Simulizi: Mke Wangu Juliana

Simulizi: Mke Wangu Juliana

SEHEMU YA 62

Deborah alilia sana, alihuzunika, maisha yake yalikuwa ya majonzi kupita kawaida, alikonda mno, aliteseka lakini wazazi wake hawakutaka kujali kabisa.

Alitia huruma, kila mtu aliyekuwa akimwangalia alimsikitikia kwani hakuonekana kuwa kama yule Deborah wa kipindi cha nyuma, huyu alikuwa mwingine kabisa.

Mawazo yakawa makubwa, akaanza kupata vidonda vya tumbo vilivyoanza kumtesa na kumpa maumivu makali, akaanza kuchagua aina ya vyakula ambavyo alitakiwa kula, vingine aliambiwa asile, hasa vile vilivyokuwa na asidi.

Wazazi wake walimuonea huruma lakini kamwe hawakutaka kujutia kile walichokifanya, waliamini kilikuwa kitu kizuri kwa sababu walifanya kila lililokuwa bora, hawakutaka binti yao aangukie kwenye mikono ya mwanaume ambaye angeshindwa kumfanyia kitu chochote hasa kumpa maisha ambayo aliyahitaji.

Walizungumza naye kila siku, kila walipoongea naye, alionekana kuwa na majonzi mazito, hasira kali dhidi ya wazazi wake.
Alitamani kuufumbua mdomo wake na kuwaambia ni kwa namna gani alikuwa akiwachukia lakini alishindwa kufanya hivyo kwa kuwa tu aliwaheshimu, ila moyoni mwake aliwachukia kupita kawaida.

Hakuonana na John, mwanaume huyo alifukuzwa kazi, hakupata hata muda wa kwenda nyumbani kwake, kila alipokuwa, mama yake alikuwepo, alikuwa kama mlinzi kwake, alitakiwa kurudi nyumbani mara tu anapomaliza kazi.

Kwa kuwa waliamini kitendo cha kumuona John kingemfanya kurudi tena nyuma, wakaamua kuhama kanisa, yote hayo ni kwa sababu hawakutaka kuona binti yao akiungana na mwanaume huyo tena.

Maisha yalikuwa ni ya mateso mno, hakuyapenda lakini alitakiwa kuyaishi kila siku katika maisha yake. Siku ziliendelea kukatika na baada ya miezi saba ya kuwa na maisha yenye maumivu makali ndipo akapata mwanaume aliyemwambia alikuwa akimpenda mno.

Mwanaume huyo aliitwa Jericho Michael, mmoja wa kijana aliyetoka kwenye familia iliyokuwa na uwezo mkubwa kama wao.
Jericho hakumpata hivihivi, aliwatumia wazazi wake ambao walikwenda kuzungumza na wazazi wa Deborah na wao wakazungumza na binti yao na hatimae wawili hao kuwa wapenzi.
 
SEHEMU YA 63

Maisha hayakuwa kama yalivyokuwa kwa John. Japokuwa John hakuwa na kitu lakini alimfanya kuwa mwanamke spesho maishani mwake.

Alimpa furaha, alipenda sana kumchekesha, kumtania na mambo mengine tofauti na alivyokuwa akifanya Jericho, muda mwingi mwanaume huyo alikuwa siriazi sana, yaani ni kama mtu ambaye hakupenda utani.

Hilo Deborah alilizoea, hata wanaume aliowahi kuwa nao kabla ya John walikuwa hivyohivyo, wakali, siriazi sana, hawakuwa na matani kwa kuwa tu walijua walikuwa na pesa hivyo ni vigumu kukimbiwa na wanawake.

Maisha hayakusubiri, waliendelea kuwa pamoja mpaka pale ambapo sasa waliona ni muda sahihi wa kuoana. Lilikuwa jambo gumu kwa Deborah kwa kuwa bado moyo wake ulikuwa kwa mwanaume mmoja ambaye mpaka mwaka unakatika hakuweza kumona tena.

Alimwambia Jericho alihitaji muda, hakutakiwa kukurupuka kwenye suala la kuingia kwenye ndoa kwani alihitaji mambo fulani kuyaweka sawa.

Kijana huyo akaamua kuzungumza na wakwe zake ili wamuwekee mambo vizuri, hakutaka kumkosa Deborah, alimpenda na alitamani sana kuwa mke wake.

“Tatizo nini Deborah?” aliuliza mama yake.
“Bado moyo wangu haupo sawa!” alijibu.
“Kwa sababu gani?”

“Namuwaza sana John! Ninampenda kupita kawaida,” alimjibu mama yake.
Mwanamke huyo akakaa kimya, hakuamini alichokisikia, kilimkera lakini hakutakiwa kuonyesha hasira zozote, akaachia tabasamu kama mtu ambaye aliguswa na kile alichoambiwa.

“Usijali! Kuna siku utamsahau tu!” alisema.
“Hivi mama kwa nini mliamua kuniachanisha na John?” aliuliza huku akimwangalia mama yake.

“Kwa kuwa hakufai kabisa.”
“Ni kwa sababu masikini?” aliuliza.
“Hilo ndilo kubwa zaidi!”
“Uliolewa na baba akiwa tajiri?”
“Hapana!”
“Ikawaje wazazi wako walikubali uolewe naye?” aliuliza.

“Deborah! Acha maneno hayo. Tunahitaji uolewe na Jericho,” alisema mama yake kwa hasira na kutoka ndani ya chumba hicho.
Maneno ya binti yake yalimgusa, ni kweli kile alichokizungumza.

Aliolewa na Abraham wakati kijana huyo akiwa masikini wa kutupwa lakini baadaye walipambana wote na kupata maisha waliyokuwanayo kipindi hicho.
 
SEHEMU YA 64

Kama yeye alikubali kuolewa na Abraham akiwa masikini, kwa nini wao walikataa binti yao kuolewa na John kwa kuwa alikuwa masikini?

Hilo lilimuuma sana, akahisi akihukumiwa moyoni mwake, alitokwa na jasho jingi, alionekana kuogopa sana. Mumewe aliporudi, hakutaka kukaa kimya, alimwambia ukweli kila kitu kilichotokea.

“Kwa hiyo yeye anataka kuwa kama sisi?” aliuliza mzee Abraham huku akionekana kuwa na hasira.

“Ila alichoongea kina maana kubwa!”
“Hakina maana! Usimpe nafasi ya kuulaghai moyo wako!” alisema mzee Abraham.
Mzee Abraham alikuwa na msimamo uleule, alichokitaka ni kuona binti yake akiolewa na mwanaume aliyekuwa na pesa kwani hakupenda kuona binti yake akipitia maisha yaliyojaa mateso makubwa.

Baada ya miezi miwili mbele, hatimaye Deborah na Jericho wakawa mume na mke, harusi ambayo ilifungwa katika Kanisa la KKKT. Hiyo ndiyo ilikuwa ndoto ya wazazi wao, kuwaona wakiona na kuwa mume na mke.
|
|

Mama yake Juliana alikuwa na furaha tele baada ya kuona binti yake akiwa amefanikiwa kumpata John, ni kweli alikuwa kijana masikini, asiyekuwa na uwezo lakini moyo wake ulionyesha kuwa mwanaume mpambanaji kupita kawaida.

John aliendelea kufanya biashara ya samaki, alitia huruma, hakuwa na maisha mazuri lakini alitakiwa kupambana kwa sababu tu alihitaji kufunga ndoa na mwanamke aliyekuwa akimpenda mno kipindi hicho.

Siku zilikatika, alizidi kuweka akiba mpaka kufikia kiasi cha shilingi milioni moja. Haraka sana akawaandaa watu kwa ajili ya kwenda kutoa mahari.

Mama Juliana hakuhitaji kitu, alizungumza hivyo hata na kaka zake ambao walikuwa wajomba wa Juliana na kuwaambia hakuhitaji kitu chochote kutoka kwa John kwa kuwa alikuwa mwanaume masikini aliyekuwa akiyapambania maisha yake.

Wakakubaliana, wakawaruhusu watu hao waingie kwenye mchakato wa ndoa na hatimaye baada ya miezi mitatu mbele, watu hao wakaoana na kuwa mume na mke.
 
SEHEMU YA 64

Kama yeye alikubali kuolewa na Abraham akiwa masikini, kwa nini wao walikataa binti yao kuolewa na John kwa kuwa alikuwa masikini?

Hilo lilimuuma sana, akahisi akihukumiwa moyoni mwake, alitokwa na jasho jingi, alionekana kuogopa sana. Mumewe aliporudi, hakutaka kukaa kimya, alimwambia ukweli kila kitu kilichotokea.

“Kwa hiyo yeye anataka kuwa kama sisi?” aliuliza mzee Abraham huku akionekana kuwa na hasira.

“Ila alichoongea kina maana kubwa!”
“Hakina maana! Usimpe nafasi ya kuulaghai moyo wako!” alisema mzee Abraham.

Mzee Abraham alikuwa na msimamo uleule, alichokitaka ni kuona binti yake akiolewa na mwanaume aliyekuwa na pesa kwani hakupenda kuona binti yake akipitia maisha yaliyojaa mateso makubwa.

Baada ya miezi miwili mbele, hatimaye Deborah na Jericho wakawa mume na mke, harusi ambayo ilifungwa katika Kanisa la KKKT. Hiyo ndiyo ilikuwa ndoto ya wazazi wao, kuwaona wakiona na kuwa mume na mke.
|
|

Mama yake Juliana alikuwa na furaha tele baada ya kuona binti yake akiwa amefanikiwa kumpata John, ni kweli alikuwa kijana masikini, asiyekuwa na uwezo lakini moyo wake ulionyesha kuwa mwanaume mpambanaji kupita kawaida.

John aliendelea kufanya biashara ya samaki, alitia huruma, hakuwa na maisha mazuri lakini alitakiwa kupambana kwa sababu tu alihitaji kufunga ndoa na mwanamke aliyekuwa akimpenda mno kipindi hicho.

Siku zilikatika, alizidi kuweka akiba mpaka kufikia kiasi cha shilingi milioni moja. Haraka sana akawaandaa watu kwa ajili ya kwenda kutoa mahari.

Mama Juliana hakuhitaji kitu, alizungumza hivyo hata na kaka zake ambao walikuwa wajomba wa Juliana na kuwaambia hakuhitaji kitu chochote kutoka kwa John kwa kuwa alikuwa mwanaume masikini aliyekuwa akiyapambania maisha yake.

Wakakubaliana, wakawaruhusu watu hao waingie kwenye mchakato wa ndoa na hatimaye baada ya miezi mitatu mbele, watu hao wakaoana na kuwa mume na mke.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom