Simulizi: Mke Wangu Juliana

Simulizi: Mke Wangu Juliana

SEHEMU YA 65

Maisha yalikuwa ya furaha, hawakuwa na pesa nyingi lakini walikuwa na amani tele, waliyafurahia maisha hayo, walikuwa watu wa kupambana na kwa sababu John alipata pesa kidogo alizokuwa ameweka akiba, akamwambia mke wake ni lazima akafungue biashara ya kufanya.

Juliana akaanza kufuatilia biashara ya kuuza vitenge kutoka nchini Kongo na kupeleka hapo Kigoma. Ilikuwa ni biashara nzuri, akaridhia kuifanya na hivyo kumwambia mume wake.
Halikuwa tatizo, wakawekeza kwenye biashara hiyo na hatimaye kuanza huku wakichukua fremu sokoni mjini ambapo huko ndipo alipokuwa akiuza vitenge hivyo.

Ilikuwa biashara nzuri, iliyokuwa ikiingiza kiasi kikubwa cha pesa. Maisha yao yakaanza kubadilika na kitu cha kwanza alichokisema John ni lazima wadogo wa mke wake wahamishwe shule, watoke kwenye shule ya chini na kupelekwa kwenye shule ambayo ilikuwa na hadhi kidogo.

Hilo likamfurahisha mkewe na mkwewe, japokuwa alikuwa na uwezo wa kukataa lakini familia ya mke wake ilikuwa kitu cha kwanza kabisa katika maisha yake.

Aliendelea kuuza samaki huku upande wa pili mke wake akiendelea kuuza vitenge. Maisha yalibadilika kwa kiasi kikubwa mno.

Wakahama Mwanga na kuamia Mlole, mlimani kabisa mbapo walikuwa na uwezo wa kuuangalia mtaa wote wa Mwanga na Mjimwema.

Ilikuwa ni furaha kwao, mafanikio hayo ni kwa sababu tu waliamua kupambana, hawakulala, walifanya kila liwezekanalo kuhakikisha wanafanikiwa na kupiga hatua.

Baada ya wiki kadhaa hatimaye Juliana akamwambia mumewe kuhusu suala la ujauzito, tayari aliziona dalili zilizoonyesha alikuwa na mimba.

Ilikuwa ni furaha kwao, kila mmoja alionekana kulifurahia jambo hilo hivyo kitu walichokifanya ni kumsubiri mtoto kwa hamu kubwa, walikuwa na presha kupita kawaida.
Kila wakati John alikuwa akilibusu tumbo la mke wake, alifurahia, alitamani kuona mtoto akizaliwa mapema hata kabla ya kuzeeka.

Kwa kuwa alikuwa na presha, baada ya miezi kadhaa wakaamua kwenda kuangalia ili kujua jinsia ya mtoto, walipokwenda huko akaambiwa mke wake alikuwa na ujauzito wa watoto mapacha
 
SEHEMU YA 66

“Unasemaje?” alimuuliza daktari huku akiwa haamini.
“Watoto mapacha!” alijibu daktari huku akionyesha sura ya tabasamu pana, hakuishia hapo, vilevile akawaonyesha kwenye karatasi gumu ambalo lilipiga picha humohumo tumboni.

Kila mmoja alikuwa na furaha, John akazidi kutafuta zaidi kwani aliamini kuwalea watoto mapacha halikuwa jambo dogo, ilikuwa ni lazima ujitoe kwa kiasi kikubwa mno.

Maisha yalikuwa na furaha tele, ile mimba ikawafanya kupendana zaidi na zaidi. Miezi ikakatika, waliendelea kwenda kliniki pamoja, baada ya miezi nane kutimia, wakaenda hospitalini kuangalia hali ya watoto tumboni.

Walipofika huko, Juliana akachukuliwa na kupelekwa kwenye chumba maalumu na kuanza kuangaliwa. Kila mmoja alipigwa na mshtuko baada ya kuona wale watoto mapacha wakiwa tumboni huku wakiwa wameungana.

Daktari alishangaa, aliangalia zaidi na zaidi, alitoa macho, katika maisha yake hakuwahi kuona watoto wa namna hiyo zaidi ya kuwasoma kwenye makala mbalimbali, kwa mfano wa Abby na Brittany, watoto wa Kimarekani waliokuwa wameungana mpaka ukubwani kwao.

“Mungu wangu!” alisema kwa mshtuko.
John na Juliana walionyeshwa picha hizo, hawakuamini, pale alipokuwa amelala, Juliana akaanza kulia, hakuamini kama tumbo lake lilibeba watoto mapacha walioungana.

Aliumia mno, John alikosa nguvu na kujikuta akikaa kwenye kiti, alihuzunika lakini baadaye akagundua kufanya hivyo ilikuwa ni ujinga kwa kuwa yeye ndiye aliyetakiwa kumpoza mke wake na si kuonyesha huzuni.

Akasimama na kumsogelea mke wake aliyekuwa kitandani na kuanza kumbembeleza, mwanamke huyo alikuwa akilia, moyo wake ulimuuma kwani hakuamini kwa maisha ya mateso aliyokuwa amepitia, bado Mungu aliwapa jaribu jingine, watoto mapacha waliokuwa wameungana.

“Nyamaza mke wangu!” alisema John.
“Watoto wetu wameungana! Watoto wetu wameungana mume wangu,” alisema Juliana huku akilia kitandani pale.
|
|

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 66

“Unasemaje?” alimuuliza daktari huku akiwa haamini.
“Watoto mapacha!” alijibu daktari huku akionyesha sura ya tabasamu pana, hakuishia hapo, vilevile akawaonyesha kwenye karatasi gumu ambalo lilipiga picha humohumo tumboni.

Kila mmoja alikuwa na furaha, John akazidi kutafuta zaidi kwani aliamini kuwalea watoto mapacha halikuwa jambo dogo, ilikuwa ni lazima ujitoe kwa kiasi kikubwa mno.

Maisha yalikuwa na furaha tele, ile mimba ikawafanya kupendana zaidi na zaidi. Miezi ikakatika, waliendelea kwenda kliniki pamoja, baada ya miezi nane kutimia, wakaenda hospitalini kuangalia hali ya watoto tumboni.

Walipofika huko, Juliana akachukuliwa na kupelekwa kwenye chumba maalumu na kuanza kuangaliwa. Kila mmoja alipigwa na mshtuko baada ya kuona wale watoto mapacha wakiwa tumboni huku wakiwa wameungana.

Daktari alishangaa, aliangalia zaidi na zaidi, alitoa macho, katika maisha yake hakuwahi kuona watoto wa namna hiyo zaidi ya kuwasoma kwenye makala mbalimbali, kwa mfano wa Abby na Brittany, watoto wa Kimarekani waliokuwa wameungana mpaka ukubwani kwao.

“Mungu wangu!” alisema kwa mshtuko.
John na Juliana walionyeshwa picha hizo, hawakuamini, pale alipokuwa amelala, Juliana akaanza kulia, hakuamini kama tumbo lake lilibeba watoto mapacha walioungana.

Aliumia mno, John alikosa nguvu na kujikuta akikaa kwenye kiti, alihuzunika lakini baadaye akagundua kufanya hivyo ilikuwa ni ujinga kwa kuwa yeye ndiye aliyetakiwa kumpoza mke wake na si kuonyesha huzuni.

Akasimama na kumsogelea mke wake aliyekuwa kitandani na kuanza kumbembeleza, mwanamke huyo alikuwa akilia, moyo wake ulimuuma kwani hakuamini kwa maisha ya mateso aliyokuwa amepitia, bado Mungu aliwapa jaribu jingine, watoto mapacha waliokuwa wameungana.

“Nyamaza mke wangu!” alisema John.
“Watoto wetu wameungana! Watoto wetu wameungana mume wangu,” alisema Juliana huku akilia kitandani pale.
|
|

Je, nini kitaendelea?
Jamani John na Juliana hadi huruma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 67

Moyo wa Juliana ulikuwa na huzuni mno, hakuamini kama yeye ndiye aliyekuwa akipitia maisha hayo, yalimuumiza, yaani walipewa umasikini, uliwasumbua maisha hayo yote na baada ya kuanza kufanikiwa tayari Mungu aliwapa tatizo jingine, lililoonekana kuwa kubwa kuliko hata uwezo wao.

John aliendelea kumfariji mke wake, aache kulia kwani machozi yake yasingebadilisha kile kilichokuwa kimetokea, kama watoto kuungana tumboni, wangeendelea kuwa hivyohivyo.

Baada ya hapo wakarudi nyumbani, kila mmoja alikuwa kimya, bado Juliana aliendelea kuhuzunika na machozi kutiririka mashavuni mwake.

Walipofika, John akawa na muda mwingine wa kumfariji mke wake na kumwamba hapakuwa na tatizo lolote lile, alitakiwa kupumzika na kusahau kilichokuwa kimetokea.

Maisha yaliendelea, John akawa bize na mkewe, hakutaka kumpa nafasi ya kuwa peke yake kwa kipindi kirefu kwa sababu hali hiyo ingemfanya kuanza kufikiria kilichokuwa kimetokea.

Alimwambia hakutakiwa kuwa na majonzi kwani bado Mungu alikuwa na makusudi na maisha yao, hivyo kila kitu kilichotokea walitakiwa kumshukuru Mungu.
“Tumshukuru Mungu kwa kila kitu,” alisema John huku akimwangalia mkewe.

“Kuna wengine hawana watoto, wanatamani hata kupata watoto walioungana lakini imeshindikana, sisi tunapewa watoto hao, kwa nini tusimshukuru Mungu?” aliuliza John huku akimwangalia mke wake.

Siku ziliendelea kukatika, John hakutaka kukaa kimya, alikuwa na uwezo wa kipesa kiasi hivyo alichokifanya ni kuzungumza na mchungaji wake, alimwambia kila kitu kwani kwa jinsi hali ilivyokuwa, siku ya kujifungua ingefika walitakiwa kuelekea jijini Dar es Salaam ili ajifungue salama.

“Ni miezi mingapi imebaki?” aliuliza mchungaji.
“Mwezi mmoja!”
“Una pesa za safari ya kuelekea Dar es Salaam?” aliuliza mchungaji.

“Pesa ninazo, hilo si tatizo!”
“Ila bado kuna kitu kinatakiwa kufanyika. Watoto wako wameungana wapi?” aliuliza mchungaji swali lililomfanya John kuvuta kumbumbuku ya picha aliyoonyeshwa.
“Makalioni!”

“Bado wanaweza kutenganishwa!” alisema mchungaji.
“Kutenganishwa?” aliuliza John huku akionekana kushangaa.
 
SEHEMU YA 68

“Ndiyo! Kuna watoto walizaliwa na kutenganishwa, huwa inafanyika hivyo ila si kwa Tanzania, ni lazima watoto wasafirishwe na kupelekwa nchini India ambapo huwa wanatenganishwa huko, nadhani hapa utatakiwa kutumia pesa zaidi!” alisema mchungaji.

“Kiasi gani?”
“Sijajua! Ila si chini ya milioni arobaini!” alijibu mchungaji.
John akabaki kimya, kile alichoambiwa kilimtisha kwani kiasi kilichotajwa kilikuwa kikubwa mno ambacho hakuwahi kufikiria kabla.

Akaondoka na kurudi nyumbani, alichokifanya ni kuzungumza na mke wake, hakumficha, alimwambia kila kitu kwamba siku chache kabla ya kujifungua walitakiwa kwenda jijini Dar es Salaam ambapo wangepanga chumba huko na kulipia kodi na kusubiri siku ya kujifungua.

Halikuwa tatizo, wakakubaliana na wiki moja kabla ya kujifungua, wakaondoka na kuelekea jijini Dar es Salaam na walipofika wakapanga chumba maeneo ya Kijitonyama.

Baada ya siku kadhaa, Juliana akaanza kujisikia uchungu hivyo John kumchukua na kuelekea naye katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Akapokewa na kuingizwa katika chumba kwa ajili ya kujifungua. Kabla ya kuanza kazi hiyo John akamuita daktari na kumwambia kuhusu watoto wale.

Dokta alishangaa, hakuwahi kumzalisha mwanamke mwenye watoto wa namna hiyo. Akaenda kwenye kile chumba cha leba na kuongea na wenzake, akawaambia kuhusu kile alichoambiwa.

Wote walishangaa kama yeye alivyoshangaa, walikuwa na hamu ya kuwaona watoto wa namna hiyo kwani walisikia tu sehemu mbalimbali na hawakuwahi kuwaona kwa macho.

Muda huo bado Juliana alikuwa akiendelea kulia uchungu wa kujifungua, pale kitandani alipokuwa alijikunjakunja huku na kule, na kuna wakati alihisi kama angeweza kufa kitandani hapo.

Baada ya dakika kadhaa madaktari wakaanza kazi yao, na kwa sababu waliambiwa watoto hao waliungana, madaktari wengine wakaongezekana kuhakikisha mwanamke huyo anajifungua salama.

John alikuwa nje ya chumba hicho, hakutulia, kulikuwa na benchi lakini hakukaa, muda wote alikuwa akitembea huku na kule akimuomba Mungu, alihitaji kuona mkewe akijifungua salama.
 
SEHEMU YA 69

Alikuwa nje ya chumba hicho kwa zaidi ya saa moja, akaanza kusikia sauti za watoto wakilia kutoka ndani ya chumba kile. Akashtuka, akapiga magoti na kumshukuru Mungu.

Machozi yalikuwa yakimtoka, Juliana alijifungua lakini mpaka muda huo hakujua kama mkewe alikuwa mzima ama alifariki, akawa na hamu ya kutaka kulifahamu hilo.

Aliendelea kubaki hapo kwa dakika kadhaa, mlango ukafunguliwa na daktari kutoka. Haraka sana akamfuata na kuanza kuongea naye, alijua watoto wake walikuwa salama, alihitaji kuijua hali ya mke wake.

“Daktari! Mke wangu anaendeleaje?” aliuliza John huku akimwangalia daktari huyo.
“Naomba twende ofisini tukaongee!”
“Hapana daktari! Naomba uniambie kwanza hali ya mke wangu!” alimwambia daktari huyo.

“Twende ofisini!”
“Unataka kunitoa hapa ili muitoe maiti yake muipeleke mochwari?” aliuliza John, tayari mashavu yake yakaanza kujawa machozi yaliyoanza kutiririka kutoka machoni.
“Twende ofisini!” alisema daktari, hakutaka kumpa jibu hapo kuhusu mkewe.

John akahisi akiishiwa nguvu za miguu, kinyonge akaanza kuongozana na daktari huyo kuelekea katika ofisini yake ambayo haikuwa mbali kutoka hapo.

“Pole sana...mkeo amefariki wakati wa kujifungua,” aliisikia sauti hiyo kutka moyoni mwake, sauti iliyosema maneno yaliyomuumiza kupita kawaida.
*
*
Maisha ya ndoa kati ya Deborah na Jericho yalikuwa yakiendelea. Mwanaume huyo alimpenda mkewe kupita kawaida, alimsikiliza, kumuheshimu na kumpa kila aina ya maisha aliyokuwa akiyahitaji kwa kipindi hicho.

Kwa Deborah, alikubaliana na kila kitu lakini hakuacha kumkumbuka John. Mwanaume huyo alikuwa mtu wa tofauti kuliko wanaume wote ambao aliwahi kukutana nao kipindi cha nyuma.

Jericho alilifahamu hilo, alijua ni kwa jinsi gani mkewe alimpenda John hivyo alijitahidi kufanya kila kitu kumfurahisha ili amsahau lakini haikuwezekana kabisa.

Ni mwaka na nusu ulipita lakini bado Deborah alikuwa na mawazo tele juu ya John, na kilichomfanya kuwa katika hali hiyo ni kwa sababu tu wazazi waliamua kumuachanisha naye na wakati moyo wake ulikuwa ukimuhitaji kupita kawaida.
 
SEHEMU YA 69

Alikuwa nje ya chumba hicho kwa zaidi ya saa moja, akaanza kusikia sauti za watoto wakilia kutoka ndani ya chumba kile. Akashtuka, akapiga magoti na kumshukuru Mungu.

Machozi yalikuwa yakimtoka, Juliana alijifungua lakini mpaka muda huo hakujua kama mkewe alikuwa mzima ama alifariki, akawa na hamu ya kutaka kulifahamu hilo.

Aliendelea kubaki hapo kwa dakika kadhaa, mlango ukafunguliwa na daktari kutoka. Haraka sana akamfuata na kuanza kuongea naye, alijua watoto wake walikuwa salama, alihitaji kuijua hali ya mke wake.

“Daktari! Mke wangu anaendeleaje?” aliuliza John huku akimwangalia daktari huyo.
“Naomba twende ofisini tukaongee!”
“Hapana daktari! Naomba uniambie kwanza hali ya mke wangu!” alimwambia daktari huyo.

“Twende ofisini!”
“Unataka kunitoa hapa ili muitoe maiti yake muipeleke mochwari?” aliuliza John, tayari mashavu yake yakaanza kujawa machozi yaliyoanza kutiririka kutoka machoni.
“Twende ofisini!” alisema daktari, hakutaka kumpa jibu hapo kuhusu mkewe.

John akahisi akiishiwa nguvu za miguu, kinyonge akaanza kuongozana na daktari huyo kuelekea katika ofisini yake ambayo haikuwa mbali kutoka hapo.

“Pole sana...mkeo amefariki wakati wa kujifungua,” aliisikia sauti hiyo kutka moyoni mwake, sauti iliyosema maneno yaliyomuumiza kupita kawaida.
*
*
Maisha ya ndoa kati ya Deborah na Jericho yalikuwa yakiendelea. Mwanaume huyo alimpenda mkewe kupita kawaida, alimsikiliza, kumuheshimu na kumpa kila aina ya maisha aliyokuwa akiyahitaji kwa kipindi hicho.

Kwa Deborah, alikubaliana na kila kitu lakini hakuacha kumkumbuka John. Mwanaume huyo alikuwa mtu wa tofauti kuliko wanaume wote ambao aliwahi kukutana nao kipindi cha nyuma.

Jericho alilifahamu hilo, alijua ni kwa jinsi gani mkewe alimpenda John hivyo alijitahidi kufanya kila kitu kumfurahisha ili amsahau lakini haikuwezekana kabisa.

Ni mwaka na nusu ulipita lakini bado Deborah alikuwa na mawazo tele juu ya John, na kilichomfanya kuwa katika hali hiyo ni kwa sababu tu wazazi waliamua kumuachanisha naye na wakati moyo wake ulikuwa ukimuhitaji kupita kawaida.
Jamani sasa mtunzi mbona umemuua Juliana mapema hivi jamani....so sad kwa kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 70

Siku ziliendelea kukatika, maisha yalikuwa ya kawaida. Mume wake alikuwa akifanya kazi katika Shirika la Ndege la ATCL. Wao wote kwa pamoja walikuwa na maisha mazuri, walipendana na kuheshimiana kwa kila kitu.

Baada ya mwezi mmoja shirika hilo likahitaji kupunguza wafanyakazi kwa sababu halikuwa likiingiza pesa kama kipindi kingine kutokana na mashirika mengine ya ndege kuongezeka.

Kwenye orodha ya watu ambao walitakiwa kupunguzwa kazi haraka sana, naye Jericho alikuwa miongoni mwao. Ilikuwa ni taarifa ya ghafla sana, hakuwa amejipanga na siku ambayo alikabidhiwa barua hiyo, hakuamini macho yake, alikuwa akitetemeka huku moyo wake ukiwa na huzuni kupita kawaida.

Akaondoka na kuelekea nyumbani, alitaka kumpigia simu kumwambia Deborah kuhusu kitu hicho lakini akasita, hakutakiwa kumwambia kwenye simu, jambo hilo lilikuwa siriazi, hivyo alitakiwa kumwambia ana kwa ana.

Usiku ulipoingia, Deborah akarudi nyumbani, alimkuta mumewe akiwa kwenye hali ambayo hakuitegemea hata kidogo, alibadilika, hakuwa na furaha kabisa.

Akamuuliza, jibu ambalo alilitoa ni kumpa barua ile Deborah, akaichukua na kuanza kuisoma, hakuamini alichokiona, alibaki akitetemeka, kijasho chembamba kikianza kumtoka.

“Umefukuzwa kazi?” aliuliza Deborah huku akimwangalia mume wake.
“Ndiyo! Shirika halina pesa, mashirika ya ndege yamekuwa mengi sana,” alijibu Jericho huku akimwangalia mke wake.

Akamuinua kutoka pale alipokaa, akamkumbatia na kumwambia kufukuzwa kazi haikuwa mwisho wa kila kitu, kama kweli walipendana, basi hawakutakiwa kuangalia kazi ama kitu chochote kile.

Jericho akaanza kuwa kwenye hali ya majonzi, kitendo cha kufukuzwa kazi kilimfanya kutokuwa na furaha hata kidogo. Maisha hayakuwa magumu kwa kuwa mke wake alikuwa akiendelea kufanya kazi na kulipwa vizuri.

Deborah hakuwa na dharau, alimpa kila kitu mume wake, alimuheshimu kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma. Wazazi wa pande zote mbili wakajua kilichotokea, walimuonea huruma Jericho lakini hawakuwa na cha kufanya.
 
SEHEMU YA 71

Kwa kuwa alikuwa na vyeti vizuri kwa mambo ya akaunti, ikambidi Deborah akazungumze na bosi wake, mzee Masako ili kama itawezekana basi mwanaume huyo apate kazi katika kampuni hiyo kwa kuwa bado kulikuwa na upungufu.

Mzee huyo alimwambia Deborah hapakuwa na nafasi ya kazi yoyote ile ila alitakiwa kuangalia katika makampuni mengine.

Deborah hakutaka kukubali, alijua kabisa kampuni hiyo ilikuwa na nafasi ya kazi hivyo alichokifanya ni kuzungumza na uongozi mkuu uliokuwa jijini Dar es Salaam ambapo walimwambia wangeangalia kama kuna uwezekano basi mwanaume huyo apewe kazi.

Alihangaika kwa ajili ya mume wake, hakutaka kuona akielekea kazini na wakati mume wake alikuwa nyumbani tu.

Alimpambani kwa kipindi cha mwezi mzima bado hakupokea majibu kutoka jijini Dar es Salaam.

Alichokifanya ni kwenda kuomba ushauri kwa baba yake, alihitaji kufahamu kama inawezekana basi aende Dar es Salaam ambapo huko angekwenda yeye mwenyewe.
Alichoshauriwa ni kwenda huko, alitakiwa kuomba ruhusa kazini kuonyesha kama baba yake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa hivyo kwenda huko Dar.

“Inakupasa uende, haina jinsi! Ninafurahi sana kuona unapambana kwa ajili ya mume wako,” alisema baba yake huku uso wake ukiwa na tabasamu pana.

“Nadhani hata John ningempambania hivi, ila hamkutaka kunielewa,” alisema maneno yaliyomfanya mzee huyo kuwa kimya.

Baada ya siku mbili, akasafiri na kwenda Dar es Salaam. Alipofika huko, akachukua chumba katika Hoteli ya Cat iliyokuwa Kariakoo ambapo akatulia na siku iliyofuata akaondoka kuelekea huko makao makuu ya kampuni hiyo.

Alipewa maelekezo yote, mtu ambaye alitakiwa kuonana naye siku hiyo, alipofika, akawasiliana naye na hivyo kukutana ofisini na kuanza kuongea.
 
SEHEMU YA 72

“Wewe ndiye Deborah?” aliuliza mwanaume huyo, alikuwa meneja kwenye kampuni hiyo.

“Umenijuaje?”
“Uliomba kuja kuonana nami kutoka huko Kigoma, ama si wewe?” aliuliza.
“Ndiye mimi!”

Walizungumza, alimwambia kuhusu hali ya mume wake, alifanya kazi kwa miaka sita, alikuwa mtu mwenye sifa nzuri katika kampuni hiyo, hivyo waliongea mambo mengi na meneja huyo, Bwana Kinyora alimwambia angefanya kila juhudi mume wake aajiriwe kwenye kampuni hiyo.
“Nitajitahidi kwa hali na mali!” alisema mwanaume huyo.

Baada ya kumaliza mazungumzo hayo, akatoka na kurudi hotelini, alipofika njiani, akaamua kununua Gazeti la Nipashe ambapo kulikuwa na taarifa ya mwanaume mmoja aliyekuwa akitafuta msaada wa watoto wake walioungana kupelekwa nchini India kwa ajili ya kutenganishwa.

Aliiangalia habari hiyo, hakuona picha ya mwanaume huyo wala watoto hao walioungana lakini alipoangalia namba ile ambayo walitakiwa wasamaria wema watume pesa, aliifahamu vilivyo, ilikuwa namba ambayo haikuwahi kutoka kichwani mwake.

“John!” alijikuta akisema kwa mshtuko, akaamua kuipiga, mwanaume huyo akapokea.
“Halooo!” aliita.
“Halo John!” aliita msichana huyo.
“Deborah?”

“Ndiyo! Ni mimi hapa!” alijibu Deborah! Tayari machozi yakaanza kumtoka, kile alichokuwa amekisoma kwenye gazeti kilimuumiza kupita kawaida.

Yule John, kijana masikini alikuwa akihitaji kiasi cha shilingi milioni hamsini na tano ili watoto wake walioungana wakatenganishwe nchini India.
|
|

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 70

Siku ziliendelea kukatika, maisha yalikuwa ya kawaida. Mume wake alikuwa akifanya kazi katika Shirika la Ndege la ATCL. Wao wote kwa pamoja walikuwa na maisha mazuri, walipendana na kuheshimiana kwa kila kitu.

Baada ya mwezi mmoja shirika hilo likahitaji kupunguza wafanyakazi kwa sababu halikuwa likiingiza pesa kama kipindi kingine kutokana na mashirika mengine ya ndege kuongezeka.

Kwenye orodha ya watu ambao walitakiwa kupunguzwa kazi haraka sana, naye Jericho alikuwa miongoni mwao. Ilikuwa ni taarifa ya ghafla sana, hakuwa amejipanga na siku ambayo alikabidhiwa barua hiyo, hakuamini macho yake, alikuwa akitetemeka huku moyo wake ukiwa na huzuni kupita kawaida.

Akaondoka na kuelekea nyumbani, alitaka kumpigia simu kumwambia Deborah kuhusu kitu hicho lakini akasita, hakutakiwa kumwambia kwenye simu, jambo hilo lilikuwa siriazi, hivyo alitakiwa kumwambia ana kwa ana.

Usiku ulipoingia, Deborah akarudi nyumbani, alimkuta mumewe akiwa kwenye hali ambayo hakuitegemea hata kidogo, alibadilika, hakuwa na furaha kabisa.

Akamuuliza, jibu ambalo alilitoa ni kumpa barua ile Deborah, akaichukua na kuanza kuisoma, hakuamini alichokiona, alibaki akitetemeka, kijasho chembamba kikianza kumtoka.

“Umefukuzwa kazi?” aliuliza Deborah huku akimwangalia mume wake.
“Ndiyo! Shirika halina pesa, mashirika ya ndege yamekuwa mengi sana,” alijibu Jericho huku akimwangalia mke wake.

Akamuinua kutoka pale alipokaa, akamkumbatia na kumwambia kufukuzwa kazi haikuwa mwisho wa kila kitu, kama kweli walipendana, basi hawakutakiwa kuangalia kazi ama kitu chochote kile.

Jericho akaanza kuwa kwenye hali ya majonzi, kitendo cha kufukuzwa kazi kilimfanya kutokuwa na furaha hata kidogo. Maisha hayakuwa magumu kwa kuwa mke wake alikuwa akiendelea kufanya kazi na kulipwa vizuri.

Deborah hakuwa na dharau, alimpa kila kitu mume wake, alimuheshimu kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma. Wazazi wa pande zote mbili wakajua kilichotokea, walimuonea huruma Jericho lakini hawakuwa na cha kufanya.
Wazazi wa Debora wangemtoa mtoto wao kwa Jericho na kumtafutia Mume mwingne..kwao pesa si ndiyo muhimu kuliko furaha ya binti yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom