Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

SEHEMU YA 24

Hilo likawarahisishia mawasiliano, wakaanza kuwasiliana kwa karibu, kutumiana picha na mambo mengine. Mapenzi yalikuwa na raha tele, hakukuwa na mtu ambaye aliamini kama watu hao wangeweza kuachana siku moja.

Dickson hakutaka kuvumilia, alichokifanya ni kumtambulisha Nandy kwa wazazi wake, alitaka wamfahamu kuwa huyo ndiye alikuwa msichana wa maisha yake ambaye alitegemea kutengeneza familia pamoja naye.

Hilo halikuwa tatizo, wazazi wakamkubali kwa mikono miwili na kuahidi kugharamia kila kitu katika siku ambayo wao wangeamua kufuanga ndoa.

Maisha yalikuwa ya raha na furaha, kila mmoja alikuwa akimpenda mwenzake na mbele yao waliyaona maisha ya ndoa yakiwa yamewasogelea kwa karibu.

Wanawake wengi wakamuonea wivu Nandy kwa kuwa alikuwa na mpenzi aliyekuwa na uzuri wa sura, wengi wakatamani kumpiku na kumchukua kijana huyo lakini kwa Dickson hakukuwa na nafasi tena, moyo wake haukugawa mapenzi, yote hayo yalibaki kwa msichana mmoja tu, huyo alikuwa Nandy.

Wakati hayo yote yakiendelea, nchini Uingereza bado Linda alichanganyikiwa kupita kawaida. Hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea nchini Tanzania kwani kwa jinsi Dickson alivyokuwa akimpotezea, muda mwingine alihisi kabisa kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.

Alichokifanya ni kuwasiliana na rafiki yake, Dotnata aliyekuwa Tanzania na kumwambia aende akampeleleze Dickson ili kuona kama alikuwa na mwanamke mwingine au la.

Hiyo haikuwa kazi kubwa kwa Dotnata, akaanza kazi hiyo ambapo baada ya wiki tu akampigia simu Linda na kumwambia kile alichokuwa amebaini.

“Shoga nakutumia wimbo,” alisema Dotnata, kwa kile alichokuwa amegundua, ilikuwa ni lazima kutumiwa wimbo hata kabla ya kuambiwa.

Akafungua WhatsApp na kukuta ametumiwa wimbo wa Unaibiwa ulioimbwa na Rayvanny, hilo lilimchanganya, hayo yalikuwa majibu ya kile alichokuwa amemtuma Dotnata.

“Unamaanisha kuna mtu anamega penzi langu?” aliuliza Linda huku akionekana kuvimba kwa hasira.
“Ndiyo hivyo! Ila hako kadada kazuri!” alisema Dotnata kwani hata naye alipomuona Nandy, alichanganyikiwa.
“Unanichanganya! Hivi kweli Dicky anaweza kunifanyia hivi? Sikubali,” alisema Linda.
 
SEHEMU YA 25

Moyo wake uliuma kupita kawaida, alitamani kurudi nchini Tanzania na kufanya maamuzi magumu. Kwa kipindi hiko ilishindikikana kwani ndiyo ulikuwa mwaka wa mwisho kumalizia masomo yake chuoni hapo.

Alisoma huku akiwa na maumivu makali moyoni mwake, alikumbuka maisha aliyoishi na Dickson, walipendana sasa ilikuwaje leo hii awe na mwanamke mwingine?

Baada ya mwaka kumalizika, akaamua kurudi nchini Tanzania, hakujua angefanyaje, hakujua ni kwa namna gani angeweza kumfuata na kumwambia yale yote aliyosikia na wakati mwanaume huyo hakuwa akimtaka.

Kwake, ilimuwia vigumu sana, ili kumpata Dickson basi alitakiwa kufanya kitu fulani hatari sana ambacho kingemfanya mwanaume huyo kukubaliana naye na hatimaye kuoana kanisani.

Mtu ambaye alimtegemea alikuwa msichana mwingine aliyekuwa akiishi Manzese, msichana huyu aliitwa Amina. Alikuwa binti wa uswahilini, mwenye makalio makubwa, kila wakati alipokuwa akitembea uswahili, makalio yake yalikuwa yakicheza kwenda huku na kule.

Alijua kuwatega wanaume, mtaani alikuwa mtu hatari, wanawake wenye ndoa zao hawakumpenda kwa kuwa alikuwa mwiba mkali kwenye maisha yao kiasi cha kuzitetemesha ndoa hizo.

Aliyatumia makalio hayohayo kuwachukulia waume zao kitu ambacho kiliwafanya wanawake wengi kumchukia na kumuona kuwa ni adui namba moja.
 
SEHEMU YA 26

Kumpata Amina wala halikuwa tatizo, alimfuata mpaka kwao Manzese na kuanza kuongea naye. Alimpa kazi hiyo, kwa Amina, hilo wala halikuwa tatizo, kwanza akainuka na kuanza kumuonyeshea Linda jinsi alivyokuwa amejaaliwa.

Akayatingisha makalio yake, yalikuwa laini sana na mbaya zaidi kwa ndani hakuwa amevaa nguo yoyote ile hivyo kuifanya dela kuingia kwa ndani. Alitamanisha kiasi kwamba hata Linda mwenyewe alitamani kuwa mwanaume ili amfaidi mtoto mzuri kama Amina.

“Kwa hiyo kazi yenyewe ni ipi?’ aliuliza Amina huku akimwangalia Linda.
“Nataka umtege, yaani umtege mpaka ategeke. Naujua udhaifu wake, anapenda sana wanawake,” alisema Linda.
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Na makalio anayapenda?”

“Sidhani lakini hakuna mwanaume anayechukia makalio. Hata kule Uingereza tu ukiwa na makalio makubwa, wewe utavuma mji mzima,” alisema Linda.
“Sawa. Kwa hiyo inakuwaje sasa kwenye kufanya hiyo kazi?” aliuliza Amina.

Akaanza kumwambia namna ambavyo kazi hiyo ilitakiwa kufanyika. Kwa Amina, ilikuwa nyepesi sana, ni kama kumsukuma mlevi kwenye mteremko wa mlima.
Akamwambia Linda kwamba alikuwa tayari, alimhakikishia kwamba kwa kutumia makalio yake basi kazi ile ingefanikiwa kwa urahisi sana, hivyo alichokifanya ni kumpa namba ya Dickson kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.

“Ukifanikiwa nakupa shilingi milioni tatu,” aliahidi Linda.
“Basi ziandae kabisa manake kwenye kazi hii hakuna kushindwa,” alisema msichana huyo aliyekuwa akiyaamini makalio yake kumpata mwanaume zaidi ya kumwamini Mungu wake aliyemuumba.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 27

Dickson alikuwa amekaa ndani ya chumba chake, hosteli katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kichwa chake kilikuwa na mawazo tele juu ya mpenzi wake aliyekuwa akimpenda kwa moyo wote.

Kwa kipindi hicho, hakukuwa na kitu chochote alichokuwa na hamu nacho kama kuona akimuoa Nandy ambaye kwake alikuwa amekufa na kuoza.

Aliwaambia wazazi wake kuhusu msichana huyo, walimzoea na kumpenda na hata wakati mwingine kumpigia simu na kumsalimia. Walikuwa karibu kitu ambacho kwa Dickson kilimfurahisha kwani kuungwa mkono na wazazi katika jambo kama hilo halikuwa la kupuuzia.

Wakati kichwa chake kikiwa na mawazo tele, mara simu yake ikaanza kuita, akaichukua na kuangalia kioo cha simu ile, mtu aliyekuwa akipiga hakuwa akimfahamu kwani namba ilikuwa ngeni kabisa kwenye simu yake.

Akaanza kujiuliza kama ilikuwa sahihi kuipokea au la, akaamua kuipokea.
“Halo,” ilisikika sauti nyororo ya msichana kutoka upande wa pili.

Kwa jinsi sauti ile ilivyosikika, moyo wake ukapiga paaa. Ilikuwa sauti nyororo kupita kawaida, ilipita sikioni mwake, ikatetemesha misuli yote na kwenda kuuchanganya moyo wake vilivyo. Pale kitandani, akajiweka vizuri.

Hakukuwa na kujiuliza zaidi, alijua kwamba kwa jinsi sauti ile ilivyokuwa nzuri ilikuwa ni lazima msichana huyo naye awe mzuri kama sauti ile ilivyokuwa.
Akaanza kumuumba msichana wake kichwani kutokana na ile sauti aliyokuwa akiisikia kwenye simu yake, msichana aliyemuumba muda huo alikuwa bonge moja la msichana ambaye hata ukizunguka Tanzania nzima, hutoweza kumpata.

“Halooo!” naye aliita.
Msichana huyo hakuwa mwingine, alikuwa Amina. Akaanza kuongea naye, alimwambia kwamba alikuwa akimtafuta rafiki yake aliyeitwa Ashura. Kwa jinsi alivyokuwa akiongea, alivyoiremba sauti yake bado iliendelea kumvuruga Dickson na kumchanganya zaidi.

“Utakuwa umekosea namba dada.”
“Jomoniiiii! Kweli nimekosea namba kaka’ngu?” aliuliza Amina, hako kasuati kake bado kalikuwa na msisimko moyoni mwa Dickson.

“Yeah! Umekosea!”
“Sawa. Basi nashukuru baby boy!” alisema Amina, alivyosema Baby Boy, mapigo ya moyo wa Dickson yakaongeza kasi.
 
SEHEMU YA 28

Huo ndiyo ulikuwa udhaifu wake mkubwa, alipenda sana wanawake japokuwa moyo wake ulikuwa umezama na kuoza kwa Nandy. Kila alipokuwa akiongea na msichana huyo ndivyo alivyozidi kuchanganyikiwa naye.

Mwisho wa siku wakaanza kupiga stori za kawaida na kuzoeana huku Amina akimwambia Dickson kwamba katika maisha yake alikuwa amekutana na mwanaume kimwili mara moja tu, tena maumivu aliyoyasikia siku hiyo, hakutaka kurudia tena.

“Huwa inauma kwa siku moja tu, baada ya pale, mambo yanakuwa mukide,” alisema Dickson kwani alijua kuwa aliyekuwa akiongea naye alikuwa msichana wa uswahilini hivyo naye akaanza kuingiza mikato ya kiswahili.
“Basi sawa.”

“Nimefurahi sana. Hebu nitumie picha zako!”
“Upo WhatsApp bebi?”
“Nipo!”
“Sawa nakutumia!”
Kwa kipindi cha dakika chache tu tayari alikuwa amemsahau Nandy, msichana mpya akamuingia moyoni mwake na hakutaka kusikia la mtu yeyote yule.
Akaingia WhatsApp huku tayari akiwa amesave namba ile kama Cute Ammy.

Baada ya dakika chache, picha zaidi ya kumi na tano zikaingia kwenye simu yake, alipozipakua na kuziangalia, Dickson bado nusu azimie kwa mshtuko.
Hakuamini kama angekutana na mwanamke aliyekuwa na kalio kama lile alilokuwa akiliona, alichanganyikiwa, aliliangalia mara mbilimbili, lilikuwa kama pembe la ng’ombe, hata lilipokuwa likifunikwa khanga bado lilionekana tu.

Macho yakamtoka, ashki ya kufanya mapenzi na Amina ikamkamata kwa kiwango cha juu kabisa. Wakati akiwa amepigwa butwaa, akatumiwa video ilioyomuonyesha msichana huyo akikatika kitandani huku akiwa amevaa taiti na cheni kiunoni.

“Mamaaaaaaaaa..” alijikuta akisema kwa sauti, akainuka kabisa kitandani ili aone vizuri kwani alihisi kama anapitwa.
Udenda ukamtoka, alikuwa kama fisi aliyeona mzoga. Hakutaka kuchelewa, hapohapo akampigia simu.

“Amina. Naomba nikuone!” alisema Dickson huku akionekana kuchachawa.
“Jomoniiiiiii!”
“Please naomba nikuone! Siwezi kuvumilia, nitakulaje kwa macho na wakati nina mikono!”

“Utaweza?”
“Nijaribu!”
“Basi sawa. Kwa sasa nipo Dodoma, nitakuja kesho, nitapanda basi la asubuhi, nahisi saa kumi nitakuwa huko,” alisema msichana huyo, hakuwa Dodoma, alikuwa chumbani kwake huko Manzese.
 
SEHEMU YA 29

“Hapana! Nakutumia nauli ya ndege uwahi. Ngoja nikutumie,” alisema Dickson.
Hakutaka kuchelewa, haraka sana akaingia kwenye huduma za kibenki kwenye simu yake na kumtumia msichana huyo kiasi cha shilingi laki tano. Hakutaka kuona akichelewa kufika Dar, alitaka kumuona haraka sana.

Amina alipoipokea pesa hiyo, akasimama, akanyoosha mikono yake kama ishara ya kumshukuru Mungu kwa makalio makubwa aliyompa kwani ndiyo yalikuwa yakimfanya kuwachuna wanaume vilivyo.

“Mungu ahsante kwa haya makalio, hakika ulijua kuyaumba,” alisema Amina.
Upande wa pili Dickson alikuwa amechanganyikiwa, akili yake iliruka, muda wote alikuwa akiziangalia picha za msichana huyo, zilimchanganya kupita kawaida.

Hakuacha kuchati naye, muda mwingi alikuwa akichati naye na kumwambia jinsi alivyokuwa na hamu ya kukutana naye. Siku hiyo hakutaka hata kuwasiliana na Nandy, mtu wa kwanza aliyekuwa kichwani mwake alikuwa huyo Amina.

Usiku, mawazo yote yalikuwa kwa msichana huyo, hakuacha kuwasiliana naye na kurudia kuziangalia picha zile mara kwa mara.
“Ila naomba nikuulize kitu bebi!” alisema Amina.
“Uliza tu!”
“Una mpenzi?”
“Hapana! Sina! Nimekuwa peke yangu kwa kipindi kirefu sana mpenzi,” alijibu Dickson.

“Kweli?”
“Haki ya Mungu tena.”
“Basi kwanza nitumie picha zako na wewe.”
“Haina shida.”
Dickson hakutaka kuchelewa, muda huo alikuwa radhi kufanya kitu chochote kile lakini si kumkosa Amina aliyekuwa na makalio makubwa. Akamtumia picha zaidi ya tano hukohuko WhatsApp.

Amina alipozipata picha za kijana huyo na kuziangalia, hakuamini kama mtu huyo ndiye aliyekuwa akichati naye. Dickson alionekana kuwa kijana mwenye sura nzuri kupita kawaida.

Tabasamu lake lilimpagawisha Amina, alichanganyikiwa, katika maisha yake japokuwa alitembea na wanaume wengi lakini hakuwahi kutembea na mwanaume aliyekuwa na sura nzuri kama alivyokuwa Dickson.

Aliambiwa kuucheza mchezo mbaya sana na Linda lakini kwa jinsi Dickson alivyokuwa na sura nzuri, akajiuliza kwa nini asitulie naye na kufikiria kujenga maisha?
 
SEHEMU YA 30

“Hivi kweli niucheze mchezo ule jamani kwa mwanaume mwenye sura nzuri kama huyu? Mh! Mbona Linda ananipa wakati mgumu!” alijisemea.
Baada ya kumaliza kuwasiliana na Dickson, akaamua kuwasiliana na Linda na kumwambia kila kitu kilichokuwa kikiendelea kwamba alifanikiwa kwa kiasi kikubwa kazi ile aliyokuwa amempa.

Kwa msichana huyo ilikuwa ni furaha tele kwani miongoni mwa vitu ambavyo hakuwa akitamani kuviona ni Dickson akimuoa Nandy ambaye kwake alionekana kama adui mpya katika maisha yake.

“Sasa onana naye kwa siku ya kwanza, muonyeshee mambo mazito, kitandani tawala sana mchezo mpaka achanganyikiwe,” alisema Linda kwenye simu.
“Haina shida, nitafanya kama nacheza baikoko au segele,” alisema Amina huku akiwa na uhakika wa kufanikiwa kwa kie ambacho angekwenda kukicheza kwa mwanaume huyo.

Siku iliyofuata akawasiliana na Dickson na kumwambia apange sehemu ambayo walitakiwa kuonana. Hilo halikuwa tatizo, Dickson akamwambia sehemu ambayo walitakiwa kukaa na kuzungumza.

Ilikuwa ni kwenye hoteli ya Mmarekani Royal iliyokuwa Sinza jijini Dar es Salaam. Wakati Dickson akiingia mahali hapo, kila mtu alibaki akiliangalia gari alilokuja nalo, lilikuwa la kifahari mno, kila mtu aliliangalia huku wakiwashtua wenzao ambao hawakuwa wameliona.

Baada ya sekunde chache, Dickson akateremka, kila mtu alibaki akimshangaa, wasichana waliokuwa mahali hapo wakabaki wakimwangalia.

Dickson alikuwa na sura ya ajabu, alikuwa mwanaume ambaye alibarikiwa sura, iliwezekana kuwa zaidi ya wanaume wote nchini Tanzania kipindi hicho.
Hotelini hapo,wakaonana, uzuri wa Dickson ulikuwa umeongezeka machoni mwa Amina, alibaki akimwangalia mwanaume huyo, hakuamini kama mtoto wa Manzese kama yeye ambaye alizoea kupata wanaume wababaishaji sasa alikuwa njiani kulala na mwanaume aliyekuwa na sura nzuri kama Dickson.

Wakabaki wakiongea tu kwenye mgahawa wa hotelini hapo. Amina alijua kuongea na mwanaume alijua jinsi ya kumfanya mwanaume kumdatisha. Wakiwa hapohapo kwenye viti, akaupeleka mkono wake katika miguu ya Dickson na kuanza kumminyaminya kwa kutumia kucha zake ndefu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom