SEHEMU YA 62
Basi walifika kwenye hoteli na kushuka kisha wakakaa na kuagiza chakula ambapo walikuwa wakila na kuongea mambo mbalimbali,
“Sasa mke wangu, nikuombe kitu kimoja”
“Kitu gani hiko?”
“Unaonaje Angel akimaliza kidato cha nne tumpeleke Africa kusini”
“Mmmh hapana jamani, inamaana hutaki kumuona Angel nyumbani eeh!”
“Sina maana hiyo mke wangu, ila nilitaka kumtenganisha na hawa wanaume wakware”
“Kwani huko Afrika kusini hakuna wakware? Ningekuwa naenda kuishi nae sawa, ila kwenda kuishi peke yake hapana jamani, nataka nione watoto wangu wote pamoja, ila ninapokosea kwenye malezi nijue mume wangu”
“Sawa, nimekuelewa mke wangu. Ila nilikuwa natoa wazo tu hilo”
“Huko tuendage sisi wenyewe, ila watoto wangu hapana jamani”
Mara mama Angel alishangaa kushikwa bega, kugeuka hivi ni mtu ambaye alikuwa akifahamiana nae vizuri sana, ambaye alimwambia kwa mshangao,
“Kheee Erica!”
“Jamani Fetty kumbe upo!”
Basi walikumbatiana kwa furaha kisha Fetty alikaa na kumsalimia baba Angel pia huku akisema,
“Kweli nimeamini katika dunia kuna mapenzi ya dhati, kwa hakika nyie mlipendana yani hadi leo mpo pamoja?”
Mama Angel na baba Angel walitabasamu huku baba Angel akimwambia,
“Ndio, penzi la kweli lipo ila cha muhimu ni kumpata mtu ambaye atakupenda kweli na utampenda kweli. Katika mapenzi si vizuri kukurupuka, yani ukikurupuka lazima ukutane na mauzauza na mbeleni yakakushinda”
“Kweli kabisa uyasemayo, kama mimi najuta kukurupuka kuolewa”
Mama Angel alimuuliza,
“Kivipi? Si uliolewa na Bahati wewe?”
“Ndio, nilijua atanipenda na kunijali vile alivyokuwa akikupenda wewe na kukusumbua kumbe hakuna kitu wala nini?”
“Kheee jamani, tena nimekumbuka kuhusu Bahati (Kisha akimuangalia mumewe na kumuuliza) Hivi yule Samir sio mtoto wa Bahati kweli? (Alimuangalia Fetty na kumuuliza) Bahati hana mtoto wa kuitwa Samir?”
“Kafanyeje huyo Samir?”
“Ni anamsumbua mwanangu balaa, yani hadi kichwa kinaniuma sababu ya huyo mtoto, haogopi kitu na haogopi mtu yeyote, yani anachojua yeye ni usumbufu tu basi”
“Duh! Pole, huyo Samir simfahamu labda kama alizaaga na kumficha ila kuna mambo ya Bahati yanatia hadi kichefuchefu”
“Mambo gani hayo?”
“Yani huwezi amini, Bahati alizaa na yule mkewe aliyemuacha na kunioa mimi, kumbe alizaa pia na mdogo wa mke wake, halafu kumbe Bahati alimbaka mama mkwe wake na yule mama akapata ujauzito na kwenda kuutoa ila kumbe iligoma kutoka, kwahiyo Bahati kazaa na familia nzima, yani ninavyokwambia hadi kichefuchefu kuanza kufikiria hayo”
“Mmmh mbona mtihani huo pole”
Baba Angel aliwaaga kidogo kuwa anakwenda maliwatoni kwani aliona hao wanawake hawakawii hata kuzungumzia na yeye, basi aliondoka na kuwaacha pale ambapo Fetty aliendelea kuongea,
“Asante shoga yangu, kikweli nimechoka yani nimechoka kabisa, maana hao watoto wote wamebwagwa pale nyumbani, halafu kumbuka mimi nina mtoto pia nilizaa na yule kichwa rungu, kwahiyo jumla wanne, halafu Bahati nimezaa nae watoto wawili jumla watoto sita, na sijui huko nje kama hana watoto wengine, umenipa habari zakina Samir tena kichwa kinanipasuka hapa”
“Kwahiyo wewe umekuja hapa hotelini mwenyewe?”
“Ndio, nimekuja kupumzisha mawazo jamani, ile sio ndoa bali ni ndoano, yani kukurupuka huku kubaya sana. Leo alikuja yule mama mkwe wake, uwiii katukana jamani, katukana mkoo wangu mzima, kiukweli najuta kumfahamu Bahati, najuta kuolewa nae”
“Ila wewe ulikuwa huyajui hayo wakati unaolewa nae?”
“Mimi nilijua tu kazaa na yule mke wake, na vile mkewe alikuwa mshirikina basi niliona ana sababu madhubuti kabisa ya kuachana na mkewe. Kuna kipindi alikuwa akinisumbua hatari wakati nina mimba ya huyu mtoto wa mwisho, si ndio wakanibwagia watoto wote, nimepata shida shoga yangu balaa. Ila wanaume hawa sio wa kuwaamini jamani, mwanaume sio mama yako wala sio baba yako”
“Ila mimi mume wangu namuamini”
“Usimuamini kivile, siku ukiletewa mtoto aliyezaa huko wapi sijui nadhani utapata ugonjwa wa kupooza, jamani usimuamini mwanaume, ni kweli anakupenda ila usimuamini kupitiliza. Hebu ona toka ameenda chooni hadi sasa hajarudi mmmh!”
“Mmmh na wewe Fetty jamani, hadi shemeji yako unamnanga mmmh!!”
“Hivi kwanza Bahati hajakusumbua? Kuna kipindi wimbo wake ulikuwa ni wewe, oooh mke wangu alikuwa ni Erica, sijui Erica ndio aliumbwa kwaajili yangu, jamani mwanaume ana wazimu yule sijapata kuona”
“Mmmh makubwa”
Muda huo huo baba Angel alitoka maliwatoni na kwenda pale kwenye meza ambapo alimtaka mkewe waondoke, kwahiyo mkewe na Fetty walibadilishana namba, kisha wakamuaga pale,
“Ila na mimi ndio narudi kwangu”
Basi wakaagana nae na kuondoka eneo lile.