bayona_stories
Member
- Apr 19, 2023
- 77
- 123
NILINUSURIKA KUCHOMWA MOTO 1
Nilikuwa nimekaa zangu sina hili wala lile, mara simu ikaingia kutoka kwa rafik yangu, akanimbia leo unaonaje tukachek mechi pale uwanjani? Nikamwambia sina uhakika kama nitapata ticket, akaniambia hilo ndo tatizo la ushamba wako. Tickets tutapata, kwanza leo hatuchezi na timu kubwa kwamba hayo mambo yataleta shida, nikamwambia sawa basi tutaingia.
Alikuwa shabiki wa timu ambayo na mimi nilikuwa shabiki wa timu hiyo hiyo, hivyo tukakubaliana kwenda kuicheki hiyo mechi. Nilijiandaa mida ilipofika, na kwa sababu umbali kutoka ninapokaa mpaka uwanja wa mpira ulipo sio mkubwa, niliamua tu kutembea kwa mguu wakati huo nikiwa nimekubaliana na rafiki yangu Johnson kukutana pale pale uwanjani.
Nilifika sehemu fulani ambapo nilikuta watu wengi wakiwa wamekusanyika, kuna mtu alikuwa amekamwatwa pale
Alikuwa amepigwa vibaya sanaaa, na watu wengi wamemzunguka, wakiwa wamemfunga kamba za miguu na mikono.
Nikajaribu kuwauliza watu ni nini kinaendelea, mtu mmoja akanieleza
kuwa huyu amekamatwa akiiba betri ya gari ambayo ilikuwa imewekwa juu ya gari lile, sasa plan ilichorwa kuanzia kwa wenzake halafu yeye anapokea na kupeleka sehemu nyingine,
Ikiwa na maana kuwa aliyetoa Betri pale sio yeye, ni mtu mwingine ambaye aliivusha na kumpa mwingine
Huyo mwingine ndo akampa yeye, na yeye kuna mtu alikuwa anaenda kumpa, ndivyo wezi wanavyofanya huku, unakuta kwenye line wapo kama watano, sasa ili iwe vigumu kukamata kitu chako, wanachokifanya ni kupokezana tu, ili ukimshtukia mmoja ukija kumsearch usipate kitu, na hao wote
watano kwa pamoja hutaweza kuwajua. Ndio maana huku ukishaibiwa kitu sahau kuhusu kukipata.
Lakini za mwizi siku zote huwa ni Arobaini, katika line ya hawa leo huyu ndo kapatikana. Kuna mzee mmoja ni kama kaushtukia mchezo akajitoa mwanga kupiga kelele na kumrukia ndo watu
wote hawa tukafika na kuanza kumshughulikia. Huyu mzee kajitoa mwanga kwa sababu ukiwaharibia hivi baadaye wanaanza kukuwinda, wanaweza kukuchoma visu mpaka kukuua, ndio maana wengi wakiona wananyamaza, hawasemi kitu wala kufanya kitu.
Lakini tutakachomfanyia huyu itakuwa funzo
kwa wenzake wanaotutaabisha usiku na mchana. Walimpiga vibaya sana, kila mmoja anapiga anapoona
Akajitokeza baba mmoja akasema ole wa mtu yeyote hapa aite polisi, ukigundulika na wewe tunakujumlisha naye, maana nyie mtakuwa wamoja.
Hawa wajinga ukiwapeleka polisi kesho wametoka
Na wanaendelea na uhalifu wao, sisi ndio tutawashughulikia wenyewe.
Muda huo anaongea watu wanaendelea kumpa kipondo jamaa, wengine hata hawakusikiliza anasema nini, japo alikuwa akitumia sauti ya juu. Ila wengi walisapport hakuna kuita polisi hakuna kuita polisi
Kipigo kiliendelea na jamaa alikuwa hatamaniki. Alipigwa mpaka ungetamani umuondoe pale hata kama ni mwizi mkubwa kiasi gani. Ila sasa wananchi wenye hasira kali huwezi kuwaeleza chochote hapo.
Yule baba aliyekuwa anasema mtu yeyote asiite polisi alikuwa ana hasira sanaa na hao jamaa (wezi) yaani alikuwa anakaza apigwe apigwe!
Sasa akapata wazo akasema, huyu jamaa tumchome moto, mimi natoa petroli kwa gharama yangu leteni mipira tumchome moto,
Yule mwizi alibembelezaa
Japo ndo hivo maneno yalikuwa hayawezi hata kutoka vizuri lakini alibembeleza sana wasimchome na wakati huo wameshamvunja hadi miguu
Yule baba akasema kama unataka kusalimika tuambie uliyekuwa unaenda kumpasia betri ni nani na uliipokea kutoka kwa nani?
Jamaa hawezi hata kuongea
Wakamuuliza, tuambie ulikuwa unampasia nani? Leo lazima tuwapate wote. Usiposema tunakuchoma moto unakufa unawaacha.
Alikuwa hawezi hata kuongea,
Alinyoosha kidole kuelekea upande niliokuwepo mimi akasema huyo halafu akawa hawezi kuongea tena.
Sasa mimi nilikuwa mtu ambaye sijarusha hata jiwe moja kwa huyo mwizi kwa sababu hata siwezi yaani. Na hilo ndo likawa kosa kubwa
Watu waligeuka
wote wakasema kumbe ni wewe, kuna kama wawili walikuwa wanatetea ambao waliniona nikija plus yule aliyenisimulia kinachoendelea,
Lakini wapiii, watu wote hasira zao zikaamia kwangu maana mtu mwingine aliyekuwa pembeni yangu alikuwa ni yule aliyeibiwa na wengine walikuwa ni akina mama na wengine sikumbuki, Nilivutwa na kuingizwa kati,
Watu wanapiga kelele, wachomeni wote wachomeni wote wachomeni wote,
Nikawa napambana kuwaambia mimi simjui huyu mtu, mimi ni mpita njia nimekuta mwizi anapigwa nikasimama…wakati huo wapo wanaonitetea pia ila ni wachache sanaaa, wengine hata hawaelewi chochote ila wamekazia apigwe achomwe moto
Eeh bhana ile siku sitakaa niisahau,
ila kukutoa tu wasiwasi, ni kuwa bado niko hai ndo maana nipo hapa nakusimulia,
Sasa nini kilitokea? Na niliponaje?!
Tukutane sehemu ya mwisho inayofuata nikumalizie kisa hiki
Nilikuwa nimekaa zangu sina hili wala lile, mara simu ikaingia kutoka kwa rafik yangu, akanimbia leo unaonaje tukachek mechi pale uwanjani? Nikamwambia sina uhakika kama nitapata ticket, akaniambia hilo ndo tatizo la ushamba wako. Tickets tutapata, kwanza leo hatuchezi na timu kubwa kwamba hayo mambo yataleta shida, nikamwambia sawa basi tutaingia.
Alikuwa shabiki wa timu ambayo na mimi nilikuwa shabiki wa timu hiyo hiyo, hivyo tukakubaliana kwenda kuicheki hiyo mechi. Nilijiandaa mida ilipofika, na kwa sababu umbali kutoka ninapokaa mpaka uwanja wa mpira ulipo sio mkubwa, niliamua tu kutembea kwa mguu wakati huo nikiwa nimekubaliana na rafiki yangu Johnson kukutana pale pale uwanjani.
Nilifika sehemu fulani ambapo nilikuta watu wengi wakiwa wamekusanyika, kuna mtu alikuwa amekamwatwa pale
Alikuwa amepigwa vibaya sanaaa, na watu wengi wamemzunguka, wakiwa wamemfunga kamba za miguu na mikono.
Nikajaribu kuwauliza watu ni nini kinaendelea, mtu mmoja akanieleza
kuwa huyu amekamatwa akiiba betri ya gari ambayo ilikuwa imewekwa juu ya gari lile, sasa plan ilichorwa kuanzia kwa wenzake halafu yeye anapokea na kupeleka sehemu nyingine,
Ikiwa na maana kuwa aliyetoa Betri pale sio yeye, ni mtu mwingine ambaye aliivusha na kumpa mwingine
Huyo mwingine ndo akampa yeye, na yeye kuna mtu alikuwa anaenda kumpa, ndivyo wezi wanavyofanya huku, unakuta kwenye line wapo kama watano, sasa ili iwe vigumu kukamata kitu chako, wanachokifanya ni kupokezana tu, ili ukimshtukia mmoja ukija kumsearch usipate kitu, na hao wote
watano kwa pamoja hutaweza kuwajua. Ndio maana huku ukishaibiwa kitu sahau kuhusu kukipata.
Lakini za mwizi siku zote huwa ni Arobaini, katika line ya hawa leo huyu ndo kapatikana. Kuna mzee mmoja ni kama kaushtukia mchezo akajitoa mwanga kupiga kelele na kumrukia ndo watu
wote hawa tukafika na kuanza kumshughulikia. Huyu mzee kajitoa mwanga kwa sababu ukiwaharibia hivi baadaye wanaanza kukuwinda, wanaweza kukuchoma visu mpaka kukuua, ndio maana wengi wakiona wananyamaza, hawasemi kitu wala kufanya kitu.
Lakini tutakachomfanyia huyu itakuwa funzo
kwa wenzake wanaotutaabisha usiku na mchana. Walimpiga vibaya sana, kila mmoja anapiga anapoona
Akajitokeza baba mmoja akasema ole wa mtu yeyote hapa aite polisi, ukigundulika na wewe tunakujumlisha naye, maana nyie mtakuwa wamoja.
Hawa wajinga ukiwapeleka polisi kesho wametoka
Na wanaendelea na uhalifu wao, sisi ndio tutawashughulikia wenyewe.
Muda huo anaongea watu wanaendelea kumpa kipondo jamaa, wengine hata hawakusikiliza anasema nini, japo alikuwa akitumia sauti ya juu. Ila wengi walisapport hakuna kuita polisi hakuna kuita polisi
Kipigo kiliendelea na jamaa alikuwa hatamaniki. Alipigwa mpaka ungetamani umuondoe pale hata kama ni mwizi mkubwa kiasi gani. Ila sasa wananchi wenye hasira kali huwezi kuwaeleza chochote hapo.
Yule baba aliyekuwa anasema mtu yeyote asiite polisi alikuwa ana hasira sanaa na hao jamaa (wezi) yaani alikuwa anakaza apigwe apigwe!
Sasa akapata wazo akasema, huyu jamaa tumchome moto, mimi natoa petroli kwa gharama yangu leteni mipira tumchome moto,
Yule mwizi alibembelezaa
Japo ndo hivo maneno yalikuwa hayawezi hata kutoka vizuri lakini alibembeleza sana wasimchome na wakati huo wameshamvunja hadi miguu
Yule baba akasema kama unataka kusalimika tuambie uliyekuwa unaenda kumpasia betri ni nani na uliipokea kutoka kwa nani?
Jamaa hawezi hata kuongea
Wakamuuliza, tuambie ulikuwa unampasia nani? Leo lazima tuwapate wote. Usiposema tunakuchoma moto unakufa unawaacha.
Alikuwa hawezi hata kuongea,
Alinyoosha kidole kuelekea upande niliokuwepo mimi akasema huyo halafu akawa hawezi kuongea tena.
Sasa mimi nilikuwa mtu ambaye sijarusha hata jiwe moja kwa huyo mwizi kwa sababu hata siwezi yaani. Na hilo ndo likawa kosa kubwa
Watu waligeuka
wote wakasema kumbe ni wewe, kuna kama wawili walikuwa wanatetea ambao waliniona nikija plus yule aliyenisimulia kinachoendelea,
Lakini wapiii, watu wote hasira zao zikaamia kwangu maana mtu mwingine aliyekuwa pembeni yangu alikuwa ni yule aliyeibiwa na wengine walikuwa ni akina mama na wengine sikumbuki, Nilivutwa na kuingizwa kati,
Watu wanapiga kelele, wachomeni wote wachomeni wote wachomeni wote,
Nikawa napambana kuwaambia mimi simjui huyu mtu, mimi ni mpita njia nimekuta mwizi anapigwa nikasimama…wakati huo wapo wanaonitetea pia ila ni wachache sanaaa, wengine hata hawaelewi chochote ila wamekazia apigwe achomwe moto
Eeh bhana ile siku sitakaa niisahau,
ila kukutoa tu wasiwasi, ni kuwa bado niko hai ndo maana nipo hapa nakusimulia,
Sasa nini kilitokea? Na niliponaje?!
Tukutane sehemu ya mwisho inayofuata nikumalizie kisa hiki