SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA SITINI NA NANE
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA SITINI NA SABA: Lakini kabla mzee Mahadh haja ufikia mlango mara wakamuona Idd akirudi ndani kwa haraka, nusu amkumbe baba yake pale mlangoni, ikionyesha wazi kuwa Idd alikuwa anakimbia kitu kule nje, na wakati wanashangaa na kujiuliza kulikoni, mara wanamuona mwanamke mmoja mtu mzima akiingia pale mlangoni, “weeeee! weeeee! we kaka leo hunikimbii, naomba unilipe….” ghafla yule mwanamke alisita na kusimama akionekana kuwa hakutegemea kama ange kuta watu wengine pale ndani, “weye unaingiaje humu ndani namna hiyo hebu toka nje weweee” aling’aka mzee Mahadhi huku akimdaka yule mwanamke mtu mzima na kuanza kumsukumia nje……… ENDELEA……..
Maana tayari Mahadhi alisha hisi kuwa yule mwanamke alikuwa na tatizo na kijana wake Idd,na alipo jaribu kumsukumia nje mwanamke alikuwa mbishi kutii amri hiyo, “hapana mzee wangu huyu kaka lazima leo anilipe, yaani yote aliyo nifanyia halafu asinilipe hata shilingi, na aishie kunivunjia meno yangu” alilalamika yule mwanamke mtu mzima, huku wajumbe wote wakishangaa wasijuwe nini kinatokea, lakini kwa muonekano wa mwanamke yule wa uchovu wa mwili na sura kila mmoja akavutika kumsikiliza kujuwa alikuwa na nini na huyu kijana Idd, “hapana Mahadhi, hebu muache huyo mama aje atuleze shida yake” alisema mwenyekiti, huku yeye na wezake wakimtazama yule mwanamke kwa mshangao, “baba mtimue, ametumwa huyu Malaya, mfukuzeni humu ndani” alipaza sauti Idd, akishindwa kujizuiwa kutamka lugha chafu ndani ya baraza la wazee, “kijana chunga mdomo wako, upo kwenye baraza la wazee” alikemea mmoja wa wajumbe.
Mahadhi aliona kila dalili ya kijana wake kudhalilika, maana zile mbio alizokimbia kule nje ni wazi alikuwa anamkimbia mschana huyu, ikionyesha kuwa alikuwa na kisa nae, hakujuwa atamuokoaje kijana wake ambae alikuwa anazijuwa vyema tabia zake za ulevi na uzinzi, japo hakumuwekea wazo la kuwa atakuwa amefanya zinaa na mwanamke huyu mkongwe, “mama vua viatu vyako hapo mlangoni kisha njoo ueleze unatatizo gani” alisema mwenyekiti, na hapo mschana yule ambae sio mwingine ila ni Sinamengi, alifanya kama aliyo elekzwa na kisha kuingia ndani na kuonyeshwa upande wa kukaa, Mahdhi nae akarudi tena barazani na kukaa, “lakini mwenyekiti tutawezaje kumruhusu mwanamke kama huyu kuingia humu barazani, isitoshe umesha ambiwa kuwa ni mwanamke mwenda ovyo” alisema Mahadhi, ambae aliona wazi mambo yana haribika mbele ya baraza, “kama ni wa hovyo aliwezaje kufahamiana na Kijana wako” alisema mwenyekiti huku wengine wakiunga mkono kasoro wachache ambao toka mwanzo walionekana kumkandamiza bwana Mahamud, walianza kujiona wajinga na kuanza kuyakumbuka maneno ya Mahamud kuwa “bwana Mahadhi nadhani unashindwa kuelewa kuwa huyu kijana wako ni mtu wa aina gani, au pengine unafahamu lakini una wapumbaza wajumbe wa baraza ili wakuunge mkono kwa kile unacho kifanya, nadhani hata wao wange mfahamu wasinge jiuliza ile messeji imetokea wapi” hapo mmoja wao akaingilia kati, “lakini mwenyekiti inawezekana swala lao likawa ni swala binafsi la bwana Idd na huyu mama, kwanini wasiende kuliongea wenyewe faragha na sio hapa hadharani” alishauri mjumbe huyo kwa sauti ya kuhamaki, “mzee wangu naomba hili swala tuliongee mbele yenu, Kwa sababu najuwa hawezi kunisikiliz hata nyie wenyewe mumeona alivyo nikimbia”, alisema mwana mama Sina mengi kwa sauti ya kuombeleza, “sawa hata mimi naona kuwa maadamu swala hili limeingia humu ndani wacha tulimalize humu humu, inaonekana Idd ameshindwa kumalizana nae huko nje” alisema mwenyekiti, ambae alishaanza kuona dalili mbaya toka kwa Idd, ni kutokana na lugha chafu aliyoitumia kwa mwanamke yule bila kuangalia kama yupo na wazee wenye heshima zao.
Hapo idadi ya watu wengi ikaunga mkono uamuzi wa mwenyekiti, japo Mahadhi na wenzake hawa kuonyesha kuridhika na maamuzi yale na ndipo Idd alipoona kuwa anaenda kuumbuka live live, na pengine mchezo mchafu aliotaka kuufanya kwa Soraya ungethibitishwa mbele yake, hapo akainuka ghafla,“jamani kama munamsikiliza huyu changu mimi natoka nje” alisema Idd huku ana anza kutembea kuufuata mlango, “hivi huyu ndie kijana ambae tunahitaji amchumbie binti wa Mahamud, mbona nidhamu yake ni sawa na wala madawa ya kulevya wa huko mtaani, anafanya nini sasa, hebu kaa hapa” alisema mmoja wa wajumbe kwa sauti iliyojaa hasira, lakini Idd hakusimama wala kugeuka akaendelea kutoka nje, “hebu mzuieni asitoke” alisema mwenyekiti, na hapo ndipo Idd aliposimama na kuwageukia wale wazee ambao walikuwa wanamtazama kwa mshangao, “nani anizuie? kama mumeshindwa kuongea na huyu mwarabu koko nimuoe binti yake sasa munataka nini kwangu, kaeni na huyo changudoa muongee nae” alisema Idd, kwa sauti ya kibabe, kisha akaelekea nje, “sasa naanza kuamini kuwa huyu kijana ni muovu, hata ule ujumbe mchafu aliuandika yeye mwenyewe” alisema mwenyekiti na wajumbe wengine wakamuunga mkono kasoro mzee Mhadhi na wenzake wachache ambao walikuwa wanahisi kufedheheka mioyoni mwao, maana kabla hata hawajatoka mule ndani tayari maneno ya Mahamud yalishaanza kutimia kwa muonekano wa matendo ya Idd.****
Talib alifika kule mwembechai moja kwa moja nyumbani kwa Zido na kuwakuta wakina Vitusi Zido na wale wengine wanne, ambao hali zao zilikuwa zimesha tengemaa kasoro yule alievunjika mkono, “oyaaa! yule fala anazidi kunipanda kichwani” alisema Talib, huku anasogelea Vitus na kumpokea kipisi cha bangi, “duh! fala yupi tena?” aliuliza Zido, huku ana chakua majani ya bangi mengine na kuanza kuyasokota kwenye karatasi lake maalumu, “ni yule boya Higgno, et ndie mtu anaemgonga Soraya” alisema Talib kama vile anasimulia kituko cha ajabu sana, huku wakina Zido wakiangua kicheko cha mwaka, “kumbe yule boya ni shemeji yako?” aliuliza Vitus, huku wakiendelea kucheka kwa sauti kubwa, hapo Talib akawasimulia jinsi alivyo gundua jambo hilo na yeye kuongea uongo kwa shangazi yake, “dah! dogo anazali kweli, lakini kwa ubabe alio uonyesha mbele ya Soraya lazima demu aingie mtego” alisema mmoja kati ya wale vijana wanne, “lakini tayari nimeshampa kesi, nimepakaza kuwa yeye ndie aliepanga mchongo wote” alisema Talib na kuwaeleza wenzake jinsi ilivyo ongea na shangazi yake, “sema kama alianza kunishtukia hivi, ila hakuna ubaya, kinachotakiwa ni sisi kumaliza mchezo, wao wakimkamata mpaka sijui wagundue kuwa sio yeye tayari sisi tumesha fika mbali na mambo yetu” alisema Talib akiendelea kuvuta bangi, “mh! talib una uhakika na unacho kisema, maana michongo miwili yote imefeli” alisema Vitus, akionyesha mashaka juu ya swala hilo, “nyie musiwe na wasi wasi, cha msingi pale mukivuka muna mfunga kamba mlinzi, kisha nawapa funguo munazama ndani munakomba mkwanja kisha munatoka zenu, wao mpaka washtuke ni kesho asubuhi” alisema Talib kwa sauti ya dharau, sauti ambayo kwa vyovyote vile ungejuwa kuwa alikuwa na uhakika wa kufanikiwa mpango ule, “basi poa, sasa mchongo lini?” aliuliza Zido akionyesha kukubali mpango ule, “kesho usiku, inabidi tufanye faster kabla hawaja muuliza yule boya” alisema Talib, hapo wakina Vitus wakatazamana, kisha wakamtazama Talib huku wana kubali kwa kichwa.********
Wakina Soraya wakiwa ndani ya gari waliweza kumuona Idd anatoka kwenye ukumbi wa baraza akiwa mbio mbio na kuelekea ndani ya gari la baba yake na kutulia ndani yake bila kuondoka, “huyu atakuwa amekimbia au wamemtoa ili waongee na yule mwanamke?” aliuliza Laylah, “sijui hebu kwanza tuendelee kutazama” alisema Soraya, huku wote wakiwa wanatazama kule mbele yao.
Ukweli licha ya kuwa alikuwa anatazama kule msikitini ambako Sinamengi alikuwa ameshaenda, lakini Soraya bado mawazo yake yalikuwa kwa Higgno, “Higgno amesema kuwa na yeye ametafuta mshenga” alisema Soraya, “lakini Soraya, huyo mwanaume atawezaje kutafuta mshenga wakati sehemu ya kukaa haieleweki?” aliuliza Laylah, “mimi ndie niliemueleza kuwa inabidi tufuate utaratibu wa kunichumbia, sidhani kama swala sehemu ya kuishi itakuwa ni tatizo kwetu” alisema Soraya, huku wakiendelea kutazama kule msikitini, “una maanisha unataka kumfanyia kila kitu Higgno?” aliuliza Laylah, akionyesha mshangao kwa mwanamke kuandaa maisha ya ndoa yeye na mwanaume wake, “hapana sitofanya kila kitu peke yangu ila tutasaidiana” alisema Soraya macho yake sasa yalikuwa kwenye gari alilo ingia Idd, “lakini huoni kwamba yeye atakupendea mali na sio mapenzi ya kweli?” aliuliza Laylah, akionyesha mashaka juu ya uamuzi wa Soraya, swali ambalo Soraya nadhani hakulipenda, “nipo tayari kumfanya chochote ili Higgno azidi kunipenda, halafu Higgno sio mwenye tamaa, kama angekuwa na tamaa basi angekuwa amesha mzonga zonga baba toka zamani, si unajuwa kuwa anamfahamu?” aliuliza Soraya akiendelea kutazama kule kwenye gari, “lakini kweli yule kaka anaonekana mwenye mapenzi ya kweli” alisema Laylah.*******
Ukweli mama Soraya kutwa nzima ya siku ile alikuwa ametulia nyumbani kwake akiwaza na kutafakari juu ya kile alichoambiwa na mtoto wa kaka yake yaani Talib kwamba yule kijana mpole ndie aliepanga utekaji wa Soraya, na kisha kwenda kumuokoa, “kwa lengo gani haswa?” alijiuliza mama Soraya, “lakini huyu huyu ndie alie muokoa Soraya siku chache zilizopita toka kwa Idd, na kama angekuwa na nia ya kumteka si angemteka siku ile ambayo alikuwa amelewa” aliendelea kuwaza mama Soraya, ambae kwa upande mwingine aliona kuwa maneno ya Talib yalikuwa na ukweli ndani yake, Kwa sababu ni kweli Soraya alikuwa anamfadhiri baba wa kijana huyo kujenga duka lake ambalo lilikuwa limeunguwa moto, “na kama hivyo basi wawili hawa wanafahamiana muda mrefu, na vipi kuhusu Talib ameyajuwaje yote hayo, na Soraya ndiyo kusema tayari amesha fanya mapenzi na yule kijana?” aliwaza mama Soraya ambae alikuwa anatamani sana kumueleza mume wake juu ya hilo lakini alikuwa ameshaishiwa salio.*******
Baada ya kuhakikisha ukumbi umetulia mwenyekiti alimruhusu mwana mama yule aanze kuongea, “haya mama unaweza kujitambulisha na kutuleza una shida gani na Idd, maana sisi ndie wazee wake na tunaweza kukusaidia” alisema Mwenyekiti akimtazama Sinamengi, kwa maana ya kumpa nafasi ya kueleza shinda yake, ili wamsikie na kumsaidia, “mimi naitwa Sina mengi, ni mfanyakazi wa kuchile bar” kusikia hivyo tu! tayari watu wote mule ndani wakajuwa binti huyu anataka kuongea nini, “jamani kama ni muhudumu wa bar mimi sipo tayari kusikiliza upuuzi wake, wacha niondoke” alisema Mahadhi huku anainuka , “bwana Mahadhi naomba labda nikuambie kitu, endapo utatoka ndani ya baraza hili basi kuanzia leo hauto ruhusiwa kuswali kwenye msikiti wowote” alisema Mwenyekiti na hapo Mahadhi akakaa chini na Sina mengi akaendelea kueleza, “siku ya alkhamis saa nne asubuhi nikiwa kazini alikuja yule kijana alietoka nje na kunikabidhi juice kweny chupa, akinieleza kuwa ameweka dawa za kulevya na kwamba atakuja na mschana ambae ataagiza juice na mimi nimletee hiyo, akiwa na lengo la kumuingilia kimwili mara baada ya kulewa, pia aliniomba nimchukulie chumba kwenye hoteli ile ile ya kuchile, chumba ambacho tungemuingiza yule mschana baada ya kulewa ili yeye akamuingilie kimwili, akiahidi kunilipa fedha mara baada ya kumaliza kazi hiyo” alieleza Sinamengi, huku wote wakimsikiliza kwa umakini, na bila kubakisha neno Sinamengi akasimulia kila kitu kilichotokea jioni ya siku ile, kwamba yule mschana mrembo wa kiarabu alifanikiwa kukimbia, “na yule kijana kuamua kulala na mimi” alisimulia mwana mama Sina mengi, na kueleza mchezo mchafu uliofanyika usiku ule, Idd akimwingilia kwa njia ya kinyume na maumbile, “na mbaya zaidi Asubuhi akavunja meno yangu ya bandia na kuondoka bila hata kunipa shilingi moja, mimi ninacho omba ni hela ya kwenda kununulia meno mengine” alimaliza kusema Sinamengi na kumuacha kila mmoja akisisimkwa na simulizi ile, “huu ni mpango mwingine wa kumchafua Idd, hakika huyu mwanamke nampeleka polisi” alisema Mahadhi kwa sauti ya Jazba, “nipo tayari hata kuongea polisi, lakini kumbuka yule mschana pia anafahamu kuwa aliwekewa dawa kwenye Juice, na yeye atathibitisha” alisema Sinamengi kwa sauti ya kujiamini, “Mahadhi niwazi kabisa unafahamu kila anachofinya kijana wako Idd na bila shaka unaweza ukawa una ushirikiana na kijana wako kujaribu kufanya uovu huu na kumchafua bwana Mahamud ili upate fulsa ya kumchumbia binti yake” alisema Mwenyekiti, “tena hawana nia nzuri katika swala la kumchumbia Soraya binti Mahamud, nadhani ni tamaa za utajiri ndizo zilizo walazimisha kufanya hivyo” alisema mwingine na Mahadhi uzalendo ukamsinda, “hapo sasa munanikosea adabu, nitashirikiana nae vipi katika swala kama hilo, na vipi kama huyu mwanamke ametumwa kuja kuchafua” alisema Mahadhi kwa jazba, “inawezekana ametumwa kuja kuchafua kwa kueleza kila kitu, lakini bado swala linabakia pale pale Mahadhi, kuwa kijana wako alikuwa na mpango mbaya na binti yangu, kwa kweli kabisa ninajuta sana kukuweka karibu na mimi” alisema Mahamud kwa sauti ya msisitizo, ilyoonyesha kuchukizwa, “basi yaishe bwana Mahamud, umefanikisha nitamuambia Idd aachacne na Soraya” alisema Mahadhi huku anasimama na kutaka kutoka nje, “Mahadhi kuhusu Idd kuachana na Soraya hilo nilisha lipanga toka siku nilipogundua maisha ya Idd alipokuwa nje ya nchi, tunachokifanya hapa ni kuhakikisha watu wanafahamu tabia halisi ya kijana wako na wewe unalipia gharama za meno za huyu mama, na pia nakusanya ushahidi ili nikufikishe mahakamani kwa kosa la kuandika ujumbe wa kunichafua” alisema Mahamud, kisha akasimama na kusogea mbele kwa mwenyekiti, “samahani naomba niwahi nikaswali halafu nikafanye makusanyo, maana ni alaasiri sasa, alisema Mahamud na wote wakashtuka na kutazama saa zao, “kweli saa tisa, lakini kabla hatujaondoka ni muhimu kufahamu kiasi cha fedha anachotakiwa kukipata huyu mwanamke, pia bwana Mahamud tutahitaji kukutana tena na kulizungumzia swala hili vizuri, maana haipendezi kuona sisi wenyewe tuna pelekana polisi kwa mambo kama haya” alisema mwenyekiti na mzee Mahamud akakubali swala la kukutana, pia Mahadhi akatakiwa kutoa kiasi cha fedha elfu ishirini kwaajili ya Sinamengi.
Hakika wapo walio mpongeza bwana Mahamud kwa jinsi alivyoweza kujiondoa kwenye ile kashfa na tuhuma kubwa ya ajabu, pia wapo walio shindwa hata kumtazama usoni kutokana na kushadadia kitu ambacho hawakujuwa kuna nini nyuma ya panzia.*******
Naam Soraya na Laylah wakiwa bado wametulia pale pale ndani ya gari wanatazama kule msikitini, mara wakamuona Sinamengi akitoka kwenye ukumbi wa baraza la wazee na kuanza kuja upande wao, “huyoooo! anatoka, msubiri kwanza apite halafu tutamfuata nyuma” alishauri Soraya huku wakimtazama Sinamengi aliekuwa anakuja kwa mwendo wa haraka haraka na uso wake ukionyesha dalili ya furaha huku nyuma yake wakianza kuonekana wazee wakitoka kwenye ukumbi na kuelekea kwenye bomba la maji kuchukuwa udhu maana tayari adhana ilianza kusikika, “mh! muda umeenda eeh! saa tisa hii” alisema Laylah, huku anatazama saa yake ya kwenye simu na wakati huo tayari Sinamengi alikuwa anakatiza pembeni ya gari lao, huku mawazo yake yakiwa huko anakoelekea.
Baada ya Sinamengi kupita na kupotelea mbele kidogo na wao wakawasha gari na kumfuata nyuma mpaka walipomfikia, wakamchukuwa kwenye gari na kuelekea nae NPF kwenye hospital ya meno, huku njiani Sinamengi akiwasimulia kila kitu jinsi kilivyo kuwa kuanzia Idd alipomuona na kukimbilia ndani, na kule ndani jinsi mambo yalivyo kuwa mpaka maamuzi na msimamo wa Mahamud.
Baada ya kumfikisha Hospital na kumuacha Sinamengi, wakina Soraya wakaelekea nyumbani ambako walimkuta mama Soraya akiwa anatoka kuswali, “assalam alaykum” alisalimia Soraya, mara baada ya kuingia ndani akiwa amemuacha Laylah nje ana egesha gari vizuri, “waalaykum salaam naona unatembea vizuri sasa?” aliuliza mama Soraya, huku akimtazama mwanae kwa jicho la shaka, “ndio mama nimeshapewa dawa” alisema Soraya kwa sauti ya wasi wasi, huku akijichekesha chekesha, “ulimueleza nini doctor mpaka akakupa dawa na umepewa dawa gani kwa kitu kama hicho? kwani umeambiwa huo ni ugonjwa?” aliuliza mama Soraya huku akiachia tabasamu la kusanifu, Soraya akatazama chini kwa aibu, “anaitwa Higgno, ni mtoto wa mzee alieunguliwa na duka sio?” aliuliza tena mama Soraya, hapo Soraya akainua uso wake kumtazama mama yake kwa mshangao……….. ITAENDELEA


TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA SITINI NA TISA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA SITINI NA NANE: waalaykum salaam naona unatembea vizuri sasa?” aliuliza mama Soraya, huku akimtazama mwanae kwa jicho la shaka, “ndio mama nimeshapewa dawa” alisema Soraya kwa sauti ya wasi wasi, huku akijichekesha chekesha, “ulimueleza nini doctor mpaka akakupa dawa na umepewa dawa gani kwa kitu kama hicho? kwani umeambiwa huo ni ugonjwa?” aliuliza mama Soraya huku akiachia tabasamu la kusanifu, Soraya akatazama chini kwa aibu, “anaitwa Higgno, ni mtoto wa mzee alieunguliwa na duka sio?” aliuliza tena mama Soraya, hapo Soraya akainua uso wake kumtazama mama yake kwa mshangao………..SONGA NAYO ……..
Kitu ambacho mama yake akajuwa ni kweli alicho ambiwa na Talib, “mama kwahiyo unanifuatilia?” aliuliza Soraya ambae ni kweli mpaka dakika hiyo alikuwa amemdanganya mama yake kuwa ameumia goti lakini ni kwamba yalikuwa ni maumivu ya kitumbuani kutokana na kupewa dudu kwa mara ya kwanza, “kwahiyo ni kweli unae msaidia ni baba yake Higgno sio?” aliuliza mama Soraya akionekana kuwa makini sana bila dalili ya utani au mchezo, mara nyingi huwa hivi wakati anapokuwa na jambo lililomkera, “hapana mama, sio baba yake Higgno, ila pia wazazi wa Higgno wanakaa…” alisema Soraya kwa mshangao, kabla hajasita kidogo na kukumbuka jambo fulani, ni kwamba licha ya Higgno kumueleza kuwa wazazi wake wanaishi Luhila pia mzee Frank alimueleza kuwa anakijana wake na hata siku ya jana asubuhi alikutana na mzee Frank kule chem chem alimueleza kuwa anaenda kumpa taarifa kijana wake, na hata leo Higgno amekuja mjini na amesema yupo na baba yake na wana toka mjini na alikuwa kwenye gari ambalo lilionekana kuwa ni gari la wazi, kwahiyo inawezekana kuwa ni kweli Higgno ni mtoto wa mzee Frank, “mh! inawezekana mama, lakini mimi nilikuwa sijui, nadhani hata Higgno hajui kuwa namfahamu baba yake” alisema Soraya kwa sauti ya mashaka akionyesha bado anajiuliza mama yake amelijuwaje jina la Higgno, wakati miaka yote hii walikuwa wanahangaika kumtafuta kijana huyu bila mafanikio, “inawezekana vipi, kwahiyo hujawahi kukutana na Higgno nyumbani kwa wazazi wake?” aliuliza mama Soraya, akionyesha wazi kuwa anahisi Soraya anadanganya, maana alishaanza kuamini maneno ya Talib kuwa mchezo huu ulipangwa na kuratibiwa na Higgno ambae alijifanya anatoa msaada kumbe anahitaji kumnasa Soraya, kisha kujichumia utajiri, “mama kama nilivyo kuambia, yule mzee tulimsababishia ajali siku ile nilipokuwa na Idd, na kuhusu Higgno nadhani hakuna asiejuwa, kwani kuna tatizo gani juu ya Higgno?” aliuliza Soraya kwa sauti ya kuhamaki, ni baada ya kuona kuna dalili za kumshuku vibaya Higgno, ambae yeye ana uhakika wa asilimia nyingi kabisa kuwa Higgno ni mvulana pekee mwenye mapenzi juu yake, ukiachilia kuwa kijana mwema na mpole kupata kumuona, “kwa taarifa yako huyo mwanaume sio mtu mzuri, na anashirikiana na baba yake kujifanya ni watu wema kwako ili wapate wanacho hitaji” alisema mama kwa sauti iliyojaa jazba na hasira, “we mama muogope mungu na maandiko yake, kijana wa watu hata hanijuwi nakaa wapi, ni mtoto wa nani, leo hii aanze kupanga mipango hiyo, tena kwa miaka yote hiyo, mbona basi angeweza kunipata toka ni kiwa form two au angekubali kuongozana na wewe siku ile nilivyoleweshwa madawa” alisema Soraya kwa sauti iliyojaa busara na mshangao kwa mama yake, “unajuwa pengine alipanga na Idd kufanya hivyo” alisema mama Soraya kwa sauti ya jazba, “kwahiyo baba anahusika katika mpango huo, maana yeye ndie alieniambia kuwa nimsindikize Idd kule bomba mbili?” aliuliza Soraya kwa jazba pia, si unajuwa mtu akishapenda, “baba yako alidanganywa tu ule mpango ni wa Idd na baba yake” alisema mama Soraya kwa sauti ya jazba na Hasira pia, “lakini yule mwanamke alie tuhudumia amesema kuwa ulikuwa ni mpango wa idd ili aniingilie kimwili na nilimwambia aende akaseme barazani kwenye kikao, sasa Higgno anahusika vipi?” aliuliza Soraya, hapo mama Soraya akatulia kidogo kabla ya kuongea kwa upole, “lakini Soraya, hukupaswa kukufanya nae chochote mpaka tumchunguze kwanza” alisema mama Soraya kwa sauti ya upole, hapo Soraya alijuwa mama yake anamaanisha nini, akatazama chini kwa aibu, “lakini mama sikujuwa kama tutafanya hivi, mimi nilikuwa namjaribu kama anaweza kuzalisha” alisema Soraya kwa sauti ya upole, “mama yangu Nanyoni, nani alikuambia mwanaume anajaribiwa? na kwanini uliamua kumjaribu?” aliuliza mama Soraya kwa sauti ya chini yenye mshtuko na mshangao, huku akikaribia kucheka kwa upuuzi wa binti yake, “niliona mtu mwenyewe haonyeshi dalili za…” alisita Soraya alieongea kwa sauti ya uoga, huku bado akitazama chini, “dalili kama zipi Soraya?” aliuliza mama Soraya kwa sauti ya chini, bado ikiwa na mshangao, “za kuwa na uwezo, kwasababu hakuwahi kuwa na mwanamke, pia hata nilipolala nae siku ya kwanza alikuwa anaogopa kunigusa” alisema Soraya kwa sauti ya uoga kama mwanzo iliyojaa aibu, “mh! sasa umeuona urijali wake, haya subiri uthibitisho wa mimba” alisema mama Soraya huku anataka kuondoka, “lakini mama jujaniambia umejuwaje, kuhusu higgno na kwamba yule mzee ni baba yake, kwasababu nilimuomba awe mshenga wa Higgno?” aliuliza Soraya huku anamtazama mama yake ambae alisimama na kutulia kidogo kama anawaza amtaje au asimtaje.******
Hakuna siku Mzee Mahadhi alijona kuwa na bahati mbaya kama siku hii ya leo, hata alipokuwa anaswali alaasiri alikuwa akifanya vile vitendo, vya takbira kufunga swala kurukuu na kusujudu, ni sababu aliwaona wenzake wakifanya hivyo, lakini kiukweli mawazo yake haya kuwepo kabisa mahali pale, alikuwa anawaza fedheha aliyoipata, maana hata mambo ambayo hakutegemea kuwa yange fahamika yamefahamika, “sijui amejuwaje huyu mshenzi kuwa Idd alikuwa hivyo huko msumbiji?” hilo ni moja ya swali ambalo lilimsumbua , na swali la pili lilikuwa ni vipi ataongea na bwana Mahamud kumuomba msamaha juu ya yale yaliyotokea, “nitamwambia kuwa sihusiki na jambo hilo, ni kwamba Idd ameniingiza kwenye mkenge” aliwaza Mahdhi akiwa katika swala.
Naam sio kwamba alimaliza kuswali ni kwamba alitoka nje baada ya kuwaona wenzake wanamaliza na kutoka nje, na alipofika nje aliweza kuwaona wenzake wakimfuata Mahamud na kumuomba radhi kwa kile walichokifanya ndani ya ukumbi wa baraza la wazee na kumpa pole kwa kashfa aliyozushiwa, “kwa niaba ya wazee wote tuliopo hapa na tulioshiriki kikao hiki, nikutake radhi bwana Mahamud kwa hii dhahama, lakini imekuwa vyema tumelizungumza na kubaini ukweli, maana tungebaki na viulizo huku kashfa inasambaa, nadhani kwenye swala ya ijumaa nitalizungumaza swala hili na kuliweka sawa” alisema mwenyekiti, ambae ni kama aliongea baada ya wenzake waliokuwa pembeni wanasikiliza majibu ya Mahamud juu ya msamaha wao, toka kwa Mahamud ambae alikuwa pembeni ya gari lake, “hakuna tatizo mwenyekiti, ila nitahakikisha nampata mtu aliefanya hivi, na nitampeleka mahakamani ushahidi wa sms ninao” alisema Mahamud ambae alikuwa ameonyesha kukasirishwa na jambo hilo japo alishukuru kufanikiwa kuwaelewesha wajumbe wa baraza, huku akimshukuru Sinamengi kwa ujio wake pale msikitini, japo hakuelewa ilikuwaje mpaka akafika pale msikitini, alitamani kumuona tena ili ampe zawadi, “nashukuru sana bwana Mahamud kwa kuelewa jambo hili na kutusamehe kwa ujumla wetu, maana kila mmoja alikuwa ana hasira za wazi kabisa juu yako, akiamini kuwa ule ujumbe ni wa kweli, pia tunaomba utualike kwenye harusi ya mwanao, na kwa heshima ndoa ifungwe kwenye msikito huu” alisema mwenyekiti wote wakacheka kwa furaha, “siwezi kuacha kuwa karibisha kwenye siku hiyo muhimu na yakipekee kwenye familia yangu” alisema bwana Mahamud akionyesha kuondokewa na hasira yote kisha wakaagana na kila mmoja akaelekea kwenye gari lake, na wasio na magari ambao idadi yao ilikuwa kubwa wakaondoka zao kwa miguu huku kila mmoja akikiri kuwa Idd sio kijana mwema, hata wao waliapia kuwa wasinge weza kukubali binti zao au wajirani zao au wandugu zao wachumbiwe na Idd.
Mahadhi ambae muda wote alikuwa mbali anawatazama wenzake, sio kwamba hakutaka kwenda kuungana na wenzake kuomba msamaha, ila yeye hakujuwa ataanzaje kujieleza mbele ya Mahamud kwa kile alicho kifanya, yeye alichokifanya ni kumvizia mwenyekiti mara tu baada ya kumaliza kumuomba msamaha bwana Mahamud, na alipomuona mwenyekiti ana chanja mbuga kuelekea mtaa wa shule ya mfaranyaki akamkimbilia haraka, hakujuwa kama kijana wake Idd alikuwa amejibanza ndani ya gari akiwatazama wazee waliokuwa wanatawanyika kuelekea makwao.
“Kumradhi mwenyekiti, ninahitaji muda wako kidogo” alisema mzee Mahadhi, kwa sauti ya kinyonge, mara tu baada ya kumfikia mwenyekiti, “bwana Mahadhi kabla hujaongea naweza kujuwa nini unataka kuongea, lakini kiukweli huwezi kusema ulikuwa hujuwi hila za mwanao Idd, kiukweli umetumaanisha vibaya sana, na nina kuambia ukweli bwana Mahadhi kama hauto mfuata mapema Mahamud na kumuomba msamaha basi utaozea jela, na hakuna atake kusikitikia, maana umefanya vibaya sana, kuhusu kijana wako hilo hata mimi sijui” alisema mwenyekiti akionyesha kuwa amechukizwa kweli kweli, “mwenyekiti, ukweli shetani alinipitia, nakuomba tafadhari nisaidie juu ya hili, siwezi kurudia tena ujinga kama huu” alisema Mahadhi kwa sauti ya kuomboleza, kitu ambacho mwenyekiti hakukijuwa ni kwamba, sio kuwa Mahadhi alikuwa anajutia alicho kifanya ila alikuwa anaogopa kupelekwa mahakamani.
Hapo mwenyekiti akatulia kidogo kama anawaza atoe jibu gani, kisha akamtazama bwana Mahadhi, “sawa bwana Mahadhi nadhani tutahitaji muda wa kukaa na kuona namna ya kwenda kwa Mahamud” alisema mwenyekiti na kisha wakaagana na kila mmoja akaelekea upande wake, wakati mwenyekiti akiendelea na safari yake huku Mahadhi akirudi kule msikitini ambako aliliacha gari lake.
Mahadhi alishtuka sana baada ya kumkuta Idd ndani ya gari, lakini aliingia ndani ya gari na kuondoa gari na safari ikiwa ni ya kimya kimya, hakuna hata mmoja aliemsemesha mwenzake mpaka walipofika nyumbani na kuingia ndani, “hivi we mpuuzi uliwezaje kulala na bibi kama yule?” aliuliza Mahadhi kwa hasira huku akimtazama Idd aliekuwa anachukuwa chupa ya pombe kali na kumimina kwenye glass, kisha bila kumjibu baba yake akajimiminia ile glass kwa mkupuo mmoja akiimeza ile pombe kwa kukunja sura na kuiweka glass tupu mezani, “baba hayo maswali sio mahala pake, huu wakati inabidi tukomalie mpango wetu” alisema Idd huku anachukuwa sigara yake na kuiwasha, “baradhuri mkubwa, yaani hiyo mipango yako nuksi bado unaiwazia?” aliongea Mahadhi kwa sauti iliyojaa hasira, huku anaelekea chumbani kwake, “bwana hee kama wewe umegwaya mimi nitakomaa mwenyewe” alisema Idd, huku anamimina pombe kwenye glass, “utakomaa nayo ukiwa jela” alisema Mahadhi huku anaingia chumbani kwake.*******
Naam kule nyumbani kwa Mahamud, mama Soraya baada ya kujiuliza akaona hakuwa na budi kumtaja mbea wake, “ameniambia Talib, ni baada ya kusikia maongezi yetu asubuhi” alisema mama Soraya kisha akataka kuondoka, “mh! unamsikiliza huyo mvuta bangi?” aliuliza Soraya kwa sauti ya mshangao, hapo mama Soraya akasimama na kugeuka kumtazama mwanae, sura ameikunja kwa hasira, “we! Soraya, acha kumuita mwenzio mvuta bangi, na tunapaswa kuheshimu na kuyathamini mabadiliko yake, kama bangi alishaacha siku nyingi” alisema mama Soraya kwa sauti ya ukali yenye kuonya, “mama unajidanganya, kwa taarifa yako nimemuona kwa macho yangu anavuta bangi ndani mwake huku amewasha udi ili harufu isitoke nje” alisema Soraya kisha akatoka na kuelekea chumbani kwake..... ITAENDELEA MUWE NA USIKU MWEMA
 
"Mama yangu Nanyoni"
Nimecheka hadi basi, ina ladha halisi ya Lugha ya Wangoni:
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA SABINI
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA SITINI NA TISA: Talib, ni baada ya kusikia maongezi yetu asubuhi” alisema mama Soraya kisha akataka kuondoka, “mh! unamsikiliza huyo mvuta bangi?” aliuliza Soraya kwa sauti ya mshangao, hapo mama Soraya akasimama na kugeuka kumtazama mwanae, sura ameikunja kwa hasira, “we! Soraya, acha kumuita mwenzio mvuta bangi, na tunapaswa kuheshimu na kuyathamini mabadiliko yake, kama bangi alishaacha siku nyingi” alisema mama Soraya kwa sauti ya ukali yenye kuonya, “mama unajidanganya, kwa taarifa yako nimemuona kwa macho yangu anavuta bangi ndani mwake huku amewasha udi ili harufu isitoke nje” alisema Soraya kisha akatoka na kuelekea chumbani kwake. ENDELEA NAYO……..
Akimuacha mama yake akiwa mdomo wazi kwa mshangao, “Talib bado anavuta bangi?” aliwaza mama Soraya akiwa haamini masikio yake, na wakati huo akatazama dirishani kutazama nyumba ndogo anayo ishi Talib na hapo macho yake yakakutana na Talib aliekuwa anatokea upande wa getini na kuelekea kwenye nyumba hiyo, mkononi akiwa amebeba kijimfuko cha rambo alicho kiviliga kiasi cha kujaa kwenye kiganja cha mkono wake, mama Soraya alimkazia Talib macho ya mshangao, sio kwaajili ya kile alicho kiviliga mkononi, ila alivutiwa na mwendo wa mtoto wa kaka yake huyu, ambao ulikuwa ni waharaka uliojaa tahadhari nyingi, maana alikuwa akitembea huku mara kwa mara akitazama nyuma na pembeni kama vile alikuwa anahakikisha kuwa hakuna aliemuona, na alipoufikia mlango aliufungua haraka na kuingia ndani kisha akafunga mlango, “mh! kwanini yupo hivi huyu?” alijiuliza mama Soraya, huku akiwa ameganda Dirishani, “au alichosema Soraya ni cha kweli?” alijiuliza tena mama Soraya huku akiendelea kutazama kule kule, “lakini hapana, huyu Soraya ameamua kumsema mwenzie vibaya kwa hasira tu! ni kwasababu amemsema kuhusu Higgno” alisema mama Soraya huku anatembea kuelekea chumbani kwake.*****
Naam habari za kulazwa kwa mzee Komba leo zilikuwa ni simulizi kwenye vilabu vya pombe, huku marafiki zake ndio wakiwa waongeaji wakuu wa swala lile, japo walimkimbia mwenzao katika ugonjwa na hata walipo muona mke wa bwana Komba akija kunywa ulanzi hawakushtuka zaidi walimkaribisha kwa mbwembwe na kumuuliza habari za mgonjwa, na yeye kuwaeleza bila kusita, wapo walioshangaa uwepo wake mahali pale, kwa kuwa alitakiwa awe anamhudumia mgonjwa, lakini wapo waliokaa nae na kuendelea kunywa nae pombe kama kawaida.*********
Mahamud baada ya kutoka msikitini, alianza kuzunguka kwenye ofisi zake huku njia mzima akiwaza juu ya mambo mawili, moja ni kuhusu kilichotokea msikitini, aliwaza jinsi watu walivyo mjengea hoja ya kuwa anatembea na binti yake huku wengine wakishupalia kabisa, japo walimuomba radhi baada ya kuthibitisha lakini kiukweli bado aliona amesha fedheheka kwa tuhuma zile ambazo alikuwa na uhakika kuwa alieziunda ni Mahadhi na kijana wake Idd, ambao wameumbuliwa na yule mwanamke ambae japo muokenano wake haukuwa mzuri, lakini amekuwa mkombozi wake, sasa je? ni nani aliemueleza kuwa kuna kikao pale msikitini kiasi cha yeye kuja mpaka pale, “ila wale washenzi lazima niwaonyeshe kuwa mimi sio wakunichezea” alijisemea Mahamud.
Pili, Mahamud alikuwa anawaza kuhusu kijana mpole mwene roho na tabia za kipekee, aliwaza matukio na toka siku ile kule Msamala alipo vamiwa na wanyang’anyi na yeye kumuokoa, pia aliwaza tukio la leo la kijana yule kuokota pochi yake iliyo sheheni fedha na kumkabidhi, lakini pia kilicho mshangaza zaidi ni kitendo cha kukataa kumchumbia binti yake akidai kuwa anamchumba tayari, “anawezaje kukataa nafasi ambayo wengi wanaitafuta bila mafanikio?” aliwaza Mahamud akiwa anaendelea kufanya makusanyo, “haina shida nitakuwa mshenga wake, na nitajitahidi kumsaidia afanikiwe katika maisha yake, nitampatia kazi na nitampatia fedha kidogo za kuanzia maisha” aliwaza Mahamud, ambae saa kumi na mbili za jioni alikuwa amesha maliza mizunguko yake na kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwake akiwa na habari mbili moja nzuri na moja mbaya, nzuri ikiwa habari ya kikao cha baraza la wazee kilivokuwa na yeye kufanikiwa kuweka sawa tuhuma alizopewa, na pia jinsi wakina Mahadhi walivyo umbuliwa na mwanamke alieshiriki kuweka dawa kwenye Juice ya Soraya, habari ambayo ni mbaya kwake ilikuwa ni ile ya kukutana na kijana aliemsaidia siku ile, yaani Higgno, kijana ambae alitegemea ange muozesha binti yake Soraya, lakini bahati mbaya kijana huyu tayari anamchumba japo yeye amejitolea kuwa mshenga, lakini kiukweli kwake na kwa familia yake zilikuwa ni habari mbaya sana *********
Baada ya kumaliza kumsaidia baba yake kushusha mizigo toka kwenye gari na kuweka ndani ya nyumba kubwa aliondoka kuelekea shambani mida ya saa kumi na mbili jioni, na kwa kuwa muda ulikuwa umeenda sana mzee Frank alimuazima mwanae baiskeri yake na kumtaka airudishe kesho mapema ili aje amsaidie kupanga vitu dukani, duka ambalo tayari lilikuwa limesha ezekwa kusakafiwa na kuwekwa lip kwenye kuta zake, hivyo waliamini mpaka kesho saa nne litakiwa limesha kamilika na kupachika mbao za flemu kwaajili ya kupangia bidhaa, “jitahidi umpigie mzee Mahamud hiyo kesho ili aweze kukupatia hiyo kazi, mana huwezi kuoa bila kazi” hayo ni maneno ya baba yake Higgno, kabla hajaondoka pale nyumbani.
Akiwa amefunga mfuko wake kwenye kitako cha baiskeri hii mpya, Higgno aliparaza pederi za baiskeri kueleka matogoro na kisha chem chem ili aingie msitu wa pembezoni mwa milima hii ya matogoro kuitafuta Mahilo mashambani, huku njia nzima akijikumbushia matukio mfululizo yanayo onyesha kuwa mwenye bahati, maana ukiachilia kunyanduana na mschana mrembo Soraya, ambae amempatia fedha na simu, pia Higgno alifurahi sana kwa kukutana na mzee Mahamud, ambae licha kuonyesha kumchukulia kama kijana muhimu kwake na kuuthamini msaada wake wa kumuokoa siku ile na hata leo alipomuokotea wallet yake, pia Higgno alifurahi sana kuahidiwa kazi na mzee Mahamud na kitendo chake cha kujitolea kuwa mshenga wake.
Baada ya kufika nyumbani kwake, Higgno aliweka baiskeri yake nje akiifunga kwa kufuri la waya na kuingia ndani ambako alibadili nguo zake na kuelekea mtoni ambako alienda kuchota maji kwa kurudia mara mbili, akibeba ndoo mbili mbili kwa kila safari moja, na alipoona amemaliza, akaongeza kuni kwenye moto wake, na alipohakikisha umekolea vizuri kwa kiwango alichohitaji akaanza mazoezi yake ya karate.*********
Soraya alitumia masaa matatu akiwa chumbani kwake ana waza hili na lile, na kikubwa ni kwamba alihisi wazazi wake hawakupenda aolewe na Higgno, maana toka mwanzo walionyesha dalili za kutokumuamini kijana huyu, “alianza baba na sasa mama, eti amemsikia Talib, sasa Talib ni mtu wa kumsikiliza” aliwaza Soraya, ambae aliendelea kuwaza na kuwazuwa, “hivi ni kweli yule mzee Frank ni baba yake Higgno?” Soraya alipo waza hilo alijikuta anachukuwa simu yake na kumpigia Higgno, simu ambayo iliita bila kupokelewa hata aliporudia mara kadhaa haikupokelewa pia, “hivi inawezekana kweli Higgno alipanga mpango wa mimi kutekwa?” alijiuliza Soraya, huku anaweka simu pembeni, “lakini kama ni rafiki zake aliwezaje kuwapiga kiukweli ukweli?” aliwaza Soraya, ambae aliendelea kujiuliza maswali mengi, likiwa na kwanini afanye vile, wakati mara ya mwisho mama yake alimuambia aende kwao na alikataa, “ina maana ananidanganya kuwa hajui kuwa mimi ni mtoto wa Mahamud, halafu Higgno alikuwa kule kule porini wakati wale watu nimekutana nao chem chem, na pia Higgno na baba yake hawana uwezo wa kuwa na gari wala pikipiki kama walivyo kuwa wale jamaa, sasa kwanini Talib ana sema hivyo na amejuwaje kuhusu hayo yote?” ukweli maswali yalikuwa ni mengi sana, “nikweli Talib anamfahamu Higgno, kwasababu Higgno alisimulia kuwa aliwahi kumchukulia mwanamke wake, na walisoma wote Luhuwiko, lakini ameyajuwaje haya yanayo nihusu mimi na amejuwaje kama wameunguliwa duka” alijiuliza Soraya lakini alikosa majibu.
Naam baada ya kuwaza kwa muda mrefu, ndipo akakumbuka jambo, “wale watekaji walikuwa wanawasiliana na mtu ambae alikuwa anawapa taarifa za nyumbani, tena aliwatumia messeji ya kuwa baba alikuwa anataka kuwaamba polisi, na wao wakampigia baba kumtishia” alijiwazia Soraya, ambae alijuwa kabisa ile simu ambayo waliitumia wale jamaa ilianguka chini, pale mmoja wao alipopigwa na kuanguka chini na sasa ipo kwa Higgno, hivyo lazima sms na majina ya watu waliokuwa wanawasiliana yatakuwepo kwenye simu ile, na wakati huo adhana ikasikika kwa mbali toka kwenye speeker za msikiti wa mkoa.
Soraya aliinuka na kuelekea bafuni kutia udhu, kisha akaelekea kwenye chumba cha ibada ambako alikutana na mama yake, ambae pia alikuwa anaingia kwenye chumba hicho sambamba na baadhi ya waschana wakazi pamoja na Laylah, ambae ni kama alimsusa nje, na kabla hawajaanza kuswali mara mzee Mahamud akaingia ndani ya chumba kile na kujiunga na familia yake kuanza kuswali swala ya magharibi na mpaka wana maliza Talib hakuonekana, “jamani nina habari njema za huko kwenye baraza” alianza kueleza mzee Mahamud, ambae alikuwa ameingia pale nyumbani muda mfupi kabla ya swala, na watu wengine walishaondoka na kuwabakia wanafamilia tu, yaani mzee Mahamud mwenyewe mke wake na binti yao Soraya, “tupe hizo habari njema na sisi tukupe za kwetu” alisema mama Soraya wakiwa wamekaa kwenye zuria la manyoya mule ndani ya chumba cha ibada, “Mahadhi na kijana wake wameumbuka vibaya sana” alisema Mahamud na kuanza kuwa simulia mwanzo mpaka mwisho wa kikao na jinsi yule mwanamke alivyoingia akifukuzana na Idd, “kwa kweli sijui alijuwaje kama Idd yupo pale” alisema Mahamud kwa sauti ya kufurahia, “ni mimi ndie niliemuelekeza aje pale alisema Soraya na kueleza jinsi alivyokutana na Sinamengi akimpa shariti la kwenda msikitini kudai fedha yake kwa Idd, vinginevyo angempeleka polisi, “ulifanya vizuri sana mwanangu, ila tuna bahati pia mbaya” alisema Mahamud, “ipi tena mume wangu?” aliuliza mama Soraya, huku Soraya akiwa ametoa macho kwa mshangao akiombea maongezi hayo yasiwe yanayo muhusu Higgno, “tutaongea baadae, nadhani Soraya halimuhusu, labda na nyie munipe habari yenu” alisema Mahamud, na hapo Soraya akashusha pumzi, “lakini aliombea hiyo habari ya mama yake isimuhusu Higgno, “mume wangu tayari Soraya amesha kutana na yule kijana Mpole, na yule mzee ambae Soraya anamsaidia ni baba wa kijana yule, japo Soraya anasema hajuwi” alisema mama Soraya na hapo mapigo ya moyo ya Soraya yakaanza kwenda kasi, “lakini habari ambaypo tumeipata kwa kweli kijana yule sio mtu mzuri” alisema mama Soraya kwa sauti ya upole ya kinyonge ya kuhuzunika, “kwanini sio mtu mzuri?” aliuliza Mahamud kwa mshangao, na hapo mama Soraya akamsimulia mume wake kuhusu, aliyoyasikia kwa Talib, “hebu subiri kidogo mama, jambo hilo hata mimi niliwahi kulitilia mashaka ndio maana nilipanga kumuuliza maswali ambayo akiweza kuyajibu nitampa zawadi yake na sitoingilia maamuzi yao na Soraya alisema Mahamud kwa sauti ya ung’amuzi, “ndiyo hivyo mume wangu ilipaswa kijana huyu, akamatwe na awataje wenzake wote” alisema mama Soraya kwa msisitizo, Soraya alionekana kutulia kimya kabisa, ameinamisha kichwa chini……….. ENDELEA


TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA SABINI NA MOJA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA SABINI, “kwanini sio mtu mzuri?” aliuliza Mahamud kwa mshangao, na hapo mama Soraya akamsimulia mume wake kuhusu, aliyoyasikia kwa Talib, “hebu subiri kidogo mama, jambo hilo hata mimi niliwahi kulitilia mashaka ndio maana nilipanga kumuuliza maswali ambayo akiweza kuyajibu nitampa zawadi yake na sitoingilia maamuzi yao na Soraya alisema Mahamud kwa sauti ya ung’amuzi, “ndiyo hivyo mume wangu ilipaswa kijana huyu, akamatwe na awataje wenzake wote” alisema mama Soraya kwa msisitizo, Soraya alionekana kutulia kimya kabisa, ameinamisha kichwa chini……….. ENDELEA NAYO…….
Sio kwamba alikubaliana na wazazi wake ila ni hasira iliyomshika juu ya Talib kumuharibia juu ya mahusiano yake, “kwani Talib anamfahamu huyo kijana, na kama anamfahamu kwanini hakutuambia toka mwanzo kuwa anamfahamu?” aliuliza Mahamud akimtazama Soraya, ambae alikuwa ametazama chini hasira imemshika kwa nguvu sana, alipokosa jibu Mahamud akahamisha macho na kuyapeleka kwa mke wake, “alisoma nae Luhuwiko sekondari” alijibu mama Soraya, na kwa sauti ya kuwa na uhakika, “kwahiyo tutafanyaje ili akamatwe na kuhojiwa?” aliuliza Mahamud huku anamtazama mke wake, “labda tumuulize Soraya atatusaidiaje kumkamatisha kijana huyo?” alisema mama Soraya huku anamtazama Soraya aliekuwa bado ameinamisha chini kichwa chake, “eti Soraya utaweza kutuonyesha anapoishi huyo kijana, wala usiwe na wasi wasi, akionekana kuwa hakuwa na hatia basi ataachiliwa” alisema Mahamud akimtazama mwanae, ambae sasa aliinua uso na hapo ndipo walipo gunduwa kuwa Soraya alikuwa anabubujikwa na machozi, “mimi sina cha kuwasaidia, ila fanyeni munacho hitaji kukifanya, lakini mkae mukijuwa kuwa, munae mfanyia hivyo ndie mchumba wangu na ndie mkwe wenu mtarajiwa” alisema Soraya, kisha akainuka na kutoka kwenye kile chumba cha ibada akaelekea chumbani kwake, “mh! mama Soraya, unajuwa tumesha mkosesha amani Soraya?” alisema Mahamud kwa sauti ya tahadhari, “sasa unadhani najali, bora akasirike tu kuliko kutuletea wezi” alisema mama Soraya kwa sauti ya kutokujali, kisha akainuka sambamba na mume wake kuelekea nje ya chumba cha swala.
Naam wakati baba na mama Soraya wakiwa wanaelekea Chumbani kwao, wakamuona Soraya anakuja nyuma yao, “mama mimi naenda kwa kina Laylah nitakujakesho” alisema Soraya, kwa sauti kavu ambayo ilionyesha wazi kuwa bado alikuwa katika kilio cha kwikwi, “wewe hata bado hujapona vizuri na leo unaenda tena?” aliuliza mama Soraya kwa mshangao na mshtuko na kufanya Mahamud ashtuke, “hajapona nini, kwani Soraya anaumwa?” aliuliza Mahamud kwa mshangao na hapo ndipo mama Soraya alipogundua kuwa aliropoka jambo bila kutazama mazingira.
Mama Soraya akatafuta jibu la haraka, kwa mume wake, “ndiyo alijiumiza goti leo asubuhi wakati anatoka kwakina Laylah” alisema Mama Soraya, na hapo Mahamud akamtazama Soraya, akamuona bado ana uso wa uhuzuni, hooo! pole sana mwanangu, ndio maana nikaona kimya hukuja ofisini, unaendeleaje kwa sasa?” aliuliza Mahamud huku akishusha macho na mkono ili atazame kwenye goti alipoumia binti yake, lakini kabla hajamgusa tayari Soraya alisharudisha mguu nyuma, “nimesha pona baba” alisema Soraya, ambae sauti yake bado ilionyesha kuwa alikuwa ameingia kwenye huzuni kubwa sana, japo hakuwa analia kama ilivyokuwa mwanzo, “Soraya mwanangu, hupaswi kuwa hivyo, sio kwamba sisi tumesema moja kwa moja huyo kijana wako anahusika na jambo hili, ila lazima tufanye uchunguzi juu ya habari hizi, hatutaki uingie moja kwa moja kwenye matatizo, wewe mwenyewe si umeona jinsi ulivyo nusurika kwa Idd?” aliongea Mahamud kwa sauti ya upole na ya kubembeleza, “baba huwezi kujuwa jinsi ninavyo jisikia moyoni mwangu, na siwezi kuwafanya na nyie mjisikie kama mimi, ila nitakosa shukrani na fadhira kama nitaungana na nyie kusikiliza maneno ya Talib, kwajinsi Higgno alivyo nisaidia, tena bila kuomba chochote toka kwangu” alisema Soraya kwa sauti iliyojaa machungu, hapo kikapita kimya kifupi kama vile wazazi wa Soraya walikuwa wanatafakari juu ya maneno ya Soraya.
Wakiwa wametumia sekunde kadhaa ndipo Mahamud alipo ongea, “ni kweli mwanangu tunapaswa kuwa na shukrani kwa kijana yule japo inawezekana pia akawa amefanya kama Talib anavyosema, lakini tunapaswa kutumia busara katika kumchunguza kijana huyu” alisema Mahamud kwa sauti iliyojaa busara ya hali ya juu, “sijwakataza kufanya hivyo, lakini je itakuwaje kama sio kweli, na itakuwaje akagunduwa kuwa, licha ya yote aliy yafanya lakini hatumuamini?” aliuliza Soraya, hapo Mahamud akamtazama mke wake kama vile anahitaji yeye ndie ajibu, lakini mama Soraya hakuwa na jibu, hivyo Mahamud akatoa hitimisho, “ni kweli Soraya, atajisikia vibaya sana na kutuona kuwa hatuna shukrani, sasa fanya kitu kimoja, mualike rafiki yako hapa nyumbani aje ashiriki chakula cha mchana pamoja na sisi aje na wazazi wake, lengo ni kumshukuru na kumkaribisha hapa nyumbani kama rafiki yako” alisema Mahamud, na hapo Soraya aka onekana uso wake ukichanua kwa tabasamu, “asante baba kwa kunielewa binti yako” alisema Soraya kwa sauti iliyoanza kupata matumaini na kuonekana kuwa na furaha mpya, “lakini Soraya ukae ukijuwa kama huyo mtu wako ikibainika alipanga huu mchezo, hakika ataozea jela, nitamuambia Talib aendelee kuchunguza na nikipata ushahidi sitomsikiliza mtu yoyote, nitampeleka polisi akashtakiwe” aliongea mama Soraya kwa hasira na chuki nyingi sana, hakika ungeshangaa kwanini amebadilika ghafla hivi.*******
Baada ya kurudi toka matembezi, ambako alikuwa ameenda kuwatembelea rafiki zake na washirika wake wakubwa kule mwembe chai kijana Talib alijifungia ndani kwake akijiwashia udi wake kama ilivyo kawaida na kujilaza juu ya kochi, huku anajivutia bangi yake taratibu huku anawaza jinsi ya kuutekeleza mpango wake wa kuiba fedha za mjomba wake, “nikikamata ule mkwanja kwanza naenda Dar na chukuwa gari moja la ukweli natufuta demu mmoja mkali, hata wa kwenye kaole (kikundi cha sanaa, kilichokuwa kina onyesha tamthilia zake kwenye kituo kimoja cha runinga) nakula nae kuku week nzima, halafu nageuka, kisha nanunua mjengo wa maana, nakufungua bar moja matata sana kule Lizaborn” hizo ndio ndoto za Malengo ya Talib, ambae aliendelea kupanga mipango yake, “halafu kabla sijaondoka naenda kuchoma tena duka la kina Higgno kama litakuwa limesha funguliwa, ikiwezekana na choma na nyumba yao, inawezekana vipi fala kama yule awe na Soraya” aliendelea kuwaza na mwisho akapitiwa na usingizi.
Bangi na uchovu vilimfanya alale kwa masaa mawili na aliposhtuka tayari ilikuwa ni saa moja kasoro, njaa ikiwa inamchamanda kweli kweli, lakini muda wa chakula cha jioni ulikuwa bado, hivyo alicho kifanya na nikusokota bangi yake na kuanza kuivuta huku akiwa amewasha udi wake.*******
Naam bada ya kumaliza mazoezi yake, Higgno alioga na kuanza mapishi yake akitegemea leo mgeni wake angekula kama jana, hivyo alipika wali na samaki, akakata kachumbari pembeni na mpaka mida hii ya saa moja kasoro alikuwa ametulia na pembni ya moto nje ya kibanda chake anamsubiri mgeni wake, huku kichwani mwake anajikumbusha kilichotokea jana usiku kati yake na Soraya, pia aliwaza kuhusu bahati yake ya kukutana tena na mzee Mahamud.******
Ukweli ni kwamba mama Soraya alianza kuumia kwa kuona mwanae tayari amesha ondolewa uschana wake na kijana ambae siku zote wamemchukulia kama kijana mpole mwenye moyo wa pekee ambae amejitolea kumlinda binti yao katika mazingira hatarishi, lakini sasa, amepata habari kuwa kijana huyo amefanya mchezo wa kuandaa watu ambao ni marafiki zake wajifanye kuwa ni watekaji na yeye kuja kumsaidia, ikiwa ni mbinu ya kumnasa binti yao, “nipo pamoja na wewe mama, lakini na hakika kuwa Higgno siku ukimjuwa na kumfahamu ukweli hauta amini” alisema Soraya kisha akaondoka zake kutoka nje, akiwaacha baba na mama yake wakimsindikiza kwa macho mpaka alipotoweka, kisha waka tazamana na sekunde chache wakasikia ngurumo ya gari ilikiondoka, “hata mimi nilikuwa na mashaka hayo hayo, lakini mama Soraya, umeenda mbali sana ni bora tungekaa nalo wenyewe hilo jambo na kufanya uchunguzi wa kimya kimya” alisema Mahamud, kwa sauti ya kumlaumu mke wake, “tatizo nini baba Soraya, kwamba Soraya amekasirika?, lakini yule ni binti yetu lazima tuwe makini juu ya hili” alisema mama Soraya, “halafu ni kweli Soraya anaenda kwa Laylah, au anaenda kwa huyo kijana wake” aliuliza Mahamud, “tena nimekumbuka baba Soraya, kwanini tusimuambie Talib amfuatilie Soraya ili tupajuwe anapoenda?” aliuliza mama Soraya akiwa kama anatoa ushauri, “hapo umeongea jambo la msingi mke wangu, kama angekuwepo ningempa hiyo kazi” alisema Mahamud, “atakuwepo chumbani kwake, halafu sijui kwanini hajaja kuswali” alisema mama Soraya na hapo mzee Mahamud akakumbuka jambo, “kwanza huyu Talib mbona anatembea usiku sana, unajuwa ile juzi alirudi saa saba za usiku?” aliuliza mzee Mahamud akiwa kama vile amekumbuka jambo, “lakini huyu ni mtoto wa kiume, pengine anaenda kwa wanawake wake” alisema mama Soraya wote wakacheka kidogo, “wacha nikamtazame kama atakuwepo nimpe gari langu ili awawahi kabla hawajafika mbali” alisema mama Soraya, huku anageuka na kutoka nje ya nyumba huku mume wake akiingia chumbani, maana muda wote huu bado walikuwa wamesimama nje ya mlango wa chumba chao.
Mama Soraya alitembea kwa haraka sana kuelekea kwenye ile nyumba ndogo anayoishi Talib, akiwa na lengo la kumueleza Talib aondoke haraka sana kuwafuata wakina Soraya, kilicho mpa moyo ni kitendo cha kuona taa inawaka kwenye nyumba ile ambayo kila alipoisogelea alianza kusikia harufu ya udi, “anapenda udi kama vile anafuga majini” aliwaza mama Soraya, na hapo akakumbuka jambo, “nilimuona kwa macho yangu anavuta bangi ndani kwake huku amewasha udi” yalikuwa maneno ya Soraya yaliyo jirudia kichwani mwake, na kupunguza mwendo ghafla kisha akaubadili kabisa mwendo wake na kuanza kutembea kwa taadhari akiufuata ukuta wa nyumba hiyo wa upande wa kulia na kwenda kujibanza pembeni ya kidogo ya dirisha la nyumba hiyo, kisha akachungulia ndani, ya nyumba ile kwa tahadhari kubwa, naam alichokiona humo ndani kilimfanya aache mdomo wazi………. ITAENDELEA BAADAEEEEE....
 
Mama soraya anataka kuharibu mambo
mama Soraya huyo tushamkaba, akishakuwa mzee Mahamoud ameongea na Higno tayari, Soraya ameshajua kuwa Frank ni Baba yake Higgno tunakoelekea kuzuri
 
Abou Shaymaa Mwamba upo vizuri kwenye uandishi na una reflect maisha halisi ya watu hongera sana nakupa maua yako, ukiachana na tembele la uwani, nyuma ya mlango wa adui na asali haitiwi kidole una simulizi gani zingine ambazo zipo humu nizitafute maana kwa hizi tu unaonyesha uwezo uliotukuka keep it up brother.
 
Weee imefika patamu, mama Soraya anaona misokoto ya bangi, Higno sasa ataalikwa mjengoni mara anakuja kugundua mshenga wake ndio baba mzaa chema wake
 
Hebu tuone hicho kitu kizito, maana hata safari ya kumfuatilia Soraya itakufa

Ila Soraya ataenda kuchukua simu geton kwa Higgy ili amsafishe mpenzi wake
Kabla hajasafishwa Talib atajichomoa kwenye msala
 
Back
Top Bottom