissa kana kwamba walikuwa wanajaribu kumchunguza.

“Alissa, mimi na mtoto wangu hatuwezi kuishi bila Seidrick…” Melissa aliendelea kulia. Alionekana mnyonge sana, jambo lililowafanya watu waliokuwa karibu kutetea haki kwa ajili yake.

Lily na Jamila, ambao walikuwa wameambatana na Alissa Kwenye kampuni hiyo kuwasilisha zabuni ya vipuri vya vivuko, walimmkemea Alissa,

“Alissa, unawezaje kuwa mkatili hivyo? Unawezaje kujaribu kuumiza mtoto? Una wazimu?”

"Kama msemo unavyoenda, uzuri ni kama vitafunio."

"Alissa, najua kwanini Bw. Seidrick ameamua kuagiza vipuri vya Ferry kupitia Universal Group sasa..."

Alissa aliwatazama wenzake alioambatana nao, hasa Lily na Neema na kusema, “Mnawajibika kwa uwajibikaji wa kisheria ukinitusi bila ushahidi. Sijawahi kufanya, kwa hivyo sitawajibika. Nina haki ya kuendelea na uchunguzi wa kisheria kwa kashfa ya Melissa na nyie leo. Ni hayo tu. Tafadhali fikirieni hilo mara mbili.”

Alissa hakugombana nao tena, bali alitembea kuelekea kwenye lifti.

Tayari walikuwa wameingia kwenye fujo. Alissa hakutaka kuwatilia maanani tena. Na hakukasirika kwa sababu ya kashfa zao. Badala yake, angefanya vizuri zaidi katika kazi yake.

Sam na Seidrick walikuwa wakaguzi wakuu wa hati za zabuni, na Alissa angemaliza kazi yake vyema.

Alissa alikuwa wa mwisho kueleza hati yake ya zabuni. Alipomaliza na kutoka, Ruben, msaidizi wa ofisi wa Seidrick, akasogea mbele na kumwambia, “Bi Maziku, Bwana Seidrick anakualika kuzungumza naye ofisini kwake.”

"Ruben, sidhani kama ninapaswa kuzungumza naye kwa sasa." Alissa alimkataa.

“Bi Maziku, sitakulazimisha. Na ningependa kukuomba msamaha kwa jina la Mr. Seidrick kwa kashfa kutoka kwa Melissa." Ruben alimwomba msamaha kwa upole.

“Basi tafadhali mwambie Bwana Seidrick amsimamie mke wake mwenyewe. La sivyo, ninaogopa kwamba atafanya hivyo tena.” Na kisha Alissa akageuka nyuma na kuondoka.

Miaka mitano iliyopita, aliamua kumwacha alipofanya chaguo lake mwenyewe, na hakutaka kukubali msamaha wake.

Sura ya 235

Ruben akaachana na Alissa kisha akageukia ofisi ya Seidrick.

Seidrick alisimama tuli mbele ya dirisha, mikono yake ikiwa kwenye mifuko yake.

"Alikataa?" Seidrick hakutazama nyuma na alijua kwamba Ruben alikuja peke yake.

"Bwana Masolwa, nilishindwa kumbakiza Miss Maziku." Ruben alisimama mbele ya ofisi kubwa, akiinamisha kichwa chini kwa aibu.

“Haina uhusiano wowote na wewe. Nilijua hatakuja kuniona. Nilitaka tu kujaribu."

Seidrick alikuwa tayari kwa matokeo, lakini bado alihisi kukata tamaa kidogo.

"Vipi kesi ya Alissa kuzaa mtoto miaka mitano iliyopita?" Seidrick akageuka na kuuliza.

Alikuwa na shauku kubwa ya kujua kilichotokea miaka mitano iliyopita. Je, ni sababu gani iliyomfanya Alissa, ambaye alikuwa akimpenda sana wakati huo, ajifungue mtoto ghafla?

Kwa mtazamo wa tabia na mapenzi ya Alissa kwake, asingefanya vile.
Lazima kuna sababu. Huenda alikumbana na matatizo fulani au mtu fulani alimlazimisha kufanya hivyo.

Alishtuka sana na kushtushwa na Alissa ambaye alikuwa amemshika mtoto mikononi mwake hata hakuwa na muda wa kufikiria, na kusema bila kufikiri na kufanya mambo ya kikatili. Sasa alijuta kwamba hakusikiliza maelezo yake.

"Nilithibitisha tu kwamba Miss Linder alitoweka kwa zaidi ya mwaka mmoja kabla ya mtoto wake kuzaliwa. Kuhusu alichokifanya, alipataje mimba au baba wa mtoto ni nani bado haijulikani.” Ruben alizika kichwa chake chini. Alijiona hana nguvu. Hakuweza kupata chochote.

“Zaidi ya mwaka…” Seidrick alikunja uso. Hiyo ilimaanisha kuwa alikuwa amepanga kuzaa mtoto huyu, "Je, alikuwa karibu na mwanamume yeyote wakati huo?"

"Kabla ya Bi Maziku kutoweka, hakuwa karibu na mtu yeyote isipokuwa wewe." Ruben akanyamaza, kisha akaendelea, “Bw. Masolwa, kuna jambo moja ambalo sijui kama niseme.”

"Endelea." Seidrick aliketi kwenye kiti cha kuzunguka na kumtazama.

"Inawezekana kuwa mtoto wa Bi Maziku ni wako?" Ruben alidhani inawezekana.

Macho ya Seidrick yalitiwa giza mara moja. Ruben alikanusha haraka, “Bw. Masolwa, samahani, ninakisia tu.”

"Ni sawa." Seidrick alirudisha macho yake na kutikisa kichwa, "Ninatumai kuwa mtoto si wangu."

Yeye na Alissa walikuwa vijana walipokuwa pamoja, na alimheshimu. Alissa alikuwa msichana mzuri na mapenzi yao yalikuwa mepesi sana.
Muda wote wangetazamana, wangehisi dunia ni tamu.

Walikuwa wameshikana tu mikono na kumbusu, na hawakufanya chochote nje ya mstari, hivyo mtoto hakuweza kuwa wake.
Ruben aliona Seidrick akionekana kufadhaika.

“Endelea na suala hilo. Lazima nijue ukweli.” Seidrick aliamua kwamba bila kujali ukweli ni upi, lazima ajue ni nini kilikuwa kimetokea, ili tu kuweka sawa mawazo yake.

Ruben aliitikia kwa kichwa kisha akasema, “Bw. Masolwa, Alichokifanya Miss Melissa kwenye ukumbi leo kimechapishwa kwenye Mtandao na kusambazwa mtandaoni.
Itaathiri sifa ya Kampuni, wala haipendezi kwako na Miss Alissa. Uvumi unadai kwamba ulimtelekeza mke na mtoto wako kwa ajili ya Miss Alissa… Miss Alissa anachukuliwa kuwa bibi na anazomewa vibaya sana kwenye mtandao.”

"Dhibiti maoni ya umma, na uandike kichwa cha habari... Iachie idara ya PR." Vidole vya Seidrick vilivuka. "Ina athari mbaya sana kwa Alissa. Usimpe shida. Tabia ya aibu ya Melissa inaweza kuwekwa hadharani inapobidi.”

"Bwana. Masolwa, huwezi kufanya hivi. Ukiweka hadharani kile Bi Melissa alikuwa amefanya, ingemuumiza, lakini itakuumiza na wewe pia. Kufikia wakati huo, wewe na familia ya Masolwa mngekuwa mzaha.”

Ruben alikuwa sahihi. Baada ya yote, Melissa na Timothy walikamatwa na polisi. Ikiwa ingewekwa wazi, Seidrick na familia ya Masolwa wangekuwa mzaha.

Hata kama hawakuthubutu kusema chochote juu juu, watu wangewasengenya nyuma ya migongo yao.
Unyonge huo haukuwa ambao wanadamu wote wangeishi nao.

"Je! una wazo bora zaidi?" Seidrick alimuuliza Ruben, “Melissa alichanganya watu kwa makusudi. Anathubutu kumkashifu Alissa kwa sababu ana uhakika kuwa sitafichua tabia yake ya kukosa aibu. Ananilazimisha niifanyie kazi hii ndoa! Lakini naweza kuvumilia hili tena na tena?

“Nisipomfundisha somo atafikiri ninamuogopa! Nataka tu ajue kuwa siogopi chochote nikiweza kumuondoa! Hata nikijigeuza mzaha!”

Ruben aliweza kuhisi azimio la Seidrick kuvunja ndoa hii. Kwa kuwa alikuwa amefuata mwongozo wa Seidrick kwa miaka mingi, aliweza kumuelewa.

"Bwana. Masolwa, nitafanya niwezavyo.” Ruben hakutaka bosi wake anayeheshimiwa awe mzaha.

"Nenda ukafanye biashara yako." Seidrick alisema.

Ruben kisha akaondoka kwenda kushughulika na Melissa.

Naye Alissa aliyehusika na tukio hilo alikuwa amelipuliwa na wanamtandao waliokuwa wakitumia maneno machafu kadri walivyoweza.

Tweet ya Alissa ilijaa maoni hasi. Katika kujibu maoni hayo, Alissa alichapisha tu chapisho ili kufafanua kuwa hajawahi kuingilia uhusiano kati ya Seidrick na Melissa, na kwamba alikuwa ameolewa na anaishi maisha ya furaha. Na kisha akazima sehemu ya maoni.

Baada ya hapo, alizingatia kazi. Lakini kila wakati kulikuwa na watu ambao walipenda kusengenya, haswa Lily na wenzake.

“Siamini Alissa angemtongoza shemeji yake. Alisema ana mume… lakini hatujawahi kumuona mume wake. Haishangazi angeendesha gari la kifahari la Range Rover. Bwana Seidrick ni mkarimu kweli kweli!”

"Ni aibu sana kwamba bado anatembea kwa urefu wakati yeye ni hawara."

"Lazima tuvue kinyago chake na kila mtu aone sura yake halisi!"

Lakini hivi karibuni, mwenendo ulikuwa umebadilika kabisa kwenye mtandao. Mtu fulani alikuwa amefichua mambo ya Melissa na Timothy.

Mbali na hilo, kulikuwa na rekodi za polisi, video na picha zinazoonyesha kuwa Melissa na Timothy walinaswa katika Hoteli ya Luck. Ni habari hii pekee ingeweza kuondoa shaka ya Alissa na ikathibitisha kuwa Melissa alikuwa mwongo.

Alichokifanya Melissa kilimrudisha nyuma. Wanamtandao walikasirika kwa kutumiwa na Melissa kumshambulia Alissa, na walipoona ushahidi ndipo waliamka, jambo ambalo liliamsha kumkemea kwao Melissa. Walimwomba Alissa msamaha kwa kumkosea Alissa, kisha wakamzomea Melissa kuwa ni muongo na mwanamke asiye na haya!

Alikuwa mcheshi! Hakuwa na haya kama nini! Melissa alichukua nafasi ya Alissa ili kuzomewa na wanamtandao, jambo ambalo lilifanya watu wengi wamjue!

Wakiwa hospitalini Melissa aliona mpango wake umeshindikana akazomewa, akadondosha simu yake kwa hasira!

Sura ya 236

Alissa pia hakufikiria kwamba jambo hilo lingebadilika haraka sana. Kulikuwa na ushahidi thabiti ulioonyesha kile ambacho Melissa alikuwa amefanya, na huo ungekuwa unyanyapaa wake kwa maisha yake yote. Hangeweza kuamsha huruma ya watumiaji wa mtandao tena, na hakuna mtu ambaye angemwamini.

Melissa alikuwa ameanguka kwenye shimo, na ilikuwa vigumu kwake kuinuka tena.

Lakini, habari hizo zilikuwa na ushawishi mbaya kwa Seidrick na familia ya Masolwa. Baada ya yote, mara tu kashfa ya Melissa na Timothy ilipofichuliwa, ingevutia kejeli za wengine dhidi ya Seidrick. Katika mduara wao, watu kila wakati walikuwa wakicheza na kuwaonea watu, na Seidrick anaweza kuchekwa kwa muda mrefu, lakini Alissa hakuwashambulia watu wakati walikuwa wanyonge, wala hakuonyesha huruma.

Haijalishi ni nani aliyemfichua Melissa, mtu huyo alikuwa amemuokoa Alissa, hivyo alimshukuru mtu huyo.

Alissa alimchukua Doris kutoka chekechea baada ya kazi. Baada ya misukosuko yote ya siku, Alissa alipata umaarufu.

Mbele ya sura tata za wazazi wale, alikuwa mtulivu. Hata hivyo, haikuwa kosa lake na hakuwa na chochote cha kujisikia hatia.

"Doris alichukuliwa na baba yake," mwalimu alisema wakati Alissa alipofika kumchukua Doris.

“Kweli?" Kendrick alirudi na kumchukua Doris lakini hakumpigia simu. Alissa alishangaa sana.

Alissa alimshukuru mwalimu na kuondoka shule ya chekechea. Baada ya kuingia kwenye gari, alichukua simu yake na kuona ujumbe wa Kendrick, “Nimemchukua Doris. Rudi ukitoka kazini.”

Kuangalia meseji, Alissa alimkumbuka yule mtu mrefu na mzuri. Aliinamisha midomo yake na alikuwa katika hali nzuri. Na kisha akaendesha gari hadi kwenye makazi ya Lake City.

Lakini kabla ya kwenda nyumbani, alisimama kwenye duka moja la vinywaji vikali na kuchukua chupa ya divai nzuri na kwenda nayo nyumbani.

Alitaka kuzungumza vizuri na Kendrick usiku huo na kumjulisha anachofikiria.

Nora alikuwa sahihi. Kendrick asingejua mawazo yake ikiwa hangezungumza. Ikiwa alitaka kupigania furaha yake na kumpa hisia ya usalama, anapaswa kuzungumza.

Kurudi kwa makazi ya Lake City, Alissa hakuona mwanga wowote kwenye jumba hilo nje. Alijiuliza Kendrick amerudi.

Alifungua mlango na kubadilisha viatu vyake mlangoni, akabeba mvinyo hadi sebuleni.

Hakika hapakuwa na taa sebuleni, ila mwanga ulitoka kwenye chumba cha kulia chakula.

Alielekea kwenye chumba cha kulia chakula, ambako maua na vinara vya taa viliwekwa kwenye meza ndefu. Mwangaza wa mishumaa nyeupe ulilainisha hali ya chumba.

Kutoka jikoni akatoka mtu mrefu akiwa na sahani mbili za nyama mikononi mwake na kuziweka kila mwisho wa meza.

Na kisha akachukua rundo la maua juu ya meza na kwenda hadi kwa Alissa. “Hizi ni kwa ajili yako. Unayapenda?"

"Asante." Mpango mtamu ulikuwa wa kimapenzi, aliwaza Alissa.

Yule mtu baridi alimpa mshangao tena na tena. Alihisi joto sana kwa kile alichokifanya, na alihisi macho yake yalikuwa yamepungua.

“Umeleta nini?” Kendrick aliona furushi mkononi mwake na akauliza, “Divai nyekundu?”

“Ndiyo.” Alissa aliweka divai nyekundu kwenye meza, “Niliinunua nikiwa njiani kuelekea nyumbani, na ninataka kushiriki nawe.”

"Tunafikiria sawa, lakini mimi nilikuwahi zamani." Kendrick alitazama chipa kubwa yavinyo na glasi mbili kwenye meza,

"Nitaipokea tu kama zawadi kwa ajili yangu."

“Asante.” Alissa alikubali kwa urahisi.

"Keti chini na ujaribu nyama yangu ya ng'ombe." Kendrick alimsaidia Alissa kuvuta kiti maridadi cheupe.

Alissa alikaa chini kwa upole. Ghafla alimfikiria binti yake, “Doris yuko wapi? Mwalimu alisema umemchukua mtoto.”

"Ni wakati wetu sasa. Nimemuacha Doris kwa Miss Nora. Uwe na uhakika.” Kendrick alimpa mguso wa uhakika kwenye bega lake jembamba na kumimina mvinyo kwenye kikombe kilichokuwa mbele yake.

Alitembea hadi upande wa pili wa meza, akajaza glasi yake, kisha akaketi.

Walikaa kwenye ncha tofauti za meza. Kendrick alinyanyua kombe lake na kumtazama Alissa, “Furahia. Hongera.”

“Hongera.” Alissa alichukua glasi yake, pia, na kutabasamu kwake.

Katika mwanga wa mishumaa, nuru hiyo laini ililainisha sura yake ya joto. Macho na nyusi zake zilikuwa za kupendeza, na midomo yake n
Nyekundu kama ua linalochanua taratibu.

Walimaliza glasi zao za divai nyekundu. Kendrick alisimama na kumiminia mvinyo zaidi Alissa.

Kendrick, katika shati nyeupe rahisi, alikuwa amesimama kwenye mwanga wa mishumaa, ambayo ilielezea mwili wake wenye nguvu. Mikono ilikunjwa ili kudhihirisha mikono yake yenye nguvu na rangi ya ngozi yenye afya, ikionyesha uanaume na nguvu za mwanaume. Alionekana kuvutia sana katika mkao wake mrefu.

Alissa, akiwa ameinamisha kichwa kidogo nyuma, alikuwa na rangi ya waridi iliyofifia kwenye uso wake mzuri. Alikuwa na hirizi ya kuvutia ambayo hakuijua.

Kendrick alinyoosha mkono wake kwake na kusema, "Mpenzi, tafadhali cheza nami." Alissa alitabasamu na kuweka mkono wake mkononi. Akamchukua kirahisi na kumvuta juu.

Kendrick alishika kiuno chake kwa mkono mmoja na mkono mwingine. Wakakaribiana na kuanza kucheza kwa upole. Wimbo mzuri ulitoka mahali fulani na wakakumbatiana kwa upole na mdundo wa muziki huo.

Kendrick taratibu akaweka mikono yake yote miwili kiunoni, huku Alissa akiizungusha mikono yake shingoni. Alimtazama, na katika macho yake laini, muhtasari wake ulichorwa sana moyoni mwake.

Kendrick, kana kwamba anashawishiwa na macho yake, aliinamisha kichwa chake.

Kwa upande mwingine, Alissa alifumba macho na kuhisi pumzi zikimfunika.

Busu lake lilikuwa la upole lakini la kutawala, laini lakini lenye nguvu.

Na alihisi kuwa midomo yake ilikuwa laini na tamu kuliko vile alivyotarajia. Alizionja, na kisha akaingizwa katika kumbusu.
Walibusiana sana na kwa upendo.

Baada ya muda, alimfungua na kumshika karibu na mikono yake. Alissa aliweza kuhisi nguvu zake, kana kwamba atamsugua kwenye mfupa wake.

Alijiruhusu kushikiliwa mikononi mwake, ingawa hakuweza kupumua, na akaitikia kumbatio lake kwa kuimarisha mikono yake kiunoni mwake.

"Kula nyama, la sivyo haitakuwa na ladha nzuri inapokuwa baridi." Pumzi ya Kendrick ilikuwa nzito kidogo, "Tutafurahia usiku pamoja."

Alissa akaitikia kwa kichwa, wakarudi kwenye nafasi zao na kuanza kufurahia nyama.

Kendrick alifanya kazi nzuri sana ya kuandaa steak. Ilionja vizuri kama wapishi katika migahawa maarufu.

Walitumia usiku mwororo pamoja, wakifurahia wakati wa kimapenzi.

Asubuhi iliyofuata, Kendrick aliandaa kifungua kinywa kibinafsi baada ya kutoka kukimbia asubuhi. Baada ya kuoga, alibadilisha nguo zake, akiwa amevaa shati jeupe na suti iliyonyooka na ya gharama. Siku zote alionekana mzuri wa ajabu.

Baada ya kifungua kinywa, Kendrick na Alissa walienda kufanya kazi pamoja. Wakiwa njiani akatoa hati na kumpa Alissa.

"Hii ni nini?" Alissa alimuuliza.
“Fungua tu.” Alisema Kendrick kwa utulivu.

Alissa akaipokea, akaifungua taratibu na kilichoandikwa mle ndani kilimshtua.
 
USINIACHE 5:
Sura ya 237

Alissa alipotazama “makubaliano ya Talaka”, macho yake yaliumwa, paji la uso lililegea, na pua yake ilikuwa inauma. Machozi yalimtia ukungu.

Alipumua kwa siri, akijaribu kutoruhusu kuona kwake kufifia.
Alizuia machozi yake na kuuliza, "Kwa nini unanipa hii?"

“Nataka kukupa haki yako. Ukitaka kuwa hufdrphufdrpru mmru, nitatimiza matakwa yako.” Kendrick huyu hakujali sana, tofauti kabisa na yule ambaye alikuwa mpole na mpole jana yake usiku.

Alissa aliikazia macho ile hati huku moyo wake ukimsisimka kidogo. “Nitimize matakwa yangu? Ninahitaji kutimiza matakwa gani?"

"Sitamlazimisha mtu ambaye si mali yangu kukaa nami." Kendrick alionekana kufanikiwa,” nimefanya kila nililoweza kwa ajili yako. Kuhusu talaka, unaweza kufikiria.”

"Kama ulivyosema, makubaliano ya miaka mitatu yamefikia kikomo, na una haki ya kurudisha uhuru wako. Sitakulazimisha kubaki. Kuna faida gani kukaa na mimi wakati wewe si mali yangu? Nitakupa fidia kidogo zaidi ya yale niliyokuahidi hapo mwanzo. Au nitajaribu niwezavyo kutimiza mahitaji yako kama utaendelea kuwa na mimi. Asante kwa kuwa mke wangu kwa miaka mitatu."

Hakika ya kutosha. Je, hakumwelewa, akifikiri kwamba hampendi?

"Bwana Mayala ni mkarimu sana." Alissa akatabasamu kidogo, “wewe tumesaini mkataba, umekubali kunipa milioni 200. Pesa imelipwa, na sitachukua nyingine yoyote. Pia nakushukuru kwa moyo wako.…”

Alikuwa mpole na mwenye joto sana jana usiku, lakini kwa nini alikuwa baridi sana usiku mmoja baadaye? Chakula cha jioni cha kuwasha mishumaa jana yake usiku, dansi, busu, wakati wa kimapenzi… Je, vyote vilikuwa vya uwongo?

Kwa hiyo jana usiku aliposema kwamba wangelala pamoja, alikuwa akijiandaa kwa talaka?

Ikiwa aliamua kumtaliki, kwa nini alimwacha usiku mwororo kiasi kwamba alikuwa ameshikamana naye? Haikuwa nzuri kwake, ilikuwa ni kumfanya azame katika mapenzi yake na kumfanya amchukie.

Kwanza alimpa ndoto nzuri, kisha akaivunja bila huruma!

"Tumekubaliana." Alissa akaitikia kwa kichwa.

“Vizuri.”

Alissa aliweka mbali makubaliano ya talaka. Kiburi chake na kujiona kwake kulimfanya akandamize maneno yote aliyotaka kusema na kuyaficha moyoni mwake. Sasa kwa kuwa alikuwa amefanya uamuzi huo, hakukuwa na sababu ya kuendelea kumsumbua.

Alissa hakuongea tena njia nzima, Kendrick akachungulia tu dirishani.
Kabla ya kufika kwenye tawi la kampuni ya Universal Group, Alissa alimwambia dereva, “Simama hapa, tafadhali.”

Dereva akaegesha gari. Alissa aliusukuma mlango na kutoka nje, akijaribu kujifanya aonekane mtulivu na kusema, “Kwaheri, Bw.
Mayala.”

Alisema angempenda, atamsaidia, na kuwa naye milele… Je! alikuwa amesahau alichosema?

Alissa akaufunga mlango wa gari, akajiweka sawa na kutembea taratibu kuelekea kwenye kampuni. Mgongo wake ulitoa alama ya ukaidi.

Baada ya kutoka nje ya gari, Kendrick aliendelea kumwangalia mgongoni hadi alipomkosa machoni...

Kendrick aliinua ngumi kwenye midomo yake, huku nyusi zake nene zikikunjamana.

Haya hayakuwa matokeo aliyotaka, lakini yule aliyempenda hakuwa yeye, na hakutaka kuacha ganda lisilo na moyo.

Akachagua kumuacha na kujiachia.

Lilikuwa ni jambo la mwisho aliloweza kumfanyia. Alitaka tu awe na furaha.

“Twende zetu.” Kendrick akamwambia dereva na kutazama pembeni.

Alissa hakujua hata jinsi alivyopanda ngazi au kuingia ofisini. Alikuwa kama mfu anayetembea sasa.

Alissa aliiweka ile hati kwenye dawati na kuitazama kwa muda mrefu.

Hakupata akili mpaka simu yake ilipoita, “Huyu ni Alissa…”

"Alissa, ni wewe uliyeweka hizo video na picha za Melissa na Timothy mtandaoni?" alihoji Sam.

Alissa alishangaa. “Si mimi.”

"Alissa, najua unaichukia familia ya Masolwa, Seidrick na Melissa, lakini unapaswa kukumbuka kuwa wewe ndiye ulikosea, sio Seidrick! Unataka kumharibia Melissa na kurudi kwa Seidrick, hiyo ni biashara yako. Kwa nini unapaswa kuharibu familia ya Masolwa? Kama
umewahi kumpenda sana Seidrick, usingefanya hivi! Kwa nini unapaswa kuiweka familia ya Masolwa katikati ya dhoruba na kuwafanya watu watucheke!” Sam akaruka.

"Alissa, familia ya Masolwa inateseka kwa sababu ya hii. Sifa yetu iko katika hali tete. Seidrick sio tu ya anachekwa, lakini pia anakabiliwa na hatari ya kusimamishwa na Bodi ya wanahisa kwa sababu ya athari zake binafsi kwa Kundi la kampuni, wanahisa wanatumai kwamba anaweza kusimamishwa kazi na kuchukua likizo ya kutokuwepo! Unajua maana yake?"

"Alissa, tayari umemshusha Seidrick mara moja, tafadhali usimwangamize wakati huu!"

Alissa alimsikiliza kimya kimya, kisha akasema kwa upole, “Bwana. Masolwa, ninawahurumia Masolwa Family na kampuni yenu, lakini sitaepuka kutokana na nilichofanya, na sitalaumiwa kwa jambo lolote ambalo sijafanya.”

"Ingekuwa nani kama si wewe?" Sam hakuweza kufikiria mtu yeyote ambaye alikuwa na chuki kwa familia Masolwa na Seidrick.

“Si mimi.” Tena Alissa alikanusha.

"Kwamba nirudishe maneno yangu? Pole kwa kukusumbua." Sam alikata simu.

Alissa alitazama kioo cha simu kwa muda mrefu, kisha akaiweka simu kwenye meza yake huku akiipapasa paji lake la uso.
Kwa nini kila kitu kilihusiana naye? Kwa nini maisha yake ya amani yalivurugwa kila mara na wengine?

Upande mwingine. Kendrick alikuwa amerudi ofisini. Chale alijitokeza na kuripoti, “Bw. Mayala, Bi. Mayala alitoweka kwa muda kabla ya kujifungua mtoto wake, na mwanamume zaidi ambaye alikuwa amewasiliana naye wakati huo alikuwa babake, Alex.

Kwa hivyo, baba mzazi wa mtoto ana uwezekano mkubwa wa kuwa Seidrick. Baada ya yote, yeye na Bi. Mayala walikuwa wamechumbiana wakati huo.

"Chale, usiniambie chochote ambacho huna uhakika nacho." Kendrick alipunguza hasira yake, “Na mimi nakwambia mtoto hakika si wa Seidrick. Alissa alisema hamjui baba ni nani. Nina hakika hakudanganya.”

Kendrick alimtazama juu. “Huwezi kujua alienda wapi alipotoweka? Chale, baada ya miaka mitano hujafanya maendeleo yoyote!”

"Bwana Mayala, samahani. Lakini nina ujumbe muhimu sana kwako. Ilitokea miaka mitano iliyopita, lakini nadhani hiyo ni taarifa muhimu.” Chale alitamani angeweza kujikomboa.

"Endelea." Kendrick alisema kwa ubaridi.

Sura ya 238

Yule mwanamke uliyekuwa na uhusiano wa karibu miaka mitano iliyopita alikuja kufanya kazi katika Hoteli ya Full Kipupwe mwezi Machi na kutoweka miezi mitatu baadaye baada ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wewe kwa usiku mmoja. Bi. Mayala alitoweka mwezi wa Machi pia na alionekana zaidi ya mwaka mmoja baadaye kujifungua mtoto…” Chale hakuendelea, bali alimtazama tu Kendrick.

Kendrick alitazama kwa ukali na nyusi zake zikiwa zimekunjamana.

"Walitoweka kwa wakati mmoja, na mwanamke huyo hakutokea tena baada ya kutoweka. Ningethubutu kukisia kwamba mwanamke huyu angekuwa na uhusiano wowote na Bi. Mayala?” Chale alizungumza tu kwa upole.

"Jina la mwanamke huyo lilikuwa nani miaka mitano iliyopita?" Kendrick aliuliza.

"Aliitwa Rosy Masolwa." Chale alikumbuka jina hilo vizuri sana. Ni mwanamke huyu ambaye alikuwa ameharibu maisha yake ya kipaji katika familia ya Mayala, na ambaye alimfanya Kendrick kutilia shaka uwezo wake na kumfanya ajisikie hafai.

“Rosy Masolwa…” Kendrick alilitafakari jina hilo. "Inaandikaje?"

"Ni ROSY, na TABALO." Chale akatoa bahasha nyingine na kuiweka kwenye meza ya Kendrick. "Na nilifanikiwa kupata picha ya mwanamke huyu. Ninaweza kupata nusu ya maelezo yake mafupi tu na hayana ukungu, lakini angalau inatupa fununu.”

Kendrick akaichukua ile bahasha na kuichomoa picha ambayo hakika ilipigwa kwa mwanga hafifu.
Mwanamke huyo alikuwa amejipodoa vipodozi vinene, na mtazamo wake wa sura ya mwanamke ulikuwa sawa.

"Pima picha hii uone ni nani." Kadiri alivyokuwa akimwangalia mwanamke huyo ndivyo alivyozidi kuhisi kumfahamu. Na hapo akamkumbuka yule mwanamke aliyemfanya awe mraibu miaka mitano iliyopita.

Sasa, hata hivyo, aliweza kuhisi furaha na kuridhika kwa usiku huo na Rose.

Ilimfanya ajione ni mtu mmoja, lakini mwonekano wa Rose haukuwa kama wa mwanamke huyo.

Siku zote alifikiri alikuwa amefikiria sana.

Lakini sasa alihisi sana kwamba hakukosea.

“Rosy Masolwa…” Wakati Kendrick alirudia jina hilo, alitabasamu, na kufikiria kitu. Jinsi Seidrick na Alissa walivyokuwa watamu! Hata jina la uwongo lilikuwa mchanganyiko wa majina yao.

Kendrick ghafla akahisi anadanganywa.

Macho yake yalikuwa meusi kama shimo, yakionekana kumeza kila kitu.

Ikiwa Alissa alikuwa kweli ndiye mwanamke miaka mitano iliyopita, basi Doris ... anaweza kuwa binti yake mwenyewe.

Kwa mawazo hayo, Kendrick alijawa na matarajio na hamu.

Lakini pia alikuwa na wasiwasi sana. Alijisikia vibaya sana kwa kudanganywa na kudanganywa, na alikatishwa tamaa na Alissa! Alikuwa kama mpumbavu tangu mwanzo hadi mwisho!

Alikunja ngumi, akafumba macho na kuwaza kwa muda. Na kisha akasimama. “Nina jambo muhimu sana la kufanya.
Tafadhali shughulikia masuala ya kampuni."

"Bwana Mayala, kuna mkutano muhimu leo. Huwezi kukosekana.” Chale alimkumbusha.

“Sasa nina mambo muhimu zaidi ya kufanya!” Kendrick alifikiri jibu lilikuwa mbele, na alihitaji tu kuthibitisha.

Kendrick aliondoka haraka, na kutoweka nje ya ofisi kama upepo.

"Bwana Mayala…” Chale alilalama, akitazama ofisi tupu, “hao wazee si rahisi kushughulika nao!”

Kendrick hakujali. Alitoka nje ya eneo la maegesho ya gari lake la Maserati na kuelekea shule ya chekechea ya Doris.

Akiwa baba Doris, Kendrick aliweza kuingia chekechea kiulaini na kumchukua Doris.

“Baba, mbona umekuja kunichukua mapema?” Doris aliketi kwenye gari na kumuuliza, “Je, umenimiss sana?”

"Baba yuko sawa." Kendrick aliuona uso wa furaha wa Doris kupitia kioo cha nyuma.

“Kwa hiyo tunaenda wapi?” Doris alitazama mandhari ya mtaani iliyokuwa ikipita nje.

“Baba atakupeleka mahali kwanza, na mkachunguze pamoja. Maadamu utashirikiana nami, baba atakutimizia matakwa yako yote." Kendrick akamwambia Doris.

"Nitamsikiliza baba yangu." Doris alimuamini kabisa Kendrick. "Nitafanya chochote ambacho baba anataka nifanye."

“Mtoto mzuri.” Kendrick alitabasamu.

Punde walifika katika kituo cha tathmini katika hospitali ya jiji hilo.

Kendrick alikuwa ameweka miadi kabla hawajafika, hivyo mtu akawapokea walipofika.

"Bado ni mchanga, kwa hivyo chukua sampuli mdomoni mwake." Kendrick hakutaka mtoto ateseke, hivyo kukusanya sampuli kwa njia hii ilikuwa bora kwa mtoto.

“Ndiyo.” Nesi alitabasamu kwa Doris na kusema, “Njoo pamoja nami, mtoto. Tunakwenda kupima.”

"Nataka kukaa na baba." Doris hakutaka kuachana naye.
"Sawa, tutakuwa pamoja." Kendrick alinyoosha mkono na kuzisugua nywele zake laini.

Kendrick na Doris walimaliza mkusanyo wa sampuli ya mucosa ya mdomo kwenye chumba cha sampuli.

Doris alikuwa mpole kama kondoo muda wote.

Baada ya nesi kuwajulisha kuwa wanaweza kuondoka, Doris alimshika mkono Kendrick kutoka hospitalini. Doris hakumuuliza Kendrick kwanini walifanya vipimo hata baada ya kuingia kwenye gari.

Kendrick alimtazama Doris na kutaka kumwambia, “Baby, hutaki kujua baba alikuleta hospitali kwa ajili ya vipimo gani? Kwa nini usiniulize?”

“Najua unazo sababu zako, na utanieleza unapotaka. Nakuamini." Doris alikuwa mtu mzima na mwenye mawazo sana.

Kendrick alihisi huzuni kwa kuwa alikuwa na busara, lakini pia alifurahishwa kwa sababu ya kumwamini kwa asilimia mia moja.
Kuaminiwa na binti yake mwenyewe lilikuwa jambo la kujivunia.

"Ndio, baba atakuambia kwa nini wakati ujao." Kendrick aliiomba hospitali kuongeza kasi.

Wangeweza kujua matokeo katika siku mbili au tatu.

Ikiwa matokeo ya vipimo vya babana mtoto yalithibitisha kuwa Doris alikuwa binti yake wa kibaolojia, basi mwanamke huyo miaka mitano iliyopita lazima awe Alissa! Nodi za wakati zililingana kikamilifu, na kunaweza kuwa hakuna uwezekano mwingine isipokuwa huu.

Bila shaka, Kendrick alitumaini sana kwamba Doris alikuwa binti yake mwenyewe, ambaye alikuwa na damu yake na ya familia ya Mayala. Alitaka aishi katika familia ya Mayala.

Alitaka kumpa Doris mapenzi zaidi na kufidia yote aliyopoteza miaka hii.

“Sasa niambie unataka kwenda wapi? Baba hayupo kazini leo na atakuwa nawe.” Kendrick alikuwa katika hali nzuri na akamwambia binti yake.

“Naweza kwenda mahali Baba anapofanya kazi?” Doris alimshangaa.

"Kwa nini uende mahali ambapo baba anafanya kazi?" Aliuliza Kendrick.

“Kwa sababu nataka kuona jinsi Baba alivyo kazini.” Doris alishangaa, “Lazima uwe makini, sivyo?”

"Sio serious tu." Kendrick alikuwa tofauti kabisa na alikuwa kazini. “Unajua wananiitaje?”

"Nani?"

Sura ya 239

Kendrick alikutana na macho ya Doris kwenye kioo cha nyuma.
Aligeuza midomo yake,
“Ibilisi.”

Macho ya Doris yasiyo na hatia yalijaa mshangao na mshtuko. "Hapana! Baba yangu ni mzuri na mpole. Anawezaje kuwa shetani?”

“Hufikirii kuwa mimi ni shetani kwa sababu mimi ni baba yako,” Kendrick macho yake yalikuwa laini, “lakini mimi ni mkali na hata mkatili kwa kampuni! Sio aina ya mwanaume ambaye ungependa, na baba hataki umuogope, kwa hivyo ni bora tuende mahali pengine."

"Je, baba anaogopa nitasumbua kazi yako?" Doris akatikisa kichwa kidogo. “Nitakuwa vizuri baba. Nitakaa tu kimya bila kukusumbua.”

“Unataka tu kumtazama baba akifanya kazi?” Kendrick hakufikiri angeweza kumwambia hapana.

“Ndiyo.” Doris alitikisa kichwa, macho yake makubwa yakiwa yamejaa matarajio, “Naweza?”

“Sawa basi.” Kendrick aliendesha gari hadi ofisini.

Kendrick akaegesha gari lake, akafungua mlango, akamchukua Doris na kuelekea kwenye lifti.

Walichukua lifti hadi ghorofa ya juu. Walipomuona Kendrick, wafanyakazi wote walimsalimia. Walishusha pumzi na kutothubutu kuwachukulia poa.

Japokuwa wote walikuwa wanamuogopa Kendrick, lakini pia walikuwa na shauku ya kutaka kujua yule binti mdogo aliyekuwa amemshika ni nani.

Suala la Kendrick kuoa lilikuwa linajulikana kwa wote, lakini hawakuwahi kumuona Bi Mayala, wala hawakuwahi kusikia kuwa Kendrick ana mtoto.

Kendrick alimpeleka Doris kwenye ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji. Doris alitazama kuzunguka ofisi kubwa, yenye starehe na kusema, “Baba, kampuni yako ni kubwa sana na ofisi yako ni kubwa sana, pia.”

"Hili ni jengo la kukodishwa, na ofisi mpya itakapokamilika, itakuwa nzuri zaidi."

Jengo jipya la ofisi ya Nyanza Group huko Geita lilikuwa tayari linajengwa, na Geita ingekuwa kituo muhimu zaidi cha Nyanza Gold.

"Baba ni nzuri." Doris alimsifia baba yake.

Kendrick alivua koti lake la suti, akaweka kwenye meza yake, na kuita Sekretari wake, “Masie, nipe kikombe cha kahawa na kikombe cha juisi.
Na nunua vitafunio vya watoto na matunda."

“Ndiyo, Bw. Mayala.”

Kendrick alimsogelea Doris na kuketi kwenye kochi la ngozi. “Mpenzi, niambie tu unataka kula nini. Nitakuwa na mtu tayari kwa hilo. Baba lazima afanye kazi na hawezi kucheza na wewe. Utachoka peke yako?”

“Baba maadamu nitakutazama sitakuchoka. Unaweza kunipa vitabu vya watoto. Nitasoma kwa utulivu, na sitakusumbua." Doris alisisitiza. Aliogopa kuwa Kendrick asingependa awe naye.

“Vizuri.” Kendrick alimtazama Doris kwa makini.

Uso na nyusi zake zilifanana na Alissa, lakini aliitazama pua yake na hali yake ya joto, na aliiona sawa na yeye alipokuwa mtoto.

Moyoni mwa Kendrick tayari alikuwa ameshamchukulia Doris kama binti yake wa kumzaa, na sasa alidhani kuwa Doris ni binti yake.

“Baba nenda kazini. Ni lazima ufanye kazi kwa bidii, na upate pesa za kunisaidia mimi na mama yangu.” Doris alimsihi Kendrick.

“Mama ana kazi. Huenda hataki Baba amtegemeze.” Kendrick alivuka vidole vyake.

Ingawa Alissa hakuwa na nia ya kazi ya kutosha kuacha kila kitu, hakika hakuwa mama wa nyumbani.

Alihitaji kazi. Alitaka uhuru na kujiheshimu. Alitaka kutambuliwa na kuthaminiwa kupitia juhudi na kazi yake.

“Baba, mama ana nguvu. Ameteseka sana miaka hii, na hatamwambia mtu yeyote kwamba amechoka, na ataificha tu moyoni. Kwa hiyo, yeye huwapa wengine hisia kwamba hajali chochote na yeye ni mwenye nguvu, lakini kwa kweli, yeye ni tete na laini. Natumai tu kwamba baba anaweza kujua zaidi kuhusu hisia za ndani za mama…” Doris alizungumza mengi mara kwa mara alipoona uso wa baba yake. "Je, baba huchoka ikiwa ninazungumza sana?"

"Hapana." Kendrick akagusa kichwa chake. "Hakuna kitu baba anapenda zaidi ya mtoto wake. Baba anapenda kusikia chochote mtoto anasema.”

“Baba alisema hivyo kwa sababu unaogopa Doris atakuwa na wivu? Unampenda mama zaidi, sawa?" Doris alijifanya kama anajua kila kitu.

Kendrick akatabasamu kwa upole, “Hakuna kinachoweza kukuepuka. Ikiwa mama yako ni mwerevu kama wewe, baba angekuwa mtulivu zaidi.”

"Ina maana baba hajui chochote?" Doris alikuwa mwerevu sana, “Usikasirike, baba. Mama anahitaji tu mtu wa kumsukuma. Niachie mimi hilo. Utaridhika.”

Doris alikipapasa kifua chake kidogo kwa hiari, huku akijiamini sana.

Wakati huo huo mlango ukagongwa na katibu Masie akaleta kahawa na juisi safi.

Hakuweza kujizuia kumtazama tena Doris. Alidhani Doris anaonekana mrembo.

"Asante." Doris alikuwa na adabu.

"Karibu." Masie alitabasamu kwa upole.

Chale aliingia na Masie. Alipomwona Doris, alisema, “Binti mdogo, kwa nini hukwenda shule ya chekechea leo?”

"Anko Chale, nitakuwa na Baba leo.” Doris na Chale walijuana vizuri sana.

"Hii ni nzuri, njoo hapa mara nyingi zaidi. Ninaamini kuwa na wewe hapa, kampuni lazima iwe ya kuvutia zaidi." Katika mawazo ya Chale, akiwa na Doris hapa, Kendrick angekuwa mpole zaidi.

Lakini mara tu alipomaliza kuzungumza, Kendrick alimtazama kwa baridi na kumuuliza, “Je, Chale analalamika kuhusu jambo fulani?”

"Sithubutu." Chale alimtazama Doris.

“Baba, Uncle Chale lazima awe na jambo muhimu la kukuambia.” Doris alisimama kumtetea Chale.

“Ndiyo?” Kendrick alikuwa karibu kusikia hivyo.

"Bwana Mayala, wanahisa wanataka urudi Geita na kudhibiti hali ya dharura. Unaweza kuacha mambo hapa kwa makamu mkurugenzi na waandamizi.” Chale aliwasilisha maoni ya wanahisa.

"Ninapaswa kuchukua ushauri wa wanaume hao kwa kile ninachotaka kufanya?" Kendrick alikunja uso, “Kama hawaniamini, wanifukuze kazi tu.”

Chale alitabasamu na kusema, “Bw. Mayala, hawakumaanisha hivyo. Hao wazee wangekufukuzaje? Mwenyekiti wa bodi ni mzee Bw.
Mayala, na mnamiliki hisa nyingi. Nani anaweza kulinganisha faida unayoleta kwa Nyanza Group kila mwaka? Bonasi za kila mwaka wanazopokea haziwaziwi, na watakuwa wazimu ikiwa wanataka kukufuta kazi.

"Bwana Mayala, kuna jambo moja zaidi nataka kukuambia." Chale akamtazama tena Doris.

Kendrick alijua ni kuhusu Alissa, hivyo akamwambia Masie, “Masie, mpeleke Doris kwenye duka la vitabu ili kuchukua vitabu vya watoto. Mtunze vizuri.”

"Uwe na uhakika, Bw. Mayala." Masie alimfikia Doris.

"Doris, twende nami." Doris alikuwa mjanja sana akatoka ofisini na Masie.

Kendrick aliinuka kutoka kwenye kochi la ngozi na kutembea nyuma ya dawati. "Endelea."

"Bwana. Mayala, picha ya Rosy Masolwa na ile ya Bi. Mayala zinafanana baada ya kulinganishwa. Inathibitisha kwamba wao ni mtu yule yule.” Chale alimwambia Kendrick matokeo.

Sura ya 240

Chale hakutarajia kwamba mwanamke huyo miaka mitano iliyopita alikuwa kweli Alissa. Alikuwa akimtafuta kwa muda mrefu sana.

Ikawa mtu waliyekuwa wakimtafuta alikuwa mbele yao. Huyo ndiye alikuwa Bi Mayala halisi.

Kwa kuwa ni Bi Mayala, Chale angemeza tu kutotaka kwake na hasira yake yote. Hakuweza kumletea Bi Mayala shida. Katika hali hiyo, Chale angefukuzwa na Bw. Mayala.

Kendrick hakushtuka sana wala kushangaa, maana tayari alishabahatisha jibu. Alihitaji tu kuijaribu.
Sasa baada ya kupata jibu, alizidi kumkatia tamaa Alissa.

Alikuwa amemficha mambo mengi kwa muda mrefu, na alionekana kama mpumbavu mbele yake.

"Bwana Mayala.” Chale alipoona Kendrick haitiki muda mrefu, akamuita kwa sauti ya chini.

"Endelea." Kendrick alikumbuka mawazo yake.

"Kwa hivyo Bi. Mayala ndiye mwanamke miaka mitano iliyopita." Chale alihitimisha.

Kendrick alimkazia macho. "Najua hilo."

"Na jambo fulani kuhusu Bi. Mayala miaka mitano iliyopita lilikuwa limepatikana." Chale aligusa pua yake kwa njia ya kuchosha. “Miaka mitano iliyopita, Bi
Mayala alimzaa Doris kwa siri. Baada ya siku 40 za kupumzika, aliruhusiwa kutoka hospitalini, lakini akakutana na Seidrick. Seidrick kisha akavunja uchumba na yeye na akapendekeza kumuoa Melissa.

"Na kisha Bi. Mayala alifukuzwa kutoka kwa familia ya Maziku, na Bi. Mayala alitoweka kutoka Mwanza na kwenda Dar es Salaam, ambapo aliishi kwa miaka mitano iliyofuata. Hivi majuzi alirejea Mwanza. Na Melissa alicheza jukumu muhimu katika jambo zima. Alimzunguka Bi
Mayala…”

“Najua yote kuhusu hilo. Unaweza kuondoka sasa hivi.”

Kendrick alipunga mkono na Chale akaondoka, kisha akajiegemeza kwenye kiti chake.

Alissa alimchagua kuzaa naye mtoto ili kuokoa Seidrick, ambayo ilithibitisha kwamba aina yake ya damu au uboho ziliendana na Seidrick.
Lakini kwa nini yeye au Seidrick hakuja kwake, lakini akazaa mtoto?

Lakini, hata Seidrick au Alissa angemuomba atoe mchango kwa wakati huo, anheweza kukataa, hivyo Alissa angejihatarisha kumpa dawa kisha akafanya naye mapenzi ili apate mimba ajifungue mtoto, na akategemea kumuokoa Seidrick.

Lakini alikumbuka kwamba alikuwa amempa kidonge… Ikawa alijifanya tu kumeza kidonge, lakini hakukinywa.

Kwa bahati nzuri Alissa alipata mimba ya mtoto na kumuokoa Seidrick, lakini Seidrick alifikiri kuwa Alissa ndiye aliyemsaliti, hivyo mpaka sasa bado hakujua kuwa mtoto aliezaa na Alissa ndiye aliyeokoa maisha yake.

Mwokozi wake halisi alikuwa Alissa, au kwa sehemu, yeye.

Lakini katika jambo hili zima, alikuwa kibaraka tu, na Doris alikuwa chombo, jambo ambapo Melissa alikuwa sahihi.
Kendrick hakuweza kukanusha.

Alijiuliza tu Seidrick akijua kuwa Alissa alimuokoa, je atajuta na kumkubali tena? Alissa alikuwa na hisia kubwa kwake. Wangependana tena wakati kutoelewana kwao kumeondolewa?

Na kisha yeye na Doris wangekuwa watu wa kupindukia ...

Kwa kufikiria uwezekano huo, Kendrick hakuweza kutulia, na alihisi kutokuwa na utulivu na wasiwasi.

Ndio maana hakutaka kumfungia Alissa kwake, akampa makubaliano ya talaka na kumwacha huru. Ikiwa hangeweza kumpa furaha aliyotaka, angemwacha aende kutafuta anachotaka.

Wakati anatafakari, mlango wa ofisi hiyo ukasukumwa. Mwanamke mwenye sura nzuri aliingia. Alikuwa amevalia gauni dogo la V-shingo nyeusi na nyeupe, lililoonyesha umbo lake la kuvutia. Kifua nono na tako nene pamoja na miguu nyembamba ilikuwa imevutia watu wengi.

Nywele zake ndefu na zilizopinda zilitiwa rangi ya kitani nyepesi, ambayo ilimpa haiba safi na ya kigeni. Kwa kujipodoa kwa utamu, alionekana mrembo sana na wa kike sana.

“Kaka Kendrick.” Mwanamke huyo alitembea kwa kasi na sauti yake ilikuwa laini na tamu.
Kendrick akamtazama Tina, kisha akakunja uso, “Kwa nini umekuja hapa?”

"Kaka Kendrick, nimekukumbuka, kwa hivyo nikaja hapa." Familia ya Mwita na familia ya Mayala walikuwa marafiki kwa muda mrefu, na walikuwa na uhusiano mzuri sana.

Baba yake Kendrick na baba Tina walikuwa marafiki wa karibu, hivyo walitegemea sana Kendrick na Tina wangeweza kuoana. Lakini, Kendrick hakutaka.

Wazazi wa Kendrick na Tina walikuwa wamefunguka na hawakuwalazimisha, lakini Tina alikuwa ameamua kuolewa na Kendrick. Alitaka kuwa mwanamke anayestahili Kendrick, kwa hivyo alienda nje ya nchi kwa masomo zaidi na alionekana mbele ya Kendrick kwa njia bora na kamilifu.

"Hii ni ofisi yangu na unaweza kukutana nami nyumbani." Kendrick alikuwa ameweka wazi kuhusu mtazamo na hisia zake kwa Lina. Siku zote alimchukulia kama dada yake.

"Nilikufuata Geita nikaambiwa ulikuja Mwanza. Nilisikia kwamba utakaa hapa kwa muda mrefu, na siwezi kusubiri kukuona, kwa hiyo nilikuja na Kabula." Tina alimwendea Kendrick, akasema kwa upole na kuuma midomo yake kama jeli, "Kaka Kendrick, kwa nini hkunisubiri?"

“Kwa nini?” Kendrick alijiuliza. Hakumuahidi chochote.

"Kwanini hukunisubiri hadi nirudi?" Tina hakuridhika kidogo na kusema, "Kaka Kendrick, unawezaje kuoana na mtu mwingine wakati mimi sipo?"

“Tina, sikuoa hivi karibuni. Nimemuoa miaka mitatu iliyopita.” Kendrick alieleza, “Nilikuambia nilikufikiria wewe kama dada tu, kwa hiyo sikutaka kukupotezea muda.

“Kaka Kendrick, ni afadhali unipoteze muda wangu.” Ni kwa njia hii tu angeweza kuhisi alikuwa naye akilini. “Isitoshe, mimi si dada yako. Unanichukulia kama dada yako, lakini sikukuchukulia kama kaka yangu.”

“Umekuwa ukiniita kaka Kendrick tangu ukiwa mdogo.” Kendrick alisema.

Tina alikosa la kusema. Alizunguka meza na kumjia Kendrick, “Sitakuita tena kaka Kendrick kuanzia leo.
Nikuite Kendrick au mpenzi wangu?”

"Tina, usiwe na wasiwasi." Kendrick alijaribu kuiondoa mikono yake, lakini alimshikilia kwa nguvu na kukataa kumruhusu aende. "Mimi sio mtu asiyebadilika. Natafuta furaha yangu tu.”

“Tina, nimeoa.” Kendrick tena alisema kuwa tayari alikuwa ameoa. “Unaharibu sifa yako. Ninakuchukulia kama dada yangu, kwa hivyo ninakuvumilia. Kama ungekuwa mtu mwingine, ningekufukuza ofisini kwangu.”

Tina alijua kuwa Kendrick anasema ukweli, lakini hakuwa tayari kumwachia. Alifanya kazi kwa bidii ili kujiboresha, ili tu kujifanya kuwa anastahili kuwa na yeye. Hata hivyo, alipomaliza masomo yake, alisikia kuhusu ndoa ya Kendrick kutoka kwa Kabula, na hakuweza kutulia, hivyo akaruka kurudi Geita mara moja.

“Kwa nini? Kwa nini huwezi kunipa nafasi? Mimi si mzuri vya kutosha?" Macho ya Tina yalikuwa yamelowa, lakini alijaribu kuyazuia machozi yake.

Sura ya 241

Macho ya Tina yenye kumetameta na yasiyo na hatia yaliutazama uso wa Kendrick mzuri na mkomavu. Alivutiwa naye tangu alipoona sura yake alipokuwa mtoto. Sambamba na mafanikio na talanta ya Kendrick, alimpenda zaidi. Alimpenda mtu huyu, ambaye alikuwa mzuri na mwenye akili.

Pia alikua, kiasi cha kustahili kuwa naye, lakini alioa… Hili lilikuwa jambo ambalo hangeweza kukubali, jambo ambalo lilimhuzunisha sana.

“Tina, wewe ni mzuri. Wewe ni mrembo, mchangamfu, na mwerevu… lakini hisia hazina uhusiano wowote na sifa hizi.” Macho ya Kendrick yalikuwa mazito huku akikandamiza uchungu aliokuwa nao. "Itatuepushia sisi sote wasiwasi mwingi. Ikiwa hisia zinaweza kutegemea viwango hivi,
kusingekuwa na watu wengi wanaoteseka kutokana na mapenzi duniani...

“Tina, wewe ni mzuri. Unastahili kupendwa, lakini wewe na mimi hatujakusudiwa kuwa—”

Maneno ya Kendrick yalikatishwa na yeye kwa wasiwasi huku akimuuliza, “Kwa nini hatujakusudiwa? Nadhani tuna maana sana kwa kila mmoja. Unaona, tulikua pamoja tangu ujana. Familia zetu zimekuwa marafiki wa karibu kwa muda mrefu. Baba yangu na Bw. Mayala ni kama ndugu. Sisi ni jozi kamili kulingana na mwonekano wetu, malezi ya familia, kiwango cha elimu na utu. Ni kwamba hutaki kunipa nafasi.”

"Hiyo ni kwa sababu sitaki kukuona ukiumia, kwa sababu hutatarajia chochote ikiwa huna nafasi." Kendrick akautoa mkono wake mrefu kutoka mikononi mwake. Alisimama na kuiweka mikono yote miwili mabegani mwake. "Hii ndiyo njia bora ya kukulinda na kukuthamini."

“Kendrick Mayala, sihitaji. Nataka unipende pia.” Tina alimtaja kwa jina lake kamili huku macho yakimtoka na kuumia sana.

“Tina, umekuwa msichana mwenye busara machoni pangu. Usiwe mkaidi.” Kendrick alihisi wasiwasi.

Alipokuwa mtoto, Tina alipenda kuishi katika jumba la kifahari la familia ya Mayala. Alikuwa mchumba wake wa utotoni. Utu wake ulikuwa wa kupendeza na wa kuvutia, kwa hivyo kila mtu alimpenda sana. Kwa vile mama yake alifariki akiwa mtoto, Kendrick alikuwa hapendi kuongea na watu. Tina hakuwahi kutishika na hali yake ya ubaridi huku akimfuata bila kuchoka akitaka kucheza naye.

Kendrick kila wakati alimtendea Tina kama dada mdogo. Kwa kuwa kulikuwa na wavulana wawili tu katika familia, wote walimpenda. Mbali na kutompa mapenzi, Kendrick alimbembeleza na kumthamini.

Bado alikumbuka Tina akifukuziwa na Dylan Ethan, wakati wa shule ya upili. Alimfuata hata kwenye jumba la familia ya Mayala.
Kendrick akamshika mkono Tina na kutokea. “Hautamsumbua tena Tina. Vinginevyo, sitakutendea wema.”

"Kendrick, sikuogopi hata kidogo linapokuja suala la kumfukuzia Tina." Dylan alidhamiria na hakurudi nyuma. “Nampenda Tina. Niko huru kumfukuzia. Huna haki ya kuingilia kati.”

"Dylan, unaweza kuacha kunisumbua? Nilikuambia kuwa sikupendi!” Tina hakuweza kumpenda Dylan hata kidogo alipokuwa akimfuatilia bila kuchoka. Alichukizwa hata. "Tayari nina mtu ninayempenda."

"Ni haki yako kuwa na mtu unayempenda, lakini huna haki ya kunizuia kukupenda." Dylan alikuwa akiendelea na kichaa chake katika harakati zake za mapenzi.

"Dylan, amini usiamini, nitakung'oa meno!" Kendrick alianza kuinua mikono yake huku macho yake yakitoa ishara za hatari.
Lakini Dylan bado hakuwa na hofu hata kidogo. "Ninafaa kupigwa kwa ajili ya Tina!"

“Basi nitahakikisha kwamba unahisi kwamba inafaa.” Kendrick alikuwa anataka kumkimbilia na kumpiga Dylan, lakini Tina akamvuta nyuma. Alikunja uso kwa kuchanganyikiwa. “Unanirudisha nyuma kwa ajili ya nini? Nisipomfundisha somo, ataendelea kukusumbua.”

"Kendrick, sitaki umpige yeye kwa niaba yangu na kuniharibia hisia zangu kamili juu yako." Midomo laini ya Tina ilijikunja, “Acha nifanye mwenyewe.”

Tina alijiweka wazi kwa Dylan. “Dylan, nina mpenzi. Ninampenda sana, kwa hivyo bora ukate tamaa. Sitakubali kuwa mpenzi wako.”

“Hata kama una mpenzi, bado ninaweza kukupenda…” Dylan bado hakukata tamaa. “Tina, nipe nafasi tu. Hakika nitakutendea vyema na kusikiliza kila kitu utakachosema.”

“Haina maana. Ninampenda yeye tu.” Tina akatikisa kichwa na kukataa tena.

“Halafu… yeye ni nani? Je! ni nini kizuri kwake… kinachokufanya unikatae? Yeye ni bora kuliko mimi kivipi?" Dylan hakuwa tayari kukubali ukweli.

"Yeye ni mzuri kwa kuwa ninampenda." Tina alisimama pembeni ya Kendrick. Aligeuza kichwa na kumwangalia yule mtu mrefu kando yake huku macho yake yakimetameta. "Kendrick ni mpenzi wangu, pekee yangu."

Kendrick alishangaa kidogo lakini alibaki ametulia juu juu.

Alijua kwa macho ya Tina kuwa angesema vile.

Bila shaka alijiona tu kuwa yeye ndiye kisingizio cha Tina kumkataa Dylan ili akate tamaa kabisa.
Kwa kweli hakufikiria sana wala kwa kina maana alimchukulia kama dada yake mwanzo mwisho.

Dylan aliposikia kuwa ni Kendrick, macho yake yalimtoka kwa mshtuko. Hakuwa tayari kabisa kukubali ukweli. “Tina, kuna nini kizuri kwake? Daima ana kujieleza baridi juu ya uso wake. Hawajali sana wasichana shuleni hata hawaangalii. Unapenda nini kwake? Hatakuwa mwema kwako.”

"Unajuaje kuwa sitamtendea vizuri?" Kendrick alichukua hatua ya kumshika Tina mkono. “Sasa umepata jibu lako, acha kumsumbua Tina bila aibu. Yeye ni wangu. Kumbuka hilo!”

Tina aliridhika sana na majibu ya Kendrick. Aliuma midomo yake kirahisi, na macho yake yakajaa furaha.

“Dylan, umesikia alichosema Kendrick. Usinifuate tena.” Tina alikuwa na Kendrick tu machoni mwake, hivyo hakuweza kumuona mtu mwingine yeyote.

“Hata ukiwa na uchumba, maadamu haujaolewa, sitakata tamaa! Tina, nitaruhusu wakati uthibitishe kwamba ninakupenda kuliko yeye!” Ingawa Dylan aliumia moyoni, bado alikuwa mkaidi.

“Ondoka ukishamaliza!” Kendrick alikaza macho yake ya baridi kidogo. "Sitakuwa mwema kwako tutakapokutana tena."

“Sihitaji uwe mzuri! Nina imani na upendo wangu kwa Tina. Ataelewa kuwa mimi ndiye ninayempenda zaidi.” Dylan alikasirika huku akiondoka. Hakuweza kukubali kuwa Kendrick na Tina walikuwa pamoja.

Baada ya Dylan kuondoka, Kendrick aliuachia mkono wa Tina. “Tina, nimesema hayo maneno sasa hivi kwa sababu hali ilikuwa ya dharura. Natumai hutaelewa vibaya. Ni kwamba Dylan sasa hivi hafai kwako.”

“Kendrick, huna haja ya kueleza zaidi. Naelewa." Tina akatabasamu kidogo. “Lakini kuna mambo nataka kukuambia. Nilichosema hivi punde ni kweli. Nakupenda. Nataka uwe mpenzi wangu… Pia najua haiwezekani sasa, lakini ninatazamia siku utakapokuwa mpenzi wangu wa kweli.”

“Tina, wewe ni dada yangu tu…”

Baada ya yote, siku hii haikufika kama ilivyotarajiwa. Akawa mume wa mwanamke mwingine, lakini bado alikuwa akimngoja.

Sura ya 242

Kumbukumbu zake za utotoni na Kendrick zilimhuzunisha alipozikumbuka sasa.

Macho yake yalikuwa yametokwa na machozi, lakini alijizuia kulia. "Kendrick, ninachofanya leo ni sawa na kile Dylan alifanya miaka kumi iliyopita. Ninaendelea kukufukuzia licha ya kukataliwa nawe… Ikiwezekana, natamani nisingekuwa nimeenda ng'ambo ili nisije nikachelewa hatua moja, na usingekuwa umeibiwa na mtu mwingine…”

Aliuma midomo yake na kuhisi mawimbi ya maumivu yakitiririka ndani kabisa ya moyo wake kiasi kwamba hakuweza kutuliza wala kudhibiti hisia zake. Mwishowe, machozi yalitiririka usoni mwake.

“Tina, sijaibiwa na mtu mwingine. Nimekupata mwanafamilia, mtu ambaye atakuthamini na kukupendezesha kama mimi. Je, haingekuwa vyema kuwa na mtu mmoja zaidi wa kukupenda kuanzia sasa na kuendelea? Kwa nini ufikiri kwamba niliibiwa kutoka kwako? Tulia na usijali, sawa?" Sauti ya Kendrick ilikuwa ya upole iwezekanavyo.

Ilikuwa vigumu kwake kumtazama akilia. Baada ya yote, alikuwa msichana ambaye alimpenda kama dada kutoka utoto hadi utu uzima. Hakuweza kuvumilia kumuona akiumia.

Ikiwa ni mtu mwingine aliyemfanya alie, bila shaka hangemwacha aondoke. Lakini mtu huyu alikuwa mwenyewe, na hakuweza kujiruhusu kusukumwa.

Hii haikuwa tu juu ya hisia na ndoa, lakini pia juu ya heshima yake kwa mke wake. Alitaka Tina ajue undani wake.
“Inaonekana ameushinda moyo wa Kendrick. Je, kweli atakutendea kwa fadhili kama wewe?” Tina akamuuliza.

“Bila shaka, amini ladha yangu,” Kendrick alimfariji na kumtuliza. "Utakuwa mzuri sana mara tu utakapomjua."

"Basi nataka kukutana naye. Naweza?" Tina aliomba. “Nyie mmefunga ndoa bado sikuwapa hata zawadi ya harusi, kwa hiyo nitawafanyia chakula. Vipi leo? Niko hapa Mwanza tayari. Nataka kukutana naye.”

“Iwapo atakutendea vizuri na anaweza kukupa furaha, basi sitakuwa na wasiwasi. Sitaki kitu kingine chochote. Nitakuwa dada yako na kuwapa vijana wako matakwa yangu ya dhati. Pia nitamheshimu na kumpenda jinsi ninavyokuheshimu na kukupenda.”

Tina alivumilia mawimbi makali ya hisia alizohisi. Alitaka kukutana na upande mwingine kwa sababu tu kwa kumjua adui yake na yeye mwenyewe angeweza kushinda. Alihitaji kujua yule mhusika mwingine alikuwa nani, la sivyo, angewezaje kusema kwamba anampenda mpinzani huyo wa mapenzi wakati hakuwahi kukutana naye?

Kendrick alisita. Alimpa Alissa makubaliano ya talaka siku hiyo. Alijiuliza kama alikuwa amemaliza kuzingatia.

Ikiwa alikubali talaka, basi asingeweza kumwomba ajifanye kuwa wanandoa wenye upendo mbele ya Tina.

Hakumwambia Tina kuhusu mpango wake wa kuachana na Alissa kwa sababu tu hakutaka kumpa Tina matumaini. Hata angeachwa, bado angemfikiria Tina kuwa dada, na mtazamo wake kwake hautabadilika.

“Amekuwa na shughuli nyingi sana kazini hivi majuzi. Nitamuuliza. Ikiwa ana wakati, nitapanga nyinyi kukutana. Ikiwa sivyo, basi wakati ujao." Kendrick alimuona ametulia na kujisikia raha.

“Kama siwezi kuonana naye leo, basi Kendrick naomba unifanyie chakula na kunipeleka karibu. Yeye yuko bize na kazi na hata hivyo hawezi kutumia muda na wewe. Vipi unipe muda wako badala yake?” Tina alipendekeza. Kwa kweli, alitaka kuwa peke yake naye zaidi ya kukutana na mpinzani wake wa upendo. Alikuwa nje ya nchi kwa miaka mitatu na hakuwa amekaa naye vizuri kwa muda mrefu.

“Sawa. Nitakusindikiza,” Kendrick hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali.

“Huwezi kurejea ahadi yako kwangu,” Tina alithibitisha tena.

"Hakuna majuto," Kendrick alisema.

Wakati huu, Tina alikimbilia mikononi mwa Kendrick, akiizungusha mikono yake vizuri kwenye kiuno chake chembamba.

Alikuwa mikononi mwake na alihisi harufu yake karibu naye alipokuwa akipumua, harufu ambayo aliimiss sana.

Kwa kweli hakutaka kamwe kuondoka mikononi mwake. Alitaka tu mikono na kifua chake kwa matumizi yake ya kipekee milele… Angeweza hakika kujaribu kumrudisha.

Kendrick kwa silika alitaka kumfikia na kumsukuma mbali, lakini alipoweka mkono wake begani mwake, sauti yake ilikuwa nyororo na ya kusikitisha. “Kendrick, hukunikumbatia nilipotoka nje ya nchi. Hivi ndivyo unavyonipokea? Nataka tu kukukumbatia. Ninakosa kukumbatiwa kwako kwa joto. ”
“Tina, hatufanani tena na tulipokuwa watoto. Hata kaka na dada wasikumbatiane kwa ukaribu sana,” Kendrick alisema huku akijaribu kumsukuma.

Wakati huu, mlango wa ofisi ulisukumwa, na sura ndogo ikaingia ndani kwa furaha lakini ilishtushwa na tukio lililokuwa mbele yake.

“Binti mdogo, punguza mwendo…” Masie alikimbia kwa nyuma lakini akaona tukio ambalo hakupaswa kuliona.

Aligeuka kwa busara na kuinamisha kichwa chini, akitumia vitendo kuashiria kuwa hajaona chochote.

Kendrick alimuona Doris akiwa amesimama na kumsukuma Tina. Mwisho alikuwa na aibu kidogo.

“Sweetie, njoo hapa. Ngoja nimtambulishe Tina kwako.” Kendrick alimpungia mkono Doris.

Muda si muda Doris akarudi katika hali yake ya kawaida. Akiwa na tabasamu zuri usoni mwake, alikimbia na kuushika mkono wa Kendrick. “Baba, tazama. Masie alinipeleka kununua, na tukanunua vitabu vingi.”

Doris alimwita Kendrick “baba” kwa uwazi sana hivi kwamba Tina alihisi kukosa raha.

Hakushtuka hata kidogo kwamba Doris angetokea na kumwita Kendrick kama “baba” kwa sababu alisikia kutoka kwa Kabula kwamba Kendrick alioa mwanamke ambaye alikuwa na mtoto. Ingawa Kendrick alikuwa na uhakika kuwa mtoto huyu ni wake, alishuku kuwa hakuwa binti wa Kendrick wa kumzaa.

Tina alikasirika zaidi alipofikiria hili. Kendrick alikuwa tayari kukubali na kuoa mwanamke mwenye mtoto? Ni aina gani ya nguvu za kichawi alizokuwa nazo mwanamke huyu ambazo zilimfanya Kendrick kuwa “mtiifu”?

Alijisikia vibaya kwa Kendrick na yeye mwenyewe! Kwa hiyo ilibidi akutane na kumfahamu mwanamke huyu! "Nina furaha mradi unavipenda." Kendrick aligusa sehemu ya juu ya nywele zake. "Sweetie, hii ni -"

“Baba, ninakipenda sana kitabu hiki. Unaweza kunifundisha jinsi ya kukisoma? Kuna maneno mengi ndani yake ambayo siyajui.” Mara moja Doris akatoa kitabu ili Kendrick akione.

“Huyu ni Tina. Vipi nimuombe akufundishe kusoma?” Kendrick alitaka kuwasogeza wawili hao karibu. “Tina, huyu ni binti yangu, Doris.”

"Doris ni mzuri sana." Tabasamu la Tina likazidi kuongezeka. “Unaweza kuniruhusu nikufundishe?”

“Baba, naona tusimsumbue Tina kwa kitu kama hiki. Baada ya yote, yeye ni mgeni." Doris alitabasamu kwa Tina lakini tayari alimuweka Tina kuwa mhalifu aliyemtongoza baba yake.

"Tina pia anachukuliwa kuwa dada mdogo wa baba, yeye ni shangazi yako. Sio mgeni."

"Lakini kwa Doris, kila mtu isipokuwa baba na mama ni mgeni. Sisi watatu tu ndio familia." Doris alisema kwa uso wa umakini.

'Hamna nafasi kwa kirukanjia kama wewe kumtongoza baba wakati mama hayupo! Nikiwa hapa, hakika hautafanikiwa.' Doris aliwaza.

Sura ya 243

Kusikia alichokisema Doris, Tina akiwa amesimama karibu na Doris, aliona aibu sana kiasi kwamba alishindwa kuendelea na tabasamu usoni mwake.

Tina na Kendrick wote walikuwa wasikivu, na waliweza kuhisi uhasama wa Doris dhidi ya Tina.

Kendrick alichuchumaa na kuushika mkono wa Doris. “Baba alikua na shangazi Tina. Yeye ni kama dada yangu mwenyewe, kwa hivyo ni sawa kumwita shangazi yake.

"Baba, kwa kuwa ulikua naye, nadhani ni sawa kumwita dada yake." Doris alimchukulia Tina kama kizazi chake kwa makusudi, ili awatenganishe Tina na baba yake, “Baba, tazama dada Tina alivyo. Inaonekana ni mzee sana kumwita shangazi yake."

Kendrick alihisi mnyonge kuhusu Doris, na akasema, “Wewe ni…”

Doris alikuwa mtoto tu, na haikushangaza kwamba alijali sana.
Doris hakujali kuhusu kile baba yake alisema, “Nina tatizo gani?” Macho yake yasiyo na hatia yalitiririka, kana kwamba anasema, "Je, niliwakatisha jambo nyinyi wawili?"

Kendrick alibana pua yake ndogo na kusema kwa upole, "Nenda juu ya kochi na usome." Doris, bila shaka, hakutaka kufanya hivyo, “Baba, je, mama anamjua dada Tina?”

Tina akajibu, “Nimerudi kutoka nje ya nchi na nimemkumbuka sana baba yako, nikatoka Geita kuja Mwanza kumuona baba yako. Baba yako na mimi tumefahamiana tangu tukiwa watoto, na tulikuwa karibu. Sisi ni kama familia, hivyo mimi na wewe ni familia.”

“Mimi na wewe hatuna uhusiano wa damu; unawezaje kuwa familia yangu?" Doris hakutaka kuwa katika familia na Tina. Mwanamke yeyote ambaye alitaka kuwa na baba yake alikuwa mpinzani wa mama yake katika upendo na adui yake. Doris akajibu, “Familia inapaswa kuwa na uhusiano wa damu, sivyo?”

"Doris, baba yako na mama yako hawana uhusiano wa damu, mbona ni familia?" Tina hakufurahishwa na msichana mdogo aliyekwenda kinyume naye, kwa hiyo alisema kwa makusudi.

Tina alifikiri jambo hilo lingemwacha Doris hoi, lakini Doris alimkatisha tamaa. Yule mdogo akajibu, “Hawana undugu wa damu, lakini wana uhusiano wa kisheria, na ni wapenzi. Na wewe je? Unahusiana na sheria au kwa damu?"

Macho makubwa meusi na meupe ya Doris yaliangaza kwa tabasamu tamu.
Nani angeweza kufikiria kuwa binti huyu wa miaka mitano angeweza kusema kwa ufasaha kiasi cha kumjibu Tina, na kumwacha kwa aibu? Tina alikosa la kusema kwa muda. Aliuma meno, na hakuweza kufikiria jinsi alivyoaibishwa na msichana wa miaka mitano.

Alishusha pumzi ndefu ili kujituliza, “Sina undugu na baba yako kwa sheria wala kwa damu, lakini mimi ni familia katika moyo wake, na inatosha.

Watu wa moyoni ndio walikuwa muhimu zaidi. Tina alipata picha nzuri.

"Moyo wa baba umejaa mimi na mama yangu, na hakuna nafasi yako, dada, kwa hivyo usijidanganye." Doris akanyoosha mkono wake na kumuuliza, “Baba, unanipenda mimi na mama zaidi, sivyo?”

"Ndio, nakupenda zaidi wewe na mama yako." Kendrick alijibu swali la Doris akimaanisha kumwambia Tina kuwa wao si watoto tena.

Tina alijua nini maana ya Kendrick, na alihuzunishwa sana na uelekeo wake.

Lakini hakutaka kuiacha. Walikua pamoja, na hakuamini kuwa Kendrick angekuwa mkatili kwake.
Maadamu kulikuwa na mwanga wa tumaini, hangekata tamaa, hata ikiwa angelazimika kungojea milele.

"Mama na mimi tunampenda zaidi baba pia." Doris alimjibu Kendrick.

Kendrick alitabasamu. Alidhani mtoto alikuwa mzuri sana.

Doris hakujali kuhusu Tina, kwa utiifu akaketi kwenye sofa ili asome.

“Doris ni mtoto tu,” Kendrick alimwambia Tina, “alichokisema hakukusudia, kwa hiyo usikiweke moyoni mwako. Lakini ninachojaribu kusema ni kwamba alichosema ni kweli. Kuna Doris na Alissa pekee moyoni mwangu, na uhusiano wetu wa muda mrefu unategemea kuwa kaka na dada. Tina, inabidi uelewe kwamba mimi nimeoa, na nina mke na binti.”

Tina alijua kuwa Kendrick ameoa, lakini hakuweza kujizuia.

“Kaka Kendrick, nimekupata.” Tina aliweza kuahirisha mambo tu, akajifanya ana akili ili Kendrick asije akapata kuudhika.
Ni kwa kudumisha uhusiano huu mzuri tu ndipo angeweza kumkaribia, au hatamwona tena.

Kendrick alifurahi, "Ni vizuri kama umeelewa."

“Uliahidi kunialika kwenye chakula cha jioni. Usirudie nyuma.” Tina alimkumbusha, “Nilikuja Mwanza kukuona, na huwezi kuniacha peke yangu.”

“Ndiyo.” Kendrick alipoona amekubali, hakuweza kukataa ombi lake.

“Sawa, kazi njema. Sitakusumbua. Nimemwacha Kabula ananisubiri kwenye mgahawa wa chini." Tina hakutaka kuwa na Doris, lakini Kendrick angekuwa peke yake ofisini, angefurahi kubaki pale.

"Endelea. Kuwa mwangalifu." Kendrick alisema.

Baada ya yote, walikuwa wanawake. Sasa kwa kuwa walikuwa hapa, na ndiye mtu pekee waliyemjua. Akiwa kaka yao, ilikuwa kawaida kwamba anapaswa kuwatunza zaidi.

Ikiwa kulikuwa na kitu kibaya kwao, hakujua jinsi ya kumuelezea baba yake au baba Tina.

“Mimi na Kabula si watoto tena. Huna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu hilo. Endelea tu na kazi. Mimi na Kabula tutarudi kabla hujatoka kazini.” Tina akampungia Kendrick na kuondoka.

Kendrick akaona mlango wa ofisi umefungwa kisha akamtupia jicho Doris aliyekuwa akijisomea kimya kwenye sofa.

Akasogea na kuketi karibu na Doris. Alipokuwa akijaribu kuwaza la kusema, Doris aliweka kitabu chake chini na kumwambia Kendrick, “Baba, mimi simpendi huyo dada.”

“Baba hawezi kukuzuia kumpenda au kutompenda mtu, lakini tunapaswa kuwa na tabia njema. Huyo shangazi ni dada wa baba, na wewe ni mdogo, hivyo unapaswa kumheshimu. Huu ndio ubora wa msingi zaidi wa watoto." Sasa Kendrick alikuwa makini zaidi, akitumaini kwamba Doris angeweza kuelewa alikuwa akiongea kwa ajili yake.

Kama binti yake, Doris kwa kawaida alikuwa mtukufu sana na alipaswa kubembelezwa na kulelewa kama binti wa kifalme. Hata hivyo, haikumaanisha kwamba angeweza kuwa wa makusudi na mwenye kiburi. Anapaswa kutenda kama mtoto alipokuwa mtoto.

Hangepingana naye isipokuwa alikuwa na umri wa kutosha kusimama na kila mtu kwa haki yake mwenyewe, lakini sasa anapaswa kujiendesha alipokuwa mtoto.

Hangeruhusu mtu yeyote amdhulumu binti yake, bila shaka. Vinginevyo, hatawahi kuwa na huruma

Sura ya 244

Doris aliinua midomo yake kidogo. Bila shaka, alijua kwamba hakumheshimu Tina hata kidogo, na kwamba alikuwa mkali sana.
Lakini alipofikiria kuwa Tina atamchukua baba yake kutoka kwa mama yake, hakuweza kujizuia kumchukia.

“Baba nafahamu, lakini huyo shangazi anakuona wewe tu. Lazima atakupenda sana… naogopa atakuondoa kwetu. Ninaogopa hautatutaka tena. Siwezi kuruhusu mama yangu kudhulumiwa au kuumizwa. Nilifanya hivyo ili kujilinda mimi na mama yangu, na sidhani kama nilifanya kosa lolote.” Doris alisisitiza wazo lake.

Kendrick alinyamaza kimya. Bila shaka alijua Doris alikuwa na wasiwasi na mama yake. “Siku zote baba amekuwa akimchukulia shangazi huyo kama dada. Ulichofikiria hakitatokea. Isipokuwa wewe na mama yako hamnitaki, sitawaacha.” Kendrick alimhakikishia, “Mbali na hilo, machoni pako, je, baba yako ni rahisi kunyang’anywa na ni rahisi kujaribiwa?”

“Baba nakuamini, lakini wakati mwingine ujanja wa mjaribu huwa na nguvu sana. Hata wenye nguvu zaidi hawana tahadhari wakati mwingine. Vipi ikiwa utadanganywa?” Doris bado alikuwa na wasiwasi. “Sina imani naye.”

Kendrick alikosa la kusema baada ya kusikia Doris alisema, “Nani amekufundisha hivyo?” Je! ulimwengu wa mtoto haupaswi kuwa rahisi? Kwa nini ulimwengu wa Doris ulikuwa mgumu sana, kana kwamba anajua kila kitu?

“Hakuna aliyenifundisha. Nilijua hilo kwa sababu nimeona na kusikia mambo mengi kuhusu hilo kwenye tv.” Doris alionekana kama mtu mzima. “Nilipokuwa katika shule ya chekechea huko Dar, niliona mtoto katika darasa langu ambaye hangemruhusu mama yake mpya amchukue. Alisema mwanamke huyo alikuwa mjaribu, na akamtongoza baba yake, na akamzaa kaka yake mdogo. Na ndio maana baba na mama yake walitengana. Alimchukia mwanamke huyo...

“Baba, shangazi Tina anataka kuwa mama yangu mpya, na mimi siwezi kukubaliana na hili na sitakubali! Mama yangu pekee ni Alissa.”

"Baba anaahidi haitatokea, na una mama mmoja tu naye ni Alissa." Kendrick alimtuliza.

“Baba usijaribiwe na huyo mwanamke! Sitaki baba na mama watengane. Sitaki kuwa kama mtoto huyo…” Doris hakujiamini sana.

Kendrick alimshika Doris mikononi mwake na kumshika mabegani. “Usiwaze sana na usiongee upuuzi. Unapaswa kumwamini baba.
Shangazi Tina na baba walikua pamoja. Ikiwa baba alimpenda, nisingengoja hadi baada ya kuoana na mama yako. Mtu pekee ambaye baba atakaa naye maisha yake yote ni mama yako.”

"Baba nakupenda." Mkono mdogo wa Doris ulishika shati la Kendrick.

"Baba anakupenda pia." Kendrick aliinamisha kichwa chake na kumbusu Doris kwenye paji la uso.

Baada ya kuzungumza na Doris, Kendrick alianza kufanya kazi. Alikuwa bize sana na kazi yake, akiwa na mafaili mengi ya kuangalia na maamuzi mengi ya kufanya.

Walipata chakula cha mchana ofisini. Masie aliagiza chakula chenye lishe kwa Doris, na chakula cha kawaida kwa Kendrick.

“Ni kitamu.” Doris akaweka chakula kingi mdomoni na kumtazama Kendrick kwa macho ya tabasamu. Wakati huo, Doris alionekana kama mtoto halisi.

Kendrick alisema, "Ikiwa unakipenda, baba atakuletea chakula kwenye shule yako ya chekechea kila siku."

“Hapana, chakula cha chekechea ni kizuri pia. Isitoshe, tumelipa pesa. Hatuwezi kuipoteza.” Doris alikuwa mtoto asiyejali. "Mama na baba hufanya kazi kwa bidii sana ili kupata pesa," alisema.

Midomo ya Kendrick ilipinda na akasema, "Vema, malizia haraka."

Doris alikula kwa furaha. Kumwangalia Doris, Kendrick alikuwa na hamu nzuri.

Kendrick aliongozana na Doris kusoma wakati wa mapumziko ya chakula cha mchana. Baadaye, ilimbidi ahudhurie mkutano muhimu, hivyo akamwacha Doris peke yake ofisini.

Kendrick alimwambia Masie amuombe mtu aendelee kumuangalia Doris na azingatie sana usalama wake.

Kisha Masie akampa kazi Sekretari mwingine katika Ofisi ya Sekretari Mkuu.

Lakini hawakutarajia kuwa Tina na Kabula wangekuja kumtafuta Kendrick saa tisa kamili. Walikuwa wametoka tu kwenda kufanya manunuzi na kununua vitu vingi. Sasa wote wawili walikuwa wamechoka, na walitaka kupumzika katika ofisi ya Kendrick.

Tina na Kabula hawakujua kuwa ni Doris peke yake aliyekuwepo ofisini.

Akiwaza kukasirishwa na msichana huyu hapo awali, Tina hakufikiria kuwa ni lazima ajifanye kuwa mzuri wakati Kendrick hayupo.

Ilikuwa mara ya kwanza Kabula kukutana na Doris, na jibu lake la kwanza lilikuwa kwamba Doris anafanana na Alissa.

Alinong’ona kwa Tina, “Sikujua kuwa mwanamke huyo ana binti mzuri.”

“Usidanganywe na sura yake; ana majibu ya kunya." Tina naye alidanganywa hapo awali na sura yake ya kimalaika. "Usihukuhukumu kitabu kwa jalada lake; vinginevyo, utateseka sana."

“Kweli?” Kabula hakuamini kuwa mtoto huyo anaweza kuwa mcheshi kiasi kwamba alimfanya Tina kukosa la kusema.

“Nimekutahadharisha. Ikiwa huniamini, jaribu.” Tina alikaa chini kwa uzuri.

Kabula alikaa chini na kumtazama Doris, “Baby, ni mama yako Alissa?”

Doris alikuwa akisoma kitabu kimya kimya, hakukusudia kuzungumza nao, lakini kwa kuwa sasa walikuwa wamechukua hatua ya kuzungumza naye, hangekuwa na adabu.

"Lazima nijue wewe ni nani kabla ya kujibu swali lako." Doris alitaka kujua mwanamke aliyekuwa na Tina ni nani, mwanamke huyo ana uhusiano gani kwake, na uhusiano wake na baba ni upi.

"Mimi ni dada wa Kendrick, Kabula." Kabula alijitambulisha.

“Dada mwingine? Baba yangu ana dada wangapi?" Doris akakiweka tena kile kitabu chini na kumtazama Kabula kwa mashaka. "Kabula nani?"

"Kabula Ndallo!"

“Mbona dada za baba yangu wote hawana jina la Mayala? Nyinyi si dada za baba yangu, sivyo?”
Doris alimuona kuwa ni kishawishi kingine tu cha kumtongoza baba yake.

“Sisi si dada zake kaka Kendrick, lakini wewe ni binti yake halisi?” Tina alikoroma, “Chungu kinaita birika nyeusi… Oh, hapana, angalau mimi na kaka Kendrick tumefahamiana tangu utotoni, na Kabula ni dada yake. Tulitumia wakati mwingi pamoja, sio kama wewe, ambaye ulikutana naye kwa muda mfupi sana."

Doris aliguswa na hali yake ya kuumiza. Hakuwa binti wa Kendrick mwenyewe. Ikiwa mama yake hangeolewa na mjomba mzuri, hangeweza kumwita baba.

"Una wivu kwamba sina uhusiano wa damu na baba yangu, lakini bado ananipenda na kunidekeza?" Doris hakukerwa na maneno ya Tina. "Mimi ni kama binti yake halisi moyoni mwake."

“Kwa hiyo wewe si binti halisi wa kaka yangu?” Kabula alipata ujumbe muhimu, "Kaka yangu alimdanganya baba yangu kwamba wewe ni binti yake mwenyewe na una damu ya familia ya Mayala! Ni lazima nimwambie baba kuhusu hilo, au bado atakuwa gizani.”

Sura ya 245

Baada ya kumuona Kabula akisema maneno yale kwa hasira, ghafla Doris alijisikia kufadhaika sana. Lazima alisema kitu kibaya kumkasirisha sana. Alilalamika hata kwa baba yake.

Angemuingiza baba yake kwenye matatizo. Hakuweza kumfanya alaumiwe kwa ajili yake.

Doris aliinuka kutoka kwenye sofa na kumsogelea Kabula, akisema kwa upole, “Wewe ni dada ya baba yangu, kwa hiyo nikuite shangazi,” alisema.
"Shangazi."

"Wewe si binti wa kaka yangu mwenyewe, na hustahili kuniita shangazi!" Kabula alikuwa na hasira sana sasa hivi.

"Basi wewe si dada wa baba yangu kamili, kwa nini unaweza kumwita kaka?" Doris aliuliza nyuma yake.

Kabula alikuwa hana la kusema, na uso wake ukageuka mwekundu. "We mtoto! Umejifunza maneno ya shombo kutoka kwa mama yako? Unakuwa mkorofi kwa wakubwa wako?"

"Hii haina uhusiano wowote na mama yangu!" Doris alichukia kwamba watu wanamlaumu mama yake kila wakati. “Kwa sababu wewe ni dada wa baba yangu, ningependa kukuita ‘shangazi’. Hiyo ndiyo heshima na adabu bora kwako.”

“Heshima? Unatania?" Kabula alisema kwa upole.

“Unaweza kumuuliza Tina. Pia alisema kuwa yeye ni dada wa baba yangu. Baba yangu aliniomba nimwite 'shangazi', lakini sikufanya. Je, sikukuheshimu kwa kukuita shangazi?” Doris aliongea huku akitabasamu.

Kama msemo unavyokwenda, hakuna mtu ambaye angegonga uso wa tabasamu. Kabula hakukasirika kwa kusikia kile ambacho Doris alisema, lakini Tina, ambaye alihusika, alionekana kuwa na huzuni.

“Kama ungekuwa si binti wa Kendrick kweli, nisingekupa sura ya pili. Usiwe na hisia ya ubora. Ni kwa ajili ya Kendrick tu. Wewe na mama yako mtakuwa si kitu baada ya kuondoka Kendrick!” Tina aligonga msumari kichwani na kumtazama Doris kwa dharau.

Alizaliwa katika familia ya Mwita, Tina alikuwa amejulikana kila wakati tangu utoto wake. Kwa kawaida, wale ambao wangeweza kumvutia walikuwa bora na wenye talanta zaidi kuliko yeye katika nyanja zote, na Kendrick alikuwa mtu ambaye aliabudiwa na kupendezwa.

"Hatutamwacha baba yangu, na hatutaruhusu vishawishi kama vile mnavyomfanyia baba yangu." Doris hakutaka kukasirika.

“Acha kuwa mpotofu. Tina na kaka yangu walikua pamoja tangu utotoni na walikusudiwa kila mmoja. Tina alienda ng'ambo kwa masomo zaidi, na mama yako alitoka patupu kumnyakua Kendrick! Mama yako ndiye mjaribu!” Kabula alitoa hasira yake yote kwa mtoto.

“Mama yangu si mjaribu! Kwa hivyo ni nini ikiwa walikua pamoja? Hiyo ni kwa sababu baba yangu hampendi Tina kwa hiyo hawako pamoja! Baba yangu anampenda mama yangu hivyo alimuoa.” Doris alitoa hoja. “Usifikiri kwamba kwa sababu mimi ni mtoto unaweza kunionea! Angalau naweza kujua ikiwa mmoja anampenda au hampendi mwingine!”

“Mapenzi? Mama yako anatudanganya. Hatujui jinsi alivyomtongoza kaka yangu na kumlaghai kuwa wewe ni binti yake wa kumzaa ili kumlazimisha Mzee Mayala akukubali! Mama yako anapenda pesa hivyo atamshikilia kaka yangu hata kwa ndumba! Nyinyi si chochote ila waongo! Sitaruhusu kaka yangu na familia yangu kudanganywa na nyie milele!” Kabula alidhamiria. "Hustahili kuzungumza juu ya upendo!"

"Ni wewe ambaye hustahili!" Doris akajibu tena.

"Kabula, tungewezaje kumruhusu msichana huyu kukaa katika familia ya Mayala? Familia ya Mayala itakuwa kicheko ikiwa habari itaenea." Tina aliongeza, “Nafikiri unahitaji kumwambia Mzee Francis sasa hivi.”

“Ndiyo. Siwezi kustahimili waongo wa kuchukiza kwa dakika moja!" Kabula akasimama, akatoa simu yake ya mkononi na kuanza kumpigia Francis Mayala.

Doris alifoka, “Sisi sio waongo. Usizungumze upuuzi!”

“Wewe si binti wa kaka yangu hata kidogo. Je, huo si uwongo?” Kabula hakumpenda Alissa mwanzoni, lakini alipojua kuwa mtoto huyo si wa Kendrick, alizidi kumchukia Alissa.

"Nilisema sisi sio waongo!"

“Sijali.” Kabula alimpa mgongo Doris. “Baba, kuna kitu nahitaji kukuambia…”

“Huwezi kusema.” Doris alikuwa na wasiwasi kidogo. "Hata kama kuweka mambo wazi, baba ndiye anayepaswa kufafanua, si wewe!"

“Kaka yangu mkubwa alikuficha tu, lakini sitaki. Siwezi kuruhusu baba yangu adanganywe!” Kabula alisisitiza na kumwambia Francis, "Binti ya Alissa sio binti wa kaka Kendrick..."

Doris alifanya hatua ya ujasiri kwa kufikia na kumvuta Kabula kwenye kifundo cha mkono. “Sitakuruhusu umchongee baba! Huwezi kufanya hivi!”

Kabula alimtazama tena Doris, ambaye alikuwa ameng'ang'ania mkono wake. Macho yake makubwa kama zabibu yalikuwa yakiwaka kwa hasira.

Kabula aliweka simu yake ya mkononi na kumtazama Doris akiwa amemshika mkono mdogo. Alichukizwa, “Usinishike. Ni michafu sana!”

"Baada ya hapo, alitaka kumtupa, lakini Doris alikamatwa kwa nguvu, "Mpigie simu kusema ulikuwa unazungumza upuuzi!"

“Wewe ni mgonjwa!” Kwa hasira, Kabula alimsukuma Doris na kuurudisha mkono wake.

Doris alikuwa mtoto tu. Angewezaje kuwa na nguvu kama mtu mzima? Akiwa anasukumwa na Kabula, Doris alianguka nyuma na kugonga paji la uso wake kwenye kona ya meza ya kahawa, na kisha mwili wake mdogo ukaanguka kwenye zulia.

"Ni bahati mbaya sana kukutana na mama na binti kama hawa." Kabula alifika na kukipapasa kifundo cha mkono alichokuwa amekishika Doris.

Tina akamkabidhi Kabula glasi ya maji. “Usiyatie moyoni. Haikuwa na thamani.”

Kabula alichukua maji na kuketi, lakini alimuona Doris akiwa amejilaza huku akihema. “Msichana mdogo hajaamka. Ana shida gani?”

“Itakuwa sawa?” Tina alilitazama lile umbo dogo lisilotikisika. "Nadhani alizirai baada ya kugonga meza ya kahawa."

"Haiwezekani, sikumsukuma sana." Kabula alishika glasi yake ya maji mkononi. "Ni sawa, sawa?"

"Hebu angalia." Tina alisema.

Kabula alisisitiza midomo yake, akionekana kusita.

"Nipo nawe." Tina alisema.

Na kisha wakainuka na kutembea hatua kadhaa karibu na Doris, na waliweza kuona kwamba muundo wa maua kwenye zulia la kijivu ulikuwa umetapakaa damu na ulisimama wazi dhidi ya kijivu.

Na rangi nyekundu ya damu ilichangamsha mioyo ya Kabula na Tina.

Kabula aliushika mkono wa Tina na kuchukua hatua mbili za uoga nyuma, akihema sana, “Tina… Tufanye nini sasa? Kaka anamjali sana msichana huyu mdogo. Je, atanipiga?”

"Usiwe na wasiwasi. Tulia." Tina alikunja vidole vyake vya baridi. "Tutasema ilikuwa ajali. Hatuna uhusiano wowote nayo. Na tuko wawili tu ofisini. Maadamu tunazungumza sawa, Kendrick hawezi kukufanya chochote bila ushahidi.”

"Lakini msichana mdogo atamwambia, na atakaposema ukweli, kaka yangu atamwamini." Kabula alikunja nyusi zake na hakuthubutu kufikiria jinsi Kendrick atakavyokasirika.

"Hana ushahidi wowote, sivyo?"

Sura ya 246

Tina alikuwa sahihi. Doris hakuwa na ushahidi hata kama yeye alisema ukweli, lakini Kabula bado alikuwa na wasiwasi.

"Hata kama hatuna ushahidi, kaka yangu atamwamini." Kabula aliwaza.

Tangu ajiunge na familia ya Mayala, ingawa alimwita kaka Kendrick kwa upendo, hakuwahi kumchukulia kama dada wa kweli, mbaya zaidi kuliko Tina.

Angalau alipokuwa mdogo, Kendrick alimjali Tina na kumchukulia kama dada, jambo ambalo lilikuwa bora kuliko Kabula, dada wa kambo.

Ingawa alikuwa na wivu, bado alikuwa rafiki mzuri wa Tina. Mapenzi yake kwa Kendrick yaliweza tu kuwekwa ndani ya moyo wake.
Ikiwa Tina angejua juu yake, wangekuwa wapinzani kwa upendo.

Na hakutaka kumpoteza Tina, rafiki yake wa karibu, kwa sababu Tina alikuwa amemsaidia asionewe na wengine na kumsema vyema mbele ya Kendrick.

Urafiki wao ulikuwa wa kweli. Alijua kuwa hakuwa sawa na Tina katika nyanja zote, na ilikuwa haiwezekani yeye kuwa na Kendrick, hivyo alichagua kuwa rafiki yake.

“Je, hakuna hata mmoja wetu aliye muhimu kuliko yeye, mtoto mdogo? Yeye ni binti wa kambo tu asiye na uhusiano wa damu naye.” Tina alimfariji Kabula, ambaye alionekana kuwa na wasiwasi, “Usiogope.”

“Tina, si unajua Kendrick Anampenda Alissa? Kwake hakusita hata kumdanganya baba kuwa huyu mtoto ni binti yake wa kumzaa. Angeweza hata kuchanganya uhusiano wa damu wa familia ya Mayala. Kwa nini anampenda sana Alissa?” Kabula alikasirika sana kwa kile kilichotokea.

Macho yake yakatua kwa Doris. "Mtoto huyu ni wa mwanamke," alisema, "kama atamweleza, Kendrick hatashuku. kweli nakuambia…”

“Nilimpungia mkono tu na sikujua angeumia… Tina, unajua sikukusudia kufanya hivyo. Sikukusudia kumuumiza. Kendrick ataniua.”

“Naona bado una wasiwasi. Usijali.” Uso wa Tina pia ulikuwa na huzuni. Alitazama damu kwenye zulia na kufikiria, "Kuna njia moja tu ya kufanya."

"Nini?" Kabula akaushika mkono wa Tina kwa nguvu zaidi kana kwamba ndiye mkombozi wake.

"Tumfunge mdomo wake milele." Tina alitoa suluhisho.

“Unamaanisha nini…” Kabula aliogopa kufikiria zaidi.

"Ni mtu aliyekufa tu ndiye hawezi kusema." Tina alikuwa akimuangalia kwa ukali.

Moyo wa Kabula ulikuwa mzuri. Alitetemeka kwa hofu.

"Kuua ... kumuua?" Sauti ya Kabula ilikuwa ikitetemeka.

“Hapana, amejeruhiwa na anavuja damu. Tutamwachia Mungu, tusifanye lolote.” Tina akamvuta. “Chukua tu begi lako tuondoke.
Hakikisha hujui lolote kuhusu hilo, au tutajulikana tu.”

“Ndiyo.” Kabula alitikisa kichwa haraka, lakini uso wake ulikuwa umepauka kidogo.



Baada ya yote, Tina alikuwa mkubwa kuliko Kabula, na alikuwa na uzoefu zaidi wa maisha kuliko Kabula, kwa hivyo alikuwa mtulivu.

Alimwomba Kabula amshike mkono, na wakatoka nje ya ofisi, kisha wakaondoka kwenye ghorofa ya juu na lifti. Kabula alifarijika.

"Tina, turudi Geita." Kabula aliogopa sana.

"Tukiondoka ghafla, itakuwa wazi sana. Kaka Kendrick atafikiri tulifanya hivyo.” Tina alipapasa mikono ya Kabula. “Kumbuka tu hukufanya hivi. Yeye mwenyewe alianguka sakafuni. Wangeshuku kuwa utafanya hivyo ikiwa unaogopa."

“Vuta pumzi ndefu na utulie. Pumua tena na utulie.”

Kabula aliitikia kwa kichwa na kumsikiliza Tina na kumfuata ili kujiweka sawa.

“Kwa hiyo tunaenda wapi?”

"Twende tu kwenye mgahawa ulio chini na tunywe kahawa." Tina alipendekeza.

Wakati Tina na Kabula wakiwa kwenye duka la kahawa, Kendrick alimaliza kikao na kuelekea ofisini, akifuatiwa na Masie na Chale.

Masie akausukuma mlango wa ofisi. Kendrick aliingia chumbani, akatazama huku na kule lakini hakumuona Doris.

“Doris yuko wapi?” Kendrick aliuliza.

"Bwana Mayala, nitamuuliza Jessie.” Alisema Masie.

Kendrick aliitikia kwa kichwa na kuzunguka ofisini kwake. Alikuja kwenye dawati la ofisi na kuweka nyaraka. Kwa pembe ya jicho, alishikwa na sura ya waridi kwenye sofa.

Kendrick alikunja uso na kukimbilia kwenye sofa. Hakika, alimuona Doris mdogo akiwa amelala kwenye zulia la kijivu.
Na kilichomshtua ni kwamba muundo wa maua ya damu kwenye kapeti ulikua mkubwa, jambo ambalo lilimfanya moyo wake kutetemeka.

Alipiga magoti haraka na kumlaza Doris kwa makini mikononi mwake.

Alimtikisa Doris kwa upole, “Baby, amka. Unaweza kunisikia…?"

Doris bado aliyafumba macho yake vizuri. Kulikuwa na kigaga cha damu kwenye paji la uso wake, ambayo damu ilitoka, na kuchafua kope zake ndefu na nene. Uso wake mweupe safi pia ulikuwa na rangi nyekundu ya damu, na kuufanya moyo wake kuumia.

“Chale, andaa gari!” Kendrick alipiga kelele.

Chale, aliyekuwa amesimama kando, alipigwa na butwaa, naye akakumbuka hisia zake kwa sauti ya Kendrick, “Ndiyo!” Kendrick alimnyanyua Doris na kutoka nje haraka.

Alipotoka tu ofisini, alikutana na Masie. Masie alipomuona Doris amejeruhiwa na kupoteza fahamu mikononi mwa Kendrick, alitoa macho kwa mshtuko.

Kendrick hakumtazama, bali alikuwa akitetemeka kwa sababu ya baridi ya sura iliyokuwa inatoka kwa Kendrick, kana kwamba ni upepo wa aktiki.

Masie alimfuata Kendrick na kwenda kwenye lifti kwanza na kukandamiza ghorofa ya kwanza.

"Bwana Mayala, kuna nini?” Koo la Masie lilihisi kukauka alipozungumza.

“Nataka pia kujua kilichotokea!” Macho ya Kendrick yalikuwa mazito, “Nilikuomba utafute mtu wa kumwangalia. Je, ndivyo unavyomtunza? Katibu Masie, inaonekana kwamba yeye si muhimu kwako!”

"Bwana Mayala, mimi ndiye ninayepaswa kulaumiwa kwa hili, na nitakubali adhabu hiyo.” Masie alichukua jukumu.

"Sina muda wa kushughulika na wewe sasa." Kendrick alipoona lifti imefunguliwa, akatoka mara moja.
Masie akafuata, “Bw. Mayala, ngoja niende nawe hospitali.”


Kendrick hakusema chochote. Alikaza tu nyusi zake. Ni nani aliyemuumiza Doris?

Ikiwa angempata mtu huyo, asingemuacha.



Sura ya 247

Hewa baridi kwenye lifti nyembamba ilimfanya Masie ahisi msongo wa mawazo na kukosa hewa.

Aliinamisha kichwa chake kwa hatia na kuhisi kukasirika.
Hakutarajia jambo kama hilo lingetokea kwa Doris. Ilikuwa ni kama kisu kinachoma kwenye moyo wa Bw. Mayala.

Kendrick alipofika kwenye maegesho, Chale alikuwa tayari ameshatayarisha gari. Masie aliharakisha kufungua mlango. Kendrick akiwa amemshika Doris akainama na kuingia ndani ya gari.

Masie aliingia kwenye siti ya abiria na Chale akachomoa haraka gari nje ya maegesho na kwenda kwa kasi hadi Hospitali ya karibu.

Hospitalini, mara gari liliposimama, Masie alishuka haraka na kumfungulia mlango Kendrick. Na kisha akatoka na Doris mikononi mwake na kuharakisha kwenye idara ya dharura.

"Daktari, msaada!" Maneno ya Kendrick yalikuwa rahisi lakini yenye nguvu.
Alipoonekana, sawa yake yenye nguvu ilifanya wengine wasiweze kumpuuza.

Muuguzi haraka akakisukuma kitanda cha mkononi. Kendrick akamweka Doris kitandani na kusema, “Okoa binti yangu. Ninataka tu binti yangu awe sawa."

“Usijali bwana. Tutafanya tuwezavyo. Tafadhali nenda ukapitie taratibu.” Nesi alikuwa ameliona jeraha kwenye paji la uso la Doris.

"Bwana Mayala, nitakwenda kuangalia." Masie alijitolea, kwa sababu yeye pia alihusika. "Nini taarifa za msingi za yule binti?"

"Doris Maziki, umri wa miaka 5 ..." alisema Kendrick.

Masie aliandika na kwenda kumuangalia Doris, wakati Chale alibaki na Kendrick.

Kendrick akaketi kwenye kiti. Badala ya kuchukua maji aliyopewa na Chale, aliweka mikono yake kwenye paji la uso wake na kuhisi kufadhaika.

Hajawahi kuogopa sana. Ilionekana kana kwamba shimo lisilo na mwisho lingemeza utulivu wake wote.

Kendrick hakutaka kuongea, akafumba macho na kujaribu kujituliza. Hakuweza kuvuruga mambo sasa.

Chale alisimama tu na hakusema chochote.

Alikuwa na Kendrick kwa miaka mingi na alikuwa na ufahamu mzuri wa tabia zake.

Sasa alikasirika, kwa hiyo alichotaka ni kunyamaza, na Chale ilibidi asimsumbue.

Masie baada ya kumaliza taratibu alifika na kumuona Kendrick akiwa ameweka mikono yake kwenye paji la uso na uso wake mzuri umeziba huku sura yake ikiwa haionekani.

Masie alipokuwa anakaribia kuongea, Chale alimwambia anyamaze.

Masie alisimama mara moja na kusimama kimya kando ya Chale.

Kadiri dakika zilivyozidi kwenda, Kendrick alibaki katika hali hiyo akiwa ametulia lakini akiwa na wasiwasi.

Ilikuwa ni kama atapasuliwa ...

Alionekana kumuona kaka yake akiwa amelala kwenye kitanda cha hospitali akiwa ametapakaa damu...

Kaka yake mkubwa alikuwa katika hali ya kukosa fahamu kwa miaka mingi, na aliogopa Doris angekuwa hivi

Alichukia sana hisia hii. Ilimfanya ajisikie dhaifu sana na hakuweza kufanya chochote isipokuwa kungoja ...

Angeweza tu kukubali matokeo, hata yale mabaya ...

Ghafla, chumba cha dharura kikasukumwa na nesi. Kendrick alisimama mara moja na kuuliza, "Binti yangu yuko vipi?"

"Wewe ni baba yake Doris?" Nesi akamtazama Kendrick ambaye aliitikia kwa kichwa. "Benki ya damu haina aina ya AB leo. Je, una marafiki au watu wa ukoo ambao wana aina sawa ya damu? Msichana anaihitaji.”

"Aina yangu ya damu ni AB. Unaweza kuchukua yangu.” Aina ya damu ya Kendrick ilitokea kuwa sawa na ya Doris. Familia ya Mayala ilikuwa ya aina ya damu ya AB.

Shati lake jeupe lililokuwa limetapakaa damu ya Doris, lilikuwa jeusi zaidi sasa, lakini bado lilikuwa la kutisha.

“Njoo nami.” Nesi alimpeleka Kendrick kwenye chumba cha kukusanyia damu. “Lakini mgonjwa bado anahitaji 600CC ya damu. Huwezi kufanya hivyo peke yako. Uliza mtu mwingine wa kuhamisha damu."

Chale alikuwa na wasiwasi juu ya Kendrick hivyo alimfuata, ili awe naye muda wowote.
Kendrick alikaa kwenye kiti kirefu, mikono yake ikiinuliwa juu ya viwiko vyake, ikionyesha mikono yake yenye nguvu.

Muuguzi alimfunga bomba la mpira, akaupa mkono wake dawa na kuusukuma sindano ndefu nyembamba kwenye mshipa wake wa damu wa bluu. Muuguzi alipotoa bomba la mpira, damu nyekundu iliyokolea ilitiririka kupitia mirija ya uwazi…

“Nesi, nichukue 600CC. Nahitaji tu binti yangu awe sawa.” Kendrick akamwambia nesi.

"400CC zaidi." Nesi alisema.

“Nina afya njema. Naweza kuchukua 600CC." Kendrick alipendekeza.

Nesi akamtazama kwa muda. "Sio nzuri kwako."

"Ichukue tu, na nitasaini kwamba haina uhusiano wowote na wewe." Kendrick alisisitiza, “600CC haitaniua hata hivyo. Maisha ya binti yangu ni muhimu zaidi kuliko yangu.”

"Bwana Mayala, nimezungumza na idara yetu ya rasilimali watu kuhusu hali hiyo. Ninakusanya watu wa kujitolea na nitakuwa hapa hivi karibuni.
Ninaelewa unataka kumwokoa binti yako, lakini huhitaji kujiweka hatarini. Maisha yako na ya Doris ni muhimu!”

"Nyamaza. Ninaweza kumuokoa binti yangu mwenyewe.” Kendrick akamkaripia.

"Bwana Mayala, usiwe hivyo… sijui jinsi ya kumweleza Mzee Francis.” Chale alihisi udhaifu miguuni mwake.

"Sihitaji kumwambia mtu yeyote kabla ya kumuokoa binti yangu." Kendrick akamwambia muuguzi, "Nitatia saini msamaha wa dhima."

"Bwana Mayala…” Chale alikuwa karibu kulia.

Chini ya msisitizo wa Kendrick, muuguzi angeweza tu kuchukua CC 600 nyingine. Alipendekeza Kendrick apumzike kitandani, lakini Kendrick hakutaka. Alitaka kubaki na Doris, lakini alishindwa hata kutembea na kuhisi kizunguzungu.

Chale alimsaidia Kendrick kukaa kwenye kiti kilichokuwa kando yake. Uso wake ulibadilika rangi kidogo, haswa midomo yake nyembamba.

"Bwana Mayala, kwa nini unapaswa kufanya hivi?" Chale alimtazama Kendrick na kuhisi kukasirika.

“Ni binti yangu. Nisipomwokoa, ni nani atakayemwokoa? Kendrick alifumba macho ili apumzike.

"Nimemwomba Masie akununulie uji wa lishe." Chale alinyamaza kisha akaongeza, “Itakuwa na manufaa kwa afya yako.”

Kendrick alinyanyuka taratibu baada ya kupumzika kwa muda mfupi. Bado alihisi kizunguzungu, lakini alijilazimisha kutembea.

"BwanaMayala, nina Katibu Masie pale. Tafadhali pumzika kidogo.” Paji la uso la Chale lilikunjamana, akionekana kuwa na wasiwasi.

“Uso wangu unaonekanaje? Mimi siwezi kufa.” Kendrick akasonga mbele. “Twende zetu.”

Chale alitaka kumsaidia Kendrick, lakini hakuthubutu, kwa kuhofia kwamba Kendrick angemkaripia. Lakini Kendrick alikuwa amechoka na jasho likimtoka kwenye paji la uso wake.

"Bwana Mayala, nitakusaidia hata ukinifukuza kazi.” Chale alijitolea kumsaidia Kendrick.

Kendrick alitaka kumsukuma, lakini akaacha kwa sababu ya yale Chale alikuwa amesema. Midomo yake myembamba ilinyanyuka kidogo na kumuegemea Chale.

Walipofika kwenye chumba cha dharura na kusubiri kwa muda, hatimaye Doris alitolewa nje.

Kendrick alifurahi sana hata akakaribia kuzimia aliposimama ghafla.

Sura ya 248

Kendrick akanyoosha mkono kushika ukuta. Chale alimnyanyua na kuonekana mwenye wasiwasi. "Bwana. Mayala, uko sawa? Je, ungependa kufanyiwa checkup?”

“Sijambo.” Kendrick alijiweka sawa, “Usifanye fujo.”

Chale alikuwa na wasiwasi tu kuhusu afya ya Kendrick. Afya yake ilihusiana na hatima ya Kampuni nzima ya Nyanza Gold, na familia ya Mayala pia ilimhitaji.

Francis Mayala alikuwa tayari amepoteza mwana bora, na kwa hakika hakutaka chochote kitokee kwa mwana huyu. Baada ya yote, ndiye pekee ambaye angeweza kubeba mzigo mzito wa Nyanza Group na familia ya Mayala.

Stefano Mayala alikuwa bado shuleni, mchanga sana na asiye na uzoefu.

“Nilisikia kuwa Bw. Mayala alichukua 600CC ya damu ili kumwokoa bintiye. Upendo huu wa baba unagusa, lakini afya pia ni muhimu sana.
Unaporudi nyumbani, lazima utunze afya yako vizuri na ule chakula chenye virutubisho zaidi.” Daktari alihisi Kendrick ni baba mwenye dhamana ambaye angejiumiza mwenyewe kuliko kuona mtoto wake anaumia.

“Daktari niko sawa. Vipi binti yangu?” Kendrick alishusha pumzi, akijaribu kupuuza kizunguzungu.

Daktari alianza kuzungumza juu ya Doris, “Kwa bahati nzuri, alipelekwa hospitalini kwa wakati, na ametiwa damu.
Mtoto yuko hatarini sasa. Kuhusu jeraha la paji la uso, lilishonwa nyuzi chache, na litapona.”

“Asante daktari.” Kendrick alisema. “Itaacha kovu?”

"Tuliishona kwa nyuzi nzuri sana, na kutakuwa na kovu ndogo, lakini iko kwenye paji la uso, ambayo bangs inaweza kuifunika.
Kando na hilo, kosmetology ya matibabu sasa imeendelezwa sana hivi kwamba inaweza kuondolewa," alicheka daktari.

“Vizuri.” Kendrick aliliweka hilo akilini, “Nitaenda kumuona binti yangu sasa hivi.”

Daktari akaitikia kwa kichwa. "Endelea."

Kendrick hakumwomba Chale amsaidie, bali alisisitiza kutembea hadi kwenye chumba cha faragha cha Doris.

Nesi alikuwa amemkagua na kumfunika. Nesi alipomuona Kendrick anakuja ndani ya wodi hiyo, alikuwa kwenye kizungumkuti.

Alishtushwa na sura nzuri ya Kendrick na ya kupendeza, lakini ilikuwa ni huruma kwamba mwanaume mwenye mvuto kama huyo alioa na kupata binti katika umri huo.

Japokuwa nesi alitaka kumuona Kendrick kwa muda mrefu, bado alitoka ndani ya chumba hicho na kuwaachia chumba kilichotulia.

Kendrick alimtazama Doris akiwa amelala kwenye kitanda cha hospitali huku akiwa amefumba macho yake vizuri. Hakuweza kuona macho yake yenye tabasamu kama zabibu, wala hakuweza kumsikia akimwita “Baba”. Uso wake ulikuwa mweupe kama karatasi kwa sababu alikuwa amepoteza damu nyingi sana, kama mdoli wa porcelaini ambaye angevunjwa kwa kuguswa.

"Bwana Mayala, kaa kitini." Chale akasogeza kiti nyuma ya Kendrick.

Kendrick alikaa chini lakini hakuwahi kumtolea macho Doris.

Chale alikuwa amesimama nyuma yake wakati wote. Masie alimkabidhi Chale uji wa lishe alionunua.

"Bwana Mayala, ulichukua damu nyingi sasa hivi. Kula chakula.”

"Sitaki kula." Kendrick alikuwa amejishughulisha na Doris kiasi kwamba alishindwa kula hadi alipomuona ameamka.

“Huwezi kustahimili. Nani atamtunza Doris ukiugua?” Ilibidi Chale amtumie Doris kumvuta Kendrick kula.

Kendrick alitazama nyuma na kulitazama lile bakuli la uji mkononi mwa Chale. Hakuwa na hamu kubwa ya kula na akasema, “Uweke chini sasa. Nitakula baadaye.”

"Bwana Mayala…”

“Ninakusikiliza au unanisikiliza?” Kendrick alimkodolea macho Chale yule mwongeaji.

Chale aliinamisha kichwa chake kidogo na kuonekana kaburi. "Bwana. Mayala, nina wasiwasi sana na wewe.”

“Sawa, nitakula.” Kendrick alielewa wema wa Chale, “Kwa kweli sina hamu ya kula sasa. Nitakula nikiwa na njaa.”

Chale kisha weka uji kando ya kitanda.

"Katibu Masie." Kendrick alimwita Masie.

Alisogea mbele na kuuliza, “Unahitaji nini, Bw. Mayala?”

“Ulimwomba nani amtunze Doris, na kwa nini aliumia?” Kendrick alitaka kujua nini kimetokea.

“Nilimwomba Jessie kutoka Idara ya secretary amtunze. Alisema alikuwa amemtembelea Doris mara kwa mara, lakini alikuwa na tumbo na akaenda msalani kwa muda mfupi… na ikawa hivyo.” Masie alieleza hali hiyo kwa urahisi, “Bw. Mayala, samahani, lakini uzembe wangu ndio uliomruhusu yule bibi mdogo

kuumia. Nitakubali adhabu.”

"Tutazungumza Doris atakapoamka." Kendrick alitaka kumuuliza Doris kuhusu hali hiyo kabla ya kufanya uamuzi. "Unaweza kurudi."

"Bwana Mayala ngoja nikae na wewe ili nikuhudumie. Na pia naweza kufanya shughuli mbalimbali.” Chale alitaka kumtunza Kendrick maana alikuwa ametoka kupoteza damu nyingi sana na sasa alikuwa mnyonge. Ikiwa kulikuwa na kitu kibaya kwa Kendrick, angejisikia hatia.

“Nitakaa pia.” Masie alisema.

“Chale atakaa. Unaweza kurudi.” Kendrick alinyoosha mkono kumshika Doris mkono, kisha simu ikaitwa.

Kendrick akatoa simu yake na kuona ni Tina anapiga. Kisha akakumbuka kwamba atlimuahidi kumkirimu kwa chakula cha jioni.
Doris alipoumia, alisahau yote.

“Kaka Kendrick...” Tina alimuita kwa utamu. “Umesahau kunikaribisha kwenye chakula cha jioni?”

"Tina, nina dharura kidogo kwa sasa, kwa hivyo lazima nishughulikie kwanza." Kendrick ilibidi abadilishe wakati.

"Nini? Kuna nini? Naweza kukusaidia?" Tina aliuliza kwa upole. Kweli, alijua ni kwa sababu ya Doris.

“Doris amejeruhiwa na yuko hospitalini. Lazima niwe pamoja naye.” Kendrick alisema ukweli na kukasirika.

“Doris aliumia? Je, hakuwa sawa nilipoondoka? Angewezaje kuumia? Je, ni mbaya? Sasa yukoje?” Tina aliuliza maswali mengi.

"Sijui aliumia vipi, lakini sasa hayuko hatarini, ingawa bado yuko kwenye kuzurai. Nitamuuliza nini kilitokea akiamka. Huna haja ya kuwa na wasiwasi.” Kendrick akahema kwa upole.

Tina, bila shaka, alikuwa na wasiwasi. Alikuwa na dhamiri mbaya, “Nimefarijika kwamba yuko nje ya hatari sasa. Kabula na mimi tutakuja hospitali mara moja."

“Huna haja ya kuja. Doris anahitaji amani na utulivu. Nitakaa naye tu.” Kendrick alikataa Tina kuja hapa, “Unaweza kula chakula cha jioni na Kabula. Nitakutendea kwa chakula cha jioni wakati ujao."

“Doris ameumia na anahitaji kampani yako sasa. Nipeleke kwa chakula cha jioni siku yoyote. Mimi na Kabula tutaenda hotelini kwanza,” Tina alisema, akijifanya kuwa mwenye akili timamu, “Usijali sana kuhusu hilo.”

“Vizuri. Kuwa mwangalifu." Kendrick kisha akakata simu.

Tina kisha akajisikia faraja. Kabula pembeni yake aliuliza haraka, “Tina, kaka yangu alisema nini? Anajua nilimsukuma Doris?”

"Kumbuka hukumsukuma Doris." Tiina akamwambia, " vinginevyo utajichanganya mwenyewe.

Sura ya 249

"Ndio, ndio, sikumsukuma." Kabula alitikisa kichwa sana, lakini bado alikuwa na hofu.

“Doris hajaamka. Kaka yako bado hajui lolote.” Tina aliweka simu yake chini na kumtazama Kabula. “Hata akiamka na kusema jambo, usikubali. Nitakusaidia nikiweza, Kabula. Lakini inabidi utulie, la sivyo tutateseka...

"Nitakutosa ikiwa hilo litatokea, Kabula, na usinilaumu kwa kufanya hivyo."

“Najua, Tina. nitafanya kile utakachosema.” Kabula akakunja mikono yake. “Kwa hiyo tunaweza kurudi kesho?”

Kwahiyo Kendrick angesikia lolote kutoka kwa Doris, angalau angekuwa amerudi Geita huku wazazi wake wakiwa wamemzunguka. Hilo lingekuwa bora kuliko kuwa peke yako katika Jiji la Mwanza huku akikabiliana na kaka yake.

"Na nilipendekeza kumtembelea Doris." Tina aliegemeza kidevu chake kwa mkono mmoja.

“Kwenda kwa… kumuona Doris?” Kabula aliogopa sana. “Tina, Doris angetuelekeza tunapoenda hospitali. Kendrick atamsikiliza na sisi tumehukumiwa. Sitamtembelea.”

“Umekosea.” Tina akatabasamu kwa siri, “Tukithubutu kwenda hospitali, ina maana hatuna hatia. Hata kama Doris anatuelekeza, hakuna uthibitisho. Nikiwa hapa, kaka yako hatakufanya lolote. Zaidi ya hayo, Bw. Francis na Bi Salome watakulinda. Wewe ni binti mkubwa wa familia ya Mayala. Unawezaje kukosa kujiamini kama kaka Kendrick?”

Kabula alishusha macho chini na kuonekana amepotea, “Tina, unajua sina undugu nao wa damu. Mimi ni binti wa kambo tu. Nipo kwa mgongo wa mama tu k vinginevyo mimi si mtu yeyote."

Macho yake yalikuwa yamelowa na huzuni. Ikiwa angeweza, angependa sana kuwa na uhusiano na Kendrick.

Hangeweza kumpenda juu zaidi, lakini angalau angeweza kuwa jamaa yake halisi, na angeweza kumpa upendo wa kweli.

Tina aliunyosha mkono wake na kusema kwa msamaha, “Kabula, samahani. Sikumaanisha hivyo. Nakutakia tu uwe na nguvu.”

“Naona. Sikulaumu. Kwa kweli ni kosa langu.” Kabula alimtazama Tina. "Ingekuwa vizuri kama ningekuwa mtulivu na kujiamini kama wewe."

“Haijalishi. Sipaswi kukulazimisha. Bado wewe ni mdogo.” Tina aliamua kutomlazimisha, “Uwe na uhakika, umenipata, na sitaruhusu mtu yeyote akudhuru.”

“Tina, umekuwa mzuri kwangu. Wewe ni kama dada yangu. Asante." Kabula alitabasamu kwake.
"Karibu, mimi niko upande wako." Tina alinyoosha mkono kumkumbatia Kabula.

Kabula aliegemeza kichwa chake kwenye bega lake, akijisikia salama na uhakika.

"Itakuwa vizuri kama kaka yangu angekuoa." Kabula akahema.

“Usivunjike moyo. Nitasubiri hadi kaka Kendrick ajue nimekuwa nikimsubiri.” Tina alijiamini. “Nina hakika ataelewa kuwa mwanamke huyo hafai. Na mimi ndiye anapaswa kuwa naye.”

"Tina, nipo nawe na ninasimama nawe kila wakati." Kwa macho ya Kabula, Tina alikuwa mwanamke bora ambaye angeweza kumsaidia Kendrick katika maisha na kazi.

Kendrick angemuoa Tina, angeweza kukata tamaa, lakini ilikuwa bora Kuliko kumuoa Alissa ambaye alikuwa na mtoto wa kike, hakuweza kukubali.

Kendrick pale hospitali alihisi Alissa ametoka kazini sasa. Ilibidi amwambie ukweli ili asije kumchukua Doris pale chekechea.

Mbali na hilo, alikuwa mama ya Doris na alikuwa na haki ya kujua kwamba binti yake alijeruhiwa na kulazwa hospitalini.

Kendrick akapiga namba ya Alissa na kusema, “Nimemchukua Doris.” Alissa alibana simu yake na kusema kwa sauti ya mbali, “Ulitaka kufanya nini? Kwa nini umemchukua Doris muda huu?”

“Una muda wa kufika hospitali ya Agha Khan? Tuko katika Chumba 601, idara ya kwanza ya wagonjwa wa kulazwa. Kendrick alimwambia tu mahali alipo sasa.

Moyo wa Alissa ukasisimka ghafla. "Nini tatizo?"

"Doris alijeruhiwa." Kendrick aliweza kusema ukweli tu.

“Aliumia vipi?” Alissa alimuuliza.

“Ni hadithi ndefu. Tafadhali njoo hospitali.” Kendrick aliongeza, "Kuwa makini barabarani."

Alissa alisema atafika mara moja na kukata simu.

Kendrick alimtazama Doris na kuomba kimoyomoyo aamke upesi.

Muda si mrefu, Alissa alifika chumba namba 601. Alisukuma mlango na kwenda kwa Kendrick.

Alimtazama Doris akiwa amelala bila uhai katika kitanda cha hospitali na kumuuliza, “Kwa nini Doris aliumia?”

“Ni kosa langu, Alissa. Ni kosa langu kwa kutomtunza vizuri.” Kendrick alisimama huku akijilaumu.

Macho ya Alissa yakawa mekundu. “Alikuwa akifanya vizuri shuleni. Kwa nini ulimchukua? Kwa kuwa huwezi kumtunza, kwa nini umemchukua!”

"Samahani." Kendrick hakuwahi kuomba msamaha kwa mtu yeyote, lakini sasa aliinamisha kichwa chake kizuri.

Na huyu alikuwa Alissa, mke wake, mwanamke aliyempenda, mama wa binti yake, kwa hiyo hakuwa na aibu, na hata alifikiri kwamba kuomba msamaha haitoshi.

"Je kuomba msamaha kunasaidia? Je, muda unaweza kurudi na unaweza kumruhusu Doris asiumie?” Pua ya Alissa ilikuwa inauma na kooni kulikuwa na uvimbe. Alisema kwa sauti iliyokabwa, “Unajua msemo kama si mtoto wako, hautahuzunika. Kwa sababu Doris si binti yako, hutajali!”

"Nani alisema kuwa yeye sio binti yangu?" Kendrick alijibu huku akikunja nyusi zake ndefu jambo ambalo lilimfanya Alissa ashangae.

Aliuma midomo yake myembamba kisha akasema, “Siku zote mimi humtendea Doris kama binti yangu mwenyewe. Inaniuma ninapomwona akiumizwa. Je, huoni maneno yako ni makali sana?”

“Kendrick, najua una kinyongo na mimi, lakini unaweza kutoa hasira zako kwangu. Kwanini unamuumiza Doris? Yeye ni mdogo sana; unawezaje kustahimili kufanya hivyo?" Alissa aliuma mdomo na kuendelea kumtazama kwa macho mekundu. “Sikubali msamaha wako!”

“Tulia Alissa. Najua inakuuma wewe pia, lakini mimi si bora kuliko wewe. Ningetamani sana yule atakayeumia ningekuwa mimi, si yeye!” Kendrick alimuangalia Alissa aliyekuwa akijaribu kuyazuia machozi yake na kuhisi uchungu zaidi moyoni mwake.

"Daktari alisema Doris yuko nje ya hatari. Ataweza kuamka. Tutamtazama pamoja hadi atakapoamka.”

Alissa aliogopa sana kumwona Doris mdogo akiwa amelala akiwa amejeruhiwa. Hakuweza kutulia, na hata kuchafukwa. Alimuuliza kwa ukali, "Atakuwa sawa? Hujui jinsi ilivyo ngumu! Kendrick, sitaki kukuona. Tafadhali nenda nje sasa hivi!”

“Alissa...” Kendrick alimshika bega ili kumtuliza, lakini hakutarajia Alissa angefanya hivyo…

Sura ya 250

Alissa hakutaka Kendrick amguse, hivyo kwa silika alimsukuma mbali. Kendrick alikuwa bado na kizunguzingu kutokana na udhaifu wa kutolewa damu. Kutokana na hali hiyo, Kendrick alianguka chini na kugonga kiti kilichokuwa nyuma yake.

Alissa alipigwa na butwaa . Hakutegemea kuwa Kendrick ataanguka chini. Macho yake yalimtoka kwa mshtuko.

Alitazama mikono yake akiwa haamini. Hakumsukuma kwa nguvu. Je, mtu mwenye nguvu kama Kendrick angewezaje kuanguka chini?

Alipofungua mlango, uso wa Chale ulibadilika rangi baada ya kumuona Kendrick akiwa chini.

Akaharakisha kumsaidia Kendrick kunyanyuka. Lakini Kendrick alimkataa, "Nitafanya mwenyewe."

"Kendrick, acha kuigiza." Alissa aliweza kufikiria hivyo tu. Vinginevyo, kwa nguvu za mwili za Kendrick, hangeweza kumsukuma chini.

Kendrick alishusha pumzi ndefu na kunyoosha mkono wake kushika kiti ili asimame.

"Kendrick, unajaribu kunitisha?" Alissa alimtazama Kendrick aliyesimama mbele yake, shati lake jeupe likiwa na damu. “Unadhani sitakulaumu kwa kunifanya nijisikie mwenye hatia?”

“Unaweza kunipiga unavyotaka, kunikaripia au kitu kingine chochote. Sina malalamiko.” Kendrick alizitazama kope zake zilizokuwa zimejaa machozi.

“Kuna manufaa gani kufanya hayo!” Alissa akainua midomo yake na kutazama pembeni, lakini alishindwa kuyazuia machozi yasidondoke chini.

Kwa ukaidi alinyanyua mkono wake na kuufuta, hakutaka kuwaruhusu wengine wamuone akitoa machozi.

Chale alikasirika kuona wana ugomvi hasa pale alipoona Kendrick anadhulumiwa.

"Bi. Mayala, humwelewi Bw. Mayala. Jeraha la Doris halikusababishwa na Bw. Mayala.” Chale akaona Kendrick hana nia ya kujieleza. Ilibidi achukue hatua na kuwa mtunza amani.

"Alifanya hivyo kwa njia isiyo ya moja kwa moja." Alissa kwa ukaidi aliamini kuumia kwa Doris kuna uhusiano na Kendrick. "Kama asingemchukua na kumwacha peke yake ofisini, hili lisingefanyika...

“Mimi ni mamake Doris, na nimefanya bidii kumlea tangu tangu utotoni. Nampenda na sitaki aumie. Inaniuma mara kumi kama inavyomuumiza. Je, unaweza kuhisi? Usinishauri niwe mkarimu kwani wewe hujapitia niliyopitia!”

Alissa alifikiria kile alichoteseka nacho na kwa nini Doris alikuja katika ulimwengu huu… alikuwa na deni lake. Alikuwa na deni la mtoto huyo maisha yake yote.

"Bi. Mayala, unamwelewa vibaya sana Bw. Mayala. Bw. Mayala alimchukua Doris kutoka shule ya chekechea kwa shughuli fulani kisha akamwomba acheze naye, lakini…”

"Sawa, Chale, ondoka hapa." Kendrick akamkata. "Hii ni kati yetu, kwa hivyo usiingilie hii."

"Bwana Mayala, kuna kitu lazima nimwambie Bi. Mayala.” Chale hakuguswa na kuendelea, “Doris alitaka kwenda kwa ofisi ya Bw. Mayala na kwenda kufanya kazi na baba yake. Doris ni msichana mwerevu, na hakutaka kusumbua kazi ya Bw. Mayala.”

"Bwana Mayala alimtunza vizuri Doris mwenyewe alipoenda ofisini. Lakini kulikuwa na mkutano muhimu mchana, hivyo akamwomba katibu amtunze. Lakini sekretari alishikwa na tumbo la kuhara na akaenda chooni. Na ajali ilitokea wakati huo!"

"Bwana Mayala alikasirika sana akatamani kuua watu alipoona Doris anaumia. Tulimkimbiza Doris hospitalini, lakini Doris alipoteza damu nyingi. Hospitali ilikuwa ikihitaji aina ya damu ya Doris na Bw. Mayala alichukua 600CC ya damu na kumpa Doris.”

"Mtu anaweza tu kutoa 400CC na si zaidi, lakini ili kuokoa Doris, Bw. Mayala alisisitiza kutolewa 600CC bila kujali ushauri wa muuguzi. Kutokwa na damu nyingi kulimfanya Bw. Mayala apate kizunguzungu, hivyo Bibi Mayala, hukutumia nguvu nyingi kumsukuma Bw.
Mayala, lakini alianguka.”

"Bi. Mayala, Bw. Mayala aliweka maisha ya Doris kuwa muhimu zaidi kuliko maisha yake. Hakunywa maji tangu Doris alipoumia. Daktari alimshauri apate chakula cha virutubishi, lakini alikuwa bado hajala uji wa lishe aliopewa na Masie...

"Anampenda Doris kama wewe, lakini ulimshtaki vikali. Si haki kwa Bw. Mayala!” Chale kisha akahitimisha, “Anampenda sana Doris, na kwa kweli hii ni ajali tu. Hatukutaka itokee, lakini ilitokea, na tunachopaswa kufanya sasa ni kuboresha hali ya Doris haraka iwezekanavyo...

"Ni hayo tu, nilotaka kusema.” Chale alimtazama Kendrick, “Bw. Mayala, nitakuwa nje. Ikiwa unahitaji chochote, niite tu."

Kendrick aliitikia kwa kichwa na kumtazama Chale akigeuka kuondoka.

Baada ya Chale kumaliza kuongea, Alissa na Kendrick hawakuzungumza kwa dakika kadhaa. Chumba kilikuwa kimya sana na hata tone la maji lilisikika.

Alissa alimpa mgongo Kendrick, ambaye aliendelea kumtazama mgongo wake ulionyooka na mwembamba.

Kendrick kisha akamsogelea Alissa kwa upole na kusimama nyuma yake na kumfunga mikononi mwake.

Alissa alihisi kuwa ameangukia kwenye kumbatio la joto na dhabiti. Alishusha tu kope zake na kuyafunika macho yake yenye nyota bila kukataa wala kuhangaika.

Alissa hakuweza kukataa kuwa alichosema Chale kilimgusa sana, hasa pale Kendrick alipohamisha damu yake kwa Doris… Alihisi moyo wake usiotulia ukitulia hatimaye.

Kendrick alipoona hakumsukuma alitabasamu kwa kuridhika na kusema, “Alissa, mimi ndiye ninahusika na jeraha la Doris. Samahani kwamba sikumtunza vizuri.”

Msamaha wake wa dhati ukakaa masikioni mwake. Alissa alipotulia, hakuwa mtu wa kubagua au asiye na akili.

“Mimi ndiye niliyepaswa kuomba msamaha. Nilikuwa na msukumo sasa hivi. Najua jinsi unavyompenda Doris, na sikupaswa kukuumiza kwa maneno haya makali.” Alissa alifikiri kwamba alikuwa amemsukuma Kendrick, ambaye alikuwa ametoka tu kuchukua 600CC ya damu, na alijichukia sana kwa kutokuwa na akili.

“Haijalishi. Bi. Mayala ana kila fursa mbele ya Bw. Mayala.” Kendrick alimshika mikono na kuegemeza kidevu chake begani.
“Doris ameumia, na mko karibu sana, kwa hiyo inaeleweka kwa nini una hasira. Sikulaumu wewe.”

Jibu la upole na ukarimu la Kendrick lilimfanya Alissa ajisikie mwenye hatia zaidi na hakuweza kusema chochote.

"Lazima imekuumiza baada ya kuhamisha damu nyingi." Macho ya Alissa yakatua kwenye mkono wake.

"Mimi ni mwanaume. Haijalishi kuhamisha damu kidogo sana.” Kendrick hakujali hilo.

“Unafikiri wewe ni Mungu? Usijifanye kuwa na nguvu. Ikiwa uko sawa kabisa, usingeanguka chini nilipokusukuma kidogo tu” Alissa kwa haraka akaushusha mkono wake, akageuka na kumtazama juu na chini. “Umeumia?”
 
USINIACHE 4:
Sura ya 196

Melissa angeweza tu kuruhusu Maira kupata haki kwa ajili yake. Vinginevyo, hangeweza kuiruhusu iende kwa urahisi.

“Kukupiga kwangu hakuna uhusiano wowote na Maira. Ni kati yetu. Sisi sote ni watu wazima na tunaweza kulitatua sisi wenyewe.” Alissa alikuwa na sura yenye nguvu na alikuwa makini.

“Alissa, si unatumia tu uwezo wa bwana Kendrick? Kwa nini usijitegemee?” Melissa alimwonea wivu Alissa kwa kuwa na bahati sana. Hakuwahi kufikiria kuwa baada ya kuachana na Seidrick, Alissa angeweza kuolewa na Kendrick.

Ilikuwa ni kuudhi sana kwamba Alissa alikuwa na sifa mbaya na mtoto na bado aliweza kuwa Bi Mayala.

“Ni mume wangu. Kuna ubaya gani mimi kutumia nguvu za mume wangu? Sijali kutumia uwezo wa mumeo, kama unaweza kufanya hivyo.” Alissa aliweka tabasamu zuri, lakini macho yake yalikuwa baridi na makali, “Melissa, nakuambia, sijali unataka kunifanyia nini. Lakini binti yangu ndiye msingi wangu. Ukithubutu kupima kikomo changu, sitakuacha uende kamwe!”

“Nilichosema ni ukweli tu!” Melissa bado alikuwa mkaidi na kusitasita kukiri makosa, “Je, nilisema jambo baya?”

“Acheni!” Maira alikunja kipaji na hakuweza kusikiliza maneno ya Melissa tena, “Melissa, ni ufidhuli kwako kuzungumza hivi. Alissa ni dada yako na Doris ni sawa na binti yako. Wewe pia utakuwa mama hivi karibuni. Je, huwezi kuwa mwadilifu kwa mtoto wako?”

Melissa alipepesa macho kwa wepesi na machozi yalitiririka kwenye mashavu yake mazuri, “Tangu alipoondoka na kumsaliti Seidrick nyuma, hakuwa dada yangu tena. Sitakubali kuwa mtu ambaye hana dhamiri bila kujali usalama wa Seidrick. Ni dada yangu. Seidrick ndiye aliyeokoa maisha yake wakati huo. Lakini yeye alifanya nini?

“Mama vipi bado unamlinda hivyo? Najua umempendelea Alissa kila wakati. Kwa hiyo unataka achukue nafasi yangu kama mkwe wako?"

Maira alidhihaki.,“acha kuwaza hayo matamanio. Ameolewa na Bwana Kendrick, mtu mwenye nguvu na tajiri. Unafikiri bado atakuwa tayari kuolewa katika familia ya Masolwa?"

"Mimi ndiye pekee ninayempenda Seidrick. Alissa hastahili hata kidogo!”

“Ndiyo sikatai kuwa nampendelea Alissa. Ingawa hawezi kuwa binti-mkwe wangu, ninaweza kumchukulia kama binti yangu. Je, hivyo pia ni shida?

“Na tangu uolewe na Seidrick, nimekutambua kutoka moyoni mwangu kama binti-mkwe wangu. Pia nilifanya wajibu wangu kama mama mkwe. Sikukuacha uteseke katika familia ya Masolwa na siku zote niliomba Seidrick akujali zaidi na kuongozana nawe.

"Naona jinsi ulivyo mzuri kwa Seidrick. Na sasa una mimba ya mtoto wa Seidrick. Baba yako, dada yako, Seidrick na mimi sote tunakushukuru kwa dhati. Tunajaribu tuwezavyo kukuridhisha. Chunguza dhamiri yako mwenyewe. Je, nimewahi kukutendea vibaya katika kipindi cha miaka mitano hivi hivi?”

Melissa alijua kuwa familia ya Masolwa ilikuwa nzuri na alikuwa na bahati ya kuolewa na Seidrick. Lakini Alissa alipotokea, Melissa alihisi angeachwa na kubadilishwa.

Alipoingia tu na kuona kwamba walikuwa karibu kama familia, alishtuka.
Hakuweza kumruhusu Alissa amchukue mtu yeyote kutoka kwake. Hangeruhusu!

“Mama, hamjanitendea vibaya. Lakini Alissa aliwahi kuwa mchumba wa Seidrick, na mimi ni mke halali wa Seidrick sasa. Unanifanya nijisikie vipi wakati uko karibu naye? Je, unaweza kuzuia hisia zangu?” Melissa alilipapasa tumbo lake bapa, “Hata kama ni kwa ajili ya mjukuu wako.”

“Nilizimia jana na Alissa akanipeleka hospitali. Yeye ndiye mfadhili wangu. Kama binti-mkwe wangu, baada ya kuingia, haukumshukuru tu, bali pia ulipiga kelele na kuzungumza kwa jeuri. Umefikiria juu ya mtoto wako?" Maira ilikuwa mbaya sana.

"Mama, kwa neno moja, hunipendi tena kwa sababu amerudi, sawa?" Melissa aliuma midomo yake, macho yake yakiwa yamejaa machozi na chuki.

"Hapana." Maira akatikisa kichwa, “Nyinyi ni dada. Kwa nini hamuelewani?”

"Kuelewana?" Melissa alidhihaki, “Unaweza kumuuliza ikiwa anataka kuishi pamoja nami vizuri! Bado anampenda Seidrick."

“Alissa ameolewa na Kendrick. Haifai kwako kusema maneno kama haya. Huku si tu kuwatukana Alissa na Seidrick, bali pia kujidhalilisha wewe mwenyewe!” Maira alifikiri kwamba Melissa alikuwa mkaidi sana, “Wewe ni mke wa Seidrick. Humwamini hata kidogo? Basi kwa nini mnaweza kuwa pamoja? Jambo la msingi sana kumpenda mtu ni uaminifu na heshima. Ikiwa huwezi hata kufanya hivyo, unampenda Seidrick kweli?

Melissa alinyamazishwa tena na swali la Maira, “Mama, unatilia shaka mapenzi yangu kwa Seidrick? Ikiwa sikumpenda, nisingekubali pendekezo lake muda mfupi tu baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini. Hata sikujali kama ningeweza kupata watoto naye… nilijitolea sana kwa ajili yake. Lakini sasa, bado unadhani simpendi…

“Halafu unadhani Alissa anampenda Seidrick? Ikiwa ni hivyo, angekuwa amefanya kitu kumsaliti Seidrick!” Melissa alimnyooshea kidole Alissa kwa hasira.

Hakukata tamaa kwa kuwa siku zote kuna watu wanamlinda na kumsaidia Alissa, huku yeye mwenyewe akitegemea juhudi zake za kupigania kila kitu, “Kwa kuwa unaniona hivi mama, basi bora nitoe mimba ya huyu mtoto tumboni mwangu…”

Melissa alifumba macho taratibu kwa maumivu na kugeuka kuondoka. Maira alimwita, “Melissa, huyu ni mtoto wako na wa Seidrick. Unawezaje kuwa mtu asiye na maana sana?”

"Mimi si kitu katika familia ya Masolwa, achilia mbali yeye. Hata akizaliwa hatathaminiwa.” Melissa hakukaa tena akaondoka bila kuangalia nyuma.

Maira alikunja uso, akafumba macho na kushika shuka kwa nguvu.

Kisha akainua shuka na kutoka kitandani. Wakati Melissa akivuta mpini wa mlango, aliushika mkono wa Melissa, “Melissa, huwezi kufanya hivi. Mtoto hana hatia.”

Huyu alikuwa mtoto oekee wa Seidrick. Seidrick alikuwa naye kwa shida. Asingeweza tu kumtazama Melissa akimtoa mtoto.

“Basi mimi nina hatia?” Melissa aliuliza kwa kejeli.

Kwa kweli, Melissa alijivunia ndani. Alikuwa akiweka dau kwamba Maira alimjali mtoto na hangemruhusu atoe mimba kwa urahisi.

“Alissa ameolewa na Kendrick. Hana sababu ya kuwa na uhusiano wowote na Seidrick. Hakuwezi kuwa na chochote kati yao! Niamini." Maira alimsihi kwa uhakika, macho yake yalijazwa na usafi.

“Kwa nini nikuamini?” Melissa alimtazama pembeni Alissa aliyekuwa amesimama pale.

"Melissa, usiwe na akili mbovu!" Alipoona Maira akiongea kwa unyenyekevu kwa ajili ya hili, Alissa alishindwa kuvumilia, “Usijali, sawa? Ninawezaje kuachana na Kendrick na kuwa na uhusiano na Bwana Seidrick? Mimi, Alissa, najua kabisa ninachotaka!”

"Hii ni biashara ya familia yetu. Haina uhusiano wowote na wewe!” Melissa alimtenga Alissa.

“Kwa hiyo unataka nini?” Maira alijua Melissa alikuwa na masharti.

Sura ya 197

Maira angeweza tu kufanya maelewano kwa ajili ya mtoto, wakati Melissa alitegemea mtoto huyu na alikuwa na kiburi.

Alissa kwa upande wake alikuwa mtulivu sana akiwaza tu kwamba Seidrick hapaswi kumuona Melissa namna hii. Ikiwa Seidrick angejua kwamba Melissa alikuwa akimdharau mama yake mpendwa, ingekuwaje?

“Mama niahidi kuwa hutakutana na Alissa siku zijazo. Hata ikiwa utakutana naye, unapaswa kuondoka mara moja na ukae mbali naye iwezekanavyo. Vinginevyo, sitakuwa mzuri kama nilivyo leo. Melissa alicheka baada ya kusema masharti yake, "Mama, nadhani unaweza kufanya hivyo kwa ajili ya mjukuu wako."

"Pia, Hii inaweza tu kujulikana na sisi katika wodi hii. Ikiwa mtu mwingine yeyote atajua kuhusu hilo, ninaweza kufanya lolote nikiwa sina furaha.” Akautazama mkono wake uliokuwa ukilipapasa tumbo lake.

Ilikuwa dhahiri kwamba Melissa alikuwa akimtishia Maira. Lakini Maira hakuweza kufanya lolote kwa sababu alitishiwa.

Kuona Melissa akienda mbali, Alissa alihuzunika kwa Maira.

Alissa alichukua hatua chache mbele, akapuuza sura ya Melissa ya uvivu, na kumwambia Maira, “Maira…”

"Huo ni mwito wa upendo sana. Alissa, unawezaje kumwita mama yangu hivi?” Melissa alikoroma, akitafuta shida kwa makusudi.

“Maira, nadhani kwa kweli haifai sisi kuonana tena. Kwa hivyo, sitakusumbua tena katika siku zijazo. Jitunze tu. Natumai utapona hivi karibuni.” Alissa alichukua hatua ya kuweka mawazo yake wazi mbele ya Melissa, na hakutaka kumuaibisha Maira.

Maira pia alielewa nia ya Alissa. Alissa alikuwa akichukua hatua ya kumweka waziwazi ili afanye uamuzi.

"Doris, twende." Alissa alimpungia mkono Doris aje.

Doris alinyanyuka na kuushika mkono wa Alissa.

“Huwezi kwenda sasa hivi.” Melissa alizuia njia yake, "Ulichosema sio kile alichosema. Kwa hivyo, lazima aseme mara moja."

"Melissa, usiende mbali sana." Alissa alikunja uso.

“Naenda mbali sana? Ninafanya hivi kwa manufaa ya mama.” Melissa alisema kwa kujiamini sana, “Itakuwaje awe karibu na mwanamke ambaye amemsaliti na kumuumiza mwanae? Je, amewahi kufikiria kuhusu mwanawe mwenyewe? Hawezi kutofautisha kati ya adui na watu walio upande wake! Alissa, hii ni biashara ya familia yetu. Unaingilia kati kwa uwezo gani?"

Kwa kweli Alissa hakuwa katika nafasi ya kuingilia masuala ya familia ya Masolwa, "Inaonekana kwamba baadhi ya mambo yanaweza tu kuamuliwa mbele ya wazazi wetu unaporudi nyumbani kwa Maziku."

"Unamaanisha nini?" Macho ya Melissa kisha yakaangaza kwa woga.

Timothy alikuwa ameshughulikiwa na Kendrick. Melissa hakuwa amerudi kwa familia ya Maziku katika kipindi hiki cha wakati na alikuwa akikaa katika familia ya Masolwa, ili asikutane na Alissa.

Alifikiri angekuwa salama ikiwa angejificha. Bila kutarajia, bado alikutana na Alissa hapa.
Popote alipokuwa Alissa, Melissa alihisi woga na hasira.

Maira akashusha pumzi ndefu, “Sawa. Acha kuongea. Ninakuahidi kuwa sitakutana tena na Alissa na nitaondoka mara moja nitakapomuona. Je, ni sawa?”

Maira alikunja uso, hakutaka Melissa awe mkaidi na asimwandame Alissa.

Leo, Maira aliona wazi kwamba tabia zote mbovu za Melissa zilifichwa. Lakini Seidrick bado iliwekwa gizani.

"Mama, tafadhali kumbuka ulichosema leo na ufanye, au kutakuwa na malipo." Melissa alimtazama Alissa kwa sura ya ushindi.

“Melissa, wewe bado ni binadamu? Unawezaje kuwatendea wazee wako hivi? Hata ni mama wa mwanaume unayempenda! Je! Seidrick anafahamu sura yako halisi?" Alissa alimtazama Maira ambaye alikuwa mgonjwa na mwenye huzuni, na hakuweza kujizuia tu kutaka kuingiza pua yake kwenye biashara yao.

“Mimi ni binti-mkwe wa familia ya Masolwa na mwokozi wa Seidrick. Wote wanapaswa kunishukuru.” Melissa alidhani alikuwa shujaa wa familia ya Masolwa, na kwamba walikuwa na deni kubwa la shukrani kwake.

Alissa alitikisa kichwa kwa tabasamu baridi, “Melissa, unadai kuwa ulikuwa mwokozi wa Seidrick. Kwa hiyo una ushahidi gani?"

“Nilimpa daktari damu ya kitovu na ikaokoa maisha ya Seidrick. Huo ndio uthibitisho.” Melissa alidanganya kwa uso ulionyooka.

Alikuwa amechukua mchango wa Alissa kwa Seidrick miaka mitano iliyopita. Angewezaje kukiri kwamba alikuwa akidanganya?

“Daktari yuko wapi?” Alissa aliendelea kumuuliza.

"Sijui." Melissa alionekana kukosa subira kidogo.

"Mpigieni na tutamuuliza ana kwa ana ili kuthibitisha damu ya kitovu ni ya nani." Alissa alitabasamu kwa utulivu na kumtazama Melissa, ambaye alikuwa na hatia kidogo.

"Hata hivyo sio yako." Melissa aliuma meno na kukana.

"Hiyo si lazima iwe kweli." Alissa alimtazama Doris kwa macho laini.

"Acha kuongea ujinga hapa." Melissa alimkazia macho Alissa ambaye alikuwa akimtafutia shida.

Akisikiliza mazungumzo yao, Maira alifikiri kuna kitu kibaya. Kwa hiyo, aliuliza, “Melissa, je, damu ya kitovu ni ya nani? Uliipata wapi?"

Wakati huo, Seidrick alikuwa mgonjwa na afya yake ilikuwa mbaya zaidi. Hawakuweza kupata mechi ya uboho. Daktari alisema kwamba wangeweza tu kusubiri.

Lakini wakati Seidrick alikuwa katika hatari kubwa, Melissa aliwapa matumaini, akisema kwamba amepata damu ya kitovu. Kila mtu alikuwa amezama katika furaha ya wokovu wa Seidrick na hawakuingia ndani ya kile kilichotokea.

Walitaka kumshukuru mfadhili. Lakini Melissa alikataa kwa madai kuwa mfadhili huyo hakutaka wengine wamjue yeye ni nani.
Kisha wakampa Melissa milioni 2 ili ampe mfadhili huyo kumshukuru.

Kisha wangejitayarisha kwa ajili ya zawadi na kumwomba Melissa ampe mtoaji kila mwaka kama ishara ya uthamini wao.

Hadi sasa, walikuwa hawajawahi kukutana na mtu huyo. Kila walipotaja suala la mfadhili, Melissa alikuwa akibadilisha mada ya mazungumzo.
Sasa baada ya Alissa kutaja, Maira alihisi mashaka.

"Mama, haijalishi nimeipata wapi, ni sawa kwamba Seidrick ni mzima sasa." Melissa akanyamaza na kuongeza, “Mama, unamwamini yeye au mimi? Tafadhali kumbuka kuwa mimi ni mke wa Seidrick! Hata hivyo sitamuumiza Seidrick.”

“Lakini…” Maira hakuwa na shaka na hisia za Melissa kwa Seidrick, lakini tabia yake.

“Hapana, lakini Kila kitu ninachofanya ni kwa manufaa ya Seidrick.” Melissa alikatiza harakati za Maira, “Mama, jitunze. Nitakuona wakati ujao.
Na wewe Alissa, fanya haraka uondoke hapa!”

Hakutaka kushikwa na Maira hapa. Alissa akiwa karibu, Melissa aliogopa sana.

Melissa kisha akaufungua mlango na kuondoka kwa haraka.

Maira alisimama pale, akili yake ikiwa katika msukosuko.

"Maira, usifikirie sana. Afya yako ni muhimu zaidi." Alissa alimshikilia Maira, “Nitakusaidia kulala kitandani.” Maira alilala juu ya kitanda. Uso wake ulikuwa wa rangi na wenye huzuni sana.

"Maira, nitaondoka sasa. Jitunze vizuri.”

Lakini Maira akamshika mkono, “Alissa, unajua nini kuhusu mfadhili?”

Sura ya 198

Alissa aliweka mkono wake mwingine nyuma ya mkono wa Maira na kuupapasa kidogo, akimtuliza, “Maira, mambo fulani lazima yasemwe kwa wakati ufaao. Chochote ninachojua, si wakati mwafaka sasa.”

"Hiyo inamaanisha unajua hadithi ya ndani." Macho ya Maira yaliangaza na akasema kwa matumaini.

"Sijui." Alissa alikanusha.

Maira alikuwa mama yake Seidrick. Ikiwa Maira angezungumza na Seidrick kuhusu kile kilichotokea siku hiyo, Alissa aliogopa tu kwamba Seidrick angemshuku kuwa na nia mbaya.

Na hakuwa amepata ushahidi bora na wa moja kwa moja wa kuthibitisha hilo kwa wakati huo.

Ilibidi Alissa atafute ushahidi wa chuma ili kumfanya Melissa ashindwe kusema na kushindwa kugeuka. Vinginevyo, ikiwa Melissa angerejea, angemshambulia kwa kulipiza kisasi.

Macho ya Maira, ambayo yalikuwa na mng'aro wa furaha, yakawa na huzuni.
Alissa hakutaka kusema lolote baya kuhusu Melissa. Baada ya yote, hakukuwa na watu wengi ambao walimwamini sasa.

Hakutaka kujiingiza katika jambo fulani. Hasa, Seidrick alikuwa ikimlinda sana Melissa. Zaidi ya hayo, Melissa sasa alikuwa na ujauzito wa mtoto wa Seidrick na akawa muhimu kwake.

Huu haukuwa wakati mzuri wa kumwangusha Melissa.

Alissa sasa alikuwa kama mwindaji ambaye alikuwa akingojea fursa ya kutoa pigo mbaya wakati mawindo yalikuwa yamepumzika zaidi na kujisahau.

Kwa wakati huu, mlango wa wodi ulisukumwa wazi kutoka nje. Walikuwa ni Seidrick, Alaya na Jasmin walioingia pamoja.

Walishangaa kidogo kumuona Maira akiwa amemshika Alissa mkono.

Alissa alirudisha mkono wake, “Bi. Masolwa, kwaheri."

Alissa alimchukua Doris na kuwa karibu kuondoka. Maira alimwambia Seidrick ambaye aliganda, "Seidrick, muone Alissa."

Seidrick hakusogea, akifikiri kwamba aepuke mashaka kwa sababu ya hali kati yao. Alisita kidogo kumuona Alissa.

Alaya na Seidrick walikuwa karibu zaidi na waliweza kuona kile ambacho kaka yake alikuwa akiwaza. Kwa hivyo, alitabasamu na kuweka maua mikononi mwake, "Mama, niruhusu nifanye. Nina kitu cha kuzungumza na Alissa tu.”

Kwa hayo, Alaya alitoka wodini na Alissa na kumpeleka kwenye maegesho.

"Alissa, asante kwa kumuokoa mama yangu. Sijali ulichomfanyia Seidrick hapo awali. Lakini natumai hutakuja karibu na mama yangu tena.
Baada ya yote, Melissa na Seidrick tayari wameoana na wewe pia umeolewa. Kwa hiyo, jihadhari.” Alaya alifikiria kwa muda ikabidi aseme alichokuwa anakiwaza.

“Alaya, umesema kweli. Najua la kufanya.” Alissa alielewa mara tu aliposikia, "Sitamsumbua Maira katika siku zijazo."

"Asante." Alaya aligeuka ili kurudi wodi, "Jihadhari."

Alissa aliitikia kwa kichwa na kumpeleka Doris kwenye gari ili kuondoka.

Walipokuwa wakielekea kwenye gari, Doris alimvuta mkono Alissa, “Mama, usihuzunike.”

"Kwa nini niwe na huzuni?" Alissa alimtazama mtoto wake mdogo.

“Wote hawakupendi. Lakini ninakupenda, na Baba, Nora, na Jane wote wanakupenda. hiyo inatosha. Wengine wote ni watu wasio na umuhimu.
Kwa hiyo, usifadhaike kwa sababu ya wale wasiyo muhimu.” Doris alisema kwa njia ya busara.

Alissa alichuchumaa na kuweka mikono yake kwenye mabega ya Doris, “Umesema kweli. Lakini mama hajakasirika hata kidogo. Kwa sababu mama hawapendi pia."

Doris alifunika mdomo wake kwa mikono yake na kutabasamu, akitoa ishara ya dole gumba.

“Turudi.”

Alissa alipokuwa anakaribia kuinuka, aliona watu wawili waliowafahamu wakikwepa kwenye lango la usalama.

Alifungua mlango wa gari, akamwomba Doris aketi ndani, na kusema, “Doris, msubiri mama kwa dakika chache kwenye gari. Msichana mzuri, usiseme chochote. Narudi muda si mrefu."

"Sawa." Doris hakuuliza kwa nini na alishirikiana kwa utii.

Alijua kwamba lazima mama yake awe na jambo fulani muhimu la kufanya. Ndio maana alimuacha hapa.

Alichopaswa kufanya ni kumngoja mama yake kwa utiifu na sio kufanya fujo.

Alissa alifunga gari kisha akajipenyeza hadi kwenye mlango wa usalama.

Alijibanza ukutani na taratibu akalisogelea lile jopo baridi la mlango wa chuma kigumu huku akilibana sikio lake kwa nguvu ili kujaribu kusikiliza mazungumzo ya mle ndani.

Hakika ilisikika sauti ya mazungumzo kati ya watu wawili.

“Timothy, unaweza kutulia na kunisikiliza?” ilikuwa ni sauti ya Melissa yenye sauti ya kuomba. Alikuwa tofauti kabisa na mwanamke mwenye kiburi katika wodi ya Maira hivi sasa.

"Melissa, ikiwa ungekuwa kama hivi nilivyo sasa, ungeweza kutulia?" Timothy alikasirika, “Kwa kuwa nimemkosea Kendrick, sasa nimefukuzwa nyadhifa zote na wakurugenzi. Wananilazimisha hata kutoa hisa zangu. Sasa sina chochote!

"Na hii yote ni kwa sababu yako! Usingeweka habari za uongo kuwa Alissa ni hawara kwenye ndoa ya Kendrick, nisingeomba mtu apekeke zile picha Geita. Ulisema Kendrick alimchoka Alissa na kumtelekeza. Lakini nini kilifanyika basi? Alissa ndiye Bi Mayala halisi!”

"Kwa kweli lazima ule maneno yako!" Timothy alijinyooshea uso wake mwenyewe, “Jitazame wewe kisha unitazame. Kama shemeji ya Kendrick, bado wewe ni mrembo. Lakini mimi ni kama panya! Kwa nini?”

Kusikia hivyo, Alissa alikuwa na uhakika kabisa kwamba Timothy na Melissa walikuwa katika makundi dhidi yake. Lakini wawili hao walikuwa hawajawahi kukutana. Jinsi gani walikusanyika na kula njama dhidi yake?

“Mimi … sikutarajia mambo yangekuwa hivi pia! Sisi ni washirika katika mashua moja. Ningewezaje kukudhuru? Ni yule bwege Alissa ambaye alikuwa ametuzuga na kutupotosha. Bila kutarajia, Kendrick angeshirikiana naye kikamilifu.” Melissa alishika nguo zake kwa woga kwa vidole vyake, "Namchukia Alissa zaidi kuliko wewe."

“Kuna maana gani ya kuzungumza juu yake sasa!” Timothy hakusikiliza maneno yake na kutomwamini kama hapo awali, “Je, ninaweza kurudi katika siku za zamani hata kama unasema hivi? Unaniruhusu niwe hivi hata hivyo. Kwa vile umeniumiza sana, unawezaje kutua kwa miguu yako? Tufe pamoja!”

Timothy akasogea mbele na kumshika bega kwa nguvu kiasi kwamba bega lilimuuma. Melissa alivumilia maumivu na aliogopa.

Sasa, Timothy hakuwa na kitu. Kwa hiyo, yeye pia hakuwa na cha kupoteza. Hakuweza kumhurumia.

“Unaongea upuuzi gani? Je, tunawezaje kulipiza kisasi kwa Alissa tukifa? Unataka kuiacha iende kwa urahisi hivyo?" Melissa alisema huku uso wake ukiwa laini.

“Sijui. Lakini je, inajalisha? Mpinzani ni mkali. Kumi kati yenu na mimi hatulingani na mtu mwenye nguvu kama hizo. Au bado unataka kunitumia? “Timothy alikaza macho, akawa na hekima zaidi baada ya kupata hasara.

“Si utakufa? Kwa nini tusilipize kisasi kabla ya kufa, ili wote wasiweze kuachwa. Tunapaswa kubaki hai sasa na kusubiri nafasi yetu. Tutapata nafasi.”

“Kwa nini nikuamini?” Hakuwa mjinga kama hapo awali.

Sura ya 199

Melissa alijua kwamba kulikuwa na pengo la uaminifu kati yake na Timothy. Ilibidi amfanye Timothy kumwamini tena.
"Nipe muda nitakuthibitishia." Melissa alisema kwa upole, akauvuta mkono wake ulioushika begani mwake, na akatabasamu kwa unyonge.

“Sawa, nitakupa muda unavyotaka. Ukithubutu kucheza hila, basi sitakuacha kirahisi.” Timothy aliweka tabasamu baya, kisha akainama na kuinamisha kichwa chake kumbusu Melissa.

Kichefuchefu kilimpanda Melissa huku akisikia harufu yake. Alishusha pumzi kwa siri ili kuvumiliq.
Alitabasamu kwa kujifurahisha na kuweka kidole chake cha shahada kwenye midomo yake, “Usifanye hivyo. Hii ni njia ya usalama.”

“Hakuna mtu mwingine hapa. Kwa nini huwezi kunibusu? Usisahau kwamba mara ya mwisho ulishindwa kumtumia dawa Alissa. Badala yake, ulitiwa wewe dawa. Nilikusaidia. Uliniomba nilale na wewe wakati huo. Ulifurahia kiasi gani! Kwa nini usiweze! hata kukubusu sasa?

"Melissa, unafikiri siwezi kukubusu kwa vile nimepoteza nafasi yangu, sawa?" Timothy alisema kwa ukali na kumfedhehesha Melissa.

Melissa alikuwa tayari hana raha. Isitoshe, alikuwa mjamzito na alikuwa na ugonjwa wa asubuhi. Sasa, hakuweza kujizuia kujirudisha nyuma kwa ukali.

Kuona kuwa Melissa alikuwa amechukizwa naye hata akatapika, Timothy alikasirika na kuweka sura ngumu.

“Melissa, bado ninazo picha zako za uchi. Inaonekana unataka nimtumie hizi picha na video Seidrick, ili aone jinsi mke wake anavyofurahi anapolala na mwanaume mwingine.”

Timothy alisema na kugeuka kuondoka. Melissa alimshika mkono, akizuia ugonjwa wake na kumsihi, “Timothy, si kwamba sikupendi.
Nina maumivu ya tumbo tu. Ndio maana nilikuja hospitalini. Niamini. Tazama, hii ndiyo ripoti yangu ya uchunguzi.”

Ilikuwa ni kweli kwamba hakuweza kula katika kipindi hiki cha wakati. Kwa hivyo, alienda hospitali kuchunguzwa na hakutarajia kwamba angeweza kumpumbaza Timothy na ripoti hii ya uchunguzi sasa.

Alichukua ripoti kutoka kwenye begi lake na kumpa Timothy, "Angalia, sikukudanganya."

Timothy alikodoa macho yake na kuichomoa ile ripoti kutoka mkononi mwake ili kuitazama. Baada ya kuiangalia, hasira yake iliondolewa.

“Na nimekuwa nje kwa muda mrefu sana. Ninaogopa Seidrick atakuwa na shaka. Kwa hivyo, hatuwezi kufanya wakati huu. Tufanye miadi nyingine.” Melissa aliutazama uso wake kwa makini, akisema kitu kizuri ambacho Timothy angesikiliza.

Kabla ya kupata picha hizo kutoka kwa Timothy na kushughulika na Timothy, Melissa angeweza tu kuwa mpole na mtiifu ili kumtuliza. Sasa, yeye ndiye pekee ambaye angeweza kumtegemea. Bado alikuwa na thamani fulani kwa Timothy katika kumrekebisha Alissa.

Kabla ya kumwondolea thamani yake, lazima akubaliane na matakwa yake kadiri awezavyo.

Timothy alisugua pua yake vibaya, “Chukua chumba cha hoteli siku nyingine na nitakuja kukuona. Usiniruhusu ningojee kwa muda mrefu sana.
Ninaonyeshwa unyenyekevu sasa. Wanawake wote hujificha wanaponiona. Siwezi hata kuachilia tamaa yangu. Inabidi unifariji ipasavyo.”

Aliinua mkono wake na kushika kidevu cha Melissa, akatabasamu vibaya, na kumpiga busu kali kwenye midomo.

"Na ninahitaji pesa!" Timothy alikuwa amebakiwa na pesa kidogo katika siku hizi chache.

"Nitumie nambari ya kadi yako na nitahamisha 100,000 kwako." Melissa alibaki akitabasamu na kutii.

Timothy akakaza mkono wake na kumbana kidevu, “100,000? Unadhani mimi ni mtoto wa shule? Nipe milioni kwanza.”

"Milioni moja?" Melissa alitoa macho yake kwa mshtuko, bila kutarajia kwamba atakuwa na tamaa na kutaka mara kumi ya kile alichompa, “Nawezaje kupata kiasi hicho?”

Timothy alimpandisha Melissa juu na kutembeza vidole vyake kutoka kwenye kidevu chake hadi kwenye hereni za almasi masikioni mwake, na akateleza kwenye shingo yake nyembamba hadi kwenye mkufu wa almasi uliofanana na hereni zilizo kifuani mwake. Kisha, alizunguka juu ya bega lake na chini ya mkono wake ili kumshika mkono wake wa kulia, ambapo pete ya harusi ya almasi ilikuwa inaangaza. Zote zilikuwa bidhaa za kifahari.

“Thamani ya nguo na vito unavyovaa inakaribia milioni kumi. Wewe ni binti-mkwe wa familia ya Masolwa na mwanamke wa familia ya Maziku. Je, hali yako iko vipi katika Jiji hili? Unataka kuniambia kuwa huna pesa? Unafikiri mimi ni mjinga?" Timothy alipapasa almasi laini na nzuri kwenye kidole chake, "Ni sawa ikiwa hutaki kunipa. Basi nipe tu pete yako ya ndoa.”

Melissa mara moja alikunja ngumi ili kumzuia asiiondoe, “Siwezi kukupa hii. Ikiwa Seidrick atagundua ahadi ya ndoa yangu imetoweka, ninawezaje kuelezea?"

"Hiyo ni biashara yako." Timothy alisema bila haya, “Au fanya kama nisemavyo.”

“Milioni moja ni nyingi sana. Sina pesa nyingi sana mkononi mwangu. Kwa hiyo, nipe muda wa kufikiria namna ya kupata pesa.” Akiwa amekabiliwa na bei kubwa ya Timothy, Melissa hakuwa na lingine ila kuafikiana.

"Siku moja. Lazima nipokee pesa kwenye akaunti yangu kufikia wakati huu kesho." Timothy alinyoosha mkono kwa kidole kimoja na kutoa tarehe ya mwisho.

"Milioni moja sio pesa ndogo. Kwa kweli siwezi kuipata hata siku moja.” Melissa alikosa raha na akamwomba ampe muda wa ziada, "Nipe siku tatu."

"Siku mbili. Haijadiliwi.” Hiki kilikuwa kibali cha mwisho cha Timothy.

Hakuwa na pesa nyingi sasa. Alihitaji pesa kwa ajili ya chakula, maisha, na usafiri. Isitoshe, alizoea kutumia pesa kupita kiasi. Ilikaribia kumtia wazimu kwamba sasa alikuwa na shida ya kupata pesa.

Hakuweza tena kustahimili siku za umaskini wakati hakuweza kupata chochote alichotaka.

Ilibidi awe na pesa. Vinginevyo, angewezaje kuishi?

Na Melissa ndiye alikuwa chanzo cha bora cha matatizo yake, hivyo ingebidi awe pia chanzo chake cha pesa.

“Sawa.” Melissa angeweza tu kutikisa kichwa na kusema, “Kisha nitaenda kwanza kukuletea pesa.”

“Melissa, afadhali ukumbuke kuwa sina kitu sasa. Sikuogopi wewe kucheza maujanja! Ikiwa mbaya zaidi itatokea, tutakufa pamoja!

Kwa hayo, Timothy alishusha kofia nyeusi ya besiboli kichwani mwake na kuondoka kupitia hatua ya kituo cha usalama.

Melissa kisha akashusha pumzi ya raha. Lakini alikasirika sana baada ya kuonewa na Timothy kwa wakati huu hadi akaupiga mkoba uliokuwa mkononi mwake ukutani ili kutoa hasira yake.

Alissa hakukaa sana akageuka na kuondoka kimya kimya.
Aliingia kwenye gari lake na kuondoka hospitalini kwa haraka.

Hakuwahi kufikiria kuwa Melissa angekuwa na uhusiano kama huo na Timothy. Ilimshangaza sana. Lakini hiyo ilieleza kwa nini walijuana.

Ilisemekana kuwa ukifanya madhara, utapata madhara. Mtu mwovu atanyanyaswa na mtu mwingine wa kufanana naye.

Akifikiria kuhusu mwisho wa Melissa , Alissa alikuwa katika hali nzuri zaidi.

Hakuweza kulegea na pia ilimbidi ampe Melissa zawadi. Alikasirika sana kuona Melissa akiwa na kiburi sana.

Sura ya 200

Baada ya kumfukuza Alissa, Alaya alirudi katika wodi ya Maira na kuona kwamba Maira alikuwa na huzuni.

Seidrick alikuwa akimuuliza Maira, “Mama, una tatizo gani?”

"Seidrick, sijisikii vizuri ndani." Maira akaugua. Akifikiria kile ambacho Melissa alikuwa ametoka tu kufanya katika wodi hiyo, alikuwa amepoa na kuogopa.

Melissa alikuwa daima laini na dhaifu juu ya uso. Lakini Maira hakuwahi kufikiria kwamba angekuwa mkali sana ndani.

Na mwanamke wa aina hii alikuwa mke wa mtoto wake. Kujificha kwa Melissa kulitisha sana.

"Nitakwenda kumwita daktari akuchunguze." Seidrick ilikuwa karibu kugeuka, lakini Maira akamzuia, “Ninasumbuliwa na wasiwasi wangu.
Daktari hawezi kuuponya.”

"Mama, unaweza kuona daktari wa magonjwa ya akili kwa wasiwasi wako. Nitakutafuta daktari mzuri.” Seidrick alikaa chini na kumtazama Maira.

"Wasiwasi wangu hauwezi kuponywa na daktari wa magonjwa ya akili." Maira alikuwa katika hali mbaya.

Alaya pia alikuja mbele na kutulia, “Mama, kuwa na amani. Unaweza kuzungumza nasi kuhusu hilo. Tutajaribu tuwezavyo kufanya chochote unachotaka kufanya.”

“Ndiyo hivyo mama. Tuambie tu unachotaka. Pia tuna wasiwasi tunapokuona hivi.” Seidrick alisema.

“Sijui kama niseme. Hata nikisema, naogopa kwamba hamtaamini nyote.” Maira alitazama chini na kusitasita sana.

“Mama, wewe ni wa ajabu sana leo. Je, yeye alikuambia kitu? Usimwamini na nitashughulikia kila kitu.” Seidrick aliinua mikono yake magotini na kukunja uso.

“Yeye?” Maira alimuuliza mwanawe kwa kejeli, “Unamrejelea nani?”

"Alissa." Seidrick alikutana na macho ya mama yake yenye maswali, “Yeye ndiye aliyekuleta hospitali jana. Lakini nilirudisha fadhila zote ambazo nilipaswa kurudisha. Kwa hivyo, usijisikie kama una deni kwake."

“Seidrick , haukumuelewa Alissa. Hakuja kuniomba nimrudishie kibali. Alinijali tu na alikuja kuniona.” Maira alihisi kwamba Seidrick ilikuwa na chuki kubwa dhidi ya Alissa, "Una chuki dhidi yake?"

“Sina chuki na mtu yeyote. Lakini yeye si Alissa tena tuliyemjua zamani.” Seidrick pia ilihisi kwamba Maira alikuwa mkaidi sana, "Mama, unaweza kuwa na akili timamu?"

"Wewe ndiye unapaswa kuwa na akili timamu." Maira alikandamiza hasira yake iliyokuwa ikipanda.

“Mama, alikuambia nini hasa? Inaonekana ulivurugwa na yeye.” Seidrick alikuwa na uchungu kwa kukosolewa na Maira, “Je, hujui alifanya nini wakati huo? Sasa, unamtetea. Bado wewe ni mama yangu? Hukuona kwamba mimi mwanao niliachwa naye kama mpumbavu?”

Kadri Seidrick alivyosema, uso wake uligeuka kuwa kama majivu kwa hasira. Aliuma meno na kukunja ngumi kwenye magoti yake.

“Sedrick, tulia. Usiharibu uhusiano wako na Maira.” Alaya alipiga bega la Seidrick.

“Alaya, asante kwa kuja kuniona leo. Lakini inabidi nizungumze vizuri na Seidrick sasa. Samahani." Maira hakutaka Alaya amkosee na akaeleza.

"Mama, najua. Ninaweza kukaa hapa kwa muda tu na lazima nimchukue Jasmin. Anajifunza Kiingereza." Alaya alimwambia Seidrick tena, “Seidrick, zungumza na Maira. Nitatangulia.”

Seidrick aliitikia kwa kichwa, na Alaya kisha akaondoka akiwa ametulia.

Wodi ilikuwa kimya. Sio Maira wala Seidrick aliyezungumza kwanza wakati huu. Walikuwa wakijaribu kutulia.

"Seidrick, unajua kuwa Melissa pia yuko hapa leo?" Maira alitulia kabla ya kuzungumza polepole.

“Kweli?” Seidrick bila shaka hakujua kuhusu hilo, "Alisema alitaka kurudi kwenye nyumba ya familia ya Maziku. Labda alikuja kukuona kwa muda.”

Kwa sababu Melissa alikuwa mjamzito, familia ya Masolwa ilimthamini sana. Alikuwa amejitolea kuja kumuona Maira. Lakini kila mtu alisema kuwa kulikuwa na watu wengi hospitalini. Haikufaa kwa mwanamke mjamzito. Pia haikuwa nzuri kwake na kwa mtoto. Kwa hiyo, wakamwomba abaki nyumbani.

“Alipokuja, Alissa pia alikuwa hapa…” Maira alimwambia Seidrick kilichokuwa kimetokea hivi punde, “Seidrick, je, hatukumwelewa Alissa? Kwa asili yake, hangeweza kamwe kufanya chochote kukuumiza na kukusaliti hivyo. Kwa nini alijifungua mtoto ghafla? ...
Lazima alikumbana na mambo ambayo hangeweza kushughulika nayo, au anaweza kuwa na matatizo yake mwenyewe...

"Na Melissa, nadhani ana kitu cha kutuficha. Haya ni machale yangu. Sitakudhuru kamwe. Wewe ni mwanangu. Kwa hivyo, Seidrick, lazima uwe mwangalifu zaidi."

"Mama, Alissa anaweza kuwa alipata shida gani, hata akazaa mtoto wa mtu mwingine nyuma yangu?" Wakati Alissa alipotajwa, Seidrick alikumbuka tukio hilo miaka mitano iliyopita wakati Alissa alipotoka hospitalini akiwa amemkumbatia mtoto wake, jambo ambalo liliufanya moyo wake kutetemeka kwa maumivu, “Ni yeye ndiye aliniacha nilipokuwa nikimhitaji zaidi. Wakati huo ndipo nilipoona rangi zake halisi.”

"Kuhusu Melissa, yeye ni mzuri kwangu. Sasa, ana mimba ya mtoto wangu. Ikilinganishwa na Alissa, ni wazi kuwa yeye ni bora zaidi. Mama, labda mfadhili hataki kutuona. Si jambo kubwa.”

“Siamini.” Maira alijua jinsi pigo kubwa aliloleta Alissa kwa Seidrick wakati huo.

"Mama, ninamwamini Melissa. Ninaamini tu katika kile nilichokiona. Sitamsamehe Alissa wala kumuamini.” Seidrick alinyoosha mkono na kufungua kidogo kifungo kimoja cha shati lake. Alihisi kukosa pumzi kidogo, “Mama, nitarudi kwanza.”

Hakutaka kuongea na Maira kuhusu Alissa na hakutaka hata kusikia jina lake.

"Seidrick, mama hatawahi kukudanganya. Melissa sio mpole na mstaarabu kama unavyomwona." Maira alimkumbusha tena, “Seidrick, unapingana na Alissa kwa sababu bado huwezi kumwacha aende zake, sivyo? Huwezi kuamini kwamba alikuacha ulipokuwa hatarini na akakusaliti?

"Seidrick, bado unampenda ndani."

“Namchukia!” kwa hayo, Seidrick alipiga hatua kuondoka bila kuangalia nyuma.

Alikuwa na haraka. Alipofika kwenye maegesho ya magari na kuingia kwenye gari lake, hakuendesha gari mara moja. Badala yake, aliegemea kiti chake na kufumba macho yake ili kuweka mambo hayo ya kuudhi nyuma yake.

Alijiambia asifikirie chochote wala kuathiriwa na mtu yeyote.
Lakini kadiri alivyokuwa akijaribu kujituliza ndivyo alivyokuwa akikereka.

Aliugonga kwa nguvu usukani na kuudhika kwamba bado hawezi kumkabili kwa utulivu mwanamke aliyemuumiza baada ya miaka mingi!

Hakika hakuwa kama mama yake alivyosema kwamba hangeweza kumuacha kwa sababu bado anampenda.
Hakuweza kujiachia kwa sababu alitaka kujikumbusha ili asisahau kirahisi usaliti wake na kuumia kwake.

Lakini kwa nini kulikuwa na sauti nyingine moyoni mwake ikisema kwamba haikuwa hivyo?
Hii uneirudia
 
mireille njoo basi jaman,kila saa nachungulia humu kama umeweka muendelezo
 
Alitoka katika familia yenye heshima kubwa na historia ndefu na alikuwa mtu wa nafasi. Alikuwa kiongozi wa Nyanza Group, kampuni ambayo lilidhibiti maisha ya uchumi wa jiji la Mwanza.

Hadithi ilidai kwamba mtu huyu alikuwa katili na mkali. Waliompinga hawakuishia vizuri sana. Kulikuwa na hata uvumi kwamba alipitia kuzimu kunyakua madaraka na hata kuwatoa kafara ndugu zake kudumisha utajiri wake. Alikuwa ni mtu asiyeweza kukasirishwa kirahisi.

Na mtu kama huyo angewezaje kujiumiza ili kuokoa wengine? Ikiwa hakuwa jasiri na kuamua kukata tamaa, Allisa asiangeweza kamwe kufanya hatua mbaya kama hiyo. Ili tu kuweza kumnasa Kendrick, ilibidi achunguze ni hoteli gani alipendelea kuvinjari, na kisha kugundua kuwa alipenda kula bata kwenye hoteli ya nyota tano ya Full Kipupwe, iliyopo kando ya Ziwa Victoria, Allisa alichukua hatari na kujifanya mhudumu wa bandia, akimlenga Kendrick pekee, hasa siku ambazo yeye alihisi shamba lake lipo tayari kupokea mbegu. Fursa ilipopatikana, Allisa alitia dawa ya kusisimua mwili kwenye kinywaji alichomhudumia. Hakuweza tena kujali matokeo yaliyokuwa yakimngojea. Maisha ya Seidrick yalikuwa muhimu zaidi wakati huo.

Alissa alifungua mlango kwa ufunguo wa chumba, akaingia ndani kimya kimya huku akishusha pumzi ili kusikiliza sauti. Aliposikia kelele kutoka upande wa chumba cha kulala cha master, alitembea polepole na kufungua mlango wa chumba hicho cha kulala. Taa ya kitanda ilitupa mwanga wake chini na chumba kilikuwa na mwanga hafifu.


“Nani hapo!” Yule mtu aliyekaa pembeni ya kitanda aliuweka mkono wake kwenye meza ya kitanda. Umbo lake lilikuwa limeinama kidogo na sauti yake ilikuwa ya kishindo na ya kutisha,mithili ya mashine ya kusaga mawe.

Allisa akashusha pumzi. Ilionekana kuwa dawa aliyokuwa kamchanganyia kwenye kinywaji tayari ilisababisha athari katika mwili wake. Alissa alitembea kwa uzuri, akasimama mbele ya mtu huyo, uso kwa uso naye.

Alissa aliuona uso mzuri wa Kendrick kupitia mwanga hafifu ulioakisiwa na taa iliyoanguka chini. Uso wake ulikuwa mzuri kana kwamba alipendelewa na Mungu - nyusi za juu, pua iliyonyooka, na macho meusi kama usiku na ya kina kama bahari, akiwavuta watu ndani bila hiari.

Ingawa nyusi zake nene zilikuwa zimekunjamana, na uso wake mzuri ulijaa jasho zuri, alionekana kuvutia zaidi.

“Nani hapo!” Macho ya Kendrick Mayala bado yalibaki kuwa makali. Mtazamo wa macho yake ulikuwa mkali kama upanga, na kumfanya Allisa kuwa na hatia hivi kwamba hakuthubutu kumtazama moja kwa moja.

Ijapokuwa alikaa na kumtazama Alissa, ambaye alisimama, utisho katika asili yake uliendelea kuwa na nguvu.

Alissa alitoa tabasamu kamili. Vidole vyake vyembamba vilifungua blauzi nyepesi aliyokuwa amevaa, midomo yake iliinuliwa kidogo. "Mtu anayeweza kukusaidia."

Mara tu alipoacha kuzungumza, blauzi yake ilianguka, kikifunua sketi nyembamba ya lace nyeusi ndani. Akiwa na umbo la kupendeza, la kuvutia na la kutatanisha, na lililojaa haiba, Alissa alikuwa mtongozaji.

Kwa jinsi alivyokuwa akitengenezwa, Kendrick ambaye tayari alikuwa anayumba kutokana na athari za dawa aliyochanganyiwa, alizidi kuwa na hamu ya kufanya mapenzi.

“Ondoka nje!” Akatazama pembeni na kuhema kutoka kooni.

Alissa alipuuza agizo lake la kuondoka. Aliinama na kuinuka, akichezea zoloto yake ya kuvutia na inayochomoza kwa vidole vyake vyembamba, na kusema kwa upole. "Usijali, mimi ni safi."

Kendrick alimshika kidole na uso wake ulikuwa wa baridi. “Siitaji.”

Lakini dawa hiyo ilizidi kuwa na nguvu, ikisambaa sana mwilini mwake. Aliona ni vigumu kupuuza hisia za ajabu ndani.

"Kweli hauitaji?" Alissa aliona mabadiliko katika macho ya Kendrick, rangi nyeusi zaidi, hamu zaidi. “Utakosa raha sana. Sitakusumbua; Nahitaji pesa tu ili kumtibu jamaa yangu. Milioni moja inatosha.”
Simulizi zako huwa zinavutia sana uwe una tag watu mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom