Simulizi: Tokomezo

Simulizi: Tokomezo

SIMULIZI: “TOKOMEZO” (04)
MTUNZI: XAVERY EMMANUEL (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Whatsapp: 0769765748
Namba: 0672493994
Social Net: @star_xav

“Ndugu! Nitaeleza ayo yote hadi mpenzi wangu awepo hapa. Kwa maana miaka yote niliyokaa na msichana huyo sijawai mwambia sababu ya mimi kutafutwa kwa namna hii, kila siku nampiga chenga tu kwa maana ilifikia hatua hata kumwamini mtu ilikuwa ni sumu. Siri hii naijua mimi tu peke yangu, labda kwa uchache ni hao wanaonitafuta kwa sababu wanaogopa kutolewa kwa siri yao. Mwenyezi mungu wa rehma kesho mapema pindi afikapo mpenzi wangu basi nitaweka kila kitu hadharani...... aaaagh! Ndio samahani kwa hilo mama!” alimaliza kwa kumtaka mke wangu radhi..

SEHEMU YA NNE.
Hatukuwa na lingine zaidi ya kumwandalia sehemu ya kulala pamoja na chakula, kila mda sikusita kumpa pole kwa magumu aliyopitia, ingawa sikuyafahamu bado.

Kwa kweli ukimwangalia Abdul kwa sura ya karibu unapata kila aina ya majibu ya shida duniani, sura na umbo lake limebeba maswaibu yote ya ulimwengu kabla hujapata mkasa wake. Kwa kumwangalia tu utajua kuwa kweli Abdul ni mwamba na shupavu kwani mifupa yake imegangamaa kwa michosho na maangaiko ya dunia.

Alikuwa ni mrefu kiasi, urefu uliomtosha mwenyewe kujiingizia kipato, alikuwa ni mweusi ambae rangi yake alipatikana baada ya vita kati ya rangi nyeusi na maji ya kunde, nani awe mtawala rasmi wa mwili, na hatimaye weusi ulizidi shapavu kwa majikunde na kutawala mwili mzima, yaani alikuwa mweusi wa matatizo mwili mzima. Alikua mwembamba kwa kukosa lishe ya mwili kwa mda mrefu takribani milongo tisa na ushee. Hiyo tisa, kumi alikuwa ni kipofu, lakini uzuri wa hapa; kipofu chake kilikuwa ni cha macho tu lakini sio kuona. Kweli alikuwa hana uwezo wa kuona kabisa, lakini alikuwa na uwezo wa kufanya vitu vikubwa vinavyoonekena kumshinda hata alievalia miwani maarufu kama macho manne.

Kosa kumpeleka au kumwelekeza kitu kwa mara moja, mara ya pili anafanya mwenyewe. Hivyo hatukupata shida kumwelekeza mazingira ya chumba kilivo, sehemu ya maliwato na pembe nyingine za chumba. Kila kitu kilichofuata kuhusu chumba hicho alijua yeye jinsi ya kupanga na kuweka kwa ustadi asipate shida kukitafuta. Kilikuwa ni chumba kwaajili ya wageni.

Basi tuliagana baada ya chakula na kumtaka alale salama huku mimi na mke wangu tukiliendeleza valangati la kutatua mgogoro wa mawazo kuusu mgeni wetu mpya na wapi pa kuanzia kuhusu kumpata Rose ambaye ni mpenzi wa Abdul.

“Baba eh!! kama unavyojua bhana... ‘Abilia chunga mzigo wako’, unakoenda kesho, unaenda kumchukua Rose na kurudi, marafuku tamaa!” hicho kilikuwa ni kijembe cha mke wangu kilichotokana na wivu, mke wangu amabaye tulizoea kuishi kwa matani kila kinapokutana lakini jambo jema la kumshukuru Mungu ni kwamba hakuwai kunivunjia heshima hata siku moja, toka nimtoe kwao undendeuleni.

Tuliongea kidogo na mpango wa kuwahi kwenda kumchukua Rose kwani siku iliyofuata ilikuwa sio siku ya kazi; ni jumamosi. Na hatimaye tukalala kwani kila upande ulikuwa bize kuwaza historia kali ya maisha ya kijana ambaye yupo hatihani kutolewa roho kwa sababu ambazo hakuna anayejua zaidi ya msimuliaji mwenyewe, ambaye kwa wakati huo tayari neno Fofofofo Liliendelea katika chumba chake.

“Kokolikooooo!, kokokoko kokoli…” kama ilivyo majogoo ya kila siku, siku pendwa katika historia nyingine ya maisha ikaanza. Tukajuliana hali kila mmoja, na kwa mara ya kwanza jua la asubuhi liliniwezesha kuona kabisa uso wa Abduli ukiwa na tabasamu.

Baada ya kifungua kinywa nikaaga kwenda sehemu ambayo kila mtu aliifahamu, Abduli alinipa maelezo sehemu ambayo wanaishi kwa siri na mpenzi wake Rose, niliwasiliana na Rose kujua sehemu gani tunakutana, na kwa vile nilikuwa na namba yake ya simu haikunipa shida.

Nilianza safari kwa kuchukua daladala moja kwa moja hadi Bombambili stendi, sehemu ambayo tuliahidiana kukutana. Nilishuka stendi ya Bombambili na kuanza kutafuta namba ya mwanamke ambaye Abdul alimjaa kinywani, kila kichwao yeye ni Rose, Rose, Rose hadi kero! sijui ndio mzimu wake alaaah!. Niliendelea kuongea mwenyewe kimoyomoyo kwa muda kabla maada haijabadilika kichwani mwangu na kuanza kuwaza ni aina gani ya mwanamke ambaye bwana Abdul ametunikiwa, mke mjasiri ambaye amekubali kuishi na Kipofu kwa umaskini na matokomezo kadha wa kadha, hakika nilipata msisimko sana na kupongeza baadhi ya jitihada wafanyazo wanawake katika kupigania mapendo yao. Nilipofika nikafungua simu yangu kwa kutoa nenosiri, nikatafuta namba za Rose kupitia missed call na kuipiga.

“Hallo!, hallo,... eh wapi, wapi!!, ehh hallo!” bila maelewano simu hiyo ilikata, nikaipiga tena na nikajibiwa na muhudumu ambaye alikuwa zamu siku hiyo,

“Namba unayopiga haipatikani, Jaribu tena baadae”, nikakata na kupiga tena lakini mchezo ukawa vilevile, uso wangu ukaanza kuchukia na kuendelea kuangaza uku na uko kumtafuta mtu nisie mfahamu, niliangaza sana lakini sikufanikiwa kupata nilichokitaka, mshituko wa mayo ukanipata palepale nilipokuwepo mara baada ya macho yangu kuona mwanamke ambaye kwa mbali rangi yake ya maji ya kunde ilimulika mboni ya macho yangu.

Picha ya mke wangu ikafutika kichwani kwa kuanza kutoa sifa sisizostaiki kwa mwanamke ambaye sio mke wangu.

“Jamani Mungu fundi... Lo!” nikapaza ukuu wa mungu na nikajikuta namsogelea msichana huyo, kama tujuavyo wanaume sifa zetu pindi tumuonapo mwanamke ambaye maumbile yake ni mfano tosha wa kuamsha sehemu ambazo zimelala kwa mda. Alikuwa ni mchana mwenye rangi yake, sikumbuki kama kipodozi cha kemikali kishawahi pita katika uso wake; hakika anavutia. Alikuwa na nyele ndefu nyeusi ambazo alizifunga tu kwa kamba kichwani mwake upande wa juu, utadhani anazitumia kama ngata katika kubebea mizigo mizito. Nilimsogelea kuendelea kufahadi japo mapozi tu, alikuwa anakata kucha za mkono wake kwa kutumia meno huku mkono mwingine ukiangaika na simu ndogo kabisa ambaye ilikuwa haiendani na umbo lake. Nilipoganda kuendelea kumchora ghafla alinishtua na swali.

“Kaka naweza azima simu yako mara moja?” Swali hilo halikuwa na majibu kichwani kwangu, kwani aliendelea kunichanganya kabisa kwa kutumia sauti yake iyo ambayo kama wataalam wa utengenezaji wa simu wangeigundua basi wangeinyunyiza katika teknologia ya mlio wa kuitia katika moja ya kampuni zinazofanya poa duniani. Kweli niliongeleshwa ila nilibaki nimeduwaa kwa kukosa jibu, kwani hata kilichosemwa nilikikumbuka?, nikabaki kuishia tu aah!, Ah!... na kabla sijaangaika sana kijigonga gonga akarudia kile alichosema.

“Samahani lakini.... simu!, Naazima!” Hapo kilichozungumzwa kilikaa kichwani, haraka nikatoa simu yangu na kumpa mrembo yule, macho yangu bado hayakuchomoka usoni mwake.

“Kaka mimi siwezi tumia hizi! Naomba niandikie namba....” aliongea na kunizidishia mawazo. Inakuaje kwa kizazi hiki mtu mrembo na mwenye miaka yake duniani anashindwa tumia smartphone. Nikabaki nashangaa tu. ‘Jamani kwa lika kama ya huyu dada halafu anasema eti hawezi kutumia “Smartphone” Laulaaa!’, nilipigwa na butwaa la moyomoyo ambalo hakuna alieliona zaidi ya moyo wangu wenyewe.

“Mhhh namba!” nikajikwakwamua kutoa msaada.

“0757.. 9947....” kabla hajamalizia kuitaja namba hiyo, nikainua macho yangu na kumtazama kwa makini, nilikutana na uso wa tabasamu wa mrembo yule, kilichonishangaza ni kuwa namba hizo alizokuwa anazitoa kichwani. Yaani bila kuangalia sehemu yoyote ile jambo ambalo lilinishangaza sana. Sikumbuki kama alimalizia kutaja namba za mwisho au la, lakini tukabaki tu kuangaliana, huku mimi nilimshangaa yeye na yeye akishangaa mimi kwa mshangaa yeye.

“Unamtafuta nani?” Nikajikuta namtupia swali rahisi kwake.

“Abdul..... A....” likalirudia mara mbili lile jina la Abdul, hapo nikastuka katika dimbwi la mawazo na kuanza kumkazia tena macho mrembo yule. Nilikuwa kama sijaelewa alichozungumza kwa mara nyingine. Lakini alitaja bila kusita, tena mara mbili. Kitu ambacho kilinifanya niamini ni yeye Rose ni kuwa alipotaja namba alitaja namba zangu kabisa ambazo nilitumia kuwasiliana na yeye. Nikataka kupingana na macho yangu kama yule ndio kweli mwanamke ambaye ametekwa na kijana kama Abdul. Kwa kweli baada ya jina hilo, kilichofuata ni maswali na majibu tu ambayo nilikuwa najiuliza mwenyewe bila kupata nafasi ya kujijibu.

“We ni rose?” naaam, nikamtwanga swali ambalo lilimwacha kinywa wazi!, niliuliza kutaka kuhakikisha tu. Akainamisha kichwa chini kwa hofu ya kujibu. Alikuwa anaogopa.

“Okey mimi ni Xavery!, Xav... kama unamtafuta Abdul basi hapa ndipo sehemu sahihi na muafaka kabisa, nipo nae kwangu!”. Nikamwaminisha.

“Kaka samahani, nilikuwa naitaji huduma ya simu tu basi, kama hapatikani naomba mimi niende” akainua kichwa chake chenye aibu na kuongea, hakuchukua sekunde akaanza kugeuka tayari kuondoka.

“Rose ni mimi bhana, nimeagizwa na Abdul, nimepatwa na mshangao mara baada ya kusikia namba iliyotaja ni yangu. Mwishoni ni 87! Si ndiyo?, Abdul yupo salama na anakuitaji, na mguu huu ulikuwa kwako. Sikufahamu na nisingeweza kukufahamu kwa mapema namna hii, utambulisho pekee ambao nilikuwea nao mkononi mwangu ni namba yako tu ya simu. Nimepiga sana lakini hupatikanai” nilijitahidi kutokwa na maneno ya ukweli kwa mfurulizo kwa kumwaminisha binti yule, akageuka tu na kutoa chozi jembamba lililotililika hadi mashavuni mwake, lakini hakuharibu kitu katika kung’aza uzuri wake, alipendeza hadi wakati analia. Alinisogelea na kunitaka radhi.

“Kaka angu, ni vigumu kumwamini kila mtu kwa sasa, tunatafutwa sana, sio mimi wanaoniitaji, ni Abdul, kwa maana hata tukiwa wawili mimi na yeye, basi wataanza na yeye. Nampenda sana mume wangu jamani, naomba nikamwone” alitoa ombi la mwisho kwa kilio, nilimwonea huruma kwa kweli, nikawaza shida anazopata kwa kuishi na kipofu angali yeye ni malaika namna ile, vipi kelo za wanaume wanaomsumbua kumtaka kimapenzi?. Basi nikachukua nafasi ya kumbembeleza hadi kutulia.

Tukachukua usafiri wa pikipiki, niliwaza sana tunapandaje pikipiki moja na hali ya nyuma ilivyo nzuri ya binti yule. Rose alibeba kila kitu sehemu zake za nyuma, alikuwa mwemabamba wa kukonda kwa maisha tu ila mwili ulimkaa vizuri sana, mbinuko wake wa nyuma na shepu yake ya uchanga vilionekana.

Sasa nawezaje kupanda nae pikipiki moja? Nani atakaa mbele na nani nyuma? Mwanaume nikae mbele, hapana, nikae nyuma! Lo! Na ilo sebene ya matuta njiani ikuru yangu itaweza vumilia kweli ikigusana na mlima Rose? Na akiniona mke wangu huo ni ugomvi mwingine, nikatabasamu na kuchukua pikipiki mbili, kila mmoja aliapanda yake na kuanza kuingoza njia kuelekea nyumbani.

Hatukuchukua mda mrefu tayari tulishaingia mlangoni, sikuwa na mlinzi wala haouse girl nyumbani mwangu, nikafungua mlango mwenyewe na kuingizana ndani na Rose ambaye roho yake tayari ilianza kuweuka mara baada ya kuona amekaribia sehemu ambayo roho yake imefia mazima.

Ile kuingia tu.. tukakalibisha vilio vya furaha vilivyosindikizwa na machozi. Si kwa furaha ya Roze, vipi upande wa Abdul?, kwa mara ya kwanza nikaona nyuso ya tabasamu kwa Abdul huyu jamaa ukimwangalia kwa makini unaweza sema sio kipofu. Kwa maana hakuna anachokosea yaani kila kitu anafanya sahihi utadhani ana macho yote mawili!!!

ITAENDELEA...

Starxav
 
SIMULIZI: “TOKOMEZO” (04)
MTUNZI: XAVERY EMMANUEL (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Whatsapp: 0769765748
Namba: 0672493994
Social Net: @star_xav

“Ndugu! Nitaeleza ayo yote hadi mpenzi wangu awepo hapa. Kwa maana miaka yote niliyokaa na msichana huyo sijawai mwambia sababu ya mimi kutafutwa kwa namna hii, kila siku nampiga chenga tu kwa maana ilifikia hatua hata kumwamini mtu ilikuwa ni sumu. Siri hii naijua mimi tu peke yangu, labda kwa uchache ni hao wanaonitafuta kwa sababu wanaogopa kutolewa kwa siri yao. Mwenyezi mungu wa rehma kesho mapema pindi afikapo mpenzi wangu basi nitaweka kila kitu hadharani...... aaaagh! Ndio samahani kwa hilo mama!” alimaliza kwa kumtaka mke wangu radhi..

SEHEMU YA NNE.
Hatukuwa na lingine zaidi ya kumwandalia sehemu ya kulala pamoja na chakula, kila mda sikusita kumpa pole kwa magumu aliyopitia, ingawa sikuyafahamu bado.

Kwa kweli ukimwangalia Abdul kwa sura ya karibu unapata kila aina ya majibu ya shida duniani, sura na umbo lake limebeba maswaibu yote ya ulimwengu kabla hujapata mkasa wake. Kwa kumwangalia tu utajua kuwa kweli Abdul ni mwamba na shupavu kwani mifupa yake imegangamaa kwa michosho na maangaiko ya dunia.

Alikuwa ni mrefu kiasi, urefu uliomtosha mwenyewe kujiingizia kipato, alikuwa ni mweusi ambae rangi yake alipatikana baada ya vita kati ya rangi nyeusi na maji ya kunde, nani awe mtawala rasmi wa mwili, na hatimaye weusi ulizidi shapavu kwa majikunde na kutawala mwili mzima, yaani alikuwa mweusi wa matatizo mwili mzima. Alikua mwembamba kwa kukosa lishe ya mwili kwa mda mrefu takribani milongo tisa na ushee. Hiyo tisa, kumi alikuwa ni kipofu, lakini uzuri wa hapa; kipofu chake kilikuwa ni cha macho tu lakini sio kuona. Kweli alikuwa hana uwezo wa kuona kabisa, lakini alikuwa na uwezo wa kufanya vitu vikubwa vinavyoonekena kumshinda hata alievalia miwani maarufu kama macho manne.

Kosa kumpeleka au kumwelekeza kitu kwa mara moja, mara ya pili anafanya mwenyewe. Hivyo hatukupata shida kumwelekeza mazingira ya chumba kilivo, sehemu ya maliwato na pembe nyingine za chumba. Kila kitu kilichofuata kuhusu chumba hicho alijua yeye jinsi ya kupanga na kuweka kwa ustadi asipate shida kukitafuta. Kilikuwa ni chumba kwaajili ya wageni.

Basi tuliagana baada ya chakula na kumtaka alale salama huku mimi na mke wangu tukiliendeleza valangati la kutatua mgogoro wa mawazo kuusu mgeni wetu mpya na wapi pa kuanzia kuhusu kumpata Rose ambaye ni mpenzi wa Abdul.

“Baba eh!! kama unavyojua bhana... ‘Abilia chunga mzigo wako’, unakoenda kesho, unaenda kumchukua Rose na kurudi, marafuku tamaa!” hicho kilikuwa ni kijembe cha mke wangu kilichotokana na wivu, mke wangu amabaye tulizoea kuishi kwa matani kila kinapokutana lakini jambo jema la kumshukuru Mungu ni kwamba hakuwai kunivunjia heshima hata siku moja, toka nimtoe kwao undendeuleni.

Tuliongea kidogo na mpango wa kuwahi kwenda kumchukua Rose kwani siku iliyofuata ilikuwa sio siku ya kazi; ni jumamosi. Na hatimaye tukalala kwani kila upande ulikuwa bize kuwaza historia kali ya maisha ya kijana ambaye yupo hatihani kutolewa roho kwa sababu ambazo hakuna anayejua zaidi ya msimuliaji mwenyewe, ambaye kwa wakati huo tayari neno Fofofofo Liliendelea katika chumba chake.

“Kokolikooooo!, kokokoko kokoli…” kama ilivyo majogoo ya kila siku, siku pendwa katika historia nyingine ya maisha ikaanza. Tukajuliana hali kila mmoja, na kwa mara ya kwanza jua la asubuhi liliniwezesha kuona kabisa uso wa Abduli ukiwa na tabasamu.

Baada ya kifungua kinywa nikaaga kwenda sehemu ambayo kila mtu aliifahamu, Abduli alinipa maelezo sehemu ambayo wanaishi kwa siri na mpenzi wake Rose, niliwasiliana na Rose kujua sehemu gani tunakutana, na kwa vile nilikuwa na namba yake ya simu haikunipa shida.

Nilianza safari kwa kuchukua daladala moja kwa moja hadi Bombambili stendi, sehemu ambayo tuliahidiana kukutana. Nilishuka stendi ya Bombambili na kuanza kutafuta namba ya mwanamke ambaye Abdul alimjaa kinywani, kila kichwao yeye ni Rose, Rose, Rose hadi kero! sijui ndio mzimu wake alaaah!. Niliendelea kuongea mwenyewe kimoyomoyo kwa muda kabla maada haijabadilika kichwani mwangu na kuanza kuwaza ni aina gani ya mwanamke ambaye bwana Abdul ametunikiwa, mke mjasiri ambaye amekubali kuishi na Kipofu kwa umaskini na matokomezo kadha wa kadha, hakika nilipata msisimko sana na kupongeza baadhi ya jitihada wafanyazo wanawake katika kupigania mapendo yao. Nilipofika nikafungua simu yangu kwa kutoa nenosiri, nikatafuta namba za Rose kupitia missed call na kuipiga.

“Hallo!, hallo,... eh wapi, wapi!!, ehh hallo!” bila maelewano simu hiyo ilikata, nikaipiga tena na nikajibiwa na muhudumu ambaye alikuwa zamu siku hiyo,

“Namba unayopiga haipatikani, Jaribu tena baadae”, nikakata na kupiga tena lakini mchezo ukawa vilevile, uso wangu ukaanza kuchukia na kuendelea kuangaza uku na uko kumtafuta mtu nisie mfahamu, niliangaza sana lakini sikufanikiwa kupata nilichokitaka, mshituko wa mayo ukanipata palepale nilipokuwepo mara baada ya macho yangu kuona mwanamke ambaye kwa mbali rangi yake ya maji ya kunde ilimulika mboni ya macho yangu.

Picha ya mke wangu ikafutika kichwani kwa kuanza kutoa sifa sisizostaiki kwa mwanamke ambaye sio mke wangu.

“Jamani Mungu fundi... Lo!” nikapaza ukuu wa mungu na nikajikuta namsogelea msichana huyo, kama tujuavyo wanaume sifa zetu pindi tumuonapo mwanamke ambaye maumbile yake ni mfano tosha wa kuamsha sehemu ambazo zimelala kwa mda. Alikuwa ni mchana mwenye rangi yake, sikumbuki kama kipodozi cha kemikali kishawahi pita katika uso wake; hakika anavutia. Alikuwa na nyele ndefu nyeusi ambazo alizifunga tu kwa kamba kichwani mwake upande wa juu, utadhani anazitumia kama ngata katika kubebea mizigo mizito. Nilimsogelea kuendelea kufahadi japo mapozi tu, alikuwa anakata kucha za mkono wake kwa kutumia meno huku mkono mwingine ukiangaika na simu ndogo kabisa ambaye ilikuwa haiendani na umbo lake. Nilipoganda kuendelea kumchora ghafla alinishtua na swali.

“Kaka naweza azima simu yako mara moja?” Swali hilo halikuwa na majibu kichwani kwangu, kwani aliendelea kunichanganya kabisa kwa kutumia sauti yake iyo ambayo kama wataalam wa utengenezaji wa simu wangeigundua basi wangeinyunyiza katika teknologia ya mlio wa kuitia katika moja ya kampuni zinazofanya poa duniani. Kweli niliongeleshwa ila nilibaki nimeduwaa kwa kukosa jibu, kwani hata kilichosemwa nilikikumbuka?, nikabaki kuishia tu aah!, Ah!... na kabla sijaangaika sana kijigonga gonga akarudia kile alichosema.

“Samahani lakini.... simu!, Naazima!” Hapo kilichozungumzwa kilikaa kichwani, haraka nikatoa simu yangu na kumpa mrembo yule, macho yangu bado hayakuchomoka usoni mwake.

“Kaka mimi siwezi tumia hizi! Naomba niandikie namba....” aliongea na kunizidishia mawazo. Inakuaje kwa kizazi hiki mtu mrembo na mwenye miaka yake duniani anashindwa tumia smartphone. Nikabaki nashangaa tu. ‘Jamani kwa lika kama ya huyu dada halafu anasema eti hawezi kutumia “Smartphone” Laulaaa!’, nilipigwa na butwaa la moyomoyo ambalo hakuna alieliona zaidi ya moyo wangu wenyewe.

“Mhhh namba!” nikajikwakwamua kutoa msaada.

“0757.. 9947....” kabla hajamalizia kuitaja namba hiyo, nikainua macho yangu na kumtazama kwa makini, nilikutana na uso wa tabasamu wa mrembo yule, kilichonishangaza ni kuwa namba hizo alizokuwa anazitoa kichwani. Yaani bila kuangalia sehemu yoyote ile jambo ambalo lilinishangaza sana. Sikumbuki kama alimalizia kutaja namba za mwisho au la, lakini tukabaki tu kuangaliana, huku mimi nilimshangaa yeye na yeye akishangaa mimi kwa mshangaa yeye.

“Unamtafuta nani?” Nikajikuta namtupia swali rahisi kwake.

“Abdul..... A....” likalirudia mara mbili lile jina la Abdul, hapo nikastuka katika dimbwi la mawazo na kuanza kumkazia tena macho mrembo yule. Nilikuwa kama sijaelewa alichozungumza kwa mara nyingine. Lakini alitaja bila kusita, tena mara mbili. Kitu ambacho kilinifanya niamini ni yeye Rose ni kuwa alipotaja namba alitaja namba zangu kabisa ambazo nilitumia kuwasiliana na yeye. Nikataka kupingana na macho yangu kama yule ndio kweli mwanamke ambaye ametekwa na kijana kama Abdul. Kwa kweli baada ya jina hilo, kilichofuata ni maswali na majibu tu ambayo nilikuwa najiuliza mwenyewe bila kupata nafasi ya kujijibu.

“We ni rose?” naaam, nikamtwanga swali ambalo lilimwacha kinywa wazi!, niliuliza kutaka kuhakikisha tu. Akainamisha kichwa chini kwa hofu ya kujibu. Alikuwa anaogopa.

“Okey mimi ni Xavery!, Xav... kama unamtafuta Abdul basi hapa ndipo sehemu sahihi na muafaka kabisa, nipo nae kwangu!”. Nikamwaminisha.

“Kaka samahani, nilikuwa naitaji huduma ya simu tu basi, kama hapatikani naomba mimi niende” akainua kichwa chake chenye aibu na kuongea, hakuchukua sekunde akaanza kugeuka tayari kuondoka.

“Rose ni mimi bhana, nimeagizwa na Abdul, nimepatwa na mshangao mara baada ya kusikia namba iliyotaja ni yangu. Mwishoni ni 87! Si ndiyo?, Abdul yupo salama na anakuitaji, na mguu huu ulikuwa kwako. Sikufahamu na nisingeweza kukufahamu kwa mapema namna hii, utambulisho pekee ambao nilikuwea nao mkononi mwangu ni namba yako tu ya simu. Nimepiga sana lakini hupatikanai” nilijitahidi kutokwa na maneno ya ukweli kwa mfurulizo kwa kumwaminisha binti yule, akageuka tu na kutoa chozi jembamba lililotililika hadi mashavuni mwake, lakini hakuharibu kitu katika kung’aza uzuri wake, alipendeza hadi wakati analia. Alinisogelea na kunitaka radhi.

“Kaka angu, ni vigumu kumwamini kila mtu kwa sasa, tunatafutwa sana, sio mimi wanaoniitaji, ni Abdul, kwa maana hata tukiwa wawili mimi na yeye, basi wataanza na yeye. Nampenda sana mume wangu jamani, naomba nikamwone” alitoa ombi la mwisho kwa kilio, nilimwonea huruma kwa kweli, nikawaza shida anazopata kwa kuishi na kipofu angali yeye ni malaika namna ile, vipi kelo za wanaume wanaomsumbua kumtaka kimapenzi?. Basi nikachukua nafasi ya kumbembeleza hadi kutulia.

Tukachukua usafiri wa pikipiki, niliwaza sana tunapandaje pikipiki moja na hali ya nyuma ilivyo nzuri ya binti yule. Rose alibeba kila kitu sehemu zake za nyuma, alikuwa mwemabamba wa kukonda kwa maisha tu ila mwili ulimkaa vizuri sana, mbinuko wake wa nyuma na shepu yake ya uchanga vilionekana.

Sasa nawezaje kupanda nae pikipiki moja? Nani atakaa mbele na nani nyuma? Mwanaume nikae mbele, hapana, nikae nyuma! Lo! Na ilo sebene ya matuta njiani ikuru yangu itaweza vumilia kweli ikigusana na mlima Rose? Na akiniona mke wangu huo ni ugomvi mwingine, nikatabasamu na kuchukua pikipiki mbili, kila mmoja aliapanda yake na kuanza kuingoza njia kuelekea nyumbani.

Hatukuchukua mda mrefu tayari tulishaingia mlangoni, sikuwa na mlinzi wala haouse girl nyumbani mwangu, nikafungua mlango mwenyewe na kuingizana ndani na Rose ambaye roho yake tayari ilianza kuweuka mara baada ya kuona amekaribia sehemu ambayo roho yake imefia mazima.

Ile kuingia tu.. tukakalibisha vilio vya furaha vilivyosindikizwa na machozi. Si kwa furaha ya Roze, vipi upande wa Abdul?, kwa mara ya kwanza nikaona nyuso ya tabasamu kwa Abdul huyu jamaa ukimwangalia kwa makini unaweza sema sio kipofu. Kwa maana hakuna anachokosea yaani kila kitu anafanya sahihi utadhani ana macho yote mawili!!!

ITAENDELEA...

Starxav
Karbuni Mno....... Mnooooo

Starxav
 
SIMULIZI: “TOKOMEZO” (05)
MTUNZI: XAVERY EMMANUEL (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Whatsapp: 0769765748
Namba: 0672493994
Social Net: @star_xav

Hatukuchukua mda mrefu tayari tulishaingia mlangoni, sikuwa na mlinzi wala haouse girl nyumbani mwangu, nikafungua mlango mwenyewe na kuingizana ndani na Rose ambaye roho yake tayari ilianza kuweuka mara baada ya kuona amekaribia sehemu ambayo roho yake imefia mazima. Ile kuingia tu.. tukalibisha vilio vya furaha vilivyosindikizwa na machozi. Si kwa furaha ya Roze, vipi upande wa Abdul?, kwa mara ya kwanza nikaona uso ya tabasamu kwa Abdul huyu jamaa ukimwangalia kwa makini unaweza sema sio kipofu. Kwa maana hakuna anachokosea yani kila kitu anafanya sahihi utadhani ana macho yote mawili!!!. Hakuchukua muda Abdul akaanza kutupa siri!, ile siri ambayo inajulikana na wachache tu.

SEHEMU YA TANO.
*************
“Ndugu Mwandishi, labda nianze kwa kujitambulisha vyema kabisa ambapo kila mtu sasa anijue kwa mapana. Haikuwa kusudi langu kusema ukweli huu uliojificha kwangu kwa miaka zaidi therathini na mbili, hakuna yeyote yule mwenye dhamana ya kujua wapi natoka wala wapi naelekea,” akasita kidogo kuongea na kisha kuangalia upande ambao kipenzi chake Rose alikuwepo, utadhani walionana vile, macho yao yakagongana angali mmoja alikuwa haoni na mwingine alikuwa anaona vyema kabisa, macho yao yalifumuka kama ‘tai aliponyang’anywa kitinda mimba chake’. Kisha bwana Abdul akaendelea.

“Samahani sana kipenzi changu Rose, samahani sana dunia, hamkupasa kujua kweli hii, nimefumbuliwa lindo la matataizo ambayo yamenifanya kufungua kinywa changu kwa kueleza kila kitu.

Ndugu mwandishi mimi kwa majina halisi kabisa ambayo nilibatizwa na Baba yangu mzazi Mzee Yohana, ni Denis Ephrehem, jina ambalo nilipewa halali kabisa na Padre wa kizungu aliyekuja kutubatiza kipindi chake cha likizo fupi aliyokuwa akimaliza uko wilayani Ludewa, mkoa wa Njombe.

Familia yetu ilikuwa karibu sana na kanisa katoliki la Roma, hakuna siku ikaisha hatujataja jina la Yesu Kristo wa Nazareth. Familia yetu ya Mzee Yohana na Scolastica Alfred ambaye ndio mama, ilikuwa ya amani sana, tulikuwa watoto wawili tu, mimi Denis na dada yangu kipenzi Maria….” Hapo Adbul ambaye kwa muda huo alijitambulisha kwa jina la Denis alianza kutililisha chozi lake taratibu kwa kukumbuka kitu. Rose alionekana kukosa amani baada ya kujua kwa mara ya kwanza kuwa mpenzi wake jina lake halisi ni Denis na sio Abdul kama anavyojua. Aliongopewa.

“Mwandishi dada yangu! Dada yangu mpenzi anaitwa Maria!, Mimi na Maria tulipishana miaka Minne tu toka kuzaliwa kwangu, nakumbuka alizaliwa miaka minne ya mbele baada ya kuzaliwa mimi mwaka 1986. Ukiniangalia kwa sasa utadhani mimi ni kikongwe ambaye nina miaka kuanzia sitini na mbili hadi sabini na tano; umri ambao unatosha kabisa kustafu kero na shida za dunia.

Bado kijana mimi Mwandishi, ni maisha magumu niliyopitia hadi kufanya mwili wangu kuzeeka angali umri bado upo kijana kabisa.

Mwandishi baba yangu alibahatika kuwa na baadhi ya fedha za kujikimu katika maisha, wachache wenye upumbavu kichwani wanasema ni Mali. Alikuwa na makampuni kadhaa karibia kila mji, mengine ya kuchakata tumbaku, mengine ya alizeti, mengine kuchakata mkonge, mengine sijui nini. Kwa takwimu chache ambazo familia nzima tulikuwa tunaijua ni jumla ya makampuni si chini ya kumi. Achana na zile ambazo baba aliamua kutuficha, si mimi wala mdogo wangu aliyekuwa anazijuwa. Alikuwa na makampuni kedekede.

Siku zilienda na maisha yalikuwa mazuri, sikupata bahati ya kuwajuwa ndugu wote wa upande wa baba na wale wa upande wa mama. Maisha yetu yalikuwa ndani tu, hakuna misiba wala sherehe za jirani tulizohusika nazo. Tukitoka nje basi ni kwenda shule na kurudishwa na gari. Shule zenyewe ndo hizi za Yes, No, Ofcourse. Kila hatua kwetu ilinukia pesa tu.

Baba alikuwa mtu mkubwa amabaye, hata akiomba sehemu awe kiongozi basi wapinzani wote wanarudi nyuma kwa kuogopa ushindani; pesa zilitupa kiburi mno. Nadhani huu ndio mshahara wa dhambi zetu, umenitesa sana Baba!, umemtesa Mama, Umemtesa Maria, Umenitesa mimi na kizazi chako kijacho!, ziko wapi pesa zako Baba!!”. Denisi aliishia hapo na kuanza tena kulia, kilio chake hakikuwa cha sauti, nyumba yote ilikuwa kimya sana. mke wangu alikuwa ameduwaa kwa utamu na uchachu wa machungu wa maneno alikuwa anautoa Abdul, Abdul alikuwa fundi wa lugha kweli kweli, kwa hatua hii hakuna asiyeamini kuwa mtaa ulimfunza. Baada ya kufuta chozi mwanaume akaendelea.

“Mwandishi, si unajuwa kuwa Akipangacho Mungu, binadamu katu hawezi pangua?. Usiangaike kujibu, ni kweli kabisa Mwandishi, Mungu alipanga na ikatokea.

Ilikuwa siku ya jumapili ya mwaka 2000 Jioni ya saa kumi na mbili kasoro, Nilikuwa nyuma ya kochi alilokaa Mama akiwa anaangalia televisheni ya Taifa, ulikuwa muda wa taarifa ya habari. Mimi nilikuwa naendelea kujisomea na kujiandaa na mambo yangu ya kishule kwani ndio ulikuwa mwaka wangu wa mwisho kumaliza elimu yangu ya msingi.

Lakini ghafla nilisikia kishindo cha ghafla nyuma yangu kama kitu kizito kimeanguka. Haraka nikakimbilia eneo ambalo kishindo kimesikika. Nilimwona Mama yangu mzazi akiwa chini, nilipigwa na bumbuwazi la maana kwa kushitushwa na hali hiyo. Nilianza kumwita kwa kumwamsha nikitumia sauti kubwa huku mikono yangu ikikazana kumtikisa nimwamshe. Katika kuangaza angaza nilikumbana na mwisho wa taarifa ya habari kutoka runingani. Nikatulia tuli kuimalizia..

“...Afisa wa polisi mkoa wa Morogoro amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo mnamo majira ya saa kumi na mbili jioni. Afisa ametoa angalizo kwa madereva ya magari binafsi kufuata taratibu na sheria za barabarani kuepusha ajali kama hizo. Roho ya marehemu Mzee Yohana ilazwe mahali pema peponi… Amina” Mwisho wa habari hiyo iliandamana na baadhi ya picha za gari lililochakaa kwa kujimega upande mmoja wa mbele, wahudumu wa kwanza wakifunika maiti na kupakia katika mifuko maalum ya kuhifadhia, kisha kuweka katika gari tayari kwa kuutoa mahali pale.. Picha ambazo zilionekana runingani ni picha ya ajali ya gari. Gari la Baba! Nilistuka na mikono yote kujikuta ipo juu ya kichwa changu kwa sekunde tu.. nikaja kujuwa kuwa Mama amepoteza fahamu kutokana na mshituko wa taarifa hiyo.

Nikapiga ukunga wa maana uliomwamsha hadi mdogo wangu usingizini, tuliungana kujitahidi kumwamsha Mama lakini mdogo wangu hakujua sababu na chanzo cha mama kupoteza fahamu. Sikuweza kumwambia. Mikono na sauti vilikazana kumwamsha Mama; ila akili ilikuwa mkoa wa morogoro kwenye maiti ya Baba.

Hakuna jilani yeyote aliyesikia kilio chetu. Hata kama wangesikia ni dhairi kuwa hakuna hata mmoja ambaye angethubutu kukanyaga kwetu. Hatukuwa na ushilikiano mzuri na majilani wenzetu, kwani tulijua pesa ndio kila kitu. Tulilalama mimi na mdogo wangu hadi mashangazi wa karibu walipofika mkuku baada ya kupata habari kupitia televisheni zao makwao. Walitutoa pale na kutupeleka chumbani na wao wakaendelea na taratibu za kumpa Mama huduma ya kwanza. Kutokana na kushindwa vumilia hali nilikuwanayo nilianza kugombana na mtu ambaye tulikabidhiwa chumbani humo ili awe mwangalifu kwetu, nilikuwa mbishi kwa kutaka kumwona Mama yangu yu katika hali salama.

Ubishi wangu ulipelekea kumshinda nguvu mwanamama yule wa rika, nilimtoka mikononi mwake na kupitiliza moja kwa moja katika mlango wa kutokea chumbani humo. Sikufika mbali hata, nilipiga mweleka wa nguvu katika marumaru ambazo kila siku tulimsifia fundi kuwa katumia kipaji chake kwa kuzinakshi vyema. Siku hiyo zilinisaliti, nilianguka kama jiwe na kupoteza fahamu hapohapo…” Ndugu Mwandishi. Nakupa onyo! Katu usilingie mali! Mali si kitu kwa kweli, ona sasa. Hadi marumaru nilizozizoea kuchezea na kukimbia nazo kila siku niendapo shule zimenisaliti kwa kunizimisha kabisa.

Hazina hata chembe ya huruma, zinajua kabisa nimefiwa, tena msiba mkubwa; haya ona naenda kumwona Mama yangu nazo zinanikataza, tena zinanizuia kwa kuniumiza. Mwandishi hadi Marumaru?. Lo! Kweli ‘Mbio za sakafuni huishia ukingoni’. Abdul akaongea kwa machungu na masikitiko makubwa kisha kuendelea.

ITAENDELEA..

Starxav
 
SIMULIZI: “TOKOMEZO” (06)
MTUNZI: XAVERY EMMANUEL (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Whatsapp: 0769765748
Namba: 0672493994
Social Net: @star_xav

Ndugu Mwandishi. Nakupa onyo! Katu usilingie mali! Mali si kitu kwa kweli, ona sasa. Hadi marumaru nilizozizoea kuchezea na kukumbia nazo kila siku niendapo shule zimenisaliti kwa kunizimisha kabisa. Hazina hata chembe ya huruma, zinajua kabisa nimefiwa, tena msiba mkubwa; haya ona naenda kumwona Mama yangu nazo zinanikataza kwa kuniumiza. Mwandishi hadi Marumaru?. Lo! Kweli “Mbio za sakafuni huishia ukingoni”. Abdul akaongea kwa machungu na masikitiko makubwa kisha kuendelea…

SEHEMU YA SITA
“Nilipokuja kuzinduka, ilikuwa ni siku ya mazishi, Msiba haukuwa na watu niliowazoea, majilani walikuwa wachache wenye roho ya kusamehe. Rangi nyeusi ilitapakaa kuzishinda rangi nyingine. Wanaume wakiwaka kwa suti kutoka bara la jilani, huku tai zikiwa kama kikorombwezo cha kupima kasi na uelekeo wa upepo. Zilikuwa zinapeperuka tu.

Macho yangu yalikutana na Mama ambaye alionekana amevimba macho huku bado akizidi kuendeleza kilio cha polepole bila machozi kuonekana. Sikuwa na uelewa wowote ule kuhusu msiba wala mazishi. Niliungana tu na mama kulia hadi tulipoelekea makaburini na kupumzisha mwili wa Baba yangu mzazi. Baada ya mazishi, watu wote wakapotea na kutuacha tukiwa mimi, Mama na mdogo wangu Maria. Hatukuwa na ndugu wa karbu.

Tulianza maisha mapya ya uyatima wa upande mmoja, Baba alikua ndiye kichwa na mshughulikaji wa familia, kupotea kwake kulisababisha mambo mengi sana kukwama. Mama alikuwa ni mwingi wa mawazo kwa kuwaza mustakabali wa kikao cha familia kitakacho fanyika siku ya ishirini na tisa baada ya mazishi. Tarehe maalum kabisa iliyopangwa na ndugu wa marehemu. Lengo ni kujadili masuala mbalimbali ya familia.

“Mwanangu, we ndio mkubwa hapa, we ndio Baba!, mtunze mdogo wako Baba eh! Sawa!” Mama aliongea kwa upole sana akionesha wasiwasi machoni kwake. Nilitumia kila fursa kumrudisha katika hali yake ya kawaida hadi tukaweza, nafasi kubwa na mpango huo aliufanikisha mdogo wangu Maria.

Maria alikuwa ni mchekeshaji mkubwa sana sijawai kuona, kama hutacheka basi lazima ufurahi. Licha rangi nzuri ya kuvutia kwake, Maria alikuwa kiboko ya wanaume wanaopenda mambo ya kuchipukia, kifuani kwake alibeba mzigo mwepesi uliotuna kwa ugumu wake kama makande ya wanafunzi katika shule za serikali. Hali hiyo ilifanya kila nguo nyepesi aliyovaa kutanuka kidogo hadi kutaka kutoboka kwa jinsi chuchu zake zilivyochongeka, hilo lilionekana kwa macho tu, alikuwa mzuri dada yangu sijui ni sababu ya pesa au ni malezi tu, au ndio kazi ya Mungu kama wasemavyo Manabii na Mitume!.

Basi siku ya hitimisho la mazishi lilifika, ilikuwa siku ya kikao cha familia. Kwanza likapigwa sebene la kufa mtu. Watu walikula nyama za aina tatu tofauti, ukianza na Ng’ombe mkubwa basi unamaliza na Mbuzi au supu ya kuku. Ni taratibu za familia na koo hiyo. Hakuna aliyethubutu kupinga kati yetu.

Mama hakupendezwa na mambo hayo lakini hana usemi wowote mbele ya wakubwa. Kitu cha kushangaza zaidi ni kutokumwona ndugu yoyote yule wa upande wa Mama, walijaa wote wa upande wa Baba na wengi nilikuwa siwafahamu, ila kuna sura ya Baba mdogo ambayo niliizoea sana kuliko ndugu wote pale.

Kikubwa ni kuwa hakukuwa na ushilikiano mzuri kati ya familia yetu na ndugu wa pande nyingine, walikuwa kama wametutenga hivi. Baba mdogo tu ndiye niliyemfahamu haswa, yeye alikuwa akiletwa na Baba mara nyingi nyumbani. Ndiyo walikuwa karibu kuliko wengine. Hivyo nikapata sana kumkumbuka yeye. Nakumbuka pesa nyingi niliziona kwa macho yangu kutoka kwa Baba na zikimiminika kwa kumpa mtaji Baba mdogo, na alikuwa anakuja mara moja baada ya miezi kama mitatu hivi. Mtu na mdogo wake walishibana kwelikweli.

Walipohakikisha kila mhusika wao amehudhuria kwenye kikao kile, Mzee mmoja mwenye mvi alinyanyuka na kutoa utambulisho.
“….. Binti, kiko wapi mlichokuwa mnajivunia?, mkakimbia wazazi kwa kutaka laana, mkafunga ndoa wawili tu wenyewe. Ndoa ya shetani wewe na baladhuri wako!, hukujua kuna siku mtatengana?. Vione na vitoto mlivyozaa… jamani!! mtoto wetu katutia aibu sana. Mwanamke tuliyemtafutia sisi ndio alikuwa bora mno. Yule alikuwa mcheshi, mkarimu!, eh!, mwanamke anashepu jamani sa yeye kaenda kwa dangulo na pesa zake kuokota huyu Malaya. Lo!..” Mzee aliyesimama alianza kuongea bila shida baada ya kutambulisha ndugu zake wote. Nilishangaa mno kwa matusi mazito kama yale kutua kifuani kwa Mama yangu. Kama nilivyohisi, nilimwona Mama anaanza kunyanyuka kwa nguvu na kuanza kuingilia kati suala hilo lakini kabla hajafanya lolote sauti nzito nyingine ilisikika.

“Kaa chini Alaah! Huna adabu?”, ilikuwa ni sauti ya Mzee mwingine ambaye alitambulishwa mwanzoni kuwa ni babu yangu. Yaani baba yake baba.

“Yale yalee… tulisema sisi, Mtoto… wakubwa wanaongea afu….. Mwee!”, Mwingine akachangia mada kuendeleza wimbi la ushindi, huyu alikuwa ni mwanabibi. Kama kikao hicho kilikuwa ni mchezo wa mpira wa miguu, basi mpaka sasa tulishwa fungwa goli tatu kwa sifuri katika uwanja wetu wa nyumbani.

“Hahahaha, sasa wakubwa!, hakuna namna hapo, msameheni tu. Hajui mila na taratibu tu za koo yetu, si kashaolewa!!, hakuna haja..” Baba mdogo nae alionesha dhahiri kuwa hakuwa upande wetu. Licha ya misaada yote ile lakini bado alitukana, Roho iliniuma sana kwakweli. Bado Mama hasira hazikumshuka. Alitaka usawa.

“Taratibu ni zilezile zinajulikana, sema tukumbushane tu,…” aliongea mzee yuleyule wa mwanzao, akafungua makatasi na kuendelea kuongea.

“..aah!! marehemu ameacha mali nyingi sana. Ambazo zooooote zitakuwa chini ya usimamizi wa Mdogo wake. Namaana zooote. hahaahaha” yule Mzee aliendelea kuzungumza. Mama akaonekana kutaka kutoa neno lakini kigugumizi kilimshika na bado hali yake haikuwa nzuri sana kutokana na majanga ambayo ameshindwa kuyahimili. Bado kidonda cha kifo cha mume wake kilikuwa kibichi kabisa, sasa hawa nao wanamtia pilipili kwa kutaka apone mapema, jamani binadamu hawana huruma asee. Tayari waligusia urithi wa Mali.

“Na kwa taratibu za mila na tamaduni zetu pia, Bwana Furedi utarithi mke na mali nyingine zilizopo!.” Akaendelea.

“What????!” Mama aling’aka na kuinuka kwa nguvu huku mikono ikisaidia kuifunga vyema kanga yake na kufanya mdomo kuongea bila ruhusa. Tayari alisharuhusu hasira zake kuonekana hadharani, katu sikuwahi kumwona Mama katika hali kama hii. Mama alipatwa na hasira za ajabu.

“Kurithi Mke! Nani? Mbwa huyu! Huyuuuu!....., Aaahg! habari za wapi hizi jamni!!. kwanini mnapenda kushindilia matuta ambayo yanamalengo ya kuzalisha miche mingi?, Nini nimekosa eh baba!” Mama aliongea kwa nguvu sana na baadae kupunguza sauti kwani kilio kilichukua nafasi. Alianza kulia Mama yangu.

“Mwanangu!, Ukipenda boga penda na ua lake!” Babu nae alishindilia nyundo ya maumivu kwa umakini bila kupepesa macho.

“Hiyo ni lazima, hutaki toka na hizo takataka zako mbili peleka kwenu uko wapi sijui!” Yule Mzee wa Kwanza kutufungulia kikao alikuwa mkali kwelikweli; kama pilipili kichaa. Nilipojaribu kuingilia nikavamiwa na familia nzima kwa kukosa adabu. Nikatulia tulii… Maamuzi yakapita wakashinda wao japo walitumia uwanja wa ugenini, idadi ya magoli tuliyofungwa ilitosha kabisha kufungiwa na shilikisho ya Maisha Duniani (SMD). Kwa kuwa wao ndio wenye nguvu, wakashinda.

Baada ya kutuzidi nguvu na kiongozi wa upande wetu alikuwa wa kike, tukasalimu amri!. wakatuacha nyumbani hapo na wote wakatawanyika. Ndugu wote walikuwa wanaishi mbali na sisi, wengine walivuka hadi mkoa. kwa taarifa za awali kuwa Mama na Baba waliishi mbali na familia yao kwa kuwa Baba alikanwa na wazazi wake kwa kumuoa Mama yangu. Wazazi wake hao walitaka aoe mtu wa tamaduni na kabila lao ambao wao walimteua.

Tukawa na kazi nyingine ya kumbembeleza Mama huku wote tukiendelea kuumia kwa kitendo kilichotokea, si mimi wala Maria wote tulikuwa katika umri sahihi wa kujua lipi baya na lipi jema. Maisha ya wasiwasi yalianza, tuliishi hapohapo kwani hatukuwa na pa kwenda.

Kwa maelezo ya Mama alituambia kwamba yeye hana Mama wala Baba, wote walifariki wakati wa utoto wake. Tukabaki katika jumba kubwa ambalo kwa sasa lilikuwa kama Jumba la Vilio Tanzania, kila kukicha ni kudeki machozi tu. Tuliumia mno kwa hatua waliyofikiana wanandugu. Yaani Baba mdogo ndio mrithi wa kila kitu hadi mama yangu?.

Siku ya tatu baada ya kikao alikuja Baba mdogo Frank, eti alikuja kumwona mke wake na kumwambia siku rasmi ya yeye kuja kuishi nae. Tulimwacha ajimwage na maneno yake ya kebehi na kisha akaondoka. Alikuwa amesahau kabisa misaada yote uliopitia kwa baba yangu. Kweli Dunia hadaa! Namchukia Baba Mdogo. na nitamchukia hadi kufa kwake...

ITAENDELEA…

Starxav
 
Kuna binadamu wasikitisha sana...

Hivi hii mila ya kurithi mke wa marehemu, kwa nini mwanamke asikatae kabisa kutoa ushirikano kwa anaye mrithi...

Ngoja tuone...



Cc: mahondaw
Mkuu, wengi hawakubali hiyo hali ila sasa maisha wanayoishi baada ya kukataa yanakuwa mabaya sana. fikilia unaambiwa huna chako, then huna pa kwenda utafanyaje?? weng hawapendi ila tu wanakubali kubak ili wale angalau chakula cha mali ya marehemu.

Inasikitisha sana Mkuu!!

Starxav
 
SIMULIZI: “TOKOMEZO” (07)
MTUNZI: XAVERY EMMANUEL (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Whatsapp: 0769765748
Namba: 0672493994
Social Net: @star_xav

Siku ya tatu baada ya kikao alikuja Baba mdogo Frank, eti kumwona mke wake na kumwambia siku rasmi ya yeye kuja kuishi nae. Tulimwacha ajimwage na maneno yake ya kejeri na kisha kuondoka. Alikuwa amesahau kabisa misaada yote uliopitia kwa baba yangu. Kweli Dunia hadaa!!.. Namchukia Baba Mdogo. Na nitamchukia hadi kufa kwake.

SEHEMU YA SABA.
Basi ndugu mwandishi japo kwa shida lakini maisha yaliendelea kama kawaida, shule ilikuwa inasonga vilevile tu kama kawaida kwani ndio ulikuwa mwaka wangu wa mwisho kuhitimu darasa la saba. Kitu kizuri ni kwamba baba alishalipa ada na michango yote ya shule. Siku zilizidi kwenda tu.

Ndugu Mwandishi, Baba mdogo aliamua kabisa kukata kutokuja nyumbani, ulipita zaidi ya mwezi mmoja sikuona pua yake mlangoni kwetu. Ndani ya mwezi huo mmoja tabasamu la mama likarudi tena kama awali, alianza kuzoea kabisa hali ya maisha iliyopo. Mambo yote yalienda vizuri japo si kama kipindi Baba yangu mzazi yupo. Katika biashara hakuna aliyeleta chochote wala kuelezea habari ya biashara alizokuwa anafanya Baba, labda zilikuwa chini ya mamlaka ya Baba Mdogo Frank. Na wala hatukuthubutu kuulizia mambo hayo. Tukabaki na amani yetu changa.
“Hahahaha we maria wewe! Sidhani kama shule ipo hapa. We umekaa maksihara maksihara tu!... umesema unataka kuwa nani? Hahahahaha!!” Kilikuwa ni kicheko cha mama cha mwisho cha kumalizia mwezi wa furaha. Baada ya hapo akanyanyuka na kwenda kufungua mlango kuna mtu alibisha hodi. Alipofungua mlango akakabidhiwa barua na kurudi tena ndani.

“Nataka kuwa boooonge la Mchekeshaji huhuhuhu!!, kuna siku mtanishuhudia nipo kwenye masteji makubwa huko… ah kama najiona hivi, Cheka tu stage, Churchill Show stage,.. up to Amerikaaaa oyoooo” Jibu la mdogo wangu lilinikata mbavu kwa kweli, tulicheka sana jamani, Maria alikuwa vizuri katika kuchekesha lakini kwa jitihada za masomo hapana, hakuwa na ushilikiano na kitu kinachoitwa Shule. Mbali na mdogo wangu na mimi nilikuwa na ndoto ya kuja kuwa mwandishi mhariri au mtangazaji mmoja mkubwa wa Tanzania na kufahamika dunia nzima kwa ujumla.

Mama alicheka lakini hakuonyesha hata jino lake moja, ‘Macho yalikuwa bize kufungua barua’ aliyeipokea punde. Alisoma taratibu hadi kuifikia katikati barua hiyo, tukamwona anasimama na kuelekea chumbani kwake, tulikaa hapo barazani tukiendelea tu kubishana kuhusu ndoto zetu za baadae. Hakuna aliyehisi hali tofauti ya Mama. Hadi baadae Mama akarudi na kukaa tena karibu yetu, hakuwa tena na furaha kama mwanzo, swali la kulikoni lilimwangukia miguuni mwake lakini hakujibu zaidi ya kuendelea kupandisha kamasi zake kama zimelegea na kutaka kutoka bila ruhusa. Nilijua kabisa hakuna jema linaloendelea hata macho yake yalionesha uvumbe wa machozi. Alikuwa ametoka kulia sana mda sio mrefu.

“Denis… Maria!...” Alituita kwa majina yetu halisi. Akasita kabla ya kuendelea

“Wanangu hamna chenu hapa!!” alianza kuongea kauli tusiyo elewa inamaana gani kwa upole huku akizichezea nywele za Maria, kisha akaendelea.

“Hata kama nisipokuwepo mbeleni, hakikisha mnasoma! Msikubali kuwa na rafiki mjinga hata siku moja. Bora muongozane na Shule atawapa zawadi ya elimu, vipi kwa mjinga?. Denisi wewe ni mkubwa eh!. Maria kama unavyomwona, usimwache mdogo wako..” Mama alimaliza na kutotaka mazungumzo tena, alitoka nje kabisa ya nyumba, tulimchungulia tu dilishani anavyo kata mbuga kufungua geti. Tukabaki na mawazo mengi sana ambayo mengi yalikuwa ni maswali tu. Tupo mimi namdogo wangu, maswali yetu yalikuwa mapacha kwani yanafanana kwa asilimia zote, nani atatoa majibu?. Tukabaki na huzuni zetu hadi jioni ilipotia timu na uzuri Mama alilejea nyumbani. Kila tulilomuuliza alitabasamu na kujibu “Hakuna tatizo mwanangu”. Hatukupata ufafanuzi wa kile kilichombadilisha kwa nyakati zile.

Miezi ilizidi kukatika, na shida zikawa zinaendelea kugonga mlango. Mama alikuwa ni mtu wa kumwaga machozi kila baada ya siku mbili, hatukuwa na uhakika na kilichomliza lakini machozi hayo yalisababishwa na barua anazopokea. Sikujua ni nani ambaye anatibua furaha yetu siku zote.
Kuna siku nilikuwa chumbani kama kawaida. Mlango ukagonga na mtu wa kuleta barua alikuwa mlangoni kama anavyofanya kila siku, akakabidhi barua na kuondoka zake.

Nikamwona Mama akiketi katika kochi na kuanza kuifungua barua hiyo. Alisoma taratibu hadi kuifikia mwisho, akanyanyua fito ya ukingo wa kanga yake, akapikicha macho kidogo kisha akaweka sawa nguo yake. Akanyanyuka na kuichana barua hiyo kisha vipande vya karatasi hiyo akaongozana navyo hadi chumbani kwake. Kipindi hicho bado nilikuwa nikimchungulia mlangoni kwangu, alichukua mda kutoka ndani, alipotoka alikuwa ameshavaa nguo nzuri. Nguo ambazo anapenda sana kuvaa anapoenda kanisani. Akaniita na kuniaga kuwa anatoka. Suala la anakoenda hakuligusia kabisa, nikamwacha aondoke namimi kama ilivyo ada nikamsindikiza hadi nje kwa macho hadi anapotea.

Magari yalikuwepo ndugu Mtangazaji lakini nani anaendesha?. Labda mimi ningekuwa mkubwa ningemsaidia kumpeleka mwanamke yule aendako. Baada ya kuhakikisha kuwa ameshaenda mbali kidogo nikaelekea chumbani kwa Mama kukagua kama nitakutana na vipande vya barua ile iliyomfikia mda mfupi. Kwa kuwa Mama hakuwa na tamaduni ya kufunga mlango wake labda tuwe tumetoka wote, hivyo ikawa urahisi wa kufanya uchunguzi wangu. Ndugu mwandishi hawa watu wanofanya shughuli za upelelezi we wasikie tu. Wanakutana na makubwa sana katika kazi zao. Kazi hiyo lazima uwe mkubwa kwa umri na umbo maana kila unachofanyia upepelezi ni siri ya mtu. Najuta kujiingiza kwenye taaluma hii feki ya upelelezi ambayo haikuwa chaguo langu.

Sasa nilipofungua tu mlango nikakutana na ndoo maalum la kuwekea makaratasi na mabaki ya nywele anapochana pamoja na uchafu mwingine mwepesi. Juu kabisa nikakutana na siri niliyoitaka!, Ni siri nzito maana ilichanwa na kufinyangwa finyangwa kama ule udongo ambao Mungu alitumia kutengenezea binadamu kama Samson wa derila. Nilichukua makaratisi hayo na kuiunganisha ipasavyo. Mwandiko ulikuwa mbovu kabisa, tena maandishi yote yalikuwa kwa herufi kubwa tu. Inaonekana mwandishi wa barua hiyo nilimpita kidato. Basi nikaungaunga na kupata muunganiko na maana ya barua hiyo nzito. Ilisomeka vizuri sana japo kwa shida:

“MKE WANGU MAMA DENISI KIPENDO CHANGU MAMA MARIYA
MUME WAKO NAKARIBIYA KUKUJA HIVYO KARIBUNI TU, KAMA NDIVYOSEMAGA KWENYE ILE BARUWA YANGU ILE YA MWAZO. NDO NAKUJA SASA KUONYA JAPO TAMU YA KAKA YANGU MALEEMU
MIMI NIYO MUME WAKO SASA NAKUJAGA SA KULISI MALI YANGU. ILA NIKIJA MIMI NATAKA TU PEZI LAKO NA MALI BASII. BADA YA HAPO UTAPOTELEA MBALI SITAKI KITU MIMI KIGINE ZAIDI YA MALI TU.
NI MIMIMI MUME WAKO FUREDI”

Mwisho wa barua hiyo ni mwanzo mwingine wa chozi la mtoto anayejuwa maana ya mapenzi na thamani ya mali. Machozi yalinitoka sana na kufanya karatasi ilo kuanza kulowa. Nilikumbuka kuwa sipo katika chumba changu, nikafinyanga tena lile karatasi na kutupa mule mule nilipochukua. Nikenda chumbani nikiwa na fungu la kisasi moyoni. Nilimchukia Baba Mdogo kwa kweli na koo nzima ya Baba. Nilimlaani na kuhakikisha iko siku itafika, ataingia katika kumi na nane zangu.

ITAENDELEA…

Starxav
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom