Simulizi: Mke Wangu Juliana

Simulizi: Mke Wangu Juliana

Sehemu ya 94

MIAKA KADHAA NYUMA

Hali ya hewa ilibadilika kwa kiasi fulani, lile jua lililokuwa likiwaka kipindi kifupi kilichopita likafunikwa na mawingu mazito yaliyoanza kutanda angani kitu kilichoonyesha muda wowote ule mvua kubwa ingenyesha ndani ya Jiji la Dar es Salaam.

Kijana John Marcela alikuwa ofisini kwake, aliiona saa ikienda taratibu kwa sababu siku hiyo majira ya saa tatu alitakiwa kuwepo kwenye ukumbi wa Twiga uliokuwa Makumbusho kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya harusi ya rafiki yake kipenzi Cosmas Lyaruu.

Alikuwa na hamu ya kuwaona watu hao wawili wakiwa pamoja. Alikuwa na furaha mno, alimkumbuka rafiki yake huyo ambaye alikuwa mbishi mno kila alipokuwa akimwambia kuhusu kuoa.

Waliweka madau kwamba kila mmoja angekuwa wa mwisho kabla ya mwenzake kuamua kufunga ndoa.

Kila walipokutana walikumbushiana ahadi yao lakini bila kutarajia, baada ya Cosmas kukutana na msichana aliyeitwa kwa jina la Cindy Masanja, hakuwa na ujanja tena, akajikuta akiamua kufunga naye ndoa.

John alitamani kumuona Cosmas akiwa na mke wake, hakujua ni kwa namna gani angecheka kiutani na kumwambia yeye alikuwa mshindi wa ahadi ile waliyokuwa wameiweka kwa kipindi kirefu.

Muda mwingi macho yake yalikuwa kwenye saa yake ya ukutani. Alikuwa mtoto wa trilionea mkubwa aliyekuwa na utajiri unaokadiriwa kuwa kiasi cha shilingi trilioni ishirini na nane.

Baba yake, mzee Marcela alikuwa akimiliki makampuni matano, matatu yakiwa nchini Tanzania na mawili yakiwa nchini Afrika Kusini. Yeye ndiye alikuwa mzalishaji mkubwa wa mbao, mkaa, nafaka nchini Tanzania.

Alikuwa akipewa tenda mbalimbali na serikali kama kuleta kompyuta kwenye mashule, kuingiza pembejeo na mambo mengine mengi, kwa kifupi alikuwa mtu mwenye pesa ndefu.

Kwa kuwa alikuwa na utajiri huo, aliamua kumuita kijana wake, John na kuzungumza naye, alichomwambia ni kwamba alitamani sana siku moja aone akisimamia kampuni yake mwenyewe na si zile za familia kama ilivyokuwa.
 
Sehemu ya 95

Alitamani sana kumfundisha kuhusu biashara, alikuwa na mtoto mmoja tu hivyo aliwekeza muda wake na utajiri wake kwa John huyohuyo.

Maisha ya John hayakuwa ya kuridhisha, alijua baba yake alikuwa trilionea mkubwa, aliisha maisha aliyokuwa akiyataka kipindi hicho. Alipenda sana wanawake, alilala na mwanamke yeyote aliyekuwa akimtaka kulala naye.

Alijua kuzitumbua pesa za baba yake, hakuwa mlevi, hakuwahi kwenda klabu, kuvuta bangi wala sigara ila alipenda sana kulala na wanawake.

Wanawake aliokuwa akilala nao walikuwa ni kutoka katika familia za kitajiri.

Hakuwa akilala na mwanamke aliyetoka kwenye maisha ya kimasikini, hakuwapenda kwa kuwa aliamini wengi ambao wangemkubali wangefanya hivyo kwa sababu ya pesa tu, hivyo akaamua kuwafuata wanawake waliokuwa wakitoka kwenye maisha kama aliyokuwa akiishi.

Baada ya baba yake kuona akipotea kwa kutumia sana pesa, akaamua kumuuliza ni kitu gani alitamani sana kuona akimfanyia. Hilo lilikuwa swali gumu kwa John, akaomba muda, angemjibu kwani alitamani sana kumwambia kitu ambacho kingekuwa na msingi mkubwa kwa maisha yake.

Haraka sana akamvutia waya rafiki yake, Cosmas na kumuuliza kwa staili ya kuomba ushauri na ndipo kijana huyo akamwambia amuanzishie kampuni.

“Kampuni gani?” aliuliza John.
“Kusindika samaki! Yaani uwe msambaji mkubwa wa samaki kutoka Kigoma na Mwanza kwa hapa Dar,” alijibu mwanaume huyo.
“Kwa hiyo niwe muuza samaki?” aliuliza.
“John! Sio muuza samaki bali ni mkurugenzi wa kampuni ya kusindika samaki!” alisema Cosmas.

John akakaa kimya kwa muda, akajifikiria sana lakini mwisho wa siku akakubaliana na rafiki yake huyo na hatimaye kumwambia baba yake.

Haraka sana mzee Marcela akafungua kampuni hiyo jijini Dar es Salaam huku ikiwa na matawi mkoani Kigoma na jijini mwanza ambapo kwa huko Kigoma iliitwa Kigoma Fishing Transport na Mwanza kuitwa Mwanza Fishing Transport, yalikuwa kama matawi ya kampuni yake iitwayo Fishing Company iliyokuwa na makao makuu jijini Dar es Salaam.
 
Sehemu ya 96

Matawi hayo yalitakiwa kuwaajiri wavuvi na kuwapa boti kwa lengo la kwenda ziwani kuvua samaki na kuwapeleka katika kiwanda cha kampuni hiyo ambapo waliandaliwa na kisha kusafirishwa kuelekea jijini Dar es Salaam na hapo wengine kusafirishwa kuelekea nchi mbalimbali.

Ilikuwa ni biashara kubwa kipndi hicho, ilionekana kuingiza kiasi kikubwa cha pesa. Makao makuu ya kampuni hiyo yalikuwa Tabata jijini Dar es Salaam lakini yeye akataka ofisi yake iwe Posta.

“Siwezi kukaa uswahilini kule,” alisema alipoulizwa na baba yake kuhusu ofisi yake kuwa Posta.

Wakati John akifikiria hayo yote huku akiwa ofisini kwake, mara simu yake ikaanza kuita, haraka sana akakurupuka na kuichukua kutoka mezani na kuangalia kioo.

“Peter...” alisema na kisha kuipokea.
“John! Unakuja muda gani?” lilikuwa swali kutoka kwa kijana huyo.

Hapo ndipo alipokumbuka kwamba alitakiwa kuonana na Peter na baadhi ya marafiki zake kwa kuwa walikuwa wamemuandalia zawadi Cosmas kama marafiki zake.

Hakukumbuka hilo, alipoambiwa, akakumbuka kila kitu na hivyo kumwambia muda huo walitakiwa kuonana Serena Hotel kwa lengo la kuzungumza.

“Nakuja Serena!” alisema John.
“Poa! Tunakusubiri! Ila acha gari! Kuna bonge la foleni!” alisema Peter.

“Siwezi kutoka hapa Posta ya Zamani mpaka hapo na gari! Natembea kwa miguu tu,” alisema John na kukata simu.

Hakutaka kubaki humo, haraka sana akasimama na kuondoka zake. Alipanda lifti na kuteremka. Kila mtu aliyekuwa akimwangalia, alimuheshimu, alikuwa kijana mdogo lakini mwenye pesa nyingi.

Akatoka getini na kuelekea nje, alipofika huko akaunganisha na lami kutoka upande wa bandari ya Azam ilipo, akawa anakwenda kule kulipokuwa na Hoteli ya New Africa.

Alitembea kwa mwendo wa taratibu kuelekea Posta Mpya, alipofika karibu na Sanamu la Askari macho yake yakatua kwa msichana fulani aliyekuwa amevalia gauni refu jekundu huku kichwani akiwa amezibana nywele zake.
 
Sehemu ya 97

John akasimama kwa sekunde chache na kuanza kumwangalia msichana yule, alivutia, alikuwa mpole tu kwa kumwangalia, alibeba mkoba wake huku akiwa na simu yake mfukoni.

Alikuwa mzee wa wanawake, aliwajua wanawake kama aliwazaa yeye. Mwanamke aliyekuwa msafi, alijua kwa kumwangalia tu, hata aliyekuwa mchafu wa mwili, hata kama alioga na kupaka mafuta yote duniani bado alimjua.

Akakatisha safari yake na kuanza kumfuata. Akaanza kushika barabara iliyokuwa ikienda katika Chuo Cha IFM, alikazana zaidi mpaka alipolipita duka la SH Amon, akavuka barabara na kuelekea sehemu iliyokuwa ikiuzwa vitabu mbalimbali, msichana akasimama hapo. Naye akamfuata.

Akasimama pembeni yake, meza ya vitabu iliyosimama ilikuwa mbele yake, walikuwa wakiviangalia vitabu vile kana kwamba na yeye alikuwa mteja.

Alitamani kumuongelesha lakini akasita, akaona kama angeonekana kuwa na haraka sana, hivyo alikuwa akimvutia pumzi kwanza.

“Unapenda sana kusoma vitabu?” akaamua kuuliza baada ya sekunde kadhaa bila hata salamu.

“Yeah!” alijibu msichana huyo kwa kifupi huku akiwa bize kuchukua kitabu kimoja baada ya kingine.

“Safi sana! Kuna mambo mengi yanafichwa kwenye maandishi! Naweza kukununulia kitabu ukasome?” aliuliza, msichana huyo akashtuka na kuanza kumwangalia.
“Uninunulie kitabu?”

“Ndiyo! Ila kama inawezekana!”
“Unataka kuninunulia vingapi?”
“Wewe unahitaji vingapi?”
“Meza nzima!”
“Haina shida!” alisema John na kutoa tabasamu pana.

Naye msichana huyo akatoa tabasamu.
“By the way! Naitwa John Mtoto wa Uswahilini!” alisema huku akimwangalia msichana huyo na kumpa mkono.
“Naitwa Amanda!”

“Unaelekea wapi?”
“Kuna watu nakwenda kuwaangalia hapo chuo!”
“Unasoma hapo?”
“Hapana nafanya kazi!”
“Wapi?”

“Hapo Mafco!”
“Oh! Kwenye jengo la Benjamini Mkapa?”
“Yaap!” alijibu msichana huyo.
John akashusha pumzi, ni kama aliishiwa maneno, alitulia na kuanza kujifikiria ni kwa namna gani alitakiwa kuendeleza stori na msichana huyo.

Hakutaka kumuacha, ilikuwa ni lazima aendelee kuzungumza naye, amzoee na mwisho kabisa kumuomba namba zake.
“Naomba nikununulie vitabu viwili Amanda,” alisema John.
 
Sehemu ya 98

“Si meza nzima tena?”
“Ukitaka napo hakuna shida!”
“Sawa. Nahitaji viwili nikasome!”
“Unahitaji kipi na kipi?”
“Dili la Dola Bilioni Nne na Damu ya Mwanamwali Kitandani,” alijibu msichana huyo.
“Hakuna shida.”

Akamsogelea muuzaji, mzee fulani wa makamo na kumpa kiasi cha pesa kilichohitaji na kisha kuendelea na safari, muda huu wakawa wanaongozana na kuongea pamoja.
Kila mmoja alionekana kuwa na furaha isiyo kifani, John alijisikia fahari mno, hakuamini kama hatmaye alikuwa akitembea na msichana mzuri kama Amanda.

“Naomba nichafue kitabu chako kimoja,” alisema John huku akimuomba kitabu, akapewa, akatoa kalamu yake na kuandika namba yake ya simuu.

“Naomba unitafute ukipata nafasi!” alisema huku akimrudishia.

“Sawa! Nikipata nafasi! Ahsante kwa vitabu!” alisema Amanda huku akitoa tabasamu.
“Usijali!” alisema John.

Akageuza na kuendelea na safari yake. Yaani msichana mrembo aliisitsha safari hiyo kwa muda. Ni kawaida ya wanaume wote duniani hasa wanapokutana na wanawake wazuri.

John alikutana na marafiki zake na kuanza kuongea kuhusu zawadi ambayo walitakiwa kwenda kumpa Cosmas katika sherehe yake ya ndoa ambayo alitarajiwa kufunga na mchumba wake mrembo.

Kwa kuwa alipenda sana kucheza game, wakapanga kumwandalia zawadi ya Play Station 4 itakayomfanya kuwa bize katika kipindi cha wikiendi, aache kwenda kuzurura kama kawaida yake.

Wakati wakizungumza hayo yote kichwa cha John kilikuwa na mawazo tele, alikuwa akimfikiria msichana aliyekutana naye muda mfupi uliopita. Alimwachia namna yake ya simu lakini hakuwa na uhakika kama angeweza kumpigia ama angemsubirisha kwa siku kadhaa.

Kila wakati alikuwa akiiangalia simu yake, moyo wake ulikuwa na presha kubwa, alipoisikia ikiita, haraka sana akaichukua na kuangalia kioo, alipokuta aliyekuwa akipiga si Amanda, uso wake ulikuwa na hasira mno.
 
Sehemu ya 99

Baada ya kumaliza kikao hicho kifupi, akarudi ofisini kwake ambapo akachukua gari lake na kurudi nyumbani. Mawazo hayakumtoka, yaliendelea kumvuruga kichwa chake kiasi cha kuona muda wowote ule angeweza kukonda hata kama alikuwa na pesa nyingi kiasi gani.

Ilipita siku ya kwanza, ikawa kimya, ikapita ya pili, ya tatu mpaka ya nne ndipo akapokea ujumbe kutoka kwa msichana huyo, haraka sana hakutaka kusubiri, akampigia na kuanza kuzungumza naye.
“Amanda...” aliita huku uso wake ukiwa na tabasamu.

“Niambie John!” alisema msichana huyo.
“I’ve missed you a lot,” (nimekukumbuka sana) alimwambia kwa sauti laini kabisa, ile ya kubembeleza.

“I’ve missed you too!” (nimekukumbuka pia)
“Why didn’t you check on me?” (kwa nini hukunitafuta?) aliuliza.

“I’ve been busy the whole week! By the way! How are you doing?” (nimekuwa bize wiki nzima! Unaendeaje lakini?) alisema msichana huyo.

Wakaanza kupiga stori, moyo wa John ulikuwa na furaha tele, hakuamini kama msichana huyo angeweza kumpigia simu na kuzungumza naye.

Alikuwa na hamu ya kumuona, muda mwingi alikuwa akiiangalia namba ya msichana huyo, picha yake iliganda ubongoni mwake na haikutaka kutoka hata kidogo.

Akashindwa kuvumilia, akamuomba kuonana naye katika Hoteli ya Hyatt ambapo msichana huyo akakubaliana naye na siku hiyo wakaonana.

Ilikuwa ni kwa mara ya pili, alimwangalia jinsi alivyokuwa mzuri, alivyopendeza, kwake alionekana kuwa msichana mrembo kuliko wote ambao aliwahi kukutana nao.

Waliongea na kucheka, walifurahia kupita kawaida. Kwa kuwa msichana huyo alikuwa mchangamfu sana, hakutaka kuona akiondoka, akamuomba sana kama itawezekana basi siku hiyo wakae pamoja mpaka asubuhi.

“No!” (hapana) alisema Amanda.
“Kwa sababu gani?”
“Ninaishi na wazazi wangu! Itakuwaje nikilala nje ya nyumba yetu?” aliuliza.

John akanyamaza, kile alichokizungumza msichana huyo kilikuwa sahihi kabisa, kuamua kulala naye na wakati alikuwa chini ya wazazi wake haikuwa adabu hata kidogo.

|
|

Je, nini kitaendelea?
 
Sehemu ya 98

“Si meza nzima tena?”
“Ukitaka napo hakuna shida!”
“Sawa. Nahitaji viwili nikasome!”
“Unahitaji kipi na kipi?”
“Dili la Dola Bilioni Nne na Damu ya Mwanamwali Kitandani,” alijibu msichana huyo.
“Hakuna shida.”

Akamsogelea muuzaji, mzee fulani wa makamo na kumpa kiasi cha pesa kilichohitaji na kisha kuendelea na safari, muda huu wakawa wanaongozana na kuongea pamoja.
Kila mmoja alionekana kuwa na furaha isiyo kifani, John alijisikia fahari mno, hakuamini kama hatmaye alikuwa akitembea na msichana mzuri kama Amanda.

“Naomba nichafue kitabu chako kimoja,” alisema John huku akimuomba kitabu, akapewa, akatoa kalamu yake na kuandika namba yake ya simuu.

“Naomba unitafute ukipata nafasi!” alisema huku akimrudishia.

“Sawa! Nikipata nafasi! Ahsante kwa vitabu!” alisema Amanda huku akitoa tabasamu.
“Usijali!” alisema John.

Akageuza na kuendelea na safari yake. Yaani msichana mrembo aliisitsha safari hiyo kwa muda. Ni kawaida ya wanaume wote duniani hasa wanapokutana na wanawake wazuri.

John alikutana na marafiki zake na kuanza kuongea kuhusu zawadi ambayo walitakiwa kwenda kumpa Cosmas katika sherehe yake ya ndoa ambayo alitarajiwa kufunga na mchumba wake mrembo.

Kwa kuwa alipenda sana kucheza game, wakapanga kumwandalia zawadi ya Play Station 4 itakayomfanya kuwa bize katika kipindi cha wikiendi, aache kwenda kuzurura kama kawaida yake.

Wakati wakizungumza hayo yote kichwa cha John kilikuwa na mawazo tele, alikuwa akimfikiria msichana aliyekutana naye muda mfupi uliopita. Alimwachia namna yake ya simu lakini hakuwa na uhakika kama angeweza kumpigia ama angemsubirisha kwa siku kadhaa.

Kila wakati alikuwa akiiangalia simu yake, moyo wake ulikuwa na presha kubwa, alipoisikia ikiita, haraka sana akaichukua na kuangalia kioo, alipokuta aliyekuwa akipiga si Amanda, uso wake ulikuwa na hasira mno.
Kibonge mwenzangu Yani hapa ulishanitoa madongo poromoka na kunipeleka posta kuanza kumfuatilia John kwa nyuma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sehemu ya 99

Baada ya kumaliza kikao hicho kifupi, akarudi ofisini kwake ambapo akachukua gari lake na kurudi nyumbani. Mawazo hayakumtoka, yaliendelea kumvuruga kichwa chake kiasi cha kuona muda wowote ule angeweza kukonda hata kama alikuwa na pesa nyingi kiasi gani.

Ilipita siku ya kwanza, ikawa kimya, ikapita ya pili, ya tatu mpaka ya nne ndipo akapokea ujumbe kutoka kwa msichana huyo, haraka sana hakutaka kusubiri, akampigia na kuanza kuzungumza naye.
“Amanda...” aliita huku uso wake ukiwa na tabasamu.

“Niambie John!” alisema msichana huyo.
“I’ve missed you a lot,” (nimekukumbuka sana) alimwambia kwa sauti laini kabisa, ile ya kubembeleza.

“I’ve missed you too!” (nimekukumbuka pia)
“Why didn’t you check on me?” (kwa nini hukunitafuta?) aliuliza.

“I’ve been busy the whole week! By the way! How are you doing?” (nimekuwa bize wiki nzima! Unaendeaje lakini?) alisema msichana huyo.

Wakaanza kupiga stori, moyo wa John ulikuwa na furaha tele, hakuamini kama msichana huyo angeweza kumpigia simu na kuzungumza naye.

Alikuwa na hamu ya kumuona, muda mwingi alikuwa akiiangalia namba ya msichana huyo, picha yake iliganda ubongoni mwake na haikutaka kutoka hata kidogo.

Akashindwa kuvumilia, akamuomba kuonana naye katika Hoteli ya Hyatt ambapo msichana huyo akakubaliana naye na siku hiyo wakaonana.

Ilikuwa ni kwa mara ya pili, alimwangalia jinsi alivyokuwa mzuri, alivyopendeza, kwake alionekana kuwa msichana mrembo kuliko wote ambao aliwahi kukutana nao.

Waliongea na kucheka, walifurahia kupita kawaida. Kwa kuwa msichana huyo alikuwa mchangamfu sana, hakutaka kuona akiondoka, akamuomba sana kama itawezekana basi siku hiyo wakae pamoja mpaka asubuhi.

“No!” (hapana) alisema Amanda.
“Kwa sababu gani?”
“Ninaishi na wazazi wangu! Itakuwaje nikilala nje ya nyumba yetu?” aliuliza.

John akanyamaza, kile alichokizungumza msichana huyo kilikuwa sahihi kabisa, kuamua kulala naye na wakati alikuwa chini ya wazazi wake haikuwa adabu hata kidogo.

|
|

Je, nini kitaendelea?
Nipo kusubiri muendelezo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom