Beeb
JF-Expert Member
- Aug 18, 2018
- 29,393
- 59,137
Milima haikutani binadamu wanakutana
Sent using Jamii Forums mobile app
SEHEMU YA 72
“Wewe ndiye Deborah?” aliuliza mwanaume huyo, alikuwa meneja kwenye kampuni hiyo.
“Umenijuaje?”
“Uliomba kuja kuonana nami kutoka huko Kigoma, ama si wewe?” aliuliza.
“Ndiye mimi!”
Walizungumza, alimwambia kuhusu hali ya mume wake, alifanya kazi kwa miaka sita, alikuwa mtu mwenye sifa nzuri katika kampuni hiyo, hivyo waliongea mambo mengi na meneja huyo, Bwana Kinyora alimwambia angefanya kila juhudi mume wake aajiriwe kwenye kampuni hiyo.
“Nitajitahidi kwa hali na mali!” alisema mwanaume huyo.
Baada ya kumaliza mazungumzo hayo, akatoka na kurudi hotelini, alipofika njiani, akaamua kununua Gazeti la Nipashe ambapo kulikuwa na taarifa ya mwanaume mmoja aliyekuwa akitafuta msaada wa watoto wake walioungana kupelekwa nchini India kwa ajili ya kutenganishwa.
Aliiangalia habari hiyo, hakuona picha ya mwanaume huyo wala watoto hao walioungana lakini alipoangalia namba ile ambayo walitakiwa wasamaria wema watume pesa, aliifahamu vilivyo, ilikuwa namba ambayo haikuwahi kutoka kichwani mwake.
“John!” alijikuta akisema kwa mshtuko, akaamua kuipiga, mwanaume huyo akapokea.
“Halooo!” aliita.
“Halo John!” aliita msichana huyo.
“Deborah?”
“Ndiyo! Ni mimi hapa!” alijibu Deborah! Tayari machozi yakaanza kumtoka, kile alichokuwa amekisoma kwenye gazeti kilimuumiza kupita kawaida.
Yule John, kijana masikini alikuwa akihitaji kiasi cha shilingi milioni hamsini na tano ili watoto wake walioungana wakatenganishwe nchini India.
|
|
Je, nini kitaendelea?
Sent using Jamii Forums mobile app