SEHEMU YA 145
Erica alivyofika nyumbani kwao, jambo la kwanza alianza kumsimulia mama yake kuhusu rafiki yake mpya aitwaye Samia,
“Oooh ushapata rafiki eeeh! Naimani mwanangu hautopooza tena”
“Ndio mama, nimefurahi sana ila naimani mara moja moja utaniruhusu nikamtembelee kwao”
“Hakuna hiyo kitu labda yeye ndio aje hapa”
“Sawa mama, napo hakuna tatizo”
Basi Erica aliingia chumbani kwake na alipomaliza kubadili nguo tu alienda kumwambia Erick kuhusu rafiki mpya aliyempata maana kwake ilikuwa ni kawaida kwa jambo lolote likitokea kwake basi ni lazima aje kuhadithia,
“Ooooh hongera sana mdogo wangu, nimefurahi kusikia hivyo kwani najua sasa utaanza kuwa na furaha, tatizo lako hupendi kuwa na urafiki na wasichana wenzio ila leo Mungu ni mwema maana umeweza kuwa na urafiki na msichana mwenzio kwakweli nimefurahi sana mdogo wangu”
Basi wakaongea ongea pale na kisha wote kwa pamoja kutoka na kwenda kula.
Muda wanakula, ni muda ambapo Junior na Vaileth nao walikuwa wanakula kwahiyo mezani walikuwa wanne ila macho ya Erica yalikuwa yakigonga kwa Junior na Vaileth ila aliwaona kama wakikonyezana vile, basi alikuwa akiwaangalia sana na wao hata hawakuwa na habari kuhusu lile swala na walipomaliza kula, Vaileth alitoa vyombo vyake pamoja na vyombo vya Junior huku Erica akitoa vyombo vyake na vya kaka yake.
Waliporudi chumbani, Erica alienda tena kuongea na kaka yake,
“Mmmmh leo sasa, ndio dada Vaileth na Junior nimewaona kabisa wakiwa wanakonyezana”
“Ila usishangae sana Erica, yule ndio shemeji yangu kwa Junior ujue na wewe ndio wifi yako”
“Ila mbona dada Vain i mkubwa kwa Junior?”
“Mapenzi hayana umri Erica!”
“Mmmmh!”
“Ndio hivyo, mapenzi hayachagui umri, hayachagui kabila wala rangi, mapenzi ni kama nyasi yani huota popote”
“Aaaah kumbe! Basi nimekuelewa”
Siku hiyo Erica alirudi tu chumbani kwake na kwenda moja kwa moja kulala tu.
Leo mama Angel alienda kwenye biashara yake, ila alipofika na kukaa kaka kidogo alipigiwa simu na rafiki yake Dora,
“Nipo mitaa ya ofisi yako hapa, uko wapi?”
“Mbona nipo ofisini”
“Basi nakuja”
Baada ya muda kidogo Dora aliwasilia kwenye ofisi ya mama Angel na kuanza kuongea nae mambo mengi ikiwa ni pamoja na kusifia ile ofisi yake,
“Unajua sikuwahi kuingia humu jamani, kwakweli hongera sana rafiki yangu”
“Asante”
“Kwasasa naamini kuwa mara nyingine maisha ni jinsi wewe binafsi unavyochagua, yani Mungu ni mwema kwetu ila sisi wanadamu tuna mtindo wa kulazimisha mambo na mwisho wa siku tunaharibu kusudi la Mungu katika maisha yetu. Nakumbuka mimi nilikuwa muhuni sana, na uhuni ulikuwa kama sehemu ya maisha yangu, sikutaka mtu aniambie chochote kile, yani mtu akisema swala la Dora acha uhuni basi mtu huyo nilimuona ni mbaya na sikutaka hata kumuona tena, ila kwasasa sitamani hata kidogo mwanangu Jesca kuwa na tabia kama zangu, mimi nikawa kama sijasoma vile yani kama nimesomea uhuni sasa maana kila aina ya umalaya niliifanya, kwakweli kuna muda mwingine nastahili kukupongeza sana tu”
“Mmmh ila shoga yangu nami nimepitia makubwa sana, yani dah huwa nikikumbuka hadi huwa siamini kama niliwezaje kukwepa ile misumari, loh! Nimeandamwa mimi jamani, nimeandamwa hatari, kila niliposhika palikuwa hapashikiki na kote naambulia machungu tu, ila kwa Erick nashukuru sana Mungu maana alinisimamia”
“Nakumbuka shoga yangu, na yule mjinga Sia ndio angekuvuruga kabisa nay ale madawa aliyotaka kumpa Erick, uwiii ule ndio ulikuwa muda ambapo Erick angekusahau nadhani sijui ungeenda kuolewa mke wa pili kwa Bahati maana ulikuwa na mawazo wewe”
Mama Angel alicheka kisha akamwambia,
“Tena umenikumbusha kuhusu huyo Sia”
“Eeeeh kafanyaje tena?”
Basi mama Angel alianza kumsimulia mlolongo mzima wa jinsi alivyompigia simu Tumaini na jinsi ilivyokuwa hadi muda ambao Tumaini alienda kwake akilia, kwahiyo yote alimsimulia basi Dora akamwambia,
“Mmmmh shoga yangu, unajua mimi hadi leo simuamini Sia kabisa, yani simuamini yule mwanamke kama kweli aliamua kwa moyo safi kuachana na nyie!! Sijui kwakweli ila sina imani nae”
“Ila kwanini unasema hivyo?”
“Hebu angalia hata hilo tukio la Tumaini, alimgomea kuja nae kwako, Tumaini akadanganya anaenda ofisini kwa mumewe ila hajakubali hadi kamsindikiza, haya sasa nini kimetokea baada ya kumshusha? Tumaini kamkuta mumewe na mwanamke ofisini hivyo Tumaini akapaniki na moja kwa moja akaja kwako, yani hapo jua kuwa Tumaini alivyokuja kwako basi nae alikuwa nyuma yake yani hapo tambua kuwa nyumbani kwako panajulikana na Sia tayari”
“Mmmmh!”
“Usigune, angalia tena hilo tukio huyo mwanamke kaingia dakika mbili kwenye ofisi ya kaka yako na muda kidogo Tumaini nae kaingia, kamzaba vibao kidogo kazimia, haya kazinduka Tumaini kaondoka kwa hasira na huyo mwanamke nae kaondoka, je kwanini asieleze shida yake kama ni kweli alikuwa na shida?”
“Inamaana ni ushirikina?”
“Mambo mengine sio hata ushirikina ila watu wana mbinu zao za kijasusi”
Dora alicheka kidogo kisha akasema tena,
“Yani ni hivi, yule Sia mimi simuamini ujue yani simuamini kabisa, kwa alichokifanya kwa Steve hapana kwakweli”
“Alifanyaje kwani?”
“Kwanza, alienda kujifungua kimya kimya tena kwa operesheni, hivi jamani mtu unajifungua kwa kisu kimya kimya kweli! Haya sasa, karudi kwa mumewe baada ya mwezi mmoja, hivi nani atamuamini yule mwanamke kama hajatoka kwa mwanaume wake mwingine kulelewa huko? Steve nae akachekelea tu mtoto wangu, mtoto wangu loh siku hiyo tumeenda na mama kumuona mtoto Mungu wangu yani mtoto hafanani na sisi hata ukucha, tukamuomba kwenda kupima kagoma, sasa tufanyeje jamani! Unajua Sia hajatulia kabisa, yani yule ana wanaume wengi hadi mwisho wa siku hajui baba wa mtoto ni nani, ila baada ya hayo ikawa kama akili ya Steve imerudi hivi basi tukaondoka na mdogo wetu tena kutugelesha mwanzoni alianza kumuita mtoto Steve, mwanamke shetani kabisa yule”
“Kheee kumbe ndio alifanya hivyo jamani!”
“Ndio, kuna siku nilikutana nae wakati mtoto sijui ana miezi saba nikakuta mtoto anasura nyingine yani sio ile ya udogoni, kwakweli ndio hafanani na sisi hata kidogo, kama hajazaa na wavua samaki huko ilia pate samaki wa bure sijui, nikamuuliza, ndio huyu Steve? Akasema ooh nyie si mlimkataa, nimembadilisha jina, anaitwa John, nikasema huyu mwanamke hajielewi yani anatanga tanga tu, sasa nadhani anampelekea baba yoyote na kumwambia mtoto wake na kumpa jina la huyo baba ila mtu aamini kuwa ni mwanae. Nikakumbuka hadi kipindi kile alichodai kuwa ana mimba ya Erick”
“Yani yule msichana ana wazimu ujue, sikapendi kweli. Kalinichanganya sana akili kipindi kile, ila ushanitisha tayari, inamaana amepafahamu kwangu?”
“Usichanganyikiwe ila kuwa makini tu shoga yangu yani mimi nimefanya kukutahadharisha tu na si vinginevyo”
“Sawa, nashukuru”
Kisha Dora akamkumbusha swala la kumtafutia mdogo wake kazi, kisha alimwambia kuwa atamkumbusha mumewe juu ya swala hilo.
Kwa muda huo waliongea sana hadi muda ulipofika ambapo mama Angel alienda kufatwa na mumewe ili waende nyumbani kwani mama Angel alikuwa anaenda hapo ofisini kwake ili asilale sana nyumbani.