SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA SITINI NA TANO
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA SITINI NA NNE:alisema mama Soraya, akionyesha masikitiko yake kwa kile ambacho ni kama tuhuma juu ya familia yao, “lakini mama si nilisha sema nina mchumba, si awaambie tu kuwa ninae” alisema Soraya kwa sauti ya chini huku anatazama chini, “lakini atawaambiaje kuwa una mchumba na wakati hata wewe mwenyewe humjuwi, na alichosema baba yako ndicho kinacho nihuzunisha zaidi, maana amesema kama yatatolewa mashariti ya wewe kuolewa na Idd, basi hakuna namna itabidi uolewe” alisema mama Soraya na hapo Soraya akatazamana na Laylah kwa macho ya niseme nisiseme, na kabla Laylah haja mkonyeza kwa lolote Soraya akamtazama mama yake ENDELEA……
Naam kabla haja jibu mara wote wakatazama upande wa mlango mkubwa wa kuingilia pale sebuleni wakamuona Talib anaigia pale sebuleni “shikamoo shangazi” alisalimia Talib, ambae alikuja moja kwa moja mpaka pale kwenye meza kubwa ya chakula na hapo maongezi tayari yalisha koma “marahaba,vipi ndio unaamka?” aliuliza shangazi, yaani mama Soraya, “nimeamka kitambo nilikuwa na fanya usafi tu!” alijibu Talib huku anajiandalia vitafunwa na kujimiminia chai, “halafu Talib mbona sikuelewi kuhusu biashara yako hivi inaendeleaje?” aliuliza mama Soraya kwa sauti ya mashaka, “nini biashara?”,mmmh! inaendelea vizuri tu!” Talib akashikwa na kigugumizi cha ghafla, “mh! we haya tu, maana sioni dalili ya uwepo wa biashara yoyote, sikuoni ukifuatilia mzigo nyasa wala kuagizia mzigo wowote” alisema mama Soraya wakati huo Talib mwenyewe hakujisumbua kujibu chochote, aliendelea kukandamiza chai taratibu hapo Soraya akaona kuwa hakukuwa na maongezi tena, “mama wacha mimi niwahi ofisini” alisema Soraya huku anaichukuwa simu yake mezani na kuinuka, “hivi Soraya huoni kama hutaleta picha nzuri kama utaenda ofisini ukiwa unachechemea hivyo, kwanini usiende kwanza Hospital nitampigia kumueleza” hapo Soraya alitulia kidogo, kama anawaza jambo, kisha akamtazama Laylah, wakakubaliana kwa kutikisa vichwa, “sawa mama, basi wacha niende Hospital nikatibiwe , maana baadae nitashindwa kwenda kwakina Laylah” alisema Soraya huku anaanza kutembea kueleka nje, huku akifuatiwa na Laylah, na mama yake anamtazama kwa macho ya mshangao, “mh! kwa akina Laylah tena leo!?” alisema mama Soraya kwa sauti ya chini na ya mshangao, huku anamtazama Soraya aliekuwa anaelekea nje na kuingia ndani ya gari, twende kwanza shoping halafu tukimaliza twende Luhila kwa yule mzee.
Huku ndani Talib ambae alikuwa anafuatilia maongezi ya Soraya na mama yake, alipata wazo la kuvuruga jambo hilo, maana alishajuwa kuwa Soraya anatembea na Higgno na pia anataka kumsaidia kijana wa baba huyo, lakini alipotaka kuongea jambo “na wewe endelea tu! ukae ukijuwa hapa ni kwa mjomba wako, sijui utakaa mpaka lini, maana unapewa mtaji unakula wote, unafikia hatua ya kuomba hela” alisema mama Soraya kisha akainuka na kuelekea chumbani kwake, akimuacha Talib ana tazama mlango wa ofisi ya mjomba wake, ambamo mulikuwa na lile kabati la ukutani lenye kuhifadhiwa fedha, “utajuwa tu hapa nitatoka lini” aliwaza Talib huku anaendelea kunywa chai akipanga kuwa akitoka hapo aendezake mwembe chai kwa Zido akaone maendeleo yao na kuchukuwa bangi.*******
Naam mama Hilda yaani mke wa mzee Komba aliingia nyumbani kwake, na moja kwa moja akaingia chumbani kwa Hilda ambae alimkuta bado yupo kitandani, “ndugu yangu habari za hospital sio nzuri hata kidogo” alisema mama Hilda, huku anakaa pembeni ya kitanda cha mwanae ambae bado alikuwa amelala chali na miguu ameitanua, “vipi kwani amekufa?” aliuliza Hilda kwa sauti ya mshtuko lakini sio wa kuogopa au kuhuzunika, ila ulikuwa ni wakushangilia, “afadhari angekuwa amekufa tunge juwa moja, ila kiukweli kabisa atakuwa mzigo ketu” alisema mama Hilda ambae alionekana wazi kuwa na uchovu wa kulala kwe benchi huku akiwa amelewa, “kwanini unasema hivyo mama, na vipi marafiki zake wanasemaje?” aliuliza Hilda akijaribu kujiinua na kukaa kitako, “walimkimbia usiku ule ule, yule mnafiki ndie alietusaidia hela ya mafuta na matatibabu” alisema mama Hilda huku anajilaza kwenye kitanda, huku miguu ikikanyaga chini, “mnafiki gani huyo au Higgno?” aliuliza Hilda kwa shauku, “ni baba yake, baada ya kukosa msaada wowote nurse akampigia huyo bazazi, ndio akajileta pale na vijihela vyake, akajifanya kutusindikiza mpaka Hospital, na bahati yake hakuniuliza tatizo la mgonjwa” alisema mama Hilda kwa sauti ya dharau, “kwahiyo mama Hosptal unaenda saa ngapi ili tuandae chakula kabisa” aliuliza Hilda akijitahidi kujishusha kitandani, “acha upuuzi bwana unadhani kuna kula pale, mtu ameachama mdomo kama zezeta, navyo kuambia kuwa ni mzigo ni mzigo kweli” alisema mama Hilda yani mke wa mzee Komba, ambae alionyesha kutokuwa na dalili yoyote ya kurudi Hospital, hapo Hilda nae akajirudisha kitandani na yeye alimuunga mkono mama yake.*****
Saa tano na nusu, ndio mida ambayo Kijana Higgno, alikuwa ndani ya dala dala akielekea mjini huku amevalia nguo nzuri ambazo aliletewa na Soraya jana, njia nzima kijana huyu ambae alikuwa anaenda mjini kwa mambo mawili tu, moja ikiwa ni kukutana na baba yake ambae alimuambia kuwa mipango ikikaa sawa watahitaji kununua vifaa vya dukani, pili alihitaji kufanya manunuzi kama alivyo shauriwa na Soraya kwa fedha alizompatia, muda wote alikuwa anavuta picha ya matukio ya jana usiku kule shambani na Soraya, na kuna baadhi ya matukio yalimfanya ajikute akisimamisha mnazi wake, “dah! siamini yaani demu mzuri kama yule alikuwa hajawahi kufanya chochote, hakika sitomuacha kwa namna yoyote ile” aliwaza Higgno huku safari ikindelea, wacha nikanunue pamba kali sana, maana nikiwa navaa kama hivi naweza hata kuongozana nae” aliendelea kuwaza Higgno, hata gari lilipofika mjini na kusimama kituo cha soko kuu.
Hapo Higgno akashuka akiwa mwenye furaha tele na kuanza kuzunguka madukani akinunua nguo na viatu vizuri vya kiume na vya kike kwaajili ya mpenzi wake Soraya, na hata ilipotimia saa sita na nusu ndipo alipopata wazo la kumpigia baba yake, lakini alipojaribu akagundua kuwa vocha imeisha kwenye simu yake, hapo akaanza kutafuta duka la vocha.
Naam wakati Higgno analikaribia duka hilo akaliona gari fulani ambalo halikuwa ngeni machoni mwake, na wakati akilikodolea macho gari lile kumtazama aliekuwa anashuka kama ndie anaemfahamu au sie, akamshtuka kuona anafanya kitu fulani cha bahati mbaya, ambacho hata yeye alishukuru kuwepo pale, maana kama angeona mtu mwingine basi ingekuwa tatizo kwa mtu yule ambae alikua anatamani sana kukutana nae.*****
Naam mida hii ya saa sita ndiyo mida ambayo Talib alitoka kwenye nyumba yake na kufunga mlango kisha akaanza kutembea kuelekea getini, “wewe mida ya swala inakaribia na wewe unaondoka bila hata kuaga” Talib alishtuliwa na shangazi yake, ambae alikuwa anatembea kumsogelea, “yaani shangazi unamuachia Soraya wakike afanye anavyotaka halafu mimi ndiyo una niwekea ngumu” aliongea Talib kibwege, “hebu muone kwanza, Soraya tunamuachia nini?” hapo Talib aliona kuwa hiyo ndiyo sehemu pekee ya kuvuruga kuhusu mahusiano anayo yahisi ya Soraya na Higgno na jambo lile la kumsaidia baba yake Higgno, “we! shangazi muache tu Soraya ajitawale, unadhani Soraya analala kwa Laylah, huyu analala kwa mjinga mmoja anaitwa Higgno, na hata huyo mzee anae sema sijui anafahamiana nae sijui ameunguliwa duka hakuna lolote ni baba yake Higgno” alisema Talib kwa sauti iliyojaa chuki na tahadhari kwa shangazi yake, “kwahiyo unafahamu huyo mchumba wa Soraya, je ni yule yule alie msaidiaga?” aliuliza mama Soraya kwa mshangao, “na mfahamu vizuri sana, ni pimbi mmoja tu, hana lolote, tena wala usiruhusu amuoe Soraya” alisema Talib kwa dharau na chuki, “kwahiyo huyo ni mwingine sio yule aliemsaidia?” aliuliza mama Soraya, akionekana kushangazwa na lile jambo la kuwa Talib analikuwa anamfahamu mwanaume wa Soraya, “amsaidie wapi bwana, ni mchezo tu huo, we! unadhani Soraya alitekwa kweli?” alisema Talib na kumfanya shangazi yake aache mdomo wazi kwa mshangao huku Talib akicheka kimoyo moyo “unasema Soraya kapanga huo mchezo kuturubuni sisi?” aliuliza mama Soraya kwa mshangao, maana alikuwa anamfahamu vyema binti yake kuwa hawezi kufanya mchezo, huo na pia kwa miaka yote hiyo tayari wangesha ng’amua kama ni mchezo wakupangwa.
Hapo kidogo Talib akashtuka, na kuona kuwa, hawezi kumsingizia Soraya jambo hilo, kwasababu mama yake anamfahamu vizuri, “kuhusu Soraya kuhusika sidhani, ila hao jamaa walio mteka ni rafiki zake kabisa” kauli hii ya Talib, ilimshtua zaidi mama Soraya, “weeee! ina maana miaka yote hii alikuwa anatuchezea mchezo wa kitoto kama huo?” aliuliza mama Soraya kwa sauti ya mshangao, akionyesha kuamini moja kwa moja kile alichoelezwa na mtoto wa kaka yake, “sasa je yule boya mimi ninamfahamu kitambo toka Luhuwiko sekondari, hawezi hata kurusha kofi, halafu apigane na watu sita kimchezo mchezo tu!” alisema Talib na hapo mama Soraya kwanza alivuta hisia za mwendo wa Soraya ambao alikuja nao asubuhi na kuondoka nao, akidai alijikwaa mara alijigonga kwenye mlango, pia akakumbuka tabia mpya ya Soraya ya kumkatalia mama yake kuingia ndani ya chumba chake wakati ana ishiwa pose, maana alijuwa tayari mwanae Soraya amesha tapeliwa, kitumbua chake ambacho kinakila dalili ya kuwa kimeshaondolewa utandu, “lakini Talib, unajuwa habari zako zina nichanganya sana wewe umejuwa lini haya mambo?” aliuliza mama Soraya kwa mshangao na simanzi, maana hata yeye alikuwa anafikiri kuwa kijana huyo ni mwanaume sahihi wa Soraya.
Kwanza Talib alicheka kwa dharau, “shangazi bwana, yaani mimi machale yalinicheza siku ile ya tukio, nikaamua nifanye upelelezi wangu wa chini chini hahahahaha!” alisema Talib akimalizia kwa kicheko, “yaani nimechanganyikiwa vibaya sana, huyu kijana aliwezaje kupanga mambo yote hayo, toka mwaka tisini na nane pale alipomuokoa Soraya asibakwe na wale wanafunzi wakorofi wa Songea boyz?” aliuliza mama Soraya kwa sauti ya chini kama vile ananong’ona, “nini kwani Higgno ndie aliemsaidia wakati ule…… yaani namaanisha Higgno aliwezaje wakati alikuwa boya tu?”aliongea Talib kwa mshangao, na kama shangazi angekuwa makini angegundua jambo toka kwa Talib, “ndiyo ni yeye, ndio maana nashangaa maneno yako, maana hata siku ile Idd alipomlewesha Soraya aliokolewa na huyo huyo, sasa unataka kusema yule kijana alishirikiana na Idd wakati Idd mwenyewe anamtaka Soraya kwa udi na uvumba?” aliuliza mama Soraya, likiwa swali jingine gumu kwa Talib ambalo lilimuacha mdomo wazi, “sasa unauliza nini hapo, wakati Idd mwenyewe ni mwizi tu!” alisema Talib, ambae aliona akiendelea kukaa pale anaweza kukaribisha maswali mengine magumu zaidi, na mpango wake kuvurugika, hivyo alianza kuondoka kueleka getini akimuacha shangazi yake anamsindikiza kwa macho ya mshangao, “huyu anasema nini, mbona kama haeleweki eleweki, na kwanini aseme hivi, maana naona wazi kuwa ni kama uongo, kwasababu miaka yote hii alikuwa wapi kutimiza lengo lake, na wakati tayari Soraya alikuwa anamzungumzia?” alijiuliza mama Soraya huku anaelekea ndani, “lakini kwa upande mwingine kuna ukweli ndani yake, sijui nitaanzaje kumueleza baba Soraya” alijisema mama Soraya, na alipofika sebuleni akachukuwa simu yake na kuelekea chumbani kwake huku anabofya simu yake na kumpigia baba mzee mahamud, ambayo haikuita muda mrefu ikapokelewa, “hallow baba Soraya kuna jambo nahitaji tuongee” alisema mama Soraya kwa sauti iliyoonyesha msisitizo, jambo gani hilo….” kabla mzee Mahamud hajamalizia kuuliza ghafla simu ikakatika, na alipojaribu kupiga tena simu yake haikufanikiwa kwasababu tayari alishaishiwa vocha, kumbuka kipindi hicho hakukuwa na utaratibu wa vufurushi, hivyo hakuwa na uwezo wa kutuma hata ujumbe.******
Sina mengi alikuwa ndani ya chumba cha doctor, akieleza shida yake ya meno, “unatakiwa kutoa shilingi elfu kumi na tano ili upewe meno mengine” hilo ndilo jibu ambalo Sina mwenye shilingi elfu nne baada ya kutumia shilingi elfu moja kwa nauli na chai alilopewa na doctor, jibu ambalo lilimfanya mwanamama kikongwe kuanza kuomboleza, “doctor naomba unisaidie, nipo tayari kwa lolote lile lakini fedha sina” alisema Sina, akimaanisha kuwa yupo tayari kwa rushwa ya ngono.
Lakini doctor alianza kwa kuangua kicheko, maana alilinganisha muonekano wa mwanamke huyu kikongwe mwenye sura mbaya na umbo la kuchukiza, “sikia mama, hauna chochote cha kunipa ili nikusaidie, cha msingi tafuta hata elfu saba unaweza kusaidiwa kwa mkopo, na ukizingatia umri wako ni kubwa” alisema Doctor, basi wacha nika tafute elfu tatu niongezee nitarudi tena” alisema Sina na kutoka kwenye chumba cha doctor kisha akatokomea mtaani, akielekea kati kati ya mji.*******
Mzee Mahamud ambae toka asubuhi alipofika ofisini alionyesha wazi kuwa na mawazo yanayoumiza kichwa, mida hii alikuwa njiani akieleka mjini kwa lengo la kuelekea msikitini kwa swala ya saa saba yani ile Adhuhuri, pia kuongea na wazee wa baraza.
Sasa alikuwa amesimamisha gari karibu na Soko kuu, akiwa ndani ya gari ameshikilia simu yake mkononi, “sijui anataka kusema nini mama Soraya” alijiuliza mahamud huku anabofya namba ya mke wake kwaajili ya kumpigia, akiamini mke wake aliishiwa vocha kwenye simu, na alikuwa na jambo muhimu la kuongea nae.
Mahamud alipiga namba na kuweka simu sikioni, “hauna salio la kutosha kupiga simu hii” ilisikika sauti ya kike, “hoooo! kwanini leo nimesahau kuweka vocha” alijishangaa mzee Mahamud ambae aliweka simu kwenye kiti cha pembeni cha gari lake na kuondoa gari hili aina ya Nissan patrol kuingia barabara ya chini ya Soko kuu, barabara ambayo huelekea mpaka msikiti wa mkoa, ambao upo umbali wa mita mia tu! toka sokoni hapo.
Mahamud aliendesha gari kwenye barabara ile, huku macho yake yakiwa kwenye maduka ya pembezoni mwasoko, akitazama kama anaweza kuona duka la vocha, ili aweke na kumpigia mke wake, na hata alipofanikiwa akasimamisha gari pembeni ya barabara na kuchukuwa pochi yake yenye kadi za benk kitambulisho na fedha, kisha akashuka huku anaiweka mfukoni ile pochi yake ambayo hata ufungaji wake ulikuwa ni mgumu kutokana na ujaaji wa fedha, na akiwa na uhakika kuwa ameweka ndani ya mfuko wa nyuma wa suruali yake, mzee Mahamud akaelekea kwenye moja duka alilo lilenga kuwa linauza vocha za simu, kipindi hicho zikitwa dolla, “karibu mzee” alikaribisha kwa sauti iliyojaa heshima na nidhamu ya hali ya juu mschama mdogo muuza duka, akionyesha anamfahamu mzee Mahamud tajiri mkubwa mwarabu hapa mjini Songea, asante sana, naomba dolla ya elfu kumi, “alisema Mahamud kwa sauti ya unyenyekevu iliyojaa urafiki, huku akitabasamu, japo hakuwa anamfahamu yule mschana mdogo, ikiwa ni kuonyesha kuwa ameunga mkono nidhamu ya mschana yule ambae alichangamka mara moja kuchukuwa vocha mbili za elfu tano tano na kumpatia mzee Mahamud, akiwa amesha zikwangua lakini hakupokelewa, baada yake alimuona mzee huyu anajipapasa mifuko yote, “mungu wangu nimedosha wallet yangu” alisema Mahamud, ambae kwake fedha zilizokuwepo ndani ya wallet ile sio lolote, ispokuwa kadi za benk na vitambulisho, hakika alijihisi kijacho chembamba kinamtoka huku yule binti anamtazama kwa mshangao na huruma, “nina mkosi gani jamani” alijikuta akijiuliza kwa sauti Mahamud, huku anageuka kutazama kule alikotoka hasa kwenye gari lake, ambalo lilikuwa mita kama ishirini toka pale alipokuwepo, hakuona chochote chini, yaani sehemu alizopita zaidi ya watu waliokuwa wanaendelea na pirika zao, akamgeukia yule mschana, “samahani kwa usumbufu mwanangu, nimepoteza wallet yenye fedha” alisema mzee Huyu kwa sauti ya masikitiko, “lakini mzee najuwa huwezi kunikimbia, unaweza kuchukuwa vocha kisha ukaleta siku nyingine….” alisema yule mschana ambae hata kabla hajamaliza kuongea akakatizwa na sauti tulivu ya upole, “shikamoo mzee Mahamud, umedondosha pochi yako wakati unashuka toka kwenye gari” kauli ile ilipita kichwani kwa Mahamud kama mwangwi wa mawazo, hakuamini kama ni kweli kuna mtu anaongea, lakini alipomuona yule mschana muuza duka anatazama upande wa mlango wa duka, akajuwa kuwa ni kweli kuna mtu aliongea, na sio mawazo yake, hivyo na yeye akatazama.
Naam mahamud alijikuta anatoa macho ya mshangao mara mbili, ni mshangao ulio ambatana na tabasamu jipya la matumaini, ni baada ya kumuona kijana mmoja mrefu kiasi mwenye mwili wa mazoezi, ambae leo alikuwa amevalia nadhifu, ni kijana yule yule aliemsaidia mwaka mmoja uliopita siku aliyovamiwa na wezi kwa lengo la kumpora fedha, ni kijana aliemsaidia kubadiri tairi la gari lililotobolewa na mtego wa wezi wale akiwa amesimama mbele yake amashika wallet yake akimnyoonyeshea kwa maana ya kumpa, “amakweli ukiona kiza kinashamiri basi mawio yaja” alisema Mahamud huku tabasamu likiendelea kushamili usoni mwake…… ITAENDELEA MUWE NA USIKU TUKUTANE KWA MKAPA AU HATUCHEZII?
Hatuchezi😂
 
Sina ndio mtu pekee atayekuja kusababisha Idd kuja kuumbuka mana atakuja kuyamwaga maovu yote mbele ya wazee wa msikiti,ni bora idd aachane na kusumbua mahamudu juu ya swala la ndoa
 
mambo yanazidi kunoga, ukweli wa Idd utawekwa hadharani na dada kibogoyo, Higgno amekubalika kwa kwa mzee mahmud siku ikijulikana ni yeye anapewa mtoto hapo hapo
 
Ashakum sio dharau:
Wale wenye arosro ya simulizi basi kabla ya Bosi hajatupia kipande kingine hebu tupoteze muda hapa kwa ushindi wa Simba Sports Club:

Bofya: Simulizi ya Ujasusi inaitwa:
Do not shout (usipige kelele)

Andika hivi:
"Simulizi: Do not shout (usipige kelele)" halafu sachi
Mtakuja kunishukuru humu:
Hiyo tayari mkuu, wewe ndio unasoma leo? story ya mwaka juzi
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA SITINI NA SITA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA SITINI NA TANO: Naam mahamud alijikuta anatoa macho ya mshangao mara mbili, ni mshangao ulio ambatana na tabasamu jipya la matumaini, ni baada ya kumuona kijana mmoja mrefu kiasi mwenye mwili wa mazoezi, ambae leo alikuwa amevalia nadhifu, ni kijana yule yule aliemsaidia mwaka mmoja uliopita siku aliyovamiwa na wezi kwa lengo la kumpora fedha, ni kijana aliemsaidia kubadiri tairi la gari lililotobolewa na mtego wa wezi wale akiwa amesimama mbele yake amashika wallet yake akimnyoonyeshea kwa maana ya kumpa, “amakweli ukiona kiza kinashamiri basi mawio yaja” alisema Mahamud huku tabasamu likiendelea kushamili usoni mwake……ENDELEA……..
Huku akiendelea kumtazama kijana huyu, ambae mara ya mwisho alimuona kwa sekunde kadhaa kule ofisini kwake na kuambiwa kuwa ameondoka ni kijana pekee ambae yeye Mahamud alimuona kuwa anafaa kumuoa binti yake Soraya, kijana ambae sio tu kufurahi kuonana nae, lakini pia alikutana nae katika siku muhimu sana kwake, “assalama Alaykum kijana, habari za siku nyingi” alisalimia mzee Mahamud kwa sauti ya uchangamfu na mshangao ndani yake, huku anapokea ile wallet toka kwa kijana mpole, “waalaykum salaam mzee kumbe bado unanikumbuka, nilidhania umesha nisahau” alisema Higgno kwa sauti yake tulivu lakini ni ile iliyochangamka, “nitakusahau vipi kijana wakati kila siku mimi na familia yangu hatuachi kukutaja, sijui kwanini uliondoka pale ofisini wakati nafasi yako ya kazi ipo wazi kabisa?” aliuliza Mahamud kwa, huku analipia vocha kwa yule dada ambae mpaka sasa alikuwa amekodoa macho kwa mshangao, “nili…” Higgno alisita kuongea kwasababu kama angeongea ukweli lazima angemtaja Laylah, ambae hakujuwa ni kwanini alionekana kwenye ofisi za mzee huyu siku ile, “nilipoona siitwi jina nikaondoka, nikasema nitakutafuta siku nyingine” alisema Higgno akificha siri ile, “sio tatizo, cha msingi ni kwamba leo tume kutana” alisema mzee Mahamud huku ana malizana na muuza duka, “kwa kweli imekuwa bahati kwangu” alisema Higgno, alieshika mfuko wenye vitu alivyonunua mchana ule, akionyesha wazi furaha yake ya kukutana na mzee Mahamud, ambae hakujuwa kuwa ni mkwe wake, “ok! kijana vipi unashughuri gani sasa, yaani muda huu?” aliuliza mze Mahamud, na hapo sio tu yule binti pekee aliewaza kuwa hawezi kusema kuwa alikuwa busy na shughuli fulani mbele ya mzee kama huyu, ambae ni mmoja kati ya matajiri wakubwa hapa Tanzania, hata Higgno ambae alikuwa anahitaji kazi ili aweze kumudu maisha na pengine kuweza kumnunulia mahitaji mpenzi wake Soraya, ambae mpaka sasa hakuwa anajuwa ni mtoto wa nani pale mkoani, “nimesha maliza kununua mahitaji yangu” alisema Higgno akisahau kuhusu baba yake, ambae hakuwa amewasiliana nae toka alipowasiliana nae asubuhi, “ok! basi kijana naomba uambatane na mimi kwa muda huu, maana tuna mambo mawili matatu ya kuzungumza” alisema Mahamud, huku akiongozana na Higgno kutoka nje ya duka lile, “bila shaka mzee wangu” alisema Higgno, ambae alikuwa amebaba mfuko wake huku wanaelekea kwenye gari, huku mzee Mahamud akiwaza na kumtafakari kijana huyu kuwani kijana wa pekee katika nyakati hizi za utakula kwa ujanja wako, kuwa ndie kijana anaweza kumchumbia binti yake Soraya, “vipi kijana unafamilia?” aliuliza mzee Mahamud, mara tu! baada ya kuingia ndani ya gari, akiwa na maana ya kwamba kijana huyu ana mke na watoto, “ndiyo ninayo” alijibu Higgno kwa uchangamfu, akidhania kuwa mzee huyu anauliza kama anafamilia ili kuona kama ana maisha ya aina gani, maana familia ni moja ya picha ambazo umueleze mtu, lakini haina maana kuwa asie na familia ni muhuni.
Lakini jibu ilo lilimshtua kidogo mzee Mahamud, ambae Mahamud alikuwa anaendesha gari huku Higgno akiingiza vocha kwenye simu, mahamud ambae aliamini kuwa kijana huyu ndie kijana wa pekee ambae anaweza kuwa mkwe wake kwa binti yake wa pekee, “hooo! hongera sana kijana, una watoto wa ngapi?” aliuliza mzee Mahamud, huku anampatia Higgno simu na vocha ili awez kuingiza kwenye simu ile na kuondoa gari kuelekea upande wa msikiti wa mkoa, swali lile lilimfanya Higgno acheke kidogo, “hapana mzee sijabahatika kuoa” alijibu Higgno na kumshangaza kidogo, Mahamud, “sasa wewe unaizungumzia familia ipi?” aliuliza Mahamud huku anatabasamu, “nilidhani unaniuliza kuhusu baba na mama” alisema Higgno na wote wakacheka kidogo, “”kwanini hujaoa mpaka umri huo kijana?” aliuliza Mahamud huku anaendesha gari taratibu, “bado sijapata kazi, sasa nikioa nitashindwa kumlea mke na pengine watoto wakizaliwa” alijibu Higgno kwa sauti tulivu na ya upole, kwahiyo ukipata kazi unaweza kuoa?” aliuliza Mahamud kwa sauti ambayo ilijaa urafiki, “ndiyo mzee nikipata kazi nitajitaidi nifanye kazi kwa juhudi huku anajiandaa kimaisha halafu naoa” alijibu Higgno kwa sauti tulivu iliyojaa hekima huku anamaliza kuingiza vocha kwenye simu, “unadhani ni vitu gani unahitaji kuandaa ili uweze kuoa” aliuliza Mahamud, akiwa anagesha gari pembeni ya msikiti, ambao kwa sasa ulionekana kuwa na watu kadhaa waliokuja kwa swala ya adhuhuri, wengi wao wakiwa ni wazee wa baraza la wazee, “ni sehemu nzuri ya kuishi, na uwezo wa kupata mahitaji muhimu ya familia” alijibu Higgno akicheka cheka na kumpatia mzee Mahamud simu yake, tayari alishaiweka vocha.
Baada kusikia jibu hilo bwana Mahamud akatulia kidogo kama vile anatafakari jambo juu ya kijana huyu, kisha akamtazama Higgno kwa macho makini sana, macho ambayo hata Higgno aliweza kuona umakini wake, “ok! sikia kijana, kuna jambo ambalo nililipanga siku ile uliponisaidia kule Msamala, sio kwamba nimelifikiria leo hii, na hili swala ni la mimi na wewe tu, sihitaji mtu mwingine ajuwe” alisema Mahamud huku anatazama kule walipo wenzake, ambao walikuwa wanachukuwa udhu (kujitakasa, kabla ya kuingia msikitini kwa swala) Higgno akimsikiliza kwa umakini sana, huku kifua kikijaa pumzi kwa hofu na shauku, “kijana nipo tayari kukupatia kila unacho hitaji, na nitakupatia zaidi ya unachohitaji, ukiachilia kazi ambayo uliniomba mwenyewe, pia nitakupatia nyumba, gari, fedha na biashara kubwa, kwaajili ya maisha yako, na mke wako, ambae ndie shariti langu kubwa” hapo Higgno akashtuka kidogo, ni kweli alikuwa anahitaji fedha nyumba gari na hata hiyo biashara, lakini kilichomtia shaka ni sharti ambalo bado hajaelezwa, japo aliambiwa lina muhusu binti wa tajiri huyo, sio yeye tu, vijana wengi wa hali yake ya kimaisha hawakuwa wanamfahamu binti huyo, na hawakuwahi kufahamu kama tajiri huyu ana binti.*******
Tayari mzee Frank alisha kutana na Soraya, na kuambatana nae kuelekea mjini kwaajili ya kufanya manunuzi ya duka lake jipya, huku Frank akiambatana na mke wake ambae alibeba chakula kwaajili ya mgonjwa wakimuacha Pale hospital akimueleza ward aliyo lazwa mzee Komba, na mzee Frank akiwa na Soraya na Laylah wakaelekea mjini ambako walimpatia fedha mzee Frank na kumkodia gari dogo la mizigo kwaajili ya kubebea vitu, “sasa binti yangu, umenifanyia mengi sana, na umeniomba niwe mshenga wachumba wako, mbona kijana mwenyewe simjui na wala sijawahi kumuona?” aliuliza mzee Frank, kabla ya kuondoka zake na kuanza manunuzi, Soraya alichekesha kidogo, “anakaa kule kule Luhila utakuwa unamfahamu, anaitwa Hig…. kabla hajamaliza kuongea Soraya alisita ghafla na kutazama pembeni ya barabara, akikodoa macho kwa mshangao kumtazama mwanamke mmoja mtu mzima aliekuwa anapita pembeni ya barabara, akionekana kuchoka na hali yake, tena mwingi wa mawazo, “Laylah unamuona yule mwanamke” aliuliza Soraya, na hapo sio Laylah peke yake alietazama, hata mzee Frank pia alitazama kule alikoonyesha Soraya, wakamuona yule mwanamke mtu mzima, akiwa anatembea taratibu akija usawa wa gari lao, “ndiyo nimemuona, ana nini kwani?” aliuliza Laylah, huku anageuka kumtazama Soraya ambae alimtazama mzee Frank, “samahani baba, nadhani tutawasiliana wewe unaweza kuendelea na shughuri zako za manunuzi, alisema Soraya akionyesha kuwa mwenye haraka sana, hapo mzee Frank hakuwa na lakufanya, kwasababu aliona kuwa ni mambo yasiyo muhusu, hivyo akaondoka zake na kumuacha Soraya anamtuma Laylah kwenda kumsimamisha yule mwanamke walio muona, “wa nini lakini, mbona mama wa watu kajichokea kwani unamfahamu?” aliuliza Laylah, huku akimtazama yule mwanamke ambae sasa alikuwa analivuka gari lao, “msimishe kwanza asiondoke” alisema Soraya kwa sauti ya ukali na hapo Laylah, akashuka toka kwenye gari, na kumfuata yule mwanamke, ambae tuna weza kumuona vizuri kuwa ni Sinamengi, “mama mama sahamani kidogo?” alisema Laylah, huku anamgusa begani Sinamengi, nae akageuka na kumtazama Laylah, “nani mimi?” aliuliza Sinamengi kwa mshangao, maana hakutegemea kusimamishwa na mschana mwenye hadhi ya huyu aliemsimisha, “ndiyo ni wew unaitwa na mdogo wangu yupo ndani ya gari lile pale” alisema Laylah huku akionyesha gari lao, yaani Land Rover Discovery.
Hapo moja kwa moja mwana mama Sina akapeleka mawazo yake kwenye kupata fedha za kujinunulia meno, ambayo yalikanywagwa na kijana Idd, “ok! twende zetu” alisema Sina, huku ana ongoza mwenyewe kueleka kwenye gari la Soraya.********
Mzee Mahamud akamtazama Higgno, anamuona yupo makini anamtazama akimsikiliza, “kijana nitakufanyia hayo yote endapo utakubali kumchumbia binti yangu, sijui unasemaje kijana?” aliuliza Mahamud akionyesha kuwa amesha maliza maongezi yake, hapo Higgno akatabasamu kidogo, yaani lile tabasamu la huzuni, tabasamu ambalo hata mzee Mahamud aliliona, kabla ya kuongea Higgno alishusha punzi ndefu, yaani ile ya uchovu na kuhemewa na mzigo mzito, “samahani sana mzee wangu, kikweli, nina mchumba tayari, japo tumekutana hivi karibu, lakini ni mchumba ambae kiukweli nime mpenda na yeye amenipenda, itakuwa vibaya sana nikiuumiza moyo wake kwakufanya jambo kama hilo, isitoshe mzee kwa kitendo hicho nitaonekana msaliti mbele ya binti yako, ambae atafikiria kuwa, endapo nitampata mschana mwingine ambae wazazi wake au yeye mwenye anafedha zaidi nitamuacha na kuishi nae, kwa kifupi nitakuwa sijatimiza mapenzi zaidi ya kutimiza tamaa zangu” alisema Higgno kwa sauti tulivu iliyojaa nidhamu.
Naam hapo Higgno aliweza kumuona Mahamud, akiwa ametazamisha kichwa chini kama anatafakari jambo, hapo Higgno akatulia kimya akisubiri kauli ya mzee Mahamud, huku akiwa amejwa na wasi wasi kuwa maneno yake yame mkera Mahamud na kusababisha yeye kupoteza kila kitu, yaani kazi na maelewano na mzee huyu.
Lakini Mzee Mahamud baada ya kutulia kwa sekunde kadhaa, akainua uso wake na kumtazam, ndipo Higgno alipotambua kuwa mzee Mhamud alikuwa anatabasamu, “kweli binti yangu amekosa kijana mwenye kila sifa ya kuwa mume, ok! nitakusaidia kupata kazi, utakuja kesho kutwa ofisini , labda kijana kama kuna kitu kingine ambacho utahitaji nikusaidie nje ya kukupatia kazi?” aliuliza Mahamud kwa sauti ya kirafiki kabisa, japo ilipooza kidogo, hapo kijana Higgno alitulia kidogo akiwaza na kutafakari juu ya nafasi aliyopewa na mzee Mahamud, “mzee mimi na maombi mawili toka kwako kama itakupendeza” alisema Higgno kwa sauti ile ile iliyojaa heshima, “usiwe na wasi wasi kijana, hata kama yangekuwa kumi we nieleze tu, naamini yatakuwa ndani ya uwezo wangu” alisema Mahamud akionekana wazi, alikuwa anamaanisha alichokisema, “mzee wangu, jambo la kwanza naomba usichukulie kama dharau kwa kile nilichosema juu ya kumchumbia binti yako, nadhani hata wewe unafahamu kuwa mimi ni kijana ambae sina lolote, na ni sawa na mtumishi wako, pengine hata kukaa na wewe kama hivi ni bahati kubwa kwangu….” alisema Higgno kabla Mahamud hajamkatiza, “kijana umeenda mbali sana, wala usiwe na shaka juu ya jilo ongea hilo swala jingine” alisema Mahamud, ambae alitegemea kwa kupambwa vile basi sasa unakuja mzinga (kuombwa fedha) kama ulivyo utaratibu watu wengine, hasa watu wake wa karibu hasa wanapokuwa shinda huwa wanaanza kwa kumpamba kwa maneno matamu, “la pili mzee wangu ninaomba msaada wako katika ushawishi wa wazazi wa mchumba wangu ili wasiniwekee kipingamizi chochote wakati wa kupeleka barua ya posa, nahofia wanaweza kunikatalia kutokana na hali yangu ya kipato” alisema Higgno kwa sauti iliyojaa unyonge, “kwanini umewaza hivyo kijana, kwani huyo binti ni mtoto wa nani?” aliuliza mzee Mahamud, akionyesha wazi kufadhaishwa na hali ya unyonge ya kijana huyu, ambae sio siri mpaka sasa hakuwa ameulizia jina lake, “mzee wangu kwa kweli hata wazazi wake siwajuwi, lakini nadhani nikiwajuwa na kukueleza lazima utawatambua, kwasababu ni…” kabla Higgno hajamaliza, tayari Mahamud alishadakia, “basi usiwe na wasi wasi, we kaongee na huyo mschana kisha utanijulisha, tena nikuhakikishie kuwa mimi nitakuwa mshenga wako na nitahakikisha hakuna kinacho haribika” alisema Mahamud, huku anatazama kule kwenye lango la kuingilia ndani ya msikiti ambapo walionekana watu wakiingia, “hooo! kijana hebu twende tuwahi swala, naona muda unaisha” alisema Mahamud, huku anafungua mlango wa gari nakuanza kushuka, “samahani mzee sijawahi kujifunza mafundisho ya dini ya kiislam mimi ni mkristu” alisema Higgno huku nae anafungua mlango na kushuka, hakuweza kuona mshangao wa wazi usoni kwa Mahamud, “hoo! samahani sana, kijana kumbe nimekuleta sehemu sio sahihi kwako” alisema Mzee Mahamud akipoteza ule mshangao wake kwa haraka sana, “hapana mzee wangu, sidhani kama kuna ubaya, maana kila dini inayohubiri amani, upendo, na kumcha mungu muumba, ni dini ya haki, hivyo hakuna ubaya, hata ingekuwa inawezekana ingekuwa ijumaa mtu anaingia msikitini na jumapili anaenda tena kanisani” alisema Higgno, na hapo Mahamud akamtazama Higgno, kwa namna fulani ya kumshangaa huku anatabasamu, “unakipaji kizuri sana kijana, kama ungekuwa mwalimu wa dini katika madrasa fulani basi ingekuwa faida kubwa sana kwa kizazi hiki, toka nimeanza kukuona mwaka jana umekuwa ni mtu wakushangaza kwa busara na wema wako” alisema Mahamud huku anatoa card ya biashara yani busness card, “mawasiliano ndiyo kitu pekee kilicho tutenganisha hapo mwanzo” alisema Mahamud kisha, wakaagana na kisha kila mmoja kutaka kuondoka lakini Mahamud akakumbuka jambo, “kijana, hebu subiri kidogo” alisema Mahamud, na kuanza kumfuata Higgno, ambae kwa kuona hivyo alirudi mbio kumfuata Mahamud, “nimesahau bwana” alisema Mahamud huku anaingiza mkono mfukoni na kutoa wallet yake, “chukuwa hii itakusaidia kwa mambo madogo madogo” alisema Mahamud huku anampatia noti kadhaa za elfu kumi kumi za idadi ya kumi na tano, “hapana mzee wangu nina akiba kidogo, inaweza kunifaa, nikiwa nashida nitakujulisha mzee wangu” alisema Higgno kwa unyenyekevu, huku anakutanisha viganja vya mikono yake na kuinamisha kichwa cheke, ikiwa ni ishara ya heshima kwa Mahamud, ambae sio tu kushangaa ila na kuduwaa pia, “ok! kijana wacha niwahi swala usiache kunitafuta,alisema Mahamud huku akigeuka na kuelekea msikitini, na Higgno akaelekea upande wa pili wa barabara na kuingia kwenye moja ya chochoro,, inayotumika kama njia ya mkato kuelekea soko kuu, huku kijana huyo akikumbuka kuwa anahitaji kumpigia simu baba yake ili ajuwe kama anakuja mjini au vipi.*******
Naam wakati huo wakina Idd, na baba yake walikuwa njiani wanaelekea msikitini kwa upande wa Idd sio kwamba alienda kwaajili ya swala, hapana Idd ambae mpaka mida hii alikuwa ameshalewa, akidai ni starter ya kuweza kumudu maongezi ya kwenye baraza la wazee, alikuwa anaenda mskitini kwaajili ya kushuhudia jinsi wanavyo kubaliwa kumchumbia Soraya, maana waliamini mtego waliouweka unge
saidia kutimiza hayo, hakika wawili hawa walikuwa na furaha ya hali ya juu, hata walipofika eneo la msikiti walikutana na wajumbe wengine wakiwa wamejaa kuliko siku zote, “hapa lazima Mahamud akubali haraka kutoa binti yake kwa maswali atayo tundikwa hapa, mwenyewe atakubali yaishe” alisema Mahadhi Salum, aliekuwa anaendesha gari, na sasa wanaingia eneo la msikiti, “mdingi mimi nakukubali kinyama, yaani hata wakati ule nilipo shuka bondeni (Africa ya kusini) ninge kushirikisha nadhani mpaka sasa tunge kuwa matajiri wakubwa sana hapa Songea” alisema Idd kwa sauti ya kilevi huku ana jitahidi isionekane kama amelewa, japo alikuwa anatafuna big G, yaani banzoka, lakini bado kwa mbali harufu ya pombe iliweza kusikika, “ila tukubaliane ukisha mchukuwa tu Soraya, kwanza unaninunulia gari moja zuri jipyaaaaa, halafu una…” kabla mahadhi hajaongea neno jingine, Idd akadakia mara moja, “hilo jibu baba, kwanza hujasikia kuwa yale mabus mapya yote Mahamud ana mkabidhi Soraya, amemfungulia kampuni yake, hivyo nitakuwa na mkwanja wa maana sana, baba utaoga fedha kama taka taka” alisema Idd kwa majisifu, huku baba yake anasimamisha gari mbele ya eneo la msikiti, ona kule mbele, alisema Mahadhi akimueleza Idd nae akatazama kule alikoonyesha na baba yake, wote wakamtazama mzee Mahamud ambae alikuwa anaagana na kijana fulani, kisha kila mmoja akaekelekea upande wake, yaani kijana akapotelea mtaani huku Mahamud akielekea kwenye kisima kwaajili ya kuchukuwa udhu, “ameisha pumbavu, unadhani hizo mali utazing’ang'ania peke yako mpaka lini” alisema Mahadhi wakiwa bado ndani ya gari, na wote wakacheka kwa pamoja, huku wakimtazama mzee Mahamud analifikia bomba na kuanza kuchukuwa udhu.******
Sina alipo lifikia gari tu! ghafla mlango wa gari ukafunguliwa, na hapo hapo akashangaa kumuona mwanamke alievalia niqab usoni mwake na kubakiza macho, lakini licha ya hayo lakini Sina aliweza kumkumbuka mschana huyu kuwa ni yule ambae alishirikiana na Idd kumuwekea dawa za kulevya kwenye Juice ili akabakwe, na bahati nzuri alikimbia, Sina mengi aligeuka haraka kutazama alikotoka……….. ITAENDELEA HII NI KWAAJILI YA MASHABIKI WA SIMBAAAA!!!
Tuendelee boss yushatoka ibadani
 
Kumbe...!
Basi kuna haja ya kutafuta stori nyingine ili kukata kiu wakati tunamsubiri Iddi afanye jambo lake:
stori za kijasusi ziko nyingi, zingine waletaji hawajamaliza mpaka kesho
 
Back
Top Bottom