Simulizi: Mke Wangu Juliana

Simulizi: Mke Wangu Juliana

Daah wakina john wanatuibiaga mademu zetu kila siku maishan sisi ambao hatuna vitu
 
Sehemu ya 20.

“Usiniambie kilichotokea huko! Njoo tuendelee kuuza biashara yetu,” alisema mwanamke huyo hata kabla ya salamu, aliyaona maumivu ya binti yake machoni, hakutaka kabisa kuona wakiliongelea hilo.
“Lakini kwa ni.....”

“Juliana! Nimekwambia usilizungumzie suala hilo! Naomba usilie, huna kazi, bado unaishi mwanangu, kukosa kazi haimaanishi unakufa, kuna watu wana kazi lakini wanateseka vitandani, kuna watu wana kazi lakini hawana amani hata kidogo,” alisema mama yake.
“Lakini mama....”

“Hakuna cha lakini! Huwezi kujua kwa nini unakosa kazi! Mshukuru Mungu kwa kila jambo! Cha msingi tuendelee na kazi zetu na jioni twende kanisani, si unajua leo ni Jumatano?”

“Ndiyo mama!”
“Basi tuuze harakaharaka twende huko! Pamoja na umasikini wetu, matatizo yetu lakini bado tunatakiwa kwenda ibadani. Hii pumzi tu tunayoitumia, ni baraka tosha, baraka si nyumba na magari, kuwa na pesa nyingi, kupumua tu napo tunatakiwa kutambua kwamba hii ni baraka, au hujawahi kusikia kuhusu yule tajiri Ruhuza?” alisema mama yake na kuuliza.

“Kwamba?”
“Alijiua!”
“Nakujua!”
“Sasa yule alikosa nini? Jumba kubwa, magari, pesa lakini bado akajiua!”
“Unamaanisha nini?”

“Furaha, amani ya moyo ndiyo kila kitu! Tunaweza kula bamia kila siku lakini tuna amani kuliko yule anayekula kuku nyumbani kwake! Juliana, naomba usiwe na unyonge tena, umesikia binti yangu?”

“Ndiyo mama!”
“Sawa!” aliitikia msichana huyo na kuanza kuchambua mbogamboga za majani zilizokuwa zimewekwa juu ya kiroba kilichotandikwa chini kwa ajili ya wateja waliokuwa wakifika sokoni hapo.
.
.
.

Je, nini kitaendelea?

Aisee nani atasoma hii kitu yote ndugu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom