Simulizi: Mwanafunzi Mchawi (A Wizard Student)

Simulizi: Mwanafunzi Mchawi (A Wizard Student)

SEHEMU YA NANE

Ilipoishia sehemu ya Saba ( kama hukuisoma bofya hapa)..

....Mwalimu John alidhaniwa kufariki, hivyo harakati za mazishi ziliandaliwa.. Je John alikufa kweli?

Dorice alikuwa kwenye harakati za kutoroka, lakini kuna kitu kilimshtua..

Eddy alipewa sharti la kutofanya mapenzi na Doreen lakini tayari hamu ya mapenzi ilimvaa kwa kasi ya ajabu. Je atafanya mapenzi na Doreen?..

ENDELEA...

... MIPANGO YA MAZISHI kumzika mwalimu John ilikuwa tayari imekamilika, ndugu walikuwa tayari wamewasili kwa majonzi. Huzuni iliwatawala sana kwani mwalimu John alikuwa ndiye tegemezi la familia yote kwa ujumla. Kelele za vilio zilitawala mtaa mzima aliokuwa akiishi mwalimu John, kila MTU alisema lake juu ya msiba ule lakini ukweli haukujulikana.

Make wa mwalimu John alipoteza fahamu kila Mara huku akijutia tendon alilomfanyia mumewe kwa kumpiga na upawa kichwani .Lakini alijiahidi kutomwambia mtu yoyote akihofia kukamatwa kwa kosa la mauaji. Nyuso za watu wote zilitia huruma sana kwa kuondokewa na mwalimu John kipenzi cha watu wengi.

Walimu kutoka shule ya sekondari Mabango walikuwepo pale msibani wakimuaga mwalimu mwenzao.

Jeneza la gharama lilitengenezwa, mwili wa mwalimu John ukawekwa ndani ya jeneza. Make wa mwalimu John alikuwa haamini kama mume wake ndo anapelekwa kuzikwa.. Aliachia yowe Kali lililowashtua wote pale msibani "Rudi mume wangu.. Rudi mpenzi wangu usife..." Alilia mke wa John.

Wazazi wake walikuwa wakigalagala chini kama wehu,hawakujali vumbi lililokuwa limetapakaa ardhini kutokana jua Kali la kiangazi.

Hatimaye Jeneza lililokuwa limebeba mwili wa marehemu John likaingizwa kwenye gari kwaajili ya kupelekwa makaburini huku likisindikizwa na nyimbo za huzuni zinazopigwa misibani. Watu wote wakaelekea makaburini kwani magari ya kutosha yalikuwa yamekodiwa.

Mwalimu John alikuwa ndani ya Jeneza akilia kwa sauti ili Atolewe kwani alikuwa hajafa. Lakini hakuna MTU yeyote aliyesikia kilio cha Mwalimu John wala kuhisi, " Inamaana wananizika mzimamzima?" Alijiuliza mwalimu John huku moyo wake ukiwa umezimia kwa mile akionacho.

"Haiwezekani nizikwe mzima mzima! Hapana" alisema Mwalimu John huku akijaribu kujiinua lakini mwili wake ulikuwa bado mzito kama vile umegandishwa na barafu. Akiwa ndani ya jeneza hilo akasikia kicheko kikali sana kutoka kwa Doreen.

"Doreen nisamehe tafadhali" alijitetea Mwalimu John.
Machozi yalizidi kumtoka kwa kasi sana , ndipo alipokumbuka kosa lake kwa Doreen.

Zilikuwa ni wiki mbili tangu Doreen ahamie shule ya Mabango, kutokana na uzuri na utanashati wa mwalimu John. doreen alivutiwa nae sana hivyo akaamua kumwambia ukweli mwalimu wake kuwa anampenda na anahitaji kuwa naye kimapenzi. Mwalimu John alimtazama binti yule kwa jeuri na dharau kisha akamjibu " We mtoto ni mpumbavu sana! Umezunguka kote huko ukaona uniletee umalaya wako hapa? Mbwa koko wewe hebu niondokee hapa!"
"Mwalimu John hunitaki? Unanitusi? Sasa nitakuonyesha kazi!" Alisema Doreen kwa kujiamini sana kisha akaondoka zake
.
Wakati Mwalimu John akiendelea na kumbukumbu hizo ghafla akahisi jeneza lake linanyanyuliwa Tayari kwa kumuweka kaburini...

*********
Dorice alipokuwa akitembea ghafla akazungukwa na chatu mkubwa sana kila upande. Dorice alishtuka sana, mapigo yake ya moyo yakamwenda kasi sana akiwa haelewi la kufanya.

Kutokana na woga Dorice aliangusha chini mkoba aliokuwa ameubeba lakini ghafla akakumbuka kitu. Akaokota mkoba wake kwa ujasiri sana kama vile hakumjali chatu yule kisha akatamka maneno ambayo aliyaelewa mwenyewe. Ghafla bin vuu chatu yule akatoweka kimuujiza, Dorice akaendelea na safari yake.

Alitembea mwendo wa kama dakika tano hatimaye akafanikiwa kuiacha mipaka ya shule, akaingia barabara kuu ya kokoto ambayo ilizingirwa na miti kila upande. Akaendelea kupiga hatua moja baada ya nyingine kuelekea alikokusudia.

Safari ilikuwa ndefu sana na Giza likazidi kuiteka dunia ingawa mbalamwezi ikawa taa kwa msichana yule mwenye kujiamini.

Dorice alitembea taratibu baada ya kuchoka kutokana na mwendo mrefu hatimaye akafika kwenye kijito kidogo kilichotawaliwa na ukimya wa ajabu. Hakukiwa na sauti ya vyura wala wadudu palikuwa kimya mno. Dorice akavuta pumzi ndefu na kuishusha taratibu sana kisha akaketi pembeni ya kijito kile kimya.

Alikaa karibia robo SAA nzima akiwa ameinamisha kichwa chake ghafla akasikia kishindo kizito ambacho kilimshtua mawazoni.
*********
Eddy aliendelea kumng'ang'aniza Doreen wafanye mapenzi lakini Doreen aliendelea na msimamo wake ule ule kuwa hawezi kufanya mapenzi.
"Doreen tafadhali mpenzi...!"
"Siwezi Eddy!"
"Hapana Doreen, kama ni hivyo niruhusu niwe na msichana mwingine!"
"Kwa hilo usije kuthubutu maana utahatarisha uhai wako?"
" kivipi?"
"Elewa hivo"
Eddy alishtuka kidogo lakini akaachana na mawazo hayo akaendelea kumbembeleza Doreen. Doreen aliendelea kukataa Katakata ingawa nayeye pia alitamani kufanya mapenzi na Eddy ila kuna kitu alikumbuka kikamtia hofu, akazidi kumkatalia.
Uvumilivu ulimshinda kabisa Eddy akajikuta anamtoa Sketi Doreen huku nae akishusha suruali yake. Akambwaga chini Doreen na kutaka kufanya nae mapenzi, kabla hajafanya chochote Eddy aliachia yowe Kali sana....

ITAENDELEA..
 
SEHEMU YA TISA

Ilipoishia Sehemu ya 8 ( Bofya hapa Kama Hukuisoma )

..Mwalimu John alipelekwa makuburini kwaajili ya mazishi ingawa yeye alijiona yuko hai. Dorice alikuwa njiani baada ya kutoroka shulen, na alipofika kwenye kijito kidogo alishtushwa na kishindo kikali.

Eddy alifikia hatua ya Mwisho kutaka kufanya mapenzi na Doreen lakini kabla ya kufanya hivyo aliachia yowe Kali.

SONGA NAYO UJUE KILICHOJIRI....
....VIJANA wanne wenye nguvu walinyanyua jeneza alililokuwamo Mwalimu John kisha taratibu walipiga hatua kuelekea kwenye nyumba yenye pembe NNE na kina kirefu kiasi aliyotengenezewa mwalimu John.

Sauti za vilio zilizidi kutia simanzi katika eneo lile LA makaburini. Nyimbo za huzuni zilitawala eneo hill huku kila mmoja akisikitika moyoni mwake.

Ndani ya jeneza hilo mwalimu John alikuwa akihangaika sana kuwaita vijana wale ili wasimzike lakini katu hakusikika. Alizidi kupiga kelele za kuomba msaada lakini ikabaki kuwa kazi bure. Sauti iliyojaa huzuni kuu ya mkewe Monalisa ilizidi kupenya vyema masikioni mwake, hali hii ilzidi kumtia simanzi mwalimu huyo ambaye sasa alikuwa amekata tamaa ya kuishi tena.

"Daah Doreen hafai" alijisemea mwalimu John huku machozi yakimtiririka kwa kasi kwani bado alikuwa haamini kama kweli anazikwa akiwa mzima.Vijana wale walilishusha jeneza like lenye mapambo ya kupendeza ndani ya kaburi kisha wakatulia kidogo ili mchungaji atupie neno LA mwisho.

Mchungaji alichukua udongo kidogo na kusogelea vyema kwenye shimo alilowekwa mwalimu John."Uliumbwa kwa mavumbi hakika utarudi mavumbini, Bwana alitoa Bwana ametwaa jina LA Bwana lihimidiwe... " Mchungaji aliyasema maneno hayo kwa huzuni kisha akaumwaga kaburini udongo ule aliokuwa ameushika mkononi.

Mwalimu John aliyasikia vyema maneno hayo yaliyouchoma moyo wake kama mkuki wenye sumu. Hakika mwalimu John alikiri kuwa kweli duniani kuna watu na viatu, Doreen alikuwa kiatu chakavu kisichofaa kuvaliwa hata na kichaa.

Vijana walishika vyema sepetu zao ili waanze kutupa udongo kaburini na kumzika mwalimu John lakini kabla hawajaanza kutupa udongo, kilizuka kimbunga kikali cha ghafla kilichofanya watu wapoteane. Jeneza likafunuka ghafla mwalimu John akainuka kutoka kwenye jeneza.

********
Eddy aliachia yowe Kali sana ambalo lilijirudia Mara kadhaa. Yowe hill lilitokana na maumivu makali sana aliyoyapata kwenye sehemu zake za siri. Maumivu yalikuwa makali sana hivyo alianguka chini na kupoteza fahamu.
Wakati wote huo Doreen alikuwa amebadilika sura na kuwa sura kama sura ya paka. Kucha zilimtoka kama za chui anayekabiliana na hatari. Kichwa chake kilikuwa na mapembe marefu. Hivyo akawa na umbile la kutisha sana ambalo hakuna kiumbe wa kawaida angeweza kustahimili kumtazama hata kwa nusu sekunde.

Licha ya kwamba Doreen alikuwa kwenye umbile lile la kutisha lakini alionekana mnyonge sana. Machozi ya damu yalikuwa yakimshuka taratibu kwenye macho yake. Alimsogelea Eddy na kukaa karibu yake huku akimgusa taratibu mwilini mwake.

"Eddy mpenzi wangu nakupenda sana.. Nisamehe kwa kilichotokea.. Halikuwa kusudio langu hata kidogo, ila umelazimisha... Nakupenda sana na ninakuahidi kukupenda maisha yangu yote...!" Alisikika Doreen akiongea kwa huzuni ila sauti yake ilikuwa ilikuwa nzito ya kutisha iliyoambatana na mwangwi mkali. Doreen alizidi kulia kwa huzuni sana na taratibu sura yake ilianza kujirudi. Akawa Doreen yule aliyezoeleka.

Machozi yakawa hayamkauki kwa kitendo alichomfanyia Eddy mwanaume ampendaye sana.Doreen akampandisha Eddy suruali kisha akatulia kimya akimsubiri azinduke.

Lilipita SAA zima ndipo Eddy akapiga chafya ya kwanza.. Doreen alimtazama Eddy kwa huzuni na huruma nyingi lakini Eddy hakufumbua macho. Baada ya robo SAA Eddy akapiga chafya mbili mfululizo kisha akayafumbua macho taratibu lakini hakuweza kuona chochote kutokana na Giza Nene lililozingira kila upande, Eddy akaogopa akataka kukimbia lakini mwili wake ulikuwa mchovu sana kama MTU aliyefanya kazi ngumu kupita kiasi. Akajishangaa sana .

"Eddy mpenzi. ." sauti ya Doreen ilimshtua Eddy na kumfanya ajue kuwa hayupo peke yake. Eddy akageuka na kumwona Doreen kwa mbali kwani Giza lilimzuia asionekane sana .Kumbukumbu zikamrudia Eddy kichwani akaikumbuka ile sura ya kutisha ya Doreen aliyomwona nayo kabla ya kupoteza fahamu.

"Toka! Usiniguse! Ushindweee.. !" Aliropoka Eddy huku akikikimbia bila kuelewa nguvu zimetoka wapi .
"Eddy!" Aliita Doreen lakini Eddy alikuwa tayari amekimbia.
"Oh! Shiit!" Alisema Doreen bila kuelewa la kufanya.Akasimama kwa muda kisha akaamua kuondoka zake eneo lile.

Eddy alifika bwenini kwao akakuta mlango umefungwa kwani wenzake walikuwa darasani kwa vipindi vya usiku(prep. Time). Eddy alisonya kwa hasira akiwa ameuegamia mlango huku kashika kufuli.

Ghafla wazo likamjia aliamua kwenda mlango wa dharula na kuingia bwenini. Woga ulimjaa ila hakuweza kwenda darasani aliamua kulala na kujifunika blanketi gubigubi.Usingizi ukampitia mpaka asubuhi.
"Eddy vipi mbona umelala sana, Jana ulikula mzigo kwa kasi nini?"
Alitania Jackson rafiki kipenzi wa Eddy baada ya kumwamsha.
"Vipi kumekucha" alisema Eddy kwa sauti ya nyono.
" hahah Eddy Yale mambo hayataki papara, hebu amka bhana! "

Jackson alicheka kisha akamfunua blanket Eddy.Eddy alijivutavuta kisha akaamka na kwenda bafuni kuoga .Alipofika bafuni aliwakuta wanafunzi wenzake wengi wakioga. Bila wasiwasi wowote Eddy alivua nguo zake na kuanza kuoga. Ghafla wanafunzi wenzake wakabaki kumshangaa Eddy, wakaanza kukonyezana kisha wote wakaanza kumtazama Eddy kwa wizi.
Eddy hakujua lolote akaendelea kuoga kwa kujiachia sana.
Wanafunzi hao wambeya hawakukomea hapo Bali walitoka nje na kuwaita wenzao ambao pia wakaingia bafuni mle wakijifanya kunawa nyuso zao kumbe walizuga tu, lengo kuu ilikuwa kumtazama Eddy.

*********

Dorice alishtushwa na kishindo kile pale mtoni. Akageuka kutazama nyuma , hakuamini macho yake kwani alimwona MTU mrefu sana akiwa amesimama nyuma yake. Dorice aliogopa sana akatetemeka.

"Unafanya mini hapa?" Like jitu refu lilimuuliza Dorice kwa ukali.
"Napumzika.. Nim..nimechoka" Dorice alijibu kwa kutetemeka.
"Umetoka wapi na unaenda wapi?"
"Nimetoka Mabango.. Naenda mjini..!"
"Hahahahah kwanini ukae hapa? Hii ardhi yetu.. Na muda huu ni sherehe yetu umetusumbua... Hivyo utakuwa kitoweo chetu.." Lilisema jitu lile. Dorice alitetemeka kupita kiasi, jitu lile likamsogelea Na kumshika mkono kisha wakatoweka.....

ITAENDELEA.....
 
Duh! Kila ilapoishia utamu unaongezeka. Safi sana mkuu
 
  • Thanks
Reactions: Lee
SEHEMU YA KUMI

Ilipoishia Sehemu ya 9

......Ghafla wanafunzi wenzake wakabaki kumshangaa Eddy, wakaanza kukonyezana kisha wote wakaanza kumtazama Eddy kwa wizi.

Eddy hakujua lolote akaendelea kuoga kwa kujiachia sana.
Wanafunzi hao wambeya hawakukomea hapo Bali walitoka nje na kuwaita wenzao ambao pia wakaingia bafuni mle wakijifanya kunawa nyuso zao kumbe walizuga tu, lengo kuu ilikuwa kumtazama Eddy...

SONGA NAYO UJUE KILICHOJIRI....
. . ..EDDY aliendelea kuoga bila kujua kuna watu wanapiga chabo mle bafuni. Alijua wanafunzi wale wanamtazama kwa wema tu au labda wanautazama uzuri wake aliojaaliwa na Mwenyezi Mungu ambao daima unawachanganya mabinti na hata wanawake watu wazima ambao kuna wakati walimrubuni kwa kumpa vitu vya thamani ili awakubalie lakini bado hawakumpata kijana yule kutoka kwenye familia ya kitajiri ya Mr.Alloyce.

Eddy aliendelea kuoga kwa kujiamini mpaka alipofikisha mkono kwenye maeneo yake nyeti. Ghafla alishtuka sana kama vile amepigwa shoti ya umeme, macho yalimtoka kama MTU aliyekutana na simba USO kwa USO porini.

Eddy hakuamini alichokihisi, akaamua kuyapeleka macho yake moja kwa moja mpaka kwenye bustani yake muhimu. Akagundua kuwa sehemu zake za siri hazipo. Bado Eddy hakuamini akachukua maji kwenye kiganja chake cha mkono na kuyasafisha vizuri kwani alihisi hayaoni vizuri. Jibu likabaki moja tu Sehemu zake nyeti hazikuwepo.

"What! Mbona sielewi!" Eddy alichanganyikiwa kupita kiasi. Akachukua suruali yake na kuivaa kwa wizi ili watu wasimwone lakini alikuwa tayari amechelewa kwani alikuwa tayari ameshaonwa na watu wengi tu.

Bila hata kujiosha povu la sabuni alilokuwa amejipaka mwilini, Eddy alikimbia na kuingia bwenini. Akajibwaga kitandani kwa Jackson rafiki yake bila kujali kuwa sabuni iliyoko mwilini mwake ilichafua shuka.

"Eddy! Vipi mshkaji!" Aliuliza Jackson huku akimalizia kuvaa sare zake za shule.
" Nakufa Jack... Nakufa Mimi...."
" Unakufa? Mbona sikuelewi Eddy?" Jackson alikuwa haelewi chochote kinachoendelea kuhusu Eddy ingawa taarifa zilikuwa zimesambaa kwa wanafunzi wengi wa kiume.
" Eddy! Niambie umepatwa na nini? Unaniacha njia panda.."
" Jack... Nakufa... Siwezi kuishi... Nakufa..." Eddy alizidi kulia kama mtoto mdogo aliyenyimwa maziwa kwa muda mrefu. Akili yake haikufikiria kingine zaidi ya kujiua, asingeweza kuistahimil aibu ambayo ilimjia kwa kasi bila hata kupiga hodi.
"Jack..Dunia hadaa ulimwengu shujaa.. Jack me nakufa.. Waambie wazazi wangu..Nilipenda visivyopendeka ila sio kwa matakwa yangu naamini ni shetani tu.."
Maneno hayo yaliibua simanzi nzito kwa Jackson, machozi yalimzidi nguvu hivyo yakashuka kwa kasi machoni kwa Jackson.
"Hapana Eddy huwezi kufa, hebu niambie tatizo..!"
"Hata nikikwambia huwezi kunisaidia Jack.. Huwezi amini natamani kuwa hata nyuki wa mashineni kwa sasa!"
" una maana gani!"
"Mimi sio mwanaume tena... Unafikiri nitaificha vipi aibu hii? Bora nife.. Nikapumzike na wafu wenzangu.."
"Eddy! Sio mwanaume tena kivipi?"
"Uume wangu haupo!" Eddy aliposema hayo akashindwa kujizuia kulia kwa sauti. Hivyo akalia kwa sauti Kali iliyosikika bweni zima. Kwa bahati nzuri wanafunzi karibia wote walikuwa wameondoka ili wawahi mstarini.
Jackson alitazama SAA yake ya mkononi ilikuwa tayari SAA mbili kasoro.
" Eddy! Nitarudi sasa hivi ngoja nikakuombee ruhusa kuwa unaumwa, ila please usifanye lolote. Niahidi!"

Eddy aliitikia kwa kichwa kuwa hatofanya lolote, Jackson akatoka huku akiwa na wasiwasi sana.Eddy aliona dunia inamwelemea na ni vigumu kukabiliana nayo. Machozi hayakuacha kumtiririka kila sekunde. Akili yake ikaanza kukumbuka mambo mengi, ndipo alipoupata ukweli kuwa Doreen ndiye aliyemfanyia ukatili ule Jana usiku.

Akili ya Eddy ikawa kama imefunguliwa kutoka kwenye kifungo kikali. Akamkumbuka Dorice wake, msichana ampendaye sana kuliko mwingine yeyote ila akakumbuka kuwa alishamsaliti na kumdhalilisha mbele za watu.

"U wapi Dorice mpenzi wangu! Dorice nisamehe ! Dorice haikuwa akili yangu! Nakupenda Dorice! Ingawa nakufa ila naomba unisamehe sana.... Doreen ni shetani! Hafai hata kidogo..!" Eddy alilia mpaka kamasi zilimtoka. Kichwa kikamgonga kutokana na kulia kwa muda mrefu.

Eddy aliinuka kitandani pale na kwenda moja kwa moja kwenye begi lake. Akachukua kijidaftari kidogo, akachana karatasi ndogo. Kisha akachukua kalamu akaanza kuandika ujumbe huku machozi yakililowanisha karatasi lile .

" Dorice mpenzi, nisamehe kwa yote yaliyotokea Nakupenda sana. Halikuwa kusudio langu mpaka sasa sielewi ilitokeaje. Mpaka kaburini, kumbuka upendo wangu, ujue kwamba Nakupenda! Nakufa mpenzi ila bado nakupenda!"

Eddy alimaliza kuandika ujumbe huo wa kusikitisha kisha akalikunja karatasi lile na kuliweka kitandani.Eddy alishusha suruali na kujiangalia tens sehemu zake za siri ili ahakikishe kama ni kweli. Ndio ilikuwa kweli kabisa wala so ndoto. Kilio cha Eddy kikaongezeka alishindwa kuvumilia akaona ni heri ajiondoe duniani mapema.

Eddy alifungua begi lake na kuchukua vidonge vingi alivyokuwa akivitumia kwa maumivu ya tumbo, akatafuta vidonge aina nyingine akavichanganya kwa pamoja. Lengo lake ilikuwa avitumie kama sumu ili aondokane na adha zinazomkàbili duniani. Akachukua maji yaliyokuwa kwenye kopo akalisogeza karibu. Akasali sala ya mwisho ili apokelewe vyema na malaika wa huko aendako.

*****
Doreen alikuwa darasani asubuhi ile. Alikuwa amekaa konani akiwa ametulia tuli huku madaftari yake mawili yakiwa yamefunuliwa kana kwamba alikuwa akiyasoma. Lakini tangu alipoyafunua madaftari Yale yalibaki hivyohivyo kwani Doreen alikuwa hayasomi ila aliyafunua kwaajili ya kuzuga tu. Mawazo yake yalikuwa yalikuwa mbali sana.

"Inabidi ulete uume wa mwanaume umpendaye, akiwa taabani na hamu ya mapenzi, pale anapotaka kufanya mapenzi nawewe ndipo uchukue uume wake! Umeelewa!" Maneno hayo yalijirudia kichwani mwa Doreen na kumfanya ashtuke kidogo.

Moyo ulimuuma sana Doreen kwa kumfanyia ukatili ule Eddy, alijiona yeye sio binadamu kabisa kwani hana roho ya ubinadamu. Huruma ilimshika sana, alimhurumia Eddy.

"Ataishije.. Daah! Najichukia sana kwa nilichokifanya.. Nampenda sana Eddy!" Aliwaza Doreen mpaka machozi yalimlengalenga machoni. Hakuwahi kumhurumia MTU yeyote duniani kama alivyomhurumia Eddy. Alijiona mkosaji sana kwa MTU asiye na hatia.

Licha ya yote hayo lakini Doreen hakuwa na jinsi. Ilibidi afanye vile ili atimize lengo lake lililomleta katika shule ya Mabango. Alikuwa tayari amefikia robo tatu ya kile alichotumwa. Ilibidi amalizie robo iliyobaki ya kusudio lake ndipo aibuke kinara katika ufalme ambao hauonekani kwa macho ya kawaida. Ushindi ulikuwa wake mpaka pale alipofikia.

Doreen aliwaza mambo mengi sana lakini wazo kuu lilibakia Kwa Eddy, alitamani kujua Eddy anaendeleaje kwa wakati ule lakini hakuwa tayari kumtembelea Eddy kwani aliona kama akuwa kero kubwa kwa kijana yule na ataibua chuki.
" masikini Eddy! Ila sina jinsi..!"

****
Dorice alikuwa amepelekwa kwenye utawala wa viumbe wa ajabu ambao hakuwahi kuwaona hata Siku moja. Sura na maumbo yao yalikuwa ya kutisha sana. Alijawa na woga sana, alitetemeka kama vile ampepigwa na baridi Kali. Hakuweza kuwatoroka kwani hata njia alikuwa haijui, hakuelewa amefikafikaje eneo lile. Alizidi kumwomba Mungu amsaidie na amwepushe na mabaya.

"Salam Malkia!" Alisalimia kiumbe yule aliyeambatana na Dorice kwa heshima na adabu.
Mwanamke mrembo mwenye dhahabu mwili mzima na mavazi ya kung' aa mwlini mwake akiwa ameketi kwenye kiti kizuri cha dhahabu alimwitikia kiumbe yule.
"Salam! Naona umefanya Nazi nzuri sana Leo!"
"Ndio malkia!"
"Vizuri sana, mtumishi wangu!"
Dorice alikuwa ametulia kimya akisubiri kitakachomtokea.
"Binadamu hawa jeuri sana...!"
Alisema malkia yule huku akiinua fimbo yake ya dhahabu na kumnyooshea Dorice.
Dorice aliogopa sana alijua kifo chake sasa kimewadia.
Malkia yule aliinyoosha fimbo ile ikatua moja kwa moja kwenye kifua cha Dorice.
Malkia yule akaituliza fimbo ile kwa muda wa dakika kama tano. Kisha akaachia kicheko kikali sana cha kutisha.. Doreen alizidi kupata hofu.............

ITAENDELEA.......

DOREEN ana siri nzito sana kuhusu maisha yake na hakuna aijuaye zaidi yake na mama yake mzazi kwa hapa duniani. Inamfanya awe katili kupita maelezo kwani akiwa na huruma hatoweza kufaanikiwa!!!! UKITAKA KUJUA SIRI HIYO ENDELEA KUFUATILIA SIMULIZI HII...
 
Babu hii kitu inatia sana hamu ya kuendelea kuisoma. Leo leta ata 3 basi.
 
  • Thanks
Reactions: Lee

Similar Discussions

Back
Top Bottom