Simulizi: Nyumba Iliyojaa Dhambi

Simulizi: Nyumba Iliyojaa Dhambi

SEHEMU YA 71

Huwa ninajifunza mambo mengi kuhusu mafanikio. Katika kipindi cha nyuma ambacho sikuwa na kitu nilipokuwa nikienda dukani, nilishangaa kuona vitu vikiwa na gharama kubwa mno.

Yaani home theatre inauzwa milioni moja, televisheni milioni mbili, ni gharama sana na mtu unaomba upunguziwe lakini nilipokuwa na pesa, niliona utofauti mkubwa sana.

Kwenye maduka hayohayo, bei hiyohiyo bado unakuwa na hofu kwamba inawezekana vitu hivyo ni feki hivyo unauziwa kwa bei ndogo. Yaani kitu kikiuzwa kwa milioni moja, unahisi ni feki kwa sababu tu una pesa.

Ndivyo ilivyokuwa kwa mademu. Unajua unapokuwa hauna pesa, unachukua demu yeyote yule, awe mbaya, wewe hujali. Tena demu huyo akikwambia naomba elfu kumi, unashtuka, nitampaje elfu kumi, mbona nyingi?

Na wakati kuna watu wanahonga magari.
Sikuacha tabia yangu, niliendelea kubadilisha wasichana kwa sababu ilikuwa moja ya tabia niliyokuwanayo. Esta alionekana kuwa mgumu, hakuingilika kirahisi, nilimwambia sana kwamba nilitaka kuonana naye lakini ilishindikana.

Aliniambia alikuwa bize, eti ana kazi nyingi. Alinichanganya sana na wakati mwingine nilikuwa nakwenda kwao usiku na kuonana naye sehemu fulani hivi, hapo tuliongea, sikuwa na kawaida ya kumtongoza, tangu lini mwenye pesa anatongoza ila kwa huyu Ester, sikuwa na jinsi, nilianza kupiga ndogondogo lakini aligoma kabisa.

Nikasema siyo kesi. Hapo nilipokuwa nikiishi kulikuwa na mshikaji alikuwa jirani yangu, aliitwa Ndimbo. Huyu jamaa alikuwa mchangamfu sana, alipokuwa akiniona naingia na mademu alinishangaa sana, kwake, nilionekana kuwa mtu hatari sana.

Akaanza kujenga mazoea nami, mara salamu na mambo mengine na mwisho tukawa washikaji sana. Alinijua kwamba ugonjwa wangu ni mademu, tena nilikuwa namwambia ukweli, yaani mimi zipite siku mbili bila demu, siku hiyo nitaumwa sana.

“Kwa hiyo?’ aliniuliza.
“Wewe unasoma ama?”
“Ndiyo! Nasoma hapo UDSM.”
“Acha masihara! Nasikia kuna watoto ile kishenzi hapo!” nilimwambia.
 
SEHEMU YA 72

“Kaka pale ni shida. Kama una mtoto wako, acha akasome UDOM na vyuo vingine vya Tanzania lakini si pale, kwanza wajanja lazima wang’oe, yaani utake usitake,” aliniambia.

Alinichanganya sana, alisema hapo kuna mademu wakali ile kishenzi, sikuamini sana ila nilitaka kuhakikisha kwa macho yangu. Siku moja nilimwambia kwamba nataka kwenda huko, kuwaona hao mademu, ni kweli walikuwa wazuri kweli au alinidanganya.

“Hahaha! Usije kuchanganyikiwa tu,” aliniambia huku akicheka.
Na kweli tukaenda, tulipofika huko, nilishangaa sana, macho yangu hayakutulia, ni kweli niliwahi kuona mademu wakali, wenye maumbo ila wale wa pale, duuh walikuwa balaa mno.

Watoto walijua kuvaa, kutembea, kutabasamu, wapo waliokuwa wamejazia lakini pia kulikuw na wale portable, niliwaangalia na kumuuliza ni kwa jinsi gani ningeweza kuwapata kirahisi, kama walikuwa wanahitaji pesa, nilikuwanazo.

“Tufanye house party,” aliniambia.
“Ipo vipi hiyo?” niliuliza, si unajua nilitoka kwenye maisha ya kilofa hivyo hata baadhi ya mambo sikujua kabisa.

“Yaani hiyo tunaandaa party home, kunakuwa na pombe tu, tunazichanganya kwenye ndoo moja na watu wanajichotea tu," aliniambia.

“Halafu?”
“Kunakuwa na muziki, yaani watu wanacheza, wanapiga kelele lakini mwisho wa siku wanalala,” aliniambia.
“Na ukitaka mambo yetu?”

“sasa hapo nani atakunyima? Yaani unakuwa huru, unaweza kusema namtaka huyu, unamchukua, hata wanne kwa usiku mmoja, wewe tu,” aliniambia.

Akazidi kunichanganya mno, unajua mimi mtu akishaniambia kuhusu mademu akili yangu inachanganyikiwa kabisa.

Nilimuuliza jinsi ya kuwapata hao mademu, tena wawe wakali, akasema siyo tatizo, yeye alikuwa na wake na kulikuwa na mshikaji wake ambaye naye alikuwa na mademu, yaani huyo hata ungehitaji mademu ishirini, anakuletea.

Nikamwamia ampigie simu. Ikapigwa na kumuweka loud speaker.
“Oya Juvenile...nataka niandae house party,” alisema Ndimbo, alikuwa akizungumza na huyo jamaa.
“Acha masihara...upo siriazi?’ aliuliza.

“Ndiyo! Pombe zipo za kumwaga, kama vipi tuletee mademu,wapo?” aliuliza.
 
SEHEMU YA 73

“Hahaha! Unanichukuliaje? Nakuletea mademu kama wote! Yaani tukifika hapo, mimi nakuachia mademu wako, nachukua shot zangu nakaa pembeni, nyie endeleeni na mademu,” alisema Juvenile.

“Basi poa, tuletee mademu kama wote!”
“Haina noma. Lini sasa?”
“Kesho si ndiyo Jumamosi, tunafanya kuhusu pombe usijali,” alisema.

“Haina noma. Ngoja niwacheki wachuchu.”
Yaani hakukuwa na siku ambayo nilipagawa kama siku hiyo, akili ikawaka ile kinoma, niliamini kweli nilikuwa napoteza muda wangu kudili na mademu wengine na wakati kulikuwa na mademu wa chuo, tena waliokuwa wakikaa hostel ambao ulikuwa na uwezo wa kuwafanya chochote kile.

Kwa sababu walisema kwamba kwenye shot moja inakuwa na pombe nyingi kali, hivyo nikaamua kuzitafuta pombe kali zaidi. Nilizipata kadhaa zikiwemo Spirytus (hii ni pombe kali kuliko zote duniani, ina ulevi wa 98%) na niliinunua kwa milioni mbili na kikapewa glasi zake.

Ukiachana na hiyo nikanunua Pincer, Balkan, Konyagi, Johnny Walker, Sant Anna na nyingine kisha kuziweka kwenye ndoo moja na kuzichanganya ila zile Spirytus, Pincer na Balkan niliweka vijiko viwili tu kwani zilikuwa kali ile kinoma.

Siku iliyofuata, nikazima simu, sikutaka kuwasiliana na mtu yeyote yule. Sebuleni nikatoa makochi, meza, nilibakiza televisheni na home theatre tu.

Nilinunua vitanda vingine viwili na kuweka katika chumba kingine, yaani siku hiyo nilijua kabisa uchafu ambao ungefanyika, usiku wa manane unaweza kushtukia nyumba imepaa kwa kuwa uchafu umekuwa mwingi mno.

Ilipofika majira ya saa moja, Ndimbo akafika na mademu zake, walikuwa hatari, alinitambulisha, walikuwa wanne, nawakumbuka watatu kwa majina, kulikuwa na Farida, Samiah, Nasra, huyu mwingine jina lake lilikuwa gumu.

Nikawakaribisha, hapo sebuleni walibaki wakishangaa tu, hawakuamini kama kijana mimi nilikuwa naishi maisha ya kishua kama hayo.

“Huyu ndiye bosi mtoto, anaishi hapa na hata demu wala mke,” alisema Ndimbo, basi mimi kichwa hicho.

“Pazuri!” alisema Nasra.
“Nimepapenda, natamani nisitoke,” alidakia Samiah.
 
SEHEMU YA 74

Niliwaangalia tu, baada ya dakika kadhaa Juvenile akapiga simu na kusema yupo njiani, alipofika, akaja, alikuwa ameongozana na mademu nane, wote walikuwa warembo ile balaa, kulikuwa na mademu mpaka wenye asili ya Kiarabu.

“Ndimbo! Mademu zenu hao hapo, shot zangu zipo wapi?” aliuliza hata kabla ya salamu.
“Hizo hapo, ushindwe wewe,” nilimwambia huku mziki ukiwa mkubwa.

Siku hiyo ilikuwa ni party kweli, wasichana wale wakavua nguo zao na kubaki na nguzo za ndani tu na bra.

Nikaona naishi kizembe sana na mimi nikasaula, yaani ilikuwa ni kuyafurahia maisha, ujana kwa sababu hakukuwa na nyakati nyingine za kula maisha kama hizi.
 
SEHEMU YA 75

Sikunywa pombe, mimi si mtumiaji wa hayo mambo, ila nilikuwa nikiwaangalia tu jinsi walivyokuwa wakijiachia.

Nikatoka hapo na kwenda bafuni, nikaanza kuoga, nikiwa najipaka mafuta, nikashtukia mlango ukifunguliwa na msichana mmoja kuingia, alikuwa Juliana.
“Vipi?” niliuliza.

“Na mimi nasikia joto!”
“Ila kuna AC sebuleni!” nilimwambia.
“Bado nilisikia joto!”
Sikusema kitu chochote kile, nikajiongeza kwani nilijua alihitaji nini.

Nashindwa kumtolea maelezo huyu Juliana kwa kuwa wengine watahisi natukana, ila nikisema alikuwa chura najua wote mnajua namaanisha nini.

Basi kama Adolf Hitler alisababisha Vita vya Pili vya Dunia basi leo hii mimi Edward nilisababisha Vita vya Kwanza vya Bafuni manake ilikuwa si mchezo.

Tulioga na kuinjoi kwa dakika arobaini na kuelekea sebuleni, bado macho yangu yalikuwa yakiangalia huku na kule kama popo, bado nilikuwa nalinda, nilikuwa naangalia ni chakula gani kilitakiwa kuliwa muda huo.

Kwa kuwa hata yule Samiah naye alikuwa balaa, nikamsogelea, pombe zilianza kumchukua kwani hata macho yake yalikuwa yamelegea.

“Inakuwaje?” nilimuuliza.
“Unasemaje? Unataka tukalale?” aliuliza kwa sauti kubwa huku akiusogeza mdomo karibu na sikio langu kwani kulikuwa na sauti kubwa ya muziki na tayari ilikuwa ni saa tano usiku.

“Ndiyo! Nataka tukalale na kulaliana...” nilimwambia.
“Subiri kidogo! Leo sisi ni wako,” aliniambia maneno yaliyonitia mzuka na kuona ni lazima nyumba hiyo ibomoke kwani maovu yaliyokuwa yakitarajia kufanyika yalikuwa ni zaidi ya kule kuzimu.

Itaendelea.
 
Huyu Eddo mbona atakufa na ukimwi sasa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom