Simulizi: Nyumba Iliyojaa Dhambi

Du
Sehemu ya 05

Nilimsifia sana mwanamke yule pasipo kujua kama nilikuwa nikikaribisha maumivu moyoni mwangu.

Nilitaka Issa anione kama nilikuwa na bahati kumbe ndiyo nilikuwa nikimpa demu wa kuenjoi naye.

Kila siku ilikuwa kazi yangu kumwambia Issa nimpigie simu mwanamke huyo kumbe upande wa pili naye akaanza kujitengenezea mazingira na kuanza kumtongoza, na sijui msichana huyo alidanganyika na nini, akamkubalia na kukubaliana kulala pamoja, na hilo likatokea.

Sikuwa nikifahamu kipindi hicho, nilimuona Issa kama mshikaji wangu kumbe alikuwa akinizunguka tu. Sikujua kama alikuwa na uhusiano na mwanamke huyo, sikujua kama walionana mpaka kufanya mapenzi.

Baada ya wiki moja akarudi tena. Sikufichi, mpaka muda huo sikujua hata jina lake, ila siku hiyo akaniambia kwamba aliitwa Aisha, nilifurahi sana lakini wakati alipokuja nilipokuwa, nilishangaa sana akimchangamkia mno Issa kuliko hata mimi.

Hilo likaipa wasiwasi, niliumia sana lakini nikapiga moyo konde pasipo kugundua kilichokuwa kikiendelea nyuma ya pazia.

Nilipoona wanazungumza wao tu, nikamchukua Aisha na kuondoka naye.
Alikwenda kulekule kwa siku ile, nilivimba moyoni, wivu ulinijaa, nilitamani nimuulize zaidi kuhusu Issa lakini nikaamua tu kutulia.

“Aisha! Unajua nakupenda sana,” nilimwambia, nilifanya hivyo kwa kuwa nilijua tu kama ningechelewa, Issa angeniwahi.

“Unanipenda mimi?”
“Ndiyo! Ninakupenda Aisha,” nilimwambia!”
“Huniwezi Edward!”

“Kwa nini! Unadhani kwa gitaa dogo siwezi kutumbuiza uwanja wa taifa?” nilimuuliza kwa utani huku nikicheka.

“Utanilisha nini?” aliniuliza swali dogo sana ambalo lilikuwa na maana kubwa.
Nilibaki kimya nikimwangalia, sikutarajia kupata swali kama hilo kutoka kwake.

Ni kweli alikuwa na uhuru wa kuuliza kuhusu majukumu yangu kama mwanaume kwake.

Alikuwa akipendeza sana, hii ilimaanisha kwamba kulikuwa na watu waliokuwa wakifanya kazi hiyo, yaani kulikuwa na mwanaume aliyekuwa akishughulika na mavazi tu, mwingine nauli za usafiri mwingine viatu na mwingine make up, sasa mimi ningeshughulika na nini?

Hata kama angeniambia nishughulike na vocha tu nisingeweza kutokana na kiasi cha pesa kilichokuwa kikihitajika.
 
Safi mwanaume kifuaaaaa
Sehemu ya 06

“Kwani wewe unataka nini?” nilimuuliza ili nijue.
“Matunzo! Mtoto mzuri kama mimi nitunzwe, nitolewe out, niletewe baga, pizza, ice cream, uninunulie pafyumu, ninukie, au hutai demu wako ninukie vizuri?” aliniuliza.

“Nataka! Tena napenda sana.”
“Sasa je! Utaweza kunitunza?” aliniuliza.
Mtu mzima sikujua nimjibu nini, hilo swali lilikuwa kubwa kuliko uwezo wangu.

Nilimwangalia tu, kwa kawaida hata kama huwezi, kwa mwanaume ni MARUFUKU kusema neno siwezi, ni lazima useme unaweza halafu umkimbie.

“Kwa nini nisiweze? Tena umenikumbusha, nataka siku nikuchukue tukale pizza,” nilimwambia.

“Waooo! Lini bebi?”
“Tufanye Ijumaa!” nilimwambia, siku hiyo ilikuwa Jumatatu.

Sikia! Mimi nilikuwa nasikia sana kuhusu pizza ila kiukweli sikuwahi kula hata siku moja. Nilitamani vyakula vinono lakini sikuwa na pesa.

Hebu fikiria, kwa siku napokea elfu tano, halafu hapo pizza inauzwa elfu kumi na mbili mpaka nyingine elfu hamsini, hivi ningeweza kumgharamia yote hiyo? Kwangu ilikuwa vigumu, ila nilimwambia kwamba ningemtoa out kwa sababu tu nilitaka kujitia ubabe mfukoni.

“Basi naisubiri hiyo siku! Zimebaki siku nne, nitakutafuta bebi nikale pizza,” aliniambia kwa tabasamu na kisha kuagana huku moyo wangu ukijisikia burudani sana kwa kuamini kwamba nimeshinda vita kumbe ndiyo kwanza nilikuwa nikiingia kwenye vita na watu waliokuwa na nguvu kuliko mimi.

Je, nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom