Simulizi: Mke Wangu Juliana

Simulizi: Mke Wangu Juliana

Sehemu ya 81

“Pole sana! Kama tuna nafasi ya kusaidia! Tumsaidie,” alisema Jericho bila wivu wowote ule.

Wakati akizungumza hayo, simu ya Deborah ikaanza kuita, haraka sana akaichukua na kuipokea, ilitoka kwa Bwana Kinyora ambaye alihitaji kuzungumza naye.

“Mungu ni wa ajabu sana,” alisema mzee huyo kwenye simu, Deborah akawa na hamu ya kusikia ni kitu gani alitakiwa kuambiwa.
“Kwa sababu gani?”

“Nilizungumza na wafanyakazi, wamekubali kumsaidia John kwa pesa zao wenyewe, wakatwe kwenye mishahara yao,” alisema mzee huyo.

“Unasemaje?” aliuliza Deborah huku akiwa haamini alichokuwa akikisikia.
“Wamekubali! Wamesema watachanga kiasi cha shilingi milioni sitini kwa ajili ya John!” alisema mzee huyo.

“Un...as..ema..j..e..” Aliuliza Deborah, hakuamini alichokisikia, akaanza kulia hapohapo.

“Mungu ni mkuu Deborah! Kiwanja chako umeshakiuza?” aliuliza, Deborah hakujibu, alikuwa akilia kwa uchungu, hakuamini kile alichokuwa amekisikia.

Alibaki kwenye hali hiyo kwa dakika nzima ndipo akamwambia kwamba hakukiuza ila alizungumza na mumewe, wote wakakubaliana wauze kiwanja kwa lengo la kupata pesa hizo.
“Mumeo akakubali?”

“Bila kinyongo! Ndiyo nilikuwa nazungumza naye, wewe ukapiga simu!” alisema Deborah.
“Mungu ambariki sana. Ninakuhakikishia wiki hii ataanza kazi hapohapo Kigoma,” alisema mzee huyo, hapohapo akakata simu.
|
|

Je, nini kitaendelea?
Daaaa sopoa Juliana, John, Deborah & Jericho

Mtunzi fundi ila kanitisha maana me manziangu nae Juliana j

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 82

Matangazo yaliendelea kuwekwa kwenye magazeti mbalimbali, michango ilifanikiwa, wananchi waliokuwa na wema, kuguswa walichanganya mpaka kufikia milioni kumi.
Kilikuwa kiasi kikubwa cha pesa, haraka sana mchango kutoka katika kampuni iliyokuwa ikiendeshwa na Bwana Kiyora ikawasilisha mchango wake katika hospitali ya Muhimbili na hatimaye John, mkewe na watoto wao kujiandaa kwa safari ya kwenda nchini India.

Wakati John akipewa taarifa za michango hiyo alikuwa pembeni ya mkewe aliyekuwa kimya. Hakuongea kitu chochote kile japokuwa mume wake huyo alizungumza maneno mengi likiwa la kumshukuru kwa kumzalia watoto wawili hata kama walikuwa wameungana.

Juliana alikuwa akilia tu kitandani pale, maneno ya mume wake yalimgusa kupita kawaida kwani yalionekana kutoka ndani ya moyo wake kabisa.

Baada ya dakika chache, daktari akaingia na kuwapa taarifa kwamba pesa zilipatikana, zilikuwa nyingi zaidi ya zile zilizokuwa zimechangwa hivyo walitakiwa kuanza safari haraka sana.

Hilo halikuwa tatizo, wakajiandaa, mawasiliano baina ya Muhimbili na Hospitali ya Ganga kutoka nchini India yakafanyika na hatimaye wakakubaliana watoto hao wapelekwe haraka sana.

“Kila kitu kipo tayari! Tunatarajia kuanza safari kesho,” alisema dokta, alikuwa akizungumza na John.

“Nashukuru sana! Na sisi tupo tayari!” alisema John.

John akampigia simu Deborah na kumshukuru kwa wema wake kwa kumwambia kwamba kila kitu kilifanikiwa kwa sababu yake, hakujua ni kwa namna gani alitakiwa kumshukuru ila alimwambia kungekuwa na zawadi nzuri ambayo angempa, zawadi ambayo hapakuwa hata na siku moja angeifikiria kuipata kutoka kwa mtu yeyote yule.

Wakaondoka, wakiwa ndani ya ndege ndipo Juliana akaanza kuongea japo kwa sauti ya chini. Alimwambia mume wake jinsi alivyompenda, alivyopenda watoto wake na kuwa tayari kwa kila kitu, hakuacha kumwambia ni kwa namna gani alimshukuru Mungu kwa yote yaliyokuwa yametokea katika maisha yake.

“Hilo ni la muhimu sana! Ila ninaomba unisamehe mke wangu!” alisema John huku akimwangalia mke wake.

“Hujanikosea mpenzi!”
“Hapana! Nimekukosea sana!”
“Kwa lipi?”
 
SEHEMU YA 83

“Nilitaka kucheza kamari, nimeicheza mno na ndiyo imenigharimu sana,” alisema John huku akimwangalia mke wake.

“Sijakuelewa!”
“Najua ni vigumu kunielewa! Ila cha msingi naomba tumshukuru Mungu kwa kila kitu!” alisema John.

Mkewe akakubaliana naye lakini bado moyo wake ulikuwa na maswali mengi kuhusu kamari aliyoicheza mume wake huyo. Ndege ilichukua saa kadhaa ikafika nchini India ambapo tayari gari la wagonjwa kutoka katika Hospitali ya Ganga likawa mahali hapo. Wakapakizwa na kuelekea huko.

Kitu cha kwanza kabla ya yote kilikuwa ni jopo la madaktari kuonana, walikuwa na jambo la kuzungumza na pia kuipitia ripoti ya wagonjwa kutoka katika Hospitali ya Muhimbili.

Waliijadili na kukubaliana utenganisho wa watoto ufanyike kwani ilikuwa vizuri sana kwa kuwa bado walikuwa wadogo, hawakuona kama kungetokea tatizo lolote lile.

John hakujua Kiingereza, aliongea na daktari aliyetoka naye nchini Tanzania ambaye yeye ndiye alikuwa mkalimani wake.

Ripoti hiyo ndiyo ambayo iliwaambia ni wapi walitakiwa kuanzia, kwao, hilo halikuwa suala kubwa ila kitu walichokitaka ni kuwa makini zaidi kwa kuwa mahali pale walipoungana kulikuwa na misuli mingi ya damu.

“Dk. Rajiv utasimamia upasuaji! Kuwa na madaktari sita ndani ya chumba hicho,” alisema Dk Patel ambaye ndiye alikuwa kiongozi wao ndani ya kikao hicho.

Wakakubaliana na hivyo siku iliyofuata madaktari hao wakajipanga na hatimaye kwenda ndani ya chumba hicho kwa lengo la kufanya upasuaji huo.

Kabla ya kitu chochote kile, John na mkewe, Juliana wakapelekewa karatasi za kusaini ambazo zilimaanisha kwa lolote litakalotokea ndani ya chumba kile basi walikuwa tayari kulipokea.
|
|

Mzee Abraham alikuwa akitetemeka ofisini kwake, hakuamini karatasi alizokuwa ameletewa na watu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, TRA. Aliuona mwisho wake, biashara zake alizokuwa akiziendesha zilimfanya kuwa na malimbikizo makubwa ya kodi.
 
SEHEMU YA 84

Ulikuwa mchezo wake, alijua kuucheza, alicheza na vigogo wakubwa kwa kujificha kulipa kodi kwa kuwa alikuwa akizichanga na watu wengine kutoka serikalini mpaka pale ambapo watu wa TRA walipogundua mchezo uliokuwa ukifanywa.

Walishangazwa ni kwa namna gani hawakumbaini mzee huyo, malimbikizo yake ya kodi yalikuwa makubwa mpaka kufikia bilioni mbili lakini hawakugundua kwani mbali na vigogo aliokuwa akicheza nao, pia kulikuwa na watumishi kutoka katika mamlaka hiyo ambao walistaafu.

Walimchachamalia, walimtaka kulipa kiasi hicho cha pesa vinginevyo biashara zake zingefungwa na kupelekwa mahakamani.
Pale ofisini alipokaa alichanganyikiwa, aliona kama dunia imemuelemea, alihitaji msaada na hakujua ni kwa namna gani angeweza kusaidiwa.

Alijisahau, alishindwa kuchanga karata zake vizuri na leo hii alikuwa akiingia kwenye matatizo makubwa kwa sababu tu ya madeni makubwa aliyokuwa akidaiwa na serikali.

Biashara zake zikafungwa na kutaifishwa na serikali na kumtaka kulipa kiasi hicho cha pesa, walimpa siku saba tu afanikishe malipo hayo vinginevyo wangempokonya nyumba zake tatu, magari na kumuacha mikono mitupu.

Pale ofisini alihisi kama presha ikipanda, mwili ulikuwa ukitoka jasho jingi na wakati kiyoyozi kilikuwa kimewashwa chumba kizima.

Akasimama na kuanza kuzunguka huku na kule, hakujua ni kitu gani kingetokea baada ya kunyang’anywa kila kitu, akaunti zake za benki kufungwa, yaani kiasi ambacho alibaki nacho mikononi ndicho ambacho kingeendesha maisha yake.

Akachukua simu yake na kupiga upande wa pili, mtu aliyempigia alikuwa mkurugenzi wa TRA ambaye kwa kipindi hicho alistaafu na nafasi yake kuchukuliwa na mtu mwingine.
Akazungumza naye na kuhitaji msaada wake kwani maji yalimfikia shingoni na hakuona kama angeweza kunusurika katika janga lililokuwa mbele yake.

“Hivi hukulipa tena tangu mwaka ule?” aliuliza mzee huyo, aliitwa Salumu.
“Ndiyo! Nilijisahau! Sijajua kwa nini nilijisahau namna ile,” alisema mzee Abraham.
 
SEHEMU YA 85

“Ila ulitakiwa kulipa. Kipindi kile nilikusamehe kwa sababu tulifanya mambo makubwa sana, kumbe ukahisi ingekuwa hivyohivyo? Ndugu yangu, sijui nikusaidie nini!” alisema mzee huyo maneno yaliyokuwa mwiba mkali kwa mzee Abraham.
“Naomba uzungumze na mkurugenzi!”

“Huyu aliyeingia?”
“Ndiyo!”
“Haiwezekani! Nimesikia jamaa ni mkali sana, hana masihara hata kidogo! Anafuatilia malimbikizo yote ya kodi, kwenye hili janga haupo wewe tu bali mpaka wafanyabiashara wengine,” alisema mzee huyo.

“Kwa hiyo imeshindikana?”
“Ndiyo! Kwani wamekwambia ulipie kiasi gani?”

“Bilioni mbili!”
“Daah! Wamekuonea huruma, wenzako wameambiwa bilioni kumi halafu walikuwa na malimbikizo madogo kushinda wewe,” alisema mzee Salumu.

Bwana Abraham akakata simu, shati lake lililowanishwa na jasho jingi kwani alihisi kabisa huo ndiyo ungekuwa mwisho wake. Hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya.

Aliomba ushauri kwa watu wengine lakini hapakuwa na msaada wowote ule walioweza kumpa zaidi ya kumlaumu kwa kutokulipa kodi mpaka kufikia kiasi hicho cha pesa.

Hakufanya kazi tena, kila kitu alichokuwanacho kilinyang’anywa, akaunti zake benki zilifungwa, magari yake, kampuni yote yakachukuliwa na serikali.

Alidata, akawa anaongea peke yake kama kichaa. Ofisini hakukukalika, akatoka na kurudi nyumbani kwake. Kwa jinsi alivyochanganyikiwa mpaka akataka kupata ajali ya kizembe kabisa.

Alipofika nyumbani kwake, akaingia chumbani na kutulia. Mkewe alimwangalia, alijua kulikuwa na tatizo, haikuwa kawaida kwa mume wake kuwa na muonekano huo, alichanganyikiwa na hivyo kumuuliza.

Hakuwa na jinsi, kwa kipindi hicho alitamani kupata ushauri wa mtu yeyote yule hivyo akamwambia mkewe kila kitu.

Kama alivyochanganyikiwa mumewe na yeye akachanganyikiwa, alimwangalia mume wake, kwa jinsi alivyokuwa na presha alijua kungekuwa na tatizo hivyo akampigia simu Deborah ambaye akafika nyumbani haraka sana.

“Kuna nini?” aliuliza msichana huyo huku akimwangalia baba yake.
“TRA!” alijibu mama yake.

“Wamefanya nini?”
“Wanachukua kila kitu!”
“Kisa?”
“Malimbikizo ya kodi!” alijibu mama yake.
 
SEHEMU YA 86

Deborah hakuamini alichokisikia, alichanganyikiwa, kwake, kila kitu kilichokuwa kimesikika masikioni mwake kilikuwa kama ndoto, akauliza mara kadhaa, majibu yakawa hivyohivyo kwamba ni malimbikizo ya kodi ndiyo ambayo yatafanya kupokonywa kila kitu.

“Mpaka nyumba?” aliuliza.
“Ndiyo! Wameanza na magari ya kampuni, wamezuia akaunti za benki, yaani kila kitu na baada ya siku saba wanavipiga mnada! Tutakuwa wageni wa nani sisi?” aliuliza mama yake na kuanza kulia kama mtoto mdogo.

Deborah akasogea pembeni na kuanza kulia kivyake, hakuamiani, alihisi kama alikuwa ndotoni, kila kitu kilichokuwa hakikuwa halisi.
Akamsogelea baba yake na kumwangalia.

Kumbukumbu za John zikaanza kujirudia kichwani mwake, hakutaka kumficha, alimwambia kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake kilikuwa ni malipo ya ubaya aliokuwa ameufanya.

Hawakumuelewa mpaka pale alipowaambia kuhusu John. Walimnyanyasa kijana huyo, pale alipohitaji kazi, akafanya figisu afukuzwe, alipohitaji msaada kwa watoto wake, alikuwa na uwezo wa kumsaidia lakini hakufanya hivyo.

Kwa mara ya kwanza maneno ya Deborah kuhusu John yakaanza kumuingia kichwani mwake, akaanza kujuta, alitamani kumtafuta John na kumuomba msamaha lakini alichelewa kwani huyo John alisafiri kuelekea nchini India siku tatu zilizopita.

TRA hawakuwa na utani hata kidogo, kwa kuwa kulikuwa na malimbikizo makubwa ya pesa, wakaamua kuzifunga biashara zake, kuchukua kila kitu na nyumba zake tatu zote ziliingia kwenye mnada.

Deborah hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya, akajaribu kuwasiliana na mzee Kayore na kumuhadithia kila kitu ili kama kulikuwa na uwezekano wa kuzungumza na watu wa TRA afanye hivyo lakini mzee huyo hakuweza kufanya hivyo.

“Ni vigumu sana Deborah! Nilitamani nimsaidie baba yako, ila haitowezekana!” alisema mzee huyo.

Kila alipopiga simu, hakupata msaada, alibaki na maumivu moyoni mwake. Baada ya siku saba, nyumba hizo zikapigwa mnada, zikanunuliwa na mfanyabiashara mmoja kutoka mkoani Mwanza, mwanaume aliyekuwa na pesa nyingi na hivyo wao kutakiwa kuhama humo ndani.
 
SEHEMU YA 87

Bila kupenda Deborah akawahamisha wazazi wake na kuwapangia nyumba nzima katika Mtaa wa Kilimahewa, sehemu ambayo walitakiwa kuanza maisha upya.

Afya ya mzee Abraham ilikongoroka, alikonda kwa kipindi kifupi tu, yaani kila kitu kilibadilika, bosi yeye, leo hii alikuwa amepangiwa nyumba na mtoto wake, kila pesa ambayo alikuwanayo, ilipotea.

Aliishi huko na mkewe kwa mwezi mzima, heshima aliyokuwanayo mjini ikaondoka, mbaya zaidi kila mtu alijua kilichokuwa kimetokea.

Watu ambao walikwenda kumuona nyumbani kwake hawakuamini kama alikuwa yeye, alikonda, kitambi cha pesa kikawa kama tumbo la mtu aliyekuwa akiumwa kwashakor.

Kwa kupitia pesa za mtoto wao wa mume wake walikula vizuri lakini mzee huyo hakurudi katika hali ya kawaida, kila siku alikuwa mtu wa mawazo mazito, aliona aibu na muda mwingi alijiilaumu kwa kutokulipa kodi, kitu kilichochangia kuanguka kwake.
 
SEHEMU YA 88

Mwezi wa pili ulipoingia ndipo binti yao, Deborah akawapigia simu na kuwaambia kulikuwa na mgeni aliyetaka kuwaona, alihitaji kuonana nao, wazungumze, na kuwaomba msamaha kwa yote yaliyokuwa yametokea.

“Ni nani?” aliuliza mzee huyo.
“John! Huu ndiyo muda wa kumuomba msamaha!” alijibu Deborah.
“Nikimuomba msamaha nitapata kila kitu nilichokuwanacho kabla?” aliuliza mzee huyo kwa jeuri.

“Hapana! Lakini si ulimkosea! Baba, kuomba msamaha si kitu kigumu, ni jambo dogo tu, kwani ugumu upo wapi? Inawezekana akawa masikini lakini bado anapokosewa anatakiwa kuombwa msamaha!” alisema Deborah.

Haikuishia hapo, mkewe naye alizungumza naye na kumwambia kuhusu suala la msamaha, yeye kama mama alikuwa tayari kuomba msamaha kwani kwa hakika kile walichomfanyia John hakikuwa kitu kizuri kabisa.

“Nipo tayari kuomba msamaha! Mume wangu! Tuombe msamaha!” alisema mke wake.
“Sawa,” aliitikia kwa unyonge.

Baada ya siku mbili John na mkewe Juliana wakiongozana na Deborah aliyekuwa na mume wake, Jericho wakaingia ndani ya nyumba hiyo, walionekana kuwa na afadhali ya maisha tofauti na kipindi cha nyuma.

Sura zao zilionyesha tabasamu pana lilionyesha kabisa roho zao zilikuwa safi kabisa, hapakuwa na mateso kama kipindi cha nyuma, yaani kwa kipindi hicho, mkono wa Mungu ulikuwa juu yao.

Je, nini kitaendelea?

Kumbuka kitabu cha Mikono Iliyomwaga Damu kinaendelea kupatikana kwa namba 0718069269 kwa gharama ya sh. 12,000 tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom