bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,095
RIWAYA: MAUAJI YA KASISI
MTUNZI: richard MWAMBE
WHATSAPP: +255 766 974865
UTANGULIZI
MAUAJI YA KASISI
© Richard Richard Mwambe
Ni kizaazaa katika jiji la Nairobi, Kasisi wa kanisa
katoliki anauawa katika lango kuu la kuingilia
kanisani hapo mapema alfajiri. Sajini Maria na
wasaidizi wake wanaingia kazini kuwasaka wauaji.
Nyuma ya pazia la mauaji hayo, jasusi linalotafutwa
na idara mbalimbali za usalama duniani ikiwemo ile
ya Tanzania (TSA), Bill Van Getgand, anahusishwa
na mauaji hayo kwa kuwakodi majambazi ambao
anawalipa pesa nyingi kumuua kasisi huyo na kisha
kuiba monstrance iliyotoka makao makuu ya kanisa
hilo, Vatican, kwa ajili ya adhimisho la jubilee ya
miaka 100 ya Ukristo nchini Kenya.
Idara mbalimbali za usalama duniani ikiwemo ile ya
Tanzania zinatambua uwepo wa jasusi huyo, hivyo
msako unaanza ndani ya jiji la Nairobi na viunga
vyake.
Kamanda Amata anajikuta tena katika sakata hili
gumu ambalo linaihatarisha kazi yake na maisha
yake kwa ujumla. Anarudishwa Tanzania akiwa hoi,
hajitambui. Anapopata fahamu anaamua kumrudia
jasusi huyo ili kumfunza adabu wakati huo akiwa
hatambuliki na idara yake ya usalama.
Bill anatoroka baada ya kuipata ile monstrance na
kuwaua walio jirani nae ili wasije kutoa siri endapo
watajikuta mikononi mwa polisi. Baada ya kazi nzuri
ya Kamanda Amata mpaka kugundua ni wapi jasusi
huyo yupo, idara yake inamrudisha kazini na
kumtuma ama kumkamata au kumuua kabisa jasusi
huyo anayesumbua dunia.
Ndani ya mji wa Aachen, Ujerumani Kamanda Amata
anafanya kazi ngumu akipata vikwazo kutoka shirika
la upelelezi la USA…. Nini kilijiri huko Ujerumani?
Soma riwaya hii tamu MAUAJI YA KASISI na
mwenyewe utasema hakika hii ni riwaya kali kuliko
zote…
*****************************************************
SEHEMU YA KWANZA
1
HOLY FAMILY BASILICA
NAIROBI – saa 01:00 asubuhi
HAKUNA mtu aliyeamini anachokiona mbele yake,
kila aliyepita njia alitikisa kichwa na wengine
kuangusha machozi. Polisi kutoka kituo cha kati cha
Nairobi walikuwa hapo mbele ya kanisa hilo kubwa
wakifanya uchunguzi wa hili na lile. Mwili usio na
uhai ulikuwa umelala chini na majeraha makubwa
kifuani yakiwa yameganda damu nzito. Hakuna
asiyejua mwili ule ni wa nani, kila aliyepita
alisikitika, wengine hata walighairisha safari zao za
kazini, vilio vilitawala eneo lile. Kila mtu alionekana
kuguswa kwa namna moja au nyingine na mauaji ya
Kasisi huyu wa kanisa la Roman Catholic, Rev Fr
Frederick Gichuru, hakuna aliyejua kwa nini na ni
nani aliyetekeleza mauaji haya ya kinyama. Baada
ya kumsachi hakuna cha ziada walichokikuta katika
kanzu ya kasisi huyo zaidi ya rozari iliyokuwa
mkononi mwake.
“Bila shaka alikuwa katika sala zake za asubuhi”
sauti ya kukwaruza kutoka kwa koplo
Otholong’ong’o ilipenya sikioni mwa sajenti Maria
Kariuki ambaye kwa muda huo alikuwa bado
amepigwa na butwaa. Sajenti Maria alisikitika na
kujutia nafsi yake, alijiona kama mwenye makosa
mbele ya Mungu kwa kifo hicho.
“Ndiyo, afande, daima asubuhi kabla ya misa
makasisi wa kikatoliki huwa na wajibu wa kusali
kwanza wao weyewe” Sajenti Maria alimjibu koplo
Otholong’ong’o huku ukungu mzito ukimtoka
kinywani mwake kuashiria baridi kali ya mwezi wa
sita hapo Nairobi. Bado sajenti Maria alikuwa
kajiinamia jirani kabisa na mwili ule akiuangalia kwa
makini jinsi ulivyoharibiwa kwa risasi, maganda
saba ya Colt 45 yalikuwa mkononi mwake, huku
akiyarusharusha alijinyanyua taratibu na kuamuru
mwili ule uondolewe na kupelekwa chumba cha
maiti cha hospitali ya rufaa.
§§§§§
Inspekta Simon Saitoti alimkazia macho sajenti
Maria aliyekuwa ameketi mbele yake akiwa na
jalada moja la khaki lililoandikwa juu ‘MAUAJI YA
KASISI’, alionekana kama mtu ambaye haelewi
anachoelezwa, alilivuta jalada lile na kuliperuzi
kurasa zake chache kwa dakika kadhaa, kisha
akainua macho yake kutazama ukutani ambako
kulipambwa kwa picha ya muasisi wa taifa hilo,
hayati Jomo Kenyatta.
“Umesema paroko wa kanisa hilo hamjamkuta,
sivyo?” Inspekta Saitoti alimtwanga swali sajenti
Maria.
“Ndiyo afande, na tulipowauliza masista walisema
kuwa kawaida wanakuwa na zamu ya kufanya misa
za asubuhi vigangoni, hivyo paroko alikuwa
amekwenda kigangoni” Maria alijibu kwa ukakamavu
wa kipolisi.
“Ok, mauaji kama haya hayajawahi kutokea hapa
kwetu hii ni mara ya kwanza, na naomba sana iwe
mara ya mwisho, endelea kufanya uchunguzi wa
tukio hili kwa kina ukishirikiana na koplo
Otholong’ong’o na mnipe taarifa za kina, ili tuwatie
mbaroni wauaji.”
“Sawa afande” sajenti Maria alisimama na kurudi
nyuma hatua mbili na kupiga saluti ikiwa ni kitendo
cha kuonesha heshima kwa mkubwa wake kadiri ya
nidhamu za kipolisi.
§§§§§
Kijua cha haja kililing’aza jiji kubwa la Nairobi, jiji
lenye pilikapilika za kila aina katika ukanda wa
Afrika ya Mashariki. Watu walionekana wakitembea
na kuvuka barabara kwa haraka haraka kuashiria
kuwa ukichelewa tu matatu itakugonga. Bado hali ya
ubaridi ilikuwa ikiendelea na kila mtu alionekana
kujidhatiti kwa hali hiyo.
Kwenye kituo kimoja cha basi, mwanaume mmoja
mrefu alikua amesimama akisubiri matatu, mara tu
matatu moja ikafika na muziki mkubwa ndani yake,
akaikaribia na kupanda ndani yake, mkononi alikuwa
na mfuko wa plastiki ulioandikwa UCHUMI, bila
shaka alikuwa akitoka supermarket, safari yake kwa
matatu hiyo iliishia katika kitongoji cha Uthiru Kenoo
barabara kuu ya kwenda Uganda. Kwa mwendo wa
wastani alivuka kwa kupitia daraja kubwa na kufika
upande wa pili wa barabara hiyo ambapo kuna
biashara nyingi, aliliendea gari aina ya Hammer
lililokuwa limepaki hapo, ndani yake hakukuonesha
dalili yoyote ya kuwapo mtu, alifungua mlango kwa
kidubwasha maalum na kuuweka ule mfuko katika
kiti cha mbele kisha akatokomea kusikojulikana.
Takribani nusu saa hakuna aliyeisogelea gari ile,
mara akaja mtu mwingine mnene wa haja pamoja
na mwanamke mmoja mrefu na mwenye mwii
ulioumbika vizuri, wakaingia ndani ya gari ile na
kujifungia milango.
“Shit, washakosea tena” alisikika Yule mtu mnene
akimwambia Yule mwanamke
“Nini tena?”
“Hawako makini na kazi yao, tunawalipa pesa nyingi
lakini hawajui nini cha kufanya, nguruwe wakubwa
hawa”
“Kwani nini?” Yule mwanamke alizidi kudadisi
“Ah, we yaache tu, hutakiwi kujua”
“Aaa jamani, yani umelala na mimi umenambia
vingapi mpaka hili usinambie?”
“Mambo ya kazi haya, achana nayo”.
Ile gari ilitiwa moto na kurudi mjini, hakuna ambaye
angekaa bila kulitupia macho gari hilo kwa jinsi
lilivyo na uzuri wa aina yake na gharama yake ndiyo
iliyotia kiwewe.
Moja kwa moja gari ile ilisimama karibu kabisa na
mtaa wa Koinange, mtaa unaosifika kwa
machangudoa hapo Nairobi.
“Nitakucheki usiku twende club” mtu mnene
mwenye asili ya kihindi alimwambia Yule
mwananmke na kumpa noti za shilingi elfu moja
moja tano za Kikenya.
§§§§§
Askofu mkuu wa jimbo kuu la Nairobi, Mhashamu
Gregory Julius Maina, akiwa ofisini kwake alishikwa
na huzuni kubwa kwa habari ya mauaji ya Fr
Gichuru, alimlilia na kumuombea lakini hakujua ni
nini hasa chanzo cha kifo hicho. Alitafakari na
kuumiza kichwa, kisha akainua macho yake na
kutazama jopo lile la makasisi lililokuwa mbele
yake, kila mmoja alikuwa ama akiangusha au
akijifuta machozi, ukumbi wa parokia ya Maria
Consolatha katika eneo la Westland ulikuwa
umetulia kimya kabisa kana kwamba hakukuwa na
watu ndani yake.
“Nawasalimu katika jina la Bwana” Askofu
aliwasalimu makasisi wale wapatao kama mia mbili
weupe kwa weusi.
“Amen” waliitikia.
“Nina masikitiko moyoni, kuwatangazia rasmi kifo
cha kasisi mwenzetu padre Frederick Gichuru,
paroko msaidizi wa parokia ya Familia Takatifu,
kilichotokea leo alfajiri kwa kupigwa risasi tatu
kifuani na kupoteza uhai papo hapo” alifuta machozi
na kukaa kimya kidogo, kisha akaendelea
“Tunalaani vikali kabisa mauaji haya yasiyo na
sababu inayoeleweka, hatuna cha kusema zaidi ila
sisi kama kanisa tunaiomba serikali na vyombo
vyake vya dola vifanye kazi ya kuwatia nguvuni wote
wanaohusika, na tunawaomba raia wema wanaojua
tetesi yoyote ya kifo hiki kutoa taarifa polisi au hata
kwetu ili kusaidia katika kupambana na kadhia hii.
Zaidi ya yote Bwana awasamehe kwa maana
hawajui watendalo. Ibada ya mazishi itafanyika
keshokutwa katika Basilica la Familia Takatifu”
alimaliza Askofu kutoa tamko kwa niaba ya kanisa,
kisha kuwapatia Baraka na wote wakatawanyika.
“Baba, pole kwa msiba” Kasisi mmoja alimsalimu
paroko wa Basilica la Familia Takatifu ambaye
msaidizi wake ndiye aliyeuawa asubuhi hiyo.
“Tumeshapoa, Mungu mwenyewe anajua”
Mara gari ya polisi aina ya Land Cruiser iliingia
katika viwanja vya kanisa hilo la Consolata, sajenti
Maria alikuwa wa kwanza kuteremka, akiwa ndani ya
suruali yake ya buluu na shati la buluu bahari
alipendeza kwelikweli. Alifanya juu chini kumpata
Padre Joe Smith, raia wa Marekani ambaye ni
paroko wa Basilica lililotokea mauaji, alipompata
alimuomba kuongea naye machache na wote
wakaelekea katika ofisi ya parokia hapo Consolatha.
“Pole sana baba kwa msiba, naitwa sajenti Maria
kutoka kituo cha polisi cha kati Nairobi”
“Asante, tumeshapoa” alijibu Fr Joe Smith kwa
Kiswahili chake kinachopendwa na wengi hasa
anapotoa mahubiri.
“Wakati tukio linatokea, wewe ulikuwa wapi asubuhi
hiyo?”
“Mimi nilikuwa nimekwenda kufanya misa ya
asubuhi kigangoni”
“Siku hiyo ni wewe ulitakiwa uende kigangoni?”
“Hapana, kadiri ya ratiba siku hiyo haikuwa zamu
yangu”
“Enhe sasa ilikuwaje ukaenda?”
“Fr Gichuru, usiku wa jana alinambia kuwa yeye
hajisikii vizuri, hivyo angependa kubaki parokiani”
alimjibu sajenti Maria ambaye alionekana kuandika
vitu Fulani kwenye kitabu chake.
“Je unafahamu lolote kama marehemu alikuwa na
ugomvi na mtu, au hali yoyote tofauti iliyokuwa
katika maeneo yenu kama wachungaji?”
“Kwa kweli katika siku hizi, kumekuwa na mambo
ya ajabu kabisa, kuna watu walikuwa wanakuja sana
pale parokiani na kuuliza mambo mengi kwa watoto
watumishi, wakati Fulani tulimkuta mtu anapekua
Sacristia, walipomuuliza akawachapa makofi.”
“Mlichukua hatua gani?”
“Niwaulize ninyi polisi, mimi nilipiga simu polisi na
mkaahidi kuja kufanyia uchunguzi lakini bho!
Sikuwaona”
“Sawa, msaidizi wako alikuwa na mahusiano ya
kimapenzi na mtu yeyote awe sista au mwingine
yeyote?”
Fr Joe alishtuka kidogo kwa swali hilo. Sajenti
Maria akatoa tabasamu lake lisilo nahisia hata
kidogo mbele ya watu.
“Mbona umeshtuka baba?”
“Eh nikikuuliza wewe kama una mahusiano na
kasisi hautashtuka?” wote wakacheka kisha Joe
akaendelea “Hakuna kitu kama hicho, kama kipo
basi mimi sijui”
“Haya, asante sana baba, kama nikikuhitaji
nitakutafuta” wakapeana mikono na kuagana.
Sista Rose alikuwa akibubujikwa na machozi mbele
ya sajenti Maria.
“Usilie Sista, ni maswali machache tu nataka
kukuuliza”
“Sawa afande”
“Wakati mauaji yanatokea wewe ulikuwa wapi?”
“Muda huo mimi nilikuwa natoka nyumbani kwetu
naenda kuandaa misa kanisani…
Ilivyokuwa
…Ilikuwa yapata saa kumi na moja na nusu alfajiri,
sista Rose alikuwa na zamu ya kwenda kuandaa
misa, aliamka na kujiandaa, kisha akiwa ndani ya
mavazi ya kitawa alitoka nje ya nyumba ‘coventi’
yao na kwa mwendo wa taribu na rozari yake
mkononi alikatisha kauwanja kanakotenganisha
nyumba yao na kanisa, mara alisimama ghafla
moyo wake ulifanya paaah! Hakujua kwa nini, kwa
mbali alimuona Fr Gichuru akiingia kwenye uwanja
wa kanisa hilo akiwa kwenye vazi lake jeusi na kofia
nyeusi yenye nyoya katikati, alivaa kikasisi hasa na
si mara nyingi kuonekana katika mavazi haya.
Alikuwa akitembea taratibu na mara walikutana na
sista Rose katikati ya uwanja, wakasalimiana kwa
ishara lakini Fr Gichuru alibaki kasimama
akimwangalia sista Rose, akamuonesha ishara ya
kuwa ainamishe kichwa chake, sista Rose akafanya
hivyo na Fr Gichuru akamuwekea mikono kichwani
kumbariki, mara mwanga wa taa za gari
ukawamulika kutoka getini, hakuna liyejua ni gari ya
nani, Fr Gichuru akamuacha Sr Rose aendelee na
shughuli yake yeye akaliendea geti…
Sista Rose alikuwa kajibanza kwenye ua kubwa lililo
karibu kabisa na mlango wa kuingilia sakristia,
akiangalia kinachoendelea, baada ya mabishano
mafupi kati ya Fr Gichuru na wale jamaa waliokuja
na ile gari mara alishuhudia kasisi yule akianguka
chini kwa kishindo na sauti ya kike iliamuru wengine
kupanda garini na kuondoka kwa kasi. Sista Rose
alibaki akitetemeka huku machozi yakimwagika na
si kumbubujika, alishindwa afanye nini, awaamshe
wenzake au aende kumsaidia Fr Gichuru, alikuwa
njia panda hakujua afanye nini. Gari ile ilipoondoka
alirudi nyumbani kwao akilia na kuwapa taarifa
wenzake ambao wote waliamka na kwenda kuona
tukio hilo kisha kupiga simu polisi na kwa paroko
ambaye alikuwa ameenda kigangoni kwa misa ya
alfajiri…
“Poleni kwa msiba huo mzito” sajenti Maria alitoa
pole akiwa na macho makavu kabisa, “Labda sista
niambie, unaweza kukumbuka aina ya gari
walilokuja nalo?”
“Kwa kweli ni shida kulikumbuka kwa kuwa
kulikuwa na giza na mi nilikuwa mbali kidogo” sista
alijibu.
“Kipi cha pekee unachokumbuka katika tukio hilo?”
“Sauti ya mwanamke iliyokuwa ikimhimiza
mwenzake kumaliza kazi, nilisikia wakitamka jina
‘Black Cheetah’” alimaliza na kutungua kilio.
“Ok waweza kwenda tutakapokuhitaji tutakupa
taarifa.
§§§§§
Black Cheetah, jambazi sugu linalotafutwa na polisi
ukanda wote wa Africa Mashariki, linajikuta katika
sakata jipya, sakata la mauaji ya kasisi. Kila mtu
aliamini kuwa jambazi hilo si bure tu bali linatumia
hata nguvu za giza kwa jinsi linavyoweza
kuwatoroka polisi katika mazingira ya kutatanisha
hata wenyewe kushindwa kujielewa inakuwakuwaje.
Hakuna aliyekuwa halijui jina hili, si mtoto wala mtu
mzima, jina la Black Cheetah halikuisha midomoni
mwao.
Sajenti Maria alishtushwa kusikia jina hilo likitajwa
na sista Rose kuwa aliisikia sauti ya kike ikilitamka
katika tukio hilo. Alitafakari akaona kibarua hicho si
cha kitoto ni kucheza na mtu au watu waliokomaa
kwenye taaluma.
Black Cheetah, kama anavyojiita ni kijana mtukutu,
mkakamavu, muasi aliyetoroka katika kundi lao la
M23 huko mashariki mwa Congo, aliyetokea kuwa
jambazi sugu na tishio katika ukanda wote wa
Afrika ya mashariki, alikuwa akikodiwa na matajiri
wakubwa kutekeleza mauaji au wizi wa kutumia
silaha. Mara kadhaa ameshahusishwa na wizi wa
benki uliotokea Dar es salaam Tanzania miaka
michache iliyopita, mlipuko wa bomu uliotokea
Kampala wakati watu wakiangalia mpira na matukio
mengi yaliyotukia huko Kenya ambayo hata
hatuwezi kuyaainisha hapa, kwa ujumla alikuwa
gaidi.
Mwezi mmoja uliopita
Ngong Hills Hotel-Nairobi
GARI AINA ya Hammer nyeusi ilisogea taratibu
katika maegesho ya hoteli ya Ngong Hills, watu
watatu, wanaume, wakashuka wakiwa ndani ya suti
nyeusi zilizotanguliwa na shati nyeupe, mmoja kati
yao mwenye mwili mnene alikuwa akitembea kwa
msaada wa fimbo maalum, taratibu waliingia
hotelini hapo na moja kwa moja wakaelekea
sehemu ya chakula na kuchukua meza yenye viti
vine na kuketi, kiti kimoja kilibaki wazi wakaagiza
vyakula na vinywaji na kuanza maongezi yao.
Maongezi yaliendelea na baada ya muda kidogo
kijana mmoja aliingia mahali pale akiwa kavalia koti
kubwa la bluu nyeusi akiwa na kofia kubwa aina ya
pama, kwa hatua za maringo aliijongea meza hiyo,
kila mtu alimuangalia kwa mwendo wake hususan
camera za usalama. Alifika katika meza ile na
kuvuta kiti kimoja kilichobaki kikimsubiri yeye,
akaketi na kuiweka bilauri yake vizuri kabla ya
kuimiminia kinywaji kilichokuwa hapo.
“Yes, Cheetah…” yule bwana anaetembea kwa
msaada wa fimbo alimkaribisha
“Nimeitika wito wako, bwana Bill” Cheetah alijibu.
“Vizuri, hawa ni wadau wenzangu ambao sote
tumekuita ili tukupe kazi maalum” aliendelea
“Nawasikiliza”
“Kuna kazi ndogo tunataka utufanyie” alizungumza
bwana Wambugu, akajikohoza na kuendelea
“Tunataka kitu kinachoitwa Monstrance,
kimehifadhiwa katika kanisa kuu la Familia Takatifu
hapa Nairobi, of course ni kazi ndogo tu”
“Hakuna kazi ndogo kama itahitaji kumwaga damu,
hasa damu ya watu wasio na hatia” Cheetah
alimjibu Wambugu
“No! hatumwagi damu, ni kujua ilipo na kuichukua
basi”
“Unafikiri tutaipata kwa urahisi kama unavyofikiria?
Maana ingekuwa hivyo basi hata wewe ungeenda
pale na kuichukua, lakini kama umeniita mimi
maana yake ni kwamba hiyo si kazi ndogo kwa
vyovyote lazima vyuma vitaongea” Cheetah alimaliza
kauli yake na kuinua bilauri iliyojaa kilevi na
kujimiminia kinywani mwake baada ya
kulishuighulikia pande la nyama lililokuwa ndani ya
sahani hiyo.
“Hilo nalo neno bwana Cheetah. By the way wewe
utajua la kufanya, sisi tunachotaka ni Monstrance
basi” alimaliza bwana Wambugu.
“Ok, tusipoteze muda, mimi nitaunda kikosi kazi
kitakachoweza kufanikisha kazi hiyo, lakini mjue
kule ni kanisani, wale makasisi wana mazindiko
yao, hivyo lazima mnipatie fedha iliyotakata”
“Ha ha ha ha ha hilo usitie shaka bwanaaa bwana
Cheetah” cheko la kivivu lilimtoka yule bwana
anyetembea kwa fimbo, kisha akainua simu yake na
kubofya namba kadhaa, punde tu vijana wawili
waliingia pamwe na briefcase ndogo mkononi,
ikawekwa mezani, kwa ishara ya mkono ya mkono
yule bwana alimuomba Wambugu kuifungua, baada
ya kuzungusha vijinamba Fulani mara yenyewe
ilifyatuka kuashiria kuwa kilichopo kiljaa ndani yake
kwa kukandamizwa hasa. Naam manoti yenye sura
za Moi na Kenyatta yalipangwa na kubanwa katika
mabandali kibao, Black Cheetah macho yalimtoka
pima.
“Ukifanikisha kazi basi hata briefcase hii ni mali
yako” yule bwana alizungumza kivivu.
Black Cheetah alitikisa kichwa juu chini juu chini
kuashiria amekubaliana nao. Kwa kuanzia alipewa
mabandali kadhaa katika mfuko wa plastiki.
Waliagana wane hao na Cheetah akaondoka zake
akiwaacha wao wakiendelea kutumbua mavyakula
yaliyojaa mezani hapo.
Katika maegesho ya magari, Cheetah aliisogelea
gari yake na kusimama kidogo kisha akaangalia uku
na huku, hakuona yeyote wala chochote cha
kushuku, akaingia na kukaa nyuma ya usukani,
milango ikafungwa na vyoo vyote vikabaki juu.
Aliufungu ule mfuko wa karatasi na kuhesabu
burungutu zile, si haba takribani laki mbili za Kenya,
alikenua kwa furaha na kulazimisha tabasamu
ambalo halikuendani na uso wake khasilan. Alitia
gia na kuyaacha maegesho, baada ya kulivuka geti
moja kwa moja aliningia barabara ya Ngong na
kurudi katikati ya jiji la Nairobi.
“Hivi unafikiri tutafanikiwa kuipata?”Wambugu
alimwuliza yule bwana anyetembelea fimbo
“Ha ha ha ha Wambugu unanichekesha sana, kazi
iko kwa Cheetah lazima atararua mpaka tuipate, na
tukishaitia mkononi yule Don kule Ujerumani
atatukatisha kwa pesa nyingi, si ya kitoto” aliongea
kwa sauti yake ya kivivu huku mdomoni akitafuna
vyakula aina aina.
“Don!” Wambugu alishangaa
“Yeah, Don, anaitwa Don Fredrick Schurmann, ni
tajiri sana katika mji wa Achen, yeye ndiye
anayetaka hiyo Monstrance, amesema tukiifikisha
mikononi mwake tutapata pesa nyingi sana, ha ha
ha ha !” alimaliza kwa kucheka na kunyanyua bilauri
yake iliyojaa mnvinyo wa Sant Raphael.
§§§§§
Katika bar kubwa ya Dagoreti Corner super pub,
watu walijaa sana wakiburudika kwa vinywaji, nyama
choma huku muziki laini wa The Mushroom
ukisikika kutoka katika spika kubwa zilizozunguka
eneo hilo. Hakuna aliyefikiria kesho kila mmoja
alijiachia kwa starehe zake alizoziona kuwa
zinamfaa, ilimradi siku ilipita katika mtindo huo.
Katika kona moja ya pub hiyo watu watatu waliketi
katika mtindo wa mzunguko mmoja wao alikuwa
mwanamke walionekana kana kwamba wana
mazungumzo mazito sana, hivyo hakuna mtu
ambaye alisogelea eneo lile zaidi ya mhudumu wa
pub hiyo, naye alikuja tu kuleta alichoagizwa na
kuondoka zake.
“Ndiyo vijana, kuna kazi ya kuifanya haraka
iwezekanavyo” Cheetah alianzisha mazungumzo.
“Tunakusikia mkuu” sauti pekee ya kike iliiitikia
kauli hiyo.
“Tunatakiwa kuchukua mzigo pale Holy Family
Basilica”
“Mapesa mangapi tukachukue?” aliuliza kijana
mwingine aliyeketi hapo.
“Siyo pesa Bwana Gichui, kuna kitu kinaitwa
Monstrance, mnakijua?” Cheetah aliwauliza na wote
wakatazamana.
“Monstrance!?” Mellina Wanjiku alishtuka na
kujishika kifua kwa mshangao.
“Unashtuka nini, unaijua?” Cheetah aliuliza, na yeye
alionekana kushtuka kidogo na kuanza kujiuliza
kama kapokea mbuzi kwenye gunia safari hii.
“Naijua Monstrance, ni chombo kitakatifu sana,
kukishika kwa hila inaweza kuwa matatizo kwetu”
Mellina alijibu kwa upole sana, akatulia kidogo
kisha akaendelea “Pamoja na ujambazi ninaoufanya
sikuwa kufikiri kuligeukia kanisa, kuna nini kwenye
Monstrance hiyo?” aliuliza Mellina
“Ah vile vitu vya wakatoliki huwa vinatengenezwa
kwa dhahabu tu, itakuwa ndiyo wanayoitaka” alijibu
Gichui.
Black Cheetah alijikuta kwenye mtihani mgumu,
kama kuna vitu aliviogopa ni miujiza ya Kimungu
ambayo mara nyingi aliisoma kati vitabu vitakatifu,
mtihani mkubwa! Alijiona amefanya ujinga
kutokuuliza nini kilichomo katika monstrance hiyo,
je kama wakizikuta nyingi ni ipi ya kuichukua, utata!
“Cheetah!” aliita Mellina.
Black Cheetah alishtushwa na wito huo kutoka
katika lindi la mawazo, akawatazama wanakikundi
wenzake ambao yeye aliona wangefaa kwa kazi hiyo
lakini sasa walimfanya hata yeye kushikwa na
wasiwasi.
“Ok, tunafanya kazi au hatufanyi tuchague moja”
aliwapa mtego. Baada ya kutafakari mara mbili
mara tatu wote waliamua kuingia kazini kuisaka hiyo
monstrance.
ITAENDELEA HAPAHAPA MPAKA MWISHO... ILA
UKIITAKA YOTE NIFUATE WHATSAPP UKIWA NA
Tsh 3000 MKONONI
ATT
KITABU CHA 'HARUFU YA KIFO' KITAKUWA SOKONI
MEI. KAMA WAKITAKA MAPEMA WEKA ODA KWA
KUNIANDIKIA SMS 0766974865
MTUNZI: richard MWAMBE
WHATSAPP: +255 766 974865
UTANGULIZI
MAUAJI YA KASISI
© Richard Richard Mwambe
Ni kizaazaa katika jiji la Nairobi, Kasisi wa kanisa
katoliki anauawa katika lango kuu la kuingilia
kanisani hapo mapema alfajiri. Sajini Maria na
wasaidizi wake wanaingia kazini kuwasaka wauaji.
Nyuma ya pazia la mauaji hayo, jasusi linalotafutwa
na idara mbalimbali za usalama duniani ikiwemo ile
ya Tanzania (TSA), Bill Van Getgand, anahusishwa
na mauaji hayo kwa kuwakodi majambazi ambao
anawalipa pesa nyingi kumuua kasisi huyo na kisha
kuiba monstrance iliyotoka makao makuu ya kanisa
hilo, Vatican, kwa ajili ya adhimisho la jubilee ya
miaka 100 ya Ukristo nchini Kenya.
Idara mbalimbali za usalama duniani ikiwemo ile ya
Tanzania zinatambua uwepo wa jasusi huyo, hivyo
msako unaanza ndani ya jiji la Nairobi na viunga
vyake.
Kamanda Amata anajikuta tena katika sakata hili
gumu ambalo linaihatarisha kazi yake na maisha
yake kwa ujumla. Anarudishwa Tanzania akiwa hoi,
hajitambui. Anapopata fahamu anaamua kumrudia
jasusi huyo ili kumfunza adabu wakati huo akiwa
hatambuliki na idara yake ya usalama.
Bill anatoroka baada ya kuipata ile monstrance na
kuwaua walio jirani nae ili wasije kutoa siri endapo
watajikuta mikononi mwa polisi. Baada ya kazi nzuri
ya Kamanda Amata mpaka kugundua ni wapi jasusi
huyo yupo, idara yake inamrudisha kazini na
kumtuma ama kumkamata au kumuua kabisa jasusi
huyo anayesumbua dunia.
Ndani ya mji wa Aachen, Ujerumani Kamanda Amata
anafanya kazi ngumu akipata vikwazo kutoka shirika
la upelelezi la USA…. Nini kilijiri huko Ujerumani?
Soma riwaya hii tamu MAUAJI YA KASISI na
mwenyewe utasema hakika hii ni riwaya kali kuliko
zote…
*****************************************************
SEHEMU YA KWANZA
1
HOLY FAMILY BASILICA
NAIROBI – saa 01:00 asubuhi
HAKUNA mtu aliyeamini anachokiona mbele yake,
kila aliyepita njia alitikisa kichwa na wengine
kuangusha machozi. Polisi kutoka kituo cha kati cha
Nairobi walikuwa hapo mbele ya kanisa hilo kubwa
wakifanya uchunguzi wa hili na lile. Mwili usio na
uhai ulikuwa umelala chini na majeraha makubwa
kifuani yakiwa yameganda damu nzito. Hakuna
asiyejua mwili ule ni wa nani, kila aliyepita
alisikitika, wengine hata walighairisha safari zao za
kazini, vilio vilitawala eneo lile. Kila mtu alionekana
kuguswa kwa namna moja au nyingine na mauaji ya
Kasisi huyu wa kanisa la Roman Catholic, Rev Fr
Frederick Gichuru, hakuna aliyejua kwa nini na ni
nani aliyetekeleza mauaji haya ya kinyama. Baada
ya kumsachi hakuna cha ziada walichokikuta katika
kanzu ya kasisi huyo zaidi ya rozari iliyokuwa
mkononi mwake.
“Bila shaka alikuwa katika sala zake za asubuhi”
sauti ya kukwaruza kutoka kwa koplo
Otholong’ong’o ilipenya sikioni mwa sajenti Maria
Kariuki ambaye kwa muda huo alikuwa bado
amepigwa na butwaa. Sajenti Maria alisikitika na
kujutia nafsi yake, alijiona kama mwenye makosa
mbele ya Mungu kwa kifo hicho.
“Ndiyo, afande, daima asubuhi kabla ya misa
makasisi wa kikatoliki huwa na wajibu wa kusali
kwanza wao weyewe” Sajenti Maria alimjibu koplo
Otholong’ong’o huku ukungu mzito ukimtoka
kinywani mwake kuashiria baridi kali ya mwezi wa
sita hapo Nairobi. Bado sajenti Maria alikuwa
kajiinamia jirani kabisa na mwili ule akiuangalia kwa
makini jinsi ulivyoharibiwa kwa risasi, maganda
saba ya Colt 45 yalikuwa mkononi mwake, huku
akiyarusharusha alijinyanyua taratibu na kuamuru
mwili ule uondolewe na kupelekwa chumba cha
maiti cha hospitali ya rufaa.
§§§§§
Inspekta Simon Saitoti alimkazia macho sajenti
Maria aliyekuwa ameketi mbele yake akiwa na
jalada moja la khaki lililoandikwa juu ‘MAUAJI YA
KASISI’, alionekana kama mtu ambaye haelewi
anachoelezwa, alilivuta jalada lile na kuliperuzi
kurasa zake chache kwa dakika kadhaa, kisha
akainua macho yake kutazama ukutani ambako
kulipambwa kwa picha ya muasisi wa taifa hilo,
hayati Jomo Kenyatta.
“Umesema paroko wa kanisa hilo hamjamkuta,
sivyo?” Inspekta Saitoti alimtwanga swali sajenti
Maria.
“Ndiyo afande, na tulipowauliza masista walisema
kuwa kawaida wanakuwa na zamu ya kufanya misa
za asubuhi vigangoni, hivyo paroko alikuwa
amekwenda kigangoni” Maria alijibu kwa ukakamavu
wa kipolisi.
“Ok, mauaji kama haya hayajawahi kutokea hapa
kwetu hii ni mara ya kwanza, na naomba sana iwe
mara ya mwisho, endelea kufanya uchunguzi wa
tukio hili kwa kina ukishirikiana na koplo
Otholong’ong’o na mnipe taarifa za kina, ili tuwatie
mbaroni wauaji.”
“Sawa afande” sajenti Maria alisimama na kurudi
nyuma hatua mbili na kupiga saluti ikiwa ni kitendo
cha kuonesha heshima kwa mkubwa wake kadiri ya
nidhamu za kipolisi.
§§§§§
Kijua cha haja kililing’aza jiji kubwa la Nairobi, jiji
lenye pilikapilika za kila aina katika ukanda wa
Afrika ya Mashariki. Watu walionekana wakitembea
na kuvuka barabara kwa haraka haraka kuashiria
kuwa ukichelewa tu matatu itakugonga. Bado hali ya
ubaridi ilikuwa ikiendelea na kila mtu alionekana
kujidhatiti kwa hali hiyo.
Kwenye kituo kimoja cha basi, mwanaume mmoja
mrefu alikua amesimama akisubiri matatu, mara tu
matatu moja ikafika na muziki mkubwa ndani yake,
akaikaribia na kupanda ndani yake, mkononi alikuwa
na mfuko wa plastiki ulioandikwa UCHUMI, bila
shaka alikuwa akitoka supermarket, safari yake kwa
matatu hiyo iliishia katika kitongoji cha Uthiru Kenoo
barabara kuu ya kwenda Uganda. Kwa mwendo wa
wastani alivuka kwa kupitia daraja kubwa na kufika
upande wa pili wa barabara hiyo ambapo kuna
biashara nyingi, aliliendea gari aina ya Hammer
lililokuwa limepaki hapo, ndani yake hakukuonesha
dalili yoyote ya kuwapo mtu, alifungua mlango kwa
kidubwasha maalum na kuuweka ule mfuko katika
kiti cha mbele kisha akatokomea kusikojulikana.
Takribani nusu saa hakuna aliyeisogelea gari ile,
mara akaja mtu mwingine mnene wa haja pamoja
na mwanamke mmoja mrefu na mwenye mwii
ulioumbika vizuri, wakaingia ndani ya gari ile na
kujifungia milango.
“Shit, washakosea tena” alisikika Yule mtu mnene
akimwambia Yule mwanamke
“Nini tena?”
“Hawako makini na kazi yao, tunawalipa pesa nyingi
lakini hawajui nini cha kufanya, nguruwe wakubwa
hawa”
“Kwani nini?” Yule mwanamke alizidi kudadisi
“Ah, we yaache tu, hutakiwi kujua”
“Aaa jamani, yani umelala na mimi umenambia
vingapi mpaka hili usinambie?”
“Mambo ya kazi haya, achana nayo”.
Ile gari ilitiwa moto na kurudi mjini, hakuna ambaye
angekaa bila kulitupia macho gari hilo kwa jinsi
lilivyo na uzuri wa aina yake na gharama yake ndiyo
iliyotia kiwewe.
Moja kwa moja gari ile ilisimama karibu kabisa na
mtaa wa Koinange, mtaa unaosifika kwa
machangudoa hapo Nairobi.
“Nitakucheki usiku twende club” mtu mnene
mwenye asili ya kihindi alimwambia Yule
mwananmke na kumpa noti za shilingi elfu moja
moja tano za Kikenya.
§§§§§
Askofu mkuu wa jimbo kuu la Nairobi, Mhashamu
Gregory Julius Maina, akiwa ofisini kwake alishikwa
na huzuni kubwa kwa habari ya mauaji ya Fr
Gichuru, alimlilia na kumuombea lakini hakujua ni
nini hasa chanzo cha kifo hicho. Alitafakari na
kuumiza kichwa, kisha akainua macho yake na
kutazama jopo lile la makasisi lililokuwa mbele
yake, kila mmoja alikuwa ama akiangusha au
akijifuta machozi, ukumbi wa parokia ya Maria
Consolatha katika eneo la Westland ulikuwa
umetulia kimya kabisa kana kwamba hakukuwa na
watu ndani yake.
“Nawasalimu katika jina la Bwana” Askofu
aliwasalimu makasisi wale wapatao kama mia mbili
weupe kwa weusi.
“Amen” waliitikia.
“Nina masikitiko moyoni, kuwatangazia rasmi kifo
cha kasisi mwenzetu padre Frederick Gichuru,
paroko msaidizi wa parokia ya Familia Takatifu,
kilichotokea leo alfajiri kwa kupigwa risasi tatu
kifuani na kupoteza uhai papo hapo” alifuta machozi
na kukaa kimya kidogo, kisha akaendelea
“Tunalaani vikali kabisa mauaji haya yasiyo na
sababu inayoeleweka, hatuna cha kusema zaidi ila
sisi kama kanisa tunaiomba serikali na vyombo
vyake vya dola vifanye kazi ya kuwatia nguvuni wote
wanaohusika, na tunawaomba raia wema wanaojua
tetesi yoyote ya kifo hiki kutoa taarifa polisi au hata
kwetu ili kusaidia katika kupambana na kadhia hii.
Zaidi ya yote Bwana awasamehe kwa maana
hawajui watendalo. Ibada ya mazishi itafanyika
keshokutwa katika Basilica la Familia Takatifu”
alimaliza Askofu kutoa tamko kwa niaba ya kanisa,
kisha kuwapatia Baraka na wote wakatawanyika.
“Baba, pole kwa msiba” Kasisi mmoja alimsalimu
paroko wa Basilica la Familia Takatifu ambaye
msaidizi wake ndiye aliyeuawa asubuhi hiyo.
“Tumeshapoa, Mungu mwenyewe anajua”
Mara gari ya polisi aina ya Land Cruiser iliingia
katika viwanja vya kanisa hilo la Consolata, sajenti
Maria alikuwa wa kwanza kuteremka, akiwa ndani ya
suruali yake ya buluu na shati la buluu bahari
alipendeza kwelikweli. Alifanya juu chini kumpata
Padre Joe Smith, raia wa Marekani ambaye ni
paroko wa Basilica lililotokea mauaji, alipompata
alimuomba kuongea naye machache na wote
wakaelekea katika ofisi ya parokia hapo Consolatha.
“Pole sana baba kwa msiba, naitwa sajenti Maria
kutoka kituo cha polisi cha kati Nairobi”
“Asante, tumeshapoa” alijibu Fr Joe Smith kwa
Kiswahili chake kinachopendwa na wengi hasa
anapotoa mahubiri.
“Wakati tukio linatokea, wewe ulikuwa wapi asubuhi
hiyo?”
“Mimi nilikuwa nimekwenda kufanya misa ya
asubuhi kigangoni”
“Siku hiyo ni wewe ulitakiwa uende kigangoni?”
“Hapana, kadiri ya ratiba siku hiyo haikuwa zamu
yangu”
“Enhe sasa ilikuwaje ukaenda?”
“Fr Gichuru, usiku wa jana alinambia kuwa yeye
hajisikii vizuri, hivyo angependa kubaki parokiani”
alimjibu sajenti Maria ambaye alionekana kuandika
vitu Fulani kwenye kitabu chake.
“Je unafahamu lolote kama marehemu alikuwa na
ugomvi na mtu, au hali yoyote tofauti iliyokuwa
katika maeneo yenu kama wachungaji?”
“Kwa kweli katika siku hizi, kumekuwa na mambo
ya ajabu kabisa, kuna watu walikuwa wanakuja sana
pale parokiani na kuuliza mambo mengi kwa watoto
watumishi, wakati Fulani tulimkuta mtu anapekua
Sacristia, walipomuuliza akawachapa makofi.”
“Mlichukua hatua gani?”
“Niwaulize ninyi polisi, mimi nilipiga simu polisi na
mkaahidi kuja kufanyia uchunguzi lakini bho!
Sikuwaona”
“Sawa, msaidizi wako alikuwa na mahusiano ya
kimapenzi na mtu yeyote awe sista au mwingine
yeyote?”
Fr Joe alishtuka kidogo kwa swali hilo. Sajenti
Maria akatoa tabasamu lake lisilo nahisia hata
kidogo mbele ya watu.
“Mbona umeshtuka baba?”
“Eh nikikuuliza wewe kama una mahusiano na
kasisi hautashtuka?” wote wakacheka kisha Joe
akaendelea “Hakuna kitu kama hicho, kama kipo
basi mimi sijui”
“Haya, asante sana baba, kama nikikuhitaji
nitakutafuta” wakapeana mikono na kuagana.
Sista Rose alikuwa akibubujikwa na machozi mbele
ya sajenti Maria.
“Usilie Sista, ni maswali machache tu nataka
kukuuliza”
“Sawa afande”
“Wakati mauaji yanatokea wewe ulikuwa wapi?”
“Muda huo mimi nilikuwa natoka nyumbani kwetu
naenda kuandaa misa kanisani…
Ilivyokuwa
…Ilikuwa yapata saa kumi na moja na nusu alfajiri,
sista Rose alikuwa na zamu ya kwenda kuandaa
misa, aliamka na kujiandaa, kisha akiwa ndani ya
mavazi ya kitawa alitoka nje ya nyumba ‘coventi’
yao na kwa mwendo wa taribu na rozari yake
mkononi alikatisha kauwanja kanakotenganisha
nyumba yao na kanisa, mara alisimama ghafla
moyo wake ulifanya paaah! Hakujua kwa nini, kwa
mbali alimuona Fr Gichuru akiingia kwenye uwanja
wa kanisa hilo akiwa kwenye vazi lake jeusi na kofia
nyeusi yenye nyoya katikati, alivaa kikasisi hasa na
si mara nyingi kuonekana katika mavazi haya.
Alikuwa akitembea taratibu na mara walikutana na
sista Rose katikati ya uwanja, wakasalimiana kwa
ishara lakini Fr Gichuru alibaki kasimama
akimwangalia sista Rose, akamuonesha ishara ya
kuwa ainamishe kichwa chake, sista Rose akafanya
hivyo na Fr Gichuru akamuwekea mikono kichwani
kumbariki, mara mwanga wa taa za gari
ukawamulika kutoka getini, hakuna liyejua ni gari ya
nani, Fr Gichuru akamuacha Sr Rose aendelee na
shughuli yake yeye akaliendea geti…
Sista Rose alikuwa kajibanza kwenye ua kubwa lililo
karibu kabisa na mlango wa kuingilia sakristia,
akiangalia kinachoendelea, baada ya mabishano
mafupi kati ya Fr Gichuru na wale jamaa waliokuja
na ile gari mara alishuhudia kasisi yule akianguka
chini kwa kishindo na sauti ya kike iliamuru wengine
kupanda garini na kuondoka kwa kasi. Sista Rose
alibaki akitetemeka huku machozi yakimwagika na
si kumbubujika, alishindwa afanye nini, awaamshe
wenzake au aende kumsaidia Fr Gichuru, alikuwa
njia panda hakujua afanye nini. Gari ile ilipoondoka
alirudi nyumbani kwao akilia na kuwapa taarifa
wenzake ambao wote waliamka na kwenda kuona
tukio hilo kisha kupiga simu polisi na kwa paroko
ambaye alikuwa ameenda kigangoni kwa misa ya
alfajiri…
“Poleni kwa msiba huo mzito” sajenti Maria alitoa
pole akiwa na macho makavu kabisa, “Labda sista
niambie, unaweza kukumbuka aina ya gari
walilokuja nalo?”
“Kwa kweli ni shida kulikumbuka kwa kuwa
kulikuwa na giza na mi nilikuwa mbali kidogo” sista
alijibu.
“Kipi cha pekee unachokumbuka katika tukio hilo?”
“Sauti ya mwanamke iliyokuwa ikimhimiza
mwenzake kumaliza kazi, nilisikia wakitamka jina
‘Black Cheetah’” alimaliza na kutungua kilio.
“Ok waweza kwenda tutakapokuhitaji tutakupa
taarifa.
§§§§§
Black Cheetah, jambazi sugu linalotafutwa na polisi
ukanda wote wa Africa Mashariki, linajikuta katika
sakata jipya, sakata la mauaji ya kasisi. Kila mtu
aliamini kuwa jambazi hilo si bure tu bali linatumia
hata nguvu za giza kwa jinsi linavyoweza
kuwatoroka polisi katika mazingira ya kutatanisha
hata wenyewe kushindwa kujielewa inakuwakuwaje.
Hakuna aliyekuwa halijui jina hili, si mtoto wala mtu
mzima, jina la Black Cheetah halikuisha midomoni
mwao.
Sajenti Maria alishtushwa kusikia jina hilo likitajwa
na sista Rose kuwa aliisikia sauti ya kike ikilitamka
katika tukio hilo. Alitafakari akaona kibarua hicho si
cha kitoto ni kucheza na mtu au watu waliokomaa
kwenye taaluma.
Black Cheetah, kama anavyojiita ni kijana mtukutu,
mkakamavu, muasi aliyetoroka katika kundi lao la
M23 huko mashariki mwa Congo, aliyetokea kuwa
jambazi sugu na tishio katika ukanda wote wa
Afrika ya mashariki, alikuwa akikodiwa na matajiri
wakubwa kutekeleza mauaji au wizi wa kutumia
silaha. Mara kadhaa ameshahusishwa na wizi wa
benki uliotokea Dar es salaam Tanzania miaka
michache iliyopita, mlipuko wa bomu uliotokea
Kampala wakati watu wakiangalia mpira na matukio
mengi yaliyotukia huko Kenya ambayo hata
hatuwezi kuyaainisha hapa, kwa ujumla alikuwa
gaidi.
Mwezi mmoja uliopita
Ngong Hills Hotel-Nairobi
GARI AINA ya Hammer nyeusi ilisogea taratibu
katika maegesho ya hoteli ya Ngong Hills, watu
watatu, wanaume, wakashuka wakiwa ndani ya suti
nyeusi zilizotanguliwa na shati nyeupe, mmoja kati
yao mwenye mwili mnene alikuwa akitembea kwa
msaada wa fimbo maalum, taratibu waliingia
hotelini hapo na moja kwa moja wakaelekea
sehemu ya chakula na kuchukua meza yenye viti
vine na kuketi, kiti kimoja kilibaki wazi wakaagiza
vyakula na vinywaji na kuanza maongezi yao.
Maongezi yaliendelea na baada ya muda kidogo
kijana mmoja aliingia mahali pale akiwa kavalia koti
kubwa la bluu nyeusi akiwa na kofia kubwa aina ya
pama, kwa hatua za maringo aliijongea meza hiyo,
kila mtu alimuangalia kwa mwendo wake hususan
camera za usalama. Alifika katika meza ile na
kuvuta kiti kimoja kilichobaki kikimsubiri yeye,
akaketi na kuiweka bilauri yake vizuri kabla ya
kuimiminia kinywaji kilichokuwa hapo.
“Yes, Cheetah…” yule bwana anaetembea kwa
msaada wa fimbo alimkaribisha
“Nimeitika wito wako, bwana Bill” Cheetah alijibu.
“Vizuri, hawa ni wadau wenzangu ambao sote
tumekuita ili tukupe kazi maalum” aliendelea
“Nawasikiliza”
“Kuna kazi ndogo tunataka utufanyie” alizungumza
bwana Wambugu, akajikohoza na kuendelea
“Tunataka kitu kinachoitwa Monstrance,
kimehifadhiwa katika kanisa kuu la Familia Takatifu
hapa Nairobi, of course ni kazi ndogo tu”
“Hakuna kazi ndogo kama itahitaji kumwaga damu,
hasa damu ya watu wasio na hatia” Cheetah
alimjibu Wambugu
“No! hatumwagi damu, ni kujua ilipo na kuichukua
basi”
“Unafikiri tutaipata kwa urahisi kama unavyofikiria?
Maana ingekuwa hivyo basi hata wewe ungeenda
pale na kuichukua, lakini kama umeniita mimi
maana yake ni kwamba hiyo si kazi ndogo kwa
vyovyote lazima vyuma vitaongea” Cheetah alimaliza
kauli yake na kuinua bilauri iliyojaa kilevi na
kujimiminia kinywani mwake baada ya
kulishuighulikia pande la nyama lililokuwa ndani ya
sahani hiyo.
“Hilo nalo neno bwana Cheetah. By the way wewe
utajua la kufanya, sisi tunachotaka ni Monstrance
basi” alimaliza bwana Wambugu.
“Ok, tusipoteze muda, mimi nitaunda kikosi kazi
kitakachoweza kufanikisha kazi hiyo, lakini mjue
kule ni kanisani, wale makasisi wana mazindiko
yao, hivyo lazima mnipatie fedha iliyotakata”
“Ha ha ha ha ha hilo usitie shaka bwanaaa bwana
Cheetah” cheko la kivivu lilimtoka yule bwana
anyetembea kwa fimbo, kisha akainua simu yake na
kubofya namba kadhaa, punde tu vijana wawili
waliingia pamwe na briefcase ndogo mkononi,
ikawekwa mezani, kwa ishara ya mkono ya mkono
yule bwana alimuomba Wambugu kuifungua, baada
ya kuzungusha vijinamba Fulani mara yenyewe
ilifyatuka kuashiria kuwa kilichopo kiljaa ndani yake
kwa kukandamizwa hasa. Naam manoti yenye sura
za Moi na Kenyatta yalipangwa na kubanwa katika
mabandali kibao, Black Cheetah macho yalimtoka
pima.
“Ukifanikisha kazi basi hata briefcase hii ni mali
yako” yule bwana alizungumza kivivu.
Black Cheetah alitikisa kichwa juu chini juu chini
kuashiria amekubaliana nao. Kwa kuanzia alipewa
mabandali kadhaa katika mfuko wa plastiki.
Waliagana wane hao na Cheetah akaondoka zake
akiwaacha wao wakiendelea kutumbua mavyakula
yaliyojaa mezani hapo.
Katika maegesho ya magari, Cheetah aliisogelea
gari yake na kusimama kidogo kisha akaangalia uku
na huku, hakuona yeyote wala chochote cha
kushuku, akaingia na kukaa nyuma ya usukani,
milango ikafungwa na vyoo vyote vikabaki juu.
Aliufungu ule mfuko wa karatasi na kuhesabu
burungutu zile, si haba takribani laki mbili za Kenya,
alikenua kwa furaha na kulazimisha tabasamu
ambalo halikuendani na uso wake khasilan. Alitia
gia na kuyaacha maegesho, baada ya kulivuka geti
moja kwa moja aliningia barabara ya Ngong na
kurudi katikati ya jiji la Nairobi.
“Hivi unafikiri tutafanikiwa kuipata?”Wambugu
alimwuliza yule bwana anyetembelea fimbo
“Ha ha ha ha Wambugu unanichekesha sana, kazi
iko kwa Cheetah lazima atararua mpaka tuipate, na
tukishaitia mkononi yule Don kule Ujerumani
atatukatisha kwa pesa nyingi, si ya kitoto” aliongea
kwa sauti yake ya kivivu huku mdomoni akitafuna
vyakula aina aina.
“Don!” Wambugu alishangaa
“Yeah, Don, anaitwa Don Fredrick Schurmann, ni
tajiri sana katika mji wa Achen, yeye ndiye
anayetaka hiyo Monstrance, amesema tukiifikisha
mikononi mwake tutapata pesa nyingi sana, ha ha
ha ha !” alimaliza kwa kucheka na kunyanyua bilauri
yake iliyojaa mnvinyo wa Sant Raphael.
§§§§§
Katika bar kubwa ya Dagoreti Corner super pub,
watu walijaa sana wakiburudika kwa vinywaji, nyama
choma huku muziki laini wa The Mushroom
ukisikika kutoka katika spika kubwa zilizozunguka
eneo hilo. Hakuna aliyefikiria kesho kila mmoja
alijiachia kwa starehe zake alizoziona kuwa
zinamfaa, ilimradi siku ilipita katika mtindo huo.
Katika kona moja ya pub hiyo watu watatu waliketi
katika mtindo wa mzunguko mmoja wao alikuwa
mwanamke walionekana kana kwamba wana
mazungumzo mazito sana, hivyo hakuna mtu
ambaye alisogelea eneo lile zaidi ya mhudumu wa
pub hiyo, naye alikuja tu kuleta alichoagizwa na
kuondoka zake.
“Ndiyo vijana, kuna kazi ya kuifanya haraka
iwezekanavyo” Cheetah alianzisha mazungumzo.
“Tunakusikia mkuu” sauti pekee ya kike iliiitikia
kauli hiyo.
“Tunatakiwa kuchukua mzigo pale Holy Family
Basilica”
“Mapesa mangapi tukachukue?” aliuliza kijana
mwingine aliyeketi hapo.
“Siyo pesa Bwana Gichui, kuna kitu kinaitwa
Monstrance, mnakijua?” Cheetah aliwauliza na wote
wakatazamana.
“Monstrance!?” Mellina Wanjiku alishtuka na
kujishika kifua kwa mshangao.
“Unashtuka nini, unaijua?” Cheetah aliuliza, na yeye
alionekana kushtuka kidogo na kuanza kujiuliza
kama kapokea mbuzi kwenye gunia safari hii.
“Naijua Monstrance, ni chombo kitakatifu sana,
kukishika kwa hila inaweza kuwa matatizo kwetu”
Mellina alijibu kwa upole sana, akatulia kidogo
kisha akaendelea “Pamoja na ujambazi ninaoufanya
sikuwa kufikiri kuligeukia kanisa, kuna nini kwenye
Monstrance hiyo?” aliuliza Mellina
“Ah vile vitu vya wakatoliki huwa vinatengenezwa
kwa dhahabu tu, itakuwa ndiyo wanayoitaka” alijibu
Gichui.
Black Cheetah alijikuta kwenye mtihani mgumu,
kama kuna vitu aliviogopa ni miujiza ya Kimungu
ambayo mara nyingi aliisoma kati vitabu vitakatifu,
mtihani mkubwa! Alijiona amefanya ujinga
kutokuuliza nini kilichomo katika monstrance hiyo,
je kama wakizikuta nyingi ni ipi ya kuichukua, utata!
“Cheetah!” aliita Mellina.
Black Cheetah alishtushwa na wito huo kutoka
katika lindi la mawazo, akawatazama wanakikundi
wenzake ambao yeye aliona wangefaa kwa kazi hiyo
lakini sasa walimfanya hata yeye kushikwa na
wasiwasi.
“Ok, tunafanya kazi au hatufanyi tuchague moja”
aliwapa mtego. Baada ya kutafakari mara mbili
mara tatu wote waliamua kuingia kazini kuisaka hiyo
monstrance.
ITAENDELEA HAPAHAPA MPAKA MWISHO... ILA
UKIITAKA YOTE NIFUATE WHATSAPP UKIWA NA
Tsh 3000 MKONONI
ATT
KITABU CHA 'HARUFU YA KIFO' KITAKUWA SOKONI
MEI. KAMA WAKITAKA MAPEMA WEKA ODA KWA
KUNIANDIKIA SMS 0766974865