Simulizi: Nisamehe Latifa

Simulizi: Nisamehe Latifa

Abdallahking

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2018
Posts
3,985
Reaction score
10,845
0.jpg



SIMULIZI HII IMEKAMILIKA
IMEANDIKWA NA : NYEMO CHILONGANI
CHANZO : BURE SERIES



SEHEMU YA KWANZA


Msichana mrembo mwenye asili ya Kihindi, Nahra Patel alikuwa akilia huku akikimbia kwa kasi kuelekea sehemu kulipokuwa barabara ya lami. Jasho lilimtoka, alikuwa akihema kwa nguvu, japokuwa alionekana kuchoka lakini hakutaka kusimama.
Miguuni mwake hakuwa na viatu na alikimbia katika sehemu zilizokuwa na mibamiba, lakini Nahra hakusimama, aliendelea kusonga mbele, cha ajabu hata miba haikumchoma, na kama ilimchoma, hakusikia maumivu yoyote yale.
Machozi yalitiririka mashavuni mwake, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, hakuamini msichana mrembo kama yeye, aliyesifiwa na wanaume kwamba alikuwa mithili ya malaika, leo hii alikuwa amefukuzwa kama mbwa na mwanaume ambaye kila siku alimuona kuwa ndoto ya maisha yake.
“Deo, mimi? Hapana! Kwa nini? Nimekufanya nini?” aliuliza maswali mfululizo lakini hakupata jibu, wakati huo alikuwa akikaribia barabara ya lami.
Alipofika barabarani, akatulia chini, pembezoni kabisa mwa barabara hiyo na kuanza kulia huku akiwa amekiingiza kichwa chake katikati ya mapaja yake. Machozi yaliendelea kumtoka, kila alipokumbuka namna alivyokimbizwa na mwanaume aliyemchukulia kama mume wake wa baadaye, moyo wake ulimuuma mno.
Hakuwa na sehemu ya kwenda na wala hakuwa na fedha. Wazazi wake hawakutaka kumuona kabisa kwa sababu alikuwa amebeba mimba ya kijana mwenye ngozi nyeusi na wakati yeye alikuwa Mhindi.
Mapenzi yake ya dhati, kung’ang’ania kwake kuwa na Deo ndiyo kulimfanya leo kuwa katika hali hiyo. Hapo barabarani, alikuwa mtu wa kujuta tu, kila alipokumbuka maisha aliyopitia, alibaki akimlaani Deo.
“Ubungo buku...Ubungo buku,” ilisikika sauti ya kondakta wa daladala moja iliyokuwa ikipita mahali hapo.
Nahra akauinua uso wake na kuiangalia daladala iliyosimama mbele yake, akasimama na kuanza kuifuata, alipoifikia akaingia ndani na kuondoka.
Ndani ya daladala, kila mwanaume alikuwa akimwangalia kwa matamanio, alikuwa msichana mrembo wa Kihindi mwenye sifa zote za kuitwa Malkia Cleopatra. Kwa sababu ilikuwa ni usiku na gari halikuwa na taa ndani, hakukuwa na mtu aliyeyaona machozi yake japokuwa uzuri wake ulionekana.
“Unalia nini tena Kajool?” aliuliza mwanaume aliyekaa naye, alimuita jina la muigizaji maarufu wa kike wa filamu za Kihindi, Nahra hakujibu swali hilo, bado kilio cha kwikwi kiliendelea kusikika.
Kuanzia hapo Kibaha mpaka anaingia Dar es Salaam, alikuwa mtu wa kulia tu, kumbukumbu za maisha aliyokuwa akiishi na Deo zilijirudia kama mkanda wa filamu kitu kilichomuumiza na kumliza zaidi.
Mpaka daladala inaingia Ubungo, tayari ilikuwa saa mbili usiku, Nahra akateremka na kusimama kituoni pamoja na watu waliokuwa wakisubiri usafiri.
“Niende wapi?” alijiuliza Nahra, jibu lililokuja ni kwamba alitakiwa kwenda kwa wazazi wake waliokuwa wakiishi Masaki.
Baada ya dakika kumi, akapanda daladala iliyokuwa ikielekea Masaki na safari ya kuelekea nyumbani kwao kuanza. Kama kawaida, bado alikuwa mtu wa kulia tu, kilio chake cha kwikwi hakikuisha, baada ya dakika thelathini, akafika nje ya geti la nyumba yao, akaanza kugonga.
“Nahra, umefuata nini, baba yako ataniua,” aliuliza mlinzi aliyefungua geti, hakuamini kumuona Nahra mahali hapo tena.
“Naomba niingie, nataka kuonana na baba,” alisema Nahra.
“Hapana. Naogopa Nahra. Siku ile alitaka kunipiga risasi, siwezi kukuruhusu,” alisema mlinzi huyo huku akianza kulifunga geti hilo.
“Ninataka kuingia ndani Chichi, niache niingie nikaongee na baba yangu,” alisema Nahra huku akianza kulia tena, akaanza kulisukuma geti ili mlinzi asilifunge.
Msimamo wa mlinzi ulikuwa uleule, hakutaka kumruhusu Nahra kuingia ndani. Baada ya kulazimisha sana tena kwa kusukumana, Nahra akafanikiwa kuingia ndani ya eneo la nyumba yao. Akaanza kuufuata mlango wa kuingilia sebuleni na kuanza kuugonga.
Baada ya dakika tano, mlango ukafunguliwa na wazazi wake wote wawili kutoka ndani. Macho yao yalipotua kwa binti yao aliyekuwa akilia huku akiomba msamaha, baba yake, mzee Patel akabadilika, akakunja uso kwa hasira.
“Umefuata nini hapa? Umefuata nini wewe mbwa?” aliuliza mzee Patel huku akionekana kuwa na hasira kali, Nahra hakujibu kitu, alichokifanya mzee huyo ni kurudi ndani, kama kawaida yake alikuwa ameikumbuka bunduki yake.
Mama yake, bi Aishani alimtaka Nahra aondoke kwani alijua fika mumewe alifuata bunduki lakini Nahra hakutaka kuondoka, alikuwa tayari kupigwa risasi na kufa, ila si kuondoka nyumbani hapo.
Msimamo wa Nahra ulikuwa palepale, hakutaka kuondoka mahali hapo, alikuwa radhi kumuona baba yake akimpiga risasi na kufa lakini si kukubali kirahisi kuondoka nyumbani hapo.
Alikuwa akilia, alijiona kunyanyaswa kwa kile kilichotokea, kitendo cha kutengwa na ndugu zake kisa alikuwa na mimba ya mtu mweusi kilimuumiza mno.
Hakukuwa na mtu aliyemuelewa, hata mama yake, mtu pekee aliyekuwa akimuonyeshea mapenzi ya dhati siku za nyuma, katika suala hilo alikuwa tofauti naye.
Mlango ukafunguliwa, mzee Patel kutoka huku mkononi akiwa na gobole, alichokifanya, huku akionekana kutetemeka kwa hasira, akamnyooshea Nahra gobole lile tayari kwa kumfyatulia risasi.
“Niue tu, we niue baba, ila jua kwamba nilimpenda Deo na nisingeweza kumuacha, kama mnaona nilifanya makosa, wewe niue tu kwani hata wewe utakufa tu,” alisema Nahra, alikuwa amepiga magoti huku akilia kama mtoto.
Bila bi Aishani kulipiga gobole lile, basi risasi iliyotoka ingeweza kumpiga Nahra kifuani. Mdomo wa gobole ukaenda pembeni, risasi ikatoka na kupiga ukutani. Japokuwa mtoto wao alikuwa amefanya makosa yaliyoonekana kuwa makubwa kwa kuzaa na mtu mweusi lakini hakuwa radhi kumuona Nahra akipigwa risasi na kufa.
“Punguza jazba,” alisema bi Aishani huku akimsihi mume wake asimuue Nahra.
“Usinizuie, niache nimuue huyu malaya, ametuzalilisha sana, acha nimuue,” alisema mzee Patel huku akionekana kuwa na hasira mno.
Bado Nahra aling’ang’ania kubaki mahali hapo, hakuwa na pa kwenda usiku huo, kama walivyokuwa wazazi wake, hata ndugu zake wa Kihindi walikuwa wamemtenga, sababu ilikuwa ni ileile ya kuwa na mimba ya mwanaume mweusi.
Mbali na ndugu zake, mwanaume aliyekuwa amempa mimba, Deo alikuwa amemfukuza nyumbani kwake. Hakutaka kuondoka, kama kuuawa, alikuwa tayari kufa lakini si kuondoka nyumbani hapo.
“Chichi, mtoe huyu mbwa mara moja,” alisema mzee Patel, mlinzi akasogea Nahra na kumshika Nahra, akaanza kumbeba juujuu.
Japokuwa hakupendezwa na jambo lile lakini hakuwa na jinsi, alitekeleza amri ya bosi wake kwamba Nahra alitakiwa kutolewa ndani kinguvu.
“Niacheeee, nimesema niacheeee, nimesema sitokiiiiiiiii,” alisema Nahra huku akipiga kelele.
Hiyo wala halikusaidia, Chichi akafanikiwa kumtoa Nahra ndani ya nyumba hiyo. Kwa sababu mvua ilianza kunyesha na ardhi kuanza kulowanishwa na maji, Nahra hakujali, akakaa chini na kuendelea kulia.
Katika maisha yake yote, hicho kilikuwa kipindi kigumu kuliko vyote, hakuamini kama kweli wazazi wake walimfukuza kama mbwa kisa tu alizaa na mwanaume mweusi. Hata kama alikuwa Muhindi, akajikuta akianza kuwachukia Wahindi wote kwa kile alichokuwa amefanyiwa.
“Sitorudi tena nyumbani na sitorudi tena kwa Deo, acha niendelee na maisha yangu,” alisema Nahra na kisha kusimama, akaanza kuondoka.
Alitembea kwa mwendo wa taratibu, mvua kubwa iliendelea kunyesha na kumlowanisha mno lakini hakusimama sehemu kwani nyumba zote za Masaki zilikuwa za kifahari zilizokuwa na uzio mkubwa.
Wakati mwingine alijuta kupewa mimba na Deo kwa kuwa tu jamii yake ilimtenga lakini kuna kipindi aliona kwamba hakutakiwa kujilaumu, kile kilichokuwa kimetokea, kilitokea hivyo alitakiwa kusonga mbele.
Dakika ziliendelea kusonga mbele, mpaka anafika kituoni, tayari ilikuwa ni saa tano usiku, akakaa hapo na kuanza kusubiri daladala japokuwa mkononi hakuwa na fedha yoyote ile. Baada ya dakika thelathini, daladala ndogo (hiace) ikasimama hapo na kupanda.
Safari ya kuelekea Magomeni ikaanza, hakuwa na ndugu yeyote lakini kitu pekee alichokitaka ni kufika huko tu. Mawazo yalimtawala, hakujua ni sehemu gani alitakiwa kwenda kuishi. Huku akifikiria ni wapi alitakiwa kwenda, kichwani mwake likaja jina la mwanaume mmoja, huyu aliitwa Mithun, mwanaume wa Kihindi ambaye alimpenda lakini alimkataa kwa sababu alikuwa na Deo.
“Nitakwenda Kariakoo kwa Mithun, nitamuomba anisaide,” alijisemea Nahra.
Alipofika Magomeni, akadaiwa nauli lakini hakuwa nayo. Kondakta hakuwa mkorofi, kwa muonekano wa Nahra alionekana kuwa na matatizo, akamruhusu kuondoka, safari ya Kariakoo ikaanza huku ikiwa ni saa nne usiku.
Akaanza kutembea kwa miguu, sehemu pekee aliyokuwa akiihofia ilikuwa ni Jangwani tu. Huku akiwa amefika maeneo hayo ya hatari, mbele yake akawaona vijana wawili wakiwa wamesimama, naye akasimama, ila kabla hajafanya kitu chochote, akashtukiwa akipigwa kofi moja zito kwa nyuma.
Wakati anaugulia maumivu, akajikuta akibebwa msobemsobe na kuingizwa vichakani, wanaume wengine wanne waliokuwa na pensi walikuwa wakimsubiri huku wakionekana kuwa na tamaa ya ngono, walitaka kumbaka Nahra. Alijaribu kupiga kelele ili asaidiwe lakini hakukuwa na msaada wowote ule.
Nahra aliendelea kupiga kelele, wanaume wanne waliokuwa wamesimama mbele yake walikuwa wakihangaika kufungua bukta zao huku wakizichana nguo zake. Hakukuwa na mtu yeyote aliyesikia kelele hizo alizokuwa akipiga japokuwa zilitoka kwa sauti ya juu.
“Naanza mimi,” alisema mwanaume mmoja.
“Fastafasta, usinogewe na mtoto wa Kihindi,” alisema jamaa mwingine.
Usiku huo ulikuwa ni usiku wa kuumiza mno maishani mwake, wanaume hao wanne wakaanza kumuingilia kinguvu tena kwa zamu. Alipomaliza huyu, alikuja yule.
Nahra alisikia maumivu makali, kiuno chake kikaanza kukaza, kelele alizokuwa akizipiga, zikaanza kupungua kwani kadiri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo alivyokuwa akiumia zaidi.
Hakuchukua muda mrefu, huku akiendelea kuingiliwa kichakani pale, mbele yake akaanza kuona giza, akajitahidi kuyafumbua macho yake, haikuwezekana, hapohapo akapoteza fahamu huku wanaume wale wakiendelea kumuingilia kama kawaida, tena kwa zamu.

Deo alikuwa kimya chumbani kwake, machozi yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake, hakuamini kile kilichotokea, kumfukuza Nahra nyumbani kwake kilikuwa moja ya vitendo kilichomuuma mno.
Alimpenda Nahra kwa mapenzi ya dhati, hakuwa tayari kumuona msichana huyo akipata shida yoyote ile, japokuwa alikuwa msichana wa Kihindi, kwake haikuwa tatizo, alikuwa akimpenda hivyohivyo.
Wazazi wa Nahra walionekana kuwa tatizo kwake. Mara baada ya kumpa mimba msichana huyo na kuhamia kwake kwa kuwa wazazi wake walimfukuza, wazazi hao wakawatuma wanaume wawili waliokuwa na bunduki, walichokuwa wakikitaka ni kuona Deo akimfukuza Nahra nyumbani hapo, vinginevyo, wangemuua.
Huo ulikuwa mtihani mkubwa maishani mwake, alimpenda Nahra, hakutaka apate tabu yoyote ile, kitendo cha kuambiwa amfukuze msichana huyo kilikuwa kigumu, akakataa.
Watu hao walipoona kwamba kitu hicho hakikufanyika, wakarudi kwa mara ya pili, wakati huu walionekana kuwa na hasira zaidi, kila walipomwangalia Deo usoni, waliyakumbuka maneno ya mzee Patel ambaye aliwaambia wamuue tu.
“Kijana, fanya tunachokwambia. Tumeagizwa tuje kukuua, hatuwezi, tunakuonea huruma. Fanya hivyo, tunakupa siku moja ya ziada, kesho tukija, tunakuja na sura tofauti na hizi,” alisema mwanaume mmoja huku akimwangalia Deo usoni.
Kwa jinsi walivyoonekana, kwa maneno yao yaliyowatoka midomoni mwao ilionyesha kabisa watu hao walimaanisha kile walichokiongea, Deo akakubaliana nao kishingo upande.
Siku hiyo usiku ndiyo ilikuwa siku ya kumfukuza Nahra nyumbani hapo. Alifanya hivyo huku moyo ukimuuma mno, kila alipomwangalia msichana huyo, alijisikia huruma, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali.
“Nahra, naomba unisamehe, sikutaka kukufukuza, wazazi wako ndiyo waliolazimisha kufanya hivi, ninakupenda Nahra,” alisema Deo huku akimuona Nahra akikimbia, machozi yalikuwa yakimmbubujika msichana huyo, baada ya hapo, hakujua Nahra alikimbilia wapi, usiku huo, kwake ukawa usiku wenye mateso mengi.
“Nitamtafuta tu,” alisema Deo huku akijipa uhakika kwamba angeweza kumuona tena Nahra aliyekuwa na mimba yake.
****
Nahra alikuja kupata fahamu asubuhi, alikuwa katika majani yenye unyevuunyevu, mwili wake ulikuwa ukimuwasha. Pamoja na kuwashwa huko, alikuwa akisikia maumivu makali chini ya kitovu.
Akaanza kujiuliza sababu ya yeye kuwa mahali hapo, hakukumbuka kitu chochote kile, alibaki akishangaa mpaka kumbukumbu zilipokaa sawa na kuanza kukumbuka kila kitu kilichotokea usiku uliopita, Nahra akaanza kulia, akajiangalia, sehemu zake za siri zilikuwa zimeharibiwa vibaya, akaendelea kulia mfululizo huku akijiinua kuelekea barabarani.
Kila mtu alibaki akimshangaa, alionekana msichana mrembo mno lakini muonekano wake ulikuwa tofauti kabisa, alikuwa msichana mchafu mno, kwa jinsi uzuri wake ulivyokuwa, hakutakiwa kuwa kama alivyokuwa.
“Hata kama nimechafuka na hata kama nimebakwa, bado ninahitaji kumuona Mithun, ni lazima nimfuate na anisaidie, sina kimbilio jingine zaidi yake,” alisema Nahra.
Kila alipopita, watu walimshangaa, hakuwa akitembea kawaida, alikuwa akichechemea kama mtu aliyekanyaga mwiba. Alitembea hivyohivyo mpaka alipofika maeneo ya Fire ambapo akaunganisha mpaka Mtaa wa Twiga, mtaa uliokuwa na maghorofa mengi, huko ndipo alipokuwa akiishi Mithun.
“Mungu, naomba Mithun anikubalie, anisamehe kwa kila kitu niweze kuwa naye, asahau kila kitu kilichotokea maishani mwetu,” alisema Nahra, tayari alikuwa amefika katika mlango wa nyumba ya kina Mithun, akaanza kugonga mlango, moyo wake ulijawa hofu.
Wala hazikupita dakika nyingi, mlango ukafunguliwa, mtu aliyekuwa akimuhitaji ndiye aliyefungua mlango, alikuwa Mithun.
Mwanaume huyo alibaki akimwangalia Nahra huku uso wake ukiwa kwenye mshangao mkubwa. Hakuamini kama yule aliyesimama mbele yake alikuwa Nahra yule aliyekuwa akimfahamu au alikuwa mtu mwingine.
Alikuwa mchafu mno, nguo zake zilikusanya majanimajani huku zikiwa zimetapakaa tope, kwa kumwangalia tu, Mithun alijisikia kinyaa.
“Nikusaidie nini?” aliuliza Mithun huku akijitahidi kujizuia kupumua kupitia pua yake, maji yaliyokuwa yameilowanisha nguo ya Nahra, yalikuwa yakinuka.
“Naomba unisamehe,” alisema Nahra huku akijitahidi kupiga magoti chini.
Alikuwa akilia kwa maumivu makali, alijua kwamba alifanya makosa kumkataa mwanaume huyo aliyekuwa na lengo la kumuoa na kumkubali Deo aliyekuwa amemfukuza kama mbwa.
Macho yake yalionyesha kila kitu, alikuwa akiomba msamaha lakini Mithun hakujali. Alikumbuka vema kila kitu kilichotokea katika maisha yake ya nyuma na binti huyo.
Alimpenda Nahra na kuahidi kumuoa lakini maamuzi ya msichana huyo yalikuwa kwa Deo, mwanaume mweusi aliyempa mimba na kumtimua.
“Unanuka Nahra,” alisema Mithun maneno yaliyomuumiza mno Nahra, ila kwa kuwa alikuwa na uhitaji, akavumilia.
“Naomba unisamehe Mithun.”
“Nikusamehe ili iweje? Na hicho kitumbo ukipeleke wapi? Nikusamehe wewe? Ulivyonikataa kwa maneno ya dhihaka! Nahisi umepotea njia. Kwanza unanuka sana, hivi ulioga jana?” alisema Mithun na kuuliza kwa dharau.
Kilio cha Nahra kikaongezeka zaidi, hakuamini kama maneno yale yote yalitoka Mithun. Alijitahidi kuomba msamaha lakini matokeo yale aliambulia maneno ya kejeli tu, hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, akaondoka zake huku akilia.
“Nitakwenda wapi mimi? Nitaishi vipi mimi? Bora nikajiue tu, siwezi kuendelea kuishi,” alijisemea Nahra na huku akipiga hatua kuelekea nje ya ghorofa hilo.
Huo ndiyo ulikuwa uamuzi alioufikia, hakutaka kuendelea kuishi tena, mateso na maumivu aliyoyapitia yalitosha kabisa kumfunza, hivyo alitaka kujiua kwa kuamini kwamba angekwenda kupumzika.
Akaanza kukimbia kuelekea Kariakoo Relini huku lengo lake kubwa ni kwenda Mivinjeni. Hakukuwa na kitu alichokifikiria zaidi ya kujiua tu, alitaka kuiondoa roho yake kwa kulala kwenye reli na treni kupita juu yake.
Mara baada ya kufika Kariakoo Relini, akachukua Barabara ya Kilwa na kunyoosha nayo kama alikuwa akienda Bandarini. Alipofika Mivinjeni, akaanza kuelekea katika reli iliyokuwa chini ya daraja ambako kulikuwa na vyumba vingi vya reli ya kati.
“Nitajiua tu,” alijisemea Nahra na kujibanza sehemu huku akisubiria treni ipitie na yeye kulala relini. Aliyachoka maisha yake hiyo ndiyo sababu iliyompelekea kutaka kujiua siku hiyo. Hakutaka kuendelea kuishi na wakati watu wote aliokuwa amewaamini hawakutaka kuishi na yeye.
Moyo wake ulimuuma, hakukuwa na kitu kingine alichokiona kuwa suluhisho la maisha yake zaidi ya kujiua tu. Alidhamiria kufanya hivyo kwa kuamini kwamba asingeweza kuumizwa tena, asingeweza kulia tena, huko atakapokuwa, angeishi maisha matamu milele na kuepuka ghadhabu za dunia hii.
“Pooooooo,” ilisikika honi ya treni ya mizigo, alipoisikia honi hiyo, akachungulia kwa jicho moja kutoka pale ukutani alipojibanza. Treni ile ya mizigo ilikuwa ikija kwa kasi.
Ilikuwa imetoka kituoni na kuanza safari yake, alipoiona treni hiyo kwa mbali, Nahra akasubiri mpaka ikaribie na ndiyo aende kujilaza relini na hatimaye aweze kufa na kuyaepuka mateso aliyokuwa akiyapata.
“Nisamehe Mungu! Mateso yamezidi, acha tu nijiue ili wazazi wangu wapumzike, wasinichukie tena. Pia nisamehe kwa kukiua hiki kiumbe unachokitengeneza tumboni mwangu. Mungu, sifanyi hivi kwa kupenda, najua unayajua maisha ninayopitia,” alisema Nahra huku treni ile ikiendelea kusogea zaidi.
Nahra aliendelea kuisubiria,treni ilibakisha kama hatua mia mbili kabla ya kufika pale alipotaka kujilaza. Kichwa chake kilitawaliwa na mawazo tele, alikuwa tayari kujiua lakini si kuendea kuishi kwa mateso kama aliyokuwa akiishi.
“Bora nife tu, sina haja ya kuendelea kuishi,” alisema Nahra.
Baada ya sekunde kadhaa, treni ilikuwa mbali kama hatua mia moja, alichokifanya Nahra, akakimbilia relini na kujilaza. Machozi yalimbubujika mashavuni mwake, hakuamini kama maisha yake yote aliyokuwa akiishi, mwisho wa siku alikuwa amefikia hatua ya kujiua.
“Nisamehe Mungu, sikupenda kujiua, ila sina jinsi. Acha nife na mwanangu aliyepo tumboni,” alisema Nahra, treni ya mizigo ilikuwa ikija kwa kasi, na ilibakisha hatua arobaini tu za miguu ya binadamu kabla ya kumkanyaga pale relini alipokuwa amelala. Muda wote treni ilikuwa ikipiga honi lakini Nahra hakutoka relini, alidhamiria kujiua kwa kukanyagwa na treni hiyo.
Huku treni ikiwa imebakiza kama hatua thelathini za miguu ya binadamu huku Nahra akiendelea kulala relini pale na macho yake yakiwa yamefumba, ghafla akashtuka akishikwa mikono na kuanza kuvutwa.
Hapo, akayafumbua macho yake kuangalia ni nani aliyekuwa akimvuta. Macho yake yakatua kwa kijana mmoja mchafumchafu, aliyevalia pensi ya jinzi chakavu huku mdomoni mwake akiwa na sigara.
“Toka hapo, njoo huku,” alisema kijana yule huku akimvuta Nahra kutoka katika reli ile.
Kwa kuwa kijana yule alikuwa na nguvu Nahra akajikuta akitolewa katika reli ile na treni kupita kwa kasi kubwa.
“Unataka kujiua?” aliuliza jamaa yule huku akimwangalia Nahra machoni, alikuwa akimshangaa tu.
“Ungeniacha nife, sitaki kuishi, naomba uniache nife,” alisema Nahra huku akilia kama mtoto.
“Hapana. Kwani kuna nini? Mbona msichana mrembo unataka kujiua, hebu nieleze, kuna nini,” alisema kijana yule huku akimwangalia Nahra usoni.
Kwake, Nahra alikuwa msichana mrembo kuliko mwanamke yeyote aliyewahi kumuona machoni mwake, kitendo cha binti huyo kutaka kujiua kilimshtua mno.
Nahra hakusema kitu, alibaki akilia tu. Bado moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, kiu ya kutaka kujiua iliendelea kumkamata moyoni mwake. Lawama zake zote zilikuwa kwa mwanaume huyo aliyemtoa relini, hakujua ni aina gani ya maisha aliyokuwa akiyapitia, hakujua ni jinsi gani moyo wake ulikuwa kwenye chuki kubwa dhidi ya wazazi wake na hata ndugu zake.
“Kuna nini Mhindi wewe?” aliuliza mwanaume yule.
“Nataka kufa.”
“Kwa nini? Umechoka kula ugali?”
“Hapana kaka, nataka kufa tu.”
“Hebu kwanza tutoke hapa, unaweza kuniletea msala,” alisema mwanaume yule na kuanza kuondoka mahali pale.
Wakatoka sehemu ile karibu na reli ile na kwenda juu kulipokuwa na daraja ambapo wakavuka na kuanza kutembea pembezoni mwa Barabara ya Kilwa huku wakielekea Kariakoo Relini.
Nahra alikuwa akilia tu, alikitamani mno kifo kuliko kitu chochote kile, hakuamini kama kweli mwanaume huyo alikuwa amemuokoa na wakati alidhamiri kujiua.
Alikasirika, alimkasirikia kijana huyo. Hakutaka kuzungumza chochote kile, machozi yaliendelea kumbubujika tu mashavuni mwake.
“Nini kinaendelea?” aliuliza mwanaume yule.
Hapo ndipo Nahra alipoanza kusimulia kile kilichokuwa kimetokea maishani mwake tangu alipoanza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Deo, alipopata mimba iliyompelekea kufukuzwa na wazazi wake na hata ndugu zake ambao hawakutaka hata kumuona.
Historia ya maisha yake ilimshtua mwanaume yule aliyejitambulisha kwa jina la Issa, naye akajikuta akianza kuwachukia Wahindi.
“Kwa hiyo hauna pa kuishi?” aliuliza Issa.
“Sina. Sina chochote katika maisha yangu.”
“Basi poa, kama vipi wapotezee tu, twende tukaishi gheto kwangu,” alisema Issa kwa lafudhi za kihuni.
“Unaishi wapi?”
“Tandale Kwa Mtogole.”
“Mmmh!”
“Nini tena?”
“Gari unapandia wapi?”
“Hahah! Hapa hakuna gari, tunakwenda kwa ngondi tu, tunazama hapo mbele, tunaibukia Jangwani, tukizama tena Magomeni, tunaibukia Tandale, dakika tano tu, tupo gheto,” alisema Issa huku akicheka, alikuwa akiongea maneno ya mtaani zaidi.
Kutoka katika maisha ya fedha aliyokuwa akiishi, kutembelea magari, leo hii, kila kitu kilikuwa kimebadilika. Japokuwa Issa alionekana kijana mhuni asiyekuwa na chochote, lakini hakutaka kukataa kwenda kuishi kwake. Hakuwa na kitu, huyo Issa aliyeonekana kuwa mhuni, kwa matatizo aliyokuwa nayo, kwake alionekana kuwa msaada mkubwa. Hivyo akakubaliana naye na kuanza kwenda naye huko Tandale.
****
Alichoka sana, kila wakati alikuwa akipumzika, jua lilimchoma mno huku akitokwa na jasho jingi. Issa hakutaka kujali, bado walikuwa wakiendelea na safari kwa miguu kama kawaida. Alipokuwa akipumzika, Issa alisimama na kumsubiri huku akimtia moyo kwamba ilibakia umbali kidogo kufika Tandale hivyo alitakiwa kuvumilia.
Kwa muonekano tu, Issa alikuwa kijana masikini asiye na kitu chochote cha maana nyumbani kwake. Alionekana kupigwa mno na maisha na kila alipofikiria kama kijana huyo angekuwa msaada mkubwa kwake, moyo wake ukakataa hilo.
Walichukua zaidi ya saa moja na nusu, wakafika Tandale Kwa Mtogole. Chumba kilikuwa shaghalabaghala, hakikuwa na mpangilio, kilionekana kwamba kwa zaidi ya mwezi mzima hakukuwa na usafi wowote uliofanyika.
Nahra akashusha pumzi ndefu, muonekano wa chumba kile uliomchosha mno. Aliyaonea huruma maisha yake, hakuamini kama kuanzia siku hiyo hapo ndipo alipotakiwa kuishi.
“Hapa ndiyo gheto, karibu sana mrembo,” alisema Issa huku akiachia tabasamu pana.
“Mmmh! Kuzuri,” alisema Nahra, harufu mbaya ya chumbani mule, ikaanza kuiumiza pua yake. Hilo wala hakujali sana, alichokuwa akikihitaji, ni sehemu ya kuishi tu.

Kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo moyo wa Deo ulivyozidi kuuma, hakuamini kama tayari msichana aliyempenda kwa moyo wote, Nahra hakuwa mikononi mwake tena.
Moyo wake ulikuwa kwenye majuto makubwa, japokuwa alipewa vitisho vya kuuawa endapo tu asingemfukuza Nahra lakini kumuachia likaonekana kuwa kosa kubwa kwake kwani hata kama angemchukua na kuondoka naye kwenda kuishi sehemu nyingine, aliamini watu hao wasingeweza kumpata.
Hakutaka kukaa nyumbani, alijiona kuwa na uhitaji mkubwa wa kumtafuta msichana huyo aliyeondoka nyumbani kwake usiku wa saa mbili.
Alichokifanya siku hiyo ni kuondoka nyumbani, sehemu ya kwanza ambayo ilimjia kichwani mwake ni kwenda kumuulizia nyumbani kwao, Msasani.Alipofika huko, mtu wa kwanza kabisa kuonana naye alikuwa mlinzi, Chichi.
“Namuulizia Nahra,” alisema Deo huku akionekana kutokuwa sawa.
“Daah! Deo, hata salamu?”
“Nimechanganyikiwa kidogo. Mambo vipi!”
“Poa. Nahra hayupo.”
“Hayupo! Si alikuja hapa jana usiku? Chichi, usinifiche bwana, mimi mweusi mwenzako, naomba uniitie Nahra,” alisema Deo huku akionekana kutokuwa sawa kabisa, alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa.
“Deo, siwezi kukuficha kitu, mbona zamani nilikuwa nakuitia freshi tu. Jana Nahra alikuja hapa home, mdingi wake aliwaka kinoma, akamtimua kama mbwa,” alisema Chichi.
“Unasemaje?”
“Ndiyo hivyo. Mzee katili sana, alimfukuza kama hamjui. Hapa unaweza kuniletea msala, mzee akikuona anaweza kukuua na kunifukuza kazi, kama vipi wewe jiachie tu,” alisema Chichi.
“Sawa. Haina noma, niende wapi sasa? Nikamtafutie wapi?”
“Sijajua. Popote pale wewe nenda tu,” alisema Chichi, akaingia ndani na kufunga geti.
Deo akabaki nje, alichanganyikiwa, hakujua ni wapi alitakiwa kuanzia kumtafuta msichana wake, bado alichanganyikiwa mno na hakujua mahali alipokuwa msichana wake aliyekuwa na ujauzito wake.
Hakuwa na jinsi, kwa sababu alitakiwa kuondoka na hapo nyumbani ndiyo sehemu pekee ambayo aliamini angeweza kumkuta Nahra, akaondoka zake na kurudi nyumbani huku uso wake ukiwa na huzuni mno.
*****

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA PILI

Maisha hayakuwa ya kawaida, kuishi na mtu ambaye hakuwa na malengo yoyote yale zaidi ya kuendekeza pombe na kuishi kwa kuuza vyuma chakavu, yalikuwa maisha magumu mno.
Issa hakuwa mwanaume aliyekuwa akimhitaji, lakini kwa wakati huo, hakuliangalia hilo, aliona ni bora kuishi naye hivyohivyo tu kwani hakuwa na sehemu nyingine ya kwenda, kama kwa mpenzi wake, alifukuzwa, kwa wazazi wake ndiyo kabisa hawakutaka kabisa kumuona, hivyo hapo kwa Issa kulionekana kuwa msaada mkubwa wa maisha yake.
Tofauti na matarajio yake, Issa hakumtaka kimapenzi hata siku moja, kila siku walikuwa wakilala wote lakini hakukuwa na siku aliyokuwa akimgusa kitu kilichomfanya Nahra kufikiria vibaya.
Marafiki wa Issa hawakukauka, uzuri wa Nahra ulikuwa gumzo mtaani, kila wakati, wanaume walifika nyumbani hapo na mtu pekee waliyekuwa wakitaka kumuona alikuwa Nahra tu.
Issa alikuwa mkali kwa kila mwanaume aliyemtaka Nahra, hakutaka mtu yeyote amuingilie msichana huyo na wakati alikuwa kwenye ngome yake. Wapo waliokuwa wakimfuata kwa pesa ili awaunganishie wawe naye lakini vyote hivyo, Issa aliendelea kukataa.
Siku ziliendelea kukatika, miezi ikasonga mbele mpaka tumbo la Nahra kuanza kuonekana. Hapo, Issa aliendelea kuhangaika zaidi, hakutaka kukaa nyumbani, alijitahidi kutoka kwenda mihangaikoni ili kuhakikisha kwamba chakula kinapatikana cha kutosha kwa ajili ya Nahra aliyekuwa mjauzito.
Baada ya miezi tisa kutimia, Nahra akajifungua mtoto mzuri wa kike ambaye alimpa jina la Latifa. Japokuwa alikuwa mtoto mdogo, uzuri wa sura yake haukuweza kujificha, alipokuwa akicheka, akitabasamu na hata kulia, bado uzuri wake ulikuwa palepale.
“Amechukua sura yako, mmmh! Katoto kazuri,” alisema Issa huku akimwangalia Latifa.
“Ahsante.”
“Kwa hiyo ndiyo baba yake alimkataa?”
“Ndiyo.”
“Duuh! Makubwa.”
Kila alipomwangalia mtoto wake, Latifa, Nahra aliumia, mawazo juu ya Deo yakaanza kumtawala. Moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali hakuamini kama mtoto aliyekuwa amezaliwa alikataliwa na mwanaume aliyezaa naye.
Siku zikakatika na mawazo kuzidi kumuumiza. Latifa alipofikisha kipindi cha miezi miwili tu, Nahra akaanza kuvuta sigara na kunywa pombe za kienyeji, hakufanya hayo kwa kuwa alipenda, alijitahidi kuyaondoa mawazo juu ya Deo kwa kuwa mlevi na mvutaji.
Sigara na pombe ya kienyeji, gongo hazikumpenda, ghafla, tena ndani ya miezi mitatu tu, afya yake ikaanza kubadilika, mwili ukaanza kupungua na vipele kuanza kumtoka.
Afya ikazidi kudhoofika zaidi, na mwisho wa siku, akabaki mifupa mitupu, gongo aliyokuwa akiinywa, iliuteketeza mwili wake.
Mwili uliendeea kupungua kila siku, sehemu yake kubwa aliyokuwa akiishi kwa wakati huo ilikuwa klabuni tu. Japokuwa Issa alikuwa mlevi na mvutaji sigara mzuri lakini kwa Nahra alionekana kuwa zaidi yake.
Uzuri wake haukupungua japokuwa mwili wake ulichoka mno kutokana na unywaji wa pombe za asili na uvutaji sigara. Maisha yake yakazidi kupoteza dira, wale waliokuwa wakimfuatilia, hawakumfuatilia tena, walevi aliokuwa akinywa nao klabuni ndiyo waliopata nafasi ya kumchukua na kufanya naye mapenzi.
Kwa sababu hakuwa na fedha, mlevi yeyote yule aliyemsaidia kiasi cha shilingi mia tano kwa ajili ya kununua kikombe kimoja cha gongo, naye alikuwa akimuweka kwenye foleni ya kufanya naye mapenzi usiku ndani ya choo cha klabuni hapo.
Kwa Latifa, hakupokea malezi bora, kila siku aliachwa nyumbani na hata kama ilitokea siku mama yake kumchukua na kwenda naye klabuni, alipolilia maziwa, alipewa kiasi cha pombe kunywa.
“Wewe mwanamke, utamuua huyo mtoto! Unampa gongo!” alisema mlevi mmoja, alikuwa akimwangalia Nahra kwa mshangao.
“Achana na mimi, usifuatilie maisha yangu, fanya kilichokuleta,” alisema Nahra huku akiona kila kitu alichokuwa akikifanya kuwa sawa.
Walevi wengine hawakupenda kuona jambo hilo likiendelea kutokea, walichokifanya ni kumwambia Issa ambaye alionekana kuchukizwa na kitendo hicho na hivyo kumchukua Latifa na kumpeleka kwa dada yake, Semeni aliyekuwa akiishi Manzese Midizini.
Pombe zilizidi kumkolea Nahra, wakati mwingine hakuwa akirudi kabisa nyumbani, pombe zilimkolea na kulala hukohuko klabuni.
Issa alikuwa kwenye wakati mgumu, japokuwa alimchukua mwanamke huyo kwa ajili ya kumsaidia lakini kwa kipindi hicho, kwa kiasi fulani alikuwa akijuta.
Kila siku ilikuwa ni lazima kumfuata Nahra klabuni na kumrudisha nyumbani, japokuwa lilikuwa zoezi gumu kwake lakini hakuwa na jinsi, alifanya kila kinachowezekana kuhakikisha Nahra analala nyumbani kwake.
Mwaka wa kwanza ukakatika, Nahra aliendelea kubaki katika hali ya ulevi mkubwa, na mpaka mwaka wa pili unaingia, tayari alikuwa mnywaji mkubwa kuliko wanywaji wote waliomtangulia.
“Mtoto wangu yupo wapi?” aliuliza Nahra, mwili wake ulikuwa umekonda mno huku ukiwa na vipele vingi.
“Yupo kwa dada yangu. Ameanza shule, usihofu kitu chochote kile,” alijibu Issa.
“Nataka kumuona mtoto wangu,” alisema Nahra kwa staili ya kulalamika.
“Utamuona tu. Usijali.”
“Lini?”
“Wewe unataka lini?”
“Leo.”
“Kwa leo haitawezekana. Tufanye keshokutwa,” alisema Issa.
Siku ziliendelea kukatika, Issa hakutaka kumruhusu Nahra kumuona mtoto wake. Alijua fika kwamba alifanya makosa lakini alijaribu kuepuka matatizo ambayo yangeweza kutokea endapo tu mwanamke huyo angekutana na mtoto wake.
Nahra hakuacha kumuulizia Latifa, kila siku ilikuwa ni lazima amuulize Issa kuhusu mtoto wake na jibu lake lilikuwa lilelile kwamba angekwenda naye Manzese kumuona.
Mwezi wa kwanza ukakatika tangu amuulizie Latifa, mwezi wa pili na wa tatu ikakatika na hatimaye mwaka mzima kukatika. Afya yake iliendelea kuzorota huku vipele vikiendelea kumsumbua mwilini mwake.
“Twende hospitali,” alisema Issa.
“Hapana. Siwezi kwenda.”
“Kwa nini?”
“Naogopa sindano.”
“Hapana. Utakwenda tu.”
Afya ilikuwa yake lakini kwenda hospitali ilikuwa mbinde. Alichokifanya Issa ni kumbeba na kuanza kuondoka naye kinguvu. Muda wote Nahra alikuwa akilalamika kwamba hakutaka kwenda hospitalini lakini Issa hakujali, aliendelea kumbeba mpaka walipofika katika Hospitali ya Halmashauri, Tandale.
“Apelekwe Muhimbili kwa vipimo zaidi,” alisema daktari mwenye sura ya upole na huruma, Dk. Mariamu.
Issa hakuchoka, kwa sababu alikuwa na kiasi fulani cha fedha, akachukua bajaji na safari ya kuelekea Muhimbili kuanza. Walipofika huko, vipimo vikachukuliwa na Nahra kuonekana kuwa na ugonjwa hatari wa UKIMWI.
Hiyo ilikuwa taarifa mbaya kwake, msichana aliyekuwa na mvuto kiasi cha kuwatetemesha wanaume wengi, leo hii alikwisha kabisa na kuambukizwa ugonjwa hatari wa UKIMWI.
Nahra alilia sana lakini kilio chake hakikubadilisha kitu, mtu pekee aliyekuwa akimfariji alikuwa Issa tu.
Siku zikaendelea kukatika, vipele vikaongezeka mwili huku ukiendelea kupungua mpaka kufikia hatua ya kuanza kupata mabakabaka fulani mwisho wa siku nywele zake kuanza kunyonyoka, zote hizo zilikuwa dalili za ugonjwa hatari wa UKIMWI.
Nahra aliendelea kuisha, aliharibika na kila siku alikuwa mgonjwa. Japokuwa kila siku alitamani sana kwenda klabuni kulewa lakini kwa hatua aliyofikia, hakuwa na nguvu za kuweza kusimama. Akawa mtu wa ndani tu.
“Ninakufa Issa, ninataka kumuona mtoto wangu,” alisema Nahra huku akitia huruma kitandani.
Issa hakuwa na cha kufanya, ni kweli kwa muonekano aliokuwa nao alionekana kutokuwa na muda mrefu kuendelea kuishi, alichokifanya ni kwenda kumchukua Latifa na kumletea.
Alikuwa amefanana naye kwa kila kitu kuanzia uzuri na hata ngozi ya mwili. Nahra alibaki akimwangalia mtoto wake tu, machozi yakaanza kumbubujika mashavuni pale alipokumbuka kwamba alikuwa mfu aliye hai.
Huo ukawa muendelezo wa mateso aliyoyapata, mara kwa mara alikuwa akiletewa mtoto wake na kuanza kumwangalia, moyo wake ulimuuma, alikuwa akiyauma meno yake kwa hasira na kuwapa lawama zote wazazi wake na Deo ambao walimfanya kuwa hapo.
Kila kitu kikabadilika, mtu pekee aliyekuwa akiyaangalia maisha yake ya mateso kitandani pale alikuwa Issa tu. Siku zikakatika, mwili wake ulizidi kukonda na vipele kuongezeka, kwa kumwangalia tu, usingebaki kimya, machozi yangekulenga na kusema kwamba Nahra alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakipitia mateso makali.
“Issa, kama nitakufa, naomba umsomeshe mtoto wangu mpaka chuo kikuu,” alisema Nahra huku akionekana kukata tamaa.
“Usijali, nitajitahidi, hata kama nitakosa fedha, nitakopa tu.”
“Issa, nilikwishawahi kukuelekeza nyumbani, si ndiyo?”
“Ndiyo.”
“Utaweza kupakumbuka?”
“Nafikiri nitaweza.”
“Basi hapo ndipo utakapotakiwa kwenda endapo utapata tatizo lolote kuhusu fedha,” alisema Nahra.
“Wataweza kunisaidia kweli?” aliuliza Issa.
“Watakusaidia tu, huyu ni mjukuu wao na si mtoto wao, hana kosa, watakusaidia tu, amini hilo.”
“Sawa, nitajaribu japokuwa sina uhakika, nikipata tatizo, nitakwenda huko, nisipopata, hawatoniona,” alisema Issa ambaye kila alipomwangalia Nahra, moyo wake ulimuuma mno.
Siku hiyo Nahra aliongea kwa shida sana, ilipofika saa saba mchana, mateso aliyokuwa akiyapata kitandani yakaisha na kukata roho. Huo ukawa msiba mkubwa kwa Issa, alibaki akilia sana lakini machozi yake hayakuweza kubadilisha kitu chochote kile, Nahra alifariki kwa Ugonjwa wa UKIMWI.
Alichokifanya Issa ni kuelekea nyumbani kwa kina Nahra, japokuwa alielekezwa juu kwa juu lakini alifanikiwa kufika huko. Mtu wa kwanza kabisa kumpa taarifa za msiba alikuwa mlinzi wa getini, Chichi ambaye aliwapelekea taarifa wazazi wake Nahra.
“Acha afe, tulimwambia azae na mtu mweusi,” alisema mzee Patel, Mhindi aliyekuwa na roho mbaya.
Japokuwa Wahindi wengine walipewa taarifa kuhusu msiba wa Nahra lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyejitokeza kwenda huko, walibaki majumbani mwao wakiendelea kuyafurahia maisha.
Kitendo alichokifanya Nahra cha kukubali kuzaa na mtu mwenye ngozi nyeusi, Deo kiliwachukiza mno, hawakutaka kumuona, hawakumpenda na hata hawakutaka kuufikiria uzao wake, kwao, uzao wa Nahra ukawa ni uzao wenye laana.
Baada ya kila kitu kumalizika na Nahra kuzikwa, Issa akawa na jukumu kubwa na zito la kumlea mtoto Latifa. Kila alipomwangalia, moyo wake ulimuuma mno kwani sura yake ilimkumbusha Nahra.
“Wazazi wa Nahra wana roho mbaya sana, wamemkataa Nahra na uzao wake wote,” Issa alimwambia dada yake, Semeni aliyekuwa na jukumu la kukaa na Latifa.
“Kisa?”
“Kazaa na mtu mwenye ngozi nyeusi, ni hatari sana.”
Latifa alikuwa mtoto mkimya, hakuwa mtoto wa kulialia kama ilivyokuwa kwa baadhi ya watoto. Hakukuwa na shida ya kumlea, kwa Semeni, alimchukulia kama mtoto wake wa kumzaa, huduma zote alizokuwa akiwapa watoto wake wa kuwazaa, alikuwa akimpa Latifa pia.
Mwaka wa kwanza ukakatika na wa pili kuingia, Latifa aliendelea kukua huku uzuri aliokuwa nao ukiendelea kuonekana zaidi, ulipofika mwaka wa pili, watu wakaanza kupigishana kelele kwa kudai kwamba Latifa angeweza kuwa mwanamke mrembo kuliko wanawake wote duniani, uzuri wake ulimdatisha kila mtu.
“Aiseee! Kama malaika!” alisema jamaa mmoja.
“Kwani ushawahi kumuona malaika?” jamaa mwingine akauliza huku akicheka.
“Sijawahi, lakini huyu kama malaika, amini hilo.”
Uzuri wa Latifa ukawa gumzo Manzese nzima, kila aliyekuwa na hamu ya kutaka kumuona mtoto mzuri alikuwa akiambiwa kwenda nyumbani kwa Semeni kumuona Latifa.
Mwaka wa tatu ulipoingia, Latifa akaanzishwa shule ya chekechea. Miongoni mwa watoto waliokuwa wakimya, Latifa alikuwa mmojawapo, hakuwa mzungumzaji kabisa, hakuwa mtundu, alipokuwa akikaa muda huu, hadi muda wa kutoka alikuwa hapohapo.
Mbali na ukimya wake, walimu wakagundua kitu kimoja kwamba Latifa hakuwa mtoto wa kawaida, uwezo wake darasani ulikuwa ni wa juu mno. Yeye ndiye alikuwa mwanafunzi wa kwanza kujua kusoma na kuandika japo kwa mwandiko mbaya.
Uwezo wake huo ukawashangaza walimu wote, hawakuamini kama kungekuwa na mtoto ambaye angeweza kufanya vitu hivyo kwa haraka kama alivyokuwa Latifa.
Hata mitihani ya shuleni hapo ilipokuwa ikija, Latifa alikuwa akiongoza jambo lililowafanya walimu kumpeleka darasa jingine la juu kwani uwezo wake ulikuwa ni wa kitofauti kabisa. Kwa kifupi tungesema Latifa alikuwa genius.

Mpaka anaanza darasa la kwanza, Latifa alikuwa mtoto mwenye uwezo mkubwa darasani, katika kila mtihani, alikuwa akifanya vizuri kitu kilichowashangaza sana walimu kwani hakukuwa na mwanafunzi yeyote aliyewahi kusoma shuleni hapo huku akiwa na akili nyingi kama Latifa.
Mbali na uwezo wake darasani, Latifa alikuwa mtoto mrembo ambaye usingeweza kumwangalia mara moja na kuyaamisha macho yako. Mchanganyiko wake wa rangi ulivichanganya vichwa vya watu wengi kiasi kwamba wengine wakatabiri kuwa angekuwa miongoni mwa wasichana watakaoitikisa Tanzania.
Miaka ilikatika zaidi, mpaka Latifa anaingia kidato cha kwanza katika Shule ya Wasichana ya Jangwani, uzuri wake uliendelea kuwatikisa watu wengi wakiwepo wavulana waliokuwa wakisoma katika Shule ya Wavulana ya Azania.
“Kuna demu nimekutana naye, ni mkali balaa, anasoma hapo Jangwani, aisee huyo demu ni shida,” alisikika mwanafunzi mmoja akiwaambia wenzake.
“Yupo vipi?”
“Muhindi si Muhindi, Mswahilini si Mswahili, ni noma.”
“Hahaha! Utakuwa unamzungumzia Latifa.”
“Latifa! Latifa yupi?”
“Kuna msichana wa kidato cha kwanza, ni mzuri ile mbaya, halafu ana akili kinoma,” alisema mwanafunzi mwingine.
Stori juu ya uzuri wa Latifa ndizo zilizokuwa zikisikika, uzuri wake uliendelea kumdatisha kila aliyemwangalia. Watu wakazidi kuambiana kuhusu Latifa kiasi kwamba binti huyo akaanza kupata umaarufu katika shule hizo mbili.
****
Miongoni mwa wanafunzi waliokuwa wakimpenda Latifa alikuwa Ibrahim Musa, kijana mtanashati aliyekuwa akisoma katika Shule Wavulana ya Azania. Kila siku alipokuwa akisikia stori kuhusu Latifa, Ibrahim alihisi moyo wake ukitetemeka kwa mahaba mazito.
Hisia kali za mapenzi juu ya msichana huyo zikamtawala, kila alipokaa, alimfikiria Latifa na hata katika kipindi cha kuondoka shuleni hapo, hakuwa tayari kuondoka mpaka pale alipomuona msichana huyo.
Kwa mwaka mzima Ibrahim aliendelea kumfuatilia Latifa, hakuwahi kuzungumza naye, alimuogopa, ni mara nyingi alipanga kumfuata lakini kila alipotaka kumsogelea, mapigo yake ya moyo yalidunda mno na hofu kumjaa. Wavulana wengine walimfuata Latifa lakini mwisho hakukuwa na mvulana yeyote aliyekubaliwa.
Kila alipowaangalia wavulana waliomfuata Latifa na kujiangalia yeye, alijiona kutokuwafikia hata mara moja. Hakuwa mvulana tajiri, alitoka katika familia masikini ambayo haikuwa na mbele wala nyuma.
Ibrahim alikuwa kama Latifa, japokuwa alikuwa kijana masikini lakini alikuwa na uwezo mkubwa darasani, katika kila mtihani aliofanya, aliongoza kwa maksi nyingi kiasi kwamba alikuwa gumzo kwa walimu wote.
“Nataka kuwa daktari, ila daktari bila kuwa na mke mrembo haiwezekani, Latifa atanifaa,” alisema Ibrahim.
Moyo wake uliendelea kuumia kila siku, kumfuata Latifa na kumwambia ukweli aliogopa sana. Mwaka mwingine ukaingia na kupita, mwaka wa tatu ulipoingia, Ibrahim akashindwa kuvumilia, hakuwa tayari kujiona akiteseka na wakati kulikuwa na mtu ambaye angeweza kuyatuliza mateso yake ya moyo.
Siku hii alikuwa amejipanga vilivyo, alivalia nadhifu huku akiwa amevipiga kiwi viatu vyake. Aliipanga siku hiyo kuwa maalumu kuzungumza na msichana huyo, kumwambia kila kitu kilichokuwa kikiusibu moyo wake.
Baada ya kufika shuleni, hakutaka kutoka darasani, alivumilia mpaka muda wa kutoka. Kadiri muda ulivyozidi kwenda mbele, mapigo yake ya moyo yakawa yanaongeza kasi ya udundaji, alipenda kuonana na Latifa lakini moyo wake ulijawa hofu kubwa.
Baada ya kengele kutoka, moja kwa moja akaelekea nje ya shule na kusimama barabarani. Macho yake yalikuwa katika geti la shule ile ya wasichana, alikuwa akimsubiria Latifa tu.
“Leo lazima kieleweke, siondoki mpaka nizungumze naye,” alijisemea Ibrahim.
Dakika ziliendelea kusonga mbele huku wanafunzi wakiendelea kutoka, alikuwa kama mtu anayewahesabu wanafunzi hao, mpaka mwanafunzi wa mwisho anatoka ndani ya ndani ya shule, Latifa hakuwepo.
“Mmmh! Hajafika au alipita ila sikumuona?” alijiuliza Ibrahim.
Hakutaka kuvumilia kusimama nje, alichokifanya ni kuelekea ndani ya shule ile na kukutana na walinzi, akaanza kuwauliza kuhusu Latifa, kwa sababu alikuwa maarufu, halikuwa tatizo.
“Hauna habari nini?” aliuliza mlinzi mmoja.
“Habari gani?”
Ibrahim aliyasikia mapigo ya moyo wake yakidunda kwa nguvu, hofu ikamuingia, akajikuta akianza kusali kimoyomoyo mlinzi yule asimpe taarifa mbaya kuhusu Latifa kwa kuamini kwamba moyo wake ungemuuma sana.
“Latifa alipata ajali asubuhi, nimesikia hali yake mbaya sana, aligongwa na gari hapo Jangwani na amepelekwa hospitalini huku akiwa hajitambui. Tetesi zinasema kwamba anatakiwa kusafirishwa kupelekwa India kwa matibabu zaidi,” alisema mlinzi yule, Ibrahim akachanganyikiwa.
“Unasemaje?” aliuliza Ibrahim kwa mshtuko.
“Ndiyo hivyo, yaani leo watu wamemmisi sana, si unajua alivyokuwa mkali,” alisema mlinzi yule.
Ibrahim hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, alihisi kuchanganyikiwa, alichokifanya ni kuanza kutimua mbio kuelekea Muhimbili kumwangalia, alionekana kama chizi, mapenzi yaliuendesha moyo wake vilivyo.
****
Ulisikika mlio mkubwa wa gari, watu wakapiga mayowe, wengine wakashika vichwa vyao, hawakuamini walichokiona, msichana mdogo aliyevalia sare za shule aligongwa na gari, alirushwa juu, akazungushwa, alipotua chini, hakutingisha, akatulia tuli.
Damu zilimtoka mfululizo, shati lake jeupe alilolivaa, ilikuwa vigumu kujua kama lilikuwa jeupe au jekundu, lilitapakaa damu hali iliyoonyesha kwamba msichana huyo alikuwa ameumia vibaya.
Watu waliokuwa pembezoni mwa barabara wakaanza kumfuata, dereva aliyekuwa amemgonga, hakukimbia, akateremka na kumfuata mahali pale alipoangukia. Kila mtu aliyemuona msichana huyo, alishika kinywa chake kwa mshtuko, kwa muonekano, msichana yule alionekana kufariki dunia palepale.
Kilichofanyika ni kumbeba na kumpeleka katika gari lile lililomgonga na safari ya kuelekea katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kuanza. Hakukuwa na mtu yeyote aliyegundua kwamba msichana aliyegongwa alikuwa Latifa, uso wake ulijaa damu huku akiwa ameumia vibaya kichwani.
“Mungu wangu! Huyu atakuwa amekufa,” alisema jamaa mmoja huku yeye na wenzake wakiwa garini kumpeleka Latifa hospitali.
Alipofikishwa hospitalini, akachukuliwa na kupelekwa katika chumba kilichoandikwa Theatre mlangoni, yaani chumba cha upasuaji. Kitu cha kwanza alichofanyiwa ni kuwekewa mashine ya hewa safi.
“Inatupasa tufanye kitu vinginevyo anaweza kufariki,” alisema daktari mmoja, bingwa wa upasuaji hospitalini hapo, Dk. Lyaruu.
“Kitu gani?”
“Mapigo yake ya moyo yapo chini, nipe CPR,” alisema Dk. Lyaruu.
Hapohapo mashine ya kushtulia mapigo ya moyo, Cardiopulmonary Resuscitation (CPR) ikaletwa na moja kwa moja kuanza kuyashtua mapigo ya moyo ya Latifa ambayo yalikuwa chini mno.
Kila kitu kilichofanyika mahali hapo, kilifanyika kwa harakaharaka, baada ya kuona kwamba mapigo yake ya moyo yanaanza kurudi katika hali yake, wakamtundika dripu na kuanza kuisikilizia hali yake.
Tayari wanafunzi walikwishaanza kukusanyika hospitalini hapo, kila mmoja alipatwa na mshtuko, taarifa waliyokuwa wameisikia kwamba mwanafunzi mwenzao aliyekuwa akisifika kwa urembo shuleni, Latifa alikuwa amepata ajali mbaya ya gari iliwashtua mno.
Hali iliyokuwa ikiendelea hospitalini hapo ilizidi kuwatia hofu wanafunzi kiasi kwamba kila mmoja akabaki akisali kimoyomoyo ili Mungu atende muujiza na hatimaye aweze kurudi katika hali yake ya kawaida.
“Ubongo wake umetikisika, hili ni tatizo kubwa, hebu subirini, muandaeni, nitarudi sasa hivi kuanza naye,” alisema Dk. Lyaruu.
Dk. Lyaruu akatoka ndani ya chumba hicho na baada ya dakika chache, alikuwa kwenye chumba kikubwa kilichokuwa kikitumika kwa kufanyia mikutano au vikao vya dharura.
Jopo la madaktari wanne likakutana, wote walikuwa mahali hapo kwa ajili ya kuizungumzia hali aliyokuwa nayo Latifa. Baada ya kufanyiwa uchunguzi, ripoti zikawekwa mezani na kuanza kujadiliwa.
“Ni ajali mbaya, ripoti zinaonyesha kwamba ubongo wake umetikisika na damu kuvilia kichwani, kuna vitu vinne vinaweza kutokea kama tusipofanya kitu fulani,” alisema Dk. Lyaruu na kuendelea:
“Kitu cha kwanza mgonjwa anaweza kupatwa na kichaa, hii ni hatari sana kwa afya yake,kitu cha pili mgonjwa anaweza kupoteza kumbukumbu zake jambo ambalo na jambo la tatu, mgonjwa anaweza kupata kifafa, lakini mbaya zaidi, anaweza kufariki,” alisema Dk. Lyaruu, madaktari wote walikuwa kimya wakimsikiliza.
Ilikuwa ni taarifa mbaya wasiyoitegemea, msichana mdogo ambaye alipata ajali na kuletwa hospitalini hapo alipatwa na tatizo kubwa lililoashiria kifo chake endapo tu asingeweza kutibiwa kwa ufasaha na kwa haraka.
Alikuwa msichana mdogo mno kupata mateso kama yale aliyoyapata. Msichana mrembo, mwenye akili nyingi, leo hii alipata ajali mbaya na kuufanya ubongo wake kutikisika.
“Kwa hiyo ili tuyaokoa maisha yake, ni lazima tulifungue fuvu lake, tuitoe damu hiyo, kama tutashindwa, haina budi kumsafirisha kuelekea nchini India,” alisema Dk Lyaruu, kila mmoja ndani ya chumba kile akashusha pumzi ndefu.
Kikao hicho cha dharura kikafungwa na kila mtu kuondoka katika chumba hicho. Vichwa vyao vilifikiria ni kitu gani kilitakiwa kufanyika ili Latifa aweze kupona na kurudi katika hali ya kawaida.
Hawakutaka kumuona akichanganyikiwa au kumbukumbu zake kufutika, hawakutaka kumuona akipatwa na ugonjwa wa kifafa, la zaidi, hawakutaka kumuona akifariki dunia, walitaka kumtibu na mwisho wa siku awe kama alivyokuwa kabla.
“Dokta, nini kinaendelea?” aliuliza mwanamke mmoja, alikuwa yule dereva aliyemgonga Latifa kwa gari.
“Subirini kwanza, kuna kitu kinatakiwa kufanyika,” alijibu Dk. Lyaruu huku akiwa na haraka.
“Nipo radhi kutoa kitu chochote kile, ninahitaji huyu mtoto apone, naomba mumsaidie,” alisema mwanamke yule huku akianza kububujikwa na machozi.
Alionekana kuchanganyikiwa, kitendo cha kumgonga Latifa kwa gari kilimchanganya. Kila alipokaa, hakutulia, alisimama na kuzunguka huku na kule, alionekana kama chizi.
Sehemu hiyo ya kusubiria kuwaona wagonjwa hakuwa peke yake, zaidi ya wanafunzi kumi walikuwepo mahali hapo huku kila mmoja akitaka kumuona Latifa, ambaye alikubalika, leo hii alikuwa hospitalini huku akiwa hajitambui.
Baada ya dakika ishirini, madaktari watatu na manesi wanne wakaingia ndani ya chumba cha upasuaji. Walipofika, kitu cha kwanza wakashikana mikono kwa kumzunguka Latifa na kuanza kumuomba Mungu kwa dini zao ili aweze kuwasaidia katika upasuaji uliokuwa unakwenda kufanyika ndani ya chumba hicho.
Kitu cha kwanza walichokifanya ni kumuingiza katika mashine kubwa iliyokuwa na kipimo kiitwacho Magnetic Resonance Imaging (MRI). Hicho kilikuwa kipimo maalumu ambacho hutumika katika kuangalia ni sehemu gani ya ubongo wa mwanadamu iliyokuwa imepata tatizo fulani.
Hiyo ndiyo ilikuwa hatua ya kwanza kabisa ambayo walitakiwa kuichukua ndani ya mashine ile. Kikamera kidogo ambacho kiliunganishwa na kompyuta iliyokuwa chumbani mule ikaanza kuchukua kile kilichokuwa kikiendelea.
Kila daktari akashtuka, hawakuamini kama donge kubwa la damu ambalo lilivilia ndani ya ubongo wa Latifa lilikuwa kubwa kiasi kile. Japokuwa waliwahi kupokea wagonjwa wengi wa tatizo kama lile lakini hawakuwahi kumpata mgonjwa aliyekuwa na donge kubwa la damu kama ilivyokuwa kwa Latifa.
“Hapa kazi ipo, sidhani kama itawezekana,” alisema Dk. Pius, alikuwa mtaalamu mwingine wa upasuaji hospitalini hapo.
“Ooppss…! Sikujua kama damu inaweza kuwepo kwa wingi kiasi hiki. Hili ni tatizo kubwa, inatakiwa ahamishwe haraka kwenda kwa wataalamu zaidi, vinginevyo, anaweza kufariki,” alisema Dk. Lyaruu.
Hospitali ambayo ilikuwa vichwani mwao kwa haraka sana ni Ganga Medical Center iliyokuwa nchini India, huko ndipo alipotakiwa kupelekwa kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji ambao ungegharimu dola elfu kumi, zaidi ya shilingi milioni ishirini.
“Ni fedha nyingi, atazipata vipi?” aliuliza Dk. Lyaruu.
“Labda tukazungumze na yule mwanamke aliyemgonga, tukishindwa, tuwaruhusu waandishi wa habari wa Gazeti la Uwazi waitoe taarifa yake gazetini, naamini ataweza kupata kitu chochote kile,” alisema Dk. Pius.
Walichokifanya ni kumfuata mwanamke yule ambaye muda wote alikuwa mtu wa kulia tu. Walipomwambia kwamba Latifa alitakiwa kusafirishwa nchini India kwa ajili ya matibabu, akakubaliana nao kulipia kila kitu, si milioni ishirini tu, hata ingekuwa mia moja, alikuwa radhi kufanya hivyo.
Mawasiliano na Hospitali ya Ganga yakaanza kufanyika. Mtoto mwenye sura nzuri, aliyekuwa na akili darasani, aliyetoka katika familia ya kimasikini ambapo mama yake alifariki kwa ugonjwa wa UKIMWI, alihitaji kupelekwa nchini India kwa ajili ya matibabu ya kuondoa donge kubwa la damu ubongoni mwake, kila kilichokuwa kikiendelea, Latifa alikuwa kwenye usingizi wa kifo, hakufahamu chochote kile.


Mawasiliano baina ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Hospitali ya Ganga ya nchini India yakafanyika na siku mbili baadaye, Latifa, Issa, yule mwanamke aliyemgonga, bi Rachel walikuwa ndani ya ndege ya Shirika la Ndege la Indians Airlines wakielekea nchini India.
Kama kulia, bi Rachel alilia sana lakini haikusaidia kumuinua Latifa kitandani pale, bado alikuwa amepoteza fahamu, yaani toka alipomgonga kwa gari, hakuwa amerudiwa na fahamu mpaka siku hiyo.
Safari nzima ya kutoka nchini Tanzania kuelekea India, Latifa alikuwa akipumulia kwa msaada wa mashine ya hewa safi. Kama aliyokuwa amelazwa nchini Tanzania, alikuwa vilevile mpaka walivyokuwa wakiingia nchini India.
Gari la wagonjwa kutoka Ganga Medical Center lilikuwepo uwanjani hapo na baadhi ya madaktari waliokuja kumpokea Latifa aliyekuwa hajitambui. Mara baada ya ndege kusimama na abiria wote kuteremka, naye Latifa akateremshwa huku akiwa juu ya machela, wakamuingiza ndani ya gari na kuondoka naye.
Walichukua dakika ishirini njiani, wakafika katika hospitali hiyo ambapo moja kwa moja machela ikateremshwa na kuanza kusukumwa ndani ya hospitali hiyo kwa ajili ya kuanza kazi ya upasuaji ambayo ingewachukua kwa zaidi ya mwezi mzima mpaka kuhakikisha kwamba Latifa amekuwa katika hali nzuri.
Kabla ya kitu chochote kuanza, madaktari mabingwa wa upasuaji wakakutana katika chumba maalumu na kuanza kufanya mkutano wa dharura. Zaidi ya madaktari saba walikuwa ndani ya chumba hicho, ripoti kutoka nchini Tanzania katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikawekwa mezani na kuanza kuijadili.
Kikao hicho kilichukua saa moja, kikamalizika na kugundua kwamba Latifa alikuwa amepata tatizo ambalo kitaalamu huitwa Subdural Haematoma, tatizo ambalo husababishwa na mkusanyiko mkubwa wa damu katika ubongo.
Baada ya kila kitu kuwa sawa, mara moja oparesheni ikaanza kufanyika ndani ya chumba kile. Mlango ulikuwa umefungwa, ukimya ulitawala ndani ya chumba kile, upasuaji ule haukuwa mdogo, sehemu ndogo ya utosini ikachanwa na kisu kikali na kuanza kuangalia ndani.
Ilionekana kuwa kazi kubwa, madaktari walikuwa wametulia wakiifanya kazi hiyo kwa umakini mkubwa mno. Walichukua saa nane, upasuaji ukakamilika, wakaziba sehemu waliyoiachana huku donge lile la damu likiwa limetolewa.
“What is going on? What about operation? Is it successful done? We want to see her,” (Nini kinaendelea? Upasuaji ulikuwaje? Ulifanyika kwa mafanikio? Tunataka kumuona) alisema bi Rachel huku akionekana kuwa na wasiwasi.
“It is successful done, you have to wait for twelve hours, you can go now and be back tomorrow” (Imefanyika kwa mafanikio, mnatakiwa kusubiri kwa masaa kumi na mbili, mnaweza kuondoka na kurudi kesho) alisema daktari aliyetoka katika chumba cha upasuaji ambaye koti lake kubwa lilikuwa na kichuma kilichoandikwa Dr. Patesh Munil.
Hawakuwa na jinsi, walichokifanya ni kuondoka hospitalini hapo huku ikiwa tayari imetimia saa 2:17 usiku. Kila mmoja alikuwa na mawazo, mioyoni mwao walikuwa wakiendelea kumuombea Latifa aweze kurudi katika hali yake ya kawaida.
“Mungu naomba umponye!” alisema bi Rachel huku akiwa amepiga magoti chumbani kwake, tayari mashavu yake yalilowanishwa na machozi yaliyokuwa yakimtoka.
Siku iliyofuata, asubuhi na mapema walikuwa hospitalini hapo. Walitulia katika viti vya watu wanaosubiria wagonjwa, alipotokea Dk. Munil na kuwaona, akawataka kumfuata ambapo akaenda nao mpaka katika chumba kile alicholazwa Latifa.
Kama alivyoletwa ndivyo alivyokuwa kitandani pale, kila mmoja akashindwa kuvumilia, machozi yakaanza kuwabubujika mashavuni mwao kwani picha waliyokuwa wakiiona iliwaumiza mno.
Latifa, binti mrembo na mwenye akili, kichwa chake kilifungwa bandeji huku puani akiwa na mashine iliyomsaidia kupumua.
Hayo ndiyo yalikuwa maisha waliyokuwa wakiishi, kila siku ilikuwa ni lazima wafike hospitalini hapo kwa ajili ya kumjulia hali msichana huyo. Siku ya kwanza ikakatika, siku ya pili ikaingia na kukatika, mpaka wiki inamalizika, bado Latifa hakuwa amefumbua macho.
“Atakufa?” aliuliza bi Rachel.
“Hapana, hawezi kufa, Mungu wetu ni mkuu, atamponya tu,” alisema Dr. Munil ambaye alionekana kuwa na imani kubwa.
****
Bado Latifa aliendelea kuwa kitandani hapo, kila siku ukimya ulikuwa sehemu ya maisha yake, hakuwa akizungumza kitu chochote kile na hata kula alikuwa akila kwa kutumia mipira maalumu ambayo iliunganishwa puani mwake.
Kila siku ilikuwa ni huzuni kwao, kwa bi Rachel, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali mno, kila siku alikuwa akimuomba Mungu aweze kumponya binti huyo ili moyo wake urudi kwenye amani kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.
Wiki zikakatika na hatimaye mwezi wa kwanza kumalizika, bado Latifa aliendelea kuwa kitandani pale. Mwezi mwingine ulipoingia, kidogo kwake ikaonekana kuwa nafuu, akaanza kwa kukunja vidole vya mikono yake, manesi waliokuwa ndani ya chumba hicho hawakutaka kubaki humo, wakatoka kwa kasi kumfuata Dk. Munil na kumwambia kile kilichokuwa kimeendelea chumbani.
“Kuna nini?” aliuliza Dk. Munil.
“Dokta, dokta, mgonjwa ameanza kukunja vidole vyake,” alisema nesi mmoja huku akihema kama mtu aliyekimbia umbali mrefu.
“Mgonjwa gani?”
“Latifa.”
Dk. Munil hakutaka kubaki ofisini kwake, kwa kasi ya ajabu akachomoka na kuanza kuelekea katika chumba alichokuwemo Latifa. Hakutaka kuamini, mgonjwa huyo alikuwa amekaa kitandani kwa muda wa mwezi mzima bila kutingisha kiungo chochote kile, alivyoambiwa kwamba alikuwa akikunja vidole vyake, alitaka kuhakikisha hilo.
“Kuna nini?” aliuliza bi Rachel ambaye alikuwa nje ya chumba kile.
“Subirini.”
“Kwa nini tusubiri? Manesi walitoka wakikimbia, wewe unatuambia tusubiri! Kuna nini?” aliuliza bi Rachel huku Issa akiwa pembeni akimsikiliza.
Dk. Munil hakutaka kujibu swali hilo, akaingia ndani kwa ajili ya kujihakikishia kwa macho yake. Alipofika ndani ya chumba hicho, moja kwa moja macho yake yakatua kwa Latifa aliyekuwa kitandani, akayapeleka macho yake katika vidole vyake, kwa mbali vilikuwa vikitikisika.
“Amepona,” alijikuta akisema Dk. Munil huku akipiga magoti chini na kumshukuru Mungu.
Alichokifanya Dk. Munil ni kumuita bi Rachel na Issa ndani ya ofisi yake na kuanza kuwaambia kile kilichokuwa kimetokea ambacho kwao kilionekana kama muujiza mkubwa.
Kila mmoja alijikuta akimshukuru Mungu kwa matendo makuu aliyoyafanya. Baada ya siku mbili, Latifa akaanza kufumbua macho yake na baada ya siku chache mbele, akaanza kuongea japo kwa sauti ya chini kabisa.
“Hakupata tatizo lolote?” aliuliza bi Rachel.
“Hakupata. Tulitegemea angeweza kusahau kila kitu lakini haikuwa hivyo, tukahisi kwamba angeweza kupata ukichaa lakini haikuwa hivyo pia, ni mzima wa afya, hili ni jambo la kumshukuru Mungu sana,” alisema Dk. Munil.
“Kwa hiyo ni lini hali yake inaweza kutengemaa kabisa?”
“Hivi karibuni, nadhani baada ya mwezimmoja.”
“Tunashukuru sana.”
Waliendelea kusubiria hospitalini hapo huku kila mmoja akitaka kuona Latifa akirudi katika hali yake kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma. Kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo hali yake iliendelea kuwa nzuri na baada ya mwezi mmoja iliyosemwa, akaanza kuongea kama kawaida.
“Ilikuwaje?”
“Ulipata ajali.”
“Mungu wangu!”
“Ila tunashukuru Mungu umepona.”
“Kwa hiyo hapa nipo hospitali gani? Agha Khan? Mbona Wahindi wengi?”
“Hapana. Hapa upo India.”
“Mmmh! Na wewe nani?” alimuuliza bi Rachel.
Hakutaka kuficha, moyo wake ulikuwa ukimsuta kila alipotaka kukaa kimya. Hapo ndipo alipoamua kumwambia Latifa ukweli juu ya kila kitu kilichokuwa kimetokea, hakutaka kuficha kitu chochote kile, aliamua kumwambia ukweli kwani tayari mtu huyo alikuwa amepona.
Moyo wa bi Rachel ukaanza kumpenda Latifa. Katika maisha yake yote, alikuwa amepata mtoto mmoja tu ambaye kwa wakati huo alikuwa nchini Marekani akisoma. Jina la mtoto huyo aliitwa Dorcas.
Mara baada ya kumzaa mtoto huyo, kwa bahati mbaya bi Rachel akapata ajali mbaya ya gari akiwa na mume wake. Mume wake, bwana Michael Mshana akafariki palepale huku yeye akiharibika kizazi chake na kutokuweza kubeba mimba tena.
Akaishia kuwa na mtoto mmoja tu, hakupata mwingine tena, huyo ndiye mtoto aliyekuwa akimpenda. Kitendo cha kuwa karibu na Latifa kikamfanya kutamani kuendelea kuishi na msichana huyo, hakujua Latifa alikuwa nani, hakujua kama ana wazazi wake au la, kitu alichokitaka ni kuishi naye tu.
“Nitamuomba niishi naye, nimsomeshe, nitatumia hata utajiri wangu wote ili mradi afike pale ninapotaka afike. Halafu nilisikia wakisema kwamba yeye ni genius, kama ni kweli, nitampeleka Marekani katika shule ya watoto wenye vipaji akasome, nadhani huko maisha yake yatabadilika,” alijisema bi Rachel, kila alipomwangalia Latifa, alijisikia furaha moyoni mwake. Kuhusu fedha, kwake hakuwa na tatizo lolote lile.

ITAENDELEA

CHANZO : BURE SERIES
 
SEHEMU YA TATU

Waliendelea kubaki nchini India mpaka pale Latifa aliporuhusiwa tayari kwa kurudi nyumbani. Hakuwa amepata tatizo lolote lile ambalo lingemfanya kuwa na ugonjwa wowote ule, iwe kifafa, kusahau au kupoteza maisha.
Alipohadithiwa kile kilichotokea, alibaki akilia huku akimshukuru bi Rachel kwa msaada aliompa. Waliendelea kukaa nchini India kwa wiki kadhaa na ndipo waliporudi nchini Tanzania.
“Ninataka kuishi na Latifa,” alisema bi Rachel, alikuwa akimwambia Issa.
“Haiwezekani, bado tunahitaji kukaa naye zaidi, akikuakua, tutakuruhusu uje kumchukua,” alisema Issa.
“Na mama yake yupo wapi?”
“Ni stori ndefu sana, kuna siku utajua, kitu cha msingi, acha tuendelee kukaa naye hapa, ukitaka kumuona, usihofu chochote kile, unakaribishwa sana,” alisema Issa.
Tayari kwa mtazamo wa haraka-haraka Issa aligundua kwamba Latifa alikuwa fedha, hakutaka kumruhusu kuondoka naye kwani alijua kwamba endapo bi Rachel angeamua kumchukua basi asingeweza kuwasaidia.
Mwanamke huyo alikuwa tajiri, alikuwa na kiasi kikubwa cha fedha, alimiliki vituo vya mafuta, super market na biashara nyingine zilizomuingizia fedha kila siku. Maisha yake yalitawaliwa na fedha, hakuwa na shida, aliishi maisha aliyotaka kuishi siku zote.
Alichokifanya bi Rachel ni kubadilisha maisha ya Issa, dada yake, Semeni na Latifa pia. Mara kwa mara aliwatumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kuwaendeleza katika maisha yao ya kila siku. Baada ya kuhakikisha kila kitu kimekaa sawa, akamhamisha Latifa katika Shule ya Jangwani na kumpeleka katika Shule ya St. Antony iliyokuwa Mbezi Beach.
Hakutaka msichana huyo apate tabu yoyote ile, alitaka kumsomesha mpaka atakapofikia levo ya juu kabisa kielimu. Shuleni huko, Latifa alionekana kuwa mwiba, uzuri wake ulimpagawisha kila mvulana aliyemwangalia, wasichana wenzake waliovuma kwa uzuri shuleni hapo wakaanzisha bifu na yeye, waliuogopa uzuri wake kwa kudhani kwamba angeweza kuwachukulia wavulana wao.
“Ninamchukia huyu kinyago, simpendi kweli, sijui kwa nini amehamia hapa,” alisema msichana mmoja, aliitwa Theresa, alikuwa miongoni mwa wasichana waliotesa wanaume kwa uzuri shuleni hapo.
“Achana naye shoga, asikuumize kichwa, hakuna atakayeweza kutuchukulia watu wetu,” alisema msichana mwingine.
Uzuri wa Latifa haukuishia hapo bali ulikuwa mpaka darasani, hakukuwa na mwanafunzi aliyemfikia kwa uwezo mkubwa aliokuwa nao. Japokuwa wasichana wengi warembo darasani hawakuwa na makali lakini kwa Latifa hali ilionekana kuwa tofauti kabisa.
Walimu walibaki wakishangaa, hawakuweza kuamini kama kulikuwa na mtu aliyekuwa na akili nyingi kama alivyokuwa Latifa. Katika masomo yake yote shuleni hapo, alipata alama ya A kitu kilichomfanya kuwa mwanafunzi wa kwanza katika shule hiyo kufaulu kwa kiwango hicho kikubwa.
“Hapa ni kusoma tu, mapenzi baadaye,” alisema Latifa kila alipofuatwa na wavulana, kwake, masomo yalikuwa chaguo la kwanza.
****
Ibrahim alikuwa kwenye wakati mgumu, muda mwingi alikuwa mtu wa mawazo, hakuamini kama kweli msichana aliyempenda alipata ajali na hivyo kipindi hicho alikuwa hoi kitandani huku akiwa hajitambui.
Mara kwa mara alikuwa akielekea Muhimbili kwa ajili ya kumuona lakini hakuwa akipata nafasi, na hata kama alikuwa akipata pamoja na wanafunzi wenzake, muda uliotolewa aliuona kuwa mfupi mno.
Ibrahim alimpenda Latifa, alihitaji kumuona akiamkakutoka katika usingizi wa kifo na hatimaye kuzungumza naye na kumwambia jinsi gani alimpenda na kumuhitaji. Hakuwa na nafasi hiyo tena, kipindi hicho, msichana huyo alionekana kama mfu kitandani.
Siku kadhaa zikapita, akasikia kwamba msichana huyo alikuwa amepelekwa nchini India kwa ajili ya matibabu. Moyo wake ukanyong’onyea mno, akakosa nguvu lakini pamoja na hayo, akajiahidi kwamba asingeweza kumsaliti japokuwa hakuwahi kuzungumza naye.
Ilipopita miezi miwili, akapewa taarifa mbili, moja ilimfurahisha lakini nyingine ilimhuzunisha. Yenye kufurahisha ilisema kwamba Latifa alikuwa amerudi nchini Tanzania lakini ile yenye kuhuzunisha ilisema msichana huyo alikuwa akihamishwa shule na kwenda kusoma shule moja ya watoto wa matajiri.
Taarifa hiyo mbaya ikawa kama msumali wa moto moyoni mwake, alishindwa kufahamu ni kwa sababu gani lilikuwa jambo gumu kwake kuonana na msichana huyo, baada ya wiki mbili, akaambiwa kwamba msichana huyo alianza masomo katika Shule ya St. Antony iliyokuwa Mbezi Beach.
“Nitamfuata hukohuko tu,” alijisema Ibrahim.
Hakutaka kuendelea kubaki katika moyo wa kipweke. Baada ya siku kadhaa akaamua kwenda shuleni huko kwa ajili ya kumuona msichana huyo. Alipofika katika geti la shule hilo, akaomba kuonana na Latifa, akakataliwa na mlinzi aliyekutana naye getini.
“Hii siyo shule ya uswahilini, huku uzunguni, hebu nenda huko uswahili ukaulizie kiuswahili-uswahili kama ulivyouliza, hapa ukija, unatoa taarifa kwa njia ya simu kwanza,” alisema mlinzi huyo kwa kebehi kwani kila alipomwangalia Ibrahim, alionekana kuwa na maisha mabovu.
****
Makali ya Latifa darasani hayakupungua, kwenye kila mtihani alionyesha kwamba uwezo wake ulikuwa wa juu mno, aliwaongoza wanafunzi wote kiasi kwamba wengi wakaanza kuanzisha bifu naye.
Wavulana walioendelea kumfuata, mmoja wao aliitwa Maliki Abdullahman. Alikuwa kijana mtanashati mwenye asili ya Kiarabu aliyetoka katika familia ya kitajiri, sura yake ilikuwa ya mvuto iliyowachengua wasichana wengi waliokuwa wakikutana naye barabarani.
Maliki alikuwa gumzo kila kona, wasichana walimsumbua kila siku lakini hakutaka kuwa na msichana hata mmoja. Darasani, uwezo wake haukuwa wa kawaida, alikuwa akikimbizana na Latifa japokuwa walisoma madarasa tofauti.
Aliwakataa wasichana wengi, hakupenda kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi lakini mara baada ya kumtia Latifa machoni, moyo wake ukamlipuka, hakuamini kama katika dunia hii hasa katika nchi ya Tanzania kungekuwa na msichana mrembo kama alivyokuwa Latifa.
“She is so beautiful, I just want to be with her, I will never let her go,” (Ni mrembo mno, ninataka niwe naye, kamwe sitomuacha aondoke) alisema Maliki huku akimwangalia vizuri Latifa.
Msichana huyo alionekana kuwa msichana wa ndoto zake, kila alipoelekea shuleni ilikuwa ni lazima kwenda katika darasa la kina Latifa kwa lengo la kumuona tu. Moyo wake ukatekwa, hakukuwa na msichana aliyeuteka moyo wake kama alivyokuwa Latifa.
Alijitahidi kumpiga picha kisiri na kuwa nazo kwenye simu yake, hiyo ikaonekana kutotosha, alichokifanya ni kutafuta namba yake, alipoipata, akajitahidi kuwa karibu naye kimawasiliano lakini msichana huyo alikuwa mgumu kutekeka.
“Nifanye nini? Ngoja nikamwambie ukweli. Mmh! Ila nitaweza kweli? Mbona naanza kumuogopa!” alijisemea Maliki.
Kumfuata Latifa ulikuwa mtihani mgumu, alibaki akiumia moyoni mwake huku kila siku usiku akikesha kuziangalia picha zake tu.
Wakati hayo yote yakiendelea katika maisha ya Maliki, upande wa pili, bado Ibrahim, kijana masikini aliendelea kuteseka moyoni mwake. Safari za kwenda Mbezi Beach hazikuisha, mara kwa mara alikwenda huko na alipofika karibu na eneo la shule hiyo, alikuwa akijificha.
Gari alilokuwa akiendeshwa Latifa lilipotoka katika eneo la shule, Ibrahim alitoka alipokuwa amejificha na kuanza kuliangalia, hata alipokuwa akimuona msichana huyo kwa mbali, moyo wake uliridhika.
Hiyo ndiyo ilikuwa tabia yake, aliendelea kufika shuleni hapo lakini ikafika siku ambayo alionekana kuchoka, hakutaka kuendelea tena kujificha, siku hiyo alipanga kuongea na Latifa na kumwambia ukweli.
Alipofika karibu na eneo la shule hiyo, kama kawaida akajificha na wakati gari lile lilipoanza kutoka, akasogea kule lilipokuwa na kusimama mbele yake, si dereva wala Latifa, wote wakaonekana kushtuka, kile kilichoonekana kilimshtua kila mmoja.
“Piii…piiii…piii…” dereva alipiga honi lakini Ibrahim hakuondoka, aliendelea kusimama huku lengo lake kubwa likiwa ni kuongea na Latifa siku hiyo.
“Siondoki mpaka Latifa ashuke garini, nitataka kuzungumza naye tu, siwezi kuteseka siku zote hizo,” alisema Ibrahim huku akiwa amesimama kama askari wa barabarani, honi ziliendelea kupigwa lakini hakuondoka, alisubiri Latifa ateremke.
Alichokifanya dereva yule ni kuteremka kutoka garini na kuanza kumfuata Ibrahim. Kitendo alichokifanya kijana huyo kilimkera, alimfuata huku uso wake ukionyesha dhahiri kwamba alikuwa amekasirika.
Ibrahim hakuogopa wala kukimbia, huku dereva akimfuata, macho yake yalikuwa yakiangalia kioo cha mbele cha gari lile huku akijitahidi kuyafinyafinya macho yake ili aweze kumuona Latifa aliyekuwa ndani.
“Wewe dogo kichaa nini! Mbona unazingua, hebu toka barabarani,” alisema dereva yule kwa sauti iliyojaa ukali.
“Nataka kuongea na Latifa! Sitoki mpaka niongee na Latifa!” alisema Ibrahim kwa sauti kubwa.
“Unasemaje?”
“Nataka kuongea na Latifa, mwambie ashuke kutoka garini,” alisema Ibrahim.
Maneno aliyoongea na kitendo alichokifanya, alionekana kama kutania, dereva akazidi kushikwa na hasira zaidi, akamshika Ibrahim, akamvuta pembeni na kwenda kumtupia huko huku akimpiga mikwara asirudi barabarani pale.
Ibrahim alibaki akiwa amechukia, hakuamini kama kweli dereva aliamua kumfanyia kitendo kama kile ambacho kwake alikichukulia kuwa cha kikatili wa hali ya juu.
“Kuna nini?” aliuliza Latifa huku akishangaa.
“Yule dogo chizi sana!”
“Kwa nini?”
“Eti anataka kuongea na wewe! Unamjua?”
“Mmmh! Hapana! Ndiyo kwanza namuona leo,” alisema Latifa.
Dereva akawasha gari lile na kuondoka mahali hapo. Kichwa cha Latifa kikabaki kuwa na maswali mengi juu ya sababu iliyompelekea kijana yule asiyemfahamu kutaka kuzungumza naye.
Walipompita na gari, alibaki akimwangalia, alijaribu kuvuta kumbukumbu kuona kama alikwishawahi kumuona sehemu yoyote, hakukumbuka chochote kile.
Huo ndiyo ukawa kama mwanzo wa kila kitu, Latifa akashikwa na kiu, alitaka kusikia kitu ambacho kijana yule alitaka kumwambia. Japokuwa alijitahidi kumtafuta nje ya shule kila alipokuwa akitoka, hakumuona tena, moyo wake ukashikwa na kiu zaidi, moyoni, alijuta sababu ya kutokushuka garini siku ile na kwenda kuongea naye.

Latifa aliishi kwenye mateso makubwa, kila siku akawa mtu wa mawazo tu akimfikiria kijana aliyekuja kumwangalia ambaye alitaka kuzungumza naye lakini hakuweza kushuka garini.
Siku ziliendelea kukatika, hamu aliyokuwa nayo moyoni mpaka ikaisha lakini hakufanikiwa kumuona Ibrahim tena. Aliendelea na maisha yake huku akiendelea kufanya vizuri katika masomo yake kwa kuwaongoza wanafunzi wote shuleni hapo.
Maliki, hakutaka kukata tamaa, kuna kipindi kikafika akaona ni bora kumfuata msichana huyo na kumwambia ukweli lakini hakuwa radhi kuendelea kupata mateso ya moyo. Alichokifanya katika siku ambayo alipanga kumwambia Latifa ukweli, akajiandaa vizuri, hakutaka kuonekana na kasoro yoyote ile, akajivisha ujasiri na kumfuata msichana huyo.
“Hapana Maliki, sipo tayari kuwa na mvulana yeyote yule,” alisema Latifa, alionekana kumaanisha alichokisema.
“Latifa, lakini mbona sioni tatizo lolote lile, kama kuna mtu ameuumiza moyo wako, ninataka kuwa daktari kwako, niutibu na upone kabisa, nakuahidi kutokukuumiza,” alisema Maliki huku akimwangalia Latifa machoni. Akamshika mkono ili asiondoke.
“Maliki, let me go, I’m too young to take care of someone. I’ m just thinking of my studdies, you met me here, you don’t know where I came from, please, let me go,” (Maliki, niache niondoke, mimi ni mdogo mno kumjali mtu. Ninayafikiria masomo yangu, ulinikuta hapa, hujui nimetoka wapi, niache niondoke) alisema Latifa huku akimtaka Maliki amuachie mkono.
“Laty! What is your problem? Should I say that I’m ready to die for you? Will this make you happy and trust me when I say that I love you?” (Laty! Tatizo lako nini? Natakiwa kusema kwamba nipo tayari kufa kwa ajili yako? Hii itakufanya kuwa na furaha na kuniamini ninapokwambia kwamba ninakupenda?) aliuliza Maliki.
“Let me go,” (Niache niondoke) alisema Latifa, sauti yake ilitoka kwa juu tena yenye ukali mwingi.
Maliki akaogopa, ukali alioutumia Latifa ukamtisha, akajikuta akimuachia binti huyo na kuondoka zake. Alimwangalia msichana huyo huku moyo wake ukimuuma mno, hakuamini kama uwezo wake wote wa kuongea aliokuwa nao haukumsaidia hata mara moja na mwisho wa siku kukataliwa huku akijiona.
Huo wala haukuwa mwisho, alichokifanya ni kuanza kufuatilia msichana huyo alikuwa akitoka kimapenzi na nani. Alifanya uchunguzi wake kwa siku kadhaa lakini hakubaini kitu chochote kile, aligundua kwamba msichana hiuyo alikuwa peke yake.
Latifa hakuyataka mapenzi, aliamua kuishi peke yake kwani kulikuwa na mambo mengi ya kufanya katika maisha yake. Aliendelea na maisha yake ya kuwakataa wanaume waliokuwa wakimfuatilia kila siku, japokuwa ulikuwa mtihani mzito lakini alihakikisha kwamba anafanikiwa.
“Malkia Cleopatra....” ilisikia sauti ya msichana mmoja ikimuita jina lake la utani, Latifa akageuka, msichana yule akamsogelea.
“Unasemaje Lilian?”
“Kuna mvulana amenipa hii barua, amesema nikupe.”
“Mvulana gani?”
“Wala simjui, nimekutana naye hapo nje ya shule, akanipa, akaniambia nikufikishie halafu akaondoka zake,” alisema Lilian.
“Mmmh!”
“Unamjua?”
“Hapana. Ni nani?” aliuliza Latifa.
“Sijui!”
Latifa akaichukua barua ile na kuanza kuifungua. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa kasi, mwili ukaanza kumsisimka, moyoni mwake alijua kwamba ni yule kijana aliyemuona siku ile. Alipoifungua barua ile, akaanza kuisoma, barua hiyo iliandikwa hivi....
Kwako Latifa
Nimekuwa nikikufuatilia kwa kipindi kirefu, u msichana uliyeuteka moyo wangu, nimekuwa nikiteseka kwa ajili yako kwa kipindi kirefu mno tangu ulipokuwa Sekondari ya Jangwani.
Najua haunifahamu, lakini unamkumbuka yule kijana aliyetaka kuzungumza nawe siku za karibuni? Yule kijana mchafu, asiyevutia lakini mwenye mapenzi ya dhati kwako?
Latifa, nimejaribu kila njia kukutana nawe lakini imeshindikana, sina njia nyingine ya kufanya zaidi ya kukuandikia barua hii kwa mwandiko huu mbaya.
Nilisikitika sana ulipopata ajali, kila siku nilikuwa mtu wa kukuombea dua ili upone na ninamshukuru Mungu kwa kukuponya na kukurudishia afya kama ulivyokuwa kabla.
Nilihuzunika pia kipindi cha nyuma ulipokwenda nchini India, naikumbuka picha yako ya mwisho kukuona ukiwa hospitalini, ulikuwa kimya huku sura yako ikionyesha kama haukuwa pamoja nasi.
Latifa, nina mengi ya kuzungumza lakini kubwa zaidi lililobeba hayo mengi, ni kwamba, ninakupenda mno, ninakupenda zaidi ya unavyofikiria.
Kama ningeulizwa ni kitu gani natakiwa kuwa nacho maishani mwangu sasa hivi, hakika ningekuchagua wewe.
Ninakupenda Latifa, sijajua ni jinsi gani naweza kulieleza hili, ila ukweli, ni kwamba nakupenda.
Ibrahim, Sekondari ya Azania.
Latifa akashusha pumzi nzito, hakuamini kile alichokisoma katika barua ile, akabaki akitabasamu huku akijisikia furaha moyoni mwake. Hakuamini kama barua ile aliandikiwa yeye pasipo kutegemea, kwani ilijaza maneno matamu ambayo hakuwahi kuyasoma kabla.
Siku hiyo, barua ile ilikuwa karibu yake, hakutaka kuiweka ndani ya begi, muda wote ilikuwa katika mfuko wa sketi yake, kila alipoona kwamba hakukuwa na mwalimu darasani, aliichukua na kuanza kuisoma tena, moyo wake ukafarijika mno.
Taratibu mawazo juu ya Ibrahim yakaanza kumteka, kila sehemu alipokuwa, aliifikiria barua ile huku muda mwingi akivuta kumbukumbu juu ya kijana huyo ambaye alimuona mara moja tu katika kipindi walichokuwa wakipita na gari kurudi nyumbani.
Moyo wake ukawa na hamu kubwa, akatamani kumuona huyo aliyeandika maneno matamu yaliyoukuna moyo wake vilivyo. Kwa sababu chini kabisa aliandika kwamba alitokea katika Shule ya Wavulana ya Azania, kesho akawa huko.
Uzuri wake uliendelea kuwa gumzo, wengi waliomuona walimkumbuka, alikuwa miongoni mwa wasichana walioziteka shule zote za ukanda wa mjini kuanzia Azania, Kisutu, Jangwani na shule nyingine za Kihindi.
Siku hiyo hakwenda shule, alitaka kuitumia siku hiyo kumuona mvulana huyo tu. Kila mvulana aliyepishana naye, aligeuka nyuma na kumwangalia, alionekana kuwa na uzuri usio wa kawaida, wanaume wakware, wakashindwa kuvumilia, wakabaki wakimuita kwa kumpigia miluzi tu.
Latifa hakujali, alipofika shuleni hapo, akamuulizia Ibrahim kwa lengo la kutaka kumuona mvulana huyo.
“Wapo wengi, unamuulizia yupi?” aliuliza mlinzi.
“Wala simfahamu, ila alijitambulisha kwa jina la Ibrahim.”
“Sawa! Kwa jinsi ninavyokuona, atakuwa Ibrahim Jumanne. Jamaa fulani msafimsafi hivi, ngoja nikuitie,” alisema mlinzi yule na kuondoka mahali hapo.
Latifa alibaki sehemu ya mlinzi akisubiriwa kuitiwa mtu aliyekuwa akimhitaji. Japokuwa haikuwa ikiruhusiwa mpaka mtu kwenda kwenye ofisi ya walimu, lakini mlinzi alishindwa kuvumilia, hakukubali kuona akikataa kumsaidia msichana mrembo kama Latifa.
Aliporudi, aliongozana na kijana aliyeonekana kuwa mtanashati, alipendeza alivyovaa na alinukia vizuri. Kijana huyo alipomuona Latifa, akashtuka, hakuamini kama aliuliziwa na msichana mrembo kama alivyokuwa, akamsogelea huku akiachia tabasamu pana.
“Niambie mrembo!” alisema kijana huyo.
“Safi tu! Kaka, samahani, siyo huyu,” alisema Latifa huku akimwangalia mlinzi.
“Mmmh! Siyo huyo? Basi muulize huyohuyo atakuwa anamfahamu,” alisema mlinzi yule.
Hapo ndipo Latifa alipoanza kumueleza huyo Ibrahim juu ya mtu aliyekuwa akimhitaji shuleni hapo. Kichwa cha mvulana huyo kikaanza kuwapekua Ibrahim wote waliokuwepo shuleni hapo, kila aliyemfikiria, hakulingana na maneno aliyokuwa akielezea Latifa.
“Huyo wala simfahamu!”
“Kaka, naomba unisaidie kunitafutia huyu Ibrahim, muulizie hata shule nzima, ukifanikiwa, nakupa zawadi, chukua hii kwanza,” alisema Latifa huku akimkabidhi Ibrahim shilingi elfu kumi kama kumhamasisha katika suala zima la kumtafuta Ibrahim. Jamaa akaenda kumtafuta.
Moyo wa Latifa ulikuwa kwenye mapenzi ya dhati, hakuwa radhi kuondoka na kurudi nyumbani na wakati yule aliyekwenda kumtafuta hakuwa amemuona. Alikaa sehemu hiyo ya mlinzi huku akiongea naye, kila neno aliloliongea, alionekana kuwa na uhitaji wa kumuona kijana huyo.
Zilipita dakika thelathini, Ibrahim yule akarudi na vijana watano waliokuwa na jina kama lake. Latifa akaanza kuwaangalia watu hao, japokuwa kipindi cha nyuma wakati Ibrahim alipokuja shuleni kwao hakumuona vizuri lakini kila alipowaangalia wavulana wale, moyo wake ulimwambia kwamba kipenzi chake hakuwepo.
“Hapana! Hawa ndiyo wote?” aliuliza Latifa.
“Hapana. Kuna mmoja amebaki, leo hajaja, mtoromtoro na mchafumchafu fulani hivi, nikaona siyo tatizo nikikuletea hawa wenzangu, achana na yule, hawezi kuwa yeye, kwanza kuna demu huwa anampigia misele huko Mbezi,” alisema Ibrahim.
“Ninataka kumuona pia,” alisema Latifa.
“Yupi? Huyo mchafumchafu?”
“Ndiyo! Huyohuyo! Nataka kumuona, inawezekana akawa mchafu kimwili, ila moyoni akawa na mzigo mzito wa mapenzi yangu, nahitaji kumuona, naomba unitafutie au kunipeleka kwao, nitakupa kiasi chochote utakachotaka, naomba nikamuone,” alisema Latifa huku akionekana dhahiri kuwa na uhitaji wa kumuona kijana huyo.
“Lakini inawezekana siye yeye, huoni kama utasumbuka?”
“Kusumbuka kwa ajili ya mapenzi, si tatizo kaka yangu, hata angekuwa wapi, ningemfuata. Ili niujutie usumbufu, kama siye yeye, basi nitajuta, ila kama ni yeye, hakika nitakuwa na furaha moyoni mwangu,” alisema Latifa. Mapenzi yalimteka na kumtumbukiza kwenye bwawa la mahaba.
****
Siku hiyo Latifa alidhamiria kuonana na kijana aliyejitolea kumpenda kwa mapenzi ya dhati, Ibrahim. Mara baada ya kuzungumza na kijana huyo mtanashati ambaye alimfuata na kumwambia kwamba mvulana aliyekuwa akimtaka hakuwa shuleni hapo, akataka kwenda kumuona.
Latifa hakutaka kurudi nyumbani pasipo kumuona Ibrahim, kilichotokea, akaanza kupelekwa Magomeni Kagera alipokuwa akiishi Ibrahim. Walipofika huko, kijana yule mtanashati akaelekea katika nyumba hiyo na kumuita Ibrahim waliyemfuata.
“Hayupo.”
“Amekwenda wapi?”
“Hatujui, labda rudini jioni-jioni hivi,” alisema mwanamke mmoja waliyemkuta, alikuwa mama yake Ibrahim.
“Ila hapa si ndiyo kwao?”
“Ndiyo!”
“Basi nitarudi baadaye,” alisema Latifa.
Hilo wala halikuwa tatizo, kwa sababu alikuwa amekwishapafahamu alipokuwa akiishi Ibrahim, akaahidi kurudi tena baadaye. Moyo wake ukaridhika, kitendo cha kuifahamu nyumba ile akajiona mshindi, alichokifanya ni kumpa Ibrahim yule shilingi elfu kumi nyingine na kuondoka.
Ilipofika saa 11:03 jioni, Latifa alikuwa tena nyumbani hapo, muda huu, ulionekana kuwa bahati kwa upande wake, mvulana aliyekuwa akimtafuta, aliyetaka kumuona alisimama mbele yake, hakuyaamini macho yake kwamba yule kijana aliyeandika maneno matamu yaliyoutetemesha moyo wake ndiye huyo aliyekutana naye.
Umasikini ulimtafuna mno Ibrahim, hakuonekana kuwa na uwezo kifedha kwani hata mavazi aliyokuwa ameyavaa, yalionyesha ni jinsi gani alivyokuwa masikini. Japokuwa alikuwa katika hali hiyo, kitendo cha kumuona Latifa tu kilimfurahisha, kikamrudishia furaha kubwa moyoni mwake.
“Umependeza,” Ibrahim alimwambia Latifa mara baada ya salamu, tabasamu pana lilikuwa usoni mwake.
“Nashukuru. Hapa ndiyo nyumbani?”
“Ndiyo! Ninaishi na mama.”
“Na baba yupo wapi?” aliuliza Latifa lakini Ibrahim hakujibu kitu, akabaki kimya huku uso wake ukibadilika na kuonyesha majonzi.
“Pole sana Ibrahim,” alisema Latifa huku akimshika mkono Ibrahim kwa kugundua kwamba baba yake alikuwa amefariki dunia.
“Usijali. Siamini kama umekuja kunitafuta, subiri, nina zawadi yako,” alisema Ibrahim huku akianza kupiga hatua kuelekea ndani.
Wala hakuchukua muda mrefu, akarudi nje huku akiwa na karatasi moja kubwa, iliyokunjwa, akamgawia Latifa, alipoikunjua, akakutana na sura yake, picha iliyochorwa kipindi yupo hospitalini huku akiwa ametundikwa dripu.
“Ni mimi?” aliuliza Latifa huku akichia tabasamu pana.
“Ndiyo! Hiki ndicho kilikuwa kipindi kigumu nilichowahi kukutana nacho maishani mwangu, niliumia mno, sikutarajia kumuona msichana ninayempenda akiwa kimya kitandani. Latifa, barua imeeleza kila kitu, hii picha ni kama kupigilia msumari wa mwisho moyoni mwako juu ya upendo niliokuwa nao kwako,” alisema Ibrahim kwa sauti ya mahaba.
Hapo ndipo Latifa alipogundua kwamba mbali na mvulana huyo kuwa na mapenzi mazito juu yake, pia alikuwa mchoraji mzuri. Alipoiangalia picha ile, haikuonekana kama imechorwa, ilionekana kama imepigwa kwa kamera. Latifa akashindwa kuvumilia, pasipo kutarajia, akajikuta akimsogelea Ibrahim na kumkumbatia.
****
Walihisi kwamba wao ndiyo walikuwa watu wa kwanza duniani kupendana kama walivyokuwa wakipendana, muda mwingi walikuwa pamoja huku wakizungumzia mambo mengi ambayo kwa namna moja au nyingine yaliufanya upendo wao wa dhati uweze kukua na kuwa zaidi ya hivyo ulivyokuwa.
Siku zikaendelea kukatika huku siku zikizidi kusonga mbele mpaka kufika siku ambayo wawili hao wakamaliza masomo yao ya kidato cha nne na hivyo kukaa nyumbani. Waliitumia nafasi hiyo kufanya mambo mengi likiwepo mapenzi ambalo kwa wao wote lilikuwa suala gumu mno.
Matokeo yalipotoka, Latifa alikuwa amefaulu vizuri lakini kwa Ibrahim, hakuwa amefanya vizuri kabisa. Alionekana kuwa na majonzi lakini mpenzi wake, Latifa ndiye aliyekuwa mfariji wake namba moja, kila alipokuwa akiyafikiria matokeo yale, Latifa alimsogelea, alimkubatia na kumwagia mabusu mfululizo mashavuni mwake.
Kidogo, moyo wake ulijisikia afueni huku hata matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne yakaanza kupotea kabisa.
Kwa sababu bi Rachel alikuwa na mtoto wake aliyekuwa akisoma nchini Marekani, hivyo hakutaka Latifa aendelee kusoma nchini Tanzania, alichokifanya ni kuomba ruhusa kwa mzee Issa kwamba alitaka kumpeleka msichana huyo nchini Marekani.
“Kwa hiyo unataka kumpeleka kwa Wazungu?” aliuliza mzee Issa huku akionekana kutokuamini alichokuwa akikisikia.
“Ndiyo. Atakwenda kusoma katika shule anayosoma mtoto wangu,” alisema bi Rachel.
“Sawa, hakuna tatizo, ila mtoto mwenyewe atataka?”
“Nitaongea naye.”
Hilo halikukuwa tatizo kwani hata Latifa alipofikishiwa taarifa hiyo, akakubaliana naye na hivyo kumwambia Ibrahim kwamba alitakiwa kuondoka nchini Tanzania na kwenda Marekani kusoma.
“Mmmh!”
“Nini tena mpenzi?”
“Wazungu wananiogopesha mno, hawatoweza kunilia tunda langu?” aliuliza Ibrahim.
“Najiamini, najitunza, hakuna kitu kama hicho, niamini,” alisema Latifa na kumkumbatia Ibrahim.
“Ila usiache kuchora mpenzi, naamini utafanya makubwa mno,” alisema Latifa na Ibrahim kukubaliana naye.
Hakukuwa na kipindi alichokuwa na huzuni kama kipindi hicho, Ibrahim hakuamini kama furaha yote na ya kipindi chote ndiyo ilitakiwa kuishia wakati huo.
Japokuwa Latifa alijitahidi kumwambia Ibrahim kwamba kusingekuwa na kitu chochote ambacho kingebadilika na angeendelea kulitunza penzi lake, lakini Ibrahim hakuliamini hilo.
Usiku hakulala, mawazo yake yalikuwa kwa Latifa tu. Aliwasiliana naye simuni na kumwambia juu ya wasiwasi wake wa kuporwa msichana wake lakini binti huyo aliendelea kumsisitizia kwamba alikuwa wake peke yake.
Siku zikaonekana kukatika kwa kasi sana, siku ya safari ilipofikia, Ibrahim akaonekana kama mgonjwa, mpaka ndege ya Shirika la Ndege ya American Airlines inapaa, tayari machozi yalikwishambubujika vya kutosha mashavuni mwake.
Ndege ilichukua saa kadhaa kufika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Amsterdam ambapo wakabadilisha ndege na kupanda nyingine iliyowapeleka mpaka katika Jiji la Atlanta, sehemu ambapo Latifa alitakiwa kuanza masomo yake katika Shule ya St. Luis II iliyokuwa katikati ya jiji hilo.
Siku ya kwanza tu ambayo alipelekwa shuleni hapo, wanaume wote wakapigwa na butwaa, msichana mgeni, kutoka barani Afrika katika nchi masikini ya Tanzania alionekana kuwa na uzuri usio wa kawaida.
Alikuwa msichana wa Kichotara mwenye mvuto, hipsi zilizojaa na chini ya pua yake kuwa na kidoti kilichosindikizwa na vishimo viwili mashavuni mwake. Alimvutia kila mmoja.
Siku hiyo akasajiliwa kuanza masomo shuleni hapo huku akiwa na mtu wake wa karibu, mtoto wa bi Rachel aliyeitwa Dorcas.

ITAENDELEA

CHANZO : BURE SERIES
 
SEHEMU YA NNE

Latifa akatokea kupendwa shuleni hapo kutokana na uzuri aliokuwa nao. Wanaume wengi walimtolea macho lakini hakukuwa na mtu aliyethubutu kumfuata. Hakukuwa na aliyefikiria kwamba msichana huyo alitokea nchini Tanzania, shule nzima walifikiri kwamba Latifa alitokea nchini Nigeria.
Hakukuwa na Mzungu aliyetaka kuanzisha uhusiano na msichana yeyote wa Kinajeria, waliwafahamu wasichana hao, walikuwa wajanja na wengi wao walikuwa matapeli na kama ukiwa nao zaidi, kuna siku wanakuibia kila kitu ulichokuwa nacho.
Ukaribu wa Latifa na Dorcas ukawapa wasiwasi zaidi, miongoni mwa watu waliokuwa wakorofi hata kuwasogelea alikuwa msichana Dorcas. Hakuwa msichana aliyewapenda wavulana, aliwachukia mno na chanzo cha kuwachukia kilikuwa ni jamaa aliyeitwa Michael Okonkwo, kijana wa Kinaijeria ambaye alimuibia vitu vyake vyote chumbani kwake zikiwepo fedha.
“Kuwa makini Latifa,” alisema Dorcas.
“Makini na nini?”
“Wanaume! Wanaume wa huku ni wabaya sana, ukizubaa tu, umelizwa, hasa Wanaijeria” alisema Dorcas.
“Usijali, nitakuwa hivyo.”
Dorcas hakutaka kuishia hapo, alianza kumsimulia mambo yote yaliyokuwa yakitokea shuleni hapo likiwepo suala la Wanaijeria kuwa wezi na matapeli wakubwa. Latifa akaogopa, hakutaka kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu yeyote yule.
Siku ziliendelea kukatika, alipoanza masomo ndipo watu walipojua kwamba mbali na uzuri aliokuwa nao, Latifa alikuwa mtu hatari darasani. Hakujali kama alikuwa katika ardhi ya ugenini, alichokuwa akikifanya ni kuwaongoza kwa alama nyingi darasani.
Ndani ya miezi sita tu, tayari jina lake lilikuwa miongoni mwa wanafunzi waliokuwa na kipaji darasani. Hakusoma sana, muda mwingi aliutumia chumbani lakini kila ulipokuwa ukija mtihani, Latifa alitisha kwa kupata alama za juu.
“Nataka uhusiano naye,” alisema jamaa mmoja, alikuwa mvulana mtanashati, Muhindi kutoka Jijini Mumbai nchini India.
Liban alikuwa miongoni mwa watu waliovutiwa na Latifa, kila siku katika maisha yake alitamani kuwa karibu na msichana huyo. Alimpenda kwa moyo wake wote, hakuwa tayari kumuona msichana huyo akimkosa na ndiyo maana kila siku alikuwa akimtafuta katika rada zake.
Kuwa na Latifa halikuwa jambo dogo, hakuingilika kwa kuwa tayari alikwishaambiwa maneno mengi na Dorcas juu ya tabia za wanaume wengi shuleni hapo. Moyo wake ulikuwa mgumu na hata Liban alipoanza kumchombezachombeza, Latifa hakuwa tayari.
Mbali na hilo, bado kichwa chake kilimfikiria mpenzi wake Ibrahim aliyekuwa nchini Tanzania. Hakutaka kumsaliti, alijitahidi kuutoa moyo wake kwa hali zote lakini si kumsaliti mvulana huyo. Japokuwa alikuwa kijana masikini, moyo wake ulikuwa na hamu ya kuishi naye milele.
****
Ibrahim akuwa na akili darasani, alifeli vibaya lakini mbali na akili hizo, Mungu alimpa kipaji cha uchoraji. Alipenda kuchora, kila siku katika maisha yake, asilimia kubwa alikuwa akitumia kuchora.
Alitafuta ajira magazetini, alikataliwa kwa kuwa hakuonekana kama alifaa kufanya kazi hiyo ya uchoraji. Ibrahim hakutaka kuishia hapo, aliendelea kuchora zaidi huku mbele yake akiyaona mafanikio makubwa.
Alichokifanya ni kutafuta sehemu maalum ya kufanyia kazi zake za kuchora. Hapo, akaandika bango kwa watu waliokuwa wakitaka kuchorwa, mteja wa kwanza kabisa kumpata alikuwa Nusrat, msichana wa Kiarabu aliyefika mahali hapo na kutaka kuchorwa huku akiwa na mpenzi wake.
“Kiasi gani?” aliuliza Nusrat.
“laki moja na nusu kwa mtu mmoja.”
“Sawa. Chukua hii picha, naomba unichore hivihivi, picha iwe kwenye manila kubwa, nitakuja wiki ijayo kuichukua,” alisema Nusrat huku akiingiza mkono mfukoni na kutoa kiasi hicho cha fedha na kumkabidhi Ibrahim.
Macho ya Nusrat hayakutulia, kila alipokuwa akimwangalia Ibrahim, alionyesha kwamba alikuwa na kitu fulani moyoni mwake, hakutaka kukiweka wazi kwani alionekana kuwa na hofu kubwa kwa kuwa tu mpenzi wake alikuwa pembeni yake.
Japokuwa hakutaka kuonyesha chochote kile, lakini ukweli ni kwamba alitokea kumpenda kijana huyo, hasa kipaji chake cha uchoraji ambacho kilimdatisha mno.
Nusrat alikuwa msichana mrembo aliyevutia kwa kila kitu, macho yake malegevu, umbo lake la kimisi na hipsi zilizojaa vilizidi kuongeza uzuri wa muonekano wake.
Japokuwa alipewa siku maalum kufika mahali hapo kwa ajili picha yake ingekuwa imekamilika lakini kwake ilionekana kuwa ngumu kusubiri. Alitokea kumpenda mno Ibrahim na asingekuwa tayari kuendelea kusubiri na wakati kila siku moyo wake ulikuwa kwenye mateso makali. Alichokifanya ni kuanza kuelekea kule alipokuwa akichorewa picha yake.
Kila siku alipofika hapo, alikuwa mtu wa kupiga stori tu huku muda mwingi akitumia kukaa mikao ya hasarahasara ili kumpagawisha Ibrahim. Kwa kijana huyo ilikuwa ni shida mno lakini akaamua kuvumilia kwani aliwajua wasichana vilivyo.
“Unajua sana kuchora, hivi ulijifundisha au kipaji?” aliuliza Nusrat.
“Kipaji tu. Mungu aliniumba nikiwa hivi,” alijibu Ibrahim.
“Hongera sana wangu, unajitahidi sana,” alisema Nusrat.
Kila siku akawa mtu wa kutoa pongezi tu kwa Ibrahim. Hakukuwa na siku ambayo hakwenda mahali hapo na kujifanya kuulizia picha yake na wakati moyoni mwake alimpenda.
Alivumilia mno mpaka kikafika kipindi hakutaka kuendelea kuwa na uvumilivu, aliamua kuufumbua mdomo wake na kumwambia ukweli jinsi alivyokuwa akijisikia, kwamba alimpenda mno na hakuwa akilala kwa ajili yake.
Ibrahim alivyoambiwa, hakushtuka, alilitegemea hilo kwani dalili za mvua zilikwishaanza kuonekana kwa mawingu kutanda angani, hivyo akachukulia suala hilo kuwa kawaida sana.
“Umechelewa mno Nusrat, nina mtu tayari, ninampenda na ananipenda pia,” alisema Ibrahim.
“Haiwezekani, sidhani kama nimechelewa Ibrahim. Nimetokea kukupenda, siwezi kukaa kimya kwani ninausababishia moyo wangu maumivu mazito, ninaomba uwe wangu, hata ukinifanya kuwa mtu wa pili, nitakuwa tayari kwa hilo lakini si kukukosa,” alisema Nusrat huku akionekana kuwa na uhitaji wa kuwa na kijana huyo.
Msimamo wa Ibrahim ulikuwa uleule kwamba hakutaka kuwa na binti huyo kwa kuwa tayari alikuwa na mpenzi wake aliyeahidiana naye mambo mengi, Latifa.
Siku zikaendelea kukatika, Nusrat hakukoma, alijua kwamba alikataliwa lakini hakutaka kuchoka, kila siku alifika mahali hapo na kuendelea kumwambia maneno matamu kwa kuamini kwamba kuna siku moyo wake ungebadilika na kukubaliana naye.
Alipoona kwamba Ibrahim anaendelea kuweka msisitizo kwamba alikuwa na mpenzi wake, hapo ndipo alipotumia njia nyingine ambayo aliamini kwamba angefanikiwa kwa urahisi mno, akaanza kutumia zawadi.
Kila alipofika hapo, alikuwa na vitu mbalimbali alivyoamini kwamba vingeweza kumpagawisha kijana huyo, kitu alichomwambia ni kwamba aliamua kumpa zawadi hizo kutokana na ugumu aliokuwa akiupata katika kumchorea picha yake.
Siku za kwanza ilikuwa ngumu kukubaliana na msichana huyo lakini baada ya kulia sana huku akilalamika kwamba hakuwa akithaminiwa, Ibrahim akaamua kuzipokea zawadi hizo kama fulana, chokleti na hata wakati mwingine kuletewa fedha.
Taratibu Nusrat akaanza kuyabadilisha maisha ya Ibrahim, kiasi kikubwa cha fedha alichokuwa akimpa, alikitumia katika kuyaendeleza maisha yake kwa kununua vitu vingi vya ndani na hata kulipia kodi ya chumba alichokuwa amepanga baada ya kuhama nyumbani.
Kukataa kwake kuwa mpenzi wake, mwisho wa siku msichana huyo akasisistiza kwamba wawe marafiki wa kawaida ili kumtoa wasiwasi, Ibrahim akakubaliana naye pasipo kugundua kwamba hiyo ilikuwa moja ya njia aliyoitumia msichana huyo kumteka.
Urafiki ulipokua, Nusrat akaanza kumuomba Ibrahim kutoa mitoko mbalimbali. Hilo halikuwa jambo gumu, kwa kuwa walikubaliana kwamba walikuwa marafiki tu, kijana huyo hakuwa na wasiwasi wowote ule.
Kuwa karibu na Nusrat, kutoka na kwenda sehemu mbalimbali, kupokea zawadi zake na hata kuwa naye bize kwenye simu kuongea naye nyakati za usiku kukaanza kuubadilisha moyo wa Ibrahim. Taratibu akaanza kumsahau Latifa huku akiupa nguvu msemo usemao ‘Fimbo ya mbali haiui nyoka’.
Baada ya ukaribu wao kudumu miezi miwili, mambo yakabadilika, wakaanza kubusiana na mpaka kubadilishana mate kitu kilichoufanya moyo wa Ibrahim kuendelea kumsahau kabisa Latifa, na miezi minne ilipokatika, akasahau kama alikuwa na msichana aliyeitwa kwa jina la Latifa, penzi la Nusrat likauteka moyo wake.

Liban hakutaka kukata tamaa hata mara moja, alimpenda sana Latifa na hivyo asingeweza kukaa kimya na kuona msichana huyo akipita. Kila siku shauku yake kubwa ilikuwa ni kuzungumza na msichana huyo lakini hakuweza kuipata nafasi hiyo.
Latifa hakuwa msichana mwepesi, hakuwa kama wasichana wa Kizungu ambao ukiwaambia kwenda kula chakula cha usiku, basi hukubaliana nawe na usiku huohuo kuwa wapenzi. Kwa Latifa, alitamani kuishi kama Mtanzania kwa kuamini kwamba lingekuwa jambo gumu kupatikana kwa kuwa alilelewa kama Mtanzania.
“Ninampenda sana Latifa,” alisema Liban.
Ni kweli moyo wake ulichanganyikiwa mno, japokuwa alipata nafasi ya kusoma na Latifa darasa moja lakini hakuwahi kupata nafasi ya kuzungumza naye, msichana huyo alionekana kuwa siriasi sana.
Siku zikiendelea kukatika mpaka Liban aliposema kwamba imetosha, kama kuteseka, aliteseka mno, huo ukawa wakati wa kumfuata Latifa na kumwambia ukweli wa moyo wake, kama atakubali, awe mpenzi wake na kama atakataa, basi abaki na maumivu yake moyoni.
“Ninakupenda Latifa,” alisema Liban kwa sauti ndogo aliyohakikisha kwamba aliitoa kimahaba.
“Najua, unafikiri nilikuwa sijui! Najua sana.”
“Nashukuru. Kwa hiyo inakuwaje?”
“Kuhusu nini?”
“Kuwa nami.”
“Haiwezekani.”
“Kwa nini?”
“Nina mpenzi wangu, ninampenda, ninamjali na kumthamini, mbaya zaidi, siwezi hata kumsaliti,” alisema Latifa.
Hakuwa muongeaji sana, alipoona kwamba amemaliza kile alichokizungumza na Liban, akasimama na kuondoka zake. Maneno ya Latifa yalikwenda na maumivu makali moyoni mwa Liban, hakuamini kama angeweza kuambiwa maneno yenye kuchoma moyo wake kama yale.
Alimwangalia Latifa alivyokuwa akiondoka, alionekana mrembo hasa lakini hakuwa na cha kufanya, kama kukataliwa, alikataliwa, ikambidi awe mpole tu.
Siku zikaendelea kukatika, japokuwa kwa upande wa Tanzania, Ibrahim aliamua kuanza uhusiano wa kimapenzi na msichana mwingine lakini kwa Latifa hakutaka kabisa kufanya hivyo, hakujua kilichokuwa kikiendelea, hakujua kwamba mwanaume yule aliyempa moyo wake na kumsisitizia kwamba alitakiwa kuwa nao makini tayari alianza kuwa na mwanamke mwingine.
Alimpenda mno, hakuwa akikaa zaidi ya saa moja pasipo kumbukumbuka. Kila alipoziangalia picha za Ibrahim, aliuhisi moyo wake ukiwa kwenye uhitaji mkubwa wa kuwa naye. Hakutaka kumsaliti, kwa jinsi alivyokuwa akimpenda, alihisi kwamba alionekana kila alipokuwa, yaani Ibrahim alikuwa akimfuatilia vilivyo.
Darasani aliendelea kuongoza, mpaka mwaka mzima unamalizika na matokeo kutoka, Latifa alikuwa amefanya vizuri kuliko wanafunzi wote shuleni hapo, matokeo yake yakawa ni ya alama za juu na kufunika alama zilizowekwa na genius Michael Rudzic, Mrusi aliyewahi kusoma hapo mwaka 1967 ambaye alishikiria rekodi ya kufaulu kwa alama nyingi.
“This is impossible,” (Hii haiwezekani) alisikika mwalimu mmoja mara baada ya kupata matokeo ya mitihani ile.
“She has the highest scores than what Rudzic got in 1967, she has broken the Rudzic’s record and make her own record,” (Ana alama za juu zaidi ya alizopata Rudzic mwaka 1967, amevunja rekodi ya Rudzic na kuweka rekodi yake mwenyewe,) alisema mwalimu huyo huku akionekana kutokuamini, ikambidi avue miwani yake na kuyaangalia vizuri matokeo yale.
Huo ndiyo ulikuwa ukweli, mara baada ya rekodi ya mwanaume genius kutoka nchini Urusi kudumu shuleni hapo kwa miaka mingi, hatimaye msichana kutoka Afrika, tena katika nchi iliyojiita Masikini, Tanzania alikuwa amefanya vizuri na kuvunja rekodi hiyo.
Moto wake ulimuogopesha kila mtu, wanafunzi wengine wakaanza kumtolea macho kwa kuona kwamba msichana huyo alikuwa na akili za ziada. Mpaka shule zinafungwa nchini Marekani kwa kujiandaa na majira ya joto, tayari Latifa alijipatia umaarufu mkubwa shuleni hapo.
“Tunarudi Tanzania,” alisema Dorcas.
“Ahsante Mungu! Sasa ni wakati wa kumuona tena mpenzi wangu, nilimkumbuka sana, Mungu, naomba moyo wa kumpenda mara mia zaidi ya nilivyompenda kipindi cha nyuma,” alisema Latifa huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana.
Kwa wakati huo, alihisi moyo wake kuwa kwenye mapenzi mazito zaidi ya kipindi kilichopita, alimpenda mno Ibrahim na hakuwa tayari kumpoteza, kwake, mvulana huyo alikuwa na nafasi kubwa hata zaidi ya mtu yeyote yule.
Siku ambayo walikuwa ndani ya ndege ya Shirika la Ndege la Americans Airlines, Latifa aliiona ndege ikichelewa kufika Tanzania, alitaka iende kwa kasi kuliko ilivyokuwa ikienda kwa wakati huo, muda wote mawazo yake yalikuwa kwa mpenzi wake, alimpenda na kumthamini sana.
Moyo wake ulijawa na upofu, hakujua kile kilichokuwa kikiendelea nchini Tanzania, mvulana aliyekuwa akimpenda na kumthamini, mvulana aliyempa thamani kubwa ya moyo wake, aliyemfanya kumkataa Liban, wakati huo alikuwa kwenye mapenzi ya dhati na msichana wa Kiarabu, Nusrat.
****
Latifa alikuwa kwenye presha kubwa, kitendo cha kufika nchini Tanzania, kesho yake akaanza kumtafuta Ibrahim kwenye simu. Ilikuwa kazi kubwa kwani kila namba aliyokuwa akimpigia miongoni mwa zile alizokuwa nazo, hakuwa akipatikana.
Ilimuumiza mno, alitaka kumuona mpenzi wake kwa kuamini kwamba kwa kipindi hicho alikuwa mzuri zaidi, yaani tofauti na alivyokuwa kipindi cha nyuma. Hakuacha, kila siku alimtafuta simuni lakini matokeo yalikuwa yaleyale, hakupatikana.
“Au alibadilisha simu? Hapana, inawezekana amezima tu,” alijiuliza na kujipa jibu.
Si kwamba hakupafahamu alipokuwa akiishi kijana huyo, alipafahamu lakini kitu cha kwanza alichokitaka ni kumfanyia sapraizi juu ya uwepo wake nchini Tanzania kwa kuamini kwamba angeshtuka mno.
Baada ya kukaa kwa siku mbili pasipo simu yake kupatikana, hapo ndipo alipoamua kwenda nyumbani kwao, Manzese kwa ajili ya kumuulizia, kwani tayari alikwishahisi kwamba kulikuwa na tatizo.
“Hayupo, alitoka na msichana mmoja hivi, demu wake,” alisema msichana mmoja aliyemkuta katika nyumba hiyo ya kupanga.
“Unasemaje?”
“Amegonganisha magari nini?”
“Unamaanisha nini?”
“Kwani wewe nani?”
“Naitwa Latifa.”
“Basi siyo wewe, yule anaitwa Nusrat, ni mzuri kama ulivyo wewe japokuwa umemzidi kidogo tu,” alisema msichana huyo.
“Sijakuelewa unamaanisha nini.”
“Kwani wewe ni nani kwake?”
“Mpenzi wake.”
“Kwa hiyo ana mademu wawili? Mmoja Muhindi na mmoja Mwarabu, kweli jamaa noma,” alisema msichana yule.
“Bado anaishi hapa?”
“Hapana, alihama, kahamia Magomeni.
Latifa hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, akasimama na kuelekea ndani ya gari lake, hata kabla hajaliwasha, akauegemea usukani wa gari lile na kuanza kulia. Moyoni aliumia, hakuamini kile alichokisikia kwamba mpenzi wake, aliyempenda, aliyetumia muda mwingi kwa ajili yake, leo hii alikuwa katika uhusiano na msichana mwingine.
Alilia na kulia, muda wote alijutia uamuzi wake wa kuwa na Ibrahim kiasi kwamba kuna wakati alijiona kuwa mtu mjinga alisiyestahili kupenda wala kupendwa.
“Kwa hiyo ana mademu wawili!? Mmoja Muhindi na mmoja Mwarabu, kweli jamaa noma,” maneno ya dada yule yakajirudia kichwani mwake na kumfanya kuumiza zaidi.
“Haiwezekani,” alisema Latifa na kuteremka garini.
Akamfuata msichana yule na kumuomba amuelekeze alipokuwa amehamia, kwa kuwa hakuwa anapafahamu, akamuelekeza sehemu aliyokuwa akifanyia kazi yake ya kuchora, Latifa akarudi garini na kuanza kuelekea huko.
Hakuwa makini barabarani, kichwa chake kilikuwa kimevurugika mno, mapenzi aliyoyapenda na kuyathamini, leo hii yalimfanya kubadilika na kuwa kama chizi. Alipofika karibu na Ubalozi wa Marekani, ilibakia kidogo tu agonge, bila utaalamu wa dereva mwenye gari ndogo, tayari angesababisha ajali.
“Mungu wangu! Ni nini hiki?” alijiuliza huku akijishangaa.
Aliendesha mpaka karibu na eneo ulipokuwa Ukumbi wa Maisha klabu ambapo kulikuwa na wachoraji wengi wa picha za kubandikwa ukutani. Hakutaka kuteremka, alibaki garini akianza kuangalia huku na kule kuona kama angeweza kumuona Ibrahim.
Wala hakuchukua muda mrefu, mtu aliyekuwa akitaka kumuona maeneo hayo, alifanikiwa kumuona, alikuwa amekaa chini huku akichora kama kawaida yake. Japokuwa aliambiwa maneno mengi, lakini akajikuta akifarijika, kwa mbali uso wake ukaanza kuawa na tabasamu pana.
Maneno yote aliyoambiwa na msichana yule yakaanza kupotea na kumuona mtu mbaya ambaye hakutaka kuuona upendo wake na Ibrahim ukiendelea kama kawaida. Huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana, akaushika mlango kwa ajili ya kuteremka.
Hata kabla hajafanya hivyo, mara akamuona msichana mmoja mrefu, mrembo mwenye nywele nyingi mpaka mgongoni akitembea kumfuata Ibrahim, akaacha kutoka garini na kuangalia kwa makini.
Msichana yule alipomfikia Ibrahim, akamfumba macho kwa nyuma kama wafanyavyo watoto na kisha kumbusu shavuni.
Yalikuwa ni zaidi ya maumivu, yalikuwa ni zaidi ya moto mkali uwakao moyoni mwake. Moyo wake ukawaka moto, akahisi kama kulikuwa na mtu aliyemfuata huku akiwa ameshika msumali wa moto na kisha kuuchoma moyo wake.
Kilichokuwa kikiendelea mahali pale, hakikuweza kuaminika moyoni mwake, hakuamini kama Ibrahim yuleyule aliyekuwa akimpenda na kumpa kila kitu alichotaka, leo hii alikuwa na msichana mwingine. Akashindwa kuteremka garini, akabaki humohumo na kuendelea kulia kama mtoto, picha aliyokuwa akiiona, hakika ilimuumiza.
“Ibrahim....” alijikuta akiita, hakutaka kubaki garini, akatoka na kuanza kuwafuata huku akiwa na hasira kali.
Latifa alitembea huku akiwa na hasira kali moyoni mwake, kile alichokuwa akikiona mbele yake, kiliuchoma moyo wake mno, akawa hataki kusikia la mtu yeyote yule, alichokitaka mahali hapo ni kumvamia Ibrahim na kupambana naye.
“Ibrahim...” alimuita mvulana huyo.
Ibrahim alipogeuka na macho yake kumwangalia Latifa, hakuzungumza kitu, hakuonekana kushtuka, alimwangalia msichana huyo, ghafla, tabasamu pana likaanza kuonekana usoni mwake, tabasamu lililoufanya moyo wa Latifa kuumia zaidi.
“Ibrahim mpenzi, nini kimekupata? Mbona unanifanyia hivi? Au kwa sababu ulijua sipo karibu nawe?” aliuliza Latifa huku akilia kama mtoto.
“Latifa! Mbona unakuja huku ukiongea hovyo kama chizi? Hebu punguza munkari kidogo, kaa chini, vuta pumzi mrembo,” alisema Ibrahim.
Aliongea kidharau mno, sauti yake ilionyesha ni kwa jinsi gani alikuwa na dharau kwa msichana huyo. Alimwangalia kuanzia juu na kumshusha mpaka chini, kisha akampandisha tena.
Mapenzi ya Nusrat yalimchanganya, akawa haoni, hasikii chochote kile, moyo wake ulitawaliwa na msichana huyo wa Kiarabu. Latifa aliongea sana, alilia sana lakini kila alipomwangalia, bado uso wake ulikuwa na tabasamu pana.
“Umemaliza?” aliuliza Ibrahim, Latifa aliendelea kulia.
“Unaifanyia hivi? Yaani leo unanifanyia hivi?”
“Umemaliza?”
“Ibrahim...!”
“Umemaliza?”
Latifa hakuweza kunyamaza, siku hiyo ilikuwa ni siku mbaya maishani mwake, siku iliyouchoma moyo wake, hakuamini kile alichokiona, alimpenda mno Ibrahim, moyo wake ulitekwa na mvulana huyo, alimthamini, aliwakataa wanaume wengi kwa ajili yake.
Mbali na hayo yote, alipoteza muda wake mwingi lakini mwisho wa siku, mvulana yuleyule aliyekuwa akimpenda, yuleyule aliyekuwa akimthamini alimfanyia jambo baya, alimsaliti kwa msichana mwingine wa Kiarabu, yalikuwa ni maumivu makali mno.
“Acha kulia Latifa kana kwamba huyajui mapenzi. Mapenzi ni safari tu, mapenzi yanafanana na mchezo wa mpira, kuna wakati mwingine unachezewa faulo, yeah! Hata kwenye mapenzi faulo zipo, usitegemee dakika zote mchezo utakuwa na amani tu. Kwenye mapenzi, hizi ndiyo faulo, unaweza kumpenda asiyekupenda, au unaweza kumjali mtu asiyekuwa na habari na wewe, sasa unajiliza nini? Hebu nyamaza, endelea na safari, machozi yako hayaweza kuuahirisha mchezo huu, pigana dada,” alisema Ibrahim maneno yaliyoungwa mkono na Nusrat.
“Kumbe ndiyo haka kadada ulikokuwa unakazungumzia?” aliuliza Nusrat.
“Yeah! Ndiyo hakahaka, unakaonaje baby?”
“Mmmh! Sasa kanajiliza nini?”
“Achana naye. Hakujua kama fimbo ya mbali haiui nyoka? Hebu tuendelee na mambo yetu,” alisema Ibrahim.
Alijua kwamba kuna watu waliumizwa mapenzini, alijua kwamba kuna watu walidharaulika kwa wapenzi wao, lakini kwa kile alichokuwa amefanyiwa siku ile, kilikuwa ni zaidi ya dharau, kilikuwa ni zaidi na maumivu makali moyoni mwake.
Alimwangalia Ibrahim, hakutaka kuamini kama yule ndiye kijana yuleyule aliyekuwa akimfuatilia shuleni kwao, kijana mchafu, asiyejua hata kuchana nywele, mwenye nguo zilizochakaa, asiyekuwa na uwezo wowote ule.
Leo, kijana huyohuyo aliyejaribu kuyabadilisha maisha yake ndiye aliyesimama mbele yake na kumletea dharau, moyo wake ulimuuma mno, kuna kipindi alihisi kama alikuwa usingizini, alikuwa akiota ndoto mbaya na muda mfupi angeshtuka kutoka usingizini.
“Nashukuru, nashukuru Ibrahim,” alisema Latifa huku akirudi garini.
“Poapoa, msalimie bwana Issa, mwambie naendelea vizuri,” alisema Ibrahim na hapohapo Nusrat kuanza kucheka, kicheko kilichotoka kwa dharau kubwa, kicheko kilichoongeza maumivu makali moyoni mwa Latifa.
“Utakuja tu,” alisema Latifa, akaufungua mlango wa gari na kuingia ndani. Alichanganyikiwa kupita kawaida.

Latifa alichanganyikiwa mno, kitendo cha kuona mpenzi wake aliyempenda na kumthamini akiwa amezama katika mapenzi ya mwanaume mwingine, moyo wake ulimuuma mno.
Akaliegesha gari lake katika eneo la maegesho ya magari nyumbani kwao na kisha kuteremka. Akaanza kutembea harakaharaka kuufuata mlango wa kuingia ndani kwao. Mashavu yake yaliloanishwa na machozi yaliyokuwa yakimbubujika kwa maumivu makali, kwa kuwa hakukuwa na mtu mwingine ndani ya nyumba zaidi ya mfanyanyakazi wa ndani, akaingia chumbani kwake.
Akakifuata kitanda, akakikalia na kuuchukua mto na kuuegemea huku akijifuta machozi yaliyokuwa yakimbubujika. Taswira za tukio lililopita ziliendelea kujirudia kichwani mwake kama mkanda wa filamu na kadiri alivyoendelea kukumbuka, aliumia zaidi.
“Ibrahim....nimekufanya nini mpenzi? Kwa nini umeamua kuniumiza hivi? Kwa nini mpenzi? Naomba unionee huruma, rudi kwangu, ninaumia, naomba uje kunifariji,” alisema Latifa huku akilia kama mtoto.
Huo ulikuwa mwanzo wa maumivu makali. Alimpenda sana Ibrahim na hakutaka kuona akiondoka kirahisi mikononi mwake. Alikumbuka kwamba alipoteza muda wake mwingi kumfikiria, aliwakataa wanaume wengi kwa ajili yake, leo kuona akiondoka mikononi mwake, tena kirahisi namna ile, lilikuwa jambo gumu mno.
Alichokifanya, siku iliyofuata akaondoka na kurudi kulekule Osterbay, sehemu walipokuwa na wachoraji wengi, alitaka kumuona kwa mara nyingine Ibrahim kwani hakuamini kama kile kilichotokea jana kilikuwa cha kweli au la.
Alipofika hapo, akamkuta Ibrahim akiwa peke yake, akateremka garini na kuanza kumsogelea. Kitendo cha Ibrahim kumuona Latifa, akakunja sura yake, hakufurahishwa na uwepo wake mahali hapo.
Ibrahim hakumpenda Latifa, kitendo cha kusogelewa, akaanza kumtukana. Alimtukana na kumdhalilisha kwa kumuita malaya, kumshobokea mtu asiyempenda. Latifa aliumia sana lakini neno moja tu ndilo alilokuwa akimwambia kwamba alimpenda.
“Ninakupenda,” alisema Latifa huku akilia kama mtoto na watu wakiwa wamesogea kuangalia kilichokuwa kikiendelea.
“Huna hadhi ya kutembea na mimi, mbona unakuwa na shobo wewe binti, hebu jiangalie, una hadhi ya kutembea na mimi? Kama nilishawahi kutembea na wewe hiyo kitambo tu, sahau, hebu toka niendelee na kazi yangu,” alisema Ibrahim kwa sauti ya juu, watu wote waliokuwa wakipita njia, wakasimama, na hata waliokuwa wakiyaendesha magari yao, walipoliona tukio hilo, wakasimama na kuwaangalia.
“Ninakupenda.....”
“Mimi sikupendi. Tokaaaaaaa....”
“Ninakupenda, ninakupenda Ibrahim, naomba usinifanyie hivi, kumbuka tulipotoka, kumbuka ulivyokuwa nyuma, yakumbuke maisha yako Ibrahim, msichana uliyenaye hakupendi, hata kama angeikuta hali uliyokuwa nayo zamani asingekupenda, Ibrahim, naomba ukumbuke, naomba vuta kumbukumbu mpenzi wangu,” alisema Latifa huku akianza kulia.
“Nani mpenzi wako? Mimi mpenzi wako? Hebu toka huko, unaniambia kuhusu historia inanihusu nini?” alisema Ibrahim kwa dharau, tena akiona sifa kwa watu waliowazunguka.
“Dada nenda zako tu, huoni aibu hilo limwanaume linavyokukashifu,” alisikika msichana mmoja akiongea, alionekana kushikwa na hasira.
Bado Latifa hakuwa radhi kuondoka. Maneno aliyoongea Ibrahim yalimuumiza mno lakini hakutaka kuondoka kirahisi. Alijua fika kwamba mvulana huyo alikuwa akimpenda mno ila kutokana na uwepo wa Nusrat ndiyo uliombadilisha moyo wake. Hakutaka kukubali, alichokitaka kwa wakati huo ni kuyarudisha mapenzi ya Ibrahim kwake kitu kilichoonekana kuwa kigumu kama kudeki bahari.
Kila alichokifanya kilishindikana, akarudi nyuma, akaingia garini, akapandisha vioo na kuanza kulia. Hiyo ilikuwa ni mara ya pili kukataliwa na mvulana huyo, alipoliwasha gari lake na kuondoka, moyo wake ukajiahidi kwamba asingerudi tena mahali hapo.
“Kuna nini? Mbona unalia sana?” aliuliza Dorcas.
“Kichwa kinauma.”
“Sasa ndiyo ulie namna hiyo?”
“Ndiyo.”
Alichokifanya Dorcas ni kutoka chumbani na kwenda kumchukulia dawa, akampa na kunywa. Bado kilio kiliendelea, hakunyamaza kwani kila alipokumbuka, moyo wake ulimuuma mno.
Aliendelea na maisha yake nchini Tanzania, baada ya kukatika miezi miwili, yeye na Dorcas wakarudi nchini Marekani kuendelea na maisha huku moyo wake ukiwa na jeraha kubwa la mapenzi, chuki dhidi ya Ibrahim ikaanza kuchipua moyoni mwake.
****
Kilikuwa kipindi cha baridi kali nchini Marekani, theluji zilidondoka ardhini na kuzifunika kabisa barabara kiasi kwamba ilikuwa ngumu mno kwa magari kupita kwani sehemu kubwa ya ardhi ilikuwa imefunikwa na theluiji hizo zilizoendelea kudondoka.
Kilikuwa kipindi kibaya mno ambacho hakikupendwa na Wazungu wengi kwani kiliwapa tabu sana wakati wa kuelekea kazini hata vyuoni kutokana na msongamano mkubwa wa magari uliosababishwa na magari makubwa yaliyokuwa na kazi ya kusafisha barabara kwa kuziondoa theluji hizo.
Katika kipindi hicho ambacho theluji zilikuwa zikidondoka, msichana Latifa alikuwa amejikunyata kitandani, alikuwa akihisi baridi kali mno kiasi kwamba hata lile branketi alilokuwa amejifunika aliona kutokumsaidia kabisa.
Mbali na baridi hilo, mashavu yake yalilowanishwa namachozi yaliyoendelea kumbubujika kila alipokuwa akikumbuka kile kilichotokea nchini Tanzania. Mapenzi mazito aliyokuwa nayo moyoni mwake yaligeuka na kuwa sumu kali yenye kuumiza ambayo iliujeruhi moyo wake kwa kiasi kikubwa mno.
Hakutaka kwenda darasani, alitamani kuendelea kubaki chumbani mule kwani kwa jinsi moyo wake ulivyokuwa kwa kipindi hicho, hakuona kama angeweza kusoma vizuri kutokana na jinsi alivyojisikia.
Huku akiendelea kumfikiria Ibrahim na mambo yote aliyomtendea, mara simu yake ikaanza kuita, alipoichukua na kuangalia jina, alikuwa Liban, mvulana wa Kihindi ambaye hakuacha kumwambia kwamba alimpenda.
“Where are you?” (Upo wapi?) lilikuwa swali la kwanza alilouliza Liban.
“In my room. What do you want?” (Chumbani kwangu. Unahitaji nini?)
“I want to see you,” (Nataka nikuone)
“It is impossible, I’m busy, see you later, bye,” (Haiwezekani, nipo bize, tutaonana baadaye, kwa heri) alisema Latifa na kukata simu.
Moyo wake uliwachukia wanaume, kila aliyekuwa akimwangalia, alimuona kuwa Ibrahim ambaye kwake alimchukulia kuwa na roho mbaya. Kwa Liban, hakubaki kimya, bado aliendelea kumpigia simu msichana huyo lakini hakuwa akiipokea kabisa.
Liban hakuridhika, mara baada ya kuona simu yake haikuwa ikipokelewa, akaanza kumtumia meseji nyingi za kimapenzi huku akiendelea kusisitiza ni kwa jinsi gani alikuwa akimpenda msichana huyo.
Kwa Latifa, ni kama moyo wake aliuvisha koti, hakutaka umuone mtu yeyote yule, alihitaji kuishi peke yake katika kipindi chote cha maisha yake. Mwaka huo ukakatika na mwingine kuingia.
Hakutaka kurudi nchini Tanzania, alitaka kuendelea kuishi hukohuko hivyo akaomba ruhusa kwa mama yake mlezi, bi Rachel ambaye alimkubalia japokuwa moyoni alijisikia vibaya.
Siku ziliendelea kukatika, uzuri wa latifa haukupungua, kila siku alionekana mrembo kupitiliza, wanaume waliendelea kumbabaikia lakini hakuwa radhi kuwa nao tena kipindi hicho.
Baada ya kumaliza mwaka wa mwisho wa kusoma elimu ya sekondari ndipo alipoanza masomo ya biashara katika Chuo cha UCLA ((University of California, Los Angeles).
Hapo, bado sifa za uzuri wake ziliendelea kuwa gumzo kila sehemu, watu hawakuacha kumsifia, kila alipopita, wanaume walibaki midomo wazi. Latifa hakuwa na habari na mtu, alihamia chuoni hapo peke yake baada ya kufanya vizuri katika masomo yake.
Baada ya kusoma kwa mhula wa kwanza, akakutana tena na mtu aliyekuwa akimfuatilia sana toka kitambo, huyu alikuwa Liban. Latifa alipomuona tu, akashtuka, hakutegemea kumuona mwanaume huyo chuoni hapo.
“Unafanya nini hapa?”
“Nimekuja kusoma, kama wewe.”
“Kumbe ulifaulu?”
“Ndiyo! Nilipelekwa nchini India kusoma, ila nisingeweza kuwa mbali nawe, hata kama unanikataa, siyo tatizo, kukuona kila siku moyo wangu unafarijika,” alisema Liban maneno yaliyoanza kuubadilisha moyo wa Latifa.

ITAENDELEA

CHANZO : BURE SERIES
 
SEHEMU YA TANO

Huo ulikuwa mwanzo wa ukaribu wao, wawili hao, Latifa na Liban walikuwa pamoja kila sehemu walipokuwa. Walisoma darasa moja huku kila walipokuwa wakiingia darasani, walikaa karibukaribu hali iliyoyafanya wanaume wote kugundua kwamba wawili hao walikuwa na uhusiano wa kimapenzi.
Hiyo haikuwa kazi nyepesi kwa Liban, ni kweli alimpenda mno Latifa lakini kila alipoingizia suala la uhusiano wa kimapenzi, Latifa hakutaka kukubaliana naye, bado maumivu ya Ibrahim yaliendelea kukumbushwa moyoni mwake.
Siku ziliendelea kukatika, Liban hakutaka kusikia wala kuelewa, kila alipoambiwa sitaki, hakukata tamaa, aliendelea kumwambia zaidi mpaka Latifa akachoka na mwisho wa siku, bila kulazimishwa, akajikuta akianzakubusiana na kijana huyo na hatimaye midomo yao kugusana, kilichofuata ni kubadilishana mate tu.
“Ninakupenda Latifa,” alisema Liban, alimkazia macho msichana huyo, hisia kali za kimapenzi zilionekana machoni mwake.
“Ninakupenda pia, lakini.....”
“Lakini nini?”
“Naomba usiniumize,” alisema Latifa kwa sauti ya chini.
“Siwezi kufanya hivyo, siwezi kukufanya kama huyo mpumbavu,” alisema Liban huku akiachia tabasamu pana.
Liban akawa mtu mwenye bahati mno, wanaume wengi chuoni hapo UCLA walijaribu kumfuatilia Latifa lakini mwisho wa siku walikataliwa katakata, kitendo cha Liban kumchukua kulikuwa na wanaume wengi walioumia.
Latifa hakutaka kuliacha penzi la Liban, kwa kipindi kichache alichokuwa naye alimfanya kujisikia amani moyoni mwake, ile furaha ya mapenzi ambayo watu wengi walikuwa wakiizungumzia, ikaanza kuingia moyoni mwake.
Siku zikaendelea kukatika, mpaka mwaka huo unakatika na mwaka mwingine kuingia, wawili hao waliendelea kuwa pamoja huku kila mmoja akimpa mwenzake ahadi ya kuoana na kuishi pamoja.
Mwaka wa pili ulipomalizika, wakati wa likizo ndipo Liban akamwambia Latifa kwamba angependa aende naye nchini India kwa ajili ya kuwaona wazazi wake na hatimaye waweze kufunga ndoa kwani umri ulikuwa unaruhusu.
Latifa hakuamini, hakumkatalia Liban, walikuwa wamebakiza mwaka mmoja tu wamalize chuo hivyo hiyo ikaonekana kuwa nafasi yake kujiandaa kwa ajili ya ndoa, baada ya wiki moja, wakapanda ndani ya ndege na kuelekea India.
Safari kutoka nchini Marekani mpaka India ilichukua masaa ishirini na saba ndipo ndege ilipoanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Indira Gandhi uliokuwa katika Jiji la New Delhi. Ndege iliposimama, abiria wakaanza kuteremka na kuelekea nje ya uwanja huo na kwenda kuchukua mizigo yao.
“Uliwaambia wazazi wako kuhusu mimi?” aliuliza Latifa huku uso wake ukitawaliwa na tabasamu pana.
“Hapana, ila niliwaahidi kwamba nitawafanyia sapraizi.”
“Mmmh!”
“Usiogope kipenzi, wewetwende tu, watafurahi sana mana’ke walinisisitiza sana kuhusu kuoa,” alisema Liban huku akionekana kuwa na furaha tele.
Walipofika nje ya uwanja huo, wakachukua teksi na kuanza kuelekea katika Mtaa wa Aurangzeb uliokuwa hapo New Delhi, mtaa uliokaliwa na matajiri wakiwepo waigizaji kama Aksey Kumar na Sunil Shetty.
Kutokana na wingi wa magari na Bajaj barabarani, walichukua nusu saa mpaka kufika katika mtaa huo. Teksi ikaelekea mpaka kwenye nyumba moja ya kifahari na kuanza kupiga honi, geti likafunguliwa na gari kuingizwa.
Wasichana wawili waliokuwa ndugu zake Liban wakalikimbilia gari hilo kwani walikuwa na taarifa kwamba kaka yao angefika nyumbani hapo siku hiyo.
Nyuso zao zilikuwa na tabasamu pana, hawakuamini kama kaka yao angefika siku ile nyumbani pale kutokea nchini Marekani alipokuwa akisoma. Walishindwa kuzizuia furaha zao, walipomuona akiteremka kutoka garini, wakamsogelea na kumkumbatia kwa furaha.
Hapohapo, mlango wa upande wa pili ukafunguliwa na Latifa kuteremka, hawakuonekana kushtuka kwa kuhisi kwamba yule hakuwa mgeni wao kwani teksi ile ilikuwa imekodiwa na Wahindi walikuwa na tabia ya kukodisha teksi moja zaidi ya watu watatu kutokana na idadi kubwa ya watu.
Wakamwangalia Latifa huku tabasamu yakiendelea kuwepo nyusoni mwao. Liban akaona kwamba hiyo ndiyo ilikuwa nafasi pekee ya kumtambulisha Latifa hata kabla hawajaingia ndani.
“Is she with you?” (Yupo pamoja nawe?) aliuliza dada mmoja.
“Yeah! She is my fiancee,” (Ndiyo! Ni mchumba wangu) alisema Liban huku akiwa na tabasamu pana.
“What do you say?” (Unasemaje?) aliuliza dada mmoja huku akijifanya kutokusikia kile kilichokuwa kimesemwa na Liban. Hivyo akarudia.
Hapohapo, tabasamu yakatoka nyusoni mwao, wakaanza kumwangalia Latifa kwa macho ya chuki, hawakuvutiwa naye hata mara moja. Liban akaligundua hilo, alichokifanya ni kumsogelea Latifa na kumvutia kwake kwani hakutaka ajisikie vibaya juu ya kilichokuwa kikiendelea.
“She is slut..” (Ni mwanamke mchafu..) alisema dada mwingine.
Mpaka kufikia hapo, hakukuwa na kitu cha kuficha kwamba Latifa hakuwa akihitajika ndani ya familia hiyo. Maneno yale yalimchoma mno lakini hakutaka kuonekana kama alichomwa sana, hivyo akaanza kulilazimisha tabasamu usoni mwake.
Hata nguvu za kuchukua begi lake hakuwa nazo, ni Liban ndiye aliyelichukua na kuanza kuelekea ndani. Si dada wale tu waliokuwa wakimchukia Latifa bali kila alipoonekana na watu ndani ya nyumba ile, alikuwa akichukiwa mno, hakupendwa hata kidogo.
Hakupokea mapokezi yale aliyoambiwa kwamba angepewa, mapokezi yale yalikuwa ni ya tofauti sana na maneno ya Liban, akabaki akisononeka moyoni mwake huku akitamani kurudi nyuma na kuondoka.
“Liban. Huyu ni nani?” aliuliza mama yake Liban, alikuwa amemvuta mtoto wake pembeni, japokuwa aliamini kwamba alizungumza kisiri, lakini Latifa aliweza kuyasikia maneno yale.
“Ni mchumba wangu.”
“Hapana. Huyu si mchumba wako, toka lini umeona ndugu zako wakioa wanawake wenye mchanganyiko? Hawa ni wachafu. Haiwezekani, huwezi kuwa na mwanamke mchafu. Mimi kama mama yako, nakwambia simtaki huyu mwanamke, hii ni laana,” alisema mama yake Liban.
“Lakini mama...”
“Nimesema simtaki...” mama Liban alisema kwa sauti kubwa kabisa.
Liban hakuwa na nguvu, alimheshimu sana mama yake na alimuahidi kwamba isingeweza kutokea hata siku moja akamvunjia heshima yake. Kitendo cha kuambiwa kwamba hakuwa akimtaka Latifa kuingia katika familia yao, kilimuuma sana.
Alichokifanya ni kuwapigia simu ndugu zake wengine ili waje wamwambie mama kwamba Latifa alikuwa ni chaguo lake. Kitu cha ajabu, kila ndugu aliyefika mahali pale na kumuona Latifa, hakumtaka, hawakutaka kumuona kabisa Latifa.
“Ni mwanamke mchafu, unatuletea laana kwenye ukoo,” alisema mjomba wake ambaye alimuamini kwamba alikuwa pamoja naye kwa kila kitu.
Ilikuwa ni afadhali kupigwa na risasi au kuchomwa moto, maumivu aliyoyasikia Latifa yalikuwa makubwa mno. Akajikuta akilengwa na machozi na hatimaye kuanza kububujika mashavuni mwake.
Alitamani kupotea ghafla kama mchawi na hatimaye kuibukia Tanzania, hilo halikuwezekana, kila ndugu aliyefika mahali pale, hakumtaka Latifa, sababu kubwa ikiwa ni mchanganyiko wa rangi, aina ya watu ambao walitengwa mno nchini India.
“Kwa nini mimi Mungu?” alijiuliza Latifa huku akianza kulia kama mtoto.

Latifa alitia huruma, kila muda Liban alipokuwa akimwangalia, alitamani kulia, hakukuwa na siku ambayo alimuonea huruma mtu kama siku hiyo. Moyo wake ulimpenda mno msichana huyo, kwake, alikuwa kama pumzi, alikuwa tegemeo kubwa mpaka kumpa ahadi kwamba angemuona na kuwa mama wa watoto wake, lakini mwisho wa siku, ndugu, na watu wengine wa karibu hawakumtaka msichana huyo.
Alitamani kubadilisha matokeo, ndugu zake wakubaliana naye na kuondokana na dhana potofu kwamba Latifa alikuwa na laana kutokana na mchanganyiko wake wa rangi. Ndugu wale hawakutaka kunyamaza, bado waliendelea kulalamika kwamba Liban hakutakiwa kuwa na mwanamke kama Latifa.
Latifa hakutaka kuendelea kubaki nyumbani hapo, alichokifanya ni kusimama, akachukua mabegi yake na kuondoka nyumbani hapo. Kitu kibaya ambacho kilimshangaza sana ni kwamba Liban hakuweza kumfuata, yaani ni kama mwanaume huyo alikubaliana na wazazi wake.
“Ninawachukia watu wa nchi hii,” alisema Latifa huku akilia kama mtoto.
Alitembea barabarani huku kichwa chake kikiwa chini, machozi yalikuwa yakimbubujika, kadiri alivyojitahidi kuyafuta, hayakukata, yaliendelea kutoka zaidi na zaidi. Safari yake hiyo ikaishia mbele ya hoteli kubwa ya Mumbai, hapo ndipo alipoamua kuchukua chumba, hakutaka kukaa sana, akapanga kuondoka kurudi Tanzania siku inayofuata.
****
Mapenzi yalikuwa motomoto, Ibrahim na Nusrat walijiona kuwa miongoni mwa wapenzi waliokuwa wakipendana kwa dhati kuliko watu wowote wale katika dunia hii. Muda wote walikuwa pamoja, walitaniana na kubusiana kila walipokuwa.
Kila mmoja kichwa chake kilifikiria ndoa tu, walipita vizingiti vingi vya wazazi, ndugu, jamaa na marafiki na mwisho wa siku, wote hao walikubaliana waache na hatimaye waweze kufunga ndoa na kuishi pamoja.
Kwa Ibrahim, furaha iliongezeka zaidi, kila alipokuwa akikaa, alimfikiria msichana huyo ambaye kwake alionekana kuwa kila kitu. Baada ya siku kadhaa kupita, Ibrahim akajikuta akianza kuwa karibu na mwanaume mmoja, alionekana kuwa mzee wa makamo, alikuwa na ndevu nyingi zilizokuwa na mvi, alionekana kuchoka hali iliyoonyesha kwamba maisha yalimpiga sana.
Alikutana na mzee huyu wakati akielekea Posta kwa ajili ya kukamilisha michoro yake ambayo alitakiwa kumkabidhi Balozi wa Uingereza kama zawadi pekee kutoka kwa Watanzania kabla ya kuelekea nchini mwake.
Alipokutana na mzee huyo aliyekuwa ombaomba barabarani, akajikuta akifunga breki na kuteremka. Hakujua sababu iliyomfanya kuwa na huruma kiasi hicho, alionekana kuvutiwa na mzee yule, akaufungua mlango na kuanza kumfuata.
“Naomba unisaidie hela ya kula,” alizungumza mzee yule, mavazi yake yalikuwa yamechakaa sana.
“Chukua hii,” alisema Ibrahim huku akimkabidhi mzee yule noti ya shilingi elfu kumi.
Hakutaka kukaa sana, ndani ya gari, alikosa amani, kila wakati alikuwa akimfikiria mzee yule ambaye kwake alionekana kuwa na uhitaji mkubwa. Hakutaka kuficha hisia zake, akampigia simu Nurat na kumwambia kuhusu mzee huyo.
“Ni vizuri kusaidia watu wasiojiweza,” alisema Nusrat.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa urafiki baina ya mzee masikini, ombaomba na Ibrahim. Mara kwa mara alikuwa akimfuata na kuzungumza naye mambo mengi ambayo kwa Ibrahim, yalimsisimua sana.
“Kwa hiyo ikawaje mpaka ukawa ombaomba?” aliuliza Ibrahim, alitegesha masikio yake kumsikiliza mzee yule ambaye pasipo kutegemea, akaanza kububujikwa na machozi, swali aliloulizwa, likazifanya kumbukumbu zake kurudi nyuma, akaanza kulia.
“Duniani kuna watu wabaya sana, duniani hapa, kuna watu wenye roho mbaya sana,” alisema mzee yule masikini.
“Kwa nini?”
“Nimepitia maisha magumu sana, sina kitu, nimepoteza kila kitu maishani mwangu,” alisema mzee yule.
Sauti yake ilikuwa ya chini sana, alizungumza huku akionekana kuwa na maumivu makubwa ya moyo. Kila alipoongea kidogo, alinyamaza, akameza fundo la mate na kuendelea.
Mzee huyo alimuhadithia Ibrahim mambo mengi huku akimbariki kwa kila kitu atakachokifanya katika maisha yake ya mbele. Ibrahim aliporidhika, akamuaga mzee yule tayari kwa kuondoka. Akajikuta akishikwa mkono, akageuka na kumwangalia mzee yule.
“Katika kila ukifanyacho, kumbuka kitu kimoja,” alisema mzee yule, alikuwa amemkazia macho Ibrahim.
“Kitu gani?”
“Usimfanye mwanamke akalia.”
“Nisimfanye mwanamke akalia?”
“Ndiyo! Kila chozi la mwanamke linalodondoka, huwa na laana nzito sana,” alisema mzee huyo.
“Kivipi?”
“Nipo hapa kwa sababu ya chozi la mwanamke, nipo hapa kwa kuwa nilimfanya mwanamke kulia. Hakika ningejua kama haya yangetokea, hakika ningemfanya kuwa na furaha milele, nisingeruhusu kuliona chozi lake,” alisema mzee yule, akanyamaza, akakiinamisha kichwa chake chini, akaanza kulia tena.
“Nyamaza sana mzee. Lakini kwa nini unaniambia hivi?”
“Ni kwa sababu wewe ni rafiki yangu, sipendi upate majanga kama niliyoyapata mimi, ninatamani uje kuwa na furaha kubwa maishani mwako,” alisema mzee yule.
“Maneno yako yananitisha.”
“Si kwamba nakutisha, ila ninakwambia njia za kufanikiwa, njia za kuiepuka laana maishani mwako,” alisema mzee yule.
“Usijali mzee, nitakuwa nikija mara kwa mara,” alisema Ibrahim na kuondoka. Moyoni mwake hakuweza kukumbuka chochote kuhusu Latifa japokuwa maneno yale yaliutesa sana moyo wake.
****

ITAENDELEA

CHANZO : BURE SERIES
 
SEHEMU YA SITA

Usiku hakulala, muda wote macho yake yalikuwa wazi huku akiangalia juu tu. Kichwa chake kilikuwa na mawazo lukuki, hakuamini kile kilichokuwa kimetokea nyumbani kwa mpenzi wake mara baada ya kwenda kutambulishwa.
Mpaka asubuhi inaingia, Latifa hakuwa amepata hata lepe la usingizi, usiku mzima alikuwa na mawazo tu. Hakutaka kuendelea kukaa nchini India, akajiandaa, akawasiliana na ofisi za kampuni ya ndege ya Indian Airlines na kuhitaji kuwekewa tiketi moja ya kwenda nchini Tanzania, hilo halikuwa tatizo.
“Kwa nini nina mkosi hivi? Kwa nini yote haya yananitokea mimi tu?” alijiuliza lakini hakupata jibu, bado alijiona kuwa na mkosi mkubwa maishani mwake.
Ilipofika saa kumi jioni, tena huku akiwa hajaingiza kitu chochote mdomoni, akaondoka hotelini hapo kuelekea uwanja wa ndege na ilipofika saa kumi na mbili jioni, akapanda ndege na kuanza kuelekea nchini Tanzania huku akiwa na majonzi makubwa moyoni mwake.
Kama kulia alilia sana lakini hakubadilisha kitu, kila kitu kilichokuwa kimetokea, kilitokea na hivyo alitakiwa kusahau kila kitu. Alipofika jijini Dar es Salaam, Latifa akapokelewa kwa shangwe kwa kuwa alifanikiwa sana katika elimu yake.
Alikuwa msichana mwenye uwezo mkubwa mno, alijijengea heshima kubwa chuoni kutokana na uwezo wake kuwa mkubwa, kila mtu akajivunia kuwa na mtu kama yeye hasa katika familia ya bi Rachel.
Siku zikaendelea kwenda mbele mpaka pale alipotakiwa kurudi tena chuoni nchini Marekani, akarudi zake. Chuoni huko, hakukutana tena na Liban, mwanaume huyo alikuwa amehama chuo na kuelekea katika Chuo cha Mumbai nchini India, hakurudi tena nchini Marekani.
Uzuri wa Latifa ukaendelea kuwa gumzo, hakujua ni nani aliwaambia watu kile kilichotokea, baada ya wiki kadhaa tu, kila mmoja alifahamu kilichoendelea nchini India na hivyo kumpa pole sana.
Hakutaka kujali tena, kila kitu kilichotokea maishani mwake alikichukulia kama changamoto. Japokuwa kwake ilikuwa ngumu kumsahau Liban lakini hakuwa na jinsi, baada ya miezi miwili tu, kumbukumbu juu ya Liban zikaanza kupotea kichwani mwake.
Uwezo wake wa darasani ulikuwa uleule, watu walimshangaa sana, darasani hakuwa mtu wa kawaida hata mara moja. Wanafunzi wengi walimfuata na kuanza kufundishwa naye, Latifa alikuwa tofauti huku wanachuo wengine wakisema kwamba msichana huyo alikuwa na uwezo mkubwa zaidi ya maprofesa chuoni hapo.
“Naomba kuuliza swali,” alisema Latifa, walikuwa darasani walipokuwa wakisoma.
“Uliza,” alisema profesa huku akiiweka vizuri miwani yake, kila mtu alimheshimu Latifa, hivyo kila alipoinuka na kutaka kuzungumza kitu, watu wote walikuwa kimya.
“Bila shaka mtu wa kwanza kutengeneza gari, alifikiria kuhusu gari tu na wala hakufikiria kwamba kuna mtu angekuja na kutengeneza ndege, si ndiyo?” aliuliza Latifa.
“Ndiyo!” alijibu profesa.
“Hivi kwa nini huyu mtu aliyekuja na kugundua ndege hakufikiria kutengeneza gari lenye miguu kumi badala ya minne?” aliuliza Latifa.
“Unamaanisha nini?”
“Nataka kufahamu tu.”
“Mmmh! Sijui kwa nini hakufikiria hilo.”
“Sawa. Lakini, kama Alexander Bell aligundua simu ya mezani, kwa nini mtu aliyegundua simu ya mkononi asigegundua simu za aina nyingine zinazotumia waya?” aliuliza Latifa.
“Napo sijui.”
“Kuna chochote unachojifunza kutokana na maswali yangu?”
“Hapana. Unamaanisha nini?”
“Kama jopo la madaktari duniani walikaa kwa ajili ya kutafuta dawa za kuua kansa iliyokomaa, wakakosa, hivi hatuwezi kuwa kama mtu aliyegundua ndege na simu za mkononi? Yaani namaanisha kwa kwenda mbele na kufikiria kitu kingine zaidi?” aliuliza Latifa.
“Unamaanisha nini?”
“Najua umeshajua ninachokimaanisha. Ninataka kutengeneza dawa za kuteketeza kansa katika dunia hii,” alisema Latifa kwa kujiamini.
“Unasemaje?” aliuliza profesa huku akiishusha miwani yake na kumwangalia vizuri Latifa.
“Ninataka kutengeneza dawa ya kansa, hiyo dawa itaitwa Morphimousis, nikwambie kitu profesa? Itakwenda kuokoa maisha ya watu wengi, niamini. Hii ndiyo nafasi ya kuwa bilionea ili yule Ibrahim na Liban wanitafute,” alisema Latifa, ghafla machozi yakaanza kumbubujika.
Huo ndiyo ulikuwa uamuzi aliokuwa ameuchukua, alikuwa akisomea masomo ya udaktari hivyo lengo lake kubwa kwa wakati huo lilikuwa ni kuwa daktari mkubwa ambaye angeweka historia katika dunia hii kwa kuweza kukumbukwa katika maisha yake yote, kabla na baada ya kifo.
Darasani alikuwa na akili mno, hakuwa msomaji sana lakini kila ulipokuwa ukija mtihani, kama kawaidayake alikuwa akiongoza kama kawaida yake. Latifa aliendelea kunawili kila siku lakini kwa kipindi hicho, hakutaka kuwa na mwanaume yeyote yule, alitaka kubaki peke yake mpaka atakapokufa.
Siku zilikatika, hapo ndipo alipoamua kuanza kusoma kwa juhudi hata kama alikuwa genius, alitaka kujifunza mambo mengi kuhusu mwili wa binadamu, ni kwa namna gani ulikuwa ukishambuliwa na magonjwa ya kansa na kwa namna gani angeweza kuyadhibiti magonjwa hayo.
Hilo likamfanya kushinda maabara kila siku, likamfanya kutafuta dawa nyingine ambazo alikwenda nazo humo kisha kuanza kuangalia ni kwa jinsi gani angeweza kutengeneza dawa moja ambayo ingekuwa yenye ubora mkubwa sana.
“Dawa zinapatikana kwenye miti, huko ndipo kwenyewe,” alisema Dk. Warren, alikuwa dokta mwenye uwezo mkubwa aliyeweka historia kwa kutengeneza dawa za magonjwa ya mifupa.
“Naweza nikapata wapi hiyo miti?”
“Nenda Amazon.”
“Unamaanisha msitu wa Brazil?”
“Ndiyo!”
Aliamua kwa moyo mmoja kufanya kile alichotaka kukifanya, kwenda nchini Brazil halikuwa tatizo, akajipanga na kisha kuelekea huko. Msitu ulikuwa unatisha sana lakini hakuwa na jinsi, alitakiwa kuingia na kuutafuta mti mmoja ulioitwa Mendozo, mti pekee uliokuwa na uwezo wa kutibu magonjwa mbalimbali, mti pekee ambao magome yake yalitumika kuwatibu Wabrazil.
Alipofika huko, tena huku akiwa na watu watano wenye silaha kali wakaanza kuzunguka msituni kwa malipo makubwa. Ilikuwa kazi kubwa, ya hatari na yenye kuchosha lakini hakutaka kukata tamaa, mbele yake aliyaona mafanikio makubwa, hivyo alitaka kupambana zaidi mpaka anaupata huo mti.
Walizunguka kwa kupumzika kwa kipindi cha wiki nzima na ndipo walipofanikiwa kuupata mti huo, wakachukua magome na kisha kurudi Rio De Janeiro huku kila mmoja akiwa na furaha.
Alipofika hotelini tu, kitu cha kwanza ni kuchukua magome yale na kuanza kuyafanyia kazi, alitaka kujua ni vitu gani vilikuwepo ndani ya miti ile ili mwisho wa siku na yeye aweze kuvitengeneza vitu hivyo au vinavuofanana na hivyo na mwisho wa siku kutengeneza dawa kali na yenye nguvu. Akafanikiwa katika hilo na kurudi nchini Marekani huku akiwa na sample.
“Nakwenda kuwa bilionea,” alisema Latifa, mwili ulichoka sana, alikuwa safarini kurudi nchini Marekani. Moyo wake ukafarijika mno.

Uhusiano wa kimapenzi uliwapa furaha kila mmoja, mipango yao ya ndoa iliendelea kupangwa na siku ya harusi ikawekwa tayari kwa ajili ya harusi hiyo ambayo ilionekana kufana hata kabla ya kufika.
Kila mmoja akawa na kimuemue cha kutaka kuoana, wageni wakaitwa kutoka Uarabuni tayari kwa kuhudhuria harusi hiyo kati ya Nusrat na Ibrahim. Hakukuwa na tatizo lolote lile, kila mmoja, hasa ndugu wa Nusrat walimpenda sana Ibrahim kwani ndiye alikuwa mtu pekee aliyechaguliwa na ndugu yao.
Baada ya wiki moja, hatimaye Ibrahim alivalia kanzu kubwa na kwenda ukweni kuoa. Huko, akajipatia mke wake na hatimaye maisha ya furaha kama mke na mume kuanza. Hakukuwa na mtu aliyefikiria jambo lolote lile baya, kila mmoja aliona kwamba ndoa kuwa furaha tupu pasipo kujua kwamba wakati mwingine, wanandoa hujuta sababu ya kuwafanya kuoa au kuolewa.Hawakujua hilo.
*****
Latifa akawa mtu wa kushinda maabara tu kwa ajili ya kuifanyia kazi dawa yake. Ilikuwa ni kazi kubwa lakini hakutaka kushindwa, kadiri alivyokuwa akiwafikiria wanaume walioutesa moyo wake na kumfanya kulia, hakutaka kukata tamaa kwa kuamini kwamba ni lazima angefanikiwa tu.
Siku ziliendelea kukatika, ndoto yake kubwa kwa wakati huo ilikuwa ni kuwa bilionea mkubwa baada ya kuuza dawa ya magonjwa ya kansa yaliyowatesa watu wengi duniani, hasa Wamarekani na watu wa Ulaya nzima.
Hakutaka kurudi nchini Tanzania, alikuwa bize akitengeneza dawa hiyo kwa kutumia vifaa maalumu. Wakati mwingine hakula chakula chochote kile, alishindakuanzia asubuhi mpaka usiku pasipo kuingiza chochote tumboni mwake, si kwamba hakusikia njaa, alisikia njaa lakini hakutaka kula mpaka ile hatua ambayo alitamani kuifikia kwa siku husika aifikie.
Vitabu vilimsaidia, alitumia muda wa miezi mitatu na ndipo alipoanza kuona mafanikio ya ile kazi aliyoanza nayo kwa kipindi kirefu, dawa ikaanza kukamilika kitu kilichompa furaha mno kwa kuona sasa alikuwa njiani kutimiza ndoto yake.
Hakutaka kufanya siri, alichokifanya ni kumpigia simu Dk. Dickson Myles kwa ajili ya kufika hapo maabara na kumuonyeshea kile alichokuwa amekitengeneza.
“Unaionaje?” aliuliza Latifa, usoni alikuwa na tabasamu pana.
“Ipo vizuri, umefanyaje mpaka ukapata hii dawa?” aliuliza Dk. Myles huku akionekana kushangaa.
“Ni kazi kubwa na ngumu iliyohitaji mtu ujitoe sana, usijali. Nahitaji unifanyie mipango ili niweze kukamilisha kila kitu,” alisema Latifa.
Hakutaka kumwamini mtu yeyote yule, alitumia muda mwingi sana kutengeneza dawa ile na aliona kama angemwambia mtu yeyote yule namna alivyotengeneza dawa ile basi watu wangeweza kuiga na hivyo kutengeneza haraka na kuisambaza hata kabla hajaisambaza yeye. Hakutaka kuona hilo hivyo alifanya kila kitu kuwa siri kubwa.
Baada ya siku tatu, Dk. Myles akafika na Waziri wa Afya nchini Marekani, Bwana Brian Peterson kwa ajili ya kuiona dawa hiyo. Latifa hakuwa na jinsi, aliamini kwamba huo ndiyo ungekuwa mwanzo wake hivyo akamuonyeshea.
Haikuwa dawa ya vidonge, ilikuwa ni ya kimiminika ambayo ilitakiwa kuhifadhiwa kwenye chupa na mgonjwa alitakiwa kunywa na baada ya mwezi mmoja angepona kabisa na kuwa mzima.
Kilichofanyika ni kumpigia simu dokta mkuu wa Hospitali kubwa ya St. Augustino Medical Center ambaye alifika mahali hapo na kuanza kuiangalia. Alikubaliana nayo kwa asilimia kadhaa na hivyo ilitakiwa kufanyiwa marekebisho hata kabla ya kupitishwa na kuanza kutumika.
Kulikuwa na watu wengi mno nchini Marekani waliokuwa wakisumbuliwa na magonjwa ya kansa hivyo hata tangazo lilipotolewa kwamba kulihitajika wagonjwa wawili waliosumbuliwa na kansa kwa ajili ya kufanyiwa matibabu, walipatikana kwa haraka sana tena huku wengine wakipanga mstari hospitalini kuhitaji matibabu.
Matibabu yakaanza na hatimaye wagonjwa hao kuruhusiwa kuondoka. Latifa alibaki kimya, kipindi cha mwezi mzima ambacho alitakiwa kusubiri alikuwa na presha tele, alikuwa akimuomba Mungu ili dawa ile ifanye kazi kama ilivyotakiwa na hatimaye aweze kuwa bilionea kwa ajili ya kuiuza dawa hiyo ambayo mpaka katika kipindi hicho alikuwa amekwishaisajili.
Siku zilikatika na hatimaye mwezi kumalizika. Wagonjwa wale waliofanyiwa majaribio wakapigiwa simu na kutakiwa kufika katika hospitali hiyo haraka iwezekanavyo. Wala hawakuchukua masaa mengi, wakafika na hivyo kufanyiwa tena vipimo.
Majibu yalipokamilika, jopo la madaktari sitini wakaitwa kwa ajili ya kuipitia ripoti hiyo ya majibu ya wagonjwa wale. Walikaa katika chumba kile kwa dakika kadhaa, ripoti ilipokamilika ikaletwa na kukabidhiwa Dk. Peterson, akashusha miwani yake na kuiangalia vizuri.
“It is impossible!” (Haiwezekani!) alisema Dk. Peterson kwa mshtuko huku akiangalia majibu ya vipimo.
“What do you see?” (Unaona nini?)
Hakujibu swali hilo, alichokifanya ni kuwapa karatasi ile ya majibu na kila daktari kuanza kuiangalia. Kwa miaka yote hawakuwa wamefanikiwa kupata dawa ya kansa, walikuwa na Masters, PhD, leo hii, msichana mwenye digrii moja tu, tayari alifanikiwa kutengeneza dawa ya kansa, kila mmoja akashtuka.

Malumbano yalikuwa yakisikika kutoka katika nyumba moja nzuri na iliyoonekana kuwa ya kifahari iliyojengwa Sinza Mori. Kelele zile zilizokuwa zikiendelea ziliwafanya majirani kutokutulia, kila waliposubiri zipungue japo kidogo, zilizidi kuongezeka zaidi.
Majirani wakashindwa kuvumilia, walisubiri kwa kipindi kirefu sana kuona kelele hizo zikipungua lakini hazikupungua na hivyo kutoka ndani ya nyumba zao na kuwaamuru wanyamaze lakini hawakunyamaza.
Hiyo haikuwa mara ya kwanza kwa watu hao kulumbana, maisha yao yalitawaliwa na malumbano ya mara kwa mara, kila siku walikuwa kero kwa majirani ambao mara kadhaa waliamua kuwapeleka katika Ofisi za Serikali ya Mtaa lakini hakukuwa na mabadiliko yoyote ile.
“Hivi unanijua wewe mwanamke?” aliuliza mwanaume mmoja, kijasho chembamba kilikuwa kikimtoka, mwili wake ulitetemeka kwa hasira.
“Hivi na wewe unanijua? Unaionaje hii ngozi, unaichukulia poa, sasa utaona,” alisema mwanamke huyo.
“Unajua nitakuua wewe malaya!”
“Uniue mimi! Haloo haloo, eti uniue mimi, thubutu,” alisikika mwanamke huyo.
Huyo alikuwa Ibrahim na Nusrat. Ndoa yao ilifikisha mwaka mmoja lakini iliwaka moto. Hakukuwa na furaha ndani ya ndoa, tangu waoane na kuishi pamoja, maisha yao yalitawaliwa na malumbano ya mara kwa mara.
Walipendana kipindi cha uchumba, tu waliahidiana mambo mengi lakini ndani ya ndoa kila kitu kinaonekana kubadilika. Nusrat yule aliyekuwa, msichana yule mrembo alikuwa amebadilika.
Mara kwa mara alikuwa akirudi nyumbani usiku, tena akisindikizwa na wanaume wake, watoto wa Kiarabu walioonekana kuwa na fedha nyingi, alipofika nyumbani, hakutaka kuzungumza na mume wake, moja kwa moja alikuwa akiingia ndani kulala.
Ibrahim aliumia, alivumilia lakini uvumilivu ulifika mwisho, siku hiyo aliamua kulumbana naye, japokuwa walifanya hivyo mara kwa mara lakini siku hiyo ilionekana kuwa tofauti, alikuwa na hasira mno na kila wakati alikunja ngumi.
Nusrat hakuwa msichana aliyetulia hata kidogo, alikuwa mtu aliyehusudu sana starehe kuliko mambo mengine, mara kwa mara wanapokuwa kitandani, Nusrat hakutaka kufanya tendo la ndoa na mumewe jambo lililomuumiza mno Ibrahim.
Mbali na hivyo vyote, pajani mwa msichana huyo karibu kabisa na kiuno kulichorwa tattoo moja yenye alama ya kopa ambayo pembeni iliandikwa ‘Nakupenda Nusrat’. Hicho ndicho kilichomkasirisha sana Ibrahim kwani alijua kwamba kulikuwa na mwanaume aliyeichora tattoo hiyo pajani mwa mke wake, hivyo kila siku walipokuwa wakilumbana, ilikuwa ni lazima kuizungumzia tattoo hiyo.
“Hivi haya ndiyo malipo yako? Hivi haya ndiyo malipo unayonipa baada ya kuuacha moyo wangu ukupende kwa mapenzi ya dhati? Nusrat mke wangu! Hivi ndiyo unaamua kunilipa ubaya kwa wema? Hivi hujui kwamba nilimwacha msichana aliyenipenda kwa ajili yako? ” aliuliza Ibrahim. Hapo ndipo kumbukumbu zake za maisha ya nyuma zikaanza kumrudia kwamba aliwahi kumuacha msichana aliyempenda kwa mapenzi ya dhati kwa ajili ya Nusrat ambaye leo hii alikuwa akileta ujinga ndani ya ndoa. Alishikwa na hasira lakini hakujua ni kitu gani alitakiwa kukifanya.
“Kwani nilikulazimisha umuache? Nilikulazimisha? Hebu niache niondoke, nitarudi kesho, najisikia kukesha klabu leo,” alisema Nusrat kwa dharau kubwa, alikuwa kashavalia, alichokifanya ni kuondoka nyumbani hapo kwenda klabu.
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake ya kila siku, kila alipokwenda huko, alirudishwa na wanaume wa Kiarabu wenye gari kitu kilichomuongezea maumivu makali Ibrahim mpaka kufikia hatua ya kutamani kumuua msichana huyo.
*****
“You are very bright Latifa, you are very bright,” (Una akili sana Latifa, una akili sana Latifa) yalikuwa ni maneno yaliyosikika kutoka kwa Dk. Myles, hakuwa akiamini kama kweli ile dawa ya Morphimousis aliyokuwa ameitengeneza Latifa iliweza kuwaponya wagonjwa wale waliosumbuliwa kwa kansa.
Dawa ile ikaanza kutangazwa, Wamarekani na watu wa Ulaya ambao asilimia kubwa walikuwa wagonjwa wa magonjwa ya kansa wakamsifia Latifa na kumpa heshima kubwa japokuwa alikuwa na elimu ndogo na umri mdogo wa miaka ishirini na moja tu.
Jina lake likaanza kutangazwa, vituo vya televisheni vyote vikaanza kumtangaza kama mkombozi ambaye aliletwa duniani ili kuwaokoa watu waliokuwa wakiteseka vitandani. Ingawa Latifa alipewa sifa sana na kuonekana mtu sahihi kuletwa duniani lakini kukaanza kuibuka vuguvugu kati ya Tanzania na Marekani.
Latifa alikuwa Mtanzania lakini alisomea nchini Marekani. Nchi hiyo haikutaka kumuachia Latifa kiholela kwamba aelekee nchini Tanzania na kufanya kazi na wakati elimu kubwa aliyokuwa nayo ilitokea nchini mwao.
Latifa akagombaniwa, jina lake likazidi kupenya masikioni mwa watu wengi duniani. Kwa kuwa Marekani lilikuwa taifa kubwa, wakaamua kutumia nguvu zao nyingi kumtangaza Latifa kama Mmarekani na kuipoteza nchi ya Tanzania kiasi kwamba watu wengi duniani walijua kwamba Latifa alikuwa Mmarekani.
Kupitia dawa yake, akaanza kuingiza fedha, maisha yake yakabadilika, kutokana na ongezeko la wagonjwa wa kansa, Latifa akajikuta akiingiza kiasi cha dola milioni mia moja ndani ya wiki moja tu, hizo zilikuwa ni zaidi ya shilingi bilioni mbili.
Wakati mwingine alijiona kama yupo ndotoni na muda wowote ule angeamka kutoka usingizini, umaarufu alioupata kwa ghafla sana uliyabadilisha maisha yake. Kila siku aliingiza kiasi kikubwa cha fedha, akanunua jumba kubwa na la kifahari lililokuwa Los Angeles hapohapo Marekani.
Ili kuzuia kila kitu kutoka kwa nchi kama Tanzania iliyokuwa ikitangaza kwamba Latifa alikuwa mtu wao, hapo ndipo Wamarekani wakaamua kumuajiri msichana huyo katika hospitali kubwa ya St. Luis Medical Center iliyokuwa hapohapo nchini Marekani katika Jiji la New York.
Japokuwa hakuwa amemaliza masomo yake lakini Latifa akapewa jina la udaktari rasmi na kuanza kuhudumia wagonjwa katika hospitali hiyo. Uwepo wake mahali hapo, ukawafanya wagonjwa wengi kumiminika, hawakuamini kama msichana huyo ndiye yule aliyekuwa amegundua dawa hiyo iliyomaliza matatizo ya watu wengi.
Aliwakumbuka sana Watanzania, alimkumbuka mlezi wake, bi Rachel lakini kila alipotaka kurudi nchini Tanzania, alizuiliwa kwa kupewa majukumu mengi ya kikazi jambo lililoendelea kuzua mtafaruku mkubwa kati ya Marekani na Tanzania.
Ndani ya mwaka mmoja wa mafanikio yake, Latifa akawa daktari mwenye kiasi kikubwa cha fedha, heshima yake ikaongezeka na akawa bilionea kijana kuliko wote duniani huku akimuacha vibaya mmili wa Mtandao wa Kijamii wa WorkSpace, Williams Peters aliyekuwa na umri wa miaka ishirini na mbili.
“Ni kitu gani ambacho huwezi kukisahamu maishani mwako?” aliuliza Larry King, mtangazaji wa Kituo cha Habari cha CNN.
“Ooppss...” alishusha pumzi Latifa na kuendelea:
“Kuna watu wengi wamejeruhiwa, kuna watu wamepewa vidonda ambavyo haviwezi kupona kamwe hata kama utakuja kuwa na maisha ya mafanikio kiasi gani huko mbeleni. Kwangu, siwezi kumsahau mwanaume anayeitwa Ibrahim,” alisema Latifa na kunyamaza.
“Ndiye nani?”
Latifa akanyamaza, akaingia kwenye hali ya mawazo, ghafla akaanza kububujikwa na machozi. Kila kitu kilichotokea katika maisha yake ya nyuma kikaanza kujirudia kichwani mwake.
Chuki kubwa ikamjaa moyoni mwake, hakumpenda Ibrahim, alimnyima furaha kipindi cha nyuma, alimnyanyasa kisa tu alimpenda. Hakudhania kama ingetokea siku yoyote ile angemsamehe mwanaume huyo. Kama kulia, alilia sana, hakutaka kumpenda hata siku moja na hata kile alichomfanyia katika maisha yake, hakutaka kumsamehe hata mara moja.
“Ninamchukia Ibrahim. Ninamchukia mno,” alisema Latifa huku akiyafuta machozi yake.
“Ndiye nani?”
Hapo ndipo Latifa akaanza kusimulia kile kilichokuwa kimetokea katika maisha yake ya nyuma. Alisimulia tangu siku ya kwanza alipokutana na mwanaume huyo alipomfuata shuleni kwao. Moyo wake ukajawa na maumivu makali mno. Alimpenda na kumpa penzi lake, alimthamini lakini baada ya kusafiri na kuelekea Marekani, kila kitu kikabadilika.
“Ni kitu ambacho sitokuja kukisahau. Hata ikitokea siku nikamuona shetani na Ibrahim wapo porini wanataka kuliwa na simba na nina nafasi ya kumuokoa mmoja, nitamuokoa shetani,” alisema Latifa huku akionekana kumaanisha kile alichokisema, moyo wake ulitawaliwa na chuki kubwa dhidi ya Ibrahim, mwanaume aliyeutesa moyo wake hata zaidi ya Liban.

ITAENDELEA

CHANZO : BURE SERIES
 
SEHEMU YA SABA


Mateso yakawa mateso, Ibrahim akawa mtu wa kuhuzunika kila siku, hakuona raha ya ndoa tena, kuna kipindi alikuwa akilala peke yake chumbani, Nusrat hakuwa nyumbani, alikuwa klabu akiponda raha na wanaume wake wa Kiarabu.
Yalikuwa ni maumivu yasiyoelezeka moyoni mwake, rafiki yake mkubwa kitandani akawa mto, kila alipolia, machozi yake yalidondokea kwenye mto, kila alipohitaji faraja ya kukumbatiwa, aliukumbatia mto.
Kila kitu kikabadilika, kuna kipindi alitamani kumuacha Nusrat lakini wakati mwingine alipokuwa akifikiria kwamba msichana huyo alishughulika na vitu vingi katika maisha yake likiwepo suala la kazi, alishindwa kufanya hivyo.
Nusrat aliporudi nyumbani, hakuwa mzungumzaji sana, kila alipofika, alilala popote pale kwani pombe zilimjaa kichwani mwake. Hakuwa na muda wa kuongea na mume wake, alimuona kuwa takataka kwa kuwa alijua kwamba maisha yake yalimtegemea yeye.
Siku zikakatika, Ibrahim alipoona amechoka, ameshindwa kuvumilia, hapo ndipo alipoanza kumtafuta yule mzee ambaye alikuwa akizungumza naye kipindi cha nyuma, mzee ombaomba aliyekuwa akikaa karibu na eneo la Mnazi Mmoja kwa ajili ya kuzungumza naye.
Alipofika huko, mzee yule hakuwepo kitu kilichompa wakati mgumu, akaanza kumtafuta kwa kuulizia. Haikuwa kazi nyepesi, kila alipoulizia, hakukuwa na mtu aliyejua mahali alipokuwa, hakukata tamaa, alizunguka na kuzunguka na mwisho wa siku kufanikiwa kukutana na mtu ambaye alimuelekeza alipokuwa.
“Yule mzee alizidiwa hapa, alipelekwa hospitalini, baada ya hapo hakurudi tena. Ila yupo Magomeni Mapipa, ukifika pale, ulizia kwa mzee Majeed, mzee mwenye ndevu nyingi kama Osama, huwa anaishi nje ya nyumba ya huyo mzee, kibarazani,” alisema kijana muuza maji ambaye alimfahamu fika mzee huyo.
Ibrahim hakutaka kuchelewa, kwa kuwa alikwishapewa maelekezo ya kutosha, hapohapo akaanza kuelekea huko. Njiani alikuwa na mawazo mno, kile kilichokuwa kimetokea, kilimuumiza mno hivyo akatamani kumuona mzee yule ili amshauri juu ya kile kilichokuwa kikiendelea.
Hakuchukua muda mrefu akafika Magomeni Mapipa ambapo baada ya kuulizia kwa mzee Majeed, akaelekezwa na kuelekea huko. Mazingira aliyomkuta nayo mzee yule yalimuumia mno, hakuamini kile alichokuwa akikiona kwamba mzee masikini, aliyekuwa ombaomba alikuwa kibarazani amelala, pale alipokuwa, jua kali la saa saba liliwaka na kumuunguza lakini hakujali, hakuwa na sehemu nyingine zaidi ya hiyo. Ibrahim akahisi kulia.
Japokuwa hakuwa na fedha za kutosha lakini hakutaka kumuona mzee yule akiendelea kuishi katika maisha yale, maisha yaliyojaa umasikini mkubwa ambayo kila alipokuwa akiyafikiria, alijikuta akibubujikwa na machozi tu.
Akampangia chumba katika Mtaa wa Tandale na kumtaka kukaa huko, mara kwa mara alikuwa akielekea huko na kumsaidia kiasi fulani cha fedha ambacho aliamini kabisa kingeweza kumsaidia.
Siku zikaendelea kukatika, baada ya mwezi mmoja, aliporudi ndani ya nyumba ile aliambiwa kwamba mzee yule alikuwa amepelekwa hospitalini, kidonda kile alichokuwa nacho kiliongezeka na kilizidi kuoza japokuwa alikuwa akitumia dawa.
Ibrahim akachanganyikiwa, hakutaka kubaki mahali hapo, kwa kuwa aliifahamu Hospitali ya Mwananyamala sehemu ilipokuwa, akaanza kwenda huko. Njiani, mawazo yake yalikuwa kwa mzee huyo tu, moyoni mwake alihisi kulikuwa na kitu kilichomsukuma kumsaidia mzee yule, hakujua alikuwa na nani na alikuwa na nini, msukumo moyoni mwake ulimwambia ni lazima amsaidie mzee huyo.
Alipofika hospitalini hapo, akaingia mpaka ndani na kupewa maelekezo juu ya mahali alipolazwa mzee huyo, akaelekea huko. Alipofika nje ya chumba kile alicholazwa, akaruhiswa na kuingia ndani.
Mzee yule alikuwa kwenye maumivu makali mno ya mguu wake, kidonda kile kilipelekea mguu ule kuanza kuoza. Ibrahim alipomwangalia, alishindwa kuyazuia machozi yake, yakaanza kububujika mashavuni mwake.
“Wewe ni ndugu yake?” aliuliza daktari.
“Ndiyo! Kuna nini?”
“Hebu nifuate.”
Akaanza kuondoka na daktari yule kuelekea katika ofisi yake ambayo haikuwa mbali na chumba kile. Walipofika, wakaingia ndani na moja kwa moja kutakiwa kukaa kitini.
“Ndugu yako tumemkuta ana tatizo kubwa mguuni mwake,” alisema daktari yule.
“Tatizo gani?”
“Ana kansa ya mguu. Tuliangalia, tukagundua kwamba alichomwa na kitu chenye kutu hivyo kumletea tetenasi. Ugonjwa huu umekuwa ukiua watu wengi sana, kwake, umesababisha mguu kuoza, tukiuacha hivihivi, ni lazima ataoza zaidi kitu kinachoweza kusababisha kifo chake,” alisema daktari yule.
“Ooppss..! Kwa hiyo nini kifanyike?”
“Akatwe mguu! Hicho ndicho kinachotakiwa kufanyika ili kuokoa maisha yake,” alisema daktari yule. Ibrahim akashtuka.
*****
Alihitaji kuwa bilionea, ndivyo alivyokuwa kwa kipindi hicho, maisha yake yalibadilika, Latifa yule wa kipindi cha nyuma hakuwa huyu wa sasa, alikuwa na kila kitu alichokihitaji katika maisha yake.
Jina lake lilikuwa kubwa, alisikika katika kila masikio ya mtu duniani, dawa yake ilileta mapinduzi makubwa na ilisifika kila kona. Latifa alikuwa ni zaidi ya wanamuziki, alikuwa ni zaidi ya wacheza soka na alikuwa ni zaidi ya waigizaji filamu, kila alipopita, aliheshimiwa, watu wengine waliposikia kwamba alitarajia kupita barabara fulani, walikusanyika, yaani wengine walitaka kumuona tu.
Ndugu zao waliokuwa hoi vitandani kwa sababu ya magonjwa ya kansa, walipona na kuwa wazima kabisa, walimshukuru Latifa na hakukuwa na malipo mengine ambayo wangeweza kufanya zaidi ya kumheshimu na kumpenda maisha yao yote.
Latifa hakuishia nchini Marekani, chini ya kivuli cha Umoja wa Mataifa katika Shirika cha Afya Duniani, WHO, akaanza kuzunguka nchi mbalimbali duniani. Hiyo ilimpa heshima, ilimuongezea umaarufu na kila alipokuwa akienda, watu walikusanyika na kutaka kupiga naye picha.
Latifa akawazidi umaarufu hata watu wengine, alipotua nchini Uingereza, kwa heshima kubwa, akaalikwa mpaka bungeni ambapo huko akapewa nafasi ya kuzungumza, kila neno lililotoka mdomoni mwake, lilikuwa lenye kuleta matumaini makubwa kwamba alikuwa kwenye mikakati ya kutengeneza dawa za magonjwa mengi sugu likiwemo UKIMWI.
Hakuishia barani Ulaya, alizidi kuzunguka katika nchi nyingine, alifika mpaka Urusi ambapo huko akapokewa na watu wengi wakiwemo madaktari wakubwa, walioheshimika, madaktari waliokuwa na nyadhifa za kupokelewa na viongozi wakubwa katika nchi nyingine, ila kutokana na kile alichokifanya, wote walikuwa uwanjani kumpokea.
“Ni binti mdogo mno,” kila aliyemuona Latifa alizungumzia juu ya muonekano aliokuwa nao Latifa.
“Nini kinafuata?”
“Nitataka niende na Afrika pia, japokuwa hakuna magonjwa mengi ya kansa, ila natakiwa kwenda kuwaona hata haohao wagonjwa wachache, nitaanzia na Monrovia nchini Liberia,” alisema Latifa.
Taarifa zikatolewa, nao Waafrika ambao kila siku walijiona kutengwa, wakajiandaa kumpokea mtu wao, msichana aliyekuwa maarufu mno duniani kutokana na dawa ya magonjwa ya kansa aliyekuwa ameitengeneza, Latifa.

Waliberia walijipanga katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Daniel Oduber Quiros, kila mmoja alikuwa na hamu ya kumuona Dk. Latifa ambaye alitarajiwa kuingia katika uwanja huo muda mchache ujao.
Idadi kubwa ya watu waliokuwa mahali hapo walikuwa na fulana zilizokuwa na picha za msichana huyo huku zikiwa zimeandikwa neno Hero likiwa na maana ya shujaa. Si wote waliokuwa na fulana hizo bali wengine walikuwa na mabango yaliyoandikwa maneno mengi ya kumsifia msichana huyo kutokana na ukombozi aliokuwa ameuleta duniani.
Miongoni mwa watu waliokuwa uwanjani hapo alikuwemo Waziri wa Afya nchini humo, bwana Fredrick Taylor aliyetangulizana na mkewe. Waandishi wa habari kutoka katika vyombo mbalimbali vya habari nchini humo walikuwepo uwanjani hapo huku wakiwa na vitendea kazi vyao, kikundi cha ngoma za kienyeji kilikuwa tayari huku watoto wawili waliokuwa na maua wakiwa wamewekwa tayari.
Aliyekuwa akisubiriwa hakuwa rais kutoka nchi fulani, alikuwa Latifa, msichana mwenye asili ya Kihindi ambaye mama yake alifukuzwa nyumbani na kutamani kujiua huku baadaye akisaidiwa na kijana toka Mtaa wa Tandale ambaye ndiye aliyemlea Latifa mpaka muda huo.
Baada ya saa moja, ndege binafsi ikaanza kuonekana angani, taarifa zikatolewa kwamba ndege ile iliyotarajiwa kutua ndiyo ambayo ilimbeba Latifa, wapiga picha na watu wengine wakaanza kujiandaa.
Iliposimama, ngazi ikashushwa, ikawa sawasawa na zuria jekundu. Walioanza kuteremka walikuwa watu kadhaa ambao alitangulizana nao na mwisho wa siku kuteremka Latifa mwenyewe.
Alichokiona, akashindwa kuyazuia machozi yake kububujika mashavuni mwake. Msichana yeye, aliyeteswa na mapenzi, msichana ambaye mama yake alikufa kwa Ugonjwa wa UKIMWI baada ya kufanya sana ngono na walevi wa gongo, leo hii alikuwa akipokelewa kishujaa.
“I can’t believe this,” (Siamini hili) alisema huku akionekana kushtuka.
Zaidi ya watu elfu tano walikuwa wamekusanyika ndani ya uwanja huo, walipomuona tu, wakashindwa kuvumilia, wakaanza kupiga makofi na vigelegele vya shangwe. Msichana maarufu kuliko wote duniani alikuwa akiteremka katika ngazi za ndege, alipofika chini, akaanza kusalimiana na bwana Taylor kisha kukabidhiwa maua na watoto wale, kikundi kile cha ngoma za asili kiliendelea kupiga ngoma zile kisha baada ya hapo akachukua nafasi hiyo kupiga picha na baadhi ya watu waliokusanyika uwanjani hapo kisha kupanda ndani ya gari na kuondoka.
Siku iliyofuata ilikuwa ni siku maalumu kwa Latifa kupelekwa katika hospitali ya taifa ya nchi hiyo, huko, akapata nafasi ya kuonana na wagonjwa mbalimbali waliokuwa hoi vitandani. Hakuwaacha, alizungumza nao mengi, aliwafariji na pia kuwatia nguvu kwamba wangepona magonjwa yao.
“Siamini kukuona,” alisema mgonjwa mmoja.
“Kwa nini?”
“Nilisikia mengi kuhusu wewe, nilisikia kuhusu maisha yako, yalinigusa sana, mwisho wa siku nikafikiri kwamba ni mwanamke mtu mzima, kumbe binti mdogo!” alisema mgonjwa huyo huku akimshangaa Latifa.
“Kwani hukuwahi kuniona kabla kwenye televisheni?”
“Sikuwahi! Nimekuwa nikiugua uti wa mgongo kwa mwaka wa tano sasa, siwezi kusimama, siwezi hata kukaa, maisha yangu yote kwa kipindi hicho ni kulala kitandani tu,” alisema mgonjwa huyo maneno yaliyomuumiza mno Latifa.
“Pole sana!”
“Ahsante! Karibu sana katika nchi hii yenye utajiri wa almasi zilizojaa damu,” alisema mgonjwa yule.
“Nashukuru! Ila hautakiwi kuziita almasi zilizojaa damu. Vita vilikwisha, kila kitu kimebaki na kuwa historia, sahau yaliyopita,” alisema Latifa huku akifahamu fika kwamba nchini hiyo ilikuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka kadhaa iliyopita.
Hakuishia hapo, siku hiyo alitaka kuzunguka kote, kila aliyemuona, hakuamini kama siku hiyo alikutana na msichana mwenye jina kubwa, msichana aliyeuwa bilionea mkubwa duniani.
*****
Dunia nzima ilijua uwepo wa Latifa barani Afika, kila mtu alikuwa na hamu ya kumuona msichana huyo mrembo aliyegundua dawa ya magonjwa ya kansa ambayo kwa kipindi hicho ndiyo iliyokuwa ikizungumza katika kila kona.
Watu wengi walitamani kutembelewa na msichana huyo ambaye kwa kipindi hicho alikuwa amemaliza ziara yake ya kutembelea nchini Liberia na alikuwa akijiandaa na safari nyingine ya kuelekea nchini , Kongo, Ivory Coast na sehemu nyingine barani Afrika.
Kila alipopita, Latifa aliacha gumzo kubwa, watu walimzunguka kwa lengo la kuzungumza naye. Kila alipokanyaga, vituo mbalimbali vya televisheni vilimuita na kufanya naye mahojiano, alialikwa katika shule mbalimbali kwa ajili ya kuzungumza na wanafunzi huku wakati mwingine akitembelea kambi za wakimbizi kwa lengo la kuwajulia hali na kuwakumbusha kwamba pamoja na kila kitu kilichokuwa kikitokea, bado alikuwa pamoja naye.
Alipanga kwenda nchini Tanzania, alitamani kuwaona watu aliozoea kuwaona miaka ya nyuma, alitamani kuyaona mazingira ya Tanzania ambayo aliyaacha kipindi cha nyuma. Aliikumbuka nchi hiyo, umasikini mkubwa uliokuwa umeigubika, watu waliokuwa wakifanya kazi usiku na mchana, kila alipowakumbuka, aliuona upendo mkubwa ukiendelea kuongezeka kwa Watanzania wenzake.
“Nitafika Tanzania, nitataka kutembelea sehemu zote nilizowahi kutembelea,” alisema Latifa huku akiwa kwenye Hoteli ya La Revancha iliyokuwa katikati ya Jiji la Dar nchini Senegal.
Pamoja na kutamani kufika nchini Tanzania, bado aliendelea kumkumbuka Ibrahim ambaye kwake alionekana kuwa miongoni mwa watu katili ambao hawakutakiwa kuishi katika dunia hii. Alikumbuka vilivyo kile kilichotokea kipindi cha nyuma, namna alivyotukanwa na kudharauliwa mbele ya macho ya watu, hakika aliuahidi moyo wake kwamba asingeweza kumsamehe Ibrahim.
“Siwezi kumsamehe! Mungu, naomba unisamehe ila kwa Ibrahim, siwezi kumsamehe,” alisema Latifa huku akionekana kuwa na hasira mno.
Ilikuwa ni saa 4:00 usiku, alikuwa amejiandaa kulala tayari kwa kuanza safari ya kuelekea nchini Kongo kisha kwenda Tanzania ambapo angeanzia mkoani Kigoma na kutembelea Hospitali ya Maweni kabla ya kwenda katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu.
“Ngriii...ngriiii...ngriiii....” ilisikika simu ya mezani ikiita chumbani humo. Kwa hali ya kichovu Latifa akainuka kutoka kitandani na kuifuata simu hiyo, alipoifikia, akaunyanyua mkono wa simu ile na kuupeleka sikiona.
“Hallo!” aliita.
“Hallo! Samahani, kuna mgeni wako hapa.”
“Mgeni wangu?”
“Ndiyo!”
“Anaitwa nani?”
“Anaitwa Dominick!”
“Mmmh! Sawa! Nakuja.”
Latifa alibaki akishangaa tu, jina la mgeni aliyekuwa akimhitaji lilimtia wasiwasi kwani hakujua alikuwa nani na alihitaji nini kutoka kwake. Hakutaka kujali sana, kwa kuwa alifahamu kwamba alikuwa mtu wa watu, akaamua kuvaa na kushuka mpaka mapokezini ambapo huko akaonyeshewa mwanaume aliyekuwa akimhitaji.
Kwa kumwangalia, alionekana kuwa mwanaume mpole, mtanashati ambaye alivalia shati jeupe, surali nyeusi na tai nyekundu, uso wake ulipendezeshwa na miwani ya macho iliyomfanya kuonekana msomi mwenye masta.
“How are you!” (Habari yako!) alisalimia Latifa.
“Usijali, mimi ni Mbongo mwenzanko,” alisema Dominick huku akiachia tabasamu pana usoni mwake, tabasamu lililomfanya kupendeza vilivyo.
“Hahah! Samahani! Kumbe ni Mtanzania mwenzangu! Nasikia ulikuwa ukinihitaji,” alisema Latifa.
“Yeah! Kuna mengi nataka kuzungumza nawe,” alisema Dominick.
“Yapi hayo?” aliuliza Latifa huku akishtuka.
“Usishtuke, si mapenzi, tunaweza kukaa sehemu?”
“Hakuna tatizo!”
Latifa alijisikia huru, kuwa na Mtanzania mwenzake kulimfanya kujisikia amani moyoni. Walichokifanya ni kusogea pembeni mpaka katika mgahawa uliokuwa hotelini hapo na kisha kutulia.
Kabla ya kuzungumza chochote kile, wakabaki wakiangaliana kwa sekunde kadhaa, macho ya Dominick yalionyesha dhahiri kile kilichokuwa kikiendelea moyoni mwake, alionekana kuwa katika dimbwi zito la mahaba.
“Samahani kwa kukusumbua,” alisema Dominick.
“Bila samahani!”
“Kwa jina ninaitwa Domick Simon, nimezaliwa Tanzania ila nilikuja hapa kwa ajili ya masomo yangu ya udaktari katika Chuo cha Touba kilichokuwa katika Mji wa Touba, Mashariki mwa nchi hii. Siku chache zilizopita nilisikia kwamba ungekuja hapa Senegal kwa ajili ya kutembelea wagonjwa katika ziara yako hii iliyo chini ya WHO,” alisema Dominick, Latifa alikuwa kimya akimsikiliza.
“Ndiyo!”
“Nilihitaji kujifunza mengi kutoka kwako, ninahitaji nisafiri nawe sehemu mbalimbali, nadhani kupitia wewe, naweza kupata vitu ambavyo vinaweza kunisaidia sana,” alisema Dominick huku akionekana kuhitaji msaada wa dhati.
“Mmmh!”
“Nini tena?”
“Hakuna tatizo, ila nina sharti moja,” alisema Latifa.
“Usijali Latifa, nitajigharamia kila kitu,” aliingilia Dominick.
“Simaanishi gharama.”
“Unamaanisha nini?”
“Sitaki mwisho wa siku useme kwamba unanipenda, sihitaji mapenzi kwa sasa, ninahitaji kuwa peke yangu,” alisema Latifa huku akimwangalia Dominick usoni.
“Hahaha! Yaani nikuepende wewe? Acha utani Latifa! Hilo sharti si gumu, nimekubaliana nalo,” alisema Dominick.
“Hakuna tatizo! Safari inaanza kesho asubuhi kuelekea Kongo,” alisema Latifa.
“Hakuna tatizo.”


ITAENDELEA

CHANZO : BURE SERIES
 
SEHEMU YA NANE

Dickson Simon Magembe, alikuwa mmoja wa wanafunzi waliofanya vizuri sana nchini Tanzania katika mtihani wa kidato cha sita mwaka mmoja uliopita. Uwezo wake mkubwa wa darasani uliomfanya kuongoza Tanzania nzima ukaipelekea serikali ya nchi hiyo kumdhamini kwenda kusoma nchini Marekani katika Jimbo la Los Angeles.
Kwa kuwa alilelewa katika familia iliyopenda kusaidia watu mbalimbali waliokuwa kwenye matatizo, alichokifanya ni kuiambia serikali kwamba hakutaka kwenda kusoma nchini Marekani bali alitaka kupelekwa nchini Senegal ili atakapofika huko, apate muda wa kuwatembelea watu mbalimbali waliokuwa kwenye kambi za wakimbizi ili aweze kuwasaidia.
Serikali haikukataa, ilichokifanya ni kumsikiliza na hatimaye kumdhamini kwenda nchini humo ambapo mara baada ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Touba, mara chache alikuwa akipata nafasi ya kwenda katika kambi za wakimbizi na kuzungumza nao, alifanya kila kitu kwa kutengeneza makala kwa njia ya video kwa ajili ya maisha yake ya baadaye.
Aliwazoea wakimbizi, kila alipowaona namna walivyopata tabu, alijikuta akibubujikwa na machozi mashavuni mwake. Picha mbaya za watu waliojeruhiwa vibaya, watu waliokuwa wakiteseka kwa magonjwa mabaya yakiwemo ya zinaa mara baada ya kubakwa na wanajeshi, yalimuumiza mno.
Aliishi huko kwa miaka miwili na ndipo alipoanza kusikia kuhusu Latifa. Alivutiwa naye, msaada alioutoa wa kuisaidia dunia nzima kutokana na magonjwa ya kansa akavutiwa nayo, alichokifanya ni kuanza kumfuatilia msichana huyo.
Latifa alipoanza ziara ya kutembelea nchi mbalimbali Afrika hapo ndipo akaona lingekuwa jambo la maana sana kama angeonana na msichana huyo na kuzungumza naye, kweli alifanikiwa.
Alipomwangalia Latifa, alikuwa msichana mrembo, mwenye mvuto, msichana mwenye macho mazuri, yaliyong’aa mithili ya goroli, lipsi pana, nywele ndefu zilizofika mpaka mgongoni. Moyo wake ukampenda lakini huo haukuwa muda wa mapenzi na alijiahidi kwamba asingeweza kuwa na msichana huyo katika maisha yake yote zaidi ya kufanya naye kazi tu.
Alipopewa sharti la kutokuzungumzia mapenzi, kwake halikuwa tatizo, hakuhisi kama moyo wake ulikuwa kwenye mapenzi na msichana huyo mrembo, alichokifanya ni kukubaliana naye.
Siku iliyofuata ndipo safari ya kuelekea nchini Kongo ilipoanza, walichukua ndege, wakakaa pamoja huku wakizungumza mengi. Japokuwa Latifa tayari alikuwa bilionea lakini hakutaka kujali, alikuwa na nidhamu na fedha zake na hakutaka kutumia kiasi kikubwa cha fedha pasipo kuwa na sababu.
“U mwanamke mrembo sana, umechukua wapi urembo huo?” aliuliza Dominick.
“Umeanza!”
“Nimeanza nini sasa?”
“Nilikwambia nini jana?”
“Daah! Kwani kuna kosa kama nikimsifia Mungu?”
“Hapana! Mambo ya uzuri achana nayo kwanza. Kumbuka, hapa kazi tu,” alisema Latifa, alionekana kubadilika.
“Ooh! Ok! Nilishasahau, hakuna tatizo,” alisema Dominick, akavuta Jarida la Boniventure na kuanza kulisoma.
Ndege iliendelea kukata mawingu, baada ya masaa kumi ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa N’Djili uliokuwa katika jiji kubwa la Kinshasa nchini Kongo. Ndege iliposimama, abiria wote wakaanza kuteremka.
Kama ilivyokuwa katika nchi nyingine, watu zaidi ya elfu tano walikuwa wamekusanyika uwanjani hapo tayari kwa kumpokea msichana Latifa. Kila alipofika, aliacha alama kubwa ya umaarufu wake.
Alipendwa kwa kuwa alionekana kuwa msichana mwenye huruma nyingi kuliko wote. Alipofika nje ya jengo la uwanja huo, huku akiwa na Dominick, waandishi wa habari wakaanza kumsogelea na kuanza kumpiga picha mfululizo.
“Mmh! Kumbe maisha ya mastaa yapo hivi!” alisema Dominick, alimwambia Latifa kwa sauti ya chini karibu na sikio.
“Yapo vipi?”
“Hayana raha, kila kona karaha,” alisema Dominick.
Walipofika nje kabisa, tayari mlango wa gari moja likafika uwanjani hapo, lilikuwa lina bendera ya nchi hiyo, lilikuwa la kifahari sana. Mwanaume mmoja aliyevalia suti akawafuata na kuwaambia kwamba walitakiwa kwenda kuingia ndani ya gari lile.
“Ni gari la serikali?” aliuliza Latifa.
“Ndiyo!”
“La nani?”
“Waziri Mkuu!”
“Mmmh! Mwenyewe yupo wapi?”
“Wewe twende, tutaongea mbele ya safari,” alisema mwanaume huyo, walipolifikia gari lile wakaingia ndani na kuanza kuondoka, furaha ambayo watu walikuwa nayo kipindi hicho wakaanza kulikimbiza huku wakishangalia.
“Karibu sana Latifa,” alimkaribisha mwanaume huyo aliyezungumza Kiswahili vizuri kabisa.
“Ahsante sana. Aya, nijibu sasa,” alisema Latifa.
“Nchi hii ipo kwenye matatizo sana,” alisema mwanaume yule.
“Matatizo gani?”
“Watu wanataka waziri mkuu ajiuzulu.”
“Kisa?”
“Machafuko yaliyotokea, yaani watu wana hasira naye, anaishi kwa kujifichaficha tu, kama angeonekana hata pale uwanjani, wangeweza kumuua,” alisema mwanaume yule.
“Nimekuelewa.”
Safari iliendelea mbele, walizungumza mambo mengi huku kila mmoja akimuuliza mwenzake maswali. Kila swali ambalo Latifa aliliuliza lililonekana kuwa muhimu, Dominick aliliandika kwenye notebook yake.
Hawakuchukua muda mrefu wakaingia katika jumba moja kubwa la kifahari, kwa kuliangalia kwa nje tu isingekupa wakati mgumu wa kugundua kwamba mmiliki wa jumba hilo alikuwa mmoja wa watu wenye fedha nyingi.
Gari liliposimamishwa ndani ya eneo la jumba hilo, wote watatu wakateremka. Latifa akabaki akiliangalia jumba lile la kifahari, lilikuwa moja ya majumba makubwa aliyowahi kuingia, kulikuwa na bustani nzuri ya maua, masanamu yaliyonakshiwa kwa unga wa dhahabu, kulikuwa na mbuga ndogo ya wanyama iliyokuwa imezungushiwa fensi huku ndani yake kukiwa na wanyama wachache, kulikuwa na bwawa kubwa la kuogelea, kwa kuliangalia tu, ungegundua kwamba mtu aliyekuwa akiishi ndani ya jumba hilo alikuwa mtu mwenye pesa nyingi.
Wakaingizwa ndani, kulikuwa na makochi makubwa yaliyozungushiwa vyumba vilivyokuwa na rangi ya dhahabu, kadiri Latifa na Dominick walivyokuwa wakiliangalia, bado akili yao iliwaambia kwamba mtu aliyekuwa akilimiliki jumba hilo hakuwa mtu wa mchezo kwenye mambo ya fedha.
Mara mwanaume mmoja akatokea mahali hapo, alikuwa mfupi, mwenye kitambi kikubwa, sura mbaya huku kichwani akiwa amenyoa mtindo wa kijana ujulikanao kama kiduku.
Alikuwa na umri mkubwa, kama miaka sitini lakini kwa kumwangalia, muonekano wake ulikuwa wa ujana zaidi. Alivalia fulana iliyokuwa na picha ya muimbaji wa Marekani, Jay Z, mikononi alivalia saa ya dhahabu. Miguuni, alivalia raba zilizokuwa na chata kubwa ya Nike, kwa muonekano wa harakaharaka usingeweza kugundua kama mwanaume huyo alikuwa mtu mzima.
“Karibuni sana,” aliwakaribisha huku naye akijiweka kochini.
Huyo alikuwa waziri mkuu nchini Kongo, alikuwa miongoni mwa viongozi waliochukiwa mno, machafuko yaliyokuwa yakitokea nchini humo mara kwa mara, yeye ndiye aliyekuwa akisuka mipango huku lengo lake kubwa likiwa ni kuchukua dhahabu na kuwauzia Wazungu.
Wakongo hawakumpenda, waliandamana hadharani kupinga uwepo wake nchini humo, walimchukia sana lakini hawakujua walitakiwa kufanya nini kwani kila uchaguzi mkuu ulipofika, alishinda kwa kishindo kikubwa, ila kwa kuiba kura nyingi.
“U msichana mzuri sana Latifa,” alisema bwana Nelson Savimbi huku uso wake akiupendezesha na tabasamu pana lakini uso haukubadilika, bado ulikuwa mbaya.
“Nashukuru sana.”
Walizungumza mambo mengi, Latifa aliyeonekana kuwa mchangamfu zaidi alimwambia kile kilichokuwa kimemleta nchini Kongo hivyo kuhitaji muda wa siku mbili kwa ajili ya ziara ya kutembelea hospitali za nchini humo na baadhi ya kambi za wakimbizi.
Hilo halikuwa tatizo haa kidogo, alichokifanya bwana Savimbi ni kumruhusu na hivyo kuwasiliana na wahusika na kuwaambia juu ya uwepo wa Latifa nchini humo. Baada ya kuzungumza kwa kipindi kirefu hapo ndipo walipoondoka na kuelekea katika hoteli kubwa ya nyota tano, The Bufalloes iliyokuwa katikati ya Jiji la Kinshasa.
“Nakutakia usiku mwema Latifa,” alisema Dominick.
“Ahsante! Nawe pia,” alisema Latifa na kuingia chumbani kwake.

Usiku hakulala vizuri, kichwa chke kilikuwa kikifikiria juu ya safari yake kubwa ya mafanikio aliyokuwa nayo, ilikuwa safari ndefu ambayo kwa kipindi hicho alijivunia mno kuwa hapo alipokuwa.
Hakuacha kuwakumbuka wanaume waliouumiza moyo wake, wanaume aliotokea kuwachukia kuliko wote katika dunia hii. Hakumpenda Ibrahim hata mara moja, alimchukia Liban, mwanaume wa Kihindi ambaye aliamua kumuacha kwa kuwa tu aliwasikiliza ndugu zake.
Hakutaka kujificha, alikiri kwamba kati ya watu aliokuwa akiwachukia mno basi watu hao walikuwa mstari wa juu kabisa. Usiku huo hakuacha kukumbuka kuhusu mama yake, aliambiwa kwamba mama yake aliitwa Nahra, mwanamke mrembo aliyekuwa mlevi ambaye alifukuzwa na wazazi wake mara baada ya kupewa mimba na mtu mweusi kisha kumfukuza.
Chuki yake ikaongezeka, watu aliokuwa akiwachukia wakaongezeka, pia alimchukia baba yake ambaye hakuwa akimfahamu, sababu kubwa ya kumchukia ni jinsi alivyomfukuza mama yake kisha kuingia kwenye ulevi mkubwa uliompa Ugonjwa wa UKIMWI na mwisho wa siku kufariki.
Mbali na baba yake, aliwachukia babu na bibi yake kwa upande wa mama kwa kitendo chao cha kumfukuza mama yake kisa tu alizaa na baba yake. Moyo wake ulimuuma mno ila wakati mwingine alibaki akimshukuru Mungu kwa kuamini kwamba isingekuwa hivyo, inawezekana leo hii asingekuwa hapo alipokuwa.
Siku iliyofuata, akajiandaa tayari kwa kuanza safari ya kuelekea katika hospitali mbalimbali, alipomaliza kujiandaa, akatoka nje ambapo akakutana na Dominick akiwa tayari nje, alipomuona, tabasamu pana likajengeka usoni mwake.
Hotelini hapo kulikuwa na ulinzi mkubwa, polisi walikuwa wakizunguka huku na kule kuhakikisha kwamba ulinzi unakuwa mkubwa na wa kutosha. Japokuwa Latifa hakupendwa kulindwa na silaha lakini hakuwa na jinsi, alikubaliana na kila kitu.
Wakaondoka na kuelekea katika Hospitali ya Mobutu. Idadi kubwa ya watu ilikuwa hospitalini hapo, waandishi wa habari kutoka katika vyombo mbalimbali vya habari walikuwa mahali hapo kwa ajili ya Latifa tu.
Gari lile lililombeba yeye na Dominick liliposimama, wakatoka nje, waandishi wakawasogelea na kuanza kuwapiga picha. Latifa aliachia tabasamu pana, akashindwa kuvumilia, akajikuta akibubujikwa na machozi ya furaha, akaanza kuwapungia mikono watu hao.
Alichokikuta ndani ya hospitali hiyo kilimliza, hospitali ilikuwa chafu, huduma mbovu, wagonjwa walirundikana kila chumba, hakukuwa na mpangilio wowote ule. Kila aliyezungumza naye, walimwambia wazi kwamba huduma ilikuwa mbovu hivyo waliiomba serikali iweze kuwasaidia kudumia huduma na si kula hela na kuuza madini kiholela.
“Nitawasaidia kufikisha kilio chenu,” alisema Latifa.
Ziara ya siku mbili ikafanyika kwa mafaniko makubwa, walipomaliza wakaanza safari ya kuelekea nchini Tanzania katika Mkoa wa Kigoma. Walipofika huko, wakachukuliwa na kupelekwa katika Hoteli ya Hiltop na kuchukua vyumba humo. Kama ilivyokuwa sehemu nyingine, hata huko pia watu wengi walitamani kumuona msichana huyo mdogo mwenye mafanikio na hatimaye kuwa bilionea mkubwa akiwa na umri mdogo tu.
Waandishi wa habari na watu wengine walikusanyika katika Hoteli ya Hiltop kwa ajili ya kumuona Latifa ambaye wala hakuwa na hiyana, akaonana na watu hao kwa kukaa nao sehemu fulani kisha kuanza kuzungumza nao, walikuwa kama hamsini hivi.
“Unajisikiaje kuwa Latifa?” aliuliza mwanamke mmoja.
“Najisikia kawaida, ila najiona kuwa na thamani, hiki ndicho nilichokitaka, nitambulike mimi ni nani na nina mchango gani katika jamii,” alijibu Latifa huku akiachia tabasamu.
“Na huyo ni nani? Shemeji yetu?” aliuliza mwandishi mmoja.
“Nani? Huyu? Huyu ni rafiki yangu, anaitwa Dominick, nilikuwa naye tangu Senegal,” alijibu Latifa huku akichia tabasamu pana.
“Mnapendeza kuwa pamoja, kama wapendanao,” alisema mwandishi mwingine, akawasogelea na kuwapiga picha.
Maneno yale kama yakawa yameibua kitu fulani moyoni mwa Latifa, akauhisi moyo wake ukiingiwa na kitu cha tofauti kabisa, kitu alichokuwa nacho kipindi cha nyuma mara baada ya kuisoma barua aliyoandikiwa na Ibrahim.
Alipomwangalia Dominick, mvulana huyu aliachia tabasamu pana, kitu ambacho hata yeye mwenye hakujua kilikuwa nini, akaona kuwa mwanaume mzuri mno, akahisi kuanza kumpenda.
Maswali yaliendelea zaidi, Latifa aliwajibu wote lakini kichwa chake kiliingia katika fikra nyingine kabisa, alikuwa akimfikiria huyo Dominick aliyekuwa bize akiandika. Mara baada ya kumaliza mahojiano, wakaimama na kuelekea ndani.
“Dominick...” aliita Latifa, mwanaume huyo akamsogelea na kusimama karibu yake, walikuwa koridoni katika ghorofa ya tano hotelini.
“Naaam..” aliitikia Dominick huku akimwangalia Latifa, walikuwa karibukaribu mno.
“Au basi...” alisema Latifa, akageuka na kuingia chumbani.
Kichwa chake kikaanza kusumbuka, yule Dominick ambaye alimwambia wazi kwamba hakutaka siku amwambie kwamba alikuwa akimpenda, leo hii alijikuta akianza kumfikiria, mapenzi yakaanza kuchomoza moyoni mwake.
Usiku hakulala, alibaki akimfikiria mwanaume huyo tu. Kitandani, ni mawazojuu ya Dominick ndiyo yalikuwa yakimsumbua kila wakati. Hakujua afanye nini, hakujua kama lingekuwa jambo la kawaida kumwambia mwanaume huyo kwamba alimpenda.
“Dominick...These feelings have to stop right now, I can’t bear them,” (Dominick...hisia hizi zinatakiwa kutoka sasa, siwezi kuzibeba) alisema Latifa huku akibimbirikabimbirika kitandani pale.
Alibaki na mawazo mpaka ilipofika saa nane usiku ndipo alipopatwa na usingizi. Alipoamka asubuhi, akajiandaa na kutoka nje ambapo baada ya kumuona Dominick, akajikuta akishtuka na moyo wake ukidunda kwa nguvu.
“Umeamka salama?” aliuliza Dominick huku akitoa tabasamu lilimvuruga kabisa Latifa.
“Nimeamka salama, wewe?”
“Hata mimi nipo poa.”
Siku hiyo safari ilikuwa ni kwenda katika Hospitali ya Mkoa ya Maweni na hospitali nyingine hapo Kigoma, kote huko, watu walikuwa wakijazana na kumwangalia Latifa, kila aliyemuona hakutaka kuamini kama msichana yule alikuwa Mtanzania kama walivyokuwa.
Wagonjwa wakafarijika, maneno aliyokuwa akiyazungumza msichana huyo yakawatia nguvu na kujiona wakiingiwa na nguvu za kusonga mbele. Baada ya siku nzima ya kuwatembelea wagonjwa, siku iliyofuata ilikuwa ni zamu ya kwenda katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu.
Huko, Latifa alijikuta akibubujikwa na machozi, hakuamini kama kulikuwa na watu waliokuwa wakipitia mateso makubwa kama alivyokuwa watu hao. Wengi walikuwa wagonjwa, madaktari walikuwepo kwa ajili ya kuwahudumia lakini kutokana na idadi ya wakimbizi kuwa wengi, hata wale madaktari walionekana kuwa wachache.
Siku hiyo napo akashinda hukohuko, baada ya kumaliza kila kitu, wakarudi Kigoma Mjini ambapo wakachukua ndege na kuanza safari ya kwenda Dar es Salaa, sehemu ambayo alizaliwa Latifa, sehemu kulipokuwa na watu wengi aliokuwa akiwachukia.

ITAENDELEA

CHANZO : BURE SERIES
 
SEHEMU YA TISA

Ulikuwa ni muda wa kuhangaika, kujutia kile kilichotokea na pia huo ulikuwa muda wa kulia na kusaga meno. Msichana aliyekuwa amemkataa ndiye aliyekuwa gumzo duniani, ndiye aliyesemekana kuwa na utajiri mkubwa kuliko vijana wote waliokuwa na umri chini ya miaka thelathini.
Ibrahim aliumia moyoni mwake, mafanikio ya Latifa yaliuumiza mno moyo wake, akawa mtu aliyekosa raha, amani na furaha, kila alipokuwa akikaa, alijikuta akijilaumu kwa ujinga aliokuwa ameufanya.
Latifa alikuwa msichna mzuri, mwerevu, mwenye akili na kuchanganua mambo, mbali na sifa hizo zote, msichana huyo alikuwa na sifa moja kubwa kwamba alikuwa akimpenda. Alipewa upendo wote, alithaminiwa kwa kiwango cha juu kabisa lakini badala ya kuupokea upendo ule, baada ya kuona namna gani alithaminiwa, mwisho wa siku akaona vyote hivyo havikuwa na thamani, upendo haikuwa sababu ya kuendelea kumpenda, akaamua kumuacha, akaamua kumliza, akaupa kidonda moyo wa msichana huyo, pasipo kuwa na huruma, akamwambia achukue taimu yake na yeye abaki na Nusrat, msichana aliyeamini kwamba angeishi naye milele.
Kama kulikuwa na watu waliokuwa na maumivu makali duniani, Ibrahim alikuwa wa kwanza, alilia, macho yakawa mekundu, alijuta na kujuta lakini ukweli haukubadilika, kila kitu kilibaki kilekile kwamba aliacha nazi, akajiona mjanja wa kuchagua na mwisho wa siku mikono yake ikaangukia kwa koroma.
Nusrat, yule msichana mrembo, yule msichana aliyemwambia kwamba angempenda miaka yote, leo hii alikuwa akiishi naye kimagumashi, maisha na wanaume wengine yakamteka na mwisho wa siku kujikuta akitumia muda mchache sana kuwa naye.
Ibrahim hakuficha, alimwambia mzee Deo juu ya Latifa, yule msichana mrembo aliyekuwa akivuma sana, msichana aliyekuwa bilionea.
“Msichana mwenyewe huyu hapa,” alisema Ibrahim, alikuwa akimwambia mzee Deo.
“Msichana gani?”
“Yule niliyemuacha kwa ajili ya huyu fisi,” alisema Ibrahim.
“Unamaanisha Latifa?”
“Ndiyo!”
“Sasa ilikuwaje mpaka ukamuacha mwanamke bilionea?”
“Ni ujinga, kipindi kile hakuwa na kitu, alikuwa msichana aliyejielewa, ila huyu nguchiro akanishawishi mpaka nikawa naye,” alisema Ibrahim huku akishindwa kulizuia chozi lake kububujika mashavuni mwake.
“Pole sana aisee! Latifa ni msichana mrembo, kama ningekuwepo siku hiyo, hakika ningekupiga vibao, kwa mbali anafanana na Nahra kipindi kile alichokuwa msichana wangu,” alisema mzee Deo.
“Nahra huyo mwanamke uliyezaa naye?”
“Ndiyo! Ila duniani mara nyingi watu huwa wawiliwawili,” alisema mzee Deo pasipo kujua kama yule aliyekuwa akimzungumzia alikuwa binti yake wa damu.
Ibrahim alijitolea kumsaidia mzee Deo, mara baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini, kitu cha kwanza alichokifanya ni kumpeleka nyumbani kwake huku mzee huyo akiwa na mguu moja.
Japokuwa mke wake alikasirika sana juu ya ujio huo lakini Ibrahim hakutaka kujali, alijisikia kumsaidia mzee huyo siku zote za maisha yake. Siku ambayo mzee huyo alikuja nyumbani hapo, mke wake, Nusrat alilalamika sana mpaka kufikia hatua ya kutaka kupigana lakini msimamo wa Ibrahim ukawa huohuo kwamba mzee Deo hakutakiwa kuondoka nyumbani hapo.
Baada ya siku kadhaa, wakapata taarifa kwamba Latifa alikuja nchini Tanzania na safari yake ilianzia mkoani Kigoma. Moyo wake ulifarijika mno, alitamani kuonana na msichana huyo, si kwa lengo la kumwambia wawe pamoja, kitu alichokitaka ni msamaha kutoka kwa binti huyo tu.
Alimsubiria kwa hamu kubwa, mpaka siku ambayo ilitangazwa kwamba msichana huyo aliingia jijini Dar es Salaam na watu zaidi ya elfu kumi walikwenda kumpokea uwanja wa ndege.
Ibrahmi hakutaka kukaa nyumbani, alitaka kwenda huko, naye awe mmoja wa watu waliokwenda kumpokeaLatifa. Kutokana na idadi kubwa ya watu, hakupata nafasi ya kufika mbele kabisa, alisimama kwa mbali huku akimwangalia msichana huyo ambaye alikuwa na mwanaume asiyemfahamu kabisa, moyo wake ulimwambia kwamba mwanaume huyo alikuwa mpenzi wake.
Ibrahim hakumsogelea, hakutaka kuonekana, kumuona Latifa, moyo wake ukaridhika kabisa, alichokifanya ni kugeuka na kurudi nyumbani. Njiani mawazo yalimsumbua mno, hakuamini kama kweli Latifa alikuwa vile aliyokuwa, kila alipokuwa akiufikiria ubilionea aliokuwa nao na umaarufu, aliona kwamba hata yeye pia angekuwa bilionea kwani wangechangia utajiri huo.
Alipofika nyumbani, alishangaa kuona mzee Deo akiwa nje, alikuwa akililia kama mtoto mdogo, damu zilikuwa zimetapakaa kila kona, mguu wake ambao ulikuwa haujapona inavyotakiwa ulikuwa umetoneshwa.
Ibrahim alipomuona, akamkimbilia kule alipokuwa, akainama na kumwangalia mzee huyo ambaye alikuwa na kipande cha mguu kutokana na kukatwa kwa sababu ya kansa. Alishindwa kuvumilia, akajikuta akitokwa na machozi.
“Vipi tena?” aliuliza Ibrahim.
“Mke wako.”
“Kafanya nini?” aliuliza Ibrahim huku akionekana kuwa na hasira.
“Amenifukuza kwako, kanitupa hapa nje,” alisema mzee Deo.
“Hebu subiri!”
Ibrahim akasimama na kuufuata mlango, akataka kuufungua lakini mlango haukufunguka, ulikuwa umefungwa kwa ufunguo. Wakati akiendelea kuugonga, hapohapo kwa chini akaona kikaratasi kikiwa kimepenyezwa chini mlangoni, akakichukua na kuanza kukisoma, kiliandikwa maneno machache sana yaliyosomeka ‘Sitaki nimuone huyo mzee mchafu nyumbani kwangu! Ukijifanya kiburi, hata wewe utaondoka, hujachangia hata tofali humu.’
Ibrahim akahisi moyo wake ukichomwa na kitu chenye ncha kali, aliumia mno, alijikuta akikunja ngumu na kukichanachana kikaratasi kile. Maneno yaliyoandikwa katika karatasi ile yalikuwa ya kweli kabisa kwamba hakuchangia hata tofali ndani ya nyumba ile.
Ibrahim akamfuata mzee Deo, akamnyanyua na kuanza kuondoka naye. Mzee huyo alikuwa na maumivu makali, bado damu zilikuwa zikimtoka katika kipande cha mguu alichokuwa nacho, alichokifanya ni kumpeleka hospitali.

Safari ya kwenda Dar es Salaam ikaanza rasmi, ndani ya ndege bado Latifa alionekana kuwa na mawazo lukuki, penzi lake kwa Dominick lilichanya kiasi kwamba akawa haoni wala hasikii.
Walipofika Dar, idadi ya watu elfu kumi walikuwa wamefika uwanjani hapo, ndege ile ilipoanza kutua, kila mmoja alionekana kuwa na furaha, vibendera vidogo vikaanza kupepewa, watu waliovalia fulana zilizokuwa na picha za Latifa wakajisogeza mbele kabisa.
Uwanjani hapo Latifa alikuwa amepewa heshima kubwa mno, Waziri Mkuu, bwana Abdallah Kibonde alikuwa amefika kwa ajili ya kumpokea msichana huyo huku kukiwa na kundi la watoto watatu ambao waliletwa kwa ajili ya kumkabidhi maua kama ishara ya heshima na kumpenda.
Kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo na pote alipopita Latifa kilikuwa kikirushwa laivu katika mashirika mbalimbali ya habari kama CNN, BBC, Aljazeera na mengine mengi kwani huyu Latifa alikuwa mtu mwenye nguvu kwa kipindi hicho, mtu aliyeleta mapinduzi makubwa mno.
Kila kitu kilichokuwa kikiendelea, Dominick alikuwa akikifuatilia kwa karibu zaidi. Alifurahi kuwa karibu na Latifa, kwake, alionekana kuwa msichana mwenye nyota kubwa ya kupendwa.
Miongoni mwa watu wengi waliokuwepo mahali hapo, walikuwa waandishi wa habari ambao mikono yao ilikuwa na kamera na walikuwa wakiendelea kufanya kazi yao ya kupiga picha kwa kila kilichokuwa kikiendelea.
Kila mmoja akafurahia, kumuona Latifa nchini Tanzania, ndani ya nchi aliyozaliwa kulimfurahisha kila mtu. Katika kipindi cha nyuma, aliondoka nchini Tanzania kama mtu wa kawaida, hakukuwa na mtu aliyemthamini, alionekana kuwa si kitu ila leo hii alikuwa amerudi tena, alipokelewa kishujaa zaidi ya walivyokuwa wakipokelewa viongozi wengine.
“Unajisikiaje kuwa Tanzania?” aliuliza mwandishi wa habari.
“Sina la kuongea, naomba mniache, moyo wangu una furaha mno,” alisema Latifa huku akionekana mwenye furaha mno, machozi yalikuwa yakimbubujika.
Hapohapo akachukuliwa na kuingizwa ndani ya gari la waziri huyo kisha safari ya kuelekea hotelini kuanza. Garini, Latifa alijisikia fahari mno, maisha yake yakaanza kurudi nyuma, kipindi alichokuwa akiishi Manzese kwa mama yake mlezi, bi Semeni aliyekuwa kaka yake mzee Issa ambaye kila siku alimchukulia kuwa baba yake.
Leo hii alikuwa ndani ya gari la heshima, miongoni mwa magari yaliyopandwa na viongozi wakubwa nchini. Moyo wake ulifurahi mno, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea, wakati mwingine alihisi yupo ndotoni.
“Latifa...” aliita waziri, bwana Kibonde.
“Ndiyo mheshimiwa.”
“Umeliletea sifa taifa hili, japokuwa Wamarekani wamekuwa wakikung’ang’ania lakini utaendelea kuwa Mtanzania,” alisema bwana Kibonde.
“Nashukuru sana! Ninajisikia kupendwa, ninapenda na kuvutiwa kwa kila kitu kinachotokea katika maisha yangu, kama nilivyowasaidia watu wengine, ningependa niwasaidie na Watanzania pia,” alisema Latifa huku akiachia tabasamu.
“Mama yupo hai?”
“Hapana! Alifariki miaka mingi iliyopita baada ya kuugua Ugonjwa wa UKIMWI, niliambiwa kwamba alikuwa mlevi mno,” alijibu Latifa na kubaki kimya, machozi yakaanza kumlenga.
“Pole sana! Na vipi baba?”
“Sijajua yupo wapi, nahisi amekwishakufa!”
“Kwa nini uhisi?”
“Sikuwahi kumuona, niliambiwa na baba yangu mlezi kwamba baba alimfukuza mama baada ya kugundua kwamba alikuwa mjauzito, tena hapo ni baada ya mama kufukuzwa nyumbani na wazazi wake kisha alikuwa na mimba ya mtu mweusi,” alisema Latifa.
“Pole sana! Kwa hiyo hujui kama baba yako yupo hai au la?”
“Sijui chochote kile.”
Waliendelea kuzungumza ndani ya gari, Dominick ambaye naye alipewa heshima kubwa alikuwa ndani ya gari hilo, hakuzungumza chochote kile, alibaki kimya huku masikio yake yakiwa makini kusikiliza na ubongo wake kuwa makini kukariri.
Safari ile iliendelea mpaka walipofika katika Hoteli ya Kilimanjaro, wakateremka na kisha kuingia ndani. Hakukuwa na wateja wengi, wale waliokuwepo, walitakiwa kubaki haohao na hata wale waliotaka kupanga hotelini, hawakuruhusiwa mpaka Latifa atakapoondoka.
Ratiba ilikuwa imekwishapangwa, Latifa alitakiwa kukaa hapo hotelini mpaka kesho yake ambapo angechukuliwa na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, huko, angefanya ziara ya kuzungukazunguka kwa wagonjwa kisha baadaye kupelekwa katika Hospitali ya Mwananyamala na mwisho kabisa kuitwa katika Kituo cha Televisheni cha Global.
Mawazo juu ya Dominick hayakuisha, picha ya mtu huyo ilikuwa ikimjia kichwani, alimpenda mno, hakutaka kumwambia ukweli kwani alikumbuka maneno aliyomwambia nchini Senegal kwamba asije siku akamwambia kwamba alikuwa akimpenda.
Usiku ulikuwa mrefu, alibaki akiwa amekumbatia mto tu huku mwili wake ukianza kumtetemeka, hakuwa na hamu ya kuwa na mwanaume mwingine, aliyekuwa akimtaka kipindi hicho alikuwa Dominick tu.
Baada ya kukaa mpaka saa saba usiku, Latifa akashindwa kuvumilia, alichokifanya ni kuchukua simu yake na kwenda sehemu ya majina, akaanza kulitafuta jina la Dominick.
“Mungu! Naomba anielewe,” alisema Latifa.
Alipoliona jina la Dominick, hapohapo akapiga namba hiyo na simu kuanza kuita. Wakati ikiwa inaita, mwili wake ukaanza kumtetemeka, japokuwa kulikuwa na kiyoyozi kilichokuwa kikifanya kazi lakini kijasho chembemba kikaanza kumtoka.
“Hallo!” aliita Dominick kwenye simu.
“Hallo Dominick, naomba uje chumbani,” alisema Latifa kwa sauti ndogo.
“Kuna nini?”
“Wewe njoo tu!”
“Kuna amani lakini?”
“Ipo, tena nyingi tu, naomba uje,” alisema Latifa.
“Sawa!” alijibu Dominick na kukata simu.
Moyo wake ukapoa, akajisikia amani moyoni mwake, muda huo, usiku huo ulitulia alikuwa akimsubiri mwanaume aliyekuwa na mapenzi naye, Dominick afike chumbani humo.
Mara akasikia mlago ukigongwa, akashusha pumzi ndefu, akasimama na kuanza kuufuata mlango, alivalia nguo laini ya kulalia iliyoyafanya maungo yake kuonekana vilivyo, akaufuata mlango na kuufungua, alipomuona Dominick tu, mapigo ya moyo wake yakaanza kuongeza kasi, akahisi kama moyo ungeweza kuchomoka.
“Karibu,” Latifa alimkaribishaDominick.
“Ahsante.”
Dominick akaingia ndani, yeye mwenyewe alichanganyikiwa, vazi alilovaa msichana huyo lilimuweka kwenye wakati mgumu, kila kitu maungoni mwake kilionekana wazi, wazimu ukampanda, kila alipojitahidi kujikaza kiume, akashindwa kabisa.
“Umependeza,” alisema Dominick, alishindwa kuvumilia, japokuwa lilikuwa ni vazi la kulalia tu lakini akakosa maneno, akaona bora asifie hivyohivyo tu.
“Na hili vazi?” aliuliza Latifa.
“Ndiyo! Koh koh koh...u mzuri sana Latifa,” alisema Dominick na kujikoholesha, akili yake ilihama, alichokuwa akikifikiria ni mapenzi tu.
“Nashukuru!”
Latifa alifikiri kazi ingekuwa kubwa, alijipanga vilivyo lakini mara baada ya Dominick kuingia humo ndani, akagundua kwamba kazi ilikuwa nyepesi mno, hata kumsukuma mlevi katika mteremko wa mlima ilikuwa ngumu.
Alichokifanya Latifa ni kumsogelea Dominick pale alipokaa, kabla mwanaume huyo hajajiandaa, akashtukia akivamiwa na Latifa, mwisho wa siku wakajikuta wakiangukia kitandani, kilichoendelea, kilichotokea, hakukuwa kingine zaidi ya sauti ya kitanda na mihemo ya mahaba kusikika tu.
Asubuhi kila mtu alikuwa hoi, hawakulala usiku kucha, walikesha huku wakibusiana huku na kule. Baada ya kuamka, ilipofika saa moja na nusu wakaletewa kifungua kinywa na kuanza kunywa.
Walifanyiana mapenzi ya njiwa, walilishana, walibusiana na kukumbatiana, muda mwingi Dominick alikuwa akimpakata Latifa na kumbusu kadiri alivyoweza.
“Siamini,” alisema Dominick.
“Huamini nini?”
“Eti na mimi nimelala na bilionea!”
“Haha! Hebu acha maneno yako kipenzi, niite Latifa tu jamani, hilo bilionea, wala silipendi kuitwa na mtu kama wewe,” alisema Latifa kwa sauti laini, ya mahaba, yenye kumtoa nyoka pangoni, sauti iliyozitetemesha ngoma za masikio ya Dominick.
Ilipofika saa mbili na nusu wakapigiwa simu na kuambiwa kwamba muda ulikuwa umefika hivyo walitakiwa kuanza ziara ya kuelekea katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Wakajiandaa na walipomaliza wakatoka ndani na kuelekea mapokezi ambapo huko wakakutana na dereva wa waziri ambaye akawachukua na kuanza kwenda huko huku wakitangulizana na Waziri Kibonde ambaye walimkuta garini.
Hawakuchukua muda mrefu, wakafika katika hospitali hiyo na moja kwa moja kuanza kile kilichokuwa kimempeleka nchini Tanzania. Kila alichokifanya, Dominick alikuwa akikichukua kwa kamera yake, bado alikuwa kwenye utengenezaji wa makala yake.
Baada ya kuzunguka huku na kule, kuwaona wagonjwa waliokuwa wakiteseka vitandani, Latifa akatoa msaada wa kiasi cha shilingi milioni mia tano ili kisaidie katika ununuaji wa dawa na kujenga maabara nyingine hospitalini hapo. Walipomaliza, wakaelekea katika Hospitali ya Mwananyamala, huko, alifanya kama alivyofanya Muhimbili na kuahidi kutoa kiasi kama kile kwa ajili ya utengenezaji wa maabara na kunua dawa kwa ajili ya wagonjwa katika hospitali hiyo.
“Tunashukuru kwa kila kitu. Nini kinafuata?” alisema Waziri Kibonde na kuuliza.
“Ahsante kwa kila kitu pia, tunatakiwa kwenda kwenye Kituo cha Televisheni cha Global kwa ajili ya mahojiano, baada ya hapo, nadhani tutakwenda kupumzika,” alisema Latifa.
“Sawa! Ila kuna kitu.”
“Kipi?”
“Rais amenipigia simu, amesema kwamba umealikwa ikulu kwenye chakula cha usiku na familia yako,” alisema waziri.
“Unasemaje?”
“Ndiyo hivyohivyo! Umealikwa.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Ikulu?”
“Hapohapo mjengoni.”
Latifa hakuamini, kile alichokuwa ameambiwa hakutarajia kukisikia. Leo hii aliambiwa kwamba alihitajika kwenda ikulu, hakuamini, msichana aliyekulia kwenye maisha ya kimasikini, leo hii alikaribishwa ikulu, kwake ilikuwa ni faraja tele.
“Nimefurahi, nitakuja,” alisema Latifa

ITAENDELEA

CHANZO : BURE SERIES
 
SEHEMU YA KUMI ................ MWISHO

Bi Rachel alikuwa na furaha tele, kila alipomwangalia Latifa ambaye alifika nchini Tanzania kwa ajili ya ziara yake ya kuwatembelea Watanzania wengine, moyo wake ukafarijika mno.
Kila wakati alikuwa akitazama televisheni, alimkumbuka msichana huyo, aliishi naye, yeye ndiye aliyempeleka nchini Marekani ambapo huko alisoma na binti yake, Dorcas, leo hii, yule Latifa masikini, mtoto aliyezaliwa na mwanamke mnywa gongo alikuwa maarufu duniani, tena mwenye fedha nyingi.
Baada ya Latifa kutembelea hospitali hizo, akapigiwa simu na msichana huyo na kumwambia kwamba alitakiwa kujiandaa kwani walitakiwa kuonana katika Ofisi za Kituo cha Televisheni cha Global kwa ajili ya kuzungumza mengi.
Bi Rachel alifurahi kusikia hivyo, akahisi kuthaminiwa zaidi ya mtu yeyote yule. Alichokifanya ni kuwasiliana na mzee Issa, na bi Semeni ambao hao ndiyo waliomlea Latifa kule Manzese, ila katika kipindi hicho, hata nao maisha yao yalikuwa mazuri hasa mara baada ya Latifa kuwa bilionea.
Wakafika katika jengo la kituo hicho cha televisheni na kuanza kumsubiria. Wafanyakazi wa kampuni hiyo walipoambiwa kwamba watu hao waliokuja walikuwa ndegu zake na Latifa, walijisikia wivu sana kwa kuona walikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na bahati kubwa maishani mwao.
Ilipofika saa sita mchana, gari la kifahari likaanza kuingia katika eneo la kituo hicho, mlango ukafunguliwa na Latifa kuteremka, akaanza kutembea kuelekea ndani ya jengo hilo. Alipoingia ndani na kuwaona ndugu zake, kwa futaha akawakimbilia na kuwakumbatia, machozi ya furaha yakaanza kumtoka.
“Nashukuru sana mama, nashukuru sana mama kwa msaada wako, bila wewe, nisingekuwa hapa,” alisema Latifa huku akiwa amemkumbatia bi Rachel.
“Usijali Latifa, nilifanya yote kwa kuwa nilihisi kukusaidia,” alisema bi Rachel.
Wafanyakazi wote waliokuwa mahali hapo wakaanza kuwaangalia watu hao, kumuona Latifa katika ofisi zao walijisikia fahari sana, wengine wakachukua nafasi hiyo kupiga naye picha na kuzirusha mitandaoni.
Baada ya kumaliza ishu ya kupiga picha na wafanyakazi, akaitwa katika chumba kimoja ambacho kilikuwa maalumu kwa ajili ya kufanya interview ambayo ingerushwa moja kwa moja kwenye televisheni.
“Karibu Latifa,” alikaribishwa.
Akaanza kufanyiwa maandalizi kwa ajili ya uchukuaji video, muda huo, ndugu zake walikuwa pembeni wakifuatilia kila kitu, walionekana kuwa na furaha mno. Dominick hakuacha kuchukua kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo, bado aliendelea na mchakato wake wa kumtengenezea makala msichana huyo. Baada ya kumaliza, akaitwa mbele ya kamera na kuanza kuhojiwa.
Latifa akaanza kusimulia historia ya maisha yake tangu alipofukuzwa mama yake ambayo historia yake alisimuliwa na mzee Issa, alisimulia kila kitu, baada ya kutimuliwa nyumbani kwa mama yake kisa alikuwa na mimba ya mtu mweusi, akakimbilia kwa mwanaume aliyempa ujauzito ule ambaye naye huyo aliamua kumtimua nyumbani kwake.
Ilikuwa simulizi yenye kuhuzinisha, wakati mwingine alipokuwa akisimulia, alitabasamu, kuna kipindi alifika, alibubujikwa na machozi na kuendelea mbele. Hakutaka kuacha kitu, alimzungumzia Ibrahim, jinsi alivyoutesa moyo wake, alivyomuacha mbele ya msichana mmoja wa Kiarabu, aliumia, alikosa raha, akakata tamaa ya kupenda hivyo kurudi nchini Marekani.
Alipofika huko, akasimulia kuhusu Liban, kila alipokuwa akiwazungumzia watu hao wawili, machozi yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake, aliumia mno, aliteseka moyoni mwake mpaka kipindi kingine alitamani kufa, afe ili asiweze kuteseka tena.
“Pole sana Latifa,” alisema mtangazaji aliyekuwa akimhoji.
“Ahsante sana, ila ni maisha, Mungu anaporuhusu jambo fulani litokee, huwa anakupa na mlango wa kutokea,” alisema msichana huyo.
Kipindi hicho kilichukua saa moja, alipomaliza, akasimama na kumfuata mzee Issa, akamkumbatia huku akibubujikwa na machozi mashavuni mwake, alipotoka mikononi mwake, akamfuata bi Semeni na kumkumbatia pia.
“Samahani Latifa,” alisema msichana mmoja, alikuwa mfanyakazi wa hapo.
“Bila samahani.”
“Kuna mtu anakuulizia hapo getini.”
“Nani?”
“Anaitwa Ibrahim, amesema kwamba unamfahamu,” alijibu msichana yule.
Latifa alipolisikia jina hilo, moyo wake ukapiga paaaa, akakunja uso wa hasira, machozi yakaanza kumbubujika tena, kumbukumbu zake zikaanza kurudi nyuma kama mkanda wa filamu.
*****
Kwa mara ya kwanza Kituo cha Televisheni cha Global kilitangaza kwa kusema kwamba siku ya Ijumaa kungekuwa na mahojiano maalumu na msichana bilionea mwenye asili ya Kitanzania ambaye alikuwa akiishi nchini Marekani, Latifa Issa kama alivyojulikana.
Kila mtu akatamani kukiangalia kipindi hicho kilichotarajia kuruka majira ya saa tisa alasiri. Watu wakaambiana, wakasambaziana taarifa kwamba msichana huyo bilionea, aliyeleta tumaini kubwa duniani hasa kwa wagonjwa wa kansa angehojiwa moja kwa moja kwenye televisheni.
Kila mtu alitaka kumsikiliza, kila mtu alitaka kusikia historia ya maisha yake kwamba alianzia wapi, alipitia wapi na wapi mpaka kuwa vile alivyokuwa kipindi hicho. Kila kona, stori ilikuwa moja tu kuhusu Latifa, matangazo yakatangazwa sana, watu wakashikwa na hamu kubwa ya kumsikiliza msichana huyo mrembo.
Kati ya watu waliokuwa na hamu ya kumsikiliza Latifa alikuwa Ibrahim, alijua kwamba angeumia hasa mara baada ya kumsikia msichana huyo akizungumzia kile kilichopita, hakutaka kujali sana, alichoamua kipindi hicho ni kumsikiliza tu.
Kwa kuwa alikuwa amekwishamwambia mzee Deo kuhusu Latifa, alichokifanya ni kumwambia kwamba msichana yule aliyekuwa amemkataa alitarajiwa kuhojiwa katika televisheni, hivyo akawa na hamu ya kutaka kumuona.
Siku hiyo ambayo ndiyo ilitakiwa kuonyeshwa kwa kipindi hicho, Ibrahim akaamua kumchukua mzee huyo na kumpeleka nyumbani kwake, hakumuhofia mke wake, alijua kwamba mwanamke huyo alikuwa mkorofi lakini kwenye suala la Latifa, hakutaka kusikia chochote kile.
“Umemleta kufanya nini humu?” aliuliza Nusrat huku akionekana kuwa na hasira, mbaya zaidi akaziba hata pua yake kumaanisha kwamba alikuwa akisikia harufu mbaya.
“Nimemleta, nataka kumuonyeshea yule msichana aliyenipenda, nikaamua kumuacha kwa ajili yako shetani,” alisema Ibrahim kwa kiburi.
“Ndani ya nyumba yangu?”
“Wewe mjinga nini, hebu tupishe, na ole wako ulete za kuleta, ndugu zako watakuta maiti tu humu ndani,” alisema Ibrahim, hata Nusrat alipomwangalia mumewe, alijua kwamba siku hiyo alikuwa tofauti, kama ni ng’ombe basi aliota mapembe.
Ibrahim akamchukua mzee Deo na kwenda kutulia naye kochini, akachukua rimoti ya televisheni na kisha kuiawasha. Mzee Deo alikaa kitini, hakujisikia kuangalia, hakuwa na amani kabisa kwani jinsi alivyokuwa akimwangalia Nusrat ambaye alikaa pembeni kabisa, alionekana kuwa na hasira mno.
Latifa alivyoonyeshwa kwenye televisheni, Ibrahim akajikuta akianza kububujikwa na machozi, moyo wake uliumia, kila alipokuwa akimwangalia msichana yule, akagundua kwamba aliitupa almasi jangwani na kuokota bati.
Msichana huyo mrembo, mwenye muonekano wa fedha akaanza kusimulia historia ya maisha yake. Kila mmoja akabaki kimya akimsikiliza, alianza kusimulia kuanzia mbali, tangu mama yake alipofukuzwa nyumbani kwao, alipokwenda nyumbani kwa mpenzi wake, Deo kisha kumfukuza, alionekana kuumia mno.
Mzee Deo aliposikia historia aliyokuwa akiisimulia Latifa, akashtuka, akaanza kumwangalia Latifa, akasimama kutoka katika kochi lile na kuisogelea televisheni, kila mmoja mule ndani akabaki akimshangaa.
“Ibrahim....” aliita mzee Deo, machozi yakaanza kumtoka.
“Nipo mzee....”
“Latifa ni binti yangu!” alisema mzee Deo huku akionekana kushangaa, Ibrahim akashtuka, si yeye tu, hata Nusratakashtuka.
“Unasemaje?”
“Kumbe Latifa ndiye mtoto wangu aliyezaliwa na Nahra,” alisema mzee Deo.
Hapo ndipo Ibrahim alipoanza kukumbuka mahojiano yale, alikumbuka Latifa alimtaja mtu aliyeitwa Nahra na Deo, wazazi wake waliokuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi mpaka baba yake alipomfukuza mama yake.
Mahojiano yale akayaunganisha na historia aliyowahi kusimuliwa na mzee huyo kwamba zamani alikuwa na mwanamke wa Kihindi, alimpa ujauzito lakini baadaye akafukuzwa nyumbani kwao, na alipokuja kwake, naye alimfukuza ila ni kwa sababu tu alitishiwa kuuawa na ndugu zake Nahra kwa kutumiwa watu waliokuwa na bunduki, na kama asingemfukuza basi angeuawa yeye.
“Ni mtoto wangu! Kumbe Latifa ni mtoto wangu!” alisema mzee Deo huku akijifuta machozi.
Ibrahim alishindwa kuamini, wakati mwingine alifikiri kwamba alikuwa ndotoni, katika kipindi chote alichokuwa akiishi na huyo mzee, alivyokuwa akizungumza naye kumbe alikuwa mzazi wa msichana aliyekuwa amemuacha, Latifa.
Latifa hakuwa na kipindi kirefu katika kituo kile, alichokifanya Ibrahim ni kumwambia kwamba ilikuwa ni lazima kumfuata Latifa huko na kumwambia ukweli kwamba alikuwa na baba yake nyumbani kwake.
“Ngoja nikamlete uzungumze naye,” alisema Latifa.
“Atakubali kuja?”
“Atakuja tu. Subiri,” alisema Ibrahim huku akionekana kuchanganyikiwa, hakutaka kuchelewa, akaondoka kuelekea huko, tena alikuwa akikimbia kwa kasi ajabu.

Jina la Ibrahim lilimchanganya, hakuamini kama kweli aliitwa na msichana yule kwa kuwa alikuwa akihitajika na mtu aliyejitambulisha kwa jina hilo. Huku akionekana kuwa na hasira, akatoka pamoja na ndugu zake kuonana na huyo mtu.
Alipofika, alipomwangalia Ibrahim, akajikuta akiingiwa na huruma, aliyesimama mbele yake alikuwa Ibrahim, yuleyule kijana aliyekuwa amemtesa na kumkataa kipindi cha nyuma, ila hali aliyokuwa nayo, ilimtia huruma mno.
“Ibarhim,” alijikuta akimuita kijana huyo aliyeonekana kupigwa na maisha.
“Latifa...” aliita Ibrahim, tayari machozi yakaanza kumbubujika, hata naye kumbukumbu za nyuma zikaanza kujirudia kichwani mwake.
“Umefuata nini?” aliuliza Latifa huku akiwa amesiamam.
“Kwanza naomba unisamehe kwa yote yaliyotokea, dunia imeniadhibu kwa kile nilichokufanyia,” alisema Ibrahim.
Japokuwa alijiahidi kwamba asingeweza kumsamehe mwanaume huyo lakini hakuwa na jinsi, kwa namna ambavyo alionekana mahali hapo, ilionyesha kabisa kwamba maisha yalimpiga, hivyo hakutaka kumwadhibu tena, alichokifanya ni kuukunjua moyo wake na kumsamehe kwa kila kitu kilichotokea.
“Nimekusamehe Ibrahim, dunia imekufunza,” alisema Latifa.
“Kuna kitu ninahitaji kutoka kwako.”
“Kitu gani?”
“Baba yako anateseka Latifa, kila ulichoambiwa ni kweli kilitokea, ila naye ana historia ya tofauti na hiyo uliyokuwa nayo,” alisema Ibrahim, alikuwa amemsogelea kidogo, kila mtu akashtuka.
“Baba yangu?”
“Ndiyo!”
“Nani?”
“Mzee Deo!”
“Hapana! Baba yangu kashakufa!”
“Una uhakika? Ulionyeshewa kaburi lake? Au hata picha yake unayo”
“Ibrahim, baba yangu! Haiwezekani!”
“Latifa, huu ndiyo muda wa kuusikia ukweli, twende ukamuone baba yako, ameteseka sana, kansa ya mguu ilisababisha kukatwa mguu wake, twende ukamuone, atafurahi kama akikuona,” alisema Ibrahim.
“Baba yangu......” alisema Latifa, sauti ya kilio chake ikaanza kusikika.
“Ni kweli, yupo hai, hana pa kuishi, amekuwa akiteseka miaka yote, alikuwa ombaomba mitaani, alifukuzwa kila sehemu. Nimekuwa nikiishi naye kwa kipindi kirefu pasipo kujua kwamba ni baba yako, historia aliyonisimulia, ni hiyohiyo ambayo umesimulia japokuwa kuna kitu ambacho haukukifahamu, si wewe tu bali hata marehemu mama yako hakukifahamu, nimemsaidia sana mpaka kufikia kipindi hiki. Naomba twende ukamuone, tuwahi, namjua mke wangu, anaweza hata kumuua,” alisema Ibrahim.
“Kumuua! Amuue baba yangu!”
“Ni mwanamke mwenye roho mbaya! Twende Latifa,” alisema Ibrahim, hawakutaka kusubiri, waliposikia kwamba mke wa Ibrahim angeweza kumuua mzee Deo, wote wakaingia ndani ya gari na kuanza kuelekea huko.
Garini, bado Ibrahim aliendelea kumuomba msamaha msichana huyo, alijutia matendo aliyoyafanya, hakuomba msamaha kwa kuwa Latifa alikuwa msichana bilionea, aliomba msamaha kwa kuwa alihitaji kusamehewa kwa yote aliyoyafanya.
“Ibrahi...nime...kus...ame..he..” alisema Latifa huku akilia.
Walichukua dakika kumi njiani ndipo walipofika alipokuwa akiishi Ibrahim. Kwa kuwa nyumba ilizungushiwa ukuta huku ikiwa na geti kubwa, Ibrahim akateremka na kwenda kulifungua geti lile ili gari liingizwe ndani.
Kitu cha ajabu alipofika katika eneo la nyumba hiyo, akapiga uyowe mkubwa, mbele yake alikuwepo mzee Deo, alikuwa hoi chini, kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma, muda huo napo damu zilikuwa zikimtoka katika kipande cha mguu wake, Nusrat alikuwa amemtoa ndani ya nyumba yake.
Latifa na watu wengine waliposikia uyowe huo, wakahomoka kutoka garini, wakajua kwamba kulikuwa na kitu ndani ya nyumba hiyo, walipolifungua geti dogo na kuingia ndani, wakamkuta Ibrahim akiwa amemshika mzee Deo aliyekuwa chini huku akilia, mzee huyo alikuwa hoi, damu ziliendelea kumtoka katika kipande chake cha mguu na alikuwa akilia kwa maumivu makali.
Wote wakamfuata, kila mtu aliyemwangalia, sura yake ilifanana na Latifa kwa mbali, hakukuwa na mtu aliyekuwa na ubishi kwamba mzee yule alikuwa mzazi wa Latifa.
Latifa akajikuta akianza kulia, hasira ikamkaba kooni dhidi ya Nusrat, alionekana kuwa na hasira mno.
“Hanijui, yaani pamoja na kuniumiza bado ananiumizia baba yangu! Atanitambua mimi ni nani,” alisema Latifa huku kwa kumwangalia tu ungegundua ni jinsi gani alikuwa na hasira.
Walichokifanya ni kumchukua na kumpeleka hospitalini huku Latifa akiahidi kwamba ni lazima angemuonyesha Nusrat yeye alikuwa nani.
****
Latifa alikuwa akilia tu, kila alipomwangalia baba yake, moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kama alikuwa kwenye hali ile. Watu wengine walimbembeleza anyamaze lakini hakunyamaza, hasira kali dhidi ya Nusrat ilimkamata mpaka kufikia kiasi cha kukunya ngumi.
Kitendo cha kupigwa baba yake na kuumizwa namna ile kulimuongezea hasira ya kumchukia Nusrat ambaye miaka michache nyuma alimuumiza kwa kumchukulia mwanaume wake, hakuonekana kuridhika, leo hii alimpigia baba yake.
“Nitamuonyesha,” alisema Latifa huku akionekana kuwa na hasira kali.
Hawakuchukua muda mrefu wakafika katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Japokuwa kipindi cha nyuma alisema kwamba baba yake alikuwa miongoni mwa watu aliokuwa akiwachukia kwa kuwa tu alkimfukuza mama yake lakini wakati alipokuwa akimwangalia, mateso aliyoyapata, chuki yote dhidi yake aliyokuwa nayo ikaondoka na huruma kumuingia.
Manesi waliokuwa na machela wakasogea lilipokuwa gari lile na kumpajndisha mzee Deo juu ya machela ile na kuanza kusukumwa kwenda kwenye chumba kimoja kilichoandikwa Theatre. Walipofika nje ya chumba kile, wakazuiliwa.
Watu waliokuwa wamegundua kwamba msichana aliyekuwa mbele yao alikuwa Latifa walibaki wakishangaa, hawakuamini kama kweli yule aliyesimama mbele yao alikuwa ndiye au alikuwa msichana mwingine aliyefanana naye.
“Inawezekana ndiyo yeye,” alisema jamaa mmoja huku akimwangalia Latifa ambaye machozi yalikuwa yakimbubujika tu.
“Labda! Ila awe hapa anafanya nini?”
“Sijui, hebu tusogee karibu zaidi tumuone.”
Kila aliyepita, hakuacha kumshangaa Latifa aliyekuwa akilia tu. Ibrahim alikuwa kimya, moyo wake ulimuuma, alimzoea sana mzee Deo, alikuwa rafiki yake mkubwa, alimpenda pasipo kujua kwamba mzee huyo alikuwa mzazi wa msichana aliyemuacha kipindi cha nyuma, Latifa.
Madaktari wakawa wanapishana mlangoni, wengine waliingia na wengine kutoka. Mgonjwa aliyeletwa kwao alionekana kuwa wa maana sana, ilikuwa ni bora kuleta utani kwa mgonjwa mwingine lakini baba yake Latifa.
Baada ya msaa mawili, mlango ukafunguliwa na daktari kutoka, akawaita watu hao ofisini kwake kwa lengo la kuzungumza nao. Walipofika huko, akawaweka chini.
“Hali ya mgonjwa si mbaya, alitoneshwa tu kidonda chake,” alisema Dk. Mimi, mwanamke mzuri mwenye umbo la kuvutia.
“Ila ninataka kuzungumza naye, naweza kufanya hivyo?”
“Hakuna tatizo, unaweza ila kama baada ya saa moja hivi, atahitaji muda wa kupumzika,” alisema Dk. Mimi.
“Sawa!”
Kusubiri halikuwa tatizo kabisa, alitaka kumsikia baba yake akizungumza kile alichokuwa akitaka kuzungumza. Alitaka kusikia kile ambacho hakuwa amekisikia kuhusu mama yake, kile alichosema Ibrahim kwamba mzee huyo alikuwa na la ziada.
“Nyamaza Latifa,” alisema Dominick huku akimvuta Latifa upande wake.
Walitulia kwa muda wa saa moja na ndipo walipoambiwa kwamba wangeweza kumuona mgonjwa wao. Wakainuka na kuingia ndani. Latifa alipomuona baba yake kitandani pale, uso wake ukajawa na tabasamu pana na kuanza kumsogelea.
Moyo wake ukaingiwa na hisia kali, ukapatwa na furaha kubwa kiasi kwamba alishindwa kuliuia tabasamu lake kutawala usoni mwake.
“Baba...”
“Naam mwanangu.”
“Nini kilitokea?”
“Maisha, maisha yalinipiga na ndiyo maana nipo hivi,” alijibu mzee Deo.
Latifa akanyamaza, akamsogelea baba yake kitandani pale na kumbusu katika shavu la uso huku machozi ya furaha yakimbubujika mashavuni mwake.
“Umefanana sana na mama yako,” alisema mzee Deo.
“Nani? Mimi?”
“Ndiyo! Mama yako alikuwa mrembo kama ulivyo,” alisema mzee Deo.
“Sasa kwa nini ulimfukuza wakati alipokuwa na mimba yako?”
“Nilimpenda sana mama yako, nilijitolea kwa kila kitu, nilitaka niishi naye japokuwa nyumbani kwao hawakuwa wakinipenda kisa tu nilikuwa mtu mweusi. Alipofukuzwa kwao, akakosa pa kwenda, alichoamua ni kuja nyumbani kwangu.
“Hata kabla hajafika, tayari wazazi wake waliwatuma watu wawili, walikuja huku wakiwa na bunduki, waliniambia kwamba endapo ningempokea mama yako na kuishi naye, hakika wangeniua, na waliniambia kabisa kwamba walitumwa na wazazi wake,” alisema mzee Deo na kuendelea:
“Niliogopa sana, niliona kweli ningeuawa, nilichokifanya ni kumfukuza Nahra huku nikiumia moyoni. Sikufanya vile kwa kuwa sikuwa nikimpenda, la hasha! Nilifanya vile kwa kuwa nyuma yangu niliwekewa bunduki. Alipoondoka, sikukaa nyumbani, niliondoka kwenda kumtafuta, usiku mzima nilimtafuta kila kona, ila sikufanikiwa kumpata, huo ukawa mwisho wa kuonana naye,” alisema mzee Deo, tayari naye machozi yalianza kumbubujika.
Watu wote waliokuwa mahali pale walikuwa kimya wakimsikiliza, mzee huyo alitia huruma kitandani pale, alionekana kukosa nguvu na alikuwa mtu aliyekosa tumaini kabisa.
“Nisamehe Latifa,” alisema mzee Deo.
“Nimekusamehe baba! Kila kitu kilichopita, kimepita, ni lazima tugange yajayo,” alisema Latifa, hapohapo akayapeleka macho yake usoni mwa Ibrahim aliyekuwa kimya.
“Ulimfahamu vipi Ibrahim?”
“Ni mtu ambaye amenisaidia sana, bila yeye nafikiri leo hii nisingekutana na wewe. Alinionyeshea upendo mkubwa sana, sikuamini kama kuna watu wenye roho nzuri kama alivyokuwa yeye. Nimekuwa naye kipindi chote, nilipopata tatizo, alinisaidia kwa fedha kidogo aliyokuwa nayo.
“Hakujua kama mimi ni baba yako, alinionyeshea upendo kwa kuwa aliona nastahili kufanyiwa hivyo japokuwa mke wake alikuwa ni tatizo kubwa. Binti yangu! Ibrahim alinihadithia kila kitu kuhusu wewe hata kabla hajajua kama mimi ni mzazi wako, naomba umsamehe, inawezekana mambo yote anayopitia, shida zote anazozipata ni kwa ajili ya laana yako, msamehe na sahau kila kitu,” alisema mzee Deo.
Latifa akayapeleka tena macho yake kwa Ibrahim, alipanga kutokusamehe katika maisha yake lakini kila alipokuwa akimwangalia, bado mwanaume huyo alionekana kuhitaji msamaha.
Alionekana kupigika katika maisha yake, alitia huruma lakini pamoja na hayo yote, alifanya kazi kubwa sana kumlea baba yake. Hakuwa na fedha za kutosha lakini nkiasi hichohicho kidogo alikitumia kwa ajili ya kumtibu baba yake, hakika alifganya jambo kubwa lililohitaji sifa kubwa kutoka kwake.
Hakuongea kitu, alichokifanya ni kumsogelea na kumkumbatia. Wote wawili walikuwa wakibubujikwa na machozi. Latifa hakuwa na jinsi, aliukana moyo wake na kumsamehe mwanaume huyo aliyeonekana kuhitaji sana msamaha.
“Nisamehe Latifa.”
“Nimekusamehe Ibrahim, Ahsante kwa yote uliyomfanyia baba yangu,” alisema Latifa huku akijifuta machozi.
“Naomba umsamehe Nusrat pia! Ni mwanamke mpumbavu asiyejua lile analolifanya. Naomba umsamehe.”
“Nimsamehe Nusrat?”
“Ndiyo!”
“Kwa hivi alivyomfanyia baba yangu?”
“Latifa! Hebu sahau kwanza. Wewe ni mtu mkubwa na mwenye heshima, tazama dunia nzima inakutazama wewe, usiposamehe, vipi wale vijana wanaotaka kuwa kama wewe? Nao watakapokosewa hawatakiwi kukosea kisa wewe haukusamehe? Vipi kuhusu wale watoto wanaotaka kuwa kama Latifa, kweli nao hawatakiwi kusamehe? Samahe saba mara sabini, au umesahau hilo?” aliuliza Ibrahim.
“Nakumbuka.”
“Basi naomba umsamehe!”
“Nimemsamehe!”
“Nashukuru!”
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa maisha mapya, Latifa hakuwa na kinyongo, moyo wake ulilainika na hakutaka kuwa na kingo na mtu yeyote yule, alichokiamua ni kumsahmehe kila mtu aliyewahi kumfanyia ubaya kwa makusudi au bahati mbaya.
Alikuwa mtu mwenye mafanikio, bilionea, alichokifanya ni kumsafirisha baba yake nchini Marekani, alitaka akatibiwe huko na kuishi naye hukohuko. Kwa Ibrahim, japokuwa alimfanyia mambo mabaya nyuma hakutaka kumuacha hivihivi, aliamua kumsaidia kama alivyomsaidia baba yake.
Akamnunulia nyumba kubwa Mbezi Beach na kumgawia kiasi cha shilingi milioni mia tatu kwa ajili ya kufanya biashara zake kitu ambacho kwa Ibrahim kilikuwa kitu kikubwa, baada ya wiki moja, akaamua kumpa talaka Nusrat na kumuoa mwanamke mwingine na kuishi naye nyumbani kwake huku akifungua biashara kubwa.
Kwa Latifa, akaamua kufunga ndoa ya kishria Dominick na watu hao kuishi pamoja kwa amani ni na upendo ambapo baada ya miaka miwili, wakafanikiwa kupata mtoto wa kiume waliyemuita kwa jina la Godlove.
Dawa yake ya kansa ya Morphimousis iliendelea kutikisa duniani, watu waliokuwa na magonjwa ya aina hiyo waliendelea kutibiwa na kupona. Aliendelea kuingiza kiasi kikubwa cha fedha, utajiri wake ukazidi kuongezeka maradufu.
Baada ya miaka mitano kupita, wakapata mtoto wa pili wa kike waliyempa jina la Cecilia. Latifa alikuwa na furaha tele, moyo wake ulikuwa na amani, hakuwa na kinyongo na mtu yeyote, maisha yake yalikuwa ya furaha tele.

MWISHO....

Nashukuruni sana kwa kuifuatilia simulizi hii. Mungu awabariki....TOA MAONI YAKO

CHANZO : BURE SERIES
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom