Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,977
- Thread starter
- #141
SEHEMU YA 65
Maisha yalikuwa ya furaha, hawakuwa na pesa nyingi lakini walikuwa na amani tele, waliyafurahia maisha hayo, walikuwa watu wa kupambana na kwa sababu John alipata pesa kidogo alizokuwa ameweka akiba, akamwambia mke wake ni lazima akafungue biashara ya kufanya.
Juliana akaanza kufuatilia biashara ya kuuza vitenge kutoka nchini Kongo na kupeleka hapo Kigoma. Ilikuwa ni biashara nzuri, akaridhia kuifanya na hivyo kumwambia mume wake.
Halikuwa tatizo, wakawekeza kwenye biashara hiyo na hatimaye kuanza huku wakichukua fremu sokoni mjini ambapo huko ndipo alipokuwa akiuza vitenge hivyo.
Ilikuwa biashara nzuri, iliyokuwa ikiingiza kiasi kikubwa cha pesa. Maisha yao yakaanza kubadilika na kitu cha kwanza alichokisema John ni lazima wadogo wa mke wake wahamishwe shule, watoke kwenye shule ya chini na kupelekwa kwenye shule ambayo ilikuwa na hadhi kidogo.
Hilo likamfurahisha mkewe na mkwewe, japokuwa alikuwa na uwezo wa kukataa lakini familia ya mke wake ilikuwa kitu cha kwanza kabisa katika maisha yake.
Aliendelea kuuza samaki huku upande wa pili mke wake akiendelea kuuza vitenge. Maisha yalibadilika kwa kiasi kikubwa mno.
Wakahama Mwanga na kuamia Mlole, mlimani kabisa mbapo walikuwa na uwezo wa kuuangalia mtaa wote wa Mwanga na Mjimwema.
Ilikuwa ni furaha kwao, mafanikio hayo ni kwa sababu tu waliamua kupambana, hawakulala, walifanya kila liwezekanalo kuhakikisha wanafanikiwa na kupiga hatua.
Baada ya wiki kadhaa hatimaye Juliana akamwambia mumewe kuhusu suala la ujauzito, tayari aliziona dalili zilizoonyesha alikuwa na mimba.
Ilikuwa ni furaha kwao, kila mmoja alionekana kulifurahia jambo hilo hivyo kitu walichokifanya ni kumsubiri mtoto kwa hamu kubwa, walikuwa na presha kupita kawaida.
Kila wakati John alikuwa akilibusu tumbo la mke wake, alifurahia, alitamani kuona mtoto akizaliwa mapema hata kabla ya kuzeeka.
Kwa kuwa alikuwa na presha, baada ya miezi kadhaa wakaamua kwenda kuangalia ili kujua jinsia ya mtoto, walipokwenda huko akaambiwa mke wake alikuwa na ujauzito wa watoto mapacha
Maisha yalikuwa ya furaha, hawakuwa na pesa nyingi lakini walikuwa na amani tele, waliyafurahia maisha hayo, walikuwa watu wa kupambana na kwa sababu John alipata pesa kidogo alizokuwa ameweka akiba, akamwambia mke wake ni lazima akafungue biashara ya kufanya.
Juliana akaanza kufuatilia biashara ya kuuza vitenge kutoka nchini Kongo na kupeleka hapo Kigoma. Ilikuwa ni biashara nzuri, akaridhia kuifanya na hivyo kumwambia mume wake.
Halikuwa tatizo, wakawekeza kwenye biashara hiyo na hatimaye kuanza huku wakichukua fremu sokoni mjini ambapo huko ndipo alipokuwa akiuza vitenge hivyo.
Ilikuwa biashara nzuri, iliyokuwa ikiingiza kiasi kikubwa cha pesa. Maisha yao yakaanza kubadilika na kitu cha kwanza alichokisema John ni lazima wadogo wa mke wake wahamishwe shule, watoke kwenye shule ya chini na kupelekwa kwenye shule ambayo ilikuwa na hadhi kidogo.
Hilo likamfurahisha mkewe na mkwewe, japokuwa alikuwa na uwezo wa kukataa lakini familia ya mke wake ilikuwa kitu cha kwanza kabisa katika maisha yake.
Aliendelea kuuza samaki huku upande wa pili mke wake akiendelea kuuza vitenge. Maisha yalibadilika kwa kiasi kikubwa mno.
Wakahama Mwanga na kuamia Mlole, mlimani kabisa mbapo walikuwa na uwezo wa kuuangalia mtaa wote wa Mwanga na Mjimwema.
Ilikuwa ni furaha kwao, mafanikio hayo ni kwa sababu tu waliamua kupambana, hawakulala, walifanya kila liwezekanalo kuhakikisha wanafanikiwa na kupiga hatua.
Baada ya wiki kadhaa hatimaye Juliana akamwambia mumewe kuhusu suala la ujauzito, tayari aliziona dalili zilizoonyesha alikuwa na mimba.
Ilikuwa ni furaha kwao, kila mmoja alionekana kulifurahia jambo hilo hivyo kitu walichokifanya ni kumsubiri mtoto kwa hamu kubwa, walikuwa na presha kupita kawaida.
Kila wakati John alikuwa akilibusu tumbo la mke wake, alifurahia, alitamani kuona mtoto akizaliwa mapema hata kabla ya kuzeeka.
Kwa kuwa alikuwa na presha, baada ya miezi kadhaa wakaamua kwenda kuangalia ili kujua jinsia ya mtoto, walipokwenda huko akaambiwa mke wake alikuwa na ujauzito wa watoto mapacha