Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,081
- 464,047
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 08
Hilo halikuwa tatizo, baada ya siku mbili wakarudi nchini Tanzania na hivyo kushiriki katika mkutano huo. Hakuwa na maisha ya wokovu lakini alipenda sana kusikiliza mahubiri. Kila alipokuwa akipata nafasi ilikuwa ni lazima kusikiliza mahubiri mbalimbali huku naye akimuomba Mungu kwamba siku moja baadaye aje kuwa mhubiri mkubwa kama alivyokuwa Benny Hinn.
Japokuwa alipenda sana dini na mahubiri lakini pia Dickson alipenda sana wanawake. Kwake, wanawake walikuwa kila kitu, aliwapenda, alipokuwa akiwaona moyo wake ulifarijika mno.
Mpaka kumaliza kidato cha sita, alikuwa amekwishatembea na wanawake wengi. Alipendwa kwa kuwa alitoka katika familia ya kitajiri lakini mbali na utajiri huo, Dickson alikuwa na sura nzuri mno.
Wanawake walimbabaikia na wengi kumuita Trey Songz kwa kuwa tu alifanana na mwanamuziki huyo kutoka nchini Marekani. Kila msichana aliyekuwa akimuona, hakutaka kumpita Dickson pasipo kumsalimia, kwao, kijana huyo aliitetemesha mioyo yao na hivyo kujikuta akilala na wanawake wengi hata wale ambao hakuwa akiwafikiria kabisa.
Siku ya kwanza ya mkutano huo mkubwa wa injili alikwenda katika Viwanja vya Jangwani huku akiendesha gari la thamani aina ya BMW X6 ya bluu. Alipofika sehemu ya kuegesha magari, akalisimamisha na kuteremka.
Watu waliokuwa pembeni wakabaki wakiliangalia gari hilo. Lilikuwa zuri mno, wengi wakatamani kumuona mtu ambaye angeteremka humo kwani wengi walihisi kwamba angeteremka mtu mzima, mwenye kitambi huku mkononi akiwa na saa ya thamani ya Rolex.
Mlango ukafunguliwa na Dickson kuteremka. Alivalia suruali nyeusi, tai nyeusi na shati jeupe huku akiwa na miwani ya macho. Kila mtu aliyemwangalia kijana huyo, alichanganyikiwa, hawakuamini kumuona kijana aliyekuwa na sura nzuri kama alivyokuwa Dickson.
Hilo halikuwa tatizo, baada ya siku mbili wakarudi nchini Tanzania na hivyo kushiriki katika mkutano huo. Hakuwa na maisha ya wokovu lakini alipenda sana kusikiliza mahubiri. Kila alipokuwa akipata nafasi ilikuwa ni lazima kusikiliza mahubiri mbalimbali huku naye akimuomba Mungu kwamba siku moja baadaye aje kuwa mhubiri mkubwa kama alivyokuwa Benny Hinn.
Japokuwa alipenda sana dini na mahubiri lakini pia Dickson alipenda sana wanawake. Kwake, wanawake walikuwa kila kitu, aliwapenda, alipokuwa akiwaona moyo wake ulifarijika mno.
Mpaka kumaliza kidato cha sita, alikuwa amekwishatembea na wanawake wengi. Alipendwa kwa kuwa alitoka katika familia ya kitajiri lakini mbali na utajiri huo, Dickson alikuwa na sura nzuri mno.
Wanawake walimbabaikia na wengi kumuita Trey Songz kwa kuwa tu alifanana na mwanamuziki huyo kutoka nchini Marekani. Kila msichana aliyekuwa akimuona, hakutaka kumpita Dickson pasipo kumsalimia, kwao, kijana huyo aliitetemesha mioyo yao na hivyo kujikuta akilala na wanawake wengi hata wale ambao hakuwa akiwafikiria kabisa.
Siku ya kwanza ya mkutano huo mkubwa wa injili alikwenda katika Viwanja vya Jangwani huku akiendesha gari la thamani aina ya BMW X6 ya bluu. Alipofika sehemu ya kuegesha magari, akalisimamisha na kuteremka.
Watu waliokuwa pembeni wakabaki wakiliangalia gari hilo. Lilikuwa zuri mno, wengi wakatamani kumuona mtu ambaye angeteremka humo kwani wengi walihisi kwamba angeteremka mtu mzima, mwenye kitambi huku mkononi akiwa na saa ya thamani ya Rolex.
Mlango ukafunguliwa na Dickson kuteremka. Alivalia suruali nyeusi, tai nyeusi na shati jeupe huku akiwa na miwani ya macho. Kila mtu aliyemwangalia kijana huyo, alichanganyikiwa, hawakuamini kumuona kijana aliyekuwa na sura nzuri kama alivyokuwa Dickson.